
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa mapema leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Clouds Media Group @josephkusaga kuhusu vijana kuitumia Fiesta na Clouds kama mlango wa kuingia Katika fursa mbalimbali ambazo zipo katika maeneo yao.
Serikali chini ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI imeendelea kuwainua vijana kutokana na mikopo ya 10% ambayo inatolewa bila riba na Halmashauri zote Nchini.
