
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linaendelea kumtafuta mtu mmoja aneyetuhumiwa kumuua mke wake aliyefahamika kwa jina la Logesara Chitemo Mgogo, mfanyabiashara wa pombe za kinyeji mkazi wa Ukonga Mazizini Ilala, aliyefariki dunia baadaya kuchomwa kwa kitu chenye ncha kali maeneo ya tumboni na kifuani tarehe 06/06/2022 Saa 3:00 usiku kisha mume wa mwanamke huyo alitoroka baada ya tukio hilo Upelelezi wa tukio hili unaendelea na lazima akamatwe na atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
