
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT.
MWIGULU LAMECK NCHEMBA MADELU (MB), AKIWASILISHA
BUNGENI TAARIFA YA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KWA MWAKA
2021 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2022/23
DODOMA JUNI, 2022
1
UTANGULIZI
- Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako
Tukufu lipokee na kujadili Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa
Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23.
Pamoja na hotuba hii, nawasilisha vitabu vya Taarifa ya Hali ya
Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa
Taifa wa Mwaka 2022/23. Taarifa hizo ndiyo msingi wa bajeti ya
Serikali kwa mwaka 2022/23 nitakayowasilisha katika Bunge hili
Tukufu leo alasiri. - Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda nitumie fursa hii
kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema, na
kutuwezesha kukutana kwa mara nyingine katika Bunge hili baada ya
majadiliano ya bajeti za mafungu mbalimbali. Mkutano huu wa Saba
wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muhimu
katika kujadili namna ya kuharakisha maendeleo ya nchi yetu. - Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena, nitumie fursa
hii kutoa pole kwako Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge
wote, Chama cha Mapinduzi na Watanzania wote kufuatia kifo cha
aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Marehemu Irene Alex Ndyamkama.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi,
Amina. - Mheshimiwa Spika, kwa moyo mkunjufu, napenda kutoa
pongezi zangu za dhati kwako Mheshimiwa Spika kwa kuchaguliwa
kwa kishindo kuwa Spika wa saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania. Waheshimiwa Wabunge na Wananchi kwa ujumla wana
imani kubwa sana na wewe na hawana shaka na uzoefu, weledi na
umahiri wako katika kusimamia na kuongoza shughuli za Bunge.
Aidha, napenda kuchukua fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa
Mussa Azzan Zungu (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa
2
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niungane na
Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wenzangu kuwaombea kwa
Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa nguvu, ujasiri na afya njema ili
muweze kuendelea kutekeleza majukumu yenu ya kuliongoza Bunge
letu. - Mheshimiwa Spika, Kwa namna ya kipekee, nitoe pongezi
zangu za dhati, kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake thabiti na
utumishi uliotukuka kwa watanzania unaolenga kuleta mapinduzi
makubwa ya kiuchumi na kijamii. Mheshimiwa Rais ameonesha
dhamira yake ya dhati ya kulitumikia Taifa kwa uaminifu ambapo
ameendelea kusimamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali
zinazolenga kuleta maendeleo kwa Watanzania ikiwemo: kuendelea
kutekeleza miradi mikubwa ya kielelezo na miradi mingine ya
kuchochea uchumi na kuimarisha huduma za jamii; kuendeleza
mapambano dhidi ya rushwa; na kuimarisha ushirikiano wa kikanda
na kimataifa. - Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amekuwa akiendelea
kutuongoza kwa vitendo kwa kuchukua hatua mbalimbali za
kuchochea ukuaji wa uchumi hususan sekta ya utalii ambayo
iliathirika zaidi na UVIKO-19 ikiwemo kushiriki kwenye filamu
ijulikanayo kwa jina la The Royal Tour kama Mwongoza Utalii Namba
Moja Nchini. Mheshimiwa Rais amekuwa chachu na kinara wa utalii
kupitia filamu hiyo inayolenga kukuza sekta ya utalii ambayo
inatarajiwa kuzalisha takriban ajira milioni 1.3 na fedha za kigeni dola
za Marekani bilioni 2.6. Filamu hiyo iliyozinduliwa kwa Mara ya
Kwanza Jijini New York tarehe 18 Aprili 2022 na baadaye tarehe 21
Aprili 2022 Jijini Los Angeles. Ndugu Watanzania wenzangu, hii ni
hatua kubwa sana kwa Taifa letu kwa kuwa filamu hii inapatikana
kupitia chaneli za Apple TV Plus na Amazon Prime za nchini Marekani
ambazo zinakadiriwa kuwa na watazamaji zaidi ya milioni 200
3
duniani. Ama kwa Hakika Mama Anaupiga Mwingi; na hivyo
tuna kila sababu ya kuunga mkono jitihada hizi na kwenda
pamoja na Mama. - Mheshimiwa Spika, kipekee natoa shukrani zangu za dhati
kwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini kumsaidia kazi
katika nafasi ya Waziri wa Fedha na Mipango. Kwa imani hii
aliyoionesha kwangu napenda kuwahakikishia Mheshimiwa Rais,
Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwa ujumla kuwa
nitaendelea kutekeleza majukumu yangu kwa bidii kubwa, weledi,
uaminifu, uadilifu na uzalendo wa kiwango cha hali ya juu ili
kuhakikisha matamanio ya Mheshimiwa Rais na Watanzania wote ya
kuwa na maendeleo na ustawi wa kiwango cha juu yanafikiwa. - Mheshimiwa Spika, Sote tunafahamu kuwa, nchi yetu na
dunia kwa ujumla inaendelea kushuhudia athari za UVIKO-19 ambazo
zimesababisha kushuka kwa shughuli za kiuchumi duniani, ikiwemo
uzalishaji, biashara za ndani na kimataifa, utalii na usafirishaji wa
bidhaa. Katika mwaka 2021, uchumi wa Taifa letu na wa dunia kwa
ujumla ulianza kuimarika baada ya kupitia katika kipindi cha
kukabiliana na athari za UVIKO–19. Aidha, wakati Serikali ikiendelea
na jitihada za kuimarisha uchumi, mwezi Februari 2022 kuliibuka vita
kati ya mataifa ya Urusi na Ukraine ambayo imesababisha Urusi
kuwekewa vikwazo na hivyo kusababisha kupanda kwa bei za bidhaa
mbalimbali katika soko la dunia zikiwemo mafuta na gesi. Sanjari na
kupanda kwa bei hizo, kumekuwa na uhaba wa baadhi ya bidhaa
katika soko la Dunia ikiwemo, mbolea, ngano na mafuta ya kula.
Serikali imeendelea kuchukua hatua katika kukabiliana na athari hizo
ikiwemo kupokea Mkopo wa Masharti nafuu wa shilingi trilioni 1.3
zilizoelekezwa katika sekta ya afya, elimu, maji na utalii ili kuchochea
uchumi na kukabiliana na UVIKO-19; kuongeza bajeti ya kilimo,
mifugo, uvuvi, nishati na miundombinu ya wafanyabiashara wadogo
4
maarufu kama machinga ili kuchochea uzalishaji wa ndani na
kupunguza nakisi ya urari wa biashara; na kuangalia namna bora ya
uagizaji mafuta itakayoleta unafuu wa bei kwa wananchi. Aidha,
nichukue fursa hii kulihakikishia Bunge lako Tukufu na Watanzania
wote kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili
kukabiliana na athari hizo kwa lengo la kuleta unafuu wa maisha kwa
Wananchi. - Mheshimiwa Spika, Nipende kuwashukuru wadau wote
walioshiriki katika mchakato huu nikianza na Bunge lako Tukufu chini
ya uongozi wako Mheshimiwa Spika pamoja na Naibu Spika wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, napenda
kumshukuru Mheshimiwa Sillo Daniel Baran (Mb), Mwenyekiti wa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na wajumbe wote wa Kamati
kwa ushauri wao mahiri wakati wa uandaaji wa taarifa nilizowasilisha
mbele ya Bunge lako Tukufu. - Mheshimiwa Spika, Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa
Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23
imeandaliwa kwa kuzingatia mwenendo wa viashiria vya uchumi
jumla na sekta mbalimbali kwa mwaka husika ikilinganishwa na
mwaka 2020. Aidha, maandalizi ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa
wa Mwaka 2022/23 yamezingatia vipaumbele vya Serikali
vilivyoainishwa katika Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa
Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi
Mkuu wa Mwaka 2020 na Hotuba ya Mheshimiwa Samia Suluhu
Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
akilihutubia rasmi Bunge hili la 12 la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tarehe 22 Aprili, 2021. Aidha, Mpango umezingatia Sera na
Mikakati mbalimbali ya kisekta, kikanda na kimataifa zikiwemo Dira
ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) 2050; Dira ya
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) 2050; Ajenda 2063
ya Maendeleo ya Afrika; na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.
5 - Mheshimiwa Spika, Katika kutekeleza Mpango wa mwaka
2022/23, msukumo mkubwa utawekwa katika sekta za uzalishaji
ambazo ni kilimo, mifugo, uvuvi na nishati kwa kuwa sekta hizi
huchochea uzalishaji kwa matumizi ya ndani na mauzo nje ya nchi,
hupunguza nakisi ya urari wa biashara, mfumuko wa bei na huzalisha
ajira zinazowagusa wananchi wengi. Sambamba na vipaumbele
hivyo, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi mingine ya
maendeleo ikiwemo miradi ya kielelezo ya ujenzi wa Reli kwa
Kiwango cha Kimataifa (SGR), ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme wa
Maji la Julius Nyerere – MW 2,115, uboreshaji wa Shirika la Ndege
Tanzania (ATCL) pamoja na miradi ya elimu, afya, maji, usafiri wa
anga na majini, bandari, maliasili na utalii, mapinduzi ya TEHAMA,
miundombinu ya barabara na madaraja na kuboresha mazingira ya
biashara na uwekezaji ili kukuza ustawi wa sekta binafsi nchini.
MWENENDO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2021
Uchumi wa Dunia - Mheshimiwa Spika, Taarifa ya Shirika la Fedha la Kimataifa
(IMF) ya Aprili 2022 inaonesha kuwa, uchumi wa dunia uliimarika na
kufikia wastani wa asilimia 6.1 mwaka 2021 ikilinganishwa na ukuaji
hasi wa asilimia 3.1 mwaka 2020. Kuimarika kwa uchumi wa dunia
kumetokana na hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa
na nchi mbalimbali katika kuimarisha uchumi, ikiwemo utekelezaji wa
sera za fedha na bajeti zinazochochea shughuli za uchumi
zilizoathirika na kuendelea kuimarishwa kwa huduma za afya ikiwemo
uhamasishaji na usambazaji wa chanjo kwa lengo la kupunguza
athari za UVIKO-19. Hata hivyo, uchumi wa dunia unatarajiwa
kupungua na kufikia ukuaji wa asilimia 3.6 mwaka 2022. Hii
inatokana na uwepo wa vita kati ya nchi ya Urusi na Ukraine ambayo
imesababisha kuongezeka kwa bei za vyakula na nishati hivyo,
6
kudhoofisha zaidi matarajio ya kurejea kwa shughuli za kiuchumi
zilizokuwa zimeathiriwa na UVIKO-19. Ikumbukwe kuwa Urusi ni nchi
ya pili kwa hifadhi/uzalishaji wa bidhaa za petroli duniani ambapo
inachangia wastani wa asilimia 12 katika mafuta yote yanayozalishwa
dunia ikitanguliwa na Marekani yenye mchango wa asilimia 20.
Aidha, Urusi ndiyo mzalishaji mkubwa wa nishati ya gesi na mafuta
inayotumika katika shughuli za kiuchumi barani Ulaya. Vilevile, kufikia
mwaka 2023 na kuendelea uchumi wa dunia unatarajiwa kupungua
zaidi na kufikia ukuaji wa wastani wa asilimia 3.3 kwa kipindi cha
muda wa kati iwapo vita kati ya Urusi na Ukraine vitaendelea pamoja
na kuendelea kuzidisha vikwazo vya kiuchumi kwa nchi ya Urusi.
Uchumi wa Afrika na Kikanda - Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, nchi za Kusini mwa
Jangwa la Sahara zilikuwa na ukuaji wa uchumi wa wastani wa
asilimia 4.5, ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 1.7 mwaka - Hii ilitokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa
ili kuimarisha ukuaji wa uchumi ikiwemo kuboresha huduma za afya
pamoja na kuimarika kwa bei za bidhaa zinazouzwa nje ya ukanda
huo baada ya kuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa ili kudhibiti
kuenea kwa ugonjwa wa UVIKO-19. Ukuaji wa uchumi katika ukanda
wa Kusini mwa Jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua na kufikia
wastani wa asilimia 3.8 mwaka 2022 na utaongezeka kufika wastani
wa asilimia 4.0 mwaka 2023. - Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, ukuaji wa Pato la nchi za
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ulikuwa asilimia 4.2
ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 4.3 mwaka 2020. Aidha,
ukuaji wa Pato la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ulikuwa asilimia
5.9 mwaka 2021 ikilinganishwa na ukuaji hasi wa asilimia 1.1 mwaka - Ukuaji chanya wa uchumi katika nchi wanachama wa jumuiya
hizo ulitokana na kulegezwa kwa masharti yaliyowekwa kwa ajili ya
7
kudhibiti maambukizi ya UVIKO–19 pamoja na hatua mbalimbali za
sera na kibajeti zilizochukuliwa kwa ajili ya kuchochea shughuli za
kiuchumi katika sekta zilizoathirika na ugonjwa huo.
Uchumi wa Taifa
Pato la Taifa - Mheshimiwa Spika, Ukuaji wa uchumi wa Taifa kwa kipindi
cha mwaka, 2021 ulikuwa asilimia 4.9 ikilinganishwa na ukuaji wa
asilimia 4.8 mwaka 2020. Kuongezeka kwa kiwango cha ukuaji wa
uchumi kumetokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea
kuchukuliwa na Serikali ikiwemo utekelezaji wa Mpango wa
Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO–19
na uwekezaji wa kimkakati hususan katika miundombinu ya nishati,
maji, afya, elimu, ujenzi wa barabara, reli na viwanja vya ndege.
Shughuli za kiuchumi zilizokuwa na ukuaji mkubwa katika kipindi cha
mwaka 2021 ni pamoja na Sanaa na Burudani (asilimia 19.4),
Umeme (asilimia 10.0), Uchimbaji Madini na Mawe (asilimia 9.6) na
Habari na Mawasiliano (asilimia 9.1). - Mheshimiwa Spika, Pato Ghafi la Taifa lilikuwa shilingi trilioni
161.5 mwaka 2021, ikilinganishwa na shilingi trilioni 151.2 mwaka - Aidha, mwaka 2021, Tanzania Bara ilikadiriwa kuwa na watu
milioni 57.7, ikilinganishwa na watu milioni 55.9 mwaka 2020. Kwa
mantiki hii, Wastani wa Pato kwa Mtu lilikadiriwa kufikia shilingi
2,798,224.23, sawa na dola za Marekani 1,211.77 mwaka 2021
ikilinganishwa na shilingi 2,701,039.25, sawa na dola za Marekani
1,171.51 mwaka 2020.
Mwenendo wa Bei - Mheshimiwa Spika, Mfumuko wa Bei umeendelea kuwa
ndani ya lengo la wigo wa asilimia 3 hadi 5. Mwaka 2021, mfumuko
8
wa bei uliongezeka na kufikia wastani wa asilimia 3.7 kwa mwaka
ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.3 katika kipindi cha mwaka - Aidha, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 3.8 Aprili
2022 ikilinganishwa na asilimia 3.3 Aprili 2021. Kuongezeka kwa
mfumuko wa bei kulichangiwa na sababu zilizo nje ya udhibiti wa
Serikali zikiwemo kuvurugika kwa mnyororo wa uzalishaji na
usambazaji wa bidhaa na huduma katika soko la dunia kutokana na
athari za vita baina ya Urusi na Ukraine.
Utekelezaji wa Sera ya Fedha 2021/22 - Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, malengo ya sera
ya fedha yalikuwa ni kama ifuatavyo:
(i) Ukuaji wa fedha taslimu (M0) wa wastani wa asilimia 9.9;
(ii) Ukuaji wa ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) wa
asilimia 10.0;
(iii) Ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi wa wastani wa asilimia
10.6; na
(iv) Kuwa na akiba ya fedha za kigeni inayotosha kuagiza bidhaa na
huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi kisichopungua miezi
minne. - Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania
imeendelea kutekeleza sera ya fedha yenye lengo la kuongeza
ukwasi katika uchumi, ili kuchochea ukuaji wa mikopo kwa sekta
binafsi na kusaidia kuimarisha shughuli mbalimbali za kiuchumi
zilizokuwa zimeathiriwa na janga la UVIKO-19, hali iliyosaidiwa na
mfumuko mdogo wa bei ulioendelea kubaki ndani ya lengo la asilimia
3 hadi 5. Ili kufanikisha jukumu hili, Benki Kuu ya Tanzania imekuwa
ikitumia nyenzo mbalimbali za sera ya fedha kwa ajili ya kuongeza
ukwasi katika sekta ya benki, ikiwemo kutoa mikopo ya muda mfupi
kwa mabenki, kununua fedha za kigeni kwenye soko la jumla, na
9
kuingia mikataba ya kubadilishana fedha za kigeni na mabenki
(foreign exchange swap). Vilevile, Benki Kuu ilichukua hatua za ziada
za kisera kwa ajili ya kuchochea ongezeko la mikopo nafuu kwa sekta
binafsi, hususan shughuli za kilimo. Aidha, kufuatia athari za vita vya
Ukraine ambayo imeongeza changamoto ya kuvurugika kwa
minyororo ya ugavi na kusababisha kuongezeka kwa bei ya mafuta
katika soko la dunia, pamoja na bei ya vyakula kama ngano na
mafuta ya kula, imesababisha kuongeza kwa mfumuko wa bei ya
bidhaa hizo nchini na kuhatarisha kupanda zaidi kwa mfumuko wa
bei. Hali hii imeilazimu Benki Kuu kuanza kupunguza kiasi cha ukwasi
inachoongeza kwenye uchumi ili kuanza kudhibiti hatari ya kuanza
kuongezeka kwa kasi ya mfumuko wa bei nchini.
Ujazi wa Fedha na Karadha - Mheshimiwa Spika, sambamba na utekelezaji wa sera ya
fedha inayolenga kuongeza ukwasi, ujazi wa fedha umeendelea
kukua kwa kasi ya kuridhisha. Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili
2022, wastani wa fedha taslimu uliongezeka kwa asilimia 13.8
ikilinganishwa na asilimia 2.7 katika kipindi kama hicho mwaka
uliotangulia, na lengo la wastani wa asilimia 9.9 kwa mwaka
2021/22. Vilevile, ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) ulikua
kwa wastani wa asilimia 13.1, ikilinganishwa ukuaji wa asilimia 6.8 na
lengo asilimia 10. Ongezeko hili la ukwasi kwenye uchumi limesaidia
shughuli mbalimbali za uchumi zilizokuwa zimeathirika na UVIKO-19
kuanza kufunguka kwa ujumla na kuongeza mchango kwenye Pato la
Taifa.
Mwenendo wa Mikopo kwa Sekta Binafsi - Mheshimiwa Spika, mikopo kwa sekta binafsi imeendelea
kukua kwa kasi ya kuridhisha kutokana na sera wezeshi za fedha na
bajeti, pamoja na hatua zinazoendelea kutekelezwa na serikali
10
kuboresha mazingira ya biashara, na utekelezaji wa hatua za kisera
zilizochukuliwa na Serikali kupitia Benki Kuu zenye lengo la
kuchochea ukuaji wa mikopo na kushusha viwango vya riba za
mikopo. Mikopo kwa sekta binafsi ilikua kwa wastani wa asilimia 8.4
katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022 ikilinganishwa na ukuaji
wa wastani wa asilimia 4.3 katika kipindi kama hicho mwaka
2020/21, na lengo la ukuaji wa asilimia 10.6 kwa mwaka 2021/22.
Miezi ya hivi karibuni kasi ya ukuaji wa mikopo imeongezeka na
kufikia asilimia 13.4 kwa mwaka ulioishia Aprili 2022. Sehemu kubwa
ya mikopo ilielekezwa katika shughuli binafsi ambazo zilipata asilimia
39.3 ya mikopo yote, ikifuatiwa na shughuli za biashara asilimia 16.7,
uzalishaji viwandani asilimia 10.1 na kilimo asilimia 7.9. Ni matarajio
ya serikali kuwa lengo la wastani wa asilimia 10.6 kwa mwaka
2021/22 litafikiwa kufuatia hatua za kisera na maboresho ya
mazingira ya biashara yanayoendelea kutekelezwa nchini.
Mwenendo wa viwango vya riba - Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa sera ya fedha
yamesaidia kudumisha kiwango cha kutosha cha ukwasi katika sekta
ya benki, na kupelekea utulivu wa riba za masoko ya fedha ya muda
mfupi katika viwango vya chini. Mathalani, riba ya siku moja katika
soko la fedha baina ya mabenki (overnight interbank cash market
interest rate) ilipungua hadi kufikia wastani wa asilimia 3.42 katika
kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, kutoka wastani wa asilimia
3.60 katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21. Vilevile, riba ya
dhamana za muda mfupi (Overall Treasury bills rate) ilipungua hadi
wastani wa asilimia 4.17 kutoka wastani wa asilimia 4.62 katika
kipindi kama hicho mwaka 2021. - Mheshimiwa Spika, wastani wa riba za mikopo ya benki kwa
sekta binafsi kwa ujumla ulipungua japo kwa kasi ndogo hadi
asilimia 16.44 katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022,
11
ikilinganishwa na wastani wa asilimia 16.59 katika kipindi kama hicho
mwaka 2020/21. Aidha, wastani wa riba za amana kwa ujumla
ulikuwa asilimia 6.85 katika, ikilinganishwa na wastani wa asilimia
6.70. Ni matarajio yetu kuwa hatua za kisera zinazoendelea
kuchukuliwa na Serikali kupitia Benki Kuu zitasaidia kuendelea
kupungua kwa riba za mikopo nchini na kusaidia kukuza uchumi wa
nchi na mazingira bora zaidi ya kufanya biashara.
Sekta ya Nje - Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka kinachoishia
Aprili 2022, thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ilifikia dola
za Marekani bilioni 10.62 kutoka dola za Marekani bilioni 8.56 katika
kipindi kama hicho mwaka 2021. Ongezeko hili kubwa lilitokana na
kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa zisizo asilia pamoja na mapato
yatokanayo na shuguli za utalii ikiwa ni matokeo ya hatua
zilizochukuliwa na mataifa mengine duniani kufungua mipaka yao
kuruhusu safari za kimataifa kutokana na kupungua kwa maambukizi
ya UVIKO-19. Aidha, katika kipindi hicho, thamani ya bidhaa na
huduma zilizoagizwa kutoka nje ilifikia dola za Marekani bilioni 13.29,
ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni 9.27 katika kipindi kama
hicho mwaka 2021. Ongezeko hilo linatokana na kuongezeka kwa
uagizaji wa bidhaa za walaji hususan petroli na dawa ambapo
thamani ya petroli iliongezeka kwa kiwango kikubwa kutokana na
ongezeko la bei katika Soko la Dunia pamoja na kiwango
kilichoagizwa katika kipindi hicho. - Mheshimiwa Spika, Thamani ya mauzo ya bidhaa iliongezeka
kufikia dola za Marekani bilioni 7.03 katika kipindi cha mwaka
kinachoishia Aprili 2022 ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni
6.36 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Ongezeko hilo lilitokana
na kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa asilia na zisizo asilia ikiwemo,
bidhaa za maua na mbogamboga, saruji, bidhaa za plastiki, vipodozi
12
pamoja na nafaka hususan mchele na mahindi. Aidha, thamani ya
bidhaa zilizoagizwa kutoka nje ziliongezeka kutoka dola za Marekani
bilioni 8.06 katika kipindi cha mwaka unaoishia Aprili 2021 hadi dola
za Marekani bilioni 11.09 Aprili 2022. Hali hiyo ilitokana na
kuongezeka kwa uagizaji wa malighafi, bidhaa za viwandani,
mitambo na bidhaa za petroli. - Mheshimiwa Spika, mapato yatokanayo na huduma
yaliongezeka na kufikia dola za Marekani bilioni 3.59 kwa mwaka
unaoishia Aprili 2022, ikilinganishwa na dola za Marekani bilioni 2.20
katika kipindi kama hicho mwaka 2021, ongezeko hili lilichangiwa na
idadi kubwa ya watalii waliongia nchini katika kipindi husika. Aidha,
katika kipindi husika malipo ya huduma yaliongezeka kutoka dola za
Marekani bilioni 1.22 na kufikia dola za Marekani bilioni 2.20.
Ongezeko hili lilichangiwa na ongezeko la gharama za mizigo
sambamba na ongezeko la gharama za uagizaji wa mafuta.
Akiba ya Fedha za Kigeni - Mheshimiwa Spika, akiba ya fedha za kigeni imeendelea
kuwa ya kuridhisha kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na
huduma kutoka nje ya nchi. Hadi kufikia Aprili 2022, akiba ya fedha
za kigeni ilikuwa dola za Marekani bilioni 5.46 ambayo inatosheleza
uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi cha
takriban miezi 4.8. Mahitaji ya nchi kisheria ni kuwa na kiasi cha
fedha za kigeni kinachotosheleza uagizaji wa bidhaa na huduma
kutoka nje ya nchi kwa muda usiopungua miezi 4.0. Aidha, kiwango
kilichopo kinakidhi pia lengo la kuwa na miezi isiyopungua 4.5 kwa
nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mwenendo wa Thamani ya Shilingi - Mheshimiwa Spika, thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya
13
dola ya Marekani imeendelea kuwa tulivu, ambapo dola moja ya
Marekani ilibadilishwa kwa wastani wa shilingi 2,308.87 katika soko la
jumla kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, ikilinganishwa na
wastani wa shilingi 2,309.48 katika kipindi cha Julai 2020 hadi Aprili - Hii ni sawa na kuongezeka kwa thamani ya shilingi
(appreciation) kwa wastani wa asilimia 0.03. Hali hii imechangiwa
kwa kiasi kikubwa na kuwepo kwa akiba ya kutosha ya fedha za
kigeni, utulivu wa mfumuko wa bei nchini, mwendelezo wa nakisi
ndogo katika urari wa biashara ya bidhaa, huduma na uhamishaji
mali nchi za nje, pamoja na utekelezaji wa sera thabiti za fedha na
bajeti.
Mwenendo wa sekta ya kibenki - Mheshimiwa Spika, sekta ya kibenki nchini imeendelea
kubaki imara, stahimilivu na yenye kutengeneza faida ikiwa na mtaji
na ukwasi wa kutosha. Hadi kufikia mwezi Aprili 2022, rasilimali za
benki zilifikia kiasi cha Shilingi bilioni 40,198.2, sawa na ongezeko la
asilimia 12.9 ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka jana. Aidha,
amana za benki ziliongezeka hadi kufikia kiasi cha Shilingi bilioni
28,603.3, sawa na ongezeko la asilimia 11.8, ikilinganishwa na kipindi
kama hiki mwaka 2020/21. Vilevile, hali ya mitaji ya mabenki na
ukwasi vimeendelea kuimarika hadi kufikia faida ya mtaji ya asilimia
18.4 Aprili 2022, ikilinganishwa na faida ya asilimia 10.3 kipindi kama
hiki mwaka 2020/21. - Mheshimiwa Spika, benki zimeendelea kuongeza utoaji wa
huduma za kibenki kwa wananchi wengi zaidi kwa kutumia mifumo
ya kielektroniki yenye gharama nafuu. Kwa upande mwingine, Benki
Kuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa benki na taasisi za fedha
nchini kwa kutekeleza sera wezeshi na kutoa kanuni na miongozo
mbalimbali ili kulinda uimara wa sekta hiyo. Vilevile, benki
zimeelekezwa kutekeleza mipango ya kuongeza mitaji juu ya kiwango
14
kinachotakiwa kisheria, ili kuongeza uwezo kwenye utoaji wa mikopo
kwa sekta binafsi na huduma nyingine za benki. - Mheshimiwa Spika, sekta ya benki inatarajiwa kubaki salama
na tulivu, sambamba na sera zinazotekelezwa na hatua
zinazochukuliwa na Serikali pamoja na Benki Kuu ya Tanzania katika
kuboresha mazingira ya biashara na ufanisi katika utoaji wa huduma
za fedha nchini. Aidha, Benki Kuu imeendelea kuimarisha jitihada za
kupunguza kiwango cha mikopo chechefu ambapo, hadi kufikia
mwezi Aprili 2022 kiwango cha mikopo chechefu kilipungua kufikia
asilimia 8.23 ikilinganishwa na asilimia 9.77 mwezi Aprili 2021. Benki
Kuu ya Tanzania inaendelea kufuatilia kwa karibu mikakati ya
mabenki katika kupunguza mikopo chechefu hadi kufikia kiwango
kisichozidi asilimia 5.
Deni la Serikali - Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, deni la Serikali lilikuwa
shilingi trilioni 69.44 ikilinganishwa na shilingi trilioni 60.72 kipindi
kama hicho mwaka 2021, sawa na ongezeko la asilimia 14.4. Kati ya
kiasi hicho, deni la nje lilikuwa shilingi trilioni 47.07 na deni la ndani
lilikuwa shilingi trilioni 22.37. Ongezeko la deni la Serikali lilitokana na
kupokelewa kwa mikopo mipya kutoka vyanzo vyenye masharti nafuu
na ya kibiashara kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo. Aidha,
ongezeko la deni lilitokana na kutolewa kwa hatifungani maalumu
yenye thamani ya shilingi trilioni 2.18 kwa ajili ya deni la Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) lililotokana na
michango ya watumishi wa kabla ya mwaka 1999. Taarifa ya tathmini
ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Novemba 2021 inaonesha kuwa deni
la Serikali bado ni himilivu katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na
mrefu kwa kuzingatia ukomo wa viashiria vyote vinavyokubalika
kimataifa.
15
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO
WA TAIFA WA MWAKA 2021/22 - Mheshimiwa Spika, kama unavyofahamu Serikali imekuwa
ikitekeleza Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22
ambao ni Mpango wa Kwanza katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu
wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 wenye
dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya
Watu. Kutokana na usimamizi thabiti wa Serikali chini ya Mheshimiwa
Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
utekelezaji wa Mpango umekuwa na mafanikio makubwa katika
nyanja zote ikiwemo kiuchumi, miundombinu, kijamii na uwekezaji.
Mafanikio yaliyopatikana katika sekta mbalimbali ni pamoja na:
(i) Miundombinu ya Reli: Kuendelea na ujenzi wa Reli ya Kati
ya Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway – SGR)
ambapo kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro (km 300)
utekelezaji umefikia asilimia 96.54 na kipande cha Morogoro –
Makutupora (km 422) asilimia 85.02; kusainiwa kwa mkataba
wa ujenzi wa kipande cha Makutupora – Tabora (km 368);
kuendelea na ununuzi wa mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa njia
ya reli kwa kipande cha Tabora – Isaka (km 165); kuendelea na
ununuzi wa injini, mabehewa na vifaa vya matengenezo ya njia
ya reli; na kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali
kwa ajili ya ujenzi wa njia za reli za Tabora – Kigoma (km 411),
Uvinza – Musongati – Gitega (km 282) na Kaliua – Mpanda –
Karema (km 321) kwa kiwango cha Standard Gauge. Mafanikio
mengine ni: Kukamilika kwa ukarabati wa njia ya reli ya Tanga
– Moshi – Arusha (km 470); kukamilika kwa ukarabati wa
mabehewa ya mizigo 200 yanayotumika kutoa huduma ya
usafiri kwa njia ya reli ya Meter Gauge iliyopo; kukamilika kwa
uundaji wa vichwa vya injini saba (7) vya sogeza; na
kupokelewa kwa vichwa vya treni vitatu (3), mabehewa 44 ya
16
mizigo na mtambo wa kupima ubora wa njia ya reli.
(ii) Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere – MW
2,115: Kuendelea na ujenzi wa tuta kuu la bwawa ambapo
utekelezaji umefikia asilimia 62.01, njia za kupitisha maji ya
kufua umeme asilimia 74.16, nyumba ya mitambo ya kufua
umeme asilimia 44.22, kingo za bwawa asilimia 42.82 na kituo
cha kupokea na kusafirisha umeme kV 400 asilimia 75.44. Kwa
ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 60.22.
(iii) Uboreshaji wa Shirika la Ndege Tanzania: Kupokelewa
kwa ndege tatu (3) ambapo ndege moja (1) ni aina ya Dash 8
Q400 na mbili (2) ni aina ya Airbus A220 300; kufanyika kwa
malipo ya awali ya ununuzi wa ndege tano (5) mpya ambapo
ndege moja (1) aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili
(2) aina ya Boeing 737-9, ndege moja (1) aina ya De Havilland
Dash 8-Q400 na ndege moja (1) ya mizigo aina ya Boeing 767-
300F; kuendelea na ukarabati wa karakana ya matengenezo ya
ndege ya KIMAFA katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa
Kilimanjaro (KIA); kuanzisha safari katika vituo vitatu (3) vipya
vya nje ya nchi vya Lubumbashi, Nairobi na Ndola; kurejesha
safari za ndani na nje kwa abiria; kuanzisha safari za mizigo za
kwenda Guangzhou; na kutolewa kwa mafunzo kwa marubani
102 na wahudumu 108 wa ndani ya ndege.
(iv) Miradi ya Umeme: kuendelea na ujenzi wa mradi wa kufua
umeme wa Rusumo – MW 80 ambapo utekelezaji umefikia
asilimia 91.6; kuendelea na utekelezaji wa mradi wa Kinyerezi I
Extension MW 185 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 88;
kukamilika kwa ujenzi wa vituo vya kupooza umeme vya
Singida na Dodoma katika mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
wa Msongo wa kV 400 Iringa – Singida – Shinyanga (Backbone
Transmission Investment Project – BTIP II); kuendelea na
17
ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa kV 400 Singida –
Arusha – Namanga ambapo utekelezaji umefikia asilimia 96.1;
kuendelea na ujenzi wa njia ya usafirishaji wa umeme wa kV
400 kutoka Rufiji – Chalinze – Kinyerezi – Dodoma ambapo
utekelezaji umefikia asilimia 37; kuendelea na ujenzi wa mradi
wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa kV 220 (Rusumo
– Nyakanazi) ambapo ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
umefikia asilimia 61 na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha
Nyakanazi umefikia asilimia 95; na kuunganishwa umeme kwa
jumla ya vijiji 8,688 kati ya vijiji 12,345 sawa na asilimia 70.4
ya vijiji vyote Tanzania Bara.
(v) Ujenzi na Ukarabati wa Viwanja vya Ndege: kusainiwa
kwa mkataba kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Msalato awamu ya kwanza itakayohusisha ujenzi
wa njia ya kuruka na kutua ndege pamoja na jengo la abiria;
kukamilika kwa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Geita;
kukamilika kwa upanuzi wa njia ya kutua na kuruka ndege na
kufungwa kwa mfumo wa kuongoza ndege katika Kiwanja cha
Ndege cha Dodoma; kukamilika kwa usanifu na kuendelea na
maandalizi ya ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha
Ndege cha Mwanza; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa
viwanja vya ndege vya Songea (asilimia 96), Mtwara (asilimia
89), Iringa (asilimia 44.65), Songwe (asilimia 95) na Musoma
(asilimia 10); kuendelea na maandalizi ya ujenzi na upanuzi wa
viwanja vya ndege vya Shinyanga, Kigoma, Tabora na
Sumbawanga vitakavyogharimu Euro milioni 50 sawa na shilingi
bilioni 136.85.
(vi) Uendelezaji wa Bandari: Bandari ya Dar es Salaam:
Kuboreshwa kwa gati namba 1 – 7; na kukamilika kwa ujenzi
wa gati maalumu la kuhudumia meli za magari (RoRo) na yadi
ya kuhudumia makasha. Bandari ya Mtwara: kukamilika kwa
18
ujenzi wa gati moja lenye urefu wa mita 300; na kuendelea na
ujenzi wa uzio na sakafu ngumu katika eneo la mita za mraba
75,807. Bandari ya Tanga: kukamilika kwa uongezaji wa kina
kwenye lango la kuingia meli kutoka mita nne (4) hadi mita 13
pamoja na kuweka vifaa vya kuongoza meli.
Bandari za Maziwa Makuu: Ziwa Victoria: Kukamilika kwa
ujenzi wa magati ya Nyamirembe, Magarine, Lushamba, Ntama
na Mwigobero pamoja na gati mbili (2) za majahazi katika
bandari ya Mwigobero. Ziwa Tanganyika: kukamilika kwa
ujenzi wa magati ya Kagunga, Sibwesa na Kabwe (Nkasi);
kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya Lagosa pamoja na
upanuzi wa bandari ya Kasanga; na kuendelea na ujenzi wa
Bandari za Karema, Kibirizi, Kigoma na Ujiji. Ziwa Nyasa:
kukamilika kwa ujenzi wa sakafu ngumu katika bandari ya
Kiwira na Itungi; na kukamilika kwa ujenzi wa gati na
miundombinu yake katika bandari ya Ndumbi.
(vii) Kuboresha Huduma za Usafiri na Usafirishaji wa Abiria
na Mizigo katika Maziwa Makuu
Kukamilika kwa ukarabati wa meli mbili (2) za New Butiama
Hapa Kazi Tu na New Victoria Hapa Kazi Tu; kuendelea na
ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza Hapa kazi Tu yenye uwezo
wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo ambao umefikia
asilimia 66; na kukamilika kwa ujenzi wa chelezo cha kujengea
na kukarabati meli katika Bandari ya Mwanza chenye uwezo wa
kubeba meli au chombo chenye uzito kuanzia tani moja (1)
hadi tani 4,000.
(viii) Barabara na Madaraja Makubwa: Kujengwa kwa mtandao
wa barabara kwa kiwango cha lami wenye urefu wa kilomita
216.26; na kukarabatiwa kwa kiwango cha changarawe jumla
ya kilomita 1,124.3 za barabara za mikoa. Kwa upande wa
19
barabara zinazosimamiwa na TARURA, jumla ya kilometa
232.94 za lami, kilomita 8,181.65 za changarawe, madaraja
405 na makalvati 206 yamejengwa. Miradi iliyokamilika ni
pamoja na: ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami sehemu
za Tabora – Nyahua (km 85), Nyahua – Chaya (km 85.4) na
Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35); barabara za Mbeya –
Lwanjilo (km 36) na Lwanjilo – Chunya (km 36), sehemu ya
Chunya – Makongolosi (km 39); na barabara za Mtwara –
Mnivata (km 50). Barabara zinazoendelea ni pamoja na ujenzi
sehemu ya Lusitu – Mawengi (km 50) ambapo utekelezaji
umefikia asilimia 83.79, Kidatu – Ifakara (km 68) asilimia 54.5,
Makutano – Sanzate (km 50) asilimia 94.1, Mto wa Mbu –
Loliondo sehemu ya Waso – Sale Jct (km 50) asilimia 98, na
Moronga – Makete (km 53.5) umefikia asilimia 86. Aidha,
Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya mzunguko katika jiji la
Dodoma (Dodoma outer ring road) yenye urefu wa kilometa
(112.3) na kuendelea na maandalizi ya upanuzi wa barabara
kutoka Dodoma kwenda Singida (km 50), Dodoma – Iringa (km
50), Dodoma – Arusha (km 50) na Dodoma – Morogoro (km
70).
Kwa upande wa madaraja hatua zilizofikiwa ni: kuzinduliwa na
kuanza kutumika kwa daraja la Tanzanite Dar es Salaam;
kuanza kutumika kwa daraja la Kiyegeya (Morogoro); na
kuendelea na ujenzi wa madaraja ya Kitengule (Kagera)
ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90; Wami (Pwani) asilimia
72.88; Msingi (Singida) asilimia 82; Lower Malagarasi asilimia
65; na ujenzi wa daraja la Kigongo – Busisi umefikia asilimia
40.2.
(ix) Huduma za Afya: Kuendelea na ujenzi wa Hospitali za
Halmashauri 127, ujenzi wa vituo vya afya 70, ukamilishaji wa
maboma ya zahanati 564; kukamilika kwa ukarabati wa wodi
20
namba 18 katika jengo la Sewa Haji katika haspitali ya Taifa
Muhimbili kwa ajili ya wodi za kulaza wagonjwa binafsi;
kukamilika kwa ujenzi na ufungaji wa mtambo wa kuzalisha
tiba hewa (Oxygen generating plant) katika hospitali ya Taifa
Muhimbili – Mloganzila; kukamilika kwa ujenzi wa maabara
maalumu na ufungaji wa mtambo wa kisasa (Angio-Suite)
katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili – MOI; kukamilika kwa wodi
ya watoto katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete; ukarabati
wa jengo la wagonjwa mahututi (asilimia 70), chumba cha
kufunga mashine ya MRI (asilimia 80) na kujengwa kwa kituo
cha habari kwa magonjwa ya saratani (Patient Information
Centre) katika Taasisi ya Saratani Ocean Road; ukarabati wa
jengo la wagonjwa mahututi katika hospitali ya rufaa ya
magonjwa ya kifua kikuu Kibong’oto; ukarabati wa chumba cha
X-ray na Utra-sound katika hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili
Mirembe; kujengwa kwa majengo ya kutolea huduma za afya
ya Mama na Mtoto (Maternal and Newborn Wing) katika
hospitali ya Rufaa Kanda ya Mashariki CCBRT; kuendelea na
ujenzi wa wodi za wagonjwa wa saratani (asilimia 57) na kliniki
ya wagonjwa wa macho (asilimia 65) katika hospitali ya rufaa
kanda ya ziwa Bugando; kuendelea na ujenzi wa vyumba nane
(8) vya upasuaji (asilimia 80) katika hospitali ya kanda ya
kaskazini (KCMC); kuendelea na ujenzi wa jengo la ghorofa sita
(6) la afya ya uzazi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 93
katika hospitali ya rufaa Mbeya; kuendelea na ujenzi wa jengo
la kuhudumia wagonjwa wa UVIKO – 19 (asilimia 95) katika
hospitali ya rufaa Shinyanga; kununuliwa na kusambazwa kwa
chanjo za polio, surua, rubella, kifaduro, pepopunda, homa ya
ini, homa ya uti wa mgongo na kichomi na chanjo dhidi ya
UVIKO – 19.
(x) Elimu: Kuendelea kutekeleza Sera ya elimumsingi bila ada ili
kuongeza fursa za elimu nchini ambapo hadi Aprili 2022,
21
Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 244.5; kuchapishwa na
kusambazwa kwa vitabu vya kiada 15,609,515 na kiongozi cha
mwalimu 538,006 kwa masomo yote ya Darasa la VI na VII ili
kuimarisha uwiano kati ya mwanafunzi na kitabu; kuendelea na
ujenzi wa shule mpya 232 za Sekondari za kata katika kata
zisizokuwa na shule za Sekondari; ujenzi wa shule 10 kati ya
lengo la shule 26 maalumu za bweni za wasichana kwa
masomo ya Sayansi; kutolewa kwa mafunzo kazini kwa walimu
10,000 wa sekondari wa masomo ya hisabati na sayansi;
kuwezesha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuchapisha na
kusambaza miongozo ya masomo tisa (9); kukusanywa kwa
mikopo ya shilingi bilioni 156.81 kutoka kwa wanufaika wa
mikopo iliyoiva na kugharamia mikopo yenye thamani ya
shilingi bilioni 569.0 kwa wanafunzi 177,777; na kuimarishwa
kwa Tume ya Nguvu za Atomiki kwa kuendelea na ujenzi wa
awamu ya pili wa maabara changamano.
(xi) Maji Mijini na Vijijini: Upatikanaji wa huduma ya maji hadi
Aprili 2022 umefikia wastani wa asilimia 74.5 vijijini kutoka
asilimia 72.3 Juni, 2021 na mijini asilimia 86.5 kutoka asilimia
86 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Baadhi ya miradi
iliyotekelezwa na hatua zilizofikiwa ni: kuendelea kwa ujenzi wa
mradi wa maji katika mji wa Kigoma (asilimia 95), Arusha
(asilimia 80) na mradi wa Mugango – Kiabakari – Butiama
(asilimia 42). Aidha, katika eneo linalohudumiwa na DAWASA
(mikoa ya Dar es Salaam na Pwani) utekelezaji wa miradi
umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95. Vile vile, Serikali imeanza
hatua za kutafuta suluhu ya kudumu ya tatizo la maji katika
majiji ya Dodoma na Dar es Salaam kwa kutekeleza miradi ya
Bwawa la Kidunda, bwawa la Farkwa na mradi mkubwa wa
maji kutoka ziwa Victoria hadi Dodoma.
(xii) Kilimo, Mifugo na Uvuvi
22
Kilimo: Kuzalishwa kwa mbegu bora tani 35,199.39 na miche
32,301,995 ya mazao mbalimbali; kutolewa kwa pikipiki 7,000
kwa Maafisa ugani kwa ajili ya kuimarisha huduma za ugani;
kupatikana kwa mbolea tani 436,452; kuanzishwa kwa
mashamba 67 yenye ukubwa wa hekta 205,432.45 ambayo kila
moja lina ukubwa wa kuanzia hekta 20; kuhakikiwa na
kutambuliwa kwa mashamba matano (5) ya NAFCO yenye
ukubwa wa ekari 18,980; kukamilika kwa upembuzi yakinifu na
usanifu wa kina katika skimu tatu (3) za umwagiliaji za
Mkombozi (Iringa), Idudumo (Nzega) na Ilemba
(Sumbawanga); kutolewa kwa mafunzo kwa maafisa ugani
2,486 kuhusu kilimo bora cha alizeti na pamba katika mikoa ya
Dodoma, Singida, Simiyu, Kilimanjaro, Kigoma na Manyara;
kukamilika kwa ukarabati wa ghala lenye uwezo wa kuhifadhi
tani 1,000 za mazao katika Wilaya ya Kiteto; kukamilika kwa
ukarabati wa vihenge vyenye uwezo wa kuhifadhi tani 38,000
katika Mkoa wa Arusha na ghala la Mbugani – Dodoma lenye
uwezo wa kuhifadhi tani 30,000 za nafaka; kutolewa kwa vibali
681 kwa wafanyabiashara wa viuatilifu; kuendelea na ujenzi wa
kiwanda cha mbolea cha FOMI Mkoani Dodoma chenye uwezo
wa kuzalisha tani 600,000 kwa mwaka; NFRA na CPB
zilifanikiwa kununua mahindi ya wakulima ambapo kiasi cha
shilingi bilioni 114 zilitumika; na kufanyika kwa majaribio 88 ya
kisayansi (bioefficacy field trials) kwa viuatilifu vipya.
