HOTUBA YA WAZIRI MBARAWA BUNGENI-MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI MWAKA WA FEDHA 2022/2023

HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI 

NA  UCHUKUZI,  MHESHIMIWA  

PROF. MAKAME MNYAA MBARAWA (MB),

AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA

MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI 

YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

  1. UTANGULIZI
  1. Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja kwamba, baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliyochambua utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ya mwaka wa fedha 2021/22, Bunge lako Tukufu likubali kupokea, kujadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2022/23.
  • Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutupa kibali cha kukutana leo tukiwa wazima wa afya njema. Aidha, kwa unyenyekevu mkubwa ninamuomba Mwenyezi

Mungu atuongoze katika kujadili wasilisho hili la Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi pamoja na bajeti nzima ya Serikali ili kuendelea kuchangia katika maendeleo ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

  • Mheshimiwa Spika,  naomba kutumia fursa hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi uliotukuka ambao ameuonesha tangu alipochukua kijiti cha kuongoza Taifa hili kufuatia kifo cha Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilichotokea tarehe 17 Machi, 2021. Uongozi wa Rais wa Awamu ya Sita umedhihirika kuwa wenye umakini wa hali ya juu, utendaji uliotukuka, maono yenye manufaa makubwa kwa Taifa, ujasiri, maarifa na uwajibikaji. Ninamuomba Mwenyezi Mungu amjalie Rais wetu afya njema ili aweze kutekeleza majukumu yake.
  • Mheshimiwa Spika, napenda kumpongezaMakamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Isdory Mpango kwa jinsi anavyoendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ya kuwaletea watanzania maendeleo katika nyanja mbalimbali. Ni wazi kuwa Mheshimiwa Makamu wa Rais ametekeleza majukumu yake kwa umahiri mkubwa na hivyo kuchangia katika maendeleo ya

Taifa.

  • Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kiongozi wa shughuli za Serikali hapa Bungeni, kwa uongozi wake mahiri na makini. Sote ni mashuhuda wa kazi iliyotukuka anayoifanya katika utekelezaji wa majukumu yake ndani na nje ya Bunge.
  • Mheshimiwa Spika, kwa heshima kubwa nitoe shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyokuwa nayo juu yangu kwa kuniteua kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi tarehe 12 Septemba, 2021. Hii ni mara ya pili ninahudumu katika Wizara hii na ninaahidi kwake na kwa Taifa kwa ujumla kwamba nitaitumikia nafasi hii kwa uadilifu na kwa uwezo wangu wote. Nikiwa kama msaidizi wake katika kusimamia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, natumia fursa hii kumhakikishia kwamba mimi pamoja na wenzangu tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba kazi ya kulijenga Taifa hili inaendelea ili kufikia malengo tuliyojiwekea kupitia miongozo mbalimbali ikiwemo miongozo kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020.
  • Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kukupongeza wewe binafsi kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu kuwa Naibu Spika. Hakika mnatosha na tuna imani kubwa kwamba chini ya uongozi wenu Bunge hili litatekeleza majukumu yake kwa uadilifu, umahiri na weledi mkubwa. Aidha, niwapongeze Wenyeviti wa Kamati za Bunge kwa namna wanavyolisimamia na kuliongoza Bunge letu Tukufu ili litimize majukumu yake ya kushauri na kuisimamia

Serikali. 

  • Mheshimiwa Spika, kipekee naomba kuishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu inayoongozwa na Mheshimiwa Seleman Moshi Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini, na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki pamoja na Wajumbe wote wa Kamati hiyo. Kwa ujumlaKamati imeendelea kutoa ushauri stahiki kwa Wizara na Taasisi zake katika kutekeleza majukumu yake na nikiri kwamba imefanya hivyo kwa ufanisi. Aidha, uchambuzi walioufanya kwenye Taarifa ya Utekelezaji ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2021/22 na Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2022/23 umetusaidia kwa kiasi kikubwa kuandaa Bajeti ya Wizara kwa ubora wa hali ya juu. Napenda kuiahidi Kamati hii kwamba Wizara itaendelea kupokea maoni na ushauri wao na kuufanyia kazi kwa kadri inavyowezekana kwa lengo la kuboresha utendaji na kutekeleza kwa ufanisi mipango ya Sekta za Ujenzi na Uchukuzi.
  • Mheshimiwa Spika, sambamba na salamu hizo nichukue fursa hii kutoa mkono wa pole kwa Bunge lako Tukufu kufuatia kifo cha Mbunge mwenzetu Marehemu Elias John Kwandikwa aliyefariki tarehe 02 Agosti, 2021 ambaye hadi umauti unamkuta alikuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Kabla ya hapo, Marehemu aliwahi kuhudumu katika Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kama Naibu Waziri kuanzia mwaka 2016 hadi alipoteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa tarehe 05 Disemba, 2020. Tutaendelea kuienzi michango yake katika ustawi na maendeleo ya Jimbo la Ushetu alilotoka na Taifa kwa ujumla katika nyadhifa za Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa pamoja na Naibu Waziri (Sekta ya Ujenzi). Aidha, ninatoa mkono wa pole kwa Bunge lako Tukufu kufuatia kifo cha Mbunge mwenzetu Marehemu William Ole Nasha ambaye alikuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) na Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro. Marehemu Ole Nasha alifariki tarehe 27 Septemba, 2021. Pia, natoa pole kwa Bunge lako Tukufu kwa kifo cha Mbungewa Viti Maalum (CCM), Mkoa wa Rukwa, Marehemu Irene Alex Ndyamukama aliyefariki tarehe 24 Aprili, 2022. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi, Amina.
  1. Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuwashukuru na kuwapongeza Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango kwa hotuba zao ambazo zimefafanua utendaji wa Serikali kwa mwaka 2021/22 na kutoa  mwelekeo wa mpango na bajeti kwa mwaka 2022/23. Aidha, nawapongeza Mawaziri wote waliotangulia kwa mawasilisho mazuri ya hotuba za Wizara wanazozisimamia. 
  1. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuwasilisha  Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2021/22  pamoja na Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2022/23, naomba kwa muhtasari niainishe baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika Sekta za Ujenzi na Uchukuzi ndani ya mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita.
  • MAFANIKIO YA MWAKA MMOJA WA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KATIKA

SEKTA ZA UJENZI NA UCHUKUZI

  1. Mheshimiwa Spika, sote ni mashahidi wa namna Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ilivyopata mafanikio katika sekta mbalimbali. Nitaeleza kwa kifupi mafanikio katika sekta ninazoziongoza ambazo ni Sekta ya Ujenzi na Sekta ya Uchukuzi. 
  1. Mheshimiwa Spika, majukumu ya msingi ya Sekta ya Ujenzi ni kusimamia utekelezaji wa Sera ya Ujenzi (2003) pamoja na Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani (2009); ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko; ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya viwanja vya ndege; ujenzi na ukarabati wa nyumba na majengo ya Serikali; usimamizi wa masuala ya ufundi na umeme; usimamizi wa shughuli za ukandarasi, uhandisi, ubunifu majengo na ukadiriaji majenzi; usimamizi wa maabara za vifaa vya ujenzi; usimamizi wa masuala ya usalama barabarani na mazingira katika Sekta; uboreshaji, utendaji na uendelezaji wa watumishi wa Sekta pamoja na usimamizi wa majukumu ya taasisi zilizo chini ya Sekta. 
  1. Mheshimiwa Spika,kwa upande wa Sekta ya Uchukuzi, majukumu yake ni kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uchukuzi (2003); ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya reli na bandari; usafiri na usafirishaji kwa njia ya anga, reli na bandari; utoaji wa leseni za usafirishaji; usalama katika usafirishaji; usimamizi wa huduma za hali ya hewa; kuendeleza rasilimali watu katika Sekta ya Uchukuzi na kusimamia Taasisi na Mashirika ya Umma yaliyo chini ya Sekta ya Uchukuzi.
  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutoa fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali  ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa barabara za juu katika jiji la Dar es Salaam, ujenzi wa Daraja la J.P Magufuli katika eneo la Kigongo – Busisi mkoani Mwanza,  Daraja Jipya la Wami lililopo mkoa wa Pwani, na Daraja Jipya la Selander (Tanzanite)  ambalo ujenzi wake umekamilika  na limefunguliwa  tarehe 24 Machi, 2022 na Mheshimiwa  Samia Suluhu Hassan,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Vilevile, mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa ajili ya familia 644 za wakazi wa  Magomeni Kota umekamilika na kufunguliwa rasmi na Mheshimiwa Rais tarehe 23 Machi, 2022. Kukamilika kwa mradi huu kutawawezesha wakazi hao kupata makazi bora na ya kisasa, kutoa fursa za biashara katika maduka na vizimba 186 zilivyomo ndani ya eneo la mradi. Utekelezaji wa mradi huu umezalisha wastani wa ajira 600 kwa siku kwa mafundi na vibarua baba na mama lishe. Aidha, kukamilika kwa mradi huu kumebadilisha taswira nzima ya eneo la Magomeni na kuboresha muonekano wake na ustawi wa jamii.

  1. Mheshimiwa Spika, hivi karibuni mradi wa ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje (Outer Ring Road) yenye urefu wa kilometa 112.3 katika Jiji la Dodoma umezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Tayari Makandarasi wameanza ujenzi wa barabara hiyo ambayo itakuwa ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi na kurahisisha usafirishaji wa mizigo inayotumia barabara za Ushoroba wa Kati. Vilevile, upanuzi kwa njia nane wa barabara ya Kimara – Kibaha  (km 19.2) umeendelea kutekelezwa ambapo barabara hii ikikamilika itakuwa suluhisho la changamoto ya msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro. Miradi mingine ya barabara ambayo iko hatua za ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia awamu ya sita ni pamoja na Mradi wa magari yaendayo kwa kasi awamu ya tatu katika jiji la Dar es Salaam (km 23.33) pamoja na vituo vya mabasi, barabara ya Tanga – Saadani-Bagamoyo (km 256 km) sehemu ya Mkange – Mkwaja Pangani (km 91.5) pamoja na Kipumbwi Spur (km 3.7), Malagarasi – Ilunde – Uvinza (km 51.1), Bugene – Kasulo (Benaco) – Kumunazi (km 128.5) sehemu ya Bugene – Burigi Chato National Park (km 60).
  1. Mheshimiwa Spika, miradi mingine ya barabara ipatayo 22 imepata kibali cha kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Kati ya miradi hiyo, mikataba ya kazi za ujenzi ambayo imesainiwa ni  Barabara ya Ntendo – Muze – Kilyamatundu (km 179) sehemu ya Ntendo – Kizungu (km 25);

Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (km 389) sehemu ya Mbulu – Garbabi (km 25); Matai – Kasesya (km 50.6 ); Tarime –

Mugumu (km 87.14), sehemu ya Tarime –

Nyamwaga (25);  Mpanda –  Mishamo – Uvinza –

Kanyani (km 250.4) sehemu ya Vikonge –

Luhafwe (km 25);  Makongorosi – Rungwa – Itigi – 

Mkiwa, sehemu ya Noranga – Itigi (Mrongoji) (km 25); Handeni – Kibirashi  – Kibaya  – Kwa Mtoro –

Singida (km 460) sehemu ya Handeni –

Kwediboma (km 20); Kitai – Lituhi (km 85) pamoja na Daraja la Mnywamaji, sehemu ya

Amanimakoro – Ruanda (km 35); Ntyuka Jct – Mvumi – Kikombo (km76) na Chololo –Mapinduzi (TPDF HQ (km 5) sehemu ya Ntyuka –Mvumi- Makuru (8.6) na Kikombo Jct – Chololo – Mapinduzi (TPDF HQ) (km 16.4); Kabaoni – Sitalike (km 74) sehemu ya Kibaoni –Mlele (km 50); Itoni – Ludewa – Manda (km 211.4) sehemu ya Itoni – Lusitu (km 50) na  Mianzini – Ngaramtoni (km 18).

Aidha, barabara nyingine ziko katika hatua ya manunuzi ya kupata makandarasi ambazo ni  barabara ya TAMCO – Vikawe – Mapinga (km 24); Ibanda – Itungi (km 26); Omugakorongo –

Kigarama – Murongo sehemu ya Murongo –

Kigarama  (km 50); Sengerema – Nyehunge – Kahunda sehemu ya Sengerema – Nyehunge (km 54); Nzera – Nkome (km 20); Same – Kisiwani – Mkomazi (km 97); Ubena Zomozi – Ngerengere (km 11.6); Ifakara – Kihansi (km 50); Kibada – Mwasonga – Tundwi Songani – Kimbiji (km 41); Uyole – Ifisi  (km 29); Likuyufusi – Mkenda (sehemu ya Likuyufusi – Mhukuru km 60); Bigwa – Matombo – Mvuha (km 78); Isyonje – Kikondo –

Makete (km 96.2) sehemu ya Ipelele – Iheme (km 25); Kibaoni – Sitalike (km 74) sehemu ya Mlele – Sitalike (km 24) na Kibondo – Mabamba (km 48). 

  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri kwa njia ya reli, Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea na kazi za ujenzi wa reli ya SGR kwa awamu mbili, ambapo Serikali imeendelea na ujenzi wa awamu ya kwanza  iliyogawanyika katika vipande vitano (5) kati ya Dar es Salaam na Mwanza. Utekelezaji wa ujenzi wa vipande hivyo umefikia katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Aidha, Serikali imeanza utekelezaji wa ujenzi wa reli ya SGR katika awamu ya pili kati ya Tabora na Kigoma ambapo fedha za utekelezaji huo zimeanza kutengwa katika mwaka wa fedha 2022/2023.
  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imeonesha dhamira ya dhati ya kuboresha viwanja vya ndege ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za usafiri na usafirishaji kwa njia ya  anga.   Katika kufanikisha hilo, ujenzi pamoja na uboreshaji wa viwanja vya ndege katika mikoa mbalimbali nchini umeendelea kutekelezwa. Miradi  hiyo ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa Viwanja vya Ndege vya Songea, Mtwara, Iringa, Musoma na Songwe.  Vilevile, mkataba wa Awamu ya Kwanza ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Mkoani Dodoma umesainiwa na Mkandarasi yupo katika hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi. Aidha, kuhusu Awamu ya Pili ya ujenzi wa Jengo la Abiria na Miundombinu yake katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, tayari Serikali imesaini mkataba wa ujenzi. Sanjari na kuboresha viwanja vya ndege, Serikali imeendelea kuboresha Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ambapo katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, ATCL imepokea ndege tatu (3) ambapo kati ya hizo ndege mbili (2) ni za masafa ya kati na ndege moja (1) ni ya masafa mafupi.
  2. Mheshimiwa Spika, kuhusu upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, Serikali imekamilisha ujenzi wa Gati la kushusha magari (RORO) pamoja na kuboresha Gati Namba 1 hadi 7 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa  Samia Suluhu Hassan alizindua miradi hii tarehe 04 Disemba, 2021. Matokeo ya ujenzi na maboresho haya yameanza kuonekana ambapo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania imefanikiwa kuhudumia meli kubwa ya magari katika historia yake ikiwa imeshusha magari 4,397 tarehe 09 Mei, 2022. Hii imewezekana kutokana na maboresho yaliyofanywa kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imewezesha upatikanaji wa karakana sita zinazotembea na hivyo kufikia saba kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa matengenezo ya magari katika maeneo yasiyofikia kwa urahisi. Karakana hizo zinahudumia maeneo ya pembezoni katika mikoa ya Pwani, Arusha, Mbeya, Dodoma, Mwanza, Tabora na Mtwara. Vilevile, Wizara imefunga Mfumo wa Kielektroniki wa Kukusanya Mapato (N – Card) katika kituo cha Magogoni – Kigamboni mwezi Machi, 2022. Kwa sasa watumiaji wa kivuko hiki wanatumia kadi maalum kulipia tozo kwa ajili ya kuvuka badala ya tiketi zilizokuwa zikitumika awali. Ni matarajio ya Serikali kuwa Mfumo huu utaboresha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali.

C. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI YA WIZARA NA TAASISI ZAKE KWA MWAKA WA FEDHA 2021/22

  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imegawanywa katika mafungu mawili ya kibajeti: Fungu 62 (Sekta ya Uchukuzi) na Fungu 98 (Sekta ya Ujenzi). Nitaanza na maelezo kuhusu utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2021/22 kwa Sekta ya Ujenzi ikifuatiwa na Sekta ya Uchukuzi.

C.1   SEKTA YA UJENZI 

Bajeti ya Matumizi ya Kawaida

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Sekta ya Ujenzi ilitengewa jumla ya Shilingi 38,540,787,000.00  kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 35,186,389,000.00  ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake na Shilingi 3,354,398,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.

Hadi Aprili, 2022 jumla ya Shilingi 31,578,893,459.84, sawa na asilimia 81.94  ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilikuwa zimetolewa na HAZINA kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 29,092,402,936.04 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi na Shilingi 2,486,490,523.80 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.

Bajeti ya Miradi ya Maendeleo

  • Mheshimiwa Spika, kwa upande wa miradi ya maendeleo, katika mwaka wa fedha 2021/22, Sekta ya Ujenzi ilitengewa Shilingi 1,588,703,487,200.00. Kiasi hicho kinajumuisha Shilingi 1,288,703,487,200.00 fedha za ndanina Shilingi 300,000,000,000.00 fedha za nje. Fedha za ndani zilijumuisha fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali (Consolidated Funds) ambazo ni Shilingi 652,854,360,000.00 na fedha za Mfuko wa Barabara ni Shilingi 635,849,127,200.00.

Hadi Aprili, 2022 fedha zilizopokelewa ni Shilingi 1,532,703,487,200.00 sawa na asilimia 96.48 ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2021/22. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,232,741,391,541.94  ni fedha za ndani na Shilingi 299,962,095,658.06 ni fedha za nje. Fedha za ndani zilizopokelewa zinajumuisha Shilingi 691,100,092,642.94  kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali na Shilingi 541,641,298,899.00  kutoka  Mfuko wa Barabara. 

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Miradi ya Barabara na Madaraja

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ilipanga kutekeleza miradi ya barabara kuu inayohusisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa  kilometa 467.11 kwa kiwango cha lami, ujenzi wa madaraja 14 pamoja na ukarabati wa kilometa 32.47  kwa kiwango cha lami katika barabara kuu. 

Hadi kufikia Aprili, 2022  ujenzi wa kilometa 216.26 za barabara kuu kwa kiwango cha lami umekamilika, sawa na asilimia 46 na ukarabati wa kilometa 2.5 sawa na asilimia 8 za Barabara Kuu. Aidha, utekelezaji wa miradi ya madaraja ya Kiyegeya (Morogoro), Daraja Jipya la Selander mkoani Dar es Salaam, Kitengule mkoani Kagera na Ruhuhu mkoani Ruvuma umekamilika na madaraja mengine yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

  • Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara za mikoa, Wizara kupitia TANROADS ilipanga kujenga kwa kiwango cha lami jumla ya kilometa 103.0 ambapo kilometa 72.2 zilipangwa kujengwa kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na kilometa 30.8 zilipangwa kujengwa kwa fedha za Mfuko wa Barabara. Kazi nyingine ni ukarabati kwa kiwango cha changarawe jumla ya kilometa 1,124.3. Kati ya hizo, kilometa 698.3 pamoja na madaraja/makalavati 34 yalipangwa kukarabatiwa kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na kilometa 426 pamoja na madaraja/ makalavati 32 yalipangwa kujengwa/kukarabatiwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara.

Hadi Aprili, 2022 jumla ya kilometa 34.8 za barabara za mikoa zilijengwa kwa kiwango cha lami na jumla ya kilometa 307.41 zilikarabatiwa kwa kiwango cha changarawe. Aidha, utekelezaji wa miradi ya madaraja upo katika hatua mbalimbali. Utekelezaji wa miradi  uliathiriwa kwa kuchelewa kupatikana kwa misamaha ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT). Hata hivyo, Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Mamlaka ya

Mapato Tanzania (TRA) imeandaa Mfumo wa Kielektroniki utakaorahisisha upatikanaji wa misamaha ya kodi.

  • Mheshimiwa Spika, Wizara vilevile ilipanga kufanya matengenezo ya kawaida (routine and recurrent maintenance) kwa kilometa 33,171.89, matengenezo ya muda maalum kilometa 4,783.72 matengenezo ya sehemu korofi kilometa 549.38 pamojana matengenezo ya madaraja 3,291 katika barabara kuu na barabara za mikoa. Kazi nyingine ni shughuli za udhibiti wa uzito wa magari na eneo la hifadhi za barabara na mradi wa matengenezo ya barabara kwa mikataba ya muda mrefu.

Hadi Aprili, 2022 mpango wa matengenezo katika barabara kuu na za mikoa ulikuwa umekamilika kwa asilimia 30. Aidha,jumla ya magari 3,821,559 yalikuwa yamepimwa katika vituo 66 vya mizani iliyopo nchini ambapo kati ya hayo, magari  31,055 sawa na asilimia 0.82 yalikuwa yamezidisha uzito zaidi ya asilimia 5 ya uzito unaoruhusiwa. Jumla ya Shilingi bilioni 2.97  zilikusanywa kutokana na tozo ya uharibifu wa barabara. Ili kuongeza uwazi na uwajibikaji na kupunguza vitendo vya rushwa kwenye mizani, Wizara kupitia TANROADS imeweka mifumo ya kamera (CCTV) katika mizani 13 na itaendelea kuweka katika mizani nyingine. Vilevile, Wizara inaendelea na utoaji wa vibali vya usafirishaji barabarani wa mizigo maalum nchini kwa kutumia mfumo ujulikanao Special Load Permit System

  • Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 jumla ya vibali 35,818 vilitolewa na jumla ya Shilingi bilioni 12.80 zilikusanywa kutokana na tozo ya upitishaji wa mizigo maalum. Vilevile, mvua kubwa zilizonyesha nchini kuanzia Novemba, 2021 hadi Februari, 2022 zilisababisha uharibifu mkubwa wa barabara katika mikoa 14 ambayo ni Arusha, Dodoma, Mbeya, Morogoro,

Ruvuma, Pwani, Dar es Salaam, Iringa, Manyara, Katavi, Singida, Tanga na Kilimanjaro. Matengenezo ya barabara hizo yalifanyika na kukamilika.  

  • Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi ya barabara kwa mwaka 2021/22 hadi kufikia Aprili, 2022 ni kama ifuatavyo:
  • Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Soni – Bumbuli – Dindira – Korogwe (km 74) inaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Mtwara – Newala – Masasi (km 210) umekamilika. Aidha, Serikali imekamilisha ujenzi wa sehemu ya Mtwara – Mnivata (km 50).  Mkataba wa ufadhili kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa sehemu iliyobaki ya Mnivata – Tandahimba – Newala – Masasi (km160) umesainiwa. Kwa sasa nyaraka za zabuni zimewasilishwa AfDB kwa ajili ya kupata kibali cha kutangaza (No Objection).
  • Mheshimiwa Spika, kwa Barabara ya Likuyufusi – Mkenda (km 122.50), hadi kufikia Aprili, 2022, Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika. Taratibu za kutangaza zabuni za ujenzi wa barabara hii sehemu ya Likuyufusi – Mhukuru (km 60) zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Nachingwea – Liwale (km 130), hadi kufikia Aprili, 2022, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika.
  • kwa

Ubena Zomozi – Ngerengere (km 11), hadi Aprili, 2022, usanifu wa kina umekamilika na zabuni za kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa barabara hii zimetangazwa.

  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya TAMCO – Vikawe – Mapinga (km 24), taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami zinaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina  wa Barabara ya

Makofia – Mlandizi (km 36.7) zimekamilika.

Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi.

  • Mheshimiwa Spika, kwa Barabara ya Musoma – Makojo – Busekela (km 92), hadi kufikia Aprili, 2022, ujenzi wa barabara hii unaendelea kwa sehemu ya Suguti – Kusenyi (km 5) ambapo umefikia asilimia 74. 
  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya

Kongwa Jct – Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe  

(km  98) unafanyika kwa awamu. Hadi Aprili, 2022, ujenzi wa kilometa 5.8 umekamilika na ujenzi wa kilometa tatu (3) unaendelea na umefikia asilimia 20.

  • ujenzi wa

Muhutwe – Kamachumu – Muleba (km 54) unafanyika kwa awamu. Hadi Aprili, 2022, mradi huu unaendelea na kilometa 29 zimekamilika kwa kiwango cha lami. Aidha, ujenzi wa kilometa 6.5 kwa kiwango cha lami unaendelea na umefikia asilimia 30.

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa  Barabara ya Iringa – Ruaha National Park (km 104), taratibu za kusaini makubaliano ya  mkopo kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya Muheza – Amani (km 36) unafanyika kwa awamu. Hadi Aprili, 2022, kazi za ujenzi wa kilometa 7 zinaendelea na zimefikia asilimia 98. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa ukarabati kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Mtwara – Mingoyo – Masasi (km 200), hadi kufikia Aprili, 2022, taratibu za kupata fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya kugharamia ukarabati wa barabara hii zinaendelea.
  • kwa

Kibaoni – Majimoto – Muze – Kilyamatundu (km 189) hadi kufikia Aprili, 2022, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zimekamilika kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kibaoni – Majimoto – Inyonga (km 152) na Ntendo – Muze – Kilyamatundu (km 200) kwa kiwango cha lami. Aidha, mkataba kwa ajili ya ujenzi wa  sehemu ya Ntendo – Kizungu (km 25) umesainiwa Machi, 2022. Vilevile, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Kizungu – Muze (km 12) zinaendelea.  

  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Daraja la Kigongo – Busisi (J.P. Magufuli) na Barabara Unganishi unaendelea  na hadi Aprili, 2022, mradi umefikia asilimia 40.18.  Aidha, hadi Aprili, 2022 ujenzi wa Daraja la Kitengule na Barabara Unganishi (km 18) umekamilika na kazi ya ujenzi wa barabara unganishi inaendelea na kwa ujumla mradi umefikia asilimia 73.89. Kuhusu Daraja Jipya la Wami, kazi za ujenzi zinaendelea na zimefikia asilimia 72.88. Vilevile, usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mzinga na Daraja la Ugalla, umekamilika. Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa madaraja haya.
  • Mheshimiwa Spika,  kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Morogoro – Dodoma Pamoja na Daraja la

Mkundi inaendelea. Aidha, katika mradi wa 

Barabara ya Njombe – Makete – Isyonje (km 157.4), hadi kufikia Aprili, 2022, ujenzi wa sehemu ya barabara ya Njombe – Moronga (km 53.9) kwa kiwango cha lami umekamilika na  ujenzi wa sehemu ya Moronga – Makete (km 53.5) umefikia asilimia 85. Vilevile, taratibu za manunuzi ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa kilometa 25 za sehemu ya Isyonje – Makete (km 50) zinaendelea ambapo zabuni zimefunguliwa tarehe 22 Aprili, 2022 na tathmini ya zabuni inaendelea.

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Omugakorongo – Kigarama – Murongo (km 105), hadi kufikia Aprili, 2022 mradi huu uko katika hatua za manunuzi ya kumpata

Mkandarasi wa ujenzi.

  • Mheshimiwa Spika, kwa Barabara ya Nanganga – Ruangwa – Nachingwea (km 145), hadi kufikia Aprili, 2022 ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Nanganga – Ruangwa (km 53.2) umefikia asilimia 42. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa sehemu ya Masasi – Nachingwea (km 45) na sehemu ya Ruangwa – Nachingwea (km 47).
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Mpemba – Isongole, hadi kufikia Aprili 2022, ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mpemba – Isongole (km 51.2) ulikuwa umekamilika na ujenzi wa daraja la Songwe unaendelea. Aidha, kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa kina  inaendelea ikiwa ni hatua za maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Ruanda – Iyula – Nyimbili (km 21) na Katumbasongwe – Kasumulu – Ngana – Ileje (km 90.1) kwa kiwango cha lami.
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Tanga – Pangani – Makurunge (km 174.5), hadi kufikia Mei, 2022 ujenzi wa sehemu ya Tanga – Pangani (km 50) unaendelea na umefikia asilimia 37. Aidha, mkataba wa ujenzi wa barabara ya Pangani – Mkange (km 124.5) sehemu ya Tungamaa – Mkange (km 98.9) na ujenzi wa Daraja la Pangani  umesainiwa na Mkandarasi yupo kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi.
  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya Kisarawe – Maneromango (km 54) unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi Aprili 2022, kilometa 20.1 zimekamilika na  ujenzi wa kilometa 3.3 unaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Geita – Bulyanhulu – Kahama (km 174), hadi kufikia Aprili 2022, maandalizi ya kuanza ujenzi wa sehemu ya Geita – Bulyanhulu Jct (km

58.3), Bulyanhulu Jct – Kahama (km 61.7) na

Uyogo – Nyamilangano – Nyandekwa –

Kahama (km 54) yanaendelea. 

  • Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Nyamirembe Port – Katoke (km 50) imekamilika na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Aidha, upembuzi yakinifu na Usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa sehemu ya SIDO – Chato Zonal Hospital (km 5.3) na Chato Ginery – Bwina (km 8.1) umekamilika. Vilevile, taratibu za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Geita – Nzera  (km 54) kwa kiwango cha lamizinaendelea.
  • Mheshimiwa     Spika,       kwa   mradi         wa

Barabara ya Arusha – Moshi – Himo – Holili   (km 199.51), hadi kufikia Aprili 2022, ujenzi wa sehemu ya Sakina – Tengeru na Barabara ya Mchepuo ya Arusha (km 56.51) ulikuwa umekamilika.  Vilevile, ujenzi wa barabara ya Kijenge – Usa River (Nelson Mandela AIST) (km 20) unaendelea. Aidha, Mkataba wa ujenzi wa barabara ya Mianzini – Ngaramtoni (km 18) kwa kiwango cha lami umesainiwa na kwa sasa Mkandarasi yupo kwenye hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi.

Kwa sehemu ya Tengeru – Moshi – Himo na Mizani ya Himo (km 105), tayari Serikali ya Tanzania na Serikali ya Japan zimesaini makubaliano ya mkopo kwa ajili ya upanuzi wa sehemu ya Tengeru – Usa River (km 9.3). Mkopo huo utahusisha pia ujenzi wa Daraja la Kikafu

(mita 560) na barabara unganishi (km 3.5) pamoja na ujenzi wa barabara sehemu ya Moshi Mjini (km 8.4).  Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya usimamizi wa ujenzi zinaendelea.

  • Mheshimiwa Spika, katika mradi wa ujenzi wa Barabara za Kuelekea Kwenye Mradi wa Kufua Umeme Katika Maporomoko ya Mto Rufiji (Access Roads to Rufiji Hydropower Project), hadi Aprili, 2022, ujenzi wa barabara yote ya  Bigwa – Matombo – Mvuha (km 78) kwa kiwango cha lami upo katika hatua za manunuzi ya kumpata Mkandarasi.  Aidha, taratibu za manunuzi ya Mhandisi Mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Ubena Zomozi – Mvuha – Kisaki – Mtemele Jct (km 178) kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami zinaendelea.  Vilevile, ukarabati kwa kiwango cha changarawe wa barabara ya Maneromango – Vikumburu – Mloka (km 100) na Kibiti – Mloka – Mtemele – Rufiji (km 203) unaendelea.    
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro – Dodoma (km 152.30), hadi kufikia Aprili 2022, kazi ya kubainisha itakapopita barabara mpya pamoja na uthamini wa mali zitakazoathirika kwa ajili ya kulipa fidia katika sehemu ya Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro Expressway (km 158) inaendelea. Kwa sehemu ya Mlandizi – Chalinze

(km 44), kazi ya ukarabati inaendelea.  Aidha, ujenzi wa barabara ya Kwa Mathias (Morogoro Road) – Msangani (km 8.3) unaendelea ambapo kilometa 2.95 zimekamilika na mita 400 zinaendelea kujengwa. Vilevile, kazi ya maboresho ya maeneo hatarishi (blackspots) katika mikoa ya Pwani na Morogoro imekamilika.

  • Mheshimiwa Spika, kwa Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo – Msata (km 118.10) kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imekamilika. Serikali inaendelea kutafuta fedha za ukarabati wa sehemu ya Tegeta – Bagamoyo (km 46.9) na ujenzi wa barabara ya Mbegani – Bagamoyo (km 7.2) kwa kiwango cha lami. 
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Usagara – Geita – Buzirayombo – Kyamyorwa (km 110), kazi za ujenzi zimekamilika kwa barabara ya Uyovu – Bwanga – Biharamulo (Lot 1 and Lot 2) (km 110). Aidha,Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Nyakahura – Kumubuga – Rulenge – Kabanga Nickel (km 141) kwa sehemu ya Rulenge – Kabanga Nickel

(km 32), Kumubuga –  Rulenge – Murusagamba (km 75) na Nyakahura – Kumubuga – Murusagamba (km 34).

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 389.7), miradi iliyokamilika ni ujenzi wa

Daraja la Kikwete (Malagarasi), Kidahwe – Uvinza (km 76.6), Tabora – Ndono (km 42),

Ndono – Urambo (km 51.98), Kaliua – Kazilambwa (km 56) na Urambo – Kaliua (km 28). Aidha,hadi Aprili, 2022 ujenzi wa sehemu ya

Kazilambwa – Chagu (km 36) umefikia asilimia

32.5 na ujenzi wa sehemu ya Uvinza –

Malagarasi (km 51.1) unaendelea.   

  • Mheshimiwa Spika,  katika Barabara ya Ifakara – Kihansi – Mlimba – Madeke – Kibena (km 270), taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa sehemu ya Kihansi – Mlimba – Taweta –  Madeke –  Lupembe – Kibena (km 220) kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) zipo katika hatua za mwisho kukamilika.  Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Ifakara – Kihansi (km 50)  zinaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (km 389), mradi upo katika hatua za majadiliano ya kimkataba kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa kilometa 25 za sehemu ya Mbulu –  Garbabi. Aidha, taratibu za kumpata Mkandarasi wa sehemu ya Garbabi – Haydom (km 25) zinaendelea. Kuhusu Barabara ya Marangu – Tarakea – Rongai – Kamwanga /Bomang’ombe – Sanya Juu (km 84.80), kazi za ujenzi zimekamilika kwa sehemu ya Sanya Juu – Alerai (km 32.2) na KIA – Mererani (km 26). Aidha, kilometa 14.75 za ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Kwa Sadala – Masama – Machame Junction (km 16) zimekamilika na mita 350 zinaendelea kujengwa. Kwa upande wa barabara ya Kiboroloni – Kiharara – Tsuduni – Kidia (km 10.8) ujenzi umekamilika kwa kilometa 3.07 na kilometa 1.9 zinaendelea kujengwa. Aidha, Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Tarakea – Holili (km 53) unaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Tukuyu – Mbambo – Katumba (km 60.6), ujenzi wa sehemu ya Bujesi – Mbambo (km 26) na Tukuyu – Mbambo (km 34.6) unaendelea ambapo hadi Aprili, 2022 ulifikia asilimia 60. Aidha, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mbambo – Ipinda (km 19.7) zinaendelea.  
  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Barabara ya Dodoma – Manyoni (km 127) na Barabara ya Mchepuo Kuingia Manyoni Mjini (km 4.8) unahusisha ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi (One Stop Inspection Station – OSIS) cha Muhalala (Manyoni). Mkataba wa awali wa utekelezaji wa mradi huu umesitishwa kutokana na changamoto za kimkataba ambapo utekelezaji wake ulikuwa umefikia asilimia 50. Taratibu za kumpata Mkandarasi mpya wa kumalizia kazi hizo zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, maandalizi ya ujenzi wa Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene – Itobo (km 114) yanaendelea. Aidha, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Namanyere – Katongoro – New Kipili Port (km 64.8) imekamilika. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii.
  • Mheshimiwa Spika,  katika Barabara ya Dumila – Kilosa – Mikumi (km 119), ujenzi wa sehemu ya Rudewa – Kilosa (km 24) unaedelea na umefikia asilimia84.35. Aidha, maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Kilosa – Ulaya – Mikumi (km 72) kwa kiwango cha lami yanaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port (km 162), ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami umekamilika. Aidha, ujenzi wa barabara ya Matai – Kasesya (km 50 )  sehemu ya Matai – Tatanda (km 25) upo katika hatua ya kusaini mkataba na sehemu iliyobaki ya Tatanda – Kasesya (km 25) ipo katika hatua za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Ujenzi wa Madaraja Makubwa miradi iliyotengewa fedha kwa mwaka 2021/22iliyokamilika ni ujenzi wa Daraja la Tanzanite (Dar es Salaam), Daraja la Sibiti (Singida), Daraja la Kiyegeya (Morogoro), Daraja la Magufuli (Morogoro), Daraja la Ruhuhu (Ruvuma), Daraja la Momba (Rukwa), Daraja la Mlalakuwa (Dar es Salaam), Daraja la Magara (Manyara), Daraja la Lukuledi (Lindi) na Daraja la Mara. Miradi mingine iliyokamilika ni Usanifu wa kina wa daraja la Simiyu (Mwanza), Daraja la Mitomoni (Ruvuma), Daraja la Godegode (Dodoma), Daraja la Sukuma (Mwanza), Daraja la Mkenda (Ruvuma), Daraja la Sanza (Singida) na Daraja la Mtera (Dodoma).

Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa Daraja la Msingi (Singida) ambalo utekelezaji wake umefikia asilimia 81 na ununuzi wa Madaraja ya Chuma (Steel Bridges Emergency Parts) uko katika hatua za mwisho. Aidha, kazi ya usanifu wa kina wa Daraja la Malagarasi Chini (Kigoma) inaendelea. Kuhusu ujenzi wa barabara unganishi katika Daraja la Sibiti (Singida), taratibu za manunuzi ya kumpata Mkandarasi zinaendelea.  

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa Barabara ya New Bagamoyo (Kawawa Jct – Tegeta km 18.3) kazi za upanuzi wa sehemu  ya Morocco – Mwenge (km 4.3) zimekamilika. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo (km 222.10), ujenzi wa sehemu ya Kyaka – Bugene (km 59.1) ikijumuisha ujenzi wa Daraja la Mwisa umekamilika. Aidha, mkataba wa ujenzi wa barabara ya Bugene – Kasulo –Kumunazi & Kyaka – Mutukula (km 163) sehemu ya Bugene – Burigi Chato National Park (km 60) umesainiwa na Mkandarasi yupo katika hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi. Katika barabara ya Murushaka – Nkwenda – Murongo (km 125); hadi kufikia Aprili, 2022 zabuni za ujenzi wa sehemu Kyerwa – Chonyonyo (km 50) zimetangazwa. Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa sehemu iliyobaki yenye urefu wa kilometa 75 zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, katika mradi wa Barabara ya Isaka – Lusahunga (km 242.2), kazi za ukarabati wa sehemu ya  Isaka – Ushirombo (km 132.2) na Ushirombo – Lusahunga (km 110) zimekamilika. Aidha, manunuzi ya kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ukarabati kwa kiwango cha lami wa sehemu ya  Lusahunga – Rusumo (km 92) yapo katika hatua ya mwisho. Kwa upande wa ujenzi wa Kituo cha Ukaguzi cha Nyakanazi, mkataba wa awali umesitishwa kutokana na changamoto za kimkataba. Taratibu za kumpata Mkandarasi mpya wa kumalizia kazi hizo zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora (km 259.7) ujenzi wa barabara umekamilika kwa sehemu ya Tabora – Nyahua (km 85), Nyahua – Chaya (km 85.4) na Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35).
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa ajili ya miradi ya Barabara za Mikoa  ni kilometa 770.5 na ujenzi wa madaraja 34.  Kati ya hizo, kilometa 698.3 zilipangwa kukarabatiwa kwa kiwango cha changarawe na kilometa  72.2 kujengwa kwa kiwango cha lami.

Hadi kufikia Aprili 2022, kilometa 307.41 sawa na asilimia 44.02 ya malengo ya barabara za mikoa zilikuwa zimekarabatiwa kwa kiwango cha changarawe na kilometa 34.8 sawa na asilimia 48.19 ya lengo, zimejengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, ujenzi wa madaraja ulikamilika kwa asilimia 6.42.  

  • Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili 2022, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea kwa ajili ya ukarabati wa

Barabara ya Mwanza/Shinyanga Border – Mwanza (km 102) kwa kiwango cha lami.   

  • Mheshimiwa Spika, katika mradi wa barabara za kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam, hadi Aprili, 2022 miradi iliyokamilika ni ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana (km14), Tegeta – Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi (km 20) sehemu ya Mbezi Mwisho – Goba,  Tangi Bovu – Goba (km 9), Kimara Baruti –  Msewe – Changanyikeni (km 2.6), Banana – Kitunda – Kivule – Msongola, (km 14.7) sehemu ya Kitunda– Kivule (km 3.2), Ardhi – Makongo – Goba (sehemu ya Goba – Makongo km 4) na Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road (sehemu ya Mbezi Mwisho – Goba km 7), Wazo Hill – Madale (km 9) na Wazo Hill (Madale) – Goba (km 5).

Mradi unaoendelea kutekelezwa ni ujenzi wa barabara ya Ardhi – Makongo – Goba (sehemu ya Ardhi –Makongo km 5) ambao hadi Aprili, 2022 umefikia asilimia 84. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi  wa upanuzi wa  barabara ya Mwai Kibaki (km 9),  Mjimwema – Kimbiji – Pembamnazi (km 27), Kongowe – Mjimwema – Kivukoni Ferry (km 25.1), Kibamba – Kisopwa – Kwembe – Makondeko (km 14.66) sehemu ya Mloganzila – Mloganzila Citizen (km 4) na Goba – Matosa – Temboni (km 6).

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Nyamuswa – Bunda – Kisorya (km 106), ujenzi wa barabara ya Kisorya – Bulamba (km 51) umekamilika na ujenzi wa barabara ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba (km 56.4)

unaendelea na umefikia asilimia 35.Vilevile,  upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Kolandoto – Lalago – Ng’oboko – Mwanhuzi (km 122) umekamilika na barabara hii itajengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi kufikia Aprili 2022, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Daraja la Itembe kwenye barabara hii zinaendelea.  

  • Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Ndundu – Somanga (km 60) umekamilika. Aidha, Serikali inaendelea na maandalizi ya ukarabati wa sehemu za Kongowe – Ndundu (km 160.65) na

Nangurukuru – Mbwemkuru (km 95).

  • Mheshimiwa Spika,  hadi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Barabara ya Kasulu – Manyovu pamoja na barabara za kuingia Kasulu Mjini (km 68) ulikuwa unaendelea na umefikia asilimia 18. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa Barabara ya Mzunguko katika Jiji la Dodoma City Outer Dual Carriageway Ring Road Lot1 & 2 (km 112.3), ujenzi wa sehemu ya Nala – Veyula – Mtumba – Ihumwa Dry Port (km 52.3) unaendelea na umefikia asilimia 2.23 na ujenzi wa sehemu ya  Ihumwa Dry Port – Matumbulu – Nala (km 60) umefikia asilimia 3.

Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Makulu Jct. – Ntyuka R/About – Image R/About – Bahi R/About (km 6.3) imekamilika. Taratibu za kukamilisha mkopo wa mradi huu kutoka Serikali ya Japan zinaendelea. Aidha,  mkataba wa ujenzi wa barabara ya Ntyuka Jct – Mvumi – Kikombo Jct. (km 76.07) na Chololo – Mapinduzi (JWTZ HQ) (km 5) sehemu ya Ntyuka Jct. – Ng’ong’ona Jct (km 8.6) na sehemu ya Kikombo Jct – Chololo – Mapinduzi (TPDF HQ) (km 16.4) umesainiwa na Mkandarasi yupo katika hatua za kuanza ujenzi.Vilevile, taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri atakayefanya kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya Upanuzi wa Barabara Kuu zinazoingia Katikati ya Jiji la Dodoma (km 220)  zipo katika hatua ya mwisho.

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Kidatu –  Ifakara – Lupiro – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 512), hadi Aprili 2022, kazi za ujenzi kwa sehemu ya Kidatu – Ifakara (km 66.9) zilikuwa zinaendelea na zimefikia asilimia 51.1. Aidha, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa sehemu ya Ifakara – Lupiro – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 396) umekamilika naSerikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi.  
  • Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Barabara ya Tabora – Ipole – Koga – Mpanda (km 383) umekamilika. Mradi huu ulihusisha ujenzi wa sehemu ya Usesula – Komanga (km 115),  Komanga – Kasinde (km 120),  Tabora – Sikonge (Usesula) (km 30) na Kasinde – Mpanda (km 118).   
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Makutano – Natta – Mugumu/Loliondo – Mto wa Mbu (km 235), hadi Aprili 2022, kazi za ujenzi wa barabara ya Makutano – Natta

(Sanzate) (km 50) zilikuwa zimefikia asilimia 94 na kwa sehemu ya Sanzate – Natta (km 40) ujenzi umefikia asilimia 11.  Aidha, kazi za ujenzi kwa barabara ya Loliondo – Mto wa Mbu (km 213); Sehemu ya Waso – Sale (km 50) zimefikia asilimia 97.36 na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Natta – Mugumu (km 45) 

yanaendelea. Vilevile, mkataba wa ujenzi wa kwa kiwango cha lami wa barabara ya Tarime – Mugumu (km 86): sehemu ya Tarime – Nyamwaga (km 25) umesainiwa na Mkandarasi yupo katika hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi. Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Nyamwaga – Mugumu (km 61) zinaendelea.  

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Ibanda – Itungi Port/Kajunjumele – Kiwira Port (km 66.6), taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Ibanda – Itungi Port (km 26) zinaendelea.

Aidha,kazi za ujenzi wa sehemu ya Kikusya – Ipinda – Matema (km 39.1) zimekamilika na ukarabati wa barabara ya Uyole – Kasumulu, sehemu ya Ilima Escarpment (km 3) zimefikia asilimia 95. Maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Kajunjumele (Iponjola) – Kiwira Port (km 6) yanaendelea na ujenzi wa Kasumulu/ Songwe – Tanzania/Malawi Border OSBP unaendelea na umefikia asilimia 80. 

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Nzega – Tabora (km 289.7), ujenzi wa sehemu ya Nzega – Puge (km 58.6) na Puge – Tabora (km 56.1) umekamilika.Maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Nzega – Kagongwa (km 65) yanaendelea na mkataba wa kufanya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ukarabati wa sehemu ya Shelui – Nzega (km 110)umesainiwa.  
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Sumbawanga – Mpanda – Nyakanazi (km

541.5), ujenzi wa sehemu za Sumbawanga –

Kanazi – Kizi – Kibaoni (km 151.6), Sitalike – Mpanda – Ifukutwa – Vikonge (km 73.65) umekamilika.Aidha, Mkataba wa  ujenzi wa sehemu ya Vikonge – Luhafwe (km 25) umesainiwa na taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Luhafwe – Bulamata (km 37.35) zinaendelea.  

Hadi kufikia Aprili 2022,Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Kibaoni – Sitalike (km 71.0): sehemu ya Kibaoni – Mlele (km 50) umesainiwa tayari kwa kuanza ujenzi. Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Sitalike – Mlele (km 21) zinaendelea. Vile vile,  Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa sehemu ya Kizi – Lyambalyamfipa – Sitalike (km 86.31).

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya

Nyanguge – Musoma, Mchepuo wa Usagara – Kisesa na Bulamba – Kisorya (km 202.25) ujenzi wa sehemu ya Usagara – Kisesa (Mwanza Bypass, km 16.35) na ukarabati wa sehemu ya Simiyu/Mara Border – Musoma (km 85.5) umekamilika. Aidha,  Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ukarabati wa Barabara ya Nyanguge –

Simiyu/Mara Border (km 100.4)

  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Magole – Mziha – Handeni (km 149.2), mradi umekamilika kwa sehemu ya Magole – Turiani (km 48.8). Aidha, hadi kufikia Aprili, 2022 maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Turiani – Mziha – Handeni (km 104) yalikuwa yanaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Ujenzi wa

Barabara za Juu (Flyovers) Jijini DSM na

Barabara Unganishi umeendelea kutekelezwa ambapo kazi zilizokamilika ni ujenzi wa Mfugale Flyover na “Interchange” ya Ubungo (Kijazi Interchange).  Aidha,kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mradi wa Ujenzi wa Barabara za Juu (Flyovers) kwenye Makutano Nane (8) ya Barabara za Jijini Dar es Salaam (Mwenge, Morocco, Magomeni, Selander, Fire, Osterbay, Buguruni na Tabata) zimekamilika. Vilevile, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Mabey Flyovers Jijini Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza.  

  • Mheshimiwa Spika,  kuhusu Barabara ya Mwigumbi – Maswa – Bariadi – Lamadi (km 181.8), mradi umekamilika kwa sehemu za Bariadi – Lamadi (km 71.8), Mwigumbi – Maswa (km 50.3) na Maswa – Bariadi (km 49.7). Aidha, ujenzi wa barabara ya Mchepuo wa Maswa (km 11) unaendelea na umefikia asilimia 10. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa sehemu ya Isabdula (Magu) – Bukwimba Station – Ngudu – Ng’hungumalwa (km 53).
  • Mheshimiwa Spika,  hadi kufikia Aprili 2022, maandalizi ya ujenzi wa Barabara ya Tabora – Ipole – Rungwa (Sehemu ya Ipole – Rungwa, km 172) yalikuwa yanaendelea.  Aidha, katika Barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi (km 341.25), ujenzi wa sehemu  ya

Kidahwe – Kasulu (km 63.0) na Nyakanazi – Kakonko (Kabingo) (km 50) umekamilika. Aidha, ujenzi wa sehemu ya Kanyani Junction –

Mvugwe (km 70.5) umefikia asilimia 17.14, Mvugwe – Nduta Junction (km 59.35) umefikia asilimia 25, Kibondo Junction – Kabingo (km 62.5) umefikia asilimia 20na Nduta Junction – Kibondo (km 25.9) umefikia asilimia 44.1. Vilevile, taratibu  za manunuzi ya Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibondo – Mabamba (km 48) zinaendelea.

  • Mheshimiwa Spika, kazi za ujenzi wa Barabara ya Kwenda Kiwanja cha Ndege cha Mafia (km 16) zimekamilika. Kuhusu mradi wa ujenzi wa Daraja la Nyerere (Kigamboni) na Barabara Unganishi, ujenzi wa Daraja la Nyerere, barabara ya Kigamboni (Daraja la Nyerere) – Vijibweni (km 1.5)  na barabara ya Tungi – Kibada (km 3.8) umekamilika.  Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibada – Mwasonga – Tundwisongani Jct/Tundwisongani – Kimbiji (km 41.0) zinaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ukarabati kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mutukula – Bukoba – Muhutwe – Kagoma (km 112) zinaendelea. Aidha, kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Bukoba – Busimbe – Maluku – Kanyangereko – Ngongo (km 19.1) na Kanazi (Kyetema) – Ibwera – Katoro – Kyaka II (km 60.7) zinaendelea. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa upanuzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (km 19.2) ikijumuisha Upanuzi wa Madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji, ujenzi wa barabara hii unaendelea. Hadi Aprili, 2022 mradi umefikia asilimia 86 baada ya nyongeza ya kazi za mkataba. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa Barabara ya Kisarawe – Mlandizi (km 119) kwa kiwango cha lami. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa ujenzi wa Barabara ya Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju (km 34.0), hadi kufikia Aprili, 2022 kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara  za Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju (km 21.3) na Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho (km 12.7)  kwa ajili ya kuijenga kwa njia sitailikuwa katika hatua ya manunuzi.  Serikali inaendelea kutafuta fedha za kazi hizi. 
  • Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara ya

Muleba – Kanyambogo – Rubya (Leopord Mujungi km 18.5) katika mradi wa Barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 172.5) umekamilika.

  • Mheshimiwa Spika, mkataba wa kufanya

Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa Barabara ya Singida – Shelui (km 110) umesainiwa.Kuhusu Barabara ya Dar es Salaam – Mbagala (Kilwa Road) – Gerezani (Sehemu ya Kamata – Bendera Tatu km 1.3) hadi Aprili, 2022 kazi za Upanuzi wa Daraja la Gerezani zilikuwa zimefikia asilimia 78.8. Utekelezaji wa mradi ulisimama kutokana na changamoto za UVIKO 19. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha za upanuzi na ukarabati wa sehemu ya Mbagala Rangi Tatu – Kongowe (km 3.8).  

  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Msimba – Ruaha Mbuyuni/Ikokoto Mafinga (km 535.25) kazi za ukarabati kwa sehemu ya Mafinga – Igawa (km 137.9) na usanifu wa kina wa sehemu ya Mafinga – Mgololo (km 78) umekamilika.  Aidha, hadi kufikia Aprili, 2022, maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Rujewa – Madibira – Mafinga (km 152.0) yanaendelea. Kuhusu barabara ya  Morogoro – Iringa (Tumbaku Jct. Mangae/Melela – Mikumi – Iyovi) (km 158.45), taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati wa barabara hiyo zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Same – Mkumbara – Korogwe (km 147.5), upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa sehemu za Same – Himo (km 76.0) na Mombo – Lushoto (km 32) umekamilika na Serikali inaendelea kutafuta fedha za ukarabati kwa kiwango cha lami wa barabara hizi. Aidha, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya upembuzi na usanifu wa kina wa barabara ya Lushoto – Magamba – Mlola (km 34.5).

Kwa upande wa barabara ya Same – Kisiwani – Mkomazi (km 97); upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika. Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii kwa sehemu yenye urefu wa kilometa 5.2 amepatikana.

  • Mheshimiwa Spika, katika mradi wa Barabara ya Mbeya – Makongolosi (km 267.9), kazi za ujenzi zimekamilika kwa sehemu za Mbeya – Lwanjilo – Chunya (km 72) na Chunya – Makongolosi (km 39).  Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Noranga – Itigi – Mkiwa (km 56.9) umesainiwa. Aidha,Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa barabara ya Makongolosi – Rungwa – Noranga (km 356) na Mbalizi – Makongolosi (km 50) kwa kiwango cha lami.
  • Mheshimiwa Spika, katika Barabara ya Itoni – Ludewa – Manda (km 211), kazi za ujenzi kwa kiwango cha zege kwa sehemu ya  Lusitu – Mawengi (km 50) zinaendelea na zimefikia asilimia 85. Aidha, hadi kufikia Aprili 2022, mkataba wa ujenzi wa sehemu ya barabara ya Itoni – Lusitu (km 50) umesainiwa.
  • Mheshimiwa Spika, katika mradi wa Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 460), mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Handeni – Mafuleta (km 20) umesainiwa na sehemu ya Mafuleta – Kibirashi (km 30) zipo katika hatua za manunuzi ya Mkandarasi wa ujenzi. Aidha, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya  Kongwa – Kibaya – Arusha (km 430)  na Singida – Sepuka – Ndago – Kizaga (km 75) umekamilika.
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Makambako – Songea na Barabara ya Mzunguko ya Songea (km 295), hadi kufikia Aprili 2022, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwenye barabara ya mchepuo ya Songea umekamilika.  Aidha, taratibu za kupata fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya kugharamia ukarabati wa barabara ya Makambako – Songea (km 295) zinaendelea.
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa Barabara ya Dodoma – Iringa (km 273.3), hadi kufikia Aprili 2022, ujenzi kwa kiwango cha lami wa mita 450 za Barabara ya Mchepuo wa Iringa (km 7.3) ulikuwa umekamilika na ujenzi wa madaraja madogo kwenye sehemu iliyobaki unaendelea. Aidha, kazi za uimarishaji wa matabaka ya barabara katika barabara ya  Iringa – Dodoma (km 266) zinaendelea.
  2. Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi wa Barabara ya Dodoma – Babati (km 263.4) umekamilika kwa sehemu ya Dodoma – Mayamaya – Mela – Bonga – Babati (km

250.8). Aidha, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mchepuo wa Babati (km 15.5) umekamilika.

  1. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara  ya Masasi – Songea – Mbamba Bay (km 623) umekamilika. Kuhusu  sehemu ya Kitai – Lituhi (km 90), ujenzi  kwa kiwango cha lami wa kilometa 5 umekamilika na mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Amanimakoro – Ruanda (km 35) umesainiwa tarehe 14 Aprili, 2022. Aidha, taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu iliyobakia kilometa 50 za barabara hii zinaendelea. 
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa

Barabara za Chuo cha Uongozi (Uongozi

Institute, km 8.8) Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.  

  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara za Igawa – Songwe – Tunduma na Mchepuo wa Mbeya (km 273.40), hadi kufikia Aprili 2022, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina  wa barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (km 218.0)  na Uyole – Songwe (Mbeya Bypass, km

48.9) umekamilika. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ukarabati wa sehemu ya Uyole – Ifisi (km 29) zinaendelea. Aidha, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Iwambi – Mbalizi Bypass (km 6.5) ziko katika hatua za manunuzi.

  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu  mradi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Pili Hadi Tano (BRT Phase II – V: km 69.8), kazi za ujenzi wa barabara ya Mabasi

Yaendayo Haraka Awamu ya Pili (CBD –

Mbagala, km 20.3)zimefikia asilimia 50. Aidha, mkataba wa ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tatu (CBD – Gongolamboto km 23.33)umesainiwa. Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Nne (Ali Hassan Mwinyi – Morocco – Mwenge – Tegeta  na Mwenge – Ubungo km 30.12). Kuhusu mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tano unaohusisha ujenzi wa barabara ya Bandari ya Dar es Salaam – Mandela – Kawawa – Kigogo – Tabata – Segerea (km 26.5), kazi ya upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina umekamilika. 

Kuhusu Maboresho ya Barabara za BRT Awamu ya Kwanza (Jangwani), hadi kufikia Aprili, 2022, kazi ya usanifu wa kina zimekamilika katika eneo la Jangwani chini ya Mradi wa Maboresho ya Usafiri Dar es Salaam (DUTP) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

  1. Mheshimiwa Spika,  kuhusu mradi wa Ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (Institute of Construction Technology – ICoT), hadi Aprili, 2022, ujenzi wa jengo jipya la Taaluma na Utawala ICoT Morogoro upo katika hatua ya kumpata Mkandarasi. Aidha,

Ujenzi wa Makao Makuu ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), unaendelea na mradi umefikia asilimia 40.5.

  1. Mheshimiwa Spika, fedha za Mfuko wa Barabara zinatumika kutekeleza miradi mbalimbali ya barabara nchini. Kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa mwaka 2021/22 katika Barabara Kuu kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kilometa 5,310 za barabara.  Hadi  Aprili, 2022  hatua iliyofikiwa katika miradi hiyo ni kama ifuatavyo:

a.     Miradi ambayoUpembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina umekamilika:

                               i.      Barabara ya Musoma – Makojo –

Busekela (km 92) ii. Barabara ya Mtwara Pachani – Lusewa – Lingusenguse – Nalasi

(km 211) iii. Barabara ya    Kiranjeranje     –

Namichiga – Ruangwa (km 120) iv. Barabara ya Kibaoni – Majimoto

– Inyonga (km 152) 

                             v.       Barabara za Mkiu – Liganga

Madaba (km 112); Liganga – Nkomang’ombe (km 70) na Nkomang’ombe – Coal Power

Plant (km 4.14) vi. Barabara ya  Utete – Nyamwage

(km 34) 

                          vii.               Barabara ya Mbamba Bay –

Lituhi  (km 121)  viii. Barabara ya  Magu – Bukwimba – Ngudu – Hungumalwa (km 64)

  • Miradi ambayoUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina unaendelea: 

i. Barabara ya Mpanda – Ugalla – Kaliua – Ulyankulu – Kahama

(km 457) ii. Barabara ya Babati (Dareda) –

Dongobeshi (km 60) iii. Barabara ya Soni – Bumbuli –

Dindira – Korogwe (km 70) iv. Barabara ya Mkuyuni – Nyakato

(km 10)

                             v.               Barabara ya Nangurukuru –

Liwale  (km 210) vi. Barabara ya Singida Bypass (km

46) vii. Barabara ya Songea Bypass (km

11) viii. Barabara ya Mpwapwa – Gulwe – Rudi – Chipogoro; Sehemu ya

Kibakwe – Chipogoro (km 75.84)

  1. Barabara ya Ntendo – Muze

Kilyamatundu (km 200)

  • Barabara   ya    Ushirombo        –

Nyikonga – Geita (Katoro)  (km

59) xi.   Barabara ya Makete – Ndulamo –

Nkenja – Kitulo (km 42)

xii.     Barabara ya  Namanyere – Katongoro – New Kipili Port (km

64.8)  xiii.      Barabara ya  Kagwira – Ikola –

Karema (km 112) xiv.    Barabara ya Singida Mjini –

Ilongero – Haydom (km 93)  xv. Barabara ya  Goba – Matosa – Temboni/Morogori Road Jct And Makabe/Mbezi Mwisho – Goba Jct

– Msakuzi (km 15)  xvi. Barabara ya  Mbalizi – Mkwajuni

                                          (Galula        –        Mkwajuni        –

Makongolosi (km 61) xvii.      Barabara ya  Mwanza Urban Along Mwanza – Nyanguge (km

25)xviii. Barabara ya  Bariadi – Kisesa – Mwandoya – Ngoboko –Mwanhuzi

– Sibiti –Mkalama – Iguguno 

(Sehemu ya Mkalama – Iguguno)

(km 89) xix. Barabara ya  Bariadi – Salama – Ng’haya – Magu (km 76) 

  • Barabara ya Nyakato – Veta

Buswelu (km 3)

  • Barabara     ya    Simanjiro

(Orkesumet) – Kia – Mererani (Part of Kongwa Ranch – Kiteto –

Simanjiro – Kia (km 60)

  • Barabara ya Ulemo – Kinampanda – Gumanga –

Mkalama (km 49) xxiii. Barabara ya  Airport – Igombe – Nyanguge (km 46)

  • Miradi ambayo ipo katika taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina: 

                               i.      Mteremko wa Mlima Kitonga (km

10) ii. Barabara ya Morogoro (Tumbaku Roundabout) – Mangae/Melela – Mikumi – Iyovi  (km 156.45) na

Daraja la Doma iii. Barabara ya Morogoro (Msamvu Roundabout) – Morogoro Centre –

Bigwa Junction (km 10) iv. Barabara ya Mlandizi – Chalinze

– Chalinze – Morogoro

v. Daraja la Kyabakoba na Kamashango na Barabara za unganishi katika barabara ya

Mhutwe – Kamachumu – Muleba vi.       Daraja la Bujonde

                          vii.     Upanuzi wa Barabara ya Arusha

– Kisongo (km 8.8)   

                        viii.               Barabara ya Omurushaka –

Murongo (km 125)     

  • Miradi Mingine inayotekelezwa ni:
  1. Kuimarisha Uwezo wa Maabara (Central Material Labolatory – CML) Katika Kupima Vifaa vya Ujenzi na

Kuanzisha Teknolojia ya Kisasa ya

(Asphalt Mix Design)

Kazi ya kuimarisha uwezo wa maabara ya vifaa vya ujenzi na mafunzo mbalimbali kwa ajili ya utumiaji wa Mwongozo wa uchanganyaji wa lami zilikuwa zinaendelea.

  1. Mifumo ya Kompyuta (Software) kwa Ajili ya Usanifu wa Barabara na Kuandaa Mipango ya Usafiri (Highway

/Transport Planning)

Taratibu za ununuzi wa mifumo ya kompyuta ya kufanya tathmini za kiuchumi (HDM 4) na leseni za kutumia mfumo wa usanifu wa kina (MIDAS) zinaendelea. 

Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Vivuko na Maegesho ya Vivuko 

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) iliendelea kutekeleza miradi ya ujenzi  na ukarabati wa maegesho ya vivuko. Hadi Aprili, 2022, miradi iliyokamilika ni upanuzi wa jengo la abiria katika maegesho ya Magogoni – Kigamboni upande wa Kigamboni Jijini Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kukamilisha usimikaji wa mfumo wa kielektroniki wa kukatia tiketi (N-Cards System). Kazi nyingine zilizokamilika ni ujenzi wa maegesho ya Nyamisati – Mafia upande wa Nyamisati na ujenzi wa miundombinu ya Kayenze – Bezi upande wa Kayenze. 

Miradi inayoendelea ni ujenzi wa maegesho ya Kayenze – Kanyinya; maegesho ya Zumacheli katika kivuko cha Chato – Nkome na ujenzi wa maegesho ya Nyamisati – Mafia upande wa Mafia. Vilevile,  ukarabati wa maegesho ya vivuko unaendelea katika vituo vya Magogoni – Kigamboni,  Iramba – Majita na Nyakarilo – Kome. Kazi nyingine zinazoendelea ni ujenzi wa nyumba ya watumishi upande wa Bezi; ujenzi wa miundombinu katika kituo cha Musoma – Kinesi upande wa Musoma (Mwigobelo) na Chato; ujenzi wa miundombinu ya kituo cha Mwaya – Kajunjumele (Itungi Port) na ujenzi wa maegesho ya Mlimba – Malinyi.

Miradi iliyo katika hatua za manunuzi ni ujenzi wa maegesho ya vivuko vya Ikuza – Muleba, Ijinga – Kahangala na Bwiro – Bukondo  pamoja na miundombinu ya vituo nane (Bugolora, Ukara, Kome, Maisome, Kahunda, Nkome, Kisorya na

Kinesi).  

  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya ununuzi wa vivuko, hadi Aprili, 2022, ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Kisorya na Rugezi (Mwanza) upo katika hatua za awali za ujenzi. Vivuko vitakavyotoa huduma kati ya Ijinga – Kahangala (Magu), Bwiro – Bukondo (Mwanza), Nyakarilo – Kome (Geita), kivuko cha pili cha Nyamisati – Mafia (Pwani) na ununuzi wa vifaa vya karakana za TEMESA kwa ajili ya kuboresha huduma ya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali vipo katika hatua mbalimbali za manunuzi. Aidha, mradi wa kusanifu na kusimika Mfumo wa Kusimamia Uendeshaji wa Huduma za Vivuko unaendelea.
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya Ukarabati wa Vivuko iliyopangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2021/22 hadi Aprili, 2022, ukarabati mkubwa wa MV Mafanikio na MV Sabasaba umekamilika.  Miradi inayoendelea ni ukarabati wa MV Musoma, Old MV Ruvuvu, MV Nyerere na MV Kilombero II pamoja na ukarabati wa mitambo ya ICoT. Miradi iliyo katika hatua za manunuzi ni pamoja na ukarabati MV Mara, MV Ujenzi, MV Ruhuhu, MV Misungwi, MV Kome II,  MV Kyanyabasa na MV Tanga. 

Utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) iliendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa nyumba  na majengo ya Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22.
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022, ujenzi wa nyumba 20 za Viongozi Jijini Dodoma umefikia asilimia 90 na ujenzi wa nyumba 150 za makazi ya Watumishi wa Umma katika eneo la Nzuguni Jijini Dodoma umefikia asilimia 90. Aidha, hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa nyumba za Majaji ni Kilimanjaro (asilimia 70), Mtwara (asilimia 75),  Shinyanga (asilimia 75)  na Tabora (asilimia 98.5). 
  1. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara kupitia TBA ilipanga kuanza ujenzi wa nyumba za  makazi kwa ajili ya watumishi wa Umma Ilala Kota. Hata hivyo, mradi huu umehamishwa kutoka Ilala kwenda Magomenikutokana na kutokamilika kwa maandalizi ya eneo la mradi. Hadi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 15.

Kuhusu mradi wa ukarabati wa nyumba 40 za Viongozi Dodoma, hadi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 75.7. Kwa upande wa ukarabati wa nyumba 30 za Viongozi mikoani pamoja na matengenezo kinga ya majengo ya

Magomeni Kota, utekelezaji umefikia asilimia 98.Ukarabati wa nyumba 40 kati ya 66 zilizohamishiwa TBA kutoka CDA unaendelea ambapo hadi Aprili, 2022 umefikia asilimia 70. Aidha, utekelezaji wa ukarabati wa nyumba zilizokuwa zinamilikiwa na TAMISEMI/NHC katika mikoa 20 zilizohamishiwa TBA umefikia asilimia 32. Vilevile, ununuzi wa samani kwa nyumba za Ikulu Ndogo umefanyika katika Mkoa wa Dodoma.

  1. Mheshimiwa Spika, mradi mwingine unaotekelezwa ni Ujenzi na Ukarabati wa Karakana za TEMESA na TBA. Ujenzi wa karakana mpya ya Mkoa wa  Simiyu Awamu ya I umekamilika na ujenzi wa karakana ya TEMESA Mkoa wa Simiyu Awamu ya II na maeneo mengine unaendelea. Aidha, ukarabati wa karakana za TEMESA mikoa ya Mbeya, M.T Depot – Dar es Salaam, Pwani, Vingunguti, karakana ya TEMESA Wilaya ya Same na Karakana ya samani TBA Dodoma umekamilika. 

Miradi ya karakana inayoendelea ni pamoja na ununuzi wa vifaa vya karakana, mfumo wa kuratibu uendeshaji wa vivuko (Electronic Ferries Management Information System – EFMIS) pamoja na ujenzi wa karakana ya Mkoa wa Simiyu Awamu ya II. Ukarabati wa karakana ya Arusha na Ruvuma upo katika hatua ya usanifu.  Vilevile, mradi wa ununuzi na uendeshaji wa karakana zinazohamishika upo katika hatua ya manunuzi na maeneo kwa ajili ya kuanzisha karakana mpya za Wilaya yamepatikana katika maneo ya Simanjiro, Kyela, Chato, Mafia na Masasi.

Usalama Barabarani  na Mazingira

  1. Mheshimiwa Spika, miradi yausalama barabarani na kudhibiti uzito wa magari yanayotumia          barabara           zetu iliyopangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2021/22 ni pamoja na  ufungaji wa vifaa vya kisasa vya upimaji (load cells) katika mizani 42 iliyopo katika shoroba zote za barabara kuu nchini.  Hadi Aprili, 2022 uwekaji wa vifaa vya kisasa vya upimaji wa magari umefanyika katika mizani ya Nala, Mpemba, Njuki na Makuyuni. Aidha, taratibu za manunuzi ya kumpata Mshauri Elekezi wa kufanya maboresho katika Mfumo wa Kukusanya       Taarifa           za      Ajali Barabarani zimekamilika     na           mkataba    wa     kazi   hii unaandaliwa. 
  1. Mheshimiwa     Spika,      mradi         mwingine uliopangwa kutekelezwa ni Usimikaji wa Mfumo wa Uangalizi wa Utendaji Kazi (Weighbridge

Management System) katika mizani 42. Hadi Aprili, 2022, manunuzi ya kumpata Mshauri Elekezi atakayefanya usimikaji wa mfumo huo yanaendelea.  Aidha, Wizara inaendelea na taratibu za manunuzi ya kuwapata Washauri Elekezi  kwa ajili ya kufanya tathmini ya usalama barabarani ili kubaini athari za kijamii na kiuchumi pamoja na kufanya mapitio ya miongozo ya usalama barabarani.  

  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya mazingira, Wizara ilipanga kuandaa mkakati wa kukabili majanga kwa Sekta ya Ujenzi (Works Sector Disaster Management Strategy) na kuanzisha mfumo wa kusimamia na kukusanya taarifa za mazingira (Environmental Information Management System). Kazi nyingine ni kufanya mapitio ya miongozo ya tathmini na usimamizi wa mazingira ya Sekta ya Ujenzi na kuandaa mpango wa usimamizi wa mazingira wa miaka mitano (Sector Environment Action Plan, 2021 – 2026). Hadi sasa, maandalizi ya taratibu za manunuzi ya kuwapata Washauri Elekezi kwa ajili ya miradi hii yanaendelea.

MIRADI YA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA

VIWANJA VYA NDEGE

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Wizara ilipanga kuendelea na ujenzi wa viwanja vipya vya Ndege vya Geita, Simiyu na Msalato. Aidha, Wizara ilipanga kufanya ukarabati, upanuzi na uboreshaji wa jumla ya viwanja vya Ndege 23 nchini ambavyo ni pamoja na Viwanja vya Ndege vya Kigoma, Mpanda, Tabora, Songwe, Mwanza, Arusha, Mtwara, Sumbawanga, Shinyanga, Iringa, Musoma, Songea, Dodoma, Tanga, Lake Manyara, Lindi, Moshi, Bukoba, Julius Nyerere International (JNIA) na Viwanja vingine vya Ndege vya Mikoa.
  1. Mheshimiwa Spika, uboreshaji na ukarabati wa Viwanja vya Ndege vya Sumbawanga, Shinyanga, Tabora na Kigoma vinatekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB). Hadi kufikia Aprili, 2022, Mfadhili (EIB) tayari ametoa fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi kwa viwanja vya Sumbawanga, Shinyanga na Tabora. Kwa upande wa Kiwanja cha Ndege cha Kigoma, mradi upo katika hatua ya manunuzi ya kupata Mkandarasi wa ujenzi.
  1. Mheshimiwa Spika, katika Kiwanja cha Ndege cha Songwe kazi za ukarabati wa barabara ya kutua na kuruka ndege pamoja na eneo la usalama (Runway End Safety Area-RESA) zimekamilika na kazi za usimikaji wa taa za kuongozea ndege (Airfield Ground Lighting – AGL) zimefikia asilimia 90. Aidha, Mkandarasi kwa ajili ya kazi ya kumalizia jengo la abiria anaendelea na utekelezaji umefikia asilimia 17 ya kazi alizoingia mkataba na hivyo kufanya jumla ya asilimia 81 ya utekelezaji wa jengo la abiria.
  1. kuhusu Kiwanja cha

Ndege cha Mwanza, Serikali imekamilisha usanifu wa Jengo la Abiria litakalokuwa na uwezo wa kuhudumia takriban abiria milioni mbili kwa mwaka. Aidha, mazungumzo na Washirika wa Maendeleo yanaendelea kwa ajili ya kupata fedha za kugharamia ujenzi wa jengo hilo pamoja na miundombinu yake.

  1. Mheshimiwa Spika, kazi ya upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara inaendelea na utekelezaji umefikia asilimia 89. 
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato,  ulipaji wa fidia kwa ajili ya wananchi watakaoathiriwa na utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 98. Aidha, Mkataba wa Awamu ya Kwanza (Package 1) kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege, maegesho ya ndege, mitambo na taa za kuongozea ndege pamoja na barabara za maungio umesainiwa na Mkandarasi yupo katika maandalizi ya kuanza ujenzi. Vilevile, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kusaini Mkataba wa Awamu ya Pili (Package II) kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Abiria, Jengo la kuongozea ndege, Kituo cha Zimamoto, Kituo cha Hali ya Hewa na Vituo vidogo nane (8) vya kufua umeme kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
  1. kuhusu kiwanja cha

Ndege cha Musoma, kazi ya upanuzi na ukarabati wa barabara ya kutua na kuruka ndege, maegesho ya ndege,  barabara ya kiungio na uzio wa usalama inaendelea na utekelezaji umefikia asilimia 10. Aidha, kazi ya upanuzi na ukarabati wa kiwanja cha Ndege cha Songea inaendelea na utekelezaji umefikia asilimia 95 katika kazi za ‘airside pavement’. Kwa ujumla, utekelezaji wa mradi wote umefikia asilimia 75.  Vilevile, katika Kiwanja cha Ndege cha Moshi, Serikali inaendelea na ukamilishaji wa taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya uboreshaji wa Viwanja vya ndege vya Lindi, Bukoba, Mpanda na Arusha.

  1. Mheshimiwa Spika, katika kiwanja cha Ndege cha Iringa, ukarabati na upanuzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege, maegesho ya ndege, mitambo na taa za kuongozea ndege, barabara ya kiungio na uzio wa usalama (Awamu ya Kwanza) umefikia asilimia 45. Kwa upande wa Kiwanja cha Ndege cha Geita, hadi kufikia Aprili, 2022, Awamu ya Kwanza ya mradi huu inayohusisha ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege, maegesho ya ndege na barabara ya kiungio imekamilika na mradi upo kwenye muda wa matazamio (Defect Liability Period – DLP). Aidha, Serikali inaendelea na usanifu wa kina wa Jengo la Abiria na Jengo la kuongozea ndege.
  2. mradi wa ukarabati na upanuzi wa Viwanja vya ndege vya Tanga, Lake Manyara na Iringa (Awamu ya II) utatekelezwa chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia. Kwa sasa Serikali inaendelea na majadiliano kwa ajili ya ufadhili wa miradi hii. Kwa upande wa kiwanja cha Ndege cha Tanga, hadi Aprili, 2022 Serikali imekamilisha uthamini wa mali zilizopo kwenye eneo la mradi na kwa sasa jitihada za kutafuta fedha za kulipa fidia kwa wananchi hao zinaendelea. Aidha, kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Lake Manyara ulipaji wa fidia kwa wananchi wote watakaopisha ujenzi umekamilika.

UTENDAJI WA TAASISI ZILIZO CHINI YA

SEKTA YA UJENZI

Bodi ya Mfuko wa Barabara

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Bodi ilipanga kukusanya jumla ya Shilingi 908,355,896,000.  Kati ya fedha hizo, Shilingi 635,849,127,200 ni kwa ajili ya kugharamia kazi za barabara za Kitaifa (Barabara Kuu na Barabara za Mikoa) ambazo husimamiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.  Aidha, kiasi cha Shilingi 272,506,768,800 zilitengwa kwa ajili ya kugharamia kazi za barabara za Wilaya ambazo husimamiwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI. 

Kati ya fedha hizo, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) ilitengewa Shilingi 63,038,082,471;TANROADS Shilingi 567,342,742,235; Ofisi ya Rais – TAMISEMI Shilingi 27,016,321,059 na TARURA Shilingi 243,146,889,529.  Mgawanyo

       huo       ni       baada        ya       kutoa        Shilingi 

7,811,860,706.00 kwa ajili ya kugharamia shughuli za uendeshaji wa Mfuko kwa mujibu wa sheria.

  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022,

Bodi imekusanya jumla ya Shilingi 541,641,298,899.00 sawa na asilimia 85 ya bajeti ya mwaka. Makusanyo hayo ya Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 yaliongezeka kwa asilimia 6 ikilinganishwa na makusanyo ya kipindi kama hicho kwa mwaka wa fedha 2020/21.  Ongezeko hili limechangiwa zaidi na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kutokana utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati pamoja na kupungua kwa maambukizi ya virusi vya Korona.  Ongezeko hili halijumuishi ongezeko lilitokana na nyongeza ya Shilingi 100 kwa lita ya petroli na dizeli kwa kuwa makusanyo yake hayakuwekwa kwenye akaunti ya Mfuko wa Barabara bali yalihamishiwa moja kwa moja TARURA kwa ajili ya kugharamia kazi za barabara za Wilaya.

  1. Mheshimiwa Spika, vilevile, Bodi iliendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuimarisha uwezo wa Mfuko kugharamia kazi za barabara pamoja na usimamizi wa kazi hizo.  Hatua hizo ni pamoja na kufanya utafiti wa uwezekano wa kukusanya mapato ya Mfuko kutoka kwenye tozo ya matumizi ya barabara kwa kuzingatia uzito na umbali kwa gari husika; tozo za barabara na madaraja na tozo kwenye matumizi ya gesi asilia inayotumika kuendeshea magari.
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi imeandaa na kuwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mfuko.  Moja ya mapendekezo yaliyowasilishwa ni kutambua tozo za gesi na nishati nyingine zinazoweza kuendesha vyombo vya moto barabarani kama chanzo cha mapato ya Mfuko wa Barabara sambamba na dizeli na petroli.
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi pia imeandaa Mfumo wa kielektroniki wa kuwawezesha watumiaji wa barabara kutoa taarifa juu ya hali za barabara na kazi za barabara kwa kutumia simu janja. Utoaji wa elimu pamoja na utambulishaji wa mfumo unaendelea kwa wananchi kwenye mikusanyiko mbalimbali.  Aidha, Bodi inaratibu ukusanyaji wa taarifa na takwimu mbalimbali zinazohusu matumizi ya teknolojia ya gharama nafuu kwa lengo la kuzitumia kuhamasisha matumizi ya teknolojia hizo kwenye kazi za matengenezo ya barabara.

Wakala wa Majengo Tanzania

  1. Mheshimiwa Spika, katika fedha 2021/22 Wakala wa Majengo Tanzania ulipanga kuendelea na ujenzi wa nyumba za viongozi, watumishi wa umma, ukarabati wa nyumba za Serikali, Ujenzi wa nyumba za Waheshimiwa Majaji katika mikoa mbalimbali na ujenzi wa nyumba za makazi Ikulu Dodoma. 
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022  hatua iliyofikiwa katika Miradi inayotekelezwa kwa Kutumia Vyanzo vya Ndani vya Wakala  ni umaliziaji wa miradi  mitatu ya ujenzi katika mikoa ya Dar es Salaam ambao umekamilika, Arusha ambao umefikia asilimia 85 na Pwani umefikia asilimia 20.  
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu utekelezaji wa Miradi Inayotekelezwa kwa Kutumia Fedha za Ruzuku, hadi Aprili, 2022 ujenzi wa nyumba 20 za Viongozi Jijini Dodoma umefikia asilimia

90; ujenzi wa nyumba tano (5) za majaji Tanzania Bara katika mikoa ya Kilimanjaro, Dar es salaam, Mtwara, Shinyanga na Tabora upo hatua mbalimbali za utekelezaji na  mradi wa nyumba za Makazi Magomeni Kota upo katika ujenzi wa sakafu ya kwanza.

  1. Mheshimiwa Spika, Kazi nyingine  ni mradi wa ukarabati wa nyumba 40 za Viongozi Jijini Dodoma umefikia asilimia 48.7; ukarabati wa nyumba 30 za viongozi mikoani na matengenezo kinga katika eneo la Magomeni Kota umefikia asilimia 96.3. Ukarabati wa nyumba 66 zilizokuwa za CDA na kuhamishiwa TBA umefikia asilimia 70. Vilevile, ukarabati wa nyumba zilizokuwa zinamilikiwa na TAMISEMI/NHC katika mikoa 20 zilizohamishiwa TBA upo hatua za mwanzo za utekelezaji. Aidha, ununuzi wa samani kwa nyumba za Ikulu Ndogo upo hatua za manunuzi.  Ukarabati wa karakana sita (6) za TBA mikoa ya Arusha, Mwanza, Dodoma, Tabora, DSM na Mbeya unaendelea na  ukarabati wa karakana ya Dodoma umekamilika.
  1. Mheshimiwa Spika, Wakala wa Majengo umeendelea kutekeleza Miradi ya Washitiri inayohusisha Ubunifu na Ujenzi; Ujenzi na Ukarabati pamoja na Ushauri na Usimamizi (Project Management).Hadi Aprili, 2022, Wakala umetekeleza jumla ya miradi 17 ya Ubunifu na Ujenzi.  Miradi hiyo ni  ujenzi wa jengo la Ofisi ya makao makuu ya TANROADS – Dodoma upo asilimia 40; ujenzi wa jengo la ofisi ya Tume ya Maadili – Dodoma upo asilimia  47; ujenzi wa ofisi ya TANESCO Wilaya ya Chato umefikia asilimia 90; ujenzi wa Ofisi ya TANESCO Mkoa wa Geita umefikia asilimia 93; ujenzi wa Hospitali ya Rufaa-Geita umefikia asilimia 94; ujenzi wa wodi, kazi za nje na jengo la mionzi (radiology) awamu ya pili katika hospitali ya rufaa Wilaya ya Chato umefikia asilimia 85 kwa upande wa jengo la mionzi na kwa upande wa wodi ujenzi umefikia asilimia  30; ujenzi wa wodi ya wazazi na watoto katika hospitali ya Sekou Toure – Mwanza umefikia asilimia 91 na ujenzi wa jengo la utawala ofisi ya Wilaya Butiama – Mara umefikia asilimia 70.
  1. Mheshimiwa Spika,  vilevile, hadi Aprili, 2022 Wakala umetekeleza jumla ya miradi 17 ya ujenzi na ukarabati ambapo utekelezaji wa baadhi ya miradi hiyo ni: ujenzi wa jengo la ofisi la TANESCO makao makuu Dodoma (asilimia 95); ujenzi wa jengo la Upasuaji, hospitali ya rufaa ya Mbeya awamu ya pili (asilimia 75); ukarabati wa majengo ya Chuo cha Ufundi cha Wilaya ya Karagwe (KDVTC) (asilimia 80);  ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (asilimia 55); usimikaji wa mtambo wa Chiller kwenye ofisi za Bunge (asilimia 55);  ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Loliondo Arusha (asilimia 30) na  ujenzi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songwe awamu ya III (asilimia 83).  
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya Ushauri,Wakala umetekeleza jumla ya miradi 52. Utekelezaji wa baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na: Kutoa huduma ya ushauri kwenye ujenzi wa ofisi ya Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (PCCB) eneo la NCC Dodoma ambao umefikia asilimia 17; Ujenzi wa jengo la utawala la Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ambao umefikia asilimia 71; Ujenzi wa jengo la Mabweni chuo cha Mipango Dodoma ambao umefikia asilimia 95; Ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya mji wa Kondoa ambao umefikia asilimia 95; Ukarabati wa jengo la Utawala la ofisi za Bunge awamu ya pili ambao umefikia asilimia 65; Ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe awamu ya pili ambao umefikia asilimia 53; ujenzi wa jengo la soko la mifugo Buzirayombo awamu ya kwanza ambao umefikia asilimia 82 na Ujenzi wa jengo la ofisi ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dodoma umekamilika.
  1. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wakala umetekeleza miradi mbalimbali ya Usimamizi. Miradi hiyo ni pamoja na usimamizi wa ujenzi wa Vihenge (Silos) vya kuhifadhia nafaka pamoja na maghala kwa ajili ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) katika mikoa nane ya Dodoma, Katavi, Manyara, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga na Songwe ambao umefikia asilimia 52. Aidha, kazi nyingine ni usimamizi wa ujenzi wa majengo ya Kituo cha pamoja cha Forodha Mpakani cha Kasumulu (One Stop Border Post) awamu ya pili Kasumulu umefikia asilimia 80.
  1. Mheshimiwa Spika, vilevile, katika mwaka wa fedha 2021/22 Wakala umeendelea kutekeleza mradi wa Mji wa Serikali eneo la Mtumba Jijini Dodoma. Baadhi ya miradi  inayoendelea kutekelezwa ni Ujenzi wa jengo la ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambao umefikia asilimia 25. Aidha, Wakala unafanya usimamizi wa ujenzi wa majengo ya ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi (asilimia 17); Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo (asilimia 13); Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara (asilimia 12); Wizara ya Mambo ya Ndani (asilimia 14); Wizara ya Nishati na Madini (asilimia 14);  Wizara ya Sheria na Katiba  (asilimia 14); Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (asilimia 11); Mamlaka ya Serikali Mtandao (asilimia 11); Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (asilimia 13); Wizara ya Kilimo (asilimia 11); TAMISEMI (asilimia 12); Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (asilimia 9); Wizara ya Afya  (asilimia 9) na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

(asilimia 16.5).

Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) ulipanga kufanya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali; kusimika na kufanya matengenezo ya mifumo ya umeme, elektroniki, majokofu na viyoyozi kwenye majengo ya Serikali na kutoa ushauri wa Kihandisi kwa miradi ya usimikaji wa mifumo ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na majokofu katika nyumba ya Serikali. Kazi nyingine ni kuendesha shughuli za usafiri wa Vivuko vya Serikali zinazohusisha ujenzi na ukarabati wa vivuko, maegesho na miundombinu ya vivuko (majengo na uzio).
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa maegesho ya vivuko, kazi zilizopangwa ni kukamilisha upanuzi wa eneo la maegesho ya Kigamboni katika kivuko cha Magogoni – Kigamboni, maegesho ya Zumacheli katika kivuko cha Chato – Nkome,  ujenzi na ukarabati wa maegesho ya Nyamisati – Mafia na ukarabati na ujenzi wa maegesho ya vituo vitano (5) vya vivuko (Kilambo-Namoto, Utete – Mkongo, Iramba – Majita, Nyakarilo – Kome na Kasharu – Buganguzi).Ujenzi wa miundombinu (jengo la abiria, ofisi na uzio) katika vituo kumi (10) vya vivuko (Bugorola, Ukara, Kome, Nyakarilo, Maisome, Kahunda, Nkome, Kisorya, Musoma na Kinesi). Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa maegesho ya Kayenze – Kanyinya, Muleba – Ikuza na maegesho ya Ijinga – Kahangala (Magu) na Bwiro – Bukondo (Ukerewe).
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022, upanuzi wa jengo la abiria katika maegesho ya Magogoni – Kigamboni upande wa Kigamboni Jijini Dar es Salaam umekamilika ikiwa pamoja na kukamilisha usimikaji wa mfumo wa kielektroniki wa kukatia tiketi (N-Cards System). Mradi wa maegesho ya Zumacheli katika kivuko cha Chato – Nkome uko katika hatua ya maandalizi ya kuanza ujenzi. Aidha, ujenzi wa maegesho ya Nyamisati – Mafia upande wa Nyamisati umekamilika na upande wa Mafia ujenzi unaendelea. Vilevile, ukarabati wa maegesho unaendelea katika vituo viwili (2) vya vivuko vya Iramba – Majita na Nyakarilo – Kome na vituo vitatu vilivyobaki vipo katika hatua ya upembuzi yakinifu. Vilevile, ujenzi wa miundombinu (jengo la abiria, ofisi na uzio) ya vituo viwili (2) unaendelea katika kituo cha Musoma – Kinesi upande wa Musoma (Mwigobelo) na Chato.  Vituo vingine nane (8) vipo katika hatua ya manunuzi ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi.
  1. Mheshimiwa Spika  kuhusu Ukarabati wa Vivuko Wakala ulipanga kukamilisha ukarabati wa vivuko MV Musoma, MV Mara, MV Ujenzi, MV Kome II, MV Misungwi, MV Mafanikio,

MV Kyanyabasa, Old MV Ruvuvu, MV Ruhuhu, MV Tegemeo na MV Tanga. Kazi nyingine ni ukarabati wa kivuko MV Nyerere na ukarabati wa kivuko MV Kilombero II na kukihamishia eneo la Mlimba – Malinyi. 

  1. Mheshimiwa Spika,  hadi Aprili, 2022 ukarabati wa kivuko MV Mafanikio na MV Tegemeo umekamilika. Aidha, ukarabati unaendelea katika vivuko MV Musoma na umefikia asilimia 73, Old MV Ruvuvu (asilimia 60)  na MV Nyerere (asilimia 40).  Mikataba ya ukarabati wa MV Mara, MV Ujenzi, MV Ruhuhu, MV Misungwi, MV Kome II na MV Kilombero II imesainiwa     na      Makandarasi       wapo          katika maandalizi ya kuanza ukarabati. Vilevile, miradi ya ukarabati wa vivuko MV Kyanyabasa na MV Tanga ipo katika hatua mbalimbali za manunuzi ya Makandarasi.
  1. Mheshimiwa Spika,  kuhusu mradi wa Ujenzi wa Vivuko Vipya na Mifumo, Wakala ulipanga kujenga vivuko vipya vya Kisorya – Rugezi, Ijinga – Kahangala, Bwiro – Bukondo,

Nyakarilo – Kome, kivuko cha pili cha Nyamisati – Mafia na ununuzi wa vifaa vya karakana za TEMESA kwa ajili ya kuboresha huduma ya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya

Serikali. 

  1. Mheshimiwa Spika,  hadi Aprili, 2022 mradi wa ujenzi wa kivuko kipya cha Kisorya – Rugezi uko hatua za awali za utekelezaji

(mobilization). Vilevile, taratibu za manunuzi kwa ajili ya ujenzi wa vivuko vya Ijinga – Kahangala, Bwiro – Bukondo, Nyakarilo – Kome na kivuko cha pili cha Nyamisati – Mafia zinaendelea. Aidha, Wakala upo katika hatua za manunuzi ya vifaa vya karakana za TEMESA kwa ajili ya kuboresha huduma ya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali pamoja na mradi wa kusanifu na kusimika Mfumo wa Kielektroniki wa Kusimamia Uendeshaji wa Huduma za Vivuko (Electronic Ferries Management  Information System – EFMIS).

  1. Mheshimiwa Spika,  kwa upande wa mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Karakana, Wakala ulipanga kufanyaukarabati wa Karakana 11 zilizopo Mwanza, Arusha, Mtwara, Mbeya, M.T Depot – Dar es Salaam, Tabora, Kigoma, Mara, Ruvuma, Pwani na Vingunguti; ujenzi wa Karakana mpya ya Kisasa Jijini Dodoma; ununuzi wa karakana zinazotembea sita (6); uanzishaji wa karakana za Wilaya katika wilaya ya Same, Simanjiro, Masasi, Ukerewe, Chato na Kyela; ujenzi wa Karakana tano (5) za TEMESA katika mikoa mipya ya Songwe, Simiyu, Geita, Njombe na Katavi. Kazi nyingine ilikuwa ni ununuzi wa Mfumo wa Taarifa za Matengenezo ya Magari ya Serikali.
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 ukarabati wa karakana za TEMESA mikoa ya Mbeya, M.T Depot – Dar es Salaam, Pwani na Vingunguti umekamilika. Aidha, ujenzi wa jengo la Ofisi ya makao makuu ya Wakala umefikia asilimia 95 na ujenzi wa Karakana mpya ya Kisasa Jijini Dodoma unaendelea. Kuhusu mradi wa ukarabati wa karakana za Wilaya, ukarabati wa karakana ya wilaya ya Same umekamilika. Aidha, karakana nyingine zilizosalia zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji ikiwemo manunuzi ya maeneo pamoja na kulipia vibali vya ujenzi. Hatua za ununuzi wa karakana zinazotembea sita (6) zinaendelea.

Vilevile, ujenzi wa Karakana katika mkoa mpya wa Simiyu Awamu ya I umekamilika.  Mipango ya ujenzi wa karakana katika mikoa mingine mipya ya Songwe, Geita, Njombe na Katavi ipo katika hatua mbalimbali. Aidha,  ununuzi wa Mfumo wa Taarifa za Matengenezo ya Magari ya Serikali unaendelea.

  1. Mheshimiwa Spika, Wakala pia ulipanga kutekeleza Miradi ya Washitiri na Ushauri iliyohusisha  kufanya matengenezo ya magari 51,824, kusimika mifumo ya umeme 323, elektroniki 28, Viyoyozi na Majokofu 1,607. Aidha,  Wakala ulipanga kutoa ushauri wa kihandisi kwa miradi ya usimikaji wa mifumo ya umeme, mitambo na elektroniki 118 pamoja na kusimamia mifumo 64 ya umeme, mitambo na elektroniki.
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022

       Wakala     umefanya    matengenezo     ya     magari

22,406, umesimika mifumo ya umeme 90,

elektroniki 10, Viyoyozi na Majokofu 19. Aidha,  Wakala umesimamia miradi ya usanifu ya umeme, mitambo na elektroniki 38.

Bodi ya Usajili wa Wahandisi

  1. Mheshimiwa Spika, majukumu ya Bodi hii ni kuratibu na kusimamia mienendo na shughuli za kihandisi zinazofanywa na Wahandisi pamoja na Kampuni za Ushauri wa kihandisi. Lengo ni kulinda maslahi ya taifa na watumiaji wa huduma hizo. Katika mwaka wa fedha 2021/22, Bodi ilipanga kusajili Wahandisi 3,056, Mafundi Sanifu 400 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi 15
  1. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2022 Bodi imesajili Wahandisi 1,716, Mafundi Sanifu 160 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi 07 na kufikisha jumla ya Wahandisi waliosajiliwa katika ngazi mbalimbali kuwa 32,982 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi kuwa 389.  Kati ya jumla ya Wahandisi waliosajiliwa, 30,211 ni wa ndani na 2,771 ni wageni.  Kampuni za Ushauri wa Kihandisi za ndani ni 267 na za kigeni ni 122.  Katika kipindi hicho, Bodi ilifuta usajili kwa Wahandisi Watalaam 101, Wahandisi Washauri 10 na Kampuni za Ushauri wa

Kihandisi 11 kwa kukiuka Sheria ya Usajili wa Wahandisi. Aidha, katika kipindi hicho, jumla ya miradi 187 ilikaguliwa.  Vilevile, Bodi imesajili miradi 502 kati ya miradi 600 iliyojipangia mwaka huu pamoja na viwanda na Majengo 59 kati ya 130 iliyojipangia.

  1. Mheshimiwa Spika, Bodi pia iliandaa warsha 3, moja ikiwa kwa Wahandisi Wataalam wanaosimamia mafunzo kwa vitendo kwa wahandisi wahitimu, Wahandisi vijana wanaochipukia kwa Mafundi Sanifu. Vilevile, Bodi iliendelea kuwaapisha  Wahandisi Wataalam Kiapo cha Utii kwa Taaluma (Professional Oath) ambapo jumla ya wahandisi 4,940 hadi sasa wamekwishaapishwa. Aidha, Bodi iliendelea kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Mafunzo kwa Vitendo kwa Wahandisi Wahitimu 3,172. Jumla ya wahandisi wahitimu 10,097 wameshapitia  Mpango huu tangu uanzishwe  mwaka  2003. 
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi pia iliandaa na kuadhimisha Siku ya Wahandisi ya mwaka 2021 (Annual Engineers’ Day 2021) ambayo ilihudhuriwa na wahandisi zaidi ya 3,468. Mada iliyojadiliwa katika siku ya hiyo ilikuwa ni “Athari za Mapinduzi ya nne ya Viwanda kwenye miundombinu na viwanda kuchochea uchumi wa kati endelevu” (The Impact of 4th Industrial Revolution on Infrastructure and Industry for sustainability of middle income economy).

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na

Wakadiriaji Majenzi

  1. Mheshimiwa Spika, Bodi hii ina jukumu la kusajili, kusimamia na kuratibu mwenendo wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi pamoja na Kampuni zao za ushauri. Aidha, Bodi ina jukumu la kukagua sehemu zinakofanyika shughuli za ujenzi ili kuhakikisha ubunifu na usimamizi wa ujenzi unafanywa na wataalam waliosajiliwa. Katika mwaka wa fedha 2021/22, Bodi ilipanga kusajili Wataalam  150,  katika fani za Wabunifu Majengo, Wakadiriaji Majenzi, Wabunifu wa Ndani wa Majengo, Wabunifu wa Nje wa Majengo,  Wasanifu Teknolojia ya majengo, Watathmini Majengo, Wasimamizi Ujenzi na Wasimamizi Miradi. Aidha, Bodi ilipanga kusajili  Kampuni 20 za fani hizo. 
  1. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2022 Wataalamu 57 wamesajiliwa na Bodi, ikiwa ni asilimia 38 ya lengo na kampuni 13 zimesajiliwa ikiwa ni asilimia 65 ya lengo. Aidha, wahitimu 178 wamepatiwa mafunzo ikiwa ni asilimia 99 ya lengo na miradi ya ujenzi 705 ilikuwa imesajiliwa ambayo ni asilimia 71 ya lengo. Vilevile, miradi ya ujenzi 1655 ilikaguliwa ikiwa ni asilimia 64 ya lengo. Katika miradi ambayo ilikutwa na kasoro, wataalam au waendelezaji wake walichukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria ikiwemo kutozwa faini au kufunguliwa mashtaka mahakamani. 

Bodi pia iliendesha mitihani ya kitaalamu kwa wahitimu 88 katika fani za Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi,  kufanya mikutano mitano (5) na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na kuendesha mashindano ya insha.

Bodi ya Usajili wa Makandarasi

  1. Mheshimiwa Spika, majukumu ya Bodi hii ni kusajili na kuratibu shughuli za ukandarasi nchini na kuendeleza Makandarasi kwa maslahi ya watumiaji wa huduma hizo. Katika mwaka wa fedha 2021/22, Bodi ilipanga kusajili Makandarasi 9,400 na kukagua jumla ya miradi ya ujenzi 3,100. Vilevile, Bodi ilipanga kuendesha kozi sita (6) za mafunzo katika mikoa ya Morogoro, Mwanza, Mbeya, Dar es Salaam,

Singida na Kilimanjaro. 

  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022, Bodi ilisajili Makandarasi wapya 638 hivyo kufanya jumla ya Makandarasi waliosajiliwa kufikia 12,740. Aidha, jumla ya miradi 2,268 ilikaguliwa sawa na asilimia 73 ya malengo. Miradi 545 sawa na asilimia 24 ilipatikana na mapungufu mbalimbali yakiwemo kutozingatia usalama kazini, kutosajili miradi na kufanya kazi za thamani inayozidi kiwango kinachoruhusiwa kwa daraja husika. Makandarasi waliokutwa na mapungufu hayo walichukuliwa hatua mbalimbali kwa mujibu wa sheria ikiwemo kutozwa faini, kupewa onyo, kusimamishwa kufanya biashara ya ukandarasi na kufutiwa usajili. 
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi pia iliendesha kozi za mafunzo kupitia Mpango Maalum wa Mafunzo Endelevu kwa Makandarasi (Sustainable Structured Training Programme – SSTP) katika mikoa ya Mwanza, Dodoma, Iringa na Dar es Salaam. Jumla ya Makandarasi 364 walishiriki katika mafunzo hayo. Bodi pia iliendelea kuendesha Mfuko wa Kusaidia Makandarasi (Contractors Assistance Fund – CAF) unaotoa dhamana za zabuni na malipo ya awali kwa Makandarasi wa ndani ili kuwezesha ushiriki wa Makandarasi hao katika zabuni na utekelezaji wa miradi mbalimbali. Hadi Aprili, 2022, Mtaji wa mfuko huu ni Shilingi bilioni 3.9. Aidha, idadi ya wanachama wa Mfuko iliongezeka kutoka 1,167 mwaka wa fedha 2020/21 hadi kufikia 1,277 mwaka 2021/22.  

Baraza la Taifa la Ujenzi

  1. Mheshimiwa Spika, majukumu ya Baraza la Taifa la Ujenzi ni kushughulikia maendeleo ya Sekta ya Ujenzi yanayojumuisha kutoa ushauri wa kiufundi kwa Serikali na wadau wengine wa Sekta ya Ujenzi, uratibu wa shughuli za utafiti na mafunzo ya kisekta kwa ujumla. Jukumu lingine ni ukusanyaji na uwekaji wa taarifa za ujenzi, tathmini ya utendaji kazi wa Sekta ya Ujenzi, uanzishwaji wa mfuko wa mafunzo, uhamasishaji wa ubora wa kazi, ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa kiufundi (technical audit) na utatuzi wa migogoro ya ujenzi.
  1. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili, 2022, kazi zilizofanyika ni pamoja na kuendelea na mapitio ya Sheria iliyoanzisha Baraza na kuandaa Kanuni zake; kutoa ushauri wa kitaalam katika maeneo ya gharama na mabadiliko ya gharama za ujenzi  kwa taasisi na Kampuni sita (6) na kuendelea kuratibu utatuzi wa migogoro inayotokea kwenye miradi ya ujenzi kwa kutumia utaratibu wa ‘’Adjudication’’ na ‘’Arbitration’’  ambapo jumla ya mashauri 19 yamepokelewa na kuratibiwa.

Kazi nyingine ni kuendelea kufanya tafiti kuhusu ushiriki wa washauri wataalamu wa ndani (local consultants) katika kutekeleza miradi ya ujenzi ukilinganisha na ushiriki wa washauri wa kigeni (foreign consultants), kufanya marejeo na kuboresha Kanuni ya kukokotoa bei za Kandarasi za ujenzi na tathmini ya matumizi ya utaratibu wa Force Account katika kutekeleza miradi ya ujenzi. Tafiti zote ziko katika hatua ya ukusanyaji wa taarifa (data).

  1. Mheshimiwa Spika, Baraza pia limefanya kaguzi za kiufundi (technical audit) kwenye miradi ya barabara na madaraja mkoani Rukwa. Jumla ya miradi 46 ikiwemo miradi 38 ya barabara na 8 ya madaraja yenye jumla ya thamani ya Shilingi  bilioni 7.8 imekaguliwa. Vilevile, Baraza limeendelea kukusanya takwimu na taarifa mbalimbali za Sekta ya Ujenzi kwa mwaka 2021/22 ili kuwezesha wadau wa Sekta ya Ujenzi kufuatilia ukuaji wa Sekta. Aidha, Baraza liliendelea kukusanya bei za vifaa vya ujenzi na kuandaa viwango vya mabadiliko ya bei hizo kwa kila mwezi (monthly labour/materials price indices) kama mwongozo wa mabadiliko ya bei za miradi.
  1. Mheshimiwa Spika, kazi nyingine ni kushirikiana na Bodi ya Mfuko wa wa Barabara (RFB) katika kuandaa mwongozo wa bei  na gharama za ujenzi na ukarabati wa barabara hapa nchini; kukusanya taarifa mbalimbali za Sekta ya Ujenzi ambazo zitatumika katika Kituo maalum cha kutoa taarifa za Sekta ya Ujenzi; kuratibu Mpango wa Kukuza Uwazi na

Uwajibikaji (Construction Sector Transparency Initiatives – CoST) katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa umma  na kuendesha mafunzo katika eneo la usimamizi wa miradi ya ujenzi. Kozi mbili ziliendeshwa ambazo ni kozi ya usuluhishi wa migogoro katika mikataba ya ujenzi na kozi ya Matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki katika usimamizi wa miradi ya ujenzi. 

Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia Katika Sekta ya Ujenzi na Usafirishaji (Tanzania

Transportation Technology Transfer Centre)

  1. Mheshimiwa Spika, Kituo hiki kilianzishwa kwa lengo la kuimarisha/kuboresha Sekta ya Ujenzi na Usafirishaji kwa ujumla kwa kutumia mbinu ya ukusanyaji na  usambazaji wa teknolojia kwa wadau.
  1. Mheshimiwa Spika, katika  kutekeleza majukumu hayo, hadi Aprili, 2022 Kituo kimeendelea kuratibu na kutekeleza kazi za uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi ICoT na kufanikisha kuanza kwa udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2021/22 katika fani za Civil, Electrical na Mechanical kwa ngazi ya diploma (NTA Level 5). Hadi kufikia Aprili, 2022 mitaala kwa ngazi za NTA Level 5 na 6 imekamilika na kupitishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE). Aidha, Kituo kimeshiriki katika mafunzo mbalimbali ya ndani ya nchi kuhusu teknolojia, ubunifu na mikakati mbalimbali kuboresha miundombinu yetu katika Sekta ya Ujenzi na Usafirishaji.
  1. Mheshimiwa Spika, kwa sasaKituo kinaendelea na maandalizi ya mwisho ya kuchapisha nakala 300 za Jarida Na. 5 lenye mada mbalimbali zinazohusu teknolojia, usalama barabarani, taarifa za miradi mbalimbali ya kimkakati na agenda mbalimbali za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha miundombinu ya usafirishaji. Aidha, Kituo kimeendelea kuimarisha huduma za Maktaba Mtandao kupitia ICoT ili kuendelea kutoa huduma kuhusu Sekta ya Ujenzi na Usafirishaji kwa lengo la kuboresha mifumo na upashanaji habari za teknolojia.

C.2   SEKTA YA UCHUKUZI

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Sekta ya Uchukuzi iliidhinishiwa jumla ya Shilingi 2,120,049,821,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi

91,743,411,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara na Taasisi zake na Shilingi 2,028,306,410,000.00 ni kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya  Maendeleo. 

Bajeti ya Matumizi ya Kawaida

  1. Mheshimiwa Spika, kati ya Shilingi 91,743,411,000.00 zilizoidhinisha kwa ajili ya matumizi ya Kawaida, Shilingi

64,672,467,000.00 ni fedha za Mishahara na Shilingi 27,070,944,000.00 ni fedha za Matumizi Mengineyo kwa Wizara na Taasisi zilizo chini ya Sekta ya Uchukuzi.  Hadi kufikia Aprili, 2022 jumla ya Shilingi 71,098,606,554.69 sawa na asilimia 77 zilikuwa zimetolewa ambapo Shilingi 50,345,322,476.00 zilikuwa kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi na Shilingi 20,753,284,078.69 zilikuwa kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

Bajeti ya Maendeleo 

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, Sekta ya Uchukuzi ilitengewa jumla ya Shilingi 2,028,306,410,000.00 kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,828,306,410,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 200,000,000,000.00 ni fedha za nje. Hadi kufikia Aprili, 2022 jumla ya

Shilingi 2,515,524,352,520.58 sawa na asilimia 124 ya fedha zilizoidhinishwa zilikuwa zimetolewa na Hazina kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi   

2,398,724,922,636.18 ni fedha za ndani na Shilingi  116,799,429,884.40 ni fedha za Nje.   

  1. Mheshimiwa Spika, baada ya kupokea fedha hizo, Wizara (Sekta ya Uchukuzi) iliendelea kutekeleza shughuli zake katika maeneo mbalimbali kama ifuatavyo:

HUDUMA ZA USAFIRI MIJINI NA VIJIJINI

Udhibiti wa Usafiri kwa Njia ya Barabara 

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imeendelea kusimamia na kudhibiti usafiri katika sekta ndogo za reli na  barabara. Aidha, LATRA imeendelea kuwasajili madereva na wahudumu wa  magari ya biashara kwa lengo la kuwarasimisha ili kuboresha ufanisi katika sekta ya usafirishaji. Hadi kufikia Aprili, 2022 jumla ya madereva wa magari ya biashara 9,933 walikuwa wamesajiliwa. Vilevile, Serikali kupitia LATRA na eGA inaendelea kutengeneza mfumo utakaotumika kuthibitisha madereva wanaoendesha vyombo vya usafiri vinavyofanya biashara  (commercial drivers certification). Lengo la kuthibitisha madereva ni kupata madereva wenye sifa za kuendesha vyombo vinavyodhibitiwa ili kuimarisha na kuboresha usalama na huduma za usafiri kwa njia ya barabara. Mfumo huo pia utatumika kuthibitisha madereva wa treni ili kuboresha usalama na huduma za usafiri wa reli hapa nchini na kupunguza ajali.
  1. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Data Kimtandao (National Internet Data Centre – NIDC) imeendelea kuboresha mfumo wa tiketi za kielektroniki kwa mabasi ya abiria (Electronic Ticketing System). Aidha, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya uchukuzi, imekamilisha taratibu muhimu kabla ya mfumo huo kuanza kutumika ikiwa ni pamoja na kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizojitokeza wakati wa majaribio ya mfumo huo. Vilevile, baadhi ya taasisi za fedha zimeonesha utayari wa kutoa tiketi za kielektroniki kupitia wakala wa benki zao nchini na hivyo kupunguza hitaji la kuwa na kiwango cha fedha kwenye mashine za kukatia tiketi (float). Mfumo huu, utasaidia kudhibiti upotevu wa mapato ya wasafirishaji na hivyo kuwezesha kukua kwa uwekezaji kwenye sekta ya usafirishaji, kuwawezesha abiria kupata huduma ya tiketi wakiwa mahali popote, kupata taarifa sahihi za mapato ya wasafirishaji ambazo zitasaidia ukusanyaji kodi za serikali, kuwezesha urasimishaji wa ajira za madereva na watendaji wengine kwenye mabasi na hivyo kupunguza migogoro na kupanua wigo wa ulipaji kodi, kuwezesha serikali kupata takwimu sahihi za huduma za usafirishaji abiria ambazo zitasaidia kuboresha mipango ya serikali na kupata taarifa sahihi za abiria wanaosafiri na hivyo kuimarisha masuala ya kiudhibiti.
  1. Mheshimiwa Spika, LATRA imeendelea kufuatilia mwenendo wa mabasi ya masafa marefu na treni kwa kutumia mfumo maalum (Vehicle Tracking System – VTS) ili kuimarisha shughuli za udhibiti wakati wote na mahali popote vyombo hivi vilipo. Hadi Mwezi Aprili, 2022, jumla ya mabasi 6,956 na vichwa vya treni 18 vilikuwa vimeunganishwa kwenye mfumo huo.Aidha, kazi ya kuboresha mfumo na kuufunga kwenye mabasi yanayotoa huduma kwenye njia fupi inaendelea. Miongoni mwa faida za mfumo huu ni kama ifuatavyo:- 
    1. Kuimarisha usalama barabarani na kwenye reli;
    1. Kuboresha ubora wa huduma kwa wateja;  iii. Kusaidia wasafirishaji kusimamia biashara ya uchukuzi kikamilifu; na

iv. Kudhibiti matumizi ya mafuta kwenye vyombo husika na hivyo kupunguza gharama za uendeshaji. Kutokana na kudhibiti mwendokasi wa magari, gari linalotumia mfumo wa VTS linapunguza matumizi ya mafuta kati ya asilimia 20 hadi 30 kutokana na kuendeshwa kwa mwendo wa wastani.  

  1. Mheshimiwa Spika, Kifungu cha 5 (f) cha Sheria ya LATRA, 2019 kinaitaka Mamlaka kuthibitisha ubora wa magari yanayotoa huduma kibiashara na mitambo ya reli. Katika jitihada za kuongeza ufanisi wa usafiri ardhini, kupunguza gharama za uendeshaji kwa watoa huduma pamoja na kuongeza usalama na ubora wa huduma za usafiri wa ardhini, Serikali kupitia LATRA imekamilisha upembuzi yakinifu kuhusu njia bora ya kuanzisha na kuendesha vituo vya ukaguzi wa lazima kwa magari ya biashara (Mandatory Inspection for commercial vehicles) ambapo taarifa ya Mshauri Elekezi imekamilika. Aidha, LATRA inaendelea kufanya upembuzi yakinifu ili kuunganisha mifumo ya LATRA na vituo vikuu vya mabasi vya Dodoma na Magufuli – Mbezi, Dar es Salaam ili kusaidia wasafiri na wadau mbalimbali kupata taarifa sahihi za safari za mabasi katika vituo hivyo.
  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, LATRA kwa kushirikiana na eGA, imeanza taratibu za kutengeneza mfumo utakaotumika kwenye mita za  kukokotoa gharama za magari ya usafiri wa kukodi (private hire transport services) kama teksi za kawaida na teksi mtandao. Magari hayo kwa mujibu wa Kanuni yanatakiwa kuwa na mita za nauli (fare meters) ili kukokotoa gharama halisi ambayo mteja anatakiwa kulipa mwisho wa safari. Mfumo huu utakapokamilika utasaidia kupunguza malalamiko, kuboresha usafiri wa kukodi, kuongeza tija kwa wamiliki na wasafiri pamoja na kuimarisha udhibiti wa huduma hiyo.   

Udhibiti wa Usafiri  kwa Njia ya Reli 

  1. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, LATRA ilifanya ukaguzi wa njia na mitambo ya reli kwa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kutoka Dar es Salaam hadi Tunduma; ukaguzi kwenye miundombinu na vitendea kazi vinavyotumika katika njia ya reli ya Kati na reli ya kwenda Moshi hadi Arusha; na kufanya uchunguzi wa vyanzo vya ajali za treni. Ukaguzi huo umewezesha kutoa taarifa iliyowasilishwa TRC na TAZARA ili kuboresha miundombinu na kufanya matengenezo ya mitambo inayotumika kwenye usafiri wa reli. Vilevile, LATRA imefanya kaguzi mbalimbali katika ujenzi unaoendelea wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge Railway – SGR) ili kujiridhisha na ubora wake, viwango vya kazi na usalama. Changamoto za kiusalama zilizobainika wakati wa kaguzi hizo ziliwasilishwa TRC kwa ajili ya kuzifanyia kazi wakati ujenzi wa reli unaendelea.
  1. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia LATRA ilifanya ukaguzi wa mabehewa na vichwa vya treni vilivyonunuliwa kutoka nchi ya Malaysia ili kuhakikisha kuwa vichwa hivyo vinakidhi viwango vya ubora kwa matumizi na kuboresha huduma za usafiri wa reli zinazotolewa na TRC. Serikali ilifanyia majaribio vichwa vyote vitatu (3) kwa ajili ya reli ya zamani (Meter Gauge Rail) na vilikidhi vigezo vyote vya kiusalama na hivyo kuruhusiwa kwa ajili ya matumizi ya kusafirisha abiria pamoja na mizigo.

Huduma za Usafiri wa Treni Mijini

  1. Mheshimiwa Spika, Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaendelea kutoa huduma kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kusafirisha abiria na mizigo. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, abiria katika Jiji la Dar es Salaam waliohudumiwa kati ya Stesheni ya Kamata – Ubungo – Pugu ni 2,570,740 ikilinganishwa na abiria 2,307,394 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 11.4. Ongezeko hilo limetokana na uboreshaji wa huduma. Aidha, TAZARA imeendelea kutoa huduma za usafiri wa abiria Jijini Dar es Salaam kati ya Stesheni za Dar es Salaam na Mwakanga. Katika kipindi cha Julai hadi Aprili, 2022, abiria waliohudumiwa kati ya Stesheni hizi mbili ni 1,529,787 ikilinganishwa na abiria 1,619,846 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na upungufu wa asilimia 9.4. Sababu za kushuka kwa idadi ya abiria ni kutokana na upungufu wa Mabehewa ya abiria. Pamoja na changamoto za usafiri wa reli katika Jiji la Dar es Salaam, njia hii ya usafiri imechangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza adha ya usafiri kwa maeneo yanayopitiwa na reli ya TRC na TAZARA katika Jiji la Dar es Salaam.

Shirika la Reli Tanzania (TRC)

  1. Mheshimiwa Spika, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeendelea kusimamia, kuboresha na kuendeleza miundombinu na huduma za usafiri wa reli yenye jumla ya urefu wa Kilometa 2,706 kwa ajili ya kuhudumia nchi jirani za Burundi, Rwanda, Uganda na DRC kupitia Kigoma. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, TRC ilisafirisha tani 337,617 za mizigo ikilinganishwa na tani 257,747 zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 30.1. Sababu za ongezeko la mzigo ni ukabarati wa miundombinu ya reli ya MGR mabehewa 240 ya mizigo. Kwa upande wa abiria, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, abiria wa masafa marefu 345,246 walisafirishwa ikilinganishwa na abiria 391,612 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21. Upungufu huu umetokana na kupungua kwa safari za treni kutoka safari nne (4) kwa wiki hadi safari mbili (2) kwa wiki kwa Kigoma na Mwanza kulikosababishwa na kuharibika kwa mabehewa nane (8) kufuatia ajali ya treni ya abiria iliyotokea Wilaya ya Bahi, Dodoma tarehe 2 Januari, 2021.
  1. Mheshimiwa Spika, katika Hotuba ya mwaka 2021/22, tuliahidi kuendelea na ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Standard Gauge kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza (km 1,219), hususani kwenye vipande viwili vya awali, Dar es Salaam hadi Morogoro (km 300) na Morogoro hadi Makutupora (km 422). Ninapenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa Wizara imeendelea kusimamia ujenzi wa vipande hivyo vya reli na hadi kufikia Aprili, 2022 kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro kimefikia asilimia 96.54 na tayari majaribio ya kuingiza umeme wa kuendeshea treni kwenye mfumo (Power system energization) yamekwishaanza. Aidha, kwa kipande cha reli kutoka Morogoro hadi

Makutupora (km 422), kazi ya ujenzi imekamilika kwa asilimia 85.02 na inatarajiwa kukamilika Februari, 2023. 

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na ujenzi wa reli ya SGR katika kipande cha reli cha Mwanza – Isaka (Lot. 5) chenye urefu wa kilomita 341 (kilomita 249 za njia kuu na kilomita 92 njia za kupishania treni) unaofanywa na Mkandarasi wa ubia wa kampuni za China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) na China Railway Construction

Corporation Limited (CRCC) za nchini China. Jiwe la msingi la ujenzi wa reli wa kipande hiki liliwekwa tarehe 14 Juni, 2021 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Thamani ya Mkataba wa ujenzi huu ni Dola  za Marekani bilioni 1.326 sawa na fedha za Kitanzania shilingi trilioni 3.062 ikijumuisha na kodi.  Aidha, ujenzi wa kipande hicho hadi Aprili, 2022 umefikia asilimia 6.8 na kazi kubwa inayoendelea ni ya usanifu na ujenzi wa tuta. 

  1. Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zinazoendelea katika kipande  cha Mwanza – Isaka ni pamoja na utwaaji wa ardhi ambapo hadi Aprili, 2022 jumla ya Kilomita 134 kati ya 249 tayari zimekwishatwaliwa na kukabidhiwa kwa Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi; usanifu wa awali wa njia ya reli umekamilika kwa asilimia 100; usanifu wa kina umefikia asilimia 93; utafiti wa udongo na mifumo ya maji (Geotechnical and hydrological study) umefikia asilimia 65.82; ufungaji wa mitambo ya kokoto, zege, kiwanda cha mataruma; ujenzi wa kambi ya Fela umefikia asilimia 93.4, Bukwimba asilimia 93.33, Seke asilimia 100, Malampaka asilimia 98.94 na Luhumbo asilimia 66.29. Sambamba  na hilo, ujenzi wa tuta umeshaanza na umefikia asilimia 13.7.
  1. Mheshimiwa Spika, kuhusu kipande cha Makutupora  hadi Tabora chenye urefu wa km 368 (km 294 njia kuu na km 74 njia za kupishania), Mkataba wa Ujenzi  wa kipande hicho ulisainiwa tarehe 28 Disemba, 2021 kati ya TRC na Mkandarasi ambaye ni Kampuni ya Yapi Merkezi kutoka Uturuki na maandalizi ya ujenzi yanaendelea. Kwa upande wa ujenzi wa kipande kilichobaki katika awamu ya kwanza cha Tabora – Isaka (km 165), Serikali ipo katika hatua za mwisho za ununuzi wa mkandarasi.   
  2. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi wa awamu ya pili ya reli ya Standard Gauge ambapo  ujenzi wa kipande cha Tabora – Kigoma (km 411) upo katika hatua za manunuzi ya Mkandarasi. Aidha, Serikali ya Tanzania na Burundi zimesaini makubaliano ya kuanza ujenzi na kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa njia ya  reli ya Uvinza-Musongati-Gitega (km 282).  Vilevile, Serikali ya Burundi na DRC tayari zilishatangaza zabuni ya kufanya upembuzi yakinifu kutoka Gitega mpaka KinduDRC ili reli hiyo iweze kutoka Bandari ya Dar es Salaam mpaka Kindu-DRC.
  1. Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha utoaji wa huduma kwa wakati pindi ujenzi utakapokamilika, Serikali inaendelea na taratibu za ununuzi wa vichwa vya treni, mabehewa na mitambo itakayotumika kutoa huduma ya usafiri kwenye reli ya Standard Gauge kati ya Dar es Salaam na Morogoro. Napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali inatarajia kupokea mabehewa ya abiria 30 na vichwa vya treni ya njia kuu viwili (2) kwa awamu tatu kuanzia Septemba, 2022 hadi Machi, 2023. 
  1. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2021/22, miradi mingine ya reli

iliyotekelezwa ni pamoja na:-

  1. Kukamilisha kazi ya ukarabati wa vitendea kazi ikiwemo vichwa vya sogeza saba (7); 
  2. Kusaini mkataba wa ununuzi wa vichwa  vya treni vya umeme 17  na seti 10 za treni ya kisasa kwa ajili ya uendeshaji wa treni hiyo; 
  3. Kusaini mkataba wa ununuzi wa mabehewa ya abiria 59 yatakayotumika kutoa huduma katika reli ya Standard

Gauge

  1. Kusaini Mkataba wa ununuzi wa mabehewa 1,430 yatakayotumika kutoa huduma kwenye reli ya kisasa; 
  2. Ununuzi wa mabehewa ya abiria 30 na vichwa vya treni ya njia kuu viwili (2) kwa ajili ya kuanza kutoa huduma katika reli ya SGR kipande cha Dar es Salaam – Morogoro. Mabehewa 6 na

vichwa 2 vitawasili Mei, 2022; 

  • Ununuzi wa vichwa vya treni vitatu (3) na mabehewa ya mizigo 44 kwa ajili ya MGR ambayo yaliwasili mwezi Oktoba,

2021; vii. Kukamilisha kazi ya usanifu wa kina kwa kuinua kiwango cha njia ya Reli Kati ya Tabora – Kigoma na Kaliua –

Mpanda; na viii. Kukamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali  kwa ajili ya ujenzi wa reli ya Uvinza – Musongati – Gitega.

  1. Mheshimiwa Spika,       Shirika       la      Reli

Tanzania linakabiliwa na changamoto zifuatazo:-

  1. Uchakavu wa miundombinu ya njia ya reli iliyopo katika vipande vya IsakaMwanza, Tabora – Kigoma, Kaliua – Mpanda na Ruvu junction-Mruazi, Tanga – Arusha; kutokana na miundombinu hii kujengwa muda mrefu; 
    1. Uvamizi, uharibifu na hujuma kwa miundombinu ya reli, hususan reli zenyewe, mataruma, vifungio, madaraja, viwanja na nyumba;
    1. Mafuriko ya mara kwa mara kwenye eneo korofi la Kilosa – Gulwe – Igandu

(km 120);  iv. Uchache wa vitendea kazi (vichwa vya treni na mabehewa); 

v. Uchakavu wa karakana za kutengenezea vitendea kazi, vipuri mbalimbali na mashine zitumikazo katika karakana hizo. 

Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia

(TAZARA)

  1. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imeendelea kutekeleza jukumu lake la msingi la kutoa huduma za kusafirisha abiria na mizigo kwa njia ya reli kati ya Dar es Salaam, Tanzania na New Kapiri Mposhi, Zambia. Jukumu lingine ni kulinda na kuimarisha miundombinu ya reli yenye jumla ya urefu wa km 2,153 ikijumuisha njia za kupishania, pamoja na maeneo yote yaliyo ndani ya ukanda wa reli (Mita 50 pande zote kutoka katikati ya reli). Mamlaka hii inamilikiwa na Serikali mbili za Tanzania na Zambia kwa hisa za asilimia 50 kwa 50.
  1. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, Mamlaka ilisafirisha jumla ya tani 180,597 za mizigo ikilinganishwa na tani 173,490 zilizosafirishwa kwa kipindi kama hicho 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 4.0. Ongezeko hili limechangiwa na kukarabatiwa kwa Injini saba (7) zilizofungwa vipuri vipya (42 Traction Motors) pamoja na matengenezo ya njia ya reli hasa kwenye maeneo korofi ya reli. Aidha, katika kipindi hicho, Mamlaka ilisafirisha jumla ya abiria 2,025,210 ikilinganishwa na jumla ya abiria   2,153,009 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21. Abiria hawa wanajumuisha treni ya njia ndefu, treni ya Udzungwa na treni ya mjini. Idadi hiyo ni sawa na upungufu wa asilimia 5.9 uliosababishwa na kufungwa kwa njia kutokana na matengenezo ya daraja la Chambeshi, Zambia na pia mmomonyoko wa udongo uliotokea kilometa 211 upande wa Tanzania. Hata hivyo, utaratibu wa treni za abiria kutovuka mipaka kutokana na janga la UVIKO-19 unaendelea. Treni hizi kwa sasa zinafanya safari kati ya Dar es Salaam na Mbeya kwa upande wa Tanzania na kati ya Nakonde na New Kapiri Mposhi kwa upande wa Zambia
  1. Mheshimiwa Spika, kufuatia utaratibu wa kuruhusu waendeshaji binafsi ili kuongeza mapato, Mamlaka imeingia mkataba wa kutumia njia ya reli kwa kulipia tozo (Open Access Fee) na Kampuni ya Ms Callabash Freight Limited kutoka Zambia. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, Kampuni hii ilisafirisha jumla ya tani za mizigo 88,597 ikilinganishwa na tani za mizigo 222,904 zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho katika mwaka 2020/21 kupitia bandari ya Dar es Salaam kwenda au kutoka nchi za Zambia na DR Congo. Usafirishaji wa mizigo wa Kampuni hii umeshuka kwa asilimia 60.3 kutokana na kufungwa kwa daraja la Chambeshi kule Zambia toka mwezi Octoba 2021 hadi sasa, na pia mmomonyoko wa udongo uliotokea kati ya stesheni za Fuga na Kisaki (Km 211) ambapo njia ilifungwa kwa muda wa miezi miwili kuanzia tarehe 16 Februari hadi 18 Aprili, 2022).
  1. Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zilizotekelezwa na TAZARA katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ni pamoja na kuendelea kubeba mizigo mbalimbali ikiwemo mali ghafi na mitambo ya Ujenzi wa Mradi wa kujenga bwawa la Julius Nyerere (Julius Nyerere Hydro Power Project – JNHPP) la kufua umeme wa maji wa MW 2,115 katika bonde la Mto Rufiji; kufanya matengenezo ya kiwango cha juu, kati na chini kwa mabehewa 585 ya mizigo na mabehewa 41 ya abiria; kubadilisha mataruma ya zege 7,084 na mataruma ya mbao 2,266; na kusambaza na kushindilia kokoto zenye uzito wa tani 16,500.

USAFIRI NA UCHUKUZI KWA NJIA YA MAJI

Udhibiti wa Huduma za Usafiri kwa njia ya Maji

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imeendelea kusimamia utekelezaji wa majukumu ya kudhibiti ulinzi na usalama wa vyombo vya usafiri kwa njia ya maji na kudhibiti uchafuzi wa mazingira majini utokanao na shughuli za usafiri majini, pamoja na kulinda maslahi mapana ya nchi kuhusu Sekta ya usafiri majini. 
  1. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC) limeimarisha uratibu wa zoezi la utafutaji na uokoaji katika ajali zinazotokea majini; limeendelea na utoaji wa elimu kuhusu umuhimu na majukumu ya Kituo cha Kuratibu Utafutaji na Uokoaji Majini (Maritime Rescue Coordination Centre – MRCC/ISC) kilichopo Dar es Salaam pamoja na kushiriki mikutano ya Kitaifa na Kikanda kwa lengo la kuweka mikakati ya kufanikisha zoezi la utafutaji na uokoaji endapo ajali inatokea baharini.  Aidha, Shirika limeendelea kushirikiana na wadau wa usafiri kwa njia ya maji katika kufanya chunguzi za ajali za vyombo vya usafiri majini kila zinapotokea na kutoa taarifa kwa umma juu ya chanzo na matokeo ya ajali. Aidha, Shirika limeanza kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa boti moja (1) ya Utafutaji na Uokoaji na ununuzi wa boti mbili (2) kwa ajili ya kutumika katika maziwa makuu.
  1. Mheshimiwa Spika,  katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, TASAC haikupokea taarifa ya ajali kwa vyombo vya usafiri majini vyenye uzito kuanzia Tani 50 na zaidi. Kwa vyombo vidogo vyenye uzito chini ya Tani 50 TASAC ilipata taarifa za ajali zipatazo tano (5) ikilinganishwa na ajali sita (6) zilizotokea katika kipindi cha mwaka wa 2020/21. Shirika limefanya uchunguzi na kugundua kwamba kutokuwepo kwa matukio ya ajali ya vyombo vya usafiri kwa njia ya maji kwa kipindi husika kulichochewa na kuboreshwa kwa kanuni za usimamizi wa vyombo vya usafiri kwa njia ya maji; kuongezeka kwa uelewa wa wananchi kuhusu sheria na kanuni za kuzingatia katika matumizi ya vyombo vya usafiri majini; na kurahisishwa kwa utoaji wa taarifa za hali ya hewa kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri kwa njia ya maji.
  1. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwezi Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 maeneo manne (4) ya bandari yalikaguliwa kwa kuzingatia miongozo na kanuni za Shirika la Bahari Duniani (IMO). Maeneo hayo katika

Bandari ya Dar es Salaam ni Mizigo ya kichele (General Cargo), Gati la Mafuta la Kurasini (Kurasini Oil Jetty – KOJ), Gati la Mafuta Nje ya Bandari ya Dar es Salaam (Single Bouy Mooring – SBM) na Kitengo cha Kontena (Tanzania International Container Terminal Services – TICTS). 

  1. Mheshimiwa Spika, Shirika linadhibiti umahiri wa wataalam wa usafiri kwa njia ya maji. Kwa kuzingatia hili, hadi kufikia Aprili, 2022 TASAC ilitoa jumla ya vyeti 12,424 vya Umahiri na Ustadi kwa Mabaharia. Aidha, vyeti vya umahiri na ustadi vilitolewa kwa kuzingatia marekebisho ya Manila katika Mkataba wa Standards of Training, Certification and Watchkeeping (STCW) kwa Mabaharia wa mwaka 2010 ambao ulianzisha mfumo mpya wa kutoa vyeti vya STCW na masharti ya uhakiki na mabadiliko ya Pasipoti ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo iliweka mahali pa kuzaliwa kutoka mkoa hadi wilaya.
  1. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha ushindani, TASAC ilipanga kuendelea kutoa leseni kwa watoa huduma zinazodhibitiwa na kusimamia masharti ya leseni hizo; kuhakikisha utoaji wa huduma bora kwa watoa huduma zinazodhibitiwa; kuweka vigezo na viwango vya ubora wa huduma kwa watoa`huduma za bandari na usafiri kwa njia ya maji; na kuweka usawa wa ushindani wa kibiashara. Katika kipindi cha mwezi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 Shirika lilifanya ukaguzi na ufuatiliaji wa bandari nchini ili kuhakiki uzingatiaji wa viwango vya utendaji kazi na vigezo vya huduma ambapo asilimia 65 kati ya lengo la asilimia 85 ya vigezo vya utendaji vilifikiwa. Ukaguzi ulibaini kuwa, waendeshaji wa bandari hawakuweza kufikia kiwango kilichowekwa kuhusiana na ujazo wa eneo la kutunza shehena bandarini (Yard Density), muda wa meli kuingia na kutoka bandarini (Ship Turn Around Time), muda wa kukaa mizigo (Dwell Time) kutokana na ujenzi unaoendelea katika Bandari ya Dar es Salaam pamoja na ongezeko la shehena.
  • Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 Shirika liliongeza idadi ya vituo vya bandari vilivyofuatiliwa kutoka 18 kwa Mwaka 2020/21 hadi kufikia vituo 30 mwezi Aprili, 2022. Aidha, TASAC ilisajili watoa huduma za bandari asilimia 75.1 kwa kuzingatia Kanuni za Huduma za Bandari ikilinganishwa na lengo la asilimia 80. Ufanisi huu ulifikiwa kutokana na ziara za mara kwa mara za ufuatiliaji na tathmini. Aidha, asilimia 79 kati ya lengo la asilimia 84 ya watoa huduma za usafirishaji kwa njia ya maji walizingatia viwango vya Utendaji na vigezo vya huduma za usafirishaji zilizodhibitiwa. 
  • Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia majukumu yake, TASAC ilifanikisha ugomboaji wa shehena kwa wastani wa siku saba (7) baada ya kupokea nyaraka zote muhimu za mteja. Aidha, TASAC imeweka wafanyakazi 23 ambao ni wataalam wa ugomboaji wa shehena katika vituo mbalimbali vya forodha vya kanda na Masoko ya Madini ili kuwezesha ugomboaji wa shehena kwa wakati ulio chini ya mamlaka ya kipekee ya TASAC. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 Shirika lilitoa mafunzo ya umahiri ya ugomboaji wa shehena kwa watumishi 74, mafunzo hayo yalijikita katika sheria za forodha, kanuni za utekelezaji na taratibu zinazosimamia taratibu za forodha. Pia, Shirika lilitoa mafunzo kuhusu namna bora ya kufanya tathmini na uainishaji wa forodha kwa mujibu wa Sheria ya Ushuru wa Pamoja wa Nchi za Afrika Mashariki.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 kwa kuzingatia majukumu ya kipekee ya uwakala wa meli, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC) limehudumia meli 388 ikiwa ni zaidi ya lengo lililopangwa la kuhudumia meli 340. Hii, ni sawa na meli 48 zaidi ya lengo lililopangwa, sawa na asilimia 14%. Aidha, Shirika limehudumia makundi sita (6) ya meli sawa na asilimia 86% ya makundi saba (7) ya meli yaliyopangwa kuhudumiwa katika kipindi husika. Makundi ya meli hizo zilizohudumiwa ni meli za mafuta, utalii, kijeshi, kukodisha, maonyesho na meli zinazokuja kwa dharura. Vilevile,  Shirika limefanikiwa kuhudumia mabaharia 956 wanaotoka melini kwa sababu mbalimbali ikiwemo mapumziko ya likizo, kuisha kwa muda wa mikataba ya kazi na pia mabaharia wanaoingia nchini kwa ajili ya kuja kuanza rasmi kazi melini.
  • Mheshimiwa Spika, shughuli za udhibiti wa usafiri wa njia ya maji pamoja na biashara ya meli zina changamoto nyingi na mojawapo ni kukidhi matarajio makubwa ya wadau na wananchi kwa kuboresha huduma zinazotolewa na TASAC. Changamoto kubwa zinazolikabili

Shirika ni:- 

i.     Uwepo        wa     mifumo      na     teknolojia isiyojitosheleza     katika        shughuli    za

Udhibiti na Biashara ya Meli; ii. Uhaba wa meli za kufanyia mafunzo

(seatime) na ajira za mabaharia; iii. Upungufu wa wataalam wenye ujuzi katika usanifu na ujenzi wa meli (Naval

Architects and Hydrographic Surveyors);  iv. Kuchelewa kwa utoaji wa leseni kwa watoa huduma za uendeshaji wa bandari (private port terminal operators) ambapo kwa mujibu wa matakwa ya kikanuni, ili watoa huduma hao waweze kupatiwa leseni ya uendeshaji, wanatakiwa wawe na Mkataba wa ukodishaji kati yao na TPA kuhusu eneo la uendeshaji; na

v. Taasisi ambazo ni wadau wa usafiri wa njia ya maji kuwa na mifumo isiyoongea ili kutoa huduma katika dirisha moja kwenye mifumo.

  • Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto hizo,TASAC imeweka mikakati ifuatayo:-
  1. Kuendelea kuimarisha mifumo ya TEHAMA ambayo hutumika katika shughuli za Udhibiti na Biashara ya

Meli;

  1. Kuajiri wataalam na kuwaendeleza waliopo, hasa katika maeneo ya Naval Architects and Hydrographic Surveyors – wapima ramani na maeneo ya kuweka

Aids to Navigation;

  1. Kuendelea kuhimiza TPA iingie makubaliano na watoa huduma za uendeshaji bandari (private port terminal operators) ili waweze kutimiza takwa hilo na kuweza kupata leseni. 

Huduma za Uchukuzi Baharini

  • Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Meli ya China na Tanzania (SINOTASHIP) inayojishughulisha na huduma za uchukuzi wa masafa marefu baharini inamilikiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Katika mwaka 2021, kampuni iliendelea kutoa huduma za uchukuzi baharini kwa kutumia meli yake moja yenye uwezo wa kubeba jumla ya tani 57,000 kwa wakati mmoja.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Januari, 2021 hadi Disemba 2021,  SINOTASHIP ilisafirisha jumla ya tani 613,112 za shehena ya mizigo ukilinganisha na jumla ya tani 609,010 zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho katika mwaka 2020. Hili ni ongezeko la tani 4,102 za mizigo. Pia, katika kipindi hicho kampuni iliendelea na biashara ya uwakala na hivyo kuongeza idadi ya meli zilizohudumiwa. Jumla ya makasha 56,198 yalihudumiwa katika bandari ya Dar es Salaam ikilinganishwa na makasha 49,990 ya mwaka 2020 sawa na ongezeko la asilimia 12.42. Mafanikio hayo yamepatikana kutokana na mchango wa Meli za COSCO na

Oriental Overseas Container Line (OOCL) ya China.

Huduma za Uchukuzi Katika Maziwa

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) imeendelea kutoa huduma za uchukuzi na usafiri kwenye Maziwa Makuu ya Victoria, Tanganyika na Nyasa. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, Kampuni hiyo ilisafirisha abiria 242,107 ikilinganishwa na abiria 230,149 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 5.2. Kuhusu usafirishaji wa mizigo, katika kipindi cha Julai hadi Aprili 2022, jumla ya tani za mizigo 20,484.67 zilisafirishwa ikilinganishwa na tani za mizigo 15,965.32  zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 28.31. Ongezeko hilo limetokana na Kampuni kujitangaza. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, MSCL imeendelea kutekeleza kazi zifuatazo:
    • Mradi wa Ujenzi wa meli ya MV Mwanza (Hapa Kazi Tu) yenye Uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo katika Ziwa Victoria: Ujenzi wa meli hii umefikia asilimia 66;
    • Mradi wa ukarabati mkubwa wa meli ya MV Umoja. Meli hii ina uwezo wa kubeba tani 1,200 za mizigo na hufanya safari zake kati ya Tanzania na nchi jirani za Kenya na Uganda katika Ziwa Victoria. Utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 25; na
    • Mradi wa ukarabati mkubwa wa meli ya MT Sangara katika Ziwa Tanganyika. Meli hii ina uwezo wa kubeba mafuta lita 400,000 na hufanya safari zake kati ya Tanzania na nchi jirani za DR Congo, Burundi na Zambia. Utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 19.4.
  • Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na upungufu wa watumishi kwa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) katika mwaka 2021/22, MSCL imeajiri watumishi wapya 26 katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022. Aidha, Serikali imetoa kibali cha kuajiri watumishi wengine 49 wa fani ya uendeshaji wa meli. Utekelezaji wa vibali hivyo unaendelea na utakamilika kabla Juni, 2022.

Huduma za Bandari

  • Mheshimiwa Spika,       Mamlaka   ya

Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeendelea kusimamia Bandari za Mwambao na za Maziwa Makuu kwa: kuendeleza miundombinu na huduma za kibandari; kuweka viwango na masharti kwa watoa huduma za bandari nchini; kusimamia na kudhibiti huduma za bandari, kulinda mazingira na usalama wa bandari kwa viwango vinavyokubalika; pamoja na kuweka mazingira mazuri yatakayowavutia wawekezaji kuwekeza katika sekta ya bandari. Aidha, Mamlaka imeendelea kutangaza bandari kimasoko pamoja na kushirikisha na kusimamia sekta binafsi katika uendeshaji wa shughuli za kibandari.

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, TPA ilihudumia shehena ya tani za mapato milioni 11.341 na kukusanya mapato ya Shilingi bilioni 888.93 ikilinganishwa na shehena ya tani za mapato (revenue) milioni 10.01 iliyohudumiwa na kukusanya Shilingi bilioni 751.293 katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la mapato la asilimia 18.32. Aidha, jumla ya magari 162,340 yalipakuliwa katika Bandari ya Dar es Salaam ikilinganishwa na magari 119,854 yaliyopakuliwa katika kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 35.5. 
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu uhudumiaji wa makasha, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, Kitengo cha Shehena Mchanganyiko cha Mamlaka kilihudumia makasha 137,416 ikilinganishwa na makasha 78,573 yaliyohudumiwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 74.9. Aidha, Kitengo cha TICTS kilihudumia makasha 522,668 ikilinganishwa na makasha 524,326 yaliyohudumiwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 0.3. 
  • Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TPA inaendelea na utekelezaji wa awamu ya pili ya uboreshaji wa Bandari ya Tanga. Mkataba wa mradi wa uboreshaji wa Bandari hii ulisainiwa Julai, 2020 kati ya TPA na M/S China Harbour Engineering Co. Ltd. na ulianza kutekelezwa mwezi Septemba 2020 kwa gharama ya Shilingi bilioni 256.8. Kazi zitakazotekelezwa kwenye Mradi huu zinajumuisha kuongeza kina cha lango la kuingia na kugeuzia meli na kuimarisha na kuboresha Gati namba 1 na 2. Hadi kufikia Aprili, 2022 kazi za mradi zilikuwa zimekamilika kwa asilimia 40. Kuhusu ujenzi wa Gati la kupokelea mafuta kutoka Uganda lililoko eneo la Chongoleani, TPA inaendelea na maandalizi ya ujenzi.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (TAMISEMI) inatambua changamoto na athari za uwepo wa bandari zisizo rasmi (bandari bubu) katika pwani ya Bahari ya Hindi na kwenye Maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa. Utafiti uliofanyika unaonyesha kwamba hadi Juni, 2021 kulikuwa na jumla ya Bandari zisizo rasmi 693. Kati ya hizo, bandari 239 ziko katika mwambao wa bahari ya Hindi, bandari 329 katika Ziwa Victoria, bandari 108 katika Ziwa Tanganyika, na bandari 17 katika Ziwa Nyasa. Athari za uwepo za bandari hizi ni hatari za kiulinzi, kiusalama na upotevu wa mapato ya Serikali. Aidha, kuna ushindani usio sawia (unfair competition) baina ya bandari rasmi na zisizo rasmi pamoja na biashara inayofanywa baina ya hizo bandari mbili tofauti. Wizara kwa kushirikiana na TAMISEMI imezielekeza Taasisi zinazohusika na suala hili kuendelea na zoezi la kutathmini bandari zisizo rasmi ili kuishauri Serikali kuzirasimisha kwa lengo la kuimarisha usalama, kuongeza fursa za ajira na mapato ya Serikali. Hadi Aprili 2022, jumla ya bandari zisizo rasmi 20 zilikuwa zimeainishwa katika awamu ya kwanza kwa ajili ya kuzifanyia tathmini ya kina ili kuzirasimisha.  
  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zilizotekelezwa katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 katika miradi ya kuboresha Bandari za Mwambao wa Bahari ya Hindi za  Dar es Salaam na Mtwara ni pamoja na: 

i. Kukamilisha awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam kupitia mradi wa Dar es Salaam Maritime

Gateway Project (DMGP);  ii. Kuendelea na kazi za kupanua, kuchimba na kuongeza kina cha lango la kuingilia na kutokea meli katika Bandari ya Dar es Salaam ambapo hadi kufikia Aprili, 2022 zilikuwa zimekamilika kwa asilimia 40; na

iii. Kuandaa makabrasha ya zabuni ya ujenzi wa barabara unganishi kuelekea kwenye gati jipya katika Bandari ya Mtwara. 

  • Mheshimiwa Spika, kazi zilitekelezwa katika bandari za Maziwa Makuu ni pamoja na kuendelea na ujenzi wa Bandari ya Karema katika Ziwa Tanganyika unaohusisha ujenzi wa gati, majengo ya abiria, maghala ya mizigo na ofisi mbalimbali; uongezaji wa kina, breakwaters na usawazishaji wa eneo. Mradi umekamilika kwa asilimia 90. Aidha, ujenzi wa mradi wa Magati ya Kibirizi na Ujiji katika Ziwa Tanganyika unaohusisha ujenzi wa Gati, majengo ya abiria, maghala ya mizigo, minara ya matanki ya maji, ofisi ya meneja wa bandari, uzio na nyumba ya mlinzi umekamilika kwa asilimia 65. Vilevile, mradi wa ujenzi wa Gati la Ndumbi katika Ziwa Nyasa na ghala la kuhifadhia makaa ya mawe umekamilika na upo katika kipindi cha uangalizi.
  • Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Ziwa Victoria, hatua zilizofikiwa ni pamoja na: kukamilika kwa ujenzi wa magati ya Nyamirembe, Magarine, Lushamba, Bukoba, Ntama, Chato awamu ya kwanza, Muleba na Gati mbili (2) za Majahazi katika Bandari ya Mwigobero. Kazi nyingine zilizofanyika ni kununuliwa kwa vifaa vya kuhudumia mizigo na meli (fork lifts); kuendelea na ukarabati wa majengo na ofisi za Bandari za Ziwa Victoria; kuboresha eneo la kushukia abiria Mwanza North; na kukamilika kwa ukarabati wa Link Span ya Bandari ya Mwanza South. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2021/22 Serikali kupitia TPA inaendelea na maandalizi ya kupanua miundombinu ya Bandari za Mwanza North, Mwanza South, Bukoba na Kemondo ili kuweza kuhudumia meli zinazoendelea kuongezeka katika Ziwa Victoria.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu ununuzi wa vifaa na mitambo kwa ajili ya kutoa huduma za kibandari, TPA imefanikiwa kununua vifaa na mitambo vifuatavyo: 

i. Reach Stacker saba (7) zenye uwezo wa kubeba tani 45 kila moja, kwa Bandari za

Dar es Salaam, Tanga na Kigoma;  ii.        Meli za Rubani (Pilot boats) tatu (3) kwa Bandari za Dar es Salaam, Tanga na

Mtwara; iii. Winchi (All Terrain Mobile Crane) tano (5) ambapo kati ya hizo tatu (3) zenye uwezo wa kubeba tani 60 na mbili (2) zenye uwezo wa kubeba tani 25 kwa Bandari za Dar es

Salaam, Itungi na Mtwara;  iv. Magari ya Zimamoto mawili (2) kwa Bandari za Dar es Salaam na Mtwara;

          v.                  Winchi ya kuhudumia makasha tupu

(Empty Container Handler) moja (1) yenye uwezo wa kubeba tani 8 kwa Bandari ya

Tanga; vi. Mashine za kunyanyulia mizigo (Forklifts) mbili (2) moja yenye uwezo wa kubeba tani 16 na moja (1) yenye uwezo wa kubeba tani

50 kwa Bandari ya Tanga; vii. Mashine ya kunyanyulia mizigo (Forklift) moja (1) yenye uwezo wa kubeba tani 50; 

  • Kifaa cha kunyanyulia makasha (SemiAutomatic Container Spreader) nne (4) zenye ukubwa wa futi mbili (2) kwa ishirini (20) na futi mbili (2) kwa arobaini (40) kwa Bandari ya Tanga; na 
  • Kifaa cha kupakulia shehena ya kichele (Grab) moja (1) yenye uwezo wa tani 15 kwa

Bandari ya Tanga

USAFIRI NA UCHUKUZI KWA NJIA YA ANGA

Udhibiti wa Huduma za Usafiri kwa Njia ya

Anga

  • Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeendelea kutoa huduma za kudhibiti usafiri wa anga, viwanja vya ndege, masuala ya kiusalama na kiuchumi katika utoaji wa huduma za usafiri kwa njia ya anga na uongozaji ndege kupitia vituo 14 vya Dar es Salaam, Zanzibar, Mwanza, Arusha, Pemba, Tabora, Kigoma, Dodoma, Iringa, Songwe, Mtwara, Tanga, Songea na Kilimanjaro. Pia, Mamlaka imeendelea kutoa huduma za uongozaji ndege zinazoruka na kupita katika anga la juu katika nchi za Rwanda na Burundi futi 24,500 kwenda juu kutoka usawa wa bahari kama ilivyokasimiwa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga duniani (ICAO). 
  • Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TCAA pia imeendelea kudhibiti Viwanja vya Ndege vinavyomilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Sekta Binafsi. Lengo ni kuimarisha utoaji huduma, kukuza utalii nchini na kuendelea kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni za uendeshaji wa Viwanja vya Ndege zinafuatwa.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kusaini upya na kupitia Mikataba ya usafiri wa Anga kati yake na nchi nyingine (Bilateral Air Services Agreements – BASA) ili kufungua soko la usafiri wa anga kwa lengo la kuboresha huduma za usafiri wa anga, kuvutia mashirika mengine kutoa huduma nchini na kuimarisha ushindani katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga nchini. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 Serikali imeingia mikataba mipya ya usafiri wa Anga (BASA) kati yake na nchi za Cape Verde na Ugiriki.  Aidha, BASA kati ya Tanzania na nchi za Oman, Uingereza, DRC, Nigeria, Qatar, Rwanda na Kenya ilipitiwa upya. Hivyo, hadi Aprili, 2022 Tanzania ilikuwa imeingia Mikataba na nchi 78 ikilinganishwa na nchi 76 ambazo Tanzania imeingia Mikataba nayo katika mwaka

       2020/21.        Kati         ya        Mikataba          hiyo,

Makampuni/Mashirika ya Ndege 20 kutoka nchi 18 yalikuwa yameanza kufanya safari za ndege 115 kwa juma kati ya Tanzania na nchi hizo hadi kufikia Aprili, 2022.

  • Mheshimiwa Spika, TCAA ilifanya ukaguzi wa ndege nane (8) ambazo ziliingia nchini kwa mara ya kwanza. Ndege hizo zimepewa vyeti vya awali vya ubora (Certificate of Airworthiness). Aidha, TCAA ilihuisha (renewal) usajili wa ndege 87 baada ya ukaguzi na kutoa vyeti vya ubora wa kuendelea kufanya kazi hapa nchini. Pia, jumla ya ndege sita (6) ziliondolewa kwenye daftari la usajili baada ya kumalizika kwa mikataba ya ukodishaji. Daftari la usajili wa ndege kwa sasa lina jumla ya ndege 394.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ajali moja (1) ilitokea katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara. Aidha, ndege ndogo inayomilikiwa na Kampuni ya PAMS Foundation ya mkoani Arusha ilipotea ikiwa na rubani kati ya Matemanga wilayani Tunduru na Kingupira kwenye hifadhi ya Selous na ilitafutwa kwa siku 28 bila mafanikio. Pia, katika kipindi hicho cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 matukio mawili ya ajali (incidents) yalijitokeza katika Hifadhi ya Serengeti na katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Amani Abeid Karume.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, idadi ya abiria waliotumia usafiri wa anga ni 1,748,278 ikilinganishwa na abiria 2,964,636 waliotumia usafiri huo katika kipindi kama hicho cha mwaka wa fedha 2020/21 sawa na upungufu wa asilimia 41. Aidha, idadi ya abiria waliosafiri ndani ya nchi ni 1,079,125 ikilinganishwa na abiria 1,969,120 waliosafiri katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na upungufu wa asilimia 45. Pia, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 idadi ya abiria waliosafiri kimataifa walikuwa ni 669,153 kutoka abiria 995,508 waliosafiri katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21 sawa na upungufu wa asilimia 33.

Sababu kubwa ya kupungua abiria ni uwepo wa janga la UVIKO – 19.

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 mizigo iliyosafirishwa nchini ni tani 2,070.30 ikilinganishwa na tani 3,568.26 zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020/21. Aidha, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, mizigo iliyosafirishwa kimataifa ni tani 12,115.05 ikilinganishwa na tani 22,944.55 zilizosafirishwa katika mwaka wa fedha 2020/21. Pia, miruko ya safari za ndege ilikuwa 70,931 ikilinganishwa na miruko 128,023 kwa mwaka 2020/21.  

Kushuka kwa utendaji huu katika usafirishaji wa abiria, mizigo na miruko ya ndege kwa kiasi kikubwa kunatokana na mlipuko wa UVIKO-19 unaoendelea duniani kote. Hata hivyo, takwimu hizi zinatarajiwa kuongezeka kutokana na  kupungua kwa ugonjwa huu ulimwenguni.

  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zilizotekelezwa katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ni:
    • Kuhakiki na kuboresha michoro inayoonesha taratibu za utuaji wa ndege kwa kutumia vifaa vya mawasiliano vya angani (Satellite) na vya ardhini katika viwanja vya

Zanzibar, Dodoma, Tabora na Kigoma; 

  1. Matengenezo kinga na marekebisho ya mitambo ya kuongozea ndege katika vituo vya mawasiliano vya Gairo na Nyanshana pamoja na viwanja vya ndege vya Julius Nyerere cha Dar es Salaam (JNIA), Amani Abeid Karume cha Zanzibar (AAKIA), Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro

(KIA), Mwanza, Dodoma na Songwe;  iii.       Kufanya matengenezo kinga katika mtambo wa kufundishia waongoza ndege wa Chuo cha Usafiri wa Anga;

  1. Uhuishaji wa muundo wa anga katika Tanzania           (Dar es       Salaam      Flight Information        Region        Airspace

Restructuring Project) ambapo taratibu mpya za kuwezesha ndege kutua katika viwanja vya Zanzibar, Dodoma, Tabora na Kigoma zilifanyika pamoja na kuhakiki ubora;

  • Kuendelea kutoa leseni za muda mfupi kwa ndege za nje kufanya kazi nchini; 
  • Kuandaa na kuwa mwenyeji wa mafunzo ya utatuzi wa changamoto za kisheria. Kozi hii ilifadhiliwa na Umoja wa Ulaya kupitia taasisi ya Africa Mashariki ya Civil Aviation Safety and Security Oversight Agency (CASSOA) ambapo wataalamu 40 kutoka nchi sita za Afrika ya Mashariki walihudhuria;
  • Kupitia na kuboresha rasimu ya usanifu na nyaraka za zabuni kwa ajili

ya ufungaji wa taa za kuongozea ndege katika uwanja wa kimataifa wa Amani Abeid Karume ikiwa ni uchambuzi wa awali wa kiusalama (safety assessment) wa pamoja na maegesho mapya kwenye kiwanja hicho;

  • Kukamilisha maandalizi muhimu kwa ajili ya kuingia rasmi kwenye mfumo wa leseni za kidigitali za watalaam wote wa usafiri wa anga. Hatua hii itaongeza ufanisi na kupunguza muda wa utoaji leseni;
  • Kukamilisha mafunzo ya ndani kwa maafisa wanaotoa taarifa za anga kutoka viwanja vya ndege vya

Kilimanjaro, Arusha, Tanga na Zanzibar (AAKIA) juu ya mabadiliko ya utoaji wa huduma kwa kuzingatia menejimenti ya habari za usalama wa anga;

  • Utafutaji wa ndege ndogo aina ya BatHawk yenye namba za usajili 5H MXO iliyopotea tarehe 18 Oktoba, 2021 kati ya Matemenga wilayani Tunduru na Kingupira kwenye Mbuga ya Taifa ya

Mwalimu Nyerere; na  xi.    Kuzinduliwa kwa mradi wa uimarishaji udhibiti wa usalama wa usafiri wa anga Tanzania wa  Dola za Marekani

1,000,000.

Huduma za Viwanja vya Ndege

  • Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imeendelea kutoa huduma kwa kuzingatia Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali ya Usafiri wa Anga. Mamlaka hii ina jukumu la kusimamia, kuendesha, kuboresha na kuendeleza viwanja vya ndege 58 vinavyomilikiwa na Serikali. Kazi zilizotekelezwa katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ni kusimamia shughuli za uendeshaji wa Viwanja vya Ndege nchini na kuhakikisha huduma zinaendelea kutolewa kikamilifu; kuboresha huduma za ulinzi na usalama katika Viwanja hivyo pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali kwa watumishi.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TAA na Wizara ya Afya inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha masuala ya kiafya kwa wasafiri wanaotumia Viwanja vya Ndege nchini na hii imekuwa ni chachu ya kuimarisha shughuli za usafiri wa anga nchini. TAA kwa kushirikiana na Wizara ya Afya imetenga maeneo maalumu kwa ajili ya utoaji wa huduma mbalimbali zinazohusiana na UVIKO – 19 kwa abiria.
  • Mheshimiwa Spika, uendeshaji, uendelezaji na usimamizi wa Viwanja vya ndege unaongozwa na Kanuni za Kitaifa na Kimataifa. Ili kukidhi matakwa hayo na kuendelea kuvutia mashirika ya ndege, Serikali kupitia TAA imeendelea kuboresha ulinzi na usalama katika viwanja vya ndege nchini. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, kazi ya Ujenzi wa uzio wa usalama katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza ilikamilika na pia Mamlaka imefunga mfumo wa ufuatiliaji mienendo ya shughuli za kiusalama na uendeshaji (CCTV) katika Kiwanja cha Ndege cha Tanga.Aidha, Mamlakailiandaa na kukamilishaprogramu za ulinzi na usalama katika viwanja vya ndege vya Lake Manyara, Arusha, Mwanza, Iringa, Mafia, Lindi, Mpanda, Tanga, Tabora, Songea, Songwe, Moshi na Nachingwea. Vile vile, Mamlaka ilifanya zoezi la kujipima na dharura ya uokozi majini (Water Rescue Emergency drill) katika Kiwanja cha ndege cha Bukoba.
  • Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha huduma za Zimamoto Viwanjani, Serikali kupitia TAA imeendelea kuhakikisha kunakuwepo na madawa ya kuzima moto, vifaa mbalimbali vya uokoaji pamoja na kufanya matengenezo ya magari ya Zimamoto katika Viwanja vya Ndege. Aidha, TAA imepokea magari mawili ya Zimamoto kutoka kwenye Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza.
  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine iliyotekelezwa na TAA ni upanuzi wa eneo la ukaguzi wa abiria wanaosafiri katika Kiwanja cha Ndege Dodoma. Uboreshaji huu umewezesha idadi ya abiria wanaoweza kuhudumiwa kuongezeka kutoka abiria 20 hadi 50 kwa wakati mmoja. Katika Kiwanja cha Ndege cha Arusha, kazi ya ujenzi wa maegesho mapya ya ndege (Remote Apron) kwa kiwango cha lami imekamilika na maegesho hayo yana uwezo wa kuegesha ndege 12 aina ya Caravan yenye uzito chini ya tani 20 kwa wakati mmoja. Aidha, kazi ya maboresho ya eneo la maegesho ya magari (Car Parking) kwa kiwango cha lami imekamilika. Maegesho hayo yana uwezo wa kuegesha magari 250 kwa wakati mmoja. Aidha, maboresho ya maegesho ya zamani ya ndege (Main Apron) katika kiwanja hicho yamefikia asilimia 70 na maboresho ya Jengo la abiria yamefikia asilimia 20.
  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha ufanisi wa utoaji huduma katika Viwanja vya Ndege unaendelea kuimarika, TAA imeendelea kutoa mafunzo ya muda mfupi mara kwa mara kwa wafanyakazi wake. Hadi Aprili, 2022 TAA ilitoa mafunzo kwa jumla ya wafanyakazi 435 katika nyanja za Zimamoto na Uokoaji,

Uendeshaji, Ulinzi na Usalama. 

  • Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha TAA inaendana na kasi ya ukuaji wa shughuli za usafiri kwa njia ya anga nchini unaopelekea mahitaji ya upanuzi na ujenzi wa viwanja vipya, juhudi zimeendelea kufanyika za utwaaji, upimaji na upatikanaji wa Hatimiliki ya ardhi kwa viwanja vya ndege mbalimbali ikiwemo Songea, Biharamulo, Morogoro, Nyasurura, Mafia, Urambo, Dodoma, Iringa, Bukoba na Chunya.
  • Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza mapato yatokanayo na vyanzo vingine visivyohusiana na ndege, TAA inaendelea kuimarisha mifumo ya maegesho ya magari ambapo taratibu za ununuzi wa Wakandarasi kwa ajili ya kusimika mifumo ya kielektroniki ya maegesho ya magari katika viwanja vya ndege vya Dodoma na Mwanza zinaendelea. Aidha, TAA inatarajia kujenga hoteli ya nyota nne pamoja na majengo ya kisasa ya biashara katika Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere kwa kushirikisha Sekta Binafsi. Hadi sasa, taratibu za ununuzi ya wabia wa uwekezaji katika Miradi hiyo zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya 2021/22, zipo changamoto kadhaa zilizojitokeza ambazo ni kuendelea kwa wimbi la UVIKO – 19 duniani kunakopelekea kuathirika kwa shughuli za usafiri wa anga nchini; ukosefu wa magari ya Zimamoto na Uokoaji; ufinyu wa wigo wa bajeti; uhaba wa watumishi; uvamizi wa maeneo ya Viwanja vya Ndege kwa kukosekana uzio; na gharama kubwa za utwaaji na umilikishwaji wa maeneo ya viwanja vya ndege. 
  • Mheshimiwa Spika, baadhi ya mikakati ambayo TAA ilichukua ni pamoja na kuendelea kushirikiana na Wizara ya Afya kwa kuboresha mazingira ya kiafya katika viwanja vya ndege ili kuwapa uhakika wa usalama wa afya abiria wawapo nchini; kuhakikisha mahitaji ya uzio wa usalama pamoja na magari ya zimamoto yanajumuishwa katika miradi mikubwa ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege; kuongeza jitihada za ukusanyaji mapato ya ndani kwa kufunga mifumo ya mapato ya kielektroniki; kuendelea kuwasiliana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kupata watumishi wa kutosha; na Mamlaka inaendelea kushirikiana na taasisi zingine za Serikali kwa ukaribu ili kuhakikisha gharama za upimaji ardhi na fidia zinapungua na hivyo kuwezesha upatikanaji wa hatimiliki.  

Kampuni ya Kuendeleza Kiwanja cha Ndege cha KIA

  • Mheshimiwa Spika,      Kampuni   ya

Kuendeleza Viwanja vya Ndege ya Kilimanjaro

(Kilimanjaro Airports Development Company Limited – KADCO) ni Kampuni ya Umma iliyopewa jukumu la kuendesha na kuendeleza Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA). Kampuni hii imekuwa ikiendesha na kuendeleza KIA kwa kuzingatia viwango vya Kitaifa na Kimataifa na hivyo kuvutia watumiaji wengi. Kwa mujibu wa Katiba ya Kampuni (Memorandum and Articles of Association – MEMARTS), majukumu ya KADCO ni kusimamia shughuli zote za uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro na kukiendeleza.

  • Mheshimiwa Spika, KADCO kama kampuni nyingne za uendeshaji wa shughuli za usafiri kwa njia ya anga duniani, iliathiriwa na mlipuko wa UVIKO – 19 ulioikumba dunia. Kwa sasa, utendaji unaendelea kuimarika siku hadi siku baada ya ugonjwa huo kuanza kupungua. Pamoja na madhara yaliyotokana na mlipuko wa ugonjwa huu na athari zake katika sekta ya usafiri wa anga, hali ya utendaji wa kampuni ya KADCO imeendelea kuimarika baada ya Serikali kuhakikisha kwamba maelekezo yote ya namna ya kukabiliana na janga hili yaliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na miongozo inayotolewa mara kwa mara na Wizara ya Afya inatekelezwa. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, Kiwanja cha ndege cha KIA kimetoa huduma za usafiri wa anga kwa Mashirika ya Ndege yenye ratiba maalum za safari 11 na yale yasiyokuwa na ratiba maalum yanayoleta watalii na watu mashuhuri wanaotembelea vivutio vilivyomo nchini kama vile; Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama na visiwa vya Zanzibar. Kampuni hii inatarajia kupokea shirika jipya la ndege la Eurowings – Discover Lufthansa Group ambalo litaanza safari zake rasmi kuja KIA mwezi Juni, 2022.
  • Mheshimiwa Spika, hali ya abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro kwa kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ni kama ifuatavyo;
  1. Kumekuwa na ongezeko la abiria wa Kimataifa (International) kwa asilimia 389 kutoka abiria 28,280 hadi kufikia abiria 138,156 ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21;
  1. Kuongezeka kwa abiria wa ndani (Domestic) kwa asilimia 74 kutoka abiria 94,771 hadi 165,151 ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21;
  1. Kuongezeka kwa abiria wanaounganisha safari (Transit passengers) kwa asilimia 128 kutoka abiria 48,430 hadi 110,604 ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa

mwaka 2020/21;

  1. Kuongezeka kwa miruko ya Ndege za Kimataifa (International) kwa asilimia 239 kutoka miruko 1,374 hadi 4,336 ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21; na  
  • Kuongezeka kwa miruko ya Ndege za ndani (Domestic) kwa asilimia 104 kutoka 3,674 hadi 7,492 ikilinganishwa na kipindi kama

hicho kwa mwaka 2020/21

  • Mheshimiwa Spika, KADCO imeendelea kuyavutia mashirika mbalimbali ya ndege za kubeba mizigo kama Ethiopian Airways na Rwanda Air kutumia KIA na Mwanza ili kusafirisha bidhaa hususan zinazozalishwa nchini. Kwa kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, tani 2,359,039.00 za mizigo ziliweza kusafirishwa kwenda nje ya nchi ikilinganishwa na tani 1,473,955.91 katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21 ikiwa ni ongezeko la asilimia 60. Aidha, tani 447,516 ziliingizwa nchini katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ikilinganishwa na tani 257,753 katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21 ikiwa ni ongezeko la asilimia 74. Aidha, KADCO imekidhi matakwa ya kiusalama na vigezo vya kimataifa katika kusafirisha mizigo kwenda mataifa mbalimbali ya Ulaya na Amerika na kuthibitishwa na Shirikisho la Mashirika ya Ndege Ulimwenguni (IATA). Hatua hii imeendelea kuongeza imani kwa wateja, kuongeza wigo wa mizigo inayosafirishwa kutoka KIA na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika mapato ya kiwanja.
  • Mheshimiwa Spika, pamoja na kuendelea kuimarika kwa shughuli na makusanyo katika Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro, bado uendeshaji wa kiwanja haujarudi kama ilivyokuwa kabla ya mlipuko wa UVIKO–19, changamoto mbali mbali zilizojitokeza katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/22 ikiwa ni pamoja na uhaba wa fedha uliosababisha kuahirishwa kwa utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo iliyokuwa imepangwa kufanyika. Miradi hiyo ni pamoja na usimikaji wa mfumo wa kutibu maji ya kisima cha KIA yaliyo na madini mengi ya chumvi na fluoride; uboreshaji wa eneo la maegesho ya magari (Car Parking); na upanuzi wa eneo la kuondokea abiria (Departure lounge). Changamoto nyingine ni uvamizi wa ardhi ya KIA ambayo imeendelea kujadiliwa kwa kushirikisha wadau muhimu ikiwa ni pamoja na viongozi wa maeneo hayo na kamati iliyoundwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. 

Huduma za Usafiri kwa Njia ya Anga 

  • Mheshimiwa Spika, Mpango na Bajeti ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) katika mwaka wa fedha 2021/22 ulilenga kuendelea kutoa huduma za kusafirisha abiria na mizigo ndani na nje ya nchi. Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili 2022, ATCL iliweza kusafirisha jumla ya abiria 663,016 ikilinganishwa na abiria 432,190 waliosafirishwa katika kipindi hicho mwaka wa fedha 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 53. Pia, ATCL iliweza kusafirisha jumla ya tani 1,953 za mizigo ndani na nje ya nchi ikilinganishwa na tani 1,152 iliyosafirishwa katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 70. Ongezeko hili limechangiwa na kuanzishwa kwa safari mahususi kwa ajili ya mizigo kati ya Guangzhou – China na Dar es Salaam kuanzia mwezi Agosti, 2021 pamoja na kurejesha safari za Mumbai – India ambazo zilikuwa zimeahirishwa kutokana na athari za UVIKO – 19. Ongezeko la usafirishaji wa abiria na mizigo kwa kiwango kikubwa limechangiwa na kupungua kwa UVIKO -19.
  • Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa usafiri kwa njia angakwa taifa letu, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22 ilikamilisha ununuzi wa ndege tatu mpya na kuzikabidhi ATCL. Ndege hizo niDash 8 Q400 ndege moja (01) yenye uwezo wa kubeba abiria 76 na ndege mbili (2) aina ya Airbus A220-300 zenye uwezo wa kubeba abiria 132 kila moja. Kuongezeka kwa ndege hizo kumeifanya ATCL kuwa na jumla ya ndege mpya 11 kufikia Aprili, 2022 ikilinganishwa na ndege 8 zilizokuwepo mwezi Februari, 2020.  
  • Mheshimiwa Spika, kuongezeka kwa idadi ya ndege kumepelekea kupanuka kwa mtandao wa safari na kuongezeka kwa miruko. Kutokana na hatua hiyo, ATCL imeanzisha safari mpya za kikanda katika vituo vya Lubumbashi, Nairobi na Ndola. Vile vile, ATCL imeongeza mtandao wake wa safar za ndani ya nchi kwa kuanzisha safari kati ya Dar es Salaam, Dodoma hadi Mwanza na kurejesha safari kati ya Dar es Salaam na Mtwara. Kufunguliwa kwa vituo hivyo vipya na kurejeshwa kwa baadhi ya vituo vilivyosimamishwa kumeifanya ATCL kuwa na jumla ya vituo 26 hadi Aprili, 2022. Kati ya vituo hivyo, vituo 15 ni vya ndani ya nchi na vituo 11 ni vya nje ya nchi. Vituo vya ndani ya nchi ambavyo ATCL inafanya safari zake ni Arusha, Bukoba, Dar es Salaam, Dodoma, Geita, Iringa, Kilimanjaro, Kigoma, Mbeya, Mpanda, Mtwara, Mwanza, Songea, Tabora na  Zanzibar. Safari katika kituo cha Iringa zimesitishwa ili kupisha matengenezo ya kiwanja cha ndege. Vituo vya nje ya nchi ambavyo ATCL inafanya safari ni: Bujumbura – Burundi, Entebbe – Uganda,

Hahaya – Comoro, Guangzhou – China, Harare – 

Zimbabwe, Lubumbashi -DR Congo, Lusaka na Ndola – Zambia, Mumbai – India na Nairobi – Kenya. Aidha, maandalizi ya kurejesha safari katika kituo cha Johannesburg zilizokuwa zimesitishwa yanaendelea. Vile vile, ATCL inafanya safari za mizigo tu katika kituo cha Guangzhou wakati safari za abiria zinatarajiwa kurejeshwa kabla ya mwezi Juni 2022.

  • Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia ATCL imeendelea kujipanga kimkakati kuhakikisha inabeba abiria wengi na kuongeza mtandao wake wa safari kwa kutumia mifumo iliyopo ya kibiashara. Mfumo ambao ATCL unautumia kwa sasa ni “interlining”, code-sharing. Mfumo huu unahusisha makampuni mawili kuingia makubaliano ya kubeba abiria katika kituo ambacho kampuni moja haifanyi safari zake wakati kampuni mwenza inafanya. Kwa sasa, ATCL imeshaingia katika makubaliano haya na makampuni ya kimataifa ikiwemo Shirika la Ndege la Rwanda, Ethiopia, India na Qatar. Pia,

ATCL ipo katika hatua za mwisho za makubaliano ya kusafirisha abiria (interlining) na makampuni mengine makubwa yakiwemo Shirika la ndege la Oman, Emirates, KLM pamoja na Precision Air. Makubaliano hayo yanatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022. Sambamba na mfumo huo, ATCL imeongeza mifumo ya kuwafikia wateja kwa kukata na kulipia tiketi. Mifumo hiyo ni pamoja na mfumo wa uuzaji wa tiketi ulimwenguni (Global Distribution System – GDS); Mawakala Wakuu; Mawakala wa Kawaida; tovuti; na kulipa moja kwa moja kupitia benki ambapo kwa sasa ATCL imeingia mikataba na NMB na CRDB.

  • Mheshimiwa Spika, ili kuongeza wigo zaidi wa usafirishaji wa abiria na mizigo kikanda na kimataifa na kuifanya Tanzania kuwa kitovu kikuu (hub), Serikali kupitia ATCL imeingia mikataba ya ununuzi wa ndege tano mpya ambazo ni:  Dash 8 Q400 ndege moja (1); Boeing B737-9 Max ndege mbili (2); Boeing B787-8 Dreamliner ndege moja (1); na Boeing 767-300F ndege moja (1) ambayo ni ya mizigo. 
  • Mheshimiwa Spika, Serikali imeiwezesha ATCL kuendelea na ukarabati na maboresho ya Karakana kubwa ya matengenezo ya ndege iliyopo Mkoani Kilimanjaro (Kilimanjaro Maintenance Facility – KIMAFA) ili kupunguza gharama za ATCL kufanya matengenezo makubwa ya ndege nje ya nchi. Aidha, ninapenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba kwa sasa matengenezo yote madogo na makubwa ya ndege zote za ATCL ikiwemo ndege kubwa aina ya Boeing 787-8 Dreamliner hufanyika hapa nchini. Haya ni mafanikio makubwa ambayo ATCL imeweza kuyafikia mwaka 2021/22.
  • Mheshimiwa Spika, ATCL imeendelea kutoa mchango katika kuongeza ajira. Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Aprili, 2022 ATCL imeajiri jumla ya wafanyakazi 26 na kufanya kuwa na jumla ya watumishi 630. Kati ya watumishi hao waliopo, watumishi 110 ni wahandisi na mafundi mchundo wa ndege; watumishi 102 ni marubani; watumishi 108 ni wahudumu wa ndege; wasimamizi wa shughuli za ndege kiwanjani (operation officers) 14 ; watumishi katika eneo la biashara na masoko 110  na watumishi wengine ni 186 . Hivyo, watumishi wanaohusina moja kwa moja na biashara na uendeshaji ni asilimia 70.5 wakati watumishi wezeshi (supporting staff) ni asilimia 29.5.  ATCL imendelea kutoa huduma na stahili kwa watumishi wote kwa wakati.

HUDUMA ZA HALI YA HEWA

  • Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imeendelea kutoa, kusimamia, kudhibiti na kuratibu utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini. Mamlaka pia imeendelea kutoa tahadhari kuhusiana na hali mbaya ya hewa, kufanya tafiti za kisayansi za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi, kubadilishana taarifa za hali ya hewa katika mtandao wa dunia (Global Telecommunication System – GTS) kulingana na makubaliano ya Kimataifa pamoja na kuiwakilisha nchi katika masuala ya hali ya hewa Kikanda na Kimataifa. Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa TMA ameendelea kuhudumu katika nafasi yake ya Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organisation – WMO).
  • Mheshimiwa Spika, TMA imeendelea kutoa taarifa za mrejeo wa mwenendo wa hali ya hewa kadiri mabadiliko ya mifumo ya hali ya hewa yanavyojitokeza ambapo usahihi wa utabiri umefikia asilimia 88.3 ambao ni  juu ya asilimia 70 ya kiwango cha usahihi kinachokubalika na Shirika la Hali ya Hewa Duniani. Aidha, utabiri wa mvua za vuli kwa kipindi cha Oktoba – Disemba 2021 na ule wa Masika kwa kipindi cha Machi hadi Mei, 2022 ulitolewa. Kwa ujumla, mvua za vuli zilitarajiwa kuwa za chini ya wastani hadi wastani na zilitarajiwa kuambatana na vipindi virefu vya ukavu katika maeneo mengi yanayopata mvua za vuli. Mamlaka pia ilitoa taarifa ya utabiri wa maeneo madogo madogo kwa Wilaya 92 za Tanzania Bara na Zanzibar zinazopata misimu miwili ya mvua. Pia, Mamlaka iliandaa taarifa ya utabiri wa msimu kwa ajili ya mwezi Novemba, 2021 hadi Aprili, 2022 kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua na kuandaa utabiri wa maeneo madogo kwa Wilaya 63 za Tanzania Bara. Utabiri huo umechangia katika kutoa taarifa kwa mamlaka husika pamoja na jamii na hivyo kujiandaa kukabiliana na athari zitokanazo na hali mbaya ya hewa.  
  • Mheshimiwa Spika, usahihi wa utabiri umechangiwa kwa kiasi kikubwa na uboreshaji wa miundombinu na huduma za hali ya hewa ikiwemo ununuzi wa vifaa na mitambo ya kisasa ya kupima hali ya hewa. Serikali imeendelea kutekeleza mpango wa kuwa na mtandao wa

Rada saba (7) za hali ya hewa hapa nchini. Malipo ya ununuzi wa Rada mbili (2) za hali ya hewa zitakazofungwa Kilimanjaro na Dodoma yamefanyika kwa asilimia 80.Utengenezaji wa rada za hali ya hewa zinazotarajiwa kufungwa Kigoma na Mbeya upo katika hatua za mwisho nchini Marekani. Malipo yamefanyika kwa asilimia 80 kwa ajili ya uboreshaji wa mifumo ya rada za Dar es Salaam na Mwanza ili kuendana na teknolojia ya kisasa. Kazi ya ukarabati wa vituo vinne (4) vya hali ya hewa vilivyopo Tabora, Singida, Dodoma na Mpanda imekamilika. Pia, Mamlaka imeanza awamu ya pili ya ukarabati wa vituo vitatu (3) vya hali ya hewa vilivyopo Shinyanga, Mahenge na Songea pamoja na kuendelea na ujenzi wa Kituo cha Uangazi cha Dodoma.

  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zilizotekelezwa katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 ni: –
  1. Kuendelea na utekelezaji wa mfumo wa kudhibiti ubora wa huduma bora za hali ya hewa kwa sekta ya usafiri wa anga kulingana na viwango vya kimataifa. Mamlaka ilifanyiwa ukaguzi wa Kimataifa kati ya tarehe 6 – 10 Disemba, 2021 na kuendelea kumiliki

cheti cha ubora cha ISO 9001:2015;   

  1. Kufanya tafiti mbalimbali za hali ya hewa na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi. Jumla ya tafiti nane (8) zilichapishwa katika Majarida ya

Kimataifa ya Kisayansi;

  1. Kuendelea kufikisha huduma za hali ya hewa kwa wananchi kwa kuongeza idadi ya redio na luninga pamoja na magazeti yanayotoa matangazo ya hali ya hewa. Hadi sasa, taarifa za hali ya hewa zinatolewa katika vituo vya runinga 15 na vituo vya redio 66 pamoja na magazeti mawili (2);
    1. Uandaaji wa Kanuni za Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Na. 2 ya mwaka 2019 ambapo Kanuni saba (7) kati ya 11 za sheria hiyo zilikamilika na kuanza kutumika; 
  • Kuiwakilisha Tanzania Kikanda na Kimataifa katika masuala ya hali ya hewa. Mamlaka ilishiriki katika mikutano mbalimbali ikiwemo Mkutano Mkuu wa 26 wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi uliofanyika Glasgow,

Uingereza; na 

  • Mamlaka kuendelea kutekeleza mpango wa mafunzo kwa watumishi  71 kati yao 23 walianza masomo, watumishi 24 waliendelea na masomo na wengine 24 walihitimu mafunzo yao katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

C.3 TAASISI ZA MAFUNZO

  • Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa majukumu ya Taasisi za Mafunzo zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka 2021/22 ni kama ifuatavyo:

Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi 

  • Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (Institute of Construction Technology – ICoT) ina jukumu kuu la kutoa mafunzo katika fani za Ujenzi, Umeme na Mitambo katika ngazi za chini na kati ili kuzalisha wataalam watakaohudumia Sekta ya Ujenzi. 
  • Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022, Taasisi ilidahili Wanafunzi 64, ambapo kati yao Wanafunzi 41 walidahiliwa na kujiunga na mafunzo ya ngazi ya Astashahada (NTA Level 4) na Wanafunzi 25 wanaendelea na mafunzo kwa ngazi ya NTA Level 5. Aidha, Taasisi imetoa Mafunzo ya Ufundi Stadi kwa wanafunzi 544 kati yao wanafunzi 167 wamehitimu. Taasisi pia imetoa mafunzo ya muda mfupi kwa wanafunzi 178 na inaendelea kutoa mafunzo hayo kwa wanafunzi 36. Aidha, Taasisi imepata kibali cha kuajiri wafanyakazi 36 kwa mkataba wa mwaka mmoja ambapo taratibu za kuwapata wafanyakazi hao zipo kwenye hatua ya utekelezaji kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. Vilevile, maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Taaluma na Utawala yanaendelea na yapo katika hatua ya manunuzi ili kumpata

Mkandarasi wa ujenzi.

Vilevile, Taasisi imefanya uhamasishaji wa matumizi ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi katika Halmashauri za Mikoa sita (6) na kazi hiyo inaendelea. Aidha, Taasisi imeendesha kozi tatu (3) za matumizi ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi ambazo zilihudhuriwa na jumla ya washiriki 48. Vilevile, Taasisi imeshiriki kwenye maonesho ya mikutano mitatu (3) ya Bodi ya Wahandisi; mkutano wa Chama cha Makandarasi Wanawake na Taasisi ya Wahandisi Tanzania.

Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI)

  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Bahari Dar es Salaam (Dar es Salaam Maritime Institute – DMI) kimeendelea kutoa mafunzo ya Ujuzi na Utaalamu (Certificates of Competency) katika masuala ya usafiri kwa njia ya maji kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) na Shirika la Bahari Duniani (IMO). Aidha, Chuo hiki kinachoendesha mafunzo yake kwa kuzingatia Ubora wa Viwango vya Kimataifa yaani ISO 9001:2015 kinatambuliwa na Baraza la Usimamizi wa Elimu ya Ufundi Tanzania

(NACTE).

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Chuo kilidahili jumla ya wanafunzi 5,091 ikilinganishwa na wanafunzi 4,527 waliodahiliwa katika mwaka 2020/21 sawa na ongezeko la asilimia 12.5. Kati ya hao, wanafunzi 2,314 wamejiunga na mafunzo ya muda mfupi na wanafunzi 2,777 wamejiunga na mafunzo ya muda mrefu. Chuo kimeendelea kuwajengea uwezo watumishi wake ambapo jumla ya watumishi 16 wanaendelea na mafunzo ya muda mrefu na watumishi 99 wamehudhuria kozi za muda mfupi.  

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)

  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeendelea kutoa mafunzo, kufanya tafiti, kutoa ushauri wa kitaalam na machapisho kwa lengo la kufundisha wataalam katika njia zote za usafirishaji na uchukuzi ambazo ni barabara, anga, reli, maji na usafiri kwa njia ya mabomba. Katika mwaka wa masomo 2021/22, Chuo kilitoa mafunzo ya kozi ndefu 33 ikilinganishwa na kozi 28 zilizotolewa katika mwaka wa masomo 2020/21 ikiwa ni ongezeko la kozi tano (5) sawa na asilimia 17.86. Kwa sasa Chuo kina wanafunzi wa kozi ndefu 12,942 ikilinganishwa na wanafunzi 10,988 katika mwaka wa masomo 2020/21 ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 1,442 sawa na asilimia 13.    
  • Mheshimiwa Spika, ili kufanikisha mafunzo ya taaluma ya usafiri wa Anga, Serikali kupitia Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kimeendelea kutekeleza mradi wa kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Mafunzo ya Usafiri wa Anga na Operesheni za usafirishaji unaofadhiliwa na Benki ya Dunia. Kwa sasa, Chuo kinaendelea na ujenzi wa majengo tisa (9). Kati ya hayo, majengo matano (5) yanajengwa katika Kampasi ya Mabibo Dar-es-Salaam kwa ajili ya kufundishia Wahandisi wa Ndege na Wahudumu wa Ndani ya Ndege na majengo manne (4) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya mafunzo ya Urubani. Aidha, ujenzi wa majengo matano (5) umefikia hatua ya kumpata mkandarasi na ule wa majengo manne (4) umefikia hatua ya kusajili Mradi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ili kufanya tathmini ya Mazingira na Masuala ya Kijamii kwa ajili ya ujenzi majengo hayo.  
  • Mheshimiwa Spika, kwa upande wa vifaa vya kufundishia mafunzo ya taaluma za usafiri anga, Chuo kimeingia mkatabawa ununuzi wa ndege mbili (2) za mafunzo ya Urubani na kampuni ya TEXTRON Aviation Inc – Marekani.  Vilevile, Chuo kimeingia mkatabawa ununuzi wa vifaa kwa ajili ya mafunzo ya uhudumu ndani ya ndegena kampuni ya AVIC International Holding Co. Ltd ya China. Vifaa hivi vinatarajiwa kuwasili katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/23. Pia, Chuo kinaendelea na ununuzi wa vifaa vya kisasa vya maabara na karakana.   
  • Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia Serikali kupitia NIT inakamilisha ujenzi wa Awamu ya Tatu (3) wa Kituo cha Rasilimali Mafunzo Mabibo, Dar es Salaam. Kituo hiki kina Jengo la ghorofa sita (6) ambalo lina Maktaba yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 450 kwa wakati mmoja, madarasa yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,653pamoja na ofisi za watumishi. 
  • Mheshimiwa Spika, NIT imeendelea kuwajengea uwezo wakufunzi ili kuweza kutoa mafunzo yenye ubora na yanayoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia duniani. Katika mwaka wa fedha 2021/22, Chuo kimepeleka watumishi 15 katika mafunzo ya muda mrefu na kufanya jumla ya watumishi 65 kuwa katika mafunzo. Kati ya watumishi hao, 36 wanasoma Shahada ya Uzamivu, 20 Shahada ya Uzamili, mmoja (1) Shahada ya Kwanza, wanne (4) mafunzo maalum ya Urubani (Integrated Commercial Pilot License Course – ICPL) na wanne (4) mafunzo maalum ya ujuzi wa matengenezo ya Ndege (Basic Aircraft Maintenance Technician License). Aidha, Chuo kinaendelea kuandaa rasimu za nyaraka za uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji kwa ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China ambapo nyaraka 11 kati ya 20 zimekamilika. 
  • Mheshimiwa Spika, kupitia Kituo cha Kikanda cha Umahiri cha Mafunzo ya Usalama Barabarani kilichoanzishwa kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kinaendelea kutoa mafunzo, kufanya tafiti na huduma za ushauri wa kitaalam katika usalama barabarani kwa soko la ndani ya nchi na kikanda ili kutatua changamoto za usalama barabarani. Hadi kufikia Aprili, 2022 Chuo kimeandaa Mpango Mkakati wa miaka mitatu wa kuwafikia walengwa wa Kituo na utambuzi katika masuala ya usalama barabarani, Hadidu za Rejea (ToR) za kumpata Mshauri Elekezi atakayeandaa Mitaala na Miongozo ya kufundishia pamoja na kupata Ithibati ya kimataifa ambapo vyote vimepata idhini (No Objection) kutoka AfDB. Katika utekelezaji wa majukumu ya kituo, Chuo kimekuwa na ushirikiano na wadau mbalimbali wa masuala ya usalama barabarani wakiwemo Jeshi la Polisi,  International Road Assessment Programme (iRAP) na Tanzania Roads Association (TARA).

Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam (CATC)

  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) kimeendelea kutoa mafunzo katika taaluma za uongozaji ndege (Air Traffic Controllers), mafundi wa mitambo ya kuongozea ndege na mawasiliano (Communication, Navigation and Surveillance), wataalam wa mawasiliano ya taarifa za anga (Aeronautical Information Officers), usalama wa anga na upekuzi (Aviation Security), Wasimamizi na waandaaji wa safari za ndege (Flight Operations Officers), usafirishaji wa bidhaa hatarishi (Dangerous Goods), makosa ya kibinadamu (Human Factor) na usimamizi wa viwanja vya ndege (Airport Management).  
  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania kwa kushirikiana na chuo cha ProWings Training Limited cha Afrika Kusini kilianza kutoa mafunzo ya urushaji wa ndege zisizokuwa na rubani (Drone Pilot Training) hapa nchini kuanzia mwezi Januari, 2021. Aidha, baada ya kupata uzoefu na kuwajengea uwezo wataalam wa ndani, CATC imeanza kutoa mafunzo hayo peke yake kuanzia mwezi Januari, 2022. 
  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania ni mwanachama wa Shirika la

Kimataifa linalosimamia Usafiri wa Anga Duniani

(ICAO TRAINAIR PLUS Full Member) na kuthibitishwa na Shirika la Viwango na Ubora Duniani (ISO 9001:2015). Aidha, Chuo hiki ni mwanachama wa Baraza Kuu (Council Member) la Umoja wa Vyuo vya Mafunzo ya Safari za Anga Afrika (African Association Training Organization – AATO). Pia, Chuo hiki ni mwanachama wa

Baraza Kuu la taasisi ya kimataifa ya usafirishaji wa mizigo ya London Uingereza (CILT). Kitaifa, Chuo kimeidhinishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE). Vilevile, Chuo kimethibitishwa na TCAA kuwa kituo cha kutoa mafunzo ya wataalam wa sekta ya usafiri kwa njia ya anga ndani na nje ya nchi (Approved Training Organization (ATO).

  • Mheshimiwa Spika, idadi ya washiriki katika Chuo hiki imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka na hasa miaka ya hivi karibuni baada ya Chuo kuboresha mikakati yake ya kujitangaza ndani na nje ya nchi.Washiriki wa nje ya nchi ni kutoka Uganda, Botswana, Namibia, Swaziland, Zambia, Burundi, Rwanda, Somalia, Nigeria, Liberia, Sierra Leone na Guinea Conakry. Washiriki wa ndani ya nchi wanatoka mashirika ya ndege, viwanja vya ndege vya Serikali na binafsi, Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), mashirika mbalimbali yanayotoa huduma kwenye viwanja vya ndege, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi na wananchi kwa ujumla. Kwa mwaka 2020/21 idadi ya washiriki ilikuwa 1,206 wakati katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 washiriki walikuwa 963. Idadi hiyo ilipungua kutokana na athari za UVIKO – 19.

Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma

  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Hali ya Hewa kilichopo Kigoma kimeendelea kutoa mafunzo ya hali ya hewa katika ngazi ya awali na ya kati.  Katika mwaka 2021/22, jumla ya wanafunzi 39 walidahiliwa katika mafunzo ya hali ya hewa ambapo wanafunzi 12 ni wa ngazi ya cheti na wanafunzi 27 ni wa ngazi ya Diploma. Aidha, kazi ya ukarabati wa mabweni na majengo ya Utawala inaendelea. Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa kimeingia makubaliano (MoU) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kwa ajili ya kuanzisha mafunzo ya TEHAMA.

C.4 MASUALA MTAMBUKA

Rasilimali watu na Maendeleo ya Watumishi

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22 watumishi 36 wa Wizara (Sekta ya Ujenzi) wamehudhuria mafunzo. Kati ya hao, watumishi 10 wamehudhuria mafunzo ya muda mrefu na watumishi 26 wamehudhuria mafunzo ya muda mfupi. Kwa upande wa Sekta ya Uchukuzi, watumishi 140 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi ndani ya nchi na watumishi 9 walipatiwa mafunzo ya muda mrefu ndani na nje ya nchi. Sekta ya Uchukuzi imeandaa mpango wa miaka mitatu (3) wa Rasilimali Watu (Human Resources Plan) na Urithishanaji Madaraka (Succession Plan). Lengo la mipango hii ni kukabiliana na changamoto za uhaba wa watumishi wenye weledi kulingana na mahitaji ya Sekta. Vilevile, katika mwaka 2021/22, Sekta ya Uchukuzi imefanya mapitio ya Muundo wa Maendeleo ya Utumishi wa kada za Maafisa Usafiri ili kuendana na mahitaji ya wataalamu wa fani ya Uchukuzi na Usafirishaji ili kusimamia Sekta ya Usafiri.

Ushirikishwaji wa Wanawake Katika Kazi za

Barabara

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutoa elimu kwa wadau kuhusu ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara ikiwa ni pamoja   na      elimu          juu    ya      Mwongozo wa Ushirikishwaji        Wanawake      katika        kazi   za barabara. Aidha, Wizara iliendelea kutoa semina kwa Waratibu wa Mikoa kuhusu matumizi ya Mfumo wa Kanzidata ya Ushirikishwaji wa Wanawake. Vilevile, Wizara iliendelea kutoa mafunzo kwa Wanawake kuhusu Sheria ya Manunuzi na Matumizi ya Mfumo wa TANePS, taratibu za kusajili Kampuni na usimamizi wa vikundi vya wanawake waliopo katika vikundi au waliosajili kampuni ili waweze kusimamia na kuelekeza kikamilifu Wanawake walio tayari kushiriki kazi za barabara.

Vilevile, Wizara ilitembelea Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia         Mbeya        (MUST)       na     kuongea     na wanafunzi       Wanawake          wanaosoma         fani   za kihandisi kwa lengo la kuwashauri namna ya kuendeleza fani hizo baada ya kuhitimu masomo yao.

Maboresho ya Sheria za Kisekta 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea na taratibu za ukamilishaji wa rasimu ya Kanuni za Usajili wa Makandarasi (The Contractors

Registration criteria) chini ya Sheria ya Usajili wa

Makandarasi ya mwaka 1997. Vilevile, mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Baraza la Taifa la Ujenzi na Sheria ya Bodi ya

Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi yanaendelea kufanyiwa kazi. Wizara inaendelea na zoezi la tafsiri kwa lugha ya kiswahili kwa mapendekezo ya Sheria hizo yaliyowasilishwa na wadau. Tafsiri ya Sheria hizo katika lugha ya Kiswahili imetokana na marekebisho yaliyofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia marekebisho kwenye Sheria Mbalimbali Na. 02 ya Mwaka 2021 ambayo imefanya marekebisho kwenye Sheria ya Tafsiri ya Sheria Sura ya 1, Sheria ya Mahakama za Mahakimu Sura ya 11 na Sheria ya Mahakama za Ardhi Sura ya 216 ambazo zimefanya Kiswahili kuwa lugha ya utoaji haki. 

Serikali Kuhamia Dodoma

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuhamia Dodoma. Katika mwaka wa fedha 2021/22, taasisi tatu (3) za Sekta ya Ujenzi ambazo ni Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) zimehamia Dodoma baada ya kukamilisha ujenzi wa majengo ya Ofisi zao. Aidha, Bodi ya Usajili wa Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) inatarajia kuhamia rasmi Dodoma Juni, 2022 na hivyo kufanya jumla ya taasisi za Wizara (Ujenzi) zilizohamia Dodoma hadi mwisho wa mwaka wa fedha

2021/22 kufikia sita (6). Mikakati ya taasisi mbili

(Wakala wa Barabara Tanzania na Wakala wa Majengo ya Serikali) kuhamia Dodoma inaendelea ikihusisha ujenzi wa majengo ya ofisi za Taasisi hizo.

Masuala Mengine Yaliyotekelezwa na Wizara

  • Mheshimiwa Spika, majukumu mengine yaliyotekelezwa na Wizara ni pamoja na yafuatayo: 

i. Ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na majukumu mengine yanayosimamiwa na Wizara kupitia Mpango Kazi wa Mwaka wa

Fedha 2021/22; ii. Kuandaa na kuwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Wizara ya Fedha na Mipango Taarifa ya Hesabu ya Mwaka wa Fedha 2020/21 kwa wakati;

  1. Kuandaa Mpango wa Ununuzi wa Mwaka (Annual Procurement Plan) wa Wizara kwa mwaka wa fedha 2021/22;
    1. Kuandaa Taarifa za Takwimu za Wizara kwa mwaka 2020;
    1. Kuimarisha Mifumo ya Udhibiti wa Ndani wa Wizara; na
    1. Kupitia Mkataba wa Huduma kwa Mteja

(Client Service Charter).

C.5 CHANGAMOTO ZILIZOIKABILI WIZARA NA

MIKAKATI YA KUZITATUA

  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imekabiliwa na changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yake. Baadhi ya changamoto hizo na mikakati ya kuzitatua ni: –

       i.     Ufinyu wa Bajeti

Ufinyu wa Bajeti ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi Mengineyo ikilinganishwa na mahitaji halisi umesababisha malimbikizo ya madeni ya miradi ya maendeleo hususan, miradi ya barabara inayohusisha madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri. 

Mkakati

Serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha madai ya Makandarasi yanalipwa kwa wakati. Aidha, Serikali imeendelea na jitihada za kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa miradi mbalimbali. Hadi Aprili, 2022, Serikali imetoa fedha za maendeleo jumla yaShilingi 691,100,092,642.94kulipa madeni na madeni yaliyohakikiwa na inaendelea kutoa fedha kwa ajili ya malipo ya madeni ya miradi ya barabara inayoendelea. 

Katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Aprili, 2022, Serikali imetoa Shilingi 541,641,298,899.00 za Mfuko wa Barabara ambazo zimetumika kuwalipa Makandarasi wa ndani wanaofanya kazi za matengenezo na ukarabati wa barabara.

  1. Uvamizi wa maeneo ya Hifadhi ya Barabara 

Wananchi wamekuwa wakivamia na wakijenga katika maeneo ambayo TANROADS haijaweka alama za mwisho wa hifadhi ya barabara (Road Reserve). Hali hii husababisha usumbufu na gharama kubwa katika ujenzi wa barabara kutokana na Serikali kutakiwa kulipa fidia kubwa.

Mkakati

Wizara kupitia TANROADS imeendelea kuweka alama na kuzuia uendelezaji katika hifadhi za barabara. Aidha, Wizara imeendelea kuelimisha Umma kwa njia ya vyombo vya habari, vipeperushi, mikutano na semina ili waweze kufahamu vyema Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007.

  1. Ushiriki Hafifu wa Makandarasi wa Ndani katika Utekelezaji wa Miradi Mikubwa Uwezo mdogo wa mtaji walionao Makandarasi wa Ndani hivyo kushindwa kushiriki kikamilifu katika fursa za kazi kutokana na masharti ya upatikanaji wa dhamana za zabuni, dhamana za ushiriki wa kazi na

mitaji ya kuwezesha kufanya kazi kutoka mabenki kuwa ngumu na kutozingatia mahitaji halisi ya shughuli za kihandisi. 

Aidha, kushindwa kupata mitaji kunawafanya Makandarasi kushindwa kukua na kupata fursa ambazo zitawezesha kuwakwamua kutokana na uwezo wao mdogo.

Mkakati

Wizara kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi, Baraza la Taifa la Ujenzi na Bodi ya Usajili wa Wahandisi imeendelea kutoa mafunzo kwa Wahandisi Washauri na Makandarasi wa Ndani ili wasimamie na kutekeleza miradi kikamilifu hususan mikataba ya ujenzi na matengenezo ya barabara. Aidha, Bodi ya Usajili wa Makandarasi inaendeleza Mfuko Maalum wa Kutoa Dhamana ya kusaidia Makandarasi wadogo na wa Kati. Mfuko kwa sasa umefikisha mtaji wa ShilingiBilioni 3.9na idadi ya wanachama imefikia 1,277. Wizara kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi itaendeleza jitihada za kuhamasisha Makandarasi wa ndani kujiunga ili kuomba zabuni kwa utaratibu wa ubia. Aidha, Wizara itaendelea kuhamasisha makandarasi wa ndani waingie ubia na kampuni za nje ili wapate ujuzi na uzoefu wa utekelezzaji wa miradi mikubwa ya ujenzi. 

iv.        Mahitaji      Makubwa      ya      Fedha      za

Matengenezo ya Barabara

Mfuko wa Barabara una uwezo mdogo wa kukidhi mahitaji ya matengenezo ya barabara. Kwa sasa Mfuko una uwezo wa kugharamia asilimia 42 tu ya mahitaji halisi ya matengenezo ya barabara Tanzania Bara.

Mkakati

Wizara kupitia Bodi ya Mfuko wa Barabara imeandaa mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mfuko ili kutambua tozo za gesi na nishati nyingine zinazoweza kuendesha vyombo vya moto barabarani kama chanzo cha mapato ya Mfuko wa Barabara sambamba na dizeli na petroli.

v.         Uharibifu    wa    Barabara    kutokana    na

Uzidishaji wa Uzito wa Mizigo

Uzidishaji wa uzito wa magari unaofanywa na wasafirishaji na hivyo husababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara.

Mkakati

Wizara pamoja na taasisi yake TANROADS, ili kupunguza uharibifu wa miundombinu ya barabara imekuwa ikitoa elimu kuhusu Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Udhibiti Uzito wa Magari ya Mwaka 2016 na Kanuni zake za mwaka 2018. Aidha, Wizara kupitia (TANROADS) inasimamia utendaji kazi katika vituo vya mizani vinavyotumika kudhibiti uzito wa magari barabarani ambapo hadi sasa Wizara inamiliki jumla ya mizani 66 za kudumu na mizani 22 zinayohamishika. Mizani hiyo ipo katika Mikoa yote hapa nchini. Aidha, Wizara imefunga mizani inayopima Magari yakiwa kwenye mwendo (Weigh in Motion) katika vituo vya mizani vya Kimokouwa Mkoani Arusha, Vigwaza mkoani Pwani, Mikese na Dakawa (Morogoro), Wenda (Iringa), Nala (Dodoma), Njuki (Singida) na Mpemba (Njombe). Jitihada nyingine ni ufungwaji wa kamera za ukaguzi na usimamizi wa utendaji kazi wa watumishi wa vituo vya mizani kwa kuanza na ufungaji wa kamera hizo katika vituo 13 vya mizani ili kufanya udhibiti wa watumishi wasio waaminifu wanaoshirikiana na wasafirishaji wasio wazalendo kupitisha magari yaliyozidisha uzito bila kulipa tozo ya uzidishaji uzito. 

  • Kasi ya mabadiliko ya Kiteknolojia katika vifaa, mbinu na ubunifu kwenye sekta ya ujenzi.  

Mkakati

Wizara kupitia taasisi zake inaendelea kutumia mbinu ya mafunzo kazini (on job training) pamoja na ushirikiano na baadhi ya makampuni ya Kimataifa yenye uzoefu ili kujenga uwezo kwa Watumishi wake. Aidha, Wizara ina taasisi yenye jukumu la  usambazaji wa teknolojia mpya katika sekta ya ujenzi na usafirishaji (TANT2 Centre).

  • Tishio la Magonjwa wa UVIKO-19

Ugonjwa wa UVIKO-19 bado umeendelea kuwa tishio duniani kote. Hali hii imeendelea kuleta hofu kubwa katika Sekta ya Uchukuzi hususan kwenye vituo vya mipakani, bandari na viwanja vya ndege hivyo kuathiri Utendaji wa Taasisi zinazotoa huduma katika maeneo hayo.

Mkakati: 

Wizara inaendelea kuchukua tahadhari katika vituo vya mipakani, viwanja vya ndege na maeneo ya bandari ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona vinavyosababisha UVIKO-19. Aidha, vifaa vya kinga vimeendelea kutolewa, chanjo kwa Wafanyakazi katika maeneo hayo pamoja na utoaji wa elimu ya kinga kwenye vyombo vya usafiri. 

 viii.   Uhaba wa Wataalam katika Sekta ya Uchukuzi

Wataalam katika Sekta ndogo za usafiri wa anga, reli, hali ya hewa na usafiri majini wanatakiwa kupata elimu maalum kwenye maeneo yao ili kukidhi matakwa ya kitaalam kitaifa na kimataifa. Sekta hizi zinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa Wataalam wenye ujuzi na uzoefu. 

Mkakati: 

Wizara (Sekta ya Uchukuzi) kupitia Vyuo vyake vya Kisekta imeendelea kutoa mafunzo kwa Wataalam waliopo, kuajiri wapya na kuvijengea uwezo Vyuo hivyo. Lengo ni kuviwezesha kuzalisha rasilimali watu yenye elimu inayokidhi mahitaji ya maendeleo.

  1. Uvamizi,         uharibifu na    Wizi wa miundombinu ya Reli

Kumekuwepo na tatizo la uvamizi, uharibifu na hujuma kwa miundombinu ya reli, hususan reli zenyewe, mataruma, vifungio na madaraja kwenye baadhi ya maeneo ambako reli zinapita.

Mkakati: 

Wizara imeendelea kushirikiana na vyombo vya dola pamoja na jamii inayozunguka maeneo ya Reli ili kusimamia Sheria zilizopo kuhusu uharibifu huo pamoja na kutoa elimu na hamasa kwa jamii inayopakana na maeneo ya Reli kwa lengo la kuwaelewesha umuhimu wa kutunza na kuwafanya wananchi hao kuwa walinzi wa miundombinu hiyo

  • Mabadiliko ya Hali ya Hewa

Dunia nzima imekumbwa na tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa. Mabadiliko haya (Climate Change) yanasababisha Mifumo ya hali ya hewa kubadilika mara kwa mara na kusababisha uharibifu wa miundombinu kutokana na mafuriko. 

Mkakati: 

Wizara imeendelea kupanua Mtandao wa

Rada za Hali ya Hewa nchini. Lengo ni kufikia rada saba (7) ambazo zitatosha kuangaza nchi nzima. Wizara pia itaendelea kuongeza vifaa na kupanua mtandao wa vituo vya hali ya hewa nchini ili kuboresha utoaji wa huduma za utabiri na tahadhari juu ya matukio ya hali mbaya ya hewa kwa usahihi zaidi. Aidha, Wizara imeendelea kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kutumia huduma za hali ya hewa. 

xi.                 Upungufu wa Taa za Kuongozea Ndege

katika Viwanja vya Ndege

Viwanja vyenye taa za kuongozea ndege nchini nyakati za usiku ni vinne tu kati ya 58 vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA). Kutokuwa na taa hizo na miundombinu kwa ajili ya kuwezesha usafiri wa anga wakati wa usiku kunalazimisha makampuni ya ndege kupanga safari za ndege wakati wa mchana. Hii ni moja ya changamoto inayokabili usafiri wa anga nchini kwa sababu ndege hazitumiki kwa kiwango kinachotakiwa nyakati za usiku. 

Mkakati: 

Serikali imeendelea kuvifanyia maboresho Viwanja vya Ndege nchini ili kuwezesha ndege kuruka nyakati za usiku na pia kuboresha barabara za kurukia ndege kuweza kuhimili aina ya ndege zilizopo. 

D. MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA  SEKTA ZA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

  • Mheshimiwa Spika, Makadirio ya Bajeti ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa Sekta ya Ujenzi na Sekta ya Uchukuzi ni kama ifuatavyo:

D.1 SEKTA YA UJENZI

Makadirio ya Bajeti ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Sekta ya Ujenzi imetengewa Shilingi 44,293,050,000.00 ikiwa niBajeti ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 40,638,652,000.00 ni Bajeti ya Mishahara na Shilingi 3,654,398,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo. Aidha,  Bajeti ya Maendeleo kwa Sekta ya Ujenzi katika mwaka 2022/23 ni Shilingi 1,421,542,185,800.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,168,576,368,800.00 nifedha za ndani na Shilingi 252,965,817,000.00 ni za fedha za nje. Aidha, kati ya fedha za ndani Shilingi 599,756,467,800.00 ni fedha zilizotengwa kwa ajili ya bajeti ya Mfuko wa Barabara na fedha kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali ni Shilingi 568,819,901,000.00.

Mgawanyo wa fedha za maendeleo pamoja na miradi iliyotengewa fedha ni kama inavyooneshwa katika Kiambatisho Na.1. Maelezo kuhusu Miradi ya Maendeleo ni kama ifuatavyo:

MRADI WA KUJENGA UWEZO (INSTITUTIONAL

CAPACITY BUILDING)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 273.746 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya mradi huu kwa lengo la kujenga uwezo wa watumishi wa Sekta ya Ujenzi kwa kuwapatia mafunzo na vitendea kazi vya ofisi kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi.

MIRADI YA VIVUKO, UJENZI WA NYUMBA NA

MAJENGO YA SERIKALI

Ujenzi na Ukarabati  wa Vivuko na

Maegesho ya Vivuko

  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Ujenzi na Ukarabati  wa Vivuko na Maegesho ya Vivuko umetengewa jumla ya Shilingi milioni 13,123.08 katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili ya kazi zifuatazo:
  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 2,585.52 zimetengwa kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa Maegesho ya Vivuko. Kazi zitakazofanyika ni pamoja na upanuzi wa Jengo la Abiria katika kivuko cha Magogoni – Kigamboni kwa upande wa Kigamboni; ujenzi wa maegesho mapya ya vivuko vya Kayenze – Kanyinya, Muleba – Ikuza, Ijinga – Kahangala (Magu) na Bwiro – Bukondo (Ukerewe) pamoja na Kuboresha mfumo wa tiketi za kieletroniki kwenye vivuko vitano (5) (Magogoni – Kigamboni, Kigongo – Busisi, Kisorya – Rugezi, Pangani – Bweni na Ilagala – Kajeje).

Kazi nyingine ni ujenzi na ukarabati wa maegesho sita (6) ya Magogoni – Kigamboni, Kilambo – Namoto, Utete – Mkongo, Iramba – Majita, Nyakarilo – Kome na Kasharu – Buganguzi pamoja na ujenzi wa ofisi, majengo ya abiria na uzio kwenye vituo vitatu (3) vya vivuko ambavyo ni Kisorya – Rugezi, Nyakarilo – Kome na Bugolora – Ukara. Fedha hizi pia zitatumika kufanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya ujenzi wa maegesho ya vivuko.

  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Ujenzi wa Vivuko Vipya umetengewa Shilingi milioni 5,015.28 kwa ajili ya ujenzi wa vivuko vipya  vya Magogoni – Kigamboni,  Kisorya – Rugezi, Ijinga –

Kahangala, Bwiro – Bukondo,  Nyakarilo – Kome, Buyagu – Mbalika na Nyamisati – Mafia. Kazi nyingine ni ununuzi wa vifaa vya karakana za TEMESA pamoja na ufuatiliaji na tathmini ya miradi hiyo.

  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Ukarabati wa Vivuko umetengewa jumla ya Shilingi milioni 5,522.28 kwa ajili ya kukamilisha ukarabati wa kivuko MV Ujenzi; kuendelea na ukarabati wa Kivuko MV Musoma, MV Mara, MV TEMESA, MV Kome II, MV Misungwi, MV Nyerere, MV Kyanyabasa, MV Kitunda, MV Kazi, MV Magogoni, MV Tanga MV pamoja na ukarabati wa kivuko cha MV Kilombero II na kukihamishia Mlimba – Malinyi.  Kazi nyingine ni kufanya ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya ukarabati wa vivuko.

Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya

Serikali

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 jumla ya Shilingi milioni 59,817.37 zimetengwa kwa ajili ya mradi  wa Ujenzi na Ukarabati wa Nyumba na Majengo ya Serikali. Kazi zitakazotekelezwa ni kama ifuatavyo:
  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Viongozi wa Serikali umetengewa jumla ya Shilingi milioni 8,015.58 kwa ajili ya ujenzi wanyumba nyingine 20  za Viongozi Dodoma pamoja na kuendelea na ujenzi wa nyumba tano (5) za Majaji katika mikoa ya Kilimanjaro, Mtwara, Shinyanga, Kagera na Tabora.
  • Mheshimiwa Spika,  mradi  wa  Ujenzi wa jengo la ofisi ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (awamu II)  katika eneo la Mtumba jijini Dodoma umetengewa Shilingi milioni 11,043.69. Aidha,  mradi wa Ujenzi  wa nyumba nyingine 150 za

Watumishi wa Umma umetengewa  jumla ya Shilingi milioni 6,936.97 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba   hizo Jijini Dodoma.

  • Mheshimiwa Spika,  mradiwa Ujenzi wa jengo la makazi kwa ajili ya Watumishi wa Umma katika eneo la Temeke Kota umetengewa jumla ya Shilingi milioni 6,928.99.

Aidha,katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi wa Ujenzi wa jengo la makazi kwa ajili ya Watumishi wa Umma katika eneo la Magomeni Kota wilayani Kinondoni umetengewa Shilingi milioni 3,900.00.

  • Mheshimiwa Spika, mradi  wa  Ukarabati wa Nyumba na Ununuzi wa Samani kwa Ajili ya Ikulu Ndogo umetengewajumla ya Shilingi milioni 11,557.01. Kazi zitakazofanyika ni ukarabati wa nyumba 40 za viongozi Dodoma na nyumba 30 katika mikoa mingine pamoja na kufanyia matengenezo kinga ya nyumba za makazi za Magomeni Kota.  Kazi nyingine ni ukarabati wa nyumba 66 zilizokuwa zinamilikiwa na iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) zilizohamishiwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ukarabati wa nyumba zilizokuwa zinamilikiwa na TAMISEMI/NHC zilizohamishiwa  TBA katika mikoa 20 pamoja na ununuzi wa samani za Ikulu Ndogo.  
  • Mheshimiwa Spika,  katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi wa  Kujenga Uwezo wa Wabunifu Majengo, Wakadiriaji Majenzi na Huduma za Ushauri umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,579.19 kwa ajili ya kuwajengea uwezo Wabunifu Majengo (Architects) na Wakadiriaji Majenzi (Quantity Surveyors) kupitia Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB). Kazi nyingine ni Huduma za Ushauri, maandalizi ya Sheria ya

Majengo (Building Act), Taratibu za Ujenzi (building codes) na Viwango vya Msawazo

(Standards and Specifications) kwa ajili ya kazi na miradi ya ujenzi na ukarabati wa nyumba na majengo ya Serikali pamoja na ununuzi wa samani itakayoratibiwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC).

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi Ujenzi na Ukarabati wa Karakana za TEMESA na TBA umetengewajumla ya Shilingi milioni 8,453.16 kwa ajili ya ujenzi wa karakana  mpya ya kisasa jijini Dodoma; kuendelea kuanzisha karakana za wilaya sita (6) za Simanjiro, Masasi, Ukerewe, Chato, Mafia na Kyela; kuendelea na ujenzi wa karakana za  TEMESA katika Mikoa mipya ya Songwe, Simiyu, Geita, Njombe na Katavi; ukarabati wa karakana 12 za TEMESA mikoa ya Tabora, Mwanza, Arusha, Mtwara, Mbeya, M.T Depot – Dar es Salaam, Kigoma, Mara, Ruvuma, Pwani, Dodoma na Vingunguti pamoja na ukarabati wa karakana sita (6) za TBA katika mikoa ya Arusha, Mwanza, Morogoro Tabora, Dar es Salaam na Mbeya. 
  • Mheshimiwa Spika, mradi wa Kusanifu na kusimika Mfumo wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Matengenezo ya Magari, Umeme na Elektroniki umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,500.00 katika mwaka wa fedha

2022/23, kwa ajili ya utekelezaji wake.

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 899.76 zimetengwa kwa ajili ya Ufuatiliaji na tathmini kwenye miradi ya ujenzi na ukarabati wa Nyumba  na Majengo ya Serikali pamoja na wahitimu wa Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi.

MIRADI YA BARABARA NA MADARAJA

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23,  miradi ya barabara na madaraja itakayotekelezwa ni kama ifuatavyo:

Barabara ya Soni – Bumbuli – Dindira – Korogwe

(km 74)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni  1,000.00 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Mtwara – Newala – Masasi (km 210)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 11,010.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi wa barabara ya Mtwara – Newala – Masasi; sehemu ya Mtwara – Mnivata (km 50) na kuanza ujenzi wa sehemu ya Mnivata – Tandahimba – Newala – Masasi (km 160) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Likuyufusi – Mkenda (km 122.50) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 7,500.00 zimetengwa katika mwaka wa fedha 2022/23, kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Likuyufusi – Mkenda, sehemu ya Likuyufusi – Mhukuru (km 60) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Nachingwea – Liwale (km 130) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mhandisi Mshauri aliyefanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii.

Barabara ya Ubena Zomozi – Ngerengere (km

11.6) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 3,253.241 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za Ubena Zomozi – Ngerengere Jeshini – Ngerengere SGR Station kwa kiwango cha lami.

Barabara ya TAMCO – Vikawe – Mapinga (km

24)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 3,820.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Makofia – Mlandizi (km 36.7) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, barabara ya Makofia – Mlandizi imetengewa jumla ya Shilingi milioni 600.00 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Musoma – Makojo – Busekela (km

92) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, barabara hii imetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,950.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kongwa Jct – Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe (km 98)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, barabara hii imetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,088.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kongwa Jct – Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe (km 98.00) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Muhutwe – Kamachumu – Muleba 

(km 54) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,200.00 zimetengwakwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Muhutwe – Kamachumu – Muleba (km 54) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Iringa – Ruaha National Park (km

104) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, barabara hii imetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,000.00 kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Iringa – Ruaha National Park (km 104) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Muheza – Amani (km 36) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 1,700.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Muheza – Amani (km 36) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Mtwara – Mingoyo – Masasi (km

200) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 550.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ukarabati wa barabara ya Mtwara – Mingoyo – Masasi (km 200) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kibaoni – Majimoto – Muze – Kilyamatundu (km 189) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 7,160.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Ntendo – Muze – Kilyamatundu; sehemu ya Ntendo – Muze (km 37) na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Kibaoni – Majimoto – Inyonga (km 152) kwa kiwango cha lami.

Daraja la Kigongo – Busisi (J.P. Magufuli) na

Barabara Unganishi 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 7,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa daraja hili na barabara unganishi. 

Daraja la Mzinga 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa daraja hili katika Barabara ya Mbagala Rangi Tatu – Kongowe Jijini Dar es Salaam.

Daraja la Ugalla 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa daraja hili lililopo katika mkoa wa Katavi.

Daraja la Kitengule na Barabara Unganishi 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 1,300.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa Daraja la Kitengule pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa kilometa 18.

Barabara ya Morogoro – Dodoma (km 260) pamoja na Daraja la Mkundi 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Morogoro – Dodoma (km 260) pamoja na Daraja la Mkundi ili kuikarabati kwa kiwango cha lami.

Daraja Jipya la Wami  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa daraja hili lililopo katika barabara ya Chalinze – Segera.

Barabara ya Njombe – Makete – Isyonje (km

157.4)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,364.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara ya Njombe – Makete – Isyonje, Sehemu za Njombe – Moronga (km 53.90) na Moronga – Makete (km 53.50). Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa barabara za Isyonje – Makete; Sehemu ya Ipelele – Iheme (km 50.00) na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Njombe – Njombe Referral Hospital (km 3) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Omugakorongo – Kigarama – Murongo (km 105)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Nanganga – Ruangwa – Nachingwea

(km 145)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 7,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Masasi – Nachingwea (km 45) na kuendelea na ujenzi wa barabara ya Nanganga – Ruangwa – Nachingwea (km 100); Sehemu ya Nanganga – Ruangwa (km 53.20) kwa kiwango cha lami na kuanza ujenzi wa barabara ya Nangurukuru – Liwale (km 50).

Barabara ya Mpemba – Isongole  (km 51.2)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 10.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi wa barabara ya Mpemba – Isongole (km 51.2). 

Barabara         Ruanda – Iyula – Nyimbili (km 21)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Ruanda – Iyula – Nyimbili (km 21.00) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Katumbasongwe – Kasumulu –

Ngana – Ileje (km 90.10)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 5,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Katumbasongwe – Kasumulu – Ngana – Ileje (km 90.10) kwa kiwango cha lami.

Barabara   ya     Uyogo       –       Nyamilangano   – Nyandekwa – Kahama (km 54)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Uyogo – Nyamilangano – Nyandekwa – Kahama (km 54.0) kwa kiwango cha lami.

 Barabara ya Sengerema – Nyahunge (km 54)

  • Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Sengerema – Nyahunge (km 54.0) kwa kiwango cha lami.

Barabara       Omurushaka – Nkwenda – Murongo

(km 112)

  • Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 6,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Omurushaka – Nkwenda – Murongo (km 112) kwa kiwango cha lami.

Upanuzi wa Barabara Kuu Zinazoingia Katikati ya Jiji la Dodoma (Widening up of Dodoma

Outer Roads Sections km 220)

  • Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya upanuzi wa barabara kuu zinazoingia katikati ya Jiji la Dodoma (km 220) zinazohusisha barabara ya

Dodoma – Morogoro (km 70), Dodoma – Iringa (km 50), Dodoma – Singida (km 50) na Dodoma – Arusha (km 50).

Barabara ya Ntyuka Jct – Mvumi Hospital – Kikombo Jct. (km 76.07)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 4,600.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Ntyuka Jct – Mvumi Hospital – Kikombo Jct (km 76.07) kwa kiwango cha lami.

Barabara      Tarime – Mugumu (km 86)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Tarime – Mugumu (km 86.0) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Shelui – Nzega (km 110)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati kwa kiwango cha lami wa barabara ya Shelui – Nzega (km 110.

Barabara ya Nzega – Kagongwa (km 65)

  • Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Nzega – Kagongwa (km 65) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Isabdula (Magu) – Bukwimba

Station – Ngudu – Ng’hungumalwa (km 50)

  • Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Isabdula (Magu) –

Bukwimba Station – Ngudu – Ng’hungumalwa (km 50) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Mafinga – Mgololo (km 78)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 4,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Mafinga – Mgololo (km 78) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Nyololo – Mtwango (km 40.4)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 500.00 zimetengwa kwa ajili maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Nyololo – Mtwango (km 40.4) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kongwa – Kibaya – Arusha (km

430)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 2,500.00 zimetengwa kwa ajili maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Kongwa – Kibaya – Arusha (km 430) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Singida – Sepuka –  Ndago (km 75)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni

5,200.00 zimetengwa kwa ajili maandalizi ya kuanza ujenzi wa barabara ya Singida – Sepuka – Ndago (km 75.0) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kitai – Lituhi pamoja na Daraja la

Mnywamaji (km 90)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kitai – Lituhi (km 90.0) pamoja na daraja la Mnywamaji.

Barabara za Kuelekea Katika Vituo vya Reli ya

Kisasa ya SGR  (km 87.6)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 15,806.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za kuelekea katika vituo vya reli ya kisasa (SGR) ambazo ni Morogoro – Kihonda SGR Station (km 10), Rudewa – Kilosa SGR Station (km 3), Gulwe – Gulwe SGR Station (km 2), Igandu – Igandu SGR Station (km 27), Ihumwa – Ihumwa Marshalling Yard (km 5.50), Kizota – Zuzu SGR Station (km 2), Bahi – Bahi SGR Station (km 4), Mlandizi – Ruvu SGR Station (km 22) na barabara za ndani za kituo cha SGR cha Dodoma (Access Roads to Dodoma SGR Station).

Barabara ya Tanga – Pangani – Makurunge (km

174.5)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Shilingi milioni 5,000.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 25,054.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga – Pangani (km 50). Kazi nyingine ni kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Pangani – Mkange (km 124.5) na Daraja la Pangani.

Barabara ya Kisarawe – Maneromango – Mloka

(km 54)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 2,780.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Geita – Bulyanhulu – Kahama (km

120)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Geita – Bulyanhulu Jct (km 58.3) na Bulyanhulu Jct – Kahama (km 61.7).

Barabara ya Nyamirembe Port – Katoke (km 50)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 2,300.00 zimetengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Nyamirembe Port – Katoke (km 50), Chato Ginery – Bwina (km 8.10) na SIDO – Chato Zonal Hospital (km 5.30).

Barabara ya Geita – Nzera – Nkome (km 54) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Geita – Nzera – Nkome (km 54) sehemu ya Nzera – Nkome (km 20).

Barabara ya Arusha – Moshi – Himo – Holili (km

199.51) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 8,460.00 zinazojumuisha Shilingi milioni 4,460.00  za ndani na Shilingi milioni 4,000 za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Sakina – Tengeru na barabara ya mchepuo ya Arusha (Arusha Bypass). Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa barabara za Kijenge – Usa River (km 20), Mianzini – Ngaramtoni (km 18) na maandalizi ya upanuzi wa sehemu ya Tengeru – Moshi – Himo (km 105) pamoja na Mizani ya Himo.

Barabara za Kuelekea Kwenye Mradi wa Kufua Umeme Katika Maporomoko ya Mto Rufiji

(Access Roads To Rufiji Hydropower Project) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 9,800.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Bigwa – Matombo – Mvuha (km 78) pamoja na ukarabati kwa kiwango cha changarawe wa barabara za  Maneromango – Vikumburu – Mloka (km 100) na Kibiti – Mloka – Mtemele – Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere. Aidha, mradi huu utahusisha kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Ubena Zomozi – Mvuha – Kisaki – Mtemele Jct (km 178) sehemu ya Ngerengere – Mvuha – Kisaki – Mtemele Jct (km 166.4) ikiwa ni mandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro (km 152.3)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,730.00 kwa ajili ya kuendelea na ukarabati (overlay) wa barabara ya Mlandizi – Chalinze (km 44.24) na ujenzi wa barabara ya Kwa Mathiasi (Morogoro Road) – Msangani (km 8.3). Kazi nyingine ni kulipa madeni ya Mkandarasi aliyefanya kazi ya kuboresha maeneo hatarishi (Assorted Accident Blackspot) ya barabara ya Dar es Salaam – Morogoro na ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi (One Stop Inspection Station – OSIS) cha

Vigwaza.    Aidha,        mradi         huu unahusisha maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro kwa kiwango cha Expressway.

Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo – Msata (km

54.1)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,700.00 kwa ajili ya kuanza ukarabati na upanuzi wa barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo – Msata (Sehemu ya Tegeta –

Bagamoyo: km 46.9) na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Mbegani – Bagamoyo (km 7.2).

Barabara ya Usagara – Geita – Buzirayombo –

Kyamyorwa (km 110) 

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 10.00 katika mwaka wa fedha 2022/23, kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Makandarasi kwa sehemu za Uyovu – Bwanga (km 43) na Bwanga – Biharamulo (km 67).

Barabara ya Nyakahura – Kumubuga – Rulenge –

Kabanga Nickel Road (km 141) 

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 3,000.00 kwa ajili maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Nyakahura – Kumubuga – Murusagamba (km 34), Kumubuga – Rulenge – Murugarama (km 75) na Rulenge – Kabanga

Nickel (km 32).

Barabara ya Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 265.1)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 940.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 17,515.00 fedha za nje kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi waliojenga barabara za Ndono – Urambo (km 52), Tabora – Ndono (km 42), Kaliua – Kazilambwa (km 56) na Urambo – Kaliua (km 28). Aidha, kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Uvinza – Malagarasi (km 51.1) na Kazilambwa – Chagu (km 36) pamoja na maandalizi ya  ujenzi kwa kiwango cha lami wa Urambo Roundabout.

Barabara ya Ifakara – Kihansi – Mlimba – Madeke – Kibena (Njombe)  (km 270)

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 8,555.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,650.00 fedha za nje kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa sehemu ya Kihansi – Mlimba – Taweta – Madeke – Kibena

(km 220) kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Aidha, mradi huu utahusisha pia kuanza ujenzi wa barabara za Ifakara – Kihansi (km 50).

Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti

River – Lalago – Maswa (km 389)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (km 389.0): sehemu ya Mbulu – Haydom yenye urefu wa kilometa 50. 

Barabara ya Marangu – Tarakea – Rongai –

Kamwanga /Bomang’ombe – Sanya Juu (km

84.80)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 5,830.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara za Marangu – Rombo Mkuu – Tarakea (km 64.0), Sanya Juu – Kamwanga (sehemu ya Sanya Juu – Elerai, km 32) na KIA – Mererani (km 26.0). Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa barabara za Kwa Sadala – Masama – Machame Junction (km 16) na

Kiboroloni – Kikarara – Tsuduni – Kidia (km 10.8). Mradi huu utahusisha pia  ukarabati wa barabara ya Bomang’ombe – Sanya Juu (25 km), ujenzi wa barabara ya Tarakea – Holili (km 53.0) na barabara ya Sanya Juu – Kamwanga (sehemu ya Elerai – Kamwanga -km 44).

Barabara ya Tukuyu – Mbambo – Katumba (km

60.6)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,700.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu za Bujesi – Mbambo (km 26) na Tukuyu – Mbambo (km 36.60). Kazi nyingine ni kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mbambo – Ipinda (km 19.7). 

Barabara ya Dodoma – Manyoni (km 127) na

Barabara Kuingia Manyoni Mjini (km 4.8)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 55.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi (One Stop Inspection Station – OSIS) cha Muhalala (Manyoni).

Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene – Itobo

(km 114)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 500.00 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Tabora – Mambali – Bukene (km 114).

Barabara ya Namanyere – Katongoro – New

Kipili Port (km 64.80)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 385.00 kwa ajili ya kuendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii.

Barabara ya Dumila – Kilosa – Mikumi (km 141)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,310.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Mhandisi Mshauri wa sehemu ya Dumila – Rudewa (km 45) na kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Rudewa – Kilosa (km 24). Kazi nyingine ni maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Kilosa – Ulaya – Mikumi (km 72) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga

Port (km 107) 

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewajumla ya Shilingi milioni 8,010.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port (km 107) na kuanza ujenzi wa barabara ya Matai – Kasesya (km 50).

Ujenzi wa Madaraja Makubwa  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni

13,010.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa Madaraja ya Magufuli (Morogoro), Ruhuhu (Ruvuma), Momba (Rukwa), Mara (Mara), Magara (Manyara), Lukuledi (Lindi), Msingi (Singida) na Kiyegeya (Morogoro). Kazi nyingine ni kuanza ukarabati wa daraja la Kirumi (Mara), ujenzi wa barabara unganishi za Daraja la Sibiti (Singida) na ujenzi wa Daraja la Sukuma (Mwanza). Aidha, fedha hizi zitatumika kuanza Usanifu na Ujenzi wa Daraja la Mirumba (Katavi), ujenzi wa Madaraja ya Simiyu (Mwanza), Sanza (Singida), Mkenda (Ruvuma) na Mpiji Chini (Dar es Salaam). Vilevile mradi huu utahusisha kuanza maandalizi ya ujenzi wa Madaraja ya Mtera (Dodoma), Godegode (Dodoma), Mitomoni (Ruvuma) na madaraja ya Nzali, Kibakwe, Mpwapwa, Kerema na Munguli yaliyopo mkoani Dodoma). Miradi mingine ni kuanza upembuzi yakinifu na Usanifu wa Kina wa Daraja la Malagarasi Chini (Kigoma) pamoja na kununua madaraja ya dharura (Emergency Mabey Parts). 

Barabara ya New Bagamoyo (Kawawa Jct – Tegeta (km 17.2) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 10.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa Barabara ya Morocco – Mwenge (km

4.3).

Barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo (km

183.1)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 6,010.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi wa sehemu ya Kyaka – Bugene (km 59.1) na kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kumunazi – Kasulo – Bugene (km 133) sehemu ya Bugene – Chato

Burigi National Park (km 60).

Barabara ya Isaka – Lusahunga (km 242.20)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,065.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 15,199.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Mhandisi Mshauri wa sehemu ya Ushirombo – Lusahunga (km 110). Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi – OSIS cha Nyakanazi, kuanza ukarabati wa sehemu ya Lusahunga – Rusumo (km 92). Mradi huu utahusisha pia maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Nyakasanza – Kobero kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora (km

259.75)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 30.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,000.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa sehemu za Manyoni – Itigi – Chaya (km 89.35), Nyahua – Chaya (km 85.4) na Tabora – Nyahua (km 85). 

Barabara za Mikoa (km 734.59)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, jumla ya Shilingi milioni 61,585.00 zimetengwa kwa ajili ya barabara za mikoa na madaraja katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ukarabati wa jumla ya kilometa 672.77 kwa kiwango cha changarawe, kujenga kilometa 61.82 kwa kiwango cha lami na ujenzi wa Madaraja /Makalavati 31. Orodha ya miradi ya barabara za Mikoa itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za Bajeti ya Maendeleo kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali imeoneshwa katika Kiambatisho Na.

2. 

Barabara ya Mwanza/Shinyanga Border – Mwanza (km 102)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 385.00           zimetengwa           kwa   ajili   ya kuendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kuifanyia ukarabati barabara hii.

Mradi wa Kuondoa Msongamano Barabara za

Dar es Salaam (km    138.5)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 5,105.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi wa barabara za Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana (km 14), Mbezi Mwisho – Goba (km 7), Tangi Bovu – Goba (km 9), Kimara Baruti –

Msewe – Changanyikeni (km 2.6), Banana – Kitunda – Kivule – Msongola (km 14.7): Sehemu ya Kitunda – Kivule (km 3.2), Ardhi – Makongo – Goba; Sehemu ya Goba – Makongo (km 4), Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road (Mbezi Mwisho); sehemu ya Madale – Goba (km 5) na Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road (Mbezi Mwisho); sehemu ya Wazo Hill – Madale (km 6). 

Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa barabara ya Ardhi – Makongo – Goba; sehemu ya Ardhi – Makongo (km 5.0) na kuanza ujenzi wa barabara za Kibamba – Kisopwa – Kwembe – Makondeko (km 14.66), sehemu ya Mloganzila – Mloganzila Citizen (km 4.0), Kongowe – Mjimwema – Kivukoni Ferry Road (One Lane Widening: km 25.1), Mji Mwema – Kimbiji – Pembamnazi (km 27.0) na Goba – Matosa – Temboni (km 6.0) pamoja na kuanza upanuzi wa barabara ya Mwai Kibaki (km 9.1).

Barabara ya Nyamuswa – Bunda – Kisorya (km

107.4) 

363. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, jumla ya Shilingi milioni 2,010.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa sehemu ya Kisorya – Bulamba (km 51.0) na kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba (km

56.4).

Barabara ya Kolandoto – Lalago – Ng’oboko –

Mwanhuzi (km 122)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara za Kolandoto – Lalago (km 62) na Lalago – Ng’oboko – Mwanhuzi (km 60).

Barabara ya Ndundu – Somanga (km 60)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, jumla ya Shilingi milioni  2,100.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Ndundu – Somanga (km 60) na kuanza maandalizi ya ukarabati wa barabara za Kongowe – Malendego (km 160.65) na Nangurukuru – Mbwemkuru (km 95).

Barabara ya Kasulu – Manyovu (km 68)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 600.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 11,400.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kasulu – Manyovu pamoja na barabara za kuingia Kasulu mjini (km 68).

Barabara     ya    Dodoma    City    Outer    Dual

Carriageway Ring Road Lot1 & 2 (km 112.3)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa  jumla ya Shilingi milioni 4,900.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 31,900.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Barabara ya Mzunguko wa Nje katika Jiji Dodoma (Dodoma City Outer Dual Carriageway Ring Road) sehemu ya Nala – Veyula – Mtumba – Ihumwa Dry Port (km 52.3), sehemu ya Ihumwa Dry Port – Matumbulu – Nala (km 60) na fidia kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Mzunguko wa Ndani katika Jiji la Dodoma (Dodoma Inner Ring Road) kwa sehemu ya Bahi R/About – Image R/About – Ntyuka R/About – Makulu R/About (km 6.3). Kazi nyingine ni kuendelea na maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mzunguko wa Kati katika Jiji la Dodoma (Dodoma City Middle Ring Road) inayoanzia Nanenane – Miyuji – Mnadani Sekondari – Mkonze – Ntyuka – Nanenane (km 47.2) na  kuanza ujenzi wa barabara ya Kikombo Jct – Chololo – Mapinduzi (JWTZ HQ) (km 18).

Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi

– Londo – Lumecha/ Songea (km 499)  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/22, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 4,600.00 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Kidatu – Ifakara (km 66.9) na kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara za Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha (km 396) na Chalinze – Magindu – Lukenge – Seregete B – Kabwe Jct – Mkulazi (km 77.50). Mradi huu utahusisha pia ukarabati kwa kiwango cha changarawe wa barabara ya Dakawa Jct – Mbigiri (km 7) na barabara zenye jumla ya kilometa 50 kuelekea mashamba ya wakulima wa miwa ya Mbigiri.

Barabara ya Tabora – Ipole – Koga – Mpanda

(km 365.36) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 40.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 5,870.00 fedha za nje kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa sehemu za Usesula – Komanga (km 115.5), Komanga – Kasinde (km 112.8), Kasinde – Mpanda (km 111.7) na Tabora – Sikonge (km 30).

Barabara      ya      Makutano      –      Natta      –

Mugumu/Loliondo – Mto  wa Mbu (km 235)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,520.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara za Makutano – Sanzate (km 50) na Waso – Sale Jct (km 49), kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Sanzate – Natta (km 40.0) na maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Natta – Mugumu (km 35).

Barabara ya Ibanda – Itungi Port (km 26)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 5,700.00 kwa ajili ya kuanza ukarabati wa barabara za Ibanda – Itungi (km 26) na maandalizi ya ujenzi wa sehemu ya Iponjola – Kiwira Port (km 6). Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi mpakani Kasumulu/Songwe

(Kasumulu/Songwe – Tanzania/Malawi Border – OSBP), pamoja na kulipa madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa barabara ya Kikusya – Ipinda – Matema Beach (km 39.1) na barabara ya Uyole – Kasumulu (sehemu ya Ilima Escarpment, km 3).

Barabara ya Nzega – Tabora (km 289.7)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 20.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa sehemu za

Nzega – Puge (km 58.6) na Puge – Tabora (km

56.1).

Barabara     ya    Sumbawanga    –    Mpanda    –

Nyakanazi (km 803.6)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa         jumla         ya Shilingi    milioni 19,600.00 kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa sehemu za Sumbawanga – Kanazi (km 75), Kanazi – Kizi – Kibaoni (km 76.60), Sitalike – Mpanda (km 36) na Mpanda – Ifukutwa – Vikonge (km 37.65). Kazi nyingine ni kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara za Mpanda – Mishamo – Uvinza; Sehemu ya Vikonge – Uvinza (km 159), Kibaoni – Sitalike (km 71) na Kagwira – Ikola – Karema Port (km 112). Mradi huu utahusisha pia maandalizi ya ujenzi wa barabara ya  Kizi – Lyambalyamfipa – Sitalike (km 86.31). na Lyazumbi – Kabwe (km 65).

Barabara ya Nyanguge – Musoma/ Usagara – Kisesa Bypass (km 214.25) 

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 530.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Makandarasi wa barabara za Simiyu/Mara Border – Musoma (km 85.5) na Usagara – Kisesa (Mwanza Bypass km 17.35). Kazi nyingine ni kuanza maandalizi ya ukarabati wa sehemu ya Nyanguge – Simiyu/Mara Border (km 100.4) na kulipa madeni ya Mkandarasi wa mradi wa upanuzi wa barabara ya kuelekea Uwanja wa Ndege wa Mwanza na Daraja la Furahisha.

Barabara ya Magole – Mziha – Handeni (km

149.2)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,010.00 kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Mkandarasi wa barabara ya Magole – Turiani (km 45.2) na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Turiani – Mziha – Handeni (km 104). 

Ujenzi wa Barabara za Juu (Flyovers) Jijini

DSM na Barabara Unganishi  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 570.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,000.00 fedha za nje kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya Ubungo (Ubungo        Interchange) pamoja       na     kuanza maandalizi ya kuboresha makutano ya barabara katika maeneo ya KAMATA, Magomeni, Mwenge, Tabata/Mandela, Morocco, Buguruni, Mbezi Mwisho, Fire pamoja na makutano ya barabara za Kinondoni/Ali Hassan Mwinyi na Selander (Ali Hassan Mwinyi/UN Road Jct). Aidha, kazi nyingine ni kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa Mabey Flyovers katika jiji la Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza.

Barabara ya Mwigumbi – Maswa – Bariadi – Lamadi (km 121) 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,220.00 kwa ajili ya kulipa madai ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara za Mwigumbi – Maswa (km 50.3) na Maswa – Bariadi (km 49.7). Aidha, kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mchepuo wa Maswa (Maswa Bypass; km 11). 

Barabara ya Tabora – Ipole – Rungwa (Sehemu

ya Ipole – Rungwa (km 172) 

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 650.00 katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi (km 341.25) 

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa         jumla         ya Shilingi    milioni 13,020.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 44,328.00 fedha za nje kwa ajili ya kulipa madai ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara za Kidahwe – Kasulu (km 63.0) na Nyakanazi – Kakonko (km 50). Kazi nyingine ni kuendelea na ujenzi wa barabara za Kanyani Junction – Mvugwe (km 70.5), Mvugwe – Nduta

Junction (59.35), Nduta Junction – Kibondo Junction – Kabingo (62.5), na Nduta Junction – Kibondo (25.9). Aidha, kazi nyingine ni kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibondo – Mabamba (km 48).

Barabara ya Kwenda Kiwanja cha Ndege cha

Mafia (Mafia Airport Access Road (km 16)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu

umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,010.00 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ya Kilindoni – Ras Mkumbi (km 54.4) pamoja na kulipa madai ya Mkandarasi na Mhandisi

Mshauri wa ujenzi wa barabara hii.

Daraja la Kigamboni (Nyerere) na Barabara

Unganishi 

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 6,910.00 kwa ajili ya mchango wa Serikali kwenye ujenzi wa Daraja la Nyerere, kulipa madai ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa barabara za Daraja la Nyerere – Vijibweni na Tungi – Kibada (km 3.8). Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa barabara ya Kibada – Mwasonga – Tundwisongani Jct/Tundwisongani – Kimbiji (km

41).

Barabara ya Mutukula – Bukoba – Muhutwe – Kagoma (km 215.8)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 600.00 kwa ajili ya kuendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara za Bukoba Mjini – Busimbe – Maruku – Kanyangereko – Ngongo (km

19.10) na Kanazi (Kyetema) – Ibwera – Katoro – Kyaka II (km 60.70). Kazi nyingine ni kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara  ya Mutukula – Bukoba – Muhutwe – Kagoma (km 136.00).

Fedha za Matengenezo na Ukarabati wa

Barabara  

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 599,756.4678 kwa ajili ya matengenezo       na     ukarabati   wa     barabara, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, udhibiti wa uzito wa magari, usalama barabarani na mazingira, matengenezo na ukarabati wa Vivuko pamoja na kujenga uwezo wa Wizara na Taasisi zinazosimamia masuala ya Barabara na Vivuko. Fedha hizi zinasimamiwa na Bodi ya Mfuko wa Barabara.

Ujenzi wa Njia za Magari Mazito na Maegesho ya Dharura Katika Barabara Kuu ya Ukanda wa Kati (Providing Lane Enhancement Including Climbing Lanes, Passing Bays, Rest and

Emergency Lay Bays on Central Corridor)  

  • Mheshimiwa     Spika,      mradi         huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 300.00 kwa ajili ya maandalizi ya kuanza kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa maeneo ya kujenga njia za magari mazito kwenye miinuko na kujenga maegesho ya dharura katika Barabara Kuu ya Ukanda wa Kati. Aidha, mradi huu utajumuishwa kwenye Usanifu wa Kina kabla ya kufanya ukarabati wa barabara za Ukanda wa Kati zilizopangwa kufanyiwa Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina ambazo ni Morogoro – Dodoma (km 260.00), Singida – Shelui (km 110.00) na Shelui – Nzega (km 110.00) ambazo zimepangwa kufanyiwa usanifu wa kina.

Upanuzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (km

25.7) Ikijumuisha Upanuzi wa Madaraja ya

Kibamba, Kiluvya na Mpiji  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 2,000.00 kwa ajili ya kukamilisha upanuzi wa barabara ya Kimara – Kibaha (km 25.7); sehemu ya Kimara – Kibaha Mizani (km 19.2) na madaraja ya

Kibamba, Kiluvya na Mpiji.  

Barabara ya Kisarawe – Mlandizi (km 119) 

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 770.00 kwa ajili ya maandalizi ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

a Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju (km 34) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 400.00 zimetengwa Katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa sehemu za Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho (km 12.7) na Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju (km 21.3).

Barabara ya Kagoma – Lusahunga (km 172.50)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 10.00 kimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri wa barabara ya Muleba – Kanyambogo – Rubya (km

18.5).

Barabara ya  Singida – Shelui (km 110) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kufanya ukarabati kwa kiwango cha lami wa barabara ya Singida – Shelui (km 110) na kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Ulemo – Kinampanda – Gumanga (Singida) – Mkalama (km

46).

  1. Dar es Salaam – Mbagala (Kilwa Road) – Gerezani (sehemu ya Kamata – Bendera

Tatu: km 1.3) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 555.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 1,655.00 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa daraja la Gerezani na maandalizi ya upanuzi wa sehemu ya Mbagala Rangi Tatu – Kongowe (km 3.8).

Barabara ya Msimba – Ruaha Mbuyuni/Ikokoto

Mafinga (km 365.90)   

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 540.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ukarabati wa sehemu za Mafinga – Nyigo (km 74.1) na Nyigo – Igawa (km 63.8). Kazi nyingine ni kuendelea na maandalizi ya  ujenzi wa barabara ya Rujewa – Madibira – Mafinga (km 152) na kuendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Morogoro – Iringa sehemu ya Tumbaku Jct – Mangae/Melela – Mikumi – Iyovi (km 158.45) ikiwa ni pamoja na  daraja la Doma.
  1. Same – Mkumbara – Korogwe (km

239.5)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 8,900.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ukarabati wa sehemu za Same – Himo (km 76) na Mombo – Lushoto (km 32). Aidha, kazi nyingine ni kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara za Lushoto – Magamba – Mlola (km 34.5) na na kuendelea na ujenzi wa barabara ya Same – Kisiwani – Mkomazi (km 97).

Barabara ya Mbeya – Makongolosi – Mkiwa (km

579.9) 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 11,480.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa sehemu za Mbeya – Lwanjilo (km 36)  na Lwanjilo – Chunya (km 36). Kazi nyingine ni kukamilisha ujenzi wa sehemu ya Chunya – Makongolosi (km 39); kuendelea na ujenzi wa barabara za Itigi Mjini (km 10) na kuanza ujenzi wa sehemu za Noranga – Itigi – Mkiwa (km 56.90) pamoja na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Mbalizi – Makongolosi (km 50), Makongolosi – Rungwa – Noranga; sehemu ya Makongolosi – Rungwa (km 50).
  1. Itoni – Ludewa – Manda (km 211)  
  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 10,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa barabara ya Lusitu – Mawengi (km 50) kwa kiwango cha zege na kuanza ujenzi kwa kiwango cha zege wa sehemu ya Itoni – Lusitu (km 50).

Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander  (Tanzanite)

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 10.00 zimetengwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Daraja Jipya la Selander (km 1.03) na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa kilometa 5.2.

Barabara ya  Handeni – Kibirashi – Kijungu –

Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini – Dalai –

Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 460)   

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 8,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrojo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 460) kwa kuanzia na sehemu ya Handeni – Kibirashi (km

50).

  1. Makambako – Songea na Barabara ya Mchepuo ya Songea (Songea Bypass) (km

295)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ukarabati wa barabara ya Makambako – Songea pamoja na ujenzi wa barabara ya Mchepuo wa Songea (Songea Bypass). 

Barabara ya Dodoma – Iringa (km 267.1)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 910.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya mchepuo ya Iringa (Iringa Bypass km 7.3), kuimarisha matabaka ya barabara ya Iringa – Dodoma na kulipa madeni ya Mkandarasi wa ujenzi wa Mizani kwenye barabara ya Iringa – Dodoma. 

Barabara ya Dodoma – Babati (km 263.4)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 2,300.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa sehemu za Dodoma – Mayamaya (km 43.65), Mayamaya – Mela (km 99.35), Mela – Bonga (km 88.80) na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya mchepuo wa Babati (Babati Bypass km 15.50) pamoja na Miteremko ya Magara (Magara Escarpment) (km 3). Mradi

huu utahusisha pia ujenzi wa barabara ya Dareda – Dongobesh (km 60) kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Masasi – Songea – Mbamba Bay

(km 343.2)  

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 40.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 3,000.00 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya Makandarasi na Wahandisi Washauri wa ujenzi wa sehemu za Tunduru – Matemanga (km 59), Matemanga – Kilimasera (km 68.2), Kilimasera – Namtumbo (km 60) na Mbinga – Mbamba Bay

(km 66).

Ujenzi wa Barabara za Chuo cha Uongozi

(Uongozi Institute)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 200.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara za ndani ya eneo la Chuo cha Uongozi Bagamoyo.

Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma na

Mbeya Bypass (km 266.9)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 9,500.00 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ukarabati wa barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (km 218) sehemu ya Uyole –  Ifisi (km 29)  na kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Mbeya (Uyole – Songwe: km 48.9). Aidha, mradi huu utahusisha maandalizi ya ujenzi wa barabara ya mchepuo ya Iwambi – Mbalizi (km 6.5) kwa kiwango cha lami.

Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka

(BRT Phase I – V: km 69.8)  

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,065.00 fedha za ndani na Shilingi milioni 48,247.497 fedha za nje zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Pili. Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tatu na Nne na kuendelea na maandalizi ya maboresho ya miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka iliyojengwa katika Awamu ya Kwanza katika eneo la Jangwani. Aidha, mradi huu utahusisha kufanya maandalizi ya ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tano.

Ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (Institute of Construction

Technology – ICoT)   

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,500.00 zimetengwa kwa ajili ya usanifu na ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (Institute of Construction Technology – ICoT) mkoani Morogoro na majengo ya ICoT tawi la Mbeya.

Ujenzi wa Makao Makuu ya Wakala wa Barabara

Tanzania 

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi milioni 1,900.00 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Wakala ya Barabara (TANROADS) pamoja na Ofisi za Mikoa ya Dar es Salaam, Katavi, Geita, Simiyu, Njombe, Lindi na Songwe.

MIRADI      YA    USALAMA    BARABARANI    NA

MAZINGIRA

  • Mheshimiwa   Spika,      Wizara inaratibu shughuli za usalama barabarani, mazingira na kudhibiti uzito wa magari yanayotumia barabara zetu. Katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi wa Usalama Barabarani umetengewa jumla ya Shilingi milioni 1,648.800 kwa ajili ya  Ujenzi wa Vituo vya Ukaguzi wa Pamoja (One Stop Inspection Stations); Uwekaji wa vifaa vya kisasa vya upimaji uzito wa magari (Digital Load Cells) na  Kufanya maboresho ya mfumo wa kukusanya taarifa za ajali barabarani.

Kazi nyingine ni Kufunga Mfumo wa Ufuatiliaji wa Utendaji kazi katika vituo vya mizani; Kutoa mafunzo ya kudhibiti uzito wa magari kwa Wahandisi na Mafundi Sanifu; kufanya utafiti wa uharibifu wa barabara unaotokana na kuzidisha uzito wa magari; kuboresha baadhi ya sehemu za kuvuka barabara kwa kuziwekea rada za kuwasaidia waenda kwa miguu kuvuka barabara kwa usalama pamoja na Mapitio ya Sera  ya Usalama Barabarani.

  • Mheshimiwa Spika, mradi wa  Kujenga Uwezo wa Taasisi Katika Masuala ya Usalama Barabarani na Mazingira umetengewa Shilingi milioni 16.048 ajili ya kufanya tathmini ya usalama barabarani ili kubaini athari za kijamii na kiuchumi pamoja na kufanya mapitio ya miongozo ya usalama barabarani.
  • Mheshimiwa Spika,  mradi wa Menejimenti ya Usimamizi wa Mazingira umetengewa Shilingi milioni 119.400 zimetengwa kwa ajili ya  kuandaa mkakati wa kukabili majanga kwa Sekta ya Ujenzi (Works Sector Disaster Management Strategy), kuanzisha mfumo wa kusimamia na kukusanya taarifa za mazingira (Environmental Information Management System), kufanya mapitio ya miongozo ya tathmini na usimamizi wa mazingira ya Sekta ya Ujenzi na kuandaa mpango tekelezi wa mazingira kisekta wa miaka mitano (Sector Environmental Action Plan, 2022-2027).

MIRADI YA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA

VIWANJA VYA NDEGE

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 miradi ya ujenzi wa miundombinu ya viwanja vya ndege imetengewa jumla ya Shilingi milioni 86,102.522. Kiasi hicho kinajumuisha Shilingi milioni 54,955.206 fedha za ndani na Shilingi milioni 31,147.316 fedha za nje. Miradi ifuatayo imepangwa kutekelezwa:

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kigoma

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 7,630.90. Kati ya fedha hizo, Shilingi milioni 4,598.00 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 3,032.90 ni fedha za nje. Fedha hizi ni kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Abiria pamoja na miundombinu yake (ukarabati na upanuzi wa maegesho ya ndege, maegesho ya magari na barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani) na usimikaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege. Aidha, kazi zingine ni Ujenzi wa uzio wa usalama, jengo la kuongozea ndege na jengo la uchunguzi wa hali ya hewa.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mpanda

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 12.10 kwa ajili ya maandalizi ya kufanya usanifu wa Jengo la abiria kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo. 

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Tabora

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 3,695.32 zinazojumuisha Shilingi milioni 662.42 fedha za ndani na Shilingi milioni 3,032.90 fedha za nje kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Abiria na miundombinu yake, jengo la kuongozea ndege, barabara ya kuingia kiwanjani, maegesho ya magari, uzio wa usalama pamoja na jengo la uchunguzi wa hali ya hewa.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Songwe

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni

10,106.46 fedha za ndani kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Jengo la Abiria na mifumo yake, usimikaji wa taa za kuongozea ndege pamoja na ujenzi wa uzio wa usalama. 

Ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza

  • Mheshimiwa Spika, kiasi cha Shilingi milioni 5,300.48 fedha za ndani kwa ajili ya ujenzi wa Jengo jipya la Abiria na mifumo yake, upanuzi wa maegesho ya ndege, ukarabati wa barabara ya kuruka na kutua ndege, ujenzi wa mabega (shoulders) na ujenzi wa uzio wa usalama.

Ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Arusha

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi 242.02 kwa ajili ya ujenzi wa uzio wa usalama. 

Ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa kiasi cha Shilingi milioni 4,947.79 fedha za ndani kwa ajili ya kumalizia  ukarabati wa barabara ya kuruka na kutua ndege, viungio vyake pamoja na maegesho ya ndege. Kazi zingine ni kusimika taa na mitambo ya kuongozea ndege, ujenzi wa barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani, maegesho ya magari na uzio wa usalama.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga

  • Mheshimiwa Spika, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 3,692.90. Kati ya fedha hizo, Shilingi milioni 660.00 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 3,032.90 ni fedha za nje. Kazi zitakazohusika ni ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na kiungio chake, maegesho ya ndege, jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege, jengo la uchunguzi wa hali ya hewa, uzio wa usalama, barabara ya kuingia kiwanjani na maegesho ya magari. Kazi nyingine ni pamoja na usimikaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege.   

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga

  • Mheshimiwa Spika,  mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 

3,692.90. Kati ya hizo, Shilingi milioni 660.00 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 3,032.90 ni fedha za nje. Fedha hizo zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na kiungio chake, maegesho ya ndege, jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege, jengo la uchunguzi wa hali ya hewa, barabara ya kuingia kiwanjani, maegesho ya magari na usimikaji wa taa. Aidha, kazi nyingine ni usimikaji wa mitambo ya kuongozea ndege pamoja na ujenzi wa uzio wa usalama.

Uendelezaji wa Viwanja vya Ndege vya Mikoa

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha  2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 26,279.40 ambapo Shilingi milioni 25,784.40 ni fedha za ndani na Shilingi milioni 495.00 nifedha za nje. Kiasi hiki ni kwa ajili ya ujenzi   wa jengo la abiria na jengo la kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Mkoa wa Geita; kuendelea na ujenzi wa viwanja vya ndege katika mikoa ya Iringa, Kilimanjaro (Moshi), Ruvuma (Songea) na Mara (Musoma); kuanza maandalizi ya ujenzi wa Kiwanja kipya cha Simiyu, Kiwanja cha Lake Manyara, Tanga na Lindi pamoja na ujenzi wa uzio wa usalama pamoja na barabara ya kufanyia ukaguzi kwenye viwanja hivi. Kazi nyingine ni ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege kwa kiwango cha lami kwenye kiwanja cha ndege cha Nachingwea.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Msalato

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 20,435.72 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja kipya cha Msalato mkoani Dodoma. Kati ya fedha hizo, Shilingi milioni 1,915.00 nifedha za ndani na Shilingi milioni 18,520.72 nifedha za nje.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Bukoba

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, mradi huu umetengewa kiasi cha Shilingi milioni 12.10 fedha za ndani kwa ajili ya kazi za maandalizi ujenzi wa jengo la Watu Mashuhuri (VIP Lounge), ukarabati wa meta 200 wa barabara ya kuruka na kutua ndege pamoja na usimikaji wa taa za kuongozea ndege.

Ujenzi wa Jengo la Tatu la Abiria Katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere

(JNIA)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha fedha 2022/23, mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 54.346 fedha za ndani kwa ajili ya kuunganisha umeme wa 33 KV kutoka Gongolamboto pamoja kufanya Usanifu wa Kina wa Jengo la Pili la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha JNIA.

FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha  2022/23,  fedha za Mfuko wa Barabara ni jumla ya Shilingi 599,756,467,800.00  zitakazotumika kufanya kazi za matengenezo na ukarabati wa barabara kuu na za mikoa Kati ya fedha hizo, TANROADS imetengewa Shilingi 534,662,653,430.21 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) imetengewa Shilingi 59,406,961,492.00 kwa ajili ya kazi za ukarabati wa barabara za mikoa, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara, ukarabati na ununuzi wa vivuko, usalama barabarani pamoja na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi hiyo. Aidha, Shilingi 8,124,075,538.87 zitatumika kugharamia uendeshaji wa Bodi ya Mfuko wa Barabara. 
  • Mheshimiwa   Spika,      mgawanyo wa

Shilingi 59,406,961,492.00  zilizotengwa kwa ajili ya Wizara (Ujenzi) ni kama ifuatavyo: Shilingi 15,820,073,000.00 ni kwa ajili yakufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara zenye urefu wa kilometa 5,605; Shilingi 4,467,403,504.00 ni  kwa ajili ya manunuzi na ukarabati wa vivuko pamoja na ujenzi wa maegesho  na miundombinu ya vivuko; Shilingi 3,920,860,484.00   nikwa ajili yamiradi  ya  Usalama  Barabarani na Mazingira na Shilingi 4,467,403,504.00 ni kwa ajili ya kazi za usimamizi na ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na Wizara (Ujenzi) pamoja na kujenga uwezo wa watumishi. Aidha, Shilingi 30,731,221,000.00 zimetengwa kwa ajili yamiradi ya barabara za mikoa itakayohusisha ukarabati wa jumla ya kilometa 369.66  kwa kiwango cha changarawe, ujenzi wa kilometa 41.19 kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi na ukarabati  wa madaraja/makalavati 44  katika mikoa mbalimbali nchini. 

Mchanganuo wa miradi itakayotekelezwa kwa fedha za Mfuko wa Barabara zilizotengwa kwa ajili ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) umeonyeshwa katika Viambatisho Na. 3 na 4.

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi

534,662,653,430.21      fedha     za     Mfuko      wa

Barabara ambazo zimetengwa kwa ajili ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) zitatumika kufanya matengenezo ya barabara kuu, barabara za mikoa, madaraja na uendeshaji wa mizani 

Mchanganuo wa matumizi ya fedha hizo umeoneshwa katika Viambatisho Na. 5, 5A – 5D.

USHIRIKISHWAJI WA WANAWAKE KATIKA

KAZI ZA BARABARA 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 Wizara imepanga kuendelea kutoa mafunzo kwa Makandarasi wanawake ya namna ya kuomba zabuni na kujaza zabuni kwa ufanisi; kutoa mafunzo kwa wanawake na vikundi vya wanawake juu ya kufanya matengenezo na ukarabati wa barabara kwa kutumia teknolojia ya nguvu kazi; na kuwasaidia kusajili kampuni zao za ujenzi pamoja na kufuatilia kwa karibu kazi za barabara zinazofanywa na wanawake Makandarasi. Lengo ni kuongeza ushiriki wa wanawake katika kazi za barabara.

Vilevile, Wizara itaendelea kutembelea vyuo vya elimu ya juu ili kutoa ushauri (Mentorship and Coaching) kwa wasichana wanaosoma fani za sayansi zinazohusiana na Sekta ya Ujenzi. Aidha, Wizara itaendelea kutembelea shule za sekondari ili kuhamasisha wasichana kusoma masomo ya Sayansi na Hisabati pamoja na kuelimisha Umma juu ya ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara.

MPANGO WA KAZI WA TAASISI ZILIZO CHINI YA SEKTA YA UJENZI KWA MWAKA WA FEDHA

2022/23

Wakala wa Barabara Tanzania

  • Mheshimiwa Spika,  Katika mwaka wa fedha 2022/23, Wakala ya Barabara Tanzania umepanga kujenga barabara kuu zenye urefu wa kilometa 470.0 kwa kiwango cha lami, ukarabati wa kilometa 33.0 kwa kiwango cha lami katika barabara kuu, ujenzi wa madaraja 10, ukarabati wa daraja 1 na kufanya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa madaraja 6.
  • Mheshimiwa Spika, Miradi ya barabara za mikoa iliyopangwa kutekelezwa na Wakala ni ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara zenye urefu wa kilometa 103.01. Kati ya hizo, kilometa 61.82 zitajengwa kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na kilometa 41.19 zitajengwa kwa fedha za Mfuko wa Barabara. Vile vile, Wakala umepanga kufanya ukarabati kwa kiwango cha changarawe wa barabara zenye urefu wa kilometa 1,042.43. Kati ya hizo, kilometa 672.77 zitakarabatiwa kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na kilometa 369.66 zitakarabatiwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara. Aidha, fedha hizi zitatumika kujenga na kufanya ukarabati wa madaraja/makalavati 75 ambapo kati ya hayo madaraja/makalavati 31 yatatumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na 44 yatatumia fedha za Mfuko wa Barabara.

Kazi nyingine ni kufanya matengenezo ya barabara kuu na barabara za mikoa ambayo yatahusisha matengenezo ya kawaida (routine and recurrent maintenance) kwa kilometa 33,615.68, matengenezo ya muda maalum kilometa 4,081.70 na sehemu korofi kilometa 435.07 pamojana matengenezo ya madaraja 3,350. Mpango huu pia unajumuisha shughuli za udhibiti wa uzito wa magari na hifadhi za barabara, kazi za dharura pamoja na mradi wa matengenezo ya barabara kwa mikataba ya muda mrefu.

  • Mheshimiwa Spika, malengo mengine ni kuendelea na majukumu ya kusimamia  miradi ya ujenzi na ukarabati wa Viwanja vya Ndege. Miradi iliyopangwa kutekelezwa ni pamoja na kuanza ujenzi wa Kiwanja kipya cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, kuanza ujenzi wa Jengo la Abiria katika kiwanja cha ndege cha Mwanza pamoja na ukarabati na upanuzi wa Viwanja vya Ndege vya Kigoma, Shinyanga, Tabora, Sumbawanga, Iringa na Musoma.

Kazi nyingine zinazohusu viwanja vya ndege ni kuendelea na ujenzi wa viwanja vya Ndege vya Songea, Mtwara na Songwe. Aidha, Wakala utaendelea na ukarabati na upanuzi wa viwanja vya ndege vya Tanga, Lake Manyara, Lindi, Arusha, Bukoba, Moshi na Nachingwea.

Wakala wa Majengo Tanzania

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 Wakala wa Majengo Tanzania utaendelea kutekeleza majukumu yake kwa kutumia fedha za Ruzuku ya Serikali pamoja na fedha za ndani. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri kwa miradi ya ujenzi wa majengo ya Serikali, kujenga majengo ya Washitiri mbalimbali; kuuza Nyumba zinazojengwa na TBA kwa Watumishi wa Umma na kupangisha nyumba za Serikali kwa Watumishi wa Umma na kupangisha baadhi ya majengo ya Serikali kwa wasio watumishi wa umma ili kuongeza uwezo wa Wakala kujiendesha. 
  • Mheshimiwa Spika, miradi iliyopangwa kutekelezwa kwa kutumia fedha za ruzuku ni pamoja na ujenzi wa nyumba 20 za Viongozi Jijini Dodoma; ujenzi wa nyumba 150 za watumishi Jijini Dodoma; ununuzi wa samani kwenye Ikulu Ndogo; ujenzi wa nyumba tano (5) za majaji Tanzania Bara (Kilimanjaro, Mtwara, Shinyanga, Kagera na Tabora); ujenzi wa jengo la makazi kwa ajili ya watumishi wa Umma katika eneo la Temeke Kota wilayani Temeke na ujenzi wa jengo la Makazi kwa ajili ya watumishi wa Umma katika eneo la Magomeni Kota wilaya ya  Kinondoni.
  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine ni ukarabati wa nyumba 66 zilizokuwa zinamilikiwa na iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA); ukarabati wa nyumba za watumishi wa Umma katika mikoa 20 zilizokuwa zinamilikiwa na TAMISEMI/NHC; ukarabati wa nyumba 30 za viongozi mikoani pamoja na matengenezo kinga ya nyumba za Magomeni Kota; ukarabati wa nyumba 40 za viongozi jijini Dodoma; ukarabati wa Karakana za samani za

Wakala kwa mikoa ya Arusha, Mwanza, Morogoro, Tabora, Dar es Salaam na Mbeya pamoja na kutoa huduma ya ushauri katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi awamu ya pili katika Mji wa Serikali Mtumba – Dodoma. 

  • Mheshimiwa Spika, miradi itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za ndani za Wakala ni ujenzi wa nyumba 72 za watumishi wa Umma mikoani; ujenzi wa majengo mawili ya ghorofa kwa watumishi wa Umma Itega jijini Dodoma; upatikanaji wa Hati Miliki za viwanja vya TBA; ununuzi wa samani katika jengo la Chimala jijini Dar es Salaam; umaliziaji wa miradi miwili (2) ya ujenzi katika mikoa ya Arusha na Pwani (Simeoni-Arusha na Chalinze -Pwani) na ujenzi wa jengo la ghorofa kwa watumishi wa Umma eneo la Canadian Village Dar es Salaam.
  • Mheshimiwa Spika, miradi mingine ni ukarabati wa karakana 3 katika Mikoa ya Tanga, Iringa na Mtwara; ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkoa  wa Geita; ukarabati wa Majengo ya ofisi 20 Mikoani; ukarabati wa Majengo mbalimbali nchini pamoja na kuanza ujenzi wa maabara ya upimaji/majaribio ya malighafi za ujenzi.
  • Mheshimiwa Spika, Wakala pia umepanga kutekeleza miradi 193ya Washitiri. Miradi hiyo ni pamoja na miradi 28 ya Buni Jenga (Design and Build) ambapo  hadi sasa miradi 18 inaendelea kutekelezwa. Miradi inayoendelea inajumuisha:Ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi (Simiyu); Ujenzi wa Ofisi ya Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama (Mara); Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama (Singida); Ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Chunya (Mbeya); na Awamu ya Pili ya Ujenzi wa Ofisi ya TANESCO Wilayani Chato (Geita).
  • Mheshimiwa Spika, vilevile, Wakala utaendelea kutekeleza miradi mbalimbali katika Mji wa Serikali eneo la Mtumba Dodoma ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Aidha, Wakala utatekeleza miradi 15 ya Ushauri Elekezi kwa ujenzi wa majengo ya ofisi za Wizara na taasisi za Serikali.
  • Mheshimiwa Spika, vilevile, Wakala umepanga kutekeleza miradi 108 ya Ushauri (Consultancy) ambapo kati ya hiyo miradi 76 inaendelea. Miradi inayoendelea inajumuisha: Ujenzi wa Hosteli za Wanafunzi zitakazojengwa katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kampasi ya Karume Zanzibar, Ukumbi wa Mafunzo uliopo Iwambi Mbeya Mjini na Bweni la Wanafunzi katika Chuo cha Utawala wa Mahakama Lushoto (IJA). Kazi nyingine ni ukarabati, upanuzi na ujenzi wa miundombinu ya Mahakama Kuu Kanda ya Tabora; na Awamu ya Tatu ya Ujenzi wa Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Mufindi.
  • Mheshimiwa Spika, Wakala pia umepanga kutekeleza miradi 38 ya Ujenzi ambapo kati ya hiyo miradi 17 inaendelea. Miradi  ya ujenzi inayoendelea inajumuisha: Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe Nselewa Vwawa Awamu ya Pili, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Ngorongoro Arusha na chumba cha upasuaji na wodi ya wazazi katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Awamu ya Pili. Miradi mingine ni pamoja na  ukarabati wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Mkoa wa Manyara.
  • Mheshimiwa Spika, Wakala pia umepanga kutekeleza miradi minne (4) ya Usimamizi (Project Management) ambapo kati ya hiyo

miradi mitatu (3) inaendelea. Miradi inayoendelea  ni:  Usimamizi na Uendeshaji wa Jengo la Ukumbi wa Bunge; Ujenzi wa Kituo cha pamoja cha Forodha Mpakani cha Kasumulu (One stop Border Post) awamu ya pili;  na Ujenzi wa Vihenge (Silos) vya kuhifadhia nafaka pamoja na Maghala kwa ajili ya hifadhi ya chakula katika Mikoa nane (8) ya Dodoma, Katavi, Manyara, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga na Songwe.

Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Wakala umepanga kuendelea na usimamizi na uendeshaji wa vivuko vya Serikali, kutoa huduma ya ukodishaji wa magari na mitambo ya ujenzi wa barabara pamoja na kufanya matengenezo ya magari, usimikaji wa mifumo ya umeme, majokofu, viyoyozi na elektroniki.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi ya maegesho ya vivuko, Wakala umepanga kuendelea na upanuzi wa eneo la maegesho ya kivuko cha Magogoni – Kigamboni upande wa Kigamboni;  ujenzi wa maegesho ya  Zumacheli kwa ajili ya kivuko cha Chato- Nkome; ujenzi na ukarabati wa maegesho sita (6) katika vivuko vya Magogoni  – Kigamboni, Kilambo – Namoto, Utete – Mkongo, Iramba – Majita, Nyakarilo – Kome na Kasharu –Buganguzi; na ujenzi wa miundombinu mipya (Jengo la abiria, ofisi, na uzio) katika vivuko vya Kisorya – Rugezi, Nyakarilo – Kome na Bugolora – Ukara). Kazi nyingine ni ujenzi wa maegesho mapya ya Kayenze – Kanyinya na Muleba – Ikuza; ujenzi wa maegesho mapya manne (4) ya Ijinga – Kahangala (Magu), Bwiro – Bukondo (Ukerewe); kuhuisha  na kusimika mfumo wa kielektroniki wa kukatia tiketi (NCards System) katika vituo vya Magogoni – Kigamboni, Kigongo – Busisi, Kisorya – Rugezi, Pangani – Bweni na Ilagala – Kajeje.
  • Mheshimiwa Spika, miradi ya ujenzi na ukarabati wa vivuko iliyopangwa kutekelezwa ni kuendelea na ujenzi wa vivuko vipya sita (6) kwa ajili ya kutoa huduma katika maeneo ya Kisorya – Rugezi, Ijinga – Kahangara, Bwiro – Bukondo, Nyakarilo – Kome, Buyangu – Mbalika na Nyamisati – Mafia. Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa kivuko cha Magogoni – Kigamboni, ununuzi wa boti ndogo kwa ajili ya kutoa huduma Lindi – Kitunda na Utete – Mkongo, ununuzi wa “crane” mbili kwa ajili ya kusaidia ukarabari wa vivuko pamoja na kuendelea na ununuzi wa vifaa vya uendeshaji karakana TEMESA.  Aidha, Wakala umepanga kukamilisha ukarabati wa MV Musoma, MV Old Ruvuvu, MV Mara, MV TEMESA, MV Ujenzi, MV Kome II, MV Misungwi, MV Ruhuhu, MV Nyerere, MV Kyanyabasa, MV Tanga, MV Kitunda, MV Kazi, MV Magogoni na MV Kilombero II itakayohamishiwa  eneo la Mlimba – Malinyi.
  • Mheshimiwa Spika, kuhusu Ujenzi na Ukarabati wa Karakana, Wakala umepanga kuendelea na ujenzi wa karakana tano (5) katika mikoa mipya ambayo ni Songwe, Simiyu, Katavi, Geita na Njombe; kukamilisha ujenzi wa jengo la makao makuu ya Wakala Dodoma, kuanzisha karakana sita (6) ngazi ya wilaya katika wilaya za Simanjiro, Masasi, Ukerewe, Chato, Mafia na Kyela; na ukarabati wa karakana 12 katika mikoa ya Tabora, Mwanza, Arusha, Mtwara, Mbeya, MT Depot – Dar es Salaam, Kigoma, Mara, Ruvuma, Pwani, Dodoma na Vingunguti. Aidha, Wakala umepanga kusanifu na kusimika mfumo wa usimamizi na ufuatiliaji wa matengenezo ya magari, umeme na elektroniki pamoja na ununuzi wa jumla (bulk procurement) wa vipuri vya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali.
  • Mheshimiwa Spika, vilevile, katika mwaka 2022/23, Wakala umepanga kufanya matengenezo ya magari 30,365, matengenezo na usimikaji wa mifumo 256 ya umeme, 704 ya majokofu na viyoyozi na mifumo 25 ya elektroniki. Aidha, Wakala umepanga kutoa ushauri wa Kihandisi kwa miradi ya usimikaji wa mifumo 90 ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na majokofu na kusimamia mifumo hiyo inayofikia 50. Wakala pia utaendelea na usimamizi wa vivuko vya Serikali 33 ambavyo vinatarajiwa kutoa  huduma kwa abiria  wapatao 42,460,356; magari 1,745,311 na tani za mizigo 530,220 kwa mwaka. Vilevile, Wakala utaendelea na ukodishaji wa mitambo ya ujenzi wa barabara. 

Bodi ya Mfuko wa Barabara

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha Mfuko wa Barabara unatarajia kukusanya jumla ya Shilingi 856,794,954,000 kwa ajili ya kugharamia matengenezo ya barabara nchini.  Kati ya fedha hizo, Shilingi 599,756,467,800 ni kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Kitaifa (Barabara Kuu na Barabara za Mikoa) ambazo husimamiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Fungu 98). Vilevile, Shilingi 257,038,486,200 ni kwa ajili ya kugharamia barabara za Wilaya ambazo husimamiwa na Ofisi ya Rais –TAMISEMI (Fungu 56). 

Mgawanyo wa fedha za Mfuko wa Barabara kwa kila taasisi ni kama ifuatavyo:   Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kiasi cha Shilingi 59,406,961,492.00; TANROADS Shilingi 534,662,653,430.21; Ofisi ya Rais – TAMISEMI Shilingi 25,460,126,354.25; TARURA Shilingi 229,141,137,184.33; na Bodi ya Mfuko wa Barabara Shilingi 8,124,075,538.87. 

  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zitakazotekelezwa na Bodi ni pamoja na  kuendelea kufanya kaguzi za ubora wa kazi za barabara katika mikoa yote nchini ili kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa inakidhi thamani ya fedha zilizotumika. Vilevile, Bodi itafuatilia matumizi ya fedha zinazopelekwa kwa Wakala za barabara (TANROADS na TARURA) ili kuhakikisha kuwa zinatumika kwa madhumuni yaliyowekwa.

Bodi ya Usajili wa Wahandisi

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) imepanga kusajili Wahandisi 3,200, Mafundi Sanifu 400 na Kampuni za Ushauri wa Kihandisi nane (8).  Vilevile, Bodi imepanga kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa Wahandisi Wahitimu 3,692. Idadi hii inahusisha Wahandisi Wahitimu 2,492 watakaokuwa wanaendelea na mafunzo na 1,200 wapya wanaofadhiliwa na Serikali, Wafadhili na Sekta Binafsi.
  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine zitakazofanywa na Bodi ni kuendelea kufanya kaguzi za shughuli za kihandisi nchini ili kuhakikisha kuwa shughuli zote za kihandisi zinafanywa na wahandisi waliosajiliwa na kwa kufuata maadili ya utendaji kazi za kihandisi. Bodi pia itaendelea  kutembelea na kukagua miradi yote ya ujenzi ya kimkakati pamoja na barabara za Halmashauri, kusimamia mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa wahandisi watalaam na washauri na kuwashawishi wahandisi wataalam ili waanzishe kampuni za ushauri wa kihandisi mikoani, hivyo kusogeza huduma hii muhimu karibu na watumiaji. Aidha,  Bodi itaendelea kuhamasisha Wadau mbalimbali katika mpango wake wa kujenga Kituo cha Umahiri cha Uhandisi (Engineering Centre of Excellence) ambacho kitasaidia kutoa ushauri wa Uanzishwaji na uendelezaji wa Viwanda.

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na

Wakadiriaji Majenzi

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Bodi imepanga kusajili Wataalamu 125 katika fani za Ubunifu Majengo, Ukadiriaji Majenzi, Ubunifu wa Ndani ya Majengo, Ubunifu wa Mandhari ya Nje ya Majengo, Usanifu Teknolojia ya Majengo, Utathmini Majengo, Usimamizi Ujenzi na Usimamizi Miradi. Aidha, Bodi imepanga kusajili kampuni 22 za Ubunifu Majengo na Ukadiriaji Majenzi. Malengo mengine ni kuwajengea uwezo wahitimu 225 katika fani hizo kupitia mpango maalumu wa Mafunzo kwa Vitendo (Enhanced Articled Pupilage  Programme – EAPP).
  • Mheshimiwa Spika, vilevile, Bodi imepanga kufanya ukaguzi wa miradi ya ujenzi 3,120 katika mikoa yote ya Tanzania bara pamoja na kusajili miradi ya ujenzi 1,200. Aidha, Bodi imepanga kuendesha mitihani ya kitaalamu kwa wahitimu 218 katika fani za Ubunifu majengo na Ukadiriaji majenzi; kufanya mikutano mitano (5) na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari; na kuendesha mashindano ya insha kwa lengo la kuwahamasisha kusoma masomo ya sayansi na hatimaye kusomea taaluma zinazohusu Ubunifu Majengo na Ukadiriaji

Majenzi. 

Bodi ya Usajili wa Makandarasi

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 Bodi imepanga kusajili jumla ya Makandarasi wapya 960 na kukagua jumla ya miradi ya ujenzi 3,200. Malengo mengine ni kuendesha kozi za mafunzo katika vituo vinne (4) katika mikoa ya Arusha, Iringa, Mwanza na Dar es Salaam pamoja na kuendesha warsha moja (1) ya mafunzo ya ushirikiano wa ubia (Joint Venture) katika Jiji la Dodoma. Aidha, Bodi itaendelea na uendelezaji wa Mfuko Maalum (Contractor’s Assistance Fund – CAF) wa kutoa dhamana ya kusaidia Makandarasi wote wa ndani, pamoja na kuhamasisha walengwa kujiunga ili kuomba zabuni kwa mfumo wa ubia.

Baraza la Taifa la Ujenzi

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 Baraza limepanga kuendelea kukamilisha mapitio ya Sheria iliyoanzisha Baraza; kukamilisha uandaaji wa Kanuni za utekelezaji wa Sheria ya Baraza (NCC Act CAP 162 RE 2008); kutoa ushauri wa kiufundi na kitalaam kwa wadau wa Sekta ya Ujenzi pamoja na kuratibu utatuzi wa migogoro inayojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya ujenzi. Kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa jengo la ofisi za Baraza jijini Dodoma; kuandaa Mwongozo wa Viwango vya Kitaifa vya Utekelezaji wa Shughuli za Ujenzi (Standard Productivity Rates for Construction Activities); kukusanya na kutoa takwimu na taarifa mbalimbali zinazohusu maendeleo ya Sekta ya Ujenzi pamoja na kuendelea na mchakato wa kuanzisha Kituo Maalum cha Taarifa na Takwimu za Sekta ya

Ujenzi nchini.

  • Mheshimiwa Spika, vilevile, Baraza litaendelea kuratibu utatuzi wa migogoro inayojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya ujenzi pamoja na kufanya tafiti tano (5) kwa ajili ya kuimarisha Sekta ya Ujenzi nchini. Aidha, Baraza litaendelea na wajibu wake wa kutoa huduma za ukaguzi wa kiufundi katika miradi ya ujenzi kwa wadau wa Sekta ya Ujenzi pamoja na kuhamasisha ushiriki wa Sekta isiyo rasmi katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi kwa ubora zaidi. 

Kituo cha Usambazaji wa Teknolojia Katika Sekta ya Ujenzi na Usafirishaji Tanzania (Tanzania Transportation Technology Transfer

Centre)

  • Mheshimiwa Spika,katika mwaka wa fedha 2022/23, Kituo kimepanga kuendelea kusambaza teknolojia katika Sekta ya Ujenzi na Uchukuzi hapa nchini pamoja na majarida kutoka kwa wadau mbalimbali. Aidha, kituo kitaendelea kuandaa, kuchapisha na kusambaza majarida yake yanayoandaliwa mara nne (4) kwa mwaka yanayohusu teknolojia, maarifa na taarifa mbalimbali muhimu katika Sekta za Ujenzi na Uchukuzi.
  • Mheshimiwa Spika,kazi nyingine ni kuandaa na kuendesha mafunzo kwa wadau yanayolenga kutatua changamoto zinazoikabili Sekta za Ujenzi na Uchukuzi; kuratibu shughuli mbalimbali za uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT); kushiriki katika kuandaa na kufanyika kwa Mkutano wa Vituo vya usambazaji wa Teknolojia Afrika (10th T2 Centres Conference) unaofanyika kila mwaka pamoja na kuendesha makongamano ya

Watalaam wa taasisi mbalimbali zinazohusika na miundombinu na usafirishaji ili kujadili na kutafuta majibu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta za Ujenzi na Uchukuzi.  

D.2 UCHUKUZI

Makadirio ya Bajeti ya Matumizi ya Kawaida na

Miradi ya Maendeleo 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Sekta ya Uchukuzi (Fungu 62)

imetengewa              jumla             ya             Shilingi 

2,400,781,440,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 94,546,502,000 zimetengwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi   2,306,234,938,000   kwa   ajili   ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Mgawanyo wa fedha za maendeleo pamoja na miradi iliyotengewa fedha ni kama inavyooneshwa katika Kiambatisho Na. 6. Fedha za Matumizi ya Kawaida zinajumuisha Shilingi 67,475,558,000 kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi na Shilingi

27,070,944,000       kwa      ajili      ya       Matumizi

Mengineyo. Katika Fedha za Miradi ya Maendeleo zilizotengwa, Shilingi 2,192,771,622,000 ni fedha za Ndani na Shilingi  113,463,316,000 ni fedha za Nje.

457. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetengewa Shilingi bilioni 38.6 kutoka katika vyanzo vyake vya ndani ili kudhibiti huduma za usafiri ardhini katika sekta ndogo za usafiri wa reli, barabara na waya. Fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ifuatayo:

  1. Kufanya Upembuzi Yakinifu (Feasibility study) kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya ukaguzi wa lazima (Periodic and Mandatory Vehicle Inspection Centres under PPP Arrangement) wa magari yanayotoa huduma kibiashara katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Tabora, Dodoma, Mbeya na Kibaha(Pwani) kwa mujibu wa Kifungu cha 5(1)(f) cha Sheria ya LATRA ya Mwaka 2019.
  2. Kusambaza matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa kutahini madereva wa magari ya biashara nchi nzima (Roll out electronic Drivers Testing Software) pamoja na kusajili wahudumu wa mabasi na treni kwa mujibu wa Kifungu cha 5(1)(e) cha Sheria ya LATRA ya Mwaka 2019.
  3. Kutekeleza matumizi ya mfumo wa tiketi mtandao (e-ticketing) kwa kila basi linalofanya safari ndefu na safari za mijini kwa kila basi linalopewa leseni na LATRA na vilevile kuendelea kusimamia maboresho ya mfumo huu ili uzidi kuwa rafiki kwa watumiaji. 
  4. Kutengeneza mfumo wa mita za kukokotoa nauli (Fare meter Software) za teksi za kawaida na zile zinazotoa huduma kwenye viwanja vya ndege pamoja na pikipiki za magurudumu matatu zinazotoa huduma ya usafiri kibiashara kwa mujibu wa Kanuni ya 15(d) ya Kanuni za Usafiri wa Kukodi za Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini za mwaka 2020. 
  5. Kukamilisha uwekaji wa mfumo wa kutoa taarifa za safari za mabasi kwa wasafiri katika vituo vikuu vya mabasi vya Dodoma na Magufuli –Mbezi, Dar es Salaam pia katika simu janja na tovuti ya LATRA ili kusaidia wasafiri na wadau mbalimbali kupata taarifa sahihi za safari za mabasi katika vituo hivyo.
  6. Kuendelea kuboresha mfumo wa kufuatilia mwenendo wa mabasi ya masafa marefu na treni ili kuimarisha usalama. 
  7. Kuboresha mfumo wa utoaji leseni (Railways and Roads Information Management System) kwa kuunganisha na mifumo mingine ya Serikali ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau mbalimbali.

458. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/23, Mfuko wa Reli (Railway Infrastructure Fund) ambao unasimamiwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) umetengewa jumla ya Shilingi bilioni  294.80 fedha za ndani ili kugharamia ukarabati wa miundombinu ya reli iliyopo na kujenga reli mpya ya Standard Gauge, ukarabati wa vitendea kazi na kugharamia maandalizi ya miradi ya ujenzi wa reli. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na:-

                                i.        Ukarabati wa njia ya reli iliyopo ya

Tabora-Kigoma (Km 411), Kaliua-

Mpanda (Km 210) na Tabora-Isaka-

Mwanza (Km 385); ii.    Matengenezo ya njia ya reli ya Tanga-Arusha (Km 470) na Kilosa – Gulwe – Igandu (Km 120) na

Madaraja kati ya Godegode na

Gulwe; iii. Ufufuaji wa njia za reli zilizofungwa ikiwa ni pamoja na kipande cha

Kilosa-Kidatu (Km 108); iv.     Ukarabati wa karakana, stesheni na majengo ya Shirika la reli;

  • Ukarabati wa mfumo wa ishara na  mawasiliano wa reli iliyopo; 
  • Kuunda upya vichwa vya treni 3 vya njia kuu, ukarabati wa mabehewa 600 ya mizigo na  37 ya abiria;
  • Ununuzi wa mabehewa 245 ya mizigo, mabehewa 22 ya abiria na

injini 10 kwa ajili ya reli iliyopo;

  • Upimaji na uwekaji alama katika maeneo ya reli;
  • Ufufuaji wa mgodi wa kuzalisha kokoto wa Pangani (Tanga) na Tumbi (Tabora) na uboreshaji wa

Mgodi wa Tura; na

  • Kugharamia stadi mbalimbali kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa reli. 

459. Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi trilioni 1.263 kutoka Mfuko Mkuu wa Serikalizimetengwa ili kugharamia ujenzi wa reli mpya ya Standard Gauge, ununuzi wa injini na mabehewa ya mizigo na abiria na upembuzi yakinifu kwa ajili ya miradi ya reli. Miradi itakayotekelezwa ni pamoja na:

  1. Kukamilisha ujenzi wa reli ya Standard Gauge kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro (km 300);
  2. Kuendelea na ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Morogoro –

Makutupora (km 422);  iii. Kuendelea na ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Mwanza – Isaka (km

341); iv. Kuendelea na ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Makutupora –

Tabora (km 368);

  • Kuanza ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Tabora – Isaka (km 165);
  • Kuanza ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Tabora-Kigoma (km 411);
  • Kuendelea na ununuzi wa injini, mabehewa na mitambo kwa ajili ya matengezo ya njia wakati itakapoanza kufanya kazi; 
  • Kuendelea na taratibu za ujenzi wa reli kwa sehemu za Kaliua – Mpanda – Karema (km 321), Uvinza – Musongati 

(km 240) na Isaka – Rusumo (km 371);

  1. Kugharamia uendeshaji wa reli ya

Standard Gauge

  • Kuendelea kugharamia mafunzo ya wataalamu wa uendeshaji na usimamizi wa treni ya Standard Gauge.
  • Ulipaji     wa     fidia kwa   wananchi

wanaopisha ujenzi wa reli; na

xii. Kuendelea kukamilisha taratibu za kupata mwekezaji kwa mfumo wa ubia baina ya sekta ya Umma na binafsi (PPP) kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Tanga-Arusha-Musoma na Mtwara-Mbambay na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma. 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023Mradi wa Ukarabati wa Reli ya Kati iliyopo kutoka Dar es Salaam hadi Isaka (km 970) umetengewa jumla ya Shilingi bilioni 9.193 fedha za nje. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na:
  1. Kukamilisha ukarabati wa maeneo yaliyobaki katika eneo la MakutuporaManyoni na Kitaraka-Malongwe-

Igalula; na

  1. Kuboresha vituo vya kuhudumia mizigo vya Ilala na Isaka.
  • Mheshimiwa   Spika,       katika        mwaka

2022/23 Shirika la Reli Tanzania (TRC) linalenga kusafirisha tani za mizigo 529,000 na abiria wapatao 520,000 kwa upande wa masafa marefu, abiria 256,292 kwa treni ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro na abiria kwa usafiri wa treni ya mjini (Dar es Salaam commuter train) ni 4,262,800. 

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/23 Shirika la Reli Tanzania (TRC) limepanga kutekeleza Mpango wa miaka mitano ambao unalenga yafuatayo:-
    • Kuendelea na utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa reli ya Standard Gauge, kuinua kiwango cha reli na madaraja yaliyopo kwa kutandika reli nzito zaidi za angalau ratili 80 kwa yadi na kukarabati madaraja kuweza kupitisha tani 18.5 kwa ekseli;
    • Kushirikiana na vyombo vya dola pamoja na jamii inayozunguka miundombinu ya reli ili kuzuia uharibifu wa miundombinu ya reli;
    • Kukabarati       sehemu      korofi         za miundombinu ya reli na kununua

vitendea kazi kwa awamu;

  1. Kuweka mifumo ya TEHAMA kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma; na
  2. Kuendelea maeneo yanayomilikiwa na TRC ili kuongeza vyanzo vya mapato ya Shirika.
  3. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/23 Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imetenga jumla ya Shilingi bilioni 22.2 kutoka katika vyanzo vya mapato yake ya ndani na Shilingi bilioni 13.19 kutoka mfuko Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha miundombinu ya reli pamoja na maeneo yote yaliyo ndani ya ukanda wa reli mita 50. Fedha hizo zitatumika kutekeleza kazi zifuatazo:-
  1. Kununua mataruma 20,000 ya mbao kwa ajili ya kuwekwa katika maeneo ya madaraja na njia za kupishania; 
    1. Kununua mitambo    kwa   ajili   ya kiwanda         cha   kokoto        –         Kongolo; 

ununuzi wa excavators mbili (2); 

  1. Kufanya ukarabati wa mabehewa 14 kwa ajili ya treni ya jiji la Dar es Salaam na mabehewa saba (7) kwa ajili treni ya Udzungwa.
    1. Kusafirisha shehena ya mzigo tani 450,000 na jumla ya abiria 800,000; na
      1. Kufanya matengenezo kinga ya injini na mabehewa pamoja ukarabati wa miundombinu ya reli.
  • Mheshimiwa Spika, Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC) limetengewa jumla ya Shilingi bilioni 4.157 zikiwa ni fedha za nje kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Shilingi bilioni

92.575 zinazotokana na makusanyo yake ya

ndani. Kazi zitakazotelelezwa ni pamoja na:-  

i. Ujenzi wa Kituo cha Uratibu wa Masuala ya Utafutaji na Uokoaji katika Ziwa Victoria (Maritime Rescue Cordination

Centre – MRCC), Mwanza, Tanzania; ii. Ujenzi wa vituo vidogo vitatu (3) vya Utafutaji na Uokoaji (Search and Rescue

Centres -SARs) katika Ziwa Victoria; iii. Kukamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujezi wa boti tatu (3) za utafutaji na uokoaji zitakazotumika katika maziwa makuu. Baada ya upembuzi yakinifu na na ununuzi wa boti hizo kukamilika, mgawanyo wa boti hizo utafanyika katika maziwa husika.

  1. Kuimarisha mifumo ya utoaji leseni na ukaguzi pamoja na kuhakiki uzingatiaji wa matakwa ya leseni;
    1. Kudhibiti gharama, nauli na tozo mbalimbali za usafiri majini kwa kuzingatia Sheria na Kanuni ili kuhakikisha tozo hizo zinaleta ushindani katika soko;
    1. Kufanya ukaguzi wa meli za nje zinazokuja katika bandari za Tanzania Bara na meli zilizosajiliwa nchini ili kuhakikisha vyombo hivyo vinazingatia viwango vya ubora;
    1. Kuimarisha mifumo ya TEHAMA kwa ajili ya utoaji wa Vyeti vya Mabaharia;
    1. Kuweka mifumo thabiti ya kukabiliana na uchafuzi wa mazingira majini utokanao na meli;  
    1. Kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Usalama wa Vyombo Majini (Merchant

Shipping Act-2003);

  • Kusimamia utekelezaji wa Mikataba ya Kimataifa kuhusu Usafirishaji kwa njia ya Maji inayoratibiwa na Shirika la Bahari Duniani (International Maritime

Organization-IMO);

  • Uwakala wa ugomboaji wa shehena zilizoainishwa na Sheria ikiwa ni pamoja na madini, makinikia na mitambo inayotumika katika utafutaji na uchimbaji wa madini, bidhaa za petroli, nyara za Serikali na silaha;
    • Uwakala wa meli za mafuta, meli za kijeshi, meli za maonesho, meli za kitalii, na meli zilizokodishwa;
    • Kuhakiki shehena zinazoshushwa au kuingizwa melini kupitia katika bandari  nchini;
    • Kushirikisha wadau katika kufanya mapitio na marekebisho ya Sheria na

Kanuni mbalimbali; na xv. Kuimarisha mifumo na kukuza matumizi ya TEHAMA katika kudhibiti huduma za usafiri kwa njia ya maji na ufanyaji biashara ya meli.

  • Mheshimiwa   Spika,       katika        mwaka

2022/23, Kampuni ya Ubia kati ya Tanzania na China (SINOTASHIP) itaendelea kutoa huduma ya usafirishaji wa mizigo katika masafa marefu kwa njia ya bahari, kusimamia usalama wa mabaharia, mizigo na meli pamoja na kutoa huduma ya uwakala wa meli. Kazi

zitakazofanyika ni pamoja na:-

  1. Kuboresha ukusanyaji wa mapato ya Kampuni kutoka lengo la  Shilingi bilioni 15.48 mwaka 2021/22 hadi kufikia Shilingi bilioni 17.03 mwaka

2022/23;

  1. Kuongeza uwezo wa Kampuni kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi;
    1. Kuimarisha usalama wa meli na mizigo majini na maeneo yenye viashiria

hatarishi vya utekaji meli;

  1. Kuratibu shughuli zote za kusimamia meli za Kampuni ya Meli ya Serikali ya China (mshirika) zinazoleta mizigo katika bandari ya Dar-es salaam; na
    1. Kuratibu ukusanyaji na urudishwaji wa makasha yote yanayoleta na kuondosha mizigo kwa meli za mshirika hapa nchini.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/23, Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) itaendelea kutekeleza miradi ya ujenzi na ukarabati wa meli pamoja na kuboresha usalama wa abiria, mizigo na vyombo vya usafiri. Jumla ya Shilingi bilioni 113. 71 zimetengwa kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali ili kutekeleza kazi zilizopangwa katika kipindi hicho kama ifuatavyo:-
    • Kukamilisha ujenzi wa meli mpya ya MV. Mwanza Hapa Kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo katika ziwa Victoria;
    • Kujenga meli mpya (Container Vessel) yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 za mabehewa

ya mizigo katika Ziwa Victoria; 

  1. Kujenga meli mpya ya mizigo katika Ziwa Tanganyika yenye uwezo wa kubeba Tani 3,000 za mizigo ya makasha pamoja na chelezo ya kubeba meli yenye uwezo wa tani

4,000   iv.         Ujenzi wa meli mpya ya kubeba abiria 600 na tani 400 za mizigo katika Ziwa

Tanganyika; 

      v.        Kukarabati meli za MV Liemba, MV Umoja,

MT. Ukerewe, MT. Nyangumi na MT. Sangara;  vi. Kufanya ukaguzi wa kina (Comprehensive) kuhusu Meli ya MV Mwongozo ili iendelee kutoa huduma katika Ziwa Tanganyika;

  • Kufanya ukarabati wa boti moja (1) ya mwendokasi (Sea Warrios) kwa ajili ya kusaidia kazi za uokozi sambamba na usafirishaji wa watalii wanaotembelea kisiwa cha Gombe katika Ziwa Tanganyika; na
  • Kuendelea na ufungaji wa mifumo ya TEHAMA katika vituo vya Mwanza, Kigoma na Itungi.

467. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imetenga jumla Shilingi bilioni 100.11 fedha za nje kutoka Benki ya Dunia (WB) na Shilingi bilioni 650.00 kutoka vyanzo vya mapato vya ndani ya Mamlakakwa ajili ya kutekeleza kazi mbalimbali kama ifuatavyo:-

i. Kuendelea kuongeza kina na kupanua lango la kuingilia meli na eneo la kugeuzia meli (entrance channel and turning basin); kuboresha wa Gati Na. 8 – 11 na Gati Na.

12-15 katika Bandari ya Dar es Salaam; 

ii. Kufunga na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato na mifumo ya

TEHAMA; iii. Kuimarisha miundombinu ya reli ndani ya bandari kwa ajili ya kusafirisha mizigo kwa njia ya reli;

  1. Kuendelea na kazi za uboreshaji wa Bandari ya Tanga awamu ya pili inayohusisha ujenzi wa gati namba 1 na 2 zenye jumla ya urefu wa mita 450;
    1. Kukamilisha mradi wa kupanua na kuchimba lango la kuingilia na eneo la kugeuzia meli (entrance channel and turning basin) katika Bandari ya Tanga;
    1. Kuendelea na ujenzi wa Bandari Kavu ya

Kwala, Ruvu;

  • Kuendelea na ujenzi wa barabara inayounganisha gati jipya katika Bandari ya

Mtwara; viii. Kuendelea na ununuzi wa mitambo na vifaa mbalimbali kwa bandari zote ili kuboresha uwezo wa kuhudumia mizigo;

  1. Kuboresha Bandari za Mwanza Kusini, Mwanza Kaskazini, Bukoba na Kemondo kwa ajili ya kuongeza uwezo wa Bandari hizo kuhudumia meli kubwa zaidi katika

Ziwa Victoria; na

  • Kuendelea na ukamilishaji wa miradi ya uboreshaji wa bandari katika Maziwa ya Tanganyika.

468. Mheshimiwa        Spika,     katika       mwaka

2022/23,Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imetenga Shilingi bilioni 7.43 fedha kutoka vyanzo vyake vya ndani ili kusimamia ubora wa huduma za usafiri wa anga kulingana na viwango vya kimataifa vilivyowekwa na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (The International Civil Aviation Organization – ICAO). Aidha, TCAA inatoa leseni na kudhibiti utoaji wa huduma za usafiri wa anga; kuweka Viwango katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga na kusimamia, kukuza na kuendeleza shughuli za biashara ya usafiri wa anga ndani na nje ya nchi. Katika kufikia malengo hayo, kazi zitakazofanyika ni pamoja na:-

i. Kuendelea kuboresha mfumo wa mawasiliano kati ya rubani na waongoza ndege (VHF Area Cover Radios) katika viwanja vya Dar es salaam, Arusha, Tanga, Seronera, Manyara, Kilimanjaro, Mwanza, Kigoma, Mtwara, Songea, Gairo, Songwe,

Mbeya, Iringa na Tabora;  ii. Kuwajengea uwezo wataalamu wa kutumia mfumo mpya wa mawasiliano kati ya rubani na waongoza Ndege; 

iii. Maandalizi ya awali ya ujenzi wa Chuo cha

Kisasa cha Usafiri wa Anga;  iv. Kununua na kufunga vifaa vya kuongozea ndege (flight calibration) katika viwanja vya Ndege vya JNIA, AAKIA, KIA, Mwanza,

Tabora, Songwe, Dodoma na Pemba; 

v. Kukarabati jengo la TCAA makao makuu –

Dar es Salaam; vi. Kuendelea kuboresha shughuli za usajili wa ndege;

  • Kusimamia udhibiti wa usalama wa usafiri wa anga (Aviation Security) katika viwanja vya ndege, mashirika ya ndege pamoja na watoa huduma za usafiri wa anga;
  • Kushiriki katika mazungumzo na nchi nyingine duniani kwa ajili ya kuingia na kupitia upya mikataba ya usafiri wa anga;
  • Kusimamia na kudhibiti ubora wa viwanja vya ndege nchini;
  • Kuhakikisha matukio na ajali zinazotokana na usafiri wa anga zinapungua; xi. Kuendelea na juhudi za kutafuta fedha ili kuweza kufadhili wanafunzi wengi zaidi kwenye mafunzo ya urubani na uhandisi wa ndege;
  • Kushiriki kikamilifu katika jumuiya za kimataifa zinazohusu usafiri wa anga;
  • Kuimarisha uwezo wa Tanzania katika kusimamia sekta na kudhibiti usalama wa anga; na
  • Kuboresha miundombinu na vifaa vya kuongozea ndege.

469. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23,Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni  17.30 fedha za ndani za maendeleo kutoka Mfuko Mkuu wa Serikalikwa ajili ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ili kutekeleza yafuatayo:

  1. Uendeshaji wa Jengo la Tatu la Abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (TB III JNIA) unaohusisha matengenezo (preventive maintanance) ya mitambo na mifumo mbalimbali;
  2. Kufanya usanifu wa kina wa mfumo wa taa za kuongozea ndege katika Kiwanja cha

Kimataifa cha Julius Nyerere; iii. Kununua gari moja (1) la zimamoto kwa ajili ya Kiwanja cha Ndege cha Dodoma;

iv. Kufunga Mifumo ya kuhudumia Abiria katika Viwanja vya Ndege vya Mwanza,

Arusha, Songwe, Bukoba na Dodoma; 

  • Kujenga uzio wa usalama katika Kiwanja cha Ndege cha Dodoma; 
  • Upimaji na Upatikanaji wa Hati Miliki katika Viwanja vya Ndege mbalimbali ikiwemo Dodoma, Msalato, Songea, Lake Manyara,

Mwanza na Nachingwea; na vii. Kuendelea kutoa mafunzo kwa watumishi ili kuwaongezea ujuzi na weledi katika utendaji wao wa kazi.

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Kampuni ya Kuendeleza Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KADCO) imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 19.08 kutoka vyanzo vyake vya ndani. Katika kipindi hicho, KADCO imepanga kutekeleza miradi ifuatayo:-

i. Ujenzi wa kituo cha mafuta ya magari na mitambo (Petrol Station) pamoja na

Supermarket; ii. Upanuzi wa eneo la maegesho ya magari; iii. Kuimarisha kitengo cha kutoa huduma ya chakula kwenye ndege (Inflight Catering);

  1. Ununuzi wa mitambo ya zimamoto na uokoaji (fire Trucks); na
    1. Ukarabati wa jengo la mizigo.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23 Serikali imepanga kutumia jumla ya Shilingi bilioni 468.00 kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kutekeleza shughuli za Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kama ifuatavyo:-
  1. Kukamilisha malipo ya ununuzi wa ndege tano (5) mpya ambapo ndege moja (1) ni aina ya  Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili (2) aina ya Boeing 737-9, ndege moja (1) ya mizigo aina ya Boeing 767-300F na ndege moja (1) aina ya Dash 8 Q400;
    1. Kuendelea na ukarabati na ununuzi wa vifaa vya karakana za matengenezo ya ndege (Hangar) za JNIA na KIMAFA

(KIA);

  1. Gharama za awali za uendeshaji wa ndege tano (5) ambazo ni boeing 787 – 8, Boeing 737- 9 mbili (2), Boeing 767 –

300F na  Dash 8 Q400 (1);  iv. Kununua vifaa vya kuhudumia ndege

na abiria viwanjani; 

  • Ukarabati wa jengo la makao makuu ya ATCL na lililopo kiwanja cha ndege

cha JNIA Terminal I; 

  • Kuendelea na ukarabati wa nyumba 38

zilizopo Kilimanjaro;

  • Kujenga ghala la vifaa na vipuri vya ndege pamoja na kujenga eneo la mafunzo ya awali kwa wanaanga;
    • Kuendelea kulipa madeni ya ATCL

baada ya kazi ya uhakiki; na 

  1. Kukarabati na kujenga majengo ya kuhifadhia mizigo katika viwanja vya ndege vya JNIA, KIA na Songwe.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) itaendelea kutoa huduma za hali ya hewa kwa kuanzisha, kuendesha na kutunza vituo vya hali ya hewa pamoja na kudhibiti na kuratibu shughuli za hali ya hewa nchini Tanzania. Jumla ya Shilingi bilioni 20.00 fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi zifuatazo:

i. Kukamilisha malipo ya ununuzi wa rada mbili (2) zitakazofungwa katika viwanja vya ndege vya KIA na Dodoma; ii. Kununua rada tatu (3) kwa ajili ya kuimarisha upatikanaji wa taarifa ya hali ya hewa katika Maziwa Makuu na

Bahari ya Hindi; iii. Kuendelea na ujenzi wa maabara ya hali ya hewa na ufungaji wa mifumo husika;

  1. Kuendelea na ujenzi wa ofisi za hali ya hewa Dodoma na Kanda ya Mashariki; 
    1. Kufunga vifaa saidizi katika vituo vya hali ya hewa; na
      1. kuendelea na ujenzi wa jengo la utawala na hosteli katika Chuo cha Hali ya Hewa.

D.3  TAASISI ZA MAFUNZO

Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (Institute of

Construction  Technology – ICoT)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi Morogoro imepanga kudahili na kutoa mafunzo ya NTA level 4 kwa Wanafunzi 150 kwa Mtaala wa NACTE; kutoa mafunzo ya NTA level 5 kwa Wanafunzi 41; kutoa mafunzo ya NTA level 6 kwa wanafunzi 25; kudahili wanafunzi wapya 200 kwa mtaala wa VETA; kutoa mafunzo ya VET I kwa Wanafunzi 207; kutoa mafunzo ya VET II kwa wanafunzi 170 na kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali ya kozi za muda mfupi kwa washiriki 400 kuhusu Mafunzo ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi.
  • Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ICoT tawi la Mbeya, taasisi imepanga kutoa kozi nne (4) za matumizi ya Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi         katika        ujenzi,        ukarabati   na matengenezo ya barabara za changarawe. Aidha, Taasisi itatoa kozi moja (1) ya matumizi ya lami katika ujenzi wa barabara pamoja; kozi mbili (2) maalum za Teknolojia Stahiki ya Nguvukazi na mafunzo ya matumizi ya ”software” katika kufanya kazi za kihandisi.
  • Mheshimiwa Spika, kazi nyingine ni kuanza ujenzi wa majengo mawili mapya ya utawala kwa ajili ya ICoT Morogoro na Mbeya; ujenzi wa karakana mpya kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo; ujenzi wa maabara kwa ajili ya kufundishia fani za uhandisi ujenzi na TEHAMA na  ujenzi wa kumbi za mihadhara na maktaba ya kisasa. Vilevile, Taasisi itafanya ununuzi wa vitendea kazi na vifaa vya kufundishia, samani za Taasisi na  magari.

Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/23, Serikali imetenga Shilingi bilioni 1.00 kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali kwa ajili ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) ili kununua kifaa cha kufundishia (simulator).

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)

  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23,Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni 1.77 kutoka Mfuko Mkuu wa Seikali kwa ajili yaChuo cha Taifa cha

Usafirishaji (NIT) kutekeleza yafuatayo:

i. Ununuzi wa kifaa maalum cha mafunzo ya anga kwa wahudumu wa ndege (Full

Motion Cabin Crew Mock Up);  ii. Kununua ndege moja (1) yenye injini mbili (2) ya kufundishia marubani; 

  1. Kujenga kampasi kwa ajili ya kufundisha watalaamu wa bahari na mafuta/gesi

katika Mkoa wa Lindi; na 

  1. Kukamilisha ujenzi wa jengo la maktaba – NIT Mabibo.

D.3  MASUALA MTAMBUKA

  • Mheshimiwa   Spika,       katika        mwaka

2022/23, ili kufanikisha azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuzuia na kupambana na rushwa, Wizara kwa kushirikiana na taasisi zake imeandaa Mikakati ya Wizara ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wa Miaka Mitano (5) kuanzia 2021/22 hadi 2025/26. Aidha, mafunzo yanayohusu maadili na kuzuia vitendo vya rushwa yataendelea kutolewa kupitia semina na Mabaraza ya Wafanyakazi.

  • Mheshimiwa Spika, magonjwa yanayoambukizwa ya UKIMWI na UVIKO-19 pamoja na yasiyoambukizwa kama vile kisukari, bado ni tatizo kubwa kwa Taifa letu. Katika mwaka wa fedha 2022/23, Wizara itaendelea kutoa elimu kwa watumishi kuhusu mbinu za kujikinga na maambukizi mapya ya ugonjwa wa Ukimwi. Pia, Wizara itaendelea kuhimiza upimaji wa hiari wa VVU na magonjwa mengine yasiyoambukiza pamoja na kuhimiza ushiriki wa watumishi kwenye bonanza na michezo ikiwa ni njia mojawapo ya kuboresha afya za watumishi. Aidha, Wizara itaendelea kuhimiza watumishi wake kupata chanjo  dhidi ya UVIKO-19. 

E.       SHUKRANI

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2021/22, Wizara imepata ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali wakati ikitekeleza malengo yake. Ninapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wote walioshirikiana nasi kimawazo na kwa vitendo. Shukrani za pekee ziwaendee Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwa michango yao ambayo imesaidia katika kuimarisha huduma zitolewazo na Wizara. Ninawaomba Waheshimiwa Wabunge, wananchi na wadau mbalimbali waendelee na moyo huo katika mwaka wa fedha wa 2022/23 ili tuweze kuendeleza shughuli za Wizara hii ambazo ni muhimu katika kuchangia maendeleo ya nchi yetu.
  • Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii pia kutambua mchango mkubwa wa viongozi wenzangu katika Wizara nikianzia na Naibu Mawaziri, Mheshimiwa Godfrey Msongwe Kasekenya (Mb.) na Mheshimiwa Atupele Fred Mwakibete (Mb.); Makatibu Wakuu Bwana Gabriel Joseph Migire (Uchukuzi) na Balozi Mhandisi Aisha Salim Amour (Ujenzi); Naibu Makatibu Wakuu Bwana Ludovick  James Nduhiye (Ujenzi) na Dkt. Ally Saleh Possi (Uchukuzi).  Vilevile, kipekee napenda kuwashukuru Wakuu wa Idara,

Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara na Watumishi wote wa Wizara kwa jitihada zao katika utekelezaji wa Majukumu ya Wizara. 

  • Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kuwashukuru na kuwatambua Washirika mbalimbali wa Maendeleo ambao wamechangia katika utekelezaji wa Programu na Mipango mbalimbali ya Wizara. Napenda kuwatambua wafuatao: Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Majini (IMO), Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), OPEC Fund, Umoja wa Nchi za Ulaya, “Third World Organization for Women in Science (TWOWS)”, UNESCO, Benki ya Maendeleo ya

Afrika (AfDB), Benki ya Dunia (WB), Japan (JICA),

Korea Kusini (KOICA), Abu Dhabi Fund, Ujerumani (KfW), Uingereza (DFID), Uholanzi (ORIO), Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU), Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB), Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID), Kuwait (KFAED), Uturuki, HSBC, TMEA, Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sekretarieti ya Jumuiya ya Nchi za SADC, Nchi za Urusi, Afrika Kusini, Uingereza, Marekani, Uholanzi, Japan, India, China, Denmark, Norway, Ubelgiji, Ujerumani, Taasisi za fedha za CRDB, NSSF, PSSSF na TIB, Asasi zisizokuwa za Kiserikali; Sekta Binafsi pamoja na wengine wengi.

  • Mheshimiwa Spika, mwisho, nakushukuru tena wewe binafsi na Mhe. Naibu Spika. Hotuba hii pia inapatikana katika tovuti ya Wizara (www.mwt.go.tz).

F. MUHTASARI WA MAOMBI YA FEDHA YA WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI KATIKA

MWAKA WA FEDHA 2022/23

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/23, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inaomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 3,866,616,675,800.00 Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,465,835,235,800.00 ni kwa ajili ya

Sekta             ya           Ujenzi           na           Shilingi

2,400,781,440,000.00 ni kwa ajili ya Sekta ya Uchukuzi. Mchanganuo wa fedha zinazoombwa kwa kila Fungu ni kama ifuatavyo:

SEKTA YA UJENZI (FUNGU 98)

  • Mheshimiwa   Spika,      Shilingi

1,465,835,235,800.00 za Fungu 98 (Ujenzi) zinajumuisha Shilingi 44,293,050,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara (Ujenzi) na Taasisi ambapo Shilingi 40,638,652,000.00 ni za Mishahara ya Watumishi na Shilingi

3,654,398,000.00 ni za Matumizi Mengineyo.

Bajeti            ya         Maendeleo         ni          Shilingi

1,421,542,185,800.00 ambazo zinajumuisha Shilingi 1,168,576,368,800.00 fedha za ndani na Shilingi 252,965,817,000.00 fedha za nje.

Fedha za ndani zinajumuisha Shilingi 599,756,467,800.00 za Mfuko wa Barabara na Shilingi 568,819,901,000.00 za Mfuko Mkuu wa Serikali.

SEKTA YA UCHUKUZI (FUNGU 62)

  • Mheshimiwa Spika, Sekta ya Uchukuzi imetengewa jumla ya Shilingi 2,400,781,440,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya hizo, Shilingi 94,546,502,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo Shilingi 67,475,558,000.00 ni za Mishahara ya Watumishi na Shilingi 27,070,944,000.00 ni za Matumizi Mengineyo. Aidha, Miradi ya Maendeleo imetengewa Shilingi 2,306,234,938,000.00 Kati ya fedha hizo, Shilingi 2,192,771,622,000.00 ni fedha za Ndani na Shilingi 113,463,316,000.00 ni fedha za Nje.
  • Mheshimiwa Spika, pamoja na Hotuba hii, nimeambatanisha Miradi ya Wizara itakayotekelezwa katika mwaka wa fedha 2022/23 (Kiambatisho Na. 1-6) ikiwa ni pamoja na kiasi cha fedha kilichotengwa kutekeleza Miradi hiyo. Naomba viambatisho hivyo vichukuliwe kama sehemu ya vielelezo vya hoja hii. 
  • Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

KIAMBATISHO Na. 1

MGAWANYO WA FEDHA ZA BAJETI YA MAENDELEO KWA

MWAKA WA FEDHA 2022/23

KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
 SUBVOTE 1003: POLICY AND PLANNING DIVISION 
6267Institution Support 273.7460.00273.746GOT
 GrandTotal SUB VOTE 1003           273.7460.00273.746 
 SUBVOTE 2002: TECHNICAL SERVICES DIVISION 
4125Construction of Ferry Ramps 
   (i)To carry out expansion of Kigamboni ferry terminal. 429.670.00429.67GOT
(ii) To construct and rehebilitate ferry ramps at six (6) crossings (Magogoni – Kigamboni, Kilambo – Namoto, Utete – Mkongo, Iramba – Majita, Nyakarilo – Kome and Kasharu – Buganguzi. 569.480.00569.48GOT
(iii) To construct ferry infrastructure (waiting lounge, office and fences) for three (3) crossings (Kisorya – Rugezi, Nyakarilo – Kome, and Bugolora – Ukara).  332.220.00332.22GOT
iv) To construct new (Kayenze – Kanyinya, Muleba – Ikuza) ferry ramps. 300.000.00300.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
v)To construct four (4) new ferry ramps for Ijinga – Kahangala (Magu) and Bwiro – Bukondo (Ukerewe) crossings in Mwanza. 377.680.00377.68GOT
vi) To install and upgrade Electronic Ticketing System at five (5) ferry crossings (Magogoni – Kigamboni, Kigongo – Busisi, Kisorya – Rugezi, Pangani – Bweni and Ilagala – Kajeje). 507.580.00507.58GOT
(vii) To conduct monitoring and evaluation of ferry ramps activities. 68.890.0068.89GOT
Sub Total 2,585.520.002,585.52 
4139Procurement of Ferries
 (i)To procure one ferry to ply between Kisorya – Rugezi.  1,020.910.001,020.91GOT
(ii) To procure one new ferry to ply between Ijinga – Kahangala crossing.  584.710.00584.71GOT
(iii) To procure one ferry to ply between Bwiro – Bukondo 500.000.00500.00GOT
(iv) To procure one ferry to ply between Nyakarilo – Kome   500.000.00500.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
(v) To procure two ferries to ply between Nyamisati – Mafia and Buyagu – Mbalika crossing.  581.210.00581.21GOT
(vi) To procure tools for TEMESA workshops.  554.300.00554.30GOT
(vii) To procure one new ferry to ply between Magogoni – Kigamboni. 1,070.000.001,070.00 
(viii) To conduct monitoring and evaluation of ferries. 204.150.00204.15GOT
 Sub Total 5,015.280.005,015.28 
4144Rehabilitation of Ferries
 (i)  To complete rehabilitation of MV Musoma, MV Mara and MV TEMESA. 358.290.00358.29GOT
(ii) To rehabilitate MV Ujenzi.  380.310.00380.31GOT
(iii) To rehabilitate MV Kome II.  340.000.00340.00GOT
(iv) To complete rehabilitation of MV Misungwi.   2,121.130.002,121.13GOT
(v) To rehabilitate MV Nyerere. 600.000.00600.00GOT
(vi) To rehabilitate MV Kilombero II and demobilize it to Malinyi – Mlimba 400.000.00400.00GOT
(vii) To rehabilitate MV Kyanyabasa and MV Tanga 569.500.00569.50GOT
(viii) To rehabilitate MV Kitunda   268.450.00268.45GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
(ix) To rehabilitate MV Kazi and MV Magogoni 420.000.00420.00GOT
(x) To conduct monitoring and evaluation of ferries. 64.600.0064.60GOT
Sub Total 5,522.280.005,522.28 
6327Construction of Government Houses
 (i) To complete 5 construction of tied quarters for Judges residence in mainland Tanzania: Kilimanjaro -1, Mtwara -1, Shinyanga – 1 Kagera – 1 and Tabora -1 1,000.000.001,000.00GOT
(ii) To construct 20 houses for Government Leaders in Dodoma. 5,015.610.005,015.61GOT
(ii) To construct MoWT office block (Phase II). 11,043.6 90.0011,043.69GOT
(iii) To construct 150 houses for public Servants at Dodoma City. 6,936.970.006,936.97GOT
(iv) To construct apartments for Public Servants at Temeke Quarters. 6,928.990.006,928.99GOT
(iv) To construct apartments for Public Servants at Magomeni Quarters. 3,900.000.003,900.00GOT
(v) To procure furniture for State Lodges.  1,210.000.001,210.00GOT
(vi) To rehabilitate 40 Government 3,847.010.003,847.01GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
Leaders houses – Dodoma.      
(vii) To rehabilitate 30 Government Leaders houses in regions and maintenance of Magomeni Quarters. 3,000.000.003,000.00GOT
(viii) To rehabilitate 66 houses for Public Servants transferred to TBA from former CDA.  1,500.000.001,500.00GOT
(ix) To rehabilitate Public Servant houses to 20 regions transferred to TBA from TAMISEMI/NHC. 2,000.000.002,000.00GOT
(x) To facilitate capacity building to 62 Architects and 63 Quantity Surveyors professionals. 519.690.00519.69GOT
(xi) To Rehabilitate 12 workshops in Tabora, Mwanza, Arusha, Mtwara, Mbeya, Mt Depot, Kigoma, Mara, Ruvuma, Pwani, Dodoma and Vigunguti.  1,835.590.001,835.59GOT
(xii) To construct of five (5) new TEMESA workshops (Songwe, Simiyu, Geita, Njombe and Katavi) in newly established five (5) Regions.  1,671.400.001,671.40GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
(xiii) To construct new modern Dodoma workshop.  1,551.030.001,551.03GOT
(xiv) To rehabilitate Six (6) TBA furniture workshops in Arusha, Mwanza, Morogoro, Tabora, DSM and Mbeya.  2,450.080.002,450.08GOT
(xv) To establish district workshops in (Simanjiro, Masasi, Ukerewe, Chato, Mafia and Kyela.           945.060.00945.06GOT
(xvi) To facilitate preparation of Building Act, Building Code, Standards and Specifications for Government building. 1,200.000.001,200.00GOT
(xvii) To facilitate consultancy services for construction of MoWT office block (phase II). 862.500.00862.50GOT
(xviii) To facilitate design, supply, installation, testing and commissioning of Management System for mechanical, electrical and electronics. 1,500.000.001,500.00 
(xix) To conduct monitoring and evaluation of construction & maintenance 899.760.00899.76GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
projects for Government buildings as well as overseeing practical training for graduate Architects and Quantity Surveyors.     
 Sub Total 59,817.370.0059,817.37 
 Grand Total SUB VOTE 2002 72,940.450.0072,940.45 
 SUBVOTE 2005: ROADS DIVISION
4001Soni – Bumbuli – Dindira – Korogwe74.001,000.001,000.00GoT
4002Mtwara – Newala – Masasi
i) Mtwara – Mnivata Section 50.0010.000    10.00 GOT
ii) Mnivata – Tandahimba – Masasi Section160.001,000.00 10,000.00 11,000.00 GOT/Af DB
Sub–total210.001,010.000 10,000.000 11,010.00  
4003Likuyufusi – Mkenda (km 122.50) – ( Likuyufusi – Mhukuru Section –  km 60)122.507,500.00 –   7,500.00 GOT
4004Nachingwea – Liwale ( FS & DD)130.00500.000                –             500.00 GOT
4005Ubena Zomozi – Ngerengere
Ubena Zomozi – Ngerengere Jeshini – Ngerengere SGR Station  (Upgrading to bitumen standard)19.003,253.2413,253.241GOT
4006TAMCO – Vikawe – Mapinga24.003,820.003,820.00GOT
4007Makofia – Mlandizi 36.70600.000600.00GOT
4008Musoma – Makojo – Busekela       92.002,950.002,950.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4009Kongwa Jct – Mpwapwa- Gulwe- Kibakwe 98.001,088.001,088.00GOT
4010Muhutwe – Kamachumu – Muleba 54.001,200.001,200.00GOT
4011Iringa – Ruaha National Park104.001,000.001,000.00GOT
4012Muheza – Amani 36.001,700.001,700.00GOT
4013Mtwara – Mingoyo – Masasi (Rehabilitation)200.00550.000550.00GOT
4014Kibaoni – Majimoto – Muze – Kilyamatundu
(i) Kibaoni – Majimoto – Inyonga Section152.001,000.001,000.00GOT
(ii) Ntendo – Muze – Kilyamatundu (200 km) (Ntendo – Muze Section)37.006,160.006,160.00GOT
Sub–total189.007,160.007,160.00 
4015Kigongo – Busisi Bridge (J. P. Magufuli)  and its Approach Roads1No.7,000.07,000.00GOT
4016Mzinga Bridge1No.500.00500.00GOT
4017Ugalla Bridge 1No.500.00500.00GOT
4018Kitengule Bridge and Approach Roads (18km)1No.1,300.001,300.00GOT
4019Morogoro – Dodoma Road including Mkundi Bridge (FS & DD)260.00500.00500.00GOT
4020New Wami Bridge (Construction)1No.2,000.002,000.00GOT
4022Njombe – Makete – Isyonje Road
i) Njombe – Moronga Section53.9010.0010.00GOT
ii) Moronga – Makete Section53.501,600.001,600.000GOT
iii) Isyonje – Makete Road (Ipelele – Iheme Section)50.005,754.005,754.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
iv) Njombe  –  Njombe Referral Hospital (km 4)3.001,000.001,000.00GOT
Sub–total 8,364.008,364.000 
4023Omugakorongo – Kigarama – Murongo Road105.008,000.008,000.00GOT
4024Nanganga – Ruangwa – Nachingwea Road 
i) Masasi – Nachingwea 45.002,000.002,000.00GOT
ii) Nanganga – Ruangwa – Nachingwea, 100km; Lot 2: Nanganga – Ruangwa100.003,500.003,500.00GOT
iii) Nangurukuru – Liwale 50.001,500.00 1,500.00GOT
Sub–total145.007,000.000        –7,000.00 
4025Mpemba – Isongole Road51.2010.0010.00GOT
4026Ruanda – Iyula – Nyimbili Road 21.002,000.002,000.00GOT
4027Katumbasongwe – Kasumulu – Ngana – Ileje Road 90.105,000.005,000.00GOT
4028Uyogo – Nyamilangano – Nyandekwa – Kahama Road 500.00500.00GOT
4029Sengerema – Nyehunge – Kahunda Road (Sengerema – Nyehunge Section) 8,000.008,000.00GOT
4030Murushaka – Nkwenda – Murongo112.006,000.006,000.00GOT
4031Widening up of Dodoma Outer Roads Sections (Dodoma – Morogoro Road 70km; Dodoma – Iringa Road 50km; Dodoma – Singida220.00500.00500.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
 – 50km and Dodoma – Arusha Road 50km)     
4032Ntyuka Jct – Mvumi Hospital – Kikombo Junction76.074,600.004,600.00GOT
4033Tarime – Mugumu Road86.008,000.008,000.00GOT
4034Shelui – Nzega Road (FS & DD)110.00500.00500.00GOT
4035Nzega – Kagongwa65.00500.00500.00GOT
4036Isabdula (Magu) – Bukwimba Station – Ngudu – Ng’hungumalwa10.00500.00500.00GOT
4037Mafinga – Mgololo78.004,000.004,000.00GOT
4038Nyololo – Mtwango40.40500.00500.00GOT
4039Kongwa – Kibaya – Arusha430.002,500.002,500.00GOT
4040Singida – Sepuka – Ndago – Kizaga75.005,200.005,200.00GOT
4041Kitai – Lituhi including Mnywamaji Bridge 90.008,000.00 8,000.00GOT
4042Access Roads to SGR Stations
Morogoro – Kihonda SGR Station10.002,040.002,040.00GOT
Rudewa – Kilosa SGR Station3.00612.00612.00GOT
Gulwe – Gulwe SGR Station2.00408.00408.00GOT
Igandu – Igandu SGR Station27.005,508.005,508.00GOT
Ihumwa – Ihumwa Marshalling Yard5.501,122.001,122.00GOT
Access Roads to Dodoma SGR Station0.10200.00200.00GOT
Kizota – Zuzu SGR Station14.00612.00612.00GOT
Bahi – Bahi SGR Station4.00816.00816.00GOT
Mlandizi – Ruvu SGR22.004,488.004,488.00GOT
Sub–total 15,806.0015,806.00 
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
      
4101Tanga – Pangani – Makurunge
i)Tanga – Pangani Section50.003,000.003,000.000GOT
ii) Pangani Bridge1No.1,000.007,700.0008,700.00GOT/Af DB
iii) Pangani – Mkange section214.501,000.0017,354.00018,354.00GOT/Af DB
Sub–total174.505,000.0025,054.00030,054.000             
4102Kisarawe – Maneromango – Mloka (Kisarawe – Maneromango Section)54.002,780.002,780.00GOT
4103Geita – Bulyanhulu – Kahama 
i) Geita  –  Bulyanhulu  Jct Road58.301,000.001,000.00GOT
ii) Bulyanhulu Jct – Kahama Road61.701,000.001,000.00GOT
Sub–total120.002,000.0002,000.00 
4104Nyamirembe Port – Katoke Road
Nyamirembe Port – Katoke Road50.001,000.001,000.00GOT
Chato Ginery – Bwina Road8.10650.00650.00GOT
Sido – Chato Zonal Hospital5.30650.00650.00GOT
Sub–total63.402,300.002,300.00 
4105Geita – Nzera Road54.008,000.008,000.00GOT
 Sub–total54.008,000.00 8,000.00 
4106Arusha – Moshi – Himo – Holili
i)Sakina – Tengeru Section and Arusha bypass56.5110.0010.00GOT
ii) Tengeru – Moshi – Himo Section including Himo Weighbridge105.00500.004,000.004,500.00GOT/JI CA
iii) Kijenge – Usa River (Nelson Mandela AIST)    20.001,210.001,210.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
iv)Mianzini – Ngaramtoni18.002,740.002,740.00GOT
Sub–total199.514,460.000 4,000.00 8,460.00  
4107Access Roads to Rufiji Hydropower Project
i) Bigwa – Matombo – Mvuha – Kisaki – Rufiji Hydropower78.008,000.008,000.00GOT
ii) Ubena Zomozi – Mvuha – Kisaki – Mtemele Jct (FS & DD)178.00600.00600.00GOT
iii) Maneromango – Vikumburu – Mloka (Rehabilitation to gravel standard)100.00600.00600.00GOT
iv) Kibiti – Mloka – Mtemele – JNHHP203.00600.00600.00GOT
Sub–total559.009,800.009,800.00 
4108Dar es Salaam – Chalinze – Morogoro Express Way
i) Kibaha – Mlandizi – Chalinze – Morogoro Expressway 162.00500.00500.00GOT
ii) Backlog Rehabilitation of Mlandizi – Chalinze 44.00500.00500.00GOT
iii) Kwa Mathias (Morogoro Road) – Msangani 8.30700.00700.00GOT
iv) Improvement of Assorted Accident Blacksport (Coast) 10.0010.00GOT
v) Improvement of Assorted Accident Blacksport (Morogoro) 10.0010.00GOT
vi) Vigwaza OSIS Phase I & II1No10.0010.00GOT
vii) Msoga – Msolwa (Chalinze Bypass)10.001,000.00 1,000.00GOT
Sub–total179.932,730.0002,730.00 
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4109Wazo Hill – Bagamoyo – Msata
i)Wazo Hill – Bagamoyo – Msata (Tegeta – Bagamoyo Section)46.901,200.001,200.00GOT
ii) Mbegani – Bagamoyo7.20500.00500.00GOT
Sub–total54.101,700.001,700.00 
4110Usagara – Geita –Buzirayombo – Kyamyorwa
Uyovu – Bwanga – Biharamulo  (Lot 1 & Lot 2)110.0010.0010.00GOT
Sub–total 110.0010.00010.00 
4111Nyakahura – Kumubuga – Rulenge – Kabanga Nickel road (FS & DD)
i) Nyakahura – Kumubuga – Murusagamba road 34.001,000.001,000.00GOT
ii)Kumubuga – Rulenge – Murugarama 75.001,000.001,000.00GOT
iii)Rulenge – Kabanga Nickel road 32.001,000.001,000.00GOT
Sub – total141.003,000.003,000.00 
4112Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora
i) Uvinza – Malagarasi Road51.10300.006,515.006,815.00GOT/ OPEC/ ABUDH ABI
ii) Tabora – Ndono Road42.0010.0010.00GOT
iii) Ndono – Urambo Road52.0010.0010.00GOT
iv)Urambo – Kaliua – Ilunde – Uvinza Road (Kaliua – Kazilambwa Section)56.0010.0010.00GOT
v) Urambo – Kaliua – Ilunde – Uvinza  Road (Urambo – Kaliua section)28.0010.0010.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
vi) Urambo – Kaliua – Ilunde – Uvinza  Road (Kazilambwa – Chagu section)36.00300.0011,000.0011,300.00GOT/ OPEC
Vii) Urambo Round About 300.00 300.00GOT
Sub–total209.10940.0017,515.0018,455.00 
4113Ifakara – Kihansi – Mlimba – Madeke – Kibena (Njombe)
i) Ifakara – Kihansi Section50.008,000.008,000.00GOT
ii) Kibena – Lupembe – Madeke 130.00500.00500.00GOT
ii) Kihansi – Mlimba – Taweta – Madeke – Lupembe – Kibena 220.0055.001,650.001,705.00GOT/ AfDB
Sub–total400.008,555.001,650.0010,205.00 
4114Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (389 km)389.008,000.008,000.00GOT
4115Marangu –Tarakea  – Rongai – Kamwanga/ Bomang’ombe – Sanya Juu
i) Marangu – Rombo Mkuu – Tarakea64.0010.0010.00GOT
ii) Sanya Juu – Kamwanga (Sanyajuu – Alerai section)32.2010.0010.00GOT
iii)Sanya Juu – Kamwanga (Alerai – Kamwanga Section)44.002,000.00 2,000.000GOT
iv) Bomang’ombe – Sanya Juu25.001,000.001,000.00GOT
v) KIA – Mererani 26.0010.0010.00GOT
vi) Kwa Sadala – Masama – Machame Junction16.00900.00900.00GOT
vii) Kiboroloni – Kiharara – Tsuduni – Kidia 10.80900.00900.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
viii) Tarakea – Holili 53.001,000.001,000.00GOT
Sub–total271.005,830.000 –   5,830.00  
4116Tukuyu – Mbambo – Katumba 
i) Bujesi – Mbambo section26.001,000.001,000.00GOT
ii) Tukuyu – Mbambo section34.601,600.001,600.00GOT
iii) Mbambo – Ipinda (FS & DD)19.70100.00100.00GOT
Sub – total80.302,700.00 2,700.00 
4118Dodoma – Manyoni Road (Incl. Manyoni Access Road) 
Manyoni One Stop Inspection Station – OSIS1No55.0055.00GOT
Sub total 55.00 55.00 
4119Tabora – Mambali – Bukene – Itobo114.00500.00500.00GOT
4121Namanyere – Katongoro – New Kipili Port (FS & DD)64.80385.00385.00GOT
4123Dumila – Kilosa – Mikumi 
i) Dumila – Rudewa Section45.0010.0010.00GOT
ii) Rudewa – Kilosa Section24.001,000.001,000.00GOT
iii) Kilosa – Ulaya – Mikumi72.001,300.001,300.00GOT
Sub–total141.002,310.002,310.00 
4124Sumbawanga – Matai – Kasanga Port 
i) Sumbawanga – Matai – Kasanga Port Road107.0010.0010.00GOT
ii) Matai – Kasesya Road50.008,000.008,000.00GOT
Sub–total157.008,010.008,010.00 
4126Construction of Bridges 
i) Kirumi Bridge (Rehabilitation)1No.700.00700.00GOT
ii) Sibiti Bridge (Construction)1No.1,000.001,000.00GOT
iii) Magufuli (Kilombero) Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
iv) Ruhuhu Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
v) Momba Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
vi) Sukuma Bridge (Construction)1No.700.00700.00GOT
vii) Simiyu Bridge (Design & Construction)1No.700.00700.00GOT
Viii) Mara Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
ix) Mtera Dam Bridge 1No.500.00500.00GOT
x) Magara Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
xi) Lukuledi Bridge (Construction)1No.10.0010.00GOT
xii) Lower Malagarasi Bridge (FS & DD)1No.500.00500.00GOT
xiii) Msingi Bridge (Construction)1No.540.00540.00GOT
xiv) Steel Bridge Emergency Parts1No.300.00300.00GOT
xv) Godegode Bridge (Design & Construction)1No.1,000.001,000.00GOT
xvi) Mitomoni Bridge 1No.300.00300.00GOT
xvii) Mkenda Bridge (Construction)1No.300.00300.00GOT
xviii) Mirumba Bridge (Design Review & Construction)1No.900.00900.00GOT
xix) Sanza Bridge (Construction)1No.900.00900.00GOT
xx) Kiegeya Bridge1No.10.0010.00GOT
xxi) Lower Mpiji Bridge (Construction)1No.1,600.001,600.00GOT
xxii) Nzali Bridge1No.600.00 600.00GOT
xxiii) Kibakwe Bridge 1No.600.00 600.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
xxiv) Mpwapwa Bridge 1No.600.00 600.00GOT
xxv) Kerema Maziwa Bridge 1No.600.00 600.00GOT
xxvi) Munguli Bridge 1No.600.00 600.00GOT
Sub–total1No.13,010.0013,010.00 
4127New Bagamoyo (Kawawa Jct – Tegeta)
Widening  of  Morocco  – Mwenge4.3010.0010.00GOT
Sub–total4.3010.00010.00 
4128Kyaka – Bugene – Kasulo  
i) Kyaka – Bugene Section59.1010.0010.00GOT
ii) Kumunazi – Bugene – Kasulo and Kyaka – Mutukula (Bugene – Burigi Chato National Park section – km 60) 124.006,000.006,000.00GOT
Sub–total183.106,010.006,010.00 
4129 Isaka – Lusahunga 
i) Ushirombo – Lusahunga (Rehabilitation)110.0010.0010.00GOT
ii) Lusahunga – Rusumo  92.00500.0015,199.0015,699.00GOT/I DA
iii) Nyakasanza – Kobero58.00500.00 500.00GOT
iv) Nyakanazi One Stop Inspection Station (OSIS)1No.55.0055.00GOT
Sub–total260.001,065.0015,199.0016,264.00 
4130  Manyoni – Itigi – Tabora
 (i) Tabora – Nyahua Section85.0010.0010.00GOT
(ii) Nyahua – Chaya Section85.4010.001,000.0001,010.00GOT/  KUWAIT
(iii) Manyoni – Itigi – Chaya Section89.3510.0010.00GOT
Sub–total259.7530.001,000.001,030.00     
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4132Regional Roads Rehabilitation (26 Regions)734.5961,585.0061,585.00GOT
4133Mwanza – Shinyanga/Mwan za  Border road Rehabilitation (FS&DD)102.00385.00385.00GOT
4138De–congestion of DSM Roads
 i) Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana14.0010.0010.00GOT
ii) Tegeta – Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi (Moro Rd); Mbezi Mwisho – Goba Section7.0010.0010.00GOT
iii) Tangi Bovu – Goba 9.0010.0010.00GOT
iv) Kimara Baruti –  Msewe – Changanyikeni2.6010.0010.00GOT
v) Kibamba – Kisopwa – Kwembe – Makondeko 4.00900.00900.00GOT
vi) Banana – Kitunda – Kivule – Msongola14.7010.0010.00GOT
vii) Ardhi – Makongo – Goba (Goba – Makongo Section: 4km)4.0010.0010.00GOT
viii) Ardhi – Makongo – Goba (Ardhi – Makongo Section: 5km)5.00825.00825.00GOT
ix) Widening of Mwai – Kibaki Road9.10900.00900.00GOT
x) Kongowe – Mjimwema – Kivukoni Ferry Road (One Lane Widening) 25.10900.00900.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
xi) Mjimwema – Kimbiji – Pembamnazi27.00900.00900.00GOT
xii)Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road (Mbezi Mwisho); Wazo Hill (Madale) – Goba Section 5.0010.0010.00GOT
xiii) Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road (Mbezi Mwisho); Wazo Hill – Madale Section6.0010.0010.00GOT
xiv) Goba – Matosa – Temboni6.00600.00600.00GOT
Sub–total138.505,105.005,105.00 
4141 Nyamuswa – Bunda – Kisorya 
i) Kisorya – Bulamba section51.0010.0010.00GOT
ii) Nyamuswa – Bunda – Bulamba section56.42,000.002,000.00GOT
Sub – total107.402,010.002,010.00 
4142  Kolandoto – Lalago – Ng’oboko – Mwanhuzi 
i) Kolandoto – Lalago62.001,000.001,000.00GOT
ii) Lalago – Ng’oboko – Mwanhuzi60.001,000.001,000.00GOT
Sub – total122.002,000.002,000.00 
4143Ndundu – Somanga
i) Ndundu – Somanga60.00500.00500.00GOT
ii) Utete – Nyamwage 300.00 300.00GOT
iii) Ikwiriri – Mkongo95.00300.00 300.00GOT
iv) Kongowe –  Malendego  160.5500.00500.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
v) Nangurukuru – Mbwemkuru95.00500.00500.00GOT
Sub – total 2,100.0002,100.00 
4145Kasulu – Manyovu
Kasulu – Manyovu including Kasulu Town Links68600.0011,400.0012,000.00GOT/Af DB
Sub – total68600.0011,400.0012,000.00 
4146 Dodoma  City Outer Dual Carriageway Ring Road Lot 1 & 2 
(i) Lot 1: Nala – Veyula – Mtumba  – Ihumwa Dry Port Section52.30800.00 15,400.0016,200.00 GOT/Af DB
(ii) Lot 2: Ihumwa Dry Port – Matumbulu – Nala Section60.00800.0016,500.00017,300.00GOT/Af DB
(iii) Improvement of Dodoma City Roads ( Dodoma Inner Ring Roads: Bahi R/Abount – Image R/About – Ntyuka R/About  – Makulu R/About)) 6.301,000.001,000.00GOT
iv) Dodoma City Middle Ring Road: Nanenane – Miyuji – Mnadani  Sekondari – Mkonze – Ntyuka – Nanenane 47.201,000.001,000.00GOT
(v) Rehabilition of Kikombo Jctn –  Chololo – Mapinduzi (JWTZ HQ) Road18.001,300.001,300.00GOT
Sub – total183.804,900.0031,900.0036,800.00 
4147 Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea
i) Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea ( Forest – Londo – Kitanda)  396.001,000.001,000.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
ii) Mikumi – Kidatu – Ifakara (Kidatu – Ifakara Section- 68km)103.00600.00600.00GOT/E U/USAI D/UKAi d
iii) Chalinze – Magindu – Lukenge – Seregete B – Kabwe Jct – Mkulazi 77.50200.00 200.00GOT
iv) Dakawa Jct – Mbigiri 7.002,800.00 2,800.00GOT
Sub–total583.504,600.004,600.00 
4148 Tabora – Ipole – Koga – Mpanda      
i) Tabora (Usesula) – Koga – Mpanda; Lot 1: Usesula –  Komanga Section 115.5010.002,256.002,266.00GOT/Af DB
ii) Tabora (Usesula) – Koga – Mpanda; Lot 2: Komanga  – Kasinde Section 112.1810.001,871.001,881.00GOT/Af DB
iii) Tabora (Usesula) – Koga – Mpanda; Lot 3: Kasinde – Mpanda Section 107.6810.001,743.001,753.00GOT/Af DB
iv) Tabora – Sikonge (Usesula)30.0010.0010.00GOT
Sub–total365.3640.005,870.005,910.00 
4149 Makutano – Natta – Mugumu/Loliondo – Mto wa Mbu 
i) Makutano – Natta – Mugumu (Makutano – Sanzate Section)50.0010.00 –   10.00 GOT
ii) Makutano – Natta – Mugumu (Sanzate – Natta Section) 40.002,000.00 –   2,000.00 GOT
iii) Makutano – Natta – Mugumu (Natta – Mugumu Section)     45.00500.00 500.00 GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
iv) Loliondo – Mto wa Mbu (Waso – Sale Jct Section) 50.0010.00 10.00 GOT
Sub–total185.002,520.002,520.00 
4150 Ibanda – Itungi Port
i) Rehab. Ibanda – Itungi 26.004,180.004,180.00GOT
ii) Kikusya – Ipinda – Matema  (Tenende-Matema) 39.1010.0010.00GOT
iii) Iponjola – Kiwira Port6.00500.00500.00GOT
iv) Songwe/Kasumul u – Tanzania/Malawi Boarder OSBP1No.1,000.001,000.00GOT
v) Rehab. Uyole – Kasumulu ( Ilima Escarpment section)3.0010.0010.00GOT
Sub–total74.105,700.005,700.00 
4152 Nzega – Tabora Road 
i) Nzega – Puge Section58.6010.0010.00GOT
ii) Puge – Tabora Section56.1010.0010.00GOT
Sub–total224.7020.0020.00 
4154Sumbawanga – Mpanda – Nyakanazi Road
i) Sumbawanga – Kanazi  Section75.0010.0010.00GOT
ii) Kanazi – Kizi – Kibaoni  Section76.6010.0010.00GOT
iii) Sitalike– Mpanda  Section36.0010.0010.00GOT
iv) Mpanda – Mishamo – Uvinza (Mpanda – Ifukutwa  – Vikonge Section) 37.6510.0010.00GOT
v) Mpanda – Mishamo – Uvinza  (Vikonge – Uvinza Section)  159.008,000.008,000.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
vi) Kibaoni – Sitalike Section71.008,140.008,140.00GOT
vii) Kizi – Lyambalyamfipa – Sitalike86.31200.00200.00GOT
viii) Kagwira – Ikola – Karema Port112.002,000.002,000.00GOT
ix) Lyazumbi – Kabwe65.001,220.00 1,220.00GOT
Sub–total718.5619,600.0019,600.00 
4155Nyanguge – Musoma/ Usagara – Kisesa Bypass
i) Nyanguge – Simiyu/Mara Border100.40500.00500.00GOT
ii) Simiyu /Mara Border – Musoma85.5010.0010.00GOT
iii) Usagara – Kisesa (Mwanza Bypass)16.3510.0010.00GOT
iv) Widening of Mwanza CBD – Mwanza Airport Road and Construction of Furahisha Pedestrian Crossing Bridge12.0010.0010.00GOT
Sub–total214.25530.00530.00 
4160Magole – Mziha – Handeni 
i) Magole – Turiani 45.2010.0010.00GOT
ii) Turiani – Mziha – Handeni (104km)104.001,000.001,000.00GOT
Sub–total149.201,010.001,010.00 
4161Dar es Salaam Road Flyovers and Approaches
i) Ubungo Interchange1No.10.0001,000.0001,010.00GOT/I DA
ii) Improvement of Intersections/Jun ctions at KAMATA, Magomeni, Mwenge,  Tabata/ Mandela, Selander (Ali Hassan8Nos.500.00500.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
Mwinyi/ UN Roads JCT), Mbezi Mwisho, Buguruni and Morocco in Dar es Salaam ( DD review)     
iii)Mabey Flyovers in DSM, Dodoma and Mwanza3Nos.60.0060.00GOT
Sub–total 570.001,000.001,570.00 
4162   Mwigumbi – Maswa – Bariadi – Lamadi
i) Mwigumbi – Maswa50.3010.0010.00GOT
ii) Maswa – Bariadi49.7010.0010.00GOT
iii)Maswa Bypass Road11.01,200.001,200.00GOT
Sub–total111.001,220.001,220.00 
4163Tabora – Ipole – Rungwa (Ipole – Rungwa section 172.00650.00650.00GOT
4164Kidahwe – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi
i) Kidahwe – Kasulu63.0010.0010.00GOT
ii) Nyakanazi – Kakonko (Kabingo)50.0010.0010.00GOT
iii) Kanyani Junction – Mvugwe 70.501,000.0014,776.0015,776.00GOT/Af DB
iv) Mvugwe – Nduta Junction. 59.351,000.0014,776.0015,776.00GOT/Af DB
v) Nduta Junction – Kabingo62.501,000.0014,776.0015,776.00GOT/Af DB
vi) Nduta Junction – Kibondo 25.902,000.002,000.00GOT
vii) Kibondo – Mabamba 48.008,000.008,000.00GOT
Sub total379.2513,020.0044,328.0057,348.00 
4165Mafia Airport Access Road 
 Mafia Airport Access Road16.0010.0010.00GOT
 Kilindoni – Rasimkumbi54.41,000.00 1,000.00 
 Sub-Total70.41,010.00 1,010.00 
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4167Nyerere (Kigamboni) Bridge Construction and Its Approach Roads 
i) Nyerere (Kigamboni) Bridge1No.10.0010.00GOT
ii) Nyerere (Kigamboni) Bridge – Vijibweni Road1.5010.0010.00GOT
iii) Tungi – Kibada Road 3.8010.0010.00GOT
iv) Kibada – Mwasonga – Tundwisongani Jct/Tundwisonga ni – Kimbiji41.006,880.006,880.00GOT
Sub–total46.306,910.006,910.00 
4168Mutukula – Bukoba – Muhutwe – Kagoma (FS&DD)
i)Mutukula – Bukoba – Muhutwe – Kagoma (FS&DD)136.00200.00200.00GOT
(ii) Bukoba  Mjini – Busimbe – Maluku – Kanyangereko – Ngongo (FS & DD)19.10200.00200.00GOT
(iii) Kanazi (Kyetema) – Ibwera – Katoro – Kyaka 2 (FS & DD)60.70200.00200.00GOT
Sub–total215.80600.00600.00 
4170Support to Road Maintanance and Rehabilitation (Roads Fund) 599,756. 4678599,756.4678     GOT
4172Providing lane enhancement including climbing lanes, passing bays, rest and emergency lay bays on Central Corridor 300.00300.00GOT
4174Widening of Kimara – Kibaha road (19.2km) including19.202,000.002,000.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
 Widening of Kibamba, Kiluvya and Mpiji Bridges      
4175Upgrading of Kisarawe – Mlandizi119.00770.00770.00GOT
4178Upgrading of Pugu – Bunju (Outer Ring Road)
i) Upgrading of Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho road to 6 lanes dual carriageway (FS & DD)12.710200.00200.00GOT
ii) Upgrading of Mbezi Mwisho – Mpiji Magoe – Bunju road to 6 lanes dual carriageway (FS & DD)21.30200.00200.00GOT
Sub–total34.00400.00400.00 
4181Kagoma – Lusahunga 
 Muleba – Kanyambogo – Rubya18.5010.0010.00GOT
Sub–total18.5010.0010.00 
4184Singida – Shelui
i) Singida – Shelui Road (FS&DD)110.00500.00500.00GOT
ii) Ulemo – Kinampanda – Gumanga (Singida) – Mkalama46.00500.00 500.00GOT
Sub–total156.001,000.001,000.00 
4185 D’Salaam – Mbagala Road Upgrading (Kilwa Road) Lot 3 
i) Widening of Gerezani Bridge1.3055.001,655.001,710.00GOT/  JICA
ii) Mbagala Rangi Tatu – Kongowe3.8500.00500.00GOT
Sub–total5.10555.001,655.002,210.00 
4186 Msimba – Ruaha Mbuyuni / Ikokoto – Mafinga (TANZAM) (Rehab.)  
i) Mafinga – Igawa  137.9010.0010.00GOT
ii) Rujewa – Madibira –152.00330.00330.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
Mafinga (152km)     
iii) Strengthening of Morogoro – Iringa (Tumbaku Jctn – Mangae/Melela – Mikumi – Iyovi section) rehabilitation158.45200.00200.00GOT
Sub–total158.45540.000540.00 
4187Same – Mkumbara – Korogwe (Rehabilitation)
i) Same – Himo 76.00300.00300.00GOT
ii) Mombo – Lushoto32.00300.00300.00GOT
iii) Lushoto – Magamba – Mlola 34.50300.00300.00GOT
iv) Same – Kisiwani – Mkomazi  (97km): Same – Kisiwani Section97.008,000.008,000.00GOT
Sub–total240.108,900.008,900.00 
4188Mbeya – Makongolosi – Mkiwa Road
i) Mbeya – Lwanjilo36.0010.0010.00GOT
ii) Lwanjilo – Chunya 36.0010.0010.00GOT
iii) Chunya – Makongolosi 39.0010.0010.00GOT
iv) Noranga – Itigi – Mkiwa56.908,000.008,000.00GOT
v) Mbalizi – Makongolosi56.00750.00750.00GOT
vi) Makongolosi – Rungwa – Noranga -356km (Makongolosi – Rungwa Section)356.00800.00800.000GOT
vii) Itigi Township roads10.001,900.001,900.00GOT
Sub–total589.9011,480.00        –11,480.00         
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4190  Itoni – Ludewa – Manda 
i) Lusitu – Mawengi Section50.002,000.002,000.00GOT
ii) Itoni – Lusitu Section50.008,000.008,000.00GOT
Sub–total100.0010,000.00        –10,000.00 
4191New Selander Bridge (Tanzanite Bridge)1No.10.0010.00GOT      
4193 Handeni – Kibirashi – Kibaya – Singida  
Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba Kwa Mtoro – Singida 460 km (Handeni – Kibirashi Section )50.008,000.008,000.00GOT
Sub–total50.008,000.008,000.00 
4194Makambako – Songea  
Makambako (Lwangu) – Songea 295.00500.00500.00GOT
Songea Bypass11.00200.00 200.00GOT
Ramadhani – Ilembula Hospital – Iyayi75.00300.00 300.00GOT
Sub–total381.001,000.00 –   1,000.00  
4195 Dodoma – Iringa  
i) Iringa Bypass7.30400.00400.00GOT
ii) Weighbridge along Iringa – Dodoma Road1No10.0010.00GOT
iii) Strengthening of Iringa – Dodoma266.00500.00500.00GOT
Sub–total273.30910.000910.00 
4196 Dodoma – Babati  
i) Dodoma – Mayamaya   43.6510.0010.00GOT
ii) Mayamaya – Mela99.3510.0010.00GOT
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
iii) Mela – Bonga88.8010.0010.00GOT
iv) Babati Bypass 12.00120.00120.00GOT
v) Dongobesh – Dareda60.002,000.00 2,000.00GOT
vi) Magara Escarpment3.00150.00150.00GOT
Sub–total306.82,300.002,300.00 
4197 Masasi – Songea – Mbamba Bay
i) Namtumbo – Kilimasera60.0010.0010.00GOT
ii) Kilimasera – Matemanga68.2010.0010.00GOT
iii) Matemanga – Tunduru59.0010.0010.00GOT
iv) Mbinga – Mbamba Bay66.0010.003,000.003,010.00GOT/Af DB
Sub–total343.2040.003,000.003,040.00 
4198Access Road to Uongozi Institute8.80200.00200.00 
4199 Igawa – Songwe – Tunduma and Mbeya Bypass 
i) Igawa – Songwe – Tunduma (Widening of Uyole – Ifisi section to dual carriageway)298,500.00 08,500.00GOT
ii) Uyole – Songwe (Mbeya Bypass)40.00500.000500.00GOT
iii) Iwambi – Mbalizi Bypass (upgrading to bitumen std)6.50500.000500.00GOT
Sub–total75.59,500.000        –9,500.00 
4285  Bus Rapid Transport Programme
i) Bus Rapid Transit (BRT) Infrastructure (Phase II): Kilwa Road corridor from CBD to Mbagala20.355.0032,000.0032,055.00GOT/Af DB
ii) Bus Rapid Transit (BRT) Infrastructure Phase III : Nyerere Road corridor23.3330.0012,947.49712,977.50GOT/I DA
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
from CBD to Gongolamboto      
iii) Bus Rapid Transit (BRT) Infrastructure Phase IV Alli Hassan Mwinyi – Morocco – Mwenge Tegeta; Mwenge Ubungo Roads 30.1230.003,300.003,330.00GOT/I DA
iv) Improvement of BRT Infrastructures (Phase I: Kimara – Kivukoni) – Jangwani Area1No.700.00700.00GOT
v) Bus Rapid Transit (BRT) Infrastructure (Phase V):  250.00250.00GOT/ AFD
Sub–total73.751,065.0048,247.49749,312.50 
6304Construction of Institute of Construction Technology (ICOT) Headquarters Building (Desig and Build)1No.1,500.001,500.00GOT
6383 Construction of TANROADS HQ (Design & Construction)  
 i) Construction of TANROADS HQ (Design & Build)1No.1,800.00–   1,800.00 GOT
ii) Construction of TANROADS Regional Managers’ Offices (Dar es Salaam, Katavi, Geita, Simiyu, Njombe, Lindi and Songwe)7Nos.100.00 –   100.00 GOT
Sub–total 1,900.00 –   1,900.00  
 TOTAL Subvote 2005 1,038,622.708 221,818.497 1,260,441.206            
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
 SUBVOTE 5002: SAFETY AND ENVIRONMENT UNIT 
4136Road Safety Activities 1,648.80 00.001,648.800GOT
6221Institution to Support Road Safety and Environment 16.0480.0016.048GOT
6571EMA Implementation Support Programme 119.4000.00119.400GOT
 TOTAL Subvote 5002 1,784.258     0.001,784.258 
 SUBVOTE 6001: AIRPORTS CONSTRUCTION UNIT   
4156Construction of Kigoma Airport 
 Upgrading and Rehabilitation of Kigoma Airport Phase II 4,598.003,032.907,630.90GOT/ EIB
Sub Total 4,598.003,032.907,630.90 
4158Construction of Mpanda Airport  
 Upgrading and Rehab. of Mpanda Airport  12.100.0012.10GOT
Sub Total 12.100.0012.10 
4159Construction of Tabora Airport 
 Upgrading and Rehabilitation of Tabora Airport Phase III 662.423,032.903,695.32GOT/ EIB
Sub Total 662.423,032.903,695.32 
4206Construction of Songwe Airport 
 Construction of New Songwe Airport Phase III 4,105.7104,105.71GOT
Construction of New Songwe Airport Phase IV 6,000.7506,000.75GOT
Sub Total 10,106.46        010,106.46 
4209Construction of Mwanza Airport 
 Upgrading of Mwanza Airport (LOT 3) 5,300.480.005,300.48GOT
Sub Total 5,300.480.005,300.48 
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
4210Construction of Arusha Airport 
Rehabilitation and Upgrading of Arusha Airport   242.020.00242.02GOT
Sub Total 242.020.00242.02 
4220Construction of Mtwara Airport 
Rehabilitation and Upgrading of Mtwara Airport Phase I 4,947.790.004,947.79GOT
Sub Total 4,947.790.004,947.79 
4221Construction of Sumbawanga Airport  
Upgrading and Rehabilitation of Sumbawanga Airport  660.003,032.903,692.90GOT/ EIB
Sub Total 660.003,032.903,692.90 
4222Construction of Shinyanga Airport   
Upgrading and Rehabilitation of Shinyanga Airport  660.003,032.903,692.90GOT/ EIB
Sub Total 660.003,032.903,692.90 
4226Development of Regional Airports   
Construction of New Geita Region Airport 2,689.960.002,689.96GOT
Upgrading and Rehabilitation of Iringa Airport 5,341.50322.005,663.51GOT/ WB
Upgrading and Rehabilitation of Musoma Airport 5,276.400.005,276.40GOT
Upgrading and Rehabilitation of Songea Airport 4,425.720.004,425.72GOT
Upgrading and Rehabilitation of Dodoma Airport 12.100.0012.10GOT
Upgrading and Rehabilitation of Tanga Airport 96.80107.00203.80GOT/ WB
Upgrading and Rehabilitation of Lake Manyara Airport 330.0066.00396.00GOT/ WB
KasmaJina la MradiUrefu (km)Bajeti kwa Mwaka 2022/23 (Shilingi Milioni)Chanzo cha  Fedha
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
Upgrading and Rehabilitation of Lindi Airport 2,494.860.002,494.86GOT
Construction of New Simiyu Airport 55.040.0055.04GOT
Upgrading and Rehabilitation of Moshi Airport 2,530.930.002,530.93GOT
Rehabilitation and Upgrading of other regional Airports 2,531.080.002,531.08GOT
Sub Total 25,784.40 495.0026,279.40 
4286Construction of Msalato Airport
Construction of the New Greenfield Airport at Msalato (Phase 1-Lot1) 1,915.0018,520.7220,435.72GOT/ AfDB
Sub Total 1,915.0018,520.7220,435.72   
4287Construction of Bukoba Airport 
Rehabilitation and Upgrading of Bukoba Airport Phase I & II 12.100.0012.10GOT
Sub Total 12.100.0012.10 
4289Construction of Terminal III at JNIA 
Complete with associated infrustructures and facilities.   39.910.0039.91GOT
Rehabilitation and Expansion of Terminal II Building including associated facilities at JNIA  14.4360.0014.436GOT
Sub Total 54.3460.0054.346 
 Total Sub Vote 6001 54,955.20631,147.32086,102.526 
      

                   GRAND TOTAL                                1,168,576.368 252,965.817 1,421,542.185 

KIAMBATISHO NA. 2

MCHANGANUO WA MIRADI YA BARABARA ZA MIKOA INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO MKUU WA SERIKALI (KASMA 4132) KWA MWAKA WA

FEDHA 2022/2023

Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
1Arusha
 Upgrading of Mbauda – Losinyai to DSD0.4134.20
Rehab. Olokii (T/Packers) – Losinyai Road2.0118.86
Rehab. Mto wa Mbu – Loliondo Road3.1108.79
Rehab. Karatu Jnct. – Mangola – Matala  Road3.1108.79
Upgrading to DSD Usa river – Momela – Arusha National Park Road0.4110.00
DSD Kilala – Nkoaranga Road0.4258.50
Rehab. Monduli Juu (Ingusero) – Kitumbeine Road 2.068.86
Rehab. Noondoto Jnct– Kitumbeine Road  3.1110.00
Rehab. Karatu – Arusha/Manyara border towards Mbulu (Karatu – Kilimapunda)2.068.86
Upgrading to DSD of Kijenge – Usa river Road (Nelson Mandela University – 9 km) 0.8243.10
Rehab. Kimba – Makao – Matala 3.1110.00
Rehab. Waso – Kleins Gate1.968.13
Njiapanda – Matala; Opening up new Trunk Road to Gravel Std2.068.86
Njiapanda – Matala; 10 Concrete drifts100%67.65    
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Nduruma Bridge along Kijenge – Usa West and upgrading its approaches 100%310.00
Upgrading of Monduli – Engaruka0.4110.00
Sub–Total: Arusha24.92,064.60
2Coast
 Rehab. Mbuyuni – Saadan road 3.1110.00
Rehab Kilindoni – Rasmkumbi road  3.1110.00
Rehab. Mkuranga – Kisiju road3.1108.90
Rehab.  Makofia – Mlandizi – Maneromango Road3.1108.90
Rehab. Mbwewe – Lukigura Road 3.1108.90
Upgrading to DSD Kwa Mathias – Nyumbu – Msangani Road  0.5143.00
Upgrading to DSD of Bagamoyo Township Roads 0.5143.00
Upgrading of Utete – Nyamwage Road 2.4181.50
Rehab. Kibiti – Bungu – Nyamisati road2.1145.20
Upgrading of to bitumen standard Kisarawe – Maneromango0.399.00
Upgrading to bitumen standard Kilindoni – Rasmkumbi road  0.399.00
Upgrading to bitumen standard Mkuranga – Kisiju road   (Mkuranga – Msifuni)0.7220.00
Construction of Makurunge bridge and approaches along Kibaha – Mpuyani100%116.52
Rehab. Kibaha – Kiluvya – Kisarawe to grave standard2.172.60
Construction of Mbambe Bridge along Mkongo –100%55.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Ikwiriri road  
Upgrading to Bitumen Standard of Kwa Mfipa Jct – Kwa Mfipa Uongozi College (2.2km)3.5800.00
Rehab of Vikindu – Vianzi – Sangatini to Gravel Standard3.1110.00
Sub–Total: Coast 34.62,731.52
3Dar es Salaam 
 Upgrading  Chanika – Mbande Road   0.6193.60
Rehab. Ukonga – Mombasa – Msongola Road2.379.86
Rehab. Uhuru Road (DSD) 0.4126.50
Rehab. Shekilango Road (DSD) 0.4126.50
Rehab. Sam Nujoma Road (DSD) 0.4126.45
Rehab. Banana – Kitunda – Kivule – Msongola Road2.379.86
Rehab. United Nations Road (DSD) 0.4126.50
Upgrading to DSD Mbagala Mission – Kijichi – Zakhem Road  0.266.55
Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi Shule/Morogoro Road (20km)0.379.86
Upgrading of Kibamba – Kisopwa0.4132.00
Widening of Mwai Kibaki road to dual Carriageway0.4132.00
Upgrading of Boko – Mbweni – Mpiji to bitumen standard0.4132.00
Upgrading of Kibada – Chekeni Mwasonga Kimbiji to bitumen standard(48.9km)0.6176.00
Goba -Matosa -Temboni2.379.86
Kimara – Bonyokwa Kinyerezi2.379.86
Widening of Mbagala Rangi Tatu-Kongowe road to dual0.4127.05
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Carriageway  
Upgrading to DSD of Kunguru – TATEDO to Bitumen Standard0.4121.00
Upgrading of  Makabe Jct – Msakuzi (8.0 km)0.4135.30
Upgrading of Mjimwema – Pembamnazi to bitumen standard – (30km)0.4135.30
Sub – Total: Dar es Salaam 15.22,256.05
4Dodoma 
 Rehab. Kolo – Dalai (Mrijo chini – Goima section) 4.1145.20
 Upgrading Mbande – Kongwa – Suguta   0.272.60
 Rehab. Pandambili – Mlali – Ng’ambi (Mpwapwa – Suguta section)  3.7132.00
 Rehab. Zemahero – Kinyamshindo (Kwamtoro – Kinyamshindo section)  4.1105.70
 Upgrading to DSD Shabiby – Dodoma/Arusha round about0.260.50
 Rehab. Mnenia – Itololo – Madege Road3.1108.90
 Rehab. Manchali Kongwa – Hogoro Jctn (Kongwa – Hogoro Jctn)  4.1105.70
 Rehab. Gubali – Haubi Road4.1145.20
 Rehab. Olbolot – Dalai – Mnenia – Kolo – ( Kolo – Dalai section)3.1108.90
 Upgrading to DSD Mtumba – Vikonje – Chatiwa – Msanga – Chamwino Ikulu (20 km) & Chamwino Spur (1km)1.1363.00
 Construction of Mwanjiri and Suguta Bridges along Pandambili – Mlali – Ng’ambi100%181.50
 Rehabilitation to gravel standard of Chenene – Itiso –3.1200.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Izava – Dosidosi road (IzavaDosidosi section)   
 Rehabilitation of Bihawana Jct. – Chaligongo road3.1200.00
 Upgrading to Bitumen Standard of Ntyuka Jct.Mvumi Hospital -Kikombo Jct 0.6194.70
 Rehabilitation to gravel standard of Changaa – Hondomoira – Hanang/Ntomoko (New road)3.1108.90
 Upgrading of Kongwa Jct – Mpwapwa – Kibakwe (Kongwa Jct – Mpwapwa Section) 0.7220.00
 Rehab of Mlowa Barabarani – Mvumi Makulu (14.5km)3.2113.30
 Construction of Nzali Bridge100%350.00
 Sub–Total: Dodoma 41.62,916.10
5Geita 
 Rehab. Busisi – Nyang’wale – Geita Road3.2112.09
Upgrading of Mkuyuni – Busara Road0.4112.09
Rehab. Nyang’hwale – Nyang’holongo Road2.379.86
Rehab. Geita – Nzera – Kome Road3.2112.09
Rehab. Ushirombo – Nyikonga – Katoro/ Buseresere Road3.2112.09
Upgrading to DSD Geita – Bukombe Road  0.4111.10
Rehab. Bukombe – Nyikonga Road2.379.86
Upgrading of Chato Port – Chato Ginnery to DSST 0.4111.65
Rehab. Butengolumasa – Iparamasa – Masumbwe Road  3.2112.09
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 DSD Upgrading Geita Township Roads 0.5156.20
Rehab Itare – Katende Road 2.379.86
Rehab. Senga-Sungusila Ibisabageni-Ikoni Road2.379.86
Rehab. Masumbwe – Mbogwe – Nyikonga – Butengolumasa  road2.379.86
Rehab. Ushirombo – Nanda – Bwelwa road3.2112.09
Upgrading to DSD Mugaza – Kasenda0.4112.09
Upgrading to DSD Masumbwe roads0.6173.91
Rehabilitation of Masumbwe – Mbogwe – Kashelo3.2112.09
Rehabilitation of Senga – Kakubilo – Nyabalasana – Sungusila -Senga3.2112.09
Rehab. Bwelwa – Kharumwa3.2112.09
Upgrading to DSD Katoro and Buseresere Township roads0.7205.70
Upgrading to DSD UshiromboTownship roads0.399.55
Upgrading to DSD Muganza – Kasenda road0.397.35
Sub–Total: Geita40.52,475.66
6Iringa 
 Rehab. Paved section of Iringa – Msembe (Ruaha National Park) Road4.1143.00
Rehab. Paved section of Iringa – Pawaga Road0.3108.90
Rehab. Igowole – Kasanga – Nyigo Road2.172.60
Rehab. Izazi – Mboliboli – Pawaga – Mlowa Road3.1108.90
Rehab. Iringa – Idete Road3.1108.90
Rehab. Mbalamaziwa – Kwatwanga  Road  2.172.60
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Construction of Lukosi II bridge along Ilula – Kilolo Road100%110.22
Construction of Lukosi I bridge along Ilula – Kilolo road100%66.00
Upgrading of Iringa – Idete Road to Bitumen Standard0.5154.00
Rehab. Nyololo – Kibao – Mtwango Road3.1108.90
Rehab. Ihawaga – Mgololo Road3.1108.90
Rehab. Kinyanambo C – Kisusa road 2.172.60
Rehab. of Pawaga junction – Itunundu (Pawaga)3.0105.60
Upgrading of Tosamaganga Jctn – Tosamaganga Hospital (11km)3.0885.00
Upgrading to Bitumen Standard of Ihemi Jct – Ihemi Uongozi Institute (4km)3.1912.28
Nyigo – Ihawaga – Mgololo :Rehabilitation to gravel standard3.0106.70
Pawaga junction – Itunundu(Pawaga) – Rehabilitation  to bitumen  standard0.4110.00
Samora R/A – Msembe : Upgrading to bitumen standard 0.4110.00
Sub–Total: Iringa 36.23,465.10
7Kagera 
 Upgrading to DSD of Muhutwe – Kamachumu – Muleba0.6400.00
Rehab. Katoma – Kanyigo Road (Kajai swamp)5.1330.00
Upgrading to DSD Bugene – Kaisho – Murongo road (Rwabunuka Escarpment0.6200.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Sect.)    
Upgrading to DSD of Bukoba (CRDB) – Kabango Bay Road0.8240.00
Rehab. Murugarama – Rulenge – Nyakahura Road4.2150.00
Rehab. Kashalunga – Ngote – Kasindaga Road3.4120.00
Upgrading to DSD of Kyakailabwa – Nyakato Road0.4120.00
Upgrading to DSD of Kakunyu – Kagera Sugar Junction0.4120.00
Upgrading to DSD of Muleba – Kanyambogo – Rubya (Muleba District roads)0.8242.00
Opening of Mutukula – Minziro5.0150.00
Rehabilitation to DSD of Magoti – Makonge – Kanyangereko0.4140.00
Rehabilitation to DSD of Muleba – Nshamba0.7204.04
Sub–Total: Kagera 16.82,416.04
8Katavi 
 Rehab. Kagwira – Karema Road  3.8135.00
Rehab. Mamba – Kasansa (Mamba – Kibaoni section) 2.172.60
Rehab. Mwese – Kibo Road 2.172.60
Rehab. Mpanda (Kawajense) – Ugalla road 2.172.60
Ugalla Bridge (design and Construction)100%150.00
Rehab. Majimoto – Inyonga Road 3.4121.00
Rehab. of Kibaoni – Mamba Road 3.4121.00
Rehab. Kibaoni – Majimoto – Kasansa – Muze – Kilyamatundu (Kibaoni – Majimoto)   3.4121.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Inyonga – Ilunde Road3.1110.00
Rehab. Uzega – Kamsisi – Mapili Road  5.0177.65
Rehab. Bulamata – Ifumbula (Mishamo HQ) – Mishambo Jct18.4650.00
Construction of 2 Box Culverts along Bulamata – Ifumbula – Mishambo Jctn road100%650.00
Rehabilitation Works along Ifukutwa – Mwese – Lugonesi (Katavi/Kigoma Border) Regional Road R5622.1145.86
Upgrading to Bitumen standard  along Inyonga Township (Inyonga – Majimoto) Road 2km 0.4121.00
Upgrading to Bitumen Standard along Usevya Town Section (2km)0.4122.10
Rehab. Uzega – Nsekwa – Inyonga (km 17)4.1145.20
Rehab. Kamsisi – Songambele – Mapili (km 36)4.1145.20
Upgrading of Mpanda Municipal Council District road to Bitumen Standard 0.4121.00
Upgrading of District Road Kibo – Igagala – Mpanda road to Bitumen Standard 0.4121.00
Rehab of Kaulolo – Sangali – Masigo5.4189.19
Sub–Total: Katavi 64.03,564.00
9Kigoma 
 Rehab. Simbo – Ilagala – Kalya 3.2112.20
Rehab. Mwandiga – Chankere – Gombe – Jct. – Kagunga   3.2512.20
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehabilitation of Kalya – Sibwesa Harbor Port along Simbo – Kalya road2.1255.2
Rehabilitation of KitahanaMabamba road3.5124.74
Rehabilitation of Kifura- Nyaruyoba- Nyange road2.172.60
Rehabilitation of KibondoKumuhama road4.5160.60
Rehabilitation of MinyinyaNyange road2.172.60
Construction of Lubona Bridge along Mwandiga – Chankere – Mwamgongo100%121.00
Upgrading to Bitumen Standard of Uvinza town roads section0.4112.20
Upgrading to DSD of Nguruka town roads0.4121.00
Opening of Buhigwe – Mugera – Kitanga – Kumsenga3.4121.00
Construction of Rigid Pavement at Msebei along Katavi Border – Kanyani0.4113.74
Rehabilitation of Mkongoro – Chankere2.172.60
Buhigwe – Nyamugali – Muyama – Mugera – Katundu  (FS & DD)100%200.00
Buhigwe – Bukuba – Janda – Kirungu – Munzeze (FS & DD)100%200.00
Upgrading to bitumen standard Kakonko town road section0.4110.00
Rehabilitation of Lufubu JctUgalaba – Ubanda-Mwese along Simbo – Kalya road1.966.00
Rehabilitation of Kalinzi- Mkabogo-Kwitanga road1.966.00
Upgrading to DSD of Buhigwe town  0.3100.70
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Upgrading to DSD of Buhigwe town section0.3200.70
Sub–Total: Kigoma 32.82,814.38
10Kilimanjaro 
 Upgrading to DSD Mwanga – Kikweni Vuchama/Lomwe Road  2.3726.00
Rehab. Uru – Kishumundu Parish – Materuni Road0.272.60
Rehab. Holili – Tarakea  Road0.272.60
Rehab.  Kibosho  Shine – Mto Sere Road0.3108.90
Rehab. Sanya Juu – Rongai – Tarakea  0.5145.20
Upgrading to DSD of Kawawa – Pakula – Nduoni,  Nduoni – Marangu Mtoni 1.8550.00
Upgrading to DSD of Kibosho Shine – Kwa Raphael  – International School 0.8242.00
Upgrading to DSD of Makanya – Suji (14km) 0.8842.00
Upgrading to DSD of Masama – Tema (3 km)0.4121.00
Construction of Mamba Bridge along Same – Kisiwani – Mkomazi Road100%160.50
Rehab. Lang’ata Kagongo – Mwanga2.193.60
Rehab. Lembeni – Kilomeni – Ndorwe2.193.60
Sub–Total: Kilimanjaro 12.23,228.00
11Lindi 
 Rehab. Ngongo  – Ruangwa Jct Road (Milola mountains) 4.4156.20
Rehab. Nangurukuru – Liwale 4.4156.20
Rehab. Tingi – Kipatimu 4.4156.20
Rehab. Nanganga – Mandawa         4.4156.20
Rehab. Nachingwea – Kilimarondo  4.4156.20
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Upgrading to DSD at Nane Nane (Ngongo) Roads 0.8253.00
Rehab. Masasi – Nachingwea 2.9101.75
Rehab. Ngongo- Mandawa Ruangwa2.9101.75
Upgrading to DSD Kwamkocho – Kivinje District Roads0.8253.00
Upgrading of 5km Nachingwea Town Roads0.5318.30
Upgrading of Liwale Town Roads0.5315.88
 Sub–Total: Lindi 30.62,124.68
12Morogoro 
                               Bridge Construction along  Mvomero – Ndole – Kibati  100%126.50
Upgrading to DSD Liwambanjuki hills along Lupiro – Malinyi 0.6187.00
Rehab.Ubena Zomozi – Ngerengere 2.072.05
Rehab. Miyombo – Lumuma – Kidete (Moro/Dodoma border)  3.2114.40
Construction of Mtibwa Bridge across Wami river along Dakawa/ Wami Mbiki game reserve – Lukenge/ Songambele 100%126.50
Construction of Vented Drift (1 No.) and Box culverts (2Nos) along  Gairo – Iyongwe 100%126.50
Upgrading of Gairo town roads along Ngungu and Gairo –Nongwe road section0.5156.75
Rehab.Gairo – Iyogwe Road 3.2114.40
Spot improvement of Ifakara – Mbingu Section (20 km) along Ifakara – Taweta – Madeke Regional Road    2.072.05
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehabilitation of Mvomero – Ndole – Kibati Regional Road3.6126.50
Upgrading to DSD Standard of Sangasanga – Langali (Mzumbe Univerty – Mlali Section)0.278.10
Construction of Duthumi Bridge along Morogoro (Bigwa) – Kisaki 100%78.10
Rehabilitation of Mzumbe University Roads   (32.1km)0.5160.38
Upgrading of Mlimba Township Road0.8819.00
Sub–total: Morogoro 25.02,358.23
13Mbeya
 Rehab. Mbalizi – Shigamba – Isongole (Mbalizi – Shigamba Sect 52 km ) 4.0139.92
Rehab. Ilongo – Usangu Road 4.0139.92
Construction of Mbaka & Mwalisi Bridge along Katumba – Tukuyu  Road100%233.20
Rehab. Matema – Ikombe  Road4.0139.92
Rehab. Katumbasongwe– Njisi (Ipyana – Katumba Songwe section ) 4.0139.92
Upgrading to DSD of Katumba – Lwangwa – Mbambo – Tukuyu road0.7220.00
Rehabilitation Rujewa – Madibira – Kinyanambo Road (Rujewa – Madibira Section) to gravel standard4.0139.92
Rujewa – Madibira – Kinyanambo, Upgrading to  Bitumen Standard 0.5165.00
Rehabilitation of Mbalizi – Mkwajuni – Makongolosi to gravel standard    4.0139.92
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Mbalizi – Mkwajuni – Makongolosi, Upgrading to bitumen standard0.4132.00
Rehab. Isyonje – Kikondo – Makete to gravel Standard3.1109.67
Igawa – Mbarali, Upgrading to  bitumen standard0.4221.00
Opening up of Luteba – Ipelele3.9136.40
 Sub–total: Mbeya 32.82,056.79
14Manyara 
 Rehab. Losinyai – Njoro 3.7130.00
Rehab. Kilimapunda – Kidarafa 4.0140.00
Constr. Concrete slab  Along Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu (Rift Valley Section) 0.5150.00
Rehab. Arusha/ Manyara border – Mbulu 3.3115.00
Rehab. Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu Road 3.3115.00
Upgrading of Mbulu township roads0.4120.00
Rehab. Nangwa – Gisambalang Road3.4121.00
Rehab. Mogitu – Haydom Road2.484.70
Babati – Kiru – Mbulu 2 (Rigid Pavement Construction on Steep Grade)0.4220.00
Rehab. Kijungu – Sunya – Dongo3.4121.00
Singe – Orkesumet/Kibaya link3.7130.00
Uprading to DSD of Dareda – Dongobesh (Dongobesh Township)0.6290.00
Magara Escarpment (Concerete Pavement)0.6293.60
Rehab. Kibirashi – Kijungu – Kibaya 3.5121.81
Sub–total: Manyara 29.62,152.11
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
15 Mara 
 Rehab. Nyamwaga – Mriba – Itiryo – Kegonda 4.5159.72
Rehab. Muriba – Kegonga 4.5159.72
Rehab. Murangi – Bugwema 3.4119.79
Upgrading to DSD Nyankanga – Rung’abure 0.5159.72
Rehab. Mugumu – Fort Ikoma 3.4350.79
Upgrading to DSD of  Mika – Utegi – Shirati  0.7231.00
Rehab. Kinesi Jct. – Kinesi2.3129.86
Rehab. Nyankanga – Rung’abure 3.4119.79
DD of Masonga – Kirongwe (TZ/Kenya border)100%208.45
Rehabilitation of Murangi – Bugwema road2.172.60
Upgrading to DSD of Makoko Urban road0.4160.00
Rehab. Balili – Mugeta – Manchimwelu – Ringwani road 2.172.60
Rehab. Nywamigura – Gwitiryo2.172.60
Sub–total: Mara 30.02,016.64
16Mtwara 
 Rehab. Mnongodi – Mdenganamadi – Kilimahewa – Michenjele (border road) 3.4121.00
Rehab. Magamba – Mitema – Upinde. 3.4121.00
Rehab. Newala – Mkwiti – Mtama road (Amkeni – Kitangali Section) 3.1108.90
Rehab  Mangamba – Mnazi bay  3.1108.90
Rehab. Mangamba – Mnazi Bay (Incl. Mtwara Mikindani Bypass)     4.1145.20
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Upgrading to DSD Kinolombedo Escarpment along Newala – Mkwiti rd 1.2363.00
Rehab. Mbuyuni – Makong’onda – Newala Road4.1145.20
Construction of Miesi, Nakalola and Shauri Moyo Bridges100%217.00
Rehab. Namikupa- Mitema – Upinde(border road) 3.1108.90
Rehab. Madimba – Tangazo – Namikupa and Tangazo – Kilambo 4.1145.20
Rehabilitation of Msangamkuu Access Roads2.587.12
Upgrading of Nanyamba Township roads to DSD0.5219.40
Upgrading to DSD of Nangomba – Nanyumbu road0.5148.50
Sub–total: Mtwara 33.12,039.32
17Mwanza 
 Rehab. Bukongo – Rubya – Bukongo – Masonga Road 2.8100.00
Rehab. Nyakato – Buswelu – Mhonze 2.8100.00
Rehab. Bukwimba – Kadashi – Maligisu  2.8100.00
Rehab. Mwanangwa – Misasi  – Salawe  2.8100.00
Rehab. Ngudu –  Nyamilama – Hungumalwa 2.8100.00
Rehab. Misasi Jct – Ihelele  to  Mza – Shy Water Project 2.8100.00
Rehab.  Kamanga – Katunguru – Sengerema 2.8100.00
Rehab. Buhingo – Ihelele 3.1108.90
Rehab. Rugezi – Masonga 3.1108.90
Rehab. Sabasaba – Kiseke – Buswelu 3.1110.00
Sengerema -Nyehunge – Kahunda Road (FS & DD)  100%116.60
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Construction of Buyogo Bridges along Ng’wamhaya – Itongoitale road100%116.60
Nabili box culvert100%110.00
Wingi 3 box culvert100%110.00
Rehab. Masonga – Rugezi  3.1110.00
Rehab. of Bukokwa Nyakalilo2.277.00
Rehab of Sengerema – Ngoma2.277.00
Rehab of Magu – Mahaha2.277.00
Rehab of Bupandwamhela – Kanyala2.277.00
Rehab of Nyambiti Jct – Malya2.277.00
Rehab of Nyehunge – Kahunda2.277.00
Rehab of Sengerema – Nyamazugo2.277.00
Rehab of Mabuki – Luhala2.175.83
Sub–total: Mwanza 50.62,205.83
18Njombe 
 Upgrading to DSD  Ndulamo – Nkenja – Kitulo – Mfumbi 0.9280.00
Opening up Lupembe – Madeke – Taweta road along Kibena – Lupembe 3.4120.00
Rehab. Mkiu – Madaba  3.4120.00
Rehab. Mlevela – Mhaji – Ibumila3.4120.00
Upgrading to DSD Makambako Township roads0.3200.00
Upgrading to DSD of Mlangali Bypass (5km) 0.6200.00
Upgrading to DSD of Ludewa – Lupingu Road Ludewa Town Section 0.6200.00
Upgrading to DSD of Njombe  Township Roads0.4120.00
Upgrading to DSD of Makete Township Roads      0.4120.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Opening up of Lupembe – Madeke – Taweta/Mfuji (Lupembe – Mfuji section Njombe/Morogoro Border) 53km).3.1110.00
Upgrading to Bitumen Standard of Mkiu – Mavanga – Madaba Road0.4120.00
Upgrading to Bitumen Standard of Nkomang’ombe – Mchuchuma Road (7Km)0.4120.00
O   pening of Ipelele-Luteba (Njombe/Mbeya Bdr)4117.56
Sub–total: Njombe 17.71,947.56  
19Rukwa 
 Rehab. Kasansa – Mamba – Muze (Kizungu escarpment) 5.7200.00
Rehab. Laela – Mwimbi – Kizombwe Road3.4119.79
Rehab. Kalepula Jctn – Mambwenkoswe 3.8133.10
Rehab. Nkundi – Kate – Namanyere Road4.4143.00
Rehab. Kaengesa – Mwimbi Road3.1100.00
Rehab. Mtowisa – Ilemba Road4.4140.00
Upgrading to Bitumen Standard of Access Road to Kaegesha Seminary School3.3410.00
Rehab. Katongoro – Kipili (Kipili New Port) Road3.1100.00
Rehab. Msishindwe – Mambwekenya Road3.1110.99
Rehab. Kitosi – Wampembe3.1110.99
Kasansa – Kilyamatundu Bridge Rehabilitation (replacement of 10 vented drifts by Box culverts)    100%170.00
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Ilemba – Kaoze – Kilyamatundu (Kaoze – Kilyamatundu)2.370.86
Rehabilitation of Ilemba – Kaoze2.370.86
Rehab. Kale – Luse – Kantalemwa Road3.1100.00
Rehab. To DSD of Laela – Mwimbi – Kizombwe Road3.3100.00
Sub–total: Rukwa 49.02,079.56
20Ruvuma 
 Upgrading to DSD Unyoni – Kipapa –  Chamani – Mkoha (Mawono Escarpment) 0.4133.10
Rehab. Lumecha – Kitanda – Londo road (Kitanda – Londo Section.) Ruvuma/ Morogoro Border 2.379.86
Upgrading Hanga – Kitanda (Mhangazi sect.) Road0.379.86
Upgrading  to DSD Mbinga – Mbuji – Litembo – Mkili road (Myangayanga escarpment) 0.4133.10
Rehab. Nangombo – Chiwindi road (Ng’ombo – Chiwindi Sect.) 2.379.86
Upgrading of Lumecha – Kitanda – Londo Road (Hanga Section) 0.4133.10
Opening up of Kigonsera – Kilindi – Hinga (Kilindi – Hinga sect) Road1.760.50
Construction of a Box culvert at Mbesa along Tunduru – Nalasi road 100%96.80
Rehab. Mbambabay – Liuli Road 2.796.80
Construction of Box culvert and approach roads at Mnywamaji river along Kitai – Lituhi Road  100%96.80
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Namtumbo – Likuyu Road2.172.60
Opening up of Mbinga – Mbuji -Litembo – Mkili road (Litembo – Mzuzu – Mkili section)2.172.60
Rehab.  Namabengo – Mbimbi – Luega road2.172.60
Rehab. Mletele – Matimila – Mkongo Road2.172.60
Construction of Box culvert and approach roads  along Mbambabay – Lituhi100%96.80
Construction of Mitomoni Bridge at Ruvuma River along Unyoni – Liparamba – Mkenda (Mitomoni) 100%60.50
Rehabilitation works along Unyoni – Maguu – Kipapa1.790.40
Opening of Kigonsera – Kilindi – Hinga (Kilindi – Hinga sect)1.760.50
Rehabilitation of Unyoni – Liparamba1.760.50
Rehabilitation of Naikesi – Mtonya road1.760.50
Rehabilitation of Mpitimbi – Ndongosi – Nambendo1.760.50
Upgrading of Tunduru – Nalasi Road, Tunduru Town Section to DSSD1.0500.00
Sub–total: Ruvuma 32.562,269.88
21Simiyu 
 Rehab. Sola – Bushashi– Sakasaka road 4.1145.20
Rehab. Bariadi – Kasoli – Salama  4.1145.20
Rehab. Ngulyati – Miswaki – Ngasamo 3.4121.00
Rehab. Mwandete – Mwamanoni road    4.1145.20
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Malya – Malampaka – Ikungu road 5.1181.50
Rehab. Maswa – Lalago Road5.1181.50
Upgrading to DSD Ikungu – Malampaka Road1.7544.50
Rehab. Nyashimo – Dutwa unpaved5.3188.76
Upgrading to DSD Lamadi – Wigelekelo Trunk Road (Assess road to Simiyu referal Hospita at Maperani area) (Design and Build approach)0.4237.00
 Sub–total: Simiyu 33.51,889.86
22Singida 
 Rehab. Manyoni – Ikasi – Chaligongo Road4.0139.70
Rehab. Sekenke – Shelui Road4.0139.70
Rehab. Ikungi – Kilimatinde Road1.967.10
Rehab. Iguguno – Nduguti – Gumanga Road4.0139.70
Rehab. Mkalama – Mwangaza – Kidarafa Road 4.0139.70
Rehab. Kisaga – Sepuka – Mlandala Road (Sepuka – Mlandala Sect.) 4.0139.70
FS&DD: Sanza Bridge (100m Span) along Manyoni East – Heka – Sanza – Chali Igongo (Dom/Sgd Border)  100%67.10
Rehab. Sibiti – Matala Road and 4 Box culverts100%67.10
Rehab. Kinyamshindo – Kititimo1.967.10
Construction of Reinforced concrete drift, Box Culverts and approaches along Kiomboi – Kiriri – Chemchem100%115.50
Heka – Sasilo – Iluma (Sasilo – Iluma section)  2.9103.40
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Iyumbu – Mgungira – Mtunduru – Magereza (Singida)2.9103.40
Rehab. of Njuki – Ilongero – Ngamu Road4.0139.70
Widening of Kilondahatar Bridge100%165.50
Widening of Misigiri – Kiomboi road to bitumen standard 0.4166.60
Construction of Itigi Township roads to Bitumen Standard0.5148.50
Sub–total: Singida 34.21,909.50
23Shinyanga
 Rehab. Kahama – Chambo Road3.5125.29
Upgrading to DSD of Regional Roads along Kahama township 0.5165.22
Rehab. Old Shinyanga – Salawe Road5.3187.00
Rehab. Nyandekwa – Uyogo – Sunga Road7.0246.29
Upgrading of Mwanangwa – Misasi – Salawe – Solwa – Kahama0.8247.50
Rehab. Muhulidede – Tulole2.485.36
Upgrading to DSD of Ushetu District Roads1.1344.30
Upgrading DSD of Buyange – Busoka (Kahama) section of Geita – Kahama Regional Road and Bulyanhulu Jct – Bulyanhulu Mine (Kakola)0.9271.70
Rehabilitation of Ntobo – Busangi – Ngaya – Nduku – Mwakuhenga – Mwankuba – Buluma – Jana – Didia5.3187.00
  1,859.66
 Sub–total: Shinyanga 26.8   
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
24Songwe             
 Constr. of  Mpona Bridge along Galula – Namkukwe Road100%172.70
Rehab. Saza – Kapalala Road 2.8100.10
Rehab. Mlowo – Kamsamba Road ( Itumbula – Kamsamba Section)3.9136.40
Upgrading of  Shigamba – Isongole Road ( Itumba Town)0.7233.20
Rehab. Shigamba – Itumba –  Isongole road3.2112.20
Rehab. Isansa – Itumpi road  2.8100.10
Upgrading to bitumen standard at Vwawa/Mbozi (7km) and Mlowo Kamsamba regional roads (3km) 0.9293.70
Upgrading to bitumen standard at Mkwajuni town along Chang’ombe – Mkwajuni – Patamera regional road0.7233.20
Rehabilitation of Shigamba – Ibaba Road3.9136.40
Rehabilitation of Mahenje – Hasamba – Vwawa3.9136.40
Upgrading of Mahenje – Hasamba – Vwawa to Bitumen Standard0.6231.50
 Sub-total: Songwe23.41,885.90
25Tabora 
 Rehab. Puge – Ziba Road 4.5157.30
Rehab. Kaliua – Uyowa – Makazi Road5.1180.00
Rehab. Mambali – Bukene Road5.5193.60
Rehab. Sikonge – Usoke Road (Tutuo – Usoke) 4.5157.30
Opening up of Tura – Iyumbu Road4.5157.30
Rehab. Tabora – Mambali – Itobo – Kahama 4.2150.00
Rehab. Sikonge – Mibono – Kipili 4.8169.40
Na.Jina la MradiUrefu (Km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Mambali – Itobo – Kahama Road4.8169.40
Opening up of Ulyankulu – Urambo2.690.75
Opening of Bukumbi – Muhulidede2.690.75
Opening of Kishelo – Kitunda road4.2150.00
Rehab of Ng’hwande – Ulyankulu – Kaliua – Ugala 3.2112.90
Sub–total: Tabora 50.41,778.70
26Tanga
 Rehab of Songe – Vyadigwa – Mziha Road4.5159.72
Rehab. Kwekivu – Kwalugalu Road (Kwekivu – Iyogwe) 4.5159.72
Rehab. Mlalo – Mng’aro Road4.5159.72
Construction of new  concrete” T ” beam bridge (Single span 10m ) along Kwaluguru – Kiberashi Road (Kigwangulo Bridge)100%159.72
Upgrading to DSD of Kiberashi – Songe Road (Songe Township)0.9266.20
Upgrading to DSD of Mkinga Township Road0.9266.20
Rehab. Tanga – Pangani – Buyuni to gravel standard4.5159.72
Rehab. Lushoto –  Magamba – Mlola3.8133.10
Construction of New Box culvert along Bombomtoni – Mabokweni Road100%176.66
Upgrading of Utofu – Majani Mapana – Duga Mwembeni (4 km) Road to Bitumen Standard0.6180.39
Sub–total: Tanga 24.11,821.15
 ERB SEAP Programme 726.00
 Monitoring (MoWT-WORKS) 532.18
 TOTAL REGIONAL ROADS (CONSOLIDATED)734.5961,585.00

KIAMBATISHO Na. 3 

MIRADI INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA

MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA 2022/23 (KASMA 2326)

Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  A: BARABARA KUU 
1.  2326Review                      and Preparations                of Standards & Specifications  750,800,000.00 
2.  2326Enhancement of Testing of construction materials through introduction of modern technology performance based appropriate asphalt mix design guideline and improvement of infrastructure and other facilities for Central Materials Laboratory (CML) 750,000,000.00 
3.   2326Monitoring of Road and Bridge projects, maintenance of supervision vehicles, fuel and other road related administrative costs (MOWTC)   1,400,000,000.00 
4.  2326Software                     for Highway/Transport Planning and Design including training of TANROADS staff 90,000,000.00 
5.  2326Capacity Building in construction Industry (including harmonisation   of activities being carried out by ICoT  741,640,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
     
6.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Mpanda    –    Ugalla    – Kaliua – Ulyankulu – Kahama457 5,000,000.00 
7.  2326Facilitation and Supervision of road projects (TANROADS)  650,000,000.00 
8.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Improvement of the Kitonga Escarpment road section10 220,000,000.00 
9.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Upgrading of Kibaoni – Majimoto – Inyonga road152 57,000,000.00 
10.  2326Feasibility Study and Detailed Design for upgrading of Singida Urban – Ilongero – Haydom Road93 175,000,000.00 
11.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Mkuyuni – Nyakato Road to Bitumen Standard10 5,000,000.00 
12.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design                      for Rehabilitation of Morogoro (Tumbaku Jct) – Mangae/Melela – Mikumi – Iyovi including Doma Bridge.156460,000,000.00 
13.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering10 5,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  Design for Morogoro (Msamvu Roundabout) – Morogoro Centre – Bigwa Junction    
14.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Omurushaka – Murongo road.125 180,000,000.00 
15.  2326Feasibility study and Detailed design of the road linking the Simanjiro (Orkesumet) – KIA – Mererani (Part of Kongwa Ranch – Kiteto – Simanjiro – KIA)119 500,000.00 
16.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of the Singida Bypass.46 500,000.00 
17.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Nyakato    –    VETA    – Buswelu   Road3 120,000,000.00 
18.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Rehabilitation of Kibaha – Mlandizi – Chalinze road section75 90,000,000.00 
19.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of Mpwapwa – Gulwe – Rudi – Chipogoro Road ( Kibakwe – Chipogoro Road Section)76 500,000.00 
20.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction200 228,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  of Ntendo – Muze – Kilyamatundu Road  
21.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of Mbamba Bay – Lituhi Road113 90,000,000.00 
22.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of Nangurukuru – Liwale Road230 90,000,000.00 
23.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of Ushirombo – Nyikonga – Geita (Katoro) Road59275,000,000.00 
24.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Construction of Makete – Ndulamo – Nkenja – Kitulo Road42 5,000,000.00 
25.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading  of Makabe jct/Mbezi Mwisho – Goba Jct – Msakuzi and Kimara Bonyokwa – Kinyerezi roads,15 90,000,000.00 
26.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design     of     Magu     – Bukwimba – Ngudu – Hungumalwa Road64 305,000,000.00 
27.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Mbalizi – Mkwajuni (Galula – Mkwajuni – Makongolosi section)61 5,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  Road  
28.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading Utete – Nyamwage Road34 90,000,000.00 
29.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Decogestion to Dual Carriageway of Mwanza Urban along Mwanza – Nyanguge Road Section25 50,000,000.00 
30.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Widening of Arusha – Kisongo to Dual Carriageway – Four Lanes Road9 280,000,000.00 
31.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Airport – Igombe – Nyanguge.46 500,000.00 
32.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Namanyere – Katongoro – New Kipili Port Road65 230,000,000.00 
33.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Kagwira – Ikola – Karema Road112350,000,000.00 
34.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Mkalama – Gumanga – Nduguti – Iguguno Shamba Road89 400,000,000.00 
35.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of76140,000,000.00
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  Bariadi – Salama – Ng’haya – Magu Road  
36.  2326Feasibility Study and detailed design of Upgrading of Ulemo – Kinampanda                – Gumanga (Singida) – Mkalama  46 180,000,000.00 
37.  2326Feasibility Study and detailed design of Kyabakoba              and Kamashango bridges along Muhutwe – Kamachumu – Muleba road2 Nos 500,000.00 
38.  2326Feasibility Study and detailed design of Bujonde Bridge (Mbeya)1 Nos 90,000,000.00 
39.  2326Feasibility Study and detailed design of Old Korogwe – Kwamdolwa – Magoma – Mabokweni.127.54 300,000,000.00 
40.  2326Feasibility Study and detailed design of Longido – Siha38 185,000,000.00 
41.  2326Feasibility Study and detailed design of Tengeru – Mererani28 140,000,000.00 
42.  2326Feasibility Study and detailed design of Geita – Nzera – Nkome Port58.30 280,000,000.00 
43.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Chalinze – Manga along Chalinze – Segera road93360,000,000.00
44.  2326Feasibility Study and detailed design of Mjonga (60m), Chakwale (100m) and Nguyami (75m) Bridges (Morogoro)3 Nos 280,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
45.  2326Feasibility Study and detailed design of Bungu – Nyamisati40.2 230,000,000.00 
46.  2326Feasibility Study and detailed design of Babati (Dareda) – Dongobesh60 150,000,000.00 
47.  2326Feasibility Study and detailed design of Mbulu – Magugu (Mbuyu wa Mjerumani)63 120,133,000.00 
48.  2326Feasibility Study and detailed design of Katesh – Haydom68 280,000,000.00 
49.  2326Feasibility Study and detailed design of Kimotorok – Sukuro – Terati/Rotiana128 400,000,000.00 
50.  2326Feasibility Study and detailed design of Ngopito – Kimotorok  – Singe (Babati)255 270,000,000.00 
51.  2326Detailed design of Kuruya – Kinesi jct road18.42 185,000,000.00 
52.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Upgrading of Ikungi (Singida) – Londoni – Kilimatinde (Solya) (R431)117.9 400,000,000.00 
53.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Upgrading of Nanenane – Miyuji – Mnadani Sekondari  – Ntyuka Jct -Nanenane 47.2415,000,000.00 
54.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Mika – Utegi – Shirati – Ruari port and Masonga – Kirogwe roads48.73340,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
55.  2326Feasibility Study and Detailed Design for Nyankanga – Rung’abure  Road91 280,000,000.00 
56.  2326Feasibility Study and detailed Design for Nyankumbu – Kharumwa – Nyang’jolongo – Kahama road149 300,000,000.00 
57.  2326Detailed Design for  Geita town section (Mtakuja – Buhalahala) along Nyamuhama – Bwanga – Ibanda Trunk Road (T003) 24 90,000,000.00 
58.  2326Detailed design of Mkuranga – Kisiju (Pwani)39 140,000,000.00 
59.  2326Detailed Design of Kiluvya – Mpuyani (Pwani)19.8 90,000,000.00 
60.  2326Road Master Plan  185,000,000.00 
61.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Bariadi – Kisesa – Mwandoya – Ngh’oboko Road102 140,000,000.00 
62.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Nyakahanga – Nyabiyonza – Nyakakika 96 140,000,000.00 
63.  2326Detailed Engineering Design for Upgrading of Mkongo 2 – Ikwiriri Road 24.74 90,000,000.00 
64.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of  90,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  Katumba – Kafwafwa – Kyimo  
65.  2326Feasibility Study and Detailed Engineering Design for Upgrading of Mbalizi – Shigamba52 90,000,000.00 
66.  2326Detailed Design of Sanga Bridge1 No 90,000,000.00 
67.  2326Detailed Engineering Design for Rehabilitation of Old Bagamoyo Road43.17310,000,000.00
68.  2326Feasibility Study and Detailed Design Ihumwa – Hombolo – Mayamaya Road  55200,000,000.00
69.  2326Operational cost for Road Doctor Survey van System with Laser Scanner, Ground Penetrating Radar and Light Weight Deflector 150,000,000.00 
70.  2326Acquisition of Design Software, Training on the Use of Design Software and Costs for Annual Fees 500,000,000.00
  Jumla        Ndogo         – Barabara Kuu5,60515,820,073,000. 00
 2326B:    BARABARA    ZA    MIKOA     – (Kiambatisho Na.4)30,731,221,000. 00
  C: VIVUKO 
71.  2326Construction of new ferry infrustructure (Ticket room, waiting lounge, office and toilet) at Itungi Port in Mbeya. 100,000,000.00
72.  2326Expansion of waiting lounge of Kigamboni ferry terminal   150,000,000.00
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
73.  2326Design, develop, supply, install, configure and commisioning of Electronic Ferry Management Information System (EFMIS) at TEMESA and MOWT 1,116,532,798.00
74.  2326To construct Mlimba – Malinyi ferry ramps 522,542,708.00
75.  2326Procurement of Heavy plant and spare parts for 33 ferries maintenance. 1,134,022,105.72
76.  2326Procurement of one new ferry to ply between Buyangu – Mbalika 400,000,000.00
77.  2326To strengthening ferry safety and trainings. 134,022,105.72
78.  2326Rehabilitation of roadwork plants at TEMESA Morogoro Workshop and Institute of construction Technology (ICoT). 50,000,000.00
79.  2326Rehabilitation of ferries; MV Misungwi 100,000,000.00
80.  2326Rehabitation of ferries; MV Ruhuhu Old, MV Ruvuvu, MV Magogoni and MV Kigamboni. 358,217,472.00
81.  2326Facilitation, supervision, and related administration of ferry projects (TEMESA) 223,370,175.00
82.  2326Ferry related administrative activities, monitoring and evaluation of ferry projects 312,718,245.28
  Jumla Ndogo – Vivuko 4,467,403,504.00
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
  D:ROADS         RELATED ACTIVITIES  
83.  2326Road Related Administrative Activities. 3,152,984,546.00
84.  2326Institutional support including M&E for road projects and capacity building. 1,314,418,958.00
  Jumla Ndogo- (Road Related Activities) 4,467,403,504.00
  E:         MASUALA         YA        USALAMA             BARABARANI   NA MAZINGIRA
85.  2326Operationalization of an Electronic System for issuing Abnormal Load Permit (e-permit), Road Accident Information System, 24 hours weighbridge management systeam and speed control camera along the TANZAM Highway.   1,300,000,000.00 
86.  2326Review Design, Supply, Install,Test and Commissioning of the Weighbridge Management System to the  42 Weighbridges CCTV Camera System  1,500,000,000.00 
87.  2326Conduct Road Safety Awareness Campaigns 80,000,000.00 
88.  2326Conduct a Study on Road Safety Assessment of Traffic Accidents and Establish a Collision Costing Model   70,000,000.00 
89.  2326Conduct Simulation of the Impact and Cost of Vehicle Overloading on Pavement Damage     70,000,000.00 
90.  2326Review and Printing of Road Safety Guidelines     50,000,000.00 
Na.KasmaJina la MradiUrefu (km/Na)Bajeti (Shilingi)
91.  2326Support to Environment Management Projects in the Road Sector   215,000,000.00 
92.  2326Improvement of Road Safety by Reducing Road Crashes at Signalized and Non-signalized Intersections by Carrying out Micro- simulation   100,000,000.00 
93.  2326Skill Development on Road Safety Profession   80,000,000.00 
94.  2326Improving  Road Safety by Identifying BlackSpot Areas along the Major Transport Corridors   200,000,000.00 
95.  2326Conduct           Awareness Campaigns on atherence to the east africa vehicle load control Act, 2016   50,000,000.00 
96.  2326Monitoring and evaluation of roads, vehicles and ferries safety, maintenance of vehicles, fuel and other related road safety administrative cost.    205,860,484.00 
  Jumla Ndogo – Usalama wa Barabarani na Mazingira   3,920,860,484.00 
  JUMLA KUU (A+B+C+D+E) 59,406,961,492.00

NB: Mchanganuo wa miradi ya Barabara za Mikoa umeoneshwa kwenye Kiambatisho Na.4

KIAMBATISHO NA. 4

 MCHANGANUO WA MIRADI YA BARABARA ZA MIKOA INAYOTEKELEZWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO

WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
1Arusha  
Rehab. Longido – Kitumbeine – Lengai (Kitumbeine – Lengai)2.895.000
Rehab. KIA – Majengo Road3.0100.000
Rehab. Tengeru jct – Cairo Road3.3110.000
Construction of Box culvert along Nelson Mandela  – AIST100%160.000
Upgrading to DSD Kijenge – USA River4.1140.000
Upgrading of Mianzini – Timbolo – Olringaringa Road to Bitumen Standard (18km)4.8160.000
Sub – total: Arusha18.1765.000
2Coast  
Rehab. Pugu – Kisarawe – Masaki – Msanga – Chole  – Vikumburu  Road (Maneromango – Vikumburu section – km 36)2.1 70.000
Rehab.Makofia – Mlandizi – Maneromango( Mlandizi – Maneromango section- km 36)1.7 55.000
Upgrading of TAMCO – Vikawe – Mapinga0.3 85.000
Rehab. Utete – Nyamwage 1.4 45.000
Upgrading to DSD Bagamoyo Township Roads0.3 80.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Bungu – Nyamisati road1.7 55.000
Rehab. Vikumburu – Mloka Road1.7 55.000
Constuction of Makurunge Bridge and approaches along Kibaha – Mpuyani 100% 95.000
Rehabilitation of Kiparang’anda – Kibulu road2.4 80.000
Upgrading of Utete – Nyamwage to bitumen standard0.3 100.000
Upgrading to paved road Mlandizi – Maneromango road 0.3 100.000
Sub–Total:  Coast12.1 820.000
3Dar es Salaam  
Upgrading of Chanika – Mbande 0.4 130.000
Rehab. Uhuru Road (1km)0.3 90.000
Upgrading Boko – Mbweni road to DSD (6.9km)0.4 130.000
Upgrading to DSD Feri – Tungi – Kibada 0.5 150.000
Rehabilitation of United Nations roads0.3 90.000
Upgrading to DSD Kunguru – TETEDO (5km) 0.4 115.000
Construction of Drainage System and Acess Roads along Baraka Street at Ununio – Mbweni Road100% 560.000
Rehabilitation of Ardhi Univesity Access Roads (1.65km)0.6 185.000
Upgrading of Kibamba – Kibwegere – Mpiji Magoe road (20Km)  120.000
Rehabilitation of Ardhi University Access Roads  140.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Improvement of Drainage System and second Access to Plot No. 711/3 Kawe Dar es salaam  110.000
Sub–Total: Dar es Salaam 3.91 1,820.000
4Dodoma  
Upgrading of Mbande – Kongwa Junction – Mpwapwa to Paved standard0.4 110.000
Construction of Baura Bridge and approaches100% 100.000
Upgrading of Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe – Chipogoro Road (Including Gulwe Bridge) 0.3 100.000
Rehab. Gubali – Haubi 2.2 75.000
Rehab. Hogoro Jct – Kibaya 2.3 80.000
Rehabilitation to gravel standard of Olbolot – Dalai – Kolo2.3 80.000
Rehabilitation to gravel standard of Chenene – Itiso – Izava – Dosidosi road (Izava-Dosidosi section) 2.3 80.000
Rehabilitation to gravel standard of Mbande – Kongwa – Suguta (Ugogoni-Suguta section) 1.7 55.000
Upgrading to Bitumen standard of Ihumwa – Hombolo – Gawaye0.2 55.000
Upgrading to Bitumen standard of Kikombo Jct – Chololo – Mapinduzi (Army HQ)0.4 110.000
Rehabilitation to gravel standard of Kibaigwa – Manyata Jct. – Ngomai – Njoge – Dongo (Dodoma/Manyara Boarder)2.2 75.000
Design and Start Construction of Kelema Maziwani Bridge along100% 90.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Kondoa – Bicha – Dalai Road  
Design and Construction of Munguri Bridge along Kondoa Mtriangwi /Gisalalag100% 60.000
Construction of Mpwapwa Bridge along Pandambili – Mpwapawa – Ng’ambi, R.470100% 70.000
Rehab of Chimwaga – Chinyoya – Kikuyu2.1 70.000
Rehab of Emausi – Mlimwa – Wajenzi2.2 75.000
 Rehab of Nanenane – Miyuji – Mkonze1.8 60.000
Sub–Total: Dodoma20.4 1,345.000
5Geita  
Rehab. Chibingo – Bukondo road 2.2 75.000
Rehab. of Geita – Nkome Mchangani2.2 75.000
Rehab. of Geita – Nyarugusu –  Bukoli2.3 80.000
Upgrading to DSD Mkuyuni road0.4 130.000
Upgrading Muganza – Kasenda0.3 85.000
Rehab. Kibehe – Kikumbaitale2.3 80.000
Upgrading to DSD of Geita township roads0.4 130.000
Rehab. Itare – Katende  road1.5 50.000
Rehab. Ipalamasa – Mbogwe – Masumbwe 2.2 75.000
Rehab. Chato – Rubambagwe2.8 95.000
Rehab. Majengo – Kalema – Gatini (Majengo – Gatini Section)1.5 50.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Mipogoloni – Nakasagala1.5 50.000
Upgrading to DSD Masumbwe roads0.4 130.000
Upgrading to DSD Ushirombo township0.4 130.000
Rehabilitation of Masumbwe – Mbogwe – Kashelo1.6 55.000
Rehabilitation of Senga – Kakubilo – Nyabalasana – Sungusila –Senga1.6 55.000
Rehab. Bwelwa – Kharumwa road1.7 55.000
Sub – total: Geita25.5 1,400.000
6Iringa  
Rehab. Nyololo – Igowole – Kibao – Mtwango – Mgololo3.9 135.000
DSD Iringa – Msembe (Kalenga jct – Ipamba Hospital)0.5 150.000
Rehab. Nyololo – Kibao2.8 95.000
Rehab. Ilula – Kilolo 3.3 115.000
Rehabilitation of Kleruu Teachers College Access Roads (3.8km) to gravel standard3.3 115.000
Upgrading to DSD of Iringa – Msembe – Mapogoro (Kalenga Jct) – Ipamba Hospital (0.7km)  0.5 150.000
Sub – total: Iringa14.3 760.000
7Kagera  
Rehab. Kajai Swamp(1.5km) along Katoma – Bukwali road5.5 190.000
Rehab. Muhutwe  – Kamachumu – Muleba 5.5 190.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Bugene – Kaisho – Murongo (Rwabununka Escarpment). 5.0 170.000
Upgrading to DSD of Muleba – Kanyambogo – Rubya Road.0.8 255.000
Reha. Nyakahanga – Nyabionza – Nyakakika4.28 140.000
Upgrading to DSD of Kyakailabwa – Nyakato0.6 170.000
Upgrading to DSD of Katoma – Kanyigo0.5 140.000
Upgrading to DSD of Magoti – Makonge – Kanyangereko.0.4 120.000
Sub – total: Kagera22.6 1,375.000
8Katavi  
Rehab. Mamba – Kasansa2.4 85.000
Rehab. Mpanda – Ugalla0.0 –
Rehab. Mnyamasi – Ugalla1.5 50.000
Rehab. Kibo – Mwese1.3 45.000
Rehab. Inyonga – Ilunde3.0 105.000
Rehab. Kagwira – Karema1.5 50.000
Rehab. Kibaoni – Majimoto1.5 50.000
Rehab. Mpanda – Mnyamasi Jct1.5 50.000
Rehab. Mnyamasi – Mnyamasi Jct1.5 50.000
Rehab. Inyonga – Kavuu –Majimoto1.5 50.000
Rehab. Uzega – Kamsisi2.8 95.000
Upgrading to bitumen standard Inyonga Township road0.4 112.000
Upgrading to bitumen standard Usevya Township road0.3 105.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Upgrading to Bitumen standard  along Majimoto town center Road 1km 0.3 100.000
Sub–Total: Katavi19.7 947.000
9Kigoma  
Construction of Lwegele Bridge along Simbo – Ilagala – Kalya road100% 50.000
Rehabilitation of Kalya – Sibwesa Harbor Port1.5 50.000
Upgrading to Bitumen standard Katonga – Ujiji (construction of road embankment)0.3 90.000
Rehabilitation of Mwandiga – Chankere – Mwamgongo – Kagunga 2.6 90.000
Rehabilitation of Buhigwe – Bulimanyi – Kumsenga road 2.6 90.000
Rehabilitation of Bulimba – Lubalisi Section along Simbo – Kalya road1.7 55.000
Construction of Buhagara Bridge along Mwandiga – Chankere – Mwamgongo100% 55.000
Construction of sub structure at upper most Malagarasi river along Buhigwe – Kitanga – Kumsenga100% 85.000
Widening of Mwandiga – Mwanga Junction to dual carriageway0.3 85.000
Construction of Kamelavaha I and II Box Culverts  along Kalya – Sibwesa Harbor Port100% 55.000
Construction of Ikubulu I Box Culvert along Bulimba – Lubalisi road100% 55.000
Rehabilitation of Makere – Herushingo rod5.0 30.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Construction of Kabogo Box Culvert Culvert along Kalya – Sibwesa Harbor Port100% 45.000
Sub–Total: Kigoma9.0 835.000
10Kilimanjaro  
Upgrading to DSD Mwanga – Kikweni Vuchama/Lomwe 0.9 280.000
Rehab.Mwembe  – Myamba – Ndungu8.3 280.000
Upgrading to DSD of Makanya – Suji0.6 190.000
Upgrading of Masama – Machame Jct0.3 95.000
Rehab. Mandaka – Kilema Hospital7.0 390.000
Rehab. Kifaru – Handeni – Lang’ata4.1 140.000
Rau – Uru – Shimbwe Road3.0 105.000
Rehab. to paved Standard of Entrance Road and Roads within Tanzania Police College Moshi0.6 30.000
Sub–Total: Kilimanjaro24.9 1,510.000
11Lindi  
Rehab. Nanjilinji – Kiranjeranje – Namichiga 2.7 95.000
Rehab. Nangurukuru – Liwale 3.0 105.000
Rehab. Nachingwea – Lukuledi 2.7 95.000
Upgrading to DSD Ruangwa township roads0.4 130.000
Construction of Lukuledi bridge along Luchelengwa – Ndanda Road100% 110.000
Rehab. Ngongo – Ruangwa Jct Road (Milola Mountains) 2.7 90.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehabilitation of Tingi – Kipatimu (Upgrading of Ngoge Mountains 5km to DSD)0.3 90.000
Rehab of Ngongo – Ruangwa road3.0 100.000
Sub–Total: Lindi14.9 815.000
12Manyara  
Construction of Babati – Orkesumet/Kibaya (new access road)6.9 235.000
Rehab. Kibaya – Kibereshi road 3.3 112.000
Rehab. Nangwa – Gisambang – Kondoa Border3.3 112.000
Rehab. Mogitu – Haydom 3.3 112.000
Rehab. Magara Escarpment (concrete pavement) along Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu0.3 86.000
Babati – Kiru – Mbulu 2 (Rigid Pavement Construction on Steep Grade)0.3 86.000
Rehab Kutish Flood Plain along Singe – Kitomorok to raising embarkment and Culvert1.5 51.000
Sub–Total: Manyara18.9 794.000
13Mara  
Rehab. Musoma – Makojo Road2.7 95.000
Rehab. Balili – Mgeta – Manchimweli – Rimwani Road2.3 77.000
Upgrading to DSD Nyamuswa – Bunda – Kisorya – Nansio Road (Nansio – Kisorya)0.3 98.000
Upgrading to DSD Mika – Utegi – Shirati Road 0.5 98.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Upgrading to DSD Tarime – Nyamwaga road (Tarime – Nyamwigura Sect.) 0.5 103.000
Rehab. Makutano ya Kinesi – Kinesi1.7 57.000
Rehab. Nyamwigura – Gwitiryo1.7 57.000
Upgrading of Makoko Urban Road0.3 94.000
Upgrading to DSD Nyankanga – Rung’abure 0.3 93.000
Rehab. Nyankanga – Rung’abure 1.2 42.000
Rehabilitation of Mugumu – Fort Ikoma road including improvement of Mugumu urban drainage system2.8 94.000
Rehab of Muriba – Kegonga2.8 96.000
Upgrading to DSD of Kuruya – Kinesi0.3 90.000
Sub – total: Mara17.4 1,094.000
14Mbeya  
Rehab. Mbalizi – Shigamba – Isongole 3.0 102.000
Upgrading to DSD Igawa – Rujewa – Ubaruku0.2 60.000
Rehab. Ilongo – Usangu Road3.5 117.000
Upgrading of Access Road to MUST0.8 234.000
Rehab. Igurusi – Utengule – Luhanga road 3.2 108.000
Rehab. Kiwira – Isangati road 1.6 54.000
Upgrading to bitumen standard ( Mbalizi- Galula) Mbalizi – Mkwajuni – Makongolosi 0.6  187.000
Upgrading to DSD of Ushirika – Mpuguso0.4 108.000
Sub – total: Mbeya13.2 970.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
15Morogoro  
Rehab. Mahenge – Mwaya – Ilonga Road2.8 95.000
Upgrading to DSD Standard of Mlima Nyani and Mlima Simba Escarpment0.5 140.000
Rehab. Gairo – Nongwe Road3.6 121.000
Rehab. Ifakara – Taweta – Madeke Road (Taweta – Madeke Section) including Kidete Bridge3.6 121.000
Upgrading of Mahenge Township Road0.3 90.000
Rehab. Mchombe/Lukolongo – Ijia (Ijia Bridge)0.8 30.000
Rehab. Ifakara – Taweta – Madeke including crossing of Mgeta River for Mchombe/Lukolongo – Ijia0.8 30.000
Rehabilitation of Iyogwe – Chakwale – Ngiloli Road (6km)2.8 95.000
Construction of two relief box culverts along Dakawa/Wami Mbiki Game reserve – Lukenge/Songambele road 100% 115.000
Rehabilitation of Sokoine Agricultural Univesity Access Roads3.9 130.000
Rehabilitation of Mzumbe University Access Roads3.9 130.000
Upgrading to DSD of Gairo Primary School – Malimbika District Hospital Jct0.8 103.000
Sub – total: Morogoro23.7  1,200.000    
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
16Mtwara  
Upgrading to DSD Newala Township Roads 2.8 138.000
Rehab.Tandahimba – Litehu – Mkwiti Road0.5 98.000
Construction of Likwamba Bridge and approaches 3.6 95.000
Upgrading to DSD Kinorombedo Escarpment along Mkwiti (Kinorombedo) – Kitangali – Newala3.6 92.000
Rehab. Namikupa – Mitemaupinde (border road)0.3 67.000
Construction of Miesi, Nakalola and Shauri Moyo Bridges0.8 51.000
Rehabilitation  of Nangomba – Nanyumbu road to gravel standard0.8 64.000
Upgrading to DSD of Msijute Nanyamba2.8 93.000
Construction of Miesi, Chingwe, Makanya, Mwiti, Mchauru and Mbangala Bridges100% 84.000
Sub – total: Mtwara23.7782.000
17Mwanza  
Rehab. Kayenze – Nyanguge 1.8 60.000
Rehab. Kabanga Ferry – Mugogo – Nyakabanga 2.4 82.000
Rehab. Magu – Bukwimba – Ngudu – Hungumalwa Road2.5 84.000
Rehab. Lumeji – Nyashana Road 2.4 82.000
Construction of Sukuma (Simiyu II) bridge along Magu – Mahaha  100% 84.000
Rehab. Inonelwa – Kawekamo 2.1 72.000
Rehab. Ng’hwamhaya – Itongoitale2.0 67.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Road  
Rehab. Nyambiti – Sumve JCT – Fulo 2.1 72.000
Rehab. Sengerema – Kahunda (Nyehunge – Kahunda) Road2.5 84.000
Rehab. Mwanagwa – Misasi – Buhingo – Ihelele 2.4 82.000
Widening of Mwanza – Airport0.1 22.000
Nyakato – Mhonze0.3 84.000
Decongestion of urban roads in Mwanza (Nyakato Veta – Buswelu road section)0.3 84.000
Rehab. of Bukongo – Murutunguru2.5 84.000
Rehab of Ikoni – Sima Road2.4 82.000
Rehab of Sengerema – Katunguru1.5 51.000
Rehab of Mwanangwa – Salawe2.5 84.000
Rehab of Isandula – Magu – Jojiro1.4 47.000
Rahab of Nyangh’wale – Wingi 31.4 47.000
Upgrading to DSD of Mwanangwa – Misasi – Salawe2.2 75.000
Upgrading to DSD of Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge – Nzera – Nkome2.8 95.000
Sub – total: Mwanza31.2 1,524.000
18Njombe  
Rehab. Ndulamo – Nkenja – Kitulo – Mfumbi 1.4 47.000
Rehab. Njombe – Ndulamo – Makete0.0 –
Rehab. Kibena – Lupembe – Lufuji1.7 55.000
Rehab. Njombe – Iyayi Road 2.2 75.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab of Ikonda – Lupila – Mlangali (Lupila– Mlangali) 2.8 90.000
Upgrading to DSD Ludewa Townships0.2 55.000
Upgrading to DSD Igwachanya township roads0.3 90.000
Rehab. Igwachanya (Cholowe – Usuka – Kanamalenga – Ikingula (Mang’elenge)1.7 55.000
Rehab. Kikondo – Makete Road 2.0 66.000
Upgrading to DSD of Ikondal Hospital Road 0.5 150.000
Opening up of Lake Nyasa Off Shore Road along Lupingu – Makonde – Lumbila Road2.5 85.000
Upgrading to Bitumen Standard of Njombe Regional Hospital Road (1.7Km)0.3 93.000
Rehabilitation of Roads towards Tea Plantation Farms in Njombe (40 km)2.8 93.000
Rehabilitation of Ludewa – Lupingu road (28 km)   2.5 85.000
Upgrading to DSD of Makambako JWTZ Access Road (4Km)0.3 93.000
Sub–Total: Njombe21.0 1,132.000
19Rukwa  
Rehab. Ntendo – Muze (Kizungu hill)  Section to DSD0.8 250.000
Rehab.  Kasansa – Muze Road along Kasansa – Kamsamba 1.9 65.000
Rehab. Miangalua – Kipeta0.8 30.000
Rehab. Lyazumbi – Kabwe2.5 85.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Kalambanzite – Ilemba0.8 30.000
Rehab. Katongoro – Kipili (Kipili – Kipili New Port section – 4.5km)1.8 60.000
Upgrading to DSD Kizwite – Mkina0.2 55.000
Rehab. Laela – Mwimbi – Kizombwe3.0 102.000
Construction of Culvert along Kale – Luse – Kantalewa100% 46.000
Rehab. Kalepula Junction – Mambwenkoswe2.5 85.000
Rehabilitation of Kaengesa – Mwimbi – Mosi (Mwimbi – Mosi Section)3.7 125.000
Rehabilitation of Nkundi – Kate – Mkangale3.0 100.000
Rehab. Mtowisa – Ilemba – Kaoze – Kilyamatundu5.5 190.000
Sub–Total: Rukwa27.7 1,223.000
20Ruvuma  
Rehab. Azimio – Lukumbule – Tulingane (Lukumbule – Tulingane) 1.7 56.000
Opening up of Londo – Kilosa – Kwa Mpepo 0.8 30.000
Rehab. Chamani – Matuta – Mango – Kihagara Road 2.2 74.000
Upgrading to DSD Kilimo Mseto – Makambi Road 0.2 74.000
Upgrading to Otta seal Hilly section along Mtwara Pachani – Mkongo – Sasawala – Nalasi Road  0.2 75.000
Design and Start Construction of Fundi Mbanga Bridge along Tabora – Fundi Mbanga Road100% 20.000
Rehab Kitahi – Lituhi1.0 32.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehab. Matimila – Mkongo Road2.2 76.000
Rehab. Mpitimbi – Ndongosi – Nambendo Road2.2 75.000
Rehab. Mjimwema – Ngapa – Tunduru/Nachingwea Border1.7 56.000
Upgrading to DSD Unyoni – Kipapa – Chamani – Mkoha (Mawono Escarpment ) 0.3 90.000
Construction of Ruhuhu Bridge along Kitai – Kipingu (Ruvuma/Njombe Brd)100% 55.000
Construction of Mitomoni Bridge at Ruvuma River along Unyoni – Liparamba – Mkenda (Mitomoni) 100% 56.000
Construction of Ngapa bridge along Mindu – Ngapa (Nachingwea Border)100% 56.000
Rehabilitation of Unyoni – Liparamba1.7 56.000
Opening up of Songea Town bypass road (11.0km section)  1.9 65.000
Upgrading to DSD of Naikesi – Mtonya road (1.0km hilly section)0.2 60.000
Sub – Total: Ruvuma16.3 1,006.000
21Shinyanga  
Rehab Shinyanga – Old Shinyanga Road0.8 28.000
Construction of Vented Drift along Isagenye – Budekwa – Mwabalatu 100% 28.000
Rehab. Kahama – Bulige – Mwakitolyo – Solwa 1.7 56.000
Rehab Nyandekwa – Uyogo – Ng’hwande1.5 50.000
Rehab. Nyandekwa Jct – Butibu 0.8 30.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rehabilitation of Mwabomba – Ushetu3.0 100.000
Rehabilitation of Bugomba A – Ulowa – Uyowa2.5 85.000
Rehabilitation of Ntobo – Busangi – Ngaya – Nduku – Mwakuhenga – Mwankuba – Buluma – Jana – Didia and 2 Bridges2.8 93.000
Upgrading to Bitumen Standard of Kahama – Chambo0.3 85.000
Upgrading to Bitumen Standard of Kolandoto – Mhunze – Mwangongo0.3 84.000
Rehabilitation of Bulungwa – Ushetu1.6 55.000
Rehabilitation of Uyogo – Ulowa1.6 53.000
Upgrading to Bitumen Standard of Shinyanga – Old Shinyanga – Bubiki0.3 84.000
Sub – Total: Shinyanga17.1 831.000
22Songwe  
Rehab. Gagula – Namkukwe 2.2 75.000
Rehab. Igamba – Msangano – Utambulila2.2 75.000
Rehab. Isongole II – Isoko2.2 75.000
Rehab. Zelezeta – Isansa – Itaka2.2 75.000
Rehab. Hasamba – Nyimbili – Izyila – Itumba2.0 67.000
Rehab Ibungu (Rungwe) – Ibungu (Ileje) 3.3 110.000
Raising Embakment Msangano – Tindingoma  (6km) section along Igamba – Utambalila2.5 85.000
Rehabilitation of Kafwafwa – Ibungu (Ileje) 2.8 94.000
Sub–Total: Songwe19.4 656.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
23Simiyu  
Rehab Lugulu – Kadoto – Mallya0.8 28.000
Rehab. Maswa – Kadoto – Shishiyu – Jija – Maligisu Road2.8 93.000
Rehab. Mkoma – Makao road4.1 140.000
Rehab. Ngulyati – Miswaki – Ngasamo road2.8 93.000
Bridge major repair (Box culvert 3Cells) along Mwandoya – Ng’hoboko100% 140.000
Construction of new box culvert at access road to new Simiyu referral Hospital at Maperani area (Bariadi – Lamadi access road).100% 85.000
Nkoma – Makao District Road (Box Culvert Construction)100% 70.000
Sub – total: Simiyu10.5 649.000
24Singida  
Rehab. Soweto (Kiomboi) – Kisiriri – Chemchem Road & Construction of Reinforced Concrete Drift, Box Culvert and approaches  100% 75.000
Rehab Mkalama – Mwangeza – Kidarafa Road0.8 32.000
Construction of Msosa Box Culvert and Approach Roads along Iyumbu (Tabora border) – Mgungira – Mtunduru – Magereza Road100% 75.000
Rehab. Kizaga – Sepuka – Mlandala section2.2 75.000
Upgrading of Access Road to Kio       mboi Hospital0.2 45.000
Construction of 2 Box Culverts along Sepuka – Mlandala – Mgungira100% 85.000
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Construction of 2 Box Culverts along Sekenke – Tulya – Tygelo100% 85.000
Construction of Reinforcement Concrete Drift, Box Culverts and Approaches along Kisiriri – Chemchem Road100% 30.000
Rehab. Shelui – Sekenke – Tulya – Tygelo (Sekenke – Tygelo Road Section)2.5 80.000
Rehab. Heka – Sasilo – Iluma (Sasilo – Iluma section)2.5 80.000
Rehab. Sibiti – Matala and Construction of 2 Box Culverts100% 110.000
Rehab. of Ikungi – Londoni – Kilimatinde1.0 37.000
Sub – total: Singida9.2 809.000
25Tabora  
Rehab. Tutuo – Izimbili – Usoke 3.3 112.238
Rehab Nzega – Itobo – Bukooba1.7 56.119
Rehab. Sikonge – Mibono – Kipili 5.0 168.357
Rehab. Mambali – Bukene – Itobo3.9 130.945
Opening up of Kishelo – Kitunda3.3 112.238
Rehab. Kaliua – Lumbe road section3.3 112.238
Upgrading to DSD Urambo Township0.5 140.298
Opening of Igunga – Mbutu – Igurubi road1.2 39.180
Sub – total:Tabora22.1871.613
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
26Tanga  
Rehab. Mlalo – Mng’aro3.0102.000
Rehab. Muheza – Maramba2.792.000
Rehab. Mbaramo – Misozwe – Maramba – Kasera 2.792.000
Upgrading to DSD Magamba – Mlola 0.4107.000
Upgrading of Amani – Muheza to DSST0.4107.000
Rehab Bumbuli – Dindira – Korogwe1.862.000
Construction of 2 New Box Culverts along kwa Luguru – Kwekivu Jct 100%25.000
Construction of New Concrete T Beam Bridge (Multispan of 10m) along Songe – Kibereshi Road (Songe Bridge)100%20.000
Upgrading to DSD of Muheza 1 – Boza jct 0.4116.000
Rehabilitation of Bobomtoni – Mabokweni road0.930.000
Rehabilitation of Handeni – Kiberashi – Songe Road1.345.000
Rehabilitation of Kiomoni – Mjesani – Mlingano Road4.1140.000
Rehab of Songe – Vyadigwa – Mziha road 2.275.000
Sub – Total  – Tanga15.91,013.000
27Monitoring of roads and bridges projects, Maintanance of supervision vehicles , fuel and other road related activities (MoWT – Works) 1,000.000
Road Classfication activities  256.608
 Sub – Total    1,256.608
Na.                  Jina la MradiUrefu (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 SPECIFIC ROAD RELATED PROJECTS  
 Institute of Construction Technology (ICoT) – Mbeya Campus 875.000
Institute of Construction Technology (ICoT) – Morogoro Campus 975.000
Women Participation Unit (WPU) 250.000
Tanzania Transportation Technology Transfer Centre (TanT2 – Centre) 428.000
   Sub – total 2,528.00
 TOTAL REGIONAL ROADS410.85 30,731,221,000.00

KIAMBATISHO  NA. 5 

MUHTASARI WA MPANGO WA MATENGENEZO YA BARABARA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA

BARABARA MWAKA WA FEDHA 2022/23

BARABARA KUU

S/NMaintenance ActivityANNUAL PLAN 
PhysicalFinancial
UnitQtyEstimates (Tshs. Mio.)
1.0Routine & Recurrent – Pavedkm8,496.3453,213.788 
2.0Routine & Recurrent – Unpavedkm2,478.6011,807.217 
3.0Periodic Maintenance – Pavedkm 224.41 67,098.924 
4.0Periodic Maintenance            – Unpavedkm440.2810,093.848 
5.0Spot Improvement – Pavedkm17.70 8,860.000 
6.0Spot Improvement – Unpavedkm39.10 1,736.019 
7.0Bridges Preventive MtceNos.1,288 3,704.451 
8.0Bridges            Major RepairsNos.50 13,333.418 
 SUB-TOTAL Routine & Recurrentkm10,974.94 65,021.005 
 SUB-TOTAL Periodic & Spot Maintenancekm 721.49  87,788.791 
 SUB-TOTAL BridgesNos.1,338 17,037.869 
 JUMLA YA MAKADIRIO BARABARA KUU     169,847.665  
BARABARA ZA MIKOA 
S/NMaintenance ActivityANNUAL PLAN 
PhysicalFinancial
UnitQtyEstimates (Tshs. Mio.)
1.0Routine & Recurrent – Pavedkm1,953.08 12,367.619 
2.0Routine & Recurrent – Unpavedkm20,687.66 87,168.075 
S/NMaintenance ActivityANNUAL PLAN
PhysicalFinancial
UnitQtyEstimates (Tshs. Mio.)
3.0Periodic Maintenance – Pavedkm53.8 15,425.886 
4.0Periodic Maintenance          – Unpavedkm 3,346.62  60,598.531 
5.0Spot Improvement – Pavedkm43.27 24,934.794 
6.0Spot Improvement – Unpavedkm335.00 10,722.941 
7.0Bridges Preventive MtceNos.1,843 5,132.561 
8.0Bridges Major RepairsNos.16930,419.981 
 SUB-TOTAL Routine & Recurrentkm22,640.74 99,535.694 
 SUB TOTAL Periodic & Spot Maintenancekm 3,778.78   111,682.152 
 SUB TOTAL BridgesNos.2,012 35,552.542 
 Jumla ya Makadirio ya Barabara za Mikoa  246,270.389
 Jumla Barabara Kuu na za Mikoa (Mfuko wa Barabara)Routine (km)33,615.68416,618.054   
Periodic & Spot Improvement (km)4,500.28
Bridges (Nos)3,350
EMERGENCY  WORKS
1.0Emergency in FY 2022/23   21,648.708
 Sub Total   21,648.708
PMMR PROJECT PHASE TWO
1.0Works Implementation (BRT)   1,942.767 
2.0Works Implementation (2 Regions)   1,851.535 
         Sub Total    3,794.302 
WEIGHBRIDGE IMPROVEMENTS & MAJOR REPAIRS
1.0Improvements & Major Repairs   2,730.000 
2.0Improvement of   600.000 
S/NMaintenance ActivityANNUAL PLAN
PhysicalFinancial
UnitQtyEstimates (Tshs. Mio.)
 Weighbridge ICT and Network Equipment   
 Sub Total   3,330.000 
HQ BASED MAINTENANCE ACTIVITIES
1.0Road Mtce Manag. Systems    890.000 
2.0Road Data Collection   880.000 
3.0Bridge             Mtce Management System   500.000 
4.0Maintenance     Cost for Crane Lorry   45.000 
5.0Road Safety, Social and Environmental Activities   1,800.000 
6.0Road                 Act Enforcement   980.000 
7.0Corrugated Metal Pipe Culverts, Gabion Boxes and  Matresses   1,000.000 
8.0Important Signs for People              with Disabilities   750.000 
9.0Pavement Monitoring & Evaluation (CML)   741.153 
 Sub  Total   7,586.153
ADMINISTRATION AND SUPERVISION (Non Works)
1.0Administration Cost   24,522.664 
2.0Supervision Cost   25,218.312 
 Sub Total   49,740.976 
WEIGHBRIDGE OPERATIONS (Non Works)
1.0Weighbridge Operations   31,944.460 
 Sub  Total   31,944.460 
 JUMLA KUU YA MAKADIRIO YA FEDHA ZA MATENGENEZO (Mfuko wa Barabara)    534,662.653

KIAMBATISHO NA. 5(A 1)

MATENGENEZO YA KAWAIDA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA KUU

  • Barabara Kuu za Lami 
MkoaLengo (km)Bajeti  (Shilingi Milioni)
Arusha315.860 1,617.635 
Coast513.66 3,688.000 
Dar             es Salaam122.27 3,115.190 
Dodoma552.19 3,812.696 
Geita236.18 970.570 
Iringa393.89 3,030.910 
Kagera611.92 2,547.258 
Katavi74.90 255.797 
Kigoma299.39 1,179.421 
Kilimanjaro292.84 2,371.148 
Lindi347.97 3,194.806 
Manyara206.41 771.693 
Mara220.25 1,667.512 
Mbeya353.20 3,158.490 
Morogoro464.90 3,621.580 
Mtwara279.17 1,599.798 
Mwanza258.02 1,679.999 
Njombe201.21 899.997 
Rukwa136.33 1,635.823 
Ruvuma704.85 1,958.010 
Shinyanga225.11 1,299.991 
Simiyu212.26 1,287.300 
Singida386.30 3,317.000 
Songwe231.34 1,163.674 
Tabora528.67 1,549.999 
Tanga327.25 1,819.491 
Jumla         ya Barabara Kuu za Lami8,496.34 53,213.788 
  • Barabara Kuu za Changarawe/Udongo
MkoaLengo (km)Bajeti  (Shilingi Milioni)
Arusha128.52 128.737 
Dar es Salaam26.50 153.000 
Iringa68.01 501.342 
Kagera222.00 1,021.200 
Katavi247.75 1,439.505 
Kigoma106.02 632.310 
Mara86.00 585.000 
Mbeya187.00 1,026.755 
Morogoro398.10 1,615.015 
Njombe155.295 610.500 
Rukwa120.60 820.000 
Ruvuma213.77 1,069.323 
Shinyanga51.85 197.631 
Simiyu120.78 578.200 
Singida169.90 848.699 
Tabora176.50 580.000 
Jumla ya Barabara za Kuu za Changarawe/ Udongo2,478.60 11,807.217 
JUMLA KUU – Fedha za matengenezo ya Barabara kuu (Lami na Changarawe/ Udongo)10,974.94 65,021.005 

KIAMBATISHO NA. 5(A 2)

MATENGENEZO YA KAWAIDA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA ZA MIKOA

  • Barabara za Mikoa za Lami 
MkoaLengo (km)Bajeti  (Shilingi Milioni)
Arusha52.61 465.369 
Coast39.04 262.978 
Dar es Salaam272.21 2,407.360 
Dodoma47.86 211.754 
Geita161.22 623.048 
Iringa42.31 237.896 
Kagera122.63 506.591 
Katavi34.39 137.660 
Kilimanjaro176.34 1,293.865 
Lindi46.79 352.550 
Manyara42.46 228.447 
Mara101.70 698.123 
Mbeya74.60 184.565 
Morogoro70.38 634.269 
Mtwara147.29 714.160 
Mwanza29.46 183.998 
Njombe39.53 162.36 
Rukwa72.88 396.130 
Ruvuma32.00 178.758 
Shinyanga29.34 204.952 
Simiyu15.11 66.660 
Singida58.50 495.732 
Songwe13.50 150.744 
Tabora45.21 218.113 
Tanga185.72 1,351.535 
Jumla ya Barabara za Mikoa za Lami 1,953.08 12,367.619 
  • Barabara za Mikoa za Changarawe/Udongo 
MkoaLengo (km)Bajeti           (Shilingi Milioni)
Arusha665.13 3,267.643 
Coast836.71 2,030.680 
Dar es Salaam  1,040.130 
Dodoma981.85 3,919.851 
Geita530.95 3,115.000 
Iringa712.71 4,228.018 
Kagera909.14 4,227.591 
Katavi642.83 2,066.086 
Kigoma668.44 3,624.477 
Kilimanjaro591.97 2,613.250 
Lindi841.75 3,213.302 
Manyara1,408.09 3,349.999 
Mara859.37 3,606.998 
Mbeya614.70 3,497.175 
Morogoro1,059.10 5,477.644 
Mtwara762.67 2,031.040 
Mwanza826.28 3,118.962 
Njombe640.13 2,671.477 
Rukwa759.74 3,816.033 
Ruvuma1,213.48 5,224.635 
Shinyanga697.30 3,186.656 
Simiyu577.39 2,800.161 
Singida846.63 4,585.031 
Songwe615.80 3,791.536 
Tabora1,129.17 2,597.332 
Tanga1,296.33 4,067.369 
Jumla ya Barabara za Mikoa za Changarawe/ Udongo 20,687.66 87,168.075 
Jumla Kuu ya Fedha za matengenezo Barabara za Mikoa (Lami na Changarawe/ Udongo) 22,640.7499,535.694
JUMLA KUU – Fedha Za Matengenezo Ya Barabara Kuu Na Mikoa (Lami Na Changarawe/Udongo)33,615.68164,556.699

KIAMBATISHO NA. 5 (B 1)

MATENGENEZO       YA       MUDA       MAALUMU       (PERIODIC

MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA

KUU

(a)Barabara Kuu za Lami

MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
ArushaMakuyuni                      – Ngorongoro Gate 6.32 2,127.055
Sub total6.32  2,127.055
CoastKibaha – Mlandizi1.66 968.052
Mlandizi – Chalinze 3.32 1,843.909
Kongowe                        – Kimanzichana8.30 1,843.909
Kimanzichana – Kibiti0.55 645.368
Kibiti   –           Ikwiriri             – Nyamwage1.84 1,121.613
Bagamoyo – Msata0.46 507.075
Sub total16.13  6,929.925
Dar es SalaamNyerere Road0.92 2,536.785
Sub total0.92  2,536.785
Dodoma  Mtera (Dodoma/Iringa Boarder) –  Dodoma)6.45 2,425.450
Sub total6.45  2,425.450
Geita  Bwanga – Katoro – Ibanda (Geita/Mza Brd)4.61 1,646.869
Sub total4.61  1,646.869
Iringa TANZAM Highway2.77 1,015.680
Mafinga – Mgololo0.92 338.560
Sub total3.69  1,354.240
KageraMutukula – Bukoba –5.07 585.472
MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
   Kagoma-Kalebezo  
Bukoba – Bukoba Port1.84 388.182
Rusumo – Lusahunga 0.92 560.952
Kobero             –             Ngara – Nyakasanza2.77 145.959
Kyaka1 – Bugene4.61 151.182
Sub total15.21  1,831.748  
KataviMpanda      –       Msobwe (Katavi/Kigoma Bdr)0.46 189.001
Sub total0.46 189.001
Kigoma    Kanyani – Kasulu 0.92 27.659
Kigoma – Kidahwe – Kanyani18.16 1,216.980
Mwandiga – Manyovu3.50 196.883
Kigoma – Mwanga – Ujiji2.30 1,129.394
Tabora Brd – Uvinza – Kidahwe18.44 1,175.492
Sub total43.33  3,746.407
Kilimanjaro      Same – Himo Jct – KIA Jct5.53 1,610.627
Himo   Jct       –             Holili Customs0.92 322.131
Sub Total6.45  1,932.757
Lindi     Mtegu (Mtwara/Lindi Bdr) – Mingoyo – Mkungu4.61 1,371.628
Malendegu – Lindi – Mingoyo 8.30 871.459
Sub total12.91  2,243.087
Manyara    Bereko     –     Babati      – Minjingu2.03 1,843.909
Gehandu – Babati0.92 1,040.633
Subtotal2.95 
MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
   2,884.541
MaraMara/Simiyu      border- Sirari0.92 414.879
Musoma – Makutano chini0.92 414.879
Sub total1.84 829.76
Mbeya  TANZAM Highway4.61 2,302.827
Mbeya – Rungwa1.84 1,087.082
Sub total6.45  3,389.909
Morogoro        TANZAM Highway3.69 1,198.541
Morogoro – Dodoma9.22 2,858.058
Mikumi                          – Mahenge/Londo0.92 460.977
 Msamvu – Bigwa Jct.1.84 1,290.736
Sub total15.67  5,808.312
Mtwara       Mtwara – Mtegu9.22 1,524.424
Mkungu – Masasi3.69 1,060.247
Masasi – Mangaka7.38 1,170.578
Sub total20.28  3,755.249
Mwanza  Ibanda(Geita     Bdr)      – Usagara – Mwanza – Simiyu Bdr5.53 1,616.684
Shinyanga     border      – Kisesa3.69 1,447.247
Sub total9.22  3,063.931
NjombeLukumburu                   – Makambako8.301,235.491
Sub total8.30  1,235.491
RuvumaLumesule                      – Lukumbulu 8.30 2,829.039
Songea – Mbinga – Mbamba Bay3.69 1,221.336
Sub total11.994,050.375  
MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
ShinyangaTinde       –        Kahama- Wendele0.92 331.987
Sub total0.92 331.987
Simiyu  Ditiwa (Mza/Simiyu Brd) – Simiyu/Mara Brd2.12 430.921
Lamadi – Sapiwi – Bariadi – Wigelekelo0.88 826.246
Sub total3.00  1,257.168
SingidaKintinku (Dod/Singida Border)            – Singida/Tabora Border (Paved)5.07 2,824.407
Singida     –      Gehandu (Sgd/M’ra Border)0.92 815.008
Sub total5.99  3,639.415
SongweTANZAM Highway2.58 1,727.677
Tunduma-Mkutano (Songwe/Rukwa )0.28 184.307
 Sub total2.86  1,911.984
Tabora    SGD/TBR  Border – Nzega13.83 5,534.303
Nzega – Manonga (Shy Brd)0.92 276.586
Tabora        R/abt-Puge- Tazengwa         R/about- Kitangili-Nzega1.84 921.954
Kizengi – Tabora R/About – Miemba R/About0.92 691.466
Kaliua        –         Kaliua (Kasungu)0.92 553.173
  Sub total18.44  7,977.482
 TOTAL224.4167,098.924

(b) Barabara Kuu za Changarawe/Udongo

MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
Arusha Matala – Njia Panda30.28 804.465
Sub total30.28 804.465
Dar es Salaam   Nyerere Road (Unpaved Shoulders)6.00 60.000
New     Bagamoyo       Road (Unpaved shoulders)3.00 160.000
Sub total9.00 220.000
Iringa Mafinga – Mgololo (SPM)4.00 97.650
Sub total4.00 97.650
Kagera Bugene – Kasulo5.00 129.760
Omugakorongo                 – Murongo2 -Murongo3.00 100.000
Sub total8.00 229.760
Katavi  Lyambalyamfipa               – Mpanda – Uvinza86.00 2,026.850
Sub total86.00 2,026.850
KigomaKatavi/Kigoma            Brd             – Kasulu45.00 1,071.760
Kibondo         Police          – Mabamba jct – Burundi Brd19.00 460.020
Sub total64.00 1,531.780
Mara  Makutano Juu – Ikoma Gate 15.00 362.600
Sub total15.00 362.600
Mbeya  Mbeya        –          Rungwa (Mbeya/Singida Border) 21.00 509.770
Ibanda – Kiwira Port2.00 48.560
Sub total23.00 558.330
Morogoro  Kidatu             –             Ifakara             – Mahenge9.00 210.150
Lupiro – K/K/Mpepo – Londo22.00 510.760
Subtotal31.00 720.910
Njombe  Itoni – Ludewa – Manda33.00 789.820
Sub total33.00 789.820  
MkoaJina la BarabaraLengo (km)(Shilingi Milioni)
RuvumaLondo – Lumecha12.00 272.850
Likuyufusi – Mkenda (TZ/MOZ Brd)18.00 409.280
Sub total30.00 682.130
ShinyangaKolandoto – Mwangongo17.00 410.950
Sub total17.00 410.950
SimiyuMwangongo (Shy/Simiyu Brd)            –              Sibiti (Simiyu/Singida Brd)10.00 239.340
Subtotal10.00 239.340
Singida  Rungwa – Itigi – Mkiwa50.00 823.330
Sibiti (Shy/Sgd Brd) – Matala/Sibiti (Ars/Sgd Brd)5.00 95.933
Sub total55.00 919.263
Tabora    Rungwa (MBY/TBR Brd.) – Ipole 25.00 500.000
Sub total25.00 500.000
TOTAL440.2810,093.848

KIAMBATISHO NA. 5(B – 2)

MATENGENEZO YA MUDA MAALUMU (PERIODIC MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA

ZA MIKOA

  • Barabara za Mikoa za Lami
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Millioni)
ArushaKijenge – Usa river1.00 297.220
Sub total1.00 297.220
CoastMakofia-Mlandizi1.00 21.813
Sub total1.00 21.813
Dar           es SalaamDesignated Roads    
Kibamba-KwembeMakondeko5.00 220.000
Kigogo Round about – Jangwani1.77 354.084
Taifa Road (DUCE – Mandela Jctn)0.44 354.084
Sub total7.21 928.17
Dodoma  Chimwaga Jct – Chimwaga – Ihumwa1.00265.590
Sub total1.00265.590
 Geita    Msega (Geita/Kagera Bdr) – Bwanga4.50 1,064.023
Sub total4.50 1,064.023
Kagera         Bukoba CRDB – Kabangobay2.00 470.180
Kyamyworwa – Geita/Kagera brd1.50 250.000
Sub total3.50 720.180
KataviKawajense – Mnyamasi2.80 250.000
Kibaoni- Usevya-Majimoto4.20 339.243
Sub total7.00 589.243
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Millioni)
Kilimanjaro  Moshi(Fonga Gate) – Kikuletwa1.00 284.330
Sub total1.00 284.33
  ManyaraDareda – Dongobesh2.00 1,000.000
Sub total2.00 1,000.000
Mara    Nyankanga                   – Rung’abure ( 3.0 km Upgrading to DSD trouble spot)2.80 2,204.627
Mika      –      Utegi        ( Upgrading )0.65 693.306
Musoma     –      Makoko (Musoma Town  roads)0.30 234.067
Subtotal3.75 3,132.000
Morogoro  Mahenge – Ilonga2.00 556.273
Gairo – Nongwe1.48 486.620
Sub total3.48 1,042.893
Mwanza Mwanza -Kayenze Jct  -Airport 7.001,200.00
Nyakato – Buswelu – Mhonze2.00 2,731.660
Sub total9.002,731.660
Rukwa  Kizwite – Mkima1.00 1,252.320
Sub total1.00 1,252.320
Simiyu              Nyashimo – Ngasamo- Dutwa0.20 43.890
Bariadi- Salama0.20 66.000
Bariadi – Kisesa0.20 66.000
Mkula 1 – Mkula 20.10 28.875
Sub total0.70 204.765
Ruvuma                Mbinga – Litembo – Mkiri1.00 243.290
Sub total1.00 243.290
SingidaMisigiri            –             Kiomboi DBST4.00 400.000
Ikungi – Kilimatinde1.00 900.000
Iyumbu – Magereza1.20 700.000
Sub total6.20 2,000.000  
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Millioni)
Tabora  Miemba -Ulyankulu1.00 558.390
Sukonge – Kipili1.30 1,000.000
Ulyankulu – Urambo School2.00 1,222.000
Sub total4.30 2,780.39
TOTAL53.89 15,425.886
  • Barabara za Mikoa za Changarawe/Udongo
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Arusha              Mto     wa      Mbu      – Loliondo11.36 224.226
Kijenge – Usa River2.00 39.457
Usa          River           – Oldonyosambu 13.07 257.920
T/Packers – Losinyai 16.36 322.879
Karatu                        – Kilimapunda 28.03 552.992
Mbauda – Losinyai2.00 39.458
Longido                       – Oldonyolengai JCT11.29 222.793
Tengeru -Mererani24.36 480.712
Longido – Siha7.53 148.528
Wasso – Klens Gate3.76 74.264
Kimba – Makao5.65 111.396
Sub total125.41 2,474.625
Coast   Mbuyuni – Saadani8.00 259.925
Saadan(Kisauke)Makurunge3.00 349.042
Mbwewe – Lukigura Bridge4.00 133.676
Mandera – Saadani5.00 166.153
Chalinze – Magindu4.00 148.528
Makofia – Mlandizi 5.00 235.418
Mlandizi                     – Maneromango4.50 149.844
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Kiluvya – Mpuyani10.00 317.453
Pugu-Maneromango10.00 466.538
ManeromangoVikumburu7.20 229.224
Vikumburu Mloka7.00 296.163
Mkongo 2 – Ikwiriri6.50 259.925
Mkuranga – Kisiju4.20 289.012
Bungu – Nyamisati6.40 358.245
Utete – Nyamwage6.70 172.293
Kilindoni                     – Rasmkumbi7.00 410.848
Tamco – Vikawe – Mapinga2.00 109.168
Ubena Jct. – Lugoba2.00 92.454
Sub total102.50 4,443.908
Dar es Salaam    Kimara     –      Mwisho Bonyokwa- Kinyerezi5.00 297.057
Sub total5.00 297.057
Dodoma            Mtiriangwi/Gisambal ag – Kondoa5.00 114.690
Chali                  Igongo (Dodoma/Singida Boarder)                      –  Chidilo        Jct.          – Bihawana Jct.9.00 206.441
Olbolot – Dalai – Kolo15.00 344.069
Zamahero                   – Kwamtoro                   – Kinyamshindo10.00 229.379
Chenene – Izava5.00 114.690
Hogoro        Jct.          – Dosidossi10.00 229.379
Ntyuka Jct. – Mvumi -Kikombo Jct5.00 114.690
Chamwino – Ikulu Jct – Chamwino Ikulu – Dabalo – Itiso   10.00 229.379
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Pandambili – Mlali – Suguta – Mpwapwa – Ng’ambi15.00 344.069
Mpwapwa – Gulwe – Kibakwe – Rudi – Chipogoro15.00 344.069
Chunyu – Msagali2.50 61.114
Kibaigwa – Manyata Jct. – Ngomai – Njoge – Dongo(Dodoma/Man yara Boarder)8.00 183.503
Mpwapwa                   – Makutano Jct. – Pwaga Jct – Lumuma (Dodoma Morogoro Boader8.00 183.503
Ihumwa – Hombolo – Mayamaya 8.00 183.503
Sub total125.50 2,882.48
            Geita   Nyankanga (Kagera/Geita Bdr) – Nyamirembe Port14.00 184.250
Mkungo                      – Kasozibakaya (Kagera/Geita Bdr)1.00 33.496
Nyamadoke (Geita/Mwz Bdr) – Nzera6.00 136.002
Mtakuja – Bukoli – Buyange(Geita/Shy Bdr)20.00 323.768
Wingi 3(Mwz/Geita Bdr) – Nyang’holongo (Geita/Shy Bdr)26.00 417.678
Nyankumbu               – Nyang’hwale  20.00 253.979
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Chibingo – Bukondo Port14.00 167.494
Busarara                    – Rubambangwe10.00 267.997
Mugusu       –        Port Nungwe12.00 229.985
Nzera Jct (Geita) – Nzera – Nkome28.00 410.968
Katoro – Ushirombo30.00 502.490
Ushirombo – NandaBwelwa10.00 100.495
Muganza                     – Nyabugera – Mwelani2.00 71.327
Kibehe                        – Kikumbaitale2.00 61.645
Senga – Sungusila – Ibisabageni-Ikoni10.00 256.769
Butengolumasa – Iparamasa – Mbogwe – Masumbwe15.10 292.347
Sub total 222.17  3,710.692
Iringa  Igomaa (Iringa/Mbeya Border)                       – Kinyanambo ‘A’20.00 362.588
Samora        R/A         – Msembe 54.00 978.988
Ihawaga- Igowole18.00 326.332
Pawaga                  Jct- Itunundu5.00 90.647
Subtotal97.00 1,758.555
KageraBukoba       Crdb        – Kabangobay3.09 129.304
Kyaka-2 – Kanazi – Kyetema.3.09 161.535
Muhutwe                    – Kamachumu              – Muleba4.83 83.469
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Rusumo custom – Ngara4.83 85.567
Murugarama              – Rulenge – Nyakahura5.42 94.075
Magoti – Makonge – Kanyangereko1.93 87.131
Bugene – Nkwenda – Kaisho – Murongo 24.83 118.674
Amushenye                – Ruzinga 1.55 64.652
Katoma – Bukwali1.55 64.652
Kamachumu              – Ndolage1.55 28.758
Kasharunga – Ngote – Kasindaga1.55 55.873
Mwogo – Makonge – Ruhija2.90 48.169
Kigusha – Ntoma – Katembe0.97 21.536
Kamukubwa               – Nagetageta1.93 35.894
Izigo – Binego1.45 33.820
kigarama – Mabira – Kyerwa3.88 64.243
Sub total45.36 1,177.350
Katavi  Sitalike – Kibaoni – Kasansa17.00 304.565
Ifukutwa – Lugonesi14.50 244.376
Kagwira – Karema14.50 402.312
Majimoto – Inyonga17.40 304.565
Inyonga Jct – Ilunde – Kishelo17.40 304.565
Bulamata – Ifumbula – Ilango11.60 240.156
Sub total92.40 1,800.539
Kigoma             Ngara         Brd           – Nyaronga  – Kakonko18.00 297.057
B’Mulo        Brd          –5.00 82.433
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Nyaronga            
Mabamba       Jct        – Mabamba – Kifura13.00 215.366
Mugunzu – BukililoKinonko9.00 148.528
Kisili – Mahembe – Buhigwe21.00 347.557
Kalenze – Munzeze – Janda14.00 222.793
Simbo – Ilagala – Kalya71.00 1,153.324
Rusesa – Nyanganga – Kazuramimba4.50 74.264
Manyovu – Janda15.00 259.925
Buhigwe                     – Herushingo                – Kumsenga23.00 371.321
Sub total 193.500  3,172.568
Ki limanjaroKawawa – Nduoni3.00 53.856
Kwa Sadala – Kware – Lemira15.00 269.290
Mshiri – Kokirie1.00 17.950
Mamsera – Mahida5.00 89.763
Tarakea Jct-Tarakea Nayemi48.00 861.725
Kifaru     –     Butu      – Kichwa cha Ng’ombe25.00 448.816
Same-KisiwaniMkomazi49.00 879.705
Sub total 146.00  2,621.104
Lindi              Kilwa       Masoko       – Liwale (Naiwanga Jct – Njinjo)25.00 420.150
Liwale                         – Nachungwea- Lukuledi           30.00 504.180
Ngongo  – Ruangwa Jct)5.00 84.030
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
           Matangini – Chiola – Likunja5.00 84.030
Nachingwea                – Nanganga (Lindi/Mtwara Bdr)10.00 168.060
Nachingwea                – Kilimarondo15.00 251.615
Kiranjeranje                – Namichiga5.00 84.030
Mikao (Lindi/Mtwara Bdr) – Mtama10.00 168.060
Chekeleni                    – Likwachu (Lindi/Mtwara Bdr)10.00 168.060
Chiola – Ruponda20.00 336.120
Sub total 135.00  2,268.334
ManyaraLosinyai       East        – Losinyai 3.51 60.466
Kilimapunda               – Kidarafa 21.04 362.857
Losinyai – Njoro 21.04 362.857
Mbuyu                     wa Mjerumani – Mbulu 1 7.21 124.314
Lolkisale – Emboreti Jct3.51 60.466
Dareda – Dongobesh 11.92 205.587
Mogitu – Haydom 14.30 241.905
Ngarenaro(Babati)             – Mbulu 26.31 108.836
Singe – Sukuro Jct17.06 294.160
Kimotorok – Ngopito 12.17 209.796
Orkesumet – Gunge 5.88 101.404
Mererani – Landanai -Orkesumet        5.31 91.597
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Nangwa                       – Gisambalang 3.51 60.466
Kibaya – Olboloti3.51 60.466
Kibaya – Dosidosi 11.62 200.314
Dongo – Sunya – Kijungu10.51 181.292
Kibaya – Kiberashi9.31 160.502
Sub total167.71 2,887.28
Mara  Shirati – Kubiterere12.00 210.922
Mika – Ruari port15.00 264.396
Tarime – Natta25.00 439.429
Sirorisimba                 – Majimoto-Mto Mara18.00 290.651
Nyankanga                 – Rung’abure19.00 290.651
Musoma – Makojo29.00 523.831
Manyamanyama             – Nyambui5.00 97.070
Muriba Jct – Kegonga 13.00 227.823
Nyamwaga – Muriba4.00 64.589
Kuruya – Utegi10.00 175.249
Masonga  – Kirongwe4.00 71.806
 Balili – Mugeta chini.16.00 258.356
Mugeta                        – Manchimwelu          (Gusuhi)- Rig’wani6.00 96.884
Mugumu       –        Fort Ikoma9.00 177.620
 Nyamwigura              – Gwitiryo3.00 48.442
Kinesi Jnc- Kinesi4.00 64.589
Murito             -Gebaso- Mangucha 6.00 96.884
Kitaramanka               – Manguga- Busegwe5.00 80.736
Mugumu (Bomani) Tabora B-Kleins gate19.00 306.798
Sub total222.00 3,786.726
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Mbeya     Ushirika – Lutengano 1.90 34.860
Mbalizi – Chang’ombe2.90 52.290
Mbalizi – Shigamba 2.90 52.290
Kiwira – Isangati 2.90 52.290
Ilongo – Usangu2.90 52.290
Igurusi – Utengule Luhanga2.90 52.290
Rujewa – Madibira – Mbarali/Mfindi Brd5.80 86.548
Kikondo I – Mwela 1.90 34.860
Vensi – Maseshe Mswiswi 1.90 34.860
Kyimo – Kafwafwa1.90 34.860
Katumba – Lwangwa – Mbambo 5.80 86.548
Muungano – Lubele (Kasumulu) 1.00 34.861
Katumba                     – Lutengano – Kyimbila 1.90 34.860
Isyonje     –      Kikondo  (Iringa/Mbeya Border) 3.90 52.290
 Sub total 40.50 695.996
Morogoro       Dumila – Kilosa – Mikumi20.18 299.745
Sangasanga – Langali 19.19 285.160
Bigwa – Kisaki20.54 305.048
Msovini – Mikese12.86 190.993
Ifakara – Taweta42.41 629.976
Mahenge – Ilonga11.61 172.412
Madamu – Kinole1.16 17.244
Ngilori – ChakwaleIyongwe5.48 81.446
Ubena – Kiganila – Mvuha1.16 17.244
Gairo – Nongwe21.70 322.285
Sub total156.29 2,321.552  
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
    
Mtwara             Lukuledi – Masasi – Newala18.00 169.642
Nangomba                  – Nanyumbu9.67 150.009
Mbuyuni – Newala8.00 148.595
Mkwiti -Kitangari – Amkeni10.00 154.793
Matipa – Litehu – Kitama 11.60 161.404
Mpapura – Mikao – Kinolombedo (Linoha – Matipa)10.00 154.793
Msijute – Nanyamba23.00 191.973
Mahuta        Jct         – Malamba                    – Namikupa26.10 230.902
Madimba – Tangazo Kitaya- Mnongodi – Namikupa22.00 303.600
Tangazo – Kilambo9.67 150.009
Madimba – Mkaha Jct – Mitemaupinde28.00 315.291
Sub total176.04 2,131.009
Mwanza             Bupandwamhela       – Kanyala 4.00 76.789
Rugezi – Nansio – Bukongo –  Masonga10.00 191.973
Bukonyo                     – M/tunguru                 – Bulamba -Bukongo5.00 95.987
Bukokwa – Nyakaliro8.00 153.578
Sengerema – Ngoma4.00 76.789
Nyakato – Buswelu – Mhonze8.00 153.578
Nyehunge – Kahunda20.00 326.354
Kamanga                    – Nyamadoke24.00 441.538
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 (Geita/Mwanza Bdr)  
Sengerema                 – Katunguru13.00 249.565
Nyamazugo JCT (Sengerema) – Nyamazugo15.00 287.960
Kayenze        jct          – Kayenze – Nyanguge19.00 353.871
Mabuki – Jojiro – Luhala (Mwanza/Simiyu Bdr)8.00 153.578
Ngudu           2            – Nyamilama                 – Hungumalwa4.00 76.789
Ng’hwamhaya – kawekamo – Itongoitale      (Mz/Shy Bdr)14.00 268.762
Magu   –           Kabila             – Mahaha(Mwanza/Si miyu Bdr)18.00 345.552
Isandula     (Magu)     – Bukwimba -Ngudu 1 -Jojiro9.00 153.578
Fulo – Sumve JCT – Nyambiti 12.00  268.762
Nyang’hwale JCT – Ngoma – Wingi 3 (Mza/Geita Bdr) 5.00  95.987 
Mwanangwa – Misasi – Inonelwa – Salawe (Mza/Shy) 13.00  249.565 
Salama – Ng’hwaya 8.00  153.578 
Sub total221.00 4,174.135      
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Njombe  Kitulo – Matamba – Mfumbi  10.00 180.767
Mkiu      –       Ruhuhu Bridge (Njombe/Ruvuma border)15.00 246.788
Kikondo – Makete – Njombe20.00 280.088
Ibumila – Mlevela2.50 47.232
Ilunda – Igongolo2.00 31.228
Chalowe                      – Igwachanya                – Mn’gelenge6.50 98.853
Ikonda – Lupila – Mlangali15.00 316.931
Ndulamo – Nkenja – Kitulo I10.00 135.099
Njombe (Ramadhan) – Iyayi9.00 159.965
Ludewa – Lupingu5.50 83.733
Halali – Ilembula – Itulahumba8.00 122.989
Madeke – Kibena20.00 300.943
Kandamija – Kipingu2.00 31.228
Sub total125.502,035.84
Rukwa                 Mtimbwa – Ntalamila4.50113.624
Mtowisa – Ilemba10.00252.498
Kanazi – Namanyere – Kirando4.20106.049
Ntendo – Muze4.20106.049
Kaengesa – Mwimbi4.50113.624
Muze – Mtowisa4.50113.624
Laela – Mwimbi – Kizombwe4.20106.049
Kizwite – Mkima4.50113.624
Kasansa – Muze4.50113.624 
Kalepula       Jct         –4.20106.049
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Mambwenkoswe  
Ilemba – Kalambazite3.95 99.640
Sub total53.25 1,344.458
Ruvuma   Ruhuhu Bridge – Madaba Jct13.00 219.518
Peramiho – Kingole6.19 104.596
Mtwara     Pachani     – Nalasi48.00 810.535
Unyoni – Kipapa15.00 253.291
Mbinga – Litembo – Mkiri5.00 84.430
Mbambabay – Lituhi20.00 337.711
Kigonsera – Mbaha5.00 84.428
Kitai       –        Kipingu (Mbinga/Ludewa Brdr)20.00 337.717
Namtumbo – Likuyu5.00 84.431
Tunduru – Nalasi – Chamba13.00 219.512
Nangombo                  – Chiwindi5.00 84.428
Tanga(Pachani)          – Lugari5.00 84.430
Unyoni  Mpapa – Mkenda (Tz/Moz. Bdr )30.00 506.584
Mindu        JCT          – Nachingwea10.00 168.861
Mlilayoyo – Hanga4.83 84.444
Sub total205.02 3,464.92
Shinyanga    Itongoitale – Bunambiyu – Mwapalalu5.00 89.763
Buyange                     – Bulyanhulu     Jct             – Busoka19.00 341.096
Nyang’holongo (Gta/Shy      Brd)       –6.00 107.713
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Nyambula    
Ilogi – Bulyanhulu mine10.00 179.526
Kahama – Bulige – Mwakitolyo – Solwa5.00 89.763
Kanawa Jct – Kalitu – Manonga             River (Tbr/Shy Bdr)11.00 197.476
Kishapu – Buzinza19.00 341.096
Kanawa  – Mihama10.00 179.526
Kalitu                         – Mwamashele15.00 199.823
Shinyanga – Bubiki6.00 107.713
Salawe (Shy/Mz Brd) – Old Shinyanga21.20 375.285
Ukenyenge      JCT             – Ukenyenge2.80 53.856
Nyandekwa     Jct      – Nyandekwa – Butibu8.00 143.620
Nyandekwa – Uyogo – Ng’hwande (Shy/Tbr Brd)30.00 537.291
Bukooba – Kagongwa6.00 107.713
Sub total174.00 3,051.260
Simiyu      Luguru – Kadoto – Malya4.00 72.779
Bariadi – Kisesa – Mwandoya HC4.00 71.294
Nkoma – Makao4.00 71.294
Sub total 12.00  215.37 
Singida            Kidarafa             (Mny/Sgd Brd) – Nkungi5.00 71.244
Shelui – Sekenke – Tulya – Tygelo5.00 71.244
 Sepuka – Mlandala – Mgungira20.00 248.336
Iguguno Shamba –5.00 71.244
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Nduguti  – Gumanga  
Ilongero -Mtinko – Ndunguti5.00 71.244
Njuki – Ilongero – Ngamu5.00 71.244
Sabasaba – Sepuka – Ndago – Kizaga5.00 71.244
Ikungi – Londoni – Kilimatinde (Solya)5.00 71.244
Manyoni East – Heka – Sanza – Chali Igongo  10.00 142.488
Soweto (Kiomboi) – Kisiriri – Chemchem5.00 71.244
Iyumbu (Tbr/Sgd Brd) – Mgungira – Mtunduru                   – Magereza (Sgd)15.00 212.346
Kinyamshindo            – Kititimo5.00 71.244
Sub total90.00 1,244.365
SongweMlowo – Kamsamba  (Songwe/Rukwa Border)10.21 142.697
Chang’ombe                – Patamela7.98 108.450
Kafwafwa – Ibungu7.42 99.317
Saza – Kapalala 5.57 79.910
Isongole II – Isoko11.13 159.821
Zelezeta – Isansa – Itaka4.64 62.787
Igamba – Msangano – Utambalila5.57 79.910
Isansa – Itumpi3.70 48.517
Shigamba – Ibaba 9.28 125.973
Mahenje – Hasamba – Vwawa 4.64 62.785
Galula – Namkukwe 4.64 79.910
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Ihanda – Ipunga – Niumba42.69 455.692
Sub total117.47 1,505.769
Tabora          Miemba R/about – Ulyankulu12.00 185.661
Mambali        jct         – Mambali8.00 146.097
Ulyankulu – Kaliua8.00 111.396
Kaliua – Limbe – Ugalla8.00 111.396
Manonga – Igurubi10.00 148.528
Puge – Nkinga Jct10.00 148.528
Bukooba – Nzega8.00 110.070
Singonge – Kipili10.00 148.937
Ulyankulu – Urambo12.00 185.921
Kishelo- Kitunda15.00 383.025
Tura – Iyumbu10.00 163.961
Designated Roads –
Mbutu – Igurubi10.00 185.661
Sub total121.00 2,029.18
Tanga           Nyasa – Magamba5.00 86.206
Lushoto – Umba Jct5.00 86.206
Nkelei – Lukozi4.00 68.962
Malindi – Mtae6.00 103.458
Magamba – Mlola2.00 34.488
Vuga – Vuga Mission5.00 86.206
Bombomtoni – Umba Jct5.00 86.206
Old        Korogwe        – Bombomtoni10.00 172.412
Bombomtoni              – Mabokweni10.00 172.412
Boza Jct – Muheza 110.00 172.412
Mlingano       Jct        – Kiomoni Jct8.00 137.937
Tanga-M/Papa -Boza – Buyuni5.00 86.206
Mkalamo Jct – Mkata5.00 86.206
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 1  
Bombani – Kimbe2.00 34.482
Maguzoni       –       Old Korogwe5.00 86.206
Manyara       Brd        – Handeni – Kilole Jct8.00 137.953
Umba Jct – Mkomazi Jct5.00 86.206
Muheza – Bombani – Kwamkoro10.00 172.412
Silabu – Dindira20.00 344.824
Kwalugulu                  – Kibirashi5.00 86.206
Soni     –           Dindira             – Kwameta20.00 344.824
Mbaramo – Maramba 14.00 68.962
Tunguli Msamvu – Kibati jct4.00 68.962
Maramba        2         – Kwasongoro2.00 34.488
Vibaoni 2 – Mziha10.00 172.412
Kwekivu     Jct           – Iyogwe 5.00 86.206
Sub total180.00 3,103.46
 TOTAL 3,346.62   60,598.531

KIAMBATISHO NA.5 (C- 1)

MATENGENEZO YA SEHEMU KOROFI (SPOT IMPROVEMENT) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA

MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA KUU

  • Barabara Kuu za Lami 
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Coast  Mandera – Manga1.00 600.000
Kimanzichana – Kibiti0.10 280.000
Bunju – Bagamoyo0.70 310.000
Sub total1.80 1,190.000
Dar es Salaam  Kilwa Road 0.50 80.000
New Bagamoyo1.00 700.000
Mandela Road1.00 500.000
Nyerere Road (Shoulders, service roads, walk way, cyclists path )6.00 100.000
Installation of Marker posts, Bush Clearance & Preservation of Road reserve1.00 900.000
New Bagamoyo Road (Concrete Shoulder repair).0.50 300.000
Morogoro Road (Shoulder service roads, Access0.40 500.000
Sub total10.40 4,180.000
NjombeItoni – Ludewa – Manda Bay2.00 1,490.000
Sub total2.00 1,490.000
Singida   Kintinku (Dod/Singida Border) – Singida/Tabora Border (Paved)0.70 300.000
Sub total0.70 300.000    
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
TaboraMalendi (SGD/ TBR BDR) – Nzega1.30 1,000.000
Pangale         –         Miemba R/about1.00 200.000
Kizengi – Miemba0.50 500.000
Sub total2.80 1,700.000
TOTAL17.70 8,860.00
  • Barabara Kuu za Changarawe/Udongo
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Dar es salaamMorogoro Road(Construction Unpaved2.00 1,000.000
Sub total2.00 1,000.000
Iringa    Mafinga – Mgololo (SPM)3.00 12.000
Sub total3.00 12.000
Katavi  Mpanda – Uvinza1.80 27.000
Sub total1.80 27.000
Mara     Makutano Juu – Ikoma Gate 6.00 120.000
Sub total6.00 120.000
Mbeya  Mbeya – Rungwa (Mbeya/Singida Border) 1.00 24.870
Sub total1.00 24.870
Njombe  Itoni – Ludewa – Manda7.50 92.330
Sub total7.50 92.330
Rukwa              Sumbawanga – Lyamba Lya Mfipa (Chala – Paramawe & Kizi – Lyamba Lya Mfipa sections)1.00 20.829
Sumbawanga – Kasesya (Matai – Kasesya section)1.00 20.829
Sub total2.00 41.659
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Ruvuma           Londo – Lumecha0.10 1.500
Likiyufusi – Mkenda (Tz/Moz Brdr)0.30 3.500
Sub total0.40 5.000
Simiyu  Mwangongo (Shy/Simiyu     Brd)       – Sibiti5.00 120.410
Sub total5.00 120.410
Tabora              Rungwa (Mbeya Brd) – Ipole10.00 293.000
Sub total10.00 293.000
TOTAL39.10 1,736.02

KIAMBATISHO NA.5 (C- 2)

MATENGENEZO YA SEHEMU KOROFI (SPOT IMPROVEMENT) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA KWA

MWAKA WA FEDHA 2022/23 – BARABARA ZA MIKOA

  • Barabara za Mkoa za Lami
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Dar es SalaamKigamboni – Kibada – Dsm C/Brd1.00 940.000
Goba-Wazo      Hill-     Tegeta Kibaoni3.00 10.000
Ukonga Jct. – Chanika 0.50 700.000
Chanika -Mbande -Mbagala Rangi Tatu1.00 1,500.000
Sub Total5.503,279.000
CoastTAMCO-Vikawe-Mapinga0.80 850.000
Pugu-Maneromango0.40 850.804
Mkuranga-Kisiju0.80 850.000
Utete-Nyamwage0.80 850.000
Sub Total2.803,400.804
KataviKibaoni – Usevya3.00 1,600.000
Inyonga Jct – Ilunde3.00 1,500.000
Sub Total6.00 3,100.00
LindiTingi – Kipatimo (Ngoge hills)1.00 407.310
Ngongo – Ruangwa Jct (Milola Hills)1.00 407.310
Sub Total2.00 814.620
ManyaraDareda – Dongobesh1.50 850.000
Sub Total1.50 850.000
MaraNyankanga – Rung’abure 3.00 2,700.000
Musoma         –          Makoko (Musoma Town  roads)0.30 300.000
Sub Total3.303,000.000
   Mbuyuni – Newala1.40 500.700
Mkwiti – Kitangari – Amkeni1.40 500.700
MkoaJina la Barabara Lengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
MtwaraMadimba         –             Tangazo           – Namikupa1.40 500.700
Msijute – Nanyamba2.20 650.500
Newala Urban (Upgrading)1.40 500.700
Sub Total10.203,172.200
NjombeNdulamo – Nkenja – Kitulo I1.501,267.500
Njombe (Ramadhan) – Iyayi1.501,080.000
Sub Total3.00  2,347.500
ShinyangaShinyanga – Bubiki1.50 902.280
Sub Total1.50 902.280
SimiyuNyashimo – Ngasamo – Dutwa0.30 92.000
Sola Jct – Sakasaka1.00 643.000
Bariadi – Salama1.20 665.500
Bariadi – Kisesa (Urban Section)1.20 681.000
Maswa – Kadoto1.50 909.100
Mkula1 – Mkula 20.25 68.800
Sub Total5.453,059.400
SongweMahenje          –             Hasamba         – Vwawa 0.80 400.000
Sub Total0.80 400.000
TangaLushoto – Umba Jct0.60 601.270
Sub Total0.60 601.270
KigomaKasili – Mahembe -Buhigwe0.40 4.500
Simbo – Ilagala – Kalya0.20 3.000
Mugunzu        –        Bukililo- Kinonko0.02 0.200
Buhingwe-      Herushingo- Kumsenga 0.020
Sub Total0.62 7.720
 TOTAL43.2724,934.794
  • Barabara za Mkoa za Changarawe/Udongo
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Coast  Mbuyuni-Saadani0.55 6.500
Saadani – Makurunge3.40 35.500
Chalinze – Magindu3.25 34.500
Mbwewe – Lukigura Bridge6.92 69.200
Mandera – Saadani4.40 45.000
Makofia – Mlandizi1.35 15.000
Mlandizi – Maneromango5.25 52.500
Kiluvya –  Mpuyani1.45 16.750
Pugu-Maneromango1.72 18.950
Maneromango                      – Vikumburu3.40 34.000
Sub total31.69 327.900
Dar es Salaam                  Kibamba  Shule – Magoe Mpiji 1.00 1,500.000
 Makabe     Jct     –       Mbezi Msakuzi 0.40 270.000
 Temboni – Matosa –  Goba 1.81 200.000
 Chanika- Mbande 1.00 1,690.572
 Mjimwema- Pemba mnazi 1.00 350.000
 Buyuni II -Tundwisongani 0.60 90.000
 Sub Total 5.81  4,100.572  
 Designated Roads   
 Ununio – Mpigi Bridge 0.70 700.000
 Shaurimoyo                  Road (Karume) 0.70 129.000
 Sub Total 1.40 829.000
Dodoma          Chali                           Igongo (Dodoma/Singida Boarder)  –       Chidilo Jct. – Bihawana Jct.1.00 25.600
Olbolot – Dalai – Kolo1.00 25.600
Kondoa – Bicha- Dalai1.00 25.600
Zamahero – Kwamtoro – Kinyamshindo1.00 25.600
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Chenene – Izava1.00 25.600
 Hongoro – Dosidosi1.00 25.000
Chamwino – Ikulu Jct- Chamwino Ikulu-Dabalo- Itiso1.00 25.600
Pandambili – Mlali – Suguta – Mpwapwa – Suguta1.50 38.400
 Mpwapwa     –     Gulwe      – Kibakwe       –       Rudi        – Chipogoro1.00 25.600
 Mpwapwa – Makutano Jct –         Pwaga         Jct          – Lumuma(Dodoma Morogoro Brd) 1.00 25.600
Sub total10.50 268.200 
Geita     Mtakuja-Bukoli -Buyange4.40 86.000
Wingi3(Mwz/GeitaBrd-6.00 110.000
Katoro – Ushirombo5.60 104.000
Sub total16.00 300.000
Iringa       Samora R/A – Msembe 1.00 2.000
Pawaga Jct – Itunundu (Pawaga)2.00 9.000
Ilula – Kilolo5.00 19.500
Sub total8.00 30.500
Katavi    Ugalla – Mnyamasi0.35 5.250
Sitalike – Kasansa0.90 12.500
Ifukutwa – Lugonesi0.75 12.500
Kagwira – Karema0.40 6.000
Majimoto – Inyonga1.15 17.250
Inyonga Jct – Ilunde – Kishelo1.35 20.750
Sub total4.90 74.250      
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
Lindi  Tingi ( Njia nne) Kipatimo0.10 1.500
Kilwa           masoko            – Nangurukuru –  Liwale Road0.70 10.500
Sub total0.80 12.000
Manyara                              Kilimapunda – Kidarafa 1.35 31.248
Losinyai – Njoro 3.51 81.518
Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu 1 0.32 7.487
Lolkisale – Emboreti Jct0.56 13.030
Dareda – Dongobesh 1.10 25.550
Mogitu – Haydom 0.96 22.400
Ngarenaro(Babati) – Mbulu 20.54 12.626
Singe – Sukuro Jct4.04 93.909
Kimotorok – Ngopito 2.28 52.926
Orkesumet – Gunge 0.71 16.586
Mererani – Landanai Orkesumet0.90 20.963
Kibaya – Olboloti0.61 14.064
Kibaya – Dosidosi 1.54 35.681
Dongo – Sunya – Kijungu1.66 38.449
Kibaya – Kiberashi1.45 33.564
Sub total21.53 500.001
MaraShirati – Kubiterere5.00 97.500
Tarime – Natta6.00 117.000
Sirorisimba – MajimotoMto Mara4.00 78.000
Nyankanga – Rung’abure5.00 97.500
Musoma – Makojo4.00 78.000
Muriba Jct – Kegonga 7.00 136.500
Nyamwaga – Muriba1.00 19.500
Kuruya – Utegi4.00 78.000
 Balili – Mugeta chini.3.00 58.500
Mugumu – Fort Ikoma3.00 58.500
 Nyamwigura – Gwitiryo2.00 39.000
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Kinesi Jnc- Kinesi4.00 78.000
 Mugumu (Bomani) -Tabora B-Kleins gate8.00 156.000
Sub total56.001,092.000
MbeyaBujesi – Itete  0.40 6.000
Ushirika – Lutengano 0.10 1.500
Ipyana – Katumba Songwe 0.30 4.500
Mbalizi – Chang’ombe0.20 2.250
Mbalizi – Shigamba 0.30 4.500
Kiwira – Isangati 0.80 11.250
Igurusi            –             Utengule             Luhanga0.10 1.000
Rujewa     –     Madibira       – Mbarali/Mfindi Brd3.20 61.500
Kyimo – Kafwafwa0.30 3.750
Muungano        –         Lubele (Kasumulu) 1.00 18.750
Katumba – Lwangwa – Mbambo 1.00 22.000
Katumba     –      Lutengano- Kyimbila0.40 5.750
Masebe – Kyejo0.20 2.250
Ngana           –             Lubele (Kasumulu)0.70 9.750
Isyonje         –           Kikondo  (Iringa/Mbeya Border) 0.60 9.750
Sub total9.60 164.500
MorogoroMvomero – Ndole – Kibati – Lusanga0.01 0.090
Kiswira – Tawa0.10 1.500
Miyombo – Lumuma – Kidete0.26 2.600
Gairo – Nongwe0.19 2.350
Sub total0.56 6.540
MtwaraDumila – Kilosa – Mikumi0.15 2.250
Bigwa – Kisaki0.03 0.380
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Ifakara – Taweta0.25 2.800
 Gairo – Nongwe0.08 0.800
Sub total0.51 6.230
MwanzaNgudu 1 – Ngudu 2 – Malya(Mza/Simiyu Brd)0.90 14.000
Sub total0.90 14.000
Njombe  Kitulo II – Matamba – Mfumbi3.50 15.000
Mkiu           –           Ruhuhu Bridge(Njombe/Ruvuma Border)1.15 17.250
Kikondo II – Njombe2.90 43.500
Ilunda – Igongolo0.30 4.500
Ikonda – Lupila – Mlangali0.20 3.000
Ndulamo – Nkenja – Kitulo I0.50 6.000
Ramadhani – Iyayi0.45 6.750
Halali   –           Ilembula             – Itulahumba0.50 6.000
Kibena     –     Lupembe      – Madeke(Njombe/Morogoro border)4.50 75.000
Sub total14.00 177.000
Rukwa  Nkundi -Kate – Namanyere2.00 41.556
Mtimbwa – Ntalamila1.00 20.778
Kizwite – Mkima1.00 20.778
Kaengesa – Mwimbi1.00 20.778
Kasansa – Muze1.00 20.778
Muze – Mtowisa1.00 20.778
Mtowisa – Ilemba1.10 22.856
Ilemba – Kaoze1.20 24.934
Kaoze – Kilyamatundu1.00 20.778
Kalepula            Jct             – Mambwenkoswe1.00 20.778
Laela       –       Mwimbi        – Kizombwe2.00 41.556
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Msishindwe                          – Mambwekenya2.00 41.556
 Kanazi      –        Namanyere- Kirando1.00 20.778
Ntendo – Muze1.00 20.778
Sub total17.30 359.459
RuvumaPeramiho – Kingole1.35 21.750
Mtwara Pachani – Nalasi0.30 4.500
Unyoni – Kipapa0.10 1.500
Mbambay – Lituhi0.50 0.750
Kigonsera – Mbaha0.05 0.750
Kitai – Kipingu0.20 3.000
Tunduru         –           Nalasi             – Chamba0.40 6.000
Nangombo – Chiwindi0.10 1.000
Tanga(Pachani) – Lugari0.15 2.250
Unyoni  Mpapa – Mkenda (Tz/Moz. Bdr )0.15 2.250
Mlilayoyo – Hanga0.10 2.000
Naikesi – Mtonya0.15 2.250
Sub total3.55 48.000
ShinyangaMuhulidede – Tulole0.10 1.500
Sub Total0.10 1.500
SimiyuSola Jct – Mwandoya – Sakasaka3.00 73.000
Nkoma – Makao3.00 73.000
Sub total6.00 146.000
SongweMlowo       –         Kamsamba  (Songwe/Rukwa Border)10.00 220.000
Chang’ombe – Patamela10.00 232.320
 Kafwafwa – Ibungu5.00 110.000
Saza – Kapalala 5.00 110.000
Ndembo – Ngana5.00 110.000
Hasamba – Izyila – Itumba1.00 12.000
Ruanda – Nyimbili 0.10 1.000
MkoaJina la BarabaraLengo (km)Bajeti (Shilingi Milioni)
 Iseche – Ikonya0.70 9.750
 NAFCO – Magamba 0.10 0.520
Isansa – Itumpi1.00 17.000
Malenje – Lungwa 0.30 2.000
Sub total38.20 824.590
TaboraMiemba R/about – Usagali – Ulyankulu5.00 83.590
Mwambali – Bukumbi1.0020.000
Mambali Jct – Mambali4.5075.000
Mambali – Itobo2.5050.000
Ng’wande – Ulyankulu4.0050.000
Ulyankulu – Kaliua5.0080.000
Kaliua – Lumbe – Ugala4.0070.000
Manonga – Iborogero1.0015.000
Ziba – Choma1.0015.000
Puge – Nkinga1.0015.000
Bukooba – Nzega1.0015.000
Sikonge – Mibono – Kipili10.00110.320
Ulyankulu       –        Urambo School5.0080.000
Kishelo – Kitunda5.0046.280
Tura – Iyumbu6.0090.000
Designated Roads  
Mbutu – Igurubi5.0070.000
Bukumbi – Muhuludede5.0070.000
Sub total66.00955.19
TangaMalindi –  Mtae0.304.500
Magamba – Mlola0.101.500
Sub total0.406.000
 TOTAL 335.0010,722.941

KIAMBATISHO NA. 5 (D-1):

MATENGENEZO YA KAWAIDA YA MADARAJA (PREVENTIVE MAINTENANCE) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA

BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

  • Barabara Kuu 
Na.MkoaIdadi                  ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
1Arusha6825.747
2Coast91101.400
3Dar es Salaam1021.000
4Dodoma130305.637
5Geita1856.428
6Iringa122399.973
7Kagera12983.723
8Katavi2884.000
9Kigoma54155.500
10Kilimanjaro25169.630
11Lindi30317.997
12Manyara60120.000
13Mara25323.525
14Mbeya169179.840
15Morogoro70331.385
16Mtwara9384.000
17Mwanza184.516
18Njombe3296.000
19Rukwa1527.000
20Ruvuma1480.000
21Shinyanga34199.990
22Simiyu15140.500
23Singida20200.000
24Songwe2014.652
25Tabora930.000
26Tanga672.008
Jumla1,2883,704.451
  • Barabara za Mikoa
Na.MkoaIdadi ya MadarajaGharama (Milioni)
1Arusha3056.644
2Coast3942.374
3Dar es Salaam2987.050
4Dodoma178415.546
5Geita63100.360
6Iringa66250.028
7Kagera12269.032
8Katavi97263.000
9Kigoma140111.600
10Kilimanjaro35266.590
11Lindi25120.000
12Manyara63138.000
13Mara60450.000
14Mbeya144114.080
15Morogoro2871,034.133
16Mtwara1136.000
17Mwanza156.000
18Njombe6231.000
19Rukwa4575.600
20Ruvuma81409.500
21Shinyanga54317.314
22Simiyu21166.760
23Singida23230.000
24Songwe13380.750
25Tabora25153.000
26Tanga958.200
Jumla1,8435,132.561

KIAMBATISHO NA.5 (D – 2)

MATENGENEZO MAKUBWA YA MADARAJA (BRIDGE MAJOR REPAIR) KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA BARABARA

KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23

(a)Barabara Kuu

MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Arusha              Matala – Njiapanda2 542.890
Sub total2 542.890
Dar           es SalaamAlong New Bagamoyo road3 120.000
Along Mbezi Shule  and Tegeta2 2,200.000
Sub total5 2,320.000
Dodoma   Along Mtera(Dodoma/Iringa)1 1,200.000
Sub total1 1,200.000
Iringa    Along TANZAM Highway3 400.000
Along Iringa – Mtera (Iringa/Dodoma             Brd) road1 80.000
 Bridge along Mafinga – Mgololo (SPM) road1 50.000
Sub total10530.000
 Kagera  Rugazi Bridge along Mutukula – Bukoba Kalebezo1 166.830
Sub total1 166.830
Lindi Bridge                     along Marendegu – Mingoyo road 1 144.930
Sub total1 144.930
ManyaraBridges along Bereko – Minjingu2 500.000
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Sub total2 500.000
Mara Bridge                      along Mara/Simiyu border – Sirari road2 3,868.807
Sub total2 3,868.807
MbeyaBridges along TANZAM Highway3 133.954
Sub total3 133.954
MorogoroBridges along TANZAM Highway4 116.000
Bridges along Morogoro – Dodoma4 750.000
Bridge along Mikumi- Mahenge1 60.000
Sub total9 926.000
MwanzaSimiyu Bridge along Ibanda(Geita Bdr) – Usagara – Mwanza – Simiyu Bdr2 1,100.000
Sub total2 1,100.000
Njombe    Lukumburu                      – Makambako 2 25.000
Itoni – Ludewa – Manda (Ibani, Mkondachi &Nsungu)3 60.000
Sub total5 85.000
RukwaBridge                       along  Sumbawanga – Lyamba Lya     Mfipa     (Chala       – Paramawe Section) 1 420.000
Sub total1 420.000
RuvumaMkayukayu Bridge along Likuyufusi – Mkenda (Tz/Moz Brdr)3 400.000
Along Londo – Lumecha2 65.000
Sub total5 465.000
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
SimiyuAlong         Lamadi           – Wigelekelo1 135.007
Sub total1 135.007
    Singida  Kintinku – Singida – Malendi1 100.000
Rungwa – Itigi – Mkiwa2 250.000
Sibiti – Matala1 200.000
Sub total4 550.000
TaboraSGD/TBR Brd – Nzega6 125.000
Sub total6 125.000
Songwe    Mkutano Bridge along TANZAM Highway1 120.000
Sub total1 120.000
 TOTAL50 13,333.418

(b)  Barabara za Mikoa

MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Arusha  Usa river – Oldonyosambu1 814.432
Tengeru – Mererani1 236.000
Sub total2 1,050.432
CoastKisauke Barley Bridge along Saadan (Kisauke) – Makurunge1 100.000
Along Makofia – Mlandizi1 550.000
Along Kiluvya – Mpuyani1 250.000
Mbambe Bridge (tImber) along Mkongo 2 – Ikwiriri1 40.000
Sub total4 940.000
   Kifuru – Pugu Station1 30.000
Mkoa  Dar        es SalaamJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Sangatini along Kivukoni –      Kibada      –       Tundwi Songani1700.000
Bonyokwa Bridge along Kimara         Mwisho          – Bonyokwa – Kinyerezi350.000
Sub total5780.000
DodomaAlong Mtiriangwi/GisambalagKondoa1150.000
Chaligongo Drift along Chali Igongo – Chidilo Jct. – Bihawana Jct., R.4333105.000
Busi Drift along Olbolot – Dalai – Kolo, R.4614330.000
Chenene- Izava1 150.000
Ntyuka Jct – Mvumi- Kikombo1 180.000
Along Chamwino Ikulu1 55.000
Mbande     –     Kongwa      – Suguta1 150.000
Pandambili       –        Mlali- Suguta-Mpwapwa              – Ng’ambi2 475.000
Mpwapwa-Gulwe- Kibakwe5 270.000
Along Kibwaigwa-Manyata Jct-Ngomai1 180.000
Along        Mpwapwa         – Makutano1 80.000
Sub total21 2,125.000
Geita Swakala Bridge along Ushirombo – Nanda  – Bwelwa 1 70.000
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
 Ikulwa      Bridge       along Nyankumbu                       – Nyangh’wale Road  1 80.000
Sub total2 150.000
Iringa A bridge along Samora R/A – Msembe road1 118.000
Bridge along             IgomaKinyanambo road1 95.875
Bridge along Samora R/A – Msembe road1 120.000
Bridge     along      Ihawaga- Igowole road1 220.000
Nyalengu     bridge      along Ilula – Kilolo road1 88.000
Mgega       bridge        along Mbalamaziwa                     – Kwatwanga road1 95.000
Sub total6 736.875
KageraBridge along Nyabihanga- Kasambya- Minziro1 58.000
Bridge along Rutenge – Rubale-Kishoju2 116.000
Sub total3 174.000
KataviBridge along Katete – Kibaoni3 200.510
Bridge along Sitalike – Kasansa1 98.000
Bridges along Kagwira – Karema 2 196.000
 Bridges along Inyonga – Ilunde2 196.000
Sub total8 690.510
KigomaBridges along Simbo – Ilagala – Kalya6 950.000
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Bridge along Buhigwe – Herushingo – Kumsenga1 270.000
 Sub total7 1,220.000
KilimanjaroBridges along Tarakea Jct- Tarakea Nayemi2 465.750
Bridges      along       Kifaru- Butu-Kichwa                 cha Ng’ombe2 222.000
Bridge       along        Same- Kisiwani-Mkomazi1 302.950
Bridge along Same kwa Mgonja-BangalalaMkanya1 317.900
Bridge along MwembeNdungu4 585.800
Mwanga – Lang’ata1 481.200
Sub total11 2,375.600
LindiBridges along Liwale – Nachingwea1 90.000
Bridges along Kilwa Masoko – Nangurukuru3 190.000
Bridges along Tingi – Kipatimu road2 100.000
Bridges                       along Kiranjeranje – Nanjirinji2 160.000
Bridges along Matangini Chiola – Likunja1 90.000
Sub total9 630.000
ManyaraBridges along Mbuyu wa Mjerumani2 200.000
Bridge along Dareda – Dongobesh1 300.000
Bridge along Dongo – Sunya – Kijungu1 200.000
Sub total4 700.000  
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
MaraSerengeti A bridge along Mugumu – Tabora B – Kleins gate2 500.000
Bridge along Tarime – Natta1 250.000
Bridge along Nyank’anga – Rung’abure 1 200.000
Sub total4 950.000
Mbeya        Bridge along Mbalinzi – Chang’ombe  1 150.000
Bridge along Madibira – Mbalali1 635.000
Bridge along Kiwira – Isangati 1 350.000
Sub total3 1,135.000
Morogoro      Bridge along Mvomero – Lusanga1 60.000
Bridge along Dumila – Kilosa – Mikumi1 150.000
Bridge along Msovini Mikese1 110.000
Bridge along Ngilori – Chakwale- Iyogwe1 120.000
Sub total4 440.000
Mtwara   Bridge (Mkaha Jct – Mapili – Mitemaupinde)4 1,929.870
Sub total4 1,929.870
MwanzaBridge along Nyakato – Buswelu – Mhonze1 510.000
Sub total1 510.000
Njombe  Mkiu    – Ruhuhu(Njombe/Ruvuma Border)1 350.000
Mlangali – Ikonda1 130.000 
Chalowe – Igwachanya –1 215.000
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Usuka     –      Kanamalenga (Mtemela Bridge)  
Sub total3 695.000
Rukwa             Bridge along  Kasansa – Muze  Road1 460.000
Bridge along  Kaengesa – Mwimbi  Road1 230.000
Along   Muze- Mtowisa Road1 230.000
 Ilemba – Kaoze Regional Road1 230.000
Along Mtowisa – Ilemba  Regional Road3 629.916
Bridge along  Kalepula – Mambwenkoswe  Road1 230.000
Bridge along Laela – Mwimbi – kizombwe Regional1 230.000
 Kanazi – Namanyere – Kirando Regional Road2 460.000
Ntendo – Muze  Regional Road1 230.000
 Ilemba – Kalambazite Regional Road1 230.000
Sub total13 3,159.916
RuvumaBridge along Peramiho – Kingole1 65.000
Bridges     along       Mtwara Pachani – Nalasi4 210.000
Bridge along Unyoni – Kipapa1 65.000
Bridge along Mbinga – Litembo – Mkiri  1 65.000
Bridges                        along3 414.347
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Mbambabay – Lituhi  
Bridge along Kigonsera – Mbaha1 75.000
Liwinda,         Ndiva           & Mnywamaji Bridges along Kitai           –             Kipingu (Mbinga/Ludewa Brdr)3 100.000
Lihutika          Bridge along Namtumbo – Likuyu1 85.000
Nasanga     Bridge       along Azimio – Tulingane1 65.000
Ndongochi Bridge along Nangombo – Chiwindi1 65.000
Pisi & Lumeme Bridges along Unyoni  Mpapa – Mkenda (Tz/Moz. Bdr )2 65.000
Naikesi – Mtonya1 75.000
Lumesule Bridge along Mindu Jct – Nachingwea Bdr1 85.000
Sub total21 1,434.347
Shinyanga     Along Buyange – Busoka1 145.000
Along   Nyang’holongo             – Nyambula1 320.000
Along Kishapu – Buzinza1 150.000
Kanawa – Mihama1 450.000
Salawe – Oldshinyanga1 150.000
Bukooba – Kagongwa1 150.000
Nyandekwa Jct – Butibu2 450.000
Wishiteleja Bridge along Ngundangali – Wishiteleja2 700.000
Sub total10 2,515.00
SimiyuBridges along Bariadi – Salama             1 401.400
Mwandoya – Ng’oboko1 274.860
Bridges along Sola Jct –2 425.360
MkoaJina la BarabaraIdadi ya MadarajaBajeti (Shilingi Millioni)
Sakasaka Regional Road.  
 Sub total4 1,101.620
SingidaShelui – Tygelo1 300.000
Kidarafa (Mny/Sgd Brd) – Nkungi1 100.000
Iguguno- Shamba1 100.000
Njuki – Ilongero- Ngamu1 100.000
Sub total5 600.000
SongweSaza 1 Bridge along Saza – Kapalala3 1,336.000
Sub total3 1,336.000
TaboraBridge       Major        Repair  along         Ng’wande           – Ulyankulu  1 112.967
“Bridges along Mibono – Kipili 2 291.700
“Bridges along Tura – Iyumbu2 195.494
“Bridges along Tutuo – Usoke1 800.000
Sub total6 1,400.161
Tanga   Old           Korogwe             – Bombomtoni Road1 293.250
Mkalamo- Mkata1 320.500
Bombani – Kimbe2 324.100
Mbaramo – Maramba1 271.200
Kwaluguru – Kiberashi Road1 381.600
Sub total6 1,590.650
TOTAL169 30,419.981
 GRAND TOTAL (TRUNK & REGIONAL ROADS BRIDGES) 219 43,753.399

KIAMBATISHO NA. 6

MGAWANYO WA FEDHA ZA MAENDELEO KWA SEKTA YA

UCHUKUZI NA TAASISI ZAKE KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

NA. YA MRADIJINA LA MRADIMAKADIRIO KWA MWAKA 2022/2023  (Sh. Milioni)  CHANZO CHA FEDHA
FEDHA ZA NDANIFEDHA ZA NJEJUMLA
12345 (3+4)6
 KIFUNGU 1003: SERA NA MIPANGO 
6267 Institutional Support  
Operationalization of TB III JNIA17,300.0017,300.00GoT 
 Dar Es Salaam Maritime Institute (DMI)1,000.001,000.00 
4201Lake Victoria Maritime and Transport Project4,157.244,157.24AfDB
4227Dar es Salaam Maritime Gateway Project (DMGP)100,112.82100,112.82WB
 JUMLA NDOGO18,300.00104,270.06122,570.06 
 KIFUNGU 2005: MIUNDOMBINU YA UCHUKUZI 
4213Rail       Infrastructure Fund 294,801.62294,801.62GoT
4216Tanzania Intermodal Railway Project (TIRP II)9,193.259,193.25WB
4281Construction of New Standard Gauge Rail 1,263,000.00 1,263,000.00GoT
  JUMLA NDOGO  1,557,801.6 2 9,193.25  1,566,994.87 
 KIFUNGU 2006: HUDUMA ZA UCHUKUZI 
4290TMA radar, Equipment and Infrastructure20,000.0020,000.00GoT
4294Acquisition           of               New Aircrafts (ATCL)468,000.00468,000.00GoT
NA. YA MRADIJINA LA MRADIMAKADIRIO KWA MWAKA 2022/2023  (Sh. Milioni)  CHANZO CHA FEDHA
FEDHA ZA NDANIFEDHA ZA NJEJUMLA
12345 (3+4)6
4295Procurement and Rehabilitation of Marine Vessels (MSCL)113,706.82113,706.82GoT
   6377Infrastructure Development and Procurement of Training          Equipment (NIT)1,770.001,770.00GoT
4211Rail Rehabilitation and SBU Improvement for TAZARA13,193.1713,193.17GoT
 JUMLA MDOGO616,669.99– 616,669.99 
 JUMLA2,192,771.62113,463.312,306,234.93 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *