
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), amewaongoza Viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini, Kimila pamoja na Wananchi wa Mbeya katika mapokezi ya kumpokea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ambaye amewasili Mkoani Mbeya leo Agosti 3, 2022 kwa ziara ya kikazi.