Mifugo: Kuendelea na tafiti na tathmini za teknolojia bora za
ng’ombe chotara wa maziwa na uzalishaji wa nyama;
kukamilika kwa ujenzi wa majosho 95 katika mamlaka
mbalimbali za Serikali za Mitaa; kuanza kwa ujenzi wa majosho
73 katika halmashauri 58; kuzalishwa na kusambazwa kwa dozi
43,409,600 za chanjo dhidi ya magonjwa ya Mdondo, Homa ya
Mapafu ya Ng’ombe na Mbuzi, Kimeta, Chambavu,
23
Mchanganyiko wa Kimeta na Chambavu na Kutupa Mimba;
kuzalishwa kwa jumla ya dozi 50,261 za mbegu za mifugo na
kusambazwa kwa dozi 31,380 katika mikoa 19 kwa ajili ya
uhimilishaji; kununuliwa na kusambazwa kwa jumla ya pikipiki
300 ili kurahisisha utoaji wa huduma za ugani kwa Mamlaka za
Serikali za Mitaa; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa
miundombinu ya mifugo katika minada 18 nchini; kulimwa kwa
hekta 800 za malisho ya mifugo katika ranchi za Kongwa, Ruvu
na West Kilimanjaro; na kuzalishwa kwa jumla ya ndama 3,119
katika Ranchi za Kikulula, Misenyi, Kongwa, Ruvu, Mkata, West
kilimanjaro, Mzeri na Kalambo.
Uvuvi: kusainiwa kwa Mkataba na Mkandarasi China Harbour
Engineering Co. Ltd kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya uvuvi
katika eneo la Kilwa Masoko, Lindi; kuendelea na maandalizi ya
ununuzi wa meli mbili (2) za uvuvi kati ya nne (4)
zilizopangwa; kukamilika kwa mpango biashara wa ufufuaji wa
Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO); kujenga ofisi tano (5)
katika Halmashauri tano (5) kwa ajili ya kuimarisha vikundi vya
ulinzi shirikishi wa rasilimali za uvuvi; kufanyika kwa kaguzi
1,863 za kuhakiki ubora na usalama wa samaki na mazao ya
uvuvi kwenye viwanda vya kuchakata samaki, mialo, magari ya
kusafirisha samaki, maghala ya kuhifadhi samaki na masoko ya
samaki; kujenga na kuimarisha miundombinu ya mialo na
masoko ikiwemo kukamilika kwa ujenzi wa baadhi ya mialo na
kuendelea na ujenzi wa mialo pamoja na ujenzi wa soko la
samaki la Mbamba Bay; kuvuliwa kwa tani 324,752.45 za
samaki zenye thamani ya shilingi trilioni 2.18; kuuzwa nje kwa
tani 34,841.72 za samaki na Samaki hai 169,089 wa mapambo
wenye thamani ya shilingi bilioni 475.01; kujengwa kwa
maabara ya utafiti wa uvuvi katika kituo cha TAFIRI – Dar es
Salaam; na kufanyika kwa tafiti mbalimbali za mazao ya samaki
ikiwemo tafiti kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na
24
ongezeko la tindikali baharini.
(xiii) Uendelezaji wa Viwanda: Katika kutekeleza mkakati wa
kuendeleza sekta ya viwanda kwa kuweka mazingira wezeshi,
hatua iliyofikiwa ni pamoja na: kuendelea na majadiliano na
wawekezaji watakaowekeza kwenye miradi ya msingi mitatu
(3) katika eneo maalumu la uwekezaji Bagamoyo ambayo ni
Bandari ya kisasa (Modern Seaport Component), sehemu ya
kanda maalumu kwa ajili ya mizigo na usafirishaji (Logistics
Park) na sehemu ya mji wa viwanda (Port side Industrial City);
kukamilika kwa ujenzi wa mabwawa manne (4) ya kuvuna na
kuhifadhi maji yenye uwezo wa kuhifadhi maji ya mita za ujazo
1,750,000 na kuendelea na upanuzi wa mashamba ya miwa
katika kiwanda cha Sukari Mbigiri ambapo utekelezaji wa mradi
umefikia asilimia 75 kwa upande wa mashamba ya miwa na
asilimia 45 kwa upande wa ujenzi wa kiwanda; kuendelea
kuimarisha Sekta Ndogo za ngozi, nguo na mavazi, chuma na
bidhaa za chuma, mbolea na kemikali za viwandani na
uchakataji wa bidhaa zinazotokana na kilimo kama vile mafuta
ya kula, korosho, matunda, maziwa na bidhaa za maziwa.
Aidha, kupitia maonesho ya Dubai Expro Serikali ilifanikiwa
kusaini mikataba 36 ya uwekezaji yenye thamani ya shilingi
trilioni 17 pamoja na mikataba yenye thamani ya shilingi trilioni
11.7 ilisainiwa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais ya uzinduzi
wa filamu ya Royal Tour.
(xiv) Madini: kukamilika kwa ujenzi wa vituo vitatu (3) vya umahiri
katika shughuli za uchimbaji madini vya Chunya, Songea na
Mpanda; kuanzishwa kwa masoko mapya manne (4) ya madini
na vituo vipya nane (8) vya ununuzi wa madini, hivyo kufanya
jumla ya masoko ya madini kuwa 42 na vituo vya ununuzi wa
madini kufikia 75; na kusainiwa kwa mikataba ya ubia kwa ajili
ya uwekezaji wa kiasi cha takribani dola za Marekani milioni
25
1,672.57 kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
na kampuni za Madini za: Nyanzaga (NMCL) kwa ajili ya
uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu na madini ambata ya
shaba, chuma, nickel, zinc na lead kwenye eneo lenye ukubwa
wa kilomita za mraba 23.36 Sengerema; Kampuni ya Jacana
Resources Limited (Strandline Resources Limited) kwa ajili ya
uchimbaji wa madini ya Heavy Mineral Sand (Beach Sands)
Kigamboni kwenye eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba
4.45; Kampuni ya Mahenge Resources Limited (Black Rock
Mining Ltd) kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya graphite; na
Kampuni ya Petra Diamond Ltd inayoendelea na uchimbaji wa
madini ya Almasi katika mgodi wa Williamson Diamonds Limited
eneo la Mwadui. Katika mikataba hiyo Serikali itamiliki asilimia
16 ya hisa za kila kampuni.
(xv) Habari, Mawasiliano na TEHAMA: kukamilika kwa ujenzi wa
Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa kilomita 409 ambapo
kilomita 72 zimeunganisha nchi ya Msumbiji kupitia mpaka wa
Mtambaswala, kilomita 72 zimeunganisha watumiaji wa mwisho
katika ofisi za Serikali za Msalato, Mtumba na Kikombo Dodoma
na kilomita 265 zimeunganisha Manyoni – Kambi katoto
(Chunya); kukamilika kwa ukarabati wa kilomita 105 za ujenzi
wa mkongo Arusha – Namanga kupitia miundombinu ya
TANESCO; kukamilika kwa uandaaji wa ramani za mipaka ya
kiutawala katika Halmashauri 20; na kuendelea na uwekaji wa
miundombinu ya anwani za makazi nchini.
Aidha, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa kuongeza
upanuzi na usikivu wa shirika la utangazaj TBC ambapo
shughuli zilizotekelezwa ni pamoja na: Kukamilika kwa ujenzi
wa jengo la kituo cha kurushia matangazo ya masafa ya FM
katika kituo cha Kisaki mkoani Morogoro; kukamilika kwa ujenzi
na ufungaji wa mitambo ya kituo cha Redio ya Jamii Makao
26
Makuu Jijini Dodoma; kuendelea na ujenzi na ufungaji wa
mitambo ya masafa ya FM katika mikoa mipya ya Njombe,
Songwe na Simiyu, sambamba na wilaya za Kilwa, Serengeti
pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba ambapo utekelezaji
umefikia asilimia 40; kununuliwa na kufungwa kwa mitambo
miwili (2) ya kurushia matangazo kwa njia ya Satelaiti (FLY
AWAY) pamoja na mtambo wa kurusha mubashara matangazo
ya redio kwa njia ya mtandao (LIVE U); na kukamilisha ujenzi
wa jengo la Studio na ununuzi wa vifaa vya Chaneli ya
Televisheni ya TBC 2 katika ofisi za Mikocheni Dar es Salaam.
(xvi) Maliasili na Utalii: Kuanzishwa kwa mara ya kwanza kwa
Programu ya Royal Tour iliyoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan
ambayo imelitangaza Taifa na utalii katika Nyanja za kimataifa;
kuongezeka kwa idadi ya watalii kutoka nje ya nchi kutoka
watalii 620,867 mwaka 2020 hadi watalii 922,692 mwaka 2021,
sawa na ongezeko la asilimia 48.6; Hifadhi ya Taifa Serengeti
ilitangazwa na shirika la Mainland Aggregates Limited la nchini
Marekani mwaka 2021 kuwa mshindi wa pili barani Afrika na
wa 12 duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watumiaji wa
mtandao wa kijamii wa instagram; kampuni 11 za uwekezaji
zilipatiwa maeneo ya kujenga huduma ya malazi ya hoteli za
hadhi ya kitalii katika Hifadhi za Taifa Nyerere, Mikumi,
Serengeti na Arusha; na Tanzania kuwa mwenyeji katika
Onesho la Kwanza la Kimataifa la Utalii la Jumuiya ya Afrika
Mashariki (East African Regional Tourism Expo – EARTE 2021);
(xvii) Kukuza Biashara na Uwekezaji: wateja 13,836 walipatiwa
huduma katika kituo cha Huduma za Uwekezaji Mahala Pamoja
(OSC) ambapo jumla ya miradi 206 (73 wageni, 69 Watanzania
64 ubia kati ya wageni na Watanzania) ilisajiliwa yenye thamani
ya dola za Marekani milioni 769.5 na inatarajiwa kutoa ajira
27
kwa watanzania wapatao 37,451; kushiriki katika mikutano tisa
(9) ya ndani ikiwemo Maonesho ya Utalii ya Kanda ya Afrika
Mashariki (EA Regional Tourism Expo), Dubai Expo 2020,
Jukwaa la Viwanda lililofanyika Zanzibar na maonyesho ya
viwanda vidogo (SIDO Trade Fair) yaliyofanyika Kigoma; na
kutolewa kwa mikopo kwa kampuni 31 zinazozalisha na
kuchakata bidhaa zitokanazo na mazao ya mifugo na kilimo
kupitia Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kutumia
Mpango wa SANVN (SIDO, AZANIA Bank, NEEC, VETA na
NSSF).
(xviii) Utawala Bora na Utawala wa Sheria: katika
kuhakikisha kuwa utawala bora na utawala wa sheria
unashamiri nchini, Serikali imeendelea kuimarisha Mifumo na
Miundombinu ya Kitaasisi na utoaji haki, uwazi na uwajibikaji
katika utumishi wa umma, shughuli za Mfuko wa Bunge pamoja
na Mfuko wa Mahakama. Mafanikio yaliyopatikana ni:
kulijengea Bunge uwezo kwa kutoa mafunzo ya muda mfupi
kwa Waheshimiwa Wabunge na Watumishi katika maeneo ya
usimamizi wa bajeti, masuala ya kodi, utungaji wa sheria,
kuendesha shughuli za Bunge kupitia Bunge mtandao,
ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo, pamoja na
ujumuishwaji wa masuala ya jinsia katika bajeti; na kununuliwa
na kufungwa kwa vifaa vya kuhifadhi taarifa ili kuimarisha
Mamlaka ya Serikali Mtandao. Aidha, kwa upande wa
mahakama Serikali imekamilisha ujenzi wa vituo vitano (5)
Jumuishi vya utoaji Haki katika Mikoa ya Dar es Salaam
(Temeke na Kinondoni), Dodoma, Arusha na Morogoro;
kuendelea na ujenzi wa makao Makuu ya Mahakama Dodoma,
Mahakama za Mwanzo sita (6), Mahakama za Hakimu Mkazi
tatu (3) na Mahakama za wilaya sita (6); kuendelea na ujenzi
wa Mahakama za Wilaya 26, Mahakama za Mwanzo sita (6) na
kituo kimoja (1) jumuishi cha utoaji haki katika Mkoa wa
28
Mwanza. Vilevile, Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa
haki za watoto, wasichana, wanawake na wanaume;
mapambano dhidi ya rushwa; na kuendelea na ujenzi wa
majengo 24 ya Wizara katika mji wa Serikali Dodoma ili
kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi kutokea makao
makuu ya nchi Dodoma.
UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA USTAWI
WA TAIFA NA MAPAMBANO DHIDI YA UVIKO–19 - Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu katika kipindi cha
mwaka 2019, dunia ilikumbwa na mlipuko wa janga la UVIKO – 19
ambapo kwa kiasi kikubwa uliathiri afya za jamii na uchumi wa nchi
mbalimbali ikiwemo Tanzania. Katika kukabiliana na athari za mlipuko
huo, Serikali iliandaa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na
Mapambano dhidi ya UVIKO–19 (Tanzania COVID-19 Socio-economic
Response and Recovery Plan – TCRP). Mpango huo ulizinduliwa rasmi
tarehe 10 Oktoba, 2021 na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpango huo unatekelezwa
kwa kugharamiwa na mkopo nafuu usio na riba wenye thamani ya
dola za Marekani milioni 567.25 sawa na shilingi trilioni 1.3 kutoka
Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). Kati ya fedha hizo, dola za
Marekani milioni 467.3 sawa na shilingi bilioni 1,079.6 zilielekezwa
Tanzania Bara na dola za Marekani milioni 100 sawa na shilingi bilioni
231.0 zilielekezwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. - Mheshimiwa Spika, kupitia fedha hizo Serikali imeweza
kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi hususan katika
sekta ya elimu ambayo ilipokea shilingi bilioni 368.9, afya shilingi
bilioni 466.9, utalii shilingi bilioni 90.2, maji shilingi bilioni 139.4 na
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) shilingi bilioni 5.5. - Mheshimiwa Spika, katika sekta ya elimu, Serikali imeweza
kupunguza msongamano wa wanafunzi kwa kukamilisha ujenzi wa
29
vyumba vya madarasa 12,000 katika shule za sekondari, madarasa
3,000 ya vituo shikizi katika shule za msingi na mabweni 50 ya
wanafunzi wenye mahitaji maalumu pamoja na ununuzi wa
madawati, viti na meza. Aidha, ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi –
VETA unaendelea katika wilaya 25 ikijumuisha upatikanaji wa vifaa
vya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika vyuo 11. - Mheshmiwa Spika, katika sekta ya afya, hatua iliyofikiwa ni
kuanza kwa ujenzi na ukarabati wa majengo 26 ya wagonjwa
mahututi (ICU), majengo 80 ya huduma za dharura – EMD na
nyumba 150 (3 in 1) za watumishi katika ngazi ya msingi chini ya
Ofisi ya Rais – TAMISEMI na ujenzi wa wodi 38 za wagonjwa mahtuti
- ICU; wodi 20 za huduma za dharura – EMD; nyumba 26 za
watumishi, uboreshaji wa hospitali za rufaa za mikoa saba (7),
hospitali maalumu ya Mirembe; kituo cha magonjwa ya kuambukiza
Kisopwa – Dar es Salaam na kituo cha mfano cha utoaji elimu ya afya
kwa umma Njedengwa – Dodoma ziko katika hatua mbalimbali za
ujenzi. Aidha, maandalizi ya ununuzi wa vifaa tiba vya UVIKO – 19
yamekamilika ikiwemo ununuzi wa mashine 130 za Kidigitali za X –
Ray, CT – Scan 31, MRI nne (4) na Portable Echo Cardiography saba
(7) kwa ajili za Hospitali ya Taifa Muhimbili, Ocean Road, Taasisi ya
Moyo ya Jakaya Kikwete, hospitali za kanda, Hospitali za Rufaa za
Mikoa pamoja na hospitali ya Emilio Mzena Memorial na Lugalo.
- Mheshimiwa Spika, kwa upande wa sekta ya Maji, Serikali
imekamilisha taratibu za ununuzi wa seti 25 za mitambo ya kuchimba
visima katika mikoa yote nchini, seti tano (5) za mitambo ya ujenzi
wa mabwawa na seti nne (4) za vifaa vya uchunguzi wa maji chini ya
ardhi. Aidha, utekelezaji wa miradi 218 ya kuboresha huduma za maji
unaendelea katika maeneo ya mijini na vijijini yenye thamani ya
shilingi bilioni 139.4, ambapo miradi 46 ni kwa maeneo ya mijini na
miradi 172 kwa maeneo ya vijijini.
30 - Mheshimiwa Spika, sekta ya utalii ni miongoni mwa sekta
zilizopata athari za moja kwa moja kutokana na UVIKO-19. Katika
kuimarisha sekta hiyo, Serikali inaendelea na ukarabati na ujenzi wa
miundombinu mbalimbali ikiwemo malango, barabara, njia ya
watembea kwa miguu, Trails, campsite na bandas katika hifadhi zilizo
chini ya TANAPA ikiwemo Nyerere National Park, Saadani National
Park, Kilimanjaro (trails) pamoja na majengo ya kale na nyumba za
kihistoria. Vilevile, Serikali imetoa mafunzo kwa waongoza watalii
1,060 katika Hifadhi za Taifa Tarangire, Saadani, Serengeti,
Ngorongoro na Manyara ili kuimarisha udhibiti wa ubora wa huduma
za utalii katika kukabiliana na janga la UVIKO – 19. - Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Kukabiliana na Athari
za Kijamii na Kiuchumi zitokanazo na UVIKO – 19, Serikali
imewezesha kaya maskini 51,290 katika Halmashauri 35 kupitia
Mfuko wa TASAF ambapo shilingi bilioni 5.5 zimetumika. Aidha,
Serikali imewawezesha wajasiriamali vijana, wanawake, na wenye
ulemavu jumla ya shilingi bilioni 5 kupitia Mpango wa biashara wa
kuboresha miundombinu na mazingira ya wafanyabiashara wadogo
katika Halmashauri za Jiji la Dodoma, Mwanza, Arusha, Tanga,
Mbeya na Dar es Salaam pamoja na Halmashauri za Manispaa za
Kinondoni, Temeke, Ubungo na Morogoro. Vilevile, Serikali
imeendelea na hatua za upatikanaji wa mkandarasi kwa ajili ya
ukarabati wa vyuo vinne (4) vyenye mazingira hatarishi vya watu
wenye ulemavu katika mikoa minne (4) ya Tanzania Bara kwa
gharama ya shilingi bilioni 3.5.
MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2022/23 - Mheshimiwa Spika, Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa
Mwaka 2022/23 ni wa pili katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa
Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26) wenye
dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa
Maendeleo ya Watu. Mpango umeandaliwa kwa kuzingatia: Dira ya
31
Taifa ya Maendeleo 2025; Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa
wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26; Ilani ya Chama cha Mapinduzi
kwa Ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020; Mapendekezo ya
Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23; na Sera na
Mikakati mbalimbali ya kisekta, kikanda na kimataifa zikiwemo Dira
ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) 2050, Dira ya
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) 2050, Agenda 2063
ya Maendeleo ya Afrika na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.
Malengo na Shabaha za Uchumi Jumla kwa Mwaka 2022/23 - Mheshimiwa Spika, Malengo na Shabaha za Ukuaji wa
Uchumi katika kipindi cha mwaka 2022/23, ni kama ifuatavyo:
(i) Ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 4.7 mwaka 2022
na asilimia 5.3 mwaka 2023;
(ii) Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha
kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa
asilimia kati ya 3.0 hadi 7.0 katika muda wa kati;
(iii) Mapato ya ndani kufikia asilimia 14.9 ya Pato la Taifa mwaka
2022/23;
(iv) Mapato ya kodi kufikia asilimia 11.7 ya Pato la Taifa mwaka
2022/23; na
(v) Kuwa na akiba ya fedha za kigeni kwa kiwango cha kukidhi
mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje kwa
kipindi kisichopungua miezi minne (4). - Mheshimiwa Spika, Misingi itakayozingatiwa katika Mpango
wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 ni kama ifuatavyo:
(i) Kuongezeka kwa ushiriki wa sekta binafsi kwenye shughuli za
maendeleo;
(ii) Kuendelea kuhimili athari za majanga ya asili na yasiyo ya asili
kama vile ukame, vita na magonjwa ya mlipuko;
(iii) Kuendelea kuwa na utoshelevu wa chakula nchini; na
32
(iv) Uwepo wa amani, usalama, umoja, utulivu wa ndani na katika
nchi jirani.
Miradi ya Kipaumbele kwa Mwaka 2022/23 - Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali
itaendelea kukamilisha miradi ya kielelezo na ile ya kimkakati
inayoendelea. Miradi hiyo inatarajiwa kuwa na matokeo mapana na
ya haraka katika uchumi, ikiwemo kuzalisha ajira, kipato na
kuchangia zaidi kupunguza hali ya umaskini nchini. Miradi hiyo
inajumuisha: Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa
(Standard Gauge Railway – SGR); Mradi wa Kufua Umeme wa Maji
wa Julius Nyerere – MW 2,115; Kuboresha Shirika la Ndege Tanzania
(ATCL); Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika (LNG) –
Lindi; Kufua Umeme wa Maji wa Ruhudji (MW 358) na Rumakali (MW
222) – Njombe; Daraja la JPM – Kigongo – Busisi (Mwanza); Ujenzi
wa barabara na Madaraja Makubwa; kuendeleza Kanda Maalumu za
Kiuchumi ikiwemo Eneo Maalumu la Uwekezaji Bagamoyo; na
programu ya kuendeleza ujuzi adimu. - Mheshimiwa Spika, miradi ya kipaumbele kwa mwaka
2022/23 itakaendelea kuzingatia maeneo matano ya kipaumbele ya
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano, 2021/22
– 2025/26 kama ifuatavyo:
(a) Kuchochea Uchumi Shindani na Shirikishi: Msisitizo
utawekwa katika kuimarisha mazingira wezeshi ya uwekezaji
ikijumuisha kuimarisha utulivu wa uchumi jumla. Miradi
itakayotekelezwa ni pamoja na: uendelezaji wa miundombinu
na huduma; ukarabati wa njia kuu za reli ikiwemo kukamilisha
ukarabati wa njia ya reli kwa maeneo yaliyobaki kwa kipande
cha Dar es Salaam hadi Isaka (km 970); ujenzi wa barabara za
kufungua fursa za kiuchumi na zile za kuunganisha Tanzania na
33
nchi jirani ikiwemo Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo –
Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 499), Barabara ya
Mbeya – Makongolosi – Manyoni (Mkiwa) (km 528), Barabara
ya Itoni – Ludewa – Manda (km 211); barabara ya Handeni –
Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini –
Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida
(km 460); barabara ya Mafinga – Mtwango – Nyololo –
Mgololo; Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro Express Way
(km 158); barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (km 218)
na mchepuo wa Mbeya (Uyole – Songwe (km 48.9); barabara
ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa
(km 389); kukamilisha madaraja makubwa ya New Wami
(Pwani), Kitengule (Kagera), Lower Malagarasi, Mkundi
(Morogoro), Godegode (Dodoma) na Mtera (Iringa); ujenzi wa
meli katika ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa; kuendelea
kuboresha bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na
Bandari Kavu ya Ruvu; ujenzi wa viwanja vya ndege vya
Msalato, Shinyanga, Tabora, Kigoma na Lindi; kujenga njia ya
kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 ya Rufiji – Chalinze –
Dodoma; kujenga njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kV
400 ya Singida – Arusha – Namanga; kujenga njia ya
kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 ya Iringa – Mbeya –
Sumbawanga – Mpanda – Kigoma – Nyakanazi (North West
Grid Extension); kusambaza umeme vijijini kupitia REA;
uimarishaji wa Gridi ya Taifa ikijumuisha ujenzi wa vituo vipya
57 vya kupoza umeme; ujenzi wa Mkongo wa Mawasiliano wa
Taifa; kuimarisha huduma za bima hususan bima za mazao na
huduma za fedha ili kuimarisha shughuli za uwekezaji nchini;
na kuimarisha mapinduzi ya kidigitali kwa kukuza teknolojia ya
habari na mawasiliano.
(b) Kuimarisha Uwezo wa Uzalishaji Viwandani na
Huduma: miradi itajielekeza katika kuendelea kukuza sekta ya
34
kilimo kwa kutekeleza miradi ya kimkakati ya umwagiliaji,
mbegu na maghala kwa lengo la kuongeza kasi ya ukuaji wa
sekta ya kilimo kufikia wastani wa asilimia 10 na mchango wa
shughuli za umwagiliaji kwenye kilimo kufikia asilimia 50 ifikapo
mwaka 2030. Aidha, Serikali inalenga kuongeza eneo la
umwagiliaji kufikia hekta 8,500,000 pamoja na kuongeza
mauzo ya bidhaa za kilimo nje kutoka dola za Marekani bilioni
1.2 hadi dola za Marekani bilioni 5 ifikapo mwaka 2030. Baadhi
ya mikakati mahsusi itakayotekelezwa ni pamoja na kujenga
skimu za umwagiliaji, kuanzisha Mfuko wa Kutengamaza Bei za
Mazao (Price Stabilisation Fund) na mifuko ya kuendeleza
mazao, kujenga maghala ya kuhifadhi mazao kwenye vijiji ili
kukabiliana na changamoto ya upotevu wa mazao baada ya
mavuno na kuanzisha Youth Agricultural Parks; kuongeza
matumizi ya teknolojia bora katika uzalishaji, kuimarisha
huduma za ugani; kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao
ya kilimo; kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa mitaji katika
sekta ya kilimo; kuimarisha afya ya mifugo; kuimarisha taasisi
za utafiti wa kilimo za TARI na ASA; kuimarisha miundombinu
ya masoko ya mifugo na mazao yake; kufufua Shirika la Uvuvi
Tanzania – TAFICO na kuliwezesha kujiendesha kibiashara;
ujenzi wa bandari ya uvuvi – Kilwa Masoko; kununua boti 250
za kisasa aina ya fibre kwa ajili ya vyama vya ushirika vya
wavuvi; na kujenga na kukarabati vituo vya ukuzaji viumbe
maji.
Kwa upande wa viwanda, miradi itakayotekelezwa ni pamoja
na: kuendelea kuboresha Kituo cha Kuendeleza Teknolojia ya
Magari Tanzania – TATC; kuendelea kufufua Kiwanda cha
Mashine na Vipuri KMTC; kuimarisha Kiwanda cha Viuadudu;
Uendelezaji wa Viwanda Vidogo – SIDO; kuendeleza Eneo la
Kongano ya Viwanda – TAMCO; Maeneo Maalum ya Uwekezaji
(SEZ/EPZ) ya Dodoma, Manyara na Bunda; na kuendelea
35
kuweka sera na mazingira wezeshi kwa uwekezaji wa sekta
binafsi katika viwanda.
Kwa upande wa eneo la madini na huduma, miradi
itakayotekelezwa ni pamoja na: kuendelea kufungua masoko
na vituo vya madini; kuendeleza wawekezaji wadogo wa sekta
ya madini; kuendeleza utalii kanda ya kusini na kuimarisha
utalii hususan kwa kuanzisha mazao mapya ya utalii wa fukwe,
mikutano pamoja na kuimarisha utalii wa ndani; na kukabiliana
na ujangili na biashara haramu ya wanyamapori kwa lengo la
kulinda urithi na maliasili za Taifa.
(c) Kukuza Biashara na Uwekezaji: Kipaumbele kitakuwa
katika kusimamia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kuboresha
Mazingira ya Biashara ikiwemo kuimarisha mazingira ya kisera
na kisheria kuhusu uwekezaji pamoja na mifumo ya uratibu na
usimamizi wa masuala ya uwekezaji kitaifa; kuondoa utozaji
kodi mara mbili; na kulinda biashara na uwekezaji wa sekta
binafsi. Aidha, shughuli nyingine zitakazotekelezwa ni pamoja
na: kutekeleza Programu za Kuboresha Mifumo ya Udhibiti wa
Biashara; Kukuza Ushiriki wa Watanzania kwenye Miradi ya
Kimkakati na Uwekezaji; Kukuza Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi; Kukuza Sekta Binafsi; Uendelezaji wa Masoko ya
Bidhaa; Udhibiti wa Ubora wa Bidhaa; na kuimarisha masoko,
maonesho na makongamano ya uwekezaji ya kikanda na
kimataifa.
(d) Kuchochea Maendeleo ya Watu: Miradi itakayotekelezwa
inalenga kuboresha maisha ya watu: Kwa upande wa sekta ya
elimu shughuli zitakazo tekelezwa ni pamoja na: kuendelea
kugharamia elimumsingi bila ada; kugharamia mikopo ya
wanafunzi wa elimu ya juu; kuimarisha vyuo vya elimu ya juu,
vyuo vya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi na vyuo vya
36
ualimu; kuboresha Elimu ya Sekondari; uboreshaji wa
maktaba; kukamilisha maboma ya vyumba vya madarasa
yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi; kuboresha mitaala ili
iendane na mahitaji ya soko; kujenga shule mpya katika
maeneo yenye mahitaji; na kugharamia uboreshaji wa lishe
shuleni.
Kwa upande wa eneo la afya, miradi itakayotekelezwa ni
pamoja na: kuimarisha huduma za afya hususan ujenzi wa
Hospitali za Rufaa za Kanda na za Mikoa, zahanati, vituo vya
afya na hospitali za Halmashauri za Wilaya; kuimarisha
upatikanaji wa chanjo, dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi
kwa kuongeza bajeti, kutoa fedha na kuimarisha udhibiti;
kuimarisha huduma za ustawi na maendeleo ya jamii, hususan
haki za wazee, watoto na makundi maalumu; na kuendelea na
hatua za uteelezaji wa ahadi ya utoaji wa bima za afya kwa
wote;
Kwa upande wa eneo la maji safi na usafi wa mazingira miradi
itakayotekelezwa ni pamoja na: kuimarisha huduma za maji na
usafi wa mazingira vijijini; ujenzi, ukarabati na upanuzi wa
miradi ya maji katika miji mikuu ya mikoa, wilaya, miji midogo
na miradi ya kitaifa; ujenzi wa bwawa la Farkwa kwa ajili ya
kuimarisha huduma ya maji katika jiji la Dodoma; bwawa la
Kidunda kwa ajili ya kuimarisha upatikanaji wa maji jijini Dar es
Salaam; na kutekeleza mradi wa kimkakati wa kutoa maji
kutoka ziwa Victoria hadi jijini Dodoma.
Kwa upande wa eneo la ardhi, miradi itakayotekelezwa ni
pamoja na: kuendelea kupanga, kupima na kumilikisha ardhi
nchi nzima; kuimarisha mipaka ya kimataifa; kuimarisha
miundombinu ya upimaji na ramani; na kuendeleza upangaji
wa matumizi ya ardhi nchini ili kuondoa migogoro katika
37
matumizi ya ardhi.
(e) Kuendeleza Rasilimali Watu: Kuendelea na utekelezaji wa
programu na miradi mbalimbali ya kukuza ujuzi nchini ili
kuongeza ajira kwa vijana kwa kutoa mafunzo ya ufundi na
stadi za kazi kupitia programu mbalimbali zikiwemo:
kuimarisha programu ya taifa ya kukuza ujuzi nchini; kuboresha
mfuko wa maendeleo ya vijana; kuendelea na ujenzi na
ukarabati wa vituo vya ufundi kwa watu wenye ulemavu; na
kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Kazi za Staha. - Mheshimiwa Spika, maelezo ya kina kuhusu miradi ya
kipaumbele kwa mwaka 2022/23 yanapatikana katika Kitabu cha
Mpango, Sura ya Nne.
Vihatarishi vya Utekelezaji wa Mpango wa Mwaka 2022/23 - Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango unaweza
kuathiriwa na vihatarishi vya ndani na nje. Vihatarishi vya ndani ni
pamoja na: ufinyu wa rasilimali fedha kwa ajili ya kugharamia
utekelezaji wa miradi ya maendeleo; ushiriki mdogo wa sekta binafsi
katika mipango ya maendeleo; uharibifu wa mazingira na mabadiliko
ya tabianchi; na uhalifu wa kimtandao na rushwa. Vihatarishi vya nje
ni pamoja na: majanga ya asili na magonjwa ya mlipuko; mitikisiko
ya kiuchumi duniani; kubadilika kwa teknolojia; na kutopatikana kwa
misaada na mikopo kwa wakati. - Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na vihatarishi vya
utekelezaji wa Mpango, Serikali itachukua hatua mbalimbali
ikijumuisha: Kuimarisha ukusanyaji na usimamizi wa kodi kwa
kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti za kielektroniki
wanapouza bidhaa na wanunuzi kudai risiti wanaponunua bidhaa;
kuhamasisha ulipaji kodi katika sekta isiyo rasmi kwa kuijumuisha
38
kwenye mfumo rasmi wa ulipaji kodi; kuendelea kuimarisha na
kuhamasisha wananchi kuhusu uelewa wa huduma za sekta ya fedha
ikiwemo utoaji wa mikopo, uwekezaji, mitaji na bima; kuendelea
kuweka mazingira ya kuvutia uwekezaji wa sekta Binafsi wa ndani na
nje ili kupunguza gharama za uwekezaji; kusimamia miongozo na
kanuni za usimamizi wa mazingira; kuendelea kuimarisha
mapambano dhidi ya rushwa ikijumuisha kuchukua hatua za kisheria
kwa wanaobainika kuhusika na vitendo vya rushwa; kuboresha
mifumo ya kuzuia na kukabiliana na majanga; na kuweka mazingira
wezeshi kwa wawekezaji hususan viwanda vinavyozalisha bidhaa kwa
kutumia teknolojia na malighafi za ndani ili kupunguza uagizaji wa
bidhaa kutoka nje.
Ugharamiaji wa Mpango 2022/23 - Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2022/23, inakadiriwa kuwa
jumla ya shilingi bilioni 15,004.8 sawa na asilimia 36.2 ya Bajeti yote
ya Serikali zitatumika kugharamia miradi ya maendeleo ikijumuisha
miradi ya huduma za jamii. Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni
12,305.8 sawa na asilimia 82.0 ya bajeti ya maendeleo ni fedha za
ndani na shilingi bilioni 2,699.1 sawa na asilimia 18.0 ya bajeti ya
maendeleo ni fedha za nje. Katika kuongeza ushiriki wa sekta binafsi
kama injini muhimu ya utekelezaji wa miradi, Serikali itahakikisha
miradi yote inayovutia uwekezaji wa sekta binafsi inatekelezwa kwa
utaratibu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) na
Joint Venture kwa kutumia utaratibu wa Kampuni Maalumu (Special
Purpose Vehicle). - Mheshimiwa Spika, katika kuongeza ukusanyaji wa mapato
ya kugharamia Mpango, Serikali itaendelea kuweka mikakati ya
kusimamia ukusanyaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi kutoka
vyanzo mbalimbali vya ndani kwa kuchukua hatua mbalimbali
zikiwemo: Kuimarisha ukusanyaji na usimamizi wa kodi kwa
39
kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti za kielektroniki
wanapouza bidhaa na wanunuzi kuchukua risiti wanaponunua
bidhaa; kuendelea kutoa elimu kwa mlipakodi kupitia runinga, redio,
mitandao ya kijamii na semina; kupanua wigo wa kodi kwa
kuwatambua na kuwasajili wafanyabiashara katika mfumo rasmi wa
ulipaji kodi kupitia kampeni ya Mlango kwa Mlango; kuendelea
kutumia Mpango wa Usimamizi wa Viashiria Hatarishi (Compliance
Risk Management Plan) ili kubaini na kutambua wakwepaji wa kodi;
kuendelea kuimarisha usimamizi na ukaguzi wa mipaka yote kwa
kuongeza ushirikiano baina ya Mamlaka ya Mapato Tanzania na
vyombo vya ulinzi na usalama nchini ili kudhibiti bidhaa za magendo
na kupunguza tatizo la ukwepaji wa kodi; na kuimarisha mazingira
rafiki ya ulipaji kodi kwa hiari kwa kuboresha na kuhimiza matumizi
sahihi ya mifumo ya TEHAMA ikiwa ni pamoja na kuboresha mifumo
itakayosaidia na kurahisisha ulipaji kodi. - Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha Mfumo wa
Kielektroniki wa Kufuatilia Mizigo inayokwenda nchi jirani (Eletronic
Cargo Tracking System) ili kuimarisha uwezo wa usimamizi wa mizigo
inayopita kwenda nchi jirani; kuhamasisha ulipaji kodi katika sekta
isiyo rasmi kwa kuijumuisha kwenye mfumo rasmi wa ulipaji kodi;
kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuvutia wawekezaji
wapya, kukuza biashara ndogo na za kati kwa ukuaji endelevu wa
uchumi utakaowezesha kuongeza wigo wa kodi pamoja na
kuendelea kusimamia Mfumo wa Serikali wa Kielektroniki wa
Ukusanyaji wa Mapato (Government Electronic Payment Gateway –
GePG) ili kurahisisha ulipaji na kudhibiti upotevu wa mapato. - Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha
mashirikiano na Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza Mwongozo
wa Ushirikiano wa Maendeleo (Development Cooperation Framework
- DCF) ili kuhakikisha kuwa fedha kutoka kwa Washirika wa
Maendeleo zinaendelea kupatikana kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji
40
wa miradi na programu mbalimbali nchini. Aidha, Serikali kwa
kushirikiana na washirika wa Maendeleo imeanza maandalizi ya
kufanya tathmini na mapitio ya Mwongozo wa Ushirikiano
itakayoiwezesha nchi kujipanga kimkakati ili kunufaika zaidi na fursa
zilizopo kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Serikali, Sekta
binafsi na Asasi Zisizo za Kiserikali katika masuala ya ushirikiano wa
kimataifa.
Vile vile, kwa kutambua uwepo wa pengo la rasilimali fedha
zinazohitajika katika kufikia shabaha ya maendeleo ya Taifa, Serikali
imeainisha vyanzo mbadala na bunifu vitakavyotumika kugharamia
miradi ya maendeleo na hivyo kupunguza mzigo kwa bajeti ya
Serikali. Vyanzo hivyo ni utekelezaji wa Mkakati wa Ugharamiaji wa
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano sanjari na
Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha wa mwaka 2020/21-
2029/30. Katika kufikia azma hiyo, Serikali itafanya maboresho ya
sheria mbalimbali pamoja na kuweka miongozo itakayowezesha
kunufaika na vyanzo mbadala na bunifu katika utekelezaji wa
shughuli za maendeleo.
- Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ugharamiaji wa miradi
ya maendeleo itakayotekelezwa kwa utaratibu wa Ubia baina ya
Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Serikali imepanga kuwezesha
Mamlaka za Serikali zenye miradi ya PPP iliyopo katika hatua
mbalimbali za maandalizi ikiwemo Upembuzi Yakinifu na Ununuzi wa
wabia kukamilisha miradi hiyo iweze kuanza utekelezaji. Katika
mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kushirikiana na Sekta Binafsi
katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa utaratibu
wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). Baadhi
masuala yatakayotekelezwa ni pamoja na kuendelea kutafuta wabia
wa miradi mitano (5) iliyofikia katika hatua za ununuzi (procurement
stage) kwa kuitangaza katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Miradi
hiyo ni: ujenzi wa viwanda vya dawa muhimu (Kibaha), vifaa tiba
41
vitokanavyo na pamba (Mwanza) na maji tiba (Mbeya); uendeshaji
wa huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es
Salaam awamu ya kwanza; ujenzi wa hoteli ya nyota nne katika
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere; ujenzi wa kituo
changamani cha biashara (commercial Complex) katika Kiwanja cha
Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere; na ujenzi wa kiwanda cha
kutengeneza simu za mkononi chini ya Mamlaka ya Mawasiliano
Tanzania (TCRA) katika Mkoa wa Mwanza.
Ufuatiliaji, Tathmini na Utoaji wa Taarifa za Utekelezaji - Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa mipango ya
maendeleo inatekelezwa kama ilivyokusudiwa, suala la ufuatiliaji,
tathmini na utoaji wa taarifa za utekelezaji limeendelea kupewa
msukumo wa pekee katika shughuli za kila siku za Serikali. Katika
kutekeleza hilo, mwaka 2021/22, Wizara ya Fedha na Mipango
ilifanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi 225 katika sekta za Uchukuzi,
Viwanda, Elimu, Afya, Ujenzi, Utawala Bora, Kilimo, Mifugo, Maji na
Biashara inayotekelezwa na Serikali pamoja na Sekta Binafsi. Katika
mwaka 2022/23, Serikali itaendelea kutumia mbinu na viashiria
vilivyoainishwa katika Mkakati wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Mpango
wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 –
2025/26 pamoja na Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini
ya Miradi na Programu za Maendeleo kupima utekelezaji wa Mpango
wa Tatu wa Maendeleo wa Miaka Mitano na miradi ya maendeleo na
kuchukua hatua za kutatua changamoto zitakazobainika katika
utekelezaji. Vile vile, Serikali itaendelea kuzingatia miongozo
mbalimbali ya ufuatiliaji na tathmini ya Mpango ikiwemo Sheria ya
Ununuzi wa Umma, SURA 410, Sheria ya Bajeti, SURA 439 na Sheria
ya Fedha za Umma, SURA 348. Pamoja na Sheria hizo, Serikali pia
imeanza maandalizi ya Sera ya Taifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ili
kutatua changamoto za uratibu wa shughuli za ufuatiliaji na tathmini
Serikalini.
42 - Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha uwepo wa
ushirikishwaji wa kutosha katika masuala ya ufuatiliaji na tathmini,
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kushirikiana
na Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na
Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za
Mitaa pamoja na Sekta Binafsi katika kuratibu na kusimamia
ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Mpango. - Mheshimiwa Spika, Serikali inazielekeza Wizara, Idara
Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma,
Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutafsiri
malengo na viashiria vya utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa
Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 katika
Mipango na Bajeti za kisekta kwa mwaka 2022/23. Aidha, Wizara,
Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya
Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa
zinaelekezwa kuzingatia maelekezo yaliyoainishwa katika Mwongozo
wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi na Programu za
Maendeleo wa Mwaka 2022 ikiwa ni pamoja na: kuandaa Mpango
Kazi wa mwaka wa ufuatiliaji na tathmini, kutenga rasilimali fedha
zitakazowezesha shughuli za ufuatiliaji na tathmini; kuimarisha
mifumo ya ndani ya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo;
kufanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo kwa
kuzingatia mipango kazi iliyowekwa; kuendelea kuwajengea uwezo
watumishi katika tasnia ya ufuatiliaji na tathmini; na kuwa na mfumo
mmoja wa kielektroniki unaoratibu taarifa za utekelezaji, ufuatiliaji na
tathmini katika kutekeleza mipango ya maendeleo. - Mheshimiwa Spika, Serikali inazielekeza Wizara, Idara
Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma,
Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuaandaa
43
taarifa za ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi na programu
za maendeleo na kuziwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango. Ofisi ya
Rais – TAMISEMI itaratibu ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya
maendeleo inayotekelezwa katika ngazi za Sekretarieti za Mikoa na
Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuwasilisha taarifa husika Wizara ya
Fedha na Mipango.
MAJUMUISHO - Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza hapo awali, Mpango
wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 ni wa pili katika
utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka
Mitano 2021/22 – 2025/26 wenye dhima ya “Kujenga Uchumi
Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu”. Utekelezaji wa
Mpango utaendelea kuimarisha viashiria vya uchumi jumla,
kuboresha mazingira ya uwekezaji viwandani ikiwemo kuimarisha
majadiliano na wawekezaji wa ndani na nje, kuimarisha mahusiano
ya kisiasa, ulinzi na diplomasia ya uchumi na nchi nyingine,
kuendelea kutekeleza kwa kasi miradi ya maendeleo, kuendeleza
mashirikiano na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya
maendeleo pamoja na kuchochea uwekezaji viwandani hususan kwa
kutumia rasilimali watu na malighafi zinazopatikana kwa wingi nchini
ikiwemo mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, madini, misitu na gesi
asilia. - Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na jitihada za
kukabiliana na athari za majanga mbalimbali ya asili na yasiyo ya asili
yakiwemo magonjwa, vita na mabadiliko ya tabianchi. Mathalani,
tutaendelea kuimarisha utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa
Kukabiliana na Athari za UVIKO–19 pamoja na kuweka mipango
madhubuti ya kupunguza athari zitokanazo na vita inayoendelea kati
ya Urusi na Ukraine ikiwemo kudhibiti ongezeko la bei za bidhaa
mbalimbali na kushuka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi.
44 - Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha upatikanaji
na utoaji wa huduma bora kwa wananchi zikiwemo huduma za afya,
elimu, umeme na maji safi na salama mijini na vijijini, kuongeza kasi
ya utekelezaji wa miradi ya kielelezo na ya kimkakati, kuimarisha
miundombinu wezeshi ya uwekezaji na biashara kwa ajili ya masoko
ya kimataifa hususan ya nchi jirani, kuimarisha sekta za uzalishaji ili
kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi, kufungua fursa zaidi za
ajira na maendeleo ya watu.
HITIMISHO - Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Serikali ninaomba kutumia
fursa hii kuwashukuru wadau wote wa maendeleo wakiwemo
Waheshimiwa Wabunge, Sekta Binafsi, Taasisi za Elimu na Tafiti,
Asasi za Kiraia, Taasisi za Dini, Washirika wa Maendeleo na Wananchi
wote kwa namna walivyojitoa na kushiriki kikamilifu katika hatua
mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuimarisha
uchumi wa Taifa letu. Wadau hao wamekuwa na mchango mkubwa
katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo. Kwa msingi
huo, ninawaomba na kuwasihi wadau wote waendelee kushirikiana
na Serikali yetu inayoongozwa na Rais shupavu, Mheshimiwa Samia
Suluhu Hassan. - Mheshimiwa Spika, hotuba hii isingeweza kukamilika bila
jitihada kubwa zilizofanywa na watumishi wote wa Wizara ya Fedha
na Mipango. Hivyo, kwa dhati ya nafsi yangu naomba nitoe shukrani
za pekee kwa Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), Naibu Waziri wa
Fedha na Mipango, Mawaziri, Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa
Wizara zote, Viongozi wote wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za
Serikali za Mitaa, Wakuu wa Idara Zinazojitegemea, Wakala za
Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma kwa ushirikiano wao katika
maandalizi ya taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2021
45
na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23. Aidha,
ninawashukuru watendaji wote wa Wizara ya Fedha na Mipango
wakiongozwa na Katibu Mkuu Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba kwa
kujitoa usiku na mchana kukamilisha kwa wakati na kwa ubora
Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa
Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23. - Mheshimiwa Spika, mwisho lakini si kwa umuhimu, napenda
kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge na Wananchi wote kwa ujumla
kwa kutenga muda wao kunisikiliza. Aidha, napenda kuwataarifu
wadau wote kuwa, hotuba hii pamoja na vitabu vya Taarifa ya Hali
ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa
Taifa wa Mwaka 2022/23 vinapatikana katika tovuti ya Wizara ya
Fedha na Mipango ambayo ni www.mof.go.tz. - Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo naomba sasa
Bunge lako Tukufu lipokee na kujadili Taarifa ya Hali ya Uchumi wa
Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa
Mwaka 2022/23. - Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.