HOTUBA YA WAZIRI BASHE BUNGENI-Makadirio ya Mapato na Matumizi 2022/2023

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO, MHESHIMIWA HUSSEIN MOHAMED BASHE (MB), KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI  YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO  KWA MWAKA 2022/2023

YALIYOMO

DIRA …………………………………………………………………………………………………… 1

DHIMA ……………………………………………………………………………………………….. 1

Majukumu ya Wizara ……………………………………………………………………… 2

    1.1       Mchango wa Serikali katika Sekta ya Kilimo kwa

           Awamu zote Sita za Uongozi ………………………………………. 9

    1.2       Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika

           Sekta ya Kilimo ……………………………………………………………. 14 4.1.1.    Makusanyo ya Maduhuli ………………………………………… 30

     4.1.2.       Fedha Zilizoidhinishwa kwa Mafungu Yote (43,

               24 na 05) …………………………………………………………………… 30

     4.1.3.     Makusanyo ya Maduhuli ………………………………………… 30

     4.1.4.       Fedha Zilizoidhinishwa kwa Mafungu Yote (43,

               24 na 05) …………………………………………………………………… 31

               Fungu 43 ………………………………………………………………………… 32

     4.1.5.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida ……………………………. 32

     4.1.6.      Matumizi ya Bajeti ya Maendeleo ……………………….. 33

                   Fungu 05 ………………………………………………………………………… 33

     4.1.7.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida ……………………………. 33

     4.1.8.      Matumizi ya Bajeti ya Maendeleo ……………………….. 34

                   Fungu 24 ………………………………………………………………………… 34

     4.1.9.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida ……………………………. 35

    4.2. UTEKELEZAJI WA MAENEO YA KIPAUMBELE KWA

           MWAKA 2021/2022 ………………………………………………………… 36

     4.2.1.      Utafiti wa Kilimo …………………………………………………….. 36

4.2.1.1.    Utafiti wa Mbegu Bora na teknolojia za kilimo .. 36

4.2.1.2.    Vituo vya Utafiti …………………………………………………….. 39

     4.2.2.      Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo …………………… 40

4.2.2.1. Mbegu Bora ………………………………………………………….. 40 4.2.2.2. Mbolea …………………………………………………………………… 49

4.2.2.3. Viuatilifu ………………………………………………………………. 51 4.2.2.4. Zana za Kilimo ……………………………………………………. 57

4.2.3. Huduma  na Mafunzo ya Ugani ……………………………. 60 4.2.3.1.        Huduma za ugani ……………………………………………….. 60

     4.2.3.2.       Mafunzo ya Ugani ………………………………………………. 61

     4.2.3.3.       Ukarabati wa Vyuo vya Kilimo na Vituo vya

                   Mafunzo kwa Wakulima …………………………………… 66

     4.2.3.4.       Udahili wa wanafunzi katika Vyuo vya

                  Mafunzo ya Kilimo ……………………………………………… 67 4.2.4. Umwagiliaji ………………………………………………………………. 68

4.2.4.1.        Ujenzi wa Miradi ya Umwagiliaji …………………….. 68 4.2.4.2.            Ukarabati wa Miradi ya Umwagiliaji ………………. 70

     4.2.4.3.       Miradi ya Umwagiliaji Inayofanyiwa 

         Upembuzi yakinifu na Usanifu ………………………… 71 4.2.5.   Masoko na Mifumo ya Masoko …………………………….. 75 4.2.6.            Taasisi za Fedha na Upatikanaji wa Mitaji ……….. 87

4.2.7.           Uzalishaji wa Mazao ……………………………………………….. 90 4.2.7.1.        Mazao Asilia ya Biashara ………………………………….. 91                          i. Zao la Mkonge ………………………………………………….. 92                            ii. Zao la Tumbaku ………………………………………………. 92                iii. Zao la Pareto ……………………………………………………. 93                    iv. Zao la Chai ……………………………………………………….. 93                 v. Zao la Korosho ………………………………………………… 95                   vi. Zao la Kahawa ………………………………………………….. 97                              vii. Zao la Pamba ……………………………………………………. 98 4.2.7.2.       Mazao ya Chakula ………………………………………………. 99

     4.2.7.3.       Mazao yenye mahitaji makubwa 

         yanayoagizwa nje ya nchi ………………………………. 100                  i. Uzalishaji wa Miwa na Sukari …………………….. 100                          ii. Zao la Ngano ………………………………………………….. 102                         iii. Mazao ya Mbegu za Mafuta ………………………… 104 4.2.7.4.      Mazao ya Bustani ……………………………………………… 106

     4.2.8.      Uanzishaji wa Mashamba Makubwa ya Kilimo . 109

     4.2.9.    Kuimarisha Miundombinu ya Kuhifadhi Mazao 

               ya Kilimo ………………………………………………………………… 110

4.2.10. Uongezaji Thamani wa Mazao ya Kilimo ………………… 112 4.2.11. Maendeleo ya Ushirika ………………………………………… 114 4.2.11.1. Ushiriki wa Vijana katika Kilimo ………………….. 120 4.2.11.2. Uhifadhi wa Mazingira …………………………………….. 122 4.2.11.3. Lishe ……………………………………………………………………. 125 4.2.11.4. Jinsia …………………………………………………………………… 129 4.2.11.5. VVU na UKIMWI ………………………………………………… 130 5.1. Kuimarisha Utafiti ……………………………………………………. 139

     5.2.      Kuimarisha Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo . 143

     5.3.     Umwagiliaji …………………………………………………………………. 155

     5.4.      Kuimarisha Huduma za Ugani ……………………………….. 159

     5.5.      Uzalishaji wa mazao …………………………………………………. 164

5.6. Upatikanaji wa Masoko ya Mazao ya Kilimo ………. 196 5.7. Taasisi za Fedha na Upatikanaji wa Mitaji ………….. 200

     5.8.      Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo …………………………….. 202

     5.9.      Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya 

           Hifadhi ya Mazao ya Kilimo ……………………………………. 203

     5.10.        Kuhamasisha Kilimo cha Mashamba 

               Makubwa …………………………………………………………………. 204

     5.11.        Kuimarisha Kilimo Anga …………………………………….. 206

     5.12.       Maendeleo ya Ushirika ………………………………………… 207

     5.13.        Ushiriki wa Vijana katika Sekta ya Kilimo …….. 209

     5.14.       Lishe ………………………………………………………………………… 213

     5.15.        Matumizi ya Teknolojia na Mbinu za Kilimo

                 Kinachohimili Mabadiliko ya Tabianchi …………….. 215

5.16. Jinsia ……………………………………………………………………….. 216 5.17. VVU na UKIMWI …………………………………………………….. 216 7.1. Makusanyo ya Maduhuli ………………………………………….. 224 7.2. Fedha kwa Mafungu yote (43, 24 na  05) …………….. 225

     7.3.     Fedha kwa Fungu 43 ………………………………………………… 225

7.4. Fedha kwa Fungu 05 ………………………………………………… 226 7.5. Fedha kwa Fungu 24 ………………………………………………… 226

VIAMBATISHO …………………………………………………………………………….. 228

VIFUPISHO VYA MANENO

AGITF  Agricultural Inputs Trust Fund 
AMCOSAgricultural Marketing Cooperatives Societies
AMDTAgricultural Market Development Trust
AGRAAlliance for Green Revolution in Africa
ASA   Agriculture Seed Agency  
ASDP IIAgricultural Sector Development Programme II
ATMISAgriculture Trading Management Information System
AUAfrican Union
CCUChato Cooperative Union
COASCO  Cooperative Audit and Supervision

Cooperation  

COVID 19           Corona Virus Disease 

CPBCereals and other Produce Board
DASIPDistrict Agricultural Sector Investment Project
DFIDDepartment for International Development
EACEast African Community
EBARREcosystem Based Adaptation for     Rural Resilience
ERPPExpanded Rice Production Project
FAO   Food and Agriculture Organization 
IFADInternationl Fund for Agricultural Development
IMFInternational Monetary Fund
JICA  Japan  International  Cooperation Agency  
JIRCASJapan International Research Center for Agricultural Sciences
JKT  Jeshi la Kujenga Taifa  
JIRCASJapan International Research Center for Agricultural Sciences
KATCKilimanjaro Agricultural Training Centre
KATRINKilombero Agriculture Training and Research Institute
KCUKagera Cooperative Union
KDCUKaragwe District Cooperative Union
KACUKahama Agricultural Cooperative Union
MMCUMasasi Mtwara Coopetative Union
METLMohamed Enteprise Tanzania Limited
MoCUMoshi Cooperative University
MOGMufindi Outgrower Project
NAFCONational Agriculture and Food Cooperation
NBSNational Bureau of Statistics
NFRA   National Food Reserve Agency  
NHIFNational Healthy Insuarance Fund
NIDFNational Irrigation Development Fund
NMNAPNational Multisectoral Nutrition Action Plan
NMBNational Microfinance Bank
NOSCNjombe Outgrower Servince Campany
NPPACNational Plant Protection Advisory Committee
NSAAPNutrition Senstive Agriculture Action Plan
NSYIANational Strategy for Youth Involvements in Agriculture
PCIProject Concern International
REGROWResilient   Natural   Resource   Management   for   Tourism   and Growth Project
RITARegistration Insolvency and Trusteeship Agency
SACCOSSaving and Credit Cooperative Society
SADC  Southern    Africa            Development Comunity  
SAGCOT   Southern     Agricultural        Growth Corridor of Tanzania  
SATSustainable Agriculture Tanzania
SIDOSmall Industries Development Organization
SSIDPSmall Scale Irrigation Development Project
SUGECOSokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative
OCOther Charges
OSBPOne Stop Border Post
TADBTanzania Agriculture Development Bank
TPBTanzania Postal Bank
TAHATanzania Horticulture Association
TANIPACTanzania Intiative for Preventing Aflatoxin Contamination
TANECUTandahimba Newala Cooperative Union
TANSHEPTanzania Smallholder Holticulture Empowerment Project
TARITanzania Agriculture Research Institute
TBLTanzania Breweries Limited
TCDCTanzania Co-operative Develepment Commission
TICTanzania Investment Center
TEHAMATeknolojia ya Habari na Mawasiliano
TEMDOTanzania      Engineering     and    Manufacturing      Designing Organization
TFRATanzania Fertilizer Regulatory Authority
TGNPTanzania Gender Network Programme
ToTTraining of Trainers
TOSCITanzania Official Seed Certification Institute
TPHPATanzania Plant Health and Pesticides Authority
TRATanzania Revenue Authority
TSHTDATanzania Smallholder Tea Development Agency
UAEUnited Arab Emirates
UNDPUnited Nation Development Programme
UKIMWI  UVIKO-19Upungufu wa Kinga Mwilini Ugonjwa wa Virusi vya Korona
VVUVirusi Vya Ukimwi
WARCsWard Agricultural Resource Centers
WFPWorld Food Progamme

DIRA

Kuwa kitovu cha kutoa mwongozo wa Sera na huduma kuelekea kilimo cha kisasa chenye mtazamo wa kibiashara, chenye tija, ushindani na kinachozingatia mifumo bora ya kilimo na matumizi ya kilimo cha

umwagiliaji ifikapo mwaka 2025

DHIMA  

Kutoa huduma bora za kilimo, kuandaa mazingira bora kwa Wadau wa Kilimo, kuimarisha mfumo wa majadiliano ya Kisera, kuzijengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuiwezesha Sekta Binafsi kuchangia kikamilifu katika kilimo endelevu chenye tija, masoko ya uhakika na ongezeko la thamani ya mazao

1

Majukumu ya Wizara    

Majukumu ya Wizara yameainishwa katika Hati ya Idhini ya Mgawanyo wa Majukumu ya

Mawaziri (Ministerial Instrument) ya tarehe 7 Mei,

2021 ambayo ni pamoja na: –

  1. Kuandaa na kutekeleza Sera za Kilimo, Usalama wa Chakula, Umwagiliaji na

Ushirika;

  1. Kusimamia Matumizi Bora ya Ardhi ya

Kilimo; 

  1. Kufanya Utafiti, Mafunzo na Huduma za

Ugani katika Kilimo; iv.       Kusimamia Usalama wa Chakula;

v.                    Kusimamia Uhifadhi wa Kimkakati wa

Chakula; vi.       Kusimamia Maendeleo ya Ushirika na Vyama vya Ushirika;

  • Kuratibu Maendeleo ya Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo;
  • Kuendeleza Miundombinu ya Kilimo;
  • Kuratibu Masoko na kuongeza Thamani ya

Mazao ya Kilimo;

  • Kusimamia Maendeleo ya Zana za Kilimo na

Pembejeo; xi.     Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji; 

  • Kusimamia Maendeleo ya Rasilimali Watu Wizarani; 

2

  • Kusimamia leseni za stakabadhi za mazao ghalani; na
  • Kusimamia Idara zinazojitegemea, Taasisi za Serikali, Wakala, Programu na Miradi ya maendeleo iliyo chini ya Wizara.

3

1.       UTANGULIZI 

  1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lipokee Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha

2022/2023.

  • Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana hapa leo kwa ajili ya kujadili Taarifa ya Utekelezaji ya mwaka 2021/2022 na Mpango wa Bajeti kwa mwaka 2022/2023 ya Wizara ya Kilimo ambayo inagusa maisha ya watanzania.
  • Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naomba nimpongeze Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutimiza mwaka mmoja tangu ashike nafasi ya kuongoza nchi yetu. Katika kipindi hicho, sekta ya kilimo imeongezewa bajeti katika maeneo ya utafiti wa kilimo, huduma za ugani, umwagiliaji na uzalishaji wa mbegu; na kuimarisha masoko ya mazao ya kilimo. Aidha,

4

niungane na Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wenzangu kuendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aendelee kumpa afya njema ili awatumikie watanzania.

  • Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kutekeleza majukumu yake ikiwemo kuhimiza kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi na yeye mwenyewe kuwa mkulima.  
  • Mheshimiwa Spika, pianinampongeza Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa jitihada zake za kusimamia na kuendeleza mazao ya kimkakati na maendeleo ya ushirika nchini na yeye kuwa mkulima.
  • Mheshimiwa Spika, kipekee, nikupongeze wewe binafsi kwa kuchaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, niwapongeze Mheshimiwa Mussa Azan Zungu (Mb.), Naibu Spika pamoja na Wenyeviti wa Bunge Mheshimiwa Najma Murtaza Giga (Mb.) na Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile (Mb.) kwa kuendelea kukusaidia kikamilifu katika kutekeleza majukumu ya kuliongoza Bunge letu Tukufu. Nawapongeza pia Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
  • Mheshimiwa    Spika, ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniteua kuwa Waziri wa Kilimo. Ninaahidi kwa Mheshimiwa Rais, Chama Cha Mapinduzi, wananchi wa Nzega mjini na watanzania wote kwa ujumla kwamba nitatumikia nafasi ya ubunge na uwaziri kwa bidii, maarifa, weledi na uadilifu ili kuweza kufikia malengo yaliyoainishwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na matarajio ya watanzania.  
  • Mheshimiwa Spika, kwa furaha ninampongeza Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde, Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo. Nitashirikiana naye kikamilifu katika kuleta mageuzi kwenye sekta ya kilimo nchini na hivyo kuwaletea wananchi maendeleo na kuondoa umasikini na kuifanya sekta ya kilimo kuwa msingi mkuu wa ajira nchini. Pia, ninamkaribisha

Bw.      Gerald        Mweli,        Naibu         Katibu        Mkuu aliyehamishiwa Wizara ya Kilimo kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI.

  • Mheshimiwa Spika, ninapenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, chini ya uenyekiti wa Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, na Makamu Mwenyekiti wake, Mheshimiwa Almas Athumani Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kwa ushirikiano mzuri na ushauri makini ambao wameendelea kuutoa kwetu wakati wa kupitia Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2021/2022, na Mpango na Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2022/2023. Ushauri wao umezingatiwa na tunaahidi kuendelea kushirikiana kwa ukaribu na Kamati katika kuendeleza kilimo hapa nchini. 
  1. Mheshimiwa Spika, pia ninapenda kuishukuru Kamati ya Bajeti kwa maoni na ushauri walioutoa wakati wa majadiliano ya utekelezaji na Mpango wa Bajeti ya Wizara ya Kilimo. Ninapenda kutumia fursa hii kuihakikishia kamati kuwa maoni na ushauri wao umezingatiwa kwenye mpango na pia utazingatiwa katika utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2022/2023. 
  1. Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb.) pamoja na timu yake ya wataalam kwa kutupa nafasi ya kutusikiliza, kujadiliana na kushauriana kuhusu namna bora ya kutekeleza vipaumbele vya Sekta ya Kilimo na kuipa sekta kipaumbele katika Mpango wa Bajeti ya Serikali. 
  1. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwapongeza Mhe. Emmanuel Peter Cherehani kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Shinyanga, Mhe. Emmanuel Lekishon Shangai kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro na Mhe. Shamsi Vuai Nahodha kwa kuteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  1. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu limepata pigo la kuondokewa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ushetu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Elias Kwandikwa, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji Mhe. William Tate Ole Nasha na aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa Mhe. Irene Alex Ndyamkama. Ninatoa pole kwa wabunge, familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa kuondokewa na wapendwa wetu. Mungu azilaze roho za marehemu mahala pema peponi. Amina! 
  1. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya kipekee ninawashukuru viongozi na watumishi wote wa Wizara ya Kilimo kwa ushirikiano wao na bidii yao katika kazi. Ninamshukuru sana Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde (Mb), kwa ushirikiano mkubwa anaonipatia katika kutekeleza majukumu ya Wizara. Ninamshukuru Bw. Andrew Wilson Massawe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, na Profesa Siza Donald Tumbo, Naibu Katibu Mkuu pamoja na Wakurugenzi,

Wakuu wa Taasisi, Bodi na Wakala zilizo chini ya Wizara na watumishi wote wa Wizara kwa kazi nzuri na ushirikiano mkubwa wanaoendelea kuutoa.

1.1 Mchango wa Serikali katika Sekta ya Kilimo kwa Awamu zote Sita za Uongozi 

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Kwanza, ilitambua Tanzania kama nchi ya Wakulima na Wafanyakazi na kuwekeza katika kilimo hususan katika maeneo yafuatayo:- Vyuo vya Utafiti na Mafunzo, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Mashirika ya Umma yanayosimamia Kilimo, Bodi za Mazao na Vyama vya Ushirika. Pia ilihamasisha kilimo na lishe kupitia programu na kampeni mbalimbali ikiwemo Ukulima wa Kisasa, Kilimo cha kufa na kupona, Chakula ni Uhai, Mtu ni Afya, Elimu ya Kujitegemea na Siasa ni Kilimo. Aidha, katika kipindi hicho, msisitizo uliwekwa katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara na kufikia kiwango cha kuongoza kimataifa kwa baadhi ya mazao.  Mfano, Tanzania iliongoza katika uzalishaji wa zao la korosho katika Awamu hiyo  ikilinganishwa na nchi ya

Ivory Cost kama inavyoonekana katika Kielelezo Na. 1  

Kielelezo Na. 1: Ulinganisho wa Uzalishaji wa Korosho

700,000 600,000

500,000

400,000

  1. Pia, katika kipindi hicho Tanzania iliongoza katika uzalishaji wa zao la mkonge ikilinganishwa na nchi ya Kenya kama inavyoonekana katika Kielelezo Na. 2.

Kielelezo Na. 2: Ulinganisho wa Uzalishaji wa Mkonge

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Pili, ilifanya mageuzi ya uchumi yaliyokuwa kichocheo katika maendeleo ya kilimo ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Sera ya Kilimo ya mwaka 1983. Aidha, Serikali ilipunguza vikwazo katika biashara ili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa kwa ajili ya ustawi wa wananchi. 
  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Tatu, iliimarisha Taasisi na kusimamia utawala bora, ilibinafsisha Mashirika ya Umma na Mashamba ya Umma, iliboresha Bodi za Mazao kwa kuzifanya Bodi hizo kuachana na biashara na badala yake kuwa bodi za udhibiti na uendelezaji mazao. Pia kwa kipekee iliunda Wizara ya Masoko na Ushirika na kuimarisha ugatuaji wa madaraka kwa kuimarisha Serikali za Mitaa ambapo huduma za ugani za Kilimo na Mifugo zilihamishiwa TAMISEMI.
  1. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha maendeleo ya Sekta ya Kilimo, Serikali ya Awamu ya Nne ilianzisha na kutekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Kwanza (ASDP I), Programu ya Modenizesheni ya Ushirika, KILIMO KWANZA na SAGCOT. Pia, ilianzisha Benki ya Kilimo, Mpango wa Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo na taasisi mbalimbali ikiwemo Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Tume ya Maendeleo ya Ushirika. Taasisi hizo zilianzishwa ili kuendeleza ufanisi wa kutoa huduma kwa wakulima katika upatikanaji wa pembejeo, miundombinu ya kilimo na ushirika.  
  • Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Tano, ilianzisha na kutekeleza  Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II). Pia, iliboresha na kuwekeza kwenye miundombinu ya barabara, reli, bandari, nishati, viwanja vya ndege na ununuzi wa ndege kwa lengo la kuchochea uwekezaji katika sekta za uzalishaji. 
  • Pia, Serikali ilihamasisha ukuaji wa uchumi unaotegemea maendeleo ya viwanda vya kusindika na kuchakata mazao ya kilimo (Agroprocessing) ikiwemo viwanda vya sukari, mafuta ya kula, pamba na nafaka.  Aidha, ilianzisha Mpango wa Uboreshaji wa Mazingira ya Biashara (Blueprint) na kutumia sera za kikodi kulinda viwanda vya mazao ya kimkakati yakiwemo sukari na mafuta ya kula.
  • Mheshimiwa Spika, ukizingatia utekelezaji wa  awamu zote tano, Serikali  za awamu ya kwanza na Awamu ya Nne, ziliwekeza katika msingi mkuu wa uzalishaji. Serikali za Awamu ya Pili na ya Tatu zilifanya kazi kubwa ya kufungua biashara na kuweka mifumo ya kitaasisi. Serikali ya Awamu ya Tano ilifanya kazi kubwa ya kujenga miundombinu mbalimbali ambayo ni muhimu katika kuchochea uzalishaji, uongezaji wa thamani na usafirishaji.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali yaAwamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhihirisha kwa vitendo utashi wa kisiasa kwa kutambua kuwa maendeleo ya uchumi yatatokana na sekta za uzalishaji hususan Sekta ya Kilimo. Azma hiyo itafikiwa kwa kuwekeza katika maeneo ya kimkakati ya utafiti, uzalishaji wa mbegu bora, uimarishaji wa huduma za ugani, ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji na uhifadhi wa mazao na uimarishaji wa upatikanaji masoko ya mazao ya kilimo. 
  • Aidha,  Wizara inaendelea kutekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP – II) na kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kuwekeza na kufanya biashara katika Sekta ya Kilimo. 

1.2 Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita

katika Sekta ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka mmoja cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania, Serikali imeongeza bajeti ya utafiti wa kilimo kutoka Shilingi Bilioni 7.35 hadi Shilingi Bilioni 11.63, huduma za ugani kutoka Shilingi Milioni 603 hadi Shilingi Bilioni 11.5, umwagiliaji kutoka Shilingi Bilioni 17.7 hadi Shilingi Bilioni 51.48 na uzalishaji wa mbegu kutoka Shilingi Bilioni 5.42 hadi Shilingi Bilioni 10.58. 

  • Aidha, Serikali ya Awamu ya Sita imeongeza fedha za ununuzi wa nafaka kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (National Food Reserve Agency – NFRA) na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (Cerial and Other Produce Board – CPB) kutoka Shilingi Bilioni 19 mwaka 2020/2021 hadi Shilingi Bilioni 119 mwaka 2021/2022.  Hadi Aprili, 2022 fedha hizo zimewezesha ununuzi wa tani 183,045.384 za mahindi, mpunga na mtama. Hatua hiyo, itaiwezesha nchi kuwa na uhakika wa chakula na kuuza katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho, Serikali imewezesha ununuzi wa Pikipiki 7,000 kwa ajili ya maafisa ugani ili kurahisisha usafiri; vishikwambi (Tablets) 384 kwa maafisa Ugani 384; visanduku vya ufundi (Extension kits) 6,700  kwa maafisa ugani; na vifaa  vya kupima Afya ya Udongo (Soil Scanner) 143 kwa ajili ya kupima udongo kwa Halmashauri 143. Jumla ya Shilingi 9,295,000,000 zimetumika kununua vifaa hivyo.

Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimkabidhi mfano wa funguo ya pikipiki Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe katika hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa Maafisa Ugani zaidi ya 6,700 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 4 Aprili, 2022

  • Mheshimiwa Spika, eneo linalomwagiliwa limeongezeka kutoka hekta 695,045 mwaka 2020/2021 hadi hekta 727,280.6 mwaka 2021/2022 ambapo ni sawa na asilimia 60.6 ya lengo la hekta 1,200,000 ifikapo 2025 kama inavyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025. Aidha, katika kipindi hicho, Vyama vya

Umwagiliaji vilivyosajiliwa chini Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji Na. 4 ya Mwaka 2013 na Kanuni zake za mwaka 2015 vimeongezeka kutoka Vyama vya Umwagiliaji 180 mwaka 2020/2021 hadi Vyama 312 mwaka 2021/2022. 

  • Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imesimamia dhana ya kilimo ni biashara kwa kuimarisha mahusiano ya kimataifa ambayo yamefungua fursa ya masoko ya mazao ya kilimo ndani na nje ya nchi. Jitihada hizo zimewezesha kupatikana kwa fursa za masoko mapya ya mazao nje ya nchi ikiwemo soko la parachichi katika nchi za India na Afrika Kusini, ndizi nchini Kenya na  mchele nchini ubelgiji baada ya kukidhi viwango vya ubora. 
  • Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa masoko umeongeza mauzo ya mazao ya kilimo nje ya nchi ambapo mauzo ya mchele yameongezeka kutoka tani 184,521 zenye thamani ya Shilingi 176,490,000,000 mwaka 2020 hadi tani 441,908 mwaka 2021 zenye thamani ya Shilingi 476,800,000,000 mwaka 2021, mahindi kutoka tani 92,825 zenye thamani ya Shilingi 58,020,000,000 mwaka 2020 hadi tani 189,277 zenye thamani ya Shilingi 72,400,000,000 mwaka 2021, na parachichi kutoka tani 6,702 zenye thamani ya Shilingi 14,930,000,000 mwaka 2020 hadi tani 12,250 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 24,950,000,000 mwaka 2021. Kielelezo Na. 3.

Kielelezo Na. 3: Mauzo ya Parachichi

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho, Serikali imeongeza mtaji wa Benki ya Kilimo (TADB) kutoka Shilingi Bilioni 60 mwaka 2021 hadi Shilingi Bilioni 268 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 346.7. Ongezeko hilo limewezesha TADB kutoa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 116.63 kwenye miradi 197 ya maendeleo na kufanya jumla ya mikopo iliyotolewa tangu benki hiyo ianzishwe kufikia Shilingi Bilioni 482.4. Aidha, benki hiyo imewezesha wakulima 1,527,175 kupata dhamana ya mikopo ya kiasi cha Shilingi Bilioni 144.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali imewezesha benki za biashara kupunguza riba kwenye mikopo ya kilimo kutoka kati ya asilimia 17 na 20 hadi kufikia asilimia tisa (9). Hatua hiyo imewezesha wakulima kupata pembejeo kwa wakati, kufufua na kuanzisha viwanda vidogo vya kuongeza thamani. 
  • Vilevile, imefanikisha uuzaji wa soya nje ya nchi kufikia tani 53,594.35 mwaka 2020/2021 ikilinganishwa na tani 2,647 mwaka 2019/2020. Aidha, kampuni 80 za kitanzania zimesajiliwa kuuza soya nchini China. Pia, Serikali kupitia CPB imefungua vituo vya mauzo katika miji ya Juba (Sudan Kusini) na Lubumbashi (DR Congo) na kukodi ghala zenye uwezo wa kuhifadhi tani 5,000 na 2,000 mtawalia. 
  • Mheshimiwa Spika,  pia, Serikali imetoa ruzuku za pembejeo za kilimo kwa mazao ya korosho, tumbaku na pamba zenye thamani ya Shilingi 178,844,086,527.4.Kadhalika, katika kipindi hicho Serikali imewezesha uundaji wa Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika na ununuzi wa magari 15, pikipiki 137 na kompyuta 82 kwa ajili ya kuimarisha ukaguzi na usimamizi wa vyama vya ushirika nchini. Jumla ya Shilingi Bilioni 2.44 zimetumika kuunda mfumo na kununua vitendea kazi hivyo.
  • Mheshimiwa Spika,  mafanikio mengine na matokeo ya ziara ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika nchi mbalimbali ni kama ifuatavyo:
  • Nchini Ufaransa – Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania imesaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya Euro milioni 80 (sawa na Shilingi Bilioni 210) wenye lengo la kuimarisha benki hiyo ili kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu kwa sekta ya kilimo nchini.
  1. Uwekezaji mkubwa katika sekta ya Mbolea – kwa sasa Kiwanda cha Itracom Fertilizer Limited kutoka Burundi kinajenga kiwanda kikubwa cha mbolea katika Jiji la Dodoma chenye thamani ya Dola za Marekani Milioni 180 na kinatarajiwa kutoa ajira za kudumu kwa wafanyakazi takriban 3,000 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mbolea tani 600,000 kwa mwaka. 

Mbali na jitihada hizo, pia jitihada kubwa za kufungua masoko kwa ajili ya mazao ya kilimo ambapo hapo awali ilikuwa ni moja ya changamoto kubwa inayotukumba hivyo tunapenda kumshukuru Mheshimiwa Rais kutokana na juhudi zake za kuimarisha mahusiano na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na mataifa mengine jambo ambalo

limechochea; 

  1. Mauzo ya maharage kutoka Tanzania kwenda Jumuiya ya Afrika Mashariki yameongezeka na kufikia Dola za Marekani Milioni 193. 
    1. Uondoaji wa vikwazo 56 vya biashara kati ya 64 vilivyokuwepo kati ya nchi ya Tanzania na Kenya hii ikiwa ni mafanikio ya utekelezaji wa makubaliano kati ya Viongozi wa Nchi hizo mbili. Jitihada hizo zimepelekea ukuaji wa biashara kati ya Tanzania na Kenya kufikia Dola za Marekani Milioni 905. 
    1. Upatikanaji wa soko la China kwa ajili ya mazao (maharage ya soya na muhogo), jambo ambalo limetoa fursa ya soko la uhakika kwa wakulima wa mazao hayo nchini.

2. HALI YA UPATIKANAJI WA CHAKULA, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

2.1. Hali ya Upatikanaji wa Chakula 

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka mitano (2016-2021) uzalishaji wa mazao ya chakula nchini umeendelea kuwa wa kuridhisha na kuifanya nchi kujitosheleza kwa chakula kwa wastani wa asilimia 122.8 (Jedwali Na. 1). Uzalishaji mzuri wa mazao ulichangiwa na mtawanyiko mzuri wa mvua pamoja na kuongezeka kwa hamasa ya matumizi pembejeo bora kwa wakulima.  
  • Mfano, upatikanaji wa mbolea umeongezeka kutoka tani 435,178 hadi tani 465,080; uzalishaji wa mbegu bora umeongezeka kutoka tani

26,112.69 hadi tani 35,199.39. Vilevile, matumizi bora ya zana za kilimo yameimarika ambapo matumizi ya teknolojia za kisasa yamefika asilimia 52 ya shughuli zote za kilimo.

Jedwali Na. 1: Mwenendo wa uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini mwaka 2017-2022

Msimu wa UzalishajiUzalishaji wa Chakula (Tani)Mwaka wa chakulaMahitaji ya Chakula (Tani)Ziada (Tani)Utoshelevu (asilimia)
2016/201715,900,8642017/201813,300,0342,600,830120
2017/201816,891,9742018/201913,569,2853,322,686 124
2018/201916,293,6372019/202013,842,5362,565,773118
2019/202018,196,7332020/202114,404,1713,792,562126
2020/2021  18,665,2172021/202214,835,1013,830,116126
2021/2022** 

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

** Tathmini ya Awali ya uzalishaji itakamilika Juni, 2022   

  • Mheshimiwa Spika, mahitaji ya chakula kwa mwaka 2021/2022 yamefikia tani 14,835,101 ambapo tani 9,448,770 ni za mazao ya nafaka na tani 5,386,331 ni mazao yasiyo ya nafaka (Jedwali Na. 2). Mahitaji hayo yakilinganishwa na uzalishaji yanaonesha kuwa nchi imezalisha ziada ya tani 3,830,116 za chakula ambapo tani 1,425,655 ni za mazao ya nafaka na tani 2,404,461 ni mazao yasiyo ya nafaka. Kutokana na hali hiyo, Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa asilimia 126. 

Jedwali Na. 2: Uzalishaji wa Mazao ya Chakula kwa Msimu wa

2020/2021, Zao kwa   zao kwa Tani

NafakaMahindiMtama       & MaleziMcheleNganoNafaka
Uzalishaji6,908,3181,031,865.02,629,51970,28810,639,990
Mahitaji5,956,8142,087,357.81,091,778281,9389,417,888
Uhaba(- )/Ziada (+)    951,504-1,055,4931,537,741-211,6501,222,103
SinafakaMikundeNdiziMuhogoViaziYasiyo nafaka
Uzalishaji2,135,5221,392,9702,643,9151,612,8527,785,260
Mahitaji859,337990,6702,473,4371,055,4205,378,864
Uhaba(- )/Ziada (+)276,185402,300170,478557,4332,406,396

  Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha usalama wa chakula nchini kwa kununua na kuhifadhi nafaka. Katika msimu wa 2021/2022, NFRA imenunua jumla ya tani 110,713.249 za nafaka. Kiasi hicho cha nafaka kikijumuishwa na akiba ya tani 107,384.057 iliyokuwepo wakati wa kuanza msimu wa ununuzi (1 Julai, 2021) kinafanya NFRA kuwa na hifadhi ya tani 218,097.306. Aidha, NFRA imeuza tani 19,601.141 na hivyo, hadi Aprili, 2022 akiba iliyopo kwenye ghala za NFRA ni tani

198,496.165.

2.2. Umwagiliaji 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea kutekeleza Sera ya Taifa ya Umwagiliaji ya Mwaka 2010 na Mikakati yake pamoja na Mpango wa Umwagiliaji wa mwaka 2018. Hadi Aprili, 2022 eneo linalomwagiliwa ni hekta 727,280.6, sawa na asilimia 60.6 ya lengo la kufikia hekta 1,200,000 ifikapo 2025 na asilimia 2.5 ya eneo lote linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji.Aidha,eneo linalomwagiliwa lipo katika skimu 2,773. Kati ya skimu hizo, skimu 1,691 zenye ukubwa wa hekta 419,067 zinamwagiliwa kwa njia ya asili na skimu 1,082 zenye ukubwa wa hekta 308,213.6 zinamwagiliwa kwa kutumia miundombinu ya umwagiliaji iliyoboreshwa.  
  • Mheshimiwa Spika, maeneo yenye skimu zilizoendelezwa yameongeza uzalishaji na tija kwenye mazao. Kwa mfano tija kwenye zao la mpunga imeongezeka kutoka wastani wa tani 2 kwa hekta hadi kufikia wastani wa kati ya tani 4 na 5 kwa hekta; zao la mahindi tija imeongezeka kutoka tani 1.7 hadi kufikia tani 2 kwa hekta; zao la vitunguu tija imeongezeka kutoka tani 13 hadi kufikia tani 26 kwa hekta; na zao la nyanya tija imeongezeka kutoka tani 5 hadi kufikia 18 kwa hekta. Aidha, jumla ya wakulima 4,363,683 wananufaika na skimu za umwagiliaji zilizopo nchini.

Shamba la vitunguu linalomwagiliwa kwa miundombinu ya umwagiliaji ya asili katika kijiji cha Oloigeruno kitongoji cha Iltulele, mkoani Arusha  

2.3. Ushirika

  • Mheshimiwa Spika, Tume ya Maendeleo ya Ushirika (Tanzania Co-operative Development Commission – TCDC), imeendelea kutekeleza jukumu lake la msingi la kudhibiti na kuhamasisha maendeleo ya ushirika, ambapo hadi Aprili, 2022 idadi ya Vyama vya Ushirika vyenye usajili vimefikia 9,741 ikilinganishwa na vyama 9,185 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Kati ya hivyo 4,538 ni Vyama vya Ushirika wa Kilimo na Masoko (AMCOS), 3,946 ni Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) na 1,257 ni Vyama vinavyojishughulisha na kazi mbalimbali zikiwemo ufugaji nyuki, ufugaji na uvuvi. Pia idadi ya wanachama wa Vyama vya Ushirika imeongezeka kutoka wanachama 6,050,324 mwaka 2021 hadi 6,965,272 mwaka 2022. Ongezeko hilo limetokana na uhamasishaji kuhusu umuhimu wa kujiunga na ushirika.
  • Mheshimiwa Spika, Tume imeendelea kutoa leseni za uendeshaji wa Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo ambapo SACCOS 222 zimepatiwa leseni na hivyo kufanya idadi ya SACCOS zenye leseni kufikia 655. Kati ya hizo, SACCOS daraja A ni 523 na SACCOS daraja B ni 132. 
  • Mheshimiwa Spika, Vyama vya Ushirika vimekuwa chachu ya wananchi kupata huduma za kijamii ambapo kwa sasa vimeanza kutoa huduma ya bima ya afya kwa wanachama wake kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (National Health Insurance Fund-NHIF) na mabenki. Mkakati umewekwa kati ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika na NHIF kuhakikisha wanachama wa Vyama vya Ushirika wanapata huduma ya afya ya uhakika na kwa wakati. Hadi Aprili, 2022 wanachama zaidi ya 1,000,000 wamejiunga kwenye mpango huo.
  • Mheshimiwa     Spika,       katika        mwaka

2020/2021, Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limekagua vyama 6,013 kati ya lengo la kukagua vyama 6,350. Kati ya vyama vilivyokaguliwa, vyama 357 vimepata hati inayoridhisha, vyama 2,674 vimepata hati yenye shaka, vyama 1,253 vimepata hati isiyoridhisha na vyama 1,729 vimepata hati mbaya. Ukaguzi huo umebaini kuwepo kwa ubadhilifu wa mali na udhaifu katika mifumo ya udhibiti wa ndani pamoja na vyama vingi kushindwa kuandika vitabu vya hesabu, hivyo miamala ya vyama vya ushirika kutokuwa na uthibitisho wa usahihi wake.

  • Hatua zilizochukuliwa baada ya ukaguzi huo ni pamoja na kuwaondoa, kuwatengua viongozi wa Bodi za vyama na watendaji waliobainika kuhusika na ubadhilifu wa mali za vyama vya ushirika. Aidha, viongozi tisa (9) na watendaji watatu (3) wamefikishwa kwenye vyombo vya dola kwa hatua zaidi.

3. UTEKELEZAJI WA MALENGO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2021/2022

  • Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka 2021/2022, umezingatia Mwongozo wa Mpango na Bajeti ya mwaka 2021/2022; Dira ya Maendeleo ya Taifa (2025); Mpango wa Maendeleo wa Taifa Awamu ya Tatu

(2020/2021- 2025/2026) na Ilani ya Uchaguzi ya 

Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 hadi

2025. 

  • Mheshimiwa Spika, pia, utekelezaji umezingatia Malengo Endelevu ya Maendeleo 2030 (SDGs); Sera ya Taifa ya Kilimo ya Mwaka 2013; Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) na Hotuba ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoitoa tarehe 22 Aprili, 2021 alipolihutubia Bunge lako Tukufu. Pia, imezingatia masuala mtambuka ya jinsia, mazingira, lishe,  UKIMWI na vijana. 

4. MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

2021/2022

                  4.1.1.     Makusanyo ya Maduhuli 

  • Mheshimiwa     Spika,      katika        mwaka

2021/2022, Wizara ilikadiria kukusanya mapato ya Shilingi 34,495,000,000 kupitia Fungu 43 na Fungu 05 kutokana na vyanzo vyake vya makusanyo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 4,480,000,000 zinakusanywa kupitia Fungu 43 na Shilingi 30,015,000,000 zinakusanywa kupitia Fungu 05.

  • Hadi Aprili, 2022, Wizara imekusanya Shilingi 4,885,172,460 sawa na asilimia 14.16 ya makadirio. Kati ya Fedha hizo Shilingi 4,224,031,585.09 zimekusanywa na Fungu 43 na Shilingi 661,140,875 zimekusanywa na Fungu

05. 

4.1.2. Fedha Zilizoidhinishwa kwa Mafungu Yote (43, 24 na 05)

                  4.1.3.       Makusanyo ya Maduhuli 

  • Mheshimiwa     Spika,      katika        mwaka

2021/2022, Wizara ilikadiria kukusanya mapato ya Shilingi 34,495,000,000 kupitia Fungu 43 na Fungu 05 kutokana na vyanzo vyake vya makusanyo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 4,480,000,000 zinakusanywa kupitia Fungu 43 na Shilingi 30,015,000,000 zinakusanywa kupitia Fungu 05.

  • Hadi Aprili, 2022, Wizara imekusanya Shilingi 4,885,172,460.09 sawa na asilimia 14.16 ya makadirio. Kati ya Fedha hizo Shilingi 4,224,031,585.09 zimekusanywa na Fungu 43 na Shilingi 661,140,875 zimekusanywa na Fungu 05.

Jedwali Na.3: Mchanganuo wa Makusanyo ya Maduhuli (TSH)

FunguMakadirioMakusanyoAsilimia
Fungu 434,480,000,0004,224,031,585.0994.28
Fungu 0530,015,000,000661,140,8752.2
Jumla34,495,000,0004,885,172,460.0914.16

4.1.4. Fedha Zilizoidhinishwa kwa Mafungu Yote (43, 24 na 05)

                  53.   Mheshimiwa     Spika,     katika     mwaka

2021/2022, Wizara ya Kilimo ilitengewa jumla ya Shilingi 294,162,071,000 (Jedwali Na. 3) kupitia

Fungu 43, Fungu 05 na Fungu 24 kama ifuatavyo: –  

Fungu 43

54. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo kupitia Fungu 43 ilitengewa Shilingi

228,871,243,000. Kati ya fedha hizo, Shilingi 164,748,000,000 ni kwa ajili ya bajeti ya maendeleo ambapo Shilingi 82,180,000,000 ni fedha za ndani na Shilingi 82,568,000,000 ni fedha za nje. Aidha, Shilingi 64,123,243,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Kati ya Fedha hizo, Shilingi 14,428,975,000 ni mishahara ya watumishi wa Wizara na Shilingi 28,063,482,000 ni mishahara ya watumishi wa Bodi na Taasisi. Aidha, Shilingi 11,676,789,490 ni matumizi mengineyo (Other Chargers – OC) kwa Wizara na Shilingi 9,953,996,510 ni matumizi mengineyo (OC) kwa ajili ya Bodi na Taasisi. 

                  4.1.5.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida

55. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, Shilingi 54,083,072,288 sawa na asilimia  84.34 ya fedha zilizoidhinishwa za matumizi ya kawaida zimetolewa. Kati ya fedha hizo, Shilingi 17,455,234,748 ni za matumizi mengineyo ya Wizara, Taasisi na Bodi  na Shilingi 36,627,837,540 ni mishahara ya Wizara, Taasisi na Bodi. 

                  4.1.6.     Matumizi ya Bajeti ya Maendeleo

56. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 Shilingi 77,266,472,804.94 ya fedha zilizoidhinishwa zimetolewa na kutumika sawa na asilimia 46.89. Kati ya fedha hizo, Shilingi 59,354,119,664.10 ni fedha za ndani na Shilingi  17,912,353,141 ni fedha za nje.

Fungu 05

57. Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi 51,487,450,000 zilitengwa kupitia Fungu 05. Kati ya fedha hizo, Shilingi 46,500,000,000 ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambapo Shilingi 35,000,000,000 ni fedha za ndani na Shilingi 11,500,000,000 ni fedha za nje. Aidha, kati ya fedha hizo Shilingi 4,987,450,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida ambapo Shilingi 3,349,266,000 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Tume na Shilingi 1,638,184,000 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo.

                  4.1.7.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida

58. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, Shilingi 4,345,471,657.30 sawa na asilimia 87.13 ya fedha zilizoidhinishwa za matumizi ya kawaida zimetolewa. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,734,751,657.30 ni za matumizi mengineyo zikijumuisha Shilingi 582,136,857 za madeni ya watumishi na Shilingi 2,610,720,000 ni mishahara ya watumishi.

                  4.1.8.     Matumizi ya Bajeti ya Maendeleo

59. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 Shilingi 5,935,965,769.22 sawa na asilimia 12.77 ya fedha za ndani zilizoidhinishwa zimetolewa na kutumika. Kati ya fedha hizo, Shilingi 555,486,510.95 zimetumika kugharamia ujenzi wa skimu ya Kirya (hekta 800) iliyopo Wilaya ya Mwanga na Endagaw (hekta 246) iliyopo

Wilaya ya Hanang’. Aidha, Shilingi 1,487,570,916.95 zimetumika kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu za Luiche, Ibanda, Ilemba, Makwale, Tlawi na Mkombozi. Vilevile, Tume imepokea jumla ya Shilingi 3,892,908,341.32 ambazo zimetumika kulipa madeni ya wakandarasi.

Fungu 24

60. Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi 12,803,378,000 zilitengwa kupitia Fungu 24. Kati ya fedha hizo, Shilingi 5,549,009,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Shilingi 4,654,984,000 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Tume.

Aidha, Shilingi 1,000,000,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya COASCO   na Shilingi 1,599,385,000 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa COASCO.

                  4.1.9.     Matumizi ya Bajeti ya Kawaida

61. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili 2022, Shilingi 10,232,485,264.98 sawa na asilimia 79.92 ya fedha zilizoidhinishwa za matumizi ya kawaida zimetolewa. Kati ya fedha hizo, Shilingi 5,157,164,402.38 ni za matumizi mengineyo, na Shilingi 5,075,320,862.6 ni mishahara. 

Jedwali Na. 4: Mchanganuo wa Matumizi ya Fedha zilizotolewa kwa mwaka 2021/2022

NaBajeti IliyoidhinishwaFedha zilizoidhinishwaFedha zilizotolewaAsilimia
Fungu43    
1.Fedha Matumizi Kawaidaza ya64,123,243,00054,083,072,28884.334
Fedha maendeleoza164,748,000,00077,266,472,804.9446.89
Jumlandogo Fungu 43228,871,243,000131,349,545,092.9457.39
Fungu05    
2Fedha Matumizi Kawaidaza ya4,987,450,0004,345,471,657.3087.13
Fedha maendeleoza46,500,000,0005,935,965,769.2212.77
Jumlandogo Fungu 0551,487,450,00010,281,437,426.5219.96
Fungu24   
3.Fedha                    za Matumizi              ya kawaida12,803,378,00010,232,485,264.9879.92
Jumla ndogo Fungu 2412,803,378,00010,232,485,264.9879.92
Jumla Kuu294,162,071,000272,931,575,450.8692.78

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

4.2. UTEKELEZAJI WA MAENEO YA KIPAUMBELE

KWA MWAKA 2021/2022

62. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara imetekeleza vipaumbele vifuatavyo: (i) Utafiti wa kilimo; (ii) Upatikanaji wa pembejeo; (iii) Kuimarisha kilimo cha Umwagiliaji; (iv) Huduma na mafunzo ya ugani; (v) Upatikanaji wa Masoko; (vi) Kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa mitaji; na (vii) Kuimarisha Kilimo Anga. 

                  4.2.1.     Utafiti wa Kilimo

4.2.1.1. Utafiti wa Mbegu Bora na teknolojia za kilimo

  • Mheshimiwa Spika, mwaka 2021/2022, Kamati ya Taifa ya Mbegu imeidhinisha aina 18 za mbegu kwa ajili ya matumizi zitakazochangia katika upatikanaji wa mbegu bora msimu wa 2022/2023 (Kiambatisho Na. 1). Kati ya mbegu hizo, aina tano (5) zimegunduliwa na TARI na aina 13 zimegunduliwa na kampuni binafsi za mbegu. Mbegu hizo ni za mahindi (5), choroko (2), ngano (2), tumbaku (2), mpunga (1) na viazi mviringo (6). Mbegu zilizogunduliwa zitatumika kuzalisha madaraja ya mbegu za awali na msingi ili kuwapa ASA na kampuni binafsi kuzalisha mbegu zilizothibitishwa ambazo zitatumiwa na wakulima. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kuongeza matumizi ya mbegu bora, TARI imeendelea kutumia vituo vya usambazaji wa teknolojia (AgriTech Hubs) ikiwemo viwanja nane (8) vya maonesho ya kilimo na mashamba ya mfano. Hadi Aprili, 2022 mashamba ya mfano 802 yameandaliwa kwa ajili ya kufundisha wakulima. Aidha, wakulima na wadau 12,691 wamepata mafunzo ambapo tani 0.96 za mbegu za mazao ya mahindi, mpunga na mtama na miche 112,599 imesambazwa kwa wakulima kupitia vituo hivyo. 
  • Vilevile, TARI imezalisha mbegu mama tani 19.998,  mbegu za awali tani 197.77 na  mbegu za msingi tani 134.60 ambazo zinaweza kuzalisha wastani wa tani 26,000 za mbegu zilizothibitishwa za alizeti, maharage, mahindi, ngano, mtama, korosho, mpunga, ufuta, karanga, pamba na shayiri. 
  • Mheshimiwa Spika, TARI imesaini mkataba na Taasisi ya Kuendeleza Mifumo ya Masoko (Agricultural Market Development TrustAMDT) wa kuongeza uzalishaji wa mbegu bora za alizeti. Mkataba huo unahusisha kampuni ya mbegu ya BioSustain iliyopo Singida, AMINATA Quality & Consultancy ya Tanga na Highland Seed Growers ya Mbeya. Kupitia mkataba huo, tani 300 za mbegu za alizeti zitazalishwa. 
  • Mheshimiwa Spika, TARI imetafiti na kugundua nafasi mpya ya kupanda pamba ambayo ni sentimita 60 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 30 kutoka mche hadi mche badala ya nafasi ya awali ambayo ilikuwa ni sentimita 90 kwa sentimita 40. Nafasi mpya imeongeza idadi ya mimea kwa hekta kutoka miche 27,777 hadi 55,555 na hivyo kuongeza mavuno kutoka wastani wa kilo 710 hadi kilo 1,422 kwa hekta moja sawa na kutoka kilo 284 hadi 569 kwa ekari moja. 
  • Mheshimiwa Spika, TARI imegundua zana (fabricate) rahisi za kupandia pamba zenye uwezo wa kupanda mistari miwili kwa mara moja. Tafiti zinaonesha kuwa muda unaotumika kupanda mbegu za pamba kwa kutumia zana hizo ni saa moja (1) hadi masaa mawili (2) kwa kukokotwa na wanyama kazi na masaa mawili (2) hadi matatu (3) kwa kuvutwa na nguvukazi watu kutegemea hali ya shamba na udongo wake. Wakati huo upandaji kwa kutumia nguvukazi watu kudondosha mbegu kwa mkono hutumia zaidi ya masaa 11. 
  • Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii, kuwapongeza Dauson Malela, Robert Cheleo Alphonce na Dkt. Paul Saidia ambao ni watafiti wa TARI-Ukiriguru kwa ubunifu wao wa kugundua na kutengeneza mashine hiyo rahisi ya kupandia.

4.2.1.2. Vituo vya Utafiti 

  • Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha vituo vya utafiti, Wizara kupitia TARI imeendelea kujenga Ofisi ya kituo cha uzalishaji wa miche ya michikichi, TARI Kihinga, mkoani Kigoma ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 20. Aidha, Wizara imejenga na kusimika miundombinu ya umwagiliaji katika vituo vya utafiti vya TARI Uyole, Bwanga na Makutopora ambayo itaongeza uzalishaji wa mbegu za ngano, pamba, alizeti, mahindi na miche ya zabibu. 
  • Vilevile, Wizara imeendelea kuimarisha maabara za TARI Mlingano na TARI Mikocheni kwa kununua vifaa, madawa na vitendanishi vya maabara. Kadhalika, TARI imefadhili watafiti 43 wa masomo ya muda mrefu katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi. Kati ya hao, 19 ni shahada ya uzamivu, 19 shahada ya uzamili na watano (5) shahada.

4.2.2. Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo

4.2.2.1.  Mbegu Bora

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kusimamia uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora ambapo hadi Aprili 2022, tani 49,962.35   za mbegu bora zimepatikana sawa na asilimia 26.68 za mahitaji ya tani 187,197 kwa mwaka. Kati ya mbegu hizo, tani 35,199.39 zimezalishwa ndani ya nchi, tani 11,340.2 zimeingizwa kutoka nje ya nchi na Sekta Binafsi na tani 3,422.80 ni bakaa ya msimu uliopita kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 5. Kati ya mbegu bora zilizozalishwa ndani ya nchi, tani 3,033.85 zimezalishwa na ASA, tani 18,480 ni mbegu za pamba zilizozalishwa na ASA kwa kushirikiana na Bodi ya Pamba, tani 652.133 zimezalishwa na TARI na tani 13,033.41 Sekta Binafsi.
  • Mheshimiwa Spika, TARI kupitia vituo vyake vya Selian, Uyole na Kifyulilo imezalisha tani 214.8 za mbegu za ngano. Kati ya hizo, tani

0.3 ni mbegu mama, tani 24.7 mbegu za awali na tani 158.7 ni mbegu zilizothibitishwa. Kati ya mbegu zilizothibitishwa, tani 113.9 zimesambazwa kwa wakulima ambapo tani 2.3 za mbegu zilizosambazwa zimepelekwa katika skimu ya umwagiliaji Bahi ili kuongeza uzalishaji wa ngano nchini. Pia, TARI imezalisha tani 37 za mbegu za ufuta na kusambaza tani 25 kwa wakulima, na tani 18 za mbegu za karanga na kusambaza tani 15.5 kwa wakulima. 

  • Mheshimiwa Spika, kituo cha TARI Mlingano kimeendelea kuzalisha miche bora ya viungo (pilipili manga, karafuu, mdalasini na kokoa) ambapo hadi Aprili, 2022 miche 1,600 imezalishwa na miche 1,003 imesambazwa kwa wakulima wa Tanga, Morogoro, Arusha na Mtwara. Aidha, Kituo kimezalisha miche 10,000 ya matunda (machungwa, machenza, ndimu, malimau, topetope, komamanga na embe) na kusambaza miche 932 kwa wakulima katika mikoa ya Tanga, Morogoro, Dar es salaam, Lindi na Mtwara.
  • Vilevile, Bodi ya Pamba imesambaza tani 15,548 za mbegu za pamba kwa wakulima zinazotosha kupandwa kwenye shamba lenye ukubwa wa hekta 621,920.

Jedwali Na. 5: Upatikanaji wa Mbegu Bora Hadi Aprili, 2022.

Aina ya zaoUzalishaji wa ndani (Tani)Bakaa (Tani)Uagizaji toka nje (Tani)Jumla (Tani)
Mahindi 13,498.3 3,145.30 10,548.6  27,192.2 
Mpunga 576.1 0 1.0  577.1 
Mtama 106.9 3.11.3 111.3 
Alizeti 1,973.5 80.3 138.3  2,192.1 
Maharage 305.1 34 24.0  363.1 
Soya 15.6 9.7117.4 142.7 
Ufuta 43.8 00 43.8 
Kunde0.5000.5
Choroko 5.2 0.60 5.8 
Mbogamboga 25.3 122.8 293.0  441.1 
Karanga 10.2 00 10.2 
Pamba18,4800018480
Ngano 158.7 27164 349.7 
Tumbaku0.250 0.1 0.31
Nyasi001.51.5
*Pingili za muhogo28,507,814 0 028,507,814 
Viazi mviringo005151
Jumla35,199.393,422.80 11,340.2 49,962.39

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022 *Hazikujumuishwa kwenye jumla

  • ASA imesafisha na kusambaza kwa wakulima tani 2,000 za mbegu za alizeti (standard seed) zenye thamani ya Shilingi Bilioni 5.84 kwa utaratibu wa ruzuku. Mbegu hizo zimesambazwa katika mikoa ya Dodoma, Singida, Simiyu na Manyara kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula na zinatarajiwa kuzalisha tani 400,000 za alizeti zitakazozalisha mafuta ya kula wastani wa tani 100,000.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mradi wa Kukabiliana na Athari za UVIKO-19 imenunua tani 12.8 za mbegu za alizeti aina ya Hysun-33 na Supersun ambazo zimesambazwa kwa wakulima 4,362 kupitia Vyama vya Ushirika katika Mikoa ya Dodoma (Kongwa tani 2.4 na Kondoa tani 2.6), Singida (Singida DC tani 3.8 na Iramba tani 2.7) na Simiyu (Itilima tani 1.3). Aidha, hadi Aprili, 2022. ASA imezalisha mbegu-miche ya michikichi (pre-geminated seeds) 121,292 kupitia mashamba ya Mwele Tanga (60,300), Mbozi (52,000) na Bugaga (8,992).

Miche bora ya michikichi katika Kituo cha TARI Kihinga mkoani Kigoma

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, ASA imeongeza eneo la kuzalisha mbegu kwa kufungua mashamba mapya yenye ukubwa wa hekta 1,639.6.   Mashamba hayo ni Msimba – Kilosa (hekta 815), Mwele – Mkinga (hekta 305), Bugaga- Kasulu (hekta 30.8), Kilimi – Nzega (hekta 300), Namtumbo (hekta 88.8) na Msungura -Chalinze (hekta 100). Kati ya eneo hilo, hekta 1,158.6 zitatumika kwa uzalishaji wa mbegu za alizeti. 
  • Vilevile, ASA imeingia mkataba na Shamba la Msipazi na Kituo cha Kilimo Laela kuzalisha mbegu bora za alizeti. Jumla ya ekari 450 zimelimwa ambapo ekari 50 ni kwa kituo cha Laela na matarajio ni kuzalisha tani 14 za mbegu za alizeti na ekari 400 za shamba la Msipazi zinatarajia kuzalisha tani 112 za mbegu za alizeti. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kuongeza upatikanaji wa miche bora ya chai, Wakala wa Wakulima Wadogo wa Chai Tanzania (Tanzania Smallholders Tea Development Agency – TSHTDA) imezalisha miche 843,066 sawa na asilimia 108.8 ya lengo la kuzalisha miche 750,000 na uzalishaji unaendelea. Kati ya miche hiyo Wilaya ya Rungwe imezalisha miche 232,000, Njombe 152,047 na Mufindi 459,019. 
  • Vilevile, miche 6,000,000 imepandwa kwenye vitalu kupitia mradi wa Njombe Outgrower Servince Campany – NOSC. Aidha, miche bora 7,100,000 iliyokuwa inatunzwa kwenye vitalu vilivyopo katika Wilaya ya Njombe kupitia NOSC (5,100,000) na Mufindi Outgrower Project – MOG (2,000,000) imetumika kwa ajili ya kujaza mapengo katika eneo la hekta 60 pamoja na kupandwa upya kwenye eneo la hekta 200 katika tarafa ya Igominyi – Njombe. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TARI, ASA, Bodi za Mkonge, Korosho, Pareto, Kahawa na Vikundi vya wakulima imezalisha jumla ya miche bora 32,301,995 na mbegu tani  95,764.  Aidha, miche 24,447,952  na mbegu tani 95,764. zimesambazwa kwa wakulima kama inavyooneka kwenye Jedwali Na. 6. Miche ya mkonge imesambazwa kwa wakulima katika mikoa ya  Singida, Tanga, Manyara na Simiyu; na miche ya kahawa imesambazwa kwa wakulima katika mikoa ya Kagera, Ruvuma, Kilimanjaro, Songwe, Mbeya, Kigoma, Njombe, Tanga na Mara. 

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde akigawa  miche bora ya kahawa zaidi ya milioni mbili (2,000,000) 

aina ya robusta kwa Wakulima wa Kyerwa wa mkoa  wa Kagera

  • Pia, mbegu za korosho zimesambaza na Bodi ya Korosho katika Halmashauri 86 ambazo zitazalisha miche 12,706,960. Aidha, pingili za muhogo 28,507,814 zimezalishwa kupitia ASA, TARI na vikundi vya wakulima.

Jedwali Na. 6: Uzalishaji wa Mbegu na Miche kupitia Bodi za

Mazao mwaka 2021/2022

Na.Aina ya ZaoMbegu zilizoza lishwaMbegu zilizosa mbazwaMiche iliyozalishwaMiche iliyosambazwa
1Mkonge  5,046,0004,241,630
2Kahawa  7,956,3717,956,371
3Chai  13,916,0667,100,000
4Korosho90,76490,76491,51291,512
5Pareto5,0005,00000
6Mboga  1,953,0251,953,025
7Minazi  1,250,0001,250,000
8Michikichi  929,984774,737
9Viazi vitamu  1,000,4481,000,448
10Zabibu  113,63735,277
11Parachichi  44,95244,952
Jumla95,76495,76432,301,99524,447,952

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania

(Tanzania Official Seed Certification Institute – TOSCI) imeendelea kuthibiti ubora wa mbegu nchini kwa kukagua mashamba ya mbegu na kupima ubora wake kwenye maabara. Hadi Aprili, 2022 TOSCI imekagua hekta 1,654.2 za mashamba ya mbegu na kubaini yote yamekidhi vigezo vya ubora; imekusanya sampuli 1,795 na kupima ubora wake ambapo sampuli 1,591 zimekidhi vigezo vya ubora, sampuli 143 hazikukidhi vigezo vya ubora na sampuli 61 zinaendelea kufanyiwa vipimo. 

  • Mheshimiwa Spika, TOSCI imekagua maduka ya mbegu 303 na kufanya majaribio ya utambuzi wa aina 65 za mazao ya kilimo. Aidha, TOSCI imetoa mafunzo kuhusu Sheria ya Mbegu Na. 18 ya mwaka 2003 na Kanuni zake kwa wafanyabiashara 399 na mafunzo ya uzalishaji wa mbegu bora kwa wakulima 82 katika mikoa ya Morogoro, Mwanza, Tabora, Geita, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Songwe, Rukwa, Katavi, Arusha na Mtwara.

Mtaalam kutoka Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania

(TOSCI) akiendesha majaribio ya kupima ubora wa mbegu kwenye maabara ya Taasisi hiyo mkoani Morogoro

4.2.2.2. Mbolea

  • Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 tani 436,452 za mbolea zimepatikana sawa na asilimia 63 ya mahitaji ya tani 698,260 ya msimu wa 2021/2022. Kati ya hizo, tani 274,973 zimeingizwa kutoka nje ya nchi, tani 43,579 zimezalishwa nchini na tani 117,900 ni bakaa ya msimu wa 2020/2021 kama inavyoonekana kwenye Jedwali. Na. 7.

Jedwali na. 7: Upatikanaji wa Mbolea Hadi Aprili, 2022

Aina ya MboleaBakaa ya Msimu 2020/202 1Kiasi kilichoi ngizwaUzalish aji wa ndaniJumla ya Upatikan ajiMahitaji ya 2021/202 2
UREA26,06660,23886,304210,769
DAP14,32225,93240,254166,310
NPKs30,90945,8051,339 78,053147,503
Other N.13,1265,4005,499 24,0258,915
SA8,92034,72743,64732,978
CAN55950,94751,506101,618
NPSZn4,68604,68611,571
MoP4,83512,90017,7351,939
NPS1,9458,0409,985
Minjingu6,084025,732 31,8168,361
Mbolea Nyingine4,51330,984 5,008 40,5058,298
Lime1,85204,426 6,278
Dolomite4901,075 1,124
Gypsum340500 534
Jumla117,900274,973 43,579 436,452698,262

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  • Mheshimiwa Spika, mauzo ya mbolea ndani ya nchi yalikuwa tani 173,957 na nje ya nchi yalikuwa tani 43,175 na tani 192,100 zinaendelea kuuzwa. Aidha, aina 28 za mbolea mpya na visaidizi vyake vimesajiliwa ikilinganishwa na aina 17 za mbolea mpya zilizosajiliwa mwaka 2020/2021. 
  • Mheshimiwa Spika, Bodi ya Tumbaku kwa kushirikiana na Vyama vya Ushirika imesambaza mbolea tani 20,689.9 za NPK na tani 5,066.7 za CAN kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji na tija. Pia, Bodi ya Chai na TSHTDA wameendelea kuhamasisha matumizi ya mbolea katika uzalishaji wa zao la chai kupitia vyama vya ushirika ambapo wakulima 11,869 wa vyama vya ushirika vya Igominyi (Njombe), (Iringa) na RUBTCOJE (Rungwe) wamehamasika na kununua tani 1,400 za mbolea aina ya NPK, TSP na UREA.
  • Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti ubora wa mbolea nchini,Wizara kupitiaMamlaka ya

Udhibiti wa Mbolea Tanzania (Tanzania Fertilizer Regulatory Authority – TFRA) imesajili wafanyabiashara 1,813 wa mbolea na kukagua wafanyabiashara 2,371 wa mbolea. Ukaguzi huo ulibaini uwepo wa aina tisa (9) za mbolea zisizosajiliwa; uuzaji wa mbolea zilizofunguliwa; uwepo wa mbolea zenye uzani mdogo ukilinganisha na kipimo; na baadhi ya wafanyabiashara wa mbolea kufanya biashara bila vibali. Vilevile, wafanyabiashara wa mbolea 2,988 na wakaguzi 29 wamepatiwa mafunzo ya uhifadhi bora wa mbolea na mafunzo ya ukaguzi mtawalia. Pia, ujenzi wa maabara ya kupima ubora wa mbolea umefikia asilimia 38.

4.2.2.3. Viuatilifu 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha upatikanaji wa viuatilifu vya kudhibiti visumbufu vya mazao na mimea ambapo hadi Aprili, 2022, upatikanaji umefikia lita 106,000 vyenye thamani ya Shilingi 3,115,900,000. Kati ya hizo, lita 100,000 ni kwa ajili ya kudhibiti viwavijeshi, lita 5,000 kwelea kwelea na lita 1,000 kwa ajili ya nzi wa matunda. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kudhibiti visumbufu vya mazao na mimea ikiwemo nzige, panya, kwelea kwelea, viwavijeshi na nzi wa matunda kwa kufanya savei, kununua na kusambaza viuatilifu kwenye maeneo yenye milipuko pamoja na kutoa elimu kwa wakulima na maafisa ugani. 
  • Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 lita 225 za Methyl Eugeno zimesambazwa katika wilaya za Handeni (60), Muheza (50), Morogoro Mjini (45), Morogoro Vijijini (10), Bagamoyo (5), Pangani (25), na Ubungo (30) kwa ajili ya kudhibiti nzi wa matunda. Vilevile, lita 34,031 za Profenofos zimesambazwa katika Halmashauri 41 za mikoa ya Lindi, Pwani, Morogoro, Tanga, Geita, Manyara, Kilimanjaro, Dodoma, Singida, Dar es salaam, Katavi na Arusha kwa ajili ya kudhibiti viwavijeshi. Aidha, lita 561 za Duduba zimesambazwa katika Halmashauri ya Wilaya ya

Kilosa.  

  • Mheshimiwa Spika, Bodi ya Pamba iliagiza chupa (acrepacks) 12,000,000 zenye thamani Shilingi bilioni 40.34 na kusambaza kwa wakulima kwa mfumo wa ruzuku ambapo chupa 9,500,000 zimetumika katika msimu wa 2021/2022 na chupa 2,500,000 zitatumika msimu wa 2022/2023. Aidha, Bodi ya Tumbaku imeratibu upatikanaji wa mbolea na viuatilifu vyenye thamani ya Dola za Marekani milioni 32.8 na kusambaza kwa wakulima. Vilevile, Bodi ya Korosho imeratibu ununuzi wa viuatilifu vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 59.3. Ununuzi huo umefanyika kwa kutumia utaratibu wa mazao husika kujigharamia yenyewe kupitia Mifuko ya Wadau. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imedhibiti milipuko ya panya katika mikoa ya Rukwa

(Nkasi), Lindi (Kilwa), Nachingwea (Mtama, Liwale, Ruangwa na Lindi MC) na Mtwara (Nanyumbu, Tandahimba, Masasi na Newala) ambapo jumla ya kilo 812 za Zinc Phosphide zimetumika na kuokoa eneo la hekta 19,737.2 zilizolimwa mazao ya mahindi, ufuta, alizeti, karanga, mtama, muhogo na viazi vitamu. 

  • Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti visumbufu kuingia na kutoka nchini, Wizara imekagua tani 10,241,723.34 za mazao ya nafaka, bustani, mizizi, mbegu za mafuta, chai, tumbaku, kahawa, pamba, mikunde, mbao, mashudu na pumba katika vituo vya mipakani, bandari na viwanja vya ndege ambapo jumla ya vyeti 29,033 vya usafi wa mimea kwa ajili ya kuruhusu mazao kusafirishwa nje ya nchi na vyeti 2,039 vya kuruhusu mazao kuingia nchini vimetolewa.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa mafunzo ya udhibiti wa viwavijeshi kwa wakulima 200 na maafisa ugani 16 katika Kata 16 za Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero. Kadhalika, imetoa mafunzo ya mbinu za kudhibiti nzi wa matunda kwa wakulima 849 na maafisa ugani saba (7) katika Wilaya ya Handeni. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha matumizi ya taratibu na kanuni za ukaguzi wa mazao zinazofaa kuzuia visumbufu vya mimea kuingia nchini au kupeleka nje ya nchi zinazingatiwa, wataalam 34 wa Afya ya Mimea kutoka vituo vya Rusumo, Kabanga, Mutukula, na Namanga wamepatiwa mafunzo ya taratibu na kanuni za ukaguzi wa mazao ya mahindi, mchele na maharage yanayopitia katika mipaka hiyo. Aidha, Wizara imekamilisha maandalizi ya ramani ya ujenzi wa Kituo cha Utoaji wa Huduma kwa Pamoja Mipakani (One Stop Border Post – OSBP) yenye ukubwa wa mita za mraba 6,100 Manyovu – Kigoma. 
  • Mheshimiwa     Spika,       Wizara        kupitia

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (Tanzania Plant Health and Pesticides Authority – TPHPA) imeendelea kudhibiti ubora wa viuatilifu nchini ambapo hadi Aprili, 2022 maduka 233 na shehena 149 za viuatilifu zimekaguliwa na vibali 681 vimetolewa kwa wafanyabiashara wa viuatilifu. 

  • Vilevile, Wizara kupitia TPHPA imetoa mafunzo ya matumizi bora ya viuatilifu na utambuzi wa visumbufu kwa maafisa ugani, wakulima na wauzaji wa viuatilifu 806 katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Morogoro, Dar es salaam,

            Geita,      Mwanza,       Shinyanga,      Simiyu      na

Kilimanjaro. Aidha, imechambua sampuli 5,000 za mabaki ya viuatilifu kwenye mazao ya chakula katika mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Arusha, Mbeya, Lindi na Mtwara. Kati ya sampuli hizo, sampuli 2,000 ziligundulika kuwa na mabaki ya viuatilifu. 

Mtaalamu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania

(TPHPA) akiwa maabara kuchambua sampuli za mazao ili kuangalia mabaki ya viuatilifu  

Upatikanaji wa Ithibati ya Maabara

100. Mheshimiwa Spika, Wizara imekarabati maabara ya TPHPA na kununua mashine ya kuchambua sampuli za mazao, mbolea, maji na udongo. Hatua hiyo imefanikisha maabara kupata ithibati ambapo itasaidia mazao ya kilimo yatakayopimwa katika maabara hiyo, kukidhi viwango vya masoko ya kimataifa. Aidha, Wizara kupitia Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu (Tanzania

Initiatives for Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) imeendelea na ujenzi wa Kituo cha Udhibiti wa Visumbufu Kibaolojia ambao kwa sasa umefikia asilimia 65 na umegharimu jumla ya Shilingi 3,821,431,766.10.

4.2.2.4. Zana za Kilimo 

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuwezesha upatikanaji, utoaji wa huduma za kitaalam na kuhimiza matumizi ya zana bora za kilimo ili kuongeza tija na kupunguza harubu katika uzalishaji na usindikaji wa mazao ya kilimo. Hadi Aprili, 2022 matumizi ya trekta yameongezeka kutoka asilimia 23 mwaka 2020 hadi asilimia 25 mwaka 2021. Vilevile, idadi ya matrekta makubwa yameongezeka kutoka 19,604 mwaka 2020/2021 hadi 21,149 na matrekta madogo yameongezeka kutoka 8,883 mwaka 2020/2021 hadi 9,420. 
  1. Aidha, Bodi ya Pamba imenunua mashine za kupalilia 400 na kusambaza kwa wakulima katika Halmashauri zinazozalisha pamba kulingana na mahitaji.

Wizara imeendelea kuhimiza matumizi ya zana bora za kilimo ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo kama matrekta

makubwa katika shamba la Chuo cha Mafunzo Uyole mkoani Mbeya

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha Sekta Binafsi kuwekeza katika zana na mashine za kilimo kwenye mnyororo wa uzalishaji wa mazao. Hadi Aprili, 2022 Sekta Binafsi imeingiza nchini mashine na zana za kilimo kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na.

8.

Jedwali Na.8:  mashine na zana za kilimo zilizoingizwa nchini

Na.Mashine na Zana Idadi 
1.Matrekta makubwa1,729
2.Matrekta madogo653
3.Mashine kubwa za kuvuna812
4.Mashine ndogo za kuvuna516,466
5.Plau za matrekta 823,295
6.Haro za matrekta25,332
7.Mashine za kupura347,351
8.Zana za kupandia19,809
9.Majembe ya kukokotwa na wanyamakazi363,208
10.Mashine za kusindika mazao1,239,994

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imewatambua wabunifu wa zana za kilimo 16 katika mikoa ya Shinyanga (6), Dodoma (1), Mwanza (5), Arusha (1), Njombe (1), Manyara (1) na Tanga (1). Lengo la utambuzi huo ni kuwawezesha kupata mikopo yenye riba nafuu pamoja na kuwaunganisha na Taasisi za Utafiti wa Zana.
  1. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha matumizi ya zana bora za kilimo, Wizara imeingia mkataba na kampuni ya AFTRADE kuwekeza kwenye uanzishwaji wa Vituo Jumuishi vya Utoaji wa Huduma za Zana za Kilimo nchini

(mechanization hubs). 

  1. Wizara kwa kushirikiana na kampuni ya AFTRADE imefanya tathmini ya maeneo yanayofaa kuanzisha vituo hivyo.  Hadi Aprili, 2022 tathmini imebaini kuwa vituo 13 vimekidhi mahitaji ya uwekezaji huo na taratibu za kuwezesha kuanza kazi zinaendelea.  

                  4.2.3.     Huduma  na Mafunzo ya Ugani

4.2.3.1. Huduma za ugani

107. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara imenunua pikipiki 7,000, vishikwambi 384 na Extension kits 6,700 kwa ajili ya maafisa ugani kilimo. Pia, Wizara imenunua vifaa vya kupima afya ya udongo (soil scanner) 143 kwa ajili ya Halmashauri 143. Hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vifaa hivyo ilifanywa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 04 Aprili, 2022 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini, Dodoma. Jumla ya Shilingi 9,295,000,000 zimetumika kununua vifaa hivyo.

Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia wakati zoezi la ugawaji wa vitendea kazi kwa Maafisa Ugani zaidi ya 6,700 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, Jijini Dodoma, tarehe 4 Aprili, 2022

4.2.3.2. Mafunzo ya Ugani

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani 2,486 kuhusu kilimo biashara, matumizi bora ya zana za kilimo na kanuni bora za kilimo cha alizeti, zabibu, pamba, karanga, ufuta, soya, migomba na chikichi. Mafunzo hayo yaligharamiwa na Wizara kwa kushirikiana na Agricultural Market Development Trust – AMDT, Care International na Shirika la Maendeleo la Kilimo la Umoja wa Mataifa (International Fund for Agricultural Development – IFAD).
  1. Mafunzo hayo yametolewa katika mikoa ya Morogoro (Kilosa na Gairo), Njombe (Wanging’ombe na Ludewa), Ruvuma (Songea Vijijini na Namtumbo Vijijini), Kilimanjaro (Rombo, Hai na Siha), Manyara (Babati Vijijini na

Kiteto), Singida (Manyoni, Itigi na Ikungi), Dodoma (Kondoa TC, Chemba na Chamwino),  Tabora (Nzega Mjini, Nzega Vijijini, Urambo Vijijini na Kaliua Vijijini, Simiyu (Maswa, Meatu, Bariadi TC, Bariadi Vijijini, Busega na Itilima), Mara (Bunda na Serengeti), Iringa (Iringa Vijijini na Kilolo), Mbeya (Chunya na Mbarali), Songwe (Mbozi), Rukwa (Kalambo, Nkasi na Sumbawanga TC), Kigoma (Kasulu Vijijini na Kibondo), Mtwara (Masasi na Newala) na Lindi (Mtama Vijijini na Ruangwa). 

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa mafunzo ya uanzishwaji wa mashamba darasa kwa maafisa ugani 259 na wakulima viongozi 870 wa Mkoa wa Dodoma ili kuwezesha utoaji wa mafunzo ya mbinu bora za kilimo kwa vitendo kwa wakulima. Aidha, Wizara imewezesha uanzishwaji wa mashamba darasa 695, kati ya hayo alizeti ni 378 na pamba ni 317. Vilevile, imeanzisha mashamba ya mfano 672 yakiwemo ya alizeti 415 na pamba 257 katika mikoa ya Dodoma, Singida na Simiyu.  Aidha, maafisa ugani wa maeneo hayo wamepatiwa tani 10.5 za mbolea, viuatilifu (ekapack) 1,617 na viuagugu (ekapack) 1,584 kwa ajili ya kuanzisha mashamba hayo ambayo yatatumika kutoa mafunzo ya kilimo bora cha alizeti na pamba kwa wakulima kwa vitendo.
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TARI, imetoa mafunzo ya kilimo mseto na kuhamasisha matumizi ya miche ya chikichi iliyozalishwa kwa njia ya chupa (tissue culture) kwa wakulima 73,918, maafisa ugani 1,277 na wanafunzi wa shule za msingi 1,771. Pia, TARI imeanzisha  mashamba ya mfano 35 ya chikichi katika Mkoa wa Kigoma. Vilevile, TARI kwa kushirikiana na Bodi ya Mkonge imetoa mafunzo ya kilimo bora cha mkonge kwa maafisa ugani 55 na wakulima 331 katika Wilaya ya Handeni mkoa wa Tanga.
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutoa huduma za ugani kwa njia ya Mfumo wa Kielektroniki (M-Kilimo) ambao unamwezesha mkulima kupata huduma ya ushauri wa kitaalam kupitia simu ya kiganjani. Mfumo huo umelenga kutatua changamoto ya uhaba wa maafisa ugani waliopo pamoja na upatikanaji wa taarifa za masoko. Hadi Aprili, 2022 maafisa ugani 7,061 na wakulima 5,775,510 wamesajiliwa katika mfumo wa M-kilimo. Aidha, maswali 46,700 yameulizwa na kupatiwa majibu kupitia mfumo huo na Wizara inaendelea na uhamasishaji wa matumizi ya mfumo kwa wakulima. 
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mkonge imetoa mafunzo ya kilimo cha mkonge kwa wakulima 530 katika wilaya za Mkinga (364), Handeni (47), Korogwe (9), Kishapu (35), Meatu (11), Bariadi (12) na Itilima (52). Kutokana na mafunzo hayo jumla ya hekta 1,251.54 zimepandwa mkonge katika wilaya za Mkinga (hekta 451.72), Handeni 626.33), Chalinze (hekta 15), Korogwe (36.5), Kishapu (34.47), Meatu (19.52), Bariadi (23.0) na Itilima (45.0). Aidha, Bodi ya Pareto imetoa mafunzo ya kilimo bora cha pareto kwa wakulima 517 kutoka Mbeya (256), Ileje (71), Makete (88), Mufindi (71) na Manyara (31). Pia, Bodi kwa kushirikiana na kampuni za usindikaji wa pareto imetoa mafunzo ya uzalishaji wa pareto kwa vikundi vya Pashungu (52) na Shigamba (37) katika Halmashauri ya Mbeya

Vijijini.

  1. Mheshimiwa Spika, Bodi ya Korosho imetoa mafunzo ya kilimo bora kwa maafisa ugani 994 na wakulima 393 katika mikoa inayolima zao la korosho na mafunzo ya ubora wa korosho kwa maafisa ugani 229 katika mikoa ya Pwani na Tanga. Aidha, Bodi ya Kahawa imetoa mafunzo ya kilimo bora cha kahawa kwa wakulima 36,812 katika mikoa 16 inayozalisha kahawa. Kutokana na mafunzo hayo, mashamba 27,874 ya wakulima yamekarabatiwa pamoja na kuanzisha mashamba darasa 32 katika mikoa hiyo. Kadhalika, Bodi ya Sukari imetoa mafunzo ya kilimo bora cha miwa kwa wakulima 105 katika Wilaya ya Muheza kata za Muheza na Amani Mtibwa Morogoro.
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa mafunzo rejea kuhusu teknolojia za kisasa za kilimo bora cha alizeti, michikichi, soya na pamba kwa maafisa ugani 1,512 wa mikoa ya Singida, Dodoma, Manyara, Kilimanjaro, Morogoro, Ruvuma, Njombe, Tabora, Simiyu, Mara, Iringa, Songwe, Mbeya, Rukwa, Lindi, Mtwara na Kigoma. Aidha, Wizara imewezesha maafisa ugani 596 katika mikoa ya Singida (158), Dodoma (259) na Simiyu (179) kuanzisha mashamba darasa ya alizeti na pamba. 
  1. Pia, TARI imetoa mafunzo ya kanuni bora za kilimo cha zabibu kwa wakulima 865 kutoka kata za Mvumi Makulu, Mvumi Mission, Handali, Chinangali, Matumbulu, Mpunguzi, Mbabala, Hombolo, Mkonze na Chihanga na maafisa ugani 88 kutoka Halmashauri ya Kondoa (54), Mpwapwa (8) na Dodoma Jiji (26). 
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia mradi wa Agri-connect na TANSHEP imetoa mafunzo kwa wakulima 46,311 kuhusu kanuni bora za kilimo, uhifadhi wa mazao kabla na baada ya kuvuna, dhana ya ‘ANZIA SOKONI MALIZIA SHAMBANI’, na viwango vya ubora wa mazao katika mikoa ya Arusha (Ngorongoro na Arusha Vijijini), Kilimanjaro (Mwanga na Siha) na Tanga (Korogwe na Muheza). 

4.2.3.3. Ukarabati wa Vyuo vya Kilimo na Vituo vya Mafunzo kwa Wakulima 

118. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa kukarabati miundombinu ya Vyuo 12 vya Mafunzo ya Kilimo nchini ikiwemo ukarabati wa Ofisi, mabweni, mabwalo, madarasa, nyumba za watumishi, vyoo na maabara. Ukarabati wa miundombinu hiyo, upo katika hatua mbalimbali mfano ukarabati wa mabweni ya Ukiriguru, jengo la maktaba ya Chuo cha Kilimo Mtwara, majengo ya Ofisi za Vyuo vya Kilimo Tengeru, Tumbi, Uyole na Ilonga umefikia wastani wa asilimia 95. Aidha, ukarabati wa miundombinu ya Vyuo vya Kilimo Mubondo, KATRIN, KATC, Ilonga, Uyole na Inyala unaendelea na umefikia wastani wa asilimia 40. 

4.2.3.4. Udahili wa wanafunzi katika Vyuo

vya Mafunzo ya Kilimo

119. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara imedahili na kufadhili wanafunzi 2,360 wa ngazi ya Astashahada na Stashahada katika Vyuo 14 vya Mafunzo ya Kilimo. Kati ya hao, wanafunzi 1,507 ni wa mwaka wa kwanza na wanafunzi 853 ni wa mwaka wa pili. Vilevile, Wizara imedahili wanafunzi 582 wanaojigharamia wenyewe. Kati ya hao, wanafunzi 402 ni wa mwaka wa kwanza na 180 ni wa mwaka wa pili. Pia, Wizara inaendelea kutengeneza mfumo wa kielektroniki wa udahili wa wanafunzi kwa ajili ya vyuo 14 vya mafunzo ya kilimo ambao upo katika hatua za majaribio.

                  4.2.4.     Umwagiliaji 

120. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji kwa kujenga na kukarabati skimu za umwagiliaji. 

4.2.4.1. Ujenzi wa Miradi ya Umwagiliaji

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume inaendelea na ujenzi wa skimu ya Kirya (hekta 800) iliyopo Wilaya ya Mwanga na Endagaw (hekta 246) iliyopo Wilayani Hanang’ ambapo hadi Aprili, 2022 utekelezaji wa miradi hiyo umefikia asilimia 42 na 41, mtawalia. Aidha, utekelezaji wa miradi hiyo utagharimu Shilingi  1,064,674,871.20 (Kirya) na Shilingi 989,719,851.66 (Endagaw) hadi itakapokamilika. 
  1. Vilevile, mikataba kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Msanginya/Usense (hekta 106) iliyopo Wilaya ya Nsimbo na Msufini (hekta 1,000) iliyopo Wilaya ya Mvomero imesainiwa na wakandarasi wamekabidhiwa kazi kwa ajili ya utekelezaji na itagharimu Shilingi 1,963,326,966. Aidha, ujenzi wa bwawa katika skimu ya Orumwi (Siha) lenye mita za ujazo 58,000 litakalomwagilia hekta 200 umefikia asilimia 93. Ujenzi wa bwawa hilo utagharimu Shilingi 500,000,000 hadi kukamilika.  
  1. Mheshimiwa Spika, Tume kupitia Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Umwagiliaji (NIDF) inaendelea na ujenzi wa skimu ya Idudumo (hekta 300) umefikia asilimia 26. Ujenzi wa skimu hiyo utagharimu Shilingi 746,062,670 hadi kukamilika.  
  1. Vilevile, taratibu za manunuzi kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Mgambalenga (Kilolo), Mbaka (Busekelo) na Muhukuru (Songea) zimekamilika na hatua za kusaini mikataba zinaendelea. Ujenzi wa miradi hiyo utagharimu jumla ya Shilingi 1,700,000,000 na ujenzi utaanza Juni, 2022. Aidha, Tume kupitia NIDF imenunua vifaa vya karakana na kutengeneza mitambo saba (7) ambayo ni low bed (1), motor grader mbili (2), excavator tatu (3) na buldozer moja (1).   
  1. Mheshimiwa Spika, Tume kwa kushirikiana na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) inaendelea na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika skimu ya umwagiliaji ya Chita JKT kikosi cha 837KJ  (hekta 4,800) ambapo ujenzi umefikia asilimia 63. 

4.2.4.2. Ukarabati wa Miradi ya Umwagiliaji

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Tume imeendelea na ukarabati wa skimu za umwagiliaji za Kituani Mwenzae (Lushoto), Luganga (Iringa), Mseta Bondeni (Kongwa), Chinangali (Chamwino) na Fufu

(Chamwino).  Ukarabati huo, umefikia asilimia 88, 69, 12, 15, na 15 mtawalia. Aidha, ukarabati wa skimu za Karema (Katavi), Kilida (Katavi) na Lwafi Katongoro (Nkasi) utafanyika baada ya msimu wa mvua kuisha. Ukarabati wa skimu hizo utagharimu jumla ya Shilingi 917,502,356 hadi kukamilika. 

  1. Mheshimiwa Spika, taratibu za manunuzi ili kuwapata wakandarasi wa kukarabati miundombinu ya umwagiliaji katika skimu za

Lusu, Mvumi na Mwasubuya zinaendelea  ambapo tathmini ya zabuni ya skimu ya Lusu imekamilika; zabuni ya skimu ya Mvumi imefunguliwa; na zabuni ya skimu ya Mwasubuya inarudiwa kutangazwa kutokana na kutopatikana kwa wazabuni.

  1. Mheshimiwa Spika, Tume kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kutekeleza Mradi wa Kusimamia Maliasili na Kuendeleza Utalii Kusini mwa Tanzania (Resilient Natural Resource Management for Tourism and Growth Project-REGROW). Mradi huo unajenga na kukarabati skimu ya Madibira (hekta 3,000) uliopo Wilaya ya Mbarali ambapo hadi Aprili, 2022 ukarabati umefikia asilimia 27. Ujenzi na ukarabati wa mradi huo utagharimu jumla ya Shilingi 8,759,866,327.76. 
  1. Mheshimiwa Spika, maelezo ya kina ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji ni kama inavyoonekana katika Kiambatisho Na. 2.

4.2.4.3. Miradi ya Umwagiliaji Inayofanyiwa

Upembuzi yakinifu na Usanifu

  1. Mheshimiwa Spika, Tume kupitia ASDP II imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu za Mkombozi (Iringa), Idudumo (Nzega), Luiche (Kigoma/Ujiji) na Ilemba (Sumbawanga) kwa asilimia 100. Vilevile, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa la Ibanda (Sengerema/Geita),  Tlawi (Mbulu)  na skimu ya Makwale (Kyela) umefikia asilimia 65, 80 na 80, mtawalia kupitia ASDP II. Aidha, kupitia mradi wa REGROW, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika skimu nane (8) za Mbuyuni Kimani, Uturo, Isenyela, Makangarawe, Hermani, Chosi, Gonakuvagogolo na Matebete umefika asilimia 90. (Kiambatisho Na. 3). Skimu hizo zitajengwa katika mwaka wa fedha  2022/2023.
  1. Mheshimiwa Spika, Tume kupitia NIDF inaendelea na upembuzi yakinifu katika skimu 12 zenye jumla ya hekta 29,242 (Jedwali Na. 9). Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika skimu hizo utatekelezwa mwaka 2022/2023. 

Jedwali Na. 9: Skimu zinazoendelea kufanyiwa upembuzi yakinifu 

Na.Jina la Skimu/bwawaEneo (hekta)Wilaya
1.Kizi500Mpwapwa
2.Mlembule 3,000Mpwapwa
3.Masimba 1,500Iramba
4.Makondeko 3,000Newala
5.Ilemba 2,500Sumbawanga
6.Mbwasa 5,000Manyoni
7.Dirim 335Mbulu
8.Igenge-bwawa  57Misungwi
9.Mwamapuli-bwawa2,000Igunga
10.Masasi 350Chato
11.Bonde la Bahi  5,000Bahi
12.Eyasi 6,000Mbulu
Jumla 29,242 

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  1. Mheshimiwa Spika, Tume kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la Rikolto Tanzania imetoa mafunzo ya usimamizi na uendeshaji wa skimu za umwagiliaji pamoja na kilimo bora cha mpunga na mboga katika mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro ambapo wakulima 70 wamepatiwa mafunzo hayo. Pia, Tume kwa kushirikiana na Shirika la SNV chini ya mradi wa CRAFT imetoa mafunzo ya matumizi ya teknolojia bora za kilimo cha umwagiliaji kwa kuzingatia mabadiliko ya tabianchi kwa wakulima katika mikoa ya Njombe, Manyara, Iringa na Mbeya. 
  1. Vilevile, Tume kwa kushirikiana na Shirika la CARE International pamoja na Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania-SAGCOT) imetoa mafunzo ya kilimo biashara na kuunda vikundi vitano (5) vya vijana vitakavyokuwa vinazalisha mazao kwa tija na kibiashara katika skimu ya Itipingi mkoani Njombe. 
  1. Mheshimiwa Spika, Tume pia kwa kushirikiana na Shirika la Utafiti la Japan (Japan International Research Center for Agricultural Sciences – JIRCAS) inaendelea na utafiti wa matumizi bora ya maji katika skimu za Ndungu (Same), Lower Moshi (Moshi Vijijini) na skimu ya Mto wa Mbu (Monduli). Lengo la utafiti huo ni kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga kwa kuzingatia matumizi ya maji kwa ufanisi. 
  1. Aidha, Tume kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inaendelea na tathmini ya ukusanyaji wa ada za huduma za umwagiliaji, matumizi ya teknolojia zinazotumia maji kwa ufanisi na uwekezaji wa Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Serikali katika kuendeleza kilimo cha umwagiliaji nchini. Matokeo ya tathmini hiyo yatasaidia kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa ada na tozo za huduma za umwagiliaji pamoja na mapendekezo ya uwekezaji wenye tija katika sekta ya umwagiliaji.

                  4.2.5.     Masoko na Mifumo ya Masoko

  1. Mheshimiwa     Spika,       katika        mwaka

2021/2022, Wizara ya Kilimo ni moja ya Wizara zilizoshiriki kwenye Maonesho ya Dubai Expo, 2020 chini ya uratibu wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade). Maonesho hayo yalianza tarehe 01 Oktoba, 2021 na kumalizika tarehe 31 Machi, 2022 nchini Dubai – Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).  

  1. Mheshimiwa Spika, mafanikio yaliyopatikana katika maonesho hayo ni kusainiwa kwa hati saba (7) za makubaliano kwa ajili ya kushirikiana katika kuendeleza sekta ya kilimo. Mashirikiano hayo yamejikita katika maeneo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vituo vya kuchanganya mbolea na viuatilifu (fertilizer and pesticide blending facility/ies), upatikanaji na matumizi bora ya zana za kilimo, miundombinu ya umwagiliaji, uhifadhi na usafirishaji wa mazao. 

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe akisaini mkataba na

Mwakilishi wa Kampuni ya Agritech Global inayoongozwa na 

Mhe. Sheikh Ahmed Dalmook Al Maktoum. Mkataba huo unahusu ushirikiano katika uanzishwaji wa vituo vya zana za kilimo na

uchanganyaji wa mbolea. Tarehe 24 Februari, 2022 nchini Dubai.

  1. Mafanikio mengine ni ushirikiano katika kupoka na kuhodhi masoko ya mazao ya kilimo ambapo tarehe 03 Mei, 2022 shehena la kontena lenye tani 22.3 za parachichi aina ya HASS lilipokelewa Mumbai India ikiwa ni matokeo ya mkataba uliosaniwa kati ya Tanzania Horticulture Association (TAHA) na India kwa ajili ya kufungua masoko ya mazao ya mboga, matunda na viungo wakati wa maonesho ya Dubai Expo, 2020
  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara kupitia CPB imenunua mahindi tani 33,600 kutoka kwa wakulima na imeiuzia Kampuni ya Grain Industries Limited ya Kenya tani 2,000 za mahindi zenye thamani ya Shilingi 1,060,000,000. Katika jitihada za kutafuta masoko, Wizara imefanikiwa kupata masoko katika nchi za DRC, Kenya, Zimbabwe, Rwanda, Burundi na Comoro. Kutokana na jitihada hizo, ghala za kukodi zenye uwezo wa kuhifadhi tani 5,000 na tani 2,000 zimepatikana katika miji ya Juba (Sudan Kusini) na

Lubumbashi (DR Congo), mtawalia.  

  1. Aidha, Wizara imepata masoko mapya ya zao la parachichi katika nchi za India na Afrika Kusini na zao la ndizi nchini Kenya baada ya mazao hayo kukidhi viwango vya ubora.  

Maparachichi aina ya Hass yaliyokidhi vigezo yakiwa tayari kusafirishwa kuelekea Afrika Kusini kupitia Kampuni ya Kuza Afrika, wilayani Rungwe mkoani Mbeya  

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021 tani 12,250 za parachichi zenye thamani ya Shilingi Bilioni 24.95 ziliuzwa katika nchi mbalimbali kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 10.

Jedwali Na. 10: Mauzo Zao la Parachichi katika Nchi

Zilizonunua kwa mwaka 2021

NchiKiasi kilichouzwa (Tani ‘000’)Thamani (TZS Bilioni)
Uholanzi4.511.8
Uingereza1.73.0
Ufaransa1.82.8
Umoja wa Falme za Kiarabu0.71.8
Afrika Kusini0.41.4
Kenya1.81.0
Nchi nyingine1.353.15
Jumla12.2524.95

Chanzo: Mamlaka ya Mapato Tanzania 2022

  1. Mheshimiwa Spika, soko la mahindi limeendelea kukua katika nchi ya Kenya ambapo katika kipindi cha miaka mitatu (3) Tanzania imepeleka wastani wa tani 83,087 kwa mwaka sawa na asilimia 70 ya mahindi yote yanayouzwa nje ya nchi. Aidha, mauzo ya mahindi nje ya nchi ni kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 11.

Jedwali Na. 11: Uuzaji wa Mahindi Nje ya Nchi (tani).

Nchi201920202021Wastani
Kenya57,65839,154152,44983,087
Sudan Kusini2,2009,0008,0006,400
Zimbabwe1,11217,0006,037
DRC10,9614,5982,4265,995
Burundi8,8436,4131,8285,695
Rwanda9272,12313,0975,382
Uganda3,2003,9761,1752,784
Sudan5,0001,667
Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu2,940980
Nyingine562276267368
Jumla85,46582,543187,185118,398

Chanzo: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), 2022

  1. Kadhalika, soko la mchele limeendelea kukua hususan katika nchi ya Uganda ambapo katika kipindi cha miaka mitatu (3) wastani wa tani 136,377.97 kwa mwaka zimeuzwa Uganda sawa na takribani asilimia 56.42 ya mchele wote unaouzwa nje ya nchi. Mauzo ya mchele nje ya nchi ni kama inavyoonekana katika Jedwali Na.

12.

Jedwali Na. 12: Uuzaji wa Mchele Nje ya Nchi (tani).

Nchi201920202021Wastani
Uganda6,129.40124,079.50278,925.0136,377.9 7
Kenya999.246,947.30115,128.054,358.17
Rwanda9,520.3042,627.4061,131.0 37,759.57
DRC2,910.004,755.006,724.04,796.33
Burundi4502,058.8011,979.04,829.27
Zambia95780337.0404.00
India702.6234.20
Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu24551.0191.67
Malawi45410.0151.67
Nyingine7,057.80149559.02,588.60
Jumla27,185.7222,144.5475,744. 0241,691.4 3

Chanzo: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) 2022

  1. Mheshimiwa     Spika,      katika        msimu

2020/2021, Wizara imefanikisha kuuza tani 53,594.35 za soya katika nchi za India, China, Rwanda na Kenya ikilinganishwa na tani 2,647 zilizouzwa msimu wa 2019/2020. Jitihada hizo zimewezesha bei ya soya kuongezeka kutoka Shilingi 1,500 msimu wa 2019/2020 hadi Shilingi 2,200 msimu wa 2021/2022.  

  1. Vilevile, hadi Aprili, 2022 tani 231,103 za korosho ghafi; tani 144,792 za pamba; tani 60,819 za kahawa; na tani 6,875 za kakao zimeuzwa. Pia, Wizara imewezesha wakulima 500 wa mikoa ya Arusha na Manyara kuingia mkataba na Tanzania Breweries Ltd (TBL) wa kununua tani 5,000 za shayiri kwa bei ya Shilingi 850 kwa kilo. Kadhalika, CPB imeuza tani 183.22 za maharage, tani 215.96 za mchele na tani 1,023.70 za mbegu za mafuta ya alizeti.
  1. Mheshimiwa Spika, Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea,

Wanyama na Usalama wa Chakula (East African Community Protocol on Sanitary and

Phytosanitary– SPS Measures) imeridhiwa ambayo itasaidia ukuaji wa masoko ya mazao ya kilimo nje ya nchi.  Vilevile, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeandaa Mkakati na Mpango Kazi wa Masoko ya Mazao ya Kilimo (Market to Farm Agricultural Marketing Strategy and Action Plan 2021-2026). Mkakati huo umelenga kuwawezesha wakulima kufanya utafiti wa soko na kuzalisha kulingana na mahitaji ya soko. 

  1. Pia, Wizara imeandaa Mwongozo wa Mifumo ya Uuzaji wa Mazao ya Kilimo ili kuongeza ufanisi katika taratibu za usimamizi wa mauzo ya mazao ya kilimo pamoja na kuwezesha wadau kujua taratibu zitakazotumika kusimamia mauzo ya mazao ya kilimo. 
  1. Mheshimiwa     Spika,      katika        mwaka

2021/2022tani 6,794 za singa zenye thamani ya Shilingi Bilioni 21.8 na bidhaa mbalimbali za mkonge tani 711 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.14 zimeuzwa kwenye soko la ndani. Aidha, tani 20,606.64 za singa zenye thamani ya Dola za Marekani 33,773, na tani 866 za bidhaa mbalimbali za mkonge zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 2.46 zimeuzwa kwenye soko la nje. Aidha, Bodi ya Mkonge imewaunganisha wakulima wadogo 1,631 wakiwemo wa AMCOS (1,206) na Binafsi (425) kwenye soko kwa mfumo wa zabuni ambapo wameweza kuuza mkonge daraja la UG kwa Shilingi 3,700,000 kwa tani ikilinganishwa na Shilingi 3,300,000 nje ya mfumo. Pia,katika msimu wa ununuzi wa mwaka 2020/2021 tani 58,295 za tumbaku zenye thamani ya Dola za Marekani 90,515,115.04 zimeuzwa.  

Viwanda vya kati na vikubwa vimechangia kuongeza thamani zao la mkonge na kuzalisha bidhaa mbalimbali za mkonge ambazo zimeuzwa ndani na nje ya nchi

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Pareto imeendelea kusimamia uzalishaji na ununuzi wa Pareto ambapo hadi Aprili, 2022, tani 1,848 za maua ya pareto zimezalishwa na kuuzwa kwa Kampuni za Pareto Tanzania (Mafinga) na Tanextract Ltd (Mbeya) kwa ajili ya usindikaji nchini. 
  1. Mheshimiwa Spika, tani 31,360 za kahawa aina ya Arabika zenye thamani ya Dola za Marekani 87,076,720 na tani 41,668 za aina ya Robusta zenye thamani ya Dola za Marekani 55,190,253.36 zimeuzwa.
  1. Mheshimiwa Spika, hadi Aprili, 2022 ujenzi wa kituo cha udhibiti wa visumbufu kibaolojia kupitia TANIPAC umefikia asilimia 79. Aidha, ujenzi wa Kituo Mahiri cha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna umefikia asilimia tano (5). Kituo hicho kitatumika kusambaza teknolojia za usimamizi wa mazao baada ya kuvuna. 
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na TAHA, Balozi zetu katika nchi za Ulaya, Marekani na Mashariki ya Kati imeongeza wigo wa masoko kwa mazao ya bustani hasa matunda na viungo katika nchi hizo. Aidha, wanunuzi kutoka nchi mbalimbali wameonesha utayari wa kununua mazao ikiwemo matunda hasa maembe na ndimu zisizo na mbegu zinazozalishwa nchini. Mfano, uhitaji wa maembe kutoka Tanzania ni jumla ya tani 36,000 kwa mwaka na ndimu ni tani 17,400 kwa mwaka. Katika mwaka 2022/2023, Wizara kwa kushirikiana na TAHA, Serikali ya Sweden na UNDP itaanza utekelezaji wa mradi wa kuongeza uwezo wa nchi katika kuzalisha mazao hayo kwa kuwezesha upatikanaji wa miche 1,500,000, kuwajengea uwezo wakulima kuhusu mbinu bora za kisasa na teknolojia na kuwapa elimu ya biashara. Hatua hizo zitawezesha kuongeza uzalishaji wa maembe kufikia tani 120,000 na ndimu kufikia tani 27,500 ifikapo mwaka 2025/2026.

Ushiriki wa Sekta Binafsi katika Kilimo

153. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuthamini mchango wa Sekta Binafsi kama kichocheo cha ukuaji wa Sekta ya Kilimo, kuhakikisha usalama wa chakula, uongezaji wa thamani ya mazao ya kilimo, kuimarisha upatikanaji wa pembejeo, kuongeza ajira na masoko ya mazao ya kilimo. Taarifa ya utekelezaji wa ASDP II kupitia Sekta Binafsi inaonesha kuwa hadi Juni 2021 Kampuni 606 za Sekta Binafsi, Asasi za kiraia 47 na Mashirika yasiyo ya kiserikali 64 yamewekeza katika Sekta ya kilimo. 154. Aidha, Wizara imeratibu majukwaa 52 ya majidiliano na Sekta Binafsi kwa mazao asilia ya biashara, nafaka, mikunde, bustani na mbegu za mafuta ya kula kwa ajili ya kutatua changamoto za kikodi na kisera.

Wabia wa Maendeleo

155. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha mahusiano ya kimataifa kupitia wabia wa maendeleo ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kukuza uchumi kutokana na uwekezaji katika Sekta ya Kilimo. Maeneo yaliyozingatiwa katika uwekezaji wa wabia wa maendeleo ni pamoja na usimamizi wa mazao baada ya kuvuna, vijana, masoko, ujenzi wa miundimbinu ya hifadhi wa mazao, kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji, uongezaji wa thamani, upatikanaji wa mbegu bora, afya ya mimea, lishe,, huduma za ugani, mazingira na jinsia. Hadi Juni, 2021 jumla ya Shilingi 30,709, 669,050,600 zimetumiwa na wadau kutekeleza miradi 199 ya sekta ya kilimo.

4.2.6. Taasisi za Fedha na Upatikanaji wa Mitaji

  1. Mheshimiwa Spika, Taasisi za fedha zimeendelea kuwa muhimu katika upatikanaji wa mitaji katika sekta ya kilimo. Taarifa ya utekelezaji ya ASDP II hadi Juni inaonesha kuwa taasisi fedha ikiwemo benki ya CRDB, NMB, TADB na TIB zilitoa mikopo ya Shilingi 1,267,700,000,000 katika kundeleza sekta ya kilimo.
  2. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha upatikanaji wa mitaji, Wizara kwa kushirikiana na Sekta Binafsi iliunda kamati ya viongozi ya kushughulikia mifumo ya ugharimiaji wa Sekta ya Kilimo ikiwa ni pamoja na kupunguza riba ya mikopo. Matokeo ya shughuli ya Kamati hiyo ni benki za biashara za CRDB na NMB kushusha viwango vya riba ya mikopo ya kilimo kutoka asilimia 20 na 17, mtawalia hadi kufikia asilimia 9. Pia, hatua hiyo imepelekea benki ya NMB kutenga Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya kukopesha wajasiriamali katika sekta ya kilimo kupitia matawi yake 225 nchini.  
  1. Mheshimiwa Spika, kupitia kamati hiyo Wizara imefanya majadiliano na benki za biashara na kuwezesha wakulima kupata mikopo. Hadi Aprili, 2022 TADB imetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 116.36 kwa ajili ya pembejeo za kilimo kwenye mazao ya kahawa,  na kufufua vinu vya kuchambua pamba vya Kahama, Chato, Mbogwe, Bukombe, Lugeye Sola, Manawa na kiwanda cha mafuta ya chikichi cha Trolle Meesle Tanzania Ltd kilichopo mkoa wa Kigoma. 
  1. Mheshimiwa Spika, Aidha, TADB imetoa mikopo ya moja kwa moja (direct lending) yenye thamani ya Shilingi Bilioni 482.4 kwa ajili ya kuwekeza katika mnyororo wa thamani wa kilimo. Pia, TADB kupitia Mfuko wake wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo (Smallholder Credit Guarantee Scheme) imetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 144 kwa wakulima 987 pamoja na wadau wengine wa kilio hususan AMCOS na wajasiriamali wa dogo na wakati katika Sekta ya Kilimo. 
  1. Kadhalika, TABD imeingia mikataba na Benki washirika 14 katika mfuko huo ikiwemo; Benki ya Maendeleo, CRDB, NMB, TCB, AZANIA,

NBC, STANBIC, Absa, KCBL, PBZ, Uchumi Microfinance, FINCA, MuCoBa na TaCoBa ikiwa ni moja kati ya jitihada za Benki kuchangia utoaji wa mikopo kwa wakulima wadogo na Sekta ya kilimo kutoka Taasisi za Fedha nchini. Jumla ya mikopo hiyo, imewanufaisha wakulima wadogo, wakati na wakubwa zaidi ya 1,527,175 wanaojishughulisha katika mnyororo wa thamani wa kilimo. 

  1. Vilevile, TADB imeanzisha Mfuko wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo (Smallholder Farmer’ Credit Guarantee Scheme) kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa mitaji kupitia mikopo ambapo hadi Aprili, 2022 mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 125.02 imedhaminiwa na kutolewa kwa wanufaika 11,987 tangu kuanzishwa kwa mfuko kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 13. 

Jedwali Na. 13: Wanufaika wa Mikopo ya Mfuko wa Dhamana kwa Wakulima Wadogo Hadi Aprili, 2022.

Na.Mchanganuo       wa WanufaikaIdadi   ya WanufaikaThamani ya Mikopo (Tshs.)
1.Wanufaika binafsi11,73555,172,104,858.64
2.Vyama                 vya Ushirika (AMCOS)19012,741,153,300.00
3.Wafanyabiashara wadogo na wa kati6257,103,120,028.02
 Jumla11,987125,016,378,186.66

  Chanzo: Benki ya Maendeleo ya Kilimo, 2022

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mfuko wa Taifa wa Pembejeo (Agriculture Inputs Trust Fund– AGITF) imetoa mikopo 50 yenye thamani ya Shilingi 1,838,434,000kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 14. 

Jedwali Na. 14: Mikopo Iliyotolewa na AGITF Hadi Aprili, 2022.

NaAina ya MikopoIdadi ya WakopajiThamani                ya Mikopo
1.Matrekta mapya10467,950,000
2.Pembejeo10395,000,000
3Umwagiliaji5249,729,000
4Ufugaji/ Livestock5125,600,000
5.Mashine za kusindika110,000,000.00
6.Matrekta      ya       mikono (Powertiller)453,900,000.00
7.Shughuli za shamba15536,255,000
 Jumla501,838,434,000

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

                  4.2.7.     Uzalishaji wa Mazao

163. Mheshimiwa Spika, Sekta ndogo ya mazao inahusika na uzalishaji wa mazao zaidi ya 90 katika kanda saba (7) za kilimo. Mazao hayo yanajumuisha mazao ya asilia ya biashara, mazao ya mafuta, mazao ya chakula na mazao ya bustani. 

4.2.7.1. Mazao Asilia ya Biashara

164. Mheshimiwa Spika, uzalishaji wa mazao asilia ya biashara umekuwa ukipanda na kushuka kutokana na kuyumba kwa bei katika Soko la Dunia zilizosababishwa na athari za UVIKO-19. Mfano, uzalishaji wa mazao asilia ya biashara umepungua kutoka tani 1,012,429  mwaka 2017/2018 hadi tani 898,966.8 mwaka 2020/2021. Aidha, uzalishaji katika msimu wa mwaka 2021/2022 umefikia tani 938,586.81kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 15.

Jedwali Na. 15: Mwenendo wa Uzalishaji wa Mazao Asilia ya Biashara 

Zao 2017/2018 2018/20192019/2020 2020/2021 2021/2022
Pamba  222,039         348.958      348,977122,836      144,792**
Kahawa 45,245          68,147        60,65173,027        65,235**
Chai  34,010          37,193        28,71527,510         17,615*
Pareto  2,400            2,014          2,5102,412           1,895*
Tumbaku         50,522          72,325        37,54658,508          70,775
Korosho  313,826         225,053      232,682210,786 238,555.81**
Mkonge  40,635          33,271        36,37936,169.8         29,719*
Sukari  303,752         359,219      311,358367,718        370,000
Jumla 1,012,429 797,570.958   1,058,818898,966.8  938,586.81

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

* Uzalishaji unaendelea

** Msimu wa mauzo

i. Zao la Mkonge 

165. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Mkonge Tanzania imeendelea kuhamasisha uzalishaji wa mkonge na kuongeza upatikanaji wa bidhaa zake. Hadi Aprili, 2022 uzalishaji wa mkonge umefikia tani 29,719 na uzalishaji unaendelea.  Pia, Bodi imepima na kugawa mashamba yenye hekta 2,202.02 kwa wakulima wapya 939 kwa ajili ya kilimo cha mkonge. 

ii. Zao la Tumbaku

166. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Tumbaku Tanzania imehamasisha kuongeza  uzalishaji wa zao la tumbaku kutoka tani 37,546 msimu wa 2019/2020 hadi tani 58,508 msimu wa 2020/2021. Vilevile, katika msimu wa uzalishaji wa mwaka 2021/2022, wakulima wa tumbaku wameingia mkataba na kampuni za Premium

Active TZ Ltd, Alliance One TZ Ltd, Japan Tobacco International Leaf Services, Magefa Growers Ltd, Pachtec Co. Ltd, ENV Services Ltd Jespan Co. Ltd, Naile Leaf TZ Co na Biexen Co. Ltd kwa ajili ya kuzalisha tani 70,775 za tumbaku. 

iii. Zao la Pareto

167. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Pareto Tanzania imeendelea kusimamia uzalishaji na ununuzi wa pareto ambapo hadi Aprili, 2022 tani 1,895 za maua makavu ya pareto zimezalishwa na kuuzwa kwa Kampuni za pareto Tanzania (Mafinga) na Tanextract Ltd (Mbeya) kwa ajili ya usindikaji. Vilevile, Bodi imetengeneza vikaushio vinne (4) vya maua ya pareto katika Wilaya ya Mufindi (3) na Ileje (1). 

iv. Zao la Chai

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Chai Tanzania imeendelea kusimamamia uzalishaji, tija na ubora wa chai nchini. Hadi Aprili, 2022 uzalishaji wa chai kavu umefikia tani 17,615 sawa na asilimia 58.72 ya lengo la kuzalisha tani 30,000 na uzalishaji unaendelea. Kadhalika, mapato yanayotokana na mauzo ya chai nje ya nchi yameongezeka kutoka Dola za Marekani 23,586,823 kwa mwaka 2020/2021 hadi Dola za Marekani 24,857,975 mwaka 2021/2022. Aidha, wastani wa tija kwa wakulima wadogo hadi Aprili, 2022 ulikuwa ni kilo 364.73 za chai kavu sawa na asilimia 31.73 ya lengo na wakulima wakubwa ni kilo 485.03 sawa na asilima 22.07 ya lengo. 
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi kwa kushirikiana na TSHTDA imekagua mashamba makubwa 17 na kuhamasisha ufufuaji wa mashamba ya wakulima wadogo yenye ukubwa wa hekta 650 katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe na Tanga. Hadi Aprili, 2022 mashamba ya wakulima wadogo yenye hekta 201 yamefufuliwa katika mikoa ya Njombe na Mbeya. 

Bodi ya Chai imeendelea kusimamamia uzalishaji, tija na ubora wa chai nchini kupitia mashamba madogo na makubwa

  1. Vilevile, mashamba mapya ya chai yenye hekta 200 yameanzishwa katika mkoa wa Njombe. Aidha, Bodi imekagua viwanda 12 vya kusindika chai vilivyopo Mbeya, Iringa, Njombe na Tanga na kutoa elimu kuhusu kilimo bora cha chai (GAP), usindikaji bora (GMP) pamoja na sheria na kanuni za chai kwa wafanyakazi na wakulima.
  1. Pia, Bodi imeendelea kufuatilia ukarabati wa kiwanda cha chai Mponde ambapo hadi Aprili, 2022 ukarabati umefikia asilimia 75. Vilevile, Bodi imesajili kampuni mpya tano (5) za kuchanganya na kufunga chai kwenye vikasha na kufanya idadi ya kampuni kufikia 15. 

v. Zao la Korosho

  1. Mheshimiwa Spika, katika msimu wa 2021/2022 uzalishaji wa korosho umefikia tani 238,555.81 sawa na asilimia 85.2 ya lengo la kuzalisha tani 280,000 na makusanyo ya uzalishaji kwa vikundi vya ubanguaji bado yanaendelea. Kati ya kiasi hicho, tani 130,296.917 zimezalishwa Mtwara, tani 66,007.194 Lindi, tani 25,242.524 Ruvuma, tani 15,862.065 Pwani, tani 715.687 Tanga, tani

12.885 Mbeya, tani 89.084 Njombe, tani 11.670 Dar es Salaam, tani 198.931 Morogoro, tani 36.714 Singida, tani 45.000 Rukwa tani 2.184 Katavi 2.161 Tabora, tani 29.466 Dodoma, tani 2.400 kigoma na tani 0.932 katika mkoa wa

Iringa.

  1. Bodi ya Korosho Tanzania imeandaa hekta 400 katika Wilaya ya Ruangwa kwa ajili ya kuanzisha kilimo cha pamoja. Aidha, Bodi na AMCOS zimenunua vipima unyevu vitatu (3) na 161, mtawalia, kwa ajili ya udhibiti wa ubora wa korosho.

Korosho kutoka shamba la kilimo cha pamoja la Masigati, Manyoni mkoani Singida lenye ukubwa wa ekari 23,000

vi. Zao la Kahawa

               174. Mheshimiwa     Spika,      katika      mwaka

2021/2022, uzalishaji wa kahawa umefikia tani 65,235, sawa na asilimia 93 ya lengo la kuzalisha tani 70,000. Aidha, Bodi ya Kahawa Tanzania imevijengea uwezo Vyama vya Ushirika 68 katika mikoa ya Kagera, Ruvuma, Kilimanjaro, Songwe, Mbeya, Mara, Kigoma, Njombe, na Tanga kuhusu biashar a ya kahawa na namna ya kuuza kahawa katika soko la moja kwa moja.

Mti wa kahawa aina ya arabika katika shamba la West

Kilimanjaro, wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro  

vii. Zao la Pamba

175. Mheshimiwa Spika, katika msimu wa 2021/2022, Wizara kupitia Bodi ya Pamba Tanzania imeendelea kuhamasisha na kusimamia uzalishaji wa zao la pamba kwa kusambaza mbegu bora na viuatilifu pamoja na kutoa mafunzo kwa wakulima.  Uzalishaji wa pamba umeongezeka kutoka tani 122,836 mwaka 2019/2020 hadi tani 144,792 mwaka 2020/2021 ambalo ni ongezeko la asilimia 18. Ongezeko hilo limechangiwa na matumizi sahihi ya mbinu bora za kilimo kupitia kampeni zilizoendeshwa na Bodi, kuimarika kwa huduma za ugani na matumizi ya mbegu bora na viuatilifu.

Shamba la pamba la Mkulima hodari wilaya ya Itilima mkoani Simiyu

4.2.7.2. Mazao ya Chakula

176. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021, uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka kutoka tani 18,196,733 mwaka 2020 hadi tani 18,665,217, sawa na ongezeko la asilimia 2.6. Kati ya kiasi hicho, tani 10,874,425 zilikuwa ni mazao ya nafaka na tani 7,790,792 mazao yasiyo ya nafaka (Jedwali Na. 16). Ongezeko hilo lilichangiwa na huduma bora za ugani, upatikanaji wa pembejeo za kilimo, unyeshaji na mtawanyiko mzuri wa mvua na kuimarika kwa masoko ya ndani na nje ya nchi.

Jedwali Na. 16: Mwenendo wa Uzalishaji wa Mazao ya Chakula (Tani ‘000’) Mwaka 2016-2021.

Zao20172018201920202021
Mahindi 6,6816,2735,6526,7117,039
Mchele 1,5942,2202,0633,0382,688
Ngano 5057637770
Mtama, Uwele na Ulezi1,0649881,1171,0431,077
Muhogo(mkavu)1,3422,7912,7282,4272,486
Maharage na Mikunde 2,3181,8231,8881,8952,236
Ndizi (kavu)8451,1321,1351,3581,443
Viazi (Vitamu na mviringo) (kavu)2,0081,6081,6441,6471,626
Jumla 15,90216,89216,29018,19718,665

Chanzo: Wizara ya Kilimo

                 4.2.7.3. Mazao    yenye    Mahitaji    Makubwa

yanayoagizwa nje ya nchi

177. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuongeza uzalishaji wa mazao yenye mahitaji makubwa (Import substitution crops) ili kupunguza uagizaji wa bidhaa/mazao hayo kutoka nje ya nchi. Miongoni mwa bidhaa/mazao hayo ni pamoja na ngano, sukari na mafuta ya kula. Katika mwaka 2021/2022, utekelezaji wa mikakati hiyo ni kama ifuatavyo: – 

i. Uzalishaji wa Miwa na Sukari

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Sukari Tanzania imeendelea kuongeza uzalishaji wa sukari ili kufikia lengo la kuzalisha tani 700,000 ifikapo 2025. Hadi Aprili, 2022 uzalishaji wa sukari umefikia tani 370,000 sawa na asilimia 94 ya lengo la kuzalisha tani 375,000. Katika kuongeza upatikanaji wa mbegu bora za miwa, Bodi kwa kushirikiana na TARI imebaini maeneo ya Gichameda, Mawenairon na Kiru Six katika Mkoa wa Manyara yanafaa kuanzisha vitalu vya kuzalisha mbegu bora za miwa. Aidha, wakulima katika maeneo hayo wapo tayari kutoa mashamba yao kwa ajili ya kuanzisha kitalu chenye ukubwa wa ekari sita (6).
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kushirikana na wazalishaji wa sukari kutekeleza mpango wa kuongeza uzalishaji katika viwanda vya Kilombero, Kagera, Mtibwa na TPC kwa kupanua mashamba, kusimika mitambo mipya ya kuchakata miwa na kuongeza tija na kujenga miundombinu ya umwagiliaji. Hatua hizo, zinalenga kuongeza uzalishaji wa sukari kufikia jumla ya tani 635,012 mwaka 2025.
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Sukari imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi mipya ya uzalishaji wa sukari ya Bagamoyo na Mkulazi II. Ujenzi na usimikaji wa kiwanda cha sukari cha Bagamoyo chenye uwezo wa kuzalisha tani 50,000 kwa mwaka umefikia asilimia 90 na uzalishaji unatarajiwa kuanza Juni 2022. Kwa kuanzia, kiwanda hicho kinatarajiwa kuzalisha tani 35,000 za sukari ifikapo mwaka 2025. Aidha, ujenzi wa msingi wa kiwanda cha mkulazi II umefikia asilimia 30 na kitakapokamilika kitazalisha tani 50,000 kwa mwaka.
  2. Mheshimiwa Spika, miradi mingine mipya ya uzalishaji wa sukari ya Kampuni za Rai group (Rufiji – Lindi) na Lake Agro Ltd (Kasulu – Kigoma) ipo katika hatua za awali za kumilikishwa ardhi ya uwekezaji. Miradi hiyo itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 250,000 na 30,000 mtawalia. 
  1. Mheshimiwa Spika, Bodi imeingia makubaliano na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kuchemsha mbegu pamoja na ubunifu wa kiwanda kidogo cha sukari chenye uwezo wa kusindika tani 10 za miwa kwa saa.

 ii. Zao la Ngano

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, uzalishaji wa ngano umefikia tani 70,288 ikilinganishwa na mahitaji halisi ya zaidi ya tani 1,000,000 za ngano kwa mwaka. Uzalishaji mdogo wa ngano unatokana na tija ndogo, uhaba wa mbegu bora zenye uwezo wa kukidhi mahitaji ya soko na mabadiliko ya tabianchi na kubadilisha matumizi katika mashamba makubwa.  
  1. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hizo, Wizara ilitenga Shilingi 750,000,000 kwa ajili ya utafiti na uzalishaji wa zao la ngano. Aidha, Wizara kupitia TARI imeendelea kuimarisha utafiti na uzalishaji wa mbegu za ngano ambapo imekusanya sampuli 11 za ngano zinazozalishwa nchini kwa ajili ya kupima kiwango cha gluten ili kushauri aina ya mbegu zinazofaa kutumiwa na wakulima katika uzalishaji kulingana na mahitaji ya viwanda nchini. Kati ya sampuli hizo, sampuli sita (6) (Lumbesa, Mbayuwayu, Chiriku, Sifa, Kariege na Riziki C1) zimeonesha kuwa na kiwango cha gluten zaidi ya asilimia 10 kinachohitajika kwa ajili ya uokaji.  
  1. Mbegu hizo zitatumiwa na wakulima kuzalisha ngano kwa kuingia mikataba na wanunuzi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiagiza ngano kutoka nje ya nchi.
  1. Vilevile, TARI imetoa mafunzo ya mbinu bora za uzalishaji wa ngano kwa kutumia mbegu hizo kwa maafisa ugani na wakulima 1,085 kutoka Wilaya za Karatu, Monduli, Siha na Hanang’. Aidha, TARI imechimba visima viwili (2) katika kituo cha utafiti Uyole kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mbegu za ngano.  
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia CPB imeingia mkataba na wakulima 264 wa wilaya za Siha, Karatu, Monduli na Hanang’ kwa ajili ya kununua ngano itakayozalishwa na wakulima hao kwa bei ya Shilingi 800 kwa kilo. Aidha, CPB imewapatia wakulima hao tani 210 za mbegu bora za ngano na kuwaunganisha na taasisi za fedha kwa lengo la kupata mikopo ya kununua mbolea na viuatilifu.  

iii. Mazao ya Mbegu za Mafuta

  1. Mheshimiwa Spika, mafuta ya kula nchini huchangiwa na mazao ya alizeti, karanga, pamba, soya, nazi, chikichi na  ufuta ambapo, alizeti huchangia asilimia 90. Uzalishaji wa mafuta ya kula nchini ni wastani wa tani 300,000 ikilinganishwa na mahitaji ya tani 650,000 kwa mwaka. Kutokana na upungufu huo, nchi huagiza tani zipatazo 350,000 za mafuta ya kula na hugharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 470 kwa mwaka.  
  1. Mheshimiwa Spika, upungufu wa uzalishaji wa mafuta unatokana na tija ndogo ya uzalishaji ambayo inachangiwa na upatikanaji mdogo wa mbegu bora, mbolea, viuatilifu, matumizi ya mbinu duni za uzalishaji na mabadiliko ya tabianchi. 
  1. Mheshimiwa Spika, katika kuongeza uzalishaji wa mbegu za mafuta ya kula, Wizara imesambaza tani 2,000 za mbegu bora za alizeti zenye thamani ya Shilingi 5,844,993,000 kwa utaratibu wa ruzuku kwa wakulima wa mikoa ya Singida, Dodoma, Simiyu na Manyara. Mbegu hizo zitazalisha tani 400,000 za alizeti ya kukamua mafuta ambazo zitakazozalisha mafuta ya kula tani 100,000. Aidha, Wizara imeendelea kutekeleza mpango wa muda mrefu wa kuzalisha miche bora ya chikichi na kuigawa bure kwa wakulima ambapo jumla ya miche 896,029 imesambazwa kwa wakulima katika mikoa ya

Kigoma, Mbeya Mtwara, Kagera, Katavi na Tanga

  1. Vilevile, Wizara imehamasisha kampuni za usindikaji kuingia mikataba na wakulima ya kununua mbegu za mafuta ya kula. Hadi Aprili, 2022 wakulima 7,588 wa zao la alizeti wameingia mikataba na kampuni za Pyxus Agriculture Tanzania Ltd (wakulima 5,088), Qstec (wakulima

1,000), na Mwenge Sunflower Oil (wakulima 1,500) kutoka katika mikoa ya Dodoma, Singida, na Manyara ili kuzalisha tani 28,000 ambazo watawauzia kwa bei ya Shilingi 750 kwa kilo.

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022 uzalishaji wa mbegu za mafuta umefikia tani 1,713,178 ikilinganishwa na tani 1,583,669 mwaka 2020/2021. Mwenendo wa uzalishaji wa mazao ya mbegu za mafuta ni kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 17.

Jedwali Na. 17: Mwenendo wa Uzalishaji wa Mbegu za Mafuta (Tani) Mwaka 2017-2021.

Zao20172018201920202021
Alizeti  352,902543,261561,297649,437478,900
Karanga 216,167370,356376,520631,465895,219
Ufuta  56,846133,704227,821228,920236,162
Mawese  42,27740,50042,17642,38758,791
Soya  6,13521,32122,95331,46044,106
Jumla 674,3271,109,1421,230,7671,583,6691,713,178

Chanzo: Wizara ya Kilimo

4.2.7.4. Mazao ya Bustani

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, uzalishaji wa mazao ya bustani umefikia tani 7,304,722.5 ikilinganishwa na tani 7,560,010.7 mwaka 2020/2021, sawa na upungufu wa asilima 3.4 (Jedwali Na. 18).

Upungufu huo umesababishwa na athari za UVIKO 19 ambapo usafirishaji wa mazao hayo nje ya nchi uliathirika.  Aidha, uzalishaji wa viungo umepungua kutokana na mashambulizi ya magonjwa ya mimea katika maeneo ya uzalishaji hususan Wilaya ya Muheza.  

Jedwali Na. 18: Mwenendo wa Uzalishaji wa mazao ya Bustani

Zao20172018201920202021
Matunda5,243,3433,703,1244,576,9485,582,117.35,199,312**
Mboga1,298,3881,595,4891,926,9271,852,6762,011,684
Maua11,61512,62213,2401,709.51,337.5
Viungo22,06222,06280,748.2123,507.992,389
Jumla6,575,4085,333,2976,597,863.27,560,010.77,304,722.5

** Uzalishaji unaendelea Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Kituo cha Utafiti wa Mboga, Matunda, Viungo na Vikolezo (spices and herbs) Duniani (World Vegetable Centre) imefanya tathmini ya kutambua mashamba ya miti mizazi kwa ajili ya uzalishaji wa miche bora ya matunda na upatikanaji wa vikonyo katika Mkoa wa Tanga. 
  1. Mheshimiwa Spika, tathmini hiyo ilitambua mashamba 11 katika Halmashauri za Wilaya za Lushoto, Muheza, Bumbuli na Korogwe. Mashamba hayo ni Jagetal, Malindi mnadani, Songa, Kizugu, Zigi, Rangwi Mission, Muller farm, Maunchle’s farm, Sakharani farm, Omary Shebughe farm na Mbwambo farm. 
  1. Vilevile, mashamba manne (4) ambayo ni HORTI Tengeru, World Vegeteble Centre, Usa River na Shamba la kwa Bwana Mdogo yalitambuliwa katika mkoa wa Arusha. Mashamba hayo yanatoa vikonyo vya parachichi, makadamia, miembe, mdalasini, tofaa, michungwa, milimao, ndimu, michenza, mulberry na persmon (Madagascar nut). Pia, TARI imesafisha na kuzalisha kilo 30 za mbegu bora ya nyanya aina za Tengeru 97 na Tanya ambazo zilipoteza sifa zake. 
  1. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TOSCI imeandaa rasimu ya viwango vya ubora wa kuzalisha miche ya mazao ya parachichi, maembe, matofaa, zabibu, migomba, chai, kakao, kahawa, chikichi, korosho, papai, machungwa na pingili za miwa. 
  1. Aidha, Wizara imeanzisha majukwaa mawili (2) ya wadau wa zao la parachichi katika mikoa ya Mbeya na Njombe na itaendelea kuanzisha majukuwa hayo katika mikoa mingine. Lengo la kuanzisha majukwaa hayo ni kuwasaidia wakulima kupata taarifa za masoko, bei za mazao, upatikanaji wa huduma za pembejeo na huduma za ugani. Vilevile, Serikali imefuta tozo 114 zilizokuwa kero katika mazao ikiwemo zao la parachichi kwa lengo la kupunguza gharama za uzalishaji na kuvutia uwekezaji na biashara katika sekta ya mazao.

4.2.8. Uanzishaji wa Mashamba Makubwa ya Kilimo

  1. Mheshimiwa Spika, kufuatia ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika mataifa mbalimbali duniani, Wizara imepokea wawekezaji wenye nia ya kuwekeza kwenye mashamba makubwa yatakayohusisha wakulima wadogo wa mazao ya alizeti, ngano, mpunga, mahindi ya njano, soya, chikichi, zabibu na miwa.
  • Ili kufanikisha uwekezaji huo, Wizara imetambua jumla ya hekta 178,000 kwa ajili ya uanzishaji wa mashamba makubwa katika mikoa tisa (9). Vilevile,Wizara inaendelea kushirikiana na uongozi wa mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa, Pwani, Kigoma, Tabora, Dodoma na Katavi ili kutambua maeneo yanayofaa kwa uwekezaji wa mashamba makubwa kwa ajili ya uwekezaji wa mazao hayo.

4.2.9. Kuimarisha Miundombinu ya Kuhifadhi

Mazao ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kukarabati na kujenga ghala katika maeneo mbalimbali nchini. Wizara kupitia CPB imekamilisha ukarabati wa ghala la Kiteto Mkoani Manyara (tani 1,000); Mbugani Mkoani Dodoma (tani 30,000) na vihenge Mkoani Arusha (tani 38,000). Jumla ya Shilingi 700,000,000 zimetumika kukamilisha ukarabati wa ghala na vihenge hivyo. Aidha, hadi Aprili, 2022 ukarabati wa ghala tisa (9) katika Halmashauri za Wilaya za Songea na Madaba umefikia hatua mbalimbali kama ifutavyo: Songea DC – Mkongotema (89.5), Muungano Zomba (64.74), Litisha (48.67), Magagura (55.09), Lipaya (21.58); Madaba DC – Hagangadinda (57.8), Matetereka (45.13) Lilondo B (83.5) na Gumbiro (96.28). Ukarabati huo unahusisha sakafu, kuta, paa, vyoo na kuweka mfumo wa maji na unategemewa kukamilika mwezi Juni.  
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (World Food Programme-WFP) imekarabati ghala tisa (9) zenye uwezo wa kuhifadhi tani 2,700 katika mikoa ya Dodoma na Kigoma na kujenga ghala moja (1) lenye uwezo wa kuhifadhi tani 500 katika Mkoa wa Kigoma.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia NFRA imeendelea kutekeleza Mradi wa Kuongeza Uwezo wa Kuhifadhi. Hadi Aprili, 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 90.64 ambapo ujenzi wa vihenge umefikia asilimia 83.40 na ujenzi wa ghala na miundombinu mingine umefikia asilimia 66.5. Kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu hiyo kutaongeza uwezo wa Wakala wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 251,000 hadi 501,000. Mradi huo unagharimu Dola za Marekani 55.
  • Vilevile, ujenzi wa ghala 14 kupitia mradi wa TANIPAC umefikia wastani wa asilimia 60 (Jedwali Na. 19). Ghala hizo zitakapokamilika zitakuwa na uwezo wa kuhifadhi tani 21,500 za mazao, ujenzi wa ghala hazo unagharimu Shilingi 14,435,047,507.24.

Jedwali Na. 19: Ujenzi wa maghala ya 14 kupitia TANIPAC

Na.GhalaHatua       za Ujenzi (%)Uwezo (Tani)
1Nyakitonto – Kasulu462,000
2Kagezi – Kibondo451,500
3Msangila – Bukombe651,500
4Nyakasungwa – Buchosa531,500
5Ikindiro – Itilima431,500
6Busondo – Nzega901,000
7Mrijo-Chini – Chemba751,500
8Endanoga – Babati432,000
9Mangaka – Nanyumbu781,000
10Lumecha – Namtumbo222,000
11Kizimbani – Unguja551,500
12Ole Dodeani – Pemba431,000
13Chakwale – Gairo481,500
14Engusero – Kiteto162,000
 Wastani wa Utekelezaji6021,500

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

4.2.10. Uongezaji Thamani wa Mazao ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo ili kupunguza upotevu wa mazao na kuimarisha upatikanaji wa bidhaa za mazao ya kilimo pamoja na upatikanaji wa masoko. Katika mwaka 2021/2022, Wizara kupitia CPB imeongeza thamani ya mazao ya nafaka tani 4,089.96. Kati ya hizo mahindi ni tani 2,990.26 ambazo zimezalisha unga tani 2,242.695  na pumba tani  747.565 na alizeti ni tani 1,099.70 ambazo zimezalisha mafuta lita 307.916.
  • Mheshimiwa Spika, CPB imekamilisha usimikaji wa mitambo ya kiwanda cha kusindika mpunga kilichopo Mkoa wa Mwanza chenye uwezo wa kusindika tani 28,800 kwa mwaka. Vilevile, CPB imezalisha tani 4.72 za bidhaa zitokanazo na korosho (Roasted cashew kernels, White cashew kernels na Cashew apple wine) ambazo zimekidhi viwango vya kimataifa na usindikaji unaendelea.
  • Kadhalika, Wizara imetathmini uendeshaji na usimamizi wa viwanda vikubwa, vya kati na vidogo vinavyoongeza thamani ya zao la alizeti katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Tathmini hiyo imebaini kuwa viwanda vinafanyakazi chini ya uwezo wake wa kusindika kutokana na upungufu wa malighafi ya zao la alizeti. Mfano, viwanda vilivyopo Dodoma vinajitosheleza kwa wastani wa asilimia 55, Singida asilimia 60 na Manyara asilimia 30. Ili kukabiliana na changamoto hiyo, Wizara imeendelea kuhamasisha uzalishaji wa alizeti nchini.

Kiwanda cha kusindika unga na mafuta ya kula cha Bodi ya

Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) cha Jijini Dodoma

4.2.11. Maendeleo ya Ushirika

  • Mheshimiwa Spika, Tume ya Maendeleo ya Ushirika imetoa mafunzo ya biashara na masoko kwa watendaji na viongozi wakuu wa Vyama Vikuu vya Ushirika 156. Vilevile, Vyama vya Ushirika wa Kilimo na Masoko (AMCOS) vimeendelea  kukusanya na kuuza mazao na kusambaza pembejeo kwa wakulima ambapo hadi April, 2022 tani  597,298.58 za mazao yenye thamani ya Shilingi 1,552,635,769,446 ziliuzwa kupitia vyama vya ushirika na baadhi kwa kutumia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (Jedwali Na. 20).

Jedwali Na. 20: Mazao yaliyouzwa kupitia vyama vya Ushirika

Na.ZAOKIASI (TANI)THAMANI (TSHS)
1Pamba 144,792202,989,430,000
2Korosho 231,102.92488,986,356,596
3Mkonge4,934.8318,784,149,883
4Kakao4,592.7822,929,163,568
5Ufuta81,447.04195,355,744,626
6Mbaazi 3,013.543,938,150,669
7Soya1,090.201,611,939,457
8Kahawa59,278.15410,522,544,767
9Tumbaku57,367.19204,420,711,000
10.Chai9,679.933,097,578,880
 Jumla597,298.581,552,635,769,446

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

  • Mheshimiwa Spika, Tume imeendelea kuratibu usambazaji wa pembejeo za mazao ya pamba, tumbaku na korosho ambapo katika mwaka 2021/2022 pembejeo zenye thamani ya Shilingi 178,844,086,527.4zimenunuliwa na kusambazwa kwa wakulima kupitia AMCOS

(Jedwali Na. 21).  

Jedwali Na.  21: Pembejeo zilizosambazwa na Vyama vya

Ushirika 

Na.Aina        ya PembejeoKipimoKiasiThamani (Tsh)
1Mbolea Tani34,391.8063,047,095,742.4
2Mbegu Tani21,104.2417,415,820,097
3ViuatilifuTani13,561.67517,195,877,000
Lita1,452,24841,585,952,000
Tani45.1574,242,000
Ekapacks8,639,30938,876,890,588
4.VinyunyiziPc121133,100,000
5.VifungashioPc2,928,98515,108,876, 224
 Jumla  178,844,086,527.4

Chanzo: Wizara ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha usimamizi na ukaguzi wa vyama vya ushirika nchini, Wizara kupitia Tume imenunua magari 15, pikipiki 137 na kompyuta 82 ambapo jumla ya Shilingi 1,792,300,000 zimetumika kununua vifaa hivyo. Aidha, Tume imetoa mafunzo ya ukaguzi na usimamizi wa vyama vya ushirika kwa maafisa ushirika 170 kutoka mikoa 13 ya Mwanza, Tabora, Shinyanga, Geita, Mara, Kigoma, Kagera, Simiyu, Iringa, Njombe, Mtwara, Ruvuma na Lindi.  
  • Mheshimiwa Spika, Tume imeunda Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika ambao unafanyiwa majaribio katika mikoa ya Mbeya na Iringa. Lengo la Mfumo huo ni kuwa na kanzidata ya Vyama vya Ushirika na wanaushirika nchini; kusimamia utendaji wa Vyama vya Ushirika; kufuatilia ukusanyaji, uuzaji wa mazao na malipo kwa mkulima. Pia, mfumo huo utamrahisishia mkulima na mwanaushirika kupata taarifa sahihi za uwekezaji na kwa wakati wa Vyama vya Ushirika, mikopo ya pembejeo na marejesho ya mkopo kwa mkulima, bei na malipo ya mazao ya mkulima kupitia simu ya mkononi. Baada ya majaribio kukamilika mfumo huo utasambazwa nchi nzima na kuanza kutumika.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Ushirika na kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamni (Registration Insolvency and Trusteeship Agency – RITA), Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (Moshi Cooperative University – MoCU), COASCO, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (Tanzania Investiment Centre – TIC) na Bodi ya

Chai Tanzania imeandaa Miongozo 11 itakayotumika katika kusimamia Vyama vya Ushirika nchini. Miongozo hiyo inahusu maeneo ya ufilisi, uwekezaji na usajili wa rehani, utatuzi wa migogoro, ukaguzi wa vyama vya ushirika visivyo vya kifedha, ukaguzi wa vyama vya ushirika vya kifedha, udhibiti wa majanga, uwekezaji, ununuzi kwenye vyama vya ushirika, uanzishaji na uendeshaji wa mifuko ya pembejeo na usimamizi wa AMCOS za miwa nchini. 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume imeendelea kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika nchini katika sekta za kiuchumi zikiwemo uvuvi, mifugo, huduma na kilimo kwa lengo la kuimarisha mitaji ya wanachama, masoko ya mazao na kupata pembejeo kwa bei nafuu na kwa wakati.  
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara kupitia Tume imeratibu uanzishwaji wa Benki ya Taifa ya Ushirika ambayo itamilikiwa na vyama vya ushirika kwa asilimia 51 na taasisi na watu binafsi watamiliki asilimia 49. Lengo la kuanzishwa Benki hiyo ni kurahisisha upatikanaji wa mitaji kwa wanachama. Benki hiyo inatarajiwa kuzinduliwa itakapokidhi kigezo cha kuwa na mtaji wa Shilingi Bilioni 15. Tume inaendelea kuhamasisha vyama vya ushirika na wadau wengine kununua hisa katika Benki hiyo.
  • Mheshimiwa Spika, kutokana na Serikali kuweka kipaumbele cha kuimarisha huduma za ugani, Tume imehamasisha vyama vya ushirika kuajiri Maafisa ugani kwa ajili ya kutoa ushauri wa kitaalam kwa wakulima ili kuongeza tija katika kilimo. Hadi Aprili, 2022 maafisa ugani 76 waliajiriwa na Vyama vikuu vya Ushirika vya KCU Ltd, KDCU Ltd, KACU Ltd, MAMCU Ltd, TANECU Ltd na KNCU Ltd. Aidha, ajira katika vyama vya ushirika  zimeongezeka kutoka  100,100 mwaka 2020/2021 hadi 146,555 mwaka 2021/2022. Kati ya ajira zilizopatikana, za kudumu ni 31,819, za mkataba ni 28,990 na za msimu ni 85,746.
  • Vilevile, Tume imehamasisha vyama vya ushirika kuanzisha na kufufua viwanda vinavyomilikiwa na vyama hivyo ili kuongeza thamani ya mazao. Aidha, Tume imeendelea kuhamasisha Vyama Vikuu vya Ushirika kuanzisha kampuni ambapo hadi Aprili 2022, Vyama Vikuu vya Karagwe District Cooperative Union – KDCU, Kahama Cooperative Union – KACU, Chato Cooperative Union – CCU na Umoja Liwale vimeanzisha kampuni kwa ajili ya biashara za mazao.

4.2.11.1. Ushiriki wa Vijana katika Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuratibu utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Kushirikisha Vijana kwenye Kilimo Awamu ya

Kwanza (National Strategy for Youth Involvments in Agriculture – 2016-2021). Katika mwaka 2021/2022 Wizara kwa kushirikiana na Ushirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperatives – SUGECO), CUSO International  na UNDP inatekeleza mfumo wa kilimo biashara wa Kizimba Business Model kwenye eneo la ekari 1,500 katika kijiji cha Wami Luhindo Wilaya ya Mvomero ambalo limeandaliwa kwa ajili ya uzalishaji wa mazao ya bustani. Katika eneo hilo, barabara zenye urefu wa kilomita 10 zimefunguliwa na usafishaji wa shamba umefanyika katika ekari 300.

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Shirika la Kimataifa la Heifer imetoa mafunzo kuhusu ujasiriamali, usimamizi wa biashara na fedha, usalama wa chakula na kilimo biashara katika mnyororo wa thamani wa mazao ya kilimo kwa vijana 2,939. Vilevile, Wizara imetoa mafunzo kuhusu uongozi bora, utunzaji wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu na ushirikiano na wadau na utafutaji wa masoko kwa viongozi wa kamati ndogo ya Vyama vya Ushirika wa Vijana 103 kutoka AMCOS tano (5) ili kuongeza ufanisi. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (Small Industries Development Organisation – SIDO) na SUGECO imefanikiwa kuboresha biashara za vijana 1,930 katika mnyororo wa thamani wa mazao kupitia Mpango wa uatamizi wa biashara za vijana (Youth Business Incubation Program) unaoratibiwa na AMCOS za vijana.
  • Mheshimiwa Spika, mfuko maalum wa mikopo unaosimamiwa na Heifer International na Benki ya  MUCOBA umetoa mikopo ya riba nafuu yenye thamani ya Shilingi 69,899,999 kwa vijana 64 katika mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa. Vilevile, vikundi 39 vya vijana kutoka katika mikoa hiyo, vimewezeshwa kupata mikopo yenye thamani ya Shilingi 168,584,988 kutoka katika mifuko ya Youth Development Fund (YDF), SIDO, Equity Bank na Vision Fund Tanzania. Mikopo hiyo, imetolewa kwa ajili ya kuwawezesha vijana kuwekeza katika mnyororo wa thamani wa mazao ya kilimo. Aidha, mafunzo na mikopo iliyotolewa na Shirika la Heifer, imewezesha vijana 5,266 kujiajiri katika kilimo.  
  • Mheshimiwa Spika,  Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Rikolto imewajengea uwezo vijana 571 wa mikoa ya Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa na Katavi kuhusu uzalishaji wa mboga na matunda. Pia, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kilimo Endelevu (SAT) imetoa mafunzo kwa vijana 3,309 kuhusu kilimo ikolojia, ujasiriamali, uongezaji thamani wa mazao ya kilimo, matumizi ya TEHAMA pamoja na kuweka akiba kwa ajili ya kupata mitaji midogo ya kuwekeza kwenye kilimo katika Wilaya ya Mvomero. 

4.2.11.2. Uhifadhi wa Mazingira 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha utunzaji wa mazingira kwa kuzingatia matumizi ya teknolojia na mbinu za kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi ikiwemo kilimo hifadhi, kilimo hai, kilimo mseto na kilimo misitu.  Katika mwaka 2021/2022,Wizara kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo na Sekta Binafsi inaandaa Mkakati wa Kitaifa wa Kilimo Ikolojia Hai ambao utatekelezwa kwa miaka kumi kuanzia mwaka 2022 hadi mwaka 2032. Mkakati huo utatoa dira na mwongozo wa shughuli za kilimo ikolojia nchini. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa mafunzo ya kuhifadhi mazingira kwa wakulima 375 na kutengeneza mipango ya uhifadhi wa mazingira na jamii katika vijiji 15 vya Wilaya ya Karatu. Pia, Wizara imesambaza Mwongozo wa Kilimo Kinachohimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa maafisa ugani 15 wa Halmashauri za Wilaya za Kondoa, Chamwino, Chemba, Mpwapwa na Bahi. Mwongozo huo umesaidia kuelimisha jamii katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yao. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na Asasi zisizo za Kiserikali zinazojihusisha  na kuendeleza Kilimo Hifadhi imetoa mafunzo  kuhusu kilimo hifadhi kwa wakulima viongozi (Training of Trainers – ToT) 160 katika Halmashauri za Wilaya 25 za Mbeya, Bahi, Manyoni, Chamwino, Kakonko, Sengerema, Buchosa, Kwimba, Chato, Geita, Maswa, Itilima, Busega, Serengeti, Bunda, Tarime, Butiama, Arumeru, Monduli, Same, Moshi, Kilolo, Wanging’ombe na Mbeya Jiji. Mafunzo hayo yamewezesha wakulima katika maeneo hayo kuanza kulima kilimo hifadhi. 
  • Vilevile, Wizara kupitia Mradi wa Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mfumo wa Ikolojia Vijijini (Ecosystem Based Adaptation for Rural Resilience – EBARR) imewezesha uanzishwaji wa shamba darasa  moja (1)  katika Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kwa ajili ya kufundishia mbinu na teknolojia za kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi kwa zao la maharage.  
  • Mheshimiwa Spika, mradi huo umewezesha uanzishwaji wa kitalu cha mkonge chenye ukubwa wa ekari 20 katika Wilaya ya Kishapu na uchimbaji wa mfereji mkuu wenye mita 2,700 katika skimu ya umwagiliaji ya Lukenge Wilaya ya Mvomero ambao ujenzi wake umefikia asilimia 40. Pia, Mradi umewezesha uchimbaji wa visima sita (6) vilivyopo katika wilaya za Mpwapwa (3), Mvomero  (2) na Simanjiro

(1).   

4.2.11.3. Lishe

  • Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto za lishe duni hapa nchini, Wizara imeendelea kutekeleza Mpango Jumuishi wa Taifa wa Utekelezaji wa Masuala ya Lishe (National

Multisectorial Nutrition Action Plan-NMNAP) kupitia

Nutrition Sensitive Agriculture Action  Plan – NSAAP. Katika mwaka 2021/2022 Wizara kupitia, TARI kwa kushirikiana na Project Concern International – PCI imezindua mpango wa lishe mashuleni kwa kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu kilimo bora cha maharage na umuhimu wa maharage lishe. Katika kufanikisha hilo, TARI imetoa mbegu za maharage lishe katika shule za mikoa 11 ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Singida, Mara, Kagera, Iringa, Njombe, songwe, Mbeya na Geita. 

  • Vilevile, TARI imeendelea kutoa mafunzo ya usindikaji kwa wasindikaji wa bidhaa za maharage lishe wa Mkoa wa Arusha na kuwaunganisha na TBS ili waweze kupata alama ya ubora.
  • Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na matatizo ya lishe nchini hususan upungufu wa damu na udumavu kwa watoto, wajawazito na wanaonyonyesha, TARI imepima viwango vya virutubisho katika bidhaa ya unga yenye mchanganyiko wa mahindi na maharagwe lishe. Matokeo ya vipimo hivyo yameonesha kuwa bidhaa hiyo inakidhi viwango vya ubora kwa kiasi cha protini asilimia 20-28, nyuzinyuzi asilimia 56, nishati lishe asilimia 32, madini chuma 70mg/kg na madini ya zinki 33mg/kg. Kutokana na ubora wa bidhaa hiyo, TARI imeendelea kuzalisha na kusambaza bidhaa hiyo kwa walaji ambapo hadi, Aprili 2022 kilo 540 za unga lishe zimezalishwa na kusambazwa.
  • Mheshimiwa Spika, TARI imegundua aina tatu za mbegu ya mchicha (TARI AMAR1, TARIAMAR2 na TARI-AMAR3) zenye viini lishe vya protini, na madini chuma kwa wingi. Aidha, TARI imeendelea kuhamasisha matumizi ya mchicha lishe aina ya Akeri wenye protini kwa wingi  kwa kutoa mafunzo kwa wakulima na wasindikaji 1,000 na kuanzisha mashamba darasa saba (7) katika mikoa ya Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Arusha, Mwanza,  Dar es salaam na Pwani. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya teknolojia za uzalishaji wa chakula, uhifadhi bora na usindikaji wa mazao ya kilimo kupitia Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani kwa wananchi wa Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro. Vilevile, uhamasishaji wa ulaji unaofaa kwa jamii ya kitanzania ili kukabiliana na changamoto za lishe hapa nchini ulifanyika kupitia maonesho hayo. Aidha,  wataalam walitoa mafunzo  kwa vitendo kwa wananchi 1,500 kuhusu mapishi ya vyakula vya asili kwa ajili ya makundi mbalimbali katika jamii kwa kuzingatia mlo kamili na elimu kwa akina mama kuhusu makuzi, malezi na ufuatiliaji wa ukuaji na maendeleo ya mtoto.
  • Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na matatizo ya lishe nchini hususan upungufu wa damu na udumavu kwa watoto, wajawazito na wanaonyonyesha, TARI imepima viwango vya virutubisho katika bidhaa ya unga yenye mchanganyiko wa mahindi na maharagwe lishe. Matokeo ya vipimo hivyo yameonesha kuwa bidhaa hiyo inakidhi viwango vya ubora kwa kiasi cha protini asilimia 20-28, nyuzinyuzi asilimia 56, nishati lishe asilimia 32, madini chuma 70mg/kg na madini ya zinki 33mg/kg. Kutokana na ubora wa bidhaa hiyo, TARI imeendelea kuzalisha na kusambaza bidhaa hiyo kwa walaji ambapo hadi, Aprili 2022 kilo 540 za unga lishe zimezalishwa na kusambazwa kwa walaji.

Mchicha aina ya TARI AMAR1 uliogunduliwa na Taasisi ya Utafiti wa Mazao ya Kilimo (TARI- Tengeru) ya mkoani Arusha

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya teknolojia za uzalishaji wa chakula, uhifadhi bora na usindikaji wa mazao ya kilimo kupitia Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani kwa wananchi. Vilevile, uhamasishaji wa ulaji unaofaa kwa jamii ya kitanzania ili kukabiliana na changamoto za lishe hapa nchini ulifanyika kupitia maonesho hayo. Aidha,  wataalam walitoa mafunzo  kwa vitendo kwa wananchi 1,500 kuhusu mapishi ya vyakula vya asili kwa ajili ya makundi mbalimbali katika jamii kwa kuzingatia mlo kamili na elimu kwa akina mama kuhusu makuzi, malezi na ufuatiliaji wa ukuaji na maendeleo ya mtoto. 

4.2.11.4. Jinsia

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara imeendelea kuzingatia masuala ya jinsia katika utekelezaji wa Sera, Programu na Miradi mbalimbali ambapo rasimu ya Mwongozo Jumuishi wa Masuala ya Jinsia katika Kilimo (Guideline for Gender Mainstreaming in Agriculture) imeandaliwa.  Lengo la mwongozo huo ni kuweka mazingira wezeshi kwa jinsia zote kushiriki kikamilifu katika mnyororo wa thamani wa kilimo nchini. 
  • Mheshimiwa     Spika,       Wizara        kwa

kushirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania – (Tanzania Gender Networking Program-TGNP) imetoa mafunzo kwa watumishi kumi (10) wa Wizara kuhusu ujumuishwaji wa masuala ya jinsia katika Sera, Bajeti na Mipango ya Serikali kwenye Mikakati, Programu na  Miradi. 

4.2.11.5. VVU na UKIMWI  

235. Mheshimiwa Spika, Wizara imetoa elimu mahala pa kazi kuhusu maambukizi ya VVU na UKIMWI pamoja na magonjwa yasiyoambukiza kwa watumishi 473 ambapo kati ya hao, watumishi 123 walipima kwa hiari. Aidha, Wizara inaendelea kuhudumia watumishi nane (8) wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kuwapatia dawa pamoja na chakula lishe kila mwezi. Pia, Wizara inaendelea kutoa vifaa kinga ambapo hadi Aprili, 2022 kondomu 1,088,800 na kondomu dispensa 438 zimenunuliwa na kusambazwa katika  Ofisi za Wizara na Taasisi zake.

5. MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo inawasilisha bajeti mbele yako wakati dunia inaendelea kupitia changamoto kubwa ya vita kati ya Ukraine na Urusi pamoja na athari za UVIKO19. Changamoto hizo zimeleta mabadiliko ya mifumo ya kiuchumi na kwa kipekee mifumo ya uzalishaji na usambazaji wa mbolea duniani na biashara ya mazao ya kilimo. 
  • Kufuatia hali hiyo, bei ya mbolea imepanda kwa wastani wa zaidi ya asilimia 100. Mfano, DAP imepanda kwa Dola  za Marekani 396 kwa tani mwaka 2019 hadi Dola za Marekani 948 kwa tani mwaka 2022, Urea kutoka Dola za Marekani 249 kwa tani hadi Dola za Marekani 723 kwa tani, CAN imepanda kutoka Dola za Marekani 210 kwa tani hadi Dola za Marekani 520 kwa tani na SA kutoka Dola za Marekani 128 kwa tani hadi Dola za Marekani 403 kwa tani. 
  • Vilevile, bei ya mafuta ya kula duniani imepanda kutoka Dola za Marekani 1,631 Machi 2021 hadi Dola za Marekani 2,250 katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 38. Vilevile, bei ya ngano imepanda kutoka Dola za Marekani 178.24 kwa tani mwaka 2020 hadi Dola za Marekeni 294.03 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 65. Hali hiyo imesababisha nchi kukabiliwa na mfumuko wa bei unaoingia nchini kutokana na bidhaa zinazoagizwa kutoka nje ya nchi hali inayoathiri ustawi wa wananchi. Aidha, athari za UVIKO-19 na mgogoro unaoendelea kati ya Ukraine na Urusi kutokana na tafiti mbalimbali za kimataifa utaathiri mifumo ya uzalishaji na usambazaji wa bidhaa mbalimbali.
  • Mheshimiwa Spika, Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2022/2023 inalenga kujenga msingi imara wa ukuaji wa sekta ya kilimo kwa kiwango cha asilimia 10 ifikapo 2030 pamoja na kukabilina na athari za majanga ya kiuchumi na kijamii ikiwemo UVIKO 19 na vita ya Ukraine na Urusi, kulinda sekta na kupunguza matumizi ya fedha za kigeni katika uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi. Wizara inachukua hatua hizo kwa kuzingatia kuwa Sekta ya Kilimo (mazao) ni mwajiri mkuu wa nguvukazi ya Taifa na mchangiaji mkuu katika Pato la Taifa.
  • Mheshimiwa Spika, kiwango  cha ukuaji wa Sekta ya Kilimo kwa asilimia 10 kitachangia kupunguza umasikini kwa asilimia 50. Azma hiyo utaongozwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa (2025); Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano Awamu ya Tatu (2021/2022 – 2025/2026); Sera ya Taifa ya Kilimo ya mwaka 2013; Mwongozo na Mpango wa Bajeti wa mwaka 2022/2023; Ilani ya

Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 20202025; na Hotuba ya Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipolihutubia Bunge lako Tukufu tarehe 22 Aprili, 2021.  

  • Mheshimiwa Spika, Aidha, mpango umezingatia Malengo Endelevu ya Maendeleo 2030 (SDGs); masuala mtambuka ya jinsia, mazingira, lishe, mabadiliko ya tabianchi, vijana, kutokomeza ajira kwa watoto katika sekta ya kilimo, VVU na UKIMWI. 
  • Mheshimiwa Spika, ili kufikia lengo la ukuaji wa Sekta ya Kilimo kwa asilimia 10 ifikapo 2030, Bajeti ya mwaka 2022/2023 ni msingi muhimu kufikia lengo kuu hilo. Aidha, ili kufikia lengo hilo Wizara imejiwekea malengo yafuatayo:
  1. Kujitosheleza kwa mahitaji ya chakula ndani ya nchi na kuuza nje ya nchi. Pia kufanya mwelekeo wa uzalishaji wa mazao ya chakula kuwa wa kibiashara;
    1. Thamani ya mauzo ya mazao nje ya nchi kuongezeka kutoka Dola za Marekani Bilioni 1.2 hadi Dola za Marekani Bilioni 5 ifikapo mwaka 2030;
    1. Kuongeza idadi ya mashamba makubwa (Block farms/Commercial farms) kutoka 110 mwaka 2020 hadi 10,000 mwaka 2030;
    1. Kuongeza eneo la umwagiliaji kufikia hekta 8,500,000 sawa na asilimia 50 ya eneo lote linalolimwa nchini ifikapo 2030 ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kupitia kilimo cha umwagiliaji kutoka asilimia 10 hadi asilimia 50;
    1. Kutengeneza ajira za vijana na wanawake katika sekta ya kilimo zitakazofikia milioni 1 ifikapo mwaka 2025; 
    1. Kuhakikisha upatikanaji wa malighafi kwenye viwanda vya kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za kilimo kufikia asilimia

100 ifikapo 2030;  vii. Kuongeza upatikanaji wa mitaji na mikopo kutoka kwenye Sekta ya Fedha kutoka asilimia tisa (9) mwaka 2022 hadi asilimia

30 ifikapo mwaka 2030; viii. Kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kutoka asilimia 35 hadi asilimia tano (5) ifikapo mwaka 2030;

  1. Kuondoa upungufu wa mafuta ya kula na kulifanya zao la alizeti kuwa moja ya mazao yatakayozalishwa kutosheleza mahitaji ya ndani na mauzo nje ya nchi. Vilevile, kuwekeza katika mashamba makubwa ya chikichi na kuondoa mfumo wa kilimo cha chikichi kwa mashamba madogo chini ya

ekari moja (1);

  • Kuongeza mauzo ya Mazao ya Bustani (Horticulture) kutoka Dola za Marekani Milioni 750 kwa mwaka kufikia Dola za

Marekani Bilioni 2 mwaka 2030;  xi. Kujitosheleza kwa uzalishaji wa mbolea ndani ya nchi na kuvipa vipaumbele viwanda vya ndani vya mbolea na matumizi ya chokaa ili kupunguza gharama za uzalishaji; na

xii. Kujitosheleza kwa mahitaji ya mbegu bora na kuuza mbegu nje ya nchi kupitia ushirikishaji wa Sekta Binafsi.

  • Mheshimiwa Spika, matokeo yanayotarajiwa kutokana na utekelezaji wa malengo hayo siyo ya muda mfupi, bali yanajenga misingi ya kuwa na matokeo yatakayohakikisha mwendelezo wa ukuaji wa sekta ya kilimo kwa muda mrefu, ukuaji wa pato la Taifa, ajira, mapato ya fedha za kigeni, malighafi za viwanda na kujihakikishia usalama wa chakula nchini na kuuza ziada nje ya nchi. 
  • Mheshimiwa Spika, takwimu zinaonesha kuwa ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu duniani itafikia Bilioni 9.7 na Bilioni 8.5 ifikapo mwaka 2030. Afrika itafikia Bilioni 2.4 mwaka 2050 na Bilioni 1.6 mwaka 2030.  Vilevile, ifikapo mwaka

2050, Tanzania itakuwa na idadi ya watu milioni 135 na milioni 79 mwaka 2030 ambapo mahitaji ya chakula nchini yatafikia tani Milioni 18.8. Wakati huo huo mahitaji ya chakula Duniani yataongezeka kwa wastani wa asilimia 50. (FAO, 2018).  

  • Athari za mazingira zitashusha uzalishaji wa mashambani kwa asilimia nne (4). Hii ni fursa kwa atakayejiandaa na ni majanga kwa ambaye hatajiandaa hivyo matumizi ya teknolojia na uwekezaji kwenye tekenolojia ndiyo mwarobaini pekee utakaotatua hatari hii.
  • Aidha, biashara ya chakula katika soko la Afrika itafikia Dola za Marekani Trilioni 1 ifikapo mwaka 2030 hii itafungua fursa za ajira kwenye mnyororo wa thamani. Kutokana na ongezeko hilo la idadi ya watu duniani, kama Taifa lazima tujiandae sasa, ili kufaidika na fursa hiyo ya kibiashara na kujihakikishia usalama wa chakula na ukuaji endelevu wa uchumi wetu na kulifanya Taifa kuwa huru.
  • Mheshimiwa Spika, ifikapo mwaka 2030, mahitaji ya chakula yanatarajiwa kufikia tani 18,797,476 yakiwemo mahindi tani 7,417,540, mchele tani 1,368,144 na muhogo tani 3,211,432. Kutokana na ongezeko hilo la idadi ya watu duniani, kama Taifa lazima tujiandae ili kufaidika na fursa hiyo ya kibiashara na kujihakikishia usalama wa chakula na ukuaji endelevu wa uchumi.  
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara imepanga kutekeleza maeneo ya kipaumbele yafuatayo ili kufikia malengo tajwa:- 
  • Kuimarisha utafiti, 
  • Kutoa ruzuku ya mbegu za alizeti, ngano na miche ya chikichi,
  • Kuimarisha upatikanaji wa pembejeo za

kilimo, 

  1. Kuimarisha na kutoa huduma ya upimaji wa afya ya udongo ili kuwezesha wakulima kutambua aina na kiwango cha mbolea kinachohitajika katika mashamba yao;
  2. Kuendeleza kilimo cha umwagiliaji kwa kujenga miundombinu ya umwagiliaji ikiwemo ujenzi wa mabwawa ya kuvunia maji ya mvua;
  3. Kuimarisha huduma za ugani na kuhamasisha  kilimo cha ukanda kutokana na Ikolojia za kilimo (Tanzania Agricultural

Growth Corridor); vii. Kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao ya kilimo; 

viii. Kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa Mitaji ikiwa ni pamoja na kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo utakaowezesha upatikanaji wa pembejeo kwa mfumo wa ruzuku pindi inapotokea athari za kiuchumi;  ix. Kuimarisha miundombinu ya kuhifadhi mazao ya kilimo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa ghala katika ngazi ya Kijiji, Kata na Tarafa ili kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna kutoka asilimia 35 hadi 5 ifikapo mwaka 2030;  

  • Kuhamasisha Kilimo cha Mashamba makubwa ikiwa ni pamoja na kuanzisha maeneo maalum ya mashamba makubwa, kwa kuyatengenezea miundombinu na kuwapatia wananchi kwa makubaliano maalum hususan kwa zao la chikichi;
  • Kuanza kutoa ruzuku ya mbolea mwaka

2022/2023;

  • Kuimarisha Kilimo Anga, na
  • Kuimarisha maendeleo ya ushirika. 

5.1. Kuimarisha Utafiti

  • Mheshimiwa Spika, mahitaji yetu kama nchi ya mbegu bora ni tani 652,250 na sasa tunazalisha tani 35,199. Ili kuondoa tatizo hilo, Wizara imeongeza bajeti ya utafiti na uzalishaji wa mbegu za msingi kutoka Shilingi Bilioni 11.63 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi Bilioni 40.73 mwaka 2022/2023 sawa na ongezeko la asilimia 250.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kuimarisha  upatikanaji wa mbegu bora kwa kuongeza uzalishaji wa mbegu za awali za mazao ya nafaka, mikunde na mbegu za mafuta kutoka tani 226.5 hadi tani 1,453  ambazo zitakidhi mahitaji ya ASA na kampuni binafsi kuzalisha mbegu zilizothibitishwa tani 452,650.  Pia, itaongeza uzalishaji wa mbegu za awali za pamba kufikia tani 17,000. 
  • Ili kufikia lengo hilo, Wizara itajenga miundombinu ya umwagiliaji katika eneo la hekta 914 kwenye vituo 15 vya utafiti wa kilimo.

Miundombinu itakayojengwa ni pamoja na mifereji, mabwawa (Ilonga na Tumbi), kuchimba visima, kununua irrigation centre/lateral pivot, kuchimba mitaro na kutandaza mabomba.

  • Mheshimiwa Spika, TARI itajenga maabara nne (4) za kuzalisha miche kwa njia ya chupa (tissue culture) katika vituo vya TARI Mlingano, TARI Maruku, TARI Dakawa na TARI Ukiriguru. Aidha, itakarabati maabara tatu (3) na kununua vifaa na vitendanishi (reagents) katika vituo vya TARI Tengeru, TARI Uyole na TARI Mlingano. Ujenzi na ukarabati wa maabara hizo utaongeza uzalishaji wa miche kutoka 5,131,835 hadi miche 33,500,000 kwa njia ya chupa. Vilevile, Wizara itaboresha maabara ya udongo katika kituo cha TARI Mlingano ili iweze kupata ithibati na itaimarisha maabara ya baoteknolojia iliyopo katika kituo cha TARI Mikocheni. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kuongeza upatikanaji wa mbegu kwa wakulima, TARI itakusanya na kusafisha mbegu za asili kwa ajili ya matumizi ya wakulima. Vilevile, mbegu hizo zitatumiwa na TARI kuzalisha mbegu za awali na kuwapatia ASA na Sekta Binafsi kuzalisha mbegu ili kutosheleza mahitaji ya mbegu. Aidha, itahifadhi mbegu hizo za asili kwa kutumia majina halisia, (germaplasm maintenance) katika vituo vya TARI kwa ajili ya kufanya utafiti na kuboresha. Utafiti wa mbegu unalenga zaidi katika kukidhi mahitaji ya soko na kilimo cha biashara kwa kushirikiana na viwanda na wafanyabiashara.
  • Mheshimiwa Spika, TARI itazalisha teknolojia mpya zenye sifa zaidi ya zile zinazotumiwa na soko hususan zinazostahimili ukame, magonjwa na wadudu, zinazotoa mavuno mengi na zenye viinilishe vingi, ikiwa ni pamoja na ugunduzi wa mbegu bora, kanuni bora za kilimo, ukinzani wa magonjwa, rutuba ya udongo, uchumi jamii na zana bora.
  • Vilevile, TARI itanunua magari manne (4), matrekta saba (7) na zana zake na mashine tatu (3) za kuchakata mbegu kwa vituo vya TARI Seliani, TARI Ilonga na TARI Uyole. Matreka yatawezesha kuongeza eneo la mashamba ya kuzalisha mbegu kutoka hekta 285 hadi hekta 914. Pia, TARI itajenga ghala nne (4) zenye uwezo wa kuhifadhi tani 550 kila moja katika vituo vya TARI Uyole, TARI Seliani, TARI Ilonga na TARI Kifyulilo. Ujenzi huo ukikamilika TARI itakuwa na uwezo wa kuhifadhi mbegu kutoka tani 20 hadi tani 1,650 kwa vituo hivyo.  
  • Mheshimiwa Spika, TARI itajenga vyumba vya ubaridi (cold rooms) katika vituo vya TARI Selian na TARI Ilonga ambavyo vitatumika kuhifadhi mbegu na nasaba (germplasm) mbalimbali za mazao. Hatua hiyo, itapunguza gharama za kupanda mashambani nasaba kila mwaka kama ilivyo kwa sasa kwa lengo la kutunza vizazi vya mimea kwa matumizi ya utafiti wa mbegu. 
  • Mheshimiwa Spika, ili kulinda mashamba ya uzalishaji na utafiti wa mbegu dhidi ya uvamizi wa wananchi unaotokana na  kutokuwepo kwa mipaka na uzio, Wizara kupitia TARI itajenga uzio kwa mashamba matatu (3) ya Suluti (Namtumbohekta 388), Milundikwa (Nkasi – hekta 1,000) na Ifakara (Kilombero – hekta 4,715). Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi itahakiki mipaka na kupima mashamba ya vituo vya utafiti wa mbegu vya TARI Seliani na TARI Ukiriguru (Mwanahala na

Bwanga) ili kupata hati miliki.

5.2. Kuimarisha Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo

5.2.1. Mbegu Bora

  • Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa mbegu bora katika uzalishaji wa mazao ya kilimo, Wizara imedhamiria kuhakikisha inaongeza uzalishaji wa mbegu kutosheleza mahitaji ya ndani na ziada kuuzwa nje ya nchi. Mazao ya kipaumbele yatakayozingatiwa katika mpango huo ni mahindi, alizeti, soya, ufuta, ngano, maharage, kunde, mpunga, mtama, choroko, dengu, shayiri na karanga ambayo mahitaji yake ni tani 652,250 ifikapo mwaka 2030.
  • Mheshimiwa     Spika,       katika        mwaka 

2022/2023, Wizara kupitia ASA na Sekta Binafsi itazalisha jumla ya tani 127,650 za mbegu bora za mazao mbalimbali kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 22. Aidha, Wizara kupitia Taasisi zake, Halmashauri na Sekta Binafsi itazalisha jumla ya miche/pingili/vikonyo 101,000,000 ya mazao ya kahawa, korosho, chikichi, parachichi, muhogo, migomba, minazi, mkonge, Chai, viazi vitamu na  zabibu (Jedwali Na.23). Mbegu na miche itakayozalishwa itasambazwa kwa wakulima kwa utaratibu maalum utakaowekwa na Wizara.

Jedwali Na. 22: Makadirio ya Mahitaji ya Mbegu Bora za

Mazao mbalimbali kwa mwaka 2029/2030

N a.Aina ya ZaoUzalishaj i wa mazao msimu wa  2020/20 21 (Tani) Makisio ya uzalishaji wa mazao msimu wa 2022/20 23 (Tani) Mkadirio ya mahitaji ya Certified Seeds 2022/202 3 (Tani)Makisio ya uzalishaji wa 2029/20 30 (Tani) Mahitaji ya Breeder Seeds (Tani)Mahitaji ya Pre- Basic Seeds (Tani)Mahitaji ya Basic Seeds (Tani)Mahitaji ya Certified Seeds 2029/2030( Tani)
1Mahi ndi   7,039,064     7,219,000    32,500   13,000,   0.32      25.39      2,031.25                             162,500.00 
2Alizet i649,437     941,000     5,600      1,400,000     0.22      11.20      560                             28,000 
3Soya   53,594     500,000     25,000      2,000,000     30.52      488.28      7,812.50                             125,000 
4Ufuta   205,054     220,000     800      1,000,000     0.00      0.06      16.00                             4,000 
5Ngan o   70,288     150,000  7,200   1,000,000     6.25      125      2,500                             50,000 
6Maha rage   1,211,909     1,300,000     10,000      2,000,000     0.78      31.25      1,250.00                             50,000 
7Kund e   151,706     250,000     2,250      450,000     0.18      7.03      281.25                             11,250 
8Mpu nga   2,629,519     2,832,000     16,000      6,400,000     0.16      12.50      1,000                             80,000 
9Mtam a   755,832     900,000     3,200      1,600,000     0.02      1.60      160                             16,000 
1 0Chor oko   100,610     140,000     4,100      820,000     0.32      12.8      512.50                             20,500 
1 1Deng u   26,022     45,000     500      100,000     0.04      2      62.50                             2,500 
1 2Shayi ri   10,000     18,000     500      50,000     0.31      6.25      125                             2,500 
1 3Kara nga   437,124     500,000     20,000      1,000,000     100      1,000      10,000                             100,000 
JUMLA13,340,114,965,0   127,650   29,820,0   139      1,723      26,311                             652,250 

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

            Jedwali       Na.       23:       Malengo       ya       Uzalishaji       wa

Miche/Pingili/Vikonyo katika mwaka 2022/2023

NaZaoIdadi
1Parachichi20,000,000
2Zabibu 2,000,000
3Minazi2,000,000
4Mkonge10,000,000
5Michikichi5,000,000
6Migomba5,000,000
7Muhogo5,000,000
8Viazi Vitamu2,000,000
9.Korosho15,000,000
10.Kahawa20,000,000
11.Chai15,000,000
 Jumla101,000,000

Chanzo: Wizara ya Kilimo 2022

  • Mheshimiwa Spika, ili kufikia malengo hayo Wizara kupitia, ASA itaongeza eneo jipya la hekta 4,000 kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora katika mashamba ya Msimba (hekta 1,500 ), Kilimi (hekta 700), Mwele (hekta 600) na Mbozi (hekta 1,200); itajenga miundombinu ya umwagiliaji kwenye eneo lenye ukubwa wa hekta 1,791.5 katika mashamba ya mbegu ya Tengeru (hekta 5.5), Mwele (hekta 600), Arusha (hekta 400) na Kilimi (hekta 786); itajenga bwawa lenye mita za ujazo 82,000 kwa ajili ya kuhifadhi maji katika shamba la mbegu la Arusha; itachimba visima virefu nane (8) katika shamba la mbegu la Arusha; itanunua matreka sita (6) na zana zake kwa ajili ya mashamba ya Msungura, Namtumbo, Msimba, Dabaga, Mbozi na Kilimi. 
  • Mheshimiwa Spika, ASA itanunua mashine za kupandia sita (6) kwa ajili ya shamba la kuzalisha mbegu za mpunga la Kilangali. Aidha, ASA itanunua ndege zisizo na rubani (drones) tatu (3) kwa ajili ya kunyunyuzia dawa za kudhibiti magonjwa na wadudu pamoja na kujenga uzio wa mashamba ya Arusha, Kilimi na Kilangali. Jumla ya Shilingi 43,033,700,000 zimetengwa kwa ajili ya kuimarisha upatikanaji wa mbegu bora.

Uthibiti wa Ubora wa Mbegu 

  • Mheshimiwa     Spika,       katika        mwaka

2022/2023, TOSCI itaendelea kuthibiti ubora wa mbegu nchini kwa kukagua hekta 45,000 za mashamba ya mbegu; kukusanya sampuli za mbegu 4,360 na  kupima ubora wake; na kukagua wafanyabiashara wa mbegu 1,900 na ghala 100. 

  • Mheshimiwa Spika, TOSCI itafanya majaribio ya utambuzi wa aina 425 za mbegu za mazao ya kilimo. Aidha, TOSCI itapitia mwongozo wa uzalishaji wa mbegu na kuandaa viwango vya kuthibitisha ubora wa mbegu za matunda na miti. Pia, TOSCI itatoa mafunzo kuhusu Sheria ya Mbegu Na.18 ya mwaka 2003 na Kanuni zake kwa wafanyabiashara 500, wataalam wa Afya ya Mimea 25, mawakala wa mbegu 1,000, wakaguzi wa mbegu 30 na watafiti 30.

                            5.2.2.         Upatikanaji wa Mbolea 

264. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza hapo awali, athari za UVIKO-19 na vita kati ya Urusi na Ukraine imesababisha ongezeko la bei ya mbolea duniani. Kwa mfano, bei ya mbolea aina ya DAP imeongezeka kutoka Dola za Marekani 310 kwa tani mwaka 2020 hadi Dola za Marekani 1,012 kwa tani mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 226. Aidha, bei ya mbolea aina ya Urea imeongezeka kutoka Dola za Marekani 251 kwa tani mwaka 2020 hadi Dola za Marekani 1,214 kwa tani mwaka 2022 sawa na ongezeko la

asilimia 384. (Kielelezo Na. 4)

Kielelezo Na. 4:  Mwenendo wa Bei za Mbolea (Dola za

Marekani kwa Tani)

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  • Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na athari za kupanda kwa bei ya mbolea duniani, Wizara itaimarisha mfumo wa utoaji ruzuku ya pembejeo za kilimo hususan mbolea kwa mazao yote kwa kuangalia upya utaratibu wa usajili wa kampuni na mawakala wa pembejeo nchini. Wizara inatarajia kutumia Shilingi Bilioni 150 kutoa ruzuku ya mbolea kwa mazao yote kwa utaratibu utakaoelezwa wakati wa kuwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali. Ruzuku hiyo haitakuwa ya kudumu bali itatolewa kwa kipindi maalum hususan wakati yatapotokea majanga au mdororo wa kiuchumi. 
  • Mheshimiwa Spika, kupitia Bunge lako Tukufu ninaagiza kampuni na viwanda vya mbolea nchini kusajili mawakala wao TFRA ifikapo tarehe 31 Mei, 2022 ili kurahisisha utoaji na usimamizi wa ruzuku. Aidha, Wizara itasajili wasambazaji wa mbolea na vituo vyote vya mauzo hapa nchini. Katika kuboresha usimamizi wa utoaji wa ruzuku, mifuko ya mbolea itawekwa misimbomilia (bar codes) na lebo ya RUZUKU ili kutofautisha na mbolea zitakazoendelea kuuzwa sokoni bila ruzuku. Aidha, Wizara itaendelea kuwalinda na kuwawezesha wawekezaji wa viwanda vya ndani vya kuzalisha mbolea.
  • Mheshimiwa Spika, kampuni yoyote ambayo haitatekeleza agizo hili na kukubali kutumia mfumo utakaowekwa na TFRA wa kusimamia na kusajili kampuni, mawakala na kuweka mfumo wa Point of Sale (POS) kwenye maduka na ghala zao za mikoani na wilayani, Serikali haitosita kumfutia leseni yake ya biashara. Mpango huu wa ruzuku ya mbolea utawapa kipaumbele wazalishaji wa mbolea ndani ya nchi ili kulinda viwanda vyetu, ajira na usalama wa nchi.
  • Mheshimiwa Spika, Mfumo huo pamoja na kuimarisha usimamizi wa mbolea za ruzuku, pia utasaidia kuboresha usimamizi wa tasnia ya mbolea ikiwemo udhibiti wa upandishwaji holela wa bei na ubora wa mbolea. Aidha, utaratibu wa kutoa ruzuku kwa wakulima kupitia mfumo wa mazao kujigharamia yenyewe (own crop financing) utaendelea kutekelezwa
  • Mheshimiwa Spika, Tanzania ni lango kuu la kupitisha mbolea kwa nchi za Afrika Mashariki (East African Community – EAC) na za Kusini mwa Bara la Afrika (Southern African Development Community – SADC) ikiwemo Malawi, DR Congo, Zambia, Burundi, Rwanda na Uganda. Kutokana na fursa hiyo, uwepo wa viwanda vya uzalishaji wa mbolea nchini ni fursa adhimu ya biashara ya mbolea katika ukanda huu.
  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha nchi inatumia fursa za masoko ya kikanda, Wizara itaendeleza jitihada za muda mrefu za kuzalisha mbolea hapa nchini. Kwa mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya ndani vya kuzalisha mbolea ikiwemo kampuni ya ITRACOM kukamilisha ujenzi wa kiwanda chenye uwezo wa kuzalisha tani 600,000 za mbolea kwa mwaka.  
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Taasisi nyingine za serikali itawezesha upatikanaji wa vivutio vya uwekezaji wa kiwanda cha mbolea cha Minjingu ili kiweze kuongeza uzalishaji kutoka tani 100,000 hadi tani 300,000 kwa mwaka. Aidha, Wizara itaendelea na mazungumzo na Wizara ya Nishati kuhusu kufufua mradi wa kuzalisha mbolea ya Urea kwa kutumia gesi asilia uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi.  
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TFRA itaratibu uingizwaji na usambazaji wa tani 650,000 za mbolea. Aidha, TFRA itaendelea kudhibiti ubora wa mbolea kwa kukagua wafanyabiashara 3,340 wa mbolea; kutoa mafunzo ya ukaguzi wa mbolea kwa maafisa kilimo 30 wa Halmashauri za wilaya; kununua vifaa vya maabara ya uchunguzi wa ubora wa mbolea; kuanzisha Ofisi za Kanda ya Kati na Magharibi; na kuimarisha Ofisi za Kanda ya Ziwa (Mwanza), Nyanda za Juu Kusini (Mbeya) na Kanda ya Kaskazini (Arusha). Vilevile, TFRA itasajili aina mpya za mbolea na visaidizi vyake 80; itasajili maeneo ya biashara mapya 1,000 na kutoa leseni 2,000; na itaimarisha mfumo wa ukusanyaji, uchambuzi na matumizi ya taarifa za mbolea.  
  • Mheshimiwa Spika, Wizara inapitia upya muundo wa Kampuni ya Mbolea Tanzania

(Tanzania Fertilizer Company – TFC) kwa lengo la kuiwezesha kampuni hiyo kujiendesha kibiashara na kutumika kama chombo cha Serikali cha kuimarisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo hususan mbolea na viuatilifu. Katika mwaka 2022/2023, Wizara itaiwezesha TFC Shilingi bilioni 6 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake.

  • Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kuwahakikishia wazalishaji wadogo wa mbolea za kilimo hai (organic) na chokaa kuwa itaendelea kuwalea, kuwalinda na kuwahakikishia masoko ili kupunguza gharama za kuagiza mbolea za aina hiyo kutoka nje ya nchi.
  • Mheshimiwa Spika, kupitia Bunge lako Tukufu, tunawahamasisha vijana wabunifu ambao wanaweza kuzalisha mbolea za kilimo hai (organic) waje Wizara ya Kilimo ili waweze kusaidiwa.

                            5.2.3.         Viuatilifu

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kupitia TPHPA itanunua viuatilifu lita 118,500 vya kudhibiti visumbufu vya milipuko, ikiwemo lita 100,000 za kudhibiti viwavijeshi, lita 10,000 kwelea kwelea, lita 5,000 nzige, lita 3,000 nzi wa matunda na lita 500 panya; itanunua mabomba 9,250 ya kupulizia viuatilifu na kusambaza katika Halmashauri 185; itasavei na kuainisha maeneo ya mazalia ya visumbufu na kuwadhibiti; itaimarisha usimamizi wa matumizi bora na sahihi ya viuatilifu; na kuimarisha uchambuzi wa kina wa visumbufu vya kikarantini. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha matumizi ya teknolojia sahihi za kuhifadhi mazao ya nafaka katika kanda nne (4) zenye uwezo wa kuzalisha nafaka. Pia, itahamasisha uhifadhi wa asili wa mazao ya nafaka kwa kutumia mimea dawa na kupima masalia ya sumu katika sampuli 3,000 kwenye mazao ya kimkakati ili kuendana na Sheria za masalia ya sumu za kimataifa na kuwezesha upatikanaji wa masoko ya nje ya nchi. 
  • Mheshimiwa Spika, TPHPA itakagua usafi wa afya ya mimea, itatambua na kudhibiti visumbufu katika mazao ya bustani, itakagua aina 6,600 za viuatilifu na itasajili viuatilifu vipya 300. Pia, itakagua shehena 1,800 za mimea zinazotarajiwa kuingizwa nchini na kuchambua aina za viuatililifu 3,500 ili kubaini ubora na athari zake kupitia masalia kwenye mazao.

                            5.2.4.         Zana za Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, Wizara katika mwaka

2022/2023, itaendeleakushirikiana na Sekta Binafsi kutoa mafunzo ya matumizi ya zana bora za kilimo kwa wamiliki na waendeshaji wa mashine na zana za kilimo 100 katika kanda za kilimo za Kati na Kaskazini.

  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha tunaongeza tija katika uzalishaji wa mazao, Wizara kwa kushirikiana na kampuni ya AFTRADE ya BELARUS itaendelea na tathmini ya maeneo yatakayofaa kwa ajili ya uanzishwaji wa Vituo Jumuishi vya Utoaji wa Huduma za zana za kilimo nchini (mechanization hubs), ambavyo vitawezesha upatikanaji wa mashine na zana za kilimo kwa urahisi. Aidha, kwa kutegemea makubaliano yatakayofikiwa baada ya tathmini inayoendelea, kampuni hiyo imepanga kuanzisha kituo kikubwa cha umahiri wa utoaji wa huduma za zana za kilimo nchini katika mkoa wa Dodoma, ambacho kitakuwa kitovu cha utoaji huduma, ufuatialiji na uratibu wa vituo vingine vitakavyoanzishwa hapa nchini. 
  • Vilevile, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na Sekta Binafsi imepanga kutoa mafunzo ya uhamasishaji wa matumizi bora ya zana za kilimo katika zao la mpunga katika Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha KATC, ambapo mafunzo hayo pia yatawahusisha maafisa ugani na wanafunzi wa vyuo kwa kupata mafunzo kwa vitendo.

5.3. Umwagiliaji

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kujenga miundombinu ya umwagiliaji katika skimu mpya 25 zenye jumla ya hekta 53,234 (Kiambatisho Na. 4). Katika mpango huo mabwawa 14 ya kuvuna maji ya mvua yenye uwezo wa mita za ujazo 131,535,000 ambayo yatamwagilia hekta 23,484 katika skimu 15 yatajengwa (Kiambatisho Na. 5). Aidha, skimu 10 zenye hekta 29,750 zitamwagiliwa kupitia vyanzo vingine vya maji ikiwemo mito. Vilevile, Tume itaboresha, itakarabati na kukamilisha skimu 30 zenye jumla ya hekta 41,771

(Kiambatisho Na. 6).  Aidha, jumla ya Shilingi 256,175,891,826 zitatumika kutekeleza mpango huo.

  • Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa mpango huo jumla ya hekta 95,005 zitaongezeka na kuongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 727,280.6 mwaka 2021/2022 hadi hekta 822,285.6 mwaka 2022/2023 ambayo ni sawa na asilimia 68.5 ya kufikia lengo la hekta 1,200,000 ifikapo 2025.
  • Aidha, kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa miundombinu hiyo, utachangia katika kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo. Kwa mfano, uzalishaji wa zao la mpunga unatarajiwa kuongezeka kwa tani 403,020 zenye thamani ya takriban Shilingi bilioni 345.4 na vitunguu tani 374,426 zenye thamani ya takriban Shilingi bilioni

2.9 na hivyo kuongeza pato la Taifa. Vilevile, uwekezaji huo unakadiriwa kutoa ajira za moja kwa moja zipatazo 475,000. 

  • Mheshimiwa Spika, Tume pia imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mabonde na skimu za kimkakati 22 zenye jumla ya hekta 306,361. Mabonde na skimu hizo zimewekwa kwenye mpango wa ujenzi katika kipindi cha mwaka 2022/2023 na 2024/2025. Vilevile, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utafanyika katika skimu 42 zenye jumla ya hekta 91,357 ambazo zitajengwa katika mwaka 2023/2024 (Kiambatisho Na. 7). Jumla ya Shilingi 35,472,168,000 zitatumika kutekeleza mpango huo.
  • Aidha, Tume itahakiki skimu na eneo linalomwagiliwa na eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji nchini. Tume pia, itanunua magari 38 kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa miradi kupitia ofisi za umwagiliaji za mikoa, itanunua mitambo 12 kwa ajili ya ujenzi wa skimu, itanunua vifaa vya upimaji (land survey equipment) kujenga ofisi 17 za uwagiliaji za mkoa. Jumla ya Shilingi 24,826,259,000 zitatumika kutekeleza mpango huo.
  • Mheshimiwa Spika,  katika kujenga uwezo wa Vyama vya Umwagiliaji, Wizara itatoa mafunzo kwa wakulima viongozi 1,000 na Vyama vya Umwagiliaji 220 kuhusu mipango ya usimamizi na uendeshaji wa skimu za umwagiliaji. Pia. itawezesha uanzishwaji wa Vyama vya Umwagiliaji 200 na kuandaa kanuni ndogo kulingana na Sheria Na. 4 ya Taifa ya Umwagiliaji (2013) na kanuni za umwagiliaji (2015). Aidha, Tume itasambaza miongozo ya ukusanyaji wa ada za huduma ya umwagiliaji katika skimu 974 ili kuimarisha Mfuko wa Maendeleo ya Umwagiliaji. 

5.3.1. Ofisi za Wilaya za Umwagiliaji 

288. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itafungua ofisi 146 za Umwagiliaji za Wilaya. Ofisi hizo zitakuwa na Wahandisi wa umwagiliaji, Mafundi Sanifu Ujenzi na Maafisa Kilimo. Watumishi hao kwa kushirikiana na watumishi waliopo Ofisi ya Rais – TAMISEMI watasimamia miradi ya umwagiliaji katika Wilaya zao na kusimamia ukusanyaji wa ada za huduma za umwagiliaji. Aidha, watumishi hao watakuwa chini ya Ofisi za Tume ya Umwagiliaji na kuwajibika moja kwa moja Wizara ya Kilimo. Mfumo huo wa usimamizi wa miradi ya umwagiliaji utaokoa upotevu wa mapato ya takribani Shilingi 100,000,000,000 kwa mwaka.

5.4. Kuimarisha Huduma za Ugani

5.4.1. Huduma na Mafunzo ya Ugani

  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kuimarisha huduma za ugani ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao nchini.  Katika mwaka 2022/2023, Wizara itawezesha upatikanaji wa huduma ya upimaji wa afya ya udongo bure kwa wakulima kama huduma ya msingi na ya lazima. Huduma hiyo itaenda sambamba na kusajili wakulima na kuwaweka kwenye Kanzi Data maalum. Aidha, kila mkulima atapewa cheti kitakachoonesha afya ya udongo katika shamba lake ili kumwezesha mkulima kuzalisha mazao kulingana na afya ya udongo wa shamba lake. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kufikia azma hiyo, Wizara itanunua na kusambaza vifaa vya kupimia afya ya udongo kwa maafisa ugani wa Halmashauri 122; vishikwambi 6,377; visanduku vya ugani (Extension Kits) 400 katika Halmashauri 46; na  itanunua na kufunga GPS kwenye pikipiki za maafisa ugani na kuweka mfumo wa usimamizi wa huduma za ugani na kuwezesha kila afisa ugani anapata sare ambazo atavaa akiwa kazini.  Aidha, Wizara itawezesha uanzishwaji wa mashamba ya mfano 400 na mashamba darasa 400 kwa mazao ya kipaumbele katika Mikoa ya Singida, Simiyu, Morogoro, Njombe, Ruvuma, Kilimanjaro, Manyara, Tabora, Mara, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa na Dodoma. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaanzisha mfumo utakaowawezesha maafisa ugani kuwatambua wakulima bora watakaotumika kutoa huduma za ugani kwa wakulima wengine. Katika kuondokana na tatizo la upungufu wa maafisa ugani, wanafunzi wanaosoma katika vyuo vya kilimo katika ngazi zote kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Wizara itaanza mfumo wa kuwapeleka katika mafunzo ya vitendo kwa mwaka mmoja kabla ya kuhitimu masomo yao na eneo hili Serikali itashirikiana na Wadau wa Maendeleo.
  • Kadhalika, Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya

Makazi, itawezesha upimaji wa ardhi ya kilimo na kuitangaza kwenye gazeti la Serikali. Hatua hizo zinalenga kulinda ardhi ya kilimo kupitia hati miliki za mashamba, kutumia rasilimali ya ardhi kama moja wapo ya dhamana zinazoweza kutumiwa na wakulima kupata mitaji ya kuendeleza kilimo.  

  • Mheshimiwa Spika, pamoja na vitendea kazi walivyopewa maafisa ugani, Wizara itahakikisha wataalam hao wanapatiwa mafunzo sahihi kwa kuratibu utekelezaji wa program za mafunzo kwa maafisa ugani wote nchini ili waweze kutoa huduma sahihi kulingana na mazao wanayosimamia katika maeneo yao. 
  • Aidha,Wizara itaendelea kutumia TEHAMA katika kutoa huduma za ugani na taarifa za masoko kwa wadau wa kilimo. Katika mwaka 2022/2023, Wizara itatoa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa M-Kilimo kwa maafisa ugani 1,500 na kusajili wakulima wapya 2,218,415 na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo 1,375. Aidha, Wizara itatoa ushauri wa kitaalam kwa wakulima kuhusu kilimo bora na taarifa za masoko ya mazao kupitia mfumo huo. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaanzisha kituo cha huduma za mawasiliano ya kilimo (Call centre) kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa ushauri wa kitaalam na taarifa za masoko kwa wadau wa kilimo. Aidha, Wizara itaandaa mwongozo wa usimamizi wa huduma za ugani na kuusambaza kwa sekretarieti za mikoa 26 na Halmashauri 185. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Sekta Binafsi itaanza kukarabati vituo 200 vya  Rasilimali za Kilimo vya Kata (WARCs) ambavyo vitatumika kwa ajili ya shughuli za kilimo. Jumla ya Shilingi Bilioni 15,007,560,000 zimetengwa kwa ajili kuimarisha huduma za ugani.
  • Mheshimiwa Spika, ninapenda nitumie nafasi hii kupitia Bunge lako Tukufu kuzielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kutobadilisha matumizi ya Vituo vya Rasilimali za Kilimo bila idhini ya Wizara ya Kilimo. 

5.4.2. Vyuo na vituo vya Mafunzo ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, Wizara itadahili wanafunzi 2,200 katika ngazi ya Astashahada na Stashahada . Vilevile, Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia itapitia upya mitaala na mfumo mzima wa vyuo vya Kilimo kwa lengo la kutoa wahitimu wenye stadi zitakazo wawezesha kutoa huduma na ushauri kwa wakulima kwa vitendo. Ushirikiano huo pia utahusisha vijana na wakufunzi wa kilimo kupata mafunzo katika vyuo mahiri duniani. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea na ukarabati wa miundombinu ya Vyuo vya Mafunzo ya Kilimo Uyole, KATRIN, Inyala, Ukiriguru, Igurusi, Mtwara, Mlingano, HORTI – Tengeru na Vituo vya Mafunzo kwa Wakulima vya Bihawana, Ichenga na Mkindo. Vilevile, Wizara itanunua magari matatu (3), matreka mawili (2) na vifaa vya kufundishia kwa ajili ya Vyuo vya Kilimo vya Mlingano, HORTI – Tengeru, Inyala, Maruku, KATC, Mubondo, Mtwara na Vituo vya Mafunzo kwa Wakulima vya Bihawana, Ichenga na Mkindo. Jumla ya Shilingi 5,225,000,000 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati huo.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaboresha mfumo wa uendeshaji wa Maonesho ya Wakulima (Nanenane) ili kuhakikisha Viwanja vya Maonesho ya Nanenane vinakuwa vituo vya kutoa elimu na taarifa za uzalishaji na masoko mwaka mzima. Vilevile, maboresho hayo yataenda sambamba na uanzishwaji wa uwanja wa kimataifa wa maonesho ya kilimo (Tanzania International

Agricultural Trade Fair). 

5.5. Uzalishaji wa mazao

5.5.1. Mazao Asilia ya Biashara 

301. Mheshimiwa Spika, uzalishaji wa mazao asilia ya biashara unatarajiwa kuongezeka kutoka tani  919,282 mwaka 2021/2022 hadi tani 1,199,081,794 mwaka 2022/2023 ambapo mauzo ya mazao hayo nje ya nchi yanakadiriwa kufikia tani 641,515 zenye thamani ya Shilingi

1,199,081,794 (Jedwali Na. 24).

Jedwali Na.24: Makadirio ya Uzalishaji na Mauzo ya Mazao

Nje ya Nchi kwa Mwaka 2022/2023

Zao 2021/20222022/2023**Mauzo ya nje (Tani)Thamani ya Mauzo ya Nje 2023 (TZS)
Pamba  144,550 350,000 103,000 381,710,000
Kahawa 65,235 75,000 72,000 236,500,000 
Chai  11,962 30,000 25,000 42,000 
Pareto  1,848 2,800 765 6,600,000 
Tumbaku 70,775 95,000 61,750 215,507,500 
Korosho  238,597 400,000 340,000 294,372,294 
Mkonge  24,644 60,000 39,000 64,350,000 
Sukari  361,671 450,000 – 
Jumla 919,2821,462,800 641,515 1,199,081,794

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

Zao la Mkonge

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Mkonge Tanzania itasimamia Mkakati wa kuongeza uzalishaji wa zao la mkonge kutoka tani 36,169.8 mwaka 2020/2021 hadi tani 60,000 mwaka 2022/2023. Lengo hilo litafikiwa kwa kutoa elimu kuhusu kilimo bora cha mkonge na ubora wa singa kwa wakulima wadogo 8,000 na wakulima wakubwa 39 na kusimamia uzalishaji na usindikaji wa zao la mkonge. 
  • Aidha, Bodi itaendelea kusambaza miche bora 10,000,000 kwa wakulima katika

Halmashauri za Wilaya 40; kupima hekta 1,500 za mashamba na kuyagawa kwa wakulima; Pia, Bodi itahamasisha kilimo cha mkonge katika Wilaya 8 za mikoa ya Tanga, Singida na Tabora na kuwaunganisha wakulima wadogo 2,400 na soko kwa mfumo wa zabuni.  

  • Mheshimiwa Spika,  Bodi ya Mkonge itahamasisha uanzishwaji wa viwanda vidogo vinne (4) vya kuchakata mkonge katika mikoa ya Morogoro (Kilosa), Shinyanga (Kishapu), Singida (Singida Vijijini) na Tanga (Handeni). Pia itakarabati mashine ya kuchakata mkonge katika shamba la Kibaranga na itawezesha utengenezaji wa mashine moja (prototype) ya kuzalisha shira (syrup) na spirit. Vilevile, itahamasisha matumizi ya kamba na magunia ya mkonge pamoja na uwekezaji katika kuongeza thamani ya zao la mkonge. Jumla ya Shilingi 2,000,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Zao la Korosho

  • Mheshimiwa     Spika,       katika        mwaka

2022/2023, Wizara kupitia Bodi ya Korosho Tanzania imepanga kuongeza uzalishaji kutoka tani 238,555.81 mwaka 2021/2022 hadi tani 400,000. Ili kufikia malengo hayo, Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi wa upatikanaji na usambazaji wa viuatilifu tani 25,000 za Salfa ya unga, lita 1,500,000 za viuatilifu vya maji na vinyunyizi (motorized sprayers) vya viuatilifu 3,500, magunia 4,400,000 na kutoa mafunzo ya kilimo bora cha korosho na kuhamasisha uongezaji wa thamani.

  • Katika kuendeleza maeneo mapya ya uzalishaji wa zao la korosho, Wizara kupitia Bodi itaimarisha upatikanaji wa pembejeo, uanzishaji na uendelezaji wa mashamba ya pamoja (block farms) na kuanzisha viwanda vidogo vya kubangua korosho katika Halmashauri za wilaya za Kongwa na Tanga. Vilevile, Bodi itajenga ghala mbili (2) zenye uwezo wa kuhifadhi tani 2,000 kila moja katika Halmashauri za wilaya za Manyoni na Kongwa.  
  • Vilevile, Bodi itawezesha uanzishwaji wa mashamba matatu (3) ya pamoja yenye ukubwa wa hekta 7,500 katika maeneo mapya ya uzalishaji wa korosho zikiwemo Wilaya za Kisarawe, Nanyumbu na Tunduru. Vilevile, Bodi itakamilisha ujenzi wa kituo cha mafunzo ya kusindika Korosho kwa wakulima katika viwanja vya maonesho ya Nanenane vilivyopo Ngongo (Lindi). Jumla ya Shilingi 30,000,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Zao la Kahawa

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Kahawa Tanzania imepanga kuongeza uzalishaji wa kahawa kutoka tani 65,235 mwaka

2021/2022 hadi tani 72,000 mwaka 2022/2023. Lengo hilo litafikiwa kwa kukarabati mashamba yaliyopo; kutoa mafunzo ya kilimo bora cha zao la kahawa na kuimarisha mifumo ya masoko ya kahawa ikiwemo kuanzisha minada ya kahawa katika mkoa wa Kagera; kuratibu na kusimamia mikataba ya ununuzi wa kahawa. 

  • Vilevile, Wizara, kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Bodi ya Kahawa Tanzania itagawa mizani 300 kwenye vyama vya ushirika na kukarabati/kujenga ghala 50 katika Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kuimarisha masoko ya kahawa. Aidha, utekelezaji wa mpango huo utahusisha TADB na NMB ambapo jumla ya Shilingi Bilioni 29 zitatumika kufikia malengo hayo. 
  • Vilevile, Wizara kwa kushirikiana na Sekta Binafsi itawezesha uzalishaji na usambazaji wa miche bora 20,000,000 na kununua mashine mbili (2) zenye uwezo wa kukaanga tani 15 za kahawa kwa saa. Jumla ya Shilingi 300,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Zao la Pamba

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kupitia Bodi ya Pamba imepanga kuongeza uzalishaji kutoka tani 144,792 mwaka 2021/2022 hadi tani 350,000 mwaka 2022/2023. Ili kufikia lengo hilo, Bodi itasambaza tani 17,000 za mbegu bora, chupa 4,500,000 (ekapack) kwa wakulima 600,000 wa pamba; itanunua na kusambaza mashine rahisi za kupalilia 400 na kusambaza kwa wakulima 400; itahamasisha matumizi ya mbinu bora za kilimo cha pamba ikiwemo matumizi ya nafasi mpya za upandaji wa pamba (60 sm × 30 sm) kwa kutumia njia mbali mbali ikiwemo Balozi wa Pamba.
  • Mheshimiwa Spika, Bodi itasajili wakulima wa pamba kupitia Mfumo wa Kieletroniki katika mikoa 17. Ili kuhamasisha wakulima kung’oa masalia ya pamba katika mashamba yao, Bodi itanunua mashine mbili (2) (Biomass Briquette machines)   zenye uwezo wa kuzalisha tani 1.8 ya nishati mbadala ya kupikia inayotokana na masalia hayo.  Mashine hizo zitasimikwa katika Wilaya za Maswa na Meatu na kusimamiwa na AMCOS.

 Zao la Chai

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Chai Tanzania imepanga kuongeza uzalishaji wa chai kavu kutoka tani 27,510 mwaka 2020/2021 hadi tani 30,000 mwaka 2022/2023. Katika kufikia lengo hilo, Bodi kwa kushirikiana na wamiliki wa mradi wa chai Kilolo, Sekta Binafsi na Wadau wa Maendeleo pamoja na wasindikaji wa chai wa wilaya ya Mufindi itafufua shamba lenye ukubwa wa hekta 350 katika mradi wa chai Kilolo utakaogharimu takriban Shilingi milioni 300 utakaochangia kuongeza uzalishaji wa tani 405 za chai kavu. 
  • Aidha, Bodi kwa kushirikiana na TSHTDA na Shirika la Solidaridad watatoa mafunzo kuhusu ubora wa chai kwa Wakulima 200 katika Wilaya ya Kilolo ili waweze kupatiwa vyeti vya ubora vinavyotolewa na kampuni ya Rainforest Alliance kwa ajili ya kupata soko la nje.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi, TSHTDA, Sekta Binafsi na Wadau wa Maendeleo itazalisha miche ya chai 15,000,000. Kati ya hiyo, miche 7,500,000 itatumika kwenye upanuzi wa mashamba ya chai katika wilaya za Mufindi, Njombe na Kilolo na miche 7,500,000 itatumika katika kujazia mapengo ya mashamba ya wakulima wadogo katika wilaya za Lushoto, Korogwe na Bukoba. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) itakamilisha ukarabati wa kiwanda cha chai Mponde Wilayani Lushoto ambao umefikia asilimia 75. Kiwanda hicho kinatarajiwa kuongeza upatikanaji wa ajira kwa watu zaidi ya 150 na kununua majani mabichi ya chai kutoka kwa wakulima wapatao 4,000.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) itakamilisha uanzishwaji wa mnada wa chai katika eneo la Kurasini, Dar es Salaam. Mnada huo utapunguza gharama za biashara zilizokuwa zinatokana na kuuza chai katika mnada wa chai Mombasa, utaimarisha matumizi ya bandari nchini pamoja na kuongeza ajira. Uanzishwaji wa mnada utaenda sambamba na kuimarisha mahusiano na nchi za Rwanda, Burundi na Pakistan ili kupata wanunuzi watakaoshiriki katika mnada huo. Jumla ya Shilingi

2,000,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Zao la Tumbaku

318. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Tumbaku Tanzania imepanga kuongeza uzalishaji wa tumbaku kutoka tani 58,295 mwaka 2020/2021 hadi tani 95,000 mwaka 2022/2023. Malengo hayo yatafikiwa kwa kutoa mafunzo ya kilimo bora cha tumbaku kwa maafisa ugani na wakulima kupitia mashamba mawili (2) ya mfano katika mikoa ya Mbeya (Chunya) na Tabora (Urambo). Aidha, kiwanda kilichokuwa kimefungwa cha TLTC kimepata mwekezaji mpya ambaye ni kampuni ya AMY Holding Ltd ambapo katika mwaka 2022/2023 kampuni hiyo itanunua tani 10,000 za tumbaku na kuingia mikataba ya kununua tumbaku na wakulima tani 30,000. Jumla ya Shilingi 500,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Zao la Pareto

319. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi ya Pareto Tanzania itahamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa pareto kutoka tani 2,412 mwaka 2020/2021 hadi tani 2,800 mwaka 2022/2023.  Ili kufikia lengo hilo, Bodi itasambaza tani nne (4) za mbegu bora za pareto zitakazotosheleza eneo lenye ukubwa wa hekta 4,000 katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, Songwe, Arusha na Manyara; kuendelea kutoa elimu ya kilimo bora cha pareto kwa wakulima 12,000 katika mikoa hiyo; na kutoa elimu ya ushirika ili kuongeza AMCOS kutoka sita (6) hadi 10. Jumla ya Shilingi 200,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

5.5.2. Mazao ya Chakula

  • Mheshimiwa Spika, idadi ya watu duniani inatarajiwa kufikia bilioni 9.9 ifikapo mwaka 2050 ambapo kwa Tanzania inakadiriwa kufikia idadi ya watu Milioni 100. Ongezeko hilo, litaongeza mahitaji ya chakula nchini kufikia tani 33,940,132. Kati ya kiasi hicho, mahindi yanakadiriwa kuwa tani 12,917,919 na mchele tani 2,409,155 na muhogo tani 6,031,761. 
  • Katika kipindi hicho, mahitaji ya nafaka yataongezeka kufikia tani bilioni 3 zikijumuisha chakula cha binadamu na mifugo.   Hiyo ni fursa ya soko kwa mazao ya chakula yanayozalishwa hapa nchini. Ili kutumia fursa hiyo na kujitosheleza kwa chakula, katika mwaka 2022/2023, Wizara imepanga kuyaendeleza

mazao makuu ya chakula kama ifuatavyo: –

Zao la Mahindi

322. Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi kutoka tani 7,039,064 mwaka 2020/2021 hadi kufikia tani 7,219,041 ifikapo mwaka 2022/2023.  Ili kufikia lengo hilo, Wizara itaongeza uzalishaji wa mbegu bora za mahindi; itaimarisha huduma za ugani na matumizi ya TEHAMA katika kutoa huduma za ugani. Vilevile itaimarisha upatikanaji wa masoko,itajenga ghala za kisasa za kuhifadhi mazao na kukarabati ghala zilizopo na itaimarisha udhibiti wa sumukuvu ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

Zao la Mpunga

323. Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga kutoka tani 4,673,969.231 hadi kufikia tani  5,011,045 mwaka 2022/2023. Ongezeko hilo litatokana na kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji;  kuongeza tija ya uzalishaji kutoka tani 2 kwa hekta hadi tani 4 kwa hekta; kuimarisha upatikanaji wa masoko na uanzishaji wa ubia wa kilimo biashara; kuimarisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo;  kutoa mafunzo kuhusu uendelezaji wa zao la mpunga kwa wakulima na Maafisa ugani; na kuendeleza teknolojia za uzalishaji, uvunaji, uchakataji na usindikaji.  

Zao la Muhogo

324. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itahamasisha uzalishaji wa zao la muhogo kibiashara kutoka tani 7,000,000 mwaka 2021/2022 hadi tani 10,000,000 mwaka 2022/2023 katika mikoa ya Tanga, Pwani, Kigoma, Lindi na Mtwara. Ili kufikia lengo hilo, TARI itazalisha na kusambaza kwa wakulima pingili za muhogo 8,250,000.

5.5.3. Mazao yenye Mahitaji Makubwa

Uzalishaji wa Miwa na Sukari

  • Mheshimiwa Spika, mahitaji ya sukari nchini ni wastani wa tani 585,000 kwa mwaka, ambapo tani 420,000 ni sukari ya matumizi ya kawaida na tani 165,000 ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani. Upungufu wa sukari ya matumizi ya kawaida ni wastani wa tani 50,000. Aidha, wastani wa uzalishaji wa sukari nchini kwa ajili ya matumizi ya kawaida ni tani 342,409.
  • Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na upungufu huo, Wizara kupitia Bodi ya Sukari itaongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani 372,210 mwaka 2021/2022 hadi tani 450,000 mwaka 2022/2023. Lengo hilo litafikiwa kwa kutekeleza mipango ya muda mfupi ya kuimarisha udhibiti wa visumbufu, kuimarisha upatikanaji wa maji mashambani, kupunguza upotevu wa miwa kwa kuhakikisha viwanda vinafanya kazi kwa ufanisi. Mipango hiyo itaenda sambamba na kuhamasisha uzalishaji wa sukari ya viwandani. Aidha, mipango ya muda wa kati ni pamoja na kusimamia upanuzi wa viwanda vya sukari vya Kilombero, Kagera na Mtibwa ili kuongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani 372,210 hadi tani 635,012 mwaka 2025/2026 (Kiambatisho Na.8). Ongezeko hilo litatokana na kuongeza uzalishaji wa miwa kutoka tani 800,000 hadi tani 1,700,000 kwa wakulima wadogo wa mashamba ya Kilombero, upanuzi wa mashamba ya miwa ya Kagera na Mtibwa yenye ukubwa wa hekta 13,000 na 30,000 mtawalia na kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji ikiwemo ujenzi wa bwawa la kuhifadhi maji ya umwagiliaji lenye mita za ujazo 25,000,000 katika mashamba ya Mtibwa. Upanuzi wa uzalishaji katika viwanda vilivyopo ni kama inavyoonekana katika Jedwali Na.25.

Jedwali Na.25: Uwekezaji katika zao la Sukari katika Mwaka 2020-2023

NaKiwandaHekta zinazoongezwa (2025)Matarajio ya  uzalishaji (2025)Uwekezaji katika kipindi cha 2020-2023
1 
Kilombero Sugar 30,000         271,000USD Milioni 190.1
2TPC NA                 NAUSD Milioni 26.08
3Kagera Sugar-13,529         170,000USD Milioni 168.86
4Mtibwa Sugar-6,000           84,000USD Milioni 20.51

Chanzo: Wizara ya Kilimo, 2022

  • Vilevile, kutokana na changamoto ya ardhi, kiwanda cha TPC kitaongeza tija katika mashamba yaliyopo ambapo uboreshaji wa hali ya udongo katika shamba la Kahe lenye ukubwa wa hekta 240 utafanyika. Aidha, uanzishwaji wa miradi mipya ya sukari ya Bagamoyo na Mkulazi II unaendelea (Kiambatisho Na.9). Jumla ya Dola za Marekani 405.55 zitatumika kwenye upanuzi wa viwanda.
  • Mheshimiwa Spika, miradi mipya iliyo katika hatua za awali za kumilikishwa ardhi ya uwekezaji wa viwanda vya sukari ni ya kampuni ya Rai Group iliyopo Kasulu (Kigoma) unaotarajiwa kuzalisha tani 250,000 na mradi wa Rufiji (Pwani) wa Kampuni ya Lake Agro Ltd,  unaotarajiwa kuzalisha tani 30,000.
  • Aidha, Bodi itatoa mafunzo ya Kilimo bora cha miwa kwa wakulima 1,000 katika maeneo yenye viwanda vya sukari na maeneo mapya na itaanzisha mashamba darasa matatu (3) katika maeneo ya Mtibwa, Kagera na Manyara. Pia, Bodi itachimba visima vya umwagiliaji katika mashamba ya miwa. 
  • Vilevile, Bodi itawezesha upatikanaji wa maeneo yanayofaa kwa ajili ya Kilimo cha Miwa na uwekezaji katika viwanda vya sukari kwa kushirikiana na Halmashauri za wilaya husika na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Aidha, Bodi itaainisha maeneo yanayofaa kwa kilimo cha miwa na uwekezaji wa viwanda vya sukari katika mikoa ya Ruvuma, Katavi, Kigoma, Tabora, Rukwa, Lindi na Mtwara na kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwenye mashamba ya wakulima Kilombero. Jumla ya Shilingi 1,000,000,000 zimetengwa kufanikisha lengo hilo.

Mazao ya Mafuta

  • Mheshimiwa Spika, mahitaji ya mafuta ya kula nchini ni tani 650,000 kwa mwaka ikilinganishwa na uzalishaji wa ndani ambao ni tani 300,000 na takriban tani 350,000 huagizwa nje ya nchi. Kati ya kiasi kinachozalishwa nchini, tani 270,000 sawa na asilimia 90 kinatokana na zao la alizeti na kiasi kinachobaki kinachangiwa na mazao mengine ikiwemo chikichi, karanga, nazi, pamba na ufuta. 
  • Mheshimiwa Spika, ili kujitosheleza kwa mahitaji ya mafuta ya kula nchini, Wizara itatekeleza mikakati ya muda mfupi na muda mrefu. Mikakati ya muda mfupi ni pamoja na kuhamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti kwa ziada ya tani 1,400,000 ili kuziba nakisi ya tani 400,000 za mafuta ya kula. Kwa maana hiyo, mahitaji yetu ya alizeti ili kukidhi mahitaji ya ndani ni tani milioni 2.3.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imejiwekea lengo la kuzalisha tani milioni 3 za alizeti ifikapo mwaka 2025 ili kama nchi tuwe na mafuta ya alizeti tani milioni 1, tunahitaji kulima eneo lenye ukubwa wa hekta milioni 2.4. Aidha, eneo hilo la kilimo linahitaji tani 12,000 za mbegu  kwa ajili ya uzalishaji wa tani 1,000,000 za alizeti.
  • Mheshimiwa Spika, ili kufikia lengo hilo, Wizara katika mwaka 2022/2023 itachukua hatua mbili za kimkakati, pamoja na majukumu ya kawaida ya uhamasishaji na itazalisha na kugawa tani 5,000 za mbegu bora za alizeti kwa ruzuku. Jumla ya Shilingi Bilioni 11 zitatumika kuzalisha mbegu hizo. 
  • Katika mwaka 2023/2024, Wizara itagawa tani 10,000 na mwaka  2024/2025 itazalisha na kugawa tani 15,000 za mbegu bora za alizeti. Shughuli hiyo ya uzalishaji wa mbegu itafanywa na ASA  na kuingia mikataba na Kampuni binafsi kwa ajili ya kuzalisha mbegu ambazo zitagawiwa kwa wakulima kwa ruzuku.
  • Hatua ya pili, Wizara inajadiliana na Wizara ya Fedha na Mipango ili kuweka motisha ya kikodi kwa viwanda vinavyozalisha mafuta ya alizeti nchini kwa kuwaondolea kodi ya ongezeko la thamani (VAT). Utafiti uliofanywa na Wizara unaonesha kuwa Serikali itapoteza kodi kati ya Shilingi Bilioni  20.5 na Bilioni 18.9 kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitatu. Upotevu huo utapungua kila mwaka  katika kipindi cha miaka mitatu kwa kuwa viwanda vitaongeza uzalishaji kwa kuwa kwa sasa vinafanya kazi chini ya asilimia 30 ya uwezo wake. Jumla ya upotevu huo utafikia Shilingi Bilioni 59.3 katika kipindi cha miaka mitatu.
  • Baada ya kipindi cha miaka mitatu, uzalishaji katika viwanda hivyo utafikia asilimia 100 na Serikali itakusanya mapato kupitia PAYE, kodi ya mapato na ushuru wa mazao. Makusanyo hayo yataongeza mapato ya Serikali hivyo upotevu ulioelezwa ni wa muda mfupi na gharama za uzalishaji zitapungua. Hali hiyo itafanya viwanda vyetu vinavyochuja mafuta mara mbili (double refinery) kuwa shindani na kupunguza ugumu wa maisha kwa watanzania na kuwafanya watanzania kuwa na kipato cha ziada kwa kutumia fedha zao kwenye matumizi mengine ya kijamii.
  • Mheshimiwa Spika, hatua ya tatu, Wizara imeanza kuvitaka viwanda vinavyochuja mafuta mara mbili (double refinery) kununua mafuta ghafi yanayozalishwa na wazalishaji wadogowadogo (backyard processors) ambao wengi wao ni wanawake na vijana ambao wanalima alizeti na kuikamua kwa mashine ndogondogo za SIDO na kuyapanga mafuta barabarani.
  • Mheshimiwa Spika, mkulima anayelima ekari moja (1) na kukamua mafuta yake na kuuza kwa bei ya leo iliyopo sokoni anapata faida ya Shilingi 1,530,000. Mkulima anayelima ekari moja (1) na kuuza alizeti aliyovuna anapata faida ya Shilingi 420,000 tu. Wizara inaendelea kuhamasisha kutengeneza madaraja mawili ya wasindikaji ambao ni wasindikaji wa awali na wasindikaji wa upili (Primary na secondary processors).
  • Ili kumlinda mkulima, mzalishaji, muuzaji na mlaji ni lazima kama nchi tuchukue hatua ya kuondoa VAT kwenye mafuta ya kula yanayozalishwa na viwanda vya double refinery ndani ya nchi ili kuijenga sekta ya mafuta ya kula yanayozalishwa ndani ya nchi
  • Mheshimiwa Spika, zao la alizeti ni kwa ajili ya mkakati wa muda mfupi  na kwa ajili ya kujenga msingi wa kuwa nchi inayouza mafuta ya alizeti nje ya nchi. Aidha, katika miaka mitatu ya kwanza, Wizara itahamasisha uwekezaji wa kilimo katika maeneo mapya (extensive agriculture) ili kufikia lengo la hekta milioni 2.4 ifikapo 2025. Kadhalika, baada ya mwaka 2025, Wizara itahamasisha uzalishaji wa zao la alizeti kwa kuongeza tija ya zao (intensive agriculture). Kwenye eneo hili ugawaji wa mbegu utatumia

Shilingi Bilioni 17.5.

  • Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu Tanzania tumekuwa tukijitangaza na kujisifia kuwa sisi ni waanzilishi wa zao la chikichi na baadhi ya mataifa yenye uzalishaji mkubwa wa zao hilo yalichukua mbegu kwetu. Ni vyema kufahamu mambo mawili ambayo ni ukweli usiokwepeka; moja, hatukuwahi kufanya uwekezaji wa kutosha kama nchi kwenye eneo la chikichi lakini pia mfumo tuliokuwa tunautumia kuendeleza zao hili wa kuamini kuwa mkulima mdogo ataweza kugharamia zao hili na kulifanya zao hili litutosheleze kwa mafuta ya kula haikuwa sahihi ni lazima tubadili namna ambavyo tunawekeza katika zao hili.
  • Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni kuwa; ili kuwe na faida kwa mkulima na mchakataji wa mafuta ya chikichi, mashamba lazima yawe katika utaratibu wa mashamba makubwa ya pamoja (Block farms). Ili kuongeza uzalishaji na tija, Wizara katika mwaka 2022/2023 itaanza kutumia utaratibu wa mashamba makubwa ya pamoja kwa kuchukua maeneo makubwa kuanzia hekta 2,000 hadi hekta 8,000 kuyasafisha, na kuyawekea miundombinu inayostahili, kupanda miche na eneo kama litahitaji kulipiwa fidia Serikali itatwaa na kulipia fidia.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara imejiwekea lengo la kuanza safari ya kuzalisha mafuta ya chikichi tani 500,000 ifikapo mwaka 2030. Ili kufikia lengo hilo tunahitaji eneo la kilimo lenye ukubwa wa hekta 125,000 ambapo tutahitaji miche 15,625,000. Uzalishaji wa miche hiyo utafanywa na TARI, ASA na Sekta Binafsi. Kwa kuanzia, mikoa ambayo ni ya kipaumbele kwa ajili ya mkakati huu ni Kigoma, Katavi, Tabora na Pwani. Wakati Serikali inaendelea na mpango huu, Wizara inakamilisha mazungumzo na Kampuni kubwa mbili za Bakhresa na Wilmar ambao wameonesha nia ya kuwekeza katika mkoa wa Kigoma na Pwani.
  • Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala la mafuta ya kula ni hitaji la kidunia, kupitia Bunge lako Tukufu, tunawakaribisha wawekezaji kuwekeza katika mpango huo. Vilevile, Wizara itafanya mazungumzo na Wizara ya Fedha na Mipango ili kutafuta fedha Shilingi Bilioni 40 zitakazotekeleza mpango huo.
  • Mheshimiwa Spika, jambo hili la kuondoa tatizo la mafuta ya kula ni la muda mrefu. Kwa hiyo, ni lazima tukubali kuwekeza kimkakati kwa kuishirikisha Sekta Binafsi. Uwekezaji huo siyo hasara kwa nchi kwani soko la ndani na nje lipo, wakulima wapo na ardhi ya kilimo ipo na Serikali ya Awamu ya Sita ipo tayari kuwekeza.

Zao la Soya

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itahamasisha uzalishaji na uuzaji wa soya nje ya nchi kutoka tani 53,000 mwaka 2021/2022 hadi tani 88,000 mwaka

2022/2023. Ili kufikia lengo hilo, Wizara itatoa mafunzo ya kilimo bora cha soya kwa maafisa ugani 400 na wakulima viongozi 1,600 katika maeneo ya uzalishaji.

  • Vilevile, Wizara itaiwezesha TARI kufanya utafiti wa mbegu bora za soya ambazo zitakidhi mahitaji ya soko. Aidha, Wizara itaiwezesha ASA kuzalisha mbegu bora za soya tani 300 katika mashamba ya Mbozi (tani 100), Dabaga (tani 100) na Namtumbo (tani 100).

Zao la Shayiri

               349. Mheshimiwa      Spika,      katika      mwaka

2022/2023, Wizara kupitia TARI itazalisha tani 20.4 za mbegu ya shayiri katika eneo la hekta 8.8. Aidha, TARI itatunza vinasaba (germplasm) vya zao la shayiri ambapo jumla ya vizazi 56 vya shayiri vitafanyiwa tathmini kwenye mashamba ya majaribio yaliyopo Monduli, Karatu na Siha. Vilevile, TARI itaanzisha mashamba ya mfano katika Wilaya za Monduli, Karatu na Siha kwa lengo la kuwafundisha wakulima kuhusu kilimo bora cha shayiri. Pia, TARI itatoa mafunzo ya kilimo bora cha shayiri kwa wakulima 200 na maafisa ugani 20 katika Wilaya za Monduli, Karatu, Arumeru na Siha. 

Zao la Ngano

  • Mheshimiwa Spika, mahitaji ya ngano nchini ni tani 1,000,000 kwa mwaka wakati uzalishaji katika mwaka 2021/2022 ulifikia tani 70,288 ambapo tunaingiza kati ya tani 800,000 hadi 900,000 kwa mwaka na kutumia Shilingi 500,000,000,000. Ili kukabiliana na changamoto hiyo, Wizara imejiwekea lengo la kuzalisha tani milioni 1 ifikapo mwaka 2025, Wizara imepanga kugawa mbegu za ngano tani 7,200 zitakazopandwa katika eneo la hekta 60,000 ambazo zitazalisha tani 150,000 za ngano kwa kushirikiana na sekta binafsi.  
  • Vilevile,  itasimamia ufufuaji wa mashamba ya ngano yaliyopo katika mikoa ya Manyara, Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Njombe, Rukwa, Mbeya na Katavi yenye jumla ya hekta 40,200.  Ufufuaji wa mashamba katika mikoa hiyo, utaenda sambamba na uanzishwaji wa mashamba mapya katika mikoa ya Songwe na Dodoma (Bahi).  
  • Mheshimiwa Spika, pia, TARI itatafiti mbegu bora za ngano zenye sifa ya kustahimili maeneo ya joto na baridi, zinazokomaa mapema na kiwango cha protini aina ya gluteni kinachohitajika kwa uokaji. Vilevile, Wizara itawezesha ASA kuzalisha mbegu za ngano tani 700 katika mashamba ya Arusha (tani 350) na Dabaga (tani 350). Vilevile, TARI itazalisha tani 635 za mbegu ya ngano katika eneo la hekta 282 kupitia vituo vya TARI vya Selian, Uyole na Kifyulilo. Jumla ya shilingi Milioni 400 zimetengwa kwa ajili ya utafiti na uzalishaji wa mbegu.

5.5.4. Mazao ya Bustani

  • Mheshimiwa Spika, Mazao ya bustani ni pamoja na mboga, matunda, maua na viungo. Sekta ya mazao ya bustani ni moja ya sekta zinazokua kwa haraka kati ya asilimia 9 hadi 11 ikilinganishwa na sekta ya mazao ambayo ukuaji wake ni kati ya asilimia 4 hadi 5 kwa mwaka.  
  • Vilevile, kilimo cha mazao ya bustani hutoa ajira za moja kwa moja  na zisizo za moja kwa moja kwa watu takriban milioni 6.5 na ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi jumuishi kutokana na kuvutia wanawake na vijana katika tasnia hiyo. Aidha, mazao ya bustani yana mchango mkubwa katika kukabiliana na changamoto za utapiamlo.355. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2022/2023 Wizara imelenga kuimarisha uzalishaji wa mazao hayo kutoka tani 7,304,722.5 mwaka 2021 hadi tani 8,500,000 mwaka 2022. Ili kufikia lengo hilo, Wizara itasimamia uzalishaji na matumizi ya miche na vipando bora, kudhibiti visumbufu vya mazao, kutoa mafunzo kwa wakulima, kujenga miundombinu ya kuhifadhi mazao ya bustani, vituo vya huduma za pamoja (common use facilities) na vyumba vya ubaridi (cold rooms) katika maeneo ya uzalishaji.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Sekta Binafsi itajenga Common Use facilities tatu (3) katika mikoa ya Iringa (Mufindi), Dar es salaam (Kurasini – EPZA na Kilimanjaro (Hai). Aidha, Wizara inakamilisha taratibu za kupata ardhi kwa ajili ya uwekezaji huo. Vituo hivyo vitafanya kazi za kuchambua, kupanga, kufungasha na kusafirisha mazao yakiwa na alama ya “Produce of Tanzania”. Jumla ya Shilingi Bilioni 6.2 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo hivyo.
  • Mheshimiwa Spika, hatua hii ya Serikali ni kulinda zao la parachichi ambalo limekuwa likinunuliwa hapa nchini na shughuli za kufungasha zinafanyika nchi nyingine na zao letu linaondoka bila alama ya Tanzania. Miundombinu hii itajengwa na kukabidhiwa Sekta Binafsi kuiendesha na Serikali itaingia mikataba na waendeshaji ili kurudisha gharama za uwekezaji.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia TOSCI itasimamia usajili wa wazalishaji wa miche ya parachichi na kuwapa cheti cha kuwa wazalishaji kwa lengo la kudhibiti ubora na kuongeza uzalishaji wa mazao ya bustani hususan matunda na hivyo kuondoa tatizo la uzalishaji wa miche holela ili kama Taifa tusirudie tatizo lililojitokeza katika mazao kama machungwa, nanasi na embe ambayo tumekuwa tukilaumiwa kuwa hayakidhi mahitaji ya viwanda wala masoko ya kimataifa. Miche hiyo itasambazwa kwa wakulima kwa bei ya ruzuku.
  • Vilevile, Wizara itatoa mwongozo wa usimamizi na biashara ya zao la parachichi ili kumlinda mkulima, mnunuzi na mchakataji. Mwongozo huo utazinduliwa Julai, 2022 na kutoa dira na mwelekeo wa namna bora ambayo biashara ya parachichi itaendeshwa ili kuondoa tatizo la uvunaji wa parachichi ambazo hazijakomaa na kuzipeleka sokoni kwani jambo hilo linahatarisha ustawi wa biashara ya parachichi. Na baada ya mwongozo kutolewa yeyote atakayevuna parachichi ambazo hazijakomaa atachukuliwa hatua za kisheria.

Matarajio ya uzalishaji wa mazao ya kipaumbele ya bustani ni kama ifuatavyo:

Zao la Parachichi

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Sekta Binafsi itaendelea kuhamasisha wadau kuongeza uzalishaji wa zao la parachichi kutoka tani 190,000 mwaka 2018 hadi kufikia tani 215,000 mwaka 2022/2023.  Lengo hilo litafikiwa kwa kuimarisha upatikanaji wa pembejeo kwenye mashamba ya uzalishaji wa zao la parachichi, udhibiti wa visumbufu na kuimarisha huduma za ugani kwenye mashamba ya parachichi ya takriban hekta 46,002.
  • Aidha, Wizara  itawatambua na kuwasajili wazalishaji wa miche ya parachichi. Vilevile, Wizara itaendelea kushirikiana na TAHA na wadau wengine wa zao la parachichi katika utafiti, upatikanaji wa takwimu na kutafuta masoko ya mazao ya bustani. Pia, Wizara itaiwezesha TARI kupitia Vituo vya TARI Uyole na TARI Tengeru kuzalisha wa miche 20,000,000 zitakazotosheleza eneo la hekta 114,285.72. Miche hiyo itasambazwa kwa wakulima kwa bei ya ruzuku isiyozidi Shilingi 2,000 kwa mche. 

Zao la Vitunguu 

362. Mheshimiwa Spika, Wizara imepanga kuongeza uzalishaji wa zao la vitunguu kutoka tani 270,800 mwaka 2018/2019 hadi tani

320,640 mwaka 2022/2023. Ili kufikia lengo hilo, Wizara itawezesha ujenzi wa mabwawa ya kimkakati katika miradi ya umwagiliaji ya Mboli (hekta 500), Idodoma (hekta 800), Kisese (hekta 2,000), Msingi (hekta 1,200), Mughamo (1,200), Skimu za bonde la Eyasi (hekta 5,291), Tumati (hekta 270), Mongahay (hekta 300) na Tlawi (hekta 300). Pia, itajenga ghala 16 zenye uwezo wa kuhifadhi tani 144,000 na kusimikwa mashine 16 za kuratibu kiwango cha unyevu katika maeneo ya uzalishaji. 

Zao la Pilipili Kichaa

363. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendeleza zao la pilipili kichaa ambapo bei yake katika soko la dunia imefikia Dola za Marekani 9,324 kwa tani mwaka 2021/2022. Kutokana na fursa hiyo, Wizara itahamasisha uzalishaji wa zao la pilipili kichaa kutoka tani 7,270 mwaka 2018/2019 hadi tani 7,561 mwaka 2022/2023 kwa kuongeza eneo la uzalishaji kutoka hekta 4,038.9 hadi hekta 4,846.7. Pia, itahamasisha kilimo cha mashamba ya pamoja (block farming) kwa zao la pilipili kichaa kwa kuainisha mashamba na kujenga miundombinu ya kukausha na kuhifadhi katika mashamba hayo.

Zao la Zabibu

  • Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha uzalishaji wa zao la zabibu kutoka tani 16,138.8 mwaka 2018/2019 hadi tani 17,430 mwaka 2022/2023 kwa kuongeza eneo la uzalishaji kutoka hekta 3,426 hadi hekta 3,700. Vilevile, itaendelea kuhamasisha ufufuaji wa mashamba ya Mradi wa Umwagiliaji wa Zabibu Chinangali II, Gawaye, Hombolo na Dabalo pamoja na kuimarisha upatikanaji wa masoko ya zabibu. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha uwekezaji wa viwanda vidogo vya kusindika zabibu na kuongeza uzalishaji na tija kutoka tani 6.25 kwa hekta hadi kufikia tani 10 kwa hekta kwa kuimarisha huduma za ugani na kuimarisha uwezo wa TARI-Makutupora kuongeza uzalishaji wa miche kutoka 120,685 hadi 2,000,000 kwa msimu.  
  • Aidha, katika kuongeza thamani, kipato kwa mkulima na kupunguza upotevu wa zao la zabibu, Wizara itanunua mashine tatu (3) za kusindika zabibu ghafi ambapo mashine hizo zitasimikwa katika mkoa wa Dodoma.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kupitia TARI itakamilisha tathmini ya kubaini utofauti, usawa na uthabiti kwa aina tano (5) za mbegu bora za mizabibu ambapo TARI kwa kushirikiana na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu (TOSCI) watahitimisha utambuzi wa muda wa kuchipua (sprouting time) na muda wa kutoa maua (time of flowering) kwa aina hizo tano za mbegu. Pia, Wizara kupitia TARI itaendesha mafunzo ya kanuni bora za kilimo cha zabibu kwa wakulima 2,000 na maafisa ugani 50 katika wilaya zote za Mkoa wa Dodoma.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika itaimarisha maendeleo ya ushirika katika tasnia ya zabibu kwa kuongeza idadi na Thamani ya Hisa za Wanachama angalau kwa asilimia 25. Pia, Wizara itahamasisha uanzishwaji wa mashamba ya pamoja (block farming) ya zabibu ili kurahisisha utoaji wa huduma za ugani. Vilevile, Wizara itaweka mazingira bora ya uwekezaji katika tasnia ya zabibu na kuhimiza kilimo cha mkataba ili kumhakikishia mkulima soko la uhakika.

Zao la Ndizi

369. Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha uzalishaji wa zao la ndizi kibiashara kutoka tani 1,400,000 mwaka 2021/2022 hadi tani 4,604,220 mwaka 2022/2023. Ili kufikia lengo hilo, Wizara itaimarisha udhibiti wa visumbufu vya zao la migomba hususan magonjwa yanayoshambulia zao hilo. Vilevile, usambazaji wa miche bora 5,000,000 ya migomba utafanyika katika maeneo ya uzalishaji. Aidha, Wizara itatoa mafunzo kuhusu uendelezaji wa zao la ndizi kwa wakulima na Maafisa ugani pamoja na kuboresha mifumo ya masoko.

5.6. Upatikanaji wa Masoko ya Mazao ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao ya kilimo ndani na nje ya nchi kwa kufanya savei na kuimarisha mifumo ya utoaji wa taarifa za masoko.  Vilevile, Wizara itahamasisha uwekaji wa chapa (branding) kwa bidhaa zinazozalishwa na kuuzwa nje ya nchi ili kuzitambulisha na kuzitofautisha na bidhaa kutoka nchi zingine. Aidha, Wizara itatoa mafunzo kuhusu kilimo biashara na mifumo ya masoko kwa Maafisa ugani 600 na wakulima 2,000 katika mikoa 26. 
  • Vilevile, itakamilisha ujenzi wa masoko ya kimkakati matano (5) yaliyokuwa chini ya mradi wa DASIP. Masoko ya DASIP yapo katika Wilaya za Kahama, Ngara, Kyerwa, Tarime na Karagwe. Aidha, Wizara itaanzisha mnada wa chai katika eneo la Kurasini Mkoani Dar es salaam pamoja na kuanzisha kituo cha huduma za biashara ya mazao ya kilimo kitakachojengewa miundombinu ya kuhifadhi ili kurahisisha biashara ya mazao ndani na nje ya nchi. Vilevile, mauzo ya mazao kupitia vyama vya ushirika yataimarishwa kwa kujenga ghala chini ya mpango utakaohusisha Tume ya Maendeleo ya Ushirika na benki ya NMB.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaanzisha mnada wa chai eneo la Kurasini Dar es Salaam pamoja na kuanzisha kituo cha huduma za biashara ya mazao ya kilimo kitakachojengewa miundombinu ya uhifadhi. Lengo ni kurahisisha biashara ya mazao ndani na nje ya nchi na kuunganisha na Bandari ya Dar es salaam kwa kuwa na Green belt kwani sasa kusafirisha mazao ya kilimo kupitia bandari ya Dar es saalam imekuwa tatizo kubwa linalopelekea Sekta Binafsi kutumia bandari ya Mombasa.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaimarisha mauzo ya mazao ya kilimo kupitia vya Vyama vya Ushirika kwa kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuanza kutekeleza makubaliano kati ya Benki ya NMB na Tume ya Maendeleo ya Ushirika ya kujenga ghala zenye thamani ya Shilingi Bilioni 20 katika mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mtwara na Kagera, ili kukabiliana na changamoto ya ghala kwenye mazao ya korosho, pamba na kahawa.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia NFRA itanunua na kuhifadhi tani 160,000 za nafaka na itaendelea kutoa taarifa za uzalishaji wa mazao ya chakula na upatikanaji wake sambamba na kubaini maeneo yenye upungufu wa chakula kwa lengo la kuchukua hatua stahiki. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mazao Baada ya Kuvuna (2019 – 2029) ambapo Maafisa viungo wa Majukwaa ya Wilaya ya Usimamizi wa Mazao baada ya kuvuna watapewa mafunzo kuhusu usimamizi na uendeshaji wa majukwaa hayo. Pia, itakamilisha tathmini ya hali ya upotevu wa mazao ya chakula nchini kwa lengo la kuweka mikakati thabiti ya kupunguza upotevu na kuimarisha usalama wa chakula nchini.
  • Vilevile,katika kuimarisha upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi, Wizara itaimarisha huduma ya Internet katika vituo vyake vya Afya ya Mimea vilivyopo mipakani; itatoa elimu kwa watumiaji wa mfumo wa Agriculture Trade Management Information System (ATMIS).  
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia mradi wa TANIPAC itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Udhibiti wa Visumbufu Kibaolojia (Kibaha) kwa ajili kuimarisha utafiti na uzalishaji wa wadudu rafiki ili kudhibiti visumbufu vya mazao. Vilevile, itaendelea na ujenzi wa Kituo Mahiri (Mtanana – Kongwa) ambacho kitatumika kusambaza teknolojia za hifadhi na usindikaji wa mazao ya chakula pamoja na kuboresha biashara ya mazao. Pia, itaaanza ujenzi wa Maabara Kuu ya Kilimo kwa ajili ya kupima kiwango cha sumukuvu katika mazao ya mahindi na karanga. Jumla ya Shilingi Bilioni 36,130,190,912.75 zitatumika kukamilisha ujenzi huo.
  • Mheshimiwa Spika, TANIPAC itaendelea kutoa mafunzo kuhusu uzalishaji na hifadhi bora wa mazao ya mahindi na karanga kwa viongozi, waandishi wa habari, wakulima na wasafirishaji wa mazao kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kudhibiti maambukizi ya sumukuvu. 
  • Mheshimiwa Spika, ili kuwahakikishia wakulima wetu soko la mazao ya kilimo, NFRA kwa mwaka 2021/2022 imeuza tani 19,601.141 ili kupambana na mfumuko wa bei hatua iliyochangia bei ya mahindi kushuka. Katika mwaka 2022/2023, NFRA itanunua tani 100,000 za nafaka na utaratibu huu wa kununua na kuuza tutaendelea kuutumia pale ambapo bei ya mazao inashuka ili kumlinda mkulima, kuhifadhi na kuuza pale ambapo bei ya chakula inapopanda kumlinda mlaji.

5.7. Taasisi za Fedha na Upatikanaji wa Mitaji

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kushirikiana na taasisi za fedha katika kuimarisha utoaji wa mikopo yenye riba nafuu katika sekta ya kilimo. Aidha, benki za TADB, CRDB na NMB zimepanga kutoa mikopo yenye riba nafuu katika sekta ndogo ya mazao. Aidha, Wizara imepanga kujadiliana na Benki Kuu na Wizara ya Fedha ili kuangalia mfumo bora ambao utaiwezesha Sekta ya Kilimo kupata mitaji. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imepanga kujadiliana na Wizara ya Fedha na Mipango na Benki Kuu ya Tanzania ili kuangalia mfumo bora ambao utaiwezesha Sekta ya Kilimo na wakulima wadogo kupata mitaji kwani mfumo wa sasa wa ukopeshaji wa Taasisi za Fedha unaendeshwa zaidi na mfumo wa kibiashara unaozingatia dhamana isiyohamishika, mtiririko wa fedha (Cashflow) na dhamana iliyosajiliwa (registered assets). Utaratibu huo unakinzana na shughuli za kiuchumi za wakulima ambazo zinaendeshwa zaidi na mfumo ambao Taasisi za Fedha na sheria za ukopeshaji katika nchi yetu haziutambui.
  • Aidha, siyo rahisi kwa mkulima kukopeshwa kwa hati yake ya kimila na dhamana ya mazao yake. Jambo hili litakuwa ni moja ya vipaumbele vya Wizara kutaka mabadiliko katika mfumo wa ukopeshaji nchini.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kwa kushirikiana na TIRA itaendelea kukamilisha skimu kwa ajili ya Bima ya mazao ambayo itamlinda mkulima kuanzia shambani, uhifadhi na sokoni ili kuzifanya Taasisi za Fedha iwe rahisi kumpatia mikopo pale anapohitaji.
  • Vilevile, Wizara kupitia AGITF imepanga kutoa mikopo 285 yenye thamani ya Shilingi 7,450,000,000 inayojumuisha ununuzi wa matrekta makubwa, matrekta ya mikono, viuatilifu, mashine za kuongeza thamani ya mazao, viwanda vidogo vya usindikaji, ukarabati wa zana za kilimo, gharama za uendeshaji wa shamba na miundombinu ya shamba. 

5.8. Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itakamilisha utaratibu wa kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo. Mfuko huo utatumika kutoa ruzuku ya pembejeo; kuwezesha uhimilivu wa bei za mazao kutokana na athari za majanga, mdororo wa uchumi; na kugharamia uwekezaji katika miundombinu ya uzalishaji, uongezaji wa thamani na uhifadhi wa mazao ya kilimo.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara inakadiria kutumia Shilingi Bilioni 150 ambapo zitatumika njia mbalimbali za kupata fedha hizo ikiwemo ugharamiaji kupitia mapato yatokanayo na mauzo ya mazao. Katika kutekeleza hilo, Serikali haitohitaji kutoa fedha taslim bali mazao yenyewe yatajigharamia kupitia mfumo wa mazao kujihudumia yenyewe (own crop financing)

5.9. Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya

Hifadhi ya Mazao ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, idadi ya ghala zilizopo kwa ajili ya kuhifadhi mazao nchini  ni 3,473 zenye uwezo wa kuhifadhi tani 3,051,407 za mazao. Kati ya ghala hizo, ghala 3,099 zinatumika na ghala 374 hazitumiki kutokana na uchakavu. Aidha, idadi ya ghala zinazotumika hazitoshelezi mahitaji ya hifadhi ya chakula nchini na hivyo kusababisha upotevu wa mazao baada ya kuvuna kati ya asilimia 35 hadi 40.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imepanga kujenga ghala zenye uwezo wa kuhifadhi kati ya tani 300 hadi tani 1,000 katika maeneo ya uzalishaji. Katika mwaka 2022/2023, kwa kuanzia Wizara imepanga kuongeza uwezo wa kuhifadhi na kupunguza upotevu wa mazao kwa kujenga ghala 70 zenye uwezo wa kuhifadhi tani 1,000 kila moja. Ghala hizo zitajengwa katika mikoa ya Ruvuma (32), Tabora (22), Singida (8) na Dodoma (8). Jumla ya Shilingi 25, 169,500,000 zitatumika katika mpango huo.  
  • Vilevile, Wizara itakamilisha ujenzi wa ghala tisa (9) na vihenge 56 vya kisasa kupitia Mradi wa

Kuongeza Uwezo wa Kuhifadhi wa NFRA; itakamilisha ujenzi wa ghala 14 kupitia mradi wa TANIPAC; na itakamilisha ujenzi wa ghala la Mtimbila AMCOS lililopo Malinyi na ghala la Kijiji cha Mkula lililopo Ifakara. Aidha, itakamilisha ukarabati wa ghala 17 zilizopo katika

Halmashauri za Songea (10) na Madaba (7).

5.10. Kuhamasisha Kilimo cha Mashamba

Makubwa

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itasimamia ufufuaji na uendelezaji wa mashamba makubwa ya mazao ya kilimo kwa lengo la kuendeleza uwekezaji katika mazao  ya mbegu za mafuta, nafaka na mazao ya bustani. Hatua hiyo itachochea jitihada za Serikali za kuimarisha uzalishaji na tija kwenye kilimo, upatikanaji wa pembejeo na kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kisasa. Mashamba hayo ya pamoja yataanzishwa kwa mifumo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mfumo wa ushirika au uwekezaji binafsi.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itahamasisha uwekezaji katika mashamba yaliyokuwa chini ya National Agriculture and Food Corporation – NAFCO yaliyopo West Kilimanjiro ambayo hayajabinafsishwa yakiwemo Foster’s lenye hekta 290.8, Harlington lenye hekta 494.8, Journeys’ End lenye hekta 668 na Kanamodo lenye hekta 881.2 pamoja na shamba la Basotu lenye hekta 5,318. Mashamba mengine ni ya NAFCO yaliyopo Hanang’ ambayo yamebinafsishwa yakiwemo Murjanda (hekta 6,330), Setcheti (hekta 6,300), Gidagamwl (hekta 5,160) na Mulbadaw (hekta

5,490). 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo kwa kushirikia na Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara itahamasisha ufufuaji wa mashamba saba (7) ya maua yaliyofungwa kutokana na kushindwa kuendelezwa na makampuni yaliyokuwa yanazalisha maua.  Mashamba hayo ni Malalua Arusha hekta 594.4; Longido USA River hekta 83.6; Nduruma hekta 37.6; Nduruma Mangushi Farm hekta 46.1; USA River Dolly Farm hekta 20; Maji ya Chai hekta 45.6  na Chama Tengeru hekta 15.96. 
  • Mheshimiwa Spika, uendelezaji wa mashamba hayo utawezesha upatikanji wa huduma za ugani na pembejeo kwa gharama nafuu na kuchochea uanzishwaji wa vyama vya ushirika na hivyo kuongeza uzalishaji, tija na faida katika shughuli za kilimo. Utekelezaji wa mpango huo utafanikisha azma ya Wizara ya kuwavutia vijana kuwekeza katika kilimo kupitia programu ya Jenga Kesho Bora (Building a Better Tomorrow) kwa kuwahakikishia upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo.
  • Vilevile, Wizara itatekeleza mpango wa kuainisha, kupima, kutenga na kulinda ardhi ya kilimo kwa lengo la kuwa na benki ya ardhi kwa ajili ya uwekezaji wa mashamba makubwa yatakayojengewa miundombinu muhimu. Jumla ya Shilingi 3,000,000,000 zimetengwa kwa ajili ya kuanza kutekeleza mpango huo.

5.11. Kuimarisha Kilimo Anga 

395. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itakamilisha utaratibu wa ununuzi wa ndege moja (1) mpya na kukamilisha ukarabati wa ndege moja (1) ya kufanya savei ya visumbufu vya mimea na mazao ili kuondoa tatizo la kutegemea ndege za nje kwa ajili ya udhibiti wa

visumbufu vya mazao. Jumla ya Shilingi 3,000,000,000 zimetengwa kwa ajili ya mpango huo. Vilevile, pikipiki tano (5) zitanunuliwa ili kukijengea uwezo wa kudhibiti milipuko ya visumbufu Kituo cha Kilimo Anga. Pia, itanunua gari moja (1) kwa ajili ya kituo cha kudhibiti milipuko ya panya na kununua viuatilifu vya kudhibiti milipuko ya visumbufu vya mazao. Aidha, itafanya ukarabati wa Ofisi saba (7) za kanda, maabara tatu (3), na vituo vinne (4) vya ukaguzi wa afya ya mimea vilivyopo. 

5.12.  Maendeleo ya Ushirika

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitiaTume itaendelea kuratibu uanzishwaji wa Benki ya Taifa ya Ushirika ili kuchochea maendeleo ya ushirika nchini; itafanya uthamini wa mali zinazomilikiwa na vyama vya ushirika kwa lengo la kutambua thamani halisi ya soko ya mali hizo na hivyo kuviwezesha vyama kufanya uwekezaji wenye tija.  Vilevile, Tume itaanzisha Mfuko wa Bima ya Akiba na Amana za SACCOS utakaotumika kama kinga ya akiba na amana za wanachama wa SACCOS ambao SACCOS zao zitashindwa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria. Aidha, itaimarisha udhibiti na usimamizi wa vyama vya ushirika kwa kutoa mafunzo kwa maafisa ushirika 226 na kununua magari manne (4) na pikipiki 50. Pia, Tume itatoa mafunzo kwa watendaji wa vyama vya ushirika juu ya matumizi ya Mfumo wa kielekroniki katika kusimamia vyama vya ushirika ili uanze kutumiwa na vyama.
  • Mheshimiwa Spika, Tume itahamasisha vyama vya ushirika kuanzisha Makampuni ili viweze kujiendesha kibiashara. Vilevile,  itaratibu chama kikuu cha TANECU kujenga kiwanda cha kubangua korosho katika Wilaya ya Newala chenye uwezo wa kubangua tani 3,500 za korosho kwa mwaka ambacho kitatoa ajira 500 kwa wananchi. Aidha, Tume itahamasisha vyama vya ushirika kufufua vinu vya kuchakata pamba vya Sola, Mugango, Buyagu (Sengerema) na Manawavilivyopo katika mikoa ya Simiyu, Mara na Mwanza mtawalia. Vinu hivyo  vitakuwa na uwezo wa kuchakata tani 10,000 (Manawa), 3,500 (Sola) na tani 10,000 (Mugango) za pamba na vitatoa ajira 720  kwa wananchi.. Aidha, itaimarisha usimamizi wa vyama vya ushirika kwa kununua magari manne (4) na pikipiki 50.
  • Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na wizi na ubadhirifu wa fedha na mali katika vyama vya ushirika, Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) litawezeshwa kufanya ukaguzi bila utegemezi wa michango ya vyama vya ushirika kwa kuliongezea bajeti ya matumizi ya kawaida kutoka Shilingi 1,000,000,000 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi 2,380,000,000 mwaka 2022/2023. Aidha, Jumla ya Shilingi 550,000,000 zitatumika kukarabati ofisi tano (5) za COASCO katika mikoa ya Dodoma, Shinyanga, Iringa, Mwanza na Mtwara ili kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kuongeza ufanisi kwenye ukaguzi wa vyama vya ushirika.

5.13. Ushiriki wa Vijana katika Sekta ya Kilimo

  • Mheshimiwa Spika, kwa nyakati tofauti kumekuwa na dhana kuwa vijana hawapendi kilimo. Ukweli ni kwamba vijana na wanawake ni nguvukazi inayotumika katika uzalishaji kwenye Sekta ya Kilimo kwa kuzalisha na kuuza mazao ya kilimo, uuzaji wa pembejeo na uchakataji wa mazao katika ngazi ya awali.
  • Changamoto zinazowakabili vijana ni pamoja na; ukosefu wa mitaji, upatikanaji wa ardhi ya kilimo, uhaba wa miundombinu ya umwagiliaji, ujuzi na kukosekana kwa mazingira bora yanayovutia vijana na wanawake kushiriki katika kilimo. 
  • Mheshimiwa Spika, kwa kutambua changamoto zinazowakabili vijana, Wizara imepanga kuongeza ajira 1,000,000 za vijana kwenye Sekta ya Kilimo ifikapo 2025 kwa kuanzisha programu ya vijana inayojulikana kama Build Today for a Better Tomorrow. Kupitia programu hiyo, Wizara itashirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na OR-TAMISEMI kutenga maeneo ya kilimo kwa ajili ya kuanzisha maeneo maalumu ya uwekezaji wa kilimo (Agriculture parks) na mashamba ya pamoja (block farms).
  • Mheshimiwa Spika, maeneo hayo yatajengewa miundombinu ya umwagiliaji na ghala za kuhifadhia mazao. Aidha, vijana watapatiwa teknolojia za kisasa za uzalishaji,  mitaji, pembejeo za kilimo na kuunganishwa na masoko. Maeneo yaliyoanza kutengwa ni pamoja na hekta 7,664 katika Halmashauri za Wilaya za  Chamwino (hekta 6,179.2) na Bahi (hekta 1,484.8) mkoani Dodoma. 
  • Mazao ya kipaumbele yatakayozingatiwa katika utekelezaji wa mpango huo ni pamoja na alizeti, soya, ngano, sukari na mazao ya bustani. jumla ya Shilingi 3,000,000,000 zimetengwa kwa ajili ya kuanza kutekeleza mpango huo ambapo kati ya fedha hizo Shilingi 1,000,000,000 zitatumika kama dhamana ya mikopo kwa vijana. Jukumu la Serikali kwenye eneo hili litakuwa ni kutafuta ardhi, kuisafisha, kuiwekea miundombinu inayohitajika na kuwagawia vijana kuanzia ekari 10 hadi 50 kutegemea na zao. Lengo ni kuwapatia vijana ajira na kipato cha uhakika. Programu hiyo kwa majaribio itaanza mkoa wa Dodoma ili kubadili fikra na dhana kuwa kilimo hakilipi.
  • Mheshimiwa Spika, pamoja na hatua hii, Wizara kupitia Tume ya Umwagiliaji itafanya kazi ya kutambua vijana waliojiajiri kwenye Sekta ya Kilimo wanaokabiliwa na changamoto za uwekezaji kwenye mifumo ya umwagiliaji na kuwawezesha. Kupitia Bunge lako Tukufu, ninaviomba viwanda vya plastiki vianze uzalishaji wa vifaa vya kilimo vya umwagiliaji ikiwemo mabomba, mabomba ya kumwagilia kwa njia ya matone na dam liners na sisi kama Wizara tutawapa kipaumbele wazalishaji wote wa vifaa hivyo ndani ya nchi.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara itakamilisha Mkakati wa Taifa wa Kushirikisha Vijana kwenye Kilimo Awamu ya Pili (National Strategy for Youth Involvement in Agriculture – NSYIA II 2022- 2027) baada ya Mkakati wa Awamu ya Kwanza kumaliza muda wake mwaka 2021. Katika kutekeleza programu ya “Building Today for a Better Tomorrow”, programu itazingatiautekelezaji wa masuala ya NSYIA II.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia mradi wa  TANIPAC kwa kushirikiana na SIDO itawajengea uwezo vijana 420 nchini kuhusu utengenezaji wa vihenge vya chuma kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa teknolojia hiyo katika maeneo ya uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula katika ngazi ya kaya na kuongeza ajira na kipato kwa vijana. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na SUGECO itazalisha  ajira 4,800 kupitia kilimo katika ekari 500 sawa na uwekezaji wa Shilingi Bilioni 6.5 ambazo ni  mkopo kutoka Benki ya NMB. Pia, SUGECO itatambua wakulima ili kuweza kusambaza tani 1,000 za mbegu bora za mahindi ya njano na meupe; na kusambaza tani 250 za mbegu bora ya ngano. 

5.14. Lishe

  • Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kutekeleza Mpango Jumuishi wa Kitaifa wa Masuala ya Lishe (2020/2021-2025/2026) kwa kutekeleza afua mbalimbali za kukabiliana na changamoto za lishe ikiwemo udumavu, ukondefu na upungufu wa wekundu wa damu. Katika mwaka 2022/2023, Wizara kupitia mradi wa Agriconnect itatekeleza kampeni ya kitaifa ya lishe yenye lengo la kuongeza uelewa wa masuala ya lishe ili kupunguza changamoto za lishe duni na kuongeza uhimilivu katika mifumo ya chakula nchini. Njia zitakazotumika kuelimisha jamii ni pamoja na; luninga, redio, mitandao ya kijamii na kuwekwa kwenye mabasi ya safari ndefu na fupi hususan daladala kuhusu maandalizi, mapishi sahihi ya vyakula ili kupunguza upotevu wa virutubishi na ulaji unaofaa. Jumla ya watu Milioni 32 wanatarajiwa kufikiwa ifikapo mwaka 2022/2023. 
  • Mheshimiwa spika, ili kuendelea kuboresha lishe, matatizo ya udumavu kwa watoto na uoni hafifu kwa watoto na watu wazima, TARI itaendelea kuzalisha miche bora ya viazi lishe 40,000 aina ya Ejumla, Mataya, Kabode, Jewel na Naspot 13 zenye vitamin A kwa wingi. Miche hiyo itasambazwa kwenye wilaya za Mbozi, Njombe na Songea, shule za msingi na sekondari, magereza na wakulima binafsi. Aidha, kwa kushirikiana na Sekta Binafsi itazalisha na kusambaza mbegu za mahindi lishe (Pro-Vitamin A maize) katika mikoa inayoongoza kwa udumavu ya Njombe, Iringa, songwe, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Rukwa ili kuhamasisha ulaji wa mahindi lishe katika mikoa hiyo. 
  • Vilevile, aina nane (8) za mahindi lishe zenye vitamin A, madini chuma na zinki kwa wingi zitawasilishwa TOSCI kwa ajili ya kuthibitishwa na kupasishwa ubora kwa matumizi ya wakulima na wadau wa mahindi. Aidha kwa kushirikiana na mradi wa Harvest-Plus itazalisha maharage lishe (Biofortified bean-TARI06, JESCA, Selian 14 na Selian 15) na kusambaza katika mikoa ya Kigoma, Kilimanjaro, Iringa na Arusha. 
  • Aidha, vituo vitano (5) vya kukusanyia mazao (collection centres) na miundombinu sita (6) ya kutunza baridi (cold rooms) itajengwa katika maeneo ya mradi (Nyanda za Juu Kusini) ili kupunguza upotevu na kuongeza kipato cha wakulima wadogo. Aidha, mamalishe 5,000 kutoka mkoa wa Mbeya watasajiliwa na kupatiwa mafunzo ya namna bora ya kuandaa chakula salama na chenye virutubishi pamoja na kuwapatia vibanda maalum vya mfano 35 na seti za vifaa vya jikoni 500 kwa ajili ya kuandaa na kuuzia vyakula.  

5.15. Matumizi ya Teknolojia na Mbinu za Kilimo Kinachohimili Mabadiliko ya Tabianchi 

411. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itasambaza Mwongozo wa Kilimo Kinachohimili Mabadiliko ya Tabianchi katika Halmashauri za Wilaya 30 na kusambaza teknolojia bora za kilimo kinachohimili athari za mabadiliko ya tabianchi katika Halmashauri za wilaya 10. Vilevile, Wizara itakamilisha Mkakati wa Kitaifa wa Kilimo Ikolojia Hai utakaosaidia kutoa dira na mwongozo wa kilimo ikolojia nchini. 412. Aidha, Wizara  itatoa mafunzo ya mbinu bora za kilimo kinachohifadhi mazingira na kusaidia vijiji 30 vinavyozunguka ziwa Manyara kwa kutengeneza Mipango ya Usimamizi wa

Mazingira.

5.16. Jinsia

413. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kujumuisha masuala ya jinsia katika miradi, mikakati na programu za kilimo kwa kuandaa Mwongozo wa Ujumuishwaji wa Masuala ya Kijinsia katika sekta ya kilimo (Guideline for Gender Mainstreaming in Agriculture Sector). Aidha, itafuatilia utekelezaji wa miradi ya TANIPAC na Agri-Connect ili kuhakikisha utekelezaji wake unazingatia masuala ya kijinsia kama ilivyopangwa. 

5.17. VVU na UKIMWI

414. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa afya itaendelea kutoa elimu kuhusu VVU na UKIMWI na kuhamasisha upimaji wa afya kwa wafanyakazi wa Wizara zaidi ya 950 ili kujua afya zao na kuzuia maambukizi mapya. Vilevile, Wizara itaendelea kuwahudumia watumishi 15 walioathirika.

6. SHUKRANI 

  • Mheshimiwa Spika, natoa shukrani za pekee kwa wakulima kwa kazi kubwa wanazofanya na kuendeleza kilimo na kuhakikisha usalama wa nchi kwani Taifa lolote haliwezi kuwa salama kama watu wake wana njaa. Ni wazi kuwa mafanikio ya kilimo yanatokana na juhudi za wakulima na ushirikiano wanaopata kwenye Serikali yao. Vilevile, niwape pole kwa maumivu waliyoyapata kwa msimu huu ulioisha kwa gharama za pembejeo kupanda, ninafahamu wamebeba mzigo mkubwa sana niwahakikishie Serikali ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan kuanzia tarehe 1 Julai, itawapatia ruzuku ya mbolea, ili kupunguza maumivu yaliyotokana na athari za UVIKO na vita inayoendelea ya Ukraine na Urusi na kamwe mama hatawaacha wanae wasononeke na washindwe kufanya shughuli zao takatifu za kilimo na utumishi wao kwa Taifa lao. 
  • Mheshimiwa Spika,  nitumie fursa hii kuwashukuru Wadau wa Maendeleo, Washirika wa Kibiashara, Sekta Binafsi, Taasisi za Fedha na Benki za Tanzania na kwa msisitizo TADB, NMB, CRDB kwa kukubali Benki hizi tatu kushusha riba kwa wakulima mpaka asilimia 9, ninawaahidi kama Waziri wa Kilimo, nitaendelea kushirikiana na ninyi na yeyote ambaye atakubali kutoa riba kwa wakulima kwa asilimia ya tarakimu moja na kupunguza masharti ya ukopeshaji ambayo siyo rafiki kwa mkulima.  
  • Mheshimiwa Spika,  niendelee kuyashukuru Mashirika ya Kimataifa, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambao wameshirikiana na Wizara katika kuleta maendeleo kwenye nchi yetu. Naomba kutaja baadhi ya Nchi na Mashirika ya

Kimataifa kama ifuatavyo: Washirika wa Kibiashara na Maendeleo wakiwemo Serikali za Vietnam, Israel, Japan, Marekani, Uingereza, Ireland, Malaysia, China, Indonesia, Korea ya Kusini, India, Misri, Kuwait, Ubelgiji, Ujerumani, Finland, Norway, Brazil, Uholanzi, Canada, Poland na Umoja wa Falme za Kiarabu.

  • Mheshimiwa Spika, ninayashukuru pia Mashirika na Taasisi za Kimataifa zifuatazo: WFP, FAO, USAID, UNDP, IFAD, AGRA, GIZ, Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika, IMF, AU, DFID, JICA, EU, ENABEL, UNICEF, CIMMYT, ICRISAT, ASARECA, KOICA, ICRAF, IITA, IRRI, ILRI na CABI. Nyingine ni EAC, SADC, SAGCOT, ACT, TPSF, AVRDC, KILIMO TRUST, CIP,

CIAT/PABRA, UNEP, WARDA, Shirika la Kudhibiti Nzige wa Jangwani (DLCO-EA), Shirika la Kudhibiti Nzige Wekundu (IRLCO-CSA) na HELVETAS.  Wadau wengine ni, Bill and Melinda Gates Foundation, TAHA, Gatsby Trust, Rockfeller Foundation, Clinton Foundation, Aga Khan Foundation, na Asasi zisizo za kiserikali nyingi ambazo hatuwezi kuzitaja zote hapa

  • Mheshimiwa Spika,  ninaomba nirejee kumshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maelekezo yake kwangu ya kusimamia Sekta ya Kilimo na msukumo wake wa kuipa Sekta ya Kilimo kipaumbele hususan katika utafiti na uzalishaji wa mbegu, umwagiliaji na huduma za ugani. Ninaahidi kuwa nitaendelea kuwa muaminifu, mtiifu na kutekeleza majukumu yangu ya Waziri wa Kilimo kwa bidii, weledi na uadilifu kwa maslahi ya nchi yetu.
  • Mheshimiwa Spika, nirejee pia kumshukuru Mhe. Anthony Peter Mavunde (Mb) Naibu Waziri wa Kilimo na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kwa ushirikiano wa dhati anaonipatia  katika kutimiza majukumu yangu ya uwaziri.
  • Aidha, kipekee nirudie kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Nzega Mjini kwa namna wanavyoniunga mkono na kunipa ushirikiano wa dhati katika kuleta maendeleo ya jimbo letu. 
  • Mheshimiwa Spika,  kilimo ni msingi mkuu wa historia ya ustaarabu wa binadamu, msingi mkuu wa uhuru kamili wa binadamu, msingi mkuu wa mabadiliko ya kiuchumi, msingi mkuu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia kwa Taifa lolote, familia yoyote ambayo haiwezi kulisha watu wake ni sawa na mtumwa aliyefungwa minyororo. Ili tuweze kuleta mapinduzi ya kiuchumi, mapinduzi ya viwanda, elimu bora kwa jamii yetu ni lazima tuwe na uhakika wa chakula, kujilisha, kuhifadhi na kulisha wengine ili kama Taifa tuwe na uwezo wa kujiamulia na kuwaamulia wengine kwa maslahi ya Taifa letu.
  • Mheshimiwa Spika,  sisi kama Taifa hatuuzi vifaru vya kivita, hatuuzi ndege, hatuuzi Artificial Intelligence technology, kitu pekee tunaweza kutoa kwa wingi duniani ni Chakula. Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonesha utashi wa kisiasa na utayari wa kuwekeza kwenye kilimo. Nitumie fursa hii kuwaomba watanzania wenzangu kuitumia fursa ya Awamu ya Sita kuwekeza katika sekta ya kilimo na kutumia fursa ya ukuaji wa idadi ya watu duniani kama eneo la sisi kuondoa umasikini wa watu wetu na kuifanya Tanzania kuwa ghala la chakula kwa kuwa tutakuwa na uwezo wa kulisha wengine.
  • Hivyo, ninaomba watanzania wote watambue kuwa kilimo ni biashara, kilimo ni maisha.
  • Mheshimiwa Spika,  kwa kutambua ukweli kuwa kilimo ni msingi wa ustawi wa maisha ya mwanadamu na kwa utashi wa kisiasa wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuendeleza kilimo, Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2022/2023 inalengo la kukuza uchumi wa nchi kwa kuwekeza fedha katika maeneo ya kipaumbele ambayo bajeti yake imeongezeka kama ifuatavyo:-

i. Uzalishaji wa mbegu kutoka Shilingi Bilioni

10.58 hadi Shilingi Bilioni 43.03; ii. Utafiti wa kilimo kutoka Shilingi Bilioni

11.63 hadi Shilingi Bilioni 40.7; iii. Umwagiliaji kutoka Shilingi Bilioni 46.5 hadi

Shilingi Bilioni 361.5; iv. Ujenzi wa ghala kutoka Shilingi Bilioni 2.02 hadi Shilingi Bilioni 25.16;

v. Kuimarisha huduma za ugani kutoka

Shilingi Bilioni 11.5 hadi Shilingi Bilioni 15; 

426. Mheshimiwa Spika, vilevile, bajeti ya mwaka 2022/2023 imejielekeza katika:

  1. Kutoa ruzuku ya mbolea kwa mazao yote;
  2. Kuendeleza mashamba makubwa na kuongeza ushiriki wa vijana kwenye kilimo; 
  3. Kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kugharamia Sekta ya Kilimo; 
  4. Kuanzisha Ofisi za umwagiliaji za Wilaya katika Halmashauri 146;
  5. kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula kutoka tani milioni 18.6 hadi tani milioni

20.23;

  • Kuongeza uzalishaji wa mazao yenye mahitaji makubwa hususan mazao ya

alizeti, ngano na chikichi;

  • kuongeza uzalishaji wa mazao ya bustani kutoka tani milioni 7.3 kufikia tani milioni

8.5; 

  • kuimarisha upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi; 
  • Kuongeza uzalishaji wa mazao ya kimkakati yakiwemo:

o Pamba kutoka tani 144,000 hadi tani

350,000o Korosho kutoka tani 238,000 hadi tani

400,000o Tumbaku kutoka tani 58,000 hadi

95,000;o Kahawa kutoka tani 65,235 hadi tani

72,000o Zabibu kutoka tani 16,138 hadi tani

17,430o Mkonge kutoka tani 36,169.8 hadi tani

60,000 o Chai kutoka tani 11,962 hadi tani 30,000 o Uzalishaji wa mbegu za mazao ya chakula na mafuta.

Makisio ya Mahitaji ya Mbegu bora

Na. Aina ya ZaoMakisio ya uzalishaji wa mazao msimu wa 2022/2023 (Tani)Mkadirio ya mahitaji ya Certified Seeds 2022/2023 (Tani)
 1Mahindi           7,219,000                32,500 
 2Alizeti              941,000                   5,600 
 3Soya              500,000                 25,000 
 4Ngano              150,000                   7,200
 5Mpunga           2,832,000                 16,000 
 JUMLA          11,642,000                 86,300

7. MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023

7.1.  Makusanyo ya Maduhuli

  • Mheshimiwa Spika, Wizara inatarajia kukusanya Shilingi  126,117,732,000  kutokana na vyanzo mbalimbali. Kati ya fedha hizo, Shilingi 17,732,000  zitakusanywa kupitia Fungu 43 na Shilingi 126,100,000,000 zitakusanywa kupitia Fungu Na.05. 
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Bajeti ya Wizara ya Kilimo imeongezeka kwa mafungu yote matatu kutoka Shilingi 294,162,071,000 hadi Shilingi  

751,123,280,000 sawa na ongezeko la asilimia

155.34 

429. Mheshimiwa Spika, Sehemu kubwa ya fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji, miundombinu ya uhifadhi wa mazao, kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao, kuimarisha utafiti wa kilimo, uzalishaji wa mbegu na utoaji wa ruzuku. 

7.2.  Fedha kwa Mafungu yote (43, 24 na  05)

430.   Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara ya Kilimo inaliomba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi 751,123,280,000 kupitia Fungu 43, Fungu 05 na

Fungu 24 kama ifuatavyo;

7.3.  Fedha kwa Fungu 43

431.   Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Wizara inaomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 368,561,661,000 kupitia Fungu 43 kwa ajili ya matumizi ya Kawaida na Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Shilingi 268,906,114,000 ni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo ambapo Shilingi 185,978,709,000 ni fedha za ndani na Shilingi 82,927,405,000 ni fedha za nje. Aidha, Shilingi 99,655,547,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, ambapo Shilingi 49,403,470,000 ni kwa ajili ya mishahara na Shilingi 50,252,077,000 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo.

7.4. Fedha kwa Fungu 05

432.   Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi 366,768,352,000 zinaombwa. Kati ya fedha hizo, Shilingi 361,500,000,000 ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambapo Shilingi 350,000,000,000 ni fedha za Ndani na Shilingi 11,500,000,000 ni fedha za nje. Aidha, kati ya fedha zinazoombwa, Shilingi 5,268,352,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo Shilingi 3,630,168,000 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Shilingi 1,638,184,000 ni kwa ajili ya Matumizi mengineyo.

7.5. Fedha kwa Fungu 24

  • Mheshimiwa Spika, jumla ya Shilingi 15,793,267,000 zinaombwa. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,100,000,000 ni kwa ajili kutekeleza

            Miradi       ya      Maendeleo      ambapo       Shilingi

550,000,000 ni kwa ajili ya Tume na Shilingi 550,000,000 ni kwa ajili ya COASCO. Aidha, kati ya fedha zinazoombwa Shilingi 14,693,267,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo  Shilingi 5,549,009,000 ni fedha za matumizi mengineyo ya Tume na Shilingi 5,115,312,000 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Tume. Aidha, Shilingi 2,380,000,000 ni kwa ajili ya Matumizi mengineyo ya COASCO na Shilingi 1,648,946,000 ni kwa ajili ya mishahara ya COASCO.

  • Mheshimiwa Spika, hotuba hii pia inapatikana katika tovuti ya Wizara: www.kilimo.go.tz 

8. HITIMISHO

435.   Mheshimiwa Spika, NAOMBA KUTOA

HOJA

VIAMBATISHO

Kiambatisho Na. 1: Aina Mpya za Mbegu Zilizoidhinishwa

NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
1Kampuni ya Corteva Agriscience Tanzania LimitedMahindiPAN 3M-05Inastawi katika ukanda wa chini na kati (mita 0 hadi 1,200) kutoka usawa wa bahari; Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.4 kwa hekta; Inakomaa kati ya siku 120- 180; Inastahimili magonjwa ya doajani (Grey Leaf Spot) na Tarcicum Blight; na Haijazalishwa kwa teknolojia ya Uhandisi Jeni (Non GM).
2Kampuni ya Corteva Agriscience Tanzania LimitedMahindiPAN 7M-87• Inastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 700 – 1,600) kutoka
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
          usawa           wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 7.7 kwa hekta; Inakomaa kwa wastani wa siku 140; Inastahimili magonjwa ya doajani (Grey       Leaf          Spot), Kutu (Rust) na kuoza kwa sikio ( Ear rot); Flint grain; na Haijazalishwa kwa teknolojia ya    Uhandisi Jeni (Non GM)
3Kampuni ya Meru AgroTours & Consultants Co LtdMahindiMERU     HB 505Inastawi katika ukanda wa kati       (mita          500- 1,200) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 7.5 kwa hekta;
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    Ina ukinzani dhidi ya ugonjwa wa doajani (Grey Leaf Spot), Inakomaa kwa wastani wa siku 140, Haijazalishwa kwa teknolojia ya Uhandisi Jeni (Non GM) 
4Taasisi      ya Utafiti      wa Kilimo (TARI)  ChorokoTARI-G- GRAM1Inastawi ukanda wa chini wa mita 200 kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kwa wastani wa siku 90; Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 0.8 kwa hekta; na Inastahimili magonjwa ya Yellow Mosaic Virus, Cercospora Leaf Spot na Anthracnose
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
   ChorokoTARI-G- GRAM2Inastawi ukanda wa chini wa mita 200 kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kwa wastani wa siku 90; Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 0.8 kwa hekta; na Inastahimili magonjwa ya Yellow Mosaic Virus, Cercospora Leaf Spot na Anthracnose.
5Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)  NganoTARI- WHEAT1Inastawi ukanda wa kati hadi wa juu (mita         1,0002,000) kutoka usawa         wa bahari;  Ina ukinzani dhidi ya kutu (stem rust); Ina ukinzani dhidi ya
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    kuanguka (Lodging) Ina kiwango kikubwa cha gluten (38.9%) Ina kiwango kikubwa cha protini (15.4%) Inakomaa kati ya siku 97-111; na Inatoa mavuno mengi kati ya tani 4.0 hadi 4.6 kwa hekta.
   TARI- WHEAT2Inastawi ukanda wa kati na juu (mita 1000-2000) kutoka usawa wa bahari;  Ina ukinzani dhidi ya kutu (stem rust); Ina ukinzani dhidi ya kuanguka (Lodging) Ina kiwango kikubwa cha gluten (38.9%)  Ina kiwango kikubwa cha
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    protini (15.4%) Inakomaa kati ya siku 97-111; na Inatoa mavuno mengi kati ya tani 3.3 hadi 4.0 kwa hekta.
6Taasisi ya Utafiti wa Tumbaku Tanzania (TORITA)TumbakuKRK 26 RInastawi ukanda wa chini na wa kati (mita 500 – 1,950) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 2.2 kwa hekta; Ina ukinzani dhidi ya ugonjwa wa Tobacco Mosaic Virus-TMV; na  Ina ukinzani dhidi ya Rootknot nematodes Meloidogyne incognita na Javanica.  
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
  TumbakuYUNNAN 85Inastawi ukanda wa chini na wa kati (mita 500 – 1,950) kutoka usawa wa bahari;  Ina   majani mapana; Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 1.7 kwa hekta; Ina ukinzani dhidi ya ugonjwa wa Tobacco Mosaic Virus-TMV; na Ina ukinzani dhidi ya Rootknot nematodes Meloidogyne incognita na Javanica;
7.Western Seed CompanyMahindiWH509Inastawi ukanda wa kati (mita 700 1,500) kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kwa
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    muda wa siku kati ya 140- 155; White         semi flint and heavy grain; Inastahimili magonjwa ya doajani (Grey leaf spot); Inatoa mavuno ya wastani wa tani 7.9 kwa hekta.
   WH605Inastawi ukanda wa kati (mita 1500 2200) kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kati ya siku 150- 170; White         semi flint and heavy grain; Inastahimili magonjwa ya doajani (Grey leaf spot); Inatoa mavuno ya wastani wa tani 7.6 kwa
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    hekta.
8Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI)  MpungaTARI-RIC3Inastawi ukanda wa chini na kati (mita 0 -1000) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 6.3 kwa hekta; Inakomaa kati ya siku 118- 127; Ina   harufu nzuri; Inakoboreka vizuri.
9Silverlands Ndolel LimitedViazi MviringoRodeoInastawi ukanda wa kati na    wa        juu (mita 1,200 – 2,400) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 35-50 kwa hekta; Ina kiwango kikbwa cha
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    wanga (22%); Inakomaa kati ya siku 110- 120; Inafaa kwa kupika na kusindika
   ChallengerInastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 1,200 – 2,400) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 35-50 kwa hekta  Ina kiwango kikubwa cha wanga (22.5%); Inakomaa kati ya siku 110- 120; Inafaa          kwa matumizi mbalimbali ikiwemo       kupikwa       au kusindikwa; Inaathirika na Blight kwenye
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    majani; na • Ina ukinzani dhidi ya Blight kwenye mizizi.
   VoyagerInastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 1,200 – 2,400) kutoka usawa wa bahari;  Inatoa mavuno mengi ya wastani wa tani 35-50 kwa hekta; Ina kiwango kikubwa cha wanga (22.5%); Inakomaa kati ya siku 110- 120; Inafaa kwa kupika na kusindika.
   MarkiesInastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 1,200 – 2,500) kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kati
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
    ya siku 115- 125; Inatoa mavuno mengi kati ya tani 40-50 kwa hekta; Ina ukinzani dhidi ya late blight na PCN; Viazi vinalingana ukubwa.
   ArizonaInastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 1,000 – 3,000) kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kati ya siku 105- 115; Inatoa mavuno mengi kati ya tani 40-50 kwa hekta Ina ukinzani dhidi ya PCN RO1 na 4; Viazi vinalingana ukubwa.  
NA.KAMPUNI/ TAASISIZAOJINA LA MBEGUSIFA
   ManitouInastawi ukanda wa kati na wa juu (mita 1,000 – 3,000) kutoka usawa wa bahari;  Inakomaa kati ya siku 105- 115; Inatoa mavuno mengi kati ya tani 40-50 kwa hekta Inastahimili magonjwa ya Common Scald na    PCN (RO1&4, 2&3).

KIAMBATISHO NA. 2: SKIMU ZA UMWAGILIAJI ZINAZOJENGWA NA

KUKARABATIWA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2021/2022

Na.MkoaWilayaJina la  SkimuEneo linalofaa kumwagiliwa (Ha)  Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
1.KigomaUjijiLuiche3,000Ujenzi wa skimu ya umwagiliajiMaandalizi ya hadidu za rejea yamekamilika baada    ya kupata kibali kutoka Kuwait Fund. Ujenzi utaanza mwaka wa fedha 2022/23.
2.IringaIringaMgambale nga3,000Ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliajiUjenzi utaanza baada               ya kukamilika taratibu               za manunuzi
3.Kilimanja roHaiMtambo1,920Ujenzi               wa Mfereji Mkuu, Vigawa maji na tuta la kuzuia mafurikoKatika mwaka wa fedha 2022/23 upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utafanyika kwa hekta 7,000 zinazofaa kwa umwagiliaji katika skimu ya Mtambo. Aidha, ukarabati mdogo wa skimu za umwagiliaji katika Wilaya ya               Hai utaendelea kufanyika kupitia               Mfuko wa               Maendeleo ya Umwagiliaji.
Na.MkoaWilayaJina la  SkimuEneo linalofaa kumwagiliwa (Ha)  Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
4.MorogoroMorogoroMsufini1,000Ukamilishaji wa miundombinu ya umwagiliajiMkataba kwa ajili        ya ukamilishaji wa miundombinu ya umwagiliaji umesainiwa.
5.TaboraNzegaNata900Ujenzi wa banio urefu wa mita 18  Kazi               ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itafanyika katika mwaka wa fedha 2022/23. Ujenzi   wa skimu utaanza baada upembuzi yakinifu kukamilika.
6.Kilimanja ro MwangaKirya800Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliajiUjenzi   na ukarabati umefikia asilimia 40
7.MbeyaKyelaMbaka600Ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliajiUjenzi utaanza   baada          ya kukamilika taratibu               za manunuzi
8.TangaKorogweMahenge480  Ujenzi            wa Mfereji Mkuu, Vigawa maji na tuta la kuzuia mafurikoKazi       ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itafanyika kwa kujumuisha skimu za bonde la Mkomazi katika mwaka wa fedha 2022/2023. 
9.TangaKorogweKwamkumbo        400Ukarabati               wa miundombinu ya umwagiliajiKazi       ya upembuzi yakinifu               na usanifu wa kina itafanyika kwa kujumuisha skimu za bonde
Na.MkoaWilayaJina la  SkimuEneo linalofaa kumwagiliwa (Ha)  Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
      la Mkomazi katika mwaka wa fedha 2022/2023. 
10.TangaLushotoKitivo/ Kituani Mwenzae400Kurudisha Mto Umba katika njia yake ya asiliKazi       ya kurudisha mto Umba katika njia yake ya asili imefikia asilimia 80.
11.TaboraNzegaIdudumo400Ujenzi                 wa miundombinu ya umwagiliajiKazi ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji inaendelea na imefikia asilimia 25
12.RuvumaSongeaMuhuk uru350Ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliajiUjenzi utaanza baada    ya kukamilika kwa taratibu za manunuzi
13.ManyaraHanang’Endagaw        276Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliajiUjenzi   na ukarabati umefikia asilimia 30
14.Tanga MkingaMwele 200Kufanya ukarabati               wa bwawa na ujenzi    wa miundombinu ya umwagiliajiUkarabati wa sehemu iliyoharibiwa na         mafuriko umekamilika  
15.KataviNsimboMsangi nya/ Usense106Ukamilishaji wa miundombinu ya umwagiliajiMkandarasi amekabidhiwa eneo la kazi kwa ajili ya utekelezaji.
Jumla13,832  

KIAMBATISHO NA 3: SKIMU ZA UMWAGILIAJI

ZILIZOFANYIWA UPEMBUZI YAKINIFU KATIKA MWAKA WA

FEDHA 2021/2022

Na.MkoaWilayaJina la SkimuEneo lililofanyiwa upembuzi yakinifu (Ha)Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
1.Iringa Iringa Mkomboz i10,000    Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiKazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imefanyika katika hekta 6,000. Ujenzi utafanyika katika mwaka wa fedha 2022/23.
2.Mwanza/ GeitaSengerem a/Geita Ibanda3,000Upembuzi yakinifu na usanifu wa bwawa na skimu Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imefikia asilimia 65.
3.Mbeya MbaraliMbuyuni Kim      ani3,000Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
4.Dodoma KongwaNgomai2,000Upembuzi yakinifu na usanifu wa bwawa na skimuKazi hii itafanyika katika mwaka wa fedha 2022/23
5.Mbeya MbaraliUturo2000Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
6.Mbeya MbaraliChosi 1,700Upembuzi yakinifu wa Skimu yaUpembuzi yakinifu na usanifu wa
Na.MkoaWilayaJina la SkimuEneo lililofanyiwa upembuzi yakinifu (Ha)Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
     umwagiliajikina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
7.Mbeya MbaraliMatebete         1,200Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
8.Mbeya MbaraliMakang arawe1100Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
9.Mbeya MbaraliIsenyela1,000Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
10.Rukw a Sumba wanga Ilemba 800Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 80. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
11.Manyara MbuluTlawi 650Upembuzi yakinifu na usanifu wa bwawa na skimuUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika
Na.MkoaWilayaJina la SkimuEneo lililofanyiwa upembuzi yakinifu (Ha)Kazi zilizopangwa kufanyikaHatua ya utekelezaji hadi Aprili, 2022
      mwaka 2022/23. 
12.Tabora NzegaIdudumo400Upembuzi yakinifu na usanifu wa bwawa na skimuKazi ya Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imekamilika na ujenzi unaendelea.  
13.Mbeya MbaraliHerman 400Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
14.Geita Chato Nyisanzi330Upembuzi yakinifu wa bwawaKazi hii itafanyika katika mwaka wa fedha 2022/23
15.Mbeya MbaraliGonakuvagogolo250Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 90. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
16.Mbeya Kyela Makwale 200Upembuzi yakinifu wa Skimu ya umwagiliajiUpembuzi yakinifu na usanifu wa kina umefikia asilimia 80. Ujenzi utafanyika katika mwaka 2022/23.
Jumla 28,030  

KIAMBATISHO NA. 4: SKIMU MPYA ZA UMWAGILIAJI

ZITAKAZOJENGWA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika
1.IringaIringa Mkombozi 6,000Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
2.ArushaKaratuSkimu za Bonde la Eyasi6,000Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
3.MbeyaMbarali Msesule 4,500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
4.KigomaUjijiLuiche 3,000Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
5.MorogoroKilosaRudewa 2,500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
6.MbeyaKyelaMakwale 2,500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
7.TaboraUyuiIgwisi2,500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
8.RukwaSumbawangaIlemba3,000Kujenga  bwawa na miundombinu ya skimu ya umwagiliaji
9.MwanzaSengeremaIsole1,000Kujenga  bwawa na miundombinu ya umwagiliaji
10.RudewaKilosaMorogoro2,500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
11.TaboraSikongeKalupale 2,000Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
12.KataviMpandaIloba  1,200Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
13.TaboraNzegaNyida/ Lyamalagw a 1,400Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
14.SingidaMkalamaMsingi1,200Kujenga  bwawa na miundombinu ya umwagiliaji
15.DodomaChamwinoMembe1,000Kujenga  miundombinu ya

247

Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika
     umwagiliaji
16.TaboraSikongeUlyanyama 1,100Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
17.Kilimanja roMoshiKimanga Mao1,250Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
18.Tabora  UyuiMwamabo ndo1,200Kujenga miundombinu ya umwagiliaji
19.MwanzaKwimbaMahiga 900Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
20.SimiyuBariadiKisoli634Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
21.MwanzaSengeremaKatunguru 800Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
22.MwanzaBushosaMaguru Kenda500Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
23.ManyaraMbuluTlawi 350Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
24.DodomaBahiKongogo 250Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
25.MaraRoryaRabour650Kujenga  miundombinu ya umwagiliaji
  Jumla 53,234 

KIAMBATISHO NA. 5: MABWAWA YA UMWAGILIAJI YALIYOPANGWA KUJENGWA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Na.MkoaWilayaJina la BwawaUjazo wa Bwawa (mita za ujazo)Kazi zitakazofanyika
1.ShinyangaShinyangaNyida 4,500,000 Ujenzi wa bwawa
2.KigomaUjijiLuiche 2,500,000Ujenzi wa bwawa
3.SingidaMkalamaMsingi1,875,000Ujenzi wa bwawa
4.RukwaSumbawa ngaIlemba3,250,000Ujenzi wa bwawa
5.SimiyuBariadiKasoli1,890,000Ujenzi wa bwawa
6.GeitaGeitaIbanda 6,350,000Ujenzi wa Bwawa
7.DodomaChamwinoMembe5,100,000Ujenzi wa Bwawa
8.MwanzaSengeremaKatunguru 2,150,000Ujenzi wa Bwawa
9.ManyaraMbuluTlawi 1,100,000Ujenzi wa Bwawa
10.TaboraSikongeUlyanyama 3,780,000Ujenzi wa Bwawa
11.TaboraSikongeKalupale 2,260,000Ujenzi wa Bwawa
12.TaboraUyuiIgwisi2,130,000Ujenzi wa Bwawa
13.DodomaMpwapwaMsagali92,000,000Ujenzi wa Bwawa
14.TaboraUyuiMwamabondo2,650,000Ujenzi wa Bwawa
 Jumla 131,535,000 

KIAMBATISHO NA. 6: SKIMU ZA UMWAGILIAJI ZILIZOPANGWA

KUBORESHWA, KUJENGWA NA KUKARABATIWA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika 
1.Morogo roMlimbaChita JKT6,000Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwa hekta 3,000 za mwanzo kati ya hekta 6,000
2.MbeyaMbaraliMadibira3,200Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji
3.IringaKiloloMgambalen ga3,000Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji
4.Morogor oMorogoro VijijiniTulo- Kongwa3,000Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
5.KataviTanganyik aKarema3,350Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
6.MbeyaMbaraliMbuyuni Kimani3,000Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
7.Morogo roKilomberoItete850Kufanya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
8. MbeyaMbarali Uturo2,000Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
9.MbeyaMbaraliChosi1,700Ujenzi na
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika 
     kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
10.Katavi  MpandaKabagwe 1,500Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
11.KataviMpandaMwamkulu1,500Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
12.Morogo roMorogoro VijijiniMsufini1,470Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
13.MbeyaMbaraliMatebete1,200Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
14. MbeyaMbaraliMakangara we1,100Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
15.Morogo roKilomberoIdete1,000Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
16.Morogo roMorogoroMbalangwe1,000Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
17.MbeyaMbaraliIsenyela1,000Ujenzi na kufanya
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika 
     ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji 
18.Kiliman jaroMwangaKirya800Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
19.Morogoro MvomeroMgongola620Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
20.MwanzaKwimbaKimiza600Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
21.KataviMpandaKabage1500Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
22.MbeyaMbaraliHerman400Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
23.KataviNsimboUsense300Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
24.RuvumaSongeaMuhukuru300Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
25.MbeyaBusekeloMbaka300Ujenzi na kufanya ukarabati wa
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo linalofaa kwa umwagiliaji (Ha)Kazi zitakazofanyika 
     miundombinu ya umwagiliaji
26.TaboraNzegaIdudumo300Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
27.ManyaraHanang’Endagaw276Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
28.MbeyaMbarali Gonakuvago golo250Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
29.Morogoro MorogoroKiroka180Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
30.IringaMafingaMtula75Ujenzi na kufanya ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji
 Jumla41,771 

KIAMBATISHO NA. 7: SKIMU NA MABWAWA YA UMWAGILIAJI

YALIYOPANGWA KUFANYIWA UPEMBUZI YAKINIFU NA USANIFU

Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo litakalofanyi wa usanifu (Ha)Kazi zitakazofanyika 
1.KataviMpimbweMwamapuli12,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina skimu
2.IringaKiloloNyanzwa9,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa na skimu 
3.MbeyaMbaraliUkwavila9,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
4.RukwaKalamboLegeza- Mwendo5,500Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa na skimu
5. SongweMombaNaming’ongo5,000Kufanya usanifu wa kina wa skimu  
6.DodomaBahiSkimu za bonde la Bahi5,000Kufanya usanifu wa kina wa skimu sita za bonde la Bahi
7.KageraKyerwa/ KaragweSkimu ya Gereza la Kitengule4,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina skimu
8.Mwanza SengeremaButonga- Nyamazuko3,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina skimu
9.Mwanza SengeremaIgaka- Bundala3,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo litakalofanyi wa usanifu (Ha)Kazi zitakazofanyika 
     bwawa na skimu
10.IringaKiloloMgambalen ga3,000Kufanya usanifu wa kina wa mindombinu ya umwagiliaji shambani
11.DodomaMpwapwaMlembule3,000Kufanya usanifu wa kina skimu
12.DodomaKondoaKisese 3,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa na skimu
13.PwaniRufijiNgorongo Mashariki na Magharibi3,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
14.KigomaKasuluAsante Nyerere 2,300Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
15.TaboraIgungaBwawa la Mwamapuli2,000Kufanya usanifu wa kina wa bwawa
16.GeitaNyang’wale Nyamgogwa2,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina skimu
17.SingidaIrambaTyeme- Masagi 2,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa na skimu
18.Mwanza/ GeitaSengerema / GeitaIbanda1,500Kukamilisha usanifu wa kina wa bwawa na skimu 
19.KigomaKasuluKilimo Kwanza1,500Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo litakalofanyi wa usanifu (Ha)Kazi zitakazofanyika 
20.KageraBiharamuloMwiruzi1,300Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu
21.ArushaArumeruSkimu za Mto Themi1,200Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
22.MorogoroKilosa Rudewa1,000Kufanya usanifu wa kina wa mindombinu ya umwagiliaji shambani
23.TaboraNzegaNata900Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu
24.IringaIringa Mangalali750Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
25.IringaIringaLipuli560Kufanya  upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
26.DodomaMpwapwaKizi500Kufanya usanifu wa kina wa skimu
27.KigomaKakonkoMuhwazi500Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
28.GeitaChatoMasasi350Kufanya usanifu wa kina wa bwawa na skimu
29.KigomaKakonkoRuhuru350Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
30.ManyaraMbuluDirim335Kufanya usanifu wa kina wa bwawa na skimu
32.KigomaKakonkoRuhwiti300Kufanya usanifu
Na.MkoaWilayaJina la skimuEneo litakalofanyi wa usanifu (Ha)Kazi zitakazofanyika 
     wa mindombinu ya umwagiliaji
33.KigomaKakonkoKatengera300Kufanya usanifu wa mindombinu ya umwagiliaji
34.KigomaKakonkoMgunzu300Kufanya usanifu wa mindombinu ya umwagiliaji
35.KigomaKakonkoKanyonza300Kufanya usanifu wa mindombinu ya umwagiliaji
36.MorogoroMpwapwaChitemo 250Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa na skimu
37.KigomaKakonkoLukoyoyo200Kufanya usanifu wa mindombinu ya umwagiliaji
38.KigomaKakonkoChulanzo200Kufanya usanifu wa mindombinu ya umwagiliaji
39.NjombeNjombe Itipingi162Kufanya usanifu wa kina skimu
40.MtwaraNanyambaArusha Chini120Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
41.SongweMombaKasinde2,000Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
42.GeitaBukombeNampangwe350Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu
 Jumla91,357 

Kiambatisho Na. 8 Mikakati ya Kuongeza Uzalishaji wa Sukari katika Viwanda Vilivyopo Nchini

Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
1.Kilombero Sugar Co. LtdUpanuzi wa kiwanda unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani 126,000 za sasa hadi tani 271,000 ifikapo 2025/2026. Ongezeko hili ni la tani 145,000 sawa na asilimia 115.1 ya kiasi kinachozalish wa sasa na kiwanda hiki. Uzalishaji wa miwa ya wakulima wadogo utaongezeka kutoka tani 800,000 hadi tani 1,700,000Mchakato wa kupata wakandarasi wa kujenga kiwanda umekamilika. Uhamasishaji kwa wakulima watakaopeleka miwa katika kiwanda kipya umefanyika. Ajira za maafisa ugani watakaohudumia meneo mapya ya wakulima watakaolima kwa ajili ya kiwanda kipya umekamilika Ujenzi wa msingi wa Kiwanda (Foundation) umeanza      Kitalu A cha mbegu kwa ajili ya wakulima wapya kimetayarishwa  
Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
  (iv)       Uzalishaji wa        umeme utaongezeka kutoka megawati 8.3 za sasa hadi kufikia megawatt 25 
2Kagera Sugar LtdUpanuzi    wa shamba unaotarajiwa kuongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani 95,000 za sasa hadi tani 170,000           za sukari ifikapo 2024/2025. Ongezeko hili ni la tani 75,000 sawa na asilimia         78.9%          ya kiasi kinachozalish wa sasa na kiwanda hiki. Eneo lenye ukubwa wa hekta 13,000 linatarajiwa kulimwa    na kupandwa miwaJumla ya hekta 5,300 zimelimwa kati ya lengo la kulima hekta 13,000 katika shamba jipya la Kitengule na hekta 5,100 zimepandwa Katika eneo lililolimwa, jumla ya hekta 4,700 zimepandwa miwa. Ujenzi wa “mill zero umekamilika Ujenzi wa mtambo wa kufua umeme umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95.  Daraja la kuunganisha shamba la Kitengule na Kangundu kilipo kiwanda kwa sasa limekamiika na kuzinduliwa na Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mh. Prof.Makame Mbarawa 
Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
  Ujenzi        wa “mill zero” Kujenga boiler itakalokuwa na uwezeo wa kuzalisha steam kwa uzalishaji wa umeme wa megawati 20. 
3.Mtibwa Sugar Estates Ltd  Uzalishaji wa sukari kuongeza kutoka tani 47,000 za sasa hadi kufikia wastani wa tani 80,000 ifikapo mwaka 2025/2026.  Ujengaji wa mabwawa ya kuhifadhi maji         ya umwagiliaji ya ukubwa wa lita millioni 25 Ulimaji wa shamba la hekta 30,000 katika eneo la Dakawa Kuboresha ufanisi     wa kiwandaUjenzi wa bwawa la ukubwa wa lita millioni 25umekamilika Ulimaji na upandaji wa hekta 3,500 Kati ya hekta 30,000 katika shamba la Dakawa umekamilika Ufanisi wa kiwanda umefikia uwezo wa kusaga tani 141 za miwa kwa saa.    
Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
  kusaga tani 230 za miwa kwa saa ifikapo mwaka 2025/2026 (v) Kuongeza uzalishaji umeme kutoka          Megawati     4 kufikia megawati 15 ifikapo mwaka 2025/2026 
4.TPC Ltd  (i) Kutokana na changamoto ya ardhi, kiwanda cha TPC kitaongeza uzalishaji kwa kiwango kidogo kupitia eneo la shamba la kahe na mikakati ya kuongeza tija katika mashamba yaliyopo. (ii) Ogezeko     la uzalishaji(i) Hatua za kuboresha hali ya udongo katika eneo la hekta 240 za shamba la Kahe ili kuweza kupanda miwa zinaendelea.    
Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
  kutoka tani 104,210 za sasa hadi tani 114,012 Mwaka 2025/2026. Ongezeko hili lin 
5Manyara Sugar Co. Ltd(i) Kufikia uchakataji wa miwa wa tani 1,250 kwa siku ifikapo 2024/2025         baada         ya kufanya mabadiliko ya mfumo wa uchakataji kutoka mfumo wa open pan kwenda steam boiling.  (ii) Mfumowa steam boiling utaongeza ufanisi na kupunguza kupotea kwa sukari kwenye maganda yaMifumo yote miwili ya open pan na steam boiling inatumika na jumla ya tani 750 hadi 800 huchakatwa kwa siku.  
Na.Jina la KiwandaMipango ya UpanuziHatua Iliyofikiwa
  miwa (baggase) na “molasses”         na           hivyo kuongeza uzalishaji wa sukari kutoka wastani wa tani 8,000 za sasa hadi tani 10,000 za sukari ifikapo mwaka 2024/2025 

Kiambatisho Na. 9: Mipango na Hatua Iliyofikiwa Katika Miradi ya Bagamoyo na Mkulazi  

NA.MRADIMPANGO WA MRADIHATUA ILIYOFIKIWA  
1.Kiwanda cha Sukari BagamoyoKiwanda cha Sukari Bagamoyo kinatarajia kuzalisha tani 35,000 za Sukari ifikapo Mwaka 2024/2025 na baadae kuendelea hadi tani 50,000 (Maximum Capacity) baada ya kujumuisha miwa kutoka kwa wakulima wadogo watakapoanza kulima.  Ujenzi na usimikaji wa Kiwanda umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90. Inatarajiwa kuanza majaribio ya mtambo mwezi Aprili, 2022 na Uzalishaji kamili wa Sukari Juni, 2022. Ufikishaji wa umeme katika eneo la mradi umekamilika. Hekta 1,300 zimelimwa na kupandwa na hekta zingine 700 zimekwishaandali wa kwa ajili ya kupandwa miwa  Usimikaji   wa          Mifumo               wa Umwagiliaji umekamilika. Ujenzi wa mabwawa ya maji ya umwagiliaji yenye ujazo wa lita million 1.5
NA.MRADIMPANGO WA MRADIHATUA ILIYOFIKIWA  
   umekamilika.
2.Mkulazi II (Mbigili) Mradi wa Mkulazi II uliopo katika shamba la Mbigili chini ya kampuni ya           Mkulazi Holding Company unatarajia kuzalisha tani 50,000 za Sukari ifikapo mwaka 2025/2026. Eneo la mradi lina jumla ya hekta 4,856 ambazo kati ya hizo hekta 3,600 ndio zitakazotumika             kwa       ajili        ya Kilimo cha Miwa. Ujenzi wa msingi kwa ajili ya kusimika kiwanda umefikia asilimia 30. Jumla ya hekta 2,750      za mashamba ya kampuni zimelimwa na zimepandwa miwa.   Eneo la wakulima wadogo lenye ukubwa wa hekta 1,480 limelimwa ambapo hekta 850 zimepandwa Miwa.        Ujenzi wa bwawa lenye mita za ujazo Milioni 1.6 umekamilika na uchimbaji wa Mabwawa matatu, kila moja mita za ujazo, 50,000 umekamilika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *