1. Hali ya Rasilimali za Maji ……………………………………….. 5 2. Hali ya Ubora wa Maji ……………………………………………. 6
3. Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Maji Vijijini ………….. 8 4. Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Majisafi na Usafi
wa Mazingira Mijini ……………………………………………….. 8
3. UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2021/22 ….. 9
Upatikanaji wa Fedha ……………………………………………. 9
Programu na Miradi Mbalimbali Iliyotekelezwa katika
mwaka 2021/22 ………………………………………………….. 10
3.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji ……… 10
3.2.2 Huduma za Ubora wa Maji …………………………………… 27 3.2.3 Huduma za Usambazaji Majisafi na Usafi wa
Mazingira Vijijini ………………………………………………….. 33
3.2.4 Huduma za Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa
Mazingira Mijini …………………………………………………… 37
3.2.4.1 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Mikoa …………………………………………………… 38
3.2.4.2 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa ……. 51
3.2.4.3 Mradi wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya
Tabianchi katika Mkoa wa Simiyu …………………………. 57
3.2.4.4 Miradi ya Maji katika Maziwa Makuu ya Victoria,
Tanganyika na Nyasa ………………………………………….. 57
3.2.4.5 Miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa
Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 ………………. 60
3.2.5 Miradi ya Usafi wa Mazingira ………………………………… 60 3.2.6 Taasisi zilizo Chini ya Wizara ……………………………….. 65
i
3.2.7 Masuala Mtambuka …………………………………………….. 70
MAFANIKIO YALIYOPATIKANA …………………………… 73
CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA NA HATUA
ZINAZOCHUKULIWA ………………………………………….. 75
VIPAUMBELE NA MPANGO WA UTEKELEZAJI
KWA MWAKA 2022/23 ………………………………………… 78
Vipumbele vya mwaka 2022/23 …………………………….. 78
Mpango wa Utekelezaji kwa Mwaka 2022/23 ………….. 78
6.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za maji ……… 79 6.2.2 Usimamizi wa Huduma ya Ubora wa Maji ………………. 81
Huduma ya Majisafi na usafi wa Mazingira Vijijini ……. 82
Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini ……….. 83 6.2.5 Mpango wa Kuimarisha Huduma ya Uondoshaji
Majitaka …………………………………………………………….. 84
Chuo cha Maji …………………………………………………….. 85
Masuala Mtambuka …………………………………………….. 85
SHUKRANI ………………………………………………………… 86
MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023 ……… 89
ii
HOTUBA YA WAZIRI WA MAJI MHE. JUMAA HAMIDU AWESO(MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA WIZARA YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2[1]
1. UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, leo hii Bunge lako Tukufu limepokea taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, iliyochambua bajeti ya Wizara ya Maji. Naomba sasa, kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea, kujadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Kawaida na Maendeleo ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23.
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Kamati hiyo kwa kupokea na kuchambua Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23. Maoni, ushauri na maelekezo yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bungeya Kilimo, Mifugo na Maji yamezingatiwa wakati wa maandalizi ya bajeti ya Wizara yangu.Aidha, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mheshimiwa Daniel Baran Sillo Mbunge wa Babati Vijijini na wajumbe wake kwa maoni na ushauri wao uliorahisisha utekelezaji wa bajeti ya Wizara yangu
Awamu ya Sita pamoja na juhudi zakehususan katika ukusanyaji wa kodi, utafutaji wa fedha; na kuimarisha mahusiano ya kitaifa na kimataifa. Vilevile, nichukue fursa hii kuwapongeza Makamu wa Rais, Mheshimiwa Daktari Philip Isidor Mpango; na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) kwa mchango wao mkubwa katika kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuijenga Tanzania kuwa nchi ya uchumi shindani.
Aidha,naomba nikupongeze sana, wewe Mheshimiwa Dkt.Tulia Ackson (Mb) kwa kuchaguliwa kwako na Waheshimiwa Wabunge kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika. Vilevile, nawapongeza Mheshimiwa Najma Murtaza Giga (Mb) na Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha utendaji ndani ya Serikali kwa nyakati tofauti, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri ambapo aliteua Mawaziri wapya na kuwabadilishia Wizara Mawaziri wengine na kuwateua Manaibu Mawaziri. Ninaomba nitumie fursa hii kuwapongeza sana Mawaziri wenzangu wapya wote walioaminiwa na kuteuliwa nikianza na Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb.) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
(Mb), Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara; Mheshimiwa
January Yusuf Makamba (Mb) Waziri wa Nishati; Mheshimiwa Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb), Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi; Mheshimiwa Nape Moses Nnauye (Mb), Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari; Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb), Wizara ya Maliasili na Utalii; Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe (Mb), Waziri wa Kilimo; Mheshimiwa Hamad Yussuf Masauni (Mb), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; na Mheshimiwa Dkt. Angelina Sylvester Lubala Mabula (Mb), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ninaahidi kuwapa ushirikiano wa kutosha katika kulijenga Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, vilevile, nawapongeza Manaibu
Mawaziri walioteuliwa nikianza na Mheshimiwa Jumanne
Abdallah Sagini (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde (Mb), Naibu Waziri wa kilimo; Mheshimiwa Dkt. Stephen Lemomo
Kiruswa (Mb), Naibu Waziri wa Madini; Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete (Mb), Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mheshimiwa Atupele Fredy Mwakibete (Mb), Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.
Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii pia kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wapya ambao ni Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani (Mb) aliyechaguliwa kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Ushetu; Mheshimiwa Mohamed Said Issa (Mb) kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Konde; na Mheshimiwa Emmanuel Lekishon Shangai (Mb) kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Ngorongoro. Nawapongeza pia Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) naMheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha (Mb) walioteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pole kwako wewe mwenyewe Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu, Familia za Marehemu, Ndugu, Jamaa na Watanzania wote kwa misiba iliyotupata kwa kuondokewa na aliyekuwa Mbunge wa Ushetu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Elias John Kwandikwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro; Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mheshimiwa William Tate Ole Nasha; na
Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama. Michango ya Wabunge hao katika shughuli za maendeleo ya Taifa letu itakumbukwa milele daima. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu hao mahali pema peponi. Amin.
Mheshimiwa Spika, naombapia nichukue fursa hii kumshukuru, Waziri Mkuuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa (Mb) kwa hotuba yake nzuri aliyoiwasilisha hapa Bungeni ambayo inatoa dira na mwongozo wa utekelezaji wa kazi za Serikali. Hotuba hiyo imeonesha mapitio ya uendeshaji wa shughuli za Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 na Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2022/2023 pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025). Vilevile, nawapongeza Mawaziri wenzangu wote walionitangulia kuwasilisha hoja zao na Wabunge waliochangia hoja hizo.
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, napenda sasa kuchukua fursa hii kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara yangu yenye maeneo makuu manne yafuatayo:- Hali ya Sekta ya Maji nchini; Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 na Mpango na Bajeti ya Sekta kwa mwaka 2022/2023; pamoja na Changamoto na Hatua zilizochukuliwa. Maelezo ya maeneo hayo yamezingatia Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa; Sera, Mikakati ya Maendeleo ya Kitaifa na Kimataifa, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025); Sheria, Kanuni pamoja na maoni na ushauri wa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili tukufu. Maelezo ya kina kuhusu utekelezaji huo yameainishwa katika sehemu zifuatazo za hotuba hii.
2. HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI
11. Mheshimiwa Spika, napenda kutoa maelezo kuhusu hali ya Sekta ya Maji nchini kwa kuzingatia hali ya rasilimali za maji; ubora wa maji; na upatikanaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira vijijini na mijini.
2.1 Hali ya Rasilimali za Maji
MheshimiwaSpika, rasilimali za maji zilizopo nchini zinakadiriwa kuwa mita za ujazo bilioni 126 kwa mwaka ambapo rasilimali za maji juu ya ardhi ni mita za ujazo bilioni 105 na zilizopo ardhini ni mita za ujazo bilioni 21. Hadi kufikia mwezi Aprili 2022, mahitaji ya maji kwa matumizi mbalimbali nchini yanakadiriwa kuwa ni takribani mita za ujazo bilioni 47 kwa mwaka sawa na asilimia 37.37 ya maji yaliyopo nchini. Mahitaji hayo ya maji yanatarajiwa kuongezeka hadi kufikia wastani wa mita za ujazo bilioni 80 kwa mwaka ifikapo mwaka 2035.
Mheshimiwa Spika, kiwango cha maji kilichopo kwa kila mtu kwa mwaka ni takribani wastani wa mita za ujazo 2,250 kwa kuzingatia makadirio ya idadi ya watu milioni 55.9 kwa mwaka 2019. Kiwango cha chini cha mahitaji ya maji kwa mtu kwa mwaka kinachokubalika kimataifa ni wastani wa mita za ujazo 1,700 ambapo chini ya hapo nchi inahesabika kuwa na uhaba wa maji (Water Stress). Hivyo, kiasi cha maji kilichopo nchini kinaonesha kuwa nchi yetu haina uhaba wa maji.Hata hivyo, Serikali inaendelea kuwekeza katika utunzaji wa vyanzo vya maji, ujenzi wa miundombinu ya kuongeza upatikanaji wa maji; kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi; na kuboresha ufanisi katika matumizi ya maji kwa lengo la kuepusha nchi kuwa na uhaba wa maji.
Mheshimiwa Spika, maeneo mengi ya nchi yetu hususan ukanda wa kaskazini; kanda ya ziwana maeneo ya pwani yanapata mvua katika misimu miwili ya vuli (mwezi Oktoba hadi Desemba) na masika (mwezi Machi hadi Mei). Maeneo mengine hususan ya katikati ya nchi, nyanda za juu kusini na baadhi ya maeneo ya ukanda wa magharibi yanapata mvua ya msimu mmoja unaoanzia mwezi Desemba hadi Mei. Katika mwaka wa kihaidrolojia (Novemba 2020 – Oktoba 2021) wastani wa mvua iliyonyesha ni milimita 1,066.4 ambayo ni chini ya kiasi cha mvua kilichonyesha katika mwaka wa Kihaidrolojia Novemba 2019 – Oktoba 2020 kilichokuwa milimita 1,470. Aidha, mvua hizo ni juu ya wastani wa muda mrefu wa milimita 921 kwa mwaka. Hali hiyo imesababisha kiasi cha maji katika mito, mabwawa na maziwa kuendelea kuimarika katika maeneo mbalimbali nchini.
2.2 Hali ya Ubora wa Maji
Mheshimiwa Spika, usimamizi wa ubora wa maji ni muhimu katika maendeleo ya taifa letu katika kulinda afya ya jamii na vyanzo vya maji. Wizara kupitia maabara 17 za ubora wa maji nchini imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa maji katika vyanzo vya maji na mitandao ya kusambaza maji mijini na vijijini kwa lengo la kutoa maamuzi juu ya matumizi yaliyokusudiwa.
Mheshimiwa Spika, ufuatiliaji na utafiti wa ubora wa maji uliofanyika katika vyanzo vya maji nchini unaonesha hali ya ubora wa maji kutofautiana kutoka eneo moja hadi jingine. Utofauti huo unatokana na hali ya miamba ya asili, shughuli za kibinadamu, jiografia ya eneo na mabadiliko ya tabianchi. Ufuatiliaji na utafiti huo umebaini uwepo wa chumvichumvi katika mikoa ya ukanda wa pwani; madini ya fluoride mikoa ya kaskazini; chuma na manganese katika mikoa ya kusini; na kuwepo kwa vimelea vya vijidudu na tope kwenye maji katika baadhi ya maeneo ya nchi. Pamoja na changamoto hizo, mwenendo wa ubora wa maji nchini unaridhisha na vyanzo hivyo vinaweza kuendelezwa kwa matumizi mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, maji yanayosambazwa kwa jamii kupitia mifumo ya usambazaji maji mijini na vijijini yemeendelea kukidhi viwango vya ubora wa maji ya kunywa vya kitaifa katika maeneo mengi nchini. Hata hivyo, changamoto iliyopo ni uwepo wa madini ya chumvichumvi katika maeneo ya Pwani na Ukanda wa Kati katika mikoa ya Dodoma na Singida; uwepo wa madini ya Fluoride katika maeneo yaliyopo kwenye ukanda unaopitiwa na Bonde la Ufa ikiwemo mikoa ya Arusha, Manyara, Mara, Kilimanjaro, Shinyanga, Singida na Simiyu. Katika kukabiliana na changamoto za ubora wa maji yanayosambazwa, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kuwekeza katika teknolojia mbalimbali za kusafisha na kutibu maji ikiwa ni pamoja na kuweka mitambo ya kisasa ya kupunguza madini na chumvichumvi katika maji ya kunywa.
2.3 Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya MajiVijijini
18. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi waishio vijijini inafikia zaidi ya asilimia 85 ifikapo mwaka 2025, Serikali imeendelea kujenga, kukarabati, kupanua mitandao ya kusambaza maji pamoja na kuimarisha usimamizi wa huduma ya maji. Hadi mwezi Aprili 2022, upatikanaji wa huduma ya maji vijijini imefikia wastani wa asilimia 74.5 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 72.3 mwezi Machi, 2021. Kiwango hicho kinatokana na kukamilika kwa ujenzi wa miradi mipya, ukarabati na upanuzi wa miradi 303 ambayo imeanza kutoa huduma kwa wananchi wapatao 1,467,107.
2.4 Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Majisafi na Usafi
wa Mazingira Mijini
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa huduma ya majisafi ili kuweza kutoa huduma endelevu na ya uhakika. Hadi mwezi Aprili, 2022 hali ya upatikanaji wa huduma ya maji mijini ni wastani wa asilimia 86.5 ikilinganishwa na asilimia 86 ya mwezi Machi 2021. Ongezeko hilo linatokana na kukamilika kwa ujenzi wa miradi 40 iliyohusisha ukarabati, upanuzi na ujenzi wa miradi mipya. Aidha, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji inatarajiwa kuongezeka ifikapo mwezi Desemba 2022 kutokana na miradi mikubwa ya maji inayotarajiwa kukamilika ndani ya kipindi hicho ikiwemo Mradi wa kuboresha huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Arusha; Mradi wa Maji wa Mugango-Kiabakari-Butiama; Mradi wa maji wa Tinde – Shelui; pamoja na miradi inayotekelezwa kwa fedha za UVIKO-19.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuboresha huduma ya usafi wa mazingira ikiwemo uondoshaji wa majitaka katika maeneo ya mijini. Hadi mwezi Aprili 2022, hali ya uondoshaji wa majitaka umefikia asilimia 13.5. Hali ya huduma imeongezeka kutokana na mtandao wa majitaka kuongezeka kutoka kilometa 954.8 za mwaka 2020/21 hadi kilometa 1,385.8 mwezi Aprili 2022. Vilevile, maunganisho yameongezeka kutoka wateja 53,008 kwa mwaka 2020/21 hadi wateja 53,428 mwezi Aprili 2022.
Mheshimiwa Spika, katika kuboresha takwimu za hali ya upatikanaji wa huduma ya maji nchini, Wizara imetenga fedha kwa ajili ya kufanya taftishi ya kina ya upatikanaji wa huduma ya maji kulingana na idadi halisi ya watu itakayopatikana kutoka kwenye SENSA inayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti 2022.
3. UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2021/22
3.1 Upatikanaji wa Fedha
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Fungu 49
–Wizara ya Maji liliidhinishiwa jumla ya Shilingi 680,388,976,000 na kati ya fedha hizo Shilingi 33,758,976,000 zilikuwa ni fedha za matumizi ya kawaida na Shilingi 646,630,000,000 zilikuwa ni fedha za maendeleo. Aidha, wakati bajeti inaendelea kutekelezwa, Wizara ilipata Shilingi 139,354,573,798.37 kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO – 19 ili kuhakikisha wananchi wanapata majisafi, salama na yenye kutosheleza karibu na makazi yao na kuwezesha kupambana na UVIKO-19. Hatua hiyo, imewezesha bajeti ya maendeleo kuongezeka na kuwa 785,984,573,798.37 na jumla ya bajeti yote ya Wizara kwa mwaka 2021/2022 kufikia Shilingi 819,743,549,798.37.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imepokea jumla ya Shilingi 778,917,042,400.34 sawa na asilimia 95 ya bajeti iliyoidhinishwa. Kati ya fedha zilizopokelewa, Shilingi 743,760,395,570.21 ni za kutekeleza miradi ya maendeleo sawa na asilimia 95 ya bajeti ya fedha za maendeleo. Kwa upande wa fedha za Matumizi ya Kawaida, jumla ya Shilingi 35,156,646,830.13 zilipokelewa sawa na asilimia 104 ya bajeti ya fedha za Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 22,612,420,563.62 ni fedha za mishahara (PE) na Shilingi 12,544,226,266.51 ni fedha za matumizi mengineyo (OC).
3.2 Programu na Miradi Mbalimbali Iliyotekelezwa
katika mwaka 2021/22
24. Mheshimiwa Spika, katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, Wizara imeendelea kutekelezaProgramu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Programme – WSDP). Hali ya utekelezaji wa miradi katika mwaka 2021/22na mafanikio yaliyopatikana katika maeneo ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji;huduma za ubora wa maji; huduma za majisafi vijijini; huduma za usambazaji majisafi na usafi wa mazingira mijini; na utekelezaji wa kazi mbalimbali katika Taasisi zilizo chini ya Wizara na masuala mtambuka ni ifuatavyo:-
3.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji
25. Mheshimwa Spika, usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji nchini unatekelezwa kupitia Bodi za Maji za Mabonde tisa (9) ambazo zimepewa majukumu yakufanya tathmini na ufuatiliaji wa rasilimali hizo; kuhifadhi na kudhibiti uchafuzi wa vyanzo vya maji; kugawa maji kwa sekta mbalimbali kwa kuzingatia mahitaji na kiasi cha maji kilichopo; na kuendeleza rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, kazi zilizotekelezwa ni kama ifuatavyo:-
(i). Tathmini na Ufuatiliaji wa Rasilimali za Maji (a) Ujenzi na Ukarabati wa Vituo vya Kufuatilia Mwenendo wa Rasilimali za Maji
26. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi za rasilimali za maji nchini, Wizara imeendelea kujenga na kukarabati vituo vya kufuatilia mwenendo wa rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya vituo 178 kati ya 180 vilivyopangwa vimejengwa na kukarabatiwa katika Mabonde ya Rufiji (22), Wami-Ruvu (13), Pangani (15), Ruvuma (13), Ziwa Nyasa (8), Ziwa Rukwa (13), Ziwa Tanganyika (39), Ziwa Victoria (51) na Bonde la Kati vituo vinne (4). Jitihada hizo zimepelekea uwepo wa jumla ya vituo 1,257 vya kufuatilia mwenendo wa rasilimali za maji vinavyofanya kazi katika maeneo mbalimbali kwenye mabonde ya Pangani vituo (183); Wami-Ruvu (253); Rufiji (232); Ruvuma na Pwani ya Kusini (77); Ziwa Nyasa (70); Bonde la Kati (97); Ziwa Rukwa (97); Ziwa Tanganyika (79) na Ziwa Victoria vituo 169.
(b) Ugawaji wa Rasilimali za Maji na Udhibiti wa Migogoro
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji inatekeleza jukumu la kugawa maji kwa sekta zote za kijamii, kiuchumi na mazingira kwa haki, usawa na uwazi kupitia Bodi za Maji za Mabonde. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imetoa vibali vipya 451 na kufanya jumla ya vibali 10,904 vilivyotolewa nchi nzima kwa ajili ya matumizi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini. Uwepo wa vibali hivyo unasaidia katika uratibu na kuwa na takwimu sahihi za matumizi ya maji. Naomba kupitia Bunge lako niwahimize wananchi wote kwa ujumla wanaotaka kuchukua maji kutoka katika vyanzo mbalimbali wafahamu kuwa wanao wajibu wa kisheria wa kuomba vibali vya matumizi ya maji hayo kutoka katika Bodi za Maji za Mabonde.
Mheshimiwa Spika, sote tunatambua kuwa maji ni rasilimali muhimu sana kwa ustawi wa jamii, uendelevu wa mazingira na ukuaji wa uchumi. Kutokana na umuhimu huo imekuwepo migogoro ya matumizi ya maji kutokana na upungufu wa maji katika baadhi ya maeneo. Udhibiti na utatuzi wa migogoro hiyo umeendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini kupitia Bodi za Maji za Mabonde kwa kushirikiana na Jumuiya za Watumiaji Maji pamoja na Serikali za Mitaa. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya migogoro 27 ya matumizi ya maji ilijitokeza katika Mabonde ya Pangani (19); Wami-Ruvu (4); Bonde la Kati (1) na Ziwa Tanganyika (3) ambapo migogoro yote inaendelea kutafutiwa ufumbuzi. Vilevile, katika kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji, Wizara imeendelea kutoa elimu kuhusu wajibu wa wananchi katika kufuata Sheria na Kanuni za usimamizi wa Rasilimali za Maji. Elimu hiyo imetolewa kupitia majukwaa ya wadau na maadhimisho ya kitaifa kwa lengo la kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji.
(c) Udhibiti wa Uchimbaji Holela wa Visima
29. Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti uchimbaji holela wa visima, Wizara imeendelea kuratibu na kusajili kampuni za utafiti na uchimbaji wa visima pamoja na kutoa leseni na vibali vya uchimbaji kwa makampuni yanayokidhi vigezo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya leseni 155 zimetolewa na nyingine kuhuishwa ambapo leseni 70 ni za kampuni za uchimbaji; leseni 91 za wataalam wa uchimbaji (Drillers) na leseni 14 za utafiti. Aidha, jumla ya vibali 649 vya kuchimba visima vya maji katika maeneo mbalimbali nchini vimetolewa. Idadi hiyo inafikisha jumla ya vibali 3,889 vya kuchimba visima vilivyotolewa hadi sasa.
(d) Uhifadhi wa Mazingira na Vyanzo vya Maji
Mheshimiwa Spika, utunzaji wa vyanzo vya maji ni jukumu letu sote hivyo hatuna budi kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara na wadau wote. Utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji unahusisha utambuzi wa vyanzo; uwekaji wa mipaka na kutangaza maeneo ya vyanzo hivyo katika Gazeti la Serikali kama maeneo tengefu ili yalindwe kisheria. Katika kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya maji, Wizara imeendeleakutambua na kuweka mipaka kwenye vyanzo vya maji; na kuunda Jumuiya za Watumia Majikwa lengo la kuwashirikisha wananchi katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji kwa mujibu wa Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, vyanzo vya maji 48 vimewekewa mipaka kama hatua ya awali ya uhifadhi katika mabonde ya Pangani (12), Rufiji (12), Ruvuma (4), Ziwa Nyasa (3), Bonde la Kati (1), Ziwa Rukwa (8), Ziwa Tanganyika (4) na Ziwa Victoria vyanzo vinne (4).Idadi hiyo inafikisha jumla ya vyanzo 163 vilivyowekewa mipaka ambapo vyanzo 18 kati ya hivyo vimetangazwa kwenye Gazeti la Serikali ili vilindwe kisheria na vyanzo vya maji 44 vipo katika mchakato wa kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama maeneo tengefu.
Mheshimiwa Spika, katika kutimiza azma ya kushirikisha jamii kwenye utunzaji wa vyanzo vya maji na usimamizi endelevu wa matumizi ya maji, Wizara imeendelea kuunda Jumuiya za Watumia Maji (Water Users’ Associations – WUAs) katika maeneo ya vyanzo vya maji ili kuhakikisha vyanzo hivyo vinatunzwa na maji yanatumika kwa uwiano mzuri. Hadi mwezi Aprili 2022, Jumuiya 14 za Watumia Maji zimeundwa katika mabonde ya Pangani (2), Rufiji (1), Ruvuma (3), Ziwa Nyasa (1), Ziwa Rukwa (2), Ziwa Tanganyika (3) na Ziwa Victoria (2) na kufanya jumla ya Jumuiya za Watumia Maji zilizoundwa kufikia 164.
(e) Udhibiti wa Uchafuzi wa Vyanzo vya Maji
33. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kudhibitiuchafuzi wa vyanzo vya maji kwa kutoa vibali vya kutiririsha majitaka na kusimamia viwango vya majitaka yanayotiririshwa katika vyanzo. Hadi mwezi Aprili 2022, vibali 36 vya kutiririsha majitaka vimetolewa katika Bodi za Maji za Bonde ya Ziwa Victoria vibali 11 na Wami-Ruvu vibali 25. Idadi hiyo inafikisha jumla ya vibali 152 vilivyotolewa hadi sasa katika mabonde yote.
(f) Mradi wa Kunusuru Vyanzo vya Maji kupitia Mpango Endelevu wa Matumizi Bora ya Ardhi katika Mabonde Madogo ya Mito ya Zigi na Ruvu.
Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha mradi wa kunusuru vyanzo vya maji katika mabonde madogo ya Mto Zigi (Bonde la Pangani) na Mto Ruvu (Bonde la Wami-Ruvu)mwezi Desemba 2021. Lengo la mradi huo lilikuwa ni kuanzisha na kuwezesha utekelezaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi katika mabonde hayo ili kuzuia uchafuzi na uharibifu wa vyanzo vya maji. Katika mwaka 2021/22, kazi zilizotekelezwa ni pamoja na kujenga jengo moja kwa ajili ya kuweka mashine ya kuchakata viungo vya mboga katika Kijiji cha Zirai kilichopo Wilaya ya Muheza; kuandaa warsha iliyohusisha wadau wote wa kidakio cha Mto Ruvu kwa lengo la kujadiliana kwa pamoja, kutoa ushauri, kutoa utaalam pamoja na rasilimali fedha ili kunusuru vyanzo vya maji katika kidakio hicho; kuunganisha vikundi vinne (4) vya ujasiriamali (ZIMISA AMCOSS, TULO STRAWBERRY, UWAMAKIZI NA BWAWA LA SAMAKI LA MBARANGWE) na benki ya kilimo (TADB) na wafadhili wengine kwa ajili ya kupata mikopo na fursa nyingine kama vile mafunzo ili kuendeleza shughuli zao kwa lengo la kulinda vyanzo vya maji
Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huo umeleta manufaa makubwa katika vyanzo vya mito ya Zigi na Ruvu ikiwa ni pamoja na kupungua kwa uharibifu na uchafuzi wa vyanzo hivyo ambapo wananchi walioondolewa wamewezeshwa kufanya shughuli mbadala za kiuchumi; kuimarisha ushirikiano wa taasisi mbalimbali katika utunzaji wa vyanzo vya maji; kuongezeka kwa upatikanaji wa maji kwa wananchi kupitia miradi ya maji iliyojengwa na mradi; na kuongezeka kwa elimu katika jamii ikiwemo ya usimamizi wa rasilimali za maji na elimu ya ujasiriamali.
(ii). Uendelezaji wa Rasilimali za Maji a) Utafutaji wa Vyanzo Vipya vya Maji
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi waishio mijini na vijijini wanapata huduma endelevu ya maji, Wizara imeendelea na utafutaji wa vyanzo vipya vya maji katika maeneo mbalimbali nchini ili kuvihifadhi na kuviendeleza viweze kutoa huduma. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya vyanzo vipya 535 vya maji vimebainishwa vikihusisha mito, vijito, chemichemi, mabwawa, ardhi oevu na maji ya ardhini katika Mabonde ya Pangani (189); Rufiji (26); Ruvuma na Pwani ya Kusini (22); Ziwa Nyasa (5); Bonde la Kati (22); Ziwa Rukwa (265) na Ziwa Tanganyika vyanzo sita (6). Idadi hiyo inafikisha jumla ya vyanzo vya maji 2,091 vilivyotambuliwa hadi sasa katika maeneo mbalimbali nchini. Vyanzo vinavyotambuliwa na kubainika kuwa vinafaa vitaendelezwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha ukarabati wa bwawa la Mwadila lililopo Wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu. Vilevile, Wizara imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa mabwawa 16 ya Ng’walukwa, Kiloleli na Ngofila (Kishapu); Muko na Chiwanda (Momba); Zebeya na Ilambambasa (Maswa); Iseni, Mwabayanda na
Nyang’hanga (Magu); Manda (Chamwino); Dongo (Kiteto); Mtamba (Mpwapwa);Itamboleo (Mbarali); Nyange (Ifakara); pamoja na Horohoro (Mkinga). Ujenzi na ukarabati wa mabwawa hayo utagharimu kiasi cha Shilingi bilioni 13.89. Vilevile, usanifu wa malambo (Charco dams) sita (6) umekamilika katika mwambao wa barabara kuu ya DodomaBabati ikihusiha Wilaya za Bahi mawili (2) na Chemba manne (4) na tayari Wizara imeshapokea fedha kiasi cha Shilingi bilioni 1.21 kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa hayo.
b) Ujenzi na Ukarabati wa Mabwawa
38. Mheshimiwa Spika, uwezo wa nchi yetu kuhifadhi maji kwa sasa katika mabwawa yaliyopo ni mita za ujazo bilioni 5.4 tu sawa na asilimia 5.2 ya maji juu ya ardhi yanayopatikana kwa mwaka. Kwa kuzingatia umuhimu wa kujenga miundombinu mikubwa ya kuhifadhi maji kwa ajili ya usalama wa maji, Serikali imeendelea na mpango wa ujenzi wa miradi ya mabwawa ya Lugoda/Ndembera (Iringa), Songwe (Mbeya) na Bwawa la Dongo (Manyara). Vilevile, Wizara imeendelea na ujenzi wa mabwawa 8 katika vijiji vya Nsenkwa (Mlele), Mihingo (Bunda), Chole (Kisarawe), Chamwino (Chamwino), Kwamjembe (Bagamoyo), Kwenkambala (Handeni),
Kalemasha (Kalambo) na Mbuta (Mkinga). Ujenzi wa mabwawa hayo upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Aidha,Wizara imekamilisha usanifu wa kina mabwawa 12 katika Vijiji vya Itaswi – Kisaki (Kondoa), Kwamsanja (Chalinze), Kalemela
(Urambo), Mkonde (Kilindi), Msente (Kilindi), Lombouti (Kilindi), Ichemba (Kaliua), Izimbili (Kaliua), Ingwisi (Kaliua), Gendagenda (Handeni), Msomera (Handeni) na Kang’ata (Handeni). Taratibu za kuwapata wakandarasi wa ujenzi zinaendelea.
c) Uanzishwaji wa Majukwaa ya Wadau wa Maji
39. Mheshimiwa Spika, ushirikishwaji wa wadau katika usimamizi wa rasilimali za maji ni muhimu ili kuhakikisha matumizi bora na endelevu ya rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imefanikiwa kuendesha majukwaa nane (8) ya wadau katika mabonde nane. Uanzishwaji wa majukwaa hayo umefanikisha utoaji wa ushauri mbalimbali; umeongeza upatikanaji wa fedha na mwamko wa wadau juu ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji.
(iii). Usimamizi wa Rasilimali za Majishirikishi
Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina vyanzo vya majishirikishi 14 ambavyo ni Maziwa ya Victoria, Tanganyika, Nyasa, Natron, Chala na Jipe pamoja na Mito ya Kagera, Mara, Malagarasi, Momba, Mwiruzi, Umba, Ruvuma na Songwe. Idadi hiyo inaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye vyanzo vingi vya maji vinavyovuka mipaka ya nchi Barani Afrika. Usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji katika vyanzo vya majishirikishi unahusisha ushirikiano na nchi wanachama ambazo ni Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Uganda, Malawi, Msumbiji na Zambia. Nchi nyingine tunazoshirikiana nazo ni Angola, Botswana, Ethiopia, Misri, Namibia, Sudan, Sudan Kusini, Zimbabwe na Eritrea.
Mheshimiwa Spika, misingi ya ushirikiano katika rasilimali za majishirikishi ni Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1992 kuhusu uhifadhi na matumizi ya majishirikishi na maziwa makuu (The 1992 United Nations Economic
Commission for Europe Convention on the Protection and Use of Transboundary Watercourses); pamoja na Mkataba wa
Umoja wa Mataifa wa mwaka 1997 kuhusu Matumizi ya
Majishirikishi katika shughuli zisizo za usafirishaji (The 1997 UN Convention on the Law of the Non-Navigational Uses of International Watercourses) ambapo Tanzania inatekeleza mikataba hiyo.Utekelezaji wa mikataba mbalimbali ya usimamizi wa rasilimali za majishirikishi pamoja na Taasisi za Kikanda na Kimataifa zilizoanzishwa kwa ajili ya kusimamia ushirikiano huo ni kama ifuatavyo:-
(a) Mikataba ya Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi wa Majishirikishi
42. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Tanzania imeshiriki katika Mkutano wa Tisa wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa uliohusu Mkataba wa Usimamizi na matumizi ya Majishirikishi ya Maziwa Makuu uliofanyika tarehe 29 Septemba – 01 Oktoba 2021. Katika Mkutano huo, Tanzania imewasilisha mchango wake katika kuchangia amani ya dunia kupitia ushirikiano katika usimamizi wa majishirikishi, ulinzi wa maslahi ya Taifa katika matumizi ya maji kutoka katika vyanzo vya majishirikishi; na utekelezaji wa kiashiria namba 6.5.2 (Transboundary Water Cooperation) cha Lengo namba 6 la Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDG 6 – Water and Sanitation for All). Aidha, Tanzania inashiriki katika utekelezaji wa Programu ya Mkataba huo katika kipindi cha mwaka 20222024 kwa manufaa ya Taifa; pamoja na Tanzania kuzishawishi nchi nyingine inazoshirikiana nazo kuandaa mipango ya pamoja ya matumizi ya maji katika vyanzo vya majishirikishi kama vile Bonde la Mto Mara.
(b) Taasisi ya Mpito ya Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative – NBI)
Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Mpito ya Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative – NBI) ni ushirikiano baina ya nchi 11 za Bonde la Mto Nile ambazo ni Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Misri, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Sudan, Uganda pamoja na Eritrea ambayo ni mtazamaji (observer). Kupitia Taasisi hiyo, unatekelezwa Mradi wa Nile Basin Regional Hydromet System wenye lengo la kuimarisha mtandao wa kufuatilia mwenendo wa hali ya rasilimali za maji katika vyanzo kwa kukusanya takwimu. Kwa upande wa Tanzania, mradi huo utajenga vituo vinane (8) vya kisasa vya kukusanya takwimu za mtiririko wa maji katika mito mikubwa ya Mara, Kagera, Simiyu na Rusumo iliyopo katika Bonde la Ziwa Victoria. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa vituo hivyo zimekamilika. Ujenzi wa vituo hivyo unatarajiwa kuanza katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023.
Mheshimiwa Spika, vilevile, Taasisi ya NBI kwa kushirikiana na nchi wanachama inafanya utafiti wa Kimkakati wa Rasilimali za Maji (Strategic Water Resources Analysis – SWRA). Utafiti huo unalenga kutoa ushauri kuhusu namna ya kukidhi mahitaji ya maji yanayoendelea kuongezeka; na uendelevu wa usalama wa chakula na nishati kwa nchi za ukanda wa juu na ukanda wa chini wa Bonde la Mto Nile. Aidha, maandalizi ya Mpango wa Usimamizi wa Bonde la Mto
Nile unaolenga kutoa mwongozo katika upangaji na utekelezaji wa shughuli za usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji kwa ngazi ya kitaifa na kikanda yanaendelea. Kazi hiyo inafanywa na Wataalam wa Sekretarieti ya NBI kwa kushirikiana na Wataalam wa Nchi Wanachama ambapo kwa sasa ipo katika hatua za awali za ukusanyaji wa taarifa mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, mwaka 2006 Baraza la Mawaziri wa Maji wa Nchi za Bonde la Mto Nile liliazimia kuwa tarehe 22 Februari ya kila mwaka kuwa ni siku ya kumbukumbu ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo ambaponchi wanachama zitakuwa zinaadhimisha Siku ya Bonde la Mto Nile kikanda na kitaifa. Lengo ni kuhamasisha matumizi endelevu ya rasilimali za maji za Bonde la Mto Nile. Maadhimisho ya 16 ya Bonde la Mto Nile yalifanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Februari, 2022 na Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wadau wapatao 1,500 kutoka nchi wanachama wa Bonde la Mto Nile. Aidha, katika maadhimisho hayo Tanzania imeziomba nchi nyingine wanachama kubeba agenda ya kuanzisha Kamisheni ya Bonde la Mto Nile kama agenda kuu katika ushirikiano wa Bonde la Mto Nile ili kuimarisha usimamizi endelevu, matumizi ya usawa na uendelezaji wa rasilimali za maji ya Bonde la Mto Nile. Vilevile, Tanzania iliomba kuongezwa kwa lugha ya Kiswahili kama lugha ya mawasiliano katika shughuli za Bonde la Mto Nile sanjari na lugha za Kifaransa na Kiingereza.
(b) Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe
46. Mheshimiwa Spika, Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe ilianzishwa na Serikali za Tanzania na Malawi kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Bonde la
Mto Songwe (Songwe River Basin Development Program).
Programu hiyo ina lengo la kukabiliana na mafuriko ya mara kwa mara yanayosababisha kuhamahama kwa Mto Songwe kupitia ujenzi wa mabwawa ambayo pia yatatumika kwa ajili ya kuzalisha umeme wa megawati 180, kilimo cha umwagiliaji hekta 6,200 usambazaji maji pamoja na uvuvi. Vilevile, programu hii inahusisha Miradi midogo ya kijamii kama vile shule, barabara na hospitali. Hadi mwezi Aprili 2022, shughuli zifuatazo zimefanyika: kutekeleza Mradi wa Uhifadhi wa
Mazingira ya Bonde la Mto Songwe kwa kupanda miti 1,000,000 katika Wilaya ya Ileje; kuandaa Mkakati wa Jinsia katika Usimamizi wa Rasilimali za Maji 2022-2027; na kuandaa Mpango wa Kukabiliana na Mafuriko katika vijiji vya Njisi, Kabanga, Ndwanga, Mpunguti na Katumba Songwe wilyani Kyela. Vilevile, Wizara imeshiriki katika Mkutano wa kwanza wa Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe uliofanyika Lilongwe – Malawi tarehe 9 Machi, 2022 ambao uliadhimia kuwa mradi wa umeme kuwa kipaumbele kwa mataifa yote mawili na kuweka mikakati ya kutafuta fedha kiasi cha Dola za Marekani Milioni 577 kwa ajili ya ujenzi wa bwawa na mtambo wa kuzalisha umeme.
(c) Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi
47. Mheshimiwa Spika, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoko ndani ya Bonde la Mto Zambezi kupitia ukanda wa Bonde la Ziwa Nyasa. Nchi nyingine ni Angola, Botswana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Zambia pamoja na Zimbabwe. Kwa sasa Sekretariati ya Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission – ZAMCOM) inatekeleza Mpango Mkakati wa Miaka 22 kuanzia 2018-2040. Kupitia Mpango Mkakati huo, Sekretarieti ya ZAMCOM kwa kushirikiana na nchi wanachama inaandaa Programu ya
Mabadiliko ya Tabianchi 2022-2026 (The Programme for Integrated Development and Adaptation to Climate Change in the Zambezi Watercourse 2022-2026). Mradi huo utahusisha uwekezaji kwenye masuala mtambuka ambapo fedha za utekelezaji zinategemewa kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Mfuko wa Mazingira (Global Environmental Facility– GEF) pamoja na Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund – GCF). Miradi ya Tanzania inayotegemewa kujumuishwa katika mradi huo ni pamoja na Programu ya Kuendeleza Bonde la Mto Songwe yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 829 inayohusisha Sekta za Maji, Kilimo, Nishati pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
(c) Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
48. Mheshimiwa Spika, Tanzania pamoja na nchi nyingine 15 ambazo ni Angola, Botswana,Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Eswatini,Lesotho,Madagascar,Malawi,Mauritius,Msumbiji,Namibia,Seychelles,AfrikaKusini,Zambiana Zimbabwezinaunda Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern African Development Community – SADC). Hadi mwezi Aprili 2022, Tanzania imeshiriki katika Mkutano wa 40 wa Baraza la Mawaziri wa Maji na Nishati wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ulifanyika Mjini Blantyre nchini Malawi tarehe 02 Desemba, 2021. Mkutano huo ulipitisha Mpango Mkakati wa Kikanda wa Usimamizi Shirikishi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji Awamu ya Tano (Regional Strategic Action Plan on Integrated Water Resources Development and Management Phase V 2021-2025). Kupitia Mpango Mkakati huo, Tanzania inategemea kunufaika na ujenzi wa miradi ya maji katika maeneo ya mipakani (Border Post Water, Sanitation and Hygiene Response Project); miradi ya maji ya Kasumulu-Songwe kati ya Tanzania na Malawi pamoja na Nakonde-Tunduma kati ya Tanzania na Zambia.
Lengo la miradi hiyo ni kuendeleza mipango ya nchi wanachama ya kuboresha huduma za maji katika maeneo ya mipaka na yenye msongamano pamoja na kuendeleza jitihada za kukabiliana na UVIKO-19
(d) Baraza la Mawaziri wa Maji wa Afrika
Mheshimiwa Spika, Tanzania ni mwanachama wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Afrika (African Ministers’ Council on Water – AMCOW) lenye jukumu la kushughulikia masuala ya usimamizi wa maji na usafi wa mazingira katika nchi za Afrika. Katika kipindi cha mwaka 2021/22, Tanzania imeshiriki katika mkutano wa Kamati Tendaji ya Mawaziri wa Maji uliofanyika kwa njia ya mtandao mwezi Desemba, 2021. Mkutano huo uliidhinisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za AMCOW na kupitisha Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira unaosimamiwa na AMCOW. Mwongozo huo utazisaidia nchi za Afrika ikiwemo Tanzania kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 hususan lengo namba 6. Vilevile, kupitia kupitishwa kwa Mwongozo wa Usafi wa Mazingira wa Afrika (The African Sanitation Policy Guidelines) ambao unalenga kuzisaidia nchi za Afrika kuandaa Sera za Usafi wa Mazingira (Sanitation Policies) au kuboresha huduma ya usafi wa mazingira, Tanzania imewasilisha ombi la kupata msaada huo kutoka AMCOW kwa ajili ya kuboresha huduma za usafi wa mazingira nchini.
Mheshimiwa Spika, Vilevile Tanzania imeshiriki katika Kongamano la 9 la Jukwaa la Maji Duniani (9th World Water Forum 2022) ambalo liko chini ya Baraza la Maji Duniani (World Water Council) lililofanyika tarehe 21-26 Machi 2022
Mjini Dakar – Senegal. Katika Kongamano hilo, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Global Water Parnership Southern Africa wamechaguliwa kuwa katika Jopo la Ngazi ya Juu la Kimataifa linaloshughulikia uwekezaji katika Sekta ya Maji Afrika (International High Level Panel on Water Investments in Africa).
(e) Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria
Mheshimiwa Spika, Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria imeendelea kutekeleza Programu na miradi mbalimbali ikiwemo Programu ya pamoja ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji katika Bonde la Ziwa Victoria inayogharimu takribani Shilingi bilioni 83.7. Fedha hizo ni msaada uliotolewana Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya.Vilevile, Kamisheni inatekeleza Mradi wa Kikanda wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi katika Bonde la Ziwa Victoria kwa ushirikiano na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) kwa gharama ya takriban Shilingi bilioni 11.675. Hadi mwezi Aprili 2022, rasimu ya Mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria imeandaliwa kwa ajili ya kukarabati na kupanua mtandao wa majitaka wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA). Hatua hiyo itawezesha kuunganisha wateja wapya 1,600 katika mtandao wa majitaka Jijini Mwanza. Aidha, kupitia Mradi wa Kikanda wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi visima vitatu (3) vipya vyenye uwezo wa kuzalisha maji mita za ujazo 4.7, 6.4 na 8.5 vimechimbwa pamoja na kufanya ukarabati kwenye kisima kimoja katika Kijiji cha Ng’haya Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo kuendeleza shughuli za kilimo cha umwagiliaji wa mboga mboga. Kazi yakufunga pampu zinazoendeshwa kwa mfumo wa nishati ya jua kwenye visima hivyo inaendelea. Vilevile, kupitia mradi huo, mizinga ya nyuki 149 imegawiwa kwa vikundi viwili katika Kijiji cha Ng’haya ili kuwezesha wananchi kujipatia kipato kutokana na shughuli za urinaji wa asali.
Mheshimiwa Spika, kupitia Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, nchi wanachama zimeandaa rasimu ya Sera ya Maji ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na mkakati wake wa utekelezaji kwa kipindi cha miaka 10 (2022 – 2032). Sera na mkakati huo utasaidia kutoa mwongozo katika utekelezaji wa programu za maji. Vilevile, Kamisheni kwa kushirikiana na nchi wanachama imeandaa rasimu ya Mkakati wa nne (4) wa Kamisheni kwa kipindi cha 2021/22 – 2025/26. Rasimu ya Mkakati huo imeainisha vipaumbele katika kuendeleza usimamizi wa mazingira; usimamizi shirikishi wa rasilimali za maji; usimamizi wa afya ya jamii; uendelezaji wa jamii kiuchumi; na usimamizi wa shughuli za usafiri majini. Rasimu hiyo itawasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Kisekta la Kamisheni Bonde la Ziwa Victoria linalotarajiwa kukutana mwezi Mei 2022 kwa ajili ya kupitishwa.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeshiriki katika maadhimisho ya 10 ya siku ya Bonde la Mto Mara yaliyofanyika tarehe 15 Septemba, 2021 katika Wilaya ya Tarime, Mkoa wa Mara. Siku ya Bonde la Mto Mara huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha na kuelimisha wananchi waishio ndani ya Bonde la Mto Mara kuhusu utunzaji na uhifadhi wa Bonde hilo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya miti 16,000 ambayo ni rafiki kwa mazingira ilipandwa. Sambamba na zoezi la upandaji miti, kulikuwa na zoezi la uwekaji wa nguzo za alama (beacon) katika kijiji cha Murito ili kulinda eneo la umbali wa mita 60 kutoka kwenye kingo za Mto Mara kama Sheria ya Mazingira Na. 4 ya mwaka 2004 na Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimaji za Maji ya mwaka 2009 zinavyoelekeza. Jumla ya nguzo za alama 70 zilisimikwa katika umbali wa mita 100 kutoka nguzo moja hadi nyingine.
(f) Taasisi ya Global Water Partnership
54. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Global Water Partnership (GWP) imeundwa na nchi washirika 179 zilizogawanywa katika kanda 13 ikiwemo kanda ya nchi za kusini mwa Afrika (Global Water Partnership Southern Africa – GWPSA). Lengo la Taasisi hiyo ni kujenga uwezo wa nchi washirika katika kuboresha usimamizi wa rasilimali za maji katika ngazi za kimataifa, kikanda, kitaifa na ngazi ya jamii. Katika kutekeleza agenda ya kuongeza uwekezaji katika Sekta ya Maji Barani Afrika (African Water Investment Programme-AIP), Tanzania inaendelea kushirikiana na GWPSA pamoja na Global Water Partnership – Tanzania katika kupata Dola za Kimarekani bilioni 30 kila mwaka ili kufikia Lengo Namba 6 la Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa 2015-2030 linalohusu Maji na Usafi wa Mazingira kwa wote. Katika jitihada za kupata fedha hizo, Wizara ya Maji imewasilisha maandiko ya miradi mbalimbali ya kimkakati ili kupata fedha kupitia agenda hiyo. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na GWP Tanzania imeandaa Mpango Mkakati wa Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Maji katika Bodi ya Maji Bonde la Wami-Ruvu.
(iv). Kujenga Uwezo wa Taasisi zinazosimamia Rasilimali za Maji
55. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi wa Kusaidia Sekta ya Maji Awamu ya Pili (Water Sector Support Project –
WSSP II) inaendelea kuzijengea uwezo Taasisi zinazosimamia rasilimali za maji kwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji takwimu za mwenendo wa maji katika mabonde yote tisa nchini, utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji, ununuzi wa vitendea kazi na kujenga uwezo kwa wataalam. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imekamilsha uandaaji wa mipango ya utunzaji wa vidakio kwenye mabonde yote tisa nchini; ununuzi wa magari 28, pikipiki 100, baiskeli 100, vifaa vya usalama kwa ajili ya wasoma takwimu na vifaa vya ofisi kwa ajili jumuiya za watumia maji. Vilevile, Wizara inaendelea na taftishi ya kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa takwimu ili kuweza kupata takwimu kwa wakati (real time data); taftishi ya kuandaa mfumo wa kutoa taarifa za viashiria vya mafuriko (flood early warning system); na taftishi ya kutambua maeneo yenye maji chini ardhi pamoja na kuandaa ramani ya maji chini ya ardhi.
3.2.2 Huduma za Ubora wa Maji
Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Maabara za Ubora wa Maji imeendelea kusimamia na kufuatilia ubora wa maji katika mifumo ya usambazaji maji kwa matumizi ya majumbani, maji katika vyanzo na maji kwa matumizi mengine ikiwa ni pamoja na viwanda, umwagiliaji, ujenzi, utafiti na ufugaji wa samaki. Aidha, Wizara imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira kwa lengo la kudhibiti uchafuzi wa mazingira na vyanzo vya maji.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ilipanga kukusanya sampuli 15,000 kwa ajili ya kubaini mwenendo wa ubora wa maji katika vyanzo; na ubora wa maji kwa ajili ya matumizi ya majumbani, viwandani, umwagiliaji, ujenzi na utafiti. Kwa upande wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira Wizara ilipanga kukusanya na kuhakiki sampuli 2000. Utekelezaji wa mipango hiyo ni kama ifuatavyo:-
(i). Ubora wa Maji Katika Vyanzo
58. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufuatilia mwenendo wa ubora wa maji katika vyanzo ambapo hadi mwezi Aprili 2022, sampuli 607 kutoka katika vyanzo vya maji 63 vya kimkakati zilikusanywa na kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara kwa ajili ya afya ya ikolojia. Matokeo ya uchunguzi yanaonesha kuwa ubora wa maji wa vyanzo hivyo ni wa kuridhisha katika kulinda ikolojia na vyanzo vinaweza kuendelea kutumika au kuendelezwa kwa matumizi yaliyokusudiwa.
(ii). Ubora wa Maji kwa Matumizi ya Majumbani
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhakikisha maji yanayosambazwa kwa jamii yanakidhi viwango kwa kufuatilia ubora wa maji katika skimu za usambazaji maji mijini na vijijini; taasisi binafsi pamoja na vyanzo vya maji vinavyomilikiwa na watu binafsi kwa lengo la kulinda afya ya jamii. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya sampuli za maji 6,979 zimekusanywa na kuhakikiwa ubora wake kwa kulinganishwa na viwango vya ubora wa maji ya kunywa vya kitaifa ambapo, sampuli 5,932 sawa na asilimia asilimia 85 zilikidhi viwango na sampuli 1,047 sawa na asilimia 15 hazikukidhi viwango. Aidha, baadhi ya sampuli hazikukidhi viwango vya ubora wa maji kutokanana uwepo wa viwango vikubwa vya madini ya Fluoride katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Mwanza, Kilimanjaro, Manyara na Singida; Turbidity katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani na Mara; madini ya chuma katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Geita, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na Mwanza; madini ya Manganese katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mtwara, Lindi na Morogoro; chumvichumvi katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mtwara na Lindi; Color katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mara, na Mwanza. Acidity katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Lindi, Mtwara na Ruvuma. Vilevile kiwango kidogo cha dawa ya Chlorine kilionekana katika maeneo ya Mbogwe, Sengerema na Buchosa. Katika kukabiliana na changamoto hizo ushauri wa kitaalam ikiwa ni pamoja na njia sahihi za kusafisha na kutibu maji ulitolewa kwa wasambazaji wa maji mijini na vijijini.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha maji yanayomfikia mtumiaji yanaendelea kuwa na ubora unaotakiwa, Wizara imeendelea kufuatilia utekelezaji pamoja na kuzijengea uwezo Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira katika kuandaa na kutekeleza Mipango ya Usalama wa Maji inayohusisha Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Resilient Water Safety Plans –CR WSPs). Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imeweza kutoa mafunzo kwa Wataalam 16 ambao watatumika katika kuongeza kasi ya uwezeshaji wa uandaaji wa mipango ya usalama wa maji kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs).
(iii). Ubora wa Maji kwa Matumizi Mengine
61. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa maji yanayotumika katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwa ni pamoja na shughuli za viwandani, ujenzi, umwagiliaji na utafiti ili kuhakikisha maji hayo yanakidhi viwango vya ubora vinavyokubalika kwa matumizi yaliyokusudiwa. Hadi mwezi Aprili, 2022 jumla ya sampuli 366 zilikusanywa na kuhakikiwa ubora wake kwa ajili ya matumizi ya viwandani sampuli 182, ujenzi (38), umwagiliaji (14) na sampuli (132) kwa jili ya shuguli za utafiti. Matokeo yalionesha asilimia 98.2 ya sampuli zilikidhi viwango kwa matumizi yaliyokusudiwa na asilimia 1.8 ya sampuli hazikukidhi viwango kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha chumvichumvi katika maji.
(iv). Ubora wa Madawa ya Kusafisha na Kutibu Maji
62. Mheshimiwa Spika, katika kutimiza lengo la usambazaji wa majisafi na salama ni muhimu kuhakikisha madawa yanayotumika yanakidhi viwango vya ubora na yanakuwa na ufanisi katika kusafisha na kutibu maji. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imehakiki ubora wa madawa ya kusafisha maji aina ya Aluminium Sulphate (Shabu), Poly Aluminum Sulphate na Algae Floc 195-1. Kwa upande wa madawa ya kutibu maji ya kunywa, dawa aina ya Calcium Hypochlorite ilihakikiwa ubora wake kabla ya matumizi. Matokeo ya uchunguzi yalionesha madawa hayo yanakidhi viwango vinavyokubalika kwa ajili ya kusafisha na kutibu maji.
(v). Ubora wa Majitaka Yanayorudishwa Kwenye Mazingira
63. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufuatilia na kuhakiki ubora wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira kutoka majumbani, viwandani na katika taasisi kwa lengo la udhibiti wa uchafuzi wa vyanzo vya maji na mazingira. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya sampuli 256 zilikusanywa kutoka kwenye mabwawa ya kusafisha majitaka katika Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na viwanda mbalimbali.Matokeo yalionesha asilimia 46 ya sampuli za majitaka zilikidhi viwango vya kurudishwa kwenye mazingira. Sampuli ambazo hazikukidhi viwango ni kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha organic matter kinachosababisha kupungua kwa hewa ya oxygen. Aidha, Mamlaka za Maji pamoja na viwanda ambavyo majitaka yake hayakukidhi viwango, ushauri wa kitaalam ulitolewa ili kuongeza ufanisi wa mifumo ya kusafisha na kutibu majitaka.
(vi). Mkakati wa Uondoaji wa Madini ya Fluoride katika Maji ya Kunywa
64. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha usalama wa maji yanayosambazwa kwa jamii Wizara imeendelea kutekeleza Mkakati wa Uondoaji wa Madini ya Fluoride kwenye maji ya kunywa na kupikia katika mikoa iliyoathirika zaidi na madini hayo (Fluoride belt). Katika mwaka 2021/22, Wizara imejenga mitambo miwili (2) ya ngazi ya jamii ya kuondoa madini ya Fluoride kwenye maji katika kijiji cha Loiborsoit Wilaya ya Simanjiro, Mkoani Manyara. Aidha, Wizara imeendela kufuatilia ufanisi wa mitambo ya kupunguza madini ya Fluoride katika maji ya kunywa ambapo hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya mitambo 438 ngazi ya kaya ilikaguliwa na kati ya hiyo mitambo 221 ilibainika kufanya kazi kwa ufanisi na mitambo 217 ilionekana kuhitaji kubadilishwa chengachenga za mifupa ya ng’ombe. Kwa upande wa mitambo ya ngazi ya jamii, mitambo tisa (9) ilikaguliwa ambapo mitambo saba (7) ilibainika kufanya kazi kwa ufanisi na miwili (2) inahitaji kubadilishwa chengachenga za mifupa. Vilevile, Wizara imeendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya kiwango kikubwa cha madini ya Fluoride katika maji ya kunywa na matumizi sahihi ya teknolojia ya kuondoa madini hayo kupitia vyombo vya habari, mikutano na makongamano mbalimbali.
(vii). Uimarishaji wa Maabara za Maji Nchini
Mheshimiwa Spika, katika kuongeza wigo na kusogeza huduma za ubora wa maji kwa wananchi, Serikali kwa kushirikina na Shirika la OIKOS imefanikiwa kuanzisha maabara mpya ya ubora wa maji katika mkoa wa Manyara. Kuanzishwa kwa maabara hiyo kunaifanya Wizara ya Maji kufikisha jumla ya Maabara 17 za ubora wa maji nchini.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali za kuboresha huduma za ubora wa maji nchini, Wizara imeendelea kuimarisha Maabara za Ubora wa maji kwa kuzijengea uwezo ikiwa ni pamoja na kuwa na ithibati (accreditation). Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imeanza mchakato wa kuongeza idadi ya Maabara zenye ithibati kutoka saba (7) za sasa (Dar es Salaam, Singida, Shinyanga Mwanza, Musoma, Kigoma na Bukoba) hadi kufikia 11 kwa kuzipatia ithibati maabara za Morogoro, Mtwara, Iringa na Sumbawanga. Lengo ni kuboresha utoaji wa takwimu za ubora wa maji zinazotumika kutoa maamuzi kuhusu usimamizi na matumizi ya maji. Aidha, katika kuhakikisha maabara zinafanya uchunguzi wa viashiria kwa usahihi, Maabara 16 za ubora wa maji nchini zilishiriki kwenye zoezi la kujipima uwezo wa utendaji kazi za kimaabara linaloratibiwa na Shirika la SADCMET. Matokeo ya zoezi hilo yameimarishamaabara zetu katika kufanya uchunguzi wa vimelea vya vijidudu (bacteria) na viashiria vya kikemikali na maumbo.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha utendaji kazi katika maabara za maji nchini kwa kuweka mfumo wa kielektroniki wa kuendesha kazi zote za maabara (Laboratory Information Management System – LIMS). Hadi mwezi Aprili 2022, mfumo umewekwa katika maabara za Mwanza, Musoma, Kigoma na Dar es salaam ambapo wataalam kutoka maabara hizo wameendelea kupatiwa mafunzo ya matumizi ya mfumo huo. Aidha, Wizara imeendelea kuziwezesha Maabara za Ubora wa Maji kwa kuzipatia vifaa mbalimbali vya kisasa vinavyotumika kufanya uchunguzi wa Ubora wa Maji.
Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kutoa wito kwa wadau wote kutambua umuhimu wa kupima ubora wa maji kabla ya kuyatumia kwa matumizi mbalimbali ikiwa ni pamoja na matumizi ya majumbani, viwanda, ujenzi, umwagiliaji na utafiti. Aidha, viwanda na taasisi nyingine zinazotiririsha majitaka zihakikishe maji hayo yanatibiwa na kufikia viwango vinavyokubalika kabla ya kutiririshwa kwenye mazingira. Huduma za upimaji na ufuatiliaji wa ubora wa maji na majitaka zinatolewa na Wizara kupitia Maabara 17 za Ubora wa Maji zilizopo katika mikoa mbalimbali nchini.
3.2.3 Huduma za Usambazaji Majisafi na Usafi wa
Mazingira Vijijini
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ilipanga kutekeleza jumla ya miradi 1,527 ya maji na usafi wa mazingira vijijini. Kati ya miradi hiyo, miradi 1,176 inahusisha kukamilisha miradi iliyokuwa inaendelea, ujenzi wa miradi mipya, upanuzi na ukarabati wa miundombinu ya maji na miradi 351 inahusisha utafutaji wa vyanzo vya maji na maandalizi ya miradi.Vilevile, Serikali ilipanga kukarabati na kujenga mabwawa 19 na kufanya usanifu wa miradi 390.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa jumla ya miradi 303 yenye jumla ya vituo vya kuchotea maji 3,845 umekamilika na kuanza kutoa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi 1,467,107. Kiambatisho Na. 1 kinaonesha orodha ya miradi iliyokamilika vijijini katika mwaka wa fedha 2021/22. Aidha, utekelezaji wa miradi 648 unaendelea na ipo katika hatua mbalimbali na miradi 88 ipo katika hatua za ununuzi wa wazabuni na wakandarasi.Vilevile, Wizara imekamilisha usanifu wa miradi 446; utafiti wa maji chini ya ardhi kwenye maeneo 158 katika vijiji 141; ukarabati wa visima 76 katika vijiji 76; na kuchimba visima 191 katika vijiji 175. Kuchelewa kuanza utekelezaji wa baadhi ya miradi kumetokana na changamoto ya kutokukamilika kwa wakati upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi mipya iliyoibuliwa.
Mheshimiwa Spika Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo imeendelea kuimarisha huduma za maji vijijini kwa kutekeleza miradi na programu zifuatazo:- (i). Programu ya Malipo kwa Matokeo (PbR)
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID/FCDO) inatekeleza Programu ya Malipo kwa Matokeo (Payment by Results – PbR) kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira vijijini. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya Shilingi bilioni 74.636 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa programu. Aidha, jumla ya miradi 115 imekamilika kwa kufanyiwa ukarabati na upanuzi na hivyo kurejesha huduma kwenye vituo 837 vya kuchotea maji katika vijiji 170.
(ii). Programu ya Uendelevu wa Huduma ya Maji na
Usafi wa Mazingira Vijijini
73. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inatekeleza Programu ya Uendelevu wa Huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (Sustainable Rural Water Supply and Sanitation Program) inayotekelezwa kwa kipindi cha miaka sita (2019-2024) katika Mikoa 17 na Halmashauri za Wilaya 86. Kupitia Programu hiyo kiasi cha Shilingi bilioni 817.29 kilitengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ukarabati, upanuzi wa mitandao ya kusambaza maji pamoja na ujenzi wa miradi mipya itakayoibuliwa. Hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi 69 yenye jumla ya vituo 1,166 vya kuchotea maji na inanufaisha wananchi wapatao 439,302 katika vijiji 131. Aidha, ufanisi wa utekelezaji wa programu hiyo umewezesha kuongezeka kwa fedha za utekelezaji wa miradi ya maji vijijini kutoka shilingi bilioni 114 mwaka 2019/20 hadi kufikia shilingi bilioni 250 mwaka 2021/22. Ongezeko hilo la fedha litaiwezesha RUWASA kuendelea kujenga miradi mipya vijijini na hivyo kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji vijijini. Aidha, fedha hizo pia zitawezesha kujenga misingi imara ya uendelevu wa huduma muhimu ya maji kwa wananchi ikiwa ni pamoja na vyombo vya utoaji wa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSOs).
(iii). Matumizi ya Teknolojia ya Nishati Jadidifu (Renewable Energy)
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) inaendelea na utekelezaji wa Mradiwa kupunguza gharama za uendeshaji kwa kubadilisha mitambo ya dizeli kwenda mitambo inayotumia nishati ya jua (Accelerating Solar Pumping via Innovative Financing Project). Gharama za mradi ni takribani Shilingi bilioni 19.85 ambapo utekelezaji wake umeanza katika mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga, Mtwara na Tabora. Lengo la mradi huo ni kutatua changamoto za gharama kubwa za uendeshaji wa miradi ya maji vijijini hususan miradi inayotumia nishati ya mafuta ya dizeli ambayo ni ghali.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imekamilisha ufungaji wa mitambo ya kufua umeme wa jua katika skimu 33 kati ya 70 iliyopangwa kwenye mikoa ya Dodoma na Singida; kujenga vituo vya maji 342 kati ya 539 vilivyopangwa pamoja na kufunga dira za malipo ya kabla (prepaid water meter) katika vituo hivyo. Aidha, taratibu za kuwapata Wakandarasi katika mikoa ya Shinyanga na Mtwara zimekamilika ambapo utekelezaji wa ufungaji wa mitambo katika mikoa hiyo unaendelea. Vilevile, taratibu za manunuzi ya Wakandarasi kwa mkoa waTabora zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa gharama za uendeshaji wa miradi ya maji vijijini zinapungua, Wizara kwa kushirikiana na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuunganisha umeme na kufunga solar kwenye mitambo ya kusukuma maji inayotumia nishati ya dizeli. Mpango huo utanufaisha skimu 355 ambazo zitaunganishwa kwenye gridi ya taifa ya umeme na skimu nane (8) zitafungiwa mifumo ya solar.
(iv). Utekelezaji wa Miradi yenye Changamoto za Muda Mrefu
77. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji kupitia Wakala wa
Maji na Usafi wa Mazingira ilipokea jumla ya miradi 177 kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa yenye changamoto ya kutokukamilika kwa wakati na mingine kukamilika bila kutoa maji. Katika mwaka 2021/22, Serikali imekamilisha miradi 42 na hivyo kufikisha miradi 127 (Kiambatisho Na. 2) ambayo ni sawa na asilimia 71.8 ya miradi yote iliyokuwa na changamoto za muda mrefu. Aidha, Wizara inaendelea na utekelezaji wa miradi 50 iliyobaki na inatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/23.
(v). Uimarishaji wa Vyombovya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii
78. Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu miradi ya maji vijijini iliyokamilika katika baadhi ya maeneo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya kutokuwa endelevu kutokana na uwezo mdogo wa vilivyokuwa Vyombo vya Watumia Maji (Community Owned Water Supply Organizations – COWSOs) vilivyopewa jukumu la kusimamia na kuendesha miradi hiyo. Katika kuimarisha uwezo wa vyombo hivyo, Serikali kupitia Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019ilifanya maboresho ya muundo wa vyombo hivyo na sasa vinafahamika kama Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji ngazi ya Jamii (Community Based Water Supply Organisations – CBWSOs).Muundo ulioboreshwa wa CBWSOs umejumuisha wataalam wakiwemo Mafundi Sanifu wanaosimamia matengenezo ya miundombinu na Wahasibu wanaosimamia masuala ya fedha. Hadi mwezi Aprili 2022, Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii vipatavyo 2,466 vimeundwa na kuhuishwa katika mikoa 25 ya Tanzania bara. Vilevile, katika kuhakikisha kuwa huduma ya maji inakuwa endelevu, jumla ya wataalam 1,746 waliajiriwa na CBWSOs kwa mkataba ambapo kati yao Mafundi Sanifu walikuwa 940 na Wahasibu 806. Aidha,Serikali inaendelea kuhamasisha sekta binafsi kushiriki katika utoaji wa huduma ya maji ambapo jumla ya watoa huduma binafsi 66 wameingia makubaliano na CBWSOs kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma ya maji vijijini.
3.2.4 Huduma za Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa
Mazingira Mijini
79. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kutekeleza miradi ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji mbalimbali kwa kutoa maji kutoka vyanzo vya maziwa, mito, chemichemi, visima na mabwawa. Utekelezaji huo, umehusisha ujenzi wa miradi mipya, upanuzi wa miradi katika maeneo ambayo hayana miundombinu ya maji na ukarabati wa miradi yenye miundombinu chakavu pamoja na kuzijengea uwezo Mamlaka za Maji. Miradi hiyo inalenga kuboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi na usafi wa mazingira katika Miji Mikuu ya Mikoa, Miji Mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa.Katika mwaka wa fedha 2021/22, jumla ya miradi 114 ilipangwa kutekelezwa katika maeneo ya mijini. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya miradi 40 imekamilika ambapo miradi hiyo imehusisha ukarabati, upanuzi na ujenzi wa miradi mipya. Kiambatisho Na. 3 kinaonesha miradi iliyokamilika katika maeneo ya mijini. Aidha, utekelezaji wa miradi mingine unaendelea na ipo katika hatua mbalimbali. Vilevile, maunganisho ya wateja kwa huduma ya majisafi katika Mamlaka za miji mikuu ya mikoa yameongezeka kutoka wateja 942,995 mwezi Machi 2021 hadi kufikia wateja 1,074,115 mwezi Aprili 2022.
3.2.4.1 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Mikoa
80. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya majisafi katika maeneo ya Miji Mikuu ya Mikoa ili kuimarisha huduma ya maji kwa wananchi waishio maeneo hayo. Utekelezaji wa miradi katika baadhi ya miji mikuu ya mikoa ni kama ifuatavyo:-
(i). Miradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Dodoma
81. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma kwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo:
a) Mradi wa kutoa maji katika visima vya Ihumwa kwenda tanki la Njedengwa
82. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa kutoa maji katika visima vya Ihumwa kwenda tanki la
Njedengwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.4. Utekelezaji wa mradi huo ulihusisha ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa Kilomita 11.6; ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa Kilomita 4.2. Mradi huo unanufaisha wananchi wapatao 15,700 wa maeneo ya Nzuguni, Nyumba 300 na Iyumbu.
b) Ujenzi wa mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino – Ikulu
83. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino – Ikulu ambao ulihusisha ujenzi wa tanki katika eneo la Buigiri lenye uwezo wa lita milioni 2.5; na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 21.8 yanayopeleka maji kutoka tanki la Buigiri kwenda Ikulu ya Chamwino. Kukamilika kwa mradi huo umenufaisha wananchi wapatao 29,534.
c) Mradi wa kuchimba visima vipya na kukarabati visima vya zamani
84. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utafiti wa maji chini ya ardhi na uchimbaji wa visima katika maeneo oevu ili kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma. Kupitia mradi huo, jumla ya visima 10 vilipangwa kuchimbwa katika maeneo ya Zuzu visima vitatu (3); Ntyuka (1); Michese (1); Mpamaa (2); Mbwanga – Mipango (1); na Miyuji visima viwili (2). Hadi mwezi Aprili 2022, uchimbaji wa visima nane (8) umekamilika katika maeneo ya Zuzu, Ntyuka,Nala, Iyumbu na Ihumwa.
d) Mradi wa Bwawa la Farkwa
85. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kukabiliana na uhaba wa huduma ya maji katika jiji la Dodoma, Serikali imepanga kujenga bwawa la Farkwa ambalo litaongeza uzalishaji wa maji kwa zaidi ya ujazo wa lita milioni 120 kwa siku, kiasi ambacho kitatosheleza mahitaji ya maji katika Jiji la Dodoma.Hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imepata mkopo wa Dola za Marekani milioni 125.3 kutoka Benki ya Maendeleo Africa (African Development Bank – AfDB) kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi ambayo itahusisha ujenzi wa Bwawa na mtambo wa kutibu maji (Treatment Plant). Taratibu za kuwapata wataalam washauri watakaosimamia ujenzi pamoja na wakandarasi watakaojenga awamu ya kwanza ya mradi zinaendeleana ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2022/23. Mradi huo ukikamilika utaimarisha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama katika Jiji la Dodoma, Wilaya za Chemba, Bahi na Chamwino.
e) Mradi wa Kutoa Maji Ziwa Victoria hadi Dodoma
86. Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kutumia vyanzo vyenye maji ya uhakika ili kusambaza maji kwa maeneo mengi kwa pamoja. Kupitia dhana hiyo, Serikali imepanga kutekeleza mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria na kuyafikisha Jiji la Dodoma kupitia mji wa Singida. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili mradi huo uweze kutekelezwa.
(ii). Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Mkoa wa Dar es Salaam na baadhi ya Maeneo ya Mkoa wa Pwani
87. Mheshimiwa Spika, Wizara inatekeleza miradi ya kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na miji ya Kibaha, Kisarawe,
Mkuranga, Chalinze na Bagamoyo katika Mkoa wa Pwani.
Miradi inayotekelezwa ni pamoja na:-
a) Mradi wa Maji wa Mlandizi – Chalinze – Mboga
88. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya maji wa Mlandizi – Chalinze – Mboga kwa gharama ya Shilingi bilioni 18.Mradi huo ulizinduliwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 22 Machi 2022. Kazi zilizofanyika ni ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 58.9; ujenzi wa vituo viwili vya kusukuma maji katika maeneo ya Chamakweza na Msoga; na ufungaji wa pampu sita za kusukuma maji. Mradi huo umewanufaisha wananchi wapatao 120,912.
b) Mradi wa Maji wa Chalinze
89. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India inaendelea kutekeleza awamu ya tatu ya mradi wa maji wa Chalinze kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 41.3 sawa naShilingi bilioni 86.9. Mradi wa Chalinze awamu ya tatu umelenga kunufaisha vijiji 68 ambapo vijiji 19 viko kaskazini na 49 viko kusini mwa mto Wami. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia wastani wa asilimia 91.6 na kazi zilizotekelezwa ni upanuzi wa mtambo kwa kuongeza uzalishaji kutoka lita 500,000 hadi 900,000 kwa saa; ulazaji wa mabomba makuu ya kusafirisha maji (transmission mains) kutoka mtamboni kuelekea maeneo ya wateja kilomita 124.38; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wakilomita 1,022.8; ujenzi wa vituo tisa (9) vya kusukuma maji (booster stations); ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 2 eneo la Mazizi na ujenzi wa matanki mengine 18 yenye ujazo wa kuanzia lita 50,000 mpaka lita milioni 1 na ujenzi wa vituo 351 vya kutekea maji (kiosks) kwenye vijiji na vitongoji mbali mbali vilivyopo eneo la mradi.
c) Ukarabati na Upanuzi wa Mfumo wa Kusambaza
Majisafi
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kusaidia Sekta ya Maji Awamu ya Pili (Water Sector Support Project – WSSP II) imeendelea na ukarabati na upanuzi wa mfumo wa usambazaji majisafi katika Mkoa wa Dar es Salaam. Hadi mwezi Aprili 2022,utekelezaji wa mradi wa kutoa maji kutoka kwenye tanki la Chuo Kikuu Ardhi na kuyapeleka Bagamoyo umefikia asilimia 61 ambapo kazi zinazoendelea ni pamoja na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa kilomita 1,082; ujenzi wa vituo viwili vya kusukuma maji; na ujenzi wa matanki matatu ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita milioni 15. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza maji katika maeneo ya Mbezi-Makabe. Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusuma maji, ufungaji wa pampu, ujenzi wa matanki, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 70.
d) Mradi wa Maji wa Visima Virefu vya Kimbiji na Mpera
92. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji wa visima virefu katika maeneo yaKimbiji na Mpera. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji kutoka katika visima vya Kimbiji ambapo utekelezaji wake umegawanywa katika vipande vinne. Kipande cha kwanza kinahusu ujenzi wa miundombinu ya kutoa maji kwenye visima kwenda kwenye pampu ambapo mkandarasi yupo katika hatua za awali za maandalizi. Kipande cha pili kinahusu ujenzi wa kituo cha kusukuma maji pamoja na ulazaji wa bomba la kutoa maji kwenye visima kwenda kwenye tanki la kuhifadhia maji lenye uwezo wa lita milioni 15 katika eneo la Kisarawe II ambapo utekelezaji umefikia asilimia 35. Maandalizi ya utekelezaji wa vipande vya tatu na nne unaendelea.
e) Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kidunda
93. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa bwawa la Kidunda kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya kupungua kwa kina cha maji katika chanzo cha mto Ruvu ambacho ndio chanzo kikuu cha maji kwa Jiji la Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani. Vilevile, ujenzi wa bwawa hilo utasaidia kupunguza athari za mafuriko katika maeneo ya Morogoro na Pwani. Aidha, Serikali imetenga Shilingi bilioni 62.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bwawa hilo katika mwaka wa fedha 2022/23 ambapo taratibu za manunuzi ya mkandarasi atakayejenga bwawa hilo na Mtaalam Mshauri atakayesimamia ujenzi zinaendelea.
(iii). Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Arusha
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inaendelea na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya usambazaji majisafi na uboreshaji wa huduma ya uondoaji wa majitaka katika Jiji la Arusha unaogharimu Dola za Marekani milioni 233.9 sawa na takribani Shilingi bilioni 520.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, kazi zilizokamilika ni pamoja na uchimbaji wa visima 41; ujenzi wa mabwawa mapya 18 ya kutibu majitaka; na upanuzi na ukarabati wa miundombinu na mifumo ya majisafi na majitaka maeneo ya katikati ya Jiji; ujenzi wa mitambo ya kusafisha maji; ujenzi wa ofisi za kanda na ujenzi wa vyoo vya mfano. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa ofisi kuu; upanuzi wa mtandao wa majitaka nje ya CBD; upanuzi wa mtandao wa majisafi; uchimbaji wa visima 15 na ujenzi wa chujio la maji. Kwa ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 80 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 40 kwa siku hadi lita milioni 200 kwa siku hivyo kuongeza muda wa upatikanaji wa huduma ya majisafi kutoka saa 12 za sasa hadi saa 24. Vilevile, kukamilika kwa mradi kutaongeza huduma ya uondoaji wa majitaka kutoka asilimia 7.6 za sasa hadi asilimia 30.
(iv). Miradi ya kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza
96. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza kwa kutekeleza miradi ifuatayo:-
a) Mradi wa Kutoa Maji Chanzo cha Butimba
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank-EIB) pamoja na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (French Development Agency-AFD) imeendelea kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza. Katika mwaka 2021/22, Serikali imeanza ujenzi wa choteo katika Ziwa Victoria na mtambo wa kusafisha na kutibu maji katika eneo la Butimba kwa gharama ya Shilingi bilioni 69.34 ambapo hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asilimia 20.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa miundombinu ya maji kwa gharama ya Euro 6,750,397.53. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu la maji kilomita 17 kutoka chanzo cha maji cha Butimba hadi tanki la kuhifadhia maji la Buswelu; ulazaji wa mabomba ya usambazaji yenye urefu wa kilomita 8.02; ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita milioni 3 katika eneola Buswelu; ujenzi wa ofisi eneo la Sahwa; ujenzi wa jengo la mtambo wa kusukuma maji; ununuzi na ufungaji wa pampu. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa kazi hizo umefikiawastani wa asilimia 10. Kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi wapatao 105,649.
b) Mradi wa Maji wa Nyamuhongolo – Kisesa
99. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi katika maeneo ya
Nyamuhongolo – Kisesa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.18. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa kituo cha kusukuma maji katika eneo la Nyamuhongolo; ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 120,000;na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 75 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. Kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi wapatao 39,600.
c) Mradi wa kuboresha na upanuzi wa miundombinu ya Majisafi Maeneo ya Katikati na Kusini mwa Jiji la Mwanza
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa miundombinu ya Majisafi Jijini Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 17.89. Mradi huo umehusisha ujenzi wa matanki mawili (2) yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 2.95 katika maeneo ya Sahwa na Igengele-Bugarika; kulaza mtandao wa mabomba umbali wa kilomita 11.3 na kufunga pampu za kusukuma maji Nyegezi. Mradi huo unatoa huduma kwa wananchi wapatao 300,000 wa maeneo ya Sahwa, Buhongwa, Nyegezi, Kanyerere, Lwanhima, Kanindo, Fumagila, Buswelu, Lukobe, Kigala, Nsumba, Kahama,
Bujigwa, Nyamadoke na Ilalila.
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira jijini Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 38.93. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 1.2; ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 19.8 kutoka chanzo cha Butimba hadi Igoma; kufunga pampu za kusukuma maji Sahwa kupeleka tanki la Igoma; kulaza mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 5.26 kutoka tanki la Nyegezi hadi Buhongwa; na kulaza mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 0.925 kutoka Mabatini hadi Hospitali ya Bugando. Mradi unatoa huduma kwa wananchi wapatao 300,000 katika maeneo ya Bugarika, Nyegezi, Majengo, Ibanda, Utemini, Mkolani, Mwananchi, Mabatini, Kitangiri, Kiseke, Nyasaka, Mjimwema na Nyamhongolo.
(v). Miradi ya kuboresha huduma ya Majisafi katika Manispaa ya Bukoba
102. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa upanuzi wa mtandao wa majisafi katika Manispaa ya Bukoba. Utekelezaji wa Awamu ya kwanza ya mradi iliyogharimu Shilingi bilioni 2.42 umekamilika. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi vituoviwili (2) vya kusukuma maji; ufungaji wa pampu; ulazaji wa mabomba urefu wa kilomita 60; ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 500,000; na ukarabati wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 70,000. Kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi kumeongeza upatikanaji wa huduma kutoka asilimia 88 hadi asilimia 91. Utekelezaji wa awamu ya pili unaogharimu Shilingi bilioni 3.35 umefikia asilimia 35. Awamu hiyo inahusisha ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 500,000; ujenzi wa bomba kuu kutoka kituo cha kusukuma maji cha Machinjioni hadi Bugashani umbali wa kilomita 4.7; ununuzi na ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 32. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba 2022 na utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 91 hadi asilimia 98.
(vi). Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Kigoma
103. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo KfW imekamilisha utekelezaji wa mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Kigoma na wananchi wanapata huduma ya maji. Hata hivyo, kutokana na hitilafu iliyojitokeza katika eneo la choteo la maji, Serikali inaendelea na ujenzi wa choteo jipya kwa gharama ya Euro milioni 3.61 ambapo hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi umefikia asilimia 22.
(vii). Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Lindi
104. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi unaendelea ambapo kazi zilizokamilika ni pamoja na uchimbaji wa visima 10 na ufungaji wa pampu katika visima hivyo; ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 9.8 kutoka kwenye visima kwenda kwenye mtambo wa kutibu maji; ujenzi wa mtambo wa kutibu maji eneo la Ng’apa; ujenzi wa matanki mawili (2) ya kuhifadhia maji; ulazaji wa mabomba ya mtandao wa usambazaji maji yenye urefu wa kilomita 27; kujenga bwawa la majitaka na kununua gari la majitaka. Kazi zinazoendelea ni pamoja na ufungaji wa mfumo wa uendeshaji visima na uzibaji wa mivujo na kufanya majaribio ya msukumo wa maji (Pressure test) katika bomba kuu lenye urefu wa kilomita 3.6.Utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 98 na umeanza kutoa huduma kwa wananchi. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 3.6 kwa siku hadi lita milioni 15 kwa siku na wananchi wapatao 91,968 wananufaika na huduma ya majisafi na salama.
(viii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Morogoro
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (French Development Agency-AFD) inaendelea kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Mji wa Morogoro kwa gharama ya Euro milioni 84. Utekelezaji wa mradi unahusisha kufanya tathmini ya kina ya kuongeza kimo cha tuta (embarkment height) la Bwawa la Mindu kwa mita 2.5 ili kuhifadhi maji mengi zaidi; kulaza bombalenye urefu wa kilometa 2.5 kutoka Bwawa la Mindu hadi kwenye mtambo wa kutibu maji uliopo Mafiga; kujenga mtambo mpya wa kutibu maji katika eneo la Mafiga wenye uwezo wa kutibu maji kiasi cha lita milioni 54 kwa siku; kulaza bombalenye urefu wa kilometa 15 litakalopeleka maji eneo la kingolwira kutoka birika la Tumbaku; kujenga tanki la kuhifadhia majisafi lenye ujazo wa lita 450,000 litakalosambaza maji katika eneo la Kingolwira; kujenga tanki la kuhifadhi majisafi lenye ujazo wa lita 12,050,000 katika eneo la Mafiga; kufunya kampeni za kujenga uelewa kwa wananchi katika masuala ya usafi wa mazingira, utunzaji wa vyanzo vya maji na miundombinu ya maji; na kujenga uwezo wa watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro katika masuala ya uendeshaji na matengenezo ya miundombinu ya maji kwa lengo la kupunguza upotevu wa maji.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri anaendelea na kazi ya uandaji wa Mpango Kabambe wa Rasilimali za Maji (Water Resource Master plan) wa Mji wa Morogoro; na tathmini ya kuongeza kimo cha tuta la Bwawa la Mindu kwa mita 2.5. Aidha, taratibu za ununuzi wa wakandarasi watakaotekeleza mradi kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga unaendelea. Mradi unatarajiwa kukamilika mwaka 2025 na utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 35 kwa siku hadi lita milioni 89 kwa siku.
(ix). Miradi ya Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Jiji la Mbeya
Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Kiwira hadi Jiji la Mbeya. Hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri kwa ajili ya usanifu wa mradi amepatikana na tayari ameanza kazi. Mradi huo utatekelezwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa chanzo na miundombinu ya kupeleka maji katika Jiji la Mbeya. Kukamilika kwa awamu hiyo kutawanufaisha wananchi wapatao 850,000. Awamu zitakazofuata zitahusisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji katika miji ya Chunya, Inyala, Vwawa, Mlowo na Tunduma.
Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Mbeya, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Itende.Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 9; na ujenzi wa vituo vinne (4) vya kuchotea maji. Vilevile, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa maji wa Nzovwe-Isyesye unaogharimu Shilingi milioni 400. Mradi huo unahusisha ujenzi wa chanzo cha maji; ujenzi wa tanki la kukusanyia maji (Sump well); ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji; ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 5. Hadi mwezi Aprili 2022 utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 30. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022 na utawanufaisha wakazi wapatao 30,000.
(x). Mradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Tanga
109. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Jiji la Tanga unaogharimu Shilingi bilioni 9.18. Mradi huo unahusisha ujenzi wa bomba kuu lenye urefu kilomita 12.4; ujenzi wa tanki la ujazo wa lita milioni 1; na kujenga mtambo mpya na kukarabati mtambo uliopo wa kutibu maji. Hadi mwezi Aprili 2022, mradi umefikia asilimia 12 na mradi huo ukikamilika utawanufaisha wananchi wapatao 382,095.
(xi). Miradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Mji wa Babati
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji Darakuta – Magugu uliogharimu Shilingi bilioni 3.998. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa chanzo cha maji; ulazaji wa bomba kuu la kusafirisha maji lenye urefu wa kilomita 20; ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 73; ujenzi wa mtambo wa kuchuja na kutibu maji lita milioni 5 kwa siku; ununuzi wa dira za maji 4000; ujenzi wa nyumba ya mlinzi na ujenzi wa uzio kuzunguka mtambo wa kuchuja na kutibu maji. Mradi huo unanufaisha wananchi wapatao 58,941.
Vilevile, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji Dareda-Singu-Sigino-Bagara kwa gharama ya Shilingi bilioni 12.77. Mradi huo unahusisha ujenzi wa matanki matano (5) ya kuhifadhia maji yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 4.1; ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 63.31; ujenzi wa bomba kuu la ksafirisha maji lenye urefu wa kilomita 26.83; ujenzi wa vituo viwili (2) vya kusukuma maji (booster stations); ununuzi na ufungaji wa pampu mbili (2) za kusukuma maji; ujenzi wa mtambo wa kuchuja na kutibu maji; na ujenzi wa chanzo. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 150,000 pamoja na ujenzi wa chanzo. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 30. Mradi ukikamilika utanufaisha wananchi wapatao 60,000.
3.2.4.2 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa
(i). Mji wa Orkesumet
Mheshimiwa Spika, Mradi wa maji katika Mji wa Orkesumet unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu (BADEA) na Mfuko wa Nchi zinazozalisha mafuta kwa maendeleo ya kimataifa (OPEC Fund for International Development – OFID). Utekelezaji wa mradi huoumekamilika kwa gharama ya Shilingi bilioni 38.11 ambapo kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji na mtambo wa kutibu na kusafisha maji; ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 35; vituo vitatu (3) vya kusukuma maji; matanki tisa (9) yenye ujazo kuanzia lita 50,000 hadi lita milioni 1.6; mtandao wa usambazaji maji wenye urefu wa kilomita 64; vituo 10 vya kuchotea maji; birika 10 za kunyweshea mifugo; ujenzi wa ofisi; ununuzi na ufungaji wa pampu; crane; na kupeleka umeme kwenye chanzo. Mradi huu unanufaisha wakazi wapatao 52,000 pamoja na mifugo yao.
(ii). Mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Namanga na eneo la Kimokouwa.
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha mradi wa kuboresha huduma ya maji katika mji wa Namanga na eneo la Kimokouwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.88. Mradi huo umehusisha ulazaji wa mtandao wa mabomba urefu wa kilomita 40.948; ujenzi wa vituo vya kuchotea maji; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 225,000;Ukarabati wa matanki manne; ujenzi wa uziona ujenzi wa chemba za Airvalves na Washout. Mradi huo umewanufaisha wananchi wapatao 29,686.
(iii). Mradi wa Maji Mugango – Kiabakari – Butiama
114. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (Saudi Fund for Development – SFD) imeanza kutekeleza mradi wa maji utakaohudumia maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 30.69. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa choteo la maji katika Ziwa Victoria; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kusukuma maji; ujenzi wa tanki kubwa la maji safi eneo la Mugango pamoja na mantaki matano (5) katika maeneo ya Kong, Kiabakari, Butiama Hill na Bumangi; ulazaji wa bomba kuu kutoka Mugango kwenda Kiabakari hadi Butiama lenye urefu wa kilomita 48; ulazaji wa mabomba ya mtandao wa kusambaza maji wenye urefu kilomita 140; ujenzi wa ofisi na nyumba za wasimamizi wa mitambo; ukarabati wa matanki mawili (2) katika maeneo ya Kyatungwe na Bisarye; ujenzi wa vioski 40 vya maji na ununuzi wa dira za maji 2,000. Hadi mwezi Aprili, 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 54 na unatarajia kukamilika mwezi Desemba, 2022. Mradi huo utanufaisha wananchi zaidi ya 100,000 waliopo katika eneo la mradi pamoja na vijiji vilivyopo ndani ya kilomita 12 kutoka bomba kuu.
(iv). Miji ya Tinde na Shelui
115. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India kupitia Benki ya Exim-India inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji ya Tinde na Shelui. Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 10.6. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa matanki mawili (2) ya Tinde na Shelui; ukarabati wa matanki mawili katika eneo la Shelui; na ujenzi wa kituo cha kusukuma maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60.7 na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022.Mradi huo utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 86,984wa miji ya Tinde na Shelui.
(v). Mji wa Bunda
116. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Bunda unaopata maji kutoka Ziwa Victoria kwa kujenga mfumo wa kusafisha na kutibu maji katika eneo la Nyabehu. Mradi huo unagharimu Shilingi bilioni 10.60 na hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wake umefikia asilimia 90 na wananchi wameanza kupata huduma ya majisafi. Mradi huo utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 1,200,000 wa Mji wa Bunda.
(vi). Mradi wa Maji Kyaka – Bunazi
117. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa majisafi wa Kyaka – Bunazi kwa gharama ya Shilingi bilioni 15.74. Mradi huo unatekelezwa kwa vipande (Lots) viwiliambapo kipande cha kwanza kinahusisha ujenzi wa chanzo cha maji katika mto Kagera chenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 6.57 kwa siku; ulazaji wa bomba kuu urefu wa kilomita 1.6; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kutibu maji; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 2; na ujenzi wa jengo la mradi. Kipande cha pili kinahusisha ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wakilomita 14; ulazaji wa mtandao wa mabomba yakusambaza maji wenye urefu wa kilomita 60; ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji; na kuunganisha wateja wapatao 1,000. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asimilia 92 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022.
(vii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Mji wa Chato
118. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi katika mji wa Chato kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.91 ambapo wananchi wapatao 16,000 wananufaika na huduma ya majisafi. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 16.66; ukarabati wa kituo cha kusukuma maji Rubambangwe; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji yenye wa kilomita 41.94 katika mitaa ya Itale, Nyabilezi, Uwanja wa Ndege, Chato Beach, Kahumo na maeneo ya katikati ya mji; ujenzi wa matanki mawili ya kuhifadhia maji katika maeneo ya Itale (lita 300,000) na Uwanja wa Ndege (lita 150,000); ufungaji wa pampu mbili zenye uwezo wa kuzalisha lita 160,000 kwa saa kila moja; ufungaji wa Transformer pamoja na ujenzi wa njia kuu ya umeme; na ufungaji wa mtambo wa kutibu maji “Mobile Water Treatment Plant”.
(viii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji KatoroBuseresere
119. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji midogo ya Katoro na Buseresere kwa gharama ya Shilingi bilioni 4.26. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 500,000; ujenzi wa bomba kuu la kusafirisha maji kilomita 24.6 kutoka Chankorongo mpaka eneo la tanki jipya Katoro; ujenzi wa bomba la kusambaza maji kilomita 26; Ujenzi wa mtambo wa kutibu maji “ Mobile treatment Plant” na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji. Hadi mwezi Aprili2022, utekelezaji wa mradi umefikia asimilia 80 ambapo wananchi 71,100 watanufaika na huduma ya majisafi.
(ix). Mradi wa Maji Same – Mwanga – Korogwe
120. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo kutoka Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu kwa Nchi za Kiafrika (BADEA), Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha Mafuta (OFID), Mfuko wa Maendeleo wa Saudi Arabia (SFD) na Serikali ya Kuwait kupitia
Mfuko wa Maendeleo (KFD) inatekeleza Mradi wa Maji SameMwanga-Korogwe. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asilimia 70.4. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni pamoja naujenzi wa chanzo, chujio na ulazaji bomba kutoka chanzo mpaka kwenye chujio na kutoka kwenye chujio hadi tanki la Kisangara;ulazaji wa bomba kutoka Kisangara hadi Kiverenge na kutoka Kiverenge hadi Vudoi/Mwanga nakujenga miundombinu ya kusambaza maji katika miji ya Same na Mwanga.Hata hivyo, mradi huo ulikuwa na changamoto za Wakandarasi ambapo kwa sasa Serikali imechukua hatua za kupata Wakandarasi wengine ili kukamilisha kazi zilizobaki.
(x). Mradi wa maji Kayanga/Omurushaka-Karagwe
121. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa maji Kayanga/Omurushaka – Karagwe ili kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika miji ya Omurushaka na Kayanga kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.88. Mradi unahusisha uchimbaji wa visima virefu viwili (2); ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 30; ufungaji wa pampu sita (6); ujenzi wa viosk vinne (4); ununuzi wa pikipiki mbili (2); Ununuzi wa mfumo wa ankra; na ununuzi wa vitendea kazi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 95. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2022 na utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 25 hadi asilimia 40.
(xi). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji 28
122. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India kupitia Benki ya Exim – India inategemea kuanza ujenzi wa mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji 28 ya Tanzania Bara na mji mmoja visiwani Zanzibar kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 500. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kuwapata wakandarasi wa ujenzi katika miji 24 zimekamilika ambapo ujenzi wa miradi katika miji hiyo itatumia fedha za mkopo wa India na miji minne (4) ya Mafinga, Makonde, Songea na Tarime-Ryorya utekelezaji wake utafanywa kwa kutumia fedha za ndani. Mikataba ya ujenzi itasainiwa kabla ya kumalizika kwa mwaka wa fedha 2021/22.
3.2.4.3 Mradi wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko
ya Tabianchi katika Mkoa wa Simiyu
123. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya KfW kwa niaba ya Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) inatekeleza mradi wa kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabianchi katika wilaya tano (5) za Mkoa wa Simiyu ambazo ni Busega, Bariadi, Itilima, Maswa na Meatu. Katika awamu ya kwanza mradi wa maji utatekelezwa katika Wilaya za Busega, Itilima na Bariadi. Mradi huo unakadiriwa kugharimu jumla ya kiasi cha Euro milioni 171, ambapo GCFwatachangia Euro milioni 102.7, Benki ya KfW itachangia Euro milioni 26.1, Serikali ya Tanzania Euro milioni 40.7 na Wananchi kupitia nguvu zao watachangia Euro milioni 1.5. Aidha, awamu ya kwanza ya fidia kiasi cha Shilingi bilioni 1.52 kimelipwa kwa wananchi wapatao 1,201 kati ya 1,308 waliotathiminiwa. Hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri wa kujenga uwezo kwa wataalam wa Mamlaka za Maji na Wizara amepatikana na tayari amenza kazi. Vilevile, Mtaalam Mshauri wa kufanya mapitio ya usanifu na usimamizi wa mradi amepatikana na anaendelea na kazi ya mapitio ya usanifu. Serikali inaendelea na taratibu za kuwapata wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mradi.
3.2.4.4 Miradi ya Maji katika Maziwa Makuu ya
Victoria, Tanganyika na Nyasa
124. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya kandokando ya maziwa makuu wanapata huduma ya maji safi, salama na ya kutosheleza, Serikali inakamilisha usanifu wa kina kwa ajili ya kutumia chanzo cha ziwa Victoria kwenye mikoa ya Mwanza, Geita, Simiyu, Kagera na Mara; ziwa Tanganyika kwenye mikoa ya Katavi, Kigoma na Rukwa; pamoja na ziwa Nyasa katika mikoa ya Ruvuma na Njombe. Hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-
(i). Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa
Victoria
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni ya miradi 45 iliyobainishwa kutumia chanzo cha maji cha Ziwa Victoria kupeleka huduma ya maji katika vijiji vinavyozunguka ziwa hilo. Miradi hiyo itagharimu Shilingi bilioni 750.69 na itakapokamilika itahudumia wananchi wapatao 2,854,292 wa vijiji 324 vya Halmashauri za Wilaya za Geita vijiji 37, Chato (21), Nyangh’wale (9) na Mbogwe vijiji 18 katika Mkoa wa Geita; Sengerema vijiji 33, Magu (16), Misungwi (17), Buchosa (29),Ukerewe (35) na Manispaa ya Ilemela vijiji vitatu (3) katika
Mkoa wa Mwanza; Manispaa ya Bukoba (4), Bukoba
Vijijini(11), Muleba (8), Biharamulo (12), na Missenyi vijiji nane (8) katika Mkoa wa Kagera; Musoma Vijijini (32), Rorya (20) na Bunda vijiji 11 katika Mkoa wa Mara.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Serikali inaendelea na ujenzi wa mradi wa maji wa Nkome katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa gharama ya Shilingi bilioni 4.6. Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 20 ambapo ukikamilika utahudumia vijiji 17 kwenye kata za Lwezera, Nyamboge, Nzera, Katome na Nkome.
(ii). Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa Tanganyika
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kupata Wakandarasi wa ujenzi wa miradi 32 iliyobainishwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika. Miradi hiyo, itagharimu Shilingi bilioni 117.412 na inatarajiwa kuwanufaisha wakazi wapatao 616,000 wa vijiji 79 vya Halmashauri zifuatazo: – Kigoma Vijijini: vijiji 8; Uvinza: Vijiji 7; Nkasi: Vijiji 32; Kalambo: Vijiji 8; Mpimbwe: Vijiji 6; na Tanganyika: Vijiji 11.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi wa Mradi wa maji Kirando – Kamwanda uliopo katika Wilaya ya Nkasi umefikia asilimia 98 na umeanza kutoa huduma kwa wakazi wapatao 74,000 wa vijiji 8 vya Kirando, Kamwanda, Mtakuja, Itete, Chongo, Katete, Kichangani na Isasa. Mradi huo unatumia chanzo cha maji cha Ziwa Tanganyika na unagharimu Shilingi bilioni 3.07. Vilevile, Serikali imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa Kabwe unaohudumia vijiji vya Kabwe, Kabwe Camp na Udachi vilivyopo Mkoa wa Rukwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.6. Aidha, Serikali inaendelea na ujenzi wa miradi ya maji ya Korongwe utakaohudumia vijiji vya Korongwe na Karungu; na mradi wa maji Kipwa utakaohudumia vijiji vya Kipwa na Kipele kwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika.
(iii). Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa Nyasa
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na usanifu wa kina wa miradi itakayotumia chanzo cha maji cha Ziwa Nyasa. Miradi hiyo itatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwenye Mkoa wa Ruvuma na Halmashauri ya Ludewa ilipo katika Mkoa wa Njombe. Miradi hiyo inatarajiwa kuhudumia wananchi wapatao 30,000 wa vijiji 11 vya Wilaya ya Ludewa na wananchi wapatao 120,000 wa vijiji 30 vya Wilaya ya Nyasa.
3.2.4.5 Miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi
wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji ni mojawapo ya
Wizara zinazotekeleza Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 kwa lengo lakuhakikisha wananchi wa Tanzania wanapata majisafi, salama na ya kutosheleza karibu na makazi yao ili waweze kupambana na UVIKO-19.Kupitia mpango huo, Wizara imetengewa Shilingi bilioni 139.35 kwa ajili ya kutekeleza jumla ya miradi 218 ambapo miradi 172 ni ya maji vijijini na 46 ni miradi ya maji mijini pamoja na ununuzi wa seti 25 za mitambo ya kuchimba visima; seti 5 za ujenzi wa mabwawa; na seti 4 za vifaa vya utafiti wa maji chini ya ardhi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa miradi ya maji vijijini umefikia wastani wa asilimia 46 na miradi ya maji mjini asilimia 67 ambapo utekelezaji wa miradi hiyo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. Kukamalika kwa miradi hiyo kutawanufaisha zaidi ya wananchi 2,093,800. Aidha, kwa upande wa ununuzi wa mitambo mikataba ya ununuzi imesainiwa tarehe 08 Februari, 2022 na inatarajiwa kupokelewa mwishoni mwa mwezi Juni, 2022.
3.2.5 Miradi ya Usafi wa Mazingira
131. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo ya miji mikuu ya mikoa, miji mikuu ya wilaya na miji midogo. Lengo ni kuimarisha huduma ya usafi wa mazingira nchini kwa kulinda afya za wananchi na mazingira.Katika kuimarisha huduma ya uondoshaji majitaka katika maeneo ya mijini Serikali imejenga, kupanua na kukarabati miundombinu ya majitaka katika maeneo mbalimbali ya mijini. Kutokana na jitihada hizo, idadi ya wateja waliounganishwa kwenye mtandao wa majitaka imeongezeka kutoka wateja 52,661 mwezi Machi, 2021 hadi wateja 53,428 mwezi Aprili 2022.Miradi inayoendelea kutekelezwa ni pamoja na:-
(i). Mradi wa Ujenzi wa Mfumo Rahisi wa Uondoshaji Majitaka Maeneoya Milimani katika Jiji la Mwanza
132. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mfumo rahisi wa uondoshaji majitaka maeneo ya milimani katika Jiji la Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.84. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa mtandao wa mabomba ya majitaka yenye urefu wa kilomita 17.595; na kuunganisha wateja 6,042 katika maeneo ya Igogo-Sahara, Isamilo, Kabuholo na Ibungiro. Vilevile,Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa mfumo rahisi wa uondoshaji majitaka katika maeneo ya Mabatini, Kilimahewa A, Kilimahewa B na Pasiansi unaogarimu Shilingi bilioni 3.72. kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa mtandao wa mabomba ya majitaka yenye urefu wa kilomita 15.79; ujenzi wa chemba, ujenzi wa ngazi, uboreshaji wa squattingpan na kuunganisha wateja 900. Hadi mwezi Aprili 2022 utekelezaji umefikia asilimia 12.
(ii). Mradi wa Usafi wa Mazingira Eneo la Ilemela
133. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa upanuzi wa mabwawa ya kutibu majitaka katika eneo la Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 6.74. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 40.
(iii). Ujenzi wa Vyoo mashuleni katika Jiji la Mwanza
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha kwanza kwenye shule na maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza Wilaya ya Nyamagana kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.25.
Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 12 na mradi utakapokamilika utanufaisha wanafunzi 21,124 katika shule 12. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 98. Vilevile, Serikali imekamilisha ujenzi wa vyoo kipande cha pili kwenye shule na sehemu za wazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.31 Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 12 na Zahanati mbili na mradi huo unawanufaisha wanafunzi 18,679 katika shule 12.
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha tatu kwenye shule na maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza Wilaya ya Nyamagana kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.69. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 11 na mradi utakapokamilika utanufaishawanafunzi 21,124. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 63. Vilevile, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha nne kwenye shule na sehemu za wazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.79. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 10 na Zahanati mbili na mradi huo unawanufaisha wanafunzi 18,679 katika shule 10. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 55.
(iv). Mradi wa Ukarabati wa Mfumo wa Majitaka katika Maeneo ya Area C na D katika Jiji la Dodoma
136. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ukarabati wa mfumo wa majitaka katika maeneo ya Area C na Area D yaliyopo Jijini Dodoma unaogharimu Shilingi bilioni 4.96. Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ukarabati wa bomba za majitaka urefu wa kilomita 19 pamoja na kujenga chemba 1,005 za majitaka. Kazi zilizofanyika ni ukarabati wa mabomba ya majitaka urefu wa kilomita 5.959 pamoja na ujenzi wa chemba 40. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 33 na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2022.
(v). Mradi wa Upanuzi wa Mfumo wa Majitaka katika
Maeneo ya Korongoni na Longuo “A” Manispaa ya Moshi
137. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika Manispaa ya Moshi kwa kujenga mradi wa upanuzi wa mfumo wa majitaka katika kata za Korongoni na Longuo “A” kwa gharama ya Shilingi bilioni 1. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujezi wa bomba la majitaka lenye urefu wa kilomita 12.99; na ujenzi wa chemba 171. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo zimekamilika ambapo ujenzi utaanza mwezi Juni 2022.
(vi). Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Majitaka katika Mji wa Nzega
138. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya uondoshaji wa majitaka katika Mji wa Nzega kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.5. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa bwawa la majitaka na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022.
(vii). Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida
139. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida kwa gharama ya Shilingi bilioni 1. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa mabwawa ya kutibu majitaka; ujenzi wa jengo la walinzi na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili 2022,mradi umefikia hatua za mwisho za kupata mkandarasi atakaetekeleza mradi huo inaendelea na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2022.
(viii). Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Majitaka katika Mji wa Muheza
140. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika mji wa Muheza kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.03. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa miundombinu ya kutibu majitaka (Feacal Sludge Treatment Facilities – FSTF); ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka; ununuzi wa gari ya usimamizi, ujenzi wa barabara ya kufika eneo la bwawa; na ujenzi wa vyoo shuleni na stendi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2022 na kunufaisha wakazi wapatao 38,131 wa Mji wa Muheza.
(ix). Miradi ya Usafi wa Mazingira katika Maeneo ya
Vijijini
141. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza Kampeni ya Usafi wa Mazingira kwa lengo la kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo ya vijijini. Katika mwaka 2021/22, Wizara yangu inaendelea na utekelezaji wa miradi 413 ya usafi wa mazingira katika vituo vya kutolea huduma za afya na shule. Hadi mwezi Aprili 2022, miradi 137 imekamilika na miradi 276 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
3.2.6 Taasisi zilizo Chini ya Wizara
(i). Mfuko wa Taifa wa Maji
Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha Mfuko wa Taifa wa Maji kupitia Sheria Na.12 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009. Kwa sasa Mfuko unatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019. Majukumu ya Mfuko ni kutafuta fedha, kutoa fedha kwa watekelezaji wa miradi ya maji na kufuatilia matumizi ya fedha hizo. Wanufaika wa fedha za Mfuko wa Maji ni pamoja na RUWASA, Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira Mijini, Bodi za Maji za Mabonde na Wizara ya Maji.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu Na. 55 cha Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019, vyanzo vya mapato ya Mfuko ni pamoja na fedha zitakazoidhinishwa na Bunge, misaada pamoja na fedha nyingine zitakazolipwa kwenye Mfuko kwa mujibu wa Sheria nyingine. Kwa sasa chanzo pekee cha mapato ya Mfuko ni tozo ya shilingi 50 kwa kila lita ya mafuta ya diseli na shilingi 50 kwa kila lita ya petroli. Katika mwaka 2021/22, Mfuko wa Taifa wa Maji ulikadiriwa kupata mapato ya Shilingi 175,912,837,000 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ambapo hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya Shilingi 137,956,116,703.40 sawa na asilimia 78 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa huduma ya maji mijini na vijijini pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuongeza mapato ya Mfuko wa Taifa wa Maji, Mfuko umekamilisha taratibu za kuanzisha zoezi la utoaji wa mikopo ya riba nafuu (Loan Window) kwa Mamlaka za Maji na taasisi zinazotoa huduma ya maji nchini zitakazo kidhi vigezo. Mpango huo unatarajiwa kuanza katika mwaka 2022/23 na tayari Mfuko umetenga fedha za kuanzia (seed money) kiasi cha Shilingi bilioni 15. Utaratibu huo unatarajiwakuongeza wigo wa upatikanaji wa fedha kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na hivyo kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maji nchini. Aidha, Serikaliimeendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Maji katikauandaaji wa maandiko ya miradi (Fundable/Bankable Projects Write ups) kwa ajili ya kupata fedha za kutosha za ujenzi wa miradi ya maji.
(ii). Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA)
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuijengea uwezo RUWASA ili iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Katika mwaka 2021/22, jumla ya magari 33 yamenunuliwaambapo magari 17 yaligawanywa katika Wilaya 17 ambazo hazikuwa na vyombo vya usafiri. Wilaya hizo niKilindi (Tanga), Kalambo (Rukwa), Nyangw’ale, Mbogwe
Kyerwa (Kagera), Itilima (Simiyu), Kaliua (Tabora), Nsimbo na Mlele (Katavi), Mafia (Pwani) na Lindi (Lindi). Vilevile, Magari 7 yaligawanywa katika mikoa ya Manyara, Tanga, Simiyu, Songwe, Ruvuma, Njombe na Katavi; na magari 9 yalipelekwa Ofisi ya RUWASA Makao Makuu.
Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha na kuboresha usimamizi wa fedha za umma, RUWASA ilijiunga na Mifumo mbalimbali ya TEHAMA ya Serikali ikiwemo Mfumo wa Kielektroniki wa Makusanyo ya Fedha Serikalini (Government e-Payment Gateway), Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (Tanzanian National e-Procurement System) na Mfumo wa Kielektroniki wa Mipango, Bajeti na Taarifa (PLANREP). Pia, RUWASA ilianzisha Mfumo wa Utoaji Taarifa za Huduma ya Maji Vijijini (RUWASA Service Delivery Management System – RSDMS) kwa lengo lakuwezesha upatikanaji wa taarifaza utekelezaji, usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji vijijini.Mfumo umewezesha RUWASA kuongeza ufanisi katika utekelezaji, usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji vijijini.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi, RUWASA imenunua kiwanja eneo la Njedengwa Investment, chenye ukubwa wa mita za mraba 34,500 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Makao Makuu, Ofisi ya Mkoa wa Dodoma pamoja na Ofisi wilaya ya Dodoma. Vilevile, RUWASA imenunua viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za RUWASA mikoa ya Geita, Mara, Katavi na Wilaya ya Nyasa.
(iii). Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira
Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira zimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya
Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019.
Mamlaka hizo, zimepewa jukumu la kutoa huduma za majisafi na salama pamoja na usafi wa mazingira katika maeneo ya mijini. Katika kuimarisha usimamizi wa huduma ya majisafi na usafi wa Mazingira Wizara imeanzisha jumla ya Mamlaka 94 za Majisafi na Usafi wa Mazingira katika maeneo mbalimbali ya mijini. Maeneo ya Miji Mikuu ya Mikoa kuna Mamlaka 25 za Majisafi na Usafi wa Mazingira; Mamlaka saba (7) za Miradi ya Kitaifa; Mamlaka 54 katika Miji Mikuu ya Wilaya; na Mamlaka nane (8) katika Miji Midogo.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali imeendelea kuziimarisha mamlaka za maji kwa kujenga ofisi katika Mamlaka za Maji za Arusha, Bunda, Makambako, Mugango-Kiabakari na Biharamulo. Aidha, Serikali imetoa mafunzo ya kujenga uwezo wa menejimenti na Bodi za Wakurugenzi kwa Mamlaka 40 za Majisafi na Usafi wa Mazingira ili kuongeza ufanisi katika uendeshaji na usimamizi wa mamlaka hizo.
(iv). Chuo cha Maji
Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maji ni Taasisi yenye jukumu la kuandaa wataalam wa Sekta za maji na umwagiliaji. Majukumu mengine ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam na kufanya tafiti mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya Sekta. Chuo kinatoa mafunzo katika ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada. Katika ngazi ya Astashahada na Stashahada mafunzo yanayotolewa ni Uhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira (Water Supply and Sanitation Engineering); Uhandisi wa Umwagiliaji (Irrigation Engineering); Haidrojiolojia na Uchimbaji wa Visima (Hydrogeology and Water Well Drilling); Haidrolojia na Hali ya Hewa (Hydrology and Meteorology); pamoja na Teknolojia ya Maabara na Ubora wa Maji (Water Quality Laboratory Technology). Katika ngazi ya Shahada, mafunzo yanayotolewa ni katika fani ya Uhandisi wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji (Bachelor of Engineering in Water Resources and Irrigation). Vilevile, Chuo kinaendesha kozi mbalimbali za muda mfupi katika sekta za maji na umwagiliaji.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, wanafunzi 656 wa Astashahada na Stashahada wamedahiliwa. Vilevile, wanafunzi 247 wa Shahada ya kwanza ya Uhandisi wa
Rasilimali za Maji na Umwagiliaji walidahiliwa ikilinganishwa na wanafunzi 218 katika mwaka 2020/21. Kwa sasa, chuo kina jumla ya wanafunzi 2,256 ambapo wanafunzi 1,466 ni wa Astashahada na Stashahada na wanafunzi 790 ni wa Shahada ya kwanza. Aidha, katika mahafali ya Novemba 2021, jumla ya wanafunzi 494 walihitimu mafunzo yao ambapo wanafunzi 138 ni wa Shahada, 305 wa Stashahada na wahitimu 51 walikuwa wa ngazi ya Astashahada.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha taaluma bora inatolewa, Chuo kimeendelea kuwajengea uwezo watumishi wake katika ngazi za Shahada ya kwanza, Uzamili na Uzamivu. Hadi mwezi Aprili 2022, watumishi 10 wanaendelea na mafunzo ya Shahada ya Uzamivu (PhD); Watumishi watatu (3) ni Shahada ya Uzamili (Masters) na watumishi wanne (4) ni Shahada ya kwanza. Vilevile, kupitia fedha za ndani, Chuo kimekamilisha ujenzi wa zahanati, upanuzi wa maabara ya Hydraulics na ukarabati wa jengo moja la hostelilenye uwezo wa kulazawanafunzi wapatao 140. Aidha, chuo kimenunua vifaa vya maabara za Hydraulics na Hydrogeology pamoja na kompyuta 96 kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi kwa kampasi ya Singida na Kampasi kuu Ubungo.
3.2.7 Masuala Mtambuka
(i). Ujenzi wa Majengo Katika Wizara
153. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea na ujenzi wa jengo la Makao Makuu – Mtumba ambao ulianza rasmi tarehe 3 Novemba, 2021 na unagharimu Shilingi bilioni 22.97. Hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi umefikia asilimia 33 na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2022. Aidha, Wizara imekamilisha ujenzi wa ofisi za Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini katika miji ya Lindi na Mtwara. Vilevile, Wizara inaendelea na ukarabati na ujenzi wa Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde ambapo Ofisi ya Bonde la Ziwa Nyasa umefikia asilimia 60; Ziwa Rukwa (85); Wami-Ruvu (95); na Rufiji asilimia 63. Kwa upande wa Maabara za Maji, ujenzi wa maabara ya Maji Mtwara na ukarabati wa Maabara ya Dar es salaam umekamilika. Ujenzi wa Maabara ya Morogoro umefikia asilimia 95; Sumbawanga (85); Mbeya (87); na Songea asilimia 60.
(ii). Kuimarisha mifumo ya TEHAMA
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kuboresha huduma zinazotolewa na Sekta. Katika mwaka 2021/22, Wizara kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imebuni, imesanifu na kutengeneza Mifumo Jumuishi miwili ambayo niMfumo wa Taarifa za Miradi Kiganjani unaofahamika kama Maji Mobile App na Mfumo wa Pamoja wa Kusimamia Huduma za Ankara (Unified Maji Billing System) unaofahamika kama MajiIS. Mfumo wa Taarifa za Miradi Kiganjani unarahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za miradi iliyokamilika na inayoendelea katika kila mkoa pamoja kurahisisha ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maji yote nchini.
Mheshimiwa Spika, mfumo wa MajiIS umetengenezwa mahususi kwa ajili ya kusimamia ankara za maji zinazotolewa na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini pamoja na Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde. Mfumo huo umerahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kuwarahisishia ulipaji nauhakiki wa ankara za maji kulikopelekea kupungua kwa malalamiko yanayohusu ankara za maji katika Mamlaka ambazo zimeanza kutumia mfumo huo. Vilevile, mfumo umepunguza gharama na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ukilinganisha na mifumo iliyokuwa ikitumika awali.
Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya Mamlaka 68 kati ya 91 za Majisafi na Usafi wa Mazingiara za Miji Mikuu ya Mikoa, Miji ya Wilaya, Miji Midogo pamoja na Miradi ya Kitaifa zimejiunga na zinatumia Mfumo huo. Hii ni sawa na asilimia 74.7 ya Mamlaka zote zinazopaswa kujiunga kwenye Mfumo. Aidha, zoezi la kuunganisha Mamlaka zilizobakia ikiwemo Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) pamoja na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Zanzibar (ZAWA) linaendelea kwa hatua ya mafunzo.
(iii). Mapambano Dhidi ya Rushwa
157. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji wa Awamu ya Tatu (National Anti-Corruption Strategy and Action Plan – NACSAP III) kwa lengo la kupambana na vitendo vya rushwa kwenye maeneo yote ya kazi. Vilevile, Wizara iliunda Kamati ya Uongozi na Usimamizi pamoja na Kamati ya Uadilifu kwa ajili ya kusimamia mapambano dhidi ya rushwa ngazi ya Wizara na Taasisi zake. Tangu kuundwa kwa Kamati hizo, malalamiko dhidi ya viashiria vya rushwa yamepungua kwenye manunuzi ya wakandarasi na huduma zinazotolewa. Aidha,Wizara imeendelea kuzijengea uwezo kamati hizo na kuwafanyia upekuzi watumishi.
(iv). UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza
158. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza Mwongozo wa UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza kwa kutoa elimu kuhusu magonjwa hayo kwa watumishi wa Wizara na Taasisi zake. Hadi mwezi Aprili, 2022, jumla ya watumishi 3,283 walipata mafunzo maalum kuhusu kujikinga na magonjwa yasioambukiza na yanayoambukiza. Aidha, posho kwa ajili ya kununua lishe bora na usafiri kwa watumishi 21 wanaoishi na virusi vya UKIMWI imeendelea kutolewa.
(v). Jinsia
159. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha uwepo wa uwiano wa kijinsia katika Taasisi zake. Uwiano huo ni muhimu kwenye vyombo vya maamuzi, usimamizi, uendeshaji na utekelezaji wa miradi nchini.Hadi mwezi Aprili 2022, idadi ya watumishi wanawake ni 2,762 sawa na asilimia 30 ikilinganishwa na wanaume 6,445 sawa na asilimia 70. Aidha, viongozi wa ngazi mbalimbali wa Wizara na Taasisi waliopo wanawake ni 201 sawa na asilimia 24 na wanaume ni 622 sawa na asilimia 76. Vilevile, uteuzi wa kamati mbalimbali huzingatia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha watumishi wote wanashiriki kikamilifu katika kutekeleza majukumu yao. Aidha, katika kuimarisha masuala ya jinsia katika Sekta ya Maji, Wizara imeandaa mkakati wa masuala ya jinsia ambao utatoa mwongozo katika kufikia malengo ya kitaifa ya uwiano wa jinsia wa angalau theluthi moja kwa wanawake.
(vi). Rasilimali Watu katika Sekta ya Maji
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Sekta ya maji inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi, jumla ya watumishi 10,276 wanahitajika ikilinganishwa na watumishi 9,207 waliopo na hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 1,069. Kati ya watumishi waliopo wahandisi (Engineers) ni 704 ambapo 499 sawa na asilimia 70 wamesajiliwa na Bodi ya Usajili ya Wahandisi nchini (Engineers Registration Board – ERB) kama wahandisi wataalam na wahandisi 205 sawa na asilimia 30 wapo kwenye hatua mbalimbali za kusajiliwa. Lengo ni kuona kuwa wahandisi wote wanasajiliwa ndani ya kipindi cha miaka mitatu tangu walipoajiriwa ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maji inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta imeendelea kuwajengea uwezo watumishi wake kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuwapatia mafunzo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya watumishi 1,828 wamepata mafunzo ambapo kati yao watumishi 1,650 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi na watumishi 178 walipata mafunzo ya muda mrefu ndani ya nchi.
4. MAFANIKIO YALIYOPATIKANA
162. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, Sekta ya Maji imeendelea kufanya maboresho ya kiutendaji na kitaasisi ambayo yameleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara na miradi mbalimbali. Kuimarika kwa ufanisi huo katika Sekta ya Maji kumeleta mafanikio yakiwemo:-
(i).
Kuongezeka kwa kiwango cha upatikanaji wa huduma za maji nchini kutoka asilimia 72.3 vijijini na 86 mijini mwaka 2020/21 hadi asilimia 74.5 vijijini na 86.5 mijijni;
(ii).
Kukamilika kwajumla ya miradi 343 ya maji ambapo kati ya hiyo ya vijijini ni miradi 303 na mijini miradi 40. Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na Misungwi,Orkesumet, Chalinze-Mboga, na Longido;
(iii).
Kukamilika na kuanza kutumika kwa mfumo wa taarifa za miradi na huduma ya maji ambao utakuwa ukipatikana kupitia simu za kiganjani unaojulikana kwa jina la Maji Mobile Application (Maji_App). Mfumo huoumerahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za miradi ya maji pamoja na hali ya huduma ya maji nchini;
(iv).
Kukamilika na kuanza kutumika mfumo wa pamoja wa Uandaaji wa Ankara za Malipo ya Maji (Unified Billing System) unaosaidia kupunguza malalamiko ya ankara za maji kwa wateja wa huduma za maji; na
(v).
Kuimarika kwa usimamizi wa rasilimali za maji kwa kuendelea kutambua, kuweka mipaka na kuhifadhi vyanzo 178 vya maji pamoja na kuandaliwa kwa mipango ya utunzaji wa maeneo ya vidakio vya maji katika mabonde yote nchini.
5. CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA NA HATUA
ZINAZOCHUKULIWA
163. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana wakati wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2021/22, Wizara imekabiliwa na changamoto mbalimbali. Changamoto hizo na maelezo yake pamoja na hatua zinazochukuliwa kukabiliana nazoni kama ifuatavyo:-
a) Upotevu wa Maji (Non – Revenue Water)
Mheshimiwa Spika, upotevu wa maji umeendelea kuwa changamoto katika Sekta ya Maji na kusababisha hasara kwa Mamlaka za Maji zinazotekeleza na kusimamia miradi ya maji nchini. Katika mwaka 2021/22, hali ya upotevu wa maji nchini imefikia asilimia 36.2 kiwango ambapo kipo juu ya kiwango kinachokubalika kimataifa cha asilimia 20. Hali hiyo kwa sehemu kubwa inasababishwa na uchakavu wa miundombinu ya kusambaza maji; uhujumu wa miundombinu ya maji; pamoja na wizi wa maji kwa kufanya maunganisho yasiyo ya halali kwa kutumia vishoka.
Katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa maji, Wizara imeendelea kuziwezesha Mamalaka za Maji katika ukarabati na uboreshaji wa miundombinu chakavu ya maji; kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda miundombinu ya maji pamoja na kurekebisha Sheria za Maji ili ziweze kutoa adhabu kali kwa wezi wa maji na wahujumu miundombinu ya maji; kufunga dira za maji zikiwemo dira za malipo ya kabla (pre-paid meters) pamoja na bulk water meters; pamoja na kuanzisha mfumo wa pamoja wa ankara za maji (Unified Billing System) ambao umesaidia kudhibiti upotevu wa maji kwa sababu unamtaka msomaji wa mita kufika na kusoma matumizi halisi ya maji katika mita husika. Vilevile, Serikali ipo katika hatua za awali za kuanza matumizi ya mifumo wa kieletroniki wa kufuatilia taarifa za maji katika mfumo wa usambazaji maji (Supervisory Control and Data Acquisition System – SCADA). Mfumo huo utasaidia kubaini mivujo mapema na kufanya ukarabati hivyo kupunguza maji yanayopotea.
b) Mahitaji makubwa ya fedha kwa ajili ya uwekezaji wa miradi mikubwa ya maji
166. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi mikubwa ya maji ikiwemo ujenzi wa mabwawa makubwa na miradi ya kutoa maji kwenye maziwa kupeleka maeneo mbalimbali,unahitaji kiasi kikubwa cha fedha jambo linalosababisha kuchelewa kuanza utekelezaji wa baadhi ya miradi hiyo ikiwemo bwawa la Kidunda na Farkwa. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali imeendelea kutafuta fedha kutoka vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutumia fedha za ndani kutekeleza miradi mikubwa.
c) Uchelewaji wa upatikanaji wa Misamaha ya Kodi
167. Mheshimiwa Spika, washirika wa maendeleo wameendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya sekta ya maji kwa kufadhili utekelezaji wa miradi ya maji pamoja na misaada ya kitaalam. Aidha, utekelezaji wa miradi mingi ikiwemo inayofadhiliwa na washirika hao imekua ikichelewa kukamilika ndani ya muda uliopangwa kutokana na kuchelewa kutolewa kwa misamaha ya kodi kwa vifaa na mitambo inayotumika katika ujenzi wa miradi husika. Katika kukabiliana na changamoto hiyo Wizara imeendelea kuwasiliana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuweka utaratibu utakaoharakisha upatikanaji wa Misamaha ya Kodi nchini.
d) Upungufu wa Wataalam katika Sekta ya Maji
168. Mheshimiwa Spika, sekta ya maji ni sekta inayomgusa kila mwananchi kwa mahitaji ya huduma za kijamii pamoja na uchumi. Kutokana na umuhimu huo, Wizara imeendelea kuchukua hatua zote kuhakikisha huduma ya maji inamfikia mwananchi popote pale alipo nchini. Aidha, utekelezaji wa jukumu hilo unahitaji wataalam wakutosha na wenye weledi katika kutekeleza majukumu yao. Hadi mwezi Aprili 2022, Sekta ina watumishi 9,207 ambapo mahitaji ni watumishi 10,276 hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 1,069. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, kwa mwaka2021/22 Wizara na Taasisi zake kwa ujumla imeajiri watumishi 478. Aidha, Wizara imeendelea kuomba vibali vya ajira kutoka Ofisi ya Rais – UTUMISHI kwa ajili ya kupata wataalam wa kutosha na wenye sifa. Vilevile, Wizara itaendelea kuzihimiza Taasisi zake zenye upungufu wa wataalam kutenga fedha kwa ajili ya kuajiri watumishi.
e) Mabadiliko ya Tabianchi
169. Mheshimiwa Spika, athari za mabadiliko ya tabianchi zikiwemo ukame, kuchelewa kwa mvua pamoja na mafuriko zimeendelea kuathiri sekta ya maji kutokana na kukauka kwa vyanzo vya maji, kuongezeka kwa migao ya maji pamoja na kuharibika kwa miundombinu ya maji. Katika mwaka 2021/22, athari za mabadiliko ya tabianchi zimedhihirika katika vyanzo vingi vya maji kwa mfano Mto Ruvu ulipungua sana kina cha maji hali iliyosababisha kuchukua hatua za dharura kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Dar es Salaam. Hali hiyo imesababisha migao ya maji, kupungua kwa uzalishaji wa nishati ya umeme na kufa kwa mifugo. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali inaendelea kuhimiza ushiriki wa wananchi katika utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na mazingira. Vilevile, Wizara inaendelea kutekeleza mkakati wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kutekeleza miradi ya maji ambayo itatumia vyanzo vya maji vya uhakika kama vile mito mikubwa na maziwa.
6. VIPAUMBELE NA MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA
MWAKA 2022/23
6.1 Vipumbele vya mwaka 2022/23
170. Mheshimiwa Spika, vipaumbele vya Wizara kwa mwaka 2022/23 ni pamoja na kukamilisha ujenzi, ukarabati na upanuzi wa miradi inayoendelea kutekelezwa; kuanza ujenzi wa mabwawa ya kimkakati ya Kidunda na Farkwa; kuanza ujenzi wa miradi ya maji mipya ikiwemo miradi ya maji katika miji 28; kuendelea na utunzaji wa vyanzo vya maji ikihusisha kutambua, kuweka mipaka na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali ili vyanzo hivyo vilindwe kisheria; na kutekeleza miradi ya maji kwa kutumia vyanzo vya uhakika ikiwemo maziwa makuu na mito mikubwa.
6.2 Mpango wa Utekelezaji kwa Mwaka 2022/23
Mheshimiwa Spika, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Mpango wa Utekelezaji wa miradi ya maji kwa mwaka 2022/23 umeshirikisha wadau mbalimbali katika kuibua miradi ya kipaumbele wakiwemo Waheshimiwa Wabunge na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Ni matumaini yangu kwamba utaratibu huu utawezesha kufikia malengo ya Sekta ya Maji kwa haraka na uhalisia. Mpango na Bajeti umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Malengo ya Kimataifa ya Maendeleo Endelevu 2016 – 2030, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji, Sera mbalimbali za Kitaifa, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025) na Maagizo na ahadi alizozitoa Mheshimiwa Rais na Viongozi wengine wa Kitaifa.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali imepanga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji; kukamilisha miradi ya maji inayoendelea;kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua hususan kwenye maeneo kame; kuboresha usimamizi na uendeshaji wa huduma ya maji vijijini kwakuimarisha Vyombo vya Utoaji Huduma za Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs); kuongeza uhakika wa uhifadhi wa maji kwa kuimarisha kitengo cha uchimbaji wa visima na ujenzi wa mabwawa; nakuendelea kuweka msisitizo katika usimamizi wa watendaji na wakandarasi. Aidha, mipango imejikita katika maeneo yausimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji; huduma za ubora wa maji; huduma za usambazaji maji na usafi wa mazingira vijijini; huduma za usambazaji majisafi na usafi wa mazingira mijini; na utekelezaji wa kazi mbalimbali katika Taasisi zilizo chini ya Wizara na masuala mtambuka kama ifuatavyo:-
6.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za maji
(i) Utunzaji wa Vyanzo vya Maji
173. Mheshimiwa Spika, Sote tunatambua kuwa kilimo; uzalishaji wa nishati ya umeme, malighafi za viwandani; usafirishaji majini; ujenzi na shughuli nyingine kwa sehemu kubwa zinategemea uwepo wa rasilimali za maji za kutosha. Vyanzo vya maji vinamchango mkubwa sana katika uwepo wa rasilimali za maji na usalama wa maji kwa ujumla. Wizara imepanga kuendelea na mikakati ya utunzaji wa vyanzo vya maji ikihusisha kutambua, kuweka mipaka na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali ili vyanzo hivyo vilindwe kisheria. Katika mwaka 2022/23 jumla ya vyanzo 44 vitawekea mipaka na kutangaza katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha kupitia Mipango ya Utunzaji wa Vidakio vya Maji (Catchment Conservation Plans) iliyoandaliwa katika mabonde yote tisa nchini, Wizara iteendelea kuhamasisha utekelezaji wake katika Sekta mbalimbali ili kuwa na matumizi bora ya ardhi na kuimarisha uoto wa asili katika maeneo ya vyanzo vya maji.
(ii) Ujenzi wa Mabwawa
174. Mheshimiwa Spika, nchi yetu imebahatika kuwa na vyanzo vingi vya maji vikiwemo maziwa, mito, chemichemi na maji chini ya ardhi. Hata hivyo, mtawanyiko wa vyanzo hivyo hauko sawia. Baadhi ya maeneo yamekuwa na uhaba mkubwa wa maji kutokana ufinyu wa vyanzo na mabadiliko ya tabianchi. Kutokana na mtawanyiko wa watu, kuna maeneo hayajaweza kufikishiwa huduma ya maji. Katika mwaka 2022/23. Serikali imepanga kujenga mabwawa makubwa ya kimkakati yakiwemo mabwawa ya Kidunda, Farkwa, Lugoda na Songwe. Aidha, Serikali itaanza ujenzi wa bwawa la Kidunda lililochukua muda mrefu kutekelezwa baada yaRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kutoa kibali. Vilevile, Serikali itaanza ujenzi wa bwawa la Farkwa na mtambo wa kutibu maji baada ya kupata fedha za mkopo kiasi cha dola za kimarekani milioni 125.3 sawa natakriban Shilingi bilioni 280 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika. Sambamba na mabwawa makubwa ya kimkakati Serikali imepanga kujenga mabwawa ya ukubwa wa kati 23 hususan kwenye maeneo kame kwa ajili ya uvunaji wa maji ya mvua ili kuongeza uwezo wa nchi kuhifadhi maji na kuyasambaza kwa wananchi wengi zaidi.
(iii) Usimamizi Wa Rasilimali Za Maji
175. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23,Wizara itaendelea kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa takwimu za hali ya rasilimali za maji nchini; kusimamia utoaji wa vibali vya matumizi ya maji na utiririshaji wa majitaka yaliyotibiwa ili kupunguza migogoro na uchafuzi wa vyanzo vya maji; kuratibu uchimbaji wa visima vya maji nchini, kuratibu utekelezaji wa Mipango Shirikishi ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji pamoja na uendeshaji wa majukwaa ya wadau waSekta ya Maji ambayo yameonesha mchango mkubwa katika utambuzi wa changamoto, kupanga matumizi bora ya maji na upatikanaji wa fedha za usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji. Aidha, Wizara itafanya tafiti za kina kupitia Kituo Mahiri cha Rasilimali za Maji (Water Resources Center of Excellence) ili kuwa na mipango ya muda mrefu ya matumizi endelevu ya maji katika Sekta zote bila kuathiri rasilimali za maji zilizopo.
6.2.2 Usimamizi wa Huduma ya Ubora wa Maji
176. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara itaendelea kuimarisha uhakiki na ufuatiliaji wa ubora wa maji katika vyanzo na mifumo ya usambazaji kwa kukusanya na kuchunguza sampuli 15,000 za maji na sampuli 2,000 za majitaka; kutoa elimu kuhusu viwango vya ubora wa maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali; kuhakiki ubora wa madawa ya kutibu maji kabla ya manunuzi na wakati wa matumizi; kuwezesha uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Usalama wa Maji inayohimili mabadiliko ya tabianchi kwa Mamlaka za
Maji 34 na Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamiii 100; na kuendelea kuimarisha maabara za ubora wa maji kwa kuzipatia vitendea kazi,kujenga na kukarabati majengo; pamoja nakuziwezesha maabara nne (4) kupata ithibati.
6.2.3 Huduma ya Majisafi na usafi wa Mazingira Vijijini
177. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara imepanga kutekeleza jumla ya miradi 1,029 ya maji vijijini ambapo miradi 648 ni miradi inayoendelea kutekelezwa na miradi 381 nimipya. Orodha ya miradi ya maji vijijini itakayotekelezwa katika mwaka 2022/23 imeoneshwa kwenye Kiambatisho Na. 4. Aidha, Serikali imepanga kujenga mabwawa 15 katika maeneo mbalimbali ya vijijini. Orodha ya mabwawa yatakayojengwa imeoneshwa kwenye
KiambatishoNa. 5
178. Mheshimiwa Spika, Wizara pia imepanga kuandaa Mpango Kabambe wa Usafi wa Mazingira Vijijini (Rural Sanitation Master Plan) na kusanifu miradi ya majaribio ya usafi wa mazingira kwenye maeneo mbalimbali nchini. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Oman imepanga kuchimba visima virefu 20 kwenye maeneo ya vijijini katika mikoa ya Dodoma visima vitano (5), Morogoro (5), Pwani (5) na Mkoa wa Singida visima vitano (5).
(i) Mpango wa Matumizi ya Maji ya Maziwa Makuu
179. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya kandokando ya maziwa makuu wanapata huduma ya majisafi, salama na ya kutosheleza, Serikali imepanga kuanza ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji
48 vinavyozunguka Ziwa Victoria na Vijiji 37 katika Ziwa Tanganyika
(ii) Uendelevu wa Huduma ya Maji Vijijini
180. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha uendelevu wa huduma za maji na usafi wa mazingira katika maeneo ya vijijini, Serikali imepanga kuzingea uwezo CBWSOs 2466 zilizopo na kusajili CBWSOs mpya 704.
6.2.4 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini
181. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23,Wizara imepangakutekeleza jumla ya miradi 175 ya maji mijini.Orodha ya miradi ya majisafi na usafi wa mazingira mijiniitakayotekelezwa katika mwaka 2022/23 imeoneshwa kwenye Kiambatisho Na. 6.
(i) Miradi ya Kimkakati ya Majisafi katika maeneo mbalimbali ya Miji
182. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha malengo ya Kisekta ya kuwapatia wananchi huduma ya maji ya uhakika, Serikali imepanga kutekeleza miradi ya maji kwa kutumia vyanzo vya maji vya uhakika vya maziwa makuu, mito mikubwa na mabwawa. Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa kutoa maji Mto Ruvuma kupeleka Manispaa ya Mtwara – Mikindani pamoja na vijiji na vitongoji vilivyopo ndani ya kilomita 12 ya bomba kuu; mradi wa kutoa maji mto Kiwira kupeleka Jiji la Mbeya; mradi wa kutoa maji mto Rufiji kupeleka Jiji la Dar es Salaam na maeneo ya Pwani; na mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika Mkoa wa Simiyu utakaotumia maji ya Ziwa Victoria.
(ii) Mpango wa Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Jiji la Dodoma
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya huduma ya upatikanaji wa huduuma ya maji kwa wananchi wa jiji la Dodoma kutokana na ongezeko kubwa la watu baada ya makao makuu ya Serikali kuhamia Dodoma na ongezeko la shughuli za kiuchumi na kijamii. Kwa sasa mahitaji ya majisafi katika Jiji la Dodoma yanakadiriwa kuwa ni lita milioni 133.8 kwa siku ambapo uzalishaji kutoka katika vyanzo vyote vya maji ni lita milioni 66.7 kwa siku. Hivyo kuna upungufu wa maji katika jiji la Dodoma wa takribani lita milioni 67.1 kwa siku sawa na asilimia 50.2.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kutatua changamoto hiyo, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepata mkopo wa Dola za Marekani milioni 125.3 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Bwawa la Farkwa na mtambo wa kusafisha na kutibu maji ambapo ujenzi wake utaanza mwaka wa fedha 2022/23.
Mheshimiwa Spika, katika suluhisho la kudumu la kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma, Serikali inatarajia kutoa maji Ziwa Victoria na kuyafikisha katika Jiji la Dodoma kupitia mji wa Singida. Serikali inaendelea kutafuta fedha vyanzo mbalimbali ili mradi huo uweze kutekelezwa.
6.2.5 Mpango wa Kuimarisha Huduma ya Uondoshaji
Majitaka
186. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara imepanga kuendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira nchini. Miradi itakayotekelezwa ni pamoja namiradi ya usafi wa mazingira katika miji mikuu 10 ya Vwawa, Kigoma, Lindi, Sumbawanga, Singida, Njombe, Mtwara, Katavi, Tabora na Geita na miji midogo 15 ya Chalinze, Kisarawe, Bagamoyo, Kibaigwa, Igunga, Nzega, Chato, Muleba, Bunda, Mafinga, Ilula, Makambako, Korogwe, Manyoni na Rujewa. Aidha, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ya usafi wa mazingira katika miji ya Babati, Dodoma, Mbeya, Iringa na Dar es Salaam.
6.2.6 Chuo cha Maji
187. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kukiimarisha na kukitumia Chuo cha Maji kwa ajili ya kutoa wataalam wa maji watakaotumika katika usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji hususan ya vijijini pamoja na kufanya tafiti za kutatua changamoto mbalimbali katika Sekta ya Maji. Katika mwaka 2022/23, Chuo kimepanga kujenga na kukarabati majengo na miundombinu katika kampasi za Dar es Salaam, Mwanza na Singida;kununua magari mawili ya uondoshaji majitaka; kununua mtambo mmoja wa kuchimba visima; kukarabati na kujenga Hostel za wanafunzi; kudahili jumla ya wanafunzi 1,000; kununua vitendea kazi vikiwemo magari na kompyuta; na kuanzisha programu mpya tano ambazo niShahada za Uhandisi wa Usafi wa Mazingira (Sanitation Engineering), Uhandisi wa Haidrolojia (Hydrology Engineering), Haidrojiolojia na Uchimbaji wa Visima (Hydrogeology and Well Drilling), Maendeleo ya Jamii katika Maji na Usafi wa Mazingira (Community Development in Water and Sanitation) pamoja na Stashahada ya Uhandisi wa Usafi wa Mazingira (Diploma inSanitation Engineering).
6.2.7 Masuala Mtambuka
188. MheshimiwaSpika, katika mwaka 2022/23, Wizara itaendelea na mapitio ya Sera ya Maji ya mwaka 2002, kuandaa kanuni na miongozo mbalimbali chini ya Sheria za Maji ili kuhakikisha kuwa sheria za maji zinatekelezwa kikamilifu; kukamilisha marekebisho ya Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya 2009 kwa lengo la kuimarisha mfumo wa usimamizi wa rasilimali za maji;kuimarisha mifumo ya kielektroniki ili kuleta tija katika Sekta ya Maji; kuanza utekelezaji wa Mkakati wa Jinsia wa Sekta ya Maji;kutoa elimu na kuhamasisha watumishi kuendelea kupima afya zao; na kusambaza vifaa kinga katika vituo vya kazi ili kudhibiti maambukizi ya VVU.
7. SHUKRANI
Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwashukuru wadau wote waliochangia kwa namna moja ama nyingine kufanikisha utekelezaji wa shughuli za Sekta ya Maji ikiwa ni pamoja na Nchi Rafiki, Washirika wa Maendeleo, Mashirika ya Misaada ya Kimataifa, taasisi za kiserikali, mashirika ya kidini pamoja na wadau wengine. Kipekee ninapenda kuzishukuru nchi rafiki ambazo zimechangia katika maendeleo ya Sekta ya Maji nchinizikiwemo Uingereza, Ujerumani, India, Marekani,Korea Kusini, Uholanzi, Hispania, Misri, Ufaransa, Kuwait, Ubelgiji, Morocco, Italia na Saudi Arabia. Ninasema ahsanteni sana kwa ushirikiano na misaada ya kifedha na kitaalam mnayoendelea kutupatia katika Sekta ya Maji.
Mheshimiwa Spika, vilevile, ninayashukuru sana mashirika ya maendeleo na Taasisi za kimataifa kwa misaada ya kitaalam na fedha katika kuiwezesha Sekta ya maji kutekeleza majukumu yake. Mashirika na Taasisi hizo ni pamoja na Benki ya Dunia (World Bank-WB), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB), Benki ya Maendeleo ya Ujerumani
(KfW), Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha Mafuta (OPEC Fund for International Development-OFID), Mfuko wa Maendeleo wa
Kuwait (Kuwait Fund),Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (SFD),
Foreign, Commonwealth and Development Office (FCDO);
Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Shirika la Maendeleo la Ujerumani(GiZ),Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Global Environment Facility (GEF), Green Climate Fund (GCF), Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Maendeleo la Ubelgiji (BTC), Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) naShirika la Misaada la Marekani (USAID).
Mheshimiwa Spika, ninapenda pia kuyashukuru mashirika na Taasisi za kidini ambazo zimeendelea kusaidia sekta kufikia malengo yake. Mashirika na taasisi hizo pamoja na Catholic Agency for Overseas Aid and Development (CARITAS), Adventist Development Relief Agency (ADRA), Norwegian Church Aid,Livingwater International, World Islamic League, Shirika la Ahmadiya Muslim Jamaat Tanzania,Islamic
Foundation, Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA), Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Kanisa Katoliki Tanzania na Kanisa la Kianglikana Tanzania.
Mheshimiwa Spika, vilevile,ninazishukuruTaasisi zisizo za Kiserikali zinazoshiriki katika kuendeleza Sekta ya Maji. Taasisi hizo ni pamoja na Association of Tanzanian Water Suppliers (ATAWAS), OIKOS, WaterAid, Tanzania Water and Sanitation Network (TAWASANET), Wahamasishaji wa Maji, Maendeleo na Afya (WAMMA),World Vision; Worldwide Fundfor Nature(WWF), Maji na Usafi wa Mazingira (MUM),Netherlands Volunteers Services (SNV), Plan
International, Concern Worldwide, Water Mission (T), Shirika la Kimataifa la Kuhifadhi Uasili na Maliasili (IUCN) na Mashirika mengine mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee, ninaomba nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Winfried Mahundi (Mb), Naibu Waziri wa Maji; Mhandisi Anthony Damian Sanga, Katibu Mkuu; Mhandisi Nadhifa Sadiki Kemikimba, Naibu Katibu Mkuu; Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Wataalam na Watumishi wote wa Wizara ya Maji; pamoja na Maafisa Watendaji Wakuu na Watumishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara kwa ushirikiano mkubwa wanaonipatia pamoja na kujituma kwao katika kuhakikisha majukumu ya Wizara ya maji yanatimizwa. Naishukuru familia yangu kwa upendo, ushirikiano na faraja katika kipindi chote na kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu kwa ufanisi. Vilevile, ninatumia fursa hii kuwashukuru wananchi wa jimbo la Pangani kwa kuendelea kunilea nakuniamini katika kutekeleza majukumuyangu na ninaahidi kuendelea kuwa nao bega kwa bega katika kujenga jimbo letu na taifa kwa ujumla.
8. MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, ninaomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi 709,361,607,000 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23. Kati ya fedha hizo, Matumizi ya Kawaida ni Shilingi 51,462,269,000 ambapo Shilingi 16,700,534,000 sawa na asilimia 32.45 ni kwa ajili ya kugharamia Matumizi Mengineyo (OC) na Shilingi
34,761,735,000 sawa na asilimia 67.55 ni kwa ajili ya kulipa mishahara (PE) ya watumishi wa Wizara, RUWASA na Chuo cha Maji. Jumla ya bajeti ya maendeleo ni Shilingi 657,899,338,000 ambapo kati ya fedha hizo, Shilingi 407,064,860,000 sawa na asilimia 61.87 ni fedha za ndani na Shilingi 250,834,478,000 sawa na asilimia 38.13 ni fedha za nje.
Mheshimiwa Spika, ninaomba tena kutoa shukrani zangu za dhati kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba hii pia inapatikana katika tovuti ya Wizara www.maji.go.tz
Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja.
VIAMBATISHO
Kiambatisho Na. 1: Miradi 303 ya Maji Vijijini Iliyokamilika hadi Aprili 2022
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
1
Dodoma
Chemba DC
Ukarabati wa mradi wa maji kijiji cha Ovada
2,449
Ovada
17
2
Dodoma
Chamwino
Mradi wa maji kijiji cha suli
2,039
Suli
10
3
Dodoma
Chamwino
Mradi wa maji kijiji cha Mlebe
3,754
Mlebe
12
4
Dodoma
Chamwino
Mradi wa maji kijiji cha Malecela
2,605
Malecela
6
5
Dodoma
Chamwino
Mradi wa maji kijiji cha Chifukulo
4,026
Chifukulo
14
6
Dodoma
Mpwapwa
Ukarabati na upanuzi wa mradi wa maji Chipogoro
6,422
Chipogoro
10
7
Dodoma
Mpwapwa
Upanuzi wa mradi wa maji Njiapanda
945
Njiapanda
5
8
Dodoma
Mpwapwa
Ukarabati na upanuzi wa mradi wa maji Chitemo
6,807
Chitemo
7
9
Dodoma
Kongwa
Ukarabati wa Mradi wa Maji Kijiji cha Kiteto
1,480
Kiteto
8
10
Dodoma
Kondoa
Construction of Pumped Water Project for MONGOROMA Village
5,500
Mongoroma
10
11
Dodoma
Mpwapwa
Construction of Iyoma Water supply pumped scheme project
5,712
Iyoma
9
12
Dodoma
Kondoa TC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Bolisa
2,864
BOLISA & POISI
17
13
Dodoma
Kondoa TC
Ujenzi wa Mradi wa Maji MWEMBENI
2,839
MWEMBENI
5
14
Dodoma
Mpwapwa DC
Ujenzi wa mradi maji Iramba
1,223
Iramba
5
Jumla Dodoma
14
48,665
135
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
15
Geita
Bukombe DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Nampalahala
4,856
Nampalahala
8
16
GEITA
Nyang’whale DC
Ukarabati wa visima virefu vijiji vya Nyamikonze, Nyang’hwale, Nyabulanda, Mwasabuka na Lubanzo
1,500
Nyamikonze (Iyenze), Nyang’hwale, Nyabulanda, Mwasabuka na Lubando (Kaboha)
5
17
Geita
Bukombe
Ujenzi wa Mradi wa Maji Buganzu
3,504
Buganzu
8
18
Geita
Bukombe
Ujenzi wa Mradi wa Maji Ng’anzo
5,188
Ng’anzo
12
19
Geita
Chato
Ujenzi wa Mradi wa Maji Buziku
6,000
Buziku, Majengo, Luantaba
24
20
Geita
Geita
Ujenzi wa Mradi wa Maji Njia Panda
1,500
Njia Panda
6
21
Geita
Geita
Ujenzi wa Mradi wa Maji Wigembya
950
Wigembya
4
22
Geita
Geita
Ujenzi wa Mradi wa Maji Manga
2,000
Manga
7
23
Geita
Mbogwe
Ujenzi wa Mradi wa Maji Nanda
3,636
Nanda
18
24
Geita
Nyang’hwale
Ukarabati wa Mradi wa Maji Nyang’hwale
3,500
Ibambila, Kaseme
14
Jumla Geita
10
32,634
106
25
Iringa
Mufindi
Mradi wa Maji Ikweha
2,428
Ikweha
20
26
Iringa
Mufindi
Mradi wa Maji Nyigo
2,534
Nyigo
22
27
Iringa
Mufindi
Mradi wa Maji Ukami
3,027
Ukami
44
28
Iringa
Mufindi
Mradi wa Maji Ikimilinzowo
2,863
Ikimilinzowo
50
29
Iringa
Mufindi
Mradi wa Maji Lulanda
1,470
Lulanda
16
30
Iringa
Iringa
Mradi wa Maji Mafuluto
2,359
Mafuluto
38
31
Iringa
Iringa
Mradi wa maji Mkumbwanyi
1,495
Mkumbwanyi
8
32
Iringa
Kilolo
Mradi wa Maji Image
3,253
Image
16
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
33
Iringa
Kilolo
Mradi wa Maji Mawambala
4,187
Mawamala
6
34
Iringa
Kilolo
Mradi wa Maji Mtandika
3,533
Mtandika
4
35
Iringa
Mufindi
Nyololo water Supply project
8,400
Nyololo, Njiapanda
19
Jumla Iringa
11
35,549
243
36
Kagera
Biharamulo
Kufunga umeme katika chanzo cha maji Nyakanazi Kizota
5359
Nyakanazi
60
37
Kagera
Biharamulo
Construction of Storage tank 50m3 at Kabukome village
3,261
Kabukome
4
38
Kagera
Muleba
Extension of Bulyakashaju w/s to Kizinga village
4,235
Kizinga
16
39
Kagera
Muleba
Extension of Itunzi W/S
1,628
Itunzi
8
40
Kagera
Muleba
Extension of Ilogero W/S
3,880
Kafunjo
12
41
Kagera
Muleba
Extension of Izigo water supply
1,724
Bushumba, Bwarushanje
16
42
Kagera
Muleba
Extension of Katembe w/s to Nyakabango Village
3,725
Nyakabango
16
43
Kagera
Muleba
Rehabilitaion of Kasharunga W/S
13878
Kasharunga
72
44
Kagera
Muleba
Rehabilitation of10 shallow wells
2,250
Rwigembe, Bisheke, Ihangilo, Muyenje
9
45
Kagera
Bukoba
Bituntu
4,250
Bituntu
17
46
Kagera
Biharamulo DC
Mradi wa maji Nyamalagala
4,860
Nyamalagala/K ikoma
5
47
Kagera
Biharamulo DC
Mradi wa maji Kabindi
18,300
Kabindi, Chebitoke, Kikomakoma na Rukora
7
48
Kagera
Biharamulo DC
Mradi wa maji Kabukome
3,243
Kabukome
4
49
Kagera
Biharamulo DC
Mradi wa maji Nyantakala
6,101
Nyantakala
6
50
Kagera
Biharamulo
Mradi wa maji
5,236
Runazi
6
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
DC
Runazi
Jumla Kagera
15
81,930
258
51
Katavi
Nsimbo
Ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Mtakuja/Songambele
3,234
Mtakuja & Songambele
13
52
Katavi
Nsimbo
Ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Katisunga
2,214
Katisunga
6
53
Katavi
Mlele
Ujenzi wa mradi wa maji MajimotoIkulwe-Luchima
9,125
Ikulwe na Luchima
20
54
Katavi
Mpimbwe
Kasima Water Supply
1,340
KanindiKasima
4
Jumla Katavi
4
15,913
43
55
Kigoma
Buhigwe DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Munanila Phase 1
8,103
Munanila
10
56
Kigoma
Buhigwe DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Munyegera
9,834
Munyegera
24
57
Kigoma
Buhigwe DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Kimara/Kinazi
12,412
Kimara & Kinazi
12
58
Kigoma
Buhigwe DC
Ujenzi wa mradi wa Maji Bulimanyi and Nyamgali
6,198
Bulimanyi/Nya mgali
32
59
Kigoma
Buhigwe DC
Maboresho ya mradi wa maji Songambele
5,116
Songambele
0
60
Kigoma
Kakonko DC
Ukarabati wa mradi wa Maji Muhange
8,731
Muhange
0
61
Kigoma
Kakonko DC
Mradi wa Maji Kewe
4,319
Kewe&Nkuba
10
62
Kigoma
Kasulu DC
Mradi wa Maji Kitanga
20,932
Kitanga
36
63
Kigoma
Kasulu DC
Uchimbaji wa visima vierefu vijiji vya Kagerankanda, Rusesa, Makere na Asantenyerere
Kagerankanda, Rusesa, Makere na Asantenyerere
64
Kigoma
Kasulu DC
Ukarabati wa mradi wa maji Kwaga
9,532
Kwaga
0
65
Kigoma
Kasulu DC
Ukarabati wa mradi wa maji Kalela
9,532
Kalela
0
66
Kigoma
Kasulu DC
Ujenzi wa mradi wa maji Mvinza
6,368
Mvinza
40
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
67
Kigoma
Kasulu DC
Ujenzi wa mradi wa maji Kurugongo/Migunga
5,269
Kurugongo, Migunga
40
68
Kigoma
Kasulu TC
Uchimbaji wa visima virefu 6 katika vijiji vya Hwazi, Juhudi, Mdyanda, Kinkati and Kabanga
Hwazi, Juhudi, Mdyanda, Kinkati, Kabanga and Makere
Expansion of Sanza/Ntope water project to provide service to Sanza villlage.
9,588
Sanza & Ntope
22
259
Singida
Manyoni Dc
Mradi wa maji wa Kijiji cha Kinyika
2,261
Kinyika – 1
8
260
Singida
Ikungi DC
Mradi wa maji Dung’unyi
4,829
Dung’unyi & Munkinya
7
261
Singida
Ikungi DC
Mradi wa maji Ulyampiti
2,755
Ulyampiti
7
Jumla Singida
9
44,311
134
262
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Mkulwe
3,624
Mkulwe
22
Jumla Songwe
1
3,624
22
263
Tabora
Igunga
Ujenzi wa mradi wa Maguguni
2,053
Maguguni
7
264
Tabora
Sikonge
Ujenzi wa mradi wa maji Msuva
3,000
Msuva
6
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
265
Tabora
Uyui DC
Mradi wa uboreshaji wa visima vinne kwenda mtandao wa maji kwa vijiji vya Ufuluma- Iyogelo,UfulumaChali,Kizengi, Lutende
1,176
Ufuluma-Chali na Ufuluma – Iyogelo
4
266
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Mwamala kwa mwaka 2020/2021
2,634
Mwamala
56
267
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Mogwa
3,024
Mogwa
7
268
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Kayombo kwa mwaka 2020/2021
2,774
Kayombo
8
269
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Iboja-Sigili kwa mwaka 2020/2021
6,005
Iboja-Sigili
17
270
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Ubinga kwa mwaka 2020/2021
2,966
Ubinga
12
271
Tabora
Nzega DC
Mradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Lakuyi-Sagida kwa mwaka 2020/2021
3,923
Lakuyi
13
272
Tabora
Nzega DC
Ujenzi wa Mradi wa maji Mwamayunga .
2,768
Mwamayunga
36
273
Tabora
Kaliua DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Ushokola
2,700
Ushokola
10
274
Tabora
Kaliua DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Imalampaka
1,179
Imalampaka
4
275
Tabora
Kaliua DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji vya Wachawaseme,Mta kuja Magharibi na Mtakuja Mashariki
3,920
Wachawaseme, Mtakuja Magharibi, Mtakuja Mashariki
15
276
Tabora
Kaliua DC
Ujenzi wa mradi wa
7,179
Kanoge/
7
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
Maji katika Vijiji vya Kanoge na Ichemba
Ichemba
Jumla Tabora
14
45,301
202
277
Tanga
Korogwe DC
Mradi wa maji Lusanga
4,164
(3) Lusanga, Shamba kapori na Ngomeni
20
278
Tanga
Korogwe DC
Mradi wa Maji Mng’aza
1,233
Mng’aza
7
279
Tanga
Korogwe DC
Mradi wa maji Kwalukonge
3,114
(1) Magamba kwalukonge
0
280
Tanga
Korogwe DC
Mradi wa maji Kwemgunga
345
Sharaka
4
281
Tanga
Korogwe DC
Mradi wa maji Kikwazu
1493
M/Shamba
8
282
Tanga
Korogwe DC
Ukarabati wa Mradi wa maji Magundi
2,346
Magundi na kweungo
20
283
Tanga
Muheza
Ujenzi wa mradi wa maji kijiji cha Magula
856
Magula
8
284
Tanga
Muheza
Ukarabati wa mradi wa maji Kigongomawe na upanuzi wa mradi wa maji Mpapayu
6,249
Kigongomawe, Mpapyu na Kwenyefu
6
285
Tanga
Muheza
Ukarabati wa mradi wa maji Shebomeza
1,678
Shebomeza
12
286
Tanga
Muheza
Ujenzi wa Mradi wa maji Kwemdimu
1,680
Kwemdimu
12
287
Tanga
Kilindi
Mradi wa Maji Jungu/Balang’a
3,692
(3) Jungu, Balang’a na Lekitinge
19
288
Tanga
Handeni DC
Ujenzi wa Tangi la 500M3
19,069
Mkata Mashariki na Mkata maghari
0
289
Tanga
Handeni DC
Ujenzi wa mradi wa maji Malezi
3312
Kilimilang’ombe and Malezi
12
290
Tanga
Handeni DC
Ujenzi wa mradi wa maji Kwandugwa
3,237
Kwandugwa
17
291
Tanga
Handeni DC
Uchimbaji wa Visima virefu 14 katika vijiji vya Kangata, Gole, Kwa magome, Kwaluwala
9,719
kangata,gole kwa magome,kwalu wala na Mbamba
0
Na
Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Idadi ya wanufaika
Majina na idadiya Vijijivinavyonufaika
Idadi ya vituo vyaKuchota Maji
Msaje,Changalikwa, Konje,Msomera,Mba ngwi,Kibaya . Kwanyanje, Hoza, Misima na Mbamba
292
Tanga
Pangani DC
Mradi wa Maji Masaika
2,876
Masaika
13
293
Tanga
Pangani DC
Ujenzi wa Mradi wa maji Mikocheni
1,212
Mikocheni
12
294
Tanga
Pangani DC
Ujenzi wa Mradi wa maji Mbulizaga
2,200
Mbulizaga
12
295
Tanga
Pangani DC
Ujenzi wa Mradi wa maji Msaraza
1,482
Msaraza
10
296
Tanga
Pangani DC
Uchimbaji wa Visima Madang ana Jaira
Madanga na Jaira
0
297
Tanga
Mkinga
Ukarabati wa mradi wa maji Magati
9,768
Magati, Kiumbo, Mwanyumba, Mbambakofi na Mtakuja
10
298
Tanga
Mkinga
Ukarabati wa Mradi wa maji Daluni Kisiwani
2,925
Kisiwani A and Kisiwani B
12
299
Tanga
Mkinga
Upanuzi wa Mrdi wa maji Bwiti Mavovo
4,897
Bwiti and Mavovo
1
300
Tanga
Mkinga
Upanuzi wa Mradi wa maji Duga Maforoni-Horohoro
1,954
Horohoro
3
301
Tanga
Lushoto DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Kwemashai
1,728
Kwemashai
18
302
Tanga
Lushoto DC
Ujenzi wa Mradi wa Maji Shaghayu
2,314
Shaghayu
30
303
Tanga
Lushoto DC
Ukarabati wa Mradi wa Maji Mbaramo
3,456
Mbaramo
15
Jumla Tanga
27
96,999
281
Jumla KUU ya Miradi
303
1,467,107
4,147
Kiambatisho Na.2: Miradi 127 iliyokuwa na Changamoto za muda mrefu na kupatiwa ufumbuzi
Na
Mkoa
Wilaya
Jina la Mradi
Gharama za kutekeleza mradi
MwakaMradi ulipojengwa
Gharama za kutekeleza mradi
1
Arusha
Karatu
Mradi wa maji wa kusukumwa wa Matala
124,000,000
2018
204,000,000.0 0
2
Arusha
Karatu
Ujenzi wa bwawa katika kijiji cha Lemoot
82,000,000
2014
82,000,000
3
Arusha
Karatu
Getamock
14,955,000
2014
14,955,000
4
Arusha
Karatu
Kansay
150,000,000
2014
150,000,000
5
Arusha
Ngorongoro
Soitsambu- Njoroi
82,782,131.00
2015
82,782,131.00
6
ARUSHA
Karatu
Getamock
139,995,000.00
2014
139,995,000.0 0
7
ARUSHA
Karatu
Kansay
139,995,000.00
2014
139,995,000.0 0
8
ARUSHA
Monduli
Emairete/Eluwai
6,081,856.00
2016
6,081,856.00
9
Geita
Geita Mji
Kigoma Road
2008
3,000,000.00
10
Geita
Chato
Kasenga
311,660,420
2007
311,660,420
11
Geita
Bukombe DC
Msasa
185,150,936.00
2008
107,000,000.0 0
12
Kagera
Biharamulo
Mradi wa usambazaji maji Bisibo
680,927,667.00
2017
37,044,000.00
13
Kagera
Karagwe
Mradi wa Maji Chanika
805,250,968.00
2018
50,000,000.00
14
Kagera
Ngara
Munjebwe
287,300,178.00
2014
14,000,000.00
15
Kagera
Muleba
Ujenzi wa mradi Ruteme
145,063,029.2 7
16
Kagera
Ngara
Mradi wa maji Mukibogoye
100,000,000
100,000,000
17
Kagera
Karagwe
Mradi wa Maji Nyakakika
32,500,000
32,500,000
18
KAGERA
Bukoba
Ukarabati wa mradi wa maji Bituntu
80,000,000.00
80,000,000.00
19
Kagera
Ngara
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kanogeline
342,701,651.30
2014
176,225,109.0 0
20
Katavi
Tanganyika
Mradi Wa Usambazaji maji Kijiji cha Karema
342,701,651.30
2014
176,225,109.0 0
21
Katavi
Tanganyika
Mradi wa Usambazaji maji Kijiji cha Ngomalusambo
268,936,954.00
2015
169,867,109.0 0
22
Katavi
Mpanda
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Mtakumbuka
50,854,519
2018
50,854,519
23
Katavi
Mpanda
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Sungamila.
91,202,000
2014
91,202,000
24
Katavi
Mpanda
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Isinde
20,000,000
2018
20,000,000
25
Katavi
Mpanda
Mradi wa Maji ya bomba Nduwi
249,513,902
2018
249,513,902
26
Katavi
Mlele
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kilida
98,332,434
2014
98,332,434
27
Katavi
Mlele
Mradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kibaoni
159,033,822
2018
159,033,822
28
Kigoma
Kigoma DC
Mradi wa Maji Kalinzi
786,642,000.00
2018
76,000,000.00
29
Kigoma
Nkungwe
473,026,290.00
2016
150,000,000.0 0
30
KIGOMA
Kigoma DC
Mradi wa Maji Kalinzi
72,893,131.31
2018
72,893,131.31
31
KIGOMA
Kigoma DC
Mradi wa Maji Nyarubanda
139,084,330.98
2014
139,084,330.9 8
32
Kilimanjaro
Mwanga
Mamba-Mruma
11,080,000
2018
11,080,000
33
Lindi
Liwale
Mradi wa Maji Mpigamiti
678,492,300
2014
94,000,000
34
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji Chiola
340,702,913.00
2015
189,000,000
35
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji Nampemba
412,817,075.00
2015
98,331,991
36
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji wa Mnero Miembeni
88,859,000.00
2017
10,000,000
37
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji Mkonjela
465,000,000.00
2006
15,000,000
38
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji Kipara Mtua
465,000,000.00
2006
85,000,000
39
Lindi
Nachingwe a
Mradi wa Maji wa Ndomoni
205,449,000.00
2019
169,234,531
40
Lindi
Lindi
Hingawari
100,000,000
2019
100,000,000
41
MANYARA
MBULU DC
HAYDOM
1,065,442,235
2017
145,507,224.0
0
42
MANYARA
BABATI TC
Malangi
680,541,793.90
2017
74,161,200.00 0
43
MANYARA
Olbil
841,990,910
2019
–
44
MANYARA
Darakuta – Minjingu
1,731,387,268
2017
2,000,000,000
45
Mara
Bunda
Mkune
15,000,000.00
2013
12,000,000.00
46
Mara
Butiama
Mradi wa Maji Kitaramanka & Rwasereta
65,000,000
2018
65,000,000
47
Mara
Butiama
Mradi wa Maji Kongoto
41,662,292
2014
41,662,292
48
Mara
Butiama
Mradi wa Maji Kamgendi
65,000,000
2018
65,000,000
49
Mara
Butiama
Mradi wa Maji Bukabwa
72,500,000
2014
72,500,000
50
MBEYA
MBARALI
Imalilosongwe
39,374,854.17
2013
56,000,000.00
51
MBEYA
KYELA
Mradi wa Maji Lubaga
336,389,350.00
2014
–
52
MBEYA
MBEYA
Idimi/Haporoto
745,695,380.00
2018
43,300,000.00
53
MBEYA
MBEYA
Galijembe
299,623,047.00
2014
83,300,000.00
54
MBEYA
MBEYA
Mbawi/Jojo
804,480,500.00
2014
4,500,000.00
55
Morogoro
Malinyi DC
Mradi wa maji Lupunga
149,318,982
2016
3,540,000
56
Morogoro
Malinyi DC
Mradi wa maji kwa vijiji vya Malinyi ,Kipingo na Makerere
3,006,636,441
2019
114,526,380
57
Morogoro
Kilombero DC
Mradi wa Maji Idete
248,613,175.00
2017
23,176,500
58
Morogoro
Kilombero DC
Mradi wa Maji Namwawala
367,904,295.00
2017
19,604,500
59
Morogoro
Kilombero DC
Mradi wa Maji Matema
306,283,960.00
2017
42,778,546.00
60
Morogoro
Kilombero DC
Mradi wa Maji Kamwene
287,758,971.50
2015
61
Morogoro
Kilombero DC
Mradi wa Maji Miwangani
85,000,000.00
2014
62
Morogoro
Morogoro DC
Kidugalo
100,000,000
1956
100,000,000
63
Morogoro
Morogoro DC
Pangawe
41,000,000
1975
41,000,000
64
Morogoro
Morogoro DC
Seregeti B
0
2000
–
65
Morogoro
Kilosa DC
Mradi wa maji Kata ya Ruaha
2018
66
Morogoro
Kilosa DC
Mradi wa maji Kidodi
2015
5,000,000
67
Morogoro
Gairo DC
Mradi wa maji Gairo Mjini
6,120,000,000
2020
580,000,000
68
Morogoro
Gairo DC
Chiwaga/Makuyu
720,000,000
2019
69
Morogoro
Gairo DC
Chogoali
550,000,000
2019
70
Morogoro
Mvomero
Kwa Doli
219,446,000.00
2014
–
71
Morogoro
Mvomero
Doma
473,838,939.90
2015
45,300,000
72
MOROGORO
Morogoro DC
Mradi wa Maji Singisa
150,000,000.00
2018
150,000,000.00
73
MOROGORO
Ulanga DC
Mradi wa maji ya Bomba, Kijiji cha Minepa
60,000,000.00
2014
60,000,000.00
74
Mtwara
Tandahimba
MRADI WA MAJI LITEHU LIBOBE
453,493,553
2013
189,000.000.00
75
Mtwara
Tandahimba
MRADI WA MAJI JANGWANI MAHEHA
1,253,673,300
2013
43,000,000.00
76
Mtwara
Masasi
Mradi wa Maji Mkululu
1,257,497,778.80
2019
56,580,000.00
77
Mtwara
Newala
Ukarabati wa miundombinu ya maji katika vijiji 7
208,978,000.00
2018
3,000,000
78
Mtwara
Tandahimba (Tandahimba DC)
MRADI WA MAJI MKUPETE
6,000,000
2018
6,000,000
79
Mwanza
Sengerema
Karumo water Project
2011
3,000,000
80
Mwanza
Magu
Lugeye- Kigangama
1,056,740,850.00
2014
34,120,000.00
81
Pwani
Kibaha
Mradi wa maji Kipangege
151,849,500.00
2015
10,000,000.00
82
Pwani
Bagamoyo
Mradi wa maji Kijiji cha Yombo
297,637,065.00
2015
10,000,000.00
83
Pwani
Bagamoyo
Mradi wa Maji Milo
244,294,578.00
2015
85,000,000.00
84
Pwani
Kisarawe
Mradi wa Maji Chole/Kwala
1,610,205,773.11
2018
495,000,000.00
85
Pwani
Mkuranga
Mradi wa Maji Bupu
315,849,000.00
2016
825,000.00
86
Pwani
Kibiti
Mradi wa Maji Kibiti mjini
5,302,059,842.00
2012
186,329,317.20
87
PWANI
Mkuranga
Mradi wa maji MvuleniKilimahewa Kusini
9,840,207.91
9,840,207.91
88
Rukwa
Sumbawanga
Ujenzi wa mradi wa maji kijiji cha
306,704,637.52
2014
57,102,368.53
Mpui
89
Rukwa
Sumbawanga
Mradi wa maji wa Laela II
1,407,127,879.80
2016
122,400,000.00
90
Rukwa
Kalambo
Ujenzi wa Mradi wa Kasanga
100,000,000
100,000,000
91
Ruvuma
Namtumbo
MRADI WA MAJI MILONJI
724,565,490.00
2015
1,000,000.00
92
Ruvuma
Tunduru
Mradi wa maji Lukumbule
475,472,151.00
2016
1,700,000.00
93
Ruvuma
Tunduru
Mradi wa Maji Nandembo
330,165,607.00
2014
6,500,000.00
94
Shinyanga
Shinyanga
Mradi wa Maji Mwakitolyo
–
2018
–
95
Shinyanga
Kahama
Mradi wa Maji Segese
88,558,532
2014
88,558,532
96
SHINYANGA
SHINYAGA
Mradi wa Maji Didia
415,880,800.00
2014
4,000,000.00
97
Singida
Ikungi
Mradi wa Maji Nkhoiree
92,000,000
2018
92,000,000
98
Singida
Ikungi
Mradi wa Maji Ntewa awamu ya kwanza
166,632,728
2014
166,632,728
99
Singida
Ikungi
Mradi wa Maji Mgungira
10,000,000
2018
10,000,000
100
Singida
Ikungi
Mradi wa maji wa Mkiwa
76,500,000
2014
76,500,000
101
Singida
Mkalama
Mradi wa Maji Ikolo
90,000,000
2018
90,000,000
102
Singida
Mkalama
Mradi wa Maji Lyelembo
200,000,000
2014
200,000,000
103
SINGIDA
Mkalama Dc
Mradi wa maji Nyahaa
450,000,000.00
2018
450,000,000.00
104
Songwe
Ileje DC
Mtula gravity scheme
346,577,406.00
2016
105
Songwe
Ileje DC
Luswisi gravity scheme
303,056,490.00
2016
106
Songwe
Ileje DC
Malangali gravity scheme
445,818,754.00
2016
107
Songwe
Ileje DC
Ilanga, chitete , ikumbilo
1,141,300,691.
2018
108
Songwe
Ileje DC
Igumila, ndola na Ishanta
2018
109
Songwe
Ileje DC
Mtima
2018
274,200,000
110
Songwe
Ileje DC
IHANDA
392,691,800.00
2016
117,592,500.00
111
Songwe
Ileje DC
SONGWE GROUP
0
1983
–
112
Songwe
Ileje DC
RUANDA
0
1981
40,000,000.00
113
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Ikana
63,470,000.00
2016
114
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Namsinde II
37,241,800.00
2018
115
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Kasinde
41,739,600
2018
116
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Mkutano
0
2006
117
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Chiwanda
0
2008
118
Songwe
Momba DC
Mradi wa Maji Mkulwe
0
1969
–
119
Songwe
Momba DC
Mradi wa maji wa Chang’ombe
2015
312,537,500.00
120
Songwe
Momba DC
Mradi wa maji wa Mbuyuni
408,931,600.00
2014
348,600,000.00
121
Songwe
Momba DC
Mradi wa maji wa Mamkukwe
3,278
2014
122
Songwe
Tunduma
Mradi wa maji Mpemba
0
1972
200,000,000
123
SONGWE
Mradi wa maji wa Mbuyuni
80,000,000.00
2018
80,000,000.00
124
Tabora
Nzega
Mradi wa Maji Nata
526,410,520
2015
14,000,000
125
Tabora
Sikonge
Mradi wa Maji Uluwa
2,278,767,670
2015
35,000,000
126
Tanga
Pangani
Meka-Mseko
467,850,113
2018
467,850,113
127
Tanga
Muheza
Mradi wa maji Kijiji cha Kigongomawe
105,200,400.00
2014
105,200,400.00
Kiambatisho Na.3: Miradi 40 ya Maji Mjini iliyokamilika hadi mwezi Aprili, 2022
Na.
Mkoa
Jina la Mradi
Idadi ya Wanufaika
1
Arusha
Mradi wa Maji wa Longido-Kimokouwa-Namanga
29,686
2
Dar es Salaam
Improvement of Works for Water Supply Distribution System in Mkuranga District.
25,500
3
Dar es Salaam
Construction of Water Transmission main from Upper Ruvu Water Treatment Plant at Mlandizi to Mboga Village at Chalinze District
120,912
4
Dodoma
Mradi wa Maji Ihumwa – Njedengwa
15,718
5
Dodoma
Uchimbaji wa Visima virefu vitatu (3) katika eneo la Mzakwe
500,000
6
Dodoma
Ujenzi wa mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino –Ikulu
29,534
7
Geita
Uboreshaji wa huduma ya maji Mjini Chato
19,000
8
Geita
Mradi wa Uchimbaji Visima Chato
16,000
9
Iringa
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Ilula
35,651
10
Iringa
Mradi wa maji Mbugani
2,345
11
Kigoma
Ukarabati na Utanuzi wa Mradi wa Maji eneo la Makao Makuu ya Wilaya ya Uvinza
10,000
12
Lindi
Mradi wa Maji Ng’apa kijijini
8,757
13
Manyara
Mradi wa Maji Arri Harsha
30,020
14
Manyara
Mradi wa Maji Mongahay Tumati
16,000
15
Manyara
Mradi wa Maji Kateshi
12,000
16
Manyara
Mradi wa maji Orkesumet
12,000
17
Mara
Ukarabati wa Bomba Kuu la Kusafirishia Maji katika Mji wa Shirati
4,150
18
Mara
Mradi wa Kuongeza Mtandao wa Maji Mugumu
98,500
19
Mara
Ujenzi wa mtambo wa kutibu majisafi katika bwawa la Manchira
0
20
Mbeya
Mradi wa maji wa Nzovwe Isyesye
30,000
21
Mbeya
Mradi wa kuboresha huduma ya majisafi Tukuyu
84,000
22
Mbeya
Improvement of water supply services in Rujewa
5,780
23
Mbeya
Mbalizi township water supply
80,305
24
Mwanza
Mradi wa Uchimbaji Kisima kimoja na ujenzi wa miundombinu ya Maji katika shule ya Sekondari Bugatu Wilayani Magu
466
25
Mwanza
Kukamilisha Mradi wa Maji wa Shilima, Mhande na Izizimba
16,675
26
Njombe
Extension of Distribution line in Kipagamo
317
27
Njombe
Ludewa Water Supply Projects (Iwela and Mbugani)
5,100
Na.
Mkoa
Jina la Mradi
Idadi ya Wanufaika
28
Rukwa
Kujenga miundombinu ya majisafi na usafi wa mazingira katika mji wa Sumbawanga
136,414
29
Ruvuma
Mradi wa Maji Mbinga Mjini
12,000
30
Ruvuma
Mradi wa Maji Tunduru Mjini
9,000
31
Ruvuma
Mradi wa Maji Luhimbalilo-Naikesi (Namtumbo DC)
3,572
32
Ruvuma
Mradi wa Maji Mbesa (Tunduru DC)
14,771
33
Shinyanga
Extension of Water Transmission pipeline from the Lake Victoria Water Scheme (Kinanga) to Kagongwa and Isaka Towns – Lot 2
56,660
34
Shinyanga
Upanuzi wa mtandao wa majisafi Kata ya Kagongwa na mji mdogo wa Isaka
12,323
35
Shinyanga
Mradi wa Majisafi Ngongwa- Kitwana
27,095
36
Simiyu
Construction of Drinking Water Treatment Plant for Maswa Urban Water and Sanitation Authority
57,933
37
Simiyu
Ujenzi wa chujio la Maji ya kunywa Mjini Maswa
111,408
38
Tabora
Improvement of water supply services in Tabora Town
270,112
39
Tanga
Construction of Gravity Main from Mowe to Pongwe for Improvement of Water in Muheza Township
9,560
40
Tanga
Mradi wa Uboreshaji huduma ya maji safi katika Mji wa Muheza Awamu ya Pili.
31,000
Jumla
1,960,264
Kiambatisho Na. 4: Miradi 1,029 ya Maji Vijijini itakayotekelezwa katika mwaka 2022/23
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
(i) MIRADI INAYOENDELEA
1.
Arusha
Arumeru
Arusha DC
Construction of OLMULO water Project
Enot, milongoine, mbuyuni, Laroi, Terati, kisima cha Mungu, Losinyai na Mateves
522,579,261.00
2.
Arumeru
Arusha DC
Construction of Losikito water Project
Losikito and Imbibia
500,000,000.00
3.
Arumeru
Arusha DC
Drilling of 3 boreholes at Shambarai burka, Msitu wa mbogo and Mungushi villages in Meru council by june 2023
144,000,000.00
Jumla Arusha DC
3
1,166,579,261.00
4.
Arumeru
Meru DC
Construction of KIKATITI AND TUVAILA water Project on going
Imbaseni, maji ya chai, Kikatiti, Samaria, Kitefu, Maroroni and Nasholi.
500,000,000.00
5.
Arumeru
Meru DC
Construction of PATANDI water Project on going
Patandi
500,000,000.00
Jumla Meru DC
2
1,000,000,000.00
6.
Longido
Longido DC
Construction of Olmolog water Supply Project
Olmog
407,553,418.00
7.
Longido
Longido DC
Construction of Orkejelongishu water Supply
Orkejelongis hu, Lopokosek,
360,563,418.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Project
Armanie na Engushai
8.
Longido
Longido DC
Extension of Eng’atadabash i scheme to Engusero Village
Engusero
514,276,003.00
9.
Longido
Longido DC
Rehabilitation of Mairowa water Supply Scheme (Lesing’ita/Mun darara)
Lesing’ita
100,208,387.00
Jumla Longido
4
1,382,601,226.00
10.
Monduli
Monduli DC
Construction of Esilalei water supply Project
Esilalei
450,000,000.00
11.
Monduli
Monduli DC
Construction of Oldonyonado water Supply Project
Oldonyonad o
426,484,146.00
Jumla Monduli
2
876,484,146.00
12.
Karatu
Karatu DC
Construction of Laja/Ubwangw water Supply Project
Laja & Umbangw
225,395,000.00
13.
Karatu
Karatu DC
Construction of Mang’ola Juu water Project
Mang’ola Juu
191,030,757.00
14.
Karatu
Karatu DC
Construction of Chemchem water Supply Project
Chemchem
360,000,000.00
15.
Karatu
Karatu DC
Construction of Mang’ola Balazani water Supply Project
Mang’ola Barazani
360,319,000.00
16.
Karatu
Karatu DC
Rehabilitation of Endonyawet and Matala water Supply Schemes – on going
Endonyawet & Matala
253,407,200.00
Jumla Karatu DC
5
1,390,151,957.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
17.
Ngorongoro
Ngorongoro DC
Rehabilitation of Kisangiro Water Supply Project
Kisangiro, Pinyinyi (Masusu) na Olaika
150,000,000.00
18.
Ngorongoro
Ngorongoro DC
Construction of Pinyinyi water Project
Pinyinyi and Piyaya
230,000,000.00
19.
Ngorongoro
Ngorongoro DC
Improvement of Loliondo Town Water supply project
Loliondo Township
200,000,000.00
20.
Ngorongoro
Ngorongoro DC
Extension of Mbukeni, Endulen, Esere and Oldonyosambu Masusu Water Supply schemes
Mbukeni, Endulen, Esere and Oldonyosam bu Masusu
300,000,000.00
21.
Ngorongoro
Ngorongoro DC
Construction of fence and develeopment of Oloipir water source at Oloipir village
Oloipiri
180,000,000.00
Jumla Ngorongoro DC
5
1,060,000,000.00
JUMLA MKOA ARUSHA
21
6,875,816,590.00
22.
Dodoma
Chamwino
Chamwino DC
Construction of pumped Water Supply Project at Muheme Village
Muheme
200,000,000.00
23.
Chamwino
Chamwino DC
Construction of pumped Water Supply Project at Handali Village
Handali and Mjelo
326,075,265.00
24.
Chamwino
Chamwino DC
Construction of pumped Water Supply Project at Izava(Wali) Village
Izava Wali
250,000,000.00
25.
Chamwino
Chamwino DC
Construction of pumped Water
Mvumi Mission,
372,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Supply Project at Mvumi Mission Village
Chihembe and Mita
26.
Chamwino
Chamwino DC
Construction of pumped Water Supply Project at Dabalo Village
Dabalo
100,000,000.00
Jumla Chamwino
5
1,248,075,265.00
27.
Bahi
Bahi DC
Construction of water infrastructure at Ibihwa village
Ibihwa
302,453,590.00
28.
Bahi
Bahi DC
Construction of water infrastructure at Chali Makulu, Chali Isanga and Chali Chali Igongo
Chali Makulu, Chali Isanga and Chali Chali Igongo
484,523,986.00
Jumla Bahi
2
786,977,576.00
29.
Dodoma
Dodoma CC
Construction of water schemes at Nzasa-phase II, Hombolo Bwawani B- phase II, Mahoma Makulu -phase II, Mayeto & Hombolo Makulu-phase II and ChikowaPhase II
Nzasa, Chamwino and Sogeambele, Hombolo Bwawani B- phase II, Mahoma Makulu phase II, Mayeto & Hombolo Makuluphase II and Chikowa- Phase II
468,751,260.00
30.
Dodoma
Dodoma CC
Construction of Pumped Water Supply from Mzakwe Borehole to
Mbalawala, Msembeta,M atangizi,Mak ulu,Kawawa and
203,897,567.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Mbalawala, Chigongwe phase II
Muungano
Jumla Dodoma DC
2
672,648,827.00
31.
Kongwa
Kongwa DC
Construction of Water Infrastructures at Ijaka, Manghweta and Saigoni, Kinangali, Mageseni (Bwawani) and Chilanjilizi villages
Ijaka, Manghweta and Saigoni, Kinangali, Mageseni (Bwawani) and Chilanjilizi
529,517,664.00
32.
Kongwa
Kongwa DC
Completion of Mkoka, Laikala B, Masinyeti, Lengaji Village Water Supply Projects
Mkoka, Laikala B, Masinyeti, Lengaji
323,733,897.00
Jumla Kongwa
2
853,251,561.00
33.
Kondoa
Kondoa DC
Construction of Water Supply Projects for Mauno, Soera, Kikore – Mkurumuzi and Kikilo Kati Villages
Mauno, Soera, Kikore – Mkurumuzi and Kikilo Kati
494,000,000.00
34.
Kondoa
Kondoa DC
Rehabilitation of Water Supply Sheme for KISESE – SAUNA Village
Mapinduzi and Sauna
161,500,000.00
35.
Kondoa
Kondoa DC
Construction of Water Supply Project for Pahi, Sambwa, Hachwi and Mulua Villages
Pahi and Ikova, Pahi, Sambwa, Hachwi and Mulua
457,827,130.00
36.
Kondoa
Kondoa TC
Construction of Water Supply Project for
Mnarani, Miningani, Iboni,
126,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
KONDOA Town
Chemchem, Maji ya Shamba and Ubembeni
Jumla Kondoa TC
4
1,239,327,130.00
37.
Chemba
Chemba DC
Construction of Chandama Water Supply Project
Chandama and Mpendo
210,996,044.80
38.
Chemba
Chemba DC
Construction of Chemba Town Water Supply Project
Chemba
69,961,036.80
39.
Chemba
Chemba DC
Construction of Khubunko, Babayu and HamiaWater Supply projects
Khubunko, Babayu and Hamia
201,343,008.53
40.
Chemba
Chemba DC
Rehabilitation and expansion of Kelema Balai Water Supply Scheme
Kelema Balai and Kelema mashariki
280,656,110.70
41.
Chemba
Chemba DC
Rehabilitation of Songolo Water Supply scheme
Songolo
12,624,241.00
Jumla Chemba
5
775,580,441.83
42.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Construction of water infrastructure at Chinyika Mlunduzi Villages
Chinyika and Mlunduzi
162,000,000.00
43.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Construction of water infrastructure at Igoji, VinhaweManhangu, Lupeta and Makutupa
Igoji, VinhaweManhangu, Lupeta and Makutupa
300,650,645.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Villages
44.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Construction of water supply infrastructures at and PwagaMunguwi villages
Pwaga,Mung uwi,Maswala and Itende
116,750,000.00
45.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Construction and emprovement of Mtera water supply scheme
Mtera
73,849,999.00
Jumla Mpwapwa
4
653,250,644.00
JUMLA MKOA DODOMA
24
6,229,111,444.83
46.
Geita
Bukombe
bukombe DC
Construction of Msonga water supply project
Msonga
634,280,137.00
47.
Bukombe
bukombe DC
Construction of Nampalahala water supply project
Nampalahal a
185,692,403.94
48.
Bukombe
bukombe DC
Construction of Namsega water supply project
Namsega and Msangila
220,400,200.00
Jumla Bukombe DC
3
1,040,372,740.94
49.
Chato
Chato DC
Construction of Nyambogo – Ilemela water supply project
Kanyama, Ilemela and Nyambogo
1,072,000,000.00
50.
Chato
Chato DC
Construction of Muganza – Bwongera water supply project to serve 14 villages in 3 wards (PforR)
Construction of Nyamlenge water supply project in three villages of Magulilwa, Mlanda and Nyabula
Magulilwa, Mlanda and Nyabula
496,669,084.50
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
69.
Iringa
Iringa DC
Rehabilitation of Tungamalenga group scheme (Mapogoro, Kitisi, Tungamalenga , Ifunda, Itagutwa and Ihemi )
Mapogoro, Kitisi, Tungamalen ga, Ifunda, Itagutwa and Ihemi
50,000,000.00
70.
Iringa
Iringa DC
Construction of Tanangozi – Kalenga water supply project in three villages of Itagutwa, Kidamali and Nzihi Vilages in Iringa District.
Itagutwa, Kidamali and Nzihi
408,000,000.00
Jumla Iringa DC
6
3,947,933,286.88
71.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Ifwagi, Ihalimba and Ikongosi Water Supply projects
Ihalimba, Ugesa, Wami, Vikula, Nundwe, Itulavanu, Ikongosi, Ifwagi, Ifupira, Itona, Mtili, Lugongo, Mwitikilwa, Ikongosi juu na Igomtwa
30,000,000.00
72.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Mgololo Water Supply
Isaula, Kiyowela, Makungu, Lugema na mabaoni
30,000,000.00
73.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Igowole Water Supply
Ikwega,Mkal ala na
20,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Igowole
74.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Nyololo (Nyololo shule,Njojo na Lwingh’ulo )water Project
Nyololo shuleni,Njojo na Lwing’ulo
250,000,000.00
75.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Chogo, Idete,Ihanzutw a and Kisada Water Supply
Chogo, Idete, Ihanzutwa & Kisada
572,648,862.67
76.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Sadani Kihata Water Supply
Kibada, Tambalango mbe, utosi, Lugodalutali, I gombavanu na makongomi
322,559,272.00
77.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Malangali Water Supply
Isimikinyi,Ite ngule, Kigenge, Tambalang’o mbe, Mwilavila, Ipilimo,Ihowa nza, Idumulavanu na Ikangamwan i
57,909,862.67
78.
Mufindi
Mufindi DC
Construction of Lufuna and Kibao Water Supply
Sawala,Mtw ango,Lufuna na Kibao
1,907,440,728.00
Jumla Mufindi DC
8
–
3,190,558,725.34
JUMLA MKOA IRINGA
19
8,962,680,743.38
79.
Kagera
Karagwe
Karagwe
Construction of water supply project at Ihembe 1Vilage.
Ihembe I
80,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
80.
Karagwe
Karagwe
Construction of water supply project at Ahakishaka Vilage.
Ahakishaka
60,000,000.00
81.
Karagwe
Karagwe
Extension of water supply project at NyakaigaKakuraijo Villages.
Nyakaiaga & Kakuraijo
40,035,280.00
Jumla Karagwe
3
180,035,280.00
82.
Misenyi
Misenyi DC
Construction of water supply project at Byamtemba and Igayaza village
Byamtemba and Igayaza
636,711,755.54
83.
Misenyi
Misenyi DC
Construction of Kitobo water supply project
Kitobo and Kashasha
905,163,256.26
84.
Misenyi
Misenyi DC
Construction of katolerwa water supply project
Nyarugongo, Luhano, Katolerwa and Katano
547,285,590.38
85.
Misenyi
Misenyi DC
Construction of Kashenye water supply project
Kashenye, Bushago and Bukwali
200,000,000.00
86.
Misenyi
Misenyi DC
Extension of Gera water supply project to kashaka and kashekya village
Kashaka and Kashekya
500,000,000.00
87.
Misenyi
Misenyi DC
Buyango water supply project
Rutunga and Rwamachu
581,078,753.38
88.
Misenyi
Misenyi DC
Construction of Byeju water supply project
Byeju
400,000,000.00
Jumla Misenyi
7
3,770,239,355.56
89.
Ngara
Construction of MukalizaMurugina
Mukaliza and Murugina
85,510,822.40
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
water supply project
90.
Ngara
Construction of Kanyinya water supply project
kanyinya
300,000,000.00
91.
Ngara
Construction of Kabanga water supply project
Kabanga and murukukumb o
786,504,040.00
92.
Ngara
Construction of Kasange water supply project
Kasange
230,000,000.00
93.
Ngara
Construction of Mukikomero water supply project
Mukikomero
272,000,000.00
94.
Ngara
Construction of Kigina water supply project
Kigina
210,000,000.00
Jumla Ngara
6
1,884,014,862.40
95.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Kibirizi water Supply project to Kumkore,Ama ni and Kamuli
Kamuli
200,000,000.00
96.
Bukoba
Bukoba DC
Construction of water infrastructure at Nsheshe and Rukoma villages
Nsheshe and Rukoma
200,000,000.00
97.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Kabirizi water Supply Scheme to Migara
Migara
200,000,000.00
98.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Nyakabulala Water Supply Scheme to Kikomelo and Butakya
Kikomelo and Butakya
350,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
99.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Itongo-Mikoni to Kagondo water project
Kagondo
100,000,000.00
100.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Katale water supply project to Rubafu and Bumai villages
Rubafu,Buma i and Kishanje
500,000,000.00
101.
Bukoba
Bukoba DC
Construction of Mushozi water Project
Mushozi and Katangalala
186,053,177.00
Jumla Bukoba
7
1,736,053,177.00
102.
Muleba
Muleba
Construction of Kagoma water supply project
Kagoma & Nsisha
350,594,593.29
103.
Muleba
Muleba
Construction of Bulamula water supply projects
Bulamula
481,844,125.90
104.
Muleba
Muleba
Construction of Butembo water supply projects
Butembo, Kikuku & Makarwe
259,621,409.25
105.
Muleba
Muleba
Extension of Bisore water supply project
Bisore & Nyakasheny e
314,908,053.74
106.
Muleba
Muleba
Construction of Kyamyorwa water supply project
Kyamyorwa & Rulanda
408,759,519.65
107.
Muleba
Muleba
Construction of Katare water supply project
Buhanga, Bushemba, Katare & Kashozi
407,400,844.17
108.
Muleba
Muleba
Construction of Kishanda /Kabulala water supply project
Kishanda & Kabulala
48,340,846.00
109.
Muleba
Muleba
To complete the construction of
Butembo
2,271,469,392.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Butembo water supply project
Jumla Muleba
8
4,542,938,784.00
110.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Supply schem at Nyabusozi and Mbindi Villages.
Nyabusozi, Mbindi and Mwanga
100,000,000.00
111.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Projects at NyamigereKalenge water supply project
Nyamigere and Kalenge
205,000,000.00
112.
Biharamulo
Biharamulo DC
Mavota Rehabilitation water Project by construction of Storage Tank of 75 raiser of 9m
Mavota
130,000,000.00
113.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Supply schem at Nyakafundikwa -Nyakanazi Project.
Nyakafundik wa and Nyakanazi
87,494,477.60
114.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Supply schem at Mubaba Village.
Mubaba
68,187,061.50
115.
Feasibility study and detail design for the water project at Nyakahura, Mihongora, Rusese and Mabale Villages
129,103,724.00
Jumla Biharamulo
5
719,785,263.10
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
116.
Kyerwa
Construction of kimuli,Rwanya ngo and chakalisa water supply project
Kimuli,Rwan yango and Chakalisa
200,068,110.00
117.
Kyerwa
Construction of Runyinya- Chanya water supply project
Runyinya,Ch anya,Nkwen da,Muleba,R wabwere,Ny amweza,Itee ra and
345,479,988.00
118.
Kyerwa
Construction of NyamiagaNyakatera water supply
Nyamiaga,N yakatera and Kagu
350,479,988.00
119.
Kyerwa
Construction of kaisho -Isingiro water supply
Kaisho,Isingi ro,Karukwan zi ‘A’,Ibale,Kiha nga,Kaitamb uzi,Karukwa nzi’B’,Katera, Rwensinga,I shaka and Nyabishenge
325,479,988.00
120.
Kyerwa
Completion of Kigorogoro water supply
Kigorogoro,Ki shanda and Lulama
55,368,714.50
121.
Kyerwa
Completion of mabila water supply
Rushe,Mabir a,Kibimba,Ma kazi,Nyakatet e,Omukagan do and Ruhita
75,042,657.50
122.
Kyerwa
Construction of karongo rwabwere
Karongo and Rwabwere
125,479,994.00
123.
Kyerwa
Rehabilitation of songambele -kagenyi
Songambele, Kagenyi and Omukalinzi
116,083,518.00
Jumla Kyerwa
8
1,593,482,958.00
JUMLA MKOA KAGERA
44
14,426,549,680.0 6
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
124.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Katuma and Kamilala
Katuma and Kamilala
53,380,468.70
125.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Scheme at Lugonesi and Mpembe
Mpembe and Lugonesi
132,248,929.23
126.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Bulamata Village
Bulamata
146,662,000.00
127.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Extension of Karema Water Supply Scheme to Kapalamsenga and Songambele Village and Construction of Water Supply Project at Kafisha and Kasangantong we Village
Kapalamsen ga, Songambele , Kafisha and Kasanganto ngwe
100,000,000.00
128.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Vikonge Village
Vikonge
101,120,346.67
129.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Kapanga Village
Kapanga
76,249,371.54
130.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Mnyagala and Ikaka
Mnyagala and Ikaka
188,620,633.74
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Villages
131.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Kasekese, Kaseganyma, Sibwesa and Nkungwi Villages
Kasenganya ma, Kasekese, Sibwesa and Nkungwi
304,657,982.99
132.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Mazwe Village
Mazwe
125,792,334.68
133.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika DC
Construction of Water Supply Project at Isenga,. Kapemba and Ifumbula
Isenga,Kape mba and Ifumbula
200,000,000.00
134.
Katavi
Mpanda
Mpanda MC
Extension of milala water supply scheme to Kampuni village
Kampuni
160,000,000.00
135.
Katavi
Mpanda
Mpanda MC
Construction of Water Supply Project at Kakese village
Kakese& Mbugani
412,648,829.05
136.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
Construction of Water Supply Project at Kambuzi Halt village
Kambuzi Halt
175,000,000.00
137.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
Construction of Water Supply Project at Tambazi A & B villages
Tambazi A&B
464,401,588.26
138.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
Construction of Water Supply Project at Katambike
Katambike
180,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
village
139.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
Construction of Water Supply Project at Kapanda village
Kapanda
176,827,467.74
140.
Katavi
Mlele
Mpimbwe DC
Extension of Majimoto water supply and sanitation project to Usevya
Minyoso, Nyambwe, Usevya ,Ikuba, Msadya.
2,279,080,324
141.
Katavi
Mlele
Mpimbwe DC
Mradi wa Maji safi na salama katika Vijiji vya Mwamatiga, Ilalangulu (kitongoji cha Vilolo) na Mkwajuni
Mwamatiga, Ilalangulu (kitongoji cha Vilolo) na Mkwajuni
724,529,463.68
142.
Katavi
Mlele
Mpimbwe DC
Construction of stoarage tank with capacity of (1000m3) at Mamba Village.
Mamba, Majimoto, Luchima, Ikulwe, Kitupa, Mkuyuni na Migunga.
742,093,500
143.
Katavi
Mlele
Mpimbwe DC
Extension of Kibaoni Water supply project (Covid-19)
Kibaoni
557,228,142
144.
Katavi
Mlele
Mpimbwe DC
Construction of Ukingwamizi water supply project.
Ukingwamizi
87,891,340.00
145.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Extension of water supply and sanitation 16 Villages at Mlele DC
Completion of Chankele Bubango gravity water piped water Project
Chankele, Bubango
350,000,000.00
179.
Kigoma
Kigoma
Kigoma DC
Completion of rehabilitation and improvement of Nyarubanda and Kalinzi piped water scheme by installation of solar system and improvement of an intake.
Kalinzi, Nyarubanda, Kasange & Mlangala
312,309,221.00
180.
Kigoma
Kigoma
Kigoma DC
Completion of Kiziba Water Supply project
Kiziba
650,875,359.00
Jumla Kigoma DC
4
3,981,086,572.00
JUMLA MKOA KIGOMA
29
12,511,374,237.7 2
181.
Kilimanjaro
Rombo
Rombo DC
Construction of Lake Challa Water Supply Project (Wona Source)
To facilitate completion of On going projects at Magara, Boay, Hoshan, Kakoi, VilimaVitatu, Kazaroho, Geophysical survey and Drilling of 9 boreholes at Endadosh, Mwikantsi, Gijedabung, Riroda, Ayasanda, Endamaghay, Duru, Endagwe and Hewasi Villages.
Magara, Boay, Hoshan, Kakoi, VilimaVitatu, Kazaroho, Endadosh, Mwikantsi, Gijedabung, Riroda, Ayasanda, Endamagha y, Duru, Endagwe and Hewasi
1,187,531,486.19
Jumla Babati
1
1,187,531,486.19
216.
Hanang
Hanang DC
Completion of MogituGehandu water Supply Project
Gehandu
842,314,536.50
217.
Extention of Hirbadaw water
Hirbadaw
80,596,310.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Supply and Sanitation Scheme
Jumla Hanang
2
922,910,846.50
218.
Mbulu Mbulu DC
Completion of Labay, Ng’orati, Maretadu Juu, Masqaroda, Masieda – Gembakw, Endahagichan WS projects and completion of drilling 4 boreholes at Qalodaganway, Qaloda,Haydo m and Getesh
Labay, Ng’orati, Maretadu Juu, Masqaroda, Gembakw, Endahagicha n, Qalodaganwa y, Qaloda, Haydom and Getesh
1,384,971,972.0
Jumla Mbulu DC
1
0
1,384,971,972.0
219.
Mbulu
Mbulu TC
Completion of water supply project at Nambisi (hayloto) and Qalieda village in Mbulu Tc
Hayloto
198,545,402.72
Jumla Mbulu TC
1
0
198,545,402.72
220.
Simanjiro
Simanjiro DC
Completion of water supply projects at Terrat, Nadojunkin, Engonongoi and Emishiye
Terrat, Nadojunkin, Emishiye and Engonongoi
959,961,536.17
221.
Simanjiro
Simanjiro DC
Construction of Olchoronyori water supply project
Olchoronyori
232,457,646.31
JumlaSimanjiro
2
0
1,192,419,182.48
222.
Kiteto
Kiteto DC
Construction of Esuguta water supply projects by June 2023
Esuguta
218,205,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
223.
Kiteto
Kiteto DC
Construction of Kiperesa water supply projects by June 2023
Kiperesa
220,000,000.00
224.
Kiteto
Kiteto DC
Extention of Nchinila- Engusero water supply project
Engusero, Nasetan, & Ngipa
1,066,930,591.12
225.
Kiteto
Kiteto DC
Extention of Magungu-Nhati water supply project
Magungu & Nhati
342,505,408.88
Jumla Kiteto
4
0
1,847,641,000.00
JUMLA MANYARA
12
0
6,734,019,889.89
226.
Mara
Tarime
Tarime DC
Construction of water supply project for Kitawasi water Supply Project
Contruction of Kinyambwiga Piped Scheme LGA/065/20142015/W/WSDP/ 6-8 BD-C3
Kinyambwiga
220,000,000.00
229.
To complete Sanzate water project by June 2023
Sanzate
390,927,003.90
Jumla Bunda
3
610,927,003.90
230.
Musoma
Musoma DC
Construction of Kigeraetuma water supply project
Kigeraetuma, Kakisheri
300,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
231.
Musoma
Musoma DC
Construction of water supply project for District hospital & Kaboni and Kasoma villages.
Kasoma, Kaboni
47,441,142.00
Jumla Musoma DC
2
347,441,142.00
232.
Butiama
Butiama DC
Completion of on-going project (2021/2022) at Buswahili, Mwibagi, Nyasirori, Biatika, Nyamikoma, Kyankoma Villages and Improving of 4 hand Pumps in Kyatungwe, Masurura, nyambili and Mmazami villages.
Buswahili, Mwibagi, Nyasirori, Biatika, Nyamikoma, Kyankoma, nyambili, Mmazami and Masurura village
473,545,856.89
Jumla Butiama DC
1
473,545,856.89
JUMLA MKOA MARA
13
1,651,914,002.79
233.
Mbeya
Chunya
Chunya DC
Construction of Matwiga Phase II (Water Supply Project for Six Villages)
Mazimbo, Mtanila, Igangwe, Kalangali, Lupa and Ifuma
693,648,829.00
234.
Chunya
Chunya DC
Construction of water Supply Project at Kambikatoto
Miyuyu, Mnima, Chihangu, Navanga, Chilangala, Mikumbi, Mkongi, Mkoma II, Namangudu, Nangudyane , Mnyambe, Kadengwa, Maputi, Mtongwele chini, Majembe juu, Hengapano, Bahati and Mtongwele juu
250,000,000.00
328.
Newala
Newala DC
Construction of Mkoma II Water Project
Mkongi, Mkoma II, Namangudu, Nangudyane , Nachilembe
300,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
329.
Newala
Newala DC
Extension of Mnima water project to Majembe juu
Hengapano, Majembe juu and Ngapano
200,000,000.00
330.
Newala
Newala DC
Extension of Malatu water Supply Scheme to, Nameno, Mpwapwa and Songambele
Nameno, Mpwapwa and Songambele
200,000,000.00
331.
Newala
Newala DC
Extension Water supply Scheme from Lokohe to Chitekete, Mchanganuo, Nambudi, Namkonda
Chitekete, Mchanganuo , Nambudi, Namkonda
300,000,000.00
332.
Newala
Newala DC
Improvement of water supply Project in peri urban areas at Newala Town ship(Mnaida,T awala,Mitumba ti,Msilili,lidumb e,Mcholigodau ni,chiwindi,Tu maini,Kiuta,Mk unya,Matokeo, Rahaleo,Kikuy u.
Rehabilitation of gravity main, Intake, extention of Nsungu village, Sagalu sub village, and Mbongo village
Nsungu village, Sagalu sub village, and Mbongo
150,000,000.00
399.
Ludewa
Ludewa DC
Construction of pumping water supply project at Mavala
Mavala
100,000,000.00
400.
Ludewa
Ludewa DC
Construction of gravity water supply project at Madope
Madope
212,444,388.00
401.
Construction of ludewa Town water project
Ludewa Mjini
600,000,000
Jumla Ludewa
4
1,062,444,388.00
402.
Njombe
Njombe DC
Rehabilitation of pumping water supply Schemes at Lupembe and construction of Matembwe – Iyembela schemes.
Lupembe na Iyembela
100,000,000.00
403.
Njombe
Njombe DC
Construction completion of Nyombo Pumping water Scheme
Nyombo, Ninga
659,730,555.80
Jumla Njombe DC
2
759,730,555.80
404.
Njombe
Njombe TC
Construction of gravity scheme lugenge-Kisilo-
Kisilo, Ihalula na Utalingolo
75,851,638.25
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Utalingolo LOT3
405.
Njombe
Njombe TC
Construction of gravity scheme Igongwi group (Lot 1), Lot 2, Lot 3 and Lot 4
Kitulila, Madobole, Luponde and Njomlole
623,755,373.00
Jumla Njombe TC
2
699,607,011.25
406.
Njombe
Makambako TC
Construction of Ikelu Pumping Water Supply Project
Ikelu
150,000,000.00
407.
Njombe
Makambako TC
Construction of Ibatu Pumping Water Supply Project
Ibatu
50,000,000.00
408.
Njombe
Makambako TC
Construction of Usetule, Mahongole Gravity group Water Supply project
Usetule na Mahongole
250,000,000.00
409.
Njombe
Makambako TC
Construction of Mtulingala, Mbugani and Nyamande Pumping Water Supply Project
Mtulingala, Mbugani na Nyamande
50,000,000.00
Jumla Makambato TC
4
500,000,000.00
410.
Njombe
Makete DC
Construction of Maliwa- Ikete water supply project (PHASE II)
Maliwa na Ikete
150,201,500.00
411.
Njombe
Makete DC
Construction of water supply project at Uganga and Utanziwa (Phase II)
Uganga na Utanziwa
72,918,952.00
412.
Njombe
Makete DC
Construction of water supply project at
Idende, Unenamwa
149,798,500.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Idende- Unenamwa
413.
Njombe
Makete DC
Construction of water supply project at Utweve and Lupila village
Utweve, Lupila
102,650,000.00
414.
Njombe
Makete DC
Rehabilitation of Kidope Madihani water supply scheme
Kidope, Nkunga, Lumage na Madihani
101,550,050.40
415.
Njombe
Makete DC
Rehabilitation of Usalimwani, Mfumbi and Ruaha water supply scheme.
usalimwani, Mfumbi na Ruaha
120,079,500.70
416.
Njombe
Makete DC
Extension of water supply schemes in Ipelele and Ipepo village
Ipelele, Misiwa, Mbanga, Makeve, Ubiluko na Ipepo
75,955,170.30
417.
Njombe
Makete DC
Rehabilitation of Makusi, Luwumbu water supply projects
Makusi and Luwumbu
90,449,999.50
Jumla Makete DC
8
863,603,672.90
418.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Construction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Malangali and Hanjawanu)
Malangali, Hanjawanu
150,000,000.00
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Extension of Igando – Kijombe Gravity Water Supply Scheme in Mpanga na
Mpanga and Wangamiko
20,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Wangamiko Villages
419.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Extension of gravity water supply at Ng’anda- Uhekule Villages
Ng’anda, Uhekule
15,000,000.00
420.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Construction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Hanjawanu- Kijombe villages)
Hanjawanu and Kijombe
315,000,000.00
421.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Improve water supply service for WANGIWASA National water project in Wanging’ombe village
WANGIWAS A
211,200,000.00
422.
Wanging’om be DC
Extension of gravity water supply at Imalilo, Kinenulo, Msaulwa and Kilanzi Villages
Imalilo, Kinenulo, Masaulwa, Kilanzi
20,000,000.00
423.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Construction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Malangali and Hanjawanu)
Malangali, Hanjawanu
150,000,000.00
Jumla Wanging’ombe
7
881,200,000.00
JUMLA MKOA NJOMBE
25
4,766,585,627.95
424.
Pwani
Mkuranga
Mkuranga DC
Construction of water infrastructure
Kimanzichan a Kusini, Kimanzichan
286,115,838.40
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
at Kimanzichana Magharibi, Kimanzichana Kaskazini and Kimanzichana Kusini villages
a Kaskazini, Kimanzichan a Magharibi
425.
Mkuranga
Mkuranga DC
Construction of water infrastructure at Mwanambaya, Mdimni and Mkerezange villages
Mdimni, Nganje, Mkerezange, Kigoda, Mwanambay a
200,000,000.00
426.
Mkuranga
Mkuranga DC
To construct water infrastructure at Nasibugani and Njopeka villages
Nasibugani, Dondo, Sotele and Njopeka
240,000,000.00
Jumla Mkuranga
3
726,115,838.40
427.
Bagamoyo
Chalinze DC
Completion of on-going projects (Matipwili water Suppy project)
Matipwili
1,014,215,594.44
428.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Extention of Fukayosi water supply project
Fukayosi
350,344,596.0
429.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Construction of Mkoko water supply project
Mkoko
348,419,933,0
430.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Completion of Kitame water supply project
Kitame
268,992,016.39
431.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Rehabilitation of Milo and Kidogozero Water Supply Scheme
Milo and Kidogozero
583,683,499.87
Jumla Bagamoyo DC
5
2,217,235,706.70
432.
Kisarawe DC
Extension of Chole-Kwala
Pangalamwi ngereza and
479,943,996.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Water Supply Scheme for Panga la Mwingereza and KuruiChole Villages.
Kurui
433.
Kisarawe DC
Rehabilitation of Gwata, Ngongele and Vikumbur Water Supply Schemes.
Gwata, Ngongele, Vikumburu
555,784,773.16
Jumla Kisarawe
3
1,035,728,769.16
434.
Mafia
Mafia DC
Construction of Water Supply Scheme at Jimbo (Kidika) and Chunguruma (Tumbuju)
Jimbo (Kidika) and Chunguruma (Tumbuju)
70,000,000.00
435.
Mafia
Mafia DC
Construction of Kilindoni Village Water Supply Scheme in Mafia District
Kilindoni
879,937,895.13
436.
Mafia
Mafia DC
Construction of Kiegeani Village Water Supply Scheme in Mafia District
Kiegeani
279,126,916.80
437.
Mafia
Mafia DC
Construction of Kifinge Village Water Supply Scheme in Mafia District by June 2023
Kifinge
382,008,196.20
438.
Mafia
Mafia DC
Construction of Banja village Water supply Scheme in Mafia District by June 2023
Banja
408,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Jumla Mafia
5
5,161,900,406.13
439.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Mahege village
Mahege
38,850,199.50
440.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Mchungu village
Mchungu
54,319,293.88
441.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Kilulatambwe village
Kilulatambwe
136,945,357.76
442.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Mtunda village
Mtunda
152,837,278.40
443.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Mjawa village
Mjawa
141,152,243.83
444.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Nyanjati, Nyakinyo, Msindaji and Kivinja A villages
Nyanjati, Nyakinyo, Msindaji and Kivinja A villages
179,430,941.21
445.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Mlanzi village
Mlanzi
177,649,184.00
446.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water infrastructure at Bumbamsoro village
Bumbamsoro
190,028,016.00
447.
Kibiti
Kibiti DC
Rehabilitation of Water infrastucture at Mtawanya &
Mtawanya & Jaribu Mpakani
175,571,831.63
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Jaribu Mpakani villages
448.
Kibiti
Kibiti DC
Rehabilitation of Water infrastucture at Uponda Mchukwi & Mkenda/Kivinja B Villages villages
Uponda, Mchukwi & Mkenda/Kivi nja B
153,040,623.25
Jumla Kibiti
10
1,399,824,969.47
449.
Rufiji
Rufiji DC
Construction of Water Supply scheme at Nambunju
Nambunju
345,469,569.80
450.
Rufiji
Rufiji DC
Construction of Water Supply scheme at Chumbi
Chumbi
479,797,051.20
451.
Rufiji
Rufiji DC
Construction of Water Supply scheme at Tawi.
Tawi
56,218,579.28
452.
Rufiji
Rufiji DC
Construction of Water Supply scheme at Siasa
Siasa
133,409,256.75
453.
Pwani
Rufiji
Rufiji DC
Geophisical survey and Drilling of 9 bore holes in the villages of Mwaseni, Mibuyusaba, Ndundunyikanz a, Kipugira, Mbunju, Mvuleni, King’ongo, Mohoro Sec and Nyamwage.
Completion of piped water supply system at Mpunze, Sabasabini and Iponyanholo villages at ushetu DC by June 2023
Mpunze, Sabasabini and Iponyanholo
565,029,996.00
533.
Kahama
Ushetu DC
Completion of Igunda water supply Project
Igunda
58,374,998.00
534.
Kahama
Ushetu DC
Consultant service for Designing of water project and extension of lake Victoria water supply scheme to Igunda, Ukune, Kisuke, Kinamapula, Nyamilangano, mapamba, Uyogo, Bukomela, Mpunze, Ushetu and Ulowa wards in Ushetu DC
Igunda, Ukune, Kisuke, Kinamapula, Nyamilangan o, mapamba, Uyogo, Bukomela, Mpunze, Ushetu and Ulowa wards
200,000,000
535.
Kahama
Msalala DC
Extension of
Itumbili and
90,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
&Ushetu DC
Water Supply Scheme to Itumbili and Mwashigini Villages in Kahama District
Mwashigini
Jumla Kahama
12
64
3,784,375,683.00
536.
Shinyanga
Shinyanga Dc
Construction of water supply project for 6 Villages: Mawemilu,Mwa bagehu,Mwadut u,Mwenge,Mwo ngozo and Mwasenge at Shinyanga DC by June 2023
Mawemilu,M wabagehu,M wadutu, Mwenge,Mwo ngozo and Mwasenge
765,311,257.40
537.
Shinyanga
Shinyanga Dc
Construction of pipe infrastructures, storage tanks and domestic water points at 8 villages : Ishinabulandi, Bubale, Isela, Ibingo, Idodoma, Mwamala B, Ibanza and Ng’wang’alanga
Extension of Lake victoria pipaline to Nzubuka and Izugawima villages
Nzubuka and Izugawima
603,675,662.00
571.
Uyui
Uyui DC
Extension of Songambele water scheme
Songambele water scheme to
770,139,461.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
to Miyenze village
Miyenze
572.
Uyui
Uyui DC
Extension of lake victoria pipeline to Kongo and Uhuru-Mbiti villages
Kongo and Uhuru-Mbiti
265,423,571.00
573.
Uyui
Uyui DC
Extension of lake victoria pipeline to Ikongolo,Kanye nye and Kiwembe villages
Ikongolo,Kan yenye and Kiwembe
801,322,366.00
574.
Uyui
Uyui DC
Construction of Tura village water supply project
Tura
152,159,729.00
575.
Uyui
Uyui DC
Rehabilitation of 1216 of water points of piped and unpiped water schemes and Rehabilitation at 107 Villages,improv e ndono hand pump and complitionof Imrovement of 4 hand pamp to solar system at ufuluma,kizengi and Lutende vilanges in Uyui DC
Ujenzi wa mradi wa maji Igumila katika Vijiji vya Kapumpa, Mgambo, Mkola, Mwenge na Mwitikio.
Kapumpa, Mgambo, Mkola, Mwenge and Mwitikio
173,731,147.08
577.
Sikonge
Sikonge Dc
Ukarabati wa mradi wa maji Mibono
Kanyamseng a, Songambele, Mtakuja, Kiloleli, Kipanga, Lembeli, Ukondamoyo and Mibono mpya
10,000,000.00
578.
Sikonge
Sikonge Dc
Ujenzi wa mradi wa maji Igigwa – Wankolongo.
Igigwa and Wankolongo
341,679,800.00
579.
Sikonge
Sikonge Dc
Construction of Mwamayunga water project (Phase II) with 22 water point by June 2023.
Mwamayung a, Urafiki, Usunga and Isanjandugu
1,003,392,302.00
Jumla Sikonge
4
1,528,803,249.08
580.
Kaliua
Kaliua DC
Completion of Kazaroho water supply and sanitation project in Kaliua District
Kazaroho, Imalamihayo, Nsimbo
310,619,795.00
581.
Kaliua
Kaliua DC
Construction of Usimba water supply project in Kaliua District
Usimba
116,180,156.00
Jumla kaliua
5
426,799,951
582.
Igunga
Igunga Dc
Extension of water supply schemes at 9 villages(
Ndembenzi, Mwanzelwa, Itulashilanga, Ulaya,
1,200,650,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Ndembenzi, Mwanzelwa, Itulashilanga, Ulaya, Barazani, Ikunguipina, Njiapanda, Kitangili and Nkinga villages) in Igunga District -PHASE II
Barazani, Ikunguipina, Njiapanda, Kitangili and Nkinga villages
583.
Igunga
Igunga Dc
Extension of water supply schemes at 16 villages(Bukam a, Mwabakima, Johogya, Kining’inila, Mwanyangula, Iyogelo, Isakamaliwa, Kidalu, Ibole, Mwagala,Imala nguzu, Mwamakona, Kalangale,Gany awa, Mwagala and Igurubi villages) in Igunga DistrictPHASE II
Rehabillitation of Water Supply Project for DISSA Village
Dissa
76,000,000.00
667.
Kondoa
Kondoa Tc
Expansion of Water Supply Project for Tampori and Choka – Gubali Street
Choka, Gubali and Tampori
67,500,000.00
Jumla Kondoa
4
37
716,552,986.00
668.
Chemba
Chemba Dc
Rehabilitation and expansion of Kelema – Maziwani and Ovada Water Supply Scheme
Kelema Maziwani and Ovada
203,802,490.43
669.
Chemba
Chemba DC
Drilling of Eight 4 Boreholes for Handa, Chioli,
Handa, Chioli, Dinae and Donsee
157,600,000
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Dinae and Donsee
Jumla Chemba
2
6
361,402,490.43
670.
Mpwapwa
Mpwapwa Dc
To construct water infrastructure at Gulwe and Godegode Villages
Gulwe and Godegode
226,088,864.00
671.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Extension of water supply from Idilo Kisokwe to Mazae Girls Sec. School
Mazae
150,000,000
672.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Ground water exploration and drilling of 12 productive boreholes at Ngalamilo, Chaludewa, Muungano, Nyabu, Isinghu, Chibwegere, Chibwegele, Msangambuya Chamsisili, Igoji II Mkanana and Kisisi villages
Ngalamilo, Chaludewa, Muungano, Nyabu, Isinghu, Chibwegere, Chibwegele, Msangambuy a Chamsisili, Igoji II Mkanana and Kisisi villages
36,000,000
673.
Mpwapwa
Mpwapwa DC
Identification and preparation including water quality and discharge test and Design for Gravity and river springs at Lufusi, Rudi, Mbuga, Iyenge, Kinusi, Ikuyu, Winza, Vikundi and Nzugilo villages and
Lufusi, Rudi, Mbuga,Iyeng e,Kinusi,Ikuy u,Winza,Viku ndi and Nzugilo villages and Borehole designs at Msagali,and Nghambi villages
43,260,660
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Borehole designs at Msagali, and Nghambi villages
Jumla Mpwapwa
5
26
455,349,524.00
674.
DODOMA Dodoma
Geophyscial survey and drilling of boreholes at Nkulabi and Mahoma Makulu villages
Nkulabi and Mahoma Makulu
11,599,309.00
Jumla Dodoma
1
–
11,599,309.00
JUMLA MKOA DODOMA
22
95
3,022,823,053.43
675.
Geita
Bukombe
Bukombe DC
Extension of Ng’anzo water supply scheme in Ng’anzo village
Ng’anzo
228,910,560.00
676.
Bukombe
Bukombe DC
Construction of Piped Water Supply Projects for Mwalo and Iyogelo villages in Bukombe District
Mwalo and Iyogelo
259,555,544.06
Jumla Bukombe
2
3
488,466,104.06
677.
Chato
Chato DC
Construction of Imarabupina – Ichwankima water supply project
Construction of Nkelenge, ishunju, minziro and rwamashonga water supply projects
Nkelenge, ishunju, minziro and rwamashong a
900,000,000.00
689.
Missenyi
Missenyi DC
Rehabilitation of Kenyana water supply scheme
Kenyana, ruzinga and bugango
304,405,756.44
690.
Missenyi
Missenyi DC
Extension of Kibeo water supply scheme to Mwemage and mabale villages
Mwemage, mabale, Kikono, Kishojo and Rushasha
749,999,999.98
691.
Missenyi
Missenyi DC
Construction of 50 water points
kashaka and kashekya
50,000,000.00
692.
Missenyi
Missenyi DC
Geophysical survey and drilling of 16 boreholes at Byeju, Mwemage, Kitobo, Kitobo, Kyazi, Ruzinga, Rwamashonga, Katolerwa, Kijumo, Mushasha, Bubale, Nkelenge, Katendagulo, Kajumo, Mabuye, Bugorora and Minziro Villages
Byeju, Mwemage, Kitobo, Kitobo, Kyazi, Ruzinga, Rwamashong a, Kijumo, Mushasha, Bubale, Nkelenge, Katendagulo, Kajumo, Mabuye, Bugorora and Minziro and Katolerwa
386,936,701.61
Jumla Misenyi
5
–
2,391,342,458.03
693.
Kyerwa
Kyerwa DC
Construction of kimuli
Kimuli, Rwanyango
200,068,116.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Rwanyango and chakalisa water supply project
na Chakilasa
694.
Kyerwa
Kyerwa DC
Construction of Runyinya- Chanya water supply project
Runyima na Chanya
320,479,988.00
695.
Kyerwa
Kyerwa DC
Construction of NyamiagaNyakatera water supply
Nyamiaga na Nyakatera
325,479,988.00
696.
Kyerwa
Kyerwa DC
Construction of kaisho -Isingiro water supply
Kaisho na Isingiro
325,479,988.00
Jumla Kyerwa
4
–
1,171,508,080.00
697.
Ngara
Ngara DC
Construction of Kihinga water supply project
Kihinga
220,000,000.00
698.
Ngara
Ngara DC
Construction of Bugarama, Nyakariba, Kigoyi, Kasulo,Benaco( Kafua) Keza, Katerere and Ntanga water supply projects
Bugarama,Ny akariba,Kigoy i,Kasulo,Bena co,Keza,Kate rere and Ntanga
1,324,381,499.97
699.
Ngara
Ngara DC
Geophysical survey and drilling of boreholes at 8 villages in Kumubuga, Mukarehe, Nyabisindu, Mumuhamba, Kumugamba, Kagali, Muganza and Kazingati villages
Kumubuga, Mukarehe, Nyabisindu, Mumuhamba, Kumugamba, Kagali, Muganza and Kazingati villages
Kanazi, Rwagati, Kyansozi, Minazi, Katoju, Buganguzi, Muruku, Butairuka, Bwizanduru, Bulinda, Butahyaibeg a, Buguruka, Kyema na Mulahya
132,914,495.00
702.
Bukoba
Bukoba DC
Extension of Kibirizi water Supply project to Kumkore, Amani and Kamuli; Kabirizi water Supply Scheme to Migara; Nyakabulala Water Supply Scheme to Kikomelo and Butakya;
Itongo-Mikoni to Kagondo water project; Katale water supply project to Rubafu and Bumai villages
703.
Bukoba
Bukoba DC
Construction of water infrastructure at Nsheshe, Rukoma and Mushozi villages
Rukoma, Nsheshe and Mushozi & Katangalala
386,053,177.00
704.
Bukoba
Bukoba DC
Geophysical survey and drilling of twelve (12) productive boreholes at Nsheshe, Rukoma, Kishogo and Kasharu
Nsheshe, Rukoma, Kishogo and Kasharu
30,000,000.00
Jumla Bukoba
6
–
1,948,967,672.00
705.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Supply scheme at Nemba and Migango Water Project supply Projects
Nemba and Migango
715,181,508.00
706.
Biharamulo
Biharamulo DC
Construction of Water Supply projects at NyamigogoSongambele & Busiri-Midaho villages.
Nyamigogo, Songambele and Kagoma, Kikoma and Busiri
660,697,150.00
Jumla Biharamulo
2
–
1,375,878,658.00
JUMLA MKOA KAGERA
22
0
10,514,152,341.7 7
707.
Katavi
Tanganyika
Tanganyika Dc
Construction of water Supply
Bugwe
186,615,106.51
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
infrastructure at Bugwe, Bujombe and Katobo Villages
708.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
To extend Mtakuja & Songambele water supply scheme to Kapalala Secondary, Mtakuja B and HoD House
Mtakuja B
45,000,000
709.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
To extend Magula, Ibindi and Matandalani water supply scheme to Mgolokani village
Mgolokani
32,000,000
710.
Katavi
Mpanda
Nsimbo DC
To extend Mtapenda water supply project to Mtapenda C and Zahanati in Nsimbo DC
Mtapenda
25,000,000
711.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Extension of water supply and sanitation at Songambele (sub-Village Shamara and Shama at Kamsisi Village)
Kamsisi
120,000,000.00
712.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Extension of water supply and sanitation from inyonga to Ipwaga (sub- village
Ipwaga
110,046,875.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Kankele/Gizaul ole)
713.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Construction of water supply and sanitation at Isegenezya (sub-Villages Uliambogo & Mahingula)
Isegenezya
250,000,000.00
714.
Katavi
Mlele
Mlele DC
construction of water supply and sanitation at Ilunde (subVillages Ibelamafipa & Kasagala )
Ilunde
141,000,000.00
715.
Katavi
Mlele
Mlele DC
construction of water supply and sanitation at Kamalampaka (sub-Village Mpanda ndogo) Mlele Council
Kamalampak a
200,000,000.00
716.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Extension of water supply and sanitation at Kalovya (sub-Village Shama)
Kalovya
120,000,000.00
717.
Katavi
Mlele
Mlele DC
Construction of treatment plant and Raising Main at Nsenkwa Dam
Inyonga,Uten de, Mgombe, Kanoge, Nsenkwa,Mta kuja, Kaulolo, Mapili, Kamsisi, Songambele, Imalauduki, Kalovya na Kamalampak a
320,265,160.79
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
718.
Katavi
Mlele
Mpimbwe Dc
Extension of water supply and sanitation at Chamaendi (sub-Villages Chamalendi B & Mahimba) Mpimbwe Council
Chamalendi
265,000,000.00
719.
Katavi
Mlele
Mpimbwe Dc
Extension of water supply and sanitation from Usevya to Ikuba (sub- Village Ikuba, Igongwe, Mnyakasi,Ipota ,Kikulwe,Moba & Uzumbura) in Mpimbwe Council
Usevya and Ikuba
370,000,000.00
720.
Katavi
Mlele
Mpimbwe Dc
Extension of water supply and sanitation at Mirumba (sub-Villages Katete,Wampe mbe & Kashela) in Mpimbwe Council
Mirumba
135,909,232.00
721.
Katavi
Mlele
Mpimbwe Dc
Extension of water supply and sanitation from Kabunde to (sub-Village Mpilipili) in Mpimbwe Council
Kabunde
280,000,000.00
722.
Katavi
Mlele
Mpimbwe Dc
Extension of water supply and sanitation (sub-Village senta Matana,
Ikulwe
235,277,497.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Nkuswe ,Changi dalajani,Mkwak wani at Ikulwe) in Mpimbwe Council
Jumla Katavi
17
2,836,113,871.30
723.
Katavi
Mpanda
Nsimbo
To conduct Hydrological and Drill Nine (9) boreholes at the following villages Mtambo (2), Kalungu (1), Ivungwe (1), Litapunga (2), Kaburonge (1), Katumba (1) and Kabatini.
Construction of Nambilanje- Mkaranga Water Supply Project
Nambilanje and Mkarango
500,000,000.00
758.
Ruangwa
Ruangwa DC
Construction of Chunyu Water Supply Project
Chunyu
450,000,000.00
759.
Ruangwa
Ruangwa DC
Construction of Liugulu Water Supply Project
Liugulu
547,420,681.99
760.
Ruangwa
Ruangwa DC
Construction of Weir, gravity Main and Water storage tank at Mandawa
Mandawa
450,000,000.00
761.
Ruangwa
Ruangwa DC
Construction of Water storage tank at Namangale village and improvement of gravity Main from the Source to Namangale village
Namangale
200,000,000.00
762.
Ruangwa
Ruangwa DC
Construction of water project to 34 villages of
Vijiji 34 Ruangwa na Vijiji 21 Nachingwea
80,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Ruangwa District and 21 Villages of Nachingwea District from Nyangao River
Jumla Ruangwa
6
2,227,420,681.99
JUMLA MKOA LINDI
20
6,659,933,495.69
763.
Manyara Babati Babati DC
Construction of Madunga water supply project in Babati District.
Madunga, Utwari, Giding’wari, Qameyu, Endaw and Gawal
853,662,737.81
Jumla Babati
1
853,662,737.81
764.
Mbulu
Mbulu DC
Construction of Yaeda Kati, Dirim, Endalat, Endamily, Murkuchida, Endanachan, Basonyagwe, Basoderer, Bashay, Qandach, Ng’wandakw and Haydom pumped water supply project
Construction of pump house, rising main, procurement of submersible water pump and supply of electricity for Haydom water supply project in Mbulu DC
Haydom and Ng’wandakw
100,000,000.00
766.
Mbulu
Mbulu DC
To facilitate Survey and drilling of
Qamtananant
29,474,130.48
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
successful productive borehole at Qamtananant Village by June 2023
Jumla Mbulu
3
3,129,474,130.48
767.
Mbulu
Mbulu TC
Construction of Aicho pumped water supply project in Mbulu TC
Aicho
200,000,000.00
768.
Mbulu
Mbulu TC
Construction of Titiwi pumped water supply project in Mbulu TC
Titiwi
330,192,721.80
Jumla Mbulu TC
2
530,192,721.80
769.
Hanang’
Hanang’ DC
Extension of Mogitu/Gehand u Water Supply Project
Gehandu
753,957,717.50
770.
Hanang’
Hanang’ DC
Extention of Bassotu water Supply and Sanitation Scheme
Dilling’ang
600,000,000.00
771.
Hanang’
Hanang’ DC
Conduct Geophysical survey and Driiling of 16 productive Boreholes
Endagaw, Endasabhogh echan, Lambo, Masusu, Bassotughan, Qutesh, Kinyamburi, Wandela, Sagon, Dabaschand, Dirma, Mogitu, Nyasinyenda, Gidamambur a, Wareti and Qalosendo
212,923,075.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Jumla Hanang’
3
1,566,880,792.00
772.
Simanjiro
Simanjiro DC
Extension of Orkesumet Water Scheme to Lerumo village; Naberera Water Scheme to Losokonoi & Lorbene; Komolo water scheme to Olembore (Lemshuku) sub village
Lerumo, Losokonoi & Lorbene and Olembore
1,785,068,718.44
773.
Simanjiro
Simanjiro DC
Installation of 21KVA diesel generator at Kitwai B, Installation of transformer 50KVA at Oljoro No. 5 and Loongswan
Kitwai B, Oljoro No. 5 na Loongswan
112,000,000.00
774.
Simanjiro
Simanjiro DC
Construction of Einoth & Losinyai water supply project by June, 2023
Enoth na Losinyai
308,597,999.08
775.
Simanjiro
Simanjiro DC
Geological Survey and Drilling of 13 productive Boreholes
Kandasikira, Sukuro (Alaspa), Nyorit, Nadonjukini (Mwajanga), Lemkuna (Lengungum wa), Ormoti (Namalulu), Kitwai B (Losikito) and Sukuro (Katikati)
155,425,565.26
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Jumla Simanjiro
6
2,361,092,283.52
JUMLA MKOA MANYARA
15
8,441,302,665.61
776.
Mara
Tarime
Tarime
Extension of Sirari water supply project and Gimenya water supply project
Sirari and Gimenya
800,000,000.00
777.
Mara
Tarime
Tarime
Construction of water infrastructure at Kemakorere and Nyarero, Regicheri and Mnagusi, Itununu and Nyakienene villages
Kemakorere and Nyarero, Regicheri and Mnagusi, Itununu and Nyakienene
Hydrogeologic al survey and Drilling of Boreholes at Surubu,kimusi, Remagwe,Mat amankwe,turu getiNyabitocho and kobori
Surubu,kimu si,Remagwe, Mataman kwe,Turugeti ,Nyabitocho and kobori
280,000,000.00
Jumla Tarime
6
3,657,934,094.00
782.
Mara
Butiama
Butiama DC
To extend Nyamikoma Water supply scheme to Nyakiswa village
Nyakiswa
133,937,464.00
783.
Butiama
Butiama DC
To extend Biatika- Kinyariri Water supply scheme to Matongo village
Matongo
160,172,486.00
784.
Butiama
Butiama DC
To construct Water infrastructure at Ryamisanga village (Phase I) and Isaba villages
Ryamisanga and Isaba
1,009,694,037.11
785.
Butiama
Butiama DC
To construct TANESCO power line (3- Phase) to pump houses at Bukabwa, Kamgendi, KitaramankaRwasereta villages and to conduct Hydrogeologic al survey and
Bukabwa, Kamgendi, Kitaramanka -Rwasereta and sirorisimba villages
259,034,216.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Drilling of Borehole at Sirorisimba Village.
786.
Butiama
Butiama DC
Surveying and Drilling of Borehole at Sirorisimba Village.
Sirorisimba
35,000,000.00
Jumla Butiama
5
1,597,838,203.11
787.
Rorya
Rorya DC
Expansion of Kirogo Water Supply Scheme to Mori, Chereche, Dett, Ochuna & Omuga Village
Mori, Chereche, Dett, Ochuna & Omuga
500,000,000.00
788.
Rorya
Rorya DC
Expansion of Komuge Water Supply Scheme to Oliyo & Makongoro Village
Oliyo & Makongoro
540,396,000.00
789.
Rorya
Rorya DC
Construction of Mang’ore Water Supply Scheme
Mang’ore
166,000,000.00
790.
Rorya
Rorya DC
Construction of Bukura Ward Water Supply Scheme for Bubombi, Sota, Sakawa, Thabache, Roche, Osiri, Ratia & Kirongwe Villages PHASE I
Construction of NjengwaMajengo Water Supply scheme
Njengwa, Njengwa sokoni and Majengo
450,695,987.00
820.
Mtwara
Mtwara DC
Rehabilitation of Dihimba Water Supply Scheme
Dihimba, Kinyamu and Mpandomo
177,275,767.00
821.
Masasi
Masasi DC
To conduct geophysical survey and drill 5 productive boreholes in Mijelejele, Nakachindu, Chidya, Miwale and Pangani by June 2023.
Mijelejele, Nakachindu, Chidya, Miwale and Pangani
77,580,907.00
JUMLA MKOA MTWARA
5
0
2,403,493,439.54
822.
Mwanza
Ukerewe
Ukerewe DC
Extension of BukindoKagunguli Water scheme
Muhande, Buguza,Buze gwe and Nampisi villages
366,085,000.00
Jumla Ukerewe
366,085,000.00
823.
Mwanza
Misungwi
Misungwi DC
Construction of new water supply project at Kijima- Isakamawe villages
Kijina and Isakamawe
15,000,000.00
824.
Misungwi
Misungwi DC
Extension of mabalembarika
Ihelele
10,699,281.99
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
scheme to ihelele village
Jumla Misungwi
3
–
25,699,281.99
825.
Magu
Magu DC
Construction of Mahaha Water Supply Project
Mahaha
180,000,000.00
826.
Magu
Magu DC
Extension of Lugeye- Kigangama and of Kabale, Igombe, Kitongosima, Kinango and Yichobela Water Supply Schemes Water Supply Schemes
Lugeye, Kigangama and Kitongosima, Kabale, Igombe, Kitongosima, Kinango and Yichobela
130,000,000.00
Jumla Magu
2
310,000,000.00
JUMLA MKOA MWANZA
6
701,784,281.99
827.
Njombe
Ludewa
Ludewa DC
Construction of Lupingu water supply scheme (PHASE II) and Luvuyo and Mavanga, Kiyogo and Igalu water schems
Lupingu and Luvuyo and Mavanga, Kiyogo and Igalu
429,000,000.00
828.
Ludewa
Ludewa DC
Rehabilitation of Mawengi gravity water scheme
Mawengi, Lupande na Madunda
173,361,313.13
Jumla Ludewa
3
–
692,361,313.13
829.
Njombe
Njombe DC
Construction of completion of Kichiwa Pumping water Scheme
Kichiwa, maduma and Tagamenda
320,530,000.00
Jumla Njombe
1
–
320,530,000.00
830.
Makambako TC
Construction of Wangama – Mfumbi Water Supply Project
Wangama na Mfumbi
84,945,057.92
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Jumla Makambako
2
–
84,945,057.92
831.
Makete
Makete DC
Construction of Ujuni – Nkenja Water Supply Scheme
Ujuni, Nkenja
140,834,621.00
832.
Makete
Makete DC
Rehabilitation and extension of Water Supply Schemes in Ludilu, Makyala, Kijyombo, Malanduku and Ukange villages
Ludilu, Kijyombo, Makyala, Malanduku, na Ukange
170,550,000.50
833.
Makete
Makete DC
Extention of Magoye, Lupalilo and Tandala Water Supply Schemes
Magoye, Lupalilo and Tandala
150,000,000
Jumla Makete
3
836,384,622.10
834.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Construction of Igando Kijombe Gravity Water supply scheme (Hanjawanu – Kijombe Section) and Mpando- Mdandu- Sakalenga water supply schemes
Kijombe and Madandu, Sakalenga, Itulahumba
824,868,328
835.
Wanging’o mbe
Wanging’om be DC
Rehabilitation of Gravity Schemes for Kidugala, Mkeha, Masage, Mdasi,
Mdasi, Mwilamba, Ivigo, Kidugala, Mkeha and Masage
196,165729
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Mwilamba and Ivigo
836.
Wanging’o mbe
Wanging’ombe DC
Extension of Igando – Kijombe & Igando – Kijombe Gravity Water Supply Scheme in Mpanga na Wangamiko Villages
Mpanga and Wangamiko & Igando – Kijombe
325,000,000.00
Jumla Makete
3
–
716,384,622.10
837.
Wanging’o mbe
Wanging’ombe DC
Construction of Igando Kijombe Gravity Water supply scheme (Hanjawanu – Kijombe Section)
Kijombe
204,556,907.00
838.
Wanging’o mbe
Wanging’ombe DC
Construction of Gravity Scheme at MpandoMdanduSakalenga
Madandu, Sakalenga, Itulahumba
516,488,328.00
839.
Wanging’o mbe
Wanging’ombe DC
Rehabilitation of Gravity Schemes for Kidugala, Mkeha, Masage, Mdasi, Mwilamba and Ivigo
Mdasi, Mwilamba, Ivigo, Kidugala, Mkeha and Masage
425,837,700.00
Jumla Wanging’ombe
3
–
1,356,034,057.00
JUMLA MKOA NJOMBE
10
3,170,255,050.15
840.
Pwani
Mkuranga
Mkuranga DC
Construction of Piped Water Supply Project for Mbulani and Kibuyuni Villages
Mbulani, Kibuyuni, Kizomla, Kikundi, Kizapala
300,000,000.00
841.
Mkuranga DC
Construction of Piped Water
Mlamleni, Mwarusembe
250,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Supply Project for Mlamleni and Mwarusembe Villages
842.
Mkuranga
Mkuranga DC
Installation of electric power at Njopeka, Vianzi, Mfurumwamba o/Marogoro, Msorwa, Shungubweni, Kolagwa, Kilimahewa kusini/Mvuleni and Mwanadilatu Water projects
Njopeka, Vianzi, Mfurumwamb ao / Marogoro, Msorwa, Shungubweni , Kolagwa, Kilimahewa kusini / Mvuleni and Mwanadilatu
34,619,527.60
Jumla Mkuranga
3
–
584,619,527.60
843.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Construction of water Treatment Plant at Sadani Subvillage
Sadani
257,166,517.31
844.
Bagamoyo
Bagamoyo DC
Geophysical survey and Drilling of 4 boreholes at Kwakonje, Razaba, Mazizi and Gongo
Kwakonje, Razaba, Mazizi and Gongo
103,872,000.00
Jumla Bagamoyo
2
–
361,038,517.31
845.
Kisarawe
Kisarawe DC
Extension of Chole-Kwala Water Supply Scheme fto Kisangile, Titu, Yombolukinga, Mtunani and Mafumbi
Kisangile, Titu, Yomboluking a, Mtunani and Mafumbi
91,701,100.84
846.
Kisarawe
Kisarawe DC
Rehabilitation of Kului water
Kului
50,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
supply scheme
847.
Kisarawe
Kisarawe DC
Construction of Bembeza water supply project
Bembeza
555,784,773.16
848.
Kisarawe
Kisarawe DC
Geophysical survey and Drilling of 3 boreholes at Maneromango, Kidugalo and Bembeza Villages.
Maneromang o, Kidugalo and Bembeza
11,540400
Jumla Kisarawe
4
–
709,206,274.00
849.
Kibiti
Kibiti DC
Construction of water Supply infrastructure at Kikale village
Kikale
148,686,833.06
850.
Kibiti
Kibiti DC
Rehabilitation of Kibiti Urban Water Supply Scheme (Extension, Development of 10 Boreholes, Installation of Prepaid Meters, Construction of Aeration Treatment Plant)
70,000,000.00
851.
Kibiti
Kibiti DC
Geophysical survey and Drilling of 3 Productive boreholes
Kinguli, Kibiti urban and Bungu
110,775,848.74
Jumla Kibiti
2
–
329,462,681.80
852.
Rufiji
Rufiji DC
Construction of water supply infrastructure at Nambunju/Mich iwili village, Kikobo, Kungurwe, Namakono,
Nambunju/Mi chiwili village, Kikobo, Kungurwe, Namakono, Nyanda/Katu ndu and Nyawanje
150,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Nyanda/Katund u and Nyawanje
853.
Rufiji
Rufiji DC
Rehabilitation of water infrastructure at Mwaseni and Mibuyusaba village
Mwaseni na Mibuyusaba
90,000,000.00
Jumla Rufiji
2
–
240,000,000.00
854.
Kibaha
Construction of Piped Water Supply Project for Kipangege in Kibaha District
Kipangege
220,000,000.00
Jumla Kibaha
1
–
220,000,000.00
JUMLA PWANI
13
1,894,327,000.71
855.
Rukwa
Kalambo
Kalambo
Construction of Treatment plant facilities for old Matai Water Supply Project
Kateka, Matai A, Kisungamile & Santamaria
67,292,284.00
856.
Kalambo
Rehabilitation of Ulumi Water Supply Scheme Phase I
Ulumi A & Ulumi B
25,433,010.00
857.
Kalambo
Kalambo DC
Uchimbaji wa Visima virefu katika Vijiji Sita vya Safu, Jengeni, Kazonzya, Mpanga, Chisambo na Mzungwa
Safu, Jengeni, Kazonzya, Mpanga, Chisambo na Mzungwa
70,000,000.00
858.
Nkasi
Nkasi DC
Uchimbaji wa Visima virefu katika Vijiji vinne vya Myula, Londokazi, Malongwe,
Myula, Londokazi, Malongwe, Nkomanchind o na Nkana
60,300,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Nkomanchindo na Nkana
JUMLA MKOA RUKWA
4
223,025,294.00
859.
Simiyu
Meatu
Meatu Dc
Construction of water supply project in Makao Village.
Makao
617,453,607.89
860.
Meatu
Meatu Dc
Drilliong of 4 boreholes, Rehabilitation of 20 water wells, purchasing of new hand pumps and spare parts for 20 wells
Mwabuma, Lukale, Mwakisandu, Mwasengela, Tindabuligi, Lingeka, Masanga, Mwabulutago , Mwashata, Butuli na Ntobo; Mwangudo, Bulyashi, Mwamanong u na Mbushi
176,176,143.12
Jumla Meatu
2
–
793,629,751.01
861.
Busega
Busega Dc
Construction of Nyaluhande water supply project (New)
Nyaluahande, Mwamkala, Mwagindi
662,529,696.00
862.
Busega
Busega Dc
Rehabilitation of 25 wells,purchasin g of new hand pumps and spare parts for 25 wells
Construction of Byuna, Nyanguge, Halawa – Damidami, Matongo, Gasuma, Igegu, and Ibulyu water supply project
Byuna and Songambele, Nyanguge and Nyansosi, Halawa, Damidami and Nkindwabiye, Matongo, Gasuma, Bulumbaka and Mwaubingi, Igegu Mahariki, Magharibi and Sapiwi, Ibulyo and Sakwe
Drilling and development of 15 productive boreholes at Ntondo, Nkwae, Sekoutoure, Kinyamwenda, Msikii, Mwalala, Ngongoapoku, Igauri, Mwakiti, Itamka, Mkenge, Makuro, Misinko, Msimihi and Makhandi (NWF)
Ntondo, Nkwae, Sekoutoure, Kinyamwend a, Msikii, Mwalala, Ngongoapok u, Igauri, Mwakiti, Itamka, Mkenge, Makuro, Misinko, Msimihi and Makhandi
328,266,466.00
Jumla Singida DC
7
–
2,143,440,884.00
901.
Ikungi
Ikungi DC
Construction of Mpetu Pumped Piped Water Supply Scheme with 14 Public water Points in Ikungi District by June 2023
Mpetu
298,462,645.27
902.
Ikungi
Ikungi DC
Construction of Magungumka Pumped Piped Water Supply Scheme with 10 Public water Points in Ikungi District by June 2023
Magungumka
303,514,291.33
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
903.
Ikungi
Ikungi DC
Drilling and development of 10 productive boreholes at Germany, Kituntu, Kinyamwandyo , Mwasutianga, Makilawa, Utaho B, Samaka, Ngongosoro, Wibia and Mahambe in Ikungi
Germany, Kituntu, Kinyamwand yo, Mwasutiang a, Makilawa, Utaho B, Samaka, Ngongosoro, Wibia and Mahambe
192,486,000.00
Jumla Ikungi
3
–
794,462,936.60
904.
Manyoni
Manyoni DC
Rehabilitation of Majiri water supply scheme
Majiri
88,000,000.00
905.
Manyoni
Manyoni DC
Geophysical Survey and Drllingi of 11 productive bore holes
Mpapa, Igwamadete, Mbwasa (2), Sasajila, Majiri, Chicheo, Ikasi, Makasuku, Ihangwendul u and Itetema
129,592,406.89
Jumla Manyoni
2
–
217,592,406.89
906.
Manyoni
Itigi DC
Construction of water infrastructure at Muhanga village
Muhanga
300,000,000.00
907.
Manyoni
Itigi DC
Extension of Kihanju Water Supply scheme
Kihanju
30,113,872.00
908.
Manyoni
Itigi DC
Rehabilitation of Rungwa Dam at
Rungwa
277,322,807.12
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Rungwa Village.
909.
Manyoni
Itigi DC
Geophysical Survey and Drillingi of 10 productive bore holes
Construction of Nkalakala Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District (P4R)
Nkalakala
400,000,000.00
911.
Mkalama
Mkalama DC
Construction of Malaja Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District(P4R)
Malaja
330,000,000.00
912.
Mkalama
Mkalama DC
Construction of Mbigigi Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District (NWF)
Mwangeza
200,000,000.07
913.
Mkalama
Mkalama DC
Construction of Gambasimboi sub- village Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District(P4R)
Mwangeza
71,165,231.00
914.
Mkalama
Mkalama
Rehabilitation
Gumanga
68,000,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
of Gumanga Pumped Piped Water Supply Scheme (PforR)
915.
Mkalama
Mkalama DC
Rehabilitation of Miganga Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District(PforR)
Miganga
110,000,000.00
916.
To conduct Rehabilitation of Muntamba Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District
Muntamba
117,214,784.00
917.
Mkalama
Mkalama
Drilling of 11 exploratory boreholes and productuve wells for Iambi, Dominic, Tumuli, Igonia, Mwangeza, Makulo, Kidii, Singa, Lukomo, Gumanga and Lugongo villages in Mkalama District(NWF)
Construction of Njelenje Solar piped water project
Njelenje
300,000,000.00
928.
Songwe
Songwe DC
Construction of Manda Juu Solar piped water project
Manda
94,107,296.00
929.
Songwe
Songwe DC
Extension of
Mkwajuni
259,731,817.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Mkwajuni water project
930.
Songwe
Songwe DC
Rehabilitation of Ileya and Ifwenkenya water project
Ileya, Ifwenkenya
300,000,000.00
931.
Songwe
Songwe DC
Rehabilitation of Ngwala water project
Ngwala
320,000,000.00
932.
Songwe
Songwe DC
Construction of Itiziro water project
Itiziro
250,000,000.00
933.
Songwe
Songwe DC
Construction of Wanzani – Ifuko water project
Wanzani, Ifuko
20,000,000.00
934.
Songwe
Songwe DC
Construction of Namkukwe – Isanzu water project
Namkukwe, Isanzu
20,000,000.00
935.
Songwe
Songwe DC
Construction of Namambo – Ndanga water project
Namambo, ndanga
20,000,000.00
936.
Songwe
Songwe DC
Construction of Mheza – Manda water project
Mheza, Manda
20,000,000.00
937.
Songwe
Songwe DC
Construction of Mpona water project
Mpona
20,000,000.00
938.
Songwe
Songwe DC
Construction of Saza water project
Saza
20,000,000.00
939.
Songwe
Songwe DC
Construction of Ilasilo water project
Ilasilo
20,000,000.00
940.
Songwe
Songwe DC
Construction of Kanga – Tete water project
Kanga , Tete
20,000,000.00
941.
Songwe
Songwe DC
Construction of Rukwa water project
Rukwa
20,000,000.00
Jumla Songwe
17
–
2,703,839,113.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
942.
Mbozi
Mbozi DC
Construction of Shiwinga Haterere water supply project
Shiwinga, Haterere
100,000,000.00
943.
Mbozi
Mbozi DC
Construction of Msia Iganduka water supply project
Msia, Iganduka
171,930,800.00
944.
Mbozi
Mbozi DC
Construct Mbozi Mission Water Supply Project
Matula
366,515,434.00
945.
Mbozi
Mbozi DC
Construct group Water supply project for Idiwili, Nyimbili and Mpanda villages
Idiwili, Nyimbili, Mpanda
750,000,000.00
946.
Mbozi
Mbozi DC
Construction group Water Supply project for Chimbuya, Mponela and Ukwile Villages
Chimbuya, Mponela, Ukwile
600,000,000.00
947.
Mbozi
Mbozi DC
Extension of Maninga Water Scheme to Ikonya village
Maninga, Ikonya
230,000,000.00
948.
Mbozi
Mbozi DC
Construction of group Water supply project for Isansa, Mpito and Isowezya villages
Isansa, Mpito, Isowezya
720,000,000.00
949.
Mbozi
Mbozi DC
Construction of group Water supply Project for Isalalo, Wasa, Malolo and Izyeniche villages
Isalalo, Wasa, Malolo, Izyaniche
800,000,000.00
Jumla Mbozi
2
–
4,475,879,409.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
950.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in KisyeseVillage
Kisyese
225,000,000.00
951.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in MtemboVillage
Mtembo
159,885,000.00
952.
Ileje
Ileje DC
Extension of Itumba- Isongole water supply scheme
Itumba, Isongole
285,461,124.00
953.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Itega Village
Itega
80,000,000
954.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Kikota Village
Kikota
100,000,000
955.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Mswima Village
Mswima
80,000,000
956.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Ngulite Village
Ngulite
200,000,000
957.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Shuba Village
Shuba
100,000,000
958.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Chilemba Village
Chilemba
100,000,000
959.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Bulunga Village
Bulunga
80,000,000
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
960.
Ileje
Ileje DC
construction of water supply project in Sapanda Village
Sapanda
150,000,000
961.
Ileje
Ileje DC
Construction of water supply project in Lusalala Village
Lusalala
100,000,000
Jumla Ileje
2
–
2,190,346,124.00
962.
Momba
Momba DC
Completion of Mkomba water supply project Village
Mkomba
228,347,000.00
963.
Momba
Momba DC
Completion of Mpapa- Masanyinta water supply project Village
Mpapa, Masanyinta, Kasanu
436,279,073.00
964.
Momba
Momba DC
Completion of Ipito- MjiMwema water supply project Village
Mji Mwema, Migombani, Jakaya
120,215,325.00
965.
Momba
Momba DC
Completion of Uhuru- Tunduma water supply project Village
Tunduma, Makambini, Uwanjani
245,960,501.00
966.
Momba
Tunduma TC
Completion of Uhuru-Nyerere water supply project Village
Majengo Mapya, Mwl Nyerere, Msongwa
75,454,000.00
967.
Momba
Momba DC
Extension of Samang’ombe water supply project Village
Ivuna, Lwatwe, Kalungu na Samang’omb e
104,686,055.00
968.
Momba
Momba DC
Completion of Mkomba water supply project Village
Mkomba
28,347,000.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
969.
Momba
Momba DC
Completion of Mpapa- Masanyinta water supply project Village
Mpapa, Masanyinta, Kasanu
236,279,073.00
970.
Momba
Tunduma TC
Completion of Ipito- MjiMwema water supply project Village
Mji Mwema, Migombani, Jakaya
120,215,325.00
971.
Momba
Tunduma TC
Completion of Uhuru- Tunduma water supply project Village
Tunduma, Makambini, Uwanjani
155,960,501.00
972.
Momba
Momba DC
Construction of Msangano water supply project Village
Msangano, Naming’ong’ o, Makamba, Nkala, Yala, Ipata, Ntinga and Chindi
400,000,000
973.
Momba
Momba DC
Construction of Isanga, Kakozi, Kapele, Itumba and Mlomba water supply project Village
Isanga, Kakozi, Kapele, Itumba and Mlomba
190,000,000
974.
Momba
Mbozi DC
Consultancy service Momba group-Momba River
80,000,000
Jumla Momba
2
–
1,390,941,954.00
JUMLA SONGWE
27
0
11,061,006,600.0 0
975.
Tabora
Nzega
Nzega DC
Extension of lake victoria water supply to Ilagaja and Igalula villages by June 2023
Igalula and Ilagaja
475,000,000.00
976.
Nzega
Nzega DC
Extension of Lake Victoria water supply to
Gemedu
287,230,345.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
Gemedu village by June 2023
977.
Nzega
Nzega DC
extension of lake victoria water supply to Kigandu village by June 2023
Kigandu
309,000,000.00
978.
Nzega
Nzega DC
Rehabilitation and Extension of 46 Existing water supply Projects including procurements of pipes, spares, water flow meter and Fittings at different villages
Supply and Installation of power solar systems and submersible pump 7.5KW, Discharge 4m3/hr head max150m at Ikindwa and 7.5KW and Discharge of 4m3/hr head max150m at Nawa Villages by June 2023
Ikindwa and Nawa
55,403,610.00
980.
Nzega
Nzega DC
Rehabilitation of 54 Hands pump in Nzega DC by June 2023
Construction of Kigombe water tank and Mtiti water supply project
Kigombe
40,000,000.00
1008
Muheza
Muheza DC
Construction of treatment plant at water supply scheme at Ubembe, Mlingano, Kicheba, Mashewa na Misozwe
Ubembe, Kibanda Nkumba, Kicheba A, B, C, Mlingano, Misozwe, Mashewa,
40,000,000.00
1009
Muheza
Muheza DC
Construction of MIZEMBWE water supply project phase II
Mianga, Msowero, Bwembwera
44,121,931.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
1010
Muheza
Muheza DC
Constructiion of Kwedunda water supply scheme
Kwedunda
23,197,506.07
Jumla Muheza
5
14
197,319,437.07
JUMLA TANGA
18
0
2,610,220,365.95
1011
Shinyanga
Kishapu
Kishapu DC
Extension of Mwandoma water supply scheme to Mwamalasa village and Mwamalasa Secondary school by June 2023
Mwamalasa
60,094,486.40
1012
Shinyanga
Kishapu
Kishapu DC
Extension of Shagihilu water supply scheme to Shagihilu Secondary school by June 2023
Shagihilu
29,432,742.00
1013
Shinyanga
Kishapu
Kishapu DC
Extension of Mhunze to Mwabusiga Water Supply Project by June 2023
Mwabusiga
48,696,787.97
1014
Shinyanga
Kishapu
Kishapu DC
To extend Ukenyenge water supply project to Wila subvillage by June 2023
Wila
49,000,000.00
1015
Shinyanga
Kishapu
Kishapu DC
To conduct water Source development i.e geophysical survey and drilling of boreholes, sumpwell
Mangu, Mwamalasa, Somagedi, Mwalata, and Bulekela
40,787,072.00
Na.
Mkoa
Wilaya
Halmashauri
Jina la Mradi
Jina la Kijiji/ Vijiji Nufaika
Kiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka 2022/23
construction for Mangu, Mwamalasa, Somagedi, Mwalata, and Bulekela villages by June 2023
1016
Jumla Kishapu
5
9
228,011,088.37
1017
Kahama
Msalala DC
Construction of 11 hand dug wells at at Mhandu (1), Izumba (1), Ikinda (2) Nyamishiga (1), Nyaminje (1), Ndalilo (1), Wisolele (1), Kalagwa (1), Igundu (1) and Ilelema (1) villages at Msalala DC
Rehabilitation of 13 hand dug wells at Busulwangili (1), Lunguya (1), Chela (2), Mhandu (2), Buganzo (1), Kalagwa (1) na Buluma (1) na Nyakandoni (1), Bukwangu (1), Ntobo B(1), Jomu (1) in Msalala DC
Kiambatisho Na. 6: Miradi 175 ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini Itakayotekelezwa mwaka 2022/2023
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
1
Arusha
Arusha jiji
Kukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka Jijini Arusha
3,000,000,000
15,863,122,000
18,863,122,000
GoT/ AfDB
2
Arusha
Monduli
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
3
Arusha
Monduli
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Monduli-Enguiki
1,100,000,000
0
1,100,000,000
NWF
4
Arusha
Karatu
Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji kutoka visima vitatu vya maji
500,000,000
0
500,000,000
GoT
5
Arusha
Karatu
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Bwawani – Karatu
225,000,000
0
500,000,000
NWF
6
Arusha
Loliondo
Ukarabati na upanuzi wa mtandao wa maji safi.
500,000,000
0
500,000,000
GoT
7
Arusha
Mererani
Ujenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Mererani
1,400,000,000
0
1,400,000,000
NWF
8
Arusha
Oldonyo sambu
Ujenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Oldonyosambu
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
9
Arusha
Arumeru
Mradi wa Maji Embaseni – Arumeru (Ngurdoto)
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
10
Arusha
Ngorong oro
Mradi wa Maji Mageri Ngorongoro
600,000,000
0
600,000,000
NWF
291
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
11
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kujenga mitandao ya kusambaza maji katika maeneo ambayo hayana huduma hiyo katika Jiji la Dar es Salaam
2,000,000,000
22,000,000,000
24,000,000,000
GoT/ World Bank
12
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Buguruni
1,000,000,000
8,000,000,000
9,000,000,000
GoT/So uth Korea
13
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Mbezi Beach
1,000,000,000
4,624,274,955
5,624,274,955
GoT/ World Bank
14
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Kurasini
1,000,000,000
6,000,000,000
7,000,000,000
GoT/ AFD
15
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Ujenzi wa Bwawa la Kidunda
52,500,000,000
10,000,000,000
62,500,000,000
GoT/BF
16
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kuendelea na uchimbaji wa visima 20 Kimbiji na Mpera na ujenzi wa miundombinu ya majisafi.
2,820,000,000
0
2,820,000,000
GoT
17
Dar es Salaam
Dar es Salaam
Kujenga mradi wa majisafi kutoka mto Rufiji hadi Jijini Dar es Salaam
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
18
Dodoma
Dodoma
Kukarabati na kupanua mtandao wa majisafi Jijini Dodoma
2,500,000,000
7,000,000,000
9,500,000,000
GoT/Af DB
19
Dodoma
Dodoma
Kupanua na ukarabati wa mtandao wa majitaka Jijini Dodoma
2,900,000,000
4,000,000,000
6,400,000,000
GoT/N WF/ Korea
20
Dodoma
Dodoma
Ujenzi wa Mtandao wa Majisafi Mtera hadi Dodoma
500,000,000
500,000,000
1,000,000,000
GoT/W B
21
Dodoma
Dodoma
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Nala-Zuzu
400,00
0,000
0
400,000,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
22
Dodoma
Chamwin o
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Chamwino
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
23
Dodoma
Chamwin o- Mtumba
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Chamwino- Mtumba
550,000,000
0
550,000,000
NWF
24
Dodoma
Bahi
Ujenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji
400,000,000
0
400,000,000
GoT
25
Dodoma
Mpwapw a
Upanuzi na ukarabati wa mradi wa majisafi wa Mpwapwa
550,000,000
0
550,000,000
NWF
26
Dodoma
Kongwa
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao ya maji, kuunganisha na kufungia wateja dira za maji)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
27
Singida & Dodoma
Dodoma & Singida
Kujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria hadi Mikoa ya Singida na Dodoma
1,930,000,000
5,449,000,000
7,379,000,000
GoT/Af DB
28
Geita
Chato
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Chato
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
29
Geita
Chato
Ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Chato
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
30
Geita
Geita
Kuboresha mfumo wa maji katika mji wa Geita
1,100,000,000
0
1,100,000,000
GoT
31
Geita
Ushirom bo
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
32
Geita
Ushirom bo
Uboreshaji wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ushirombo
303,676,000
0
303,676,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
33
Geita
Mbogwe
Ujenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji
400,000,000
0
400,000,000
GoT
34
Geita
Katoro
Ujenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji
500,000,000
0
500,000,000
GoT
35
Geita
Katoro- Buseres ere
Upanuzi wa mtandao wa majisafi wa KatoroBuseresere awamu ya pili
400,000,000
0
400,000,000
NWF
36
Iringa
Kilolo
Ujenzi wa tanki lenye mita za ujazo 100, Kuchimba na kulaza bomba kuu kilomita 4 na ununuzi wa dira za maji 600
300,000,000
0
300,000,000
GoT
37
Iringa
Kilolo
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Isimani-Kilolo
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
38
Iringa
Mafinga
Uboreshaji wa huduma ya maji mjini Mafinga (Ihongole, Changarawe, Kinyayambo & Sao Hill
700,000,000
0
700,000,000
GoT/N WF
39
Kagera
Bukoba
Ujenzi wa mtandao wa majitaka katika manispaa ya Bukoba
2,000,000,000
0
2,000,000,000
GoT
40
Kagera
Bukoba
Kupanua mtandao wa majisafi Bukoba Mjini
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
41
Kagera
Bukoba
Upanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya pembezoni mwa mji na VETA
400,000,000
0
400,000,000
NWF
42
Kagera
Muleba
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na
300,000,000
0
300,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
kuunganisha wateja)
43
Kagera
Ngara
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
44
Kagera
Ngara
Uchimbaji wa visima na upanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ngara
492,000,000
0
492,000,000
NWF
45
Kagera
Biharam ulo
Ujenzi wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka Mji wa Biharamulo
500,000,000
0
500,000,000
GoT
46
Kagera
Biharam ulo
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi mjini Biharamulo (Biharamulo mjini, Nyarubungo, Runazi, Nyakahura, Bisibo, Nemba, Nyanza Areas)
730,269,723
0
730,269,723
GoT/N WF
47
Kagera
Kyaka- Bunazi
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Kyaka-Bunazi
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
48
Kagera
Muleba
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Muleba
328,000,000
0
328,000,000
NWF
49
Katavi
Mpanda
Kuboresha mfumo wa maji katika mji wa Mpanda (Shankala Water awamu ya II)
1,400,000,000
0
1,400,000,000
GoT/N WF
50
Kigoma, Rukwa, Lindi
Sumbaw anga, Lindi & Kigoma
Kujenga miundombinu ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji ya Kigoma,
1,800,000,000
4,000,000,000
5,800,000,000
GoT/ EU/ KfW
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
Sumbawanga na Lindi
51
Kigoma
Kibondo
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
52
Kigoma
Kibondo
Ujenzi, upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Kibondo
800,000,000
0
800,000,000
NWF
53
Kigoma
Kasulu
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
54
Kigoma
Kasulu
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Kasulu (Kata za Murubona, Murusi, Kumnyika na Kumsenga Murubona)
335,000,000
0
335,000,000
NWF
55
Kilimanj aro
Moshi
Kupanua mtandao wa kupitisha majitaka katika Manispaa ya Moshi.
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
56
Kilimanj aro
Same – Mwanga
Ujenzi wa Mradi wa majisafi Same- Mwanga- Korogwe
10,648,000,000
3,000,000,000
11,648,000,000
GoT/ NWF/B ADEA KUWAI T/SAUD FUND/ DFID
57
Kilimanj aro
Himo
Upanuzi wa mitandao, ununuzi wa dira za maji na kuunganisha
400,000,000
0
400,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
wateja
58
Kilimanj aro
Moshi Rural
Uboreshaji wa huduma ya maji (upanuzi wa mtandao wa maji)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
59
Kilimanj aro
Rombo
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Rombo Mjini
500,000,000
0
500,000,000
GoT
60
Kilimanj aro
Rombo
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Rombo (Mahorosha, Msaranga, Kwalakamu, Ngoyoni, in Rombo Mjini)
600,000,000
0
600,000,000
NWF
61
Kilimanj aro
Moshi Mjini
Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika Kata 12
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
62
Kilimanj aro
Moshi Mjini
ujenzi wa mtandao wa majisafi wa Miwaleni – Njiapanda
700,000,000
0
700,000,000
NWF
63
Lindi
Ng’apa, Mitwero na Mchinga
Kujenga miundombinu ya majisafi katika maeneo ya Ng’apa, Mwitero na Mchinga katika Mji wa Lindi
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
64
Lindi
Mitwero, Mkwaya na Kitunda
Kujenga miundombinu ya majisafi katika maeneo ya Mitwero, Mkwaya na Kitunda
500,000,000
0
500,000,000
NWF
65
Lindi
Mchinga Phase II
Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Mchinga awamu ya kwanza
1,010,000,000
0
1010000000
NWF
66
Lindi
Ruangw a
Ujenzi na upanuzi wa mtandao wa
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
majisafi katika Mji wa Ruangwa
67
Lindi
Ruangw a
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ruangwa kwenye maeneo ya hospitali ya Wilaya, Mji mpya karibu na Majaliwa stadium A’, Magereza na Shule ya Msingi Dodoma
350,000,000
0
350,000,000
NWF
68
Lindi
Liwale
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
69
Manyara
Babati
Kujenga miundombinu ya majisafi katika Mji wa Babati
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
70
Manyara
Babati, Lindi, Kigoma na Sumbaw anga
Ujenzi wa mtandao wa majisafi Mjini Babati na mtandao wa majitaka katika Miji ya Babati, Sumbawanga, Lindi na Kigoma
500,000,000
2,000,000,000
2,500,000,000
GoT/Kf W
71
Manyara
Babati
Ujenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Babati
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
72
Manyara
Orkesum ent
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Orkesment
2,300,000,000
7,500,000,000
9,500,000,000
GoT/ NWF/B ADEA
73
Manyara
Mererani
Ujenzi wa matanki mawili yenye jumla ya mita za ujazo 180, na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji.
300,000,000
0
300,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
74
Manyara
Katesh
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
75
Manyara
Bashnet
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
76
Manyara
Magugu
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
77
Manyara
Gallapo
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
78
Manyara
Sawe
Ujenzi wav tanki la kuhifadhia majisafi (2,000m3) katika maeneo ya Sawe
900,000,000
0
900,000,000
NWF
79
Manyara
Dareda
Ujenzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Dareda -Singu-DagailoySiginoi
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
80
Mara
Musoma
Ujenzi na upanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Musoma kwenye maeneo ya Kwangwa, Songambele, Bukoba, Bweri, Nyangwe and Kiara A areas
300,000,000
0
300,000,000
NWF
81
Mara
Bunda
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Bunda
2,700,000,000
0
2,700,000,000
GoT/N WF
82
Mara
Mugango
Ujenzi wa mradi wa Mugango- Kiabakari-Butiama, pamoja na vijiji
4,000,000,000
3,500,000,000
6,500,000,000
GoT/ NWF/B ADEA/ SAUDIA
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
vilivyo pembezoni mwa bomba kuu
83
Mara
Tarime
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
84
Mara
Mugumu
Kukamilisha Ujenzi wa mtambo wa kutibu majisafi katika bwawa la Manchira
300,000,000
0
300,000,000
GoT
85
Mbeya
Mbeya
Ujenzi wa miundombinu ya majisafi kutoka chanzo cha Kiwira
5,000,000,000
0
5,000,000,000
GoT/N WF
86
Mbeya
Chunya
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
87
Mbeya
Kyela
Ujenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Kyela
800,000,000
0
800,000,000
NWF
88
Mbeya
Mbalizi
Mradi wa kuboresha huduma ya Maji Iwambi na Mbalizi (Ilunga Project)
700,000,000
0
700,000,000
NWF
89
Mbeya
Mbaka
Mradi wa kuboresha huduma ya majisafi Tukuyu kutoka chanzo cha Mto Mbaka
500,000,000
0
500,000,000
NWF
90
Morogor o
Morogor o
Kukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka Mji wa Morogoro
1,000,000,000
4,000,000,000
5,000,000,000
GoT/ AfD
91
Morogor o
Morogor o
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa maji
700,000,000
0
700,000,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
Mindu
92
Morogor o
Ifakara
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
93
Morogor o
Mikumi
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
94
Morogor o
Kilosa
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa maji wa Manzese kilosa na Kingolowira
807,794,961
0
807,794,961
NWF
95
Mtwara
Mtwara
Kujenga mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma hadi Manispaa ya Mtwara-Mikindani, vikiwemo vijiji vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu
1,000,000,000
4,000,000,000
5,000,000,000
GoT/Af DB
96
Mtwara
Mtwara
Upanuzi na ukarabati wa chujio la Mangamba na Mtawanya
267,054,277
0
267,054,277
NWF
97
Mtwara
Makonde
Kukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa Makonde
1,500,000,000
0
1,500,000,000
GoT/N WF
98
Mtwara
Masasi
Ujenzi miundombinu ya majisafi katika mradi wa Masasi/Nachingwe a.
1,240,000,000
0
1,240,000,000
GoT/N WF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
99
Mtwara
Mangaka
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
100
Mtwara
Nanyam ba
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
101
Mwanza
Mwanza, Misungwi , Lamadi & Magu
Kupanua mtandao wa majitaka katika miji ya Mwanza, Bukoba na Musoma; na Kujenga mtandao wa majisafi katika miji ya Misungwi na Magu
1,000,000,000
4,000,000,000
5,000,000,000
GoT/ EIB & AFD
102
Mwanza
Mwanza Jiji
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya pembezoni mwa mji wa Mwanza; Kayenze, Igombe, Shibula, Lwanhima and Sangabuye.
350,000,000
0
350,000,000
NWF
103
Mwanza
Kwimba, Malampa ka, Sumve
Kujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria hadi miji ya Malampaka, Sumve na Malya
2,000,000,000
0
2,000,000,000
GoT
104
Mwanza
Sengere ma
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Nyasigu – Lubungo – Ngoma
900,000,000
0
900,000,000
NWF
105
Njombe
Wanging’ ombe
Kukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
mradi wa kitaifa wa Wanging’ombe
106
Njombe
Njombe
Kuboresha mfumo wa maji katika mji wa Njombe
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
107
Njombe
Njombe
Upanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Livingstine (Ijunilo)
417,000,000
0
417,000,000
NWF
108
Njombe
Njombe
Ujenzi wa mabwawa ya majitaka katika Mji wa Njombe
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
109
Njombe
Makete
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
110
Njombe
Makamb ako
Uboreshaji wa huduma ya maji maeneo ya (Majengo, Kikula, Magavani na Mlowa)
900,000,000
0
500,000,000
GoT/N WF
111
Pwani
Chalinze
Ujenzi wa mradi wa maji wa Chalinze (Awamu ya Tatu)
300,000,000
6,051,000,000
6,351,000,000
GoT/Ind ia
112
Ruvuma
Tunduru
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
113
Ruvuma
Tunduru
Uboreshaji wa mtandao wa majisafi katika mji wa Tunduru Township awamu ya II
450,000,000
0
450,000,000
NWF
114
Ruvuma
Mbinga
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu,
400,000,000
0
400,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
115
Ruvuma
Songea
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika hospitali ya rufaa ya ya Ruvuma maeneo ya Mwengemshindo
465,000,000
0
465,000,000
NWF
116
Rukwa
Sumbaw anga
Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Muze
250,000,000
0
250,000,000
NWF
117
Rukwa
Sumbaw anga
Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Kirando Kamwanda
300,000,000
0
300,000,000
NWF
118
Shinyan ga
Shinyang a
Kujenga na kukarabati mtandao wa majisafi katika Mji wa Shinyanga
300,000,000
1,000,000,000
1,300,000,000
GoT/ AFD
119
Shinyan ga
Ushetu
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
120
Shinyan ga
Isaka
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
121
Shinyan ga
Malampa ka
Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Lake Victoria kwenda miji ya Mhalo Malampaka na Mallya kwa umbali wa kilomita 79
500,000,000
0
500,000,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
122
Shinyan ga
Shinyang a
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Wilaya ya Shinyanga (Mwanubi, Didia, Iselamagazi, Kizumbi, Ibadakuli, Kolandoto, Chibe and Lubaga)
800,000,000
0
800,000,000
NWF
123
Shinyan ga
Kahama
Upanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Kata ya Kilago na Kahama
750,000,000
0
750,000,000
NWF
124
Shinyan ga
Kagongw a na Kahama
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Kata ya Isagehe; Mwenda Kulima na Kagongwa Isaka
400,000,000
0
400,000,000
NWF
125
Simiyu
Maswa
Kukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa Maswa
700,000,000
0
700,000,000
GoT
126
Simiyu
Maswa
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Maswa (Vijiji vya Mwashegeshi na Buyupi)
267,487,318
0
267,487,318
NWF
127
Simiyu
Bariadi
Kuboresha mfumo wa maji katika mji wa Bariadi
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
128
Simiyu
Bariadi
Uborreshaji wa mtandao wa majisafi Bariadi mjini kwenye maeneo ya Old Maswa and Kidinda
300,000,000
0
300,000,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
129
Simiyu
Busega, Bariadi, Laganga bilili na Mwanhu zi
Kujenga mradi wa kutoa Ziwa Victoria hadi miji ya Busega, Bariadi, Lagangabilili na Mwanhuzi
3,000,000,000
16,510,000,000
19,510,000,000
GoT/ KFW/ GCF
130
Simiyu
Laganga bilili
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
131
Simiyu
Mwanhu zi
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
132
Simiyu
Mwanhu zi
Uboreshaji wa huduma ya majisafi katika mji wa Mwanhuzi
300,000,000
0
300,000,000
NWF
133
Simiyu
Busega
Upanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Mwalukonge, Bukabile – Bulima na Lukungu
300,000,000
0
300,000,000
NWF
134
Simiyu
Maswa
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
135
Singida
Singida
Kukarabati na kupanua mtandao wa majisafi katika Mji wa Singida
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
136
Singida
Singida
Ujenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
137
Singida
Singida
Ujenzi wa mradi
300,000,000
0
300,000,000
NWF
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
wa maji wa Unyambwa
138
Singida
Manyoni
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati na upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
139
Singida
Itigi
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati na upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
140
Songwe
Vwawa
Kuboresha mfumo wa maji katika mji wa Vwawa/ Mlowo.
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
141
Songwe
Vwawa & Tundum a
Kukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka katika miji ya Vwawa na Tunduma
1,000,000,000
5,000,000,000
6,000,000,000
GoT/Kf W
142
Songwe
Vwawa
Uboreshaji wa huduma ya majisafi katika mji wa Vwawa (chanzo cha Mwansyana )
392,106,601
0
392,106,601
NWF
143
Tabora
Tabora
Ujenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Tabora
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
144
Tabora
Tabora
Ukarabati wa bomba kuu la majisafi kutoka Msange JKT hadi Tumbi Area
250,000,000
0
250,000,000
NWF
145
Tabora
Nzega
Kukarabati na kupanua mfumo wa maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na mtandao mjini Nzega (Idudumo)
2,350,000,000
0
2,000,000,000
GoT/N WF
146
Tabora
Nzega
Ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
wa Nzega
147
Tabora
Igunga
Ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Igunga
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
148
Tabora
Tinde na Shelui
Ujenzi wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda miji ya Tinde na Shelui.
340,000,000
6,560,070,000
6,900,070,000
GoT/ INDIA
149
Tabora
Sikonge
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
150
Tabora
Urambo
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
151
Tabora
Kaliua
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
152
Tabora
Izikizya
Ujenzi wa mtandao wa majisafi
400,000,000
0
400,000,000
GoT
153
Tanga
Tanga
Ujenzi wa bwawa ya kutibu majitaka na mtandao wa majitaka katika Jiji la Tanga
100,000,000
334,478,000
434,478,000
GoT/ WB
154
Tanga
Tanga
Ujenzi wa miundombinu ya majisafi na ufungaji wa pampu maeneo ya Madanga na Kimang’a
357,843,213
0
357,843,213
NFW
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
155
Tanga
Tanga
Ujenzi na ukarabati wa mradi wa majisafi wa Mabokweni areas – Kibafuta, Chongoleani, Mleni Water Supply Project in Tanga – awamu ya II
600,000,000
0
600,000,000
NFW
156
Tanga
Mkinga
Upanuzi wa mradi wa majisafi kutoka Tanga hadi mji wa Mkinga
500,000,000
0
500,000,000
NFW
157
Tanga
HTM
Kukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa HTM
1,000,000,000
0
0
GoT
158
Tanga
HTM
Ujenzi wa Chanzo cha maji cha Mandera, nyumba ya kuhifadhi pump na ukarabati wa tanki la Bongi
252,592,047
0
252,592,047
NFW
159
Tanga
HTM
Upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Segera – Kabuku
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NFW
160
Tanga
Muheza
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Muheza.
700,000,000
0
700,000,000
GoT
161
Tanga
Muheza
Uboreshaji wa hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi katika Mji wa Muheza
300,000,000
0
300,000,000
NFW
162
Tanga
Pangani
Ujenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Pangani.
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
163
Tanga
Pangani
Ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Pangani
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
164
Tanga
Muheza
Ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
wa Muheza
165
Tanga
Korogwe
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
500,000,000
0
500,000,000
GoT
166
Tanga
Songe
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
300,000,000
0
300,000,000
GoT
167
Tanga
Handeni
Uboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)
400,000,000
0
400,000,000
GoT
168
Miji ya Mipakani
Miji ya Mipakani
Ujenzi na ukarabati wa mfumo wa majisafi katika miji ya mipakani ya Holili, Horohoro, Namanga, and Sirari
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
169
Mikoa yote
Miji 28
Ujenzi na upanuzi wa mfumo wa majisafi katika Miji 28 (Muheza,Wanging’ombe,Kayanga,Makonde,Njombe,Makambako,HTM, Manyoni,Songea, Sikonge,Chunya, Kasulu,Kilwa Masoko,Rujewa, Mugumu,Geita, Chato,Zanzibar, Singida
Ujenzi na upanuzi wa mfumo wa majisafi katika Miji ya Songea, Rorya, Mafinga na Makonde
1,000,000,000
0
1,000,000,000
NWF
171
Mikoa yote
Mamlaka Zenye Upotevu Mkubwa wa Maji
Kutekeleza mikakati ya kupunguza upotevu wa maji katika Mamlaka za maji
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
172
Mikoa yote
Mamlaka zote
Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya majitaka katika miji mikuu ya mkoa
1,000,000,000
0
1,000,000,000
GoT
173
Mikoa yote
Miji Mingi
Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya maji katika miji mikuu ya wilaya na miji midogo
2,000,000,000
0
2,000,000,000
GoT
174
Mikoa yote
Miji midogo, Miji Mikuu ya Wilaya na Miradi ya Kitaifa
Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya majitaka katika miji midogo, miji mikuu ya Wilaya na Miradi ya kitaifa
1,000,000,000
4,000,000,000
5,000,000,000
GoT/Af DB
Na.
Mkoa
Mji/Eneo
Jina la Mradi/ Kazi
Kiasi cha fedha kilichotengwa
Jina la Mfadhili
Fedha za Ndani
Fedha za Nje
Jumla
175
MoW
MoW
Kujenga uwezo mamlaka za maji nchini kwa kujenga na kukarabati ofisi na kununua vitendea kazi
4,172,820,000
400,000,000
4,572,820,000
GoT/BT
JUMLA
214,951,644,140
184,731,278,000
394,407,922,140
[1]. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee napenda kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan; kwa uongozi makini na thabiti aliouonesha katika mwaka wa kwanza wa Serikali ya