HOTUBA YA WAZIRI MHE. JUMAA AWESO(MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023.

YALIYOMO

  1. UTANGULIZI ……………………………………………………….. 1
  2. HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI ………………………….. 5

1.     Hali ya Rasilimali za Maji ……………………………………….. 5 2. Hali ya Ubora wa Maji ……………………………………………. 6

3.     Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Maji Vijijini ………….. 8 4.   Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Majisafi na Usafi

wa Mazingira Mijini ……………………………………………….. 8

3.        UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2021/22 ….. 9

  1. Upatikanaji wa Fedha ……………………………………………. 9
  2. Programu na Miradi Mbalimbali Iliyotekelezwa katika

mwaka 2021/22 ………………………………………………….. 10

3.2.1   Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji ……… 10

3.2.2        Huduma za Ubora wa Maji …………………………………… 27 3.2.3         Huduma za Usambazaji Majisafi na Usafi wa

Mazingira Vijijini ………………………………………………….. 33

3.2.4     Huduma za Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa

Mazingira Mijini …………………………………………………… 37

3.2.4.1 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Mikoa …………………………………………………… 38

3.2.4.2 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa ……. 51

3.2.4.3 Mradi wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya

Tabianchi katika Mkoa wa Simiyu …………………………. 57

3.2.4.4 Miradi ya Maji katika Maziwa Makuu ya Victoria,

Tanganyika na Nyasa ………………………………………….. 57

3.2.4.5 Miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa

Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 ………………. 60

3.2.5        Miradi ya Usafi wa Mazingira ………………………………… 60 3.2.6         Taasisi zilizo Chini ya Wizara ……………………………….. 65

i

3.2.7   Masuala Mtambuka …………………………………………….. 70

  • MAFANIKIO YALIYOPATIKANA …………………………… 73
  • CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA NA HATUA

ZINAZOCHUKULIWA ………………………………………….. 75

  • VIPAUMBELE NA MPANGO WA UTEKELEZAJI

KWA MWAKA 2022/23 ………………………………………… 78

  • Vipumbele vya mwaka 2022/23 …………………………….. 78
    • Mpango wa Utekelezaji kwa Mwaka 2022/23 ………….. 78

6.2.1        Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za maji ……… 79 6.2.2         Usimamizi wa Huduma ya Ubora wa Maji ………………. 81

  • Huduma ya Majisafi na usafi wa Mazingira Vijijini ……. 82
    • Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini ……….. 83 6.2.5    Mpango wa Kuimarisha Huduma ya Uondoshaji

Majitaka …………………………………………………………….. 84

  • Chuo cha Maji …………………………………………………….. 85
    • Masuala Mtambuka …………………………………………….. 85
  • SHUKRANI ………………………………………………………… 86
  • MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023 ……… 89

ii

HOTUBA YA WAZIRI WA MAJI MHE. JUMAA HAMIDU AWESO(MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA WIZARA YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2[1]

1.        UTANGULIZI

  1. Mheshimiwa Spika, leo hii Bunge lako Tukufu limepokea taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, iliyochambua bajeti ya Wizara ya Maji. Naomba sasa, kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea, kujadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Kawaida na Maendeleo ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23.
  2. Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Kamati hiyo kwa kupokea na kuchambua Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23. Maoni, ushauri na maelekezo yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bungeya Kilimo, Mifugo na Maji yamezingatiwa wakati wa maandalizi ya bajeti ya Wizara yangu.Aidha, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mheshimiwa Daniel Baran Sillo Mbunge wa Babati Vijijini na wajumbe wake kwa maoni na ushauri wao uliorahisisha utekelezaji wa  bajeti ya Wizara yangu

Awamu ya Sita pamoja na juhudi zakehususan katika ukusanyaji wa kodi, utafutaji wa fedha; na kuimarisha mahusiano ya kitaifa na kimataifa. Vilevile, nichukue fursa hii kuwapongeza Makamu wa Rais, Mheshimiwa Daktari Philip Isidor Mpango; na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) kwa mchango wao mkubwa katika kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuijenga Tanzania kuwa nchi ya uchumi shindani.  

  • Aidha,naomba nikupongeze sana, wewe Mheshimiwa Dkt.Tulia Ackson (Mb) kwa kuchaguliwa kwako na Waheshimiwa Wabunge kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika. Vilevile, nawapongeza Mheshimiwa Najma Murtaza Giga (Mb) na Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile (Mb) kwa kuchaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge hili Tukufu.
  • Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha utendaji ndani ya Serikali kwa nyakati tofauti, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri ambapo aliteua Mawaziri wapya na kuwabadilishia Wizara Mawaziri wengine na kuwateua Manaibu Mawaziri. Ninaomba nitumie fursa hii kuwapongeza sana Mawaziri wenzangu wapya wote walioaminiwa na kuteuliwa nikianza na Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb.) Waziri wa Ulinzi na Jeshi la

Kujenga Taifa; Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji

(Mb), Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara; Mheshimiwa

January Yusuf Makamba (Mb) Waziri wa Nishati; Mheshimiwa Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb), Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi; Mheshimiwa Nape Moses Nnauye (Mb), Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari; Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb), Wizara ya Maliasili na Utalii; Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe (Mb), Waziri wa Kilimo; Mheshimiwa Hamad Yussuf Masauni (Mb), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; na Mheshimiwa Dkt. Angelina Sylvester Lubala Mabula (Mb), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ninaahidi kuwapa ushirikiano wa kutosha katika kulijenga Taifa letu.

  • Mheshimiwa Spika, vilevile, nawapongeza Manaibu

Mawaziri walioteuliwa nikianza na Mheshimiwa Jumanne 

Abdallah Sagini (Mb), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde (Mb), Naibu Waziri wa kilimo; Mheshimiwa Dkt. Stephen Lemomo

Kiruswa (Mb), Naibu Waziri wa Madini; Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete (Mb), Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; na Mheshimiwa Atupele  Fredy Mwakibete (Mb), Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.

  • Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii pia kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wapya ambao ni Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani (Mb) aliyechaguliwa kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Ushetu; Mheshimiwa Mohamed Said Issa (Mb) kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Konde; na Mheshimiwa Emmanuel Lekishon Shangai (Mb) kuwa Mbunge kupitia Jimbo la Ngorongoro. Nawapongeza pia Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) naMheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha (Mb) walioteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.  

  • Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pole kwako wewe mwenyewe Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu, Familia za Marehemu, Ndugu, Jamaa na Watanzania wote kwa misiba iliyotupata kwa kuondokewa na aliyekuwa Mbunge wa Ushetu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Elias John Kwandikwa  na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro; Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mheshimiwa William Tate Ole Nasha; na

Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama. Michango ya Wabunge hao katika shughuli za maendeleo ya Taifa letu itakumbukwa milele daima. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu hao mahali pema peponi. Amin.

  • Mheshimiwa Spika, naombapia nichukue fursa hii kumshukuru, Waziri Mkuuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa (Mb) kwa hotuba yake nzuri aliyoiwasilisha hapa Bungeni ambayo inatoa dira na mwongozo wa utekelezaji wa kazi za Serikali. Hotuba hiyo imeonesha mapitio ya uendeshaji wa shughuli za Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 na Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2022/2023 pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025). Vilevile, nawapongeza Mawaziri wenzangu wote walionitangulia kuwasilisha hoja zao na Wabunge waliochangia hoja hizo.
  • Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, napenda sasa kuchukua fursa hii kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara yangu yenye maeneo makuu manne yafuatayo:- Hali ya Sekta ya Maji nchini; Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 na Mpango na Bajeti ya Sekta kwa mwaka 2022/2023; pamoja na Changamoto na Hatua zilizochukuliwa. Maelezo ya maeneo hayo yamezingatia Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa; Sera, Mikakati ya Maendeleo ya Kitaifa na Kimataifa, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025); Sheria, Kanuni pamoja na maoni na ushauri wa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili tukufu. Maelezo ya kina kuhusu utekelezaji huo yameainishwa katika sehemu zifuatazo za hotuba hii.

2.        HALI YA SEKTA YA MAJI NCHINI

11. Mheshimiwa Spika, napenda kutoa maelezo kuhusu hali ya Sekta ya Maji nchini kwa kuzingatia hali ya rasilimali za maji; ubora wa maji; na upatikanaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira vijijini na mijini.

2.1 Hali ya Rasilimali za Maji

  1. MheshimiwaSpika, rasilimali za maji zilizopo nchini zinakadiriwa kuwa mita za ujazo bilioni 126 kwa mwaka ambapo rasilimali za maji juu ya ardhi ni mita za ujazo bilioni 105 na zilizopo ardhini ni mita za ujazo bilioni 21. Hadi kufikia mwezi Aprili 2022, mahitaji ya maji kwa matumizi mbalimbali nchini yanakadiriwa kuwa ni takribani mita za ujazo bilioni 47 kwa mwaka sawa na asilimia 37.37 ya maji yaliyopo nchini. Mahitaji hayo ya maji yanatarajiwa kuongezeka hadi kufikia wastani wa mita za ujazo bilioni 80 kwa mwaka ifikapo mwaka 2035. 
  2. Mheshimiwa Spika, kiwango cha maji kilichopo kwa kila mtu kwa mwaka ni takribani wastani wa mita za ujazo 2,250 kwa kuzingatia makadirio ya idadi ya watu milioni 55.9 kwa mwaka 2019. Kiwango cha chini cha mahitaji ya maji kwa mtu kwa mwaka kinachokubalika kimataifa ni wastani wa mita za ujazo 1,700 ambapo chini ya hapo nchi inahesabika kuwa na uhaba wa maji (Water Stress). Hivyo, kiasi cha maji kilichopo nchini kinaonesha kuwa nchi yetu haina uhaba wa maji.Hata hivyo, Serikali inaendelea kuwekeza katika utunzaji wa vyanzo vya maji, ujenzi wa miundombinu ya kuongeza upatikanaji wa maji; kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi; na kuboresha ufanisi katika matumizi ya maji kwa lengo la kuepusha nchi kuwa na uhaba wa maji.
  3. Mheshimiwa Spika, maeneo mengi ya nchi yetu hususan ukanda wa kaskazini; kanda ya ziwana maeneo ya pwani yanapata mvua katika misimu miwili ya vuli (mwezi Oktoba hadi Desemba) na masika (mwezi Machi hadi Mei). Maeneo mengine hususan ya katikati ya nchi, nyanda za juu kusini na baadhi ya maeneo ya ukanda wa magharibi yanapata mvua ya msimu mmoja unaoanzia mwezi Desemba hadi Mei.  Katika mwaka wa kihaidrolojia (Novemba 2020 – Oktoba 2021) wastani wa mvua iliyonyesha ni milimita 1,066.4 ambayo ni chini ya kiasi cha mvua kilichonyesha katika mwaka wa Kihaidrolojia Novemba 2019 – Oktoba 2020 kilichokuwa milimita 1,470. Aidha, mvua hizo ni juu ya wastani wa muda mrefu wa milimita 921 kwa mwaka. Hali hiyo imesababisha kiasi cha maji katika mito, mabwawa na maziwa kuendelea kuimarika katika maeneo mbalimbali nchini.

2.2 Hali ya Ubora wa Maji

  1. Mheshimiwa Spika, usimamizi wa ubora wa maji ni muhimu katika maendeleo ya taifa letu katika kulinda afya ya jamii na vyanzo vya maji. Wizara kupitia maabara 17 za ubora wa maji nchini imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa maji katika vyanzo vya maji na mitandao ya kusambaza maji mijini na vijijini kwa lengo la kutoa maamuzi juu ya matumizi yaliyokusudiwa.
  2. Mheshimiwa Spika, ufuatiliaji na utafiti wa ubora wa maji uliofanyika katika vyanzo vya maji nchini unaonesha hali ya ubora wa maji kutofautiana kutoka eneo moja hadi jingine. Utofauti huo unatokana na hali ya miamba ya asili, shughuli za kibinadamu, jiografia ya eneo na mabadiliko ya tabianchi. Ufuatiliaji na utafiti huo umebaini uwepo wa chumvichumvi katika mikoa ya ukanda wa pwani; madini ya fluoride mikoa ya kaskazini; chuma na manganese katika mikoa ya kusini; na kuwepo kwa vimelea vya vijidudu na tope kwenye maji katika baadhi ya maeneo ya nchi. Pamoja na changamoto hizo, mwenendo wa ubora wa maji nchini unaridhisha na vyanzo hivyo vinaweza kuendelezwa kwa matumizi mbalimbali.  
  3. Mheshimiwa Spika, maji yanayosambazwa kwa jamii kupitia mifumo ya usambazaji maji mijini na vijijini yemeendelea kukidhi viwango vya ubora wa maji ya kunywa vya kitaifa katika maeneo mengi nchini. Hata hivyo, changamoto iliyopo ni uwepo wa madini ya chumvichumvi katika maeneo ya Pwani na Ukanda wa Kati katika mikoa ya Dodoma na Singida; uwepo wa madini ya Fluoride katika maeneo yaliyopo kwenye ukanda unaopitiwa na Bonde la Ufa ikiwemo mikoa ya Arusha, Manyara, Mara, Kilimanjaro, Shinyanga, Singida na Simiyu. Katika kukabiliana na changamoto za ubora wa maji yanayosambazwa, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kuwekeza katika teknolojia mbalimbali za kusafisha na kutibu maji ikiwa ni pamoja na kuweka mitambo ya kisasa ya kupunguza madini na chumvichumvi katika maji ya kunywa. 

2.3  Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya MajiVijijini

18. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi waishio vijijini inafikia zaidi ya asilimia 85 ifikapo mwaka 2025, Serikali imeendelea kujenga, kukarabati, kupanua mitandao ya kusambaza maji pamoja na kuimarisha usimamizi wa huduma ya maji. Hadi mwezi Aprili 2022, upatikanaji wa huduma ya maji vijijini imefikia wastani wa asilimia 74.5 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 72.3 mwezi Machi, 2021. Kiwango hicho kinatokana na kukamilika kwa ujenzi wa miradi mipya, ukarabati na upanuzi wa miradi 303 ambayo imeanza kutoa huduma kwa wananchi wapatao 1,467,107.

2.4  Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Majisafi na Usafi

wa Mazingira Mijini

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuimarisha usimamizi wa huduma ya majisafi ili kuweza kutoa huduma endelevu na ya uhakika. Hadi mwezi Aprili, 2022 hali ya upatikanaji wa huduma ya maji mijini ni wastani wa asilimia 86.5 ikilinganishwa na asilimia 86 ya mwezi Machi 2021. Ongezeko hilo linatokana na kukamilika kwa ujenzi wa miradi 40 iliyohusisha ukarabati, upanuzi na ujenzi wa miradi mipya. Aidha, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji inatarajiwa kuongezeka ifikapo mwezi Desemba 2022 kutokana na miradi mikubwa ya maji inayotarajiwa kukamilika ndani ya kipindi hicho ikiwemo Mradi wa kuboresha huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Arusha; Mradi wa Maji wa Mugango-Kiabakari-Butiama; Mradi wa maji wa Tinde – Shelui; pamoja na miradi inayotekelezwa kwa fedha za UVIKO-19.
  2. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuboresha huduma ya usafi wa mazingira ikiwemo uondoshaji wa majitaka katika maeneo ya mijini. Hadi mwezi Aprili 2022, hali ya uondoshaji wa majitaka umefikia asilimia 13.5. Hali ya huduma imeongezeka kutokana na mtandao wa majitaka kuongezeka kutoka kilometa 954.8 za mwaka 2020/21 hadi kilometa 1,385.8 mwezi Aprili 2022. Vilevile, maunganisho yameongezeka kutoka wateja 53,008 kwa mwaka 2020/21 hadi wateja 53,428 mwezi Aprili 2022.
  3. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha takwimu za hali ya upatikanaji wa huduma ya maji nchini, Wizara imetenga fedha kwa ajili ya kufanya taftishi ya kina ya upatikanaji wa huduma ya maji kulingana na idadi halisi ya watu itakayopatikana kutoka kwenye SENSA inayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti 2022.

3.        UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2021/22

3.1 Upatikanaji wa Fedha

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Fungu 49

–Wizara ya Maji liliidhinishiwa jumla ya Shilingi 680,388,976,000 na kati ya fedha hizo Shilingi 33,758,976,000 zilikuwa ni fedha za matumizi ya kawaida na Shilingi 646,630,000,000 zilikuwa ni fedha za maendeleo. Aidha, wakati bajeti inaendelea kutekelezwa, Wizara ilipata Shilingi 139,354,573,798.37 kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO – 19 ili kuhakikisha wananchi wanapata majisafi, salama na yenye kutosheleza karibu na makazi yao na kuwezesha kupambana na UVIKO-19. Hatua hiyo, imewezesha bajeti ya maendeleo kuongezeka na kuwa 785,984,573,798.37 na jumla ya bajeti yote ya Wizara kwa mwaka 2021/2022 kufikia Shilingi 819,743,549,798.37.

  • Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imepokea jumla ya Shilingi 778,917,042,400.34 sawa na asilimia 95 ya bajeti iliyoidhinishwa. Kati ya fedha zilizopokelewa, Shilingi 743,760,395,570.21 ni za kutekeleza miradi ya maendeleo sawa na asilimia 95 ya bajeti ya fedha za maendeleo. Kwa upande wa fedha za Matumizi ya Kawaida, jumla ya Shilingi 35,156,646,830.13 zilipokelewa sawa na asilimia 104 ya bajeti ya fedha za Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 22,612,420,563.62 ni fedha za mishahara (PE) na Shilingi 12,544,226,266.51 ni fedha za matumizi mengineyo (OC).

3.2 Programu na Miradi Mbalimbali Iliyotekelezwa

katika mwaka 2021/22

24. Mheshimiwa Spika, katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, Wizara imeendelea kutekelezaProgramu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Programme – WSDP). Hali ya utekelezaji wa miradi katika mwaka 2021/22na mafanikio yaliyopatikana katika maeneo ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji;huduma za ubora wa maji; huduma za majisafi vijijini; huduma za usambazaji majisafi na usafi wa mazingira mijini; na utekelezaji wa kazi mbalimbali katika Taasisi zilizo chini ya Wizara na masuala mtambuka ni ifuatavyo:-

3.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji

25. Mheshimwa Spika, usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji nchini unatekelezwa kupitia Bodi za Maji za Mabonde tisa (9) ambazo zimepewa majukumu yakufanya tathmini na ufuatiliaji wa rasilimali hizo; kuhifadhi na kudhibiti uchafuzi wa vyanzo vya maji; kugawa maji kwa sekta mbalimbali kwa kuzingatia mahitaji na kiasi cha maji kilichopo; na kuendeleza rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, kazi zilizotekelezwa ni kama ifuatavyo:-

(i). Tathmini na Ufuatiliaji wa Rasilimali za Maji (a) Ujenzi na Ukarabati wa Vituo vya Kufuatilia Mwenendo wa Rasilimali za Maji

26.  Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi za rasilimali za maji nchini, Wizara imeendelea kujenga na kukarabati vituo vya kufuatilia mwenendo wa rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya vituo 178 kati ya 180 vilivyopangwa vimejengwa na kukarabatiwa katika Mabonde ya Rufiji (22), Wami-Ruvu (13), Pangani (15), Ruvuma (13), Ziwa Nyasa (8), Ziwa Rukwa (13), Ziwa Tanganyika (39), Ziwa Victoria (51) na Bonde la Kati vituo vinne (4). Jitihada hizo zimepelekea uwepo wa jumla ya vituo 1,257 vya kufuatilia mwenendo wa rasilimali za maji vinavyofanya kazi katika maeneo mbalimbali kwenye mabonde ya Pangani vituo (183); Wami-Ruvu (253); Rufiji (232); Ruvuma na Pwani ya Kusini (77); Ziwa Nyasa (70); Bonde la Kati (97); Ziwa Rukwa (97); Ziwa Tanganyika (79) na Ziwa Victoria vituo 169

(b) Ugawaji wa Rasilimali za Maji na Udhibiti wa Migogoro

  • Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji inatekeleza jukumu la kugawa maji kwa sekta zote za kijamii, kiuchumi na mazingira kwa haki, usawa na uwazi kupitia Bodi za Maji za Mabonde. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imetoa vibali vipya 451 na kufanya jumla ya vibali 10,904 vilivyotolewa nchi nzima kwa ajili ya matumizi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini. Uwepo wa vibali hivyo unasaidia katika uratibu na kuwa na takwimu sahihi za matumizi ya maji. Naomba kupitia Bunge lako niwahimize wananchi wote kwa ujumla wanaotaka kuchukua maji kutoka katika vyanzo mbalimbali wafahamu kuwa wanao wajibu wa kisheria wa kuomba vibali vya matumizi ya maji hayo kutoka katika Bodi za Maji za Mabonde.
  • Mheshimiwa Spika, sote tunatambua kuwa maji ni rasilimali muhimu sana kwa ustawi wa jamii, uendelevu wa mazingira na ukuaji wa uchumi. Kutokana na umuhimu huo imekuwepo migogoro ya matumizi ya maji kutokana na upungufu wa maji katika baadhi ya maeneo. Udhibiti na utatuzi wa migogoro hiyo umeendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini kupitia Bodi za Maji za Mabonde kwa kushirikiana na Jumuiya za Watumiaji Maji pamoja na Serikali za Mitaa. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya migogoro 27 ya matumizi ya maji ilijitokeza katika Mabonde ya Pangani (19); Wami-Ruvu (4); Bonde la Kati (1) na Ziwa Tanganyika (3) ambapo migogoro yote inaendelea kutafutiwa ufumbuzi. Vilevile, katika kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji, Wizara imeendelea kutoa elimu kuhusu wajibu wa wananchi katika kufuata Sheria na Kanuni za usimamizi wa Rasilimali za Maji. Elimu hiyo imetolewa kupitia majukwaa ya wadau na maadhimisho ya kitaifa kwa lengo la kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji.

(c) Udhibiti wa Uchimbaji Holela wa Visima

29. Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti uchimbaji holela wa visima, Wizara imeendelea kuratibu na kusajili kampuni za utafiti na uchimbaji wa visima pamoja na kutoa leseni na vibali vya uchimbaji kwa makampuni yanayokidhi vigezo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya leseni 155 zimetolewa na nyingine kuhuishwa ambapo leseni 70 ni za kampuni za uchimbaji; leseni 91 za wataalam wa uchimbaji (Drillers) na leseni 14 za utafiti. Aidha, jumla ya vibali 649 vya kuchimba visima vya maji katika maeneo mbalimbali nchini vimetolewa. Idadi hiyo inafikisha jumla ya vibali 3,889 vya kuchimba visima vilivyotolewa hadi sasa.

(d) Uhifadhi wa Mazingira na Vyanzo vya Maji

  • Mheshimiwa Spika, utunzaji wa vyanzo vya maji ni jukumu letu sote hivyo hatuna budi kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara na wadau wote. Utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji unahusisha utambuzi wa vyanzo; uwekaji wa mipaka na kutangaza maeneo ya vyanzo hivyo katika Gazeti la Serikali kama maeneo tengefu ili yalindwe kisheria. Katika kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya maji, Wizara imeendeleakutambua na kuweka mipaka kwenye vyanzo vya maji; na kuunda Jumuiya za Watumia Majikwa lengo la kuwashirikisha wananchi katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji kwa mujibu wa Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009.
  • Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, vyanzo vya maji 48 vimewekewa mipaka kama hatua ya awali ya uhifadhi katika mabonde ya Pangani (12), Rufiji (12), Ruvuma (4), Ziwa Nyasa (3), Bonde la Kati (1), Ziwa Rukwa (8), Ziwa Tanganyika (4) na Ziwa Victoria vyanzo vinne (4).Idadi hiyo inafikisha jumla ya vyanzo 163 vilivyowekewa mipaka ambapo vyanzo 18 kati ya hivyo vimetangazwa kwenye Gazeti la Serikali ili vilindwe kisheria na vyanzo vya maji 44 vipo katika mchakato wa kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama maeneo tengefu.
  • Mheshimiwa Spika, katika kutimiza azma ya kushirikisha jamii kwenye utunzaji wa vyanzo vya maji na usimamizi endelevu wa matumizi ya maji, Wizara imeendelea kuunda Jumuiya za Watumia Maji (Water Users’ Associations – WUAs) katika maeneo ya vyanzo vya maji ili kuhakikisha vyanzo hivyo vinatunzwa na maji yanatumika kwa uwiano mzuri. Hadi mwezi Aprili 2022, Jumuiya 14 za Watumia Maji zimeundwa katika mabonde ya Pangani (2), Rufiji (1), Ruvuma (3), Ziwa Nyasa (1), Ziwa Rukwa (2), Ziwa Tanganyika (3) na Ziwa Victoria (2) na kufanya jumla ya Jumuiya za Watumia Maji zilizoundwa kufikia 164.

(e) Udhibiti wa Uchafuzi wa Vyanzo vya Maji

33. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kudhibitiuchafuzi wa vyanzo vya maji kwa kutoa vibali vya kutiririsha majitaka na kusimamia viwango vya majitaka yanayotiririshwa katika vyanzo. Hadi mwezi Aprili 2022, vibali 36 vya kutiririsha majitaka vimetolewa katika Bodi za Maji za Bonde ya Ziwa Victoria vibali 11 na Wami-Ruvu vibali 25. Idadi hiyo inafikisha jumla ya vibali 152 vilivyotolewa hadi sasa katika mabonde yote.

(f) Mradi wa Kunusuru Vyanzo vya Maji kupitia Mpango Endelevu wa Matumizi Bora ya Ardhi katika Mabonde Madogo ya Mito ya Zigi na Ruvu.

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha mradi wa kunusuru vyanzo vya maji katika mabonde madogo ya Mto Zigi (Bonde la Pangani) na Mto Ruvu (Bonde la Wami-Ruvu)mwezi Desemba 2021. Lengo la mradi huo lilikuwa ni kuanzisha na kuwezesha utekelezaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi katika mabonde hayo ili kuzuia uchafuzi na uharibifu wa vyanzo vya maji. Katika mwaka 2021/22, kazi zilizotekelezwa ni pamoja na kujenga jengo moja kwa ajili ya kuweka mashine ya kuchakata viungo vya mboga katika Kijiji cha Zirai kilichopo Wilaya ya Muheza; kuandaa warsha iliyohusisha wadau wote wa kidakio cha Mto Ruvu kwa lengo la kujadiliana kwa pamoja, kutoa ushauri, kutoa utaalam pamoja na rasilimali fedha ili kunusuru vyanzo vya maji katika kidakio hicho; kuunganisha vikundi vinne (4) vya ujasiriamali (ZIMISA AMCOSS, TULO STRAWBERRY, UWAMAKIZI NA BWAWA LA SAMAKI LA MBARANGWE) na benki ya kilimo (TADB) na wafadhili wengine kwa ajili ya kupata mikopo na fursa nyingine kama vile mafunzo ili kuendeleza shughuli zao kwa lengo la kulinda vyanzo vya maji
  • Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huo umeleta manufaa makubwa katika vyanzo vya mito ya Zigi na Ruvu ikiwa ni pamoja na kupungua kwa uharibifu na uchafuzi wa vyanzo hivyo ambapo wananchi walioondolewa wamewezeshwa kufanya shughuli mbadala za kiuchumi; kuimarisha ushirikiano wa taasisi mbalimbali katika utunzaji wa vyanzo vya maji; kuongezeka kwa upatikanaji wa maji kwa wananchi kupitia miradi ya maji iliyojengwa na mradi; na kuongezeka kwa elimu katika jamii ikiwemo ya usimamizi wa rasilimali za maji na elimu ya ujasiriamali.

(ii). Uendelezaji wa Rasilimali za Maji a) Utafutaji wa Vyanzo Vipya vya Maji

  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi waishio mijini na vijijini wanapata huduma endelevu ya maji, Wizara imeendelea na utafutaji wa vyanzo vipya vya maji katika maeneo mbalimbali nchini ili kuvihifadhi na kuviendeleza viweze kutoa huduma. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya vyanzo vipya 535 vya maji vimebainishwa vikihusisha mito, vijito, chemichemi, mabwawa, ardhi oevu na maji ya ardhini katika Mabonde ya Pangani (189); Rufiji (26); Ruvuma na Pwani ya Kusini (22); Ziwa Nyasa (5); Bonde la Kati (22); Ziwa Rukwa (265) na Ziwa Tanganyika vyanzo sita (6). Idadi hiyo inafikisha jumla ya vyanzo vya maji 2,091 vilivyotambuliwa hadi sasa katika maeneo mbalimbali nchini. Vyanzo vinavyotambuliwa na kubainika kuwa vinafaa vitaendelezwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali. 
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha ukarabati wa bwawa la Mwadila lililopo Wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu. Vilevile, Wizara imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa mabwawa 16 ya Ng’walukwa, Kiloleli na Ngofila (Kishapu); Muko na Chiwanda (Momba); Zebeya na Ilambambasa (Maswa); Iseni, Mwabayanda na

Nyang’hanga (Magu); Manda (Chamwino); Dongo (Kiteto); Mtamba (Mpwapwa);Itamboleo (Mbarali); Nyange (Ifakara); pamoja na Horohoro (Mkinga). Ujenzi na ukarabati wa mabwawa hayo utagharimu kiasi cha Shilingi bilioni 13.89. Vilevile, usanifu wa malambo (Charco dams) sita (6) umekamilika katika mwambao wa barabara kuu ya DodomaBabati ikihusiha Wilaya za Bahi mawili (2) na Chemba manne (4) na tayari Wizara imeshapokea fedha kiasi cha Shilingi bilioni 1.21 kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa hayo.

b) Ujenzi na Ukarabati wa Mabwawa

38. Mheshimiwa Spika, uwezo wa nchi yetu kuhifadhi maji kwa sasa katika mabwawa yaliyopo ni mita za ujazo bilioni 5.4 tu sawa na asilimia 5.2 ya maji juu ya ardhi yanayopatikana kwa mwaka. Kwa kuzingatia umuhimu wa kujenga miundombinu mikubwa ya kuhifadhi maji kwa ajili ya usalama wa maji, Serikali imeendelea na mpango wa ujenzi wa miradi ya mabwawa ya Lugoda/Ndembera (Iringa), Songwe (Mbeya) na Bwawa la Dongo (Manyara). Vilevile, Wizara imeendelea na ujenzi wa mabwawa 8 katika vijiji vya Nsenkwa (Mlele), Mihingo (Bunda), Chole (Kisarawe), Chamwino (Chamwino), Kwamjembe (Bagamoyo), Kwenkambala (Handeni),

Kalemasha (Kalambo) na Mbuta (Mkinga). Ujenzi wa mabwawa hayo upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Aidha,Wizara imekamilisha usanifu wa kina mabwawa 12 katika Vijiji vya Itaswi – Kisaki (Kondoa), Kwamsanja (Chalinze), Kalemela

(Urambo), Mkonde (Kilindi), Msente (Kilindi), Lombouti (Kilindi), Ichemba (Kaliua), Izimbili (Kaliua), Ingwisi (Kaliua), Gendagenda (Handeni), Msomera (Handeni) na Kang’ata (Handeni). Taratibu za kuwapata wakandarasi wa ujenzi zinaendelea.

c)  Uanzishwaji wa Majukwaa ya Wadau wa Maji

39. Mheshimiwa Spika, ushirikishwaji wa wadau katika usimamizi wa rasilimali za maji ni muhimu ili kuhakikisha matumizi bora na endelevu ya rasilimali za maji. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imefanikiwa kuendesha majukwaa nane (8) ya wadau katika mabonde nane. Uanzishwaji wa majukwaa hayo umefanikisha utoaji wa ushauri mbalimbali; umeongeza upatikanaji wa fedha na mwamko wa wadau juu ya usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji.

(iii). Usimamizi wa Rasilimali za Majishirikishi

  • Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina vyanzo vya majishirikishi 14 ambavyo ni Maziwa ya Victoria, Tanganyika, Nyasa, Natron, Chala na Jipe pamoja na Mito ya Kagera, Mara, Malagarasi, Momba, Mwiruzi, Umba, Ruvuma na Songwe. Idadi hiyo inaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye vyanzo vingi vya maji vinavyovuka mipaka ya nchi Barani Afrika. Usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji katika vyanzo vya majishirikishi unahusisha ushirikiano na nchi wanachama ambazo ni Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Uganda, Malawi, Msumbiji na Zambia. Nchi nyingine tunazoshirikiana nazo ni Angola, Botswana, Ethiopia, Misri, Namibia, Sudan, Sudan Kusini, Zimbabwe na Eritrea.
  • Mheshimiwa Spika, misingi ya ushirikiano katika rasilimali za majishirikishi ni Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1992 kuhusu uhifadhi na matumizi ya majishirikishi na maziwa makuu (The 1992 United Nations Economic

Commission for Europe Convention on the Protection and Use of Transboundary Watercourses); pamoja na Mkataba wa

Umoja wa Mataifa wa mwaka 1997 kuhusu Matumizi ya

Majishirikishi katika shughuli zisizo za usafirishaji (The 1997 UN Convention on the Law of the Non-Navigational Uses of International Watercourses) ambapo Tanzania inatekeleza mikataba hiyo.Utekelezaji wa mikataba mbalimbali ya usimamizi wa rasilimali za majishirikishi pamoja na Taasisi za Kikanda na Kimataifa zilizoanzishwa kwa ajili ya kusimamia ushirikiano huo ni kama ifuatavyo:- 

(a) Mikataba ya Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi wa Majishirikishi

42. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Tanzania imeshiriki katika Mkutano wa Tisa wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa uliohusu Mkataba wa Usimamizi na matumizi ya Majishirikishi ya Maziwa Makuu uliofanyika tarehe 29 Septemba – 01 Oktoba 2021. Katika Mkutano huo, Tanzania imewasilisha mchango wake katika kuchangia amani ya dunia kupitia ushirikiano katika usimamizi wa majishirikishi, ulinzi wa maslahi ya Taifa katika matumizi ya maji kutoka katika vyanzo vya majishirikishi; na utekelezaji wa kiashiria namba 6.5.2 (Transboundary Water Cooperation) cha Lengo namba 6 la Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDG 6 – Water and Sanitation for All).  Aidha, Tanzania inashiriki katika utekelezaji wa Programu ya Mkataba huo katika kipindi cha mwaka 20222024 kwa manufaa ya Taifa; pamoja na Tanzania kuzishawishi nchi nyingine inazoshirikiana nazo kuandaa mipango ya pamoja ya matumizi ya maji katika vyanzo vya majishirikishi kama vile Bonde la Mto Mara. 

(b) Taasisi ya Mpito ya Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative – NBI)

  • Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Mpito ya Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative – NBI) ni ushirikiano baina ya nchi 11 za Bonde la Mto Nile ambazo ni Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Misri, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Sudan, Uganda pamoja na Eritrea ambayo ni mtazamaji (observer). Kupitia Taasisi hiyo, unatekelezwa Mradi wa Nile Basin Regional Hydromet System wenye lengo la kuimarisha mtandao wa kufuatilia mwenendo wa hali ya rasilimali za maji katika vyanzo kwa kukusanya takwimu. Kwa upande wa Tanzania, mradi huo utajenga vituo vinane (8) vya kisasa vya kukusanya takwimu za mtiririko wa maji katika mito mikubwa ya Mara, Kagera, Simiyu na Rusumo iliyopo katika Bonde la Ziwa Victoria. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa vituo hivyo zimekamilika. Ujenzi wa vituo hivyo unatarajiwa kuanza katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023.
  • Mheshimiwa Spika, vilevile, Taasisi ya NBI kwa kushirikiana na nchi wanachama inafanya utafiti wa Kimkakati wa Rasilimali za Maji (Strategic Water Resources Analysis – SWRA). Utafiti huo unalenga kutoa ushauri kuhusu namna ya kukidhi mahitaji ya maji yanayoendelea kuongezeka; na uendelevu wa usalama wa chakula na nishati kwa nchi za ukanda wa juu na ukanda wa chini wa Bonde la Mto Nile. Aidha, maandalizi ya Mpango wa Usimamizi wa Bonde la Mto

Nile unaolenga kutoa mwongozo katika upangaji na utekelezaji wa shughuli za usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji kwa ngazi ya kitaifa na kikanda yanaendelea. Kazi hiyo inafanywa na Wataalam wa Sekretarieti ya NBI kwa kushirikiana na Wataalam wa Nchi Wanachama ambapo kwa sasa ipo katika hatua za awali za ukusanyaji wa taarifa mbalimbali.

  • Mheshimiwa Spika, mwaka 2006 Baraza la Mawaziri wa Maji wa Nchi za Bonde la Mto Nile liliazimia kuwa tarehe 22 Februari ya kila mwaka kuwa ni siku ya kumbukumbu ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo ambaponchi wanachama zitakuwa zinaadhimisha Siku ya Bonde la Mto Nile kikanda na kitaifa. Lengo ni kuhamasisha matumizi endelevu ya rasilimali za maji za Bonde la Mto Nile. Maadhimisho ya 16 ya Bonde la Mto Nile yalifanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Februari, 2022 na Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wadau wapatao 1,500 kutoka nchi wanachama wa Bonde la Mto Nile. Aidha, katika maadhimisho hayo Tanzania imeziomba nchi nyingine wanachama kubeba agenda ya kuanzisha Kamisheni ya Bonde la Mto Nile kama agenda kuu katika ushirikiano wa Bonde la Mto Nile ili kuimarisha usimamizi endelevu, matumizi ya usawa na uendelezaji wa rasilimali za maji ya Bonde la Mto Nile. Vilevile, Tanzania iliomba kuongezwa kwa lugha ya Kiswahili kama lugha ya mawasiliano katika shughuli za Bonde la Mto Nile sanjari na lugha za Kifaransa na Kiingereza.

(b) Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe

46. Mheshimiwa Spika, Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe ilianzishwa na Serikali za Tanzania na Malawi kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Bonde la

Mto Songwe (Songwe River Basin Development Program).

Programu hiyo ina lengo la kukabiliana na mafuriko ya mara kwa mara yanayosababisha kuhamahama kwa Mto Songwe kupitia ujenzi wa mabwawa ambayo pia yatatumika kwa ajili ya kuzalisha umeme wa megawati 180, kilimo cha umwagiliaji hekta 6,200 usambazaji maji pamoja na uvuvi. Vilevile, programu hii inahusisha Miradi midogo ya kijamii kama vile shule, barabara na hospitali. Hadi mwezi Aprili 2022, shughuli zifuatazo zimefanyika: kutekeleza Mradi wa Uhifadhi wa

Mazingira ya Bonde la Mto Songwe kwa kupanda miti 1,000,000 katika Wilaya ya Ileje; kuandaa Mkakati wa Jinsia katika Usimamizi wa Rasilimali za Maji 2022-2027; na kuandaa Mpango wa Kukabiliana na Mafuriko katika vijiji vya Njisi, Kabanga, Ndwanga, Mpunguti na Katumba Songwe wilyani Kyela. Vilevile, Wizara imeshiriki katika Mkutano wa kwanza wa Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe uliofanyika Lilongwe – Malawi tarehe 9 Machi, 2022 ambao uliadhimia kuwa mradi wa umeme kuwa kipaumbele kwa mataifa yote mawili na kuweka mikakati ya kutafuta fedha kiasi cha Dola za Marekani Milioni 577 kwa ajili ya ujenzi wa bwawa na mtambo wa kuzalisha umeme. 

(c) Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi

47. Mheshimiwa Spika, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoko ndani ya Bonde la Mto Zambezi kupitia ukanda wa Bonde la Ziwa Nyasa. Nchi nyingine ni Angola, Botswana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Zambia pamoja na Zimbabwe. Kwa sasa Sekretariati ya Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission – ZAMCOM) inatekeleza Mpango Mkakati wa Miaka 22 kuanzia 2018-2040. Kupitia Mpango Mkakati huo, Sekretarieti ya ZAMCOM kwa kushirikiana na nchi wanachama inaandaa Programu ya

Mabadiliko ya Tabianchi 2022-2026 (The Programme for Integrated Development and Adaptation to Climate Change in the Zambezi Watercourse 2022-2026). Mradi huo utahusisha uwekezaji kwenye masuala mtambuka ambapo fedha za utekelezaji zinategemewa kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Mfuko wa Mazingira (Global Environmental Facility– GEF) pamoja na Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund – GCF). Miradi ya Tanzania inayotegemewa kujumuishwa katika mradi huo ni pamoja na Programu ya Kuendeleza Bonde la Mto Songwe yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 829 inayohusisha Sekta za Maji, Kilimo, Nishati pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. 

(c) Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)

48. Mheshimiwa Spika, Tanzania pamoja na nchi nyingine 15 ambazo ni Angola, Botswana, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Eswatini, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Seychelles, Afrika Kusini, Zambia na Zimbabwezinaunda Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern African Development Community – SADC). Hadi mwezi Aprili 2022, Tanzania imeshiriki katika Mkutano wa 40 wa Baraza la Mawaziri wa Maji na Nishati wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ulifanyika Mjini Blantyre nchini Malawi tarehe 02 Desemba, 2021. Mkutano huo ulipitisha Mpango Mkakati wa Kikanda wa Usimamizi Shirikishi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji Awamu ya Tano (Regional Strategic Action Plan on Integrated Water Resources Development and Management Phase V 2021-2025). Kupitia Mpango Mkakati huo, Tanzania inategemea kunufaika na ujenzi wa miradi ya maji katika maeneo ya mipakani (Border Post Water, Sanitation and Hygiene Response Project); miradi ya maji ya Kasumulu-Songwe kati ya Tanzania na Malawi pamoja na Nakonde-Tunduma kati ya Tanzania na Zambia.

Lengo la miradi hiyo ni kuendeleza mipango ya nchi wanachama ya kuboresha huduma za maji katika maeneo ya mipaka na yenye msongamano pamoja na kuendeleza jitihada za kukabiliana na UVIKO-19

(d) Baraza la Mawaziri wa Maji wa Afrika  

  • Mheshimiwa Spika, Tanzania ni mwanachama wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Afrika (African Ministers’ Council on Water – AMCOW) lenye jukumu la kushughulikia masuala ya usimamizi wa maji na usafi wa mazingira katika nchi za Afrika. Katika kipindi cha mwaka 2021/22, Tanzania imeshiriki katika mkutano wa Kamati Tendaji ya Mawaziri wa Maji uliofanyika kwa njia ya mtandao mwezi Desemba, 2021. Mkutano huo uliidhinisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za AMCOW na kupitisha Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira unaosimamiwa na AMCOW. Mwongozo huo utazisaidia nchi za Afrika ikiwemo Tanzania kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 hususan lengo namba 6. Vilevile, kupitia kupitishwa kwa Mwongozo wa Usafi wa Mazingira wa Afrika (The African Sanitation Policy Guidelines) ambao unalenga kuzisaidia nchi za Afrika kuandaa Sera za Usafi wa Mazingira (Sanitation Policies) au kuboresha huduma ya usafi wa mazingira, Tanzania imewasilisha ombi la kupata msaada huo kutoka AMCOW kwa ajili ya kuboresha huduma za usafi wa mazingira nchini.
  • Mheshimiwa Spika, Vilevile Tanzania imeshiriki katika Kongamano la 9 la Jukwaa la Maji Duniani (9th World Water Forum 2022) ambalo liko chini ya Baraza la Maji Duniani (World Water Council) lililofanyika tarehe 21-26 Machi 2022

Mjini Dakar – Senegal. Katika Kongamano hilo, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Global Water Parnership Southern Africa wamechaguliwa kuwa katika Jopo la Ngazi ya Juu la Kimataifa linaloshughulikia uwekezaji katika Sekta ya Maji Afrika (International High Level Panel on Water Investments in Africa).

 (e) Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria

  • Mheshimiwa Spika, Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria imeendelea kutekeleza Programu na miradi mbalimbali ikiwemo Programu ya pamoja ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji katika Bonde la Ziwa Victoria inayogharimu takribani Shilingi bilioni 83.7. Fedha hizo ni msaada uliotolewana Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya.Vilevile, Kamisheni inatekeleza Mradi wa Kikanda wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi katika Bonde la Ziwa Victoria kwa ushirikiano na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) kwa gharama ya takriban Shilingi bilioni 11.675. Hadi mwezi Aprili 2022, rasimu ya Mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria imeandaliwa kwa ajili ya kukarabati na kupanua mtandao wa majitaka wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA). Hatua hiyo itawezesha kuunganisha wateja wapya 1,600 katika mtandao wa majitaka Jijini Mwanza. Aidha, kupitia Mradi wa Kikanda wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi visima vitatu (3) vipya vyenye uwezo wa kuzalisha maji mita za ujazo 4.7, 6.4 na 8.5 vimechimbwa pamoja na kufanya ukarabati kwenye kisima kimoja katika Kijiji cha Ng’haya Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo kuendeleza shughuli za kilimo cha umwagiliaji wa mboga mboga. Kazi yakufunga pampu zinazoendeshwa kwa mfumo wa nishati ya jua kwenye visima hivyo inaendelea. Vilevile, kupitia mradi huo, mizinga ya nyuki 149 imegawiwa kwa vikundi viwili katika Kijiji cha Ng’haya ili kuwezesha wananchi kujipatia kipato kutokana na shughuli za urinaji wa asali. 
  • Mheshimiwa Spika, kupitia Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, nchi wanachama zimeandaa rasimu ya Sera ya Maji ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na mkakati wake wa utekelezaji kwa kipindi cha miaka 10 (2022 – 2032). Sera na mkakati huo utasaidia kutoa mwongozo katika utekelezaji wa programu za maji. Vilevile, Kamisheni kwa kushirikiana na nchi wanachama imeandaa rasimu ya Mkakati wa nne (4) wa Kamisheni kwa kipindi cha 2021/22 – 2025/26. Rasimu ya Mkakati huo imeainisha vipaumbele katika kuendeleza usimamizi wa mazingira; usimamizi shirikishi wa rasilimali za maji; usimamizi wa afya ya jamii; uendelezaji wa jamii kiuchumi; na usimamizi wa shughuli za usafiri majini. Rasimu hiyo itawasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Kisekta la Kamisheni Bonde la Ziwa Victoria linalotarajiwa kukutana mwezi Mei 2022 kwa ajili ya kupitishwa.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeshiriki katika maadhimisho ya 10 ya siku ya Bonde la Mto Mara yaliyofanyika tarehe 15 Septemba, 2021 katika Wilaya ya Tarime, Mkoa wa Mara. Siku ya Bonde la Mto Mara huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha na kuelimisha wananchi waishio ndani ya Bonde la Mto Mara kuhusu utunzaji na uhifadhi wa Bonde hilo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya miti 16,000 ambayo ni rafiki kwa mazingira ilipandwa. Sambamba na zoezi la upandaji miti, kulikuwa na zoezi la uwekaji wa  nguzo za alama (beacon) katika kijiji cha Murito ili kulinda eneo la umbali wa mita 60 kutoka kwenye kingo za Mto Mara kama Sheria ya Mazingira Na. 4 ya mwaka 2004 na Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimaji za Maji ya mwaka 2009 zinavyoelekeza. Jumla ya nguzo za alama 70 zilisimikwa katika umbali wa mita 100 kutoka nguzo moja hadi nyingine.

(f)        Taasisi ya Global Water Partnership

54. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Global Water Partnership (GWP) imeundwa na nchi washirika 179 zilizogawanywa katika kanda 13 ikiwemo kanda ya nchi za kusini mwa Afrika (Global Water Partnership Southern Africa – GWPSA). Lengo la Taasisi hiyo ni kujenga uwezo wa nchi washirika katika kuboresha usimamizi wa rasilimali za maji katika ngazi za kimataifa, kikanda, kitaifa na ngazi ya jamii. Katika kutekeleza agenda ya kuongeza uwekezaji katika Sekta ya Maji Barani Afrika (African Water Investment Programme-AIP), Tanzania inaendelea kushirikiana na GWPSA pamoja na Global Water Partnership – Tanzania katika kupata Dola za Kimarekani bilioni 30 kila mwaka ili kufikia Lengo Namba 6 la Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa 2015-2030 linalohusu Maji na Usafi wa Mazingira kwa wote. Katika jitihada za kupata fedha hizo, Wizara ya Maji imewasilisha maandiko ya miradi mbalimbali ya kimkakati ili kupata fedha kupitia agenda hiyo. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na GWP Tanzania imeandaa Mpango Mkakati wa Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Maji katika Bodi ya Maji Bonde la Wami-Ruvu. 

(iv). Kujenga Uwezo wa Taasisi zinazosimamia Rasilimali za Maji

55. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi wa Kusaidia Sekta ya Maji Awamu ya Pili (Water Sector Support Project –

WSSP II) inaendelea kuzijengea uwezo Taasisi zinazosimamia rasilimali za maji kwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji takwimu za mwenendo wa maji katika mabonde yote tisa nchini, utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji, ununuzi wa vitendea kazi na kujenga uwezo kwa wataalam. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imekamilsha uandaaji wa mipango ya utunzaji wa vidakio kwenye mabonde yote tisa nchini; ununuzi wa magari 28, pikipiki 100, baiskeli 100, vifaa vya usalama kwa ajili ya wasoma takwimu na vifaa vya ofisi kwa ajili jumuiya za watumia maji. Vilevile, Wizara inaendelea na taftishi ya kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa takwimu ili kuweza kupata takwimu kwa wakati (real time data); taftishi ya kuandaa mfumo wa kutoa taarifa za viashiria vya mafuriko (flood early warning system); na taftishi ya kutambua maeneo yenye maji chini ardhi pamoja na kuandaa ramani ya maji chini ya ardhi. 

3.2.2 Huduma za Ubora wa Maji

  • Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Maabara za Ubora wa Maji imeendelea kusimamia na kufuatilia ubora wa maji katika mifumo ya usambazaji maji kwa matumizi ya majumbani, maji katika vyanzo na maji kwa matumizi mengine ikiwa ni pamoja na viwanda, umwagiliaji, ujenzi, utafiti na ufugaji wa samaki. Aidha, Wizara imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira kwa lengo la kudhibiti uchafuzi wa mazingira na vyanzo vya maji.  
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ilipanga kukusanya sampuli 15,000 kwa ajili ya kubaini mwenendo wa ubora wa maji katika vyanzo; na ubora wa maji kwa ajili ya matumizi ya majumbani, viwandani, umwagiliaji, ujenzi na utafiti. Kwa upande wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira Wizara ilipanga kukusanya na kuhakiki sampuli 2000. Utekelezaji wa mipango hiyo ni kama ifuatavyo:-

(i).         Ubora wa Maji Katika Vyanzo 

58. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufuatilia mwenendo wa ubora wa maji katika vyanzo ambapo hadi mwezi Aprili 2022, sampuli 607 kutoka katika vyanzo vya maji 63 vya kimkakati zilikusanywa na kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara kwa ajili ya afya ya ikolojia. Matokeo ya uchunguzi yanaonesha kuwa ubora wa maji wa vyanzo hivyo  ni wa kuridhisha katika kulinda ikolojia na vyanzo vinaweza kuendelea kutumika au kuendelezwa kwa matumizi yaliyokusudiwa. 

(ii).        Ubora wa Maji kwa Matumizi ya Majumbani 

  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhakikisha maji yanayosambazwa kwa jamii yanakidhi viwango kwa kufuatilia ubora wa maji katika skimu za usambazaji maji mijini na vijijini; taasisi binafsi pamoja na vyanzo vya maji vinavyomilikiwa na watu binafsi kwa lengo la kulinda afya ya jamii. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya sampuli za maji 6,979 zimekusanywa na kuhakikiwa ubora wake kwa kulinganishwa na viwango vya ubora wa maji ya kunywa vya kitaifa ambapo, sampuli 5,932 sawa na asilimia asilimia 85 zilikidhi viwango na sampuli 1,047 sawa na asilimia 15 hazikukidhi viwango. Aidha, baadhi ya sampuli hazikukidhi viwango vya ubora wa maji kutokanana uwepo wa viwango vikubwa vya madini ya Fluoride katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Mwanza, Kilimanjaro, Manyara na Singida; Turbidity katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani na Mara; madini ya chuma katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Geita, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na  Mwanzamadini ya Manganese katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mtwara, Lindi na Morogoro; chumvichumvi katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mtwara na Lindi; Color katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Mara, na Mwanza. Acidity katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Lindi, Mtwara na Ruvuma. Vilevile kiwango kidogo cha dawa ya Chlorine kilionekana katika maeneo ya Mbogwe, Sengerema na Buchosa. Katika kukabiliana na changamoto hizo ushauri wa kitaalam ikiwa ni pamoja na njia sahihi za kusafisha na kutibu maji ulitolewa kwa wasambazaji wa maji mijini na vijijini. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha maji yanayomfikia mtumiaji yanaendelea kuwa na ubora unaotakiwa, Wizara imeendelea kufuatilia utekelezaji pamoja na  kuzijengea uwezo Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira katika kuandaa na kutekeleza Mipango ya Usalama wa Maji inayohusisha Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Resilient Water Safety Plans –CR WSPs). Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imeweza kutoa mafunzo kwa Wataalam 16 ambao watatumika katika kuongeza kasi ya uwezeshaji wa uandaaji wa mipango ya usalama wa maji kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na  Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs). 

(iii). Ubora wa Maji kwa Matumizi Mengine

61. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhakiki na kufuatilia ubora wa maji yanayotumika katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwa ni pamoja na shughuli za viwandani, ujenzi, umwagiliaji na utafiti ili kuhakikisha maji hayo yanakidhi viwango vya ubora vinavyokubalika kwa matumizi yaliyokusudiwa. Hadi mwezi Aprili, 2022 jumla ya sampuli 366 zilikusanywa na kuhakikiwa ubora wake kwa ajili ya matumizi ya viwandani sampuli 182, ujenzi (38), umwagiliaji (14) na sampuli (132) kwa jili ya shuguli za utafiti. Matokeo yalionesha asilimia 98.2 ya sampuli zilikidhi viwango kwa matumizi yaliyokusudiwa na asilimia 1.8 ya sampuli hazikukidhi viwango kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha chumvichumvi katika maji.

(iv). Ubora wa Madawa ya Kusafisha na Kutibu Maji

62. Mheshimiwa Spika, katika kutimiza lengo la usambazaji wa majisafi na salama ni muhimu kuhakikisha madawa yanayotumika yanakidhi viwango vya ubora na yanakuwa na ufanisi katika kusafisha na kutibu maji. Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imehakiki ubora wa madawa ya kusafisha maji aina ya Aluminium Sulphate (Shabu), Poly Aluminum Sulphate na Algae Floc 195-1. Kwa upande wa madawa ya kutibu maji ya kunywa, dawa aina ya Calcium Hypochlorite ilihakikiwa ubora wake kabla ya matumizi. Matokeo ya uchunguzi yalionesha madawa hayo yanakidhi viwango vinavyokubalika kwa ajili ya kusafisha na kutibu maji. 

(v). Ubora wa Majitaka Yanayorudishwa Kwenye Mazingira

63. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufuatilia na kuhakiki ubora wa majitaka yanayorudishwa kwenye mazingira kutoka majumbani, viwandani na katika taasisi kwa lengo la udhibiti wa uchafuzi wa vyanzo vya maji na mazingira. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya sampuli 256 zilikusanywa kutoka kwenye mabwawa ya kusafisha majitaka katika Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na viwanda mbalimbali.Matokeo yalionesha asilimia 46 ya sampuli za majitaka zilikidhi viwango vya     kurudishwa      kwenye    mazingira.        Sampuli      ambazo hazikukidhi viwango ni kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha organic matter kinachosababisha kupungua kwa hewa ya oxygen. Aidha, Mamlaka za Maji pamoja na viwanda ambavyo majitaka yake hayakukidhi viwango, ushauri wa kitaalam ulitolewa ili kuongeza ufanisi wa mifumo ya kusafisha na kutibu majitaka.

(vi).       Mkakati wa Uondoaji wa Madini ya Fluoride katika Maji ya Kunywa 

64. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha usalama wa maji yanayosambazwa kwa jamii Wizara imeendelea kutekeleza Mkakati wa Uondoaji wa Madini ya Fluoride kwenye maji ya kunywa na kupikia katika mikoa iliyoathirika zaidi na madini hayo (Fluoride belt).  Katika mwaka 2021/22, Wizara imejenga mitambo miwili (2) ya ngazi ya jamii ya kuondoa madini ya Fluoride kwenye maji katika kijiji cha Loiborsoit Wilaya ya Simanjiro, Mkoani Manyara. Aidha, Wizara imeendela kufuatilia ufanisi wa mitambo ya kupunguza madini ya Fluoride katika maji ya kunywa ambapo hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya mitambo 438 ngazi ya kaya ilikaguliwa na kati ya hiyo mitambo 221 ilibainika kufanya kazi kwa ufanisi na mitambo 217 ilionekana kuhitaji kubadilishwa chengachenga za mifupa ya ng’ombe. Kwa upande wa mitambo ya ngazi ya jamii, mitambo tisa (9) ilikaguliwa ambapo mitambo saba (7) ilibainika kufanya kazi kwa ufanisi na miwili (2) inahitaji kubadilishwa chengachenga za mifupa. Vilevile, Wizara imeendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya kiwango kikubwa cha madini ya Fluoride katika maji ya kunywa na matumizi sahihi ya teknolojia ya kuondoa madini hayo kupitia vyombo vya habari, mikutano na makongamano mbalimbali.

(vii). Uimarishaji wa Maabara za Maji Nchini

  • Mheshimiwa Spika, katika kuongeza wigo na kusogeza huduma za ubora wa maji kwa wananchi, Serikali kwa kushirikina na Shirika la OIKOS imefanikiwa kuanzisha maabara mpya ya ubora wa maji katika mkoa wa Manyara. Kuanzishwa kwa maabara hiyo kunaifanya Wizara ya Maji kufikisha jumla ya Maabara 17 za ubora wa maji nchini. 
  • Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali za kuboresha huduma za ubora wa maji nchini, Wizara imeendelea kuimarisha Maabara za Ubora wa maji kwa kuzijengea uwezo ikiwa ni pamoja na kuwa na ithibati (accreditation). Hadi mwezi Aprili 2022, Wizara imeanza mchakato wa kuongeza idadi ya Maabara zenye ithibati kutoka saba (7) za sasa (Dar es Salaam, Singida, Shinyanga Mwanza, Musoma, Kigoma na Bukoba) hadi kufikia 11 kwa kuzipatia ithibati maabara za Morogoro, Mtwara, Iringa na Sumbawanga. Lengo ni kuboresha utoaji wa takwimu za ubora wa maji zinazotumika kutoa maamuzi kuhusu usimamizi na matumizi ya maji. Aidha, katika kuhakikisha maabara zinafanya uchunguzi wa viashiria kwa usahihi, Maabara 16 za ubora wa maji nchini zilishiriki kwenye zoezi la kujipima uwezo wa utendaji  kazi za kimaabara linaloratibiwa na Shirika la SADCMET. Matokeo ya zoezi hilo yameimarishamaabara zetu katika kufanya uchunguzi wa vimelea vya vijidudu (bacteria) na viashiria vya kikemikali na maumbo.
  • Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha utendaji kazi katika maabara za maji nchini kwa kuweka mfumo wa kielektroniki wa kuendesha kazi zote za maabara (Laboratory Information Management System – LIMS). Hadi mwezi Aprili 2022, mfumo umewekwa katika maabara za Mwanza, Musoma, Kigoma na Dar es salaam ambapo wataalam kutoka maabara hizo wameendelea kupatiwa mafunzo ya matumizi ya mfumo huo. Aidha, Wizara imeendelea kuziwezesha Maabara za Ubora wa Maji kwa kuzipatia vifaa mbalimbali vya kisasa vinavyotumika kufanya uchunguzi wa Ubora wa Maji. 
  • Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kutoa wito kwa wadau wote kutambua umuhimu wa kupima ubora wa maji kabla ya kuyatumia kwa matumizi mbalimbali ikiwa ni pamoja na  matumizi ya majumbani, viwanda, ujenzi, umwagiliaji na utafiti. Aidha, viwanda na taasisi nyingine zinazotiririsha majitaka zihakikishe maji hayo yanatibiwa na kufikia viwango vinavyokubalika kabla ya kutiririshwa kwenye mazingira. Huduma za upimaji na ufuatiliaji wa ubora wa maji na majitaka zinatolewa na Wizara kupitia  Maabara 17 za Ubora wa Maji zilizopo katika mikoa mbalimbali nchini.

3.2.3 Huduma za Usambazaji Majisafi na Usafi wa

Mazingira Vijijini

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ilipanga kutekeleza jumla ya miradi 1,527 ya maji na usafi wa mazingira vijijini. Kati ya miradi hiyo, miradi 1,176 inahusisha kukamilisha miradi iliyokuwa inaendelea, ujenzi wa miradi mipya, upanuzi na ukarabati wa miundombinu ya maji na miradi 351 inahusisha utafutaji wa vyanzo vya maji na maandalizi ya miradi.Vilevile, Serikali ilipanga kukarabati na kujenga mabwawa 19 na kufanya usanifu wa miradi 390.
  • Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa jumla ya miradi 303 yenye jumla ya vituo vya kuchotea maji 3,845 umekamilika na kuanza kutoa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi 1,467,107. Kiambatisho Na. 1 kinaonesha orodha ya miradi iliyokamilika vijijini katika mwaka wa fedha 2021/22. Aidha, utekelezaji wa miradi 648 unaendelea na ipo katika hatua mbalimbali na miradi 88 ipo katika hatua za ununuzi wa wazabuni na wakandarasi.Vilevile, Wizara imekamilisha usanifu wa miradi 446; utafiti wa maji chini ya ardhi kwenye maeneo 158 katika vijiji 141; ukarabati wa visima 76 katika vijiji 76; na kuchimba visima 191 katika vijiji 175. Kuchelewa kuanza utekelezaji wa baadhi ya miradi kumetokana na changamoto ya kutokukamilika kwa wakati upembuzi yakinifu na usanifu wa miradi mipya iliyoibuliwa.
  • Mheshimiwa Spika Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo imeendelea kuimarisha huduma za maji vijijini kwa kutekeleza miradi na programu zifuatazo:- (i). Programu ya Malipo kwa Matokeo (PbR)
  • Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID/FCDO) inatekeleza Programu ya Malipo kwa Matokeo (Payment by Results – PbR) kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira vijijini. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya Shilingi bilioni 74.636 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa programu. Aidha, jumla ya miradi 115 imekamilika kwa kufanyiwa ukarabati na upanuzi na hivyo kurejesha huduma kwenye vituo 837 vya kuchotea maji katika vijiji 170.

              (ii).              Programu ya Uendelevu wa Huduma ya Maji na

Usafi wa Mazingira Vijijini 

73. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inatekeleza Programu ya Uendelevu wa Huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (Sustainable Rural Water Supply and Sanitation Program) inayotekelezwa kwa kipindi cha miaka sita (2019-2024) katika Mikoa 17 na Halmashauri za Wilaya 86. Kupitia Programu hiyo kiasi cha Shilingi bilioni 817.29 kilitengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ukarabati, upanuzi wa mitandao ya kusambaza maji pamoja na ujenzi wa miradi mipya itakayoibuliwa. Hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi 69 yenye jumla ya vituo 1,166 vya kuchotea maji na inanufaisha wananchi wapatao 439,302 katika vijiji 131. Aidha, ufanisi wa utekelezaji wa programu hiyo umewezesha kuongezeka kwa fedha za utekelezaji wa miradi ya maji vijijini kutoka shilingi bilioni 114 mwaka 2019/20 hadi kufikia shilingi bilioni 250 mwaka 2021/22. Ongezeko hilo la fedha litaiwezesha RUWASA kuendelea kujenga miradi mipya vijijini na hivyo kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji vijijini. Aidha, fedha hizo pia zitawezesha kujenga misingi imara ya uendelevu wa huduma muhimu ya maji kwa wananchi ikiwa ni pamoja na vyombo vya utoaji wa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSOs).

(iii). Matumizi ya    Teknolojia      ya    Nishati    Jadidifu (Renewable Energy)

  • Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) inaendelea na utekelezaji wa Mradiwa kupunguza gharama za uendeshaji kwa kubadilisha mitambo ya dizeli kwenda mitambo inayotumia nishati ya jua (Accelerating Solar Pumping via Innovative Financing Project). Gharama za mradi ni takribani Shilingi bilioni 19.85 ambapo utekelezaji wake umeanza katika mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga, Mtwara na Tabora. Lengo la mradi huo ni kutatua changamoto za gharama kubwa za uendeshaji wa miradi ya maji vijijini hususan miradi inayotumia nishati ya mafuta ya dizeli ambayo ni ghali.
  • Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imekamilisha ufungaji wa mitambo ya kufua umeme wa jua katika skimu 33 kati ya 70 iliyopangwa kwenye mikoa ya Dodoma na Singida; kujenga vituo vya maji 342 kati ya 539 vilivyopangwa pamoja na kufunga dira za malipo ya kabla  (prepaid water meter) katika vituo hivyo. Aidha, taratibu za kuwapata Wakandarasi katika mikoa ya Shinyanga na Mtwara zimekamilika ambapo utekelezaji wa ufungaji wa mitambo katika mikoa hiyo unaendelea. Vilevile, taratibu za manunuzi ya Wakandarasi kwa mkoa waTabora zinaendelea.
  • Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa gharama za uendeshaji wa miradi ya maji vijijini zinapungua, Wizara kwa kushirikiana na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuunganisha umeme na kufunga solar kwenye mitambo ya kusukuma maji inayotumia nishati ya dizeli. Mpango huo utanufaisha skimu 355 ambazo zitaunganishwa kwenye gridi ya taifa ya umeme na skimu nane (8) zitafungiwa mifumo ya solar. 

(iv). Utekelezaji wa Miradi yenye Changamoto za Muda Mrefu

77. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji kupitia Wakala wa

Maji na Usafi wa Mazingira ilipokea jumla ya miradi 177 kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa yenye changamoto ya kutokukamilika kwa wakati na mingine kukamilika bila kutoa maji. Katika mwaka 2021/22, Serikali imekamilisha miradi 42 na hivyo kufikisha miradi 127 (Kiambatisho Na. 2) ambayo ni sawa na asilimia 71.8 ya miradi yote iliyokuwa na changamoto za muda mrefu. Aidha, Wizara inaendelea na utekelezaji wa miradi 50 iliyobaki na inatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/23.

(v). Uimarishaji wa Vyombovya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii 

78. Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu miradi ya maji vijijini iliyokamilika katika baadhi ya maeneo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya kutokuwa endelevu kutokana na uwezo mdogo wa vilivyokuwa Vyombo vya Watumia Maji (Community Owned Water Supply Organizations – COWSOs) vilivyopewa jukumu la kusimamia na kuendesha miradi hiyo. Katika kuimarisha uwezo wa vyombo hivyo, Serikali kupitia Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019ilifanya maboresho ya muundo wa vyombo hivyo na sasa vinafahamika kama Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji ngazi ya Jamii (Community Based Water Supply Organisations – CBWSOs).Muundo ulioboreshwa wa CBWSOs umejumuisha wataalam wakiwemo Mafundi Sanifu wanaosimamia matengenezo ya miundombinu na Wahasibu wanaosimamia masuala ya fedha. Hadi mwezi Aprili 2022, Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii vipatavyo 2,466 vimeundwa na kuhuishwa katika mikoa 25 ya Tanzania bara. Vilevile, katika kuhakikisha kuwa huduma ya maji inakuwa endelevu, jumla ya wataalam 1,746 waliajiriwa na CBWSOs kwa mkataba ambapo kati yao Mafundi Sanifu walikuwa 940 na Wahasibu 806. Aidha,Serikali inaendelea kuhamasisha sekta binafsi kushiriki katika utoaji wa huduma ya maji ambapo jumla ya watoa huduma binafsi 66 wameingia makubaliano na CBWSOs kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma ya maji vijijini.

3.2.4        Huduma za Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa

Mazingira Mijini

79. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kutekeleza miradi ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji mbalimbali kwa kutoa maji kutoka vyanzo vya maziwa, mito, chemichemi, visima na mabwawa. Utekelezaji huo, umehusisha ujenzi wa miradi mipya, upanuzi wa miradi katika maeneo ambayo hayana miundombinu ya maji na ukarabati wa miradi yenye miundombinu chakavu pamoja na kuzijengea uwezo Mamlaka za Maji. Miradi hiyo inalenga kuboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi na usafi wa mazingira katika Miji Mikuu ya Mikoa, Miji Mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa.Katika mwaka wa fedha 2021/22, jumla ya miradi 114 ilipangwa kutekelezwa katika maeneo ya mijini. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya miradi 40 imekamilika ambapo miradi hiyo imehusisha ukarabati, upanuzi na ujenzi wa miradi mipya. Kiambatisho Na. 3 kinaonesha miradi iliyokamilika katika maeneo ya mijini. Aidha, utekelezaji wa miradi mingine unaendelea na ipo katika hatua mbalimbali. Vilevile, maunganisho ya wateja kwa huduma ya majisafi katika Mamlaka za miji mikuu ya mikoa yameongezeka kutoka wateja 942,995 mwezi Machi 2021 hadi kufikia wateja 1,074,115 mwezi Aprili 2022. 

3.2.4.1 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Mikoa

80. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya majisafi katika maeneo ya Miji Mikuu ya Mikoa ili kuimarisha huduma ya maji kwa wananchi waishio maeneo hayo. Utekelezaji wa miradi katika baadhi ya miji mikuu ya mikoa ni kama ifuatavyo:-

(i).      Miradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Dodoma 

81. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma kwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo: 

a) Mradi wa kutoa maji katika visima vya Ihumwa kwenda tanki la Njedengwa

82. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa kutoa maji katika visima vya Ihumwa kwenda tanki la

Njedengwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.4. Utekelezaji wa mradi huo ulihusisha ulazaji wa bomba kuu lenye urefu wa Kilomita 11.6; ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa Kilomita 4.2. Mradi huo unanufaisha wananchi wapatao 15,700 wa maeneo ya Nzuguni, Nyumba 300 na Iyumbu.

b) Ujenzi wa mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino – Ikulu

83. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino – Ikulu ambao ulihusisha ujenzi wa tanki katika eneo la Buigiri lenye uwezo wa lita milioni 2.5; na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 21.8 yanayopeleka maji kutoka tanki la Buigiri kwenda Ikulu ya Chamwino. Kukamilika kwa mradi huo umenufaisha wananchi wapatao 29,534.

c) Mradi wa kuchimba visima vipya na kukarabati visima vya zamani

84. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utafiti wa maji chini ya ardhi na uchimbaji wa visima katika maeneo oevu ili kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma. Kupitia mradi huo, jumla ya visima 10 vilipangwa kuchimbwa katika maeneo ya Zuzu visima vitatu (3); Ntyuka (1); Michese (1); Mpamaa (2); Mbwanga – Mipango (1); na Miyuji visima viwili (2). Hadi mwezi Aprili 2022, uchimbaji wa visima nane (8) umekamilika katika maeneo ya Zuzu, Ntyuka,Nala, Iyumbu na Ihumwa. 

d) Mradi wa Bwawa la Farkwa

85. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kukabiliana na uhaba wa huduma ya maji katika jiji la Dodoma, Serikali imepanga kujenga bwawa la Farkwa ambalo litaongeza uzalishaji wa maji kwa zaidi ya ujazo wa lita milioni 120 kwa siku, kiasi ambacho kitatosheleza mahitaji ya maji katika Jiji la Dodoma.Hadi mwezi Aprili 2022, Serikali imepata mkopo wa Dola za Marekani milioni 125.3 kutoka Benki ya Maendeleo Africa (African Development BankAfDB) kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi ambayo itahusisha ujenzi wa Bwawa na mtambo wa kutibu maji (Treatment Plant). Taratibu za kuwapata wataalam washauri watakaosimamia ujenzi pamoja na wakandarasi watakaojenga awamu ya kwanza ya mradi zinaendeleana ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2022/23. Mradi huo ukikamilika utaimarisha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama katika Jiji la Dodoma, Wilaya za Chemba, Bahi na Chamwino.

e) Mradi wa Kutoa Maji Ziwa Victoria hadi Dodoma

86. Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kutumia vyanzo vyenye maji ya uhakika ili kusambaza maji kwa maeneo mengi kwa pamoja. Kupitia dhana hiyo, Serikali imepanga kutekeleza mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria na kuyafikisha Jiji la Dodoma kupitia mji wa Singida. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili mradi huo uweze kutekelezwa.

(ii). Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Mkoa wa Dar es Salaam na baadhi ya Maeneo ya Mkoa wa Pwani

87. Mheshimiwa Spika, Wizara inatekeleza miradi ya kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na miji ya Kibaha, Kisarawe,

Mkuranga, Chalinze na Bagamoyo katika Mkoa wa Pwani.

Miradi inayotekelezwa ni pamoja na:-

a) Mradi wa Maji wa Mlandizi – Chalinze – Mboga 

88. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya maji wa Mlandizi – Chalinze – Mboga kwa gharama ya Shilingi bilioni 18.Mradi huo ulizinduliwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 22 Machi 2022. Kazi zilizofanyika ni ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 58.9; ujenzi wa vituo viwili vya kusukuma maji katika maeneo ya Chamakweza na Msoga; na ufungaji wa pampu sita za kusukuma maji. Mradi huo umewanufaisha wananchi wapatao 120,912.

b) Mradi wa Maji wa Chalinze

89. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India inaendelea kutekeleza awamu ya tatu ya mradi wa maji wa Chalinze kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 41.3 sawa naShilingi bilioni 86.9. Mradi wa Chalinze awamu ya tatu umelenga kunufaisha vijiji 68 ambapo vijiji 19 viko kaskazini na 49 viko kusini mwa mto Wami. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia wastani wa asilimia 91.6 na kazi zilizotekelezwa ni upanuzi wa mtambo kwa kuongeza uzalishaji kutoka lita 500,000 hadi 900,000 kwa saa; ulazaji wa mabomba makuu ya kusafirisha maji (transmission mains) kutoka mtamboni kuelekea maeneo ya wateja kilomita 124.38; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wakilomita 1,022.8; ujenzi wa vituo tisa (9) vya kusukuma maji (booster stations); ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 2 eneo la Mazizi na ujenzi wa matanki mengine 18 yenye ujazo wa kuanzia lita 50,000 mpaka lita milioni 1 na ujenzi wa vituo 351 vya kutekea maji (kiosks) kwenye vijiji na vitongoji mbali mbali vilivyopo eneo la mradi. 

c) Ukarabati na Upanuzi wa Mfumo wa Kusambaza

Majisafi

  • Mheshimiwa Spika, Serikali  kwa kushirikiana na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kusaidia Sekta ya Maji Awamu ya Pili (Water Sector Support Project – WSSP II) imeendelea na ukarabati na upanuzi wa mfumo wa usambazaji majisafi katika Mkoa wa Dar es Salaam. Hadi mwezi Aprili 2022,utekelezaji wa mradi wa kutoa maji kutoka kwenye tanki la Chuo Kikuu Ardhi na kuyapeleka Bagamoyo umefikia asilimia 61 ambapo kazi zinazoendelea ni pamoja na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji yenye urefu wa kilomita 1,082; ujenzi wa vituo viwili vya kusukuma maji; na ujenzi wa matanki matatu ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita milioni 15. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza maji katika maeneo ya Mbezi-Makabe. Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusuma maji, ufungaji wa pampu, ujenzi wa matanki, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 70.

d) Mradi wa Maji wa Visima Virefu vya Kimbiji na Mpera

92. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji wa visima virefu katika maeneo yaKimbiji na Mpera. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji kutoka katika visima vya Kimbiji ambapo utekelezaji wake umegawanywa katika vipande vinne. Kipande cha kwanza kinahusu ujenzi wa miundombinu ya kutoa maji kwenye visima kwenda kwenye pampu ambapo mkandarasi yupo katika hatua za awali za maandalizi. Kipande cha pili kinahusu ujenzi wa kituo cha kusukuma maji pamoja na ulazaji wa bomba la kutoa maji kwenye visima kwenda kwenye tanki la kuhifadhia maji lenye uwezo wa lita milioni 15 katika eneo la Kisarawe II ambapo utekelezaji umefikia asilimia 35. Maandalizi ya utekelezaji wa vipande vya tatu na nne unaendelea. 

e) Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kidunda

93. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa bwawa la Kidunda kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya kupungua kwa kina cha maji katika chanzo cha mto Ruvu ambacho ndio chanzo kikuu cha maji kwa Jiji la Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani. Vilevile, ujenzi wa bwawa hilo utasaidia kupunguza athari za mafuriko katika maeneo ya Morogoro na Pwani. Aidha, Serikali imetenga Shilingi bilioni 62.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa bwawa hilo katika mwaka wa fedha 2022/23 ambapo taratibu za manunuzi ya mkandarasi atakayejenga bwawa hilo na Mtaalam Mshauri atakayesimamia ujenzi zinaendelea.

(iii). Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Arusha

  • Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inaendelea na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya usambazaji majisafi na uboreshaji wa huduma ya uondoaji wa majitaka katika Jiji la Arusha unaogharimu Dola za Marekani milioni 233.9 sawa na takribani Shilingi bilioni 520.
  • Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, kazi zilizokamilika ni pamoja na uchimbaji wa visima 41; ujenzi wa mabwawa mapya 18 ya kutibu majitaka; na upanuzi na ukarabati wa miundombinu  na mifumo ya majisafi na majitaka maeneo ya katikati ya Jiji; ujenzi wa mitambo ya kusafisha maji; ujenzi wa ofisi za kanda na ujenzi wa vyoo vya mfano. Kazi zinazoendelea ni ujenzi wa ofisi kuu;  upanuzi wa mtandao wa majitaka nje ya CBD; upanuzi wa mtandao wa majisafi;  uchimbaji wa visima 15 na ujenzi wa chujio la maji. Kwa ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 80 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 40 kwa siku hadi lita milioni 200 kwa siku hivyo kuongeza muda wa upatikanaji wa huduma ya majisafi kutoka saa 12 za sasa hadi saa 24. Vilevile, kukamilika kwa mradi kutaongeza huduma ya uondoaji wa majitaka kutoka asilimia 7.6 za sasa hadi asilimia 30

(iv). Miradi ya kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza 

96. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza kwa kutekeleza miradi ifuatayo:-

                      a)     Mradi wa Kutoa Maji Chanzo cha Butimba

  • Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank-EIB) pamoja na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (French Development Agency-AFD) imeendelea kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Jiji la Mwanza. Katika mwaka 2021/22, Serikali imeanza ujenzi wa choteo katika Ziwa Victoria na mtambo wa kusafisha na kutibu maji  katika eneo la Butimba kwa gharama ya Shilingi bilioni 69.34 ambapo hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asilimia 20.
  • Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa miundombinu ya maji kwa gharama ya Euro 6,750,397.53. Kazi zinazotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu la maji kilomita 17 kutoka chanzo cha maji cha Butimba hadi tanki la kuhifadhia maji la Buswelu; ulazaji wa mabomba ya usambazaji yenye urefu wa kilomita 8.02; ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita milioni 3 katika eneola Buswelu; ujenzi wa ofisi eneo la Sahwa; ujenzi wa jengo la mtambo wa kusukuma maji; ununuzi na ufungaji wa pampu. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa kazi hizo umefikiawastani wa asilimia 10. Kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi wapatao 105,649.

b) Mradi wa Maji wa Nyamuhongolo – Kisesa 

99. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi katika maeneo ya

Nyamuhongolo – Kisesa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.18. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa kituo cha kusukuma maji katika eneo la Nyamuhongolo; ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 120,000;na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 75 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. Kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi wapatao 39,600.

c) Mradi wa kuboresha na upanuzi wa miundombinu ya Majisafi Maeneo ya Katikati na Kusini mwa Jiji la Mwanza

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa miundombinu ya Majisafi Jijini Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 17.89. Mradi huo umehusisha ujenzi wa matanki mawili (2) yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 2.95 katika maeneo ya Sahwa na Igengele-Bugarika; kulaza mtandao wa mabomba umbali wa kilomita 11.3 na kufunga pampu za kusukuma maji Nyegezi. Mradi huo unatoa huduma kwa wananchi wapatao 300,000 wa maeneo ya Sahwa, Buhongwa, Nyegezi, Kanyerere, Lwanhima, Kanindo, Fumagila, Buswelu, Lukobe, Kigala, Nsumba, Kahama,

Bujigwa, Nyamadoke na Ilalila.

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira jijini Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 38.93. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 1.2; ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 19.8 kutoka chanzo cha Butimba hadi Igoma; kufunga pampu za kusukuma maji Sahwa kupeleka tanki la Igoma; kulaza mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 5.26 kutoka tanki la Nyegezi hadi Buhongwa; na kulaza mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 0.925 kutoka Mabatini hadi Hospitali ya Bugando. Mradi unatoa huduma kwa wananchi wapatao 300,000 katika maeneo ya Bugarika, Nyegezi, Majengo, Ibanda, Utemini, Mkolani, Mwananchi, Mabatini, Kitangiri, Kiseke, Nyasaka, Mjimwema na Nyamhongolo.

(v). Miradi ya kuboresha huduma ya Majisafi katika Manispaa ya Bukoba

102. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa upanuzi wa mtandao wa majisafi katika Manispaa ya Bukoba. Utekelezaji wa Awamu ya kwanza ya mradi iliyogharimu Shilingi bilioni 2.42 umekamilika. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi vituoviwili (2) vya kusukuma maji; ufungaji wa pampu; ulazaji wa mabomba urefu wa kilomita 60; ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 500,000; na ukarabati wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 70,000. Kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi kumeongeza upatikanaji wa huduma kutoka asilimia 88 hadi asilimia 91. Utekelezaji wa awamu ya pili unaogharimu Shilingi bilioni 3.35 umefikia asilimia 35. Awamu hiyo inahusisha ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita 500,000; ujenzi wa bomba kuu kutoka kituo cha kusukuma maji cha Machinjioni hadi Bugashani umbali wa kilomita 4.7; ununuzi na ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 32. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba 2022 na utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 91 hadi asilimia 98.

(vi). Mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Kigoma

103. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo KfW imekamilisha utekelezaji wa mradi wa Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Kigoma na wananchi wanapata huduma ya maji. Hata hivyo, kutokana na hitilafu iliyojitokeza katika eneo la choteo la maji, Serikali inaendelea na ujenzi wa choteo jipya kwa gharama ya Euro milioni 3.61 ambapo hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi umefikia asilimia 22.

(vii). Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Lindi

104. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi unaendelea ambapo kazi zilizokamilika ni pamoja na uchimbaji wa visima 10 na ufungaji wa pampu katika visima hivyo; ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 9.8 kutoka kwenye visima kwenda kwenye mtambo wa kutibu maji; ujenzi wa mtambo wa kutibu maji eneo la Ng’apa; ujenzi wa matanki mawili (2) ya kuhifadhia maji; ulazaji wa mabomba ya mtandao wa usambazaji maji yenye urefu wa kilomita 27; kujenga bwawa la majitaka na kununua gari la majitaka. Kazi zinazoendelea ni pamoja na ufungaji wa mfumo wa uendeshaji visima na uzibaji wa mivujo na kufanya majaribio ya msukumo wa maji (Pressure test) katika bomba kuu lenye urefu wa kilomita 3.6.Utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 98 na umeanza kutoa huduma kwa wananchi. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 3.6 kwa siku hadi lita milioni 15 kwa siku na wananchi wapatao 91,968 wananufaika na huduma ya majisafi na salama.

(viii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Morogoro

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (French Development Agency-AFD) inaendelea kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika Mji wa Morogoro kwa gharama ya Euro milioni 84. Utekelezaji wa mradi unahusisha kufanya tathmini ya kina ya kuongeza kimo cha tuta (embarkment height) la Bwawa la Mindu kwa mita 2.5 ili kuhifadhi maji mengi zaidi; kulaza bombalenye urefu wa kilometa 2.5 kutoka Bwawa la Mindu hadi kwenye mtambo wa kutibu maji uliopo Mafiga; kujenga mtambo mpya wa kutibu maji katika eneo la Mafiga wenye uwezo wa kutibu maji kiasi cha lita milioni 54 kwa siku; kulaza bombalenye urefu wa kilometa 15 litakalopeleka maji eneo la kingolwira kutoka birika la Tumbaku; kujenga tanki la kuhifadhia majisafi lenye ujazo wa lita 450,000 litakalosambaza maji katika eneo la Kingolwira; kujenga tanki la kuhifadhi majisafi lenye ujazo wa lita 12,050,000 katika eneo la Mafiga; kufunya kampeni za kujenga uelewa kwa wananchi katika masuala ya usafi wa mazingira, utunzaji wa vyanzo vya maji na miundombinu ya maji; na kujenga uwezo wa watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro katika masuala ya uendeshaji na matengenezo ya miundombinu ya maji kwa lengo la kupunguza upotevu wa maji.
  2. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri anaendelea na kazi ya uandaji wa Mpango Kabambe wa Rasilimali za Maji (Water Resource Master plan) wa Mji wa Morogoro; na tathmini ya kuongeza kimo cha tuta la Bwawa la Mindu kwa mita 2.5. Aidha, taratibu za ununuzi wa wakandarasi watakaotekeleza mradi kwa utaratibu wa kusanifu na kujenga unaendelea. Mradi unatarajiwa kukamilika mwaka 2025 na utaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 35 kwa siku hadi lita milioni 89 kwa siku.

(ix). Miradi ya Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Jiji la Mbeya 

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Kiwira hadi Jiji la Mbeya. Hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri kwa ajili ya usanifu wa mradi amepatikana na tayari ameanza kazi. Mradi huo utatekelezwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa chanzo na miundombinu ya kupeleka maji katika Jiji la Mbeya. Kukamilika kwa awamu hiyo kutawanufaisha wananchi wapatao 850,000. Awamu zitakazofuata zitahusisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji katika miji ya Chunya, Inyala, Vwawa, Mlowo na Tunduma. 
  2. Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Mbeya, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa Itende.Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 9; na ujenzi wa vituo vinne (4) vya kuchotea maji. Vilevile, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa maji wa Nzovwe-Isyesye unaogharimu Shilingi milioni 400. Mradi huo unahusisha ujenzi wa chanzo cha maji; ujenzi wa tanki la kukusanyia maji (Sump well); ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji; ufungaji wa pampu; na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 5. Hadi mwezi Aprili 2022 utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 30. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022 na utawanufaisha wakazi wapatao 30,000.

(x). Mradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Tanga

109. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Jiji la Tanga unaogharimu Shilingi bilioni 9.18. Mradi huo unahusisha ujenzi wa bomba kuu lenye urefu kilomita 12.4; ujenzi wa tanki la ujazo wa lita milioni 1; na kujenga mtambo mpya na kukarabati mtambo uliopo wa kutibu maji. Hadi mwezi Aprili 2022, mradi umefikia asilimia 12 na mradi huo ukikamilika utawanufaisha wananchi wapatao 382,095.

(xi). Miradi ya Kuboresha Huduma ya Maji katika Mji wa Babati

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji Darakuta – Magugu uliogharimu Shilingi bilioni 3.998. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa chanzo cha maji; ulazaji wa bomba kuu la kusafirisha maji lenye urefu wa kilomita 20; ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 73; ujenzi wa mtambo wa kuchuja na kutibu maji lita milioni 5 kwa siku; ununuzi wa dira za maji 4000; ujenzi wa nyumba ya mlinzi na ujenzi wa uzio kuzunguka mtambo wa kuchuja na kutibu maji. Mradi huo unanufaisha wananchi wapatao 58,941.
  2. Vilevile, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji Dareda-Singu-Sigino-Bagara kwa gharama ya Shilingi bilioni 12.77. Mradi huo unahusisha ujenzi wa matanki matano (5) ya kuhifadhia maji yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 4.1; ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji wenye urefu wa kilomita 63.31; ujenzi wa bomba kuu la ksafirisha maji lenye urefu wa kilomita 26.83; ujenzi wa vituo viwili (2) vya kusukuma maji (booster stations); ununuzi na ufungaji wa pampu mbili (2) za kusukuma maji; ujenzi wa mtambo wa kuchuja na kutibu maji; na ujenzi wa chanzo. Kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 150,000 pamoja na ujenzi wa chanzo. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 30. Mradi ukikamilika utanufaisha wananchi wapatao 60,000.

3.2.4.2 Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Miji mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa

              (i).      Mji wa Orkesumet 

  1. Mheshimiwa Spika, Mradi wa  maji katika Mji wa Orkesumet  unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu (BADEA) na Mfuko wa Nchi zinazozalisha mafuta kwa maendeleo ya kimataifa (OPEC Fund for International Development – OFID). Utekelezaji wa mradi huoumekamilika kwa gharama ya Shilingi bilioni 38.11 ambapo kazi zilizotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji na mtambo wa kutibu na kusafisha maji; ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 35; vituo vitatu (3) vya kusukuma maji; matanki tisa (9) yenye ujazo kuanzia lita 50,000 hadi lita milioni 1.6; mtandao wa usambazaji maji wenye urefu wa kilomita 64; vituo 10 vya kuchotea maji; birika 10 za kunyweshea mifugo; ujenzi wa ofisi; ununuzi na ufungaji wa pampu; crane; na kupeleka umeme kwenye chanzo. Mradi huu unanufaisha wakazi wapatao 52,000 pamoja na mifugo yao.

(ii). Mradi wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Namanga na eneo la Kimokouwa.

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha mradi wa kuboresha huduma ya maji katika mji wa Namanga na eneo la Kimokouwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.88. Mradi huo umehusisha ulazaji wa mtandao wa mabomba urefu wa kilomita 40.948; ujenzi wa vituo vya kuchotea maji; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 225,000;Ukarabati wa matanki manne; ujenzi wa uziona ujenzi wa chemba za Airvalves na Washout. Mradi huo umewanufaisha wananchi wapatao 29,686.

(iii). Mradi wa Maji Mugango – Kiabakari – Butiama

114. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (Saudi Fund for Development – SFD) imeanza kutekeleza mradi wa maji utakaohudumia maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 30.69. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa choteo la maji katika Ziwa Victoria; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kusukuma maji; ujenzi wa tanki kubwa la maji safi eneo la Mugango pamoja na mantaki matano (5) katika maeneo ya Kong, Kiabakari, Butiama Hill na Bumangi; ulazaji wa bomba kuu kutoka Mugango kwenda Kiabakari hadi Butiama lenye urefu wa kilomita 48; ulazaji wa mabomba ya mtandao wa kusambaza maji wenye urefu kilomita 140; ujenzi wa ofisi na nyumba za wasimamizi wa mitambo; ukarabati wa matanki mawili (2) katika maeneo ya Kyatungwe na Bisarye; ujenzi wa vioski 40 vya maji na ununuzi wa dira za maji 2,000. Hadi mwezi Aprili, 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 54 na unatarajia kukamilika mwezi Desemba, 2022. Mradi huo utanufaisha wananchi zaidi ya 100,000 waliopo katika eneo la mradi pamoja na vijiji vilivyopo ndani ya kilomita 12 kutoka bomba kuu.

(iv). Miji ya Tinde na Shelui

115. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India kupitia Benki ya Exim-India inatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji ya Tinde na Shelui. Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 10.6. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa matanki mawili (2) ya Tinde na Shelui; ukarabati wa matanki mawili katika eneo la Shelui; na ujenzi wa kituo cha kusukuma maji. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60.7 na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022.Mradi huo utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 86,984wa miji ya Tinde na Shelui. 

               (v).     Mji wa Bunda

116. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Bunda unaopata maji kutoka Ziwa Victoria kwa kujenga mfumo wa kusafisha na kutibu maji katika eneo la Nyabehu. Mradi huo unagharimu Shilingi bilioni 10.60 na hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wake umefikia asilimia 90 na wananchi wameanza kupata huduma ya majisafi. Mradi huo utakapokamilika utawanufaisha wakazi wapatao 1,200,000 wa Mji wa Bunda.

(vi). Mradi wa Maji Kyaka – Bunazi

117. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa majisafi wa Kyaka – Bunazi kwa gharama ya Shilingi bilioni 15.74. Mradi huo unatekelezwa kwa vipande (Lots) viwiliambapo kipande cha kwanza kinahusisha ujenzi wa chanzo cha maji katika mto Kagera chenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 6.57 kwa siku; ulazaji wa bomba kuu urefu wa kilomita 1.6; ujenzi wa mtambo wa kusafisha na kutibu maji; ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita milioni 2; na ujenzi wa jengo la mradi. Kipande cha pili kinahusisha ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wakilomita 14; ulazaji wa mtandao wa mabomba yakusambaza maji wenye urefu wa kilomita 60; ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji; na kuunganisha wateja wapatao 1,000. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asimilia 92 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. 

(vii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Mji wa Chato 

118. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi katika mji wa Chato kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.91 ambapo wananchi wapatao 16,000 wananufaika na huduma ya majisafi. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wa kilomita 16.66; ukarabati wa kituo cha kusukuma maji Rubambangwe; ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji yenye wa kilomita 41.94 katika mitaa ya Itale, Nyabilezi, Uwanja wa Ndege, Chato Beach, Kahumo na maeneo ya katikati ya mji; ujenzi wa matanki mawili ya kuhifadhia maji katika maeneo ya Itale (lita 300,000) na Uwanja wa Ndege (lita 150,000); ufungaji wa pampu mbili zenye uwezo wa kuzalisha lita 160,000 kwa saa kila moja; ufungaji wa Transformer pamoja na ujenzi wa njia kuu ya umeme; na ufungaji wa mtambo wa kutibu maji “Mobile Water Treatment Plant”.

(viii). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji KatoroBuseresere

119. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji midogo ya Katoro na Buseresere kwa gharama ya Shilingi bilioni 4.26. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 500,000; ujenzi wa bomba kuu la kusafirisha maji kilomita 24.6 kutoka Chankorongo mpaka eneo la tanki jipya Katoro; ujenzi wa bomba la kusambaza maji kilomita 26; Ujenzi wa mtambo wa kutibu maji “ Mobile treatment Plant” na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji. Hadi mwezi Aprili2022, utekelezaji wa mradi umefikia asimilia 80 ambapo wananchi 71,100 watanufaika na huduma ya majisafi.

(ix). Mradi wa Maji Same – Mwanga – Korogwe 

120. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo kutoka Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu kwa Nchi za Kiafrika (BADEA), Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha Mafuta (OFID), Mfuko wa Maendeleo wa Saudi Arabia (SFD) na Serikali ya Kuwait kupitia

Mfuko wa Maendeleo (KFD) inatekeleza Mradi wa Maji SameMwanga-Korogwe. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji umefikia asilimia 70.4. Kazi zinazoendelea kutekelezwa ni pamoja naujenzi wa chanzo, chujio na ulazaji bomba kutoka chanzo mpaka kwenye chujio na kutoka kwenye chujio hadi tanki la Kisangara;ulazaji wa bomba kutoka Kisangara hadi Kiverenge na kutoka Kiverenge hadi Vudoi/Mwanga nakujenga miundombinu ya kusambaza maji katika miji ya Same na Mwanga.Hata hivyo, mradi huo ulikuwa na changamoto za Wakandarasi ambapo kwa sasa Serikali imechukua hatua za kupata Wakandarasi wengine ili kukamilisha kazi zilizobaki. 

(x). Mradi wa maji Kayanga/Omurushaka-Karagwe

121. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa maji Kayanga/Omurushaka – Karagwe ili kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika miji ya Omurushaka na Kayanga kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.88. Mradi unahusisha uchimbaji wa visima virefu viwili (2); ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 30;  ufungaji wa pampu sita (6); ujenzi wa viosk vinne (4); ununuzi wa pikipiki mbili (2); Ununuzi wa mfumo wa ankra; na ununuzi wa vitendea kazi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 95. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2022 na utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 25 hadi asilimia 40.

(xi). Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji 28

122. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya India kupitia Benki ya Exim – India inategemea kuanza ujenzi wa mradi wa kuboresha huduma ya maji katika miji 28 ya Tanzania Bara na mji mmoja visiwani Zanzibar kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 500. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kuwapata wakandarasi wa ujenzi katika miji 24 zimekamilika ambapo ujenzi wa miradi katika miji hiyo itatumia fedha za mkopo wa India na miji minne (4) ya Mafinga, Makonde, Songea na Tarime-Ryorya utekelezaji wake utafanywa kwa kutumia fedha za ndani. Mikataba ya ujenzi itasainiwa kabla ya kumalizika kwa mwaka wa fedha 2021/22. 

3.2.4.3 Mradi wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko

ya Tabianchi katika Mkoa wa Simiyu

123. Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya KfW kwa niaba ya Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCF) inatekeleza mradi wa kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabianchi katika wilaya tano (5) za Mkoa wa Simiyu ambazo ni Busega, Bariadi, Itilima, Maswa na Meatu. Katika awamu ya kwanza mradi wa maji utatekelezwa katika Wilaya za Busega, Itilima na Bariadi. Mradi huo unakadiriwa kugharimu jumla ya kiasi cha Euro milioni 171, ambapo GCFwatachangia Euro milioni 102.7, Benki ya KfW itachangia Euro milioni 26.1, Serikali ya Tanzania Euro milioni 40.7 na Wananchi kupitia nguvu zao watachangia Euro milioni 1.5. Aidha, awamu ya kwanza ya fidia kiasi cha Shilingi bilioni 1.52 kimelipwa kwa wananchi wapatao 1,201 kati ya 1,308 waliotathiminiwa. Hadi mwezi Aprili 2022, Mtaalam Mshauri wa kujenga uwezo kwa wataalam wa Mamlaka za Maji na Wizara amepatikana na tayari amenza kazi. Vilevile, Mtaalam Mshauri wa kufanya mapitio ya usanifu na usimamizi wa mradi amepatikana na anaendelea na kazi ya mapitio ya usanifu. Serikali inaendelea na taratibu za kuwapata wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mradi.

3.2.4.4 Miradi ya Maji katika Maziwa Makuu ya

Victoria, Tanganyika na Nyasa

124. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya kandokando ya maziwa makuu wanapata huduma ya maji safi, salama na ya kutosheleza, Serikali inakamilisha usanifu wa kina kwa ajili ya kutumia chanzo cha ziwa Victoria kwenye mikoa ya Mwanza, Geita, Simiyu, Kagera na Mara; ziwa Tanganyika kwenye mikoa ya Katavi, Kigoma na Rukwa; pamoja na ziwa Nyasa katika mikoa ya Ruvuma na Njombe. Hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo ni kama ifuatavyo:-

              (i).                  Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa

Victoria

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni ya miradi 45 iliyobainishwa kutumia chanzo cha maji cha Ziwa Victoria kupeleka huduma ya maji katika vijiji vinavyozunguka ziwa hilo. Miradi hiyo itagharimu Shilingi bilioni 750.69 na itakapokamilika itahudumia wananchi wapatao 2,854,292 wa vijiji 324 vya Halmashauri za Wilaya za Geita vijiji 37, Chato (21), Nyangh’wale (9) na Mbogwe vijiji 18 katika Mkoa wa Geita; Sengerema vijiji 33, Magu (16), Misungwi (17), Buchosa (29),Ukerewe (35) na Manispaa ya Ilemela vijiji vitatu (3) katika

Mkoa wa Mwanza; Manispaa ya Bukoba (4), Bukoba

Vijijini(11), Muleba (8), Biharamulo (12), na Missenyi vijiji nane (8) katika Mkoa wa Kagera; Musoma Vijijini (32), Rorya (20) na Bunda vijiji 11 katika Mkoa wa Mara. 

  1. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, Serikali inaendelea na ujenzi wa mradi wa maji wa Nkome katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa gharama ya Shilingi bilioni 4.6. Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 20 ambapo ukikamilika utahudumia vijiji 17 kwenye kata za Lwezera, Nyamboge, Nzera, Katome na Nkome.

(ii).     Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa   Tanganyika

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kupata Wakandarasi wa ujenzi wa miradi 32 iliyobainishwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika. Miradi hiyo, itagharimu Shilingi bilioni 117.412 na inatarajiwa kuwanufaisha wakazi wapatao 616,000 wa vijiji 79 vya Halmashauri zifuatazo: – Kigoma Vijijini: vijiji 8; Uvinza: Vijiji 7; Nkasi: Vijiji 32; Kalambo: Vijiji 8; Mpimbwe: Vijiji 6; na Tanganyika: Vijiji 11.
  2. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi wa Mradi wa maji Kirando – Kamwanda uliopo katika Wilaya ya Nkasi umefikia asilimia 98 na umeanza kutoa huduma kwa wakazi wapatao 74,000 wa vijiji 8 vya Kirando, Kamwanda, Mtakuja, Itete, Chongo, Katete, Kichangani na Isasa. Mradi huo unatumia chanzo cha maji cha Ziwa Tanganyika na unagharimu Shilingi bilioni 3.07. Vilevile, Serikali imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa Kabwe unaohudumia vijiji vya Kabwe, Kabwe Camp na Udachi vilivyopo Mkoa wa Rukwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.6. Aidha, Serikali inaendelea na ujenzi wa miradi ya maji ya Korongwe utakaohudumia vijiji vya Korongwe na Karungu; na mradi wa maji Kipwa utakaohudumia vijiji vya Kipwa na Kipele kwa kutumia chanzo cha Ziwa Tanganyika.

(iii). Miradi ya Maji Itakayotumia Chanzo cha Ziwa Nyasa

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na usanifu wa kina wa miradi itakayotumia chanzo cha maji cha Ziwa Nyasa. Miradi hiyo itatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwenye Mkoa wa Ruvuma na Halmashauri ya Ludewa ilipo katika Mkoa wa Njombe. Miradi hiyo inatarajiwa kuhudumia wananchi wapatao 30,000 wa vijiji 11 vya Wilaya ya Ludewa na wananchi wapatao 120,000 wa vijiji 30 vya Wilaya ya Nyasa.

                      3.2.4.5     Miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi

wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji ni mojawapo ya

Wizara zinazotekeleza Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 kwa lengo lakuhakikisha wananchi wa Tanzania wanapata majisafi, salama na ya kutosheleza karibu na makazi yao ili waweze kupambana na UVIKO-19.Kupitia mpango huo, Wizara imetengewa Shilingi bilioni 139.35 kwa ajili ya kutekeleza jumla ya miradi 218 ambapo miradi 172 ni ya maji vijijini na 46 ni miradi ya maji mijini pamoja na ununuzi wa seti 25 za mitambo ya kuchimba visima; seti 5 za ujenzi wa mabwawa; na seti 4 za vifaa vya utafiti wa maji chini ya ardhi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa miradi ya maji vijijini umefikia wastani wa asilimia 46 na miradi ya maji mjini asilimia 67 ambapo utekelezaji wa miradi hiyo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. Kukamalika kwa miradi hiyo kutawanufaisha zaidi ya wananchi 2,093,800. Aidha, kwa upande wa ununuzi wa mitambo mikataba ya ununuzi imesainiwa tarehe 08 Februari, 2022 na inatarajiwa kupokelewa mwishoni mwa mwezi Juni, 2022.

3.2.5 Miradi ya Usafi wa Mazingira

131. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo ya miji mikuu ya mikoa, miji mikuu ya wilaya na miji midogo. Lengo ni kuimarisha huduma ya usafi wa mazingira nchini kwa kulinda afya za wananchi na mazingira.Katika kuimarisha huduma ya uondoshaji majitaka katika maeneo ya mijini Serikali imejenga, kupanua na kukarabati miundombinu ya majitaka katika maeneo mbalimbali ya mijini. Kutokana na jitihada hizo, idadi ya wateja waliounganishwa kwenye mtandao wa majitaka imeongezeka kutoka wateja 52,661 mwezi Machi, 2021 hadi wateja 53,428 mwezi Aprili 2022.Miradi inayoendelea kutekelezwa ni pamoja na:-

(i). Mradi wa Ujenzi wa Mfumo Rahisi wa Uondoshaji Majitaka Maeneoya Milimani katika Jiji la Mwanza

132. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mfumo rahisi wa uondoshaji majitaka maeneo ya milimani katika Jiji la Mwanza kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.84. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa mtandao wa mabomba ya majitaka yenye urefu wa kilomita 17.595;  na kuunganisha wateja 6,042 katika maeneo ya Igogo-Sahara, Isamilo, Kabuholo na Ibungiro. Vilevile,Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa mfumo rahisi wa uondoshaji majitaka katika maeneo ya Mabatini, Kilimahewa A, Kilimahewa B na Pasiansi unaogarimu Shilingi bilioni 3.72. kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa mtandao wa mabomba ya majitaka yenye urefu wa kilomita 15.79; ujenzi wa chemba, ujenzi wa ngazi, uboreshaji wa squatting pan na kuunganisha wateja 900. Hadi mwezi Aprili 2022 utekelezaji umefikia asilimia 12.

(ii). Mradi wa Usafi wa Mazingira Eneo la Ilemela

133. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa upanuzi wa mabwawa ya kutibu majitaka katika eneo la Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 6.74. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 40.

(iii). Ujenzi wa Vyoo mashuleni katika Jiji la Mwanza

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha kwanza kwenye shule na maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza Wilaya ya Nyamagana kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.25.

Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 12 na mradi utakapokamilika utanufaisha wanafunzi 21,124 katika shule 12. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 98. Vilevile, Serikali imekamilisha ujenzi wa vyoo kipande cha pili kwenye shule na sehemu za wazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.31 Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 12 na Zahanati mbili na mradi huo unawanufaisha wanafunzi 18,679 katika shule 12. 

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha tatu kwenye shule na maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza Wilaya ya Nyamagana kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.69. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 11 na mradi utakapokamilika utanufaishawanafunzi 21,124. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 63. Vilevile, Serikali inatekeleza ujenzi wa vyoo kipande cha nne kwenye shule na sehemu za wazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.79. Kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa vyoo katika shule 10 na Zahanati mbili na mradi huo unawanufaisha wanafunzi 18,679 katika shule 10. Hadi mwezi Aprili, 2022 utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 55.

(iv). Mradi wa Ukarabati wa Mfumo wa Majitaka katika Maeneo ya Area C na D katika Jiji la Dodoma

136. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ukarabati wa mfumo wa majitaka katika maeneo ya Area C na Area D yaliyopo Jijini Dodoma unaogharimu Shilingi bilioni 4.96. Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ukarabati wa bomba za majitaka urefu wa kilomita 19 pamoja na kujenga chemba 1,005 za majitaka. Kazi zilizofanyika ni ukarabati wa mabomba ya majitaka urefu wa kilomita 5.959 pamoja na ujenzi wa chemba 40. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 33 na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2022.

(v). Mradi wa Upanuzi wa Mfumo wa Majitaka katika

Maeneo ya Korongoni na Longuo “A” Manispaa ya Moshi

137. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika Manispaa ya Moshi kwa kujenga mradi wa upanuzi wa mfumo wa majitaka katika kata za Korongoni na Longuo “A” kwa gharama ya Shilingi bilioni 1. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja na ujezi wa bomba la majitaka lenye urefu wa kilomita 12.99; na ujenzi wa chemba 171. Hadi mwezi Aprili 2022, taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo zimekamilika ambapo ujenzi utaanza mwezi Juni 2022. 

(vi). Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Majitaka katika Mji wa Nzega 

138. Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya uondoshaji wa majitaka katika Mji wa Nzega kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.5. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa bwawa la majitaka na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili2022, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2022.

(vii). Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida

139. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida kwa gharama ya Shilingi bilioni 1. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa mabwawa ya kutibu majitaka; ujenzi wa jengo la walinzi na ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka. Hadi mwezi Aprili 2022,mradi umefikia hatua za mwisho za kupata mkandarasi atakaetekeleza mradi huo inaendelea na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2022.

(viii). Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Majitaka katika Mji wa Muheza

140. Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya majitaka katika mji wa Muheza kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.03. Utekelezaji wa mradi unahusisha ujenzi wa miundombinu ya kutibu majitaka (Feacal Sludge Treatment Facilities – FSTF); ununuzi wa gari la uondoshaji wa majitaka; ununuzi wa gari ya usimamizi, ujenzi wa barabara ya kufika eneo la bwawa; na ujenzi wa vyoo shuleni na stendi. Hadi mwezi Aprili 2022, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2022 na kunufaisha wakazi wapatao 38,131 wa Mji wa Muheza.

(ix). Miradi ya Usafi wa Mazingira katika Maeneo ya

Vijijini

141. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza Kampeni ya Usafi wa Mazingira kwa lengo la kuboresha huduma ya usafi wa mazingira katika maeneo ya vijijini. Katika mwaka 2021/22, Wizara yangu inaendelea na utekelezaji wa miradi 413 ya usafi wa mazingira katika vituo vya kutolea huduma za afya na shule. Hadi mwezi Aprili 2022, miradi 137 imekamilika na miradi 276 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

3.2.6 Taasisi zilizo Chini ya Wizara

(i). Mfuko wa Taifa wa Maji

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha Mfuko wa Taifa wa Maji kupitia Sheria Na.12 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009. Kwa sasa Mfuko unatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019. Majukumu ya Mfuko ni kutafuta fedha, kutoa fedha kwa watekelezaji wa miradi ya maji na kufuatilia matumizi ya fedha hizo. Wanufaika wa fedha za Mfuko wa Maji ni pamoja na RUWASA, Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira Mijini, Bodi za Maji za Mabonde na Wizara ya Maji.
  2. Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu Na. 55 cha Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019, vyanzo vya mapato ya Mfuko ni pamoja na fedha zitakazoidhinishwa na Bunge, misaada pamoja na fedha nyingine zitakazolipwa kwenye Mfuko kwa mujibu wa Sheria nyingine. Kwa sasa chanzo pekee cha mapato ya Mfuko ni tozo ya shilingi 50 kwa kila lita ya mafuta ya diseli na shilingi 50 kwa kila lita ya petroli. Katika mwaka 2021/22, Mfuko wa Taifa wa Maji ulikadiriwa kupata mapato ya Shilingi 175,912,837,000 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ambapo hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya Shilingi 137,956,116,703.40 sawa na asilimia 78 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa huduma ya maji mijini na vijijini pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji.
  3. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuongeza mapato ya Mfuko wa Taifa wa Maji, Mfuko umekamilisha taratibu za kuanzisha zoezi la utoaji wa mikopo ya riba nafuu (Loan Window) kwa Mamlaka za Maji na taasisi zinazotoa huduma ya maji nchini zitakazo kidhi vigezo. Mpango huo unatarajiwa kuanza katika mwaka 2022/23 na tayari Mfuko umetenga fedha za kuanzia (seed money) kiasi cha Shilingi bilioni 15.  Utaratibu huo unatarajiwakuongeza wigo wa upatikanaji wa fedha kwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na hivyo kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maji nchini. Aidha, Serikaliimeendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Maji katikauandaaji wa maandiko ya miradi (Fundable/Bankable Projects Write ups) kwa ajili ya kupata fedha za kutosha za ujenzi wa miradi ya maji.

(ii). Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA)

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuijengea uwezo RUWASA ili iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Katika mwaka 2021/22, jumla ya magari 33 yamenunuliwaambapo magari 17 yaligawanywa katika Wilaya 17 ambazo hazikuwa na vyombo vya usafiri. Wilaya hizo niKilindi (Tanga), Kalambo (Rukwa), Nyangw’ale, Mbogwe

(Geita), Butiama (Mara), Chunya (Mbeya), Buhigwe, Uvinza

(Kigoma),       Mkalama    (Singida),    Wangingo’mbe      (Njombe),

Kyerwa (Kagera), Itilima (Simiyu), Kaliua (Tabora), Nsimbo na Mlele (Katavi), Mafia (Pwani) na Lindi (Lindi). Vilevile, Magari 7 yaligawanywa katika mikoa ya Manyara, Tanga, Simiyu, Songwe, Ruvuma, Njombe na Katavi; na magari 9 yalipelekwa Ofisi ya RUWASA Makao Makuu.

  1. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha na kuboresha usimamizi wa fedha za umma, RUWASA ilijiunga na Mifumo mbalimbali ya TEHAMA ya Serikali ikiwemo Mfumo wa Kielektroniki wa Makusanyo ya Fedha Serikalini (Government e-Payment Gateway), Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (Tanzanian National e-Procurement System) na Mfumo wa Kielektroniki wa Mipango, Bajeti na Taarifa (PLANREP). Pia, RUWASA ilianzisha Mfumo wa Utoaji Taarifa za Huduma ya Maji Vijijini (RUWASA Service Delivery Management System – RSDMS) kwa lengo lakuwezesha upatikanaji wa taarifaza utekelezaji, usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji vijijini.Mfumo umewezesha RUWASA kuongeza ufanisi katika utekelezaji, usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji vijijini. 
  2. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi, RUWASA imenunua kiwanja eneo la Njedengwa Investment, chenye ukubwa wa mita za mraba 34,500 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Makao Makuu, Ofisi ya Mkoa wa Dodoma pamoja na Ofisi wilaya ya Dodoma. Vilevile, RUWASA imenunua viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za RUWASA mikoa ya Geita, Mara, Katavi na Wilaya ya Nyasa.

(iii). Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira 

  1. Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira zimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya

Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019.

Mamlaka hizo, zimepewa jukumu la kutoa huduma za majisafi na salama pamoja na usafi wa mazingira katika maeneo ya mijini. Katika kuimarisha usimamizi wa huduma ya majisafi na usafi wa Mazingira Wizara imeanzisha jumla ya Mamlaka 94 za Majisafi na Usafi wa Mazingira katika maeneo mbalimbali ya mijini. Maeneo ya Miji Mikuu ya Mikoa kuna Mamlaka 25 za Majisafi na Usafi wa Mazingira; Mamlaka saba (7) za Miradi ya Kitaifa; Mamlaka 54 katika Miji Mikuu ya Wilaya; na Mamlaka nane (8) katika Miji Midogo.

  1. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Serikali imeendelea kuziimarisha mamlaka za maji kwa kujenga ofisi katika Mamlaka za Maji za Arusha, Bunda, Makambako, Mugango-Kiabakari na Biharamulo. Aidha, Serikali imetoa mafunzo ya kujenga uwezo wa menejimenti na Bodi za Wakurugenzi kwa Mamlaka 40 za Majisafi na Usafi wa Mazingira ili kuongeza ufanisi katika uendeshaji na usimamizi wa mamlaka hizo.

(iv). Chuo cha Maji

  1. Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maji ni Taasisi yenye jukumu la kuandaa wataalam wa Sekta za maji na umwagiliaji. Majukumu mengine ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam na kufanya tafiti mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya Sekta. Chuo kinatoa mafunzo katika ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada. Katika ngazi ya Astashahada na Stashahada mafunzo yanayotolewa ni Uhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira (Water Supply and Sanitation Engineering); Uhandisi wa Umwagiliaji (Irrigation Engineering); Haidrojiolojia na Uchimbaji wa Visima (Hydrogeology and Water Well Drilling); Haidrolojia na Hali ya Hewa (Hydrology and Meteorology); pamoja na Teknolojia ya Maabara na Ubora wa Maji (Water Quality Laboratory Technology). Katika ngazi ya Shahada, mafunzo yanayotolewa ni katika fani ya Uhandisi wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji (Bachelor of Engineering in Water Resources and Irrigation). Vilevile, Chuo kinaendesha kozi mbalimbali za muda mfupi katika sekta za maji na umwagiliaji.
  2. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, wanafunzi 656 wa Astashahada na Stashahada wamedahiliwa. Vilevile, wanafunzi 247 wa Shahada ya kwanza ya Uhandisi wa

Rasilimali za Maji na Umwagiliaji walidahiliwa ikilinganishwa na wanafunzi 218 katika mwaka 2020/21. Kwa sasa, chuo kina jumla ya wanafunzi 2,256 ambapo wanafunzi 1,466 ni wa Astashahada na Stashahada na wanafunzi 790 ni wa Shahada ya kwanza. Aidha, katika mahafali ya Novemba 2021, jumla ya wanafunzi 494 walihitimu mafunzo yao ambapo wanafunzi 138 ni wa Shahada, 305 wa Stashahada na wahitimu 51 walikuwa wa ngazi ya Astashahada. 

  1. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha taaluma bora inatolewa, Chuo kimeendelea kuwajengea uwezo watumishi wake katika ngazi za Shahada ya kwanza, Uzamili na Uzamivu. Hadi mwezi Aprili 2022, watumishi 10 wanaendelea na mafunzo ya Shahada ya Uzamivu (PhD); Watumishi watatu (3) ni Shahada ya Uzamili (Masters) na watumishi wanne (4) ni Shahada ya kwanza. Vilevile, kupitia fedha za ndani, Chuo kimekamilisha ujenzi wa zahanati, upanuzi wa maabara ya Hydraulics na ukarabati wa jengo moja la hostelilenye uwezo wa kulazawanafunzi wapatao 140. Aidha, chuo kimenunua vifaa vya maabara za Hydraulics na Hydrogeology pamoja na kompyuta 96 kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi kwa kampasi ya Singida na Kampasi kuu Ubungo.

3.2.7 Masuala Mtambuka

(i). Ujenzi wa Majengo Katika Wizara

153. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea na ujenzi wa jengo la Makao Makuu – Mtumba ambao ulianza rasmi tarehe 3 Novemba, 2021 na unagharimu Shilingi bilioni 22.97. Hadi mwezi Aprili 2022, ujenzi umefikia asilimia 33 na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2022. Aidha, Wizara imekamilisha ujenzi wa ofisi za Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini katika miji ya Lindi na Mtwara. Vilevile, Wizara inaendelea na ukarabati na ujenzi wa Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde ambapo Ofisi ya Bonde la Ziwa Nyasa umefikia asilimia 60; Ziwa Rukwa (85); Wami-Ruvu (95); na Rufiji asilimia 63. Kwa upande wa Maabara za Maji, ujenzi wa maabara ya Maji Mtwara na ukarabati wa Maabara ya Dar es salaam umekamilika. Ujenzi wa Maabara ya Morogoro umefikia asilimia 95; Sumbawanga (85); Mbeya (87); na Songea asilimia 60.

(ii). Kuimarisha mifumo ya TEHAMA

  1. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kuboresha huduma zinazotolewa na Sekta. Katika mwaka 2021/22, Wizara kwa   kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imebuni, imesanifu na kutengeneza Mifumo Jumuishi miwili ambayo niMfumo wa Taarifa za Miradi Kiganjani unaofahamika kama Maji Mobile App na Mfumo wa Pamoja wa Kusimamia Huduma za Ankara (Unified Maji Billing System) unaofahamika kama MajiIS. Mfumo wa Taarifa za Miradi Kiganjani unarahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za miradi iliyokamilika na inayoendelea katika kila mkoa pamoja kurahisisha ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maji yote nchini. 
  2. Mheshimiwa Spika, mfumo wa MajiIS umetengenezwa mahususi kwa ajili ya kusimamia ankara za maji zinazotolewa na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini pamoja na Ofisi za Bodi za Maji za Mabonde. Mfumo huo umerahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kuwarahisishia ulipaji nauhakiki wa ankara za maji kulikopelekea kupungua kwa malalamiko yanayohusu ankara za maji katika Mamlaka ambazo zimeanza kutumia mfumo huo. Vilevile, mfumo umepunguza gharama na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ukilinganisha na mifumo iliyokuwa ikitumika awali.
  3. Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili 2022,  jumla ya Mamlaka 68 kati ya 91 za Majisafi na Usafi wa Mazingiara za Miji Mikuu ya Mikoa, Miji ya Wilaya, Miji Midogo pamoja na Miradi ya Kitaifa zimejiunga na zinatumia Mfumo huo. Hii ni sawa na asilimia 74.7 ya Mamlaka zote zinazopaswa kujiunga kwenye Mfumo. Aidha, zoezi la kuunganisha Mamlaka zilizobakia ikiwemo Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) pamoja na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Zanzibar (ZAWA) linaendelea kwa hatua ya mafunzo.

(iii). Mapambano Dhidi ya Rushwa

157. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji wa Awamu ya Tatu (National Anti-Corruption Strategy and Action Plan – NACSAP III) kwa lengo la kupambana na vitendo vya rushwa kwenye maeneo yote ya kazi. Vilevile, Wizara iliunda Kamati ya Uongozi na Usimamizi pamoja na Kamati ya Uadilifu kwa ajili ya kusimamia mapambano dhidi ya rushwa ngazi ya Wizara na Taasisi zake. Tangu kuundwa kwa Kamati hizo, malalamiko dhidi ya viashiria vya rushwa yamepungua kwenye manunuzi ya wakandarasi na huduma zinazotolewa. Aidha,Wizara imeendelea kuzijengea uwezo kamati hizo na kuwafanyia upekuzi watumishi.

(iv). UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza 

158. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza Mwongozo wa UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza kwa kutoa elimu kuhusu magonjwa hayo kwa watumishi wa Wizara na Taasisi zake. Hadi mwezi Aprili, 2022, jumla ya watumishi 3,283 walipata mafunzo maalum kuhusu kujikinga na magonjwa yasioambukiza na yanayoambukiza. Aidha, posho kwa ajili ya kununua lishe bora na usafiri kwa watumishi 21 wanaoishi na virusi vya UKIMWI imeendelea kutolewa.

(v). Jinsia 

159. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha uwepo wa uwiano wa kijinsia katika Taasisi zake. Uwiano huo ni muhimu kwenye vyombo vya maamuzi, usimamizi, uendeshaji na utekelezaji wa miradi nchini.Hadi mwezi Aprili 2022, idadi ya watumishi wanawake ni 2,762 sawa na asilimia 30 ikilinganishwa na wanaume 6,445 sawa na asilimia 70. Aidha, viongozi wa ngazi mbalimbali wa Wizara na Taasisi waliopo wanawake ni 201  sawa na asilimia 24  na wanaume ni  622 sawa na asilimia 76. Vilevile, uteuzi wa kamati mbalimbali huzingatia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha watumishi wote wanashiriki kikamilifu katika kutekeleza majukumu yao. Aidha, katika kuimarisha masuala ya jinsia katika Sekta ya Maji, Wizara imeandaa mkakati wa masuala ya jinsia ambao utatoa mwongozo katika kufikia malengo ya kitaifa ya uwiano wa jinsia wa angalau theluthi moja kwa wanawake.

(vi). Rasilimali Watu katika Sekta ya Maji

  1. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Sekta ya maji inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi, jumla ya watumishi 10,276 wanahitajika ikilinganishwa na watumishi 9,207 waliopo na hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 1,069. Kati ya watumishi waliopo wahandisi (Engineers) ni 704 ambapo 499 sawa na asilimia 70 wamesajiliwa na Bodi ya Usajili ya Wahandisi nchini (Engineers Registration Board – ERB) kama wahandisi wataalam na wahandisi 205 sawa na asilimia 30 wapo kwenye hatua mbalimbali za kusajiliwa. Lengo ni kuona kuwa wahandisi wote wanasajiliwa ndani ya kipindi cha miaka mitatu tangu walipoajiriwa ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maji inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.
  2. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta imeendelea kuwajengea uwezo watumishi wake kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuwapatia mafunzo. Hadi mwezi Aprili 2022, jumla ya watumishi 1,828 wamepata mafunzo ambapo kati yao watumishi 1,650 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi na watumishi 178 walipata mafunzo ya muda mrefu ndani ya nchi.

4.        MAFANIKIO YALIYOPATIKANA

162. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili 2022, Sekta ya Maji imeendelea kufanya maboresho ya kiutendaji na kitaasisi ambayo yameleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara na miradi mbalimbali. Kuimarika kwa ufanisi huo katika Sekta ya Maji kumeleta mafanikio yakiwemo:-

(i).Kuongezeka kwa kiwango cha upatikanaji wa huduma za maji nchini kutoka asilimia 72.3 vijijini na 86 mijini mwaka 2020/21 hadi asilimia 74.5 vijijini na 86.5 mijijni;
(ii).Kukamilika kwajumla ya miradi 343 ya maji ambapo kati ya hiyo ya vijijini  ni miradi 303 na mijini miradi 40. Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na Misungwi,Orkesumet, Chalinze-Mboga, na Longido;
(iii).Kukamilika na kuanza kutumika kwa mfumo wa taarifa za miradi na huduma ya maji ambao utakuwa ukipatikana kupitia simu za kiganjani unaojulikana kwa jina la Maji Mobile Application (Maji_App). Mfumo huoumerahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali za miradi ya maji pamoja na hali ya huduma ya maji nchini;
(iv).Kukamilika na kuanza kutumika mfumo wa pamoja wa Uandaaji wa Ankara za Malipo ya Maji (Unified Billing System) unaosaidia kupunguza malalamiko ya ankara za maji kwa wateja wa huduma za maji; na
(v).Kuimarika kwa usimamizi wa rasilimali za maji kwa kuendelea kutambua, kuweka mipaka na kuhifadhi vyanzo 178 vya maji pamoja na kuandaliwa kwa mipango ya utunzaji wa maeneo ya vidakio vya maji katika mabonde yote nchini.

5.        CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA NA HATUA

ZINAZOCHUKULIWA

163. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana wakati wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2021/22, Wizara imekabiliwa na changamoto mbalimbali. Changamoto hizo na maelezo yake pamoja na hatua zinazochukuliwa kukabiliana nazoni kama ifuatavyo:-

a) Upotevu wa Maji (Non – Revenue Water)

  1. Mheshimiwa Spika, upotevu wa maji umeendelea kuwa changamoto katika Sekta ya Maji na kusababisha hasara kwa Mamlaka za Maji zinazotekeleza na kusimamia miradi ya maji nchini. Katika mwaka 2021/22, hali ya upotevu wa maji nchini imefikia asilimia 36.2 kiwango ambapo kipo juu ya kiwango kinachokubalika kimataifa cha asilimia 20. Hali hiyo kwa sehemu kubwa inasababishwa na uchakavu wa miundombinu ya kusambaza maji; uhujumu wa miundombinu ya maji; pamoja na wizi wa maji kwa kufanya maunganisho yasiyo ya halali kwa kutumia vishoka.  
  1. Katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa maji, Wizara imeendelea kuziwezesha Mamalaka za Maji katika ukarabati na uboreshaji wa miundombinu chakavu ya maji; kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda miundombinu ya maji pamoja na kurekebisha Sheria za Maji ili ziweze kutoa adhabu kali kwa wezi wa maji na wahujumu miundombinu ya maji; kufunga dira za maji zikiwemo dira za malipo ya kabla (pre-paid meters) pamoja na bulk water meters; pamoja na kuanzisha mfumo wa pamoja wa ankara za maji (Unified Billing System) ambao umesaidia kudhibiti upotevu wa maji kwa sababu unamtaka msomaji wa mita kufika na kusoma matumizi halisi ya maji katika mita husika. Vilevile, Serikali ipo katika hatua za awali za kuanza matumizi ya mifumo wa kieletroniki wa kufuatilia taarifa za maji katika mfumo wa usambazaji maji (Supervisory Control and Data Acquisition System – SCADA). Mfumo huo utasaidia kubaini mivujo mapema na kufanya ukarabati hivyo kupunguza maji yanayopotea.

b) Mahitaji makubwa ya fedha kwa ajili ya uwekezaji wa miradi mikubwa ya maji

166. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi mikubwa ya maji ikiwemo ujenzi wa mabwawa makubwa na miradi ya kutoa maji kwenye maziwa kupeleka maeneo mbalimbali,unahitaji kiasi kikubwa cha fedha jambo linalosababisha kuchelewa kuanza utekelezaji wa baadhi ya miradi hiyo ikiwemo bwawa la Kidunda na Farkwa. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali imeendelea kutafuta fedha kutoka vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutumia fedha za ndani kutekeleza miradi mikubwa.

c) Uchelewaji wa upatikanaji wa Misamaha ya Kodi

167. Mheshimiwa Spika, washirika wa maendeleo wameendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya sekta ya maji kwa kufadhili utekelezaji wa miradi ya maji pamoja na misaada ya kitaalam. Aidha, utekelezaji wa miradi mingi ikiwemo inayofadhiliwa na washirika hao imekua ikichelewa kukamilika ndani ya muda uliopangwa kutokana na kuchelewa kutolewa kwa misamaha ya kodi kwa vifaa na mitambo inayotumika katika ujenzi wa miradi husika. Katika kukabiliana na changamoto hiyo Wizara imeendelea kuwasiliana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuweka utaratibu utakaoharakisha upatikanaji wa Misamaha ya Kodi nchini. 

d)        Upungufu wa Wataalam katika Sekta ya Maji

168. Mheshimiwa Spika, sekta ya maji ni sekta inayomgusa kila mwananchi kwa mahitaji ya huduma za kijamii pamoja na uchumi. Kutokana na umuhimu huo, Wizara imeendelea kuchukua hatua zote kuhakikisha huduma ya maji inamfikia mwananchi popote pale alipo nchini. Aidha, utekelezaji wa jukumu hilo unahitaji wataalam wakutosha na wenye weledi katika kutekeleza majukumu yao. Hadi mwezi Aprili 2022, Sekta ina watumishi 9,207 ambapo mahitaji ni watumishi 10,276 hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 1,069. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, kwa mwaka2021/22 Wizara na Taasisi zake kwa ujumla imeajiri watumishi 478. Aidha, Wizara imeendelea kuomba vibali vya ajira kutoka Ofisi ya Rais – UTUMISHI kwa ajili ya kupata wataalam wa kutosha na wenye sifa. Vilevile, Wizara itaendelea kuzihimiza Taasisi zake zenye upungufu wa wataalam kutenga fedha kwa ajili ya kuajiri watumishi.

e)        Mabadiliko ya Tabianchi

169. Mheshimiwa Spika, athari za mabadiliko ya tabianchi zikiwemo ukame, kuchelewa kwa mvua pamoja na mafuriko zimeendelea kuathiri sekta ya maji kutokana na kukauka kwa vyanzo vya maji, kuongezeka kwa migao ya maji pamoja na kuharibika kwa miundombinu ya maji. Katika mwaka 2021/22, athari za mabadiliko ya tabianchi zimedhihirika katika vyanzo vingi vya maji kwa mfano Mto Ruvu ulipungua sana kina cha maji hali iliyosababisha kuchukua hatua za dharura kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Dar es Salaam. Hali hiyo imesababisha migao ya maji, kupungua kwa uzalishaji wa nishati ya umeme na kufa kwa mifugo. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali inaendelea kuhimiza ushiriki wa wananchi katika utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na mazingira. Vilevile, Wizara inaendelea kutekeleza mkakati wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kutekeleza miradi ya maji ambayo itatumia vyanzo vya maji vya uhakika kama vile mito mikubwa na maziwa.

6. VIPAUMBELE NA MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA

MWAKA 2022/23

6.1 Vipumbele vya mwaka 2022/23

170. Mheshimiwa Spika, vipaumbele vya Wizara kwa mwaka 2022/23 ni pamoja na kukamilisha ujenzi, ukarabati na upanuzi wa miradi inayoendelea kutekelezwa; kuanza ujenzi wa mabwawa ya kimkakati ya Kidunda na Farkwa; kuanza ujenzi wa miradi ya maji mipya ikiwemo miradi ya maji katika miji 28; kuendelea na utunzaji wa vyanzo vya maji ikihusisha kutambua, kuweka mipaka na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali ili vyanzo hivyo vilindwe kisheria;  na kutekeleza miradi ya maji kwa kutumia vyanzo vya uhakika ikiwemo maziwa makuu na mito mikubwa.

6.2 Mpango wa Utekelezaji kwa Mwaka 2022/23

  1. Mheshimiwa Spika, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Mpango wa Utekelezaji wa miradi ya maji kwa mwaka 2022/23 umeshirikisha wadau mbalimbali katika kuibua miradi ya kipaumbele wakiwemo Waheshimiwa Wabunge na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Ni matumaini yangu kwamba utaratibu huu utawezesha kufikia malengo ya Sekta ya Maji kwa haraka na uhalisia. Mpango na Bajeti umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Malengo ya Kimataifa ya Maendeleo Endelevu 2016 – 2030, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji, Sera mbalimbali za Kitaifa, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020 – 2025) na Maagizo na ahadi alizozitoa Mheshimiwa Rais na Viongozi wengine wa Kitaifa.
  2. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Serikali imepanga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji; kukamilisha miradi ya maji inayoendelea;kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua hususan kwenye maeneo kame; kuboresha usimamizi na uendeshaji wa huduma ya maji vijijini kwakuimarisha Vyombo vya Utoaji Huduma za Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs); kuongeza uhakika wa uhifadhi wa maji kwa kuimarisha kitengo cha uchimbaji wa visima na ujenzi wa mabwawa; nakuendelea kuweka msisitizo katika usimamizi wa watendaji na wakandarasi. Aidha, mipango imejikita katika maeneo yausimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji; huduma za ubora wa maji; huduma za usambazaji maji na usafi wa mazingira vijijini; huduma za usambazaji majisafi na usafi wa mazingira mijini; na utekelezaji wa kazi mbalimbali katika Taasisi zilizo chini ya Wizara na masuala mtambuka kama ifuatavyo:-

6.2.1 Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za maji

(i) Utunzaji wa Vyanzo vya Maji

173. Mheshimiwa Spika, Sote tunatambua kuwa kilimo; uzalishaji wa nishati ya umeme, malighafi za viwandani; usafirishaji majini; ujenzi na shughuli nyingine kwa sehemu kubwa zinategemea uwepo wa rasilimali za maji za kutosha. Vyanzo vya maji vinamchango mkubwa sana katika uwepo wa rasilimali za maji na usalama wa maji kwa ujumla. Wizara imepanga kuendelea na mikakati ya utunzaji wa vyanzo vya maji ikihusisha kutambua, kuweka mipaka na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali ili vyanzo hivyo vilindwe kisheria. Katika mwaka 2022/23 jumla ya vyanzo 44 vitawekea mipaka na kutangaza katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha kupitia Mipango ya Utunzaji wa Vidakio vya Maji (Catchment Conservation Plans) iliyoandaliwa katika mabonde yote tisa nchini, Wizara iteendelea kuhamasisha utekelezaji wake katika Sekta mbalimbali ili kuwa na matumizi bora ya ardhi na kuimarisha uoto wa asili katika maeneo ya vyanzo vya maji.

              (ii)    Ujenzi wa Mabwawa

174. Mheshimiwa Spika, nchi yetu imebahatika kuwa na vyanzo vingi vya maji vikiwemo maziwa, mito, chemichemi na maji chini ya ardhi. Hata hivyo, mtawanyiko wa vyanzo hivyo hauko sawia. Baadhi ya maeneo yamekuwa na uhaba mkubwa wa maji kutokana ufinyu wa vyanzo na mabadiliko ya tabianchi. Kutokana na  mtawanyiko wa watu, kuna maeneo hayajaweza kufikishiwa huduma ya maji. Katika mwaka 2022/23. Serikali imepanga kujenga mabwawa makubwa ya kimkakati yakiwemo mabwawa ya Kidunda, Farkwa, Lugoda na Songwe. Aidha, Serikali itaanza ujenzi wa bwawa la Kidunda lililochukua muda mrefu kutekelezwa baada yaRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kutoa kibali. Vilevile, Serikali itaanza ujenzi wa bwawa la Farkwa na mtambo wa kutibu maji baada ya kupata fedha za mkopo kiasi cha dola za kimarekani milioni 125.3 sawa natakriban Shilingi bilioni 280 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika. Sambamba na mabwawa makubwa ya kimkakati Serikali imepanga kujenga mabwawa ya ukubwa wa kati 23 hususan kwenye maeneo kame kwa ajili ya uvunaji wa maji ya mvua ili kuongeza uwezo wa nchi kuhifadhi maji na kuyasambaza kwa wananchi wengi zaidi.

(iii) Usimamizi Wa Rasilimali Za Maji

175. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23,Wizara itaendelea kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa takwimu za hali ya rasilimali za maji nchini; kusimamia utoaji wa vibali vya matumizi ya maji na utiririshaji wa majitaka yaliyotibiwa ili kupunguza migogoro na uchafuzi wa vyanzo vya maji; kuratibu uchimbaji wa visima vya maji nchini, kuratibu utekelezaji wa Mipango Shirikishi ya Usimamizi na Uendelezaji wa Rasilimali za Maji pamoja na uendeshaji wa majukwaa ya wadau waSekta ya Maji ambayo yameonesha mchango mkubwa katika utambuzi wa changamoto, kupanga matumizi bora ya maji na upatikanaji wa fedha za usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji. Aidha, Wizara itafanya tafiti za kina kupitia Kituo Mahiri cha Rasilimali za Maji (Water Resources Center of Excellence) ili kuwa na mipango ya muda mrefu ya matumizi endelevu ya maji katika Sekta zote bila kuathiri rasilimali za maji zilizopo.

6.2.2       Usimamizi wa Huduma ya Ubora wa Maji

176. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara itaendelea kuimarisha uhakiki na ufuatiliaji wa ubora wa maji katika vyanzo na mifumo ya usambazaji kwa kukusanya na kuchunguza sampuli 15,000 za maji na sampuli 2,000 za majitaka; kutoa elimu kuhusu viwango vya ubora wa maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali; kuhakiki ubora wa madawa ya kutibu maji kabla ya manunuzi na wakati wa matumizi; kuwezesha uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Usalama wa Maji inayohimili mabadiliko ya tabianchi kwa Mamlaka za

Maji 34 na Vyombo vya Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamiii 100; na kuendelea kuimarisha maabara za ubora wa maji kwa kuzipatia vitendea kazi,kujenga na kukarabati majengo; pamoja nakuziwezesha maabara nne (4) kupata ithibati. 

6.2.3       Huduma ya Majisafi na usafi wa Mazingira Vijijini

177. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara imepanga kutekeleza jumla ya miradi 1,029 ya maji vijijini ambapo miradi 648 ni miradi inayoendelea kutekelezwa na miradi 381 nimipya. Orodha ya miradi ya maji vijijini itakayotekelezwa katika mwaka  2022/23 imeoneshwa kwenye Kiambatisho Na. 4. Aidha, Serikali imepanga kujenga mabwawa 15 katika maeneo mbalimbali ya vijijini. Orodha ya mabwawa yatakayojengwa imeoneshwa kwenye

KiambatishoNa. 5

178. Mheshimiwa Spika, Wizara pia imepanga kuandaa Mpango Kabambe  wa Usafi wa Mazingira Vijijini (Rural Sanitation Master Plan) na kusanifu miradi ya majaribio ya usafi wa mazingira kwenye maeneo mbalimbali nchini. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Oman imepanga kuchimba visima virefu 20 kwenye maeneo ya vijijini katika mikoa ya Dodoma visima vitano (5), Morogoro (5), Pwani (5) na Mkoa wa Singida visima vitano (5). 

(i) Mpango wa Matumizi ya Maji ya Maziwa Makuu

179. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya kandokando ya maziwa makuu wanapata huduma ya majisafi, salama na ya kutosheleza, Serikali imepanga kuanza ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji

48 vinavyozunguka Ziwa Victoria  na Vijiji 37 katika Ziwa Tanganyika

              (ii)    Uendelevu wa Huduma ya Maji Vijijini

180. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha uendelevu wa huduma za maji na usafi wa mazingira katika maeneo ya vijijini, Serikali imepanga kuzingea uwezo CBWSOs 2466 zilizopo na kusajili CBWSOs mpya 704. 

6.2.4       Miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini

181. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23,Wizara imepangakutekeleza jumla ya miradi 175 ya maji mijini.Orodha ya miradi ya majisafi na usafi wa mazingira mijiniitakayotekelezwa katika mwaka 2022/23 imeoneshwa kwenye Kiambatisho Na. 6.

(i) Miradi ya Kimkakati ya Majisafi katika maeneo mbalimbali ya Miji

182. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha malengo ya Kisekta ya kuwapatia wananchi huduma ya maji ya uhakika, Serikali imepanga kutekeleza miradi ya maji kwa  kutumia vyanzo vya maji vya uhakika vya maziwa makuu, mito mikubwa na mabwawa. Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa kutoa maji Mto Ruvuma kupeleka Manispaa ya Mtwara – Mikindani pamoja na vijiji na vitongoji vilivyopo ndani ya kilomita 12 ya bomba kuu; mradi wa kutoa maji mto Kiwira kupeleka Jiji la Mbeya; mradi wa kutoa maji mto Rufiji kupeleka Jiji la Dar es Salaam na maeneo ya Pwani; na mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika Mkoa wa Simiyu utakaotumia maji ya Ziwa Victoria.

(ii)      Mpango wa Kuboresha Huduma ya Majisafi katika Jiji la Dodoma

  1. Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya huduma ya upatikanaji wa huduuma ya maji kwa wananchi wa jiji la Dodoma kutokana na ongezeko kubwa la watu baada ya makao makuu ya Serikali kuhamia Dodoma na ongezeko la  shughuli za kiuchumi na kijamii. Kwa sasa mahitaji ya majisafi katika Jiji la Dodoma yanakadiriwa kuwa ni lita milioni 133.8 kwa siku ambapo uzalishaji kutoka katika vyanzo vyote vya maji ni lita milioni 66.7 kwa siku. Hivyo kuna upungufu wa maji katika jiji la Dodoma wa takribani lita milioni 67.1 kwa siku sawa na asilimia 50.2.
  2. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kutatua changamoto hiyo, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepata mkopo wa Dola za Marekani milioni 125.3 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Bwawa la Farkwa na mtambo wa kusafisha na kutibu maji ambapo ujenzi wake utaanza mwaka wa fedha 2022/23.
  3. Mheshimiwa Spika, katika suluhisho la kudumu la kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dodoma, Serikali inatarajia kutoa maji Ziwa Victoria na kuyafikisha katika Jiji la Dodoma kupitia mji wa Singida. Serikali inaendelea kutafuta fedha vyanzo mbalimbali ili mradi huo uweze kutekelezwa.

6.2.5       Mpango wa Kuimarisha Huduma ya Uondoshaji

Majitaka

186. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Wizara imepanga kuendelea kuboresha huduma ya usafi wa mazingira nchini. Miradi itakayotekelezwa ni pamoja namiradi ya usafi wa mazingira katika miji mikuu 10 ya Vwawa, Kigoma, Lindi, Sumbawanga, Singida, Njombe, Mtwara, Katavi, Tabora na Geita na miji midogo 15 ya Chalinze, Kisarawe, Bagamoyo, Kibaigwa, Igunga, Nzega, Chato, Muleba, Bunda, Mafinga, Ilula, Makambako, Korogwe, Manyoni na Rujewa. Aidha, Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ya usafi wa mazingira katika miji ya Babati, Dodoma, Mbeya, Iringa na Dar es Salaam.

6.2.6       Chuo cha Maji

187. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kukiimarisha na kukitumia Chuo cha Maji kwa ajili ya kutoa wataalam wa maji watakaotumika katika usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji hususan ya vijijini pamoja na kufanya tafiti za kutatua changamoto mbalimbali katika Sekta ya Maji. Katika mwaka 2022/23, Chuo kimepanga kujenga na kukarabati majengo na miundombinu katika kampasi za Dar es Salaam, Mwanza na Singida;kununua magari mawili ya uondoshaji majitaka; kununua mtambo mmoja wa kuchimba visima; kukarabati na kujenga Hostel za wanafunzi; kudahili jumla ya wanafunzi 1,000; kununua vitendea kazi vikiwemo magari na kompyuta; na kuanzisha programu mpya tano ambazo niShahada za Uhandisi wa Usafi wa Mazingira (Sanitation Engineering), Uhandisi wa Haidrolojia (Hydrology Engineering), Haidrojiolojia na Uchimbaji wa Visima (Hydrogeology and Well Drilling), Maendeleo ya Jamii katika Maji na Usafi wa Mazingira (Community Development in Water and Sanitation) pamoja na Stashahada ya Uhandisi wa Usafi wa Mazingira (Diploma inSanitation Engineering).

6.2.7       Masuala Mtambuka

188. MheshimiwaSpika, katika mwaka 2022/23, Wizara itaendelea na mapitio ya Sera ya Maji ya mwaka 2002, kuandaa kanuni na miongozo mbalimbali chini ya Sheria za Maji ili kuhakikisha kuwa sheria za maji zinatekelezwa kikamilifu; kukamilisha marekebisho ya Sheria Na. 11 ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya 2009 kwa lengo la kuimarisha mfumo wa usimamizi wa rasilimali za maji;kuimarisha mifumo ya kielektroniki ili kuleta tija katika Sekta ya Maji; kuanza utekelezaji wa Mkakati wa Jinsia wa Sekta ya Maji;kutoa elimu na kuhamasisha watumishi kuendelea kupima afya zao; na kusambaza vifaa kinga katika vituo vya kazi ili kudhibiti maambukizi ya VVU.

7. SHUKRANI

  1. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwashukuru wadau wote waliochangia kwa namna moja ama nyingine kufanikisha utekelezaji wa shughuli za Sekta ya Maji ikiwa ni pamoja na Nchi Rafiki, Washirika wa Maendeleo, Mashirika ya Misaada ya Kimataifa, taasisi za kiserikali, mashirika ya kidini pamoja na wadau wengine. Kipekee ninapenda kuzishukuru nchi rafiki ambazo zimechangia katika maendeleo ya Sekta ya Maji nchinizikiwemo Uingereza, Ujerumani, India, Marekani,Korea Kusini, Uholanzi, Hispania, Misri, Ufaransa, Kuwait, Ubelgiji, Morocco, Italia na Saudi Arabia. Ninasema ahsanteni sana kwa ushirikiano na misaada ya kifedha na kitaalam mnayoendelea kutupatia katika Sekta ya Maji.
  2. Mheshimiwa Spika, vilevile, ninayashukuru sana mashirika ya maendeleo na Taasisi za kimataifa kwa misaada ya kitaalam na fedha katika kuiwezesha Sekta ya maji kutekeleza majukumu yake. Mashirika na Taasisi hizo ni pamoja na Benki ya Dunia (World Bank-WB), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB), Benki ya Maendeleo ya Ujerumani

(KfW), Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha Mafuta (OPEC Fund for International Development-OFID), Mfuko wa Maendeleo wa

Kuwait (Kuwait Fund),Mfuko wa Maendeleo wa Saudia (SFD),

Foreign, Commonwealth and Development Office (FCDO);  

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Shirika la Maendeleo la Ujerumani(GiZ),Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Global Environment Facility (GEF), Green Climate Fund (GCF), Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Maendeleo la Ubelgiji (BTC), Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) naShirika la Misaada la Marekani (USAID).

  1. Mheshimiwa Spika, ninapenda pia kuyashukuru mashirika na Taasisi za kidini ambazo zimeendelea kusaidia sekta kufikia malengo yake. Mashirika na taasisi hizo pamoja na Catholic Agency for Overseas Aid and Development (CARITAS), Adventist Development Relief Agency (ADRA), Norwegian Church Aid,Livingwater International, World Islamic League, Shirika la Ahmadiya Muslim Jamaat Tanzania,Islamic

Foundation, Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA), Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Kanisa Katoliki Tanzania na Kanisa la Kianglikana Tanzania.

  1. Mheshimiwa Spika, vilevile,ninazishukuruTaasisi zisizo za Kiserikali zinazoshiriki katika kuendeleza Sekta ya Maji. Taasisi hizo ni pamoja na Association of Tanzanian Water Suppliers (ATAWAS), OIKOS, WaterAid, Tanzania Water and Sanitation Network (TAWASANET), Wahamasishaji wa Maji, Maendeleo na Afya (WAMMA),World Vision; Worldwide Fundfor Nature(WWF), Maji na Usafi wa Mazingira (MUM),Netherlands Volunteers Services (SNV), Plan

International, Concern Worldwide, Water Mission (T), Shirika la Kimataifa la Kuhifadhi Uasili na Maliasili (IUCN) na Mashirika mengine mbalimbali.

  1. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee, ninaomba nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Winfried Mahundi (Mb), Naibu Waziri wa Maji; Mhandisi Anthony Damian Sanga, Katibu Mkuu; Mhandisi Nadhifa Sadiki Kemikimba, Naibu Katibu Mkuu; Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Wataalam na Watumishi wote wa Wizara ya Maji; pamoja na Maafisa Watendaji Wakuu na Watumishi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara kwa ushirikiano mkubwa wanaonipatia pamoja na kujituma kwao katika kuhakikisha majukumu ya Wizara ya maji yanatimizwa. Naishukuru familia yangu kwa upendo, ushirikiano na faraja katika kipindi chote na kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu kwa ufanisi. Vilevile, ninatumia fursa hii kuwashukuru wananchi wa jimbo la Pangani kwa kuendelea kunilea nakuniamini katika kutekeleza majukumuyangu na ninaahidi kuendelea kuwa nao bega kwa bega katika kujenga jimbo letu na taifa kwa ujumla.

8.        MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023

  1. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, ninaomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi 709,361,607,000 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/23. Kati ya fedha hizo, Matumizi ya Kawaida ni Shilingi 51,462,269,000 ambapo Shilingi 16,700,534,000 sawa na asilimia 32.45 ni kwa ajili ya kugharamia Matumizi Mengineyo (OC) na Shilingi

34,761,735,000 sawa na asilimia 67.55 ni kwa ajili ya kulipa mishahara (PE) ya watumishi wa Wizara, RUWASA na Chuo cha Maji. Jumla ya bajeti ya maendeleo ni Shilingi 657,899,338,000 ambapo kati ya fedha hizo, Shilingi 407,064,860,000 sawa na asilimia 61.87 ni fedha za ndani na Shilingi 250,834,478,000 sawa na asilimia 38.13 ni fedha za nje.

  1. Mheshimiwa Spika, ninaomba tena kutoa shukrani zangu za dhati kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba hii pia inapatikana katika tovuti ya Wizara www.maji.go.tz
  2. Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja.

VIAMBATISHO

Kiambatisho Na. 1:  Miradi 303 ya Maji Vijijini Iliyokamilika hadi Aprili 2022

NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
1DodomaChemba DCUkarabati wa mradi wa maji kijiji cha Ovada2,449Ovada17
2DodomaChamwinoMradi wa maji kijiji cha suli2,039Suli10
3DodomaChamwinoMradi wa maji kijiji cha Mlebe3,754Mlebe12
4DodomaChamwinoMradi wa maji kijiji cha Malecela2,605Malecela6
5DodomaChamwinoMradi wa maji kijiji cha Chifukulo4,026Chifukulo14
6DodomaMpwapwaUkarabati na upanuzi wa mradi wa maji Chipogoro6,422Chipogoro10
7DodomaMpwapwaUpanuzi wa mradi wa maji Njiapanda945Njiapanda5
8DodomaMpwapwaUkarabati na upanuzi wa mradi wa maji Chitemo6,807Chitemo7
9DodomaKongwaUkarabati wa Mradi wa Maji Kijiji cha Kiteto1,480Kiteto8
10DodomaKondoaConstruction of Pumped Water Project for MONGOROMA Village5,500Mongoroma10
11DodomaMpwapwaConstruction of Iyoma Water supply pumped scheme project5,712Iyoma9
12DodomaKondoa TCUjenzi wa Mradi wa Maji Bolisa2,864BOLISA      & POISI17
13Dodoma Kondoa TCUjenzi wa Mradi wa Maji MWEMBENI2,839MWEMBENI5
14DodomaMpwapwa DCUjenzi             wa             mradi maji Iramba1,223Iramba5
Jumla Dodoma1448,665 135
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
15GeitaBukombe DCUjenzi wa Mradi wa Maji Nampalahala4,856Nampalahala8
16GEITANyang’whale DCUkarabati wa visima virefu vijiji vya Nyamikonze, Nyang’hwale, Nyabulanda, Mwasabuka na Lubanzo1,500Nyamikonze (Iyenze), Nyang’hwale, Nyabulanda, Mwasabuka na Lubando (Kaboha)5
17GeitaBukombeUjenzi wa Mradi wa Maji Buganzu3,504Buganzu8
18GeitaBukombeUjenzi wa Mradi wa Maji Ng’anzo5,188Ng’anzo12
19GeitaChatoUjenzi wa Mradi wa Maji Buziku6,000Buziku, Majengo, Luantaba24
20GeitaGeitaUjenzi wa Mradi wa Maji Njia Panda1,500Njia Panda6
21GeitaGeitaUjenzi wa Mradi wa Maji Wigembya950Wigembya4
22GeitaGeitaUjenzi wa Mradi wa Maji Manga2,000Manga7
23GeitaMbogweUjenzi wa Mradi wa Maji Nanda3,636Nanda18
24GeitaNyang’hwaleUkarabati wa Mradi wa Maji Nyang’hwale3,500Ibambila, Kaseme14
Jumla Geita1032,634 106
25IringaMufindiMradi wa Maji Ikweha2,428Ikweha20
26IringaMufindiMradi wa Maji Nyigo2,534Nyigo22
27IringaMufindiMradi wa Maji Ukami3,027Ukami44
28IringaMufindiMradi wa Maji Ikimilinzowo2,863Ikimilinzowo50
29IringaMufindiMradi wa Maji Lulanda1,470Lulanda16
30IringaIringaMradi wa Maji Mafuluto2,359Mafuluto38
31IringaIringaMradi wa maji Mkumbwanyi1,495Mkumbwanyi8
32IringaKiloloMradi wa Maji Image3,253Image16
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
33IringaKiloloMradi wa Maji Mawambala4,187Mawamala6
34IringaKiloloMradi wa Maji Mtandika3,533Mtandika4
35IringaMufindiNyololo water Supply project8,400Nyololo, Njiapanda19
Jumla Iringa1135,549 243
36KageraBiharamuloKufunga umeme katika chanzo cha maji Nyakanazi Kizota5359Nyakanazi60
37KageraBiharamuloConstruction of Storage tank 50m3 at Kabukome village3,261Kabukome4
38KageraMuleba Extension of Bulyakashaju w/s to Kizinga village4,235Kizinga16
39KageraMuleba Extension of Itunzi W/S1,628Itunzi8
40KageraMuleba Extension of Ilogero W/S3,880Kafunjo12
41KageraMuleba Extension of Izigo water supply1,724Bushumba, Bwarushanje16
42KageraMuleba Extension of Katembe w/s to Nyakabango Village3,725Nyakabango16
43KageraMuleba Rehabilitaion of Kasharunga W/S13878Kasharunga72
44KageraMuleba Rehabilitation of10 shallow wells2,250Rwigembe, Bisheke, Ihangilo, Muyenje9
45KageraBukobaBituntu4,250Bituntu17
46KageraBiharamulo DCMradi wa maji Nyamalagala4,860Nyamalagala/K ikoma5
47KageraBiharamulo DCMradi wa maji Kabindi18,300Kabindi, Chebitoke, Kikomakoma na Rukora7
48KageraBiharamulo DCMradi wa maji Kabukome3,243Kabukome4
49KageraBiharamulo DCMradi wa maji Nyantakala6,101Nyantakala6
50KageraBiharamuloMradi wa maji5,236Runazi6
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
  DCRunazi   
Jumla Kagera1581,930 258
51KataviNsimboUjenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Mtakuja/Songambele3,234Mtakuja      & Songambele13
52KataviNsimboUjenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Katisunga2,214Katisunga6
53KataviMleleUjenzi wa mradi wa maji MajimotoIkulwe-Luchima9,125Ikulwe       na Luchima20
54KataviMpimbweKasima Water Supply1,340KanindiKasima4
Jumla Katavi415,913 43
55KigomaBuhigwe DCUjenzi wa Mradi wa Maji Munanila Phase 18,103Munanila10
56KigomaBuhigwe DCUjenzi wa Mradi wa Maji Munyegera9,834Munyegera24
57KigomaBuhigwe DCUjenzi wa Mradi wa Maji Kimara/Kinazi12,412Kimara       & Kinazi12
58KigomaBuhigwe DCUjenzi wa mradi wa Maji Bulimanyi and Nyamgali6,198Bulimanyi/Nya mgali32
59KigomaBuhigwe DCMaboresho ya mradi wa maji Songambele5,116Songambele0
60KigomaKakonko DCUkarabati wa mradi wa Maji Muhange8,731Muhange0
61KigomaKakonko DCMradi wa Maji Kewe4,319Kewe&Nkuba10
62KigomaKasulu DCMradi wa Maji Kitanga20,932Kitanga36
63KigomaKasulu DCUchimbaji wa visima vierefu vijiji vya Kagerankanda, Rusesa, Makere na Asantenyerere Kagerankanda, Rusesa, Makere     na Asantenyerere 
64KigomaKasulu DCUkarabati wa mradi wa maji Kwaga9,532Kwaga0
65KigomaKasulu DCUkarabati wa mradi wa maji Kalela9,532Kalela0
66KigomaKasulu DCUjenzi wa mradi wa maji Mvinza6,368Mvinza40
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
67KigomaKasulu DCUjenzi wa mradi wa maji Kurugongo/Migunga5,269Kurugongo, Migunga40
68KigomaKasulu TCUchimbaji wa visima virefu 6 katika vijiji vya Hwazi, Juhudi, Mdyanda, Kinkati and Kabanga Hwazi, Juhudi, Mdyanda, Kinkati, Kabanga and Makere0
69KigomaKibondo DCUjenzi wa mradi wa maji Buyezi6,434Buyezi22
70KigomaKibondo DCUjenzi wa mradi wa Maji kijiji cha Mukabuye9,765Mukabuye56
71KigomaKibondo DCUjenzi wa mradi wa maji Samvura/Bunyambo8,039Samvura, Bunyambo20
72KigomaKakonkoUjenzi wa mradi wa maji Nyabibuye6,738Nyabibuye19
Jumla Kigoma 18137,322 321
73KilimanjaroSameHedaru water Suppy Project & Kizungo18,600Hedaru     na Kizungo0
74KilimanjaroSameHedaru project Mabilioni water Supply Project1,757Mabilioni0
75KilimanjaroHaiImprovement of Losaa-Kia water supply scheme34,675Sanya Station, Mtakuja, Mungushi, Chemka, Kia, Tindigani, Chemka0
76KilimanjaroHaiExtension of LosaaKia water supply scheme1,350Sanya Station, Mtakuja2
77KilimanjaroHaiImprovement of Machame Water Supply Scheme33,000Foo,      Wari, Uduru, Nshara, Nkuundoo0
78KilimanjaroHaiRehabilitation of Machame Water Supply2,525Foo,      Wari, Uduru, Nshara, Nkuundoo0
79KilimanjaroHaiExtension of Lyamungo/Umbwe water Supply Scheme1,350Kilanya, Kwatito   and Chekimaji5
80KilimanjaroHaiExtension of Uroki- Bomang’ombe water4,723Muungano0
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   Supply Scheme   
81KilimanjaroHaiExtension of UrokiBomang’ombe water Supply Scheme3,200Muungano0
82KilimanjaroHaiExtension of UrokiBomang’ombe water Supply Scheme2,376Kwa Sadala0
83KilimanjaroHaiExtension of UrokiBomang’ombe water Supply Scheme210Relai1
84KilimanjaroRomboExtension of Mrike Water Supply Project2,857Mrike6
85KilimanjaroMwanga DCKifaru WS Project6,304Kifaru and Tingatinga Kitopeni5
86KilimanjaroMwanga DCSongoa WS Project523Songoa4
87KilimanjaroMwanga DCMbore WS Project326Mbore5
88KilimanjaroMwanga DCChanjale WS Project863Chanjale10
89KilimanjaroMwanga DCExtension from Kyanga water storage tank to Simbomu1,764Simbomu16
90KilimanjaroMwanga DCRuru WS Project589Ruru and Mkisha10
91KilimanjaroMwanga DCVulue WS Project558Vuchamangofi and Mangio12
92KilimanjaroMwanga DCExtension of Kisanjuni water supply scheme to Mriti1,548Mriti10
93KilimanjaroMwanga DCRehabilitation of mbale – kisombogho – kwa sedudu line476Mbale 
94KilimanjaroMwanga DCRehabilitation of Mruma WS814Mruma6
95KilimanjaroMwanga DCExtension of Msaleni Sachi WS680Msaleni6
96KilimanjaroMwanga DCExtension of Jipe Makuyuni WS project1,515Kambi ya Simba and Jipe0
97KilimanjaroMoshi DcRehabilitation of Unamkolowany water supply scheme9,065Komakundi, Kotela, Kokirie and Mboni25
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
98KilimanjaroMoshi DcRehabilitation of Singa water supply scheme1,561Singa9
99KilimanjaroMoshi DcExtension of Soko to Ko chakindo1,835Soko and Kochakindo3
Jumla Kilimanjaro27135,044 135
100LindiLindiUpanuzi wa Mradi wa Maji Chiwewerere1,559Chiwerere10
101LindiLindiUboreshaji wa Mradi wa maji Kitohavi513Kitohavi4
102LindiLindiUpanuzi wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Nagiriki.447Nagiriki4
103LindiLindiUjenzi wa Mradi wa Maji katika vijiji vya Namupa, Muungano na Mahiwa4,386Namupa, Muungano na Mahiwa46
104LindiLindiUboreshaji na upanuzi wa Mradi wa Maji Narwadi600Narwadi6
105LindiLiwaleMradi wa maji Nyera726Nyera4
106LindiLiwaleMradi wa maji Mkundi998Mkundi4
107LindiLiwaleMradi wa maji Lilombe1,160Lilombe4
108LindiKilwaUpanuzi wa mradi wa maji pande ploti kuhudumu kijiji cha mtitimila1,015mtitimila5
109LindiKilwaUkarabati wa mradi wa maji kipatimu4,167kipatimu22
110LindiKilwaUpanuzi wa mradi wa maji Njinjo2,884Njinjo6
111LindiKilwaUkarabati wa mradi wa maji kiranjeranje4,870kiranjeranje20
112LindiKilwaukarabati wa mradi wa maji mtumbei mpopera2,154mtumbei mpopera6
113LindiRuangwa DCMradi wa maji Mtimbo616Mtimbo1
114Lindi Mradi wa maji Namienje584Namienje3
Jumla Lindi1526,679 145
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
115ManyaraMbuluKuongeza mtandao wa maji Mradi wa maji Bargish Antsi2,112Bargish Antsi6
116ManyaraMbuluKuongeza mtandao wa maji Mradi wa maji Imboru – Isale2,250Imboru – Isale4
117ManyaraHanang’Mradi wa maji Gidagharb2,259Gidagharb2
118ManyaraHanang’Mradi wa maji Dawar        4,748Dawar12
119ManyaraKitetoMradi wa maji Sunya        1,000Sunya6
120ManyaraKitetoMradi wa maji Wezamtima2,500Wezamtima10
121ManyaraKitetoMradi wa maji Ndirigish3,000Ndirigish6
122ManyaraSimanjiroMradi wa maji Terrat Longwswan2,487Terrat Longwswan14
123ManyaraBabatiMradi wa maji Madunga4,952Madunga12
124ManyaraBabatiMradi wa maji Kisangaji- Shaurimoyo, Madunga-giding’wari and Mawemairo.8,000Kisangaji- Shaurimoyo, Madunga- giding’wari and Mawemairo.26
125ManyaraBabatiMradi wa maji Tsamas4,500Tsamas40
126ManyaraBabatiMradi wa maji Sangara3,930Sangara8
127ManyaraBabatiMradi wa maji Gidabaghar2,872Gidabaghar14
Jumla Manyara1344,610160
128MaraBunda DCUjenzi wa mradi wa maji Bukama2,172Bukama28
129MaraBunda DCUkrabati wa mradi wa maji Mukune10,062Mariwanda & Sanzate10
130MaraBunda DCUpanuzi wa mradi wa Kyandege naTingirima 5,472Kyandege & Tingirima12
131MaraBunda DCUjenzi wa mradi wa f Nyamuswa/Salama kati 5,013Makongoro A’ & Makongoro B’34
132MaraMusomaMradi wa maji Buanga4,032Buanga14
133MaraMusomaMradi wa maji Butata/Kastamu7,400Butata, Kastamu32
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
134MaraRoryaUkarabati wa Mradi wa maji Nyanduga3,607Nyanduga12
135MaraRoryaMradi wa maji Nyarombo2914Nyarombo15
136MaraRoryaMradi wa maji Nyambori3334Nyambori15
137MaraRoryaUkarabati wa mradi wa mai MarasiboraNyanchabakenye12,005Marasibora, Nyanchabaken ye16
138MaraRoryaUkarabati wa Mradi wa Nyasonga, Nyamagongo11,976Nyasonga, Nyamagongo13
139MaraRoryaMradi wa maji Ngópe3097Ngópe9
140MaraBundaMradi wa maji Nyatwali3250Nyantwali7
Jumla Mara1374,334 217
141MbeyaChunyaMradi wa maji Makongolosi25,000Makongolosi, TRM, Tankin, Sokoni, Umoja, Kalungu, Manyanya, Kilombero, Machinjioni, Zahanati, Mkuyuni, mwaoga             kati, songambele, mpogoloni, bwawani, mianzini, Raiway, Kipoka, Maendeleo,Uh uru na kitete20
142MbeyaKyelaMradi wa Maji Mababu5,121Mababu32
143MbeyaKyelaMradi wa Maji Kilombero1,676Kilombero14
144MbeyaKyelaMradi wa Maji Makwale3,750Mahenge, Mpunguti, Ngeleka, Ndobo, Isuba, Sebe, Bwato and Mpegele20
145MbeyaRungweMradi wa maji1,482Kilimansanga10
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   Kilimansanga   
146MbeyaChunya DCMradi wa maji Ifumbo7,548Ifumbo49
147Mbeya Mradi wa maji Chalangwa15,039Chalangwa, Isewe, Itumba na Mbugani55
148MbeyaKyela DCExtension of pipe network from Matema gravity scheme up to Matema village and Kilombero village1,368Matema   and Kilombero14
Jumla Mbeya860,984 214
149MorogoroMvomero DCUjenzi wa mradi wa Maji Lubungo2,016Lubungo32
150MorogoroMlimba DCUpanuzi wa mradi wa maji Mang’ula1,948Msalise16
Jumla Morogoro23,964 48
151MtwaraNanyamba TCUjenzi wa mradi wa maji Nanyamba mjini18,603  Chitondola, Kilimanjaro, Mibobo, Natoto, Namkuku, Dinyecha, Nanyamba,Madi na,Nanyamba B,Namayanda,29
152MtwaraMtwara DCUkarabati wa mradi wa Maji Minyembe1,356Minyembe16
153MtwaraMtwara DCUjenzi wa mradi wa maji Namanjele – Njumbuli2,611Namanjele na Njumbuli22
154MtwaraMtwara DCUkarabati wa mradi wa maji Ndumbwe3,910Ndumbwe8
155MtwaraTandahimba DCMradi wa maji mji mdogo wa Tandahimba Mjini4,474Tandahimba6
156MtwaraMasasi DCUendelezaji wa mradi wa maji Nanganga hadi Mumburu2,569Mumburu2
157MtwaraNewala DCMradi wa Maji Mchemo4,636Mchemo -A, Mchemo-B na Mchedebwa10
158MtwaraNewala DCMradi wa Maji Chiule         705Chiule4
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
159MtwaraNewala DCMradi wa Maji Mtongwele Chini4,244Mtongwele Chini, Kadengwa na Maputi10
160MtwaraNanyamba TCMradi wa Maji Kiromba6,180kiromba chini5
161MtwaraMtwara DCMradi wa Maji Chemchem4,628Lilido, Nakada na Chemchem8
162MtwaraNanyumbu DCMradi wa maji Nangomba- Mjimwema4,620Nangomba na Mjimwema11
Jumla Mtwara1258,536 131
163MwanzaKwimbaBugunga3,204Bugunga12
164MwanzaKwimbaKiliwi5,473Kiliwi14
165MwanzaMaguYichobela6,500Yichobela26
166MwanzaMisungwiIlalambogo4,500Ilalambogo18
167MwanzaSengeremaKasomeko2,250Kasomeko10
168MwanzaBuchosaKamisa2,250Kamisa12
Jumla Mwanza624,177 92
169NjombeNjombe TCConstruction of gravity scheme Lugenge-KisiloUtalingolo LOT1–   Bomba Kuu (0)0
170NjombeNjombe TCConstruction of gravity scheme Lugenge-KisiloUtalingolo  LOT34,209Kisilo, Ihalula na Utalingolo (3)36
171NjombeNjombe DCRehabilitation of water supply infrastructure at Ikondo village(Intake, Tank, Gravity main, Pump and water points)4,095Ikondo (1)40
172NjombeMakete Extension of Tandala watar supply Project (Replacement of Rehabilitation of Ikonda water supply project)1,250Tandala (1)5
173NjombeMakete Construction new intake and gravity482Imehe (1)2
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   main (900m long), and 4 DPs for Imehe water supply project   
174NjombeNjombe DCRehabilitation of Isoliwaya water supply scheme1,847Isoliwaya17
175NjombeNjombe TCRehabilitation of water supply infrastructer at Kifanya village (Tanks and domestic points)6,709Kifanya15
176NjombeMakambako TCRehabilitation of Mawande & Utengule Intake4,207Mawande na Utengule 0
177NjombeNjombe TCImprovement of water suply service at Iduchu Village.1,494Iduchu11
178NjombeMakete DCRehabilitation of Intake,  construction of 3DPs and fence for S/T and Intake at Ipelele Water supply project 3,722Ipelele3
179NjombeMakete DCImprovement of gravity main and construction of S/T(25m3) and 2 DPs for Usagatikwa water supply project710Usagatikwa2
180NjombeMakete DCConstruction of Storage tank (25m3) and 2 DPs for Lugoda water supply project737Lugoda2
181NjombeMakete DCConstruction of storage tank (25m3) and Fences for Tank and Intake of Mlondwe (Masoli) water supply project1,091Mlondwe0
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
Jumla Njombe1330,553 133
182PwaniBagamoyoMradi wa Maji Mandawe2,136Mandawe3
183PwaniBagamoyoMradi wa Maji Mlingotini565mlingotini3
184PwaniChalinzeMradi wa Maji Matuli/Mdaula850matuli&mdaula4
185PwaniChalinzeMradi wa Maji Kwamduma/kwediu we1,426Kwamduma/kw ediuwe4
186PwaniRufiji DCRehabilitation of Msona Water Supply Scheme980Msona5
187PwaniRufiji DCRehabilitation of Mohoro Water Supply Scheme17,010Mohoro Magharibi, Mohoro Mashariki, Shela and King’ongo19
188PwaniRufiji DCRehabilitation of Mtanza Water Supply Project980Mtanza10
189PwaniRufiji DCRehabilitation of Utete Water Supply Scheme15,982UteteHC
190PwaniRufiji DCRehabilitation of Kilimani Water Supply Scheme 4298Kilimani Mashariki na Kilimani Magharibi10
191PwaniRufiji DCRehabilitation of Ruwe Water Supply Scheme3,999Ruwe10
192PwaniRufiji DCRehabilitation of Nyaminywili Water Supply Scheme2,573Nyaminywili10
193PwaniRufiji DCRehabilitation of Mtanza Water Supply Project980Mtanza10
194PwaniMkurangaUjenzi wa mradi wa maji Msorwa760Msorwa7
195PwaniMkurangaUkarabati wa mradi wa maji Mvuleni- Kilimahewa Kusini4,000Mvuleni & Kilimahewa Kusini14
196PwaniMafiaUpanuzi wa skimu ya maji Kijiji cha502Bweni vitongoji vya Saadani2
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   BWENI na Mchani/Kilakilo 
197PwaniKisaraweChole water supply Scheme2,689Chole13
198PwaniKisarawe Mradi wa Maji Boga – Mengwa. 3,491.00Boga na Mengwa16
199PwaniKibaha DcMpiji3,000Mpiji8
200PwaniMkuranga Construction of Mdimni Water Supply Project1,551Mdimni, Nganje16
201PwaniKibitiNyamisati Water Supply Project2,737Nyamisati10
202PwaniKibitiMiwaga/Ngulakula Water Supply Project1,744Miwaga, Ngulakula12
Jumla Pwani2172,253 186
203RukwaSumbawangaConstruction of Kasekela-Msila Gravity Water Supply Project4,690Kipenzi   Sub Village14
204RukwaNkasiMradi wa maji Kirando74,483Mtakuja, Shaurimoyo, Kamwanda, Itete, Chongo katete, Kichangani100
205RukwaSumbawanga DCMradi wa Maji Kizungu1,931Kizungu10
206RukwaSumbawanga DCUjenzi wa Bomba kuu mradi wa Laela23,729Mji wa Laela33
207RukwaSumbawanga DCMradi wa Maji Nkankanga24,000Nankanga & Nankanga C10
208RukwaSumbawanga DCUpanuzi wa Mradi wa Maji Milepa3,990Milepa10
209RukwaSumbawanga DCUjenzi wa Mradi wa maji Kisa6,280Kisa & Talanda22
210RukwaSumbawanga DCUpanuzi Mradi wa Maji Mtowisa14,890Mtowisa A&, Ng’ongo and Santoukia14
211RukwaNkasi DCUjenzi wa Mradi wa Maji Kisula7,850Kisula9
212RukwaNkasi DCUkarabati na Upanuzi Mradi wa Maji Kantawa4,918Kantawa7
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
213RukwaNkasi DCUkarabati na Upanuzi Mradi wa Maji Ntatumbila2,836Ntatumbila9
214RukwaNkasi DCUkarabati na upanuzi Mradi wa Maji Kate/Chonga13,714Chonga14
215RukwaKalambo DCMradi wa Maji Mambwekenya2,813Mambwekenya21
216RukwaKalambo DCMradi wa Maji Katete3,116Katete9
217RukwaKalambo DCMradi wa Maji Sopa3,440Sopa15
218RukwaKalambo DCMradi wa Maji Myunga6,280Myunga      & Mpanzi20
219RukwaKalambo DCUkarabati na Upanuzi Mradi wa Maji Kilesha16,851Kilesha, Itekesha, Ilango, Kifone& Kambo33
220RukwaKalambo DCUkarabati na upanuzi Mradi wa Maji singiwe5,968Singiwe23
Jumla Rukwa18221,779 373
221RuvumaSongeaMradi wa maji Mtiririko MpingiKikunja5,852Mpingi       na kikunja (2)48
222RuvumaSongeaMradi wa maji Mtiririko Namatuhi5,652Namatuhi (1)10
223RuvumaSongeaMradi wa maji Mtiririko Liganga5,620Liganga (1)42
224RuvumaSongeaMradi wa Maji Ndongosi3,175Ndongosi (1)30
225RuvumaMadabaMradi wa maji  Wino1,550Wino(2)40
226RuvumaMadabaMradi wa maji Mtiririko Madaba12,372Madaba (1)82
227RuvumaMadabaMradi wa maji Igawisenga2,528Igawisenga (1)36
228RuvumaSongea MCMradi wa maji Mtiririko Ndilimalitembo1,937Ndilimalitembo20
229RuvumaNyasaLikwilu water supply  scheme1,768Likwilu9
230RuvumaTunduru DCUkarabati Mradi wa maji Mbati25,000Mbati20
Jumla Ruvuma1065,454 337
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
231ShinyangaMsalala DCExtension of kagongwa – Isaka water supply scheme at Banhi Village.4,446Banhi5
232ShinyangaMsalala DCCompletion of construction of the transmission main from Mhangu to Ilogi.16,370Ilogi15
233ShinyangaMsalala DCConstruction of Kabondo and Mwakuzuka Water Supply.5,245Kabondo           and Mwakuzuka9
234ShinyangaUshetu DCConstruction of water supply scheme at Nyankende Village6,198Nyankende13
235ShinyangaUshetu DCConstruction of Piped Water Supply Scheme at Kisuke Village.4,549Kisuke7
236ShinyangaKahama TCExtension of Water piped schemes at Nyashimbi4,703Nyashimbi 4
237ShinyangaShinyanga DCRehabilitation of Mwamashele water supply project2,274Mwamashele7
238ShinyangaShinyanga DCConstruction of Water Supply transmission main from Kizumbi to Masengwa 200m3 storage tank –   Masengwa, Ikonda, ilobashi, Ibingo, Isela, Ishinabulandi, Idodoma, Ng’wamakalang a, Mwamala B, Ibanza, Bugogo,Bunong a and Bubale0  
239ShinyangaShinyanga DCRehabilitation of Kadoto water supply project2,999Kadoto10
240ShinyangaShinyanga DCExtension of Lake Victoria Project to Buduhe Village2,999Buduhe10
Jumla Shinyanga1049,783 80
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
241SimiyuBariadiGuduwi Piped Water Supply Project2,500Guduwi12
242SimiyuBariadiNtuzu Piped Water Supply Project2331Shimbale, Isanga      na Busulwa9
243SimiyuBariadiGambosi Piped Water Supply Project1500Gambosi4
244SimiyuBariadiUnunuzi wa pampu na ujenzi wa visima 6516250Mwadobana, Mwamoto, Mwamondi, Miswaki, Mwabadimu, Nkindwabiye, Ngara, Mwauchumu, Ibulyu, Bulumbaka, Ihusi, Banhemi, Ikungulyabasha shi, Zinna, Mbaranga, Mwambarange, Salalia, Gibishi, Ikungulyandili, Ihula, Gasuma, Mwaubingi, Ikinabushu, Mwamlapa, Kasoli, Matale, Gagabali, Gamihusi, Mkuyuni, Ngogote, Mwaumataondo , Songambele, Matongo65
245SimiyuBusegaUkarabati na upanuzi wa mradi wa maji Mwamanyili8300Mwamanyili, Mwanangi, Nassa Ginnery5
246SimiyuBusega Ujenzi wa mradi wa maji Mwabayanda3200Mwabayanda9
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
247SimiyuMaswaSeng’wa Piped Water Supply Project1,500Seng’wa6
248SimiyuMaswaUjenzi wa mradi wa Maji Gumari1911Gumari4
249SimiyuMaswaUpanuzi wa mradi wa Maji Kidema3159Kidema4
250SimiyuMaswaUjenzi wa mradi wa Maji Mwang’onholi4538Mwang’onholi6
251Simiyu MaswaUjenzi wa mradi wa Maji Ngulinguli- Mwamanenge7020Ngulinguli, Mwamanenge22
252SimiyuMeatuUjenzi wa mradi Mwaukoli4500Mwaukoli5
Jumla Simiyu1256,709 151
253SingidaIramba DCMradi wa maji Kijiji cha Songambele6,370Songambele20
254SingidaIramba DCMradi wa maji Kijiji cha Mgela2,560Mgela10
255SingidaIramba DCMradi wa maji Kijiji cha Kyalosangi3,992Kyalosangi10
256SingidaIramba DCMradi wa maji Kijiji cha Ujungu6,089Ujungu24
257SingidaManyoni DcMradi wa maji wa Kijiji cha Kitopeni5,867Kitopeni26
258SingidaManyoni DcExpansion of Sanza/Ntope water project to provide service to Sanza villlage.9,588Sanza & Ntope22
259SingidaManyoni DcMradi wa maji wa Kijiji cha Kinyika2,261Kinyika – 18
260SingidaIkungi DCMradi wa maji Dung’unyi4,829Dung’unyi & Munkinya7
261SingidaIkungi DCMradi wa maji Ulyampiti2,755Ulyampiti7
Jumla Singida944,311 134
262SongweMomba DCMradi wa Maji Mkulwe3,624Mkulwe22
Jumla Songwe13,624 22
263TaboraIgungaUjenzi wa mradi wa Maguguni2,053Maguguni7
264TaboraSikongeUjenzi wa mradi wa maji Msuva3,000Msuva6
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
265TaboraUyui DCMradi wa uboreshaji wa visima vinne kwenda mtandao wa maji kwa vijiji vya Ufuluma- Iyogelo,UfulumaChali,Kizengi, Lutende1,176Ufuluma-Chali na Ufuluma – Iyogelo4
266TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Mwamala kwa mwaka 2020/20212,634Mwamala56
267TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Mogwa3,024Mogwa7
268TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Kayombo kwa mwaka 2020/20212,774Kayombo8
269TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Iboja-Sigili kwa mwaka 2020/20216,005Iboja-Sigili17
270TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Ubinga kwa mwaka 2020/20212,966Ubinga12
271TaboraNzega DCMradi wa Maji ya bomba Kijiji cha Lakuyi-Sagida kwa mwaka 2020/20213,923Lakuyi13
272TaboraNzega DCUjenzi wa Mradi wa maji  Mwamayunga .2,768Mwamayunga36
273TaboraKaliua DCUjenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Ushokola2,700Ushokola10
274TaboraKaliua DCUjenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji cha Imalampaka1,179Imalampaka4
275TaboraKaliua DCUjenzi wa Mradi wa Maji katika kijiji vya Wachawaseme,Mta kuja Magharibi na Mtakuja Mashariki3,920Wachawaseme, Mtakuja Magharibi, Mtakuja Mashariki15
276TaboraKaliua DCUjenzi wa mradi wa7,179Kanoge/7
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   Maji katika Vijiji vya Kanoge na Ichemba Ichemba 
Jumla Tabora1445,301 202
277TangaKorogwe DCMradi wa maji Lusanga4,164(3) Lusanga, Shamba kapori na Ngomeni20
278TangaKorogwe DCMradi wa Maji Mng’aza1,233Mng’aza7
279TangaKorogwe DCMradi wa maji Kwalukonge3,114(1) Magamba kwalukonge0
280TangaKorogwe DCMradi wa maji Kwemgunga345Sharaka4
281TangaKorogwe DCMradi wa maji Kikwazu1493M/Shamba8
282TangaKorogwe DCUkarabati wa Mradi wa maji Magundi2,346Magundi na kweungo20
283TangaMuhezaUjenzi wa mradi wa maji kijiji cha Magula856Magula8
284TangaMuhezaUkarabati wa mradi wa maji Kigongomawe na upanuzi wa mradi wa maji Mpapayu6,249Kigongomawe, Mpapyu na Kwenyefu6
285TangaMuhezaUkarabati wa mradi wa maji Shebomeza1,678Shebomeza12
286TangaMuhezaUjenzi wa Mradi wa maji Kwemdimu1,680Kwemdimu12
287TangaKilindi Mradi wa  Maji  Jungu/Balang’a3,692(3) Jungu,  Balang’a na  Lekitinge19
288TangaHandeni DCUjenzi wa Tangi la 500M319,069Mkata Mashariki na Mkata maghari          0
289TangaHandeni DCUjenzi wa mradi wa maji Malezi3312Kilimilang’ombe and Malezi12
290TangaHandeni DCUjenzi wa mradi wa maji Kwandugwa3,237Kwandugwa17
291TangaHandeni DCUchimbaji wa Visima virefu 14 katika vijiji vya Kangata, Gole, Kwa magome, Kwaluwala9,719kangata,gole kwa magome,kwalu wala na Mbamba 0
NaMkoaHalmashauriJina la MradiIdadi ya wanufaikaMajina na idadi ya Vijiji vinavyonufaikaIdadi ya vituo vya Kuchota Maji
   Msaje,Changalikwa, Konje,Msomera,Mba ngwi,Kibaya . Kwanyanje, Hoza, Misima  na Mbamba   
292TangaPangani DCMradi wa Maji Masaika2,876Masaika13
293TangaPangani DCUjenzi wa Mradi wa maji Mikocheni1,212Mikocheni12
294TangaPangani DCUjenzi wa Mradi wa maji Mbulizaga2,200Mbulizaga12
295TangaPangani DCUjenzi wa Mradi wa maji Msaraza1,482Msaraza10
296TangaPangani DCUchimbaji wa Visima Madang ana Jaira Madanga  na Jaira0
297TangaMkingaUkarabati wa mradi wa maji Magati9,768Magati, Kiumbo, Mwanyumba, Mbambakofi na Mtakuja        10  
298TangaMkingaUkarabati wa Mradi wa maji Daluni Kisiwani2,925Kisiwani A and Kisiwani B        12
299TangaMkingaUpanuzi wa Mrdi wa maji Bwiti Mavovo4,897Bwiti           and Mavovo1
300TangaMkingaUpanuzi wa Mradi wa maji Duga Maforoni-Horohoro1,954Horohoro3
301TangaLushoto DC Ujenzi wa Mradi wa Maji Kwemashai 1,728Kwemashai18
302TangaLushoto DC Ujenzi wa Mradi wa Maji Shaghayu2,314Shaghayu30
303TangaLushoto DCUkarabati wa Mradi wa Maji Mbaramo 3,456Mbaramo15
Jumla Tanga2796,999 281
Jumla KUU ya Miradi3031,467,107 4,147

Kiambatisho Na.2: Miradi 127 iliyokuwa na Changamoto za muda mrefu na kupatiwa ufumbuzi

NaMkoaWilayaJina la MradiGharama za kutekeleza mradiMwaka Mradi ulipojengwaGharama za kutekeleza mradi
 
1ArushaKaratuMradi wa maji wa kusukumwa wa Matala124,000,0002018204,000,000.0 0  
2ArushaKaratuUjenzi wa bwawa katika kijiji cha Lemoot82,000,000 201482,000,000 
3ArushaKaratuGetamock 14,955,000 201414,955,000 
4ArushaKaratuKansay150,000,000 2014150,000,000 
5ArushaNgorongoroSoitsambu- Njoroi82,782,131.00 201582,782,131.00 
6ARUSHAKaratuGetamock139,995,000.00 2014139,995,000.0 0 
7ARUSHAKaratuKansay139,995,000.00 2014139,995,000.0 0 
8ARUSHAMonduliEmairete/Eluwai6,081,856.00 20166,081,856.00 
9GeitaGeita MjiKigoma Road 20083,000,000.00
10GeitaChatoKasenga311,660,420 2007 311,660,420 
11GeitaBukombe DCMsasa185,150,936.002008107,000,000.0 0
12KageraBiharamuloMradi wa usambazaji maji Bisibo680,927,667.00201737,044,000.00
13KageraKaragweMradi wa Maji Chanika805,250,968.00201850,000,000.00
14KageraNgaraMunjebwe287,300,178.00201414,000,000.00
15KageraMulebaUjenzi wa mradi Ruteme  145,063,029.2 7
16KageraNgaraMradi wa maji Mukibogoye  100,000,000  100,000,000 
17KageraKaragweMradi wa Maji Nyakakika  32,500,000  32,500,000 
18KAGERABukobaUkarabati wa mradi wa maji Bituntu  80,000,000.00  80,000,000.00 
19KageraNgaraMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kanogeline342,701,651.302014176,225,109.0 0
20KataviTanganyikaMradi Wa Usambazaji maji Kijiji cha Karema342,701,651.302014176,225,109.0 0
21KataviTanganyikaMradi wa Usambazaji maji Kijiji cha Ngomalusambo268,936,954.002015169,867,109.0 0
22KataviMpandaMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Mtakumbuka50,854,519 201850,854,519 
23KataviMpandaMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Sungamila.91,202,000 201491,202,000 
24KataviMpandaMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Isinde20,000,000 201820,000,000 
25KataviMpandaMradi wa Maji ya bomba Nduwi249,513,902 2018249,513,902 
26KataviMleleMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kilida98,332,434 201498,332,434 
27KataviMleleMradi wa Maji ya bomba kijiji cha Kibaoni159,033,822 2018159,033,822 
28KigomaKigoma DCMradi wa Maji Kalinzi786,642,000.00201876,000,000.00
29Kigoma Nkungwe473,026,290.002016150,000,000.0 0
30KIGOMAKigoma DCMradi wa Maji Kalinzi72,893,131.31 201872,893,131.31 
31KIGOMAKigoma DCMradi wa Maji Nyarubanda139,084,330.98 2014139,084,330.9 8 
32KilimanjaroMwangaMamba-Mruma11,080,000 201811,080,000 
33LindiLiwaleMradi wa Maji Mpigamiti678,492,300201494,000,000
34LindiNachingwe aMradi wa Maji Chiola340,702,913.00 2015189,000,000 
35LindiNachingwe aMradi wa Maji Nampemba412,817,075.00 201598,331,991 
36LindiNachingwe aMradi wa Maji wa Mnero Miembeni88,859,000.00201710,000,000 
37LindiNachingwe aMradi wa Maji Mkonjela465,000,000.00 200615,000,000 
38LindiNachingwe aMradi wa Maji Kipara Mtua465,000,000.00 200685,000,000
39LindiNachingwe aMradi wa Maji wa Ndomoni205,449,000.00 2019169,234,531
40LindiLindiHingawari100,000,000  2019100,000,000 
41MANYARAMBULU DCHAYDOM1,065,442,2352017145,507,224.0
      0
42MANYARABABATI TCMalangi680,541,793.90201774,161,200.00 0
43MANYARA Olbil841,990,9102019– 
44MANYARA Darakuta – Minjingu1,731,387,26820172,000,000,000 
45MaraBundaMkune15,000,000.00201312,000,000.00 
46MaraButiamaMradi wa Maji Kitaramanka & Rwasereta65,000,000 201865,000,000 
47MaraButiamaMradi wa Maji Kongoto41,662,292 201441,662,292 
48MaraButiamaMradi wa Maji Kamgendi65,000,000 201865,000,000 
49MaraButiamaMradi wa Maji Bukabwa72,500,000 201472,500,000 
50MBEYAMBARALIImalilosongwe39,374,854.17201356,000,000.00 
51MBEYAKYELAMradi wa Maji Lubaga336,389,350.00 2014– 
52MBEYAMBEYAIdimi/Haporoto745,695,380.00201843,300,000.00 
53MBEYAMBEYAGalijembe299,623,047.00201483,300,000.00 
54MBEYAMBEYAMbawi/Jojo804,480,500.0020144,500,000.00 
55MorogoroMalinyi DCMradi wa maji Lupunga149,318,98220163,540,000 
56MorogoroMalinyi DCMradi wa maji kwa vijiji vya Malinyi ,Kipingo na Makerere3,006,636,4412019114,526,380 
57MorogoroKilombero DCMradi wa Maji Idete248,613,175.00 201723,176,500 
58MorogoroKilombero DCMradi wa Maji Namwawala367,904,295.00 201719,604,500 
59MorogoroKilombero DCMradi wa Maji Matema306,283,960.00 201742,778,546.00 
60MorogoroKilombero DCMradi wa Maji Kamwene287,758,971.50 2015 
61MorogoroKilombero DCMradi wa Maji Miwangani85,000,000.00 2014 
62MorogoroMorogoro DCKidugalo100,000,000 1956100,000,000 
63MorogoroMorogoro DCPangawe41,000,000 197541,000,000 
64MorogoroMorogoro DCSeregeti B02000– 
65MorogoroKilosa DCMradi wa maji Kata ya Ruaha  2018 
66MorogoroKilosa DCMradi wa maji Kidodi 20155,000,000 
67MorogoroGairo DCMradi wa maji Gairo Mjini6,120,000,000 2020580,000,000 
68MorogoroGairo DCChiwaga/Makuyu720,000,000 2019 
69MorogoroGairo DCChogoali550,000,000 2019 
70MorogoroMvomeroKwa Doli219,446,000.002014– 
71MorogoroMvomeroDoma473,838,939.90201545,300,000 
72MOROGOROMorogoro DCMradi wa Maji Singisa  150,000,000.00 2018150,000,000.00
73MOROGOROUlanga DCMradi wa maji ya Bomba, Kijiji cha Minepa60,000,000.00 201460,000,000.00 
74MtwaraTandahimbaMRADI WA MAJI LITEHU LIBOBE453,493,553 2013  189,000.000.00
75MtwaraTandahimbaMRADI WA MAJI JANGWANI MAHEHA1,253,673,300 2013 43,000,000.00 
76MtwaraMasasiMradi wa Maji Mkululu1,257,497,778.80 201956,580,000.00
77MtwaraNewalaUkarabati wa miundombinu ya maji katika vijiji 7208,978,000.00 20183,000,000 
78MtwaraTandahimba (Tandahimba DC)MRADI WA  MAJI MKUPETE  6,000,000  2018  6,000,000 
79MwanzaSengerema Karumo water Project 20113,000,000
80MwanzaMaguLugeye- Kigangama  1,056,740,850.00 2014  34,120,000.00 
81PwaniKibaha Mradi wa maji Kipangege  151,849,500.00 201510,000,000.00
82PwaniBagamoyoMradi wa maji Kijiji cha Yombo  297,637,065.00 201510,000,000.00
83PwaniBagamoyoMradi wa Maji Milo  244,294,578.00 201585,000,000.00
84PwaniKisaraweMradi wa Maji Chole/Kwala  1,610,205,773.11 2018495,000,000.00
85PwaniMkurangaMradi wa Maji Bupu  315,849,000.00 2016825,000.00
86PwaniKibitiMradi wa Maji Kibiti mjini  5,302,059,842.00 2012186,329,317.20
87PWANIMkurangaMradi wa maji MvuleniKilimahewa Kusini  9,840,207.91    9,840,207.91 
88RukwaSumbawangaUjenzi wa mradi wa maji kijiji cha306,704,637.52201457,102,368.53
   Mpui   
89RukwaSumbawangaMradi wa maji wa Laela II1,407,127,879.802016122,400,000.00
90RukwaKalamboUjenzi wa Mradi wa Kasanga  100,000,000    100,000,000 
91RuvumaNamtumboMRADI WA MAJI MILONJI  724,565,490.00 20151,000,000.00
92RuvumaTunduruMradi wa maji Lukumbule  475,472,151.00 2016  1,700,000.00 
93RuvumaTunduruMradi wa Maji Nandembo  330,165,607.00 2014  6,500,000.00 
94ShinyangaShinyangaMradi wa Maji Mwakitolyo– 2018– 
95ShinyangaKahamaMradi wa Maji Segese  88,558,532 2014  88,558,532 
96SHINYANGA SHINYAGAMradi wa Maji Didia415,880,800.00 20144,000,000.00 
97SingidaIkungiMradi wa Maji Nkhoiree92,000,000 201892,000,000 
98SingidaIkungiMradi wa Maji Ntewa awamu ya kwanza166,632,728 2014166,632,728 
99SingidaIkungiMradi wa Maji Mgungira10,000,000 201810,000,000 
100SingidaIkungiMradi wa maji wa Mkiwa76,500,000 201476,500,000 
101SingidaMkalamaMradi wa Maji Ikolo90,000,000 201890,000,000 
102SingidaMkalamaMradi wa Maji Lyelembo200,000,000 2014200,000,000 
103SINGIDAMkalama DcMradi wa maji Nyahaa450,000,000.00 2018450,000,000.00
104SongweIleje DCMtula gravity scheme346,577,406.00 2016 
105SongweIleje DCLuswisi gravity scheme303,056,490.00 2016 
106SongweIleje DCMalangali gravity scheme445,818,754.00 2016 
107SongweIleje DCIlanga, chitete , ikumbilo1,141,300,691.2018 
108SongweIleje DCIgumila, ndola na Ishanta 2018  
109SongweIleje DCMtima 2018 274,200,000
110SongweIleje DCIHANDA392,691,800.002016117,592,500.00
111SongweIleje DCSONGWE GROUP01983– 
112SongweIleje DCRUANDA0198140,000,000.00 
113SongweMomba DCMradi wa Maji Ikana63,470,000.002016 
114SongweMomba DCMradi wa Maji Namsinde II37,241,800.002018 
115SongweMomba DCMradi wa Maji Kasinde41,739,6002018 
116SongweMomba DCMradi wa Maji Mkutano02006 
117SongweMomba DCMradi wa Maji Chiwanda02008 
118SongweMomba DCMradi wa Maji Mkulwe01969– 
119SongweMomba DCMradi wa maji wa Chang’ombe 2015312,537,500.00
120SongweMomba DCMradi wa maji wa Mbuyuni408,931,600.002014348,600,000.00
121SongweMomba DCMradi wa maji wa Mamkukwe3,2782014 
122SongweTunduma Mradi wa maji Mpemba01972200,000,000
123SONGWE Mradi wa maji wa Mbuyuni80,000,000.00  201880,000,000.00
124TaboraNzegaMradi wa Maji Nata526,410,520201514,000,000
125TaboraSikongeMradi wa Maji Uluwa2,278,767,670201535,000,000
126TangaPanganiMeka-Mseko467,850,113 2018467,850,113
127TangaMuhezaMradi wa maji Kijiji cha Kigongomawe105,200,400.00 2014105,200,400.00

Kiambatisho Na.3: Miradi 40 ya Maji Mjini iliyokamilika hadi mwezi Aprili, 2022

Na.MkoaJina la MradiIdadi ya Wanufaika
1ArushaMradi wa Maji wa Longido-Kimokouwa-Namanga29,686
2Dar es SalaamImprovement of Works for Water Supply Distribution System in Mkuranga District.25,500 
3Dar es SalaamConstruction of Water Transmission main from Upper Ruvu Water Treatment Plant at Mlandizi to Mboga Village at Chalinze District120,912 
4DodomaMradi wa Maji Ihumwa – Njedengwa15,718 
5DodomaUchimbaji wa Visima virefu vitatu (3) katika eneo la Mzakwe500,000
6DodomaUjenzi wa mradi wa kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi Chamwino –Ikulu29,534 
7GeitaUboreshaji wa huduma ya maji Mjini Chato19,000 
8GeitaMradi wa Uchimbaji Visima Chato16,000 
9IringaUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Ilula35,651 
10IringaMradi wa maji Mbugani2,345 
11KigomaUkarabati na Utanuzi wa Mradi wa Maji eneo la Makao Makuu ya Wilaya ya Uvinza10,000 
12LindiMradi wa Maji Ng’apa kijijini8,757 
13ManyaraMradi wa Maji Arri Harsha30,020 
14ManyaraMradi wa Maji Mongahay Tumati16,000 
15ManyaraMradi wa Maji Kateshi12,000 
16ManyaraMradi wa maji Orkesumet12,000 
17MaraUkarabati wa Bomba Kuu la Kusafirishia Maji katika Mji wa Shirati4,150 
18MaraMradi wa Kuongeza Mtandao wa Maji Mugumu98,500 
19MaraUjenzi wa mtambo wa kutibu majisafi katika bwawa la Manchira0
20MbeyaMradi wa maji wa Nzovwe Isyesye30,000 
21MbeyaMradi wa kuboresha huduma ya majisafi Tukuyu84,000 
22MbeyaImprovement of water supply services in Rujewa5,780 
23MbeyaMbalizi township water supply80,305 
24MwanzaMradi wa Uchimbaji Kisima kimoja na ujenzi wa miundombinu ya Maji katika shule ya Sekondari Bugatu Wilayani Magu466 
25MwanzaKukamilisha Mradi wa Maji wa Shilima, Mhande na Izizimba16,675 
26NjombeExtension of Distribution line in Kipagamo 317 
27NjombeLudewa Water Supply Projects (Iwela and Mbugani)5,100 
Na.MkoaJina la MradiIdadi ya Wanufaika
28RukwaKujenga miundombinu ya majisafi na usafi wa mazingira katika mji wa Sumbawanga136,414 
29RuvumaMradi wa Maji Mbinga Mjini 12,000 
30RuvumaMradi wa Maji Tunduru Mjini9,000 
31RuvumaMradi wa Maji Luhimbalilo-Naikesi (Namtumbo DC) 3,572 
32RuvumaMradi wa Maji Mbesa (Tunduru DC) 14,771 
33ShinyangaExtension of Water Transmission pipeline from the Lake Victoria Water Scheme (Kinanga) to Kagongwa and Isaka Towns – Lot 256,660 
34ShinyangaUpanuzi wa mtandao wa majisafi Kata ya Kagongwa na mji mdogo wa Isaka12,323
35ShinyangaMradi wa Majisafi Ngongwa- Kitwana 27,095
36SimiyuConstruction of Drinking Water Treatment Plant for Maswa Urban Water and Sanitation Authority 57,933 
37SimiyuUjenzi wa chujio la Maji ya kunywa Mjini Maswa111,408 
38TaboraImprovement of water supply services in Tabora Town270,112 
39TangaConstruction of Gravity Main from Mowe to Pongwe for Improvement of Water in Muheza Township9,560 
40TangaMradi wa Uboreshaji huduma ya maji safi katika Mji wa Muheza Awamu ya Pili.31,000 
  Jumla  1,960,264

Kiambatisho Na. 4:  Miradi 1,029 ya Maji Vijijini itakayotekelezwa katika mwaka 2022/23

Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
(i) MIRADI INAYOENDELEA
1.  ArushaArumeru Arusha DCConstruction of OLMULO water ProjectEnot, milongoine, mbuyuni, Laroi, Terati, kisima cha Mungu, Losinyai na Mateves522,579,261.00
2.   Arumeru Arusha DCConstruction of Losikito water ProjectLosikito and Imbibia500,000,000.00
3.    Arumeru  Arusha DC Drilling of 3 boreholes at Shambarai burka, Msitu wa mbogo and Mungushi villages in Meru council by june 2023 144,000,000.00
 Jumla Arusha DC3 1,166,579,261.00
4.   Arumeru Meru DCConstruction of KIKATITI AND TUVAILA water Project on goingImbaseni, maji ya chai, Kikatiti, Samaria, Kitefu, Maroroni and Nasholi.500,000,000.00
5.   Arumeru Meru DCConstruction of PATANDI water Project on goingPatandi500,000,000.00
 Jumla Meru  DC2 1,000,000,000.00
6.   Longido Longido DCConstruction of Olmolog water Supply ProjectOlmog407,553,418.00
7.   Longido Longido DCConstruction of Orkejelongishu water SupplyOrkejelongis hu, Lopokosek,360,563,418.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    ProjectArmanie na Engushai 
8.   Longido Longido DCExtension of Eng’atadabash i scheme to Engusero VillageEngusero514,276,003.00
9.   Longido Longido DCRehabilitation of Mairowa water Supply Scheme (Lesing’ita/Mun darara)Lesing’ita100,208,387.00
 Jumla Longido4 1,382,601,226.00
10.   Monduli Monduli DCConstruction of Esilalei water supply Project Esilalei450,000,000.00
11.   Monduli Monduli DCConstruction of Oldonyonado water Supply Project Oldonyonad o426,484,146.00
 Jumla Monduli2 876,484,146.00
12.   KaratuKaratu DCConstruction of Laja/Ubwangw water Supply Project  Laja & Umbangw225,395,000.00
13.   KaratuKaratu DCConstruction of Mang’ola Juu water Project Mang’ola Juu191,030,757.00
14.   KaratuKaratu DCConstruction of Chemchem water Supply Project Chemchem360,000,000.00
15.   KaratuKaratu DCConstruction of Mang’ola Balazani water Supply Project Mang’ola Barazani360,319,000.00
16.   KaratuKaratu DCRehabilitation of Endonyawet and Matala water Supply Schemes – on goingEndonyawet & Matala253,407,200.00
  Jumla Karatu  DC5 1,390,151,957.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
17.   NgorongoroNgorongoro DCRehabilitation of Kisangiro Water Supply ProjectKisangiro, Pinyinyi (Masusu) na Olaika150,000,000.00
18.   NgorongoroNgorongoro DCConstruction of Pinyinyi water Project Pinyinyi and Piyaya230,000,000.00
19.   NgorongoroNgorongoro DCImprovement of Loliondo Town Water supply projectLoliondo Township200,000,000.00
20.   NgorongoroNgorongoro DCExtension of Mbukeni, Endulen, Esere and Oldonyosambu Masusu Water Supply schemesMbukeni, Endulen, Esere and Oldonyosam bu Masusu300,000,000.00
21.     Ngorongoro  Ngorongoro DC Construction of fence and develeopment of Oloipir water source at Oloipir villageOloipiri  180,000,000.00   
   Jumla Ngorongoro  DC5 1,060,000,000.00
  JUMLA MKOA ARUSHA 21 6,875,816,590.00
22.  DodomaChamwinoChamwino DCConstruction of pumped Water Supply  Project at Muheme Village Muheme200,000,000.00
23.   ChamwinoChamwino DCConstruction of pumped Water Supply  Project at  Handali Village Handali and Mjelo326,075,265.00
24.   ChamwinoChamwino DCConstruction of  pumped Water Supply  Project at Izava(Wali) Village Izava Wali250,000,000.00
25.   ChamwinoChamwino DC Construction of  pumped WaterMvumi Mission,372,000,000.00
Na.Mkoa WilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Supply  Project at  Mvumi Mission Village Chihembe and Mita 
26.    ChamwinoChamwino DC Construction of pumped Water Supply  Project at  Dabalo Village Dabalo100,000,000.00
  Jumla Chamwino5 1,248,075,265.00
27.    BahiBahi DCConstruction of water infrastructure at Ibihwa villageIbihwa302,453,590.00
28.    BahiBahi DCConstruction of water infrastructure at Chali Makulu, Chali Isanga and Chali Chali IgongoChali Makulu, Chali Isanga and Chali Chali Igongo484,523,986.00
  Jumla Bahi2 786,977,576.00
29.    Dodoma Dodoma CCConstruction of water schemes at Nzasa-phase II, Hombolo Bwawani B- phase II, Mahoma Makulu -phase II, Mayeto & Hombolo Makulu-phase II and ChikowaPhase IINzasa, Chamwino and Sogeambele, Hombolo Bwawani B- phase II, Mahoma Makulu phase II, Mayeto & Hombolo Makuluphase II and Chikowa- Phase II468,751,260.00  
30.    Dodoma Dodoma CCConstruction of Pumped  Water Supply from Mzakwe Borehole toMbalawala, Msembeta,M atangizi,Mak ulu,Kawawa and203,897,567.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mbalawala, Chigongwe phase IIMuungano 
  Jumla Dodoma DC2 672,648,827.00
31.   KongwaKongwa DCConstruction of Water Infrastructures at Ijaka, Manghweta and Saigoni, Kinangali, Mageseni (Bwawani) and Chilanjilizi villagesIjaka, Manghweta and Saigoni, Kinangali, Mageseni (Bwawani) and Chilanjilizi529,517,664.00  
32.   KongwaKongwa DCCompletion of Mkoka, Laikala B, Masinyeti, Lengaji Village Water Supply Projects Mkoka, Laikala B, Masinyeti, Lengaji323,733,897.00  
 Jumla Kongwa2 853,251,561.00
33.   KondoaKondoa DCConstruction of Water Supply Projects for Mauno, Soera, Kikore – Mkurumuzi and Kikilo Kati VillagesMauno, Soera, Kikore – Mkurumuzi and Kikilo Kati494,000,000.00  
34.   KondoaKondoa DCRehabilitation of Water Supply Sheme for KISESE – SAUNA VillageMapinduzi and Sauna161,500,000.00
35.   KondoaKondoa DCConstruction of Water Supply Project for Pahi, Sambwa, Hachwi and Mulua VillagesPahi and Ikova, Pahi, Sambwa, Hachwi and Mulua457,827,130.00  
36.   KondoaKondoa TCConstruction of Water Supply Project forMnarani, Miningani, Iboni,126,000,000.00
Na.Mkoa WilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     KONDOA TownChemchem, Maji ya Shamba and Ubembeni 
  Jumla Kondoa TC4 1,239,327,130.00
37.    ChembaChemba DCConstruction of Chandama Water Supply ProjectChandama and Mpendo210,996,044.80
38.    ChembaChemba DCConstruction of Chemba Town Water Supply ProjectChemba69,961,036.80
39.    ChembaChemba DCConstruction of Khubunko, Babayu and HamiaWater Supply projectsKhubunko, Babayu and Hamia201,343,008.53  
40.    ChembaChemba DCRehabilitation and expansion of Kelema Balai Water Supply SchemeKelema Balai and Kelema mashariki280,656,110.70
41.    ChembaChemba DCRehabilitation of Songolo Water Supply schemeSongolo12,624,241.00
  Jumla Chemba5 775,580,441.83
42.    MpwapwaMpwapwa DCConstruction of water infrastructure at Chinyika Mlunduzi  VillagesChinyika and Mlunduzi162,000,000.00
43.    MpwapwaMpwapwa DCConstruction of water infrastructure at Igoji, VinhaweManhangu, Lupeta and Makutupa  Igoji, VinhaweManhangu, Lupeta and Makutupa  300,650,645.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Villages  
44.   MpwapwaMpwapwa DCConstruction of water supply infrastructures at  and PwagaMunguwi  villagesPwaga,Mung uwi,Maswala and Itende116,750,000.00
45.   MpwapwaMpwapwa DCConstruction and emprovement of Mtera water supply schemeMtera73,849,999.00
  Jumla Mpwapwa 4 653,250,644.00
  JUMLA MKOA DODOMA 24 6,229,111,444.83
46.  GeitaBukombe bukombe DCConstruction of Msonga water supply projectMsonga634,280,137.00
47.   Bukombe bukombe DCConstruction of Nampalahala water supply projectNampalahal a185,692,403.94
48.   Bukombe bukombe DCConstruction of Namsega water supply projectNamsega and Msangila220,400,200.00
  Jumla Bukombe DC3 1,040,372,740.94
49.   ChatoChato DCConstruction of Nyambogo – Ilemela water supply projectKanyama, Ilemela and Nyambogo1,072,000,000.00
50.   ChatoChato DCConstruction of Muganza – Bwongera water supply project to serve 14 villages in 3 wards (PforR)Kibehe, Nyisanzi, Bwawani, Buhungu, Nyabilele, Rutunguru, Ibanda, Muganza, Nyabugera, Katemwa, Majengo, Butarama, Mkombozi na651,851,419.90
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Bwongera 
  Jumla Bukombe DC2 1,723,851,419.90
51.   GeitaGeita DC Construction of Izumacheli Water Supply project Izumacheli189,176,250.70
52.   GeitaGeita DC Construction of NjiapandaWate r Supply project Njiapanda  209,979,718.30
53.   GeitaGeita TCConstruction of Bung’wangoko Water Supply projectBung’wangok o572,648,829.00
54.   GeitaGeita DCConstruction of 5 Wards Water Supply Project (Nkome, Katoma, Nyamboge, Nzera & Lwezera) Nkome, Mnyala, Ihumilo, Nyambaya, Kakubilo,  Nyakazeze, Katoma, Itale, Njingami, Nyamboge, Lukaya, Chelameno, Nzera, Bugando, , Lwezera, Bweya,Idoser o, Nyarubanga823,262,380.00
  JumlaGeita DC4 1,795,067,178.00
55.   MbogweMbogwe DCConstruction of Lugunga – Luhala water supply projectLugunga and Luhala317,574,955.00
56.   MbogweMbogwe DCConstruction of Kabanga – Nhomolwa  water supply projectKabanga,Nho molwa and Nyahwinga668,517,789.80
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
57.   MbogweMbogwe DCConstruction of Iponya  water supply projectIponya286,214,828.40
  Jumla Mbogwe DC3 1,272,307,573.20
58.   NyangwaleNyangwale DCTo extend Nyamtukuza water supply project to  Bululu, Ifugandi, Busolwa,  Villages by June, 2023Bululu, Ifugandi and Busolwa1,101,037,039.00
59.   NyangwaleNyangwale DCExtension of Nyamtukuza Water Project to Nyijundu VillageNyijundu, Iyogelo332,117,417.00
  Jumla Nyang’wale DC3 1,433,154,456.00
  JUMLA MKOA GEITA 15 7,264,763,368.04
60.  Iringa KiloloKilolo DCConstruction of Ifua Lot 1(First Village of Ifua) water supply project in Kilolo District.Ifua, Wotalisoli25,000,000.00
61.   KiloloKilolo DCExtention of water Scheme to Uhambingeto village (lot 1 – First Village of Uhambingeto)Uhambinget o1,643,399,478.00
62.   KiloloKilolo DCConstruction of KIMALA water Supply Projects. Kimala39,490,794.00
63.   KiloloKilolo DCconstruction of group water supply project to villages of Masege, Masalali and KihesamgagaoMasege, Masalali, Kihesa Mgagao96,298,459.16
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
64.   KiloloKilolo DCConstruction of water treatment plant at Mgowelo water schemeMgowelo20,000,000.00
  Jumla Kilolo  DC5 1,824,188,731.16
65.   Iringa Iringa DC Consruction of  Itengulinyi, Lumuli and Isupilo in Iringa District  Itengulinyi, Lumuli 1,760,155,965.00
66.   Iringa Iringa DC Extension of Mkumbwanyi  water supply project covering of  three villages of Makuka, Mbweleli and Makatapola  in Iringa District  Makuka, Mbweleli and Makatapola1,159,212,892.00
67.   Iringa Iringa DC Construction of Pawaga water supply project (Lot 2) Luganga, Ukwega, Magozi, Ilolompya, Mkombilenga . Mbuyuni, Kimande, Itunundu, Mbugani, mboliboli, Magombwe, Isele, Kinyika, Kisanga73,895,345.38
68.   Iringa Iringa DC Construction of Nyamlenge water supply project in three villages of Magulilwa, Mlanda and Nyabula  Magulilwa, Mlanda and Nyabula  496,669,084.50
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
69.   Iringa Iringa DC Rehabilitation of Tungamalenga group scheme (Mapogoro, Kitisi, Tungamalenga , Ifunda, Itagutwa and Ihemi )Mapogoro, Kitisi, Tungamalen ga, Ifunda, Itagutwa and Ihemi50,000,000.00
70.   Iringa Iringa DC Construction of Tanangozi – Kalenga water supply project in three villages of Itagutwa, Kidamali and Nzihi  Vilages in Iringa District.Itagutwa, Kidamali and Nzihi  408,000,000.00
  Jumla Iringa  DC6 3,947,933,286.88
71.   Mufindi Mufindi DC Construction of Ifwagi, Ihalimba and Ikongosi Water Supply projects Ihalimba, Ugesa, Wami, Vikula, Nundwe, Itulavanu, Ikongosi, Ifwagi, Ifupira, Itona, Mtili, Lugongo, Mwitikilwa, Ikongosi juu na Igomtwa 30,000,000.00
72.   Mufindi Mufindi DC Construction of Mgololo Water Supply  Isaula, Kiyowela, Makungu, Lugema na mabaoni 30,000,000.00
73.   Mufindi Mufindi DC Construction of Igowole Water Supply   Ikwega,Mkal ala na20,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Igowole  
74.   Mufindi Mufindi DC Construction of Nyololo (Nyololo shule,Njojo na Lwingh’ulo )water Project  Nyololo shuleni,Njojo na Lwing’ulo 250,000,000.00
75.   Mufindi Mufindi DC Construction of Chogo, Idete,Ihanzutw a and Kisada Water Supply Chogo, Idete, Ihanzutwa  & Kisada572,648,862.67
76.   Mufindi Mufindi DC Construction of Sadani Kihata Water Supply  Kibada, Tambalango mbe, utosi, Lugodalutali, I gombavanu na makongomi 322,559,272.00
77.   Mufindi Mufindi DC Construction of Malangali Water Supply   Isimikinyi,Ite ngule, Kigenge, Tambalang’o mbe, Mwilavila, Ipilimo,Ihowa nza, Idumulavanu na Ikangamwan i 57,909,862.67
78.   Mufindi Mufindi DC Construction of Lufuna and Kibao Water Supply   Sawala,Mtw ango,Lufuna na Kibao 1,907,440,728.00
  Jumla Mufindi  DC8– 3,190,558,725.34
  JUMLA MKOA IRINGA  19 8,962,680,743.38
79.  KageraKaragweKaragweConstruction  of   water supply project  at Ihembe 1Vilage.Ihembe I80,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
80.   KaragweKaragweConstruction  of   water supply project  at Ahakishaka Vilage.Ahakishaka60,000,000.00
81.   KaragweKaragweExtension   of   water supply project  at NyakaigaKakuraijo Villages.Nyakaiaga & Kakuraijo40,035,280.00
 Jumla Karagwe3 180,035,280.00
82.   Misenyi Misenyi DCConstruction of water supply project at Byamtemba and Igayaza villageByamtemba and Igayaza636,711,755.54
83.   Misenyi Misenyi DCConstruction of Kitobo water supply projectKitobo and Kashasha905,163,256.26
84.   Misenyi Misenyi DCConstruction of katolerwa water supply projectNyarugongo, Luhano, Katolerwa and Katano547,285,590.38
85.   Misenyi Misenyi DCConstruction of Kashenye water supply projectKashenye, Bushago and Bukwali200,000,000.00
86.   Misenyi Misenyi DCExtension of Gera water supply project to kashaka and kashekya villageKashaka and Kashekya500,000,000.00
87.   Misenyi Misenyi DCBuyango water supply projectRutunga and Rwamachu581,078,753.38
88.   Misenyi Misenyi DCConstruction of Byeju water supply projectByeju  400,000,000.00
  Jumla Misenyi7 3,770,239,355.56
89.   Ngara Construction of MukalizaMuruginaMukaliza and Murugina85,510,822.40
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    water supply project  
90.   Ngara Construction of Kanyinya water supply projectkanyinya300,000,000.00
91.   Ngara Construction of Kabanga water supply projectKabanga and murukukumb o786,504,040.00
92.   Ngara Construction of Kasange water supply projectKasange230,000,000.00
93.   Ngara Construction of Mukikomero water supply projectMukikomero272,000,000.00
94.   Ngara Construction of Kigina water supply projectKigina210,000,000.00
 Jumla Ngara6 1,884,014,862.40
95.   BukobaBukoba DCExtension of Kibirizi water Supply project to Kumkore,Ama ni and KamuliKamuli200,000,000.00
96.   BukobaBukoba DCConstruction of water infrastructure at Nsheshe and Rukoma villagesNsheshe and Rukoma200,000,000.00
97.   BukobaBukoba DCExtension of Kabirizi water Supply Scheme to Migara Migara200,000,000.00
98.   BukobaBukoba DCExtension of Nyakabulala Water Supply Scheme to Kikomelo and ButakyaKikomelo and Butakya350,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
99.   BukobaBukoba DCExtension of Itongo-Mikoni to Kagondo water projectKagondo100,000,000.00
100. BukobaBukoba DCExtension of Katale water supply project to Rubafu and Bumai villagesRubafu,Buma i and Kishanje500,000,000.00
101. BukobaBukoba DCConstruction of Mushozi water ProjectMushozi and Katangalala186,053,177.00
  Jumla Bukoba 7 1,736,053,177.00
102. MulebaMulebaConstruction  of Kagoma  water supply projectKagoma & Nsisha350,594,593.29
103. MulebaMulebaConstruction  of Bulamula  water supply  projectsBulamula481,844,125.90
104. MulebaMulebaConstruction  of Butembo  water supply  projectsButembo, Kikuku & Makarwe259,621,409.25
105. MulebaMulebaExtension of   Bisore water supply projectBisore & Nyakasheny e314,908,053.74
106. MulebaMulebaConstruction  of  Kyamyorwa water supply projectKyamyorwa & Rulanda408,759,519.65
107. MulebaMulebaConstruction of Katare water supply projectBuhanga, Bushemba, Katare & Kashozi407,400,844.17
108. MulebaMulebaConstruction of  Kishanda /Kabulala water supply projectKishanda & Kabulala48,340,846.00
109. MulebaMulebaTo complete the construction ofButembo2,271,469,392.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Butembo water supply project  
  Jumla Muleba 8 4,542,938,784.00
110. BiharamuloBiharamulo DCConstruction of Water Supply schem at Nyabusozi and Mbindi Villages.Nyabusozi, Mbindi and Mwanga100,000,000.00
111. BiharamuloBiharamulo DCConstruction of Water Projects at NyamigereKalenge water supply projectNyamigere and Kalenge205,000,000.00
112. BiharamuloBiharamulo DCMavota Rehabilitation water Project by construction of Storage Tank of 75 raiser of 9mMavota130,000,000.00
113. BiharamuloBiharamulo DCConstruction of Water Supply schem at Nyakafundikwa -Nyakanazi Project.Nyakafundik wa and Nyakanazi87,494,477.60
114. BiharamuloBiharamulo DCConstruction of Water Supply schem at Mubaba Village.Mubaba 68,187,061.50
115.   Feasibility study and detail design for the water project at Nyakahura, Mihongora, Rusese and Mabale Villages 129,103,724.00
  Jumla Biharamulo5 719,785,263.10
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
116. Kyerwa Construction of kimuli,Rwanya ngo and chakalisa water supply projectKimuli,Rwan yango and Chakalisa200,068,110.00
117. Kyerwa Construction of Runyinya- Chanya water supply project Runyinya,Ch anya,Nkwen da,Muleba,R wabwere,Ny amweza,Itee ra and 345,479,988.00
118. Kyerwa Construction of NyamiagaNyakatera water supply Nyamiaga,N yakatera and Kagu350,479,988.00
119. Kyerwa Construction of kaisho -Isingiro water supplyKaisho,Isingi ro,Karukwan zi ‘A’,Ibale,Kiha nga,Kaitamb uzi,Karukwa nzi’B’,Katera, Rwensinga,I shaka and Nyabishenge 325,479,988.00
120. Kyerwa Completion of Kigorogoro  water supply Kigorogoro,Ki shanda and Lulama55,368,714.50
121. Kyerwa Completion of mabila water supply Rushe,Mabir a,Kibimba,Ma kazi,Nyakatet e,Omukagan do and Ruhita75,042,657.50
122. Kyerwa Construction of karongo rwabwereKarongo and Rwabwere125,479,994.00
123. Kyerwa Rehabilitation of songambele -kagenyiSongambele, Kagenyi and Omukalinzi116,083,518.00
  Jumla Kyerwa8 1,593,482,958.00
  JUMLA MKOA KAGERA 44 14,426,549,680.0 6
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
124. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Project at Katuma and KamilalaKatuma and Kamilala53,380,468.70
125. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Scheme at Lugonesi and MpembeMpembe and Lugonesi132,248,929.23
126. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Project at Bulamata VillageBulamata146,662,000.00
127. KataviTanganyikaTanganyika DC Extension of Karema Water Supply Scheme to Kapalamsenga and Songambele Village and Construction of Water Supply Project at Kafisha and Kasangantong we VillageKapalamsen ga, Songambele , Kafisha and Kasanganto ngwe100,000,000.00
128. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Project at Vikonge VillageVikonge101,120,346.67
129. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Project at Kapanga  VillageKapanga76,249,371.54
130. KataviTanganyikaTanganyika DC Construction of Water Supply Project at Mnyagala and IkakaMnyagala and Ikaka188,620,633.74
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Villages  
131. KataviTanganyikaTanganyika DC Construction of Water Supply Project at Kasekese, Kaseganyma, Sibwesa and Nkungwi VillagesKasenganya ma, Kasekese, Sibwesa and Nkungwi304,657,982.99
132. KataviTanganyikaTanganyika DC Construction of Water Supply Project at Mazwe VillageMazwe125,792,334.68
133. KataviTanganyikaTanganyika DCConstruction of Water Supply Project at Isenga,. Kapemba and IfumbulaIsenga,Kape mba and Ifumbula200,000,000.00
134. KataviMpanda Mpanda MCExtension of milala water supply scheme to Kampuni villageKampuni160,000,000.00
135.KataviMpanda Mpanda MC Construction of Water Supply Project at Kakese villageKakese& Mbugani412,648,829.05
136.KataviMpanda Nsimbo DCConstruction of Water Supply Project at Kambuzi Halt villageKambuzi Halt175,000,000.00
137.KataviMpanda Nsimbo DCConstruction of Water Supply Project at Tambazi A & B villagesTambazi A&B464,401,588.26
138.KataviMpanda Nsimbo DCConstruction of Water Supply Project at KatambikeKatambike180,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    village  
139.KataviMpanda Nsimbo DCConstruction of Water Supply Project at Kapanda villageKapanda176,827,467.74
140.Katavi MleleMpimbwe DCExtension of Majimoto water supply and sanitation project to UsevyaMinyoso, Nyambwe, Usevya ,Ikuba, Msadya.2,279,080,324
141.KataviMleleMpimbwe DCMradi wa Maji safi na salama katika Vijiji vya Mwamatiga, Ilalangulu  (kitongoji cha Vilolo) na MkwajuniMwamatiga, Ilalangulu (kitongoji cha Vilolo) na Mkwajuni724,529,463.68
142.KataviMleleMpimbwe DCConstruction of stoarage tank with capacity of (1000m3) at Mamba Village.Mamba, Majimoto, Luchima, Ikulwe, Kitupa, Mkuyuni na Migunga.742,093,500
143.KataviMleleMpimbwe DCExtension of Kibaoni Water supply project (Covid-19)Kibaoni557,228,142
144.KataviMleleMpimbwe DCConstruction of Ukingwamizi water supply project.  Ukingwamizi  87,891,340.00
145.KataviMleleMlele DCExtension of water supply and sanitation  16 Villages at Mlele DCInyonga,Ute nde, Mgombe, Kanoge, Nsenkwa,Mt akuja, Kaulolo, Mapili, Kamsisi,3,181,559,645.42
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Songambele , Imalauduki, Kalovya na Kamalampak a 
146.KataviMleleMlele DCExtension of water supply and sanitation at Inyonga and Kalovya (Covid-19)Inyonga and Kalovya 752,977,345.96
147.KataviMleleMlele DCConstruction of Water Supply Project at Utende and Mgombe Villages Utende and Mgombe 146,352,480.00 
148.KataviMleleMlele DCDam construction at Nsenkwa Villages Inyonga, Utende, Mgombe, Kanoge, Nsenkwa, Mtakuja, Kaulolo, Mapili, Kamsisi, Songambele , Imalauduki, Kalovya na Kamalampak a1,370,668,924.26 
149.KataviMleleMlele DCExtension of water supply and sanitation 16 Villages at Mlele DCInyonga, Utende, Mgombe, Kanoge, Nsenkwa, Mtakuja, Kaulolo, Mapili, Kamsisi, Songambele , Imalauduki, Kalovya na Kamalampak3,181,559,645.42
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     a 
  JUMLA MKOA KATAVI 28– 16,021,550,763.3 4
150.Kigoma Buhigwe  Buhigwe DC Completion of Buhigwe, Kavomo, Murela and Bwega Water supply system Buhigwe, Kavomo, Murela595,000,000.00
151. Kigoma Buhigwe  Buhigwe DC Completion of Munanila and Nyakimue Water Supply Project Munanila, Nyakimue, Mkatanga, Kitambuka, Kibwigwa, Kibande, Bweranka870,266,850.23
152. Kigoma Buhigwe  Buhigwe DC Completion of Migongo- Kilelema Water Supply Project Migongo, Kilelema749,121,778.46
  Jumla Buhigwe3 2,214,348,628.69
153. KigomaKakonkoKakonko DCCompletion of Chilambo Water Supply ProjectChilambo441,733,056.00
154. KigomaKakonkoKakonko DCCompletion of Nyakayenzi (Nyamtukuza) water supply projectNyamtukuza388,001,580.03
155. KigomaKakonkoKakonko DCCompletion of Extension of Kanyonza Water Supply Scheme to Kihomoka villageKihomoka230,000,000.00
156. KigomaKakonkoKakonko DCCompletion of Extension of Kakonko Water SupplyKinonko400,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Scheme to Kinonko & Njoomlole village  
  Jumla Kakonko4 1,459,734,636.03
157. KigomaKasuluKasulu TCCompletion of Muhunga water supply projectMuhunga154,593,554.00
158. KigomaKasuluKasulu TCExtension of Mwanga B water supply projectMwanga B340,039,079.68
159. Kigoma  Extension of Mudyanda water supplyMudyanda239,960,920.09
  Jumla Kasulu TC3 734,593,553.77
160. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Kagerankanda water supply projectKagerankan da215,750,830.00
161. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Kabulanzwili water supply projectKabulanzwili85,693,973.00
162. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Chekenya water supply projectChekenya72,462,666.00
163. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Nyamnyusi water supply projectNyamnyusi76,092,531.00
164. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Rungwempya water supply projectRungwempy a107,698,028.23
165. KigomaKasuluKasulu DCCompletion of Rusesa water supply schemeRusesa, Makingi, Kakirungu100,000,000.00
 Jumla Kasulu DC6 657,698,028.23
166. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of MalagarasiMalagarasi, Mliyabibi278,240,161.39
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mliyabibi water supply project  
167. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Mwakizega, Kabeba and Rukoma water supply project Mwakizega, Kabeba283,449,457.24
168. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Chakuru water supply projectChakuru98,037,200.00
169. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Kashagulu water supply projectKashagulu143,975,021.00
170. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Mazungwe and Lugufu water supply projectMazungwe89,498,867.37
171. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Basanza Msebei water supply projectBasanza, Msebei190,000,000.00
172. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Sigunga Kangwena water supply projectSigunga120,712,112.00
173. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Herembe Kaparamsenga water supply project Herembe, Kaparamsen ga310,000,000.00
174. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Buhingu, Kalilani, Katumbi and Nkonkwa WaterBuhingu, Kalilani, Katumbi, Nkonkwa952,470,820.68
175. KigomaUvinzaUvinza DCCompletion of Karago, Kirando and Lyabusende Water Supply ProjectKarago, Kirando, Lyabusende997,529,179.32
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
  Jumla Uvinza10 3,463,912,819.00
176.KigomaKigomaKigoma DCCompletion of Mkigo Water Supply ProjectMkigo, Kasanda582,293,040.00
177.KigomaKigomaKigoma DCCompletion of Kaseke, Kidahwe and Matendo – Samwa water projectsKaseke, Kimbwela, Nyamori, Kidahwe, Matendo & Samwa2,085,608,952.00
178.KigomaKigomaKigoma DCCompletion of Chankele Bubango gravity water piped water Project Chankele, Bubango350,000,000.00
179.KigomaKigomaKigoma DCCompletion of rehabilitation and improvement of Nyarubanda and Kalinzi piped water scheme by installation of solar system and improvement of an intake.Kalinzi, Nyarubanda, Kasange & Mlangala312,309,221.00
180.KigomaKigomaKigoma DCCompletion of Kiziba Water Supply projectKiziba650,875,359.00
  Jumla Kigoma DC 4 3,981,086,572.00
  JUMLA MKOA KIGOMA29 12,511,374,237.7 2
181.KilimanjaroRomboRombo DCConstruction of Lake Challa Water Supply Project (Wona Source)Mahorosha, katangara, lerto, kibaoni, kirwa, msaranga, kisale, kirongo chini,694,137,725.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     kiwanda, Mrere, Kingachi, Usongo, Nayeme 
182.  Rombo DCCONSTRUCTI ON OF NJORO II WATER PROJECTKIKELELWA , MBOMAI AND KIBAONI461,984,617.00
  Jumla Rombo DC2 1,156,122,342.00
183. MoshiMoshi DCConstruction of water source and Gravity Main for Kirima,Utaruni na Karamsingi -MabungoKirima Juu,Otaruni, Mabungo418,389,797.00
184.  Moshi DCRehabilitation and Improvement of Marangu Water supply Scheme.Kiraracha,Kit owo,Komalya ngoe,Komela, Kyala,Mbahe, Nduweni,Arisi ,Sembeti,Lya songoro,Lya mrakana800,000,000.00
  Jumla Moshi DC2 1,218,389,797.00
185. Mwanga Mwanga DcExtension and Rehabilitation of Kileo Kivulini Water SupplyKivulini and Kileo1,045,017,170.00
  Jumla Mwanga DC1 1,045,017,170.00
186. SihaSiha DCConstruction and Extention of Lawate Fuka  water supply scheme from Namwi intake to Ngumbaru, Merali and District Hosptal .Merali and ngumbaru871,175,405.41
  Jumla Siha DC1 871,175,405.41
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
187. HaiHai DCImprovement of water supply system at Hai Town in Hai District, Kilimanjaro RegionBomang’omb e, Muungano and Bondeni1,262,067,750.00
  Jumla Hai DC1 1,262,067,750.00
188. SameSame DCConstruction of water Supply at Vuje VillageVuje302,545,597.50
189. SameSame DCConsrtuction of water Supply at Kirangare wardMakasa338,529,438.23
190. SameSame DCConstruction of Kilinjiko water supply projectKirinjiko288,529,438.24
191.  Same DCRehabilitaion  of Msindo Water supply projectMsindo139,999,950.00
  Jumla Same DC4 1,069,604,423.97
  JUMLA KILIMANJARO11 6,622,376,888.38
192.LindiKilwa Kilwa DC Construct Chumo Water Supply Project by June, 2023  Chumo103,943,000.00
193. Kilwa Kilwa DCConsyruction of Likawage Water Supply Project by Juni 2023Likawage121,909,500.00
194. Kilwa Kilwa DCConstruction of Kilwa Kisiwani Water Supply Project by Juni 2023Kilwa kisiwani745,267,774.77
195. Kilwa Kilwa DCConstruction of Marendego Water Supply Project by Juni 2023Marendego135,475,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
196. Kilwa Kilwa DCConstruction of Hotel Tatu Water Supply Project by Juni 2023Hotel Tatu106,498,000.00
197. Kilwa Kilwa DCConstruction of Kinjumbi Water Supply Project by Juni 2023Kinjumbi110,779,360.00
198. Kilwa Kilwa DCConstruction of Nakui Water Supply Project by Juni 2023Nakiu69,952,085,74
199. Kilwa Kilwa DCDriliingo of 8 boreholes and installations of handpumps. by Juni 2023Mbwemkuru, Hotel tatu, Matandu, Masanyinga, Nasawa, Zingakibaoni, Enokwe and kisimamkika200,000,000.00
  Jumla Kilwa 8– 1,523,872,634.77
200. LindiLindi DCRehabilitation of NyangaoMtama Water Supply Project by June 2023 Mkwajuni, Mbalala, Masasi, Nang’aka, Majengo A, Majengo B, Mihogoni, Makonde, Mvuleni, Nyangao A, Nyangao B, Mtakuja II591,000,000.00
201. LindiLindi DCconstruction of Navanga Corridor Water Supply Project by June 2023 Mnali, Nampunga, Simana, Nachunyu, Mmumbu, Navanga, Mmongomon go, Tipuli, Kilimani1,025,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
202. LindiLindi DCRehabilitation of Rondo Water Supply Project by June 2023Ntene A, Ntene B, Mtakuja, Ntauna, Chiodya A, Chiodya B, Mnara, 993,809,533.00
  Jumla Lindi DC302,609,809,533.00
203. Liwale Liwale DCConstruction of Mkutano Water Supply Project by June, 2023Mkutano, Kikulyungu and Chimbuko120,777,913.92
204. Liwale Liwale DCConstruction of Naujombo water Supply project Mirui, Naujombo and Lineng’ene172,722,594.49
205. Liwale Liwale DCConstruction of Mpengere Water Supply Project by June, 2023Mpengere and Kigwema427,428,090.37
206. Liwale Liwale DCConstruction of Makata Water Supply Project by June, 2023Makata and Mitawa A170,204,755.65
  Jumla Liwale 50891,133,354.43
207. NachingweaNachingwea DC Construction of Nammanga Water Supply Scheme by June 2023.Nammanga, Ruponda, Mwananyam ala and Mandawa (Ndagalimbo )290,000,000.00
208. NachingweaNachingwea DCConstruction of Mchangani Water Supply Scheme by June 2023Mchangani35,000,000.00
209. NachingweaNachingwea DCConstruction of Rweje and Kipara mnero Water SupplyRweje and Kipara Mnero120,565,252.24
210. RuangwaRuangwa DCExtension of NangangaMtakuja, Mchenganyu300,869,465.10
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Gravity Piped Schemeby June, 2023  (On going project)mba and Malolo 
211. RuangwaRuangwa DCExtension of Mandawa Gravity Piped Scheme by June, 2023  (On going project)Muhuru, Chibula, Namichiga A and Namichiga B 1,182,252,864.91
212. RuangwaRuangwa DCExtension of Makanjiro pumped piped SchemeChilangalile, Chikoko, Mmbangala and Mmawa25,000,000.00
213.   Construction of water project to  34 villages of Ruangwa District and 21 Villages of Nachingwea District from Nyangao River  Chimbila A&B, Kipindimbi, Kitandi, Likunja, Ipingo, Likwachu, Manokwe, Mbecha, Michenga A&B, Mitope, Mmawa, Mpara, Mpumbe, Mtimbo Ruangwa, Namahema A&B, Namakuku, Nandagala A&B, Njiwale, nkowe, Chienjele, Luchelegwa, Mibure, Nandanga, Ng’imbwa, Ruangwa120,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     urban. 
214.   Drilling of 10 boreholesNambilanje, Mkaranga, Nachimimba, Mkutingome, Chunyu, Liugulu, Namikulo, Nangurugai, Kipindimbi and Matambalale25,000,000.00
  Jumla Ruangwa 3 2,098,687,582.25
  JUMLA MKOA LINDI23 7,123,503,104.45
215.ManyaraBabati Babati DCTo facilitate completion of On going projects at Magara, Boay, Hoshan, Kakoi, VilimaVitatu, Kazaroho, Geophysical survey and Drilling of 9 boreholes at Endadosh, Mwikantsi, Gijedabung, Riroda, Ayasanda, Endamaghay, Duru, Endagwe and Hewasi Villages.Magara, Boay, Hoshan, Kakoi, VilimaVitatu, Kazaroho, Endadosh, Mwikantsi, Gijedabung, Riroda, Ayasanda, Endamagha y,        Duru, Endagwe and Hewasi 1,187,531,486.19
  Jumla Babati1 1,187,531,486.19
216. HanangHanang DCCompletion of MogituGehandu water Supply ProjectGehandu842,314,536.50
217.   Extention of Hirbadaw waterHirbadaw80,596,310.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Supply and Sanitation Scheme   
 Jumla Hanang2 922,910,846.50
218.                      Mbulu   Mbulu DCCompletion of Labay, Ng’orati, Maretadu Juu, Masqaroda, Masieda – Gembakw, Endahagichan WS projects and completion of drilling 4 boreholes at Qalodaganway, Qaloda,Haydo m and GeteshLabay, Ng’orati, Maretadu Juu, Masqaroda, Gembakw, Endahagicha n, Qalodaganwa y, Qaloda, Haydom and Getesh1,384,971,972.0
  Jumla Mbulu DC101,384,971,972.0
219. Mbulu Mbulu TCCompletion of water supply project at Nambisi (hayloto) and Qalieda village in Mbulu Tc Hayloto198,545,402.72
  Jumla Mbulu TC10198,545,402.72
220. Simanjiro Simanjiro DCCompletion of water supply projects at Terrat, Nadojunkin, Engonongoi and EmishiyeTerrat, Nadojunkin, Emishiye and Engonongoi 959,961,536.17
221. Simanjiro Simanjiro DCConstruction of Olchoronyori water supply projectOlchoronyori232,457,646.31
  JumlaSimanjiro201,192,419,182.48
222. KitetoKiteto DCConstruction of Esuguta water supply projects by June 2023Esuguta218,205,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
223. KitetoKiteto DC Construction of Kiperesa water supply projects by June 2023 Kiperesa220,000,000.00
224. KitetoKiteto DCExtention of Nchinila- Engusero water supply projectEngusero, Nasetan, & Ngipa1,066,930,591.12
225. KitetoKiteto DCExtention of Magungu-Nhati water supply projectMagungu & Nhati342,505,408.88
 Jumla Kiteto  401,847,641,000.00
  JUMLA MANYARA   1206,734,019,889.89
226.MaraTarimeTarime DCConstruction of water supply project for Kitawasi water Supply ProjectKitawasi,Ma surura and Masanga120,000,000.00
  Jumla Tarime 10120,000,000.00
227.  Rorya  Rorya DC Rehabilitation of Komuge water supply SchemeKyamwame, Bitiryo, komuge, Irienyi, Kuruya, Baraki & Makutano.100,000,000.00
  Jumla Rorya 1 100,000,000.00
228. BundaBunda DCContruction of Kinyambwiga Piped Scheme LGA/065/20142015/W/WSDP/ 6-8 BD-C3 Kinyambwiga220,000,000.00
229.   To complete Sanzate water project by June 2023Sanzate390,927,003.90
  Jumla Bunda 3 610,927,003.90
230. MusomaMusoma DCConstruction of Kigeraetuma water supply projectKigeraetuma, Kakisheri300,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
231. MusomaMusoma DCConstruction of water supply project for District hospital & Kaboni and Kasoma villages.Kasoma, Kaboni47,441,142.00
  Jumla Musoma DC2 347,441,142.00
232. ButiamaButiama DCCompletion of on-going project (2021/2022) at Buswahili, Mwibagi, Nyasirori, Biatika, Nyamikoma, Kyankoma Villages and Improving of 4 hand Pumps in Kyatungwe, Masurura, nyambili and Mmazami villages.Buswahili, Mwibagi, Nyasirori, Biatika, Nyamikoma, Kyankoma, nyambili, Mmazami and Masurura village473,545,856.89
  Jumla Butiama DC1 473,545,856.89
 JUMLA MKOA MARA13 1,651,914,002.79
233.MbeyaChunya Chunya  DCConstruction of Matwiga Phase II (Water Supply Project for Six Villages)Mazimbo, Mtanila, Igangwe, Kalangali, Lupa and Ifuma693,648,829.00
234. Chunya Chunya  DCConstruction of water Supply Project at KambikatotoKambikatoto300,000,000.00
235. Chunya Chunya  DCConstruction of water Supply Project at UpendoUpendo and Rola242,965,585.00
  Jumla Chunya 3 1,236,614,414.0
236.MbeyaKyelaKyela DCConstruction ofLema343,153,312.98
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    water supply project at Lema  
237. KyelaKyela DcImprovement of Sinyanga water supply projectMaendeleo, Malangali, Mbula, Njugilo, Konjula, Buponelo, Kyijila, Sinyanga, Kandete, Itope, Kukusya, Kapamisya, Malungo, Masebe, Kasala, Itunge Mashariki, Itunge Kaskazini, Itunge Kati.406,412,390.02
238. KyelaKyela DCImrovement of Ngana water supply projectIsaki, Kabanga, Ndwanga, Katumba, Mpunguti, Kilasilo, Mbako, Ipungu, Ikolo, Muungano, Lupembe, Itopebujonde, Nnyelele, Isanga, Ngonga Nsasa, Lugombo, Itenya, Itete, Mwalisi, Ushirika, Ngana, Kasumulu, Njisi, Seko700,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     and Kilambo. 
  Jumla Kyela 3 1,449,565,703.00
239. MbeyaMbeya DCRehabilitation of Isebe/Ulenje  Water ProjectIsebe and Ulenje187,005,025.00
240. MbeyaMbeya DCConstruction of Ikukwa Water ProjectIkukwa and Simboya232,586,783.38
241. MbeyaMbeya DCConstruction of TembelaIyawaya Water ProjectTembela, Idunda, Isongwa, Iyelanyala and Iyawaya210,198,897.00
242. MbeyaMbeya DCConstruction of Simambwe Water ProjectSimambwe, Usoha Njiapanda, Shibolya and Ilembo Usafwa200,567,000.00
243. MbeyaMbeya DCConstruction of Itawa Water ProjectPashungu and Shigamba137,183,853.62
244. MbeyaMbeya DCConstruction of Izyira Water ProjectInuka, Masewe and Izyira268,244,403.00
   Jumla Mbeya DC6 1,235,785,962.00
245. MbaraliMbarali DCConstruction of ongoing water infrastructure for Luduga Mawindi Scheme Lot IV and V by june 2023Itipingi, Manienga, Matemela, Ipwani and Mkandami villages281,739,160.00
246. MbaraliMbarali DCConstruction of on-going project for Itamboleo WardMatebete, Kapunga and Mbalino  villages150,000,000.00
247. MbaraliMbarali DCExtension construction of water infrastructure for Mkunywa scheme Chalisuka, Mahango and Iheha Villages220,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
248. MbaraliMbarali DCExtension construction of water infrastructure for Ruiwa schemeWimba Mahango, Motomoto, Ijumbi, Udindilwa, Malamba and Ruiwa Villages212,603,385.21
249. MbaraliMbarali DCRehabilitation of water infrastructure for Mbuyuni Schemes  Mbuyuni, Uturo, Ukwavila, Ukwama, Mtamba, Msesule, Itamba, Mabadaga, Nyangulu, Kimani, Ikovo, Ruaha and Mfumbi Village 186,000,000.00
250. MbaraliMbarali DCRehabilitation of water infrastructure for Chimala Schemes Chimala, Igumbilo, Isitu, Lyambogo, Muwale, Mwaluma,Iha hi and Mengele villages 100,000,000.00
  Jumla Mbarali6 1,150,342,545.00
251. Rungwe Rungwe DCConstruction of Masoko II  project (16  Vilages).Kiloba, Lyebe, Njugilo, Segela, Mpombo, Kyambambe mbe, Katundulu, Lubanda, Ilima, Mpumbuli, Mpakani, Matwebe,323,489,048.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Kikole, Ijigha, Masukulu na Kasyeto 
252. Rungwe Busokelo DCNtaba water supplyKambasegela , Katela, Kapulampung uti345,967,876.02
253. Rungwe Rungwe DCIdweli water projectMbeye I and Idweli300,000,000.00
254. Rungwe Rungwe DCConstruction of Lupepo / Mpombo water supplyLupepo and Mpombo200,000,000.00
255. Rungwe Busokelo DCConstruction of Kabembe water supplyKabembe, Lupata, Nsoso, Kilugu, Kibole, Kipapa, Kipyola, Busoka, Kikuba, Mpanda, Ntapisi, Kasyabone, Kifunda, Selya na Bwibuka100,000,000.00
256. Rungwe Busokelo DCConstruction of Kanyelele water supplyKanyelele and Kitema286,719,781.23
257. Rungwe Rungwe DCConstruction of Ikuti-Lyenje water supplyIkuti and Lyenje423,356,304.96
258. Rungwe Rungwe DCConstruction of Kikota water supplyKikota200,000,000.00
259. Rungwe Rungwe DCConstruction of Isaka Water Supply projectIsaka324,024,438.79
  Jumla Rungwe9 2,503,557,449.00
  JUMLA MKOA MBEYA24 8,194,121,281.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
260.MorogoroGairoGairo DCConstruction of Kumbulu Water Supply ProjectKumbulu260,000,000.00
261. GairoGairo DCConstruction of Ching’holwe- Chanjale Water Supply ProjectChanjale and Chingh’olwe280,000,000.00
262. GairoGairo DCConstruction of Chagongwe – Gairo Water Supply ProjectChagongwe, Muheza Ititu, Kisitwi, Kwipipa, Rubeho, Msingisi, Gairo Town, Kibedya and Chakwale600,000,042.00
  Jumla Gairo3 1,140,000,042.00
263. KilomberoKilombero DCConstruction of Mbingu – Igima Water Supply ProjectMbingu, Chiwachiwa, Vigaeni, Igima, Ngajengwa and Mpofu604,560,000.00
264. KilomberoKilombero DCConstruction of Mlimba Water Supply ProjectUdagaji, Chisano, Ngwasi, Mgugwe, Kalengakelu, Msolwa Mlimba, Mlimba A, Mlimba B, Miembeni, Kamwene and Viwanja Sitini641,652,139.61
265. KilomberoKilombero DCRehabilitation of Mangula Water Supply Scheme 150,000,000.00
  Jumla Kilombero3 1,396,212,139.61
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
266. MalinyiMalinyi DCConstruction of Sofi Mission Water supply ProjectSofi Mission100,000,000.00
267. MalinyiMalinyi DCImprovement of Mtimbira Water Supply SchemeKipenyo, Madibira119,905,827.48
268. MalinyiMalinyi DCConstruction of Itete-Njiwa Juu Water supply ProjectNjiwa, Njiwa juu150,000,000.00
269. MalinyiMalinyi DCConstruction of Igawa, Lugala – Kiwale Water Supply Project Igawa, Lugala284,991,332.00
270. MalinyiMalinyi DCConstruction of  Misegese –  Mchangani water Supply ProjectMisegese and Mchangani211,887,938.00
271. MalinyiMalinyi DCConstruction of NgoherangaTanga Water Supply ProjectNgoheranga and Tanga 200,301,517.00
  Jumla Malinyi6 1,067,086,614.48
272. MvomeroMvomero DCRehabilitation of Doma and Melela water Supply SchemesDoma169,761,597.10
273. MvomeroMvomero DCConstruction of Kibogoji- Pandambili Water Supply ProjectKibogoji and Pandambili130,000,000.00
274. MvomeroMvomero DCConstruction of Tchenzema – Luale Water Supply ProjectTchenzema, Kibagala, Kibuko, Londo,Luale, Masalawe130,000,000.00
275. MvomeroMvomero DCConstruction of TandaliHombozaTandali, Homboza, Pekomisege130,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply Projectse, Mlali, Lukuyu, Chehelo 
276. MvomeroMvomero DCConstruction of Lusungi – Mwarazi Water Supply ProjectLusungi, Mwarasi, Nyapeni 121,574,368.64
277. MvomeroMvomero DCImprovement and Extenssion of Turiani Water Supply SchemeMhonda, Manyiga100,000,000.00
278. MvomeroMvomero DCImprovement and Extenssion of Dakawa Water Supply SchemeKwamunzi100,000,000.00
279. MvomeroMvomero DCConstruction of Ndole-Matale water Supply ProjectNdole and Matale171,339,445.50
  Jumla Mvomero8 1,052,675,411.24
280. MorogoroMorogoro DCConstruction of Bwakira Juu gravity water projectBwakira Juu60,000,000.00
281. MorogoroMorogoro DCConstruction of Lundi pumped water projectLundi100,000,000.00
282. MorogoroMorogoro DCConstruction of MkambaraniMkonowamara – Pangawe gravity water projectMkambarani, Mkono wa Mara and Pangawe129,801,965.33
283. MorogoroMorogoro DCConstruction of Morong’anya grouped gravity water projectKibuko, Mkuyuni, Kalundwe, Kivuma, Madam, Kibwaya, Msomvi,120,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Tomondo, Kikundi, Kungwe, Lukonde, Muungamkole , Nyangwambe, Kigwasa, Lubungo, Mikese, Gwata, Maseyu Madam, Kibwaya and Kinonko 
284. MorogoroMorogoro DCCompletion of Gwata water schemeGwata160,000,000.00
285. MorogoroMorogoro DCRehabilitation of Mtamba/Mtom bozi water schemeMtamba, Mtombozi100,000,000.00
286. MorogoroMorogoro DCRehabilitation of Singisa gravity water schemeSingisa60,000,000.00
287. MorogoroMorogoro DCImprovement of pumping scheme for Ngerengere/Si nyaulime Ngerengere, Sinyaulime100,000,000.00
288. MorogoroMorogoro DCImprovement of Mvuha/Dalla gravity water projectMvuha, Dalla129,801,645.33
289. MorogoroMorogoro DCConstruction of Kikundi pumped piped water projectKikundi and Lukonde120,000,000.00
290. MorogoroMorogoro DCImprovement of Kauzeni gravity water projectKauzeni160,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
  Jumla Morogoro DC 11 1,239,603,610.66
291. KilosaKilosaConstruction of Ruaha (Kifinga- Simbalambend e- Nyanvisi- Ruaha- Kitete Msindazi- Kihelezo)Ruaha, Simbalamben e, Nyanvisi and Kitete Msindazi433,141,014.00
292. KilosaKilosaConstruction of Malolo Water Supply ProjectChabi, Malolo A na Malolo B545,745,748.75
293. KilosaKilosaConstruction of  Rudewa  Water supply ProjectRudewa batini, Rudewa Gongoni, Rudewa Mbuyuni na Peapea342,698,908.00
  Jumla Kilosa 3 1,321,585,670.75
294. UlangaUlanga Construction of Mbuyuni Water Supply Project  Mbuyuni150,000,000.00
295. UlangaUlanga Extension of  Lupiro Water Supply SchemeLupiro  50,000,000.00
296. UlangaUlanga Construction of Ebuyu Water Supply Project  Ebuyu and Euga184,988,295.00
297. UlangaUlangaImprovement of RUMWAMCHIL I water Supply SchemeRuaha, Mtukula, Mzerezi, Mgolo, and Chirombora100,000,000.00
298. UlangaUlangaConstruction of  Kikuti Water Supply ProjectKikuti100,000,000.00
299. UlangaUlangaImprovement of Mahenge Water Supply SchemeNawenge,Vig oi, Uponera and Matumbara120,000,000.00
300. UlangaUlangaImprovement of Isongo   Water Supply SchemeIsongo, Mbagura 200,000,000.00
 Jumla Ulanga 7 904,988,295.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 JUMLA MKOA MOROGORO   41 8,122,151,783.74
301.Mtwara MasasiMasasi DCConstruction of Mwena Liloya Water Scheme in MasasiMwena, Chibwini, Ndunda, Mkalapa, Chikundi, Mtunungu, Namali, Msigarila, Mbaju, Chigugu, Mkuyuni, Mbemba, Mandiwa, Mapalagwe, Chikukwe, Mwambao, Liloya, Liloya Chini,43,000,000.00
302. MasasiMasasi DCConstruction of rivango makong’onda Water Supply SchemeMakong’ond a, Mkwaya, Kiridu, Nakalala, Rivango100,000,000.00
303. MasasiMasasi DCRehabilitation and extension of existing Chipingo – Mkaliwata Water Supply SchemeChipingo, Mkaliwala, Manyuli, Mnavira, Chikolopola, Rahaleo, Namyomyo na Mapili50,000,000.00
304. MasasiMasasi DCConstruction of Chidya – Chiwata, Msokosela na Chakama Water Supply SchemeChidya, Chiwata150,000,000.00
305. MasasiMasasi DCRehabilitation of Nanganga Water Supply SchemeNanganga A, Nanganga B, Mkang’u na Mumburu410,938,879.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
306. MasasiMasasi DCRehabilitation of Mkululu Water Supply Scheme Mnolela,  lusonje, Chinolo, Mpulima, Majembe ndago, Likanga, Mputeni, Mkundi, Mkululu shuleni (Chingolopi), Mbugo, Mkwaya421,826,736.00
307. MasasiMasasi DCConstruction of Namatunu Water Supply SchemeNamatunu208,581,482.00
308. MasasiMasasi DCConstruction Mbangala – Mchoti Water Supplt SchemeNantona, Nandembo, Nalimbudi, Mbangala, Utimbe1,327,302,803.64
309. MasasiMasasi DCRehabilitation of Nambawala Water SchemeNambawala A , Nambawala B500,000,000.00
310. MasasiMasasi DCRehabilitation and extension of existing Chipingo – Mkaliwata Water Supply SchemeChipingo, Mkaliwala, Manyuli, Mnavira, Chikolopola, Rahaleo, Namyomyo na Mapili300,000,000.00
311. MasasiMasasi DCConstruction Namalembo Water Supply SchemeNamalembo450,000,000.00
312. MasasiMasasi DCRehabilitation Lulindi Water Supply SchemeMkaseka, Kivukoni, Chiwambo, Luagara, Ndwika Chini591,899,500.00
313. MasasiMasasi DCConstruction ofNanganga,250,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    2 water treatmentsNdanda 
314. MasasiMasasi DCExtension of existing Ndanda Water Supply SchemeNjenga, Mpowora, Liputu, Tuungane, Majengo200,000,000.00
315. MasasiMasasi DCExtension of existing Chipango Water Supply SchemeChipango443,899,619.00
  Jumla Masasi 15 5,447,449,019.64
316. Mtwara Mtwara DCConstruction of MitamboMsimbati  Water supply Project Mitambo, Litembe, Mngoji,Mnuy o,Ruvula,Mt andi and Msimbati736,271,230.00
317. Mtwara Mtwara DCConstruction of Mnyundo Mwatehi and Makome water supply projectMnyundo, Mwatehi, Makome, Makome B500,000,000.00
318. Mtwara Mtwara DCConstruction of Nalingu water supply projectNalingu,Mne te,Mnazi and Milamba363,728,770.00
319. Mtwara Mtwara DCExtension of Chemchem water  supply scheme to Chekeleni VillageLilido,Nakad a,Cheleni,Kit ere501,790,092.00
320. Mtwara Nanyamba TcConstruction of NgonjaKihamba Kitaya water supply schemeKihamba, Kitaya and Dindwa500,000,000.00
321. MtwaraNanyamba TCDrilling of 5 productive boreholes at Kiyanga, Kiwengulo, Ngoja,Kiyanga, Kiwengulo, Ngoja, Mayembe Juu and Nanguruwe166,825,282
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mayembe Juu and Nanguruwe  
  Jumla Mtwara DC5 2,601,790,092.00  
322. NanyumbuNanyumbu DCConstruction of Mitumbati     – Chilunda Chilunda300,000,000.00
  Jumla Nanyumbu1 300,000,000.00
323. TandahimbaTandahimba DCConstruction of Nanyuwila- Maundo Water supply Project in Tandahimba DistrictNakayaka, Mnyawa, Mchichira, Mkwajuni, Shangani, Pachani, Mnarani, Namahonga, Maundo, Chiumo, Chang’ombe, Kunandundu, Lukokoda, Ghanajuu, Ghanachini 663,712,064.00
324. TandahimbaTandahimba DCConstruction of  Mkwiti Lot 3&4 Water supply Project        in Tandahimba District.(New)Mangombya, Nannala, Nanjanga, Chidede, Mkwiti juu, Mkwiti chini, Mabeti, mmeda, Ngunja, Mahoha, Namindondi juu, Namindondi chini, Mkola juu, Litehu, Libobe, Michinji, Mkolachini654,167,305.00
 Jumla Tandahimba2 1,317,879,369.00
325. NewalaNewala DCCompletion of Miyuyu na50,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    on Going Miyuyu & Mnima Lot 6Mnima 
326. NewalaNewala DCImprovement of water supply in peri urban areas at Newala Town shipMnaida, Tawala, Mitumbati, Msilili, Lidumbe, Mcholi Godauni, Chiwhindi, Tumaini, Kiuta, Mkunya, Matokeo, Rahaleo and Kikuyu50,000,000.00
327. NewalaNewala DCCompletion of Miyuyu & Mnima Lot 1, 2, 3, 4 and 5Miyuyu, Mnima, Chihangu, Navanga, Chilangala, Mikumbi, Mkongi, Mkoma II, Namangudu, Nangudyane , Mnyambe, Kadengwa, Maputi, Mtongwele chini, Majembe juu, Hengapano, Bahati and Mtongwele juu250,000,000.00
328. NewalaNewala DCConstruction of Mkoma II Water ProjectMkongi, Mkoma II, Namangudu, Nangudyane , Nachilembe 300,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
329. NewalaNewala DCExtension of Mnima water project to Majembe juu Hengapano, Majembe juu and Ngapano   200,000,000.00
330. NewalaNewala DCExtension of Malatu water Supply Scheme to, Nameno, Mpwapwa and SongambeleNameno, Mpwapwa and Songambele200,000,000.00
331. NewalaNewala DCExtension Water supply Scheme from Lokohe to Chitekete, Mchanganuo, Nambudi, NamkondaChitekete, Mchanganuo , Nambudi, Namkonda300,000,000.00
332. NewalaNewala DCImprovement of water supply Project in peri urban areas at Newala Town ship(Mnaida,T awala,Mitumba ti,Msilili,lidumb e,Mcholigodau ni,chiwindi,Tu maini,Kiuta,Mk unya,Matokeo, Rahaleo,Kikuy u.Mnaida,Taw ala,Mitumbat i,Msilili,lidum be,Mcholigo dauni,chiwin di,Tumaini,Ki uta,Mkunya, Matokeo,Ra haleo,Kikuyu350,000,000.00
333. NewalaNewala DCConstruction of Mnolela Water SupplyMinola50,000,000.00
334. NewalaNewala DCConstruction of Chiunjila Water supply project (Mpilili na ChikweduChipamanda,C hiunjila)Mpilili and ChikweduChipamanda ,Chiunjila300,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
335. NewalaNewala DCCompletion of Covid ProjectsChiunjila, Mpilipili, Chikwedu, Mandala, Mkupete, Mnali and Namkonda50,000,000.00
336. NewalaNewala DCConstruction of Chitandi Water suply project  (luchinguamkeni,Nangw ala-machinjion, ChitandiChitandi, Nangwala, Luchingu and Amkeni 100,000,000.00
  Jumla Newala 16 2,200,000,000.00
 JUMLA MKOA MTWARA 39 11,867,118,480.6 4
337.MwanzaUkereweUkerewe DCCompletion of on-going projects (Muriti /Ihebo water Supply)Muriti, Ihebo and Itira40,000,000.00
338. UkereweUkerewe DCRehabilitation of Irugwa Water Supply ProjectSambi and Nabweko30,000,000.00
339. UkereweUkerewe DCRehabilitation of Kazilankanda_ Murutanga Water Supply ProjectMurutanga30,000,000.00
340. UkereweUkerewe DCConstruction of Sizu _Ghana Water ProjectSizu and Ghana597,970,100.00
341. UkereweUkerewe DCConstruction of Gallu_Mibungo Water ProjectsGallu, Mibungo, Murutilima, Masonga, Nakamwa,117,433,680.00
342. UkereweUkerewe DCConstruction of Ukara water Supply ProjectBwisya, Nyang’ombe, Bukiko, Kome, Chifule,126,153,278.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Chibasi, Bukungu and Nyamanga 
343. UkereweUkerewe DCConstruction of Bukondo_ Selema Water Supply ProjectBukondo and Selema100,000,000.00
344. UkereweUkerewe DCExtension of Chankamba water supply projectChankamba100,000,000.00
345. UkereweUkerewe DCExtension of Igongo water supply projectIgongo203,121,469.00
346. UkereweUkerewe DCExtension of Muhande_Buz egwe water supply projectMuhande, Buguza, Buzegwe and Nampisi366,085,000.00
 Jumla Ukerewe9 1,710,763,527.00
347. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing Mhulya water supply projectMhulya448,019,986.56
348. KwimbaKwimba DCHydrogeologica l Survey and Water Well Drilling for  16 boreholesMwapulu, Shilanona, Bugandando, Bujingwa, Goloma, Busule, Kinamweri, Mwagighi, Kitunga, Nyambuyi, Nyamatala, Mwamhembo , Mwankuba, Ibindo, Ngogo, Nyamigamba63,788,478.44
349. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing Nkalalo-Lyoma water suppy projectNkalalo, Lyoma1,828,408,657.44
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
350. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing Ng’hundyaMhulula water supply projectNg’hundya, Mhulula10,000,000.00
351. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing Walla water supply projectSuamaha, Isagala10,000,000.00
352. KwimbaKwimba DCComletion of ongoing Ligembe water supply project Ligembe10,000,000.00
353. KwimbaKwimba DCCompletion of Mwadubi and Manguluma water supply project LOT 1Mwadubi10,000,000.00
354. KwimbaKwimba DCCompletion Mwadubi and Manguluma water supply project LOT 2Manguluma20,000,000.00
355. KwimbaKwimba DCCompletion of Hungumalwa water supply projectHungumalwa , Buyogo, Ilula, Kibitilwa10,000,000.00
356. KwimbaKwimba DCCompletion of Shigumhulo – Nyamilama water supply projectShigumhulo, Nyamilama10,000,000.00
357. KwimbaKwimba DCRehabilitation of Water infrastructure at Mwamashimba scheme Mwamashimb a10,000,000.00
358. KwimbaKwimba DCRehabilitation of Water infrastructure at Sumve SchemeSumve  10,000,000.00
359. KwimbaKwimba DCRehabilitation of Water infrastructureMalya10,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    at Malya scheme   
360. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing extension of Jojiro Water Supply scheme to Malemve Malemve663,765,967
361. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing extension of Ng’huliku Water Supply scheme to ShilemboShilembo810,234,235
362. KwimbaKwimba DCCompletion of ongoing Mhulya water supply projectMhulya448,019,986.56
 JUmla Kwimba15 3,924,217,324.44
363. MisungwiMisungwi DCCompletion of Kigogo water supply projectKigongo, Bukumbi, Chole, Mwasongwe, Isamilo na Mayolwa1,463,585,076.00
364. MisungwiMisungwi DCCompletion of IlujamateBuhingo water supply projectMwagimagi, Buhunda, Mbalama, Ng’yamve, Lukanga, Kifune, Nyamayiza, Nyambiti, Busongo, Seeke, Buhingo, Kabale Songiwe na Mwasegela20,699,301.76
365. MisungwiMisungwi DCCompletion of Ukirigulu water supply projectMwalogwaba gole, Buganda,26,699,301.76
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Nyang’olongo , Nyamatala, Ngudama, Nyamle, Nyamikoma, Mwagala, Mamaye, Ibongoya A & B, Kolomije Lukelege na Bugomba, Usagala, Itende, Nyang’omang o, Idetemya na sanjo 
366. MisungwiMisungwi DCCompletion of Gunge water supply projectNguge, Maganzo and Mwalwigi12,000,000.00
367. MisungwiMisungwi DCConstruction of shilalo water supply (CBWSOs and Security guard house)Mwamboku, Ng’obo, Shilalo and Ikungumhulu16,699,301.76
368. MisungwiMisungwi DCCompletion of Fella water supply project Usagara15,754,964.97
369. MisungwiMisungwi DCCompletion of Matale, Manawa and Misasi water supply project Matale, Kasololo, Nduha , Isuka, Manawa , Misasi10,000,000.00
370. MisungwiMisungwi DCCompletion of Mwamagili- Mwagiligili water supply project Mwagiligili11,699,301.76
371. MisungwiMisungwi DCCompletion of Mabuki water supply project Mwabuki, Mwagagala and Mwanangwa5,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
372. MisungwiMisungwi DCConstruction of Mbarika – Ngaya Water supplyLutalutale, Bugisha na Ngaya12,000,000.00
373. MisungwiMisungwi DCCompletion of Nyashitanda water supply project Nyashitanda10,000,000.00
374. MisungwiMisungwi DCConstruction of Ngaya – Matale Water supplyIkula, Sumbugu24,148,770.00
375. MisungwiMisungwi DCConstruction of Igongwa Water supplyIgongwa10,000,000.00
376. MisungwiMisungwi DCExtension of Ilalambogo Water Supply Scheme to Ng’wamazengoNg’wamazen go10,000,000.00
377. MisungwiMisungwi DCGeophysical Survey and DrIllingi of 2 productive bore holesIbongoya A, Koromije5,000,000.00
 Jumla Misungwi15–   1,653,286,018.01
378. SengeremaBuchosa DC Construction of Bugoro Water Supply ProjectBugoro, Chanika, Mgogo, Lugata, Izindabo, Nyakabanga435,000,000.00
379. SengeremaBuchosa DC Construction of Kazunzu Water Supply ProjectKakobe na Nyambeba.443,452,532.00
380.  Buchosa DCHydrogeologic al Survey and Water Well Drilling for 13 boreholesKisaba, Busikimbi, Nyakabanga , Nyonga, Bugoro, Mwambao, Irenza, Luharanyoga , Katoma,122,679,990.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Kasalaji, Migukulama, Nyamkolechi wa 
381. SengeremaBuchosa DC Construction of Bupandwa Water Supply ProjectBupandwamh ela, Mnazi Mmoja, Chema, Italabusiga, Chamanyete, Mwangika, Katwe and Kahunda941,209,950.00
382. SengeremaBuchosa DC Construction of Kafunzo Water Supply ProjectKafunzo, Luhorongoma and Bilulumo440,000,000.00
383. SengeremaBuchosa DCExtension to Kasela Water SupplyKasela84,625,674.00
384. SengeremaBuchosa DCExtension to Lumeya Water SupplyLumeya42,195,403.00
385. SengeremaSengerema DC Extension of Sima water supply ProjectSima, Sogoso, Igulumuki, Igaka472,779,211.00
386. SengeremaSengerema DC Extension of Nyamililo water supply ProjectNyamilio, Kasungamile347,617,275.00
387. SengeremaSengerema DCHydrogeologica l Survey and Water Well Drilling for for 38 boreholesKagunga, Nyasigu, Lubungo, Ngoma, Sotta, Mami, Kishinda, Isebya, Tunyenye, Butonga, Igulumuki, Ijinga, Igaka, Isome, Kanyelele, Ikoni, Buzilasoga,105,645,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Sima, Sogoso, Ishishang’ holo, Nyitundu, Kahumulo, Lubanda, Ilekanilo, Kasungamile, Nyamililo, Nyamasale, Lukumbi, Nyakahako, Chifunfu, Igalagalilo, Kabusuli, Karumo, Nyamatongo, Kamanga 
388. SengeremaSengerema DC Construction of Chifunfu Water Supply ProjectChifunfu, Lukumbi and Nyakahako325,000,000.00
389. SengeremaSengerema DC Construction of Nyitundu Water Supply ProjectNyitundu, Lubanda and Kahumulo325,000,000.00
390. SengeremaSengerema DC Construction of Karumo Water Supply ProjectKarumo, Kabusiri, Kamanga and Nyamatongo375,539,696.00
391. SengeremaSengerema DCExtension to Mayuya- Elikanilo Water SupplyMayuya and Ilekanilo25,161,936.00
392. SengeremaSengerema DCRehabilitation of 5 boreholes (changing/upgr ading from handpump to solar system with DP)Nyamasale, Isole, Igulumuki and Mulaga105,645,525.00
 Jumla Sengerema154,591,552,192.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
393. MaguMagu DCTo extend Magu town water supply scheme to Sagani- Mwamabanza villages.Sagani, Mwalinha, salongwe na Mwamabanz a806,897,716.00
394. MaguMagu DCTo extend Magu town water supply scheme to Nyag’hanga – Iseni villages.Buhumbi, Nyashoshi, Nyanghanga na Iseni200,000,000.00
395. MaguMagu DCTo extend Magu town water supply scheme to Misungwi – Lumeji villages.Misungwi, Kitongo and Lumeji 164,617,358.00
396. MaguMagu DCTo implement On-going Water Supply project at Bugando – Chabula VillagesBugando, Chabula, Kongolo and Nyashigwe100,000,000.00
397. MaguMagu DCTo implement On-going project of Geophysical Survey and DrIllingi of 19 productive bore holesMwamabanz a, Mwalina, Salomwe, Salama, Bugatu, mwabulenga, Ihayabuyaga, Isangijo, Welamasong a, IHaujasa nifiwalelo, Mwamanga, Chandulu, Nhobola, Mwatelesha, Sese, Mondo, Mahaha, Kashishi, chabalogi.57,198,405.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Magu51,328,713,479.00
 JUMLA MKOA MWANZA59 13,656,552,527.0 1
398.NjombeLudewaLudewa DCRehabilitation of gravity main, Intake, extention of Nsungu village, Sagalu sub village, and Mbongo villageNsungu village, Sagalu sub village, and Mbongo150,000,000.00
399. LudewaLudewa DCConstruction of pumping water supply project at MavalaMavala100,000,000.00
400. LudewaLudewa DCConstruction of gravity water supply project at Madope Madope212,444,388.00
401.   Construction of ludewa Town water projectLudewa Mjini600,000,000
 Jumla Ludewa4 1,062,444,388.00   
402. NjombeNjombe DCRehabilitation of pumping water supply Schemes at Lupembe and construction of Matembwe – Iyembela schemes.Lupembe na Iyembela  100,000,000.00
403. NjombeNjombe DCConstruction completion of Nyombo Pumping water Scheme Nyombo, Ninga 659,730,555.80
 Jumla Njombe DC2 759,730,555.80
404. NjombeNjombe TCConstruction of gravity scheme lugenge-Kisilo-Kisilo, Ihalula na Utalingolo75,851,638.25
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Utalingolo LOT3  
405. NjombeNjombe TCConstruction of gravity scheme Igongwi group (Lot 1), Lot 2, Lot 3 and Lot 4Kitulila, Madobole, Luponde and Njomlole623,755,373.00
  Jumla Njombe TC2 699,607,011.25
406. NjombeMakambako TCConstruction of Ikelu Pumping Water Supply ProjectIkelu150,000,000.00
407. NjombeMakambako TCConstruction of Ibatu Pumping Water Supply ProjectIbatu50,000,000.00
408. NjombeMakambako TCConstruction of Usetule, Mahongole Gravity group Water Supply projectUsetule na Mahongole250,000,000.00
409. NjombeMakambako TCConstruction of Mtulingala, Mbugani and Nyamande Pumping Water Supply ProjectMtulingala, Mbugani na Nyamande50,000,000.00
 Jumla Makambato TC4 500,000,000.00
410. NjombeMakete DCConstruction of Maliwa- Ikete water supply project (PHASE II)Maliwa na Ikete150,201,500.00
411. NjombeMakete DCConstruction of water supply project at Uganga and Utanziwa (Phase II)Uganga na Utanziwa72,918,952.00
412. NjombeMakete DCConstruction of water supply project atIdende, Unenamwa149,798,500.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Idende- Unenamwa  
413. NjombeMakete DCConstruction of water supply project at Utweve and Lupila villageUtweve, Lupila102,650,000.00
414. NjombeMakete DCRehabilitation of Kidope Madihani water supply schemeKidope, Nkunga, Lumage na Madihani101,550,050.40
415. NjombeMakete DCRehabilitation of Usalimwani, Mfumbi and Ruaha water supply scheme.usalimwani, Mfumbi na Ruaha120,079,500.70
416. NjombeMakete DCExtension of water supply schemes in Ipelele and Ipepo villageIpelele, Misiwa, Mbanga, Makeve, Ubiluko na Ipepo75,955,170.30
417. NjombeMakete DCRehabilitation of Makusi, Luwumbu water supply projectsMakusi and Luwumbu90,449,999.50
 Jumla Makete DC8 863,603,672.90
418. Wanging’o mbeWanging’om be DCConstruction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Malangali and Hanjawanu)Malangali, Hanjawanu150,000,000.00
  Wanging’o mbeWanging’om be DCExtension of Igando – Kijombe Gravity Water Supply Scheme in Mpanga naMpanga and Wangamiko20,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Wangamiko Villages  
419. Wanging’o mbeWanging’om be DCExtension of gravity water supply at Ng’anda- Uhekule VillagesNg’anda, Uhekule15,000,000.00
420. Wanging’o mbeWanging’om be DCConstruction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Hanjawanu- Kijombe villages)Hanjawanu and Kijombe315,000,000.00
421. Wanging’o mbeWanging’om be DCImprove water supply service for WANGIWASA National water project in Wanging’ombe village WANGIWAS A211,200,000.00
422.  Wanging’om be DCExtension of gravity water supply at Imalilo, Kinenulo, Msaulwa and Kilanzi VillagesImalilo, Kinenulo, Masaulwa, Kilanzi20,000,000.00
423. Wanging’o mbeWanging’om be DCConstruction of gravity water supply scheme for Igando – Kijombe Phase II (Malangali and Hanjawanu)Malangali, Hanjawanu150,000,000.00
  Jumla Wanging’ombe7 881,200,000.00
  JUMLA MKOA NJOMBE25 4,766,585,627.95
424.PwaniMkuranga Mkuranga DC Construction of water infrastructureKimanzichan a Kusini, Kimanzichan286,115,838.40
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    at Kimanzichana Magharibi, Kimanzichana Kaskazini and Kimanzichana Kusini villages a Kaskazini, Kimanzichan a Magharibi 
425. Mkuranga Mkuranga DC Construction of water infrastructure at Mwanambaya, Mdimni and Mkerezange villages Mdimni, Nganje, Mkerezange, Kigoda, Mwanambay a200,000,000.00
426. Mkuranga Mkuranga DC To construct water infrastructure at Nasibugani and Njopeka villages Nasibugani, Dondo, Sotele and Njopeka240,000,000.00
  Jumla Mkuranga3 726,115,838.40
427. BagamoyoChalinze DCCompletion of on-going projects (Matipwili water Suppy project)Matipwili1,014,215,594.44
428. BagamoyoBagamoyo DCExtention of Fukayosi water supply projectFukayosi350,344,596.0
429. BagamoyoBagamoyo DCConstruction of Mkoko water supply projectMkoko348,419,933,0
430. BagamoyoBagamoyo DCCompletion of Kitame water supply projectKitame268,992,016.39
431. BagamoyoBagamoyo DCRehabilitation of Milo and Kidogozero Water Supply SchemeMilo and Kidogozero583,683,499.87
  Jumla Bagamoyo DC5 2,217,235,706.70
432.  Kisarawe DCExtension of Chole-KwalaPangalamwi ngereza and479,943,996.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply Scheme for Panga la Mwingereza and KuruiChole Villages.Kurui  
433.  Kisarawe DCRehabilitation of Gwata, Ngongele and Vikumbur Water Supply Schemes.Gwata, Ngongele, Vikumburu555,784,773.16
 Jumla Kisarawe 3 1,035,728,769.16
434. MafiaMafia DCConstruction of Water Supply Scheme at Jimbo (Kidika) and Chunguruma (Tumbuju)Jimbo (Kidika) and Chunguruma (Tumbuju)70,000,000.00
435. MafiaMafia DCConstruction of Kilindoni Village Water Supply Scheme in Mafia DistrictKilindoni879,937,895.13
436. MafiaMafia DCConstruction of Kiegeani Village Water Supply Scheme in Mafia DistrictKiegeani279,126,916.80
437. MafiaMafia DCConstruction of Kifinge Village Water Supply Scheme in Mafia District by June 2023Kifinge382,008,196.20
438. MafiaMafia DCConstruction of Banja village Water supply Scheme in Mafia District by June 2023Banja408,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Mafia5 5,161,900,406.13
439. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Mahege village Mahege38,850,199.50
440. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Mchungu village Mchungu54,319,293.88
441. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Kilulatambwe village Kilulatambwe136,945,357.76
442. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Mtunda village Mtunda152,837,278.40
443. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Mjawa village Mjawa141,152,243.83
444. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Nyanjati, Nyakinyo, Msindaji and Kivinja A villages Nyanjati, Nyakinyo, Msindaji and Kivinja A villages179,430,941.21
445. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Mlanzi village Mlanzi177,649,184.00
446. KibitiKibiti DC Construction of water infrastructure at Bumbamsoro village Bumbamsoro190,028,016.00
447. KibitiKibiti DC Rehabilitation of Water infrastucture at Mtawanya &Mtawanya & Jaribu Mpakani175,571,831.63
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Jaribu Mpakani villages   
448. KibitiKibiti DC Rehabilitation of Water infrastucture at Uponda Mchukwi & Mkenda/Kivinja B Villages villages Uponda, Mchukwi & Mkenda/Kivi nja B153,040,623.25
  Jumla Kibiti10 1,399,824,969.47
449. RufijiRufiji DCConstruction of  Water Supply scheme at NambunjuNambunju345,469,569.80
450. RufijiRufiji DCConstruction of Water Supply scheme at ChumbiChumbi479,797,051.20
451. RufijiRufiji DCConstruction of Water Supply scheme at Tawi.Tawi56,218,579.28
452. RufijiRufiji DCConstruction of Water Supply scheme at SiasaSiasa133,409,256.75
453.PwaniRufijiRufiji DCGeophisical survey and Drilling of 9 bore holes in the villages of Mwaseni, Mibuyusaba, Ndundunyikanz a, Kipugira, Mbunju, Mvuleni, King’ongo, Mohoro Sec and Nyamwage.  Mwaseni, Mibuyusaba, Ndundunyika nza, Kipugira, Mbunju, Mvuleni, King’ongo, Mohoro Sec and Nyamwage.  327,727,200.00  
 Jumla  Rufiji DC5 1,342,621,657.03
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
454. KibahaKibaha DCConstruction of Piped Water Supply Project for Kwala and construction of source in Kibaha District Kwala689,542,324.80
455. KibahaKibaha DCConstruction of Piped Water Supply Project for Kimara Misale in Kibaha DistrictKimara misake49,870,953.60
456. KibahaKibaha DCConstruction of Piped Water Supply Project for Ruvu Station in Kibaha District Ruvu station276,911,851.60
457. KibahaKibaha DCGeophysical survey and Drilling of 3 boreholes at Vinyenze, Miyombo and Masaki,   Vinyenze, Miyombo and Masaki,                    76,936,000.00   
  Jumla Kibaha DC4 1,093,261,130.00
  JUMLA MKOA PWANI34 9,833,861,078.89
458.RukwaKalamboKalambo DCConstruction of Legezamwendo Water Supply Project to serve six villages of Mkombo,Uteng ule,Mlenje,Kale mbe,Mombo and LegezamwendoMkombo,Ute ngule,Mlenje, Kalembe,Mo mbo and Legezamwen do400,000,000.00
459. KalamboKalambo DCConstruction of Matai Water Supply Project to serve four villages ofMatai B, Namlangwa, Keleni and St Maria581,425,406.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Matai B,Namlangwa, Keleni and St Maria  
460. KalamboKalambo DCConstruction of Luse Water Supply Project to serve Luse VillageLuse150,000,000.00
461. KalamboKalambo DCConstruction of Kafukula Water Supply Project to serve Kafukula VillageKafukula285,405,214.00
462. KalamboKalambo DCCompletion of Kisumba Water Supply Scheme to serve 4 villages of Kafukoka,Kisu mba,Kasote and ChisengaKafukoka,Kis umba,Kasot e and Chisenga200,000,000.00
463. KalamboKalambo DCConstruction of Extension of Sopa Water Supply Scheme to Mtuntumbe VillageMtuntumbe200,000,000.00
464. KalamboKalambo DCConstruction of Kipwa Water Supply ProjectKipwa and Kapere200,000,000.00
465. KalamboKalambo DCConstruction of Mwimbi Water Supply Project to serves two villages of Mwimbi and MajengoMwimbi and Majengo205,379,636.00
466. KalamboKalambo DCCompletion rehabilitation of KamaweKamawe300,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply Scheme  
467. KalamboKalambo DCCompletion of Kilewani Water Supply ProjectKilewani24,000,000.00
  Jumla Kalambo  DC10 2,546,210,256.00
468. Sumbawanga Sumbawanga DCRehabilitation and Extension of Mtowisa Water Projects Ng’ongo,Mto wisa B,Sontaukia, Mtowisa A447,240,945.00
469. Sumbawanga Sumbawanga DCRehabillitaion and Extension of Ilemba Water Supply Project.Ilemba A,Ilemba B and Kaswepa520,000,000.00
470. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Mkunda Group Gravity Water Supply ProjectMkunda,Kae ngesa A,Kaengesa B na Kianda600,000,000.00
471. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Lula chite Water Supply Project Lula And Chitete700,000,000.00
472. Sumbawanga Sumbawanga DCExtension of Kaseklea-Msila Gravity Water Supply Project Kasekela and Msila407,184,750.00
473. Sumbawanga Sumbawanga DCExtension of MsandaMuung ano Water Supply Project MsandaMuu ngano A   and B190,762,712.00
474. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Ngomen Water Supply Project Ngomeni233,303,628.80
475. Sumbawanga Sumbawanga DCRehabilitation  of Mpembano Water Supply Project Mpembano92,815,250.00
476. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Kalambanzite Group Gravity Water Supply ProjectKalambanzit e,Mleche,Kil embo na Mshani960,742,274.20
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
477. Sumbawanga Sumbawanga MCRehabillitaion and Extension of Katumba Water Supply Project.Katumba and Nambogo25,000,000.00
478. Sumbawanga Sumbawanga MCConstruction of Luwa Water Supply Project Luwa25,000,000.00
479. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Earth dam Water Supply scheme at ikozi  village.Ikozi,Tentula, Kazwila and Chituo60,000,000.00
480. Sumbawanga Sumbawanga DCConstruction of Kaoze Group Gravity Water Supply ProjectKaoze53,991,615.00
  Jumla Sumbawanga  DC13 4,316,041,175.00
481. NkasiNkasi DCConstructions of Korongwe Water Projects Korongwe and Forodhani502,009,085.16
482. NkasiNkasi DCConstruction of Masolo Water Supply Project Masolo151,976,616.36
483. NkasiNkasi DCConstruction of Itindi Water Supply Project Itindi372,575,308.80
484. NkasiNkasi DCConstruction of Kacheche Water Supply Project Kacheche125,016,472.40
485. NkasiNkasi DCConstruction of Lyazumbi Water Supply Project Lyazumbi28,482,317.00
486. NkasiNkasi DCConstruction of  Matala Water Supply Project Matala248,594,099.63
487. NkasiNkasi DCConstruction of  Isale Water Supply Project Isale, Msilihofu, Ifindwa, Ntuchi, Kitosi and Nkata655,294,516.65
488. NkasiNkasi DCConstruction of Kakoma127,805,563.23
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Kakoma Water Supply Project   
489. NkasiNkasi DCConstructions of Tambaruka water supply ProjectTambaruka160,000,000.00
  Jumla Nkasi  DC9 2,371,753,979.23
  JUMLA MKOA RUKWA32– 9,234,005,410.23
490.RuvumaMbingaMbinga DCConstruction of water scheme at Luhagara,Kitai, Ngima and Kuhuruku in Mbinga DCLuhagara,Kit ai,Ngima and Kuhuruku193,200,584.00
491. MbingaMbinga DCRehabilitation of Maguu Gravity Water Supply Scheme in Mbinga DCMaguu,Mku wani,Mkuka, Kindfai A and Kibandaiasili715,233,458.85
492. MbingaMbinga TC Construction of Gravity Water Supply Scheme for Mbangamao in Mbinga TC Mbangamao115,703,490.00
493. MbingaMbinga TCConstruction of Gravity Water Supply Scheme for Ruvuma chini Village in Mbinga TCRuvumachini115,703,490.00
494. MbingaMbinga TCConstruction of Tanga Gravity Water Supply Scheme in Mbinga TCTanga115,703,490.00
495. MbingaMbinga TC Construction of Gravity Water Supply Scheme for  Utiri in MbingaUtiri115,703,490.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    TC   
496. MbingaMbinga TCConstruction of Gravity Water Supply Scheme    for Kitanda Village in Mbinga TCKitanda115,703,490.00
  Jumla Mbinga DC7 1,486,951,492.85
497. Nyasa Nyasa DCConstruction of Nangombo Kilosa            water supply scheme.Nangombo, Kilosa, Luhekei and Likwilu431,135,960.00
498. Nyasa Nyasa DCConstruction of Malungu water supply scheme.Tingi   and malungu322,374,419.00
499. Nyasa Nyasa DCConstruction of Lituhi group water            supply scheme.Lituhi, Kihuru, Nkaya, Mwerampya, Ndumbi, Liweta and Mbaha780,050,519.68
500. Nyasa Nyasa DCConstruction of Liuli group water supply schemeLiuli, Nkalachi, Hongi, Mkali A and Mkali B538,000,000.00
501. Nyasa Nyasa DCConstruction of PuuluSongambele water supply scheme.Puulu, Songambele , Ngehe and Mango200,000,000.00
502. Nyasa Nyasa DCConstruction of Ngumbo group water supply schemeHinga, Ngumbo, Mbuli, Mkili, Ndonga, Liwundi, and Yola419,543,568.00
  Jumla Nyasa DC6 2,691,104,466.68
503. TunduruTunduru DCConstruction of SchemesMbesa, Lijombo,543,733,198.29
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    (Ndaje- Mbesa water supply scheme (Mbesa,Lijomb o and Airport)Airport 
504. TunduruTunduru DCConstuction of MasuguruMchoteka water supply Scheme (Masuguru,Mc hoteka,Mcheke ni,Katani,Likwe so,Mkolola and Mnemasi)Masuguru, Mchekeni, Kitani, Likweso, Mchoteka, Mkolola, and Mnemasi882,065,887.52
505. TunduruTunduru DC Extension of Kazamoyo, Majimaji, Chalinze, Sautimoja, Ligoma, Makoteni, Imani    water Schemes Majimaji, Chalinze, Sautimoja, Ligoma, Makoteni, Imani1,048,250,664.29
506. TunduruTunduru DC Rehabilitation of Namwinyu and Nalasi  Water supply Schemes Namwinyu, Namakungw a,            Nalasi, Lipepo, Chilundundu Kus, Chilundundu Kaz150,000,000.00
507. TunduruTunduru DCConducting Geophyical Survey    and Drilling of 15 productive boreholesNalasi, Azimio, Semeni, Majala, Muhuwesi, Sisikwasisi, Ligunga, Mtengashari, Angalia, Mwenge, Fudnimbang a, Malombe,520,000,000
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Namwinyu, Tumaini and Nampungu, Nakapanya, Hulia and Mchangnai ( Kazamoyo). 
  Jumla Tunduru DC5 3,144,049,750.10
508. Songea Songea DCConstruction of Mbangamawe water supply SchemeMbangamawe245,639,691.24
509. Songea Songea DCConstruction of  Kizuka, Lipaya, Lipokela   water supply Schemes Kizuka, , Lipaya, Lipokela1,209,484,448.89
510. Songea Songea DCConstruction of Lutukira   water supply SchemeLutukira, Ndelenyuma 350,000,000.00
511. Songea Songea DCConstruction of Mtyangimbole  water supply SchemeMtyangimbol e, Likalangilo na Luhimba1,150,000,000.00
512. Songea Songea DCConducting Geophyical Survey and Drilling of 9 productive boreholesLiganga, Nambendo, Chiulungu, Kitulo, Mpandangin do, Namagma.535,136,744.00  
  Jumla Songea DC5 3,490,260,884.13
513. NamtumboNamtumbo DCConstruction Luhimbalilo/Nai kes (PHASE II Distribution)Luhimbalilo and Naikesi200,000,000.00
514. NamtumboNamtumbo DCConstruction of Mgombasi Water Supply ProjectMgombasi, Nangero and Mtumbatimaji656,817,900.00
515. NamtumboNamtumboConstruction ofLigera and150,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
   DCWater Supply project at LigeraMuungano 
516. Namtumbo Namtumbo DCConducting Geophyical Survey and Drilling of 15 productive boreholesMchomro, Kilimasera, Kitanda Mtakanini, Chengena, Misufini, Mtelawamwai , Jiungeni, Namali, Matepwende, Mlilayoyo, Mageuzi.408,000,000.00
  Jumla Namtumbo DC401,414,817,900.00
 JUMLA MKOA RUVUMA 27012,227,184,493.7 6
517.ShinyangaKishapuKishapu DCCompletion of Nyasamba/Mw amishoni  water supply ProjectNyasamba and Mwamishoni309,425,025.00
518. KishapuKishapu DCCompletion of Mwangongo, Seseko   and Ngundangali Water Supply ProjectMwangongo, Ngundangali and Seseko, Kakola, Mpumbula and Dugushilu190,000,000.00
519. KishapuKishapu DCConstruction of on-going Project atMasanga/ Ndoleleji ProjectMasanga and Ndoleleja182,853,826.6
520. KishapuKishapu DCExtension of Maganzo    to Masagala Water Supply ProjectMaganzo and Masagala319,258,560.00
521. KishapuKishapu DCConstructionof Ligaga, IsagalaIgaga       A, Igaga       B,433,102,656.03
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    and Tulagana Water Supply ProjectIsagala, Mwamashele , Busongo,Bu binza, Lwagalalo, Lagana, Mihama, Beledi, Mwamadulu, Nyawa    na Mwamanota. 
522. KishapuKishapu DcCompletion of Bupigi/Butung wa        Water Supply Project Bupigi             and Butungwa  30,000,000.00 
523. KishapuKishapu DcGeophysical Survey and Drilling of three boreholes at Itilima, Nhobola and Ipeja villages Itilima, Nhobola and Ipeja94,328,844.00 
 Jumla Kishapu  728 1,558,968,911.63 
524. KahamaKahama MCExtension of Ngogwa – Kitwana water supply project to Wendele village.Wendele and Tumaini5,000,000.00
525. KahamaKahama MCExtension of Zongomera Water Supply Scheme to Nyandekwa in Kahama MunicipalNyankendwa , Lowa and Buduba9,000,000.00
526. KahamaMsalala DCConstruction of piped water supply scheme at Mwaningi and Mwazimba and RehabilitationMwaningi, Mwazimba an Bulige820,166,678.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    of Bulige water supply scheme at Msalala DC by June 2023  
527. KahamaMsalala DCExtension of Kagongwa- Isaka water supply scheme to Butondolo, Jana, Mwalugulu and Kilimbu villages at Msalala DC by June 2023Butondolo, Jana, Mwalugulu and Kilimbu720,000,000.00
528. KahamaMsalala DCExtension of Mhangu- Ilogi water Supply Scheme at Lwabakanga, Kakola No.9, Bugarama na Ilogi at Msalala Dc by June 2023Ilogi, Bugarama, Lwabakanga , Kakola 09, Kakola and Bushing’we765,605,150.00
529. KahamaMsalala DCExtension of Nduku Busangi water Scheme at Msalala DC by June 2023Busangi Nyamigege and Ntundu70,782,481.00
530. KahamaMsalala DCConstruction of piped Water Supply from Mhangu to Ilogi under Joint Water Partnership Project at Msalala DC by June 2023Ilogi, Buarama, Lwabakanga , Kakola 09, Kakola and Bushing’we200,000,000.00
531. KahamaUshetu & Msalala DCDrilling of 11of boreholes for Ubagwe,Ubagwe, Chona, Kinamapula,280,416,380.00 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Chona, Kinamapula, Uyogo, Bukomela, Makongolo, Busenda, Nyalwelwe, Izumba, Ndala, Nundu, Jomu and Ndalilo Villages.Uyogo, Bukomela, Makongolo, Busenda, Nyalwelwe, Izumba, Ndala, Nundu, Jomu    and Ndalilo 
532. KahamaUshetu DCCompletion of piped water supply system at Mpunze, Sabasabini and Iponyanholo villages at ushetu DC by June 2023Mpunze, Sabasabini and Iponyanholo565,029,996.00
533. KahamaUshetu DCCompletion of Igunda water supply ProjectIgunda58,374,998.00 
534. KahamaUshetu DCConsultant service for Designing of water project and extension of lake Victoria water supply scheme to Igunda, Ukune, Kisuke, Kinamapula, Nyamilangano, mapamba, Uyogo, Bukomela, Mpunze, Ushetu and Ulowa wards in Ushetu DCIgunda, Ukune, Kisuke, Kinamapula, Nyamilangan o, mapamba, Uyogo, Bukomela, Mpunze, Ushetu and Ulowa wards200,000,000
535. KahamaMsalala DCExtension ofItumbili and90,000,000.00 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
   &Ushetu DCWater Supply Scheme to Itumbili and Mwashigini Villages in Kahama DistrictMwashigini 
 Jumla Kahama 12643,784,375,683.00
536. Shinyanga Shinyanga DcConstruction of water supply project for 6 Villages: Mawemilu,Mwa bagehu,Mwadut u,Mwenge,Mwo ngozo and Mwasenge at Shinyanga DC by June 2023Mawemilu,M wabagehu,M wadutu, Mwenge,Mwo ngozo and Mwasenge765,311,257.40
537. Shinyanga Shinyanga DcConstruction of pipe infrastructures, storage tanks and domestic water points at 8 villages : Ishinabulandi, Bubale, Isela, Ibingo, Idodoma, Mwamala B, Ibanza and Ng’wang’alangaIsela, Ishinabulandi, Bubale Idodoma,  Ng’wang’alan ga,and Ibingo401,935,792.00  
538. Shinyanga Shinyanga MCConstruction of water project at Chibe VillageChibe 123,600,000.00
539. Shinyanga Shinyanga DcCompletion of Mwashagi water supply schemeMwashagi89,442,184.00
 Jumla Shinyanga 4 13 1,290,847,049.40 
 JUMLA MKOA WA SHINYANGA 23  105 1,380,289,233.40 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
540.SimiyuMeatuMeatu DCCompletion of on going  Inonelwa water supply project  (2021/2022)Inonelwa, Mwakaluba, Tindabulingi, Mwabusalu, Nzanza, Mwagumada, Malwilomnad ani, Mwakisandu2,265,580,113.00
  Jumla Meatu  1– 2,265,580,113.00
541. BusegaBusega DCConstruction of Kabita water supply phase IINyamikoma A, Nyamikoma B, Kabita, Kaboja, Shimanilwe627,663,118.00
  Jumla Busega 10627,663,118.00
542. ItilimaItilima DCCompletion of on going Habiya  water supply project wandulu, mwabimbi, bulolambeshi, gasawa, bumela , habiya863,135,722.29
  Jumla Itilima DC 10863,135,722.29
543. BariadiBariadi DCCompletion of Water supply project at Ngulyati,Nyams wa and Nyansonsi villages.Ngulyati,Nya mswa and Nyansonsi195,874,236.98
544. BariadiBariadi Dc Completion of  Mbiti Water supply project (Ongoing) Mbiti Sokoni,Mlima ni,Busulwa and Isengwa119,072,785.56
545. BariadiBariadi DcCompletion of  Kilalo Water supply project (Ongoing)Kilalo and Nyamisagusa85,561,470.18
  Jumla Bariadi  30400,508,492.72
 JUMLA MKOA SIMIYU 11–   4,156,887,446.01
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
546.Singida Singida  Singida DC Completion of ongoing Construction of water supply project for Mwighanji  village in Singida District by june 2023Mwighanji249,887,256.00
  Jumla Singida DC10249,887,256.00
547. IkungiIkungi DC Construction of Irisya ,Ihanja and Iglanson Pumped Piped Water Supply Schemes   in Ikungi District  (PforR) Ihanja, Isseke, Irisya and Iglansoni349,537,311.21
548. IkungiIkungi DC Construction of Matare Pumped Piped Water Supply Scheme with 18 Public Water Points in Ikungi District (Pfor) Matare129,570,543.77
549. IkungiIkungi DC Construction of Mkunguakiendo ,Minyinga and Sakaa Pumped Piped Water Supply Schemes  in Ikungi District (PforR) Mkunguakien do,Minyinga and Sakaa485,716,203.75
550. IkungiIkungi DC Construction of Minyughe Pumped Piped Water Supply Scheme with 16 Public water Points in Ikungi District (NWF) Minyughe114,960,055.50
  Jumla Ikungi DC401,079,784,114.23
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
551. ManyoniItigi DCConstruction of Aghondi Mabondeni Water Supply project Aghondi, Mabondeni150,000,000.00
552. ManyoniItigi DC Construction of Kayui Water Supply project Kayui350,000,000.00
553. ManyoniItigi DCCompletion of on going Construction of Kamenyanga Water Supply projectKamenyanga300,000,000.00
554. ManyoniManyoniCompletion of on going extension of kintiku /Lusilile Water Supply Project-Phase IIKintinku, Lusilile, Maweni, Mvumi, Ngaiti, Chikuyu, Mwiboo, Mbwasa, Mtiwe Makutupora na Chilejeho891,707,055.85
555. ManyoniManyoniCompletion of on going construction of Rift Valley water projects Chibumagwa, Mpandagani, Kinangali700,000,000.00
  Jumla Manyoni DC502,391,707,055.85
556. Mkalama Mkalama  DCConstruction of water  project  at Ishenga   village Ishenga172,119,985.00
  Jumla Mkalama  DC30172,119,985.00
557. IrambaIramba DCConstruction of Galangala and Kisharita Pumped Piped Water Supply SchemeGalangala and Kisharita575,554,144.97
558. IrambaIramba DCConstruction andMakunda and Mugundu695,456,323.03
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    rehabilitation of Makunda and Mugundu Pumped Piped Water Supply Schemes   
559. IrambaIramba DCConstruction of Kitukutu Pumped Piped Water Supply SchemeKitukutu30,000,000.00
560. IrambaIramba DCRehabilitation of Kinambeu Pumped Piped Water Supply Scheme Kinambeu30,000,000.00
  Jumla Iraba DC401,331,010,468.00
 JUMLA  MKOA SINGIDA 17– 5,224,508,879.08
561.Songwe Momba Momba DCCompletion of Mkomba water supply project VillageMkomba228,347,000.00
562. Momba Momba DCCompletion of Mpapa- Masanyinta water supply project VillageMpapa, Masanyinta, Kasanu436,279,073.00
563. Momba Momba DCCompletion of Ipito-MjiMwema water supply project VillageMji Mwema, Migombani, Jakaya120,215,325.00
564. Momba Momba DCCompletion of Uhuru- Tunduma water supply project VillageTunduma, Makambini, Uwanjani245,960,501.00
565. Momba Momba DCCompletion of Uhuru-Nyerere water supply project VillageMajengo Mapya, Mwl Nyerere, Msongwa155,454,000.00
566. Momba Momba DCExtension of Samang’ombe  water supply project VillageIvuna, Lwatwe, Kalungu na Samang’ombe204,686,055.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Momba DC601,390,941,954.00
567. IlejeIleje DCExtension of Itumba- Isongole water supply scheme 1,805,461,124.00
 Jumla Ileje DC1– 1,805,461,124.00
  JUMLA MKOA SONGWE 703,196,403,078.00
568. TaaboraUyuiUyui DC Extension of Lake Vitoria Pipeline to Nsimbo, Mayombo, Kagera, Mputi,Hiariyam oyo, Mbuyuni, Kinamagi and Vumilia villages Nsimbo,Mayo mbo,Kagera, Mputi,Hiariya moyo,Mbuyu ni,Kinamagi and Vumilia414,548,205.00
569. UyuiUyui DC Extension of lake victoria pipeline to Kigwa,Igalula,N sololo and Goweko wards KigwaB, Nzigala, Matanda, Kinamagi, Mbuyuni, Igalula, Ipululu, Vumi lia, Isenefu, Imalakaseko, Goweko, Kamama, Mwitikila, Tambukareli, Nsololo, Kimungi, itundaukulu, na Kawekapina.801,296,724.00
570. UyuiUyui DC Extension of Lake victoria pipaline to Nzubuka and Izugawima villages Nzubuka and Izugawima603,675,662.00
571. UyuiUyui DC Extension of Songambele water schemeSongambele water scheme to770,139,461.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    to Miyenze village Miyenze 
572. UyuiUyui DC Extension of lake victoria pipeline to Kongo and Uhuru-Mbiti villages Kongo and Uhuru-Mbiti265,423,571.00
573. UyuiUyui DC Extension of lake victoria pipeline to Ikongolo,Kanye nye and Kiwembe villages Ikongolo,Kan yenye and Kiwembe801,322,366.00
574. UyuiUyui DC Construction of Tura village water supply project Tura152,159,729.00
575. UyuiUyui DCRehabilitation of 1216 of  water  points of piped and unpiped water schemes and Rehabilitation at 107 Villages,improv e ndono hand pump  and complitionof  Imrovement of 4 hand pamp to solar system at  ufuluma,kizengi and Lutende vilanges in Uyui DCBukumbi, Goweko, Ibelamilundi, Miyenze, Mmale,Ndono ,Nsimbo,Nsol olo,Nzubuka, Shitage, Tura, Ufuluma, Upuge, Usagari. Ibiri, Igalula, Igulungu, Ikongolo, Ilolangulu, Isikizya, Isila, Kalola, Kigwa, Kizengi, Loya, Lutende, Mabama, Magiri, Makazi, Miswaki150,082,500.00  
  Jumla uyui 6 3,958,648,218.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
576.TaboraSikongeSikonge DcUjenzi wa mradi wa maji Igumila katika Vijiji vya Kapumpa, Mgambo, Mkola, Mwenge na  Mwitikio.Kapumpa, Mgambo, Mkola, Mwenge and Mwitikio173,731,147.08
577. SikongeSikonge Dc Ukarabati wa mradi wa maji Mibono Kanyamseng a, Songambele, Mtakuja, Kiloleli, Kipanga, Lembeli, Ukondamoyo and Mibono mpya10,000,000.00
578. SikongeSikonge Dc Ujenzi wa mradi wa maji Igigwa – Wankolongo. Igigwa and Wankolongo341,679,800.00
579. SikongeSikonge DcConstruction of Mwamayunga water project (Phase II) with 22 water point by June 2023.Mwamayung a, Urafiki, Usunga and Isanjandugu1,003,392,302.00
  Jumla Sikonge4 1,528,803,249.08
580. KaliuaKaliua DCCompletion of Kazaroho water supply and sanitation project in Kaliua District Kazaroho, Imalamihayo, Nsimbo 310,619,795.00
581. KaliuaKaliua DCConstruction of Usimba water supply project in Kaliua District Usimba116,180,156.00
  Jumla kaliua 5 426,799,951
582. IgungaIgunga DcExtension of water supply schemes at 9 villages(Ndembenzi, Mwanzelwa, Itulashilanga, Ulaya,1,200,650,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Ndembenzi, Mwanzelwa, Itulashilanga, Ulaya, Barazani, Ikunguipina, Njiapanda, Kitangili and Nkinga villages) in Igunga District -PHASE IIBarazani, Ikunguipina, Njiapanda, Kitangili and Nkinga villages 
583. IgungaIgunga DcExtension of water supply schemes at 16 villages(Bukam a, Mwabakima, Johogya, Kining’inila, Mwanyangula, Iyogelo, Isakamaliwa, Kidalu, Ibole, Mwagala,Imala nguzu, Mwamakona, Kalangale,Gany awa, Mwagala and Igurubi villages) in Igunga DistrictPHASE IIBukama, Mwabakima, Johogya, Kining’inila, Mwanyangula , Iyogelo, Isakamaliwa, Kidalu, Ibole, Mwagala,Imal anguzu, Mwamakona, Kalangale,Ga nyawa, Mwagala and Igurubi 1,956,000,000.00
584. IgungaIgunga DcCompletion of  Mangungu, Mwabubele- Kagongwa, Mwamloli, Ussongo-Ntigu- Moyofuke, Mwazizi- BukokoMtunguru, IbologeroImalilo-MatinjeImalilo, Matinje, Bukoko, Mtunguru, Mwamashiga , Kagongwa, Mangungu247,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    and MigongwaMwamashiga Water Supply Projects  
585. IgungaIgunga DCTo Rehabilitate Chibiso Water Supply scheme Chibiso50,000,000.00
586. IgungaIgunga DCTo rehabilitate Non functional water points to be functional in all 35 wards in Igunga District by June 2023 97,390,000.00
 Jumla Igunga  3,551,040,000
587.Tabora Nzega  Nzega DC Extension of Lake Victoria Project to Bukene & Mwamala Wards to Shila, Shigamba, Kagongwa, Itobo, Lakuyi, Chamwabo, Bukene, Kabanga, Uduka, Ussongwanhala , Kayombo, Mwamala, Kishili, Seki, Chaming’hwa, Kasela, Senge, Lububu, and  Udutu Shila, Shigamba, Kagongwa, Itobo, Lakuyi, Chamwabo, Bukene, Kabanga, Uduka, Ussongwanh ala, Kayombo, Mwamala, Kishili, Seki, Chaming’hwa , Kasela, Senge, Lububu, and  Udutu4,011,315,684.00
588.  Nzega  Nzega DC  Extension of Lake victoria water supply   Kaloleni and Ilelamhina villages  Kaloleni na Ilelamhina653,729,883.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
589.  Nzega  Nzega DC Extension of lake victoria water supply to  Luzuko Village  Luzuko418,345,848.00
590.  Nzega  Nzega DC Geographycal survey and Drilling of 31  boreholes at Nzega DC Ipumbuli, Upambo, Ifumba, Bujulu, Upina, Kipilimuka, Budushi, Iyombo Itima, Kakulungu, Malole, Milambo Itobo, Kawula, Ndekeli, Chambutwa, Tumbi, Mangashini, Kingamaluch a, Kipungulu, Buhulyu, Zungimulole, Kidete, Kwanzale, Gulyambi, Kahamanhala nga, Kilino, Nhabala, Semembela, Nindo, Senge, Isagenhe and Buduba  899,000,000.00
591.  Nzega  Nzega DC construction of water project at Isalalo village  Isalalo130,000,000.00
  Jumla Nzega 6 6,310,432,674.00
  JUMLA MKOA TABORA21– 15,775,724,092.0 8
592.TangaKilindiKilindi DCConstruction of water supplyKilindi, Kwamazuma240,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    project in Kilindi asili  and Misufini 
593.TangaKilindiKilindi DCExtension of Mafuleta  water supply scheme  to  Mabalanga  village from Mkuyu damMabalanga186,460,428.00
594.TangaKilindiKilindi DCConstruction of  Mafulila/ Bokwa Piped Water Supply Project  Mafulila/ Bokwa175,000,000.00
595.TangaKilindiKilindi DCConstruction  of Mafisa  water supply Project Mafisa Madukani , Mafisa Majengo110,000,000.00
596.TangaKilindiKilindi DCConstruction  of Kwamaligwa/Gi tu water supply Project Kwamaligwa, Gitu, Elerai, Gombero A&B and Kiberashi250,000,000.00
597.   Drilling of 23 boreholes at Sangeni,  Msente,  Mangidi,  Mtonga,  Mkindi,  Mswaki,  Makingo,  Kisangasa,  Mvungwe,  Kwamba,  Sambu,  Mheza,  Ngeze, Mapanga,  Makelele,  Lumotio,  Mzinga,  Kimembe,  Vunila,  Kweisapo,  Lukole,  Vyadigwa, and Sangeni,  Msente,  Mangidi,  Mtonga,  Mkindi,  Mswaki,  Makingo,  Kisangasa,  Mvungwe,  Kwamba,  Sambu,  Mheza,  Ngeze,   Mapanga,  Makelele,  Lumotio,  Mzinga,  Kimembe,  Vunila,  Kweisapo,  Lukole,  Vyadigwa, and  Kitingi220,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Kitingi  Villages.  
 Jumla Kilindi DC6– 1,181,460,428.00
598.TangaHandeniHandeni DCCompletion of on-going projects (Kwamsangazi water supply projects)Kwamsangaz i314,080,625.76
599.TangaHandeniHandeni DCExtension of Mkata-Manga Water ProjectManga 45,282,048.32
600.TangaHandeniHandeni DCExtension of Mkata Kwapala water projectKwapala 349,145,151.19
601.TangaHandeniHandeni DCConstruction of Gole water ProjectGole278,731,118.94
602.TangaHandeniHandeni DCConstruction of Kang’ata water ProjectKang’ata739,907,594.63
603. HandeniHandeni DGeophysical survey and Drilling of 22 boreholes at Nyasa, Madebe, Hedi, Kilimamzinga, Komnazi, Kweinguto, Bagamoyo, Komnyanganyo , Kwedihwahwal a, Komkonga,Tun dile Mazingara, Mkomba, Komsanga, Bangu, Kwedisewa, Kwedizando, Msasa zahanati,Nyasa, Madebe, Hedi, Kilimamzinga, Komnazi, Kweinguto, Bagamoyo, Komnyangan yo, Kwedihwahw ala, Komkonga,T undile Mazingara, Mkomba, Komsanga, Bangu, Kwedisewa, Kwedizando, Msasa zahanati, Kwedigongo, Lengome,500,144,957.16
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Kwedigongo, Lengome, Kolukole, Kwabaya Nkavunka, Zizini VillagesKolukole, Kwabaya Nkavunka, Zizin 
 Jumla Handeni DC5– 2,227,291,496.00
604.TangaPangani Pangani DCRehabilitation of water supply scheme at Kibinda (Mkwajuni)kibinda,uban gaa na mkwajuni84,000,000.00
605.TangaPangani Pangani DCRehabilitation of on going Meka – Mseko water supply schemeMeka and Mseko154,000,000.00
606.TangaPangani Pangani DCConstruction of Kwakibuyu/ Sakura water supply projectKwakibuyu/ Sakura145,000,000.00
607.TangaPangani Pangani DCConstruction of  Mkalamo water supply projectMkalamo 165,000,000.00
608.TangaPangani Pangani DCConstruction of  Mrozo water supply projectMrozo 145,000,000.00
609.TangaPangani Pangani DCExtension of Mikocheni to Mkwaja  water supply project Mkwaja 155,000,000.00
610.TangaPangani Pangani DCRehabilitation of Kipumbwi water supply Scheme. Kipumbwi156,000,000.00
611.TangaPangani Pangani DCConstruction of Mwembeni water supply projectMwembeni 143,980,000.00
612.TangaPangani Pangani DCRehabilitation of Kigurusimba water supply scheme Kigurusimba84,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
613.TangaPangani Pangani DCRehabilitation and Extension of Tungamaa  water Supply SchemeTungamaa66,000,000.00
614.TangaPangani Pangani DCRehabilitation and Extension of Sange  water Supply SchemeSange 67,340,000.00
615.   Drllingi of 17 productive bore holesMkwajuni, Ubangaa, Langoni, Mtonga, Stahabu, Mkwaja, Kovukovu,Sa nge,MZamba rauni,Choba, Mnazi Mmoja,Tunga maa,Mivumo ni,Bweni,Mkal amo,Kimangá ,Meka na Buyuni137,355,411.00
 Jumla Pangani DC12– 1,502,675,411.00
616.TangaMuhezaMuheza DC Construction of Kiwanda water supply project Kiwanda, Bombani, Kweisaka, Mangubu, Tongwe, Masimba306,470,295.00
617.TangaMuhezaMuheza DCConstruction of Mbomole/Sakal e water supply projectMbomole/Sak ale 543,397,017.30
618.TangaMuhezaMuheza DCTo undertake drilling 9 borehole Mtiti, Kwabada, Mtindilo, Kilulu, Mkuzi, Tingeni, Kwakifua, Kwafungo na Makole227,500,950.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
619.TangaMuhezaMuheza DCConstruction of Kwatango water supply projectMtiti, Kwesimba, Kwatango206,664,122.63
 Jumla Mheza DC4– 1,284,032,384.93
620.TangaMkingaMkinga DCRehabilitation of Maramba water supply to Maramba A, Maramba B and Ng’ombeniMaramba A, Maramba B and Matemboni242,761,596.70
621.TangaMkingaMkinga DCGeophysical survey and Drilling of 3 boreholes at Mbuta, Mwakijembe and Horohoro Villages.Mbuta, Mwakijembe and Horohoro75,000,000.00
622.TangaMkingaMkinga DCExtension from Tanga UWSSA to Mkinga (Mradi wa Mto Zigi) – Priority (Design stage) 25,000,000.00
623.TangaMkingaMkinga DCExtension of Mapatano WaterSupply Scheme to Machimboni, Bantu and Kwangena Villages Bantu, Kwangena, and Machimboni 275,000,000.00
624.TangaMkingaMkinga DCConstruction Daluni Kisiwani and Vuga ProjectsDaluni Kisiwani A and Daluni Kisiwani B and vuga244,719,000.00
625.TangaMkingaMkinga DCRehabilitation and extension of Gombero Water Supply Scheme and extension toGombero, Vunde Manyinyi, Jihirini and Dima200,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Vunde Manyinyi, Gombero, Kichangani, Dima and Jihirini  
626.TangaMkingaMkinga DCConstruction of Muhinduro water supply to Kwamtili, Churwa, Muheza, Mhinduro, Bamba Mavengero and Kichangani Villages Kwamtili, Churwa, Muheza, Mhinduro, Bamba Mavengero and Kichangani 190,194,814.30
627.TangaMkingaMkinga DCExtension from Tanga UWSSA to Mkinga (Mradi wa Mto Zigi) – Priority (Design stage) 350,000,000.00
 Jumla Mkinga DC8– 1,602,675,411.00
628.TangaLushotoLushoto DCExtension of  Lushoto Town water supply SchemLushoto, Magamba, Ubiri1,649,502,027.51
629.TangaLushotoLushoto DCConstruction of  Ngwelo water supply project Kihitu, Kigulunde85,693,352.92
630.TangaLushotoLushoto DCConstruction and Extension of Kwang’wenda/ Mbuzii village water supply SchemIrente,Ngulwi and Miegeo46,978,726.84
631.TangaLushotoLushoto DCConstruction of Mahezangulu water supply projectMahezangulu ,Kwemakonk o and Msamaka136,757,760.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
632.TangaLushotoLushoto DCConstruction of Kiluwai Kidundai/Wang a/ Funta water supply projectManga,Mzul ei,Kwengeza and Funta,Kiluai na Kidundai, Kishewa,Wa nga290,333,792.00
633.TangaLushotoLushoto DCConstruction of Vuga water supply project Vuga235,266,824.57
634.      
 Jumla Bumbuli DC6– 2,444,532,483.84
635.TangaKorogweKorogwe DCRehabilitation and Extension of Mtonga Water Supply Project 273,211,500.00
636.TangaKorogweKorogwe DCTo rehabilitate and extend Makuyuni water scheme to Madumu and Gomba lamu villagesMakuyuni,Ma dumu and Gombalamu300,000,097.51
637.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Kwemasimba water supply projectKwemasimba200,000,000.01
638.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Goha water supply projectGoha,Kweise wa, Mkumbara and Manga mtindiro111,000,000.00
639.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Gombero- Mapangoni water supply projectGombero- Mapangoni 124,500,000.00
640.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on goingMugobe, Nkalekwa,100,020,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    projects Magila gereza water supply projectMandera na Gereza 
641.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Chekelei water supply projectMbagai,Chep ete,Kwamkol e,Madala  Chekelei na Kwepunda150,000,000.00
642.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Mahenge- Kerenge water supply projectMahenge, Kerenge makaburini na Kerenge Kibaoni na Vingo100,000,000.00
643.TangaKorogweKorogwe DCCompletion of on going projects Kalalani water supply projectMtoni bombo and Kalalani60,400,000.00
644.TangaKorogweKorogwe DCConstruction of water supply project in Tewe village.Tewe, Mali na Kwemanolo76,720,350.48
645.TangaKorogweKorogwe DCTo rehabilitate of Magoma (Mkwajuni Sekioga) water supply schemeMakangara, Mkwajuni – Sekioga, Kijango,Mako rora na Kwemazandu200,000,000.00
646.TangaKorogweKorogwe DCTo extend Hale water supply scheme to Sisi kwa Sisi villageNgomeni, Sisikwasisi, Makinyumbi Station, Makinyumbi miembeni na Hale mjini150,000,000.00
647.TangaKorogweKorogwe DCConstruction of water supply project in Kwetonge village.Kwetonge 100,000,000.00
648.TangaKorogweKorogwe DCFeasibility study and design of 55,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mkalamo (Kweisewa) and Mkomazi Water Supply project  
 Jumla Korogwe DC14 2,000,851,948.00
 JUMLA MKOA TANGA53 12,243,579,562.7 7
  JUMLA KUU MIRADI INAYOENDELEA 648 213,978,633,687. 44
(ii) MIRADI MIPYA
649.ArushaArushaArusha DCExtension of Five villages water scheme (Lengijave tank to Engalaoni Village)- NewEngalaoni264,908,567.96
 Jumla Arusha11264,908,567.96
650. ArumeruMeru DCConstruction of Uwiro ward water Project (New)Uwiro and Kisimiri200,634,536.00
 Jumla Arumeru12200,634,536.00
651. Longido Longido DC Extension of Tingatinga water scheme to Ngereyani village and Motoon sub village – New  Ngereyani na Motoon2 51,018,216.00
 Jumla Longido1251,018,216.00
652.                      Monduli  Monduli DCExtension of Arusha City water Scheme (Ngorborb tank) to Monduli town and 13 villages in Monduli DistrictMesrani juu, Arkatan, Arkaria, Mti mmoja, Nanja, Lepurko, Losimingori, Mbuyuni, Engaroji, Naalarami, Meserani Bwawani500,000,000.00
 Jumla Monduli113500,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
653. NgorongoroNgorongoro DCContruction of  Loswash and Soitsambu Water Project NewSoitambu na Loswash242,477,866.00
 Jumla Ngorongoro1242,477,866.00
 JUMLA MKOA ARUSHA5 1,259,039,185.96
654.DodomaChamwinoChamwino DcConstruction of Storage tank 75cum on 9m riser at Nagulo VillageNagulo village90,000,000.00
655. ChamwinoChamwino DcConstruction of Storage tank 90cum on 6m riser at Mlowa Bwawani VillageMlowa bwawani 110,000,000.00
656. ChamwinoChamwino DCGeologcal survey and drilling of 1 borehole at Mpwayungu villageMpwayungu43,000,000
 Jumla Chamwino3 243,000,000.00
657. BahiBahi DcExtension of Water supply infrastructures at Chibelela villageChibelela150,000,000.00
658. BahiBahi DcRehabilitation of water supply infrastructure at Kigwe Mapinduzi, Nondwa and villagesKigwe Mapinduzi, Nondwa390,000,000.00
659. BahiBahi DCExtention of water supply scheme at Ilindi VillageIlindi100,000,000
660. BahiBahi DCGround water exploration and drilling of 4  Ng’ome/Map anga, Bahi90,000,000
Na.Mkoa WilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     productive boreholes at Ng’ome/Mapan ga, Bahi Makulu and Lukali villagesMakulu and Lukali villages 
 Jumla Bahi 46730,000,000.00
661.  KongwaKongwa DcConstruction of Water Infrastructures at Mbande VillageMbande150,000,000.00
662.  KongwaKongwa DcRehabilitation of Water Infrastructures at Tubugwe and Chamkoroma- Makole VillagesTubugwe juu, Tubugwe kibaoni, and Chamkoroma -Makole V135,629,810.00  
663.  KongwaKongwa DCGeophysical Survey and Drilling at Silale, Chiwe, Mautya, Chang’ombe, Ngomai, Nyerere, Magereza (Manyata), Wezamtima and Muungano (Songambele) Miseleni (Sejeli) VillagesSilale, Chiwe, Mautya, Chang’ombe, Ngomai, Nyerere, Magereza (Manyata), Wezamtima, Miseleni (Sejeli) and Muungano (Songambele ) 219,288,934.00
 Jumla Kongwa 315 504,918,744.00
664.  KondoaKondoa DcConstruction of Water Supply Projects for Bambare, Masawi, Kwamafunchi, Kisaki, Baura and Loo (Lusangi) andAlagwa, Masawi, Lembo, Humai, Bereko, Bambare, Madege, Bukulu (Isabe),384,350,000.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Magede Villages and Damai and Kilimani streetsKisaki, Baura and Loo (Lusangi) and Magede and Kwamafunchi , Damai street 
665. Kondoa Kondoa DCDrilling of 19 Boreholes for Itaswi, Chubi, Mongolo, Mahongo, Berabera, Loo, Sakami, Hurui Serya, Dumi, Hurumbi, Chora, Itiso, Msui, Kwamtwara, Ausia, Damai, Changombe Villages and Munguri streetsItaswi, Chubi, Mongolo, Mahongo, Berabera, Loo, Sakami and Hurui Serya, Dumi, Hurumbi, Chora, Itiso, Msui, Kwamtwara, Ausia, Damai, Changombe Villages and Munguri streets  188,702,986.00   
666. KondoaKondoa DcRehabillitation of Water Supply Project for DISSA VillageDissa76,000,000.00
667. KondoaKondoa TcExpansion of Water Supply Project for Tampori and Choka – Gubali StreetChoka, Gubali and Tampori67,500,000.00
 Jumla Kondoa437716,552,986.00
668. ChembaChemba DcRehabilitation and expansion of Kelema – Maziwani and Ovada Water Supply SchemeKelema Maziwani and Ovada203,802,490.43  
669. ChembaChemba DCDrilling of Eight 4 Boreholes for Handa, Chioli,Handa, Chioli, Dinae and Donsee157,600,000
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Dinae and Donsee  
 Jumla Chemba26361,402,490.43
670. MpwapwaMpwapwa DcTo construct water infrastructure at Gulwe and Godegode VillagesGulwe and Godegode226,088,864.00  
671. MpwapwaMpwapwa DCExtension of water supply from Idilo Kisokwe to Mazae Girls Sec. SchoolMazae150,000,000
672. MpwapwaMpwapwa DCGround water exploration and drilling of 12 productive boreholes at Ngalamilo, Chaludewa, Muungano, Nyabu, Isinghu, Chibwegere, Chibwegele, Msangambuya Chamsisili, Igoji II Mkanana and Kisisi villagesNgalamilo, Chaludewa, Muungano, Nyabu, Isinghu, Chibwegere, Chibwegele, Msangambuy a Chamsisili, Igoji II Mkanana and Kisisi villages36,000,000
673. MpwapwaMpwapwa DCIdentification and preparation including water quality and discharge test and Design for Gravity and river springs at Lufusi, Rudi, Mbuga, Iyenge, Kinusi, Ikuyu, Winza, Vikundi and Nzugilo villages andLufusi, Rudi, Mbuga,Iyeng e,Kinusi,Ikuy u,Winza,Viku ndi and Nzugilo villages and Borehole designs at Msagali,and Nghambi villages43,260,660
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Borehole designs at Msagali, and Nghambi villages  
 Jumla Mpwapwa526455,349,524.00
674.                          DODOMA  DodomaGeophyscial survey and drilling of boreholes at Nkulabi and Mahoma Makulu villages Nkulabi and Mahoma Makulu 11,599,309.00
 Jumla Dodoma111,599,309.00
 JUMLA MKOA DODOMA22953,022,823,053.43
675.Geita Bukombe Bukombe DCExtension of Ng’anzo water supply scheme in Ng’anzo villageNg’anzo228,910,560.00
676. Bukombe Bukombe DCConstruction of Piped Water Supply Projects for Mwalo and Iyogelo villages in Bukombe District Mwalo and Iyogelo259,555,544.06
 Jumla Bukombe23488,466,104.06
677. Chato Chato DCConstruction of Imarabupina – Ichwankima water supply projectNyamirembe, Kalebezo, Nyambiti, Busalala, Imalabupina, Ichwankima, Kachwamba, Idoselo, Ipandikilo, Mwangaza and Igarula28,563,319.34
678. Chato Chato DCExtension of Muganza – Bwongera water supply project to 3Mkolani, Bupandwamp uli na Katete 473,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    villages of Mkolani, Bupandwampuli and Katete villages (PforR)  
679. Chato Chato DCConstruction of water supply in Musasa village (Pfor R)Musasa261,000,000.00
680. Chato Chato DCConstruction of Bwanga and Izumangabo water supply project (Pfor R)Izumangabo na Bwanga321,000,000.00
 Jumla Chato41,083,563,319.34
681. NyangwaleNyangwale DCExtension of Nyamtukuza water supply project to Nyang’hwale, Kaseme, Ibambila and Nyaruguguna VillagesNyang’hwale, Kaseme, Ibambila and Nyaruguguna1,101,037,039.00
682. NyangwaleNyangwale DCConstruction of treatment plant at Nyamtukuza Water Supply Poroject intakeNyamtukuza, Kakora, Nyarubele, Kitongo, Ikangala, Busengwa, Izunya, Kharumwa, Kayenze, Bukwimba, Nundu, Nyang’holong o, Bulangale, Nundu, Igeka, Nhwiga, Nyijundu, Iyogelo162,155,971.00
 Jumla Nyang’wale21,263,193,010.00
 JUMLA MKOA GEITA802,835,222,433.40
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
683.IRINGAIringa Iringa DC Construction of Ikungwe water supply project in Iringa DistrictIkungwe215,740,707.00
684. Mufindi Mufindi DCConstruction of Mbalamaziwa Water SupplyKitelewasi, Idetero, Mbalamaziwa , Maguvani, Nyanyembe Kinegembasi, Ukemele Iramba and Mkangwe20,000,000.00
685. Iringa Iringa DC Rehabilitation and extension Weru water supply project to Kibebe village in Iringa DistrictWeru and Kibebe314,740,707.50
 Jumla Iringa3550,481,414.50
 JUMLA MKOA IRINGA30550,481,414.50
686.KageraKaragweKaragwe DCConstruction of water supply project at Mshabaigulu, Omukimeya, Kanoni, Rwamugurusi, Kibona, Igurwa, Kigarama Vilages.Mshabaigulu, Omukimeya, Kanoni, Rwamugurusi , Kibona, Igurwa, Kigarama1,936,373,743.77  
687. KaragweKaragwe DCGeophysical survey and drilling of 10 boreholes at Masheshe/Run yaga (2),Ruzinga/Ka kiro(2), Nyarugando, Muungano, Kituntu, Chonyonyo,Masheshe/Ru nyaga (2),Ruzinga/K akiro(2), Nyarugando, Muungano, Kituntu, Chonyonyo, Katwe, Omukakajinja .  85,700,230.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Katwe, Omukakajinja.  
 Jumla Karagwe22,022,073,973.77
688. MissenyiMissenyi DCConstruction of Nkelenge, ishunju, minziro and rwamashonga water supply projectsNkelenge, ishunju, minziro and rwamashong a900,000,000.00
689. MissenyiMissenyi DCRehabilitation of Kenyana water supply schemeKenyana, ruzinga and bugango304,405,756.44  
690. MissenyiMissenyi DCExtension of Kibeo water supply scheme to Mwemage and mabale villagesMwemage, mabale, Kikono, Kishojo and Rushasha749,999,999.98
691. MissenyiMissenyi DCConstruction of 50 water points kashaka and kashekya50,000,000.00
692. MissenyiMissenyi DCGeophysical survey and drilling of 16 boreholes at Byeju, Mwemage, Kitobo, Kitobo, Kyazi, Ruzinga, Rwamashonga, Katolerwa, Kijumo, Mushasha, Bubale, Nkelenge, Katendagulo, Kajumo, Mabuye, Bugorora and Minziro VillagesByeju, Mwemage, Kitobo, Kitobo, Kyazi, Ruzinga, Rwamashong a, Kijumo, Mushasha, Bubale, Nkelenge, Katendagulo, Kajumo, Mabuye, Bugorora and Minziro and Katolerwa386,936,701.61  
 Jumla Misenyi52,391,342,458.03
693. KyerwaKyerwa DCConstruction of kimuli Kimuli, Rwanyango200,068,116.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Rwanyango and chakalisa water supply projectna Chakilasa 
694. KyerwaKyerwa DCConstruction of Runyinya- Chanya water supply project  Runyima na Chanya320,479,988.00
695. KyerwaKyerwa DCConstruction of NyamiagaNyakatera water supply  Nyamiaga na Nyakatera325,479,988.00
696. KyerwaKyerwa DCConstruction of kaisho -Isingiro water supply Kaisho na Isingiro325,479,988.00
 Jumla Kyerwa41,171,508,080.00
697. NgaraNgara DCConstruction of Kihinga water supply projectKihinga220,000,000.00
698. NgaraNgara DCConstruction of Bugarama, Nyakariba, Kigoyi, Kasulo,Benaco( Kafua)  Keza, Katerere and Ntanga water supply projectsBugarama,Ny akariba,Kigoy i,Kasulo,Bena co,Keza,Kate rere and Ntanga1,324,381,499.97
699. NgaraNgara DCGeophysical survey and drilling of boreholes at 8 villages in Kumubuga, Mukarehe, Nyabisindu, Mumuhamba, Kumugamba, Kagali, Muganza and Kazingati villages   Kumubuga, Mukarehe, Nyabisindu, Mumuhamba, Kumugamba, Kagali, Muganza and Kazingati villages60,000,000.00  
 Jumla Ngara31,604,381,499.97
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
700. BukobaBukoba DCConsultancy service for  Ikimba water projectKiijongo, Kibanja. Kazinga, Katoro, Ruhoko, Musira, Kobunshwi, Mugajwale, Ngarama, Ruhunga, Kihumulo, Izimbya, Butulage, Kyaitoke,Ru gaze, 50,000,000.00
701. BukobaBukoba DCConstruction of MarukuKemondo Kanazi, Rwagati, Kyansozi, Minazi, Katoju, Buganguzi, Muruku, Butairuka, Bwizanduru, Bulinda, Butahyaibeg a, Buguruka, Kyema na Mulahya132,914,495.00
702. BukobaBukoba DCExtension of Kibirizi water Supply project to Kumkore, Amani and Kamuli; Kabirizi water Supply Scheme to Migara; Nyakabulala Water Supply Scheme to Kikomelo and Butakya;Kamuli &Nsheshe, Migara, Kikomelo & Butakya, Kagondo and Rubafu, Bumai &Kishanje1,350,000,000.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Itongo-Mikoni to Kagondo water project; Katale water supply project to Rubafu and Bumai villages  
703. BukobaBukoba DCConstruction of water infrastructure at Nsheshe, Rukoma and Mushozi villagesRukoma, Nsheshe and Mushozi & Katangalala386,053,177.00
704. Bukoba Bukoba DCGeophysical survey and drilling of twelve (12) productive boreholes at Nsheshe, Rukoma, Kishogo and Kasharu Nsheshe, Rukoma, Kishogo and Kasharu30,000,000.00  
 Jumla Bukoba61,948,967,672.00
705. Biharamulo Biharamulo DCConstruction of Water Supply scheme at Nemba and Migango Water Project supply ProjectsNemba and Migango715,181,508.00  
706. BiharamuloBiharamulo DCConstruction of Water Supply projects at NyamigogoSongambele & Busiri-Midaho villages.Nyamigogo, Songambele and Kagoma, Kikoma and Busiri660,697,150.00  
 Jumla Biharamulo21,375,878,658.00
 JUMLA MKOA KAGERA22010,514,152,341.7 7
707.KataviTanganyikaTanganyika DcConstruction of water SupplyBugwe186,615,106.51  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    infrastructure at Bugwe, Bujombe and Katobo Villages  
708.KataviMpanda Nsimbo DCTo extend Mtakuja & Songambele water supply scheme to Kapalala Secondary, Mtakuja B and HoD HouseMtakuja B45,000,000
709.KataviMpanda Nsimbo DCTo extend Magula, Ibindi and Matandalani water supply scheme to Mgolokani villageMgolokani32,000,000
710.KataviMpanda Nsimbo DCTo extend Mtapenda water supply project to Mtapenda C and Zahanati in Nsimbo DC Mtapenda25,000,000
711.Katavi Mlele Mlele DCExtension of water supply and sanitation at Songambele  (sub-Village Shamara and Shama at Kamsisi Village)Kamsisi120,000,000.00
712.KataviMleleMlele DCExtension of water supply and sanitation from inyonga to Ipwaga  (sub- villageIpwaga110,046,875.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Kankele/Gizaul ole)  
713.KataviMleleMlele DCConstruction of water supply and sanitation at Isegenezya (sub-Villages Uliambogo & Mahingula)Isegenezya250,000,000.00
714.KataviMleleMlele DC construction of water supply and sanitation at Ilunde (subVillages Ibelamafipa & Kasagala )Ilunde141,000,000.00
715.KataviMleleMlele DCconstruction of water supply and sanitation at Kamalampaka (sub-Village Mpanda ndogo) Mlele CouncilKamalampak a200,000,000.00
716.KataviMleleMlele DCExtension of water supply and sanitation at Kalovya (sub-Village Shama)Kalovya120,000,000.00
717.KataviMleleMlele DCConstruction of treatment plant and Raising Main at Nsenkwa DamInyonga,Uten de, Mgombe, Kanoge, Nsenkwa,Mta kuja, Kaulolo, Mapili, Kamsisi, Songambele, Imalauduki, Kalovya na Kamalampak a320,265,160.79
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
718.KataviMleleMpimbwe DcExtension of water supply and sanitation at Chamaendi (sub-Villages Chamalendi B & Mahimba) Mpimbwe CouncilChamalendi265,000,000.00
719.KataviMleleMpimbwe DcExtension  of water supply and sanitation from Usevya to Ikuba (sub- Village Ikuba, Igongwe, Mnyakasi,Ipota ,Kikulwe,Moba & Uzumbura) in Mpimbwe CouncilUsevya and Ikuba370,000,000.00
720.KataviMleleMpimbwe DcExtension of water supply and sanitation at Mirumba (sub-Villages Katete,Wampe mbe & Kashela) in Mpimbwe CouncilMirumba  135,909,232.00 
721.KataviMleleMpimbwe DcExtension of water supply and sanitation from Kabunde to (sub-Village Mpilipili) in Mpimbwe CouncilKabunde 280,000,000.00 
722.KataviMleleMpimbwe DcExtension of water supply and sanitation  (sub-Village  senta Matana,Ikulwe 235,277,497.00 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Nkuswe ,Changi dalajani,Mkwak wani at Ikulwe) in Mpimbwe Council  
 Jumla Katavi  17 2,836,113,871.30
723.KataviMpandaNsimboTo conduct Hydrological and Drill Nine (9) boreholes at the following villages Mtambo (2), Kalungu (1), Ivungwe (1), Litapunga (2), Kaburonge (1), Katumba (1) and Kabatini.Mtambo (2), Kalungu (1), Ivungwe (1), Litapunga (2), Kaburonge (1), Katumba (1) and Kabatini300,000,000
724.KataviMleleMlele DCDrilling 8 borehore at  Utende (Kafuru,Itilima, Mazelizeli, Kaliaguru,  Sungusungu, Mahameni, Mwamaguku, Nguka).Kafuru (1) Itilima (1) Mazelizeli (1)  Kaliaguru (1) Sungusungu (1)  Mahameni (1) Mwamaguku (1) Nguka (1).224,328,128.00
725.KataviMleleMpimbwe DcDrilling of  4 Borehol  at Luchima (sub- Villages Kawanga & Kiwanjani)   and Kibaoni (sub- Villages Chongwe & Ngwiro)Kawanga (1) Kiwanjani (1)  Chongwe (1)  Ngwiro (1)150,000,000.00  
 JUMLA MKOA KATAVI10 3,510,441,999.30
726.Kigoma Kibondo  Kibondo DC Construction of Mikonko waterMikonko481,656,401.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    supply project  
727.Kigoma Kibondo Kibondo DCConstruction of Lukaya water supply projectLukaya438,434,771.00
728.Kigoma Kibondo Kibondo DCConstruction of Magarama water supply projectMagarama798,460,087.00
 Jumla Kibondo31,718,551,259.00
729.KigomaKakonko  Kakonko DC Construction of water infrastructure at Kabare and Nyakiyobe villages Kabare and Nyakiyobe1,276,710,087  
730.KigomaKakonko Kakonko DCExtension of Nyamtukuza water supply Scheme to Nyanzige villageNyanzige500,000,000.00
731.KigomaKakonko Kakonko DCSolarization of Nyakayenzi BH for Kakonko Town Water Supply SchemeMbizi, Itumbiko, Kanyonza, Kihomoka, Muganza, Kiziguzigu, Kabingo, Ruyenzi, Kiyobera, Kinonko, Njoomulole220,000,000.00
732.KigomaKakonko Kakonko DCRehabilitation of Kasanda water supply SchemeKasanda, Kewe, Nkuba250,000,000.00
 Jumla Kakonko42,246,710,087.00
733.Kigoma Kasulu   Kasulu DC Construction of Kitema water supply projectKitema413,023,383.48
734.Kigoma Kasulu  Kasulu DCConstruction of Titye water supply projectTitye1,999,468,960.52
 Jumla Kasulu22,412,492,344.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
735.Kigoma Kigoma  Kigoma DC Supply and installation of pipes for pumping mainline, solar and pump for Simbo BoreholeSimbo, Machazo200,000,000.00
736.KigomaKigomaKigoma DCSupply and install of electric, pump and rising main pipes at Msimba and Kasuku boreholesMsimba & Kasuku100,000,000.00
737.   Drilling of 2 boreholes at Bitale villageBitale90,000,000.00
 Jumla Kigoma2390,000,000.00
 JUMLA MKOA KIGOMA12 6,767,753,690.00
738.KilimanjaroMwanga Mwanga DcConstruction of Masumbeni  Kadengere & Kisanjuni  WS projectMasumbeni, Kadengere and Kisanjuni200,860,725.00
 Jumla Mwanga1 200,860,725.00
739. SihaSiha DCExtension and Rehabilitation of Lawate Fuka water supply scheme from Somali tank in Embukoi village to Mkombozi and Ormelili.Embukoi,Mk ombozi,Orm elili419,648,286.84
 Jumla Siha1 419,648,286.84
740. SameSame DCConstruction of  Mroyo and Kisangazi Water Supply ProjectMroyo   and Kisangazi105,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
741. SameSame DCDriling of boreholes at Emuguri and Marondwe Emuguri and Marondwe35,000,000
 Jumla Same3 140,000,000.00
 JUMLA MKOA KILIMANJARO4760,509,011.84
742.Liindi LindiLindi DCConstruction of storage tank and rehabilitation of transmission and distribution networks at Namunda- Mnolela Water Supply Scheme Namunda, Ruhokwe & Mnolela   300,000,000.00
743. LindiLindi MCExtension of Kilangala Scheme to Mihambwe, Sanda Mkobani, Mtumbikile and Sinde villages Phase I   Kilangala A (Mihambwe), Mtumbikile & Mchinga I (Sinde and Sandamkoba ni) 340,000,000.00
744. LindiLindi MC Extension of Moka-Matimba Water Supply Scheme   Matimba 250,000,000.00
745.   Drilling of 5 boreholes by June 2023Moka,Kikomo lela, Mtumbikile, Mkumbamosi and Muungano villages  180,000,000.00
 Jumla Lindi41,070,000,000.00
746. Liwale Liwale DCConstruction of Hangai Corridor Water Supply Project Ngongowele, Mikuyu and Ngunja 427,974,252.00
747. Liwale Liwale DCConstruction of Kiangara Water Supply Project Kiangara and Litou 515,862,012.90
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
748. Liwale Liwale DCTo construct Nangano Water Supply Project Nangano 72,610,377.00
749.  Liwale DCDrilling of Five Water Well at by June 2023Tuungane, Chigugu, Mbuli, Nanjengeja and Likombora Village67,570,240.68  
 Jumla Liwale 41,084,016,882.58
750. NachingweaNachingwea DCExtension of Namikango Water Supply Project to Namikango B Namikango B 275,000,000.00
751. NachingweaNachingwea DCExtension of Namanga Water Supply Scheme to Mibondo -Ntila and Namkula Villages Mibondo, Mnero miembeni, Mkonjela, Ntila and Namkula 405,558,626.99
752. NachingweaNachingwea DCConstruction of storage tank for Naipingo water supply Namatula, Muungano, Naipingo, Mapochelo, Kihuwe and Mchonda 165,000,000.00
753. NachingweaNachingwea DCExtension of Namatula Mapochelo Water Supply Project to Mchonda Village Mchonda 166,000,000.00
754. NachingweaNachingwea DCConstruction of Naipanga Water Supply Scheme Chiumbati Shuleni, Chiwindi, Tandika, Luagala, Rahaleo, Maendeleo, Kilombelo.510,545,644.77
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Naipanga, Nagaga, Joshoni and Chekeleni  
755. NachingweaNachingwea DCConstruction of Mpiruka Water Supply Scheme Mpiruka A, Mpiruka B and Libea 620,000,000.00
756. NachingweaNachingwea DCDrilling of 3 boreholes with hand pumpsMbondo, Mituguru and Ngunichile136,391,659.36
 Jumla Nachingwea62,278,495,931.12
757. RuangwaRuangwa DCConstruction of Nambilanje- Mkaranga Water Supply Project   Nambilanje and Mkarango 500,000,000.00
758. RuangwaRuangwa DCConstruction of Chunyu Water Supply Project   Chunyu 450,000,000.00
759. RuangwaRuangwa DCConstruction of Liugulu Water Supply Project   Liugulu 547,420,681.99
760. RuangwaRuangwa DCConstruction of Weir, gravity Main and Water storage tank at Mandawa   Mandawa 450,000,000.00
761. RuangwaRuangwa DCConstruction of Water storage tank at Namangale village and improvement of gravity Main from the Source to Namangale village   Namangale 200,000,000.00
762. RuangwaRuangwa DC Construction of water project to 34 villages of Vijiji 34 Ruangwa na Vijiji 21 Nachingwea 80,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Ruangwa District and 21 Villages of Nachingwea District from Nyangao River   
 Jumla Ruangwa6   2,227,420,681.99 
 JUMLA MKOA LINDI20 6,659,933,495.69
763.Manyara       Babati      Babati DCConstruction of Madunga water supply project in Babati District.Madunga, Utwari, Giding’wari, Qameyu, Endaw and Gawal853,662,737.81
 Jumla Babati1 853,662,737.81
764. Mbulu Mbulu DCConstruction of Yaeda Kati, Dirim, Endalat, Endamily, Murkuchida, Endanachan, Basonyagwe, Basoderer, Bashay, Qandach, Ng’wandakw and Haydom pumped water supply projectYaeda Kati, Dirim, Endalat, Endamily, Murkuchida, Endanachan, Basonyagwe, Basoderer, Bashay, Qandach, Ng’wandakw and Haydom3,000,000,000.00
765. Mbulu Mbulu DCConstruction of pump house, rising main, procurement of submersible water pump and supply of electricity for Haydom water supply project in Mbulu DCHaydom and Ng’wandakw100,000,000.00
766. Mbulu Mbulu DCTo facilitate Survey and drilling ofQamtananant29,474,130.48
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    successful productive borehole at Qamtananant Village by June 2023  
 Jumla Mbulu3 3,129,474,130.48
767. Mbulu Mbulu TCConstruction of Aicho pumped water supply project in Mbulu TC Aicho200,000,000.00
768. Mbulu Mbulu TCConstruction of Titiwi pumped water supply project in Mbulu TC Titiwi330,192,721.80
 Jumla Mbulu TC2 530,192,721.80
769. Hanang’Hanang’ DCExtension of Mogitu/Gehand u Water Supply Project Gehandu753,957,717.50
770. Hanang’Hanang’ DCExtention of Bassotu water Supply and Sanitation Scheme Dilling’ang600,000,000.00
771. Hanang’Hanang’ DCConduct Geophysical survey and Driiling of 16 productive Boreholes   Endagaw, Endasabhogh echan, Lambo, Masusu, Bassotughan, Qutesh, Kinyamburi, Wandela, Sagon, Dabaschand, Dirma, Mogitu, Nyasinyenda, Gidamambur a, Wareti and Qalosendo 212,923,075.00 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Hanang’3 1,566,880,792.00
772. Simanjiro Simanjiro DCExtension of Orkesumet Water Scheme to Lerumo village; Naberera Water Scheme to Losokonoi & Lorbene; Komolo water scheme to Olembore (Lemshuku) sub villageLerumo, Losokonoi & Lorbene and Olembore     1,785,068,718.44  
773. Simanjiro Simanjiro DCInstallation of 21KVA diesel generator at Kitwai B, Installation of transformer 50KVA at Oljoro No. 5 and LoongswanKitwai B, Oljoro No. 5 na Loongswan112,000,000.00
774. Simanjiro Simanjiro DCConstruction of Einoth & Losinyai water supply project by June, 2023Enoth na Losinyai308,597,999.08
775. Simanjiro Simanjiro DCGeological Survey and Drilling of 13 productive Boreholes Kandasikira, Sukuro (Alaspa), Nyorit, Nadonjukini (Mwajanga), Lemkuna (Lengungum wa), Ormoti (Namalulu), Kitwai B (Losikito) and Sukuro (Katikati) 155,425,565.26 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Simanjiro6 2,361,092,283.52
 JUMLA MKOA MANYARA15 8,441,302,665.61
776.Mara Tarime TarimeExtension of Sirari water supply project and Gimenya water supply projectSirari and Gimenya800,000,000.00
777.Mara Tarime TarimeConstruction of water infrastructure at Kemakorere and Nyarero, Regicheri and Mnagusi, Itununu and Nyakienene villages Kemakorere and Nyarero, Regicheri and Mnagusi, Itununu and Nyakienene1,294,915,036.00  
778.Mara Tarime TarimeTo rehabilitates Hands PumpsKyoruba, Rosana, Bisarwi, Matongo, Kimusi, Regicheri, Kerende, Nkerege, Nkende and Mogabiri218,809,353.00
779.Mara Tarime TarimeTo rehabilitate exsisting Water Schemes at Sirari, surubu, borega, magoma, nyantira, Gibaso, Mtana, kewanja, Nyangoto,itiryo ,gimenya and SabasabaGimenya, Sirari, Surubu, borega, Magoma, Nyantira, gibaso, Mtana, kewanja, Nyangoto, itiryo and sabasaba200,000,000.00
780.Mara Tarime TarimeConstruction of Nyamwigura and TagotaNyamwigura and Tagota864,209,705.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply Schemes  
781.  Tarime TarimeHydrogeologic al survey  and Drilling of Boreholes at Surubu,kimusi, Remagwe,Mat amankwe,turu getiNyabitocho and koboriSurubu,kimu si,Remagwe, Mataman   kwe,Turugeti ,Nyabitocho and kobori280,000,000.00
 Jumla Tarime6 3,657,934,094.00
782.MaraButiamaButiama DCTo extend Nyamikoma Water supply scheme to Nyakiswa  villageNyakiswa133,937,464.00
783. ButiamaButiama DCTo extend Biatika- Kinyariri Water supply scheme to Matongo villageMatongo160,172,486.00
784. ButiamaButiama DCTo construct Water infrastructure at Ryamisanga village (Phase I) and Isaba villagesRyamisanga and Isaba1,009,694,037.11  
785. ButiamaButiama DCTo construct TANESCO power line (3- Phase) to pump houses at Bukabwa, Kamgendi, KitaramankaRwasereta villages and to conduct Hydrogeologic al survey  andBukabwa, Kamgendi, Kitaramanka -Rwasereta and sirorisimba villages259,034,216.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Drilling of Borehole at Sirorisimba Village.  
786. ButiamaButiama DCSurveying and Drilling of Borehole at Sirorisimba Village.Sirorisimba35,000,000.00
 Jumla Butiama5 1,597,838,203.11
787.  Rorya  Rorya DC Expansion of Kirogo Water Supply Scheme to Mori, Chereche, Dett, Ochuna & Omuga VillageMori, Chereche, Dett, Ochuna & Omuga500,000,000.00
788.  Rorya  Rorya DC Expansion of Komuge Water Supply Scheme to Oliyo & Makongoro Village Oliyo & Makongoro540,396,000.00
789.  Rorya  Rorya DC Construction of Mang’ore Water Supply SchemeMang’ore166,000,000.00
790.  Rorya  Rorya DC Construction of Bukura Ward Water Supply Scheme for Bubombi, Sota, Sakawa, Thabache, Roche, Osiri, Ratia & Kirongwe Villages PHASE IBubombi, Sota, Sakawa, Thabache, Roche, Osiri, Ratia & Kirongwe329,449,565.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
791.  Rorya  Rorya DC Hydrogeologic al survey and drilling of 2 productive borehole at Roche and Sakawa VillageRoche, Sakawa50,000,000.00
 Jumla Rorya5 1,585,845,565.00
792.Mara Serengeti  Serengeti DCConstruction of water infrastructure Nyiberekera villagesNyiberekera1,217,318,479.67
793.  Serengeti  Serengeti DCConstruction of water infrastructure Rigicha villagesRigicha  944,772,691.36
794.  Serengeti  Serengeti DCConstruction of water infrastructure at Gesarya and Kebanchabanc ha water supply schemesGesarya and Kebanchaba ncha939,775,928.97  
795.  Serengeti  Serengeti DCConstruction of water infrastructure at Nyamakobiti, Nyamitita/Keny ana and Natta Motukeri water supply schemesNyamakobiti, Nyamitita/Ken yana and Natta Motuker448,300,000.00  
796.  Serengeti  Serengeti DCHydrogeologica l survey and drilling of 5 boreholes and rehabilitation of 50 Hand pumpsNyamisingisi, Buchanchari, Marembota, Kitembele, Magange3300,000,000
 Jumla Serengeti5 3,880,167,100.00
797.  Bunda  Bunda DC To construct Water infrastructuresHunyari858,204,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    at Hunyari village phase one   
798.  Bunda  Bunda DC Extension of Water infrastructure from Buzimbwe Viilage to kabahinja villageKabahinja414,365,200.00
799.  Bunda  Bunda DC To construct and install hand pumps to four boreholes at Nyaburundu, Chingurubila, Muranda and Manchimweru villages Nyaburundu, Chingurubila, Muranda and Manchimweru125,394,988.00
800.   Construction of water supply project in 33 Villlages at Bunda Chamhriho Division Hunyari, mariwanda, nyamuswa, bukama, mugeta, nyabuzume, kiroleli, sanzate, kihumbu, etc800,000,000.00
801.   Construction of water supply project in 17 Villlages at Mwibara Kisoriya schemeKisorya, kibara A, kibara B, Mwibara, Kibara stoo, masahunga, nansimo, bunere, Nampndi, Nakatuba, Namalebe etc927,272,996.10
 Jumla Bunda5 3,125,237,184.10
802.MaraMusomaMusoma DCConstruction of water infrastructure at Murangi/LyaseMurangi, Lyasembe, Nyegina, Mkirira,984,766,004.32  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    mbe, Nyegina and Bwasi water supply projectKurukerege, Bwasi, Bugunda, Kome 
803. MusomaMusoma DCConstruction of Chumwi water supply projectChumwi, Mabuimerafur u1,171,875,685.20
804. MusomaMusoma DCConstruction of Murangi/Lyase mbe water supply projectBukumi,Bura ga,Busekera150,000,000.00
805. MusomaMusoma DCRehabilitation of hand pumpMayani, Wanyere, Tegeruka, Bwasi, Kabegi, Nyakatende, Musanja, Kataryo, Nyangoma, Saragana, Murangi50,000,000.00
806. MusomaMusoma DCConstruction of Rusoli water supply projectRusoli206,775,593.48
 Jumla Musoma 5 2,563,417,283.00
 JUMLA MKOA MARA 31216,410,439,429.1 1
807.MorogoroGairoGairo DCExtension of Madege Water supply Scheme to Ndogomi and MagengeNdogomi, Magenge and Kitaita221,458,260.00
 Jumla Gairo 1 221,458,260.00
808. KilomberoIfakara TCConstruction of Mhelule Water supply ProjectMhelule310,987,619.39
 Jumla Kilombero 1 310,987,619.39
809. MvomeroMvomero DCExtenssion and Rehabilitation of Mzumbe SangasangaSangasanga ,  Mzumbe. Vikenge100,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply Scheme  
810. MvomeroMvomero DCConstruction of Mziha water Supply ProjectMziha, Bwage, Jeula100,000,000.00
811. MvomeroMvomero DCConstruction of Mafuru Kimambira Water Supply ProjectMafuru, Kimambila100,000,000.00
 Jumla Mvomero3 300,000,000.00
812. UlangaUlanga DCConstruction of Nakafuru Water Supply ProjectNakafuru150,000,000.00
813. UlangaUlanga DCImprovement and Extension of Mwaya Water Supply Scheme to LibenangaLibenanga150,000,000.00
 Jumla Ulanga2 300,000,000.00
 JUMLA MKOA MOROGORO701,132,445,879.39
814.MtwaraNanyumbuNanyumbu DCContruction of Kamundi water Supply ProjectKamundi and Mkambata800,000,000.00
815. NanyumbuNanyumbu DCConstruction of Likokona Water Supply ProjectLikokona607,987,625.00
816. NanyumbuNanyumbu DCDrilling of 6 productive bore holes for Nakole, Nandete, Rukumbi, Mpombe, Lumesule and Mkwajuni, Nakole, Nandete, Rukumbi, Mpombe, Lumesule and Mkwajuni, 66,953,153.54
 Jumla Nanyumbu  1,474,940,778.54
817. TandahimbaTandahimba DcTo improve Makonde Transmission line fromTandahimba, Matogoro, Malopokelo & Milidu.25,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Malamba Village to Mtavala.  
818. TandahimbaTandahimba DCDrilling of 7 borehole for 6 villages in Tandahimba District.Chitoholi, Mikuyu, Malopokelo, Mchichira, Kitama& Namikupa.198,000,000.00
 Jumla Tandahimba  223,000,000,000
819. Mtwara Mtwara  DCConstruction of NjengwaMajengo Water Supply schemeNjengwa, Njengwa sokoni and Majengo450,695,987.00
820. Mtwara Mtwara  DCRehabilitation of Dihimba Water Supply SchemeDihimba, Kinyamu and Mpandomo177,275,767.00
821. MasasiMasasi DCTo conduct geophysical survey and drill 5 productive boreholes in Mijelejele, Nakachindu, Chidya, Miwale and Pangani by June 2023.Mijelejele, Nakachindu, Chidya, Miwale and Pangani77,580,907.00
 JUMLA MKOA MTWARA502,403,493,439.54
822. MwanzaUkereweUkerewe DCExtension of BukindoKagunguli Water scheme  Muhande, Buguza,Buze gwe and Nampisi villages366,085,000.00
 Jumla Ukerewe   366,085,000.00
823.MwanzaMisungwiMisungwi DCConstruction of new water supply project at Kijima- Isakamawe villagesKijina and Isakamawe15,000,000.00
824. MisungwiMisungwi DCExtension of mabalembarikaIhelele10,699,281.99
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    scheme to ihelele village  
 Jumla Misungwi 325,699,281.99
825. MaguMagu DCConstruction of Mahaha Water Supply ProjectMahaha180,000,000.00
826. MaguMagu DCExtension of Lugeye- Kigangama and of Kabale, Igombe, Kitongosima, Kinango and Yichobela Water Supply Schemes Water Supply SchemesLugeye, Kigangama and Kitongosima, Kabale, Igombe, Kitongosima, Kinango and Yichobela130,000,000.00
 Jumla Magu 2 310,000,000.00
 JUMLA MKOA MWANZA  701,784,281.99
827.NjombeLudewaLudewa DCConstruction of Lupingu water supply scheme (PHASE II) and Luvuyo and Mavanga, Kiyogo and Igalu water schemsLupingu and Luvuyo and Mavanga, Kiyogo and Igalu429,000,000.00  
828. LudewaLudewa DCRehabilitation of Mawengi gravity water scheme Mawengi, Lupande na Madunda 173,361,313.13
 Jumla Ludewa 3692,361,313.13
829. Njombe Njombe DCConstruction of completion of Kichiwa Pumping water Scheme Kichiwa, maduma and Tagamenda 320,530,000.00
 Jumla Njombe 1320,530,000.00
830.  Makambako TCConstruction of Wangama – Mfumbi Water Supply ProjectWangama na Mfumbi 84,945,057.92
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
 Jumla Makambako284,945,057.92
831. MaketeMakete DCConstruction of Ujuni – Nkenja Water Supply Scheme Ujuni, Nkenja140,834,621.00
832. MaketeMakete DCRehabilitation and extension of Water Supply Schemes in Ludilu, Makyala, Kijyombo, Malanduku and Ukange villagesLudilu, Kijyombo, Makyala, Malanduku, na Ukange  170,550,000.50
833. MaketeMakete DCExtention of Magoye, Lupalilo and Tandala Water Supply SchemesMagoye, Lupalilo and Tandala  150,000,000
  Jumla Makete 3 836,384,622.10
834. Wanging’o mbeWanging’om be DCConstruction of Igando Kijombe Gravity Water supply scheme (Hanjawanu – Kijombe Section) and Mpando- Mdandu- Sakalenga water supply schemes Kijombe and Madandu, Sakalenga, Itulahumba824,868,328
835. Wanging’o mbeWanging’om be DCRehabilitation of Gravity Schemes for Kidugala, Mkeha, Masage, Mdasi,Mdasi, Mwilamba, Ivigo, Kidugala, Mkeha and Masage196,165729
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mwilamba and Ivigo   
836. Wanging’o mbeWanging’ombe DCExtension   of Igando – Kijombe & Igando – Kijombe Gravity Water Supply Scheme in Mpanga na Wangamiko VillagesMpanga and Wangamiko & Igando – Kijombe325,000,000.00
 Jumla Makete3716,384,622.10
837. Wanging’o mbeWanging’ombe DC Construction of Igando Kijombe Gravity Water supply scheme (Hanjawanu – Kijombe Section)Kijombe204,556,907.00
838. Wanging’o mbeWanging’ombe DC Construction of Gravity Scheme at MpandoMdanduSakalengaMadandu, Sakalenga, Itulahumba516,488,328.00
839. Wanging’o mbeWanging’ombe DC Rehabilitation of Gravity Schemes for Kidugala, Mkeha, Masage, Mdasi, Mwilamba and Ivigo Mdasi, Mwilamba, Ivigo, Kidugala, Mkeha and Masage425,837,700.00
 Jumla Wanging’ombe31,356,034,057.00
 JUMLA MKOA NJOMBE10 3,170,255,050.15
840.PwaniMkurangaMkuranga DC Construction of Piped Water Supply Project for Mbulani and Kibuyuni Villages Mbulani, Kibuyuni, Kizomla, Kikundi, Kizapala300,000,000.00
841.  Mkuranga DCConstruction of Piped WaterMlamleni, Mwarusembe250,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Supply Project for Mlamleni and Mwarusembe Villages  
842. MkurangaMkuranga DCInstallation of electric power at Njopeka, Vianzi, Mfurumwamba o/Marogoro, Msorwa, Shungubweni, Kolagwa, Kilimahewa kusini/Mvuleni and Mwanadilatu Water projectsNjopeka, Vianzi, Mfurumwamb ao / Marogoro, Msorwa, Shungubweni , Kolagwa, Kilimahewa kusini / Mvuleni and Mwanadilatu34,619,527.60
  Jumla Mkuranga3                       –   584,619,527.60
843. BagamoyoBagamoyo DCConstruction of water Treatment Plant at Sadani SubvillageSadani257,166,517.31
844. BagamoyoBagamoyo DCGeophysical survey and Drilling of 4 boreholes at Kwakonje, Razaba, Mazizi and GongoKwakonje, Razaba, Mazizi    and Gongo103,872,000.00  
 Jumla Bagamoyo2361,038,517.31
845. KisaraweKisarawe DCExtension of Chole-Kwala Water Supply Scheme fto Kisangile, Titu, Yombolukinga, Mtunani and MafumbiKisangile, Titu, Yomboluking a, Mtunani and Mafumbi91,701,100.84
846. KisaraweKisarawe DCRehabilitation of Kului waterKului50,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    supply scheme  
847. KisaraweKisarawe DCConstruction of Bembeza water supply projectBembeza555,784,773.16
848. KisaraweKisarawe DCGeophysical survey and Drilling of 3 boreholes at Maneromango, Kidugalo and Bembeza Villages.Maneromang o, Kidugalo and Bembeza11,540400
 Jumla Kisarawe4709,206,274.00
849. KibitiKibiti DC Construction of water Supply infrastructure at Kikale village Kikale148,686,833.06
850. KibitiKibiti DCRehabilitation of Kibiti Urban Water Supply Scheme (Extension, Development of 10 Boreholes, Installation of Prepaid Meters, Construction of Aeration Treatment Plant) 70,000,000.00
851. KibitiKibiti DCGeophysical survey and Drilling of 3 Productive boreholesKinguli, Kibiti urban and Bungu110,775,848.74
 Jumla Kibiti2329,462,681.80
852. RufijiRufiji DCConstruction of water supply infrastructure at Nambunju/Mich iwili village, Kikobo, Kungurwe, Namakono,Nambunju/Mi chiwili village, Kikobo, Kungurwe, Namakono, Nyanda/Katu ndu        and Nyawanje150,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Nyanda/Katund u and Nyawanje  
853. RufijiRufiji DCRehabilitation of water infrastructure at Mwaseni and Mibuyusaba village Mwaseni na Mibuyusaba90,000,000.00
 Jumla Rufiji2240,000,000.00
854. Kibaha Construction of Piped Water Supply Project for Kipangege in Kibaha District Kipangege220,000,000.00
 Jumla Kibaha1220,000,000.00
JUMLA PWANI13 1,894,327,000.71
855.RukwaKalambo KalamboConstruction of Treatment plant facilities for old Matai Water Supply ProjectKateka, Matai A, Kisungamile & Santamaria67,292,284.00
856.  KalamboRehabilitation of Ulumi Water Supply Scheme Phase IUlumi   A   & Ulumi B25,433,010.00
857. KalamboKalambo DCUchimbaji wa Visima virefu katika Vijiji Sita vya Safu, Jengeni, Kazonzya, Mpanga, Chisambo na MzungwaSafu, Jengeni, Kazonzya, Mpanga, Chisambo na Mzungwa70,000,000.00
858. NkasiNkasi DCUchimbaji wa Visima virefu katika Vijiji vinne vya  Myula, Londokazi, Malongwe,Myula, Londokazi, Malongwe, Nkomanchind o na Nkana 60,300,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Nkomanchindo na Nkana   
 JUMLA MKOA RUKWA4 223,025,294.00
859.SimiyuMeatuMeatu DcConstruction of water supply project in Makao Village.Makao617,453,607.89
860. MeatuMeatu DcDrilliong of 4 boreholes, Rehabilitation of 20 water wells, purchasing of new hand pumps and spare parts for 20 wellsMwabuma, Lukale, Mwakisandu, Mwasengela, Tindabuligi, Lingeka, Masanga, Mwabulutago , Mwashata, Butuli na Ntobo; Mwangudo, Bulyashi, Mwamanong u na Mbushi176,176,143.12
 Jumla Meatu2793,629,751.01
861. BusegaBusega DcConstruction of Nyaluhande water supply project (New)Nyaluahande, Mwamkala, Mwagindi662,529,696.00
862. BusegaBusega DcRehabilitation of 25 wells,purchasin g of new hand pumps and spare parts for 25 wellsIgalukilo , Imalamate, shigala ,lutubiga ,Malili , mwang’weng e , kijereshi . Mwangale 90,000,000.00
 Jumla Busega2752,529,696.00
863. ItilimaItilima DcConstruction of water supply project at MwamtaniVillag e.Mwamtani321,639,992.71
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
864. ItilimaItilima DcGeophysical survey and Drilling of 04 boreholes and Supply and installation of 30 hand pumps on shallow wells pijulu, nkuyu, laini, habiya, mwaswale, kashishi, mbogo, mahembe, nkoma, muhunze, madilana, ngando, longalambog o, ikindilo; Mwaswale, Nkuyu, Gambasingu, Nkololo-itilima160,000,000.00
 Jumla Itilima2481,639,992.71
865. BariadiBariadi DcConstruction of Byuna, Nyanguge, Halawa – Damidami, Matongo, Gasuma, Igegu, and Ibulyu water supply projectByuna and Songambele, Nyanguge and Nyansosi, Halawa, Damidami and Nkindwabiye, Matongo, Gasuma, Bulumbaka and Mwaubingi, Igegu Mahariki, Magharibi and Sapiwi, Ibulyo and Sakwe3,310,024,852.84  
866. BariadiBariadi DcExtension of Mwamlapa Nduha Water Supply ProjectMwamlapa and Nduha195,300,000.00
867. BariadiBariadi DcExtension of Bubale To Nkololo WaterBubale and Nkololo184,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    supply Project(To increase source capacity)  
868. BariadiBariadi DcRehabilitation of 100 water Wells Mwantimba,N galita,Mwasu buya,Isengwa ,Mwagiti,Ngw angwali,Nya misagusa,Iku ngulyambeshi ,Duma,Sesel e,Nduha,Pug u,Itubukilo,Ng ulyati.Nyasosi ,Nkindwabiye ,Damidami,H alawa,Isenge, Mwaunkwaya ,Mbugani,Lul ayu,Mkuyuni, Mwahalaja,Ik ungulyabash ashi,Igabaniol o,Masewa,Isu yu,Mwauchu mu,Mwashag ata,Ihusi,Chu ngu,Gibeshi, Mwaumataon do,Mwasinasi ,Chungu,Mwa buluda,Mwad obana,Gamb osi,Nyamswa, Bulumbaka,G asuma,Mwau bingi,Igegu Magharibi,Ige gu,Ibulyu,Sak we,Nyangaka290,000,000.00
869. BariadiBariadi DcConstruction of Old -Maswa Water SupplyOld Maswa and Ngwangwali360,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Project  
870. BariadiBariadi DcDrilling of 10 boreholes Halawa, Dami dami, Old Maswa, Nyawa, Ibulyu, Ikungulyabas hashi, Nkidwabiye, Mwasubuya, Banemhi, Gasuma231,462,214.44
 Jumla Bariadi114,570,787,067.28
871. MaswaMaswa Dc Construction of water scheme at Zabazaba villageZabazaba 276,300,000.00
872. MaswaMaswa DCExtension of Seng’wa water project to– Mwabomba, Mwanundi(Pha se2)Mwanundi, Mwabomba604,117,405.89
873. MaswaMaswa DCRehabilitation of 90 wells and spare parts,purchasin g of new hand pumps for 60 wellsMwatumbe,M waliga,Kakola ,Masela,Kuli mimwabagalu ,Gulung’ washi, Igwata,Iguny a,Mwabayan da,Nhelela,M asanwa,Bush itala,Mwashe geshi,Chuga mbuli, Nguliguli, Senani, Ilamba Mbasa,Bushit ala,Kiloleli,Bu dekwa,Mwab araturu,Mwa mashindike,S231,300,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     eng’wa,Sulu, Kidaganda,M wabadimi,Kin amwigulu,Za wa,Mwabaya nda,Mwanhe gele,Kulimi,M wabagalu,Ze beya,Iwelimo, Ikungulyanko ma,Somanda ,Tamanu,Kizu ngu,Dulung’w a,Mwanga’an da,Nghaya,B ugarama,San gamwapuya, Zebeya,Ikung ulyankoma,M wakabeya,M wamitumayi,S ongambele,M baragane,So manda,Iguny a,Nghaya,Ishi ma,Hinduki. 
874. MaswaMaswa DCGeophysical & drilling of 10 productive boreholes at 10 boreholes Iwelimo,Bude kwa, Mwandete, ,Mwangh’ólo, Mwamashindi ke,Ikungulyak oma, Bugarama,M wang’anda Nyabubinza, Mwabagalu268,657,273.23
 Jumla Maswa3                       –  1,380,374,679.12
 JUMLA MKOA SIMIYU2007,978,961,186.12
875.RuvumaMbingaMbinga TCExtension/Expa nsion of Lifakara water supply schemeMkwaya39,003,817.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    to Mkwaya village  
876. MbingaMbinga DCRehibilitation of Ndongosi water supply scheme in Mbinga DCNdongosi75,875,068.00
877. MbingaMbinga DCRehibilitation of MatiriMatiri,Kilindi, Kiyaha and Barabara496,555,588.67
878. MbingaMbinga DCConstruction of Kambarage water supply scheme in Mbinga DC Ugano,Kitesa ,Malindindo, Mkeyeto and Matekela372,535,342.00
879. MbingaMbinga DCConstruction of Kitura water supply project in Mbinga DC Kitura, Mzuzu, Lisau and Mahilo646,660,273.60
 Jumla Mbinga5                       –  1,630,630,089.27
880. TunduruTunduru DCConstruction of Fundimbanga and Hulia  water supply schemes Fundimbanga , Hulia100,000,000.00
881. TunduruTunduru DC Construction of Ligunga  and Nakapanya Water supply scheme Ligunga, Nakapanya100,000,000.00
882. TunduruTunduru DC Construction of Misechela and  Msinji Water supply scheme Misechela,Lw anga, Msinji100,000,000.00
883. TunduruTunduru DC Construction of Azimio and Tuwemacho  Water supply scheme Azimio, Tuwemacho100,000,000.00
 Jumla Tunduru4                       –   400,000,000.00
884. Songea Songea DCConstruction of Lyangweni water supplyLyangweni200,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Scheme  
885. Songea Songea DCConstruction of Gumbiro water supply SchemeGumbilo181,323,320.00
 Jumla Songea2                       –   381,323,320.00
886. NamtumboNamtumbo DC Rehabilitation of Namtumbo water supply Scheme in Namtumbo DistrictLuegu, Mtwarapacha ni,Nahoro and Suluti260,000,000.00
887. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply  Project for Hanga village-LOT I Hanga210,000,000.00
888. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply Project for Mchomoro VillageMchomoro200,000,000.00
889. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply Project for Lumecha VillageLumecha and Mtakanini200,000,000.00
890. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply Project for Misufini VillageNamanguli, Misufini and Kilangalanga268,139,604.00
891. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply Project for Limamu VillageLimamu100,000,000.00
892. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped Water Supply Project for Likusanguse VillageLikusanguse150,000,000.00
893. NamtumboNamtumbo DC Construction of Piped WaterMsisima and Mnalawi150,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Supply Project for Msisima Village  
 Jumla Namtumbo                        –  1,538,139,604.00
 JUMLA RUVUMA1903,950,093,013.27
894.Singida Singida  Singida DC To construct Msikii Pumped Water Supply Scheme in Singida District by June 2023. (PforR)Msikii320,003,000.00
895.  Singida  Singida DC To construct Kinyamwenda Pumped Water Supply Scheme in Singida District by June 2023. (PforR)Kinyamwenda555,000,000.00
896.  Singida  Singida DC To construct Nkwae Pumped Water Supply Scheme in Singida District by June 2023. (PforR)Nkwae188,111,064.00
897.  Singida  Singida DC To construct Mughunga Pumped Water Supply Scheme in Singida District by June 2023. (PforR)Mughunga524,000,000.00
898.  Singida  Singida DC Geophysical survey, Drilling and development of 1 productive borehole at Mitonto (NWF)Mitonto  30,946,291.00  
899.  Singida  Singida DC Drilling and development of 5 productiveNdughwira, Semfuru, Ikiwu,197,114,063.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    boreholes at Ndughwira, Semfuru, Ikiwu, Kibaoni- Mudida, Nduamughanga -Mkuru (Pfor R)Kibaoni- Mudida, Nduamughan ga-Mkuru 
900.  Singida  Singida DC Drilling and development of 15 productive boreholes at Ntondo, Nkwae, Sekoutoure, Kinyamwenda, Msikii, Mwalala, Ngongoapoku, Igauri, Mwakiti, Itamka, Mkenge, Makuro, Misinko, Msimihi and Makhandi (NWF)Ntondo, Nkwae, Sekoutoure, Kinyamwend a, Msikii, Mwalala, Ngongoapok u, Igauri, Mwakiti, Itamka, Mkenge, Makuro, Misinko, Msimihi and Makhandi328,266,466.00  
 Jumla Singida DC72,143,440,884.00
901. IkungiIkungi DC Construction of Mpetu Pumped Piped Water Supply Scheme with 14 Public water Points in Ikungi District by June 2023 Mpetu298,462,645.27
902. IkungiIkungi DC Construction of Magungumka Pumped Piped Water Supply Scheme with 10 Public water Points in Ikungi District by June 2023 Magungumka303,514,291.33
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
903. IkungiIkungi DCDrilling and development of 10 productive boreholes at Germany, Kituntu, Kinyamwandyo , Mwasutianga, Makilawa, Utaho B, Samaka, Ngongosoro, Wibia and Mahambe in IkungiGermany, Kituntu, Kinyamwand yo, Mwasutiang a, Makilawa, Utaho      B, Samaka, Ngongosoro, Wibia    and Mahambe192,486,000.00  
 Jumla Ikungi3794,462,936.60
904. ManyoniManyoni DC Rehabilitation of Majiri  water supply scheme Majiri88,000,000.00
905. ManyoniManyoni DCGeophysical Survey and Drllingi of 11 productive bore holesMpapa, Igwamadete, Mbwasa (2), Sasajila, Majiri, Chicheo, Ikasi, Makasuku, Ihangwendul u           and Itetema129,592,406.89  
 Jumla Manyoni2217,592,406.89
906.  Manyoni  Itigi DC Construction of water infrastructure at Muhanga villageMuhanga300,000,000.00
907.  Manyoni  Itigi DC Extension of Kihanju Water Supply scheme Kihanju30,113,872.00
908.  Manyoni  Itigi DC Rehabilitation of Rungwa Dam atRungwa277,322,807.12
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Rungwa Village.  
909. ManyoniItigi DCGeophysical Survey and Drillingi of 10 productive bore holesIdodyandole, Makale, Mkatakuja, Kayui, Damweleu, Mabondeni, Ipalalya, Kintanula, Kalangali and Jeje.129,592,406.89  
 Jumla Manyoni4737,029,086.01
910. Mkalama Mkalama  DC Construction of Nkalakala Pumped Piped Water Supply Scheme   in Mkalama District (P4R) Nkalakala400,000,000.00
911. Mkalama Mkalama  DC Construction of Malaja Pumped Piped Water Supply Scheme   in Mkalama District(P4R) Malaja330,000,000.00
912. Mkalama Mkalama  DC Construction of Mbigigi Pumped Piped Water Supply Scheme   in Mkalama District (NWF) Mwangeza200,000,000.07
913. Mkalama Mkalama  DC Construction of Gambasimboi sub- village Pumped Piped Water Supply Scheme  in Mkalama District(P4R)Mwangeza71,165,231.00
914. Mkalama Mkalama  RehabilitationGumanga68,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    of Gumanga Pumped Piped Water Supply Scheme (PforR)  
915. Mkalama Mkalama  DCRehabilitation of Miganga Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama District(PforR)Miganga110,000,000.00
916.   To conduct Rehabilitation of Muntamba Pumped Piped Water Supply Scheme in Mkalama DistrictMuntamba117,214,784.00
917. MkalamaMkalamaDrilling of 11 exploratory boreholes and productuve wells for Iambi, Dominic, Tumuli, Igonia, Mwangeza, Makulo, Kidii, Singa, Lukomo, Gumanga and Lugongo villages  in Mkalama District(NWF)Iambi, Dominic, Tumuli, Igonia, Mwangeza, Makulo, Kidii, Singa, Lukomo, Gumanga and Lugongo   329,466,596.93
918. MkalamaMkalamaHydrological and Geophysical survey and Drilling of 11 exploratory boreholes and productuveIlunda, Lukomo, Nkalakala, Mwanga, Mwangeza, Nkito, Kisuluiga,116,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    wells (NWF)Asanja, Lukomo and Kinankamba  
919. MkalamaMkalamaConducting Hydrological and Geophysical survey of 11 Villages for Drilling of 11 productive boreholes in Mkalama District (NWF) Iambi, Dominic, Tumuli, Igonia, Mwangeza, Makulo, Kidii, Singa, Lukomo, Gumanga and Lugongo33,000,000.00
 Jumla Mkalama101,774,846,612.00
920. IrambaIramba DCConstruction of Nsunsu Pumped Piped Water Supply Scheme Nsunsu151,537,500.00
921. IrambaIramba DCConstruction of Nkingi Pumped Piped Water Supply SchemeNkingi137,295,000.00
922. Iramba Iramba DCGeophysical survey for 18 sites of Mayanzani, Haila, Kinkungu, Mtoa, Mbelekese, Kinalilya, Shati, Tintigulu, Misuna, Usure, Uwanza, Kikonge, Kipuma, Mwanduigemb e, Kisana, Kisimba,Mayanzani, Haila, Kinkungu, Mtoa, Mbelekese, Kinalilya, Shati, Tintigulu, Misuna, Usure, Uwanza, Kikonge, Kipuma, Mwanduige mbe, Kisana, Kisimba, Kyalosangi and Nsonga38,769,914.70
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Kyalosangi and Nsonga in Iramba District by June 2023 (NWF)  
923. IrambaIramba DCDrilling, well development, pumping test, water quality test and capping of 18 productive boreholes Mayanzani, Haila, Kinkungu, Mtoa, Mbelekese, Kinalilya, Shati, Tintigulu, Misuna, Usure, Uwanza, Kikonge, Kipuma, Mwanduige mbe, Kisana, Kisimba, Kyalosangi and Nsonga284,688,542.72
 Jumla Iramba4612,290,957.42
 JUMLA SINGIDA19 6,279,662,882.92
924.Songwe Songwe Songwe DCConstruction of Nahalyongo water Supply project Nahalyongo350,000,000.00
925. Songwe Songwe DCConstruction of Some water Supply project Some300,000,000.00
926. Songwe Songwe DCConstruction of Iseche water Supply project Iseche350,000,000.00
927. Songwe Songwe DCConstruction of Njelenje Solar piped water project Njelenje300,000,000.00
928. Songwe Songwe DCConstruction of Manda Juu Solar piped water project Manda94,107,296.00
929. Songwe Songwe DCExtension ofMkwajuni259,731,817.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Mkwajuni water project   
930. Songwe Songwe DCRehabilitation of Ileya and Ifwenkenya water project Ileya, Ifwenkenya300,000,000.00
931. Songwe Songwe DCRehabilitation of Ngwala water project Ngwala320,000,000.00
932. Songwe Songwe DCConstruction of Itiziro water project Itiziro250,000,000.00
933. Songwe Songwe DCConstruction of Wanzani – Ifuko water projectWanzani, Ifuko20,000,000.00
934. Songwe Songwe DCConstruction of Namkukwe – Isanzu  water project Namkukwe, Isanzu20,000,000.00
935. Songwe Songwe DCConstruction of Namambo – Ndanga water project Namambo, ndanga20,000,000.00
936. Songwe Songwe DCConstruction of Mheza – Manda water project Mheza, Manda20,000,000.00
937. Songwe Songwe DCConstruction of Mpona water project Mpona20,000,000.00
938. Songwe Songwe DCConstruction of Saza water project Saza20,000,000.00
939. Songwe Songwe DCConstruction of Ilasilo water project Ilasilo20,000,000.00
940. Songwe Songwe DCConstruction of Kanga – Tete water projectKanga , Tete20,000,000.00
941. Songwe Songwe DCConstruction of Rukwa water project Rukwa20,000,000.00
 Jumla Songwe 172,703,839,113.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
942. MboziMbozi DCConstruction of Shiwinga Haterere water supply projectShiwinga, Haterere100,000,000.00
943. MboziMbozi DCConstruction of Msia Iganduka water supply projectMsia, Iganduka171,930,800.00
944. MboziMbozi DCConstruct Mbozi Mission Water Supply ProjectMatula366,515,434.00
945. MboziMbozi DCConstruct group Water supply project for Idiwili, Nyimbili and Mpanda villagesIdiwili, Nyimbili, Mpanda750,000,000.00
946. MboziMbozi DCConstruction group Water Supply project for Chimbuya, Mponela and Ukwile VillagesChimbuya, Mponela, Ukwile600,000,000.00
947. MboziMbozi DCExtension of Maninga Water Scheme to Ikonya village Maninga, Ikonya230,000,000.00
948. MboziMbozi DCConstruction of group Water supply project for Isansa, Mpito and Isowezya villagesIsansa, Mpito, Isowezya720,000,000.00
949. MboziMbozi DCConstruction of group Water supply Project for Isalalo, Wasa, Malolo and Izyeniche villages Isalalo, Wasa, Malolo, Izyaniche800,000,000.00
 Jumla Mbozi24,475,879,409.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
950. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in KisyeseVillageKisyese225,000,000.00
951. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in MtemboVillageMtembo159,885,000.00
952. IlejeIleje DCExtension of Itumba- Isongole water supply scheme Itumba, Isongole285,461,124.00
953. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Itega VillageItega80,000,000
954. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Kikota VillageKikota100,000,000
955. IlejeIleje DCconstruction of water supply project in Mswima VillageMswima80,000,000
956. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Ngulite VillageNgulite200,000,000
957. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Shuba VillageShuba 100,000,000
958. IlejeIleje DCconstruction of water supply project in Chilemba VillageChilemba 100,000,000
959. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Bulunga VillageBulunga80,000,000
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
960. Ileje Ileje DCconstruction of water supply project in Sapanda VillageSapanda150,000,000
961. IlejeIleje DCConstruction of water supply project in Lusalala VillageLusalala100,000,000
 Jumla Ileje22,190,346,124.00
962. Momba Momba DCCompletion of Mkomba water supply project VillageMkomba228,347,000.00
963. Momba Momba DCCompletion of Mpapa- Masanyinta water supply project VillageMpapa, Masanyinta, Kasanu436,279,073.00
964. Momba Momba DCCompletion of Ipito- MjiMwema water supply project VillageMji Mwema, Migombani, Jakaya120,215,325.00
965. Momba Momba DCCompletion of Uhuru- Tunduma water supply project VillageTunduma, Makambini, Uwanjani245,960,501.00
966. Momba Tunduma TCCompletion of Uhuru-Nyerere water supply project VillageMajengo Mapya, Mwl Nyerere, Msongwa75,454,000.00
967. Momba Momba DCExtension of Samang’ombe water supply project VillageIvuna, Lwatwe, Kalungu na Samang’omb e104,686,055.00
968. Momba Momba DCCompletion of Mkomba water supply project VillageMkomba28,347,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
969. Momba Momba DCCompletion of Mpapa- Masanyinta water supply project VillageMpapa, Masanyinta, Kasanu236,279,073.00
970. Momba Tunduma TCCompletion of Ipito- MjiMwema water supply project VillageMji Mwema, Migombani, Jakaya120,215,325.00
971. Momba Tunduma TCCompletion of Uhuru- Tunduma water supply project VillageTunduma, Makambini, Uwanjani155,960,501.00
972. Momba Momba DCConstruction of Msangano water supply project VillageMsangano, Naming’ong’ o, Makamba, Nkala, Yala, Ipata, Ntinga and Chindi400,000,000
973. Momba Momba DCConstruction of Isanga, Kakozi, Kapele, Itumba and Mlomba water supply project VillageIsanga, Kakozi, Kapele, Itumba and Mlomba190,000,000
974. MombaMbozi DCConsultancy service Momba group-Momba River 80,000,000
 Jumla Momba21,390,941,954.00
 JUMLA SONGWE27011,061,006,600.0 0
975.Tabora Nzega  Nzega DC Extension of lake victoria water supply to Ilagaja and Igalula villages by June 2023Igalula and Ilagaja 475,000,000.00
976.  Nzega  Nzega DC Extension of Lake Victoria water supply toGemedu287,230,345.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Gemedu village by June 2023  
977.  Nzega  Nzega DC extension of lake victoria water supply to Kigandu village by June 2023Kigandu309,000,000.00
978.  Nzega  Nzega DC Rehabilitation and Extension of 46 Existing water supply Projects including procurements of pipes, spares, water flow meter and Fittings at different villages  Ikindwa, Mahene, Buhondo, Sojo, Bukene, Uhemeli, Nata, Isanga, Mwaluzwilo, Itobo, Mwambaha, Ngukumo, Nkiniziwa, Nawa, Mbagwa, Mwakashan hala, Inagana, Magengati, Usagari, Isunha, Wela, Malilita, Mwabangu, Kabale, Kilabili, Mwamalulu, Kanolo, Utwigu, Busondo, Upungu, Kampala, Ilagaja, Chamipulu, Mwanhala, Iyombo,369,758,159.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Lakuyi, Mogwa, Kayombo, Mwamala, Iboja, Ubinga, Wita, Kabanga, Gulumuni and Ntoba  
979.  Nzega  Nzega DC Supply and Installation of power solar systems and submersible pump 7.5KW, Discharge 4m3/hr head max150m at Ikindwa and 7.5KW and   Discharge of 4m3/hr head max150m at Nawa Villages  by June 2023Ikindwa and Nawa55,403,610.00
980.  Nzega  Nzega DC Rehabilitation of  54 Hands pump in Nzega DC by June 2023Upungu(1), Iyombo Itima(2),Buk ene(2),Ngog oto(1),Selem i(1),Ikindwa( 2),Kayombo( 2),Malolo(2), Buhulyu(1),I sagenhe(1), Kidete(2), Zugimlole(1), Isanzu(2), Chamwabo( 1), Itobo(2), Lakuyi(1), Iditima(1), Kahamanhal138,107,887.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     anga(2), Kilino(1), Nhabala(2), Bulunde(2), Gulumbai(1), Idubula(3),It unda(1), Kasela (2), Lububu(1), Senge(2), Udutu(1), Mwasala(2), Ilelemhina(1) , Inagana(1), Magengati(1 ), Kagando(2), Kwanzale(1), Luhumbo(2), Mogwa(2), Usalala(2)K wanzale(1) Ubinga(2), Mwakashