TAARIFA YA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KWA MWAKA 2021 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2022/23

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT.
MWIGULU LAMECK NCHEMBA MADELU (MB), AKIWASILISHA
BUNGENI TAARIFA YA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KWA MWAKA
2021 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2022/23
DODOMA JUNI, 2022
1
UTANGULIZI

  1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako
    Tukufu lipokee na kujadili Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa
    Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23.
    Pamoja na hotuba hii, nawasilisha vitabu vya Taarifa ya Hali ya
    Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa
    Taifa wa Mwaka 2022/23. Taarifa hizo ndiyo msingi wa bajeti ya
    Serikali kwa mwaka 2022/23 nitakayowasilisha katika Bunge hili
    Tukufu leo alasiri.
  2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda nitumie fursa hii
    kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema, na
    kutuwezesha kukutana kwa mara nyingine katika Bunge hili baada ya
    majadiliano ya bajeti za mafungu mbalimbali. Mkutano huu wa Saba
    wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muhimu
    katika kujadili namna ya kuharakisha maendeleo ya nchi yetu.
  3. Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena, nitumie fursa
    hii kutoa pole kwako Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge
    wote, Chama cha Mapinduzi na Watanzania wote kufuatia kifo cha
    aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu wa Bunge la Jamhuri ya
    Muungano wa Tanzania, Marehemu Irene Alex Ndyamkama.
    Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi,
    Amina.
  4. Mheshimiwa Spika, kwa moyo mkunjufu, napenda kutoa
    pongezi zangu za dhati kwako Mheshimiwa Spika kwa kuchaguliwa
    kwa kishindo kuwa Spika wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
    wa Tanzania. Waheshimiwa Wabunge na Wananchi kwa ujumla wana
    imani kubwa sana na wewe na hawana shaka na uzoefu, weledi na
    umahiri wako katika kusimamia na kuongoza shughuli za Bunge.
    Aidha, napenda kuchukua fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa
    Mussa Azzan Zungu (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa
    2
    Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niungane na
    Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wenzangu kuwaombea kwa
    Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa nguvu, ujasiri na afya njema ili
    muweze kuendelea kutekeleza majukumu yenu ya kuliongoza Bunge
    letu.
  5. Mheshimiwa Spika, Kwa namna ya kipekee, nitoe pongezi
    zangu za dhati, kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa
    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake thabiti na
    utumishi uliotukuka kwa watanzania unaolenga kuleta mapinduzi
    makubwa ya kiuchumi na kijamii. Mheshimiwa Rais ameonesha
    dhamira yake ya dhati ya kulitumikia Taifa kwa uaminifu ambapo
    ameendelea kusimamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali
    zinazolenga kuleta maendeleo kwa Watanzania ikiwemo: kuendelea
    kutekeleza miradi mikubwa ya kielelezo na miradi mingine ya
    kuchochea uchumi na kuimarisha huduma za jamii; kuendeleza
    mapambano dhidi ya rushwa; na kuimarisha ushirikiano wa kikanda
    na kimataifa.
  6. Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amekuwa akiendelea
    kutuongoza kwa vitendo kwa kuchukua hatua mbalimbali za
    kuchochea ukuaji wa uchumi hususan sekta ya utalii ambayo
    iliathirika zaidi na UVIKO-19 ikiwemo kushiriki kwenye filamu
    ijulikanayo kwa jina la The Royal Tour kama Mwongoza Utalii Namba
    Moja Nchini. Mheshimiwa Rais amekuwa chachu na kinara wa utalii
    kupitia filamu hiyo inayolenga kukuza sekta ya utalii ambayo
    inatarajiwa kuzalisha takriban ajira milioni 1.3 na fedha za kigeni dola
    za Marekani bilioni 2.6. Filamu hiyo iliyozinduliwa kwa Mara ya
    Kwanza Jijini New York tarehe 18 Aprili 2022 na baadaye tarehe 21
    Aprili 2022 Jijini Los Angeles. Ndugu Watanzania wenzangu, hii ni
    hatua kubwa sana kwa Taifa letu kwa kuwa filamu hii inapatikana
    kupitia chaneli za Apple TV Plus na Amazon Prime za nchini Marekani
    ambazo zinakadiriwa kuwa na watazamaji zaidi ya milioni 200
    3
    duniani. Ama kwa Hakika Mama Anaupiga Mwingi; na hivyo
    tuna kila sababu ya kuunga mkono jitihada hizi na kwenda
    pamoja na Mama.
  7. Mheshimiwa Spika, kipekee natoa shukrani zangu za dhati
    kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya
    Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini kumsaidia kazi
    katika nafasi ya Waziri wa Fedha na Mipango. Kwa imani hii
    aliyoionesha kwangu napenda kuwahakikishia Mheshimiwa Rais,
    Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwa ujumla kuwa
    nitaendelea kutekeleza majukumu yangu kwa bidii kubwa, weledi,
    uaminifu, uadilifu na uzalendo wa kiwango cha hali ya juu ili
    kuhakikisha matamanio ya Mheshimiwa Rais na Watanzania wote ya
    kuwa na maendeleo na ustawi wa kiwango cha juu yanafikiwa.
  8. Mheshimiwa Spika, Sote tunafahamu kuwa, nchi yetu na
    dunia kwa ujumla inaendelea kushuhudia athari za UVIKO-19 ambazo
    zimesababisha kushuka kwa shughuli za kiuchumi duniani, ikiwemo
    uzalishaji, biashara za ndani na kimataifa, utalii na usafirishaji wa
    bidhaa. Katika mwaka 2021, uchumi wa Taifa letu na wa dunia kwa
    ujumla ulianza kuimarika baada ya kupitia katika kipindi cha
    kukabiliana na athari za UVIKO–19. Aidha, wakati Serikali ikiendelea
    na jitihada za kuimarisha uchumi, mwezi Februari 2022 kuliibuka vita
    kati ya mataifa ya Urusi na Ukraine ambayo imesababisha Urusi
    kuwekewa vikwazo na hivyo kusababisha kupanda kwa bei za bidhaa
    mbalimbali katika soko la dunia zikiwemo mafuta na gesi. Sanjari na
    kupanda kwa bei hizo, kumekuwa na uhaba wa baadhi ya bidhaa
    katika soko la Dunia ikiwemo, mbolea, ngano na mafuta ya kula.
    Serikali imeendelea kuchukua hatua katika kukabiliana na athari hizo
    ikiwemo kupokea Mkopo wa Masharti nafuu wa shilingi trilioni 1.3
    zilizoelekezwa katika sekta ya afya, elimu, maji na utalii ili kuchochea
    uchumi na kukabiliana na UVIKO-19; kuongeza bajeti ya kilimo,
    mifugo, uvuvi, nishati na miundombinu ya wafanyabiashara wadogo
    4
    maarufu kama machinga ili kuchochea uzalishaji wa ndani na
    kupunguza nakisi ya urari wa biashara; na kuangalia namna bora ya
    uagizaji mafuta itakayoleta unafuu wa bei kwa wananchi. Aidha,
    nichukue fursa hii kulihakikishia Bunge lako Tukufu na Watanzania
    wote kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili
    kukabiliana na athari hizo kwa lengo la kuleta unafuu wa maisha kwa
    Wananchi.
  9. Mheshimiwa Spika, Nipende kuwashukuru wadau wote
    walioshiriki katika mchakato huu nikianza na Bunge lako Tukufu chini
    ya uongozi wako Mheshimiwa Spika pamoja na Naibu Spika wa
    Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, napenda
    kumshukuru Mheshimiwa Sillo Daniel Baran (Mb), Mwenyekiti wa
    Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na wajumbe wote wa Kamati
    kwa ushauri wao mahiri wakati wa uandaaji wa taarifa nilizowasilisha
    mbele ya Bunge lako Tukufu.
  10. Mheshimiwa Spika, Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa
    Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23
    imeandaliwa kwa kuzingatia mwenendo wa viashiria vya uchumi
    jumla na sekta mbalimbali kwa mwaka husika ikilinganishwa na
    mwaka 2020. Aidha, maandalizi ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa
    wa Mwaka 2022/23 yamezingatia vipaumbele vya Serikali
    vilivyoainishwa katika Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa
    Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi
    Mkuu wa Mwaka 2020 na Hotuba ya Mheshimiwa Samia Suluhu
    Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
    akilihutubia rasmi Bunge hili la 12 la Jamhuri ya Muungano wa
    Tanzania tarehe 22 Aprili, 2021. Aidha, Mpango umezingatia Sera na
    Mikakati mbalimbali ya kisekta, kikanda na kimataifa zikiwemo Dira
    ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) 2050; Dira ya
    Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) 2050; Ajenda 2063
    ya Maendeleo ya Afrika; na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.
    5
  11. Mheshimiwa Spika, Katika kutekeleza Mpango wa mwaka
    2022/23, msukumo mkubwa utawekwa katika sekta za uzalishaji
    ambazo ni kilimo, mifugo, uvuvi na nishati kwa kuwa sekta hizi
    huchochea uzalishaji kwa matumizi ya ndani na mauzo nje ya nchi,
    hupunguza nakisi ya urari wa biashara, mfumuko wa bei na huzalisha
    ajira zinazowagusa wananchi wengi. Sambamba na vipaumbele
    hivyo, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi mingine ya
    maendeleo ikiwemo miradi ya kielelezo ya ujenzi wa Reli kwa
    Kiwango cha Kimataifa (SGR), ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme wa
    Maji la Julius Nyerere – MW 2,115, uboreshaji wa Shirika la Ndege
    Tanzania (ATCL) pamoja na miradi ya elimu, afya, maji, usafiri wa
    anga na majini, bandari, maliasili na utalii, mapinduzi ya TEHAMA,
    miundombinu ya barabara na madaraja na kuboresha mazingira ya
    biashara na uwekezaji ili kukuza ustawi wa sekta binafsi nchini.
    MWENENDO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2021
    Uchumi wa Dunia
  12. Mheshimiwa Spika, Taarifa ya Shirika la Fedha la Kimataifa
    (IMF) ya Aprili 2022 inaonesha kuwa, uchumi wa dunia uliimarika na
    kufikia wastani wa asilimia 6.1 mwaka 2021 ikilinganishwa na ukuaji
    hasi wa asilimia 3.1 mwaka 2020. Kuimarika kwa uchumi wa dunia
    kumetokana na hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa
    na nchi mbalimbali katika kuimarisha uchumi, ikiwemo utekelezaji wa
    sera za fedha na bajeti zinazochochea shughuli za uchumi
    zilizoathirika na kuendelea kuimarishwa kwa huduma za afya ikiwemo
    uhamasishaji na usambazaji wa chanjo kwa lengo la kupunguza
    athari za UVIKO-19. Hata hivyo, uchumi wa dunia unatarajiwa
    kupungua na kufikia ukuaji wa asilimia 3.6 mwaka 2022. Hii
    inatokana na uwepo wa vita kati ya nchi ya Urusi na Ukraine ambayo
    imesababisha kuongezeka kwa bei za vyakula na nishati hivyo,
    6
    kudhoofisha zaidi matarajio ya kurejea kwa shughuli za kiuchumi
    zilizokuwa zimeathiriwa na UVIKO-19. Ikumbukwe kuwa Urusi ni nchi
    ya pili kwa hifadhi/uzalishaji wa bidhaa za petroli duniani ambapo
    inachangia wastani wa asilimia 12 katika mafuta yote yanayozalishwa
    dunia ikitanguliwa na Marekani yenye mchango wa asilimia 20.
    Aidha, Urusi ndiyo mzalishaji mkubwa wa nishati ya gesi na mafuta
    inayotumika katika shughuli za kiuchumi barani Ulaya. Vilevile, kufikia
    mwaka 2023 na kuendelea uchumi wa dunia unatarajiwa kupungua
    zaidi na kufikia ukuaji wa wastani wa asilimia 3.3 kwa kipindi cha
    muda wa kati iwapo vita kati ya Urusi na Ukraine vitaendelea pamoja
    na kuendelea kuzidisha vikwazo vya kiuchumi kwa nchi ya Urusi.
    Uchumi wa Afrika na Kikanda
  13. Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, nchi za Kusini mwa
    Jangwa la Sahara zilikuwa na ukuaji wa uchumi wa wastani wa
    asilimia 4.5, ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 1.7 mwaka
  14. Hii ilitokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa
    ili kuimarisha ukuaji wa uchumi ikiwemo kuboresha huduma za afya
    pamoja na kuimarika kwa bei za bidhaa zinazouzwa nje ya ukanda
    huo baada ya kuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa ili kudhibiti
    kuenea kwa ugonjwa wa UVIKO-19. Ukuaji wa uchumi katika ukanda
    wa Kusini mwa Jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua na kufikia
    wastani wa asilimia 3.8 mwaka 2022 na utaongezeka kufika wastani
    wa asilimia 4.0 mwaka 2023.
  15. Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, ukuaji wa Pato la nchi za
    Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ulikuwa asilimia 4.2
    ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 4.3 mwaka 2020. Aidha,
    ukuaji wa Pato la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ulikuwa asilimia
    5.9 mwaka 2021 ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 1.1 mwaka
  16. Ukuaji chanya wa uchumi katika nchi wanachama wa jumuiya
    hizo ulitokana na kulegezwa kwa masharti yaliyowekwa kwa ajili ya
    7
    kudhibiti maambukizi ya UVIKO–19 pamoja na hatua mbalimbali za
    sera na kibajeti zilizochukuliwa kwa ajili ya kuchochea shughuli za
    kiuchumi katika sekta zilizoathirika na ugonjwa huo.
    Uchumi wa Taifa
    Pato la Taifa
  17. Mheshimiwa Spika, Ukuaji wa uchumi wa Taifa kwa kipindi
    cha mwaka, 2021 ulikuwa asilimia 4.9 ikilinganishwa na ukuaji wa
    asilimia 4.8 mwaka 2020. Kuongezeka kwa kiwango cha ukuaji wa
    uchumi kumetokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea
    kuchukuliwa na Serikali ikiwemo utekelezaji wa Mpango wa
    Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO–19
    na uwekezaji wa kimkakati hususan katika miundombinu ya nishati,
    maji, afya, elimu, ujenzi wa barabara, reli na viwanja vya ndege.
    Shughuli za kiuchumi zilizokuwa na ukuaji mkubwa katika kipindi cha
    mwaka 2021 ni pamoja na Sanaa na Burudani (asilimia 19.4),
    Umeme (asilimia 10.0), Uchimbaji Madini na Mawe (asilimia 9.6) na
    Habari na Mawasiliano (asilimia 9.1).
  18. Mheshimiwa Spika, Pato Ghafi la Taifa lilikuwa shilingi trilioni
    161.5 mwaka 2021, ikilinganishwa na shilingi trilioni 151.2 mwaka
  19. Aidha, mwaka 2021, Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa na watu
    milioni 57.7, ikilinganishwa na watu milioni 55.9 mwaka 2020. Kwa
    mantiki hii, Wastani wa Pato kwa Mtu lilikadiriwa kufikia shilingi
    2,798,224.23, sawa na dola za Marekani 1,211.77 mwaka 2021
    ikilinganishwa na shilingi 2,701,039.25, sawa na dola za Marekani
    1,171.51 mwaka 2020.
    Mwenendo wa Bei
  20. Mheshimiwa Spika, Mfumuko wa Bei umeendelea kuwa
    ndani ya lengo la wigo wa asilimia 3 hadi 5. Mwaka 2021, mfumuko
    8
    wa bei uliongezeka na kufikia wastani wa asilimia 3.7 kwa mwaka
    ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.3 katika kipindi cha mwaka
  21. Aidha, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 3.8 Aprili
    2022 ikilinganishwa na asilimia 3.3 Aprili 2021. Kuongezeka kwa
    mfumuko wa bei kulichangiwa na sababu zilizo nje ya udhibiti wa
    Serikali zikiwemo kuvurugika kwa mnyororo wa uzalishaji na
    usambazaji wa bidhaa na huduma katika soko la dunia kutokana na
    athari za vita baina ya Urusi na Ukraine.
    Utekelezaji wa Sera ya Fedha 2021/22
  22. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, malengo ya sera
    ya fedha yalikuwa ni kama ifuatavyo:
    (i) Ukuaji wa fedha taslimu (M0) wa wastani wa asilimia 9.9;
    (ii) Ukuaji wa ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) wa
    asilimia 10.0;
    (iii) Ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi wa wastani wa asilimia
    10.6; na
    (iv) Kuwa na akiba ya fedha za kigeni inayotosha kuagiza bidhaa na
    huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi kisichopungua miezi
    minne.
  23. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania
    imeendelea kutekeleza sera ya fedha yenye lengo la kuongeza
    ukwasi katika uchumi, ili kuchochea ukuaji wa mikopo kwa sekta
    binafsi na kusaidia kuimarisha shughuli mbalimbali za kiuchumi
    zilizokuwa zimeathiriwa na janga la UVIKO-19, hali iliyosaidiwa na
    mfumuko mdogo wa bei ulioendelea kubaki ndani ya lengo la asilimia
    3 hadi 5. Ili kufanikisha jukumu hili, Benki Kuu ya Tanzania imekuwa
    ikitumia nyenzo mbalimbali za sera ya fedha kwa ajili ya kuongeza
    ukwasi katika sekta ya benki, ikiwemo kutoa mikopo ya muda mfupi
    kwa mabenki, kununua fedha za kigeni kwenye soko la jumla, na
    9
    kuingia mikataba ya kubadilishana fedha za kigeni na mabenki
    (foreign exchange swap). Vilevile, Benki Kuu ilichukua hatua za ziada
    za kisera kwa ajili ya kuchochea ongezeko la mikopo nafuu kwa sekta
    binafsi, hususan shughuli za kilimo. Aidha, kufuatia athari za vita vya
    Ukraine ambayo imeongeza changamoto ya kuvurugika kwa
    minyororo ya ugavi na kusababisha kuongezeka kwa bei ya mafuta
    katika soko la dunia, pamoja na bei ya vyakula kama ngano na
    mafuta ya kula, imesababisha kuongeza kwa mfumuko wa bei ya
    bidhaa hizo nchini na kuhatarisha kupanda zaidi kwa mfumuko wa
    bei. Hali hii imeilazimu Benki Kuu kuanza kupunguza kiasi cha ukwasi
    inachoongeza kwenye uchumi ili kuanza kudhibiti hatari ya kuanza
    kuongezeka kwa kasi ya mfumuko wa bei nchini.
    Ujazi wa Fedha na Karadha
  24. Mheshimiwa Spika, sambamba na utekelezaji wa sera ya
    fedha inayolenga kuongeza ukwasi, ujazi wa fedha umeendelea
    kukua kwa kasi ya kuridhisha. Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili
    2022, wastani wa fedha taslimu uliongezeka kwa asilimia 13.8
    ikilinganishwa na asilimia 2.7 katika kipindi kama hicho mwaka
    uliotangulia, na lengo la wastani wa asilimia 9.9 kwa mwaka
    2021/22. Vilevile, ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) ulikua
    kwa wastani wa asilimia 13.1, ikilinganishwa ukuaji wa asilimia 6.8 na
    lengo asilimia 10. Ongezeko hili la ukwasi kwenye uchumi limesaidia
    shughuli mbalimbali za uchumi zilizokuwa zimeathirika na UVIKO-19
    kuanza kufunguka kwa ujumla na kuongeza mchango kwenye Pato la
    Taifa.
    Mwenendo wa Mikopo kwa Sekta Binafsi
  25. Mheshimiwa Spika, mikopo kwa sekta binafsi imeendelea
    kukua kwa kasi ya kuridhisha kutokana na sera wezeshi za fedha na
    bajeti, pamoja na hatua zinazoendelea kutekelezwa na serikali
    10
    kuboresha mazingira ya biashara, na utekelezaji wa hatua za kisera
    zilizochukuliwa na Serikali kupitia Benki Kuu zenye lengo la
    kuchochea ukuaji wa mikopo na kushusha viwango vya riba za
    mikopo. Mikopo kwa sekta binafsi ilikua kwa wastani wa asilimia 8.4
    katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022 ikilinganishwa na ukuaji
    wa wastani wa asilimia 4.3 katika kipindi kama hicho mwaka
    2020/21, na lengo la ukuaji wa asilimia 10.6 kwa mwaka 2021/22.
    Miezi ya hivi karibuni kasi ya ukuaji wa mikopo imeongezeka na
    kufikia asilimia 13.4 kwa mwaka ulioishia Aprili 2022. Sehemu kubwa
    ya mikopo ilielekezwa katika shughuli binafsi ambazo zilipata asilimia
    39.3 ya mikopo yote, ikifuatiwa na shughuli za biashara asilimia 16.7,
    uzalishaji viwandani asilimia 10.1 na kilimo asilimia 7.9. Ni matarajio
    ya serikali kuwa lengo la wastani wa asilimia 10.6 kwa mwaka
    2021/22 litafikiwa kufuatia hatua za kisera na maboresho ya
    mazingira ya biashara yanayoendelea kutekelezwa nchini.
    Mwenendo wa viwango vya riba
  26. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa sera ya fedha
    yamesaidia kudumisha kiwango cha kutosha cha ukwasi katika sekta
    ya benki, na kupelekea utulivu wa riba za masoko ya fedha ya muda
    mfupi katika viwango vya chini. Mathalani, riba ya siku moja katika
    soko la fedha baina ya mabenki (overnight interbank cash market
    interest rate) ilipungua hadi kufikia wastani wa asilimia 3.42 katika
    kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, kutoka wastani wa asilimia
    3.60 katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21. Vilevile, riba ya
    dhamana za muda mfupi (Overall Treasury bills rate) ilipungua hadi
    wastani wa asilimia 4.17 kutoka wastani wa asilimia 4.62 katika
    kipindi kama hicho mwaka 2021.
  27. Mheshimiwa Spika, wastani wa riba za mikopo ya benki kwa
    sekta binafsi kwa ujumla ulipungua japo kwa kasi ndogo hadi
    asilimia 16.44 katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022,
    11
    ikilinganishwa na wastani wa asilimia 16.59 katika kipindi kama hicho
    mwaka 2020/21. Aidha, wastani wa riba za amana kwa ujumla
    ulikuwa asilimia 6.85 katika, ikilinganishwa na wastani wa asilimia
    6.70. Ni matarajio yetu kuwa hatua za kisera zinazoendelea
    kuchukuliwa na Serikali kupitia Benki Kuu zitasaidia kuendelea
    kupungua kwa riba za mikopo nchini na kusaidia kukuza uchumi wa
    nchi na mazingira bora zaidi ya kufanya biashara.
    Sekta ya Nje
  28. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka kinachoishia
    Aprili 2022, thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ilifikia dola
    za Marekani bilioni 10.62 kutoka dola za Marekani bilioni 8.56 katika
    kipindi kama hicho mwaka 2021. Ongezeko hili kubwa lilitokana na
    kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa zisizo asilia pamoja na mapato
    yatokanayo na shuguli za utalii ikiwa ni matokeo ya hatua
    zilizochukuliwa na mataifa mengine duniani kufungua mipaka yao
    kuruhusu safari za kimataifa kutokana na kupungua kwa maambukizi
    ya UVIKO-19. Aidha, katika kipindi hicho, thamani ya bidhaa na
    huduma zilizoagizwa kutoka nje ilifikia dola za Marekani bilioni 13.29,
    ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni 9.27 katika kipindi kama
    hicho mwaka 2021. Ongezeko hilo linatokana na kuongezeka kwa
    uagizaji wa bidhaa za walaji hususan petroli na dawa ambapo
    thamani ya petroli iliongezeka kwa kiwango kikubwa kutokana na
    ongezeko la bei katika Soko la Dunia pamoja na kiwango
    kilichoagizwa katika kipindi hicho.
  29. Mheshimiwa Spika, Thamani ya mauzo ya bidhaa iliongezeka
    kufikia dola za Marekani bilioni 7.03 katika kipindi cha mwaka
    kinachoishia Aprili 2022 ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni
    6.36 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Ongezeko hilo lilitokana
    na kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa asilia na zisizo asilia ikiwemo,
    bidhaa za maua na mbogamboga, saruji, bidhaa za plastiki, vipodozi
    12
    pamoja na nafaka hususan mchele na mahindi. Aidha, thamani ya
    bidhaa zilizoagizwa kutoka nje ziliongezeka kutoka dola za Marekani
    bilioni 8.06 katika kipindi cha mwaka unaoishia Aprili 2021 hadi dola
    za Marekani bilioni 11.09 Aprili 2022. Hali hiyo ilitokana na
    kuongezeka kwa uagizaji wa malighafi, bidhaa za viwandani,
    mitambo na bidhaa za petroli.
  30. Mheshimiwa Spika, mapato yatokanayo na huduma
    yaliongezeka na kufikia dola za Marekani bilioni 3.59 kwa mwaka
    unaoishia Aprili 2022, ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni 2.20
    katika kipindi kama hicho mwaka 2021, ongezeko hili lilichangiwa na
    idadi kubwa ya watalii waliongia nchini katika kipindi husika. Aidha,
    katika kipindi husika malipo ya huduma yaliongezeka kutoka dola za
    Marekani bilioni 1.22 na kufikia dola za Marekani bilioni 2.20.
    Ongezeko hili lilichangiwa na ongezeko la gharama za mizigo
    sambamba na ongezeko la gharama za uagizaji wa mafuta.
    Akiba ya Fedha za Kigeni
  31. Mheshimiwa Spika, akiba ya fedha za kigeni imeendelea
    kuwa ya kuridhisha kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na
    huduma kutoka nje ya nchi. Hadi kufikia Aprili 2022, akiba ya fedha
    za kigeni ilikuwa dola za Marekani bilioni 5.46 ambayo inatosheleza
    uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi cha
    takriban miezi 4.8. Mahitaji ya nchi kisheria ni kuwa na kiasi cha
    fedha za kigeni kinachotosheleza uagizaji wa bidhaa na huduma
    kutoka nje ya nchi kwa muda usiopungua miezi 4.0. Aidha, kiwango
    kilichopo kinakidhi pia lengo la kuwa na miezi isiyopungua 4.5 kwa
    nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
    Mwenendo wa Thamani ya Shilingi
  32. Mheshimiwa Spika, thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya
    13
    dola ya Marekani imeendelea kuwa tulivu, ambapo dola moja ya
    Marekani ilibadilishwa kwa wastani wa shilingi 2,308.87 katika soko la
    jumla kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, ikilinganishwa na
    wastani wa shilingi 2,309.48 katika kipindi cha Julai 2020 hadi Aprili
  33. Hii ni sawa na kuongezeka kwa thamani ya shilingi
    (appreciation) kwa wastani wa asilimia 0.03. Hali hii imechangiwa
    kwa kiasi kikubwa na kuwepo kwa akiba ya kutosha ya fedha za
    kigeni, utulivu wa mfumuko wa bei nchini, mwendelezo wa nakisi
    ndogo katika urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamishaji
    mali nchi za nje, pamoja na utekelezaji wa sera thabiti za fedha na
    bajeti.
    Mwenendo wa sekta ya kibenki
  34. Mheshimiwa Spika, sekta ya kibenki nchini imeendelea
    kubaki imara, stahimilivu na yenye kutengeneza faida ikiwa na mtaji
    na ukwasi wa kutosha. Hadi kufikia mwezi Aprili 2022, rasilimali za
    benki zilifikia kiasi cha Shilingi bilioni 40,198.2, sawa na ongezeko la
    asilimia 12.9 ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka jana. Aidha,
    amana za benki ziliongezeka hadi kufikia kiasi cha Shilingi bilioni
    28,603.3, sawa na ongezeko la asilimia 11.8, ikilinganishwa na kipindi
    kama hiki mwaka 2020/21. Vilevile, hali ya mitaji ya mabenki na
    ukwasi vimeendelea kuimarika hadi kufikia faida ya mtaji ya asilimia
    18.4 Aprili 2022, ikilinganishwa na faida ya asilimia 10.3 kipindi kama
    hiki mwaka 2020/21.
  35. Mheshimiwa Spika, benki zimeendelea kuongeza utoaji wa
    huduma za kibenki kwa wananchi wengi zaidi kwa kutumia mifumo
    ya kielektroniki yenye gharama nafuu. Kwa upande mwingine, Benki
    Kuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa benki na taasisi za fedha
    nchini kwa kutekeleza sera wezeshi na kutoa kanuni na miongozo
    mbalimbali ili kulinda uimara wa sekta hiyo. Vilevile, benki
    zimeelekezwa kutekeleza mipango ya kuongeza mitaji juu ya kiwango
    14
    kinachotakiwa kisheria, ili kuongeza uwezo kwenye utoaji wa mikopo
    kwa sekta binafsi na huduma nyingine za benki.
  36. Mheshimiwa Spika, sekta ya benki inatarajiwa kubaki salama
    na tulivu, sambamba na sera zinazotekelezwa na hatua
    zinazochukuliwa na Serikali pamoja na Benki Kuu ya Tanzania katika
    kuboresha mazingira ya biashara na ufanisi katika utoaji wa huduma
    za fedha nchini. Aidha, Benki Kuu imeendelea kuimarisha jitihada za
    kupunguza kiwango cha mikopo chechefu ambapo, hadi kufikia
    mwezi Aprili 2022 kiwango cha mikopo chechefu kilipungua kufikia
    asilimia 8.23 ikilinganishwa na asilimia 9.77 mwezi Aprili 2021. Benki
    Kuu ya Tanzania inaendelea kufuatilia kwa karibu mikakati ya
    mabenki katika kupunguza mikopo chechefu hadi kufikia kiwango
    kisichozidi asilimia 5.
    Deni la Serikali
  37. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, deni la Serikali lilikuwa
    shilingi trilioni 69.44 ikilinganishwa na shilingi trilioni 60.72 kipindi
    kama hicho mwaka 2021, sawa na ongezeko la asilimia 14.4. Kati ya
    kiasi hicho, deni la nje lilikuwa shilingi trilioni 47.07 na deni la ndani
    lilikuwa shilingi trilioni 22.37. Ongezeko la deni la Serikali lilitokana na
    kupokelewa kwa mikopo mipya kutoka vyanzo vyenye masharti nafuu
    na ya kibiashara kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo. Aidha,
    ongezeko la deni lilitokana na kutolewa kwa hatifungani maalumu
    yenye thamani ya shilingi trilioni 2.18 kwa ajili ya deni la Mfuko wa
    Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) lililotokana na
    michango ya watumishi wa kabla ya mwaka 1999. Taarifa ya tathmini
    ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Novemba 2021 inaonesha kuwa deni
    la Serikali bado ni himilivu katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na
    mrefu kwa kuzingatia ukomo wa viashiria vyote vinavyokubalika
    kimataifa.
    15
    MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO
    WA TAIFA WA MWAKA 2021/22
  38. Mheshimiwa Spika, kama unavyofahamu Serikali imekuwa
    ikitekeleza Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22
    ambao ni Mpango wa Kwanza katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu
    wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 wenye
    dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya
    Watu. Kutokana na usimamizi thabiti wa Serikali chini ya Mheshimiwa
    Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
    utekelezaji wa Mpango umekuwa na mafanikio makubwa katika
    nyanja zote ikiwemo kiuchumi, miundombinu, kijamii na uwekezaji.
    Mafanikio yaliyopatikana katika sekta mbalimbali ni pamoja na:
    (i) Miundombinu ya Reli: Kuendelea na ujenzi wa Reli ya Kati
    ya Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway – SGR)
    ambapo kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro (km 300)
    utekelezaji umefikia asilimia 96.54 na kipande cha Morogoro –
    Makutupora (km 422) asilimia 85.02; kusainiwa kwa mkataba
    wa ujenzi wa kipande cha Makutupora – Tabora (km 368);
    kuendelea na ununuzi wa mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa njia
    ya reli kwa kipande cha Tabora – Isaka (km 165); kuendelea na
    ununuzi wa injini, mabehewa na vifaa vya matengenezo ya njia
    ya reli; na kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali
    kwa ajili ya ujenzi wa njia za reli za Tabora – Kigoma (km 411),
    Uvinza – Musongati – Gitega (km 282) na Kaliua – Mpanda –
    Karema (km 321) kwa kiwango cha Standard Gauge. Mafanikio
    mengine ni: Kukamilika kwa ukarabati wa njia ya reli ya Tanga
    – Moshi – Arusha (km 470); kukamilika kwa ukarabati wa
    mabehewa ya mizigo 200 yanayotumika kutoa huduma ya
    usafiri kwa njia ya reli ya Meter Gauge iliyopo; kukamilika kwa
    uundaji wa vichwa vya injini saba (7) vya sogeza; na
    kupokelewa kwa vichwa vya treni vitatu (3), mabehewa 44 ya
    16
    mizigo na mtambo wa kupima ubora wa njia ya reli.
    (ii) Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere – MW
    2,115: Kuendelea na ujenzi wa tuta kuu la bwawa ambapo
    utekelezaji umefikia asilimia 62.01, njia za kupitisha maji ya
    kufua umeme asilimia 74.16, nyumba ya mitambo ya kufua
    umeme asilimia 44.22, kingo za bwawa asilimia 42.82 na kituo
    cha kupokea na kusafirisha umeme kV 400 asilimia 75.44. Kwa
    ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 60.22.
    (iii) Uboreshaji wa Shirika la Ndege Tanzania: Kupokelewa
    kwa ndege tatu (3) ambapo ndege moja (1) ni aina ya Dash 8
    Q400 na mbili (2) ni aina ya Airbus A220 300; kufanyika kwa
    malipo ya awali ya ununuzi wa ndege tano (5) mpya ambapo
    ndege moja (1) aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili
    (2) aina ya Boeing 737-9, ndege moja (1) aina ya De Havilland
    Dash 8-Q400 na ndege moja (1) ya mizigo aina ya Boeing 767-
    300F; kuendelea na ukarabati wa karakana ya matengenezo ya
    ndege ya KIMAFA katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa
    Kilimanjaro (KIA); kuanzisha safari katika vituo vitatu (3) vipya
    vya nje ya nchi vya Lubumbashi, Nairobi na Ndola; kurejesha
    safari za ndani na nje kwa abiria; kuanzisha safari za mizigo za
    kwenda Guangzhou; na kutolewa kwa mafunzo kwa marubani
    102 na wahudumu 108 wa ndani ya ndege.
    (iv) Miradi ya Umeme: kuendelea na ujenzi wa mradi wa kufua
    umeme wa Rusumo – MW 80 ambapo utekelezaji umefikia
    asilimia 91.6; kuendelea na utekelezaji wa mradi wa Kinyerezi I
    Extension MW 185 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 88;
    kukamilika kwa ujenzi wa vituo vya kupooza umeme vya
    Singida na Dodoma katika mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
    wa Msongo wa kV 400 Iringa – Singida – Shinyanga (Backbone
    Transmission Investment Project – BTIP II); kuendelea na
    17
    ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa kV 400 Singida –
    Arusha – Namanga ambapo utekelezaji umefikia asilimia 96.1;
    kuendelea na ujenzi wa njia ya usafirishaji wa umeme wa kV
    400 kutoka Rufiji – Chalinze – Kinyerezi – Dodoma ambapo
    utekelezaji umefikia asilimia 37; kuendelea na ujenzi wa mradi
    wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa kV 220 (Rusumo
    – Nyakanazi) ambapo ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
    umefikia asilimia 61 na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha
    Nyakanazi umefikia asilimia 95; na kuunganishwa umeme kwa
    jumla ya vijiji 8,688 kati ya vijiji 12,345 sawa na asilimia 70.4
    ya vijiji vyote Tanzania Bara.
    (v) Ujenzi na Ukarabati wa Viwanja vya Ndege: kusainiwa
    kwa mkataba kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha
    Kimataifa cha Msalato awamu ya kwanza itakayohusisha ujenzi
    wa njia ya kuruka na kutua ndege pamoja na jengo la abiria;
    kukamilika kwa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Geita;
    kukamilika kwa upanuzi wa njia ya kutua na kuruka ndege na
    kufungwa kwa mfumo wa kuongoza ndege katika Kiwanja cha
    Ndege cha Dodoma; kukamilika kwa usanifu na kuendelea na
    maandalizi ya ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha
    Ndege cha Mwanza; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa
    viwanja vya ndege vya Songea (asilimia 96), Mtwara (asilimia
    89), Iringa (asilimia 44.65), Songwe (asilimia 95) na Musoma
    (asilimia 10); kuendelea na maandalizi ya ujenzi na upanuzi wa
    viwanja vya ndege vya Shinyanga, Kigoma, Tabora na
    Sumbawanga vitakavyogharimu Euro milioni 50 sawa na shilingi
    bilioni 136.85.
    (vi) Uendelezaji wa Bandari: Bandari ya Dar es Salaam:
    Kuboreshwa kwa gati namba 1 – 7; na kukamilika kwa ujenzi
    wa gati maalumu la kuhudumia meli za magari (RoRo) na yadi
    ya kuhudumia makasha. Bandari ya Mtwara: kukamilika kwa
    18
    ujenzi wa gati moja lenye urefu wa mita 300; na kuendelea na
    ujenzi wa uzio na sakafu ngumu katika eneo la mita za mraba
    75,807. Bandari ya Tanga: kukamilika kwa uongezaji wa kina
    kwenye lango la kuingia meli kutoka mita nne (4) hadi mita 13
    pamoja na kuweka vifaa vya kuongoza meli.
    Bandari za Maziwa Makuu: Ziwa Victoria: Kukamilika kwa
    ujenzi wa magati ya Nyamirembe, Magarine, Lushamba, Ntama
    na Mwigobero pamoja na gati mbili (2) za majahazi katika
    bandari ya Mwigobero. Ziwa Tanganyika: kukamilika kwa
    ujenzi wa magati ya Kagunga, Sibwesa na Kabwe (Nkasi);
    kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya Lagosa pamoja na
    upanuzi wa bandari ya Kasanga; na kuendelea na ujenzi wa
    Bandari za Karema, Kibirizi, Kigoma na Ujiji. Ziwa Nyasa:
    kukamilika kwa ujenzi wa sakafu ngumu katika bandari ya
    Kiwira na Itungi; na kukamilika kwa ujenzi wa gati na
    miundombinu yake katika bandari ya Ndumbi.
    (vii) Kuboresha Huduma za Usafiri na Usafirishaji wa Abiria
    na Mizigo katika Maziwa Makuu
    Kukamilika kwa ukarabati wa meli mbili (2) za New Butiama
    Hapa Kazi Tu na New Victoria Hapa Kazi Tu; kuendelea na
    ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza Hapa kazi Tu yenye uwezo
    wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo ambao umefikia
    asilimia 66; na kukamilika kwa ujenzi wa chelezo cha kujengea
    na kukarabati meli katika Bandari ya Mwanza chenye uwezo wa
    kubeba meli au chombo chenye uzito kuanzia tani moja (1)
    hadi tani 4,000.
    (viii) Barabara na Madaraja Makubwa: Kujengwa kwa mtandao
    wa barabara kwa kiwango cha lami wenye urefu wa kilomita
    216.26; na kukarabatiwa kwa kiwango cha changarawe jumla
    ya kilomita 1,124.3 za barabara za mikoa. Kwa upande wa
    19
    barabara zinazosimamiwa na TARURA, jumla ya kilometa
    232.94 za lami, kilomita 8,181.65 za changarawe, madaraja
    405 na makalvati 206 yamejengwa. Miradi iliyokamilika ni
    pamoja na: ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami sehemu
    za Tabora – Nyahua (km 85), Nyahua – Chaya (km 85.4) na
    Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35); barabara za Mbeya –
    Lwanjilo (km 36) na Lwanjilo – Chunya (km 36), sehemu ya
    Chunya – Makongolosi (km 39); na barabara za Mtwara –
    Mnivata (km 50). Barabara zinazoendelea ni pamoja na ujenzi
    sehemu ya Lusitu – Mawengi (km 50) ambapo utekelezaji
    umefikia asilimia 83.79, Kidatu – Ifakara (km 68) asilimia 54.5,
    Makutano – Sanzate (km 50) asilimia 94.1, Mto wa Mbu –
    Loliondo sehemu ya Waso – Sale Jct (km 50) asilimia 98, na
    Moronga – Makete (km 53.5) umefikia asilimia 86. Aidha,
    Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya mzunguko katika jiji la
    Dodoma (Dodoma outer ring road) yenye urefu wa kilometa
    (112.3) na kuendelea na maandalizi ya upanuzi wa barabara
    kutoka Dodoma kwenda Singida (km 50), Dodoma – Iringa (km
    50), Dodoma – Arusha (km 50) na Dodoma – Morogoro (km
    70).
    Kwa upande wa madaraja hatua zilizofikiwa ni: kuzinduliwa na
    kuanza kutumika kwa daraja la Tanzanite Dar es Salaam;
    kuanza kutumika kwa daraja la Kiyegeya (Morogoro); na
    kuendelea na ujenzi wa madaraja ya Kitengule (Kagera)
    ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90; Wami (Pwani) asilimia
    72.88; Msingi (Singida) asilimia 82; Lower Malagarasi asilimia
    65; na ujenzi wa daraja la Kigongo – Busisi umefikia asilimia
    40.2.
    (ix) Huduma za Afya: Kuendelea na ujenzi wa Hospitali za
    Halmashauri 127, ujenzi wa vituo vya afya 70, ukamilishaji wa
    maboma ya zahanati 564; kukamilika kwa ukarabati wa wodi
    20
    namba 18 katika jengo la Sewa Haji katika haspitali ya Taifa
    Muhimbili kwa ajili ya wodi za kulaza wagonjwa binafsi;
    kukamilika kwa ujenzi na ufungaji wa mtambo wa kuzalisha
    tiba hewa (Oxygen generating plant) katika hospitali ya Taifa
    Muhimbili – Mloganzila; kukamilika kwa ujenzi wa maabara
    maalumu na ufungaji wa mtambo wa kisasa (Angio-Suite)
    katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili – MOI; kukamilika kwa wodi
    ya watoto katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete; ukarabati
    wa jengo la wagonjwa mahututi (asilimia 70), chumba cha
    kufunga mashine ya MRI (asilimia 80) na kujengwa kwa kituo
    cha habari kwa magonjwa ya saratani (Patient Information
    Centre) katika Taasisi ya Saratani Ocean Road; ukarabati wa
    jengo la wagonjwa mahututi katika hospitali ya rufaa ya
    magonjwa ya kifua kikuu Kibong’oto; ukarabati wa chumba cha
    X-ray na Utra-sound katika hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili
    Mirembe; kujengwa kwa majengo ya kutolea huduma za afya
    ya Mama na Mtoto (Maternal and Newborn Wing) katika
    hospitali ya Rufaa Kanda ya Mashariki CCBRT; kuendelea na
    ujenzi wa wodi za wagonjwa wa saratani (asilimia 57) na kliniki
    ya wagonjwa wa macho (asilimia 65) katika hospitali ya rufaa
    kanda ya ziwa Bugando; kuendelea na ujenzi wa vyumba nane
    (8) vya upasuaji (asilimia 80) katika hospitali ya kanda ya
    kaskazini (KCMC); kuendelea na ujenzi wa jengo la ghorofa sita
    (6) la afya ya uzazi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 93
    katika hospitali ya rufaa Mbeya; kuendelea na ujenzi wa jengo
    la kuhudumia wagonjwa wa UVIKO – 19 (asilimia 95) katika
    hospitali ya rufaa Shinyanga; kununuliwa na kusambazwa kwa
    chanjo za polio, surua, rubella, kifaduro, pepopunda, homa ya
    ini, homa ya uti wa mgongo na kichomi na chanjo dhidi ya
    UVIKO – 19.
    (x) Elimu: Kuendelea kutekeleza Sera ya elimumsingi bila ada ili
    kuongeza fursa za elimu nchini ambapo hadi Aprili 2022,
    21
    Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 244.5; kuchapishwa na
    kusambazwa kwa vitabu vya kiada 15,609,515 na kiongozi cha
    mwalimu 538,006 kwa masomo yote ya Darasa la VI na VII ili
    kuimarisha uwiano kati ya mwanafunzi na kitabu; kuendelea na
    ujenzi wa shule mpya 232 za Sekondari za kata katika kata
    zisizokuwa na shule za Sekondari; ujenzi wa shule 10 kati ya
    lengo la shule 26 maalumu za bweni za wasichana kwa
    masomo ya Sayansi; kutolewa kwa mafunzo kazini kwa walimu
    10,000 wa sekondari wa masomo ya hisabati na sayansi;
    kuwezesha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuchapisha na
    kusambaza miongozo ya masomo tisa (9); kukusanywa kwa
    mikopo ya shilingi bilioni 156.81 kutoka kwa wanufaika wa
    mikopo iliyoiva na kugharamia mikopo yenye thamani ya
    shilingi bilioni 569.0 kwa wanafunzi 177,777; na kuimarishwa
    kwa Tume ya Nguvu za Atomiki kwa kuendelea na ujenzi wa
    awamu ya pili wa maabara changamano.
    (xi) Maji Mijini na Vijijini: Upatikanaji wa huduma ya maji hadi
    Aprili 2022 umefikia wastani wa asilimia 74.5 vijijini kutoka
    asilimia 72.3 Juni, 2021 na mijini asilimia 86.5 kutoka asilimia
    86 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Baadhi ya miradi
    iliyotekelezwa na hatua zilizofikiwa ni: kuendelea kwa ujenzi wa
    mradi wa maji katika mji wa Kigoma (asilimia 95), Arusha
    (asilimia 80) na mradi wa Mugango – Kiabakari – Butiama
    (asilimia 42). Aidha, katika eneo linalohudumiwa na DAWASA
    (mikoa ya Dar es Salaam na Pwani) utekelezaji wa miradi
    umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95. Vile vile, Serikali imeanza
    hatua za kutafuta suluhu ya kudumu ya tatizo la maji katika
    majiji ya Dodoma na Dar es Salaam kwa kutekeleza miradi ya
    Bwawa la Kidunda, bwawa la Farkwa na mradi mkubwa wa
    maji kutoka ziwa Victoria hadi Dodoma.
    (xii) Kilimo, Mifugo na Uvuvi
    22
    Kilimo: Kuzalishwa kwa mbegu bora tani 35,199.39 na miche
    32,301,995 ya mazao mbalimbali; kutolewa kwa pikipiki 7,000
    kwa Maafisa ugani kwa ajili ya kuimarisha huduma za ugani;
    kupatikana kwa mbolea tani 436,452; kuanzishwa kwa
    mashamba 67 yenye ukubwa wa hekta 205,432.45 ambayo kila
    moja lina ukubwa wa kuanzia hekta 20; kuhakikiwa na
    kutambuliwa kwa mashamba matano (5) ya NAFCO yenye
    ukubwa wa ekari 18,980; kukamilika kwa upembuzi yakinifu na
    usanifu wa kina katika skimu tatu (3) za umwagiliaji za
    Mkombozi (Iringa), Idudumo (Nzega) na Ilemba
    (Sumbawanga); kutolewa kwa mafunzo kwa maafisa ugani
    2,486 kuhusu kilimo bora cha alizeti na pamba katika mikoa ya
    Dodoma, Singida, Simiyu, Kilimanjaro, Kigoma na Manyara;
    kukamilika kwa ukarabati wa ghala lenye uwezo wa kuhifadhi
    tani 1,000 za mazao katika Wilaya ya Kiteto; kukamilika kwa
    ukarabati wa vihenge vyenye uwezo wa kuhifadhi tani 38,000
    katika Mkoa wa Arusha na ghala la Mbugani – Dodoma lenye
    uwezo wa kuhifadhi tani 30,000 za nafaka; kutolewa kwa vibali
    681 kwa wafanyabiashara wa viuatilifu; kuendelea na ujenzi wa
    kiwanda cha mbolea cha FOMI Mkoani Dodoma chenye uwezo
    wa kuzalisha tani 600,000 kwa mwaka; NFRA na CPB
    zilifanikiwa kununua mahindi ya wakulima ambapo kiasi cha
    shilingi bilioni 114 zilitumika; na kufanyika kwa majaribio 88 ya
    kisayansi (bioefficacy field trials) kwa viuatilifu vipya.
    Mifugo: Kuendelea na tafiti na tathmini za teknolojia bora za
    ng’ombe chotara wa maziwa na uzalishaji wa nyama;
    kukamilika kwa ujenzi wa majosho 95 katika mamlaka
    mbalimbali za Serikali za Mitaa; kuanza kwa ujenzi wa majosho
    73 katika halmashauri 58; kuzalishwa na kusambazwa kwa dozi
    43,409,600 za chanjo dhidi ya magonjwa ya Mdondo, Homa ya
    Mapafu ya Ng’ombe na Mbuzi, Kimeta, Chambavu,
    23
    Mchanganyiko wa Kimeta na Chambavu na Kutupa Mimba;
    kuzalishwa kwa jumla ya dozi 50,261 za mbegu za mifugo na
    kusambazwa kwa dozi 31,380 katika mikoa 19 kwa ajili ya
    uhimilishaji; kununuliwa na kusambazwa kwa jumla ya pikipiki
    300 ili kurahisisha utoaji wa huduma za ugani kwa Mamlaka za
    Serikali za Mitaa; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa
    miundombinu ya mifugo katika minada 18 nchini; kulimwa kwa
    hekta 800 za malisho ya mifugo katika ranchi za Kongwa, Ruvu
    na West Kilimanjaro; na kuzalishwa kwa jumla ya ndama 3,119
    katika Ranchi za Kikulula, Misenyi, Kongwa, Ruvu, Mkata, West
    kilimanjaro, Mzeri na Kalambo.
    Uvuvi: kusainiwa kwa Mkataba na Mkandarasi China Harbour
    Engineering Co. Ltd kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya uvuvi
    katika eneo la Kilwa Masoko, Lindi; kuendelea na maandalizi ya
    ununuzi wa meli mbili (2) za uvuvi kati ya nne (4)
    zilizopangwa; kukamilika kwa mpango biashara wa ufufuaji wa
    Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO); kujenga ofisi tano (5)
    katika Halmashauri tano (5) kwa ajili ya kuimarisha vikundi vya
    ulinzi shirikishi wa rasilimali za uvuvi; kufanyika kwa kaguzi
    1,863 za kuhakiki ubora na usalama wa samaki na mazao ya
    uvuvi kwenye viwanda vya kuchakata samaki, mialo, magari ya
    kusafirisha samaki, maghala ya kuhifadhi samaki na masoko ya
    samaki; kujenga na kuimarisha miundombinu ya mialo na
    masoko ikiwemo kukamilika kwa ujenzi wa baadhi ya mialo na
    kuendelea na ujenzi wa mialo pamoja na ujenzi wa soko la
    samaki la Mbamba Bay; kuvuliwa kwa tani 324,752.45 za
    samaki zenye thamani ya shilingi trilioni 2.18; kuuzwa nje kwa
    tani 34,841.72 za samaki na Samaki hai 169,089 wa mapambo
    wenye thamani ya shilingi bilioni 475.01; kujengwa kwa
    maabara ya utafiti wa uvuvi katika kituo cha TAFIRI – Dar es
    Salaam; na kufanyika kwa tafiti mbalimbali za mazao ya samaki
    ikiwemo tafiti kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na
    24
    ongezeko la tindikali baharini.
    (xiii) Uendelezaji wa Viwanda: Katika kutekeleza mkakati wa
    kuendeleza sekta ya viwanda kwa kuweka mazingira wezeshi,
    hatua iliyofikiwa ni pamoja na: kuendelea na majadiliano na
    wawekezaji watakaowekeza kwenye miradi ya msingi mitatu
    (3) katika eneo maalumu la uwekezaji Bagamoyo ambayo ni
    Bandari ya kisasa (Modern Seaport Component), sehemu ya
    kanda maalumu kwa ajili ya mizigo na usafirishaji (Logistics
    Park) na sehemu ya mji wa viwanda (Port side Industrial City);
    kukamilika kwa ujenzi wa mabwawa manne (4) ya kuvuna na
    kuhifadhi maji yenye uwezo wa kuhifadhi maji ya mita za ujazo
    1,750,000 na kuendelea na upanuzi wa mashamba ya miwa
    katika kiwanda cha Sukari Mbigiri ambapo utekelezaji wa mradi
    umefikia asilimia 75 kwa upande wa mashamba ya miwa na
    asilimia 45 kwa upande wa ujenzi wa kiwanda; kuendelea
    kuimarisha Sekta Ndogo za ngozi, nguo na mavazi, chuma na
    bidhaa za chuma, mbolea na kemikali za viwandani na
    uchakataji wa bidhaa zinazotokana na kilimo kama vile mafuta
    ya kula, korosho, matunda, maziwa na bidhaa za maziwa.
    Aidha, kupitia maonesho ya Dubai Expro Serikali ilifanikiwa
    kusaini mikataba 36 ya uwekezaji yenye thamani ya shilingi
    trilioni 17 pamoja na mikataba yenye thamani ya shilingi trilioni
    11.7 ilisainiwa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais ya uzinduzi
    wa filamu ya Royal Tour.
    (xiv) Madini: kukamilika kwa ujenzi wa vituo vitatu (3) vya umahiri
    katika shughuli za uchimbaji madini vya Chunya, Songea na
    Mpanda; kuanzishwa kwa masoko mapya manne (4) ya madini
    na vituo vipya nane (8) vya ununuzi wa madini, hivyo kufanya
    jumla ya masoko ya madini kuwa 42 na vituo vya ununuzi wa
    madini kufikia 75; na kusainiwa kwa mikataba ya ubia kwa ajili
    ya uwekezaji wa kiasi cha takribani dola za Marekani milioni
    25
    1,672.57 kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
    na kampuni za Madini za: Nyanzaga (NMCL) kwa ajili ya
    uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu na madini ambata ya
    shaba, chuma, nickel, zinc na lead kwenye eneo lenye ukubwa
    wa kilomita za mraba 23.36 Sengerema; Kampuni ya Jacana
    Resources Limited (Strandline Resources Limited) kwa ajili ya
    uchimbaji wa madini ya Heavy Mineral Sand (Beach Sands)
    Kigamboni kwenye eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba
    4.45; Kampuni ya Mahenge Resources Limited (Black Rock
    Mining Ltd) kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya graphite; na
    Kampuni ya Petra Diamond Ltd inayoendelea na uchimbaji wa
    madini ya Almasi katika mgodi wa Williamson Diamonds Limited
    eneo la Mwadui. Katika mikataba hiyo Serikali itamiliki asilimia
    16 ya hisa za kila kampuni.
    (xv) Habari, Mawasiliano na TEHAMA: kukamilika kwa ujenzi wa
    Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa kilomita 409 ambapo
    kilomita 72 zimeunganisha nchi ya Msumbiji kupitia mpaka wa
    Mtambaswala, kilomita 72 zimeunganisha watumiaji wa mwisho
    katika ofisi za Serikali za Msalato, Mtumba na Kikombo Dodoma
    na kilomita 265 zimeunganisha Manyoni – Kambi katoto
    (Chunya); kukamilika kwa ukarabati wa kilomita 105 za ujenzi
    wa mkongo Arusha – Namanga kupitia miundombinu ya
    TANESCO; kukamilika kwa uandaaji wa ramani za mipaka ya
    kiutawala katika Halmashauri 20; na kuendelea na uwekaji wa
    miundombinu ya anwani za makazi nchini.
    Aidha, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa kuongeza
    upanuzi na usikivu wa shirika la utangazaj TBC ambapo
    shughuli zilizotekelezwa ni pamoja na: Kukamilika kwa ujenzi
    wa jengo la kituo cha kurushia matangazo ya masafa ya FM
    katika kituo cha Kisaki mkoani Morogoro; kukamilika kwa ujenzi
    na ufungaji wa mitambo ya kituo cha Redio ya Jamii Makao
    26
    Makuu Jijini Dodoma; kuendelea na ujenzi na ufungaji wa
    mitambo ya masafa ya FM katika mikoa mipya ya Njombe,
    Songwe na Simiyu, sambamba na wilaya za Kilwa, Serengeti
    pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba ambapo utekelezaji
    umefikia asilimia 40; kununuliwa na kufungwa kwa mitambo
    miwili (2) ya kurushia matangazo kwa njia ya Satelaiti (FLY
    AWAY) pamoja na mtambo wa kurusha mubashara matangazo
    ya redio kwa njia ya mtandao (LIVE U); na kukamilisha ujenzi
    wa jengo la Studio na ununuzi wa vifaa vya Chaneli ya
    Televisheni ya TBC 2 katika ofisi za Mikocheni Dar es Salaam.
    (xvi) Maliasili na Utalii: Kuanzishwa kwa mara ya kwanza kwa
    Programu ya Royal Tour iliyoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya
    Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan
    ambayo imelitangaza Taifa na utalii katika Nyanja za kimataifa;
    kuongezeka kwa idadi ya watalii kutoka nje ya nchi kutoka
    watalii 620,867 mwaka 2020 hadi watalii 922,692 mwaka 2021,
    sawa na ongezeko la asilimia 48.6; Hifadhi ya Taifa Serengeti
    ilitangazwa na shirika la Mainland Aggregates Limited la nchini
    Marekani mwaka 2021 kuwa mshindi wa pili barani Afrika na
    wa 12 duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watumiaji wa
    mtandao wa kijamii wa instagram; kampuni 11 za uwekezaji
    zilipatiwa maeneo ya kujenga huduma ya malazi ya hoteli za
    hadhi ya kitalii katika Hifadhi za Taifa Nyerere, Mikumi,
    Serengeti na Arusha; na Tanzania kuwa mwenyeji katika
    Onesho la Kwanza la Kimataifa la Utalii la Jumuiya ya Afrika
    Mashariki (East African Regional Tourism Expo – EARTE 2021);
    (xvii) Kukuza Biashara na Uwekezaji: wateja 13,836 walipatiwa
    huduma katika kituo cha Huduma za Uwekezaji Mahala Pamoja
    (OSC) ambapo jumla ya miradi 206 (73 wageni, 69 Watanzania
    64 ubia kati ya wageni na Watanzania) ilisajiliwa yenye thamani
    ya dola za Marekani milioni 769.5 na inatarajiwa kutoa ajira
    27
    kwa watanzania wapatao 37,451; kushiriki katika mikutano tisa
    (9) ya ndani ikiwemo Maonesho ya Utalii ya Kanda ya Afrika
    Mashariki (EA Regional Tourism Expo), Dubai Expo 2020,
    Jukwaa la Viwanda lililofanyika Zanzibar na maonyesho ya
    viwanda vidogo (SIDO Trade Fair) yaliyofanyika Kigoma; na
    kutolewa kwa mikopo kwa kampuni 31 zinazozalisha na
    kuchakata bidhaa zitokanazo na mazao ya mifugo na kilimo
    kupitia Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kutumia
    Mpango wa SANVN (SIDO, AZANIA Bank, NEEC, VETA na
    NSSF).
    (xviii) Utawala Bora na Utawala wa Sheria: katika
    kuhakikisha kuwa utawala bora na utawala wa sheria
    unashamiri nchini, Serikali imeendelea kuimarisha Mifumo na
    Miundombinu ya Kitaasisi na utoaji haki, uwazi na uwajibikaji
    katika utumishi wa umma, shughuli za Mfuko wa Bunge pamoja
    na Mfuko wa Mahakama. Mafanikio yaliyopatikana ni:
    kulijengea Bunge uwezo kwa kutoa mafunzo ya muda mfupi
    kwa Waheshimiwa Wabunge na Watumishi katika maeneo ya
    usimamizi wa bajeti, masuala ya kodi, utungaji wa sheria,
    kuendesha shughuli za Bunge kupitia Bunge mtandao,
    ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo, pamoja na
    ujumuishwaji wa masuala ya jinsia katika bajeti; na kununuliwa
    na kufungwa kwa vifaa vya kuhifadhi taarifa ili kuimarisha
    Mamlaka ya Serikali Mtandao. Aidha, kwa upande wa
    mahakama Serikali imekamilisha ujenzi wa vituo vitano (5)
    Jumuishi vya utoaji Haki katika Mikoa ya Dar es Salaam
    (Temeke na Kinondoni), Dodoma, Arusha na Morogoro;
    kuendelea na ujenzi wa makao Makuu ya Mahakama Dodoma,
    Mahakama za Mwanzo sita (6), Mahakama za Hakimu Mkazi
    tatu (3) na Mahakama za wilaya sita (6); kuendelea na ujenzi
    wa Mahakama za Wilaya 26, Mahakama za Mwanzo sita (6) na
    kituo kimoja (1) jumuishi cha utoaji haki katika Mkoa wa
    28
    Mwanza. Vilevile, Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa
    haki za watoto, wasichana, wanawake na wanaume;
    mapambano dhidi ya rushwa; na kuendelea na ujenzi wa
    majengo 24 ya Wizara katika mji wa Serikali Dodoma ili
    kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi kutokea makao
    makuu ya nchi Dodoma.
    UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA USTAWI
    WA TAIFA NA MAPAMBANO DHIDI YA UVIKO–19
  39. Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu katika kipindi cha
    mwaka 2019, dunia ilikumbwa na mlipuko wa janga la UVIKO – 19
    ambapo kwa kiasi kikubwa uliathiri afya za jamii na uchumi wa nchi
    mbalimbali ikiwemo Tanzania. Katika kukabiliana na athari za mlipuko
    huo, Serikali iliandaa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na
    Mapambano dhidi ya UVIKO–19 (Tanzania COVID-19 Socio-economic
    Response and Recovery Plan – TCRP). Mpango huo ulizinduliwa rasmi
    tarehe 10 Oktoba, 2021 na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais
    wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpango huo unatekelezwa
    kwa kugharamiwa na mkopo nafuu usio na riba wenye thamani ya
    dola za Marekani milioni 567.25 sawa na shilingi trilioni 1.3 kutoka
    Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). Kati ya fedha hizo, dola za
    Marekani milioni 467.3 sawa na shilingi bilioni 1,079.6 zilielekezwa
    Tanzania Bara na dola za Marekani milioni 100 sawa na shilingi bilioni
    231.0 zilielekezwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
  40. Mheshimiwa Spika, kupitia fedha hizo Serikali imeweza
    kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi hususan katika
    sekta ya elimu ambayo ilipokea shilingi bilioni 368.9, afya shilingi
    bilioni 466.9, utalii shilingi bilioni 90.2, maji shilingi bilioni 139.4 na
    Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) shilingi bilioni 5.5.
  41. Mheshimiwa Spika, katika sekta ya elimu, Serikali imeweza
    kupunguza msongamano wa wanafunzi kwa kukamilisha ujenzi wa
    29
    vyumba vya madarasa 12,000 katika shule za sekondari, madarasa
    3,000 ya vituo shikizi katika shule za msingi na mabweni 50 ya
    wanafunzi wenye mahitaji maalumu pamoja na ununuzi wa
    madawati, viti na meza. Aidha, ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi –
    VETA unaendelea katika wilaya 25 ikijumuisha upatikanaji wa vifaa
    vya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika vyuo 11.
  42. Mheshmiwa Spika, katika sekta ya afya, hatua iliyofikiwa ni
    kuanza kwa ujenzi na ukarabati wa majengo 26 ya wagonjwa
    mahututi (ICU), majengo 80 ya huduma za dharura – EMD na
    nyumba 150 (3 in 1) za watumishi katika ngazi ya msingi chini ya
    Ofisi ya Rais – TAMISEMI na ujenzi wa wodi 38 za wagonjwa mahtuti
  • ICU; wodi 20 za huduma za dharura – EMD; nyumba 26 za
    watumishi, uboreshaji wa hospitali za rufaa za mikoa saba (7),
    hospitali maalumu ya Mirembe; kituo cha magonjwa ya kuambukiza
    Kisopwa – Dar es Salaam na kituo cha mfano cha utoaji elimu ya afya
    kwa umma Njedengwa – Dodoma ziko katika hatua mbalimbali za
    ujenzi. Aidha, maandalizi ya ununuzi wa vifaa tiba vya UVIKO – 19
    yamekamilika ikiwemo ununuzi wa mashine 130 za Kidigitali za X –
    Ray, CT – Scan 31, MRI nne (4) na Portable Echo Cardiography saba
    (7) kwa ajili za Hospitali ya Taifa Muhimbili, Ocean Road, Taasisi ya
    Moyo ya Jakaya Kikwete, hospitali za kanda, Hospitali za Rufaa za
    Mikoa pamoja na hospitali ya Emilio Mzena Memorial na Lugalo.
  1. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa sekta ya Maji, Serikali
    imekamilisha taratibu za ununuzi wa seti 25 za mitambo ya kuchimba
    visima katika mikoa yote nchini, seti tano (5) za mitambo ya ujenzi
    wa mabwawa na seti nne (4) za vifaa vya uchunguzi wa maji chini ya
    ardhi. Aidha, utekelezaji wa miradi 218 ya kuboresha huduma za maji
    unaendelea katika maeneo ya mijini na vijijini yenye thamani ya
    shilingi bilioni 139.4, ambapo miradi 46 ni kwa maeneo ya mijini na
    miradi 172 kwa maeneo ya vijijini.
    30
  2. Mheshimiwa Spika, sekta ya utalii ni miongoni mwa sekta
    zilizopata athari za moja kwa moja kutokana na UVIKO-19. Katika
    kuimarisha sekta hiyo, Serikali inaendelea na ukarabati na ujenzi wa
    miundombinu mbalimbali ikiwemo malango, barabara, njia ya
    watembea kwa miguu, Trails, campsite na bandas katika hifadhi zilizo
    chini ya TANAPA ikiwemo Nyerere National Park, Saadani National
    Park, Kilimanjaro (trails) pamoja na majengo ya kale na nyumba za
    kihistoria. Vilevile, Serikali imetoa mafunzo kwa waongoza watalii
    1,060 katika Hifadhi za Taifa Tarangire, Saadani, Serengeti,
    Ngorongoro na Manyara ili kuimarisha udhibiti wa ubora wa huduma
    za utalii katika kukabiliana na janga la UVIKO – 19.
  3. Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Kukabiliana na Athari
    za Kijamii na Kiuchumi zitokanazo na UVIKO – 19, Serikali
    imewezesha kaya maskini 51,290 katika Halmashauri 35 kupitia
    Mfuko wa TASAF ambapo shilingi bilioni 5.5 zimetumika. Aidha,
    Serikali imewawezesha wajasiriamali vijana, wanawake, na wenye
    ulemavu jumla ya shilingi bilioni 5 kupitia Mpango wa biashara wa
    kuboresha miundombinu na mazingira ya wafanyabiashara wadogo
    katika Halmashauri za Jiji la Dodoma, Mwanza, Arusha, Tanga,
    Mbeya na Dar es Salaam pamoja na Halmashauri za Manispaa za
    Kinondoni, Temeke, Ubungo na Morogoro. Vilevile, Serikali
    imeendelea na hatua za upatikanaji wa mkandarasi kwa ajili ya
    ukarabati wa vyuo vinne (4) vyenye mazingira hatarishi vya watu
    wenye ulemavu katika mikoa minne (4) ya Tanzania Bara kwa
    gharama ya shilingi bilioni 3.5.
    MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2022/23
  4. Mheshimiwa Spika, Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa
    Mwaka 2022/23 ni wa pili katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa
    Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26) wenye
    dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa
    Maendeleo ya Watu. Mpango umeandaliwa kwa kuzingatia: Dira ya
    31
    Taifa ya Maendeleo 2025; Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa
    wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26; Ilani ya Chama cha Mapinduzi
    kwa Ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020; Mapendekezo ya
    Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23; na Sera na
    Mikakati mbalimbali ya kisekta, kikanda na kimataifa zikiwemo Dira
    ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) 2050, Dira ya
    Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) 2050, Agenda 2063
    ya Maendeleo ya Afrika na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.
    Malengo na Shabaha za Uchumi Jumla kwa Mwaka 2022/23
  5. Mheshimiwa Spika, Malengo na Shabaha za Ukuaji wa
    Uchumi katika kipindi cha mwaka 2022/23, ni kama ifuatavyo:
    (i) Ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 4.7 mwaka 2022
    na asilimia 5.3 mwaka 2023;
    (ii) Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha
    kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa
    asilimia kati ya 3.0 hadi 7.0 katika muda wa kati;
    (iii) Mapato ya ndani kufikia asilimia 14.9 ya Pato la Taifa mwaka
    2022/23;
    (iv) Mapato ya kodi kufikia asilimia 11.7 ya Pato la Taifa mwaka
    2022/23; na
    (v) Kuwa na akiba ya fedha za kigeni kwa kiwango cha kukidhi
    mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje kwa
    kipindi kisichopungua miezi minne (4).
  6. Mheshimiwa Spika, Misingi itakayozingatiwa katika Mpango
    wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 ni kama ifuatavyo:
    (i) Kuongezeka kwa ushiriki wa sekta binafsi kwenye shughuli za
    maendeleo;
    (ii) Kuendelea kuhimili athari za majanga ya asili na yasiyo ya asili
    kama vile ukame, vita na magonjwa ya mlipuko;
    (iii) Kuendelea kuwa na utoshelevu wa chakula nchini; na
    32
    (iv) Uwepo wa amani, usalama, umoja, utulivu wa ndani na katika
    nchi jirani.
    Miradi ya Kipaumbele kwa Mwaka 2022/23
  7. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali
    itaendelea kukamilisha miradi ya kielelezo na ile ya kimkakati
    inayoendelea. Miradi hiyo inatarajiwa kuwa na matokeo mapana na
    ya haraka katika uchumi, ikiwemo kuzalisha ajira, kipato na
    kuchangia zaidi kupunguza hali ya umaskini nchini. Miradi hiyo
    inajumuisha: Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa
    (Standard Gauge Railway – SGR); Mradi wa Kufua Umeme wa Maji
    wa Julius Nyerere – MW 2,115; Kuboresha Shirika la Ndege Tanzania
    (ATCL); Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika (LNG) –
    Lindi; Kufua Umeme wa Maji wa Ruhudji (MW 358) na Rumakali (MW
    222) – Njombe; Daraja la JPM – Kigongo – Busisi (Mwanza); Ujenzi
    wa barabara na Madaraja Makubwa; kuendeleza Kanda Maalumu za
    Kiuchumi ikiwemo Eneo Maalumu la Uwekezaji Bagamoyo; na
    programu ya kuendeleza ujuzi adimu.
  8. Mheshimiwa Spika, miradi ya kipaumbele kwa mwaka
    2022/23 itakaendelea kuzingatia maeneo matano ya kipaumbele ya
    Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano, 2021/22
    – 2025/26 kama ifuatavyo:
    (a) Kuchochea Uchumi Shindani na Shirikishi: Msisitizo
    utawekwa katika kuimarisha mazingira wezeshi ya uwekezaji
    ikijumuisha kuimarisha utulivu wa uchumi jumla. Miradi
    itakayotekelezwa ni pamoja na: uendelezaji wa miundombinu
    na huduma; ukarabati wa njia kuu za reli ikiwemo kukamilisha
    ukarabati wa njia ya reli kwa maeneo yaliyobaki kwa kipande
    cha Dar es Salaam hadi Isaka (km 970); ujenzi wa barabara za
    kufungua fursa za kiuchumi na zile za kuunganisha Tanzania na
    33
    nchi jirani ikiwemo Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo –
    Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 499), Barabara ya
    Mbeya – Makongolosi – Manyoni (Mkiwa) (km 528), Barabara
    ya Itoni – Ludewa – Manda (km 211); barabara ya Handeni –
    Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini –
    Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida
    (km 460); barabara ya Mafinga – Mtwango – Nyololo –
    Mgololo; Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro Express Way
    (km 158); barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (km 218)
    na mchepuo wa Mbeya (Uyole – Songwe (km 48.9); barabara
    ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa
    (km 389); kukamilisha madaraja makubwa ya New Wami
    (Pwani), Kitengule (Kagera), Lower Malagarasi, Mkundi
    (Morogoro), Godegode (Dodoma) na Mtera (Iringa); ujenzi wa
    meli katika ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa; kuendelea
    kuboresha bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na
    Bandari Kavu ya Ruvu; ujenzi wa viwanja vya ndege vya
    Msalato, Shinyanga, Tabora, Kigoma na Lindi; kujenga njia ya
    kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 ya Rufiji – Chalinze –
    Dodoma; kujenga njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kV
    400 ya Singida – Arusha – Namanga; kujenga njia ya
    kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 ya Iringa – Mbeya –
    Sumbawanga – Mpanda – Kigoma – Nyakanazi (North West
    Grid Extension); kusambaza umeme vijijini kupitia REA;
    uimarishaji wa Gridi ya Taifa ikijumuisha ujenzi wa vituo vipya
    57 vya kupoza umeme; ujenzi wa Mkongo wa Mawasiliano wa
    Taifa; kuimarisha huduma za bima hususan bima za mazao na
    huduma za fedha ili kuimarisha shughuli za uwekezaji nchini;
    na kuimarisha mapinduzi ya kidigitali kwa kukuza teknolojia ya
    habari na mawasiliano.
    (b) Kuimarisha Uwezo wa Uzalishaji Viwandani na
    Huduma: miradi itajielekeza katika kuendelea kukuza sekta ya
    34
    kilimo kwa kutekeleza miradi ya kimkakati ya umwagiliaji,
    mbegu na maghala kwa lengo la kuongeza kasi ya ukuaji wa
    sekta ya kilimo kufikia wastani wa asilimia 10 na mchango wa
    shughuli za umwagiliaji kwenye kilimo kufikia asilimia 50 ifikapo
    mwaka 2030. Aidha, Serikali inalenga kuongeza eneo la
    umwagiliaji kufikia hekta 8,500,000 pamoja na kuongeza
    mauzo ya bidhaa za kilimo nje kutoka dola za Marekani bilioni
    1.2 hadi dola za Marekani bilioni 5 ifikapo mwaka 2030. Baadhi
    ya mikakati mahsusi itakayotekelezwa ni pamoja na kujenga
    skimu za umwagiliaji, kuanzisha Mfuko wa Kutengamaza Bei za
    Mazao (Price Stabilisation Fund) na mifuko ya kuendeleza
    mazao, kujenga maghala ya kuhifadhi mazao kwenye vijiji ili
    kukabiliana na changamoto ya upotevu wa mazao baada ya
    mavuno na kuanzisha Youth Agricultural Parks; kuongeza
    matumizi ya teknolojia bora katika uzalishaji, kuimarisha
    huduma za ugani; kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao
    ya kilimo; kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa mitaji katika
    sekta ya kilimo; kuimarisha afya ya mifugo; kuimarisha taasisi
    za utafiti wa kilimo za TARI na ASA; kuimarisha miundombinu
    ya masoko ya mifugo na mazao yake; kufufua Shirika la Uvuvi
    Tanzania – TAFICO na kuliwezesha kujiendesha kibiashara;
    ujenzi wa bandari ya uvuvi – Kilwa Masoko; kununua boti 250
    za kisasa aina ya fibre kwa ajili ya vyama vya ushirika vya
    wavuvi; na kujenga na kukarabati vituo vya ukuzaji viumbe
    maji.
    Kwa upande wa viwanda, miradi itakayotekelezwa ni pamoja
    na: kuendelea kuboresha Kituo cha Kuendeleza Teknolojia ya
    Magari Tanzania – TATC; kuendelea kufufua Kiwanda cha
    Mashine na Vipuri KMTC; kuimarisha Kiwanda cha Viuadudu;
    Uendelezaji wa Viwanda Vidogo – SIDO; kuendeleza Eneo la
    Kongano ya Viwanda – TAMCO; Maeneo Maalum ya Uwekezaji
    (SEZ/EPZ) ya Dodoma, Manyara na Bunda; na kuendelea
    35
    kuweka sera na mazingira wezeshi kwa uwekezaji wa sekta
    binafsi katika viwanda.
    Kwa upande wa eneo la madini na huduma, miradi
    itakayotekelezwa ni pamoja na: kuendelea kufungua masoko
    na vituo vya madini; kuendeleza wawekezaji wadogo wa sekta
    ya madini; kuendeleza utalii kanda ya kusini na kuimarisha
    utalii hususan kwa kuanzisha mazao mapya ya utalii wa fukwe,
    mikutano pamoja na kuimarisha utalii wa ndani; na kukabiliana
    na ujangili na biashara haramu ya wanyamapori kwa lengo la
    kulinda urithi na maliasili za Taifa.
    (c) Kukuza Biashara na Uwekezaji: Kipaumbele kitakuwa
    katika kusimamia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kuboresha
    Mazingira ya Biashara ikiwemo kuimarisha mazingira ya kisera
    na kisheria kuhusu uwekezaji pamoja na mifumo ya uratibu na
    usimamizi wa masuala ya uwekezaji kitaifa; kuondoa utozaji
    kodi mara mbili; na kulinda biashara na uwekezaji wa sekta
    binafsi. Aidha, shughuli nyingine zitakazotekelezwa ni pamoja
    na: kutekeleza Programu za Kuboresha Mifumo ya Udhibiti wa
    Biashara; Kukuza Ushiriki wa Watanzania kwenye Miradi ya
    Kimkakati na Uwekezaji; Kukuza Uwezeshaji Wananchi
    Kiuchumi; Kukuza Sekta Binafsi; Uendelezaji wa Masoko ya
    Bidhaa; Udhibiti wa Ubora wa Bidhaa; na kuimarisha masoko,
    maonesho na makongamano ya uwekezaji ya kikanda na
    kimataifa.
    (d) Kuchochea Maendeleo ya Watu: Miradi itakayotekelezwa
    inalenga kuboresha maisha ya watu: Kwa upande wa sekta ya
    elimu shughuli zitakazo tekelezwa ni pamoja na: kuendelea
    kugharamia elimumsingi bila ada; kugharamia mikopo ya
    wanafunzi wa elimu ya juu; kuimarisha vyuo vya elimu ya juu,
    vyuo vya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi na vyuo vya
    36
    ualimu; kuboresha Elimu ya Sekondari; uboreshaji wa
    maktaba; kukamilisha maboma ya vyumba vya madarasa
    yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi; kuboresha mitaala ili
    iendane na mahitaji ya soko; kujenga shule mpya katika
    maeneo yenye mahitaji; na kugharamia uboreshaji wa lishe
    shuleni.
    Kwa upande wa eneo la afya, miradi itakayotekelezwa ni
    pamoja na: kuimarisha huduma za afya hususan ujenzi wa
    Hospitali za Rufaa za Kanda na za Mikoa, zahanati, vituo vya
    afya na hospitali za Halmashauri za Wilaya; kuimarisha
    upatikanaji wa chanjo, dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi
    kwa kuongeza bajeti, kutoa fedha na kuimarisha udhibiti;
    kuimarisha huduma za ustawi na maendeleo ya jamii, hususan
    haki za wazee, watoto na makundi maalumu; na kuendelea na
    hatua za uteelezaji wa ahadi ya utoaji wa bima za afya kwa
    wote;
    Kwa upande wa eneo la maji safi na usafi wa mazingira miradi
    itakayotekelezwa ni pamoja na: kuimarisha huduma za maji na
    usafi wa mazingira vijijini; ujenzi, ukarabati na upanuzi wa
    miradi ya maji katika miji mikuu ya mikoa, wilaya, miji midogo
    na miradi ya kitaifa; ujenzi wa bwawa la Farkwa kwa ajili ya
    kuimarisha huduma ya maji katika jiji la Dodoma; bwawa la
    Kidunda kwa ajili ya kuimarisha upatikanaji wa maji jijini Dar es
    Salaam; na kutekeleza mradi wa kimkakati wa kutoa maji
    kutoka ziwa Victoria hadi jijini Dodoma.
    Kwa upande wa eneo la ardhi, miradi itakayotekelezwa ni
    pamoja na: kuendelea kupanga, kupima na kumilikisha ardhi
    nchi nzima; kuimarisha mipaka ya kimataifa; kuimarisha
    miundombinu ya upimaji na ramani; na kuendeleza upangaji
    wa matumizi ya ardhi nchini ili kuondoa migogoro katika
    37
    matumizi ya ardhi.
    (e) Kuendeleza Rasilimali Watu: Kuendelea na utekelezaji wa
    programu na miradi mbalimbali ya kukuza ujuzi nchini ili
    kuongeza ajira kwa vijana kwa kutoa mafunzo ya ufundi na
    stadi za kazi kupitia programu mbalimbali zikiwemo:
    kuimarisha programu ya taifa ya kukuza ujuzi nchini; kuboresha
    mfuko wa maendeleo ya vijana; kuendelea na ujenzi na
    ukarabati wa vituo vya ufundi kwa watu wenye ulemavu; na
    kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Kazi za Staha.
  9. Mheshimiwa Spika, maelezo ya kina kuhusu miradi ya
    kipaumbele kwa mwaka 2022/23 yanapatikana katika Kitabu cha
    Mpango, Sura ya Nne.
    Vihatarishi vya Utekelezaji wa Mpango wa Mwaka 2022/23
  10. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango unaweza
    kuathiriwa na vihatarishi vya ndani na nje. Vihatarishi vya ndani ni
    pamoja na: ufinyu wa rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia
    utekelezaji wa miradi ya maendeleo; ushiriki mdogo wa sekta binafsi
    katika mipango ya maendeleo; uharibifu wa mazingira na mabadiliko
    ya tabianchi; na uhalifu wa kimtandao na rushwa. Vihatarishi vya nje
    ni pamoja na: majanga ya asili na magonjwa ya mlipuko; mitikisiko
    ya kiuchumi duniani; kubadilika kwa teknolojia; na kutopatikana kwa
    misaada na mikopo kwa wakati.
  11. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na vihatarishi vya
    utekelezaji wa Mpango, Serikali itachukua hatua mbalimbali
    ikijumuisha: Kuimarisha ukusanyaji na usimamizi wa kodi kwa
    kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti za kielektroniki
    wanapouza bidhaa na wanunuzi kudai risiti wanaponunua bidhaa;
    kuhamasisha ulipaji kodi katika sekta isiyo rasmi kwa kuijumuisha
    38
    kwenye mfumo rasmi wa ulipaji kodi; kuendelea kuimarisha na
    kuhamasisha wananchi kuhusu uelewa wa huduma za sekta ya fedha
    ikiwemo utoaji wa mikopo, uwekezaji, mitaji na bima; kuendelea
    kuweka mazingira ya kuvutia uwekezaji wa sekta Binafsi wa ndani na
    nje ili kupunguza gharama za uwekezaji; kusimamia miongozo na
    kanuni za usimamizi wa mazingira; kuendelea kuimarisha
    mapambano dhidi ya rushwa ikijumuisha kuchukua hatua za kisheria
    kwa wanaobainika kuhusika na vitendo vya rushwa; kuboresha
    mifumo ya kuzuia na kukabiliana na majanga; na kuweka mazingira
    wezeshi kwa wawekezaji hususan viwanda vinavyozalisha bidhaa kwa
    kutumia teknolojia na malighafi za ndani ili kupunguza uagizaji wa
    bidhaa kutoka nje.
    Ugharamiaji wa Mpango 2022/23
  12. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2022/23, inakadiriwa kuwa
    jumla ya shilingi bilioni 15,004.8 sawa na asilimia 36.2 ya Bajeti yote
    ya Serikali zitatumika kugharamia miradi ya maendeleo ikijumuisha
    miradi ya huduma za jamii. Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni
    12,305.8 sawa na asilimia 82.0 ya bajeti ya maendeleo ni fedha za
    ndani na shilingi bilioni 2,699.1 sawa na asilimia 18.0 ya bajeti ya
    maendeleo ni fedha za nje. Katika kuongeza ushiriki wa sekta binafsi
    kama injini muhimu ya utekelezaji wa miradi, Serikali itahakikisha
    miradi yote inayovutia uwekezaji wa sekta binafsi inatekelezwa kwa
    utaratibu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) na
    Joint Venture kwa kutumia utaratibu wa Kampuni Maalumu (Special
    Purpose Vehicle).
  13. Mheshimiwa Spika, katika kuongeza ukusanyaji wa mapato
    ya kugharamia Mpango, Serikali itaendelea kuweka mikakati ya
    kusimamia ukusanyaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi kutoka
    vyanzo mbalimbali vya ndani kwa kuchukua hatua mbalimbali
    zikiwemo: Kuimarisha ukusanyaji na usimamizi wa kodi kwa
    39
    kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti za kielektroniki
    wanapouza bidhaa na wanunuzi kuchukua risiti wanaponunua
    bidhaa; kuendelea kutoa elimu kwa mlipakodi kupitia runinga, redio,
    mitandao ya kijamii na semina; kupanua wigo wa kodi kwa
    kuwatambua na kuwasajili wafanyabiashara katika mfumo rasmi wa
    ulipaji kodi kupitia kampeni ya Mlango kwa Mlango; kuendelea
    kutumia Mpango wa Usimamizi wa Viashiria Hatarishi (Compliance
    Risk Management Plan) ili kubaini na kutambua wakwepaji wa kodi;
    kuendelea kuimarisha usimamizi na ukaguzi wa mipaka yote kwa
    kuongeza ushirikiano baina ya Mamlaka ya Mapato Tanzania na
    vyombo vya ulinzi na usalama nchini ili kudhibiti bidhaa za magendo
    na kupunguza tatizo la ukwepaji wa kodi; na kuimarisha mazingira
    rafiki ya ulipaji kodi kwa hiari kwa kuboresha na kuhimiza matumizi
    sahihi ya mifumo ya TEHAMA ikiwa ni pamoja na kuboresha mifumo
    itakayosaidia na kurahisisha ulipaji kodi.
  14. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha Mfumo wa
    Kielektroniki wa Kufuatilia Mizigo inayokwenda nchi jirani (Eletronic
    Cargo Tracking System) ili kuimarisha uwezo wa usimamizi wa mizigo
    inayopita kwenda nchi jirani; kuhamasisha ulipaji kodi katika sekta
    isiyo rasmi kwa kuijumuisha kwenye mfumo rasmi wa ulipaji kodi;
    kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuvutia wawekezaji
    wapya, kukuza biashara ndogo na za kati kwa ukuaji endelevu wa
    uchumi utakaowezesha kuongeza wigo wa kodi pamoja na
    kuendelea kusimamia Mfumo wa Serikali wa Kielektroniki wa
    Ukusanyaji wa Mapato (Government Electronic Payment Gateway –
    GePG) ili kurahisisha ulipaji na kudhibiti upotevu wa mapato.
  15. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha
    mashirikiano na Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza Mwongozo
    wa Ushirikiano wa Maendeleo (Development Cooperation Framework
  • DCF) ili kuhakikisha kuwa fedha kutoka kwa Washirika wa
    Maendeleo zinaendelea kupatikana kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji
    40
    wa miradi na programu mbalimbali nchini. Aidha, Serikali kwa
    kushirikiana na washirika wa Maendeleo imeanza maandalizi ya
    kufanya tathmini na mapitio ya Mwongozo wa Ushirikiano
    itakayoiwezesha nchi kujipanga kimkakati ili kunufaika zaidi na fursa
    zilizopo kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Serikali, Sekta
    binafsi na Asasi Zisizo za Kiserikali katika masuala ya ushirikiano wa
    kimataifa.
    Vile vile, kwa kutambua uwepo wa pengo la rasilimali fedha
    zinazohitajika katika kufikia shabaha ya maendeleo ya Taifa, Serikali
    imeainisha vyanzo mbadala na bunifu vitakavyotumika kugharamia
    miradi ya maendeleo na hivyo kupunguza mzigo kwa bajeti ya
    Serikali. Vyanzo hivyo ni utekelezaji wa Mkakati wa Ugharamiaji wa
    Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano sanjari na
    Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa mwaka 2020/21-
    2029/30. Katika kufikia azma hiyo, Serikali itafanya maboresho ya
    sheria mbalimbali pamoja na kuweka miongozo itakayowezesha
    kunufaika na vyanzo mbadala na bunifu katika utekelezaji wa
    shughuli za maendeleo.
  1. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ugharamiaji wa miradi
    ya maendeleo itakayotekelezwa kwa utaratibu wa Ubia baina ya
    Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Serikali imepanga kuwezesha
    Mamlaka za Serikali zenye miradi ya PPP iliyopo katika hatua
    mbalimbali za maandalizi ikiwemo Upembuzi Yakinifu na Ununuzi wa
    wabia kukamilisha miradi hiyo iweze kuanza utekelezaji. Katika
    mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kushirikiana na Sekta Binafsi
    katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa utaratibu
    wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). Baadhi
    masuala yatakayotekelezwa ni pamoja na kuendelea kutafuta wabia
    wa miradi mitano (5) iliyofikia katika hatua za ununuzi (procurement
    stage) kwa kuitangaza katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Miradi
    hiyo ni: ujenzi wa viwanda vya dawa muhimu (Kibaha), vifaa tiba
    41
    vitokanavyo na pamba (Mwanza) na maji tiba (Mbeya); uendeshaji
    wa huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es
    Salaam awamu ya kwanza; ujenzi wa hoteli ya nyota nne katika
    Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere; ujenzi wa kituo
    changamani cha biashara (commercial Complex) katika Kiwanja cha
    Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere; na ujenzi wa kiwanda cha
    kutengeneza simu za mkononi chini ya Mamlaka ya Mawasiliano
    Tanzania (TCRA) katika Mkoa wa Mwanza.
    Ufuatiliaji, Tathmini na Utoaji wa Taarifa za Utekelezaji
  2. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa mipango ya
    maendeleo inatekelezwa kama ilivyokusudiwa, suala la ufuatiliaji,
    tathmini na utoaji wa taarifa za utekelezaji limeendelea kupewa
    msukumo wa pekee katika shughuli za kila siku za Serikali. Katika
    kutekeleza hilo, mwaka 2021/22, Wizara ya Fedha na Mipango
    ilifanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi 225 katika sekta za Uchukuzi,
    Viwanda, Elimu, Afya, Ujenzi, Utawala Bora, Kilimo, Mifugo, Maji na
    Biashara inayotekelezwa na Serikali pamoja na Sekta Binafsi. Katika
    mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kutumia mbinu na viashiria
    vilivyoainishwa katika Mkakati wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Mpango
    wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 –
    2025/26 pamoja na Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini
    ya Miradi na Programu za Maendeleo kupima utekelezaji wa Mpango
    wa Tatu wa Maendeleo wa Miaka Mitano na miradi ya maendeleo na
    kuchukua hatua za kutatua changamoto zitakazobainika katika
    utekelezaji. Vile vile, Serikali itaendelea kuzingatia miongozo
    mbalimbali ya ufuatiliaji na tathmini ya Mpango ikiwemo Sheria ya
    Ununuzi wa Umma, SURA 410, Sheria ya Bajeti, SURA 439 na Sheria
    ya Fedha za Umma, SURA 348. Pamoja na Sheria hizo, Serikali pia
    imeanza maandalizi ya Sera ya Taifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ili
    kutatua changamoto za uratibu wa shughuli za ufuatiliaji na tathmini
    Serikalini.
    42
  3. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha uwepo wa
    ushirikishwaji wa kutosha katika masuala ya ufuatiliaji na tathmini,
    Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kushirikiana
    na Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na
    Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za
    Mitaa pamoja na Sekta Binafsi katika kuratibu na kusimamia
    ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Mpango.
  4. Mheshimiwa Spika, Serikali inazielekeza Wizara, Idara
    Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma,
    Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutafsiri
    malengo na viashiria vya utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa
    Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 katika
    Mipango na Bajeti za kisekta kwa mwaka 2022/23. Aidha, Wizara,
    Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya
    Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa
    zinaelekezwa kuzingatia maelekezo yaliyoainishwa katika Mwongozo
    wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi na Programu za
    Maendeleo wa Mwaka 2022 ikiwa ni pamoja na: kuandaa Mpango
    Kazi wa mwaka wa ufuatiliaji na tathmini, kutenga rasilimali fedha
    zitakazowezesha shughuli za ufuatiliaji na tathmini; kuimarisha
    mifumo ya ndani ya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo;
    kufanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo kwa
    kuzingatia mipango kazi iliyowekwa; kuendelea kuwajengea uwezo
    watumishi katika tasnia ya ufuatiliaji na tathmini; na kuwa na mfumo
    mmoja wa kielektroniki unaoratibu taarifa za utekelezaji, ufuatiliaji na
    tathmini katika kutekeleza mipango ya maendeleo.
  5. Mheshimiwa Spika, Serikali inazielekeza Wizara, Idara
    Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma,
    Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuaandaa
    43
    taarifa za ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi na programu
    za maendeleo na kuziwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango. Ofisi ya
    Rais – TAMISEMI itaratibu ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya
    maendeleo inayotekelezwa katika ngazi za Sekretarieti za Mikoa na
    Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuwasilisha taarifa husika Wizara ya
    Fedha na Mipango.
    MAJUMUISHO
  6. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza hapo awali, Mpango
    wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 ni wa pili katika
    utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka
    Mitano 2021/22 – 2025/26 wenye dhima ya “Kujenga Uchumi
    Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu”. Utekelezaji wa
    Mpango utaendelea kuimarisha viashiria vya uchumi jumla,
    kuboresha mazingira ya uwekezaji viwandani ikiwemo kuimarisha
    majadiliano na wawekezaji wa ndani na nje, kuimarisha mahusiano
    ya kisiasa, ulinzi na diplomasia ya uchumi na nchi nyingine,
    kuendelea kutekeleza kwa kasi miradi ya maendeleo, kuendeleza
    mashirikiano na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya
    maendeleo pamoja na kuchochea uwekezaji viwandani hususan kwa
    kutumia rasilimali watu na malighafi zinazopatikana kwa wingi nchini
    ikiwemo mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, madini, misitu na gesi
    asilia.
  7. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na jitihada za
    kukabiliana na athari za majanga mbalimbali ya asili na yasiyo ya asili
    yakiwemo magonjwa, vita na mabadiliko ya tabianchi. Mathalani,
    tutaendelea kuimarisha utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa
    Kukabiliana na Athari za UVIKO–19 pamoja na kuweka mipango
    madhubuti ya kupunguza athari zitokanazo na vita inayoendelea kati
    ya Urusi na Ukraine ikiwemo kudhibiti ongezeko la bei za bidhaa
    mbalimbali na kushuka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi.
    44
  8. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha upatikanaji
    na utoaji wa huduma bora kwa wananchi zikiwemo huduma za afya,
    elimu, umeme na maji safi na salama mijini na vijijini, kuongeza kasi
    ya utekelezaji wa miradi ya kielelezo na ya kimkakati, kuimarisha
    miundombinu wezeshi ya uwekezaji na biashara kwa ajili ya masoko
    ya kimataifa hususan ya nchi jirani, kuimarisha sekta za uzalishaji ili
    kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi, kufungua fursa zaidi za
    ajira na maendeleo ya watu.
    HITIMISHO
  9. Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Serikali ninaomba kutumia
    fursa hii kuwashukuru wadau wote wa maendeleo wakiwemo
    Waheshimiwa Wabunge, Sekta Binafsi, Taasisi za Elimu na Tafiti,
    Asasi za Kiraia, Taasisi za Dini, Washirika wa Maendeleo na Wananchi
    wote kwa namna walivyojitoa na kushiriki kikamilifu katika hatua
    mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuimarisha
    uchumi wa Taifa letu. Wadau hao wamekuwa na mchango mkubwa
    katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo. Kwa msingi
    huo, ninawaomba na kuwasihi wadau wote waendelee kushirikiana
    na Serikali yetu inayoongozwa na Rais shupavu, Mheshimiwa Samia
    Suluhu Hassan.
  10. Mheshimiwa Spika, hotuba hii isingeweza kukamilika bila
    jitihada kubwa zilizofanywa na watumishi wote wa Wizara ya Fedha
    na Mipango. Hivyo, kwa dhati ya nafsi yangu naomba nitoe shukrani
    za pekee kwa Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), Naibu Waziri wa
    Fedha na Mipango, Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa
    Wizara zote, Viongozi wote wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za
    Serikali za Mitaa, Wakuu wa Idara Zinazojitegemea, Wakala za
    Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma kwa ushirikiano wao katika
    maandalizi ya taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2021
    45
    na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23. Aidha,
    ninawashukuru watendaji wote wa Wizara ya Fedha na Mipango
    wakiongozwa na Katibu Mkuu Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba kwa
    kujitoa usiku na mchana kukamilisha kwa wakati na kwa ubora
    Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa
    Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23.
  11. Mheshimiwa Spika, mwisho lakini si kwa umuhimu, napenda
    kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge na Wananchi wote kwa ujumla
    kwa kutenga muda wao kunisikiliza. Aidha, napenda kuwataarifu
    wadau wote kuwa, hotuba hii pamoja na vitabu vya Taarifa ya Hali
    ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa
    Taifa wa Mwaka 2022/23 vinapatikana katika tovuti ya Wizara ya
    Fedha na Mipango ambayo ni www.mof.go.tz.
  12. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo naomba sasa
    Bunge lako Tukufu lipokee na kujadili Taarifa ya Hali ya Uchumi wa
    Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa
    Mwaka 2022/23.
  13. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *