
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakati akiwatambulisha Wajumbe wa Kikao kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Mei, 2022 kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi ikiwemo Nyongeza ya mshahara. Katika Kikao hicho Mhe. Rais Samia amekubali ongezeko la asilimia 23.3% kwa kima cha chini cha msharahara kwa watumishi wa umma.
