UJIO WA MADAKTARI KUTOKA CHINA NI FURSA – DKT. MWINYI


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa madaktari bingwa kutoka China ni fursa adhimu kuimarisha sekta ya Afya Zanzibar.

Dk. Mwinyi amesema timu ya madaktari bingwa kutoka China imewasili Zanzibar kuongeza nguvu katika sekta ya Afya kwa kutoa wataalamu mbalimbali wakiwemo Madaktari bingwa wa operesheni bila kupasua, magonjwa ya kina mama, magonjwa ya meno, magonjwa ya koo, macho na masikio pamoja na kutoa vifaa vya kisasa.

Madaktari hao watafanya kazi za kitabibu katika hospitali za Mikoa ya Unguja na Pemba ikiwemo Hospitali ya Mnazi Mmoja, Abdalla Mzee, Chake Chake na Kivunge.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipotembelewa Ikulu Zanzibar na Madaktari wapya kutoka China

Ujumbe huo wa Madaktari umeongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *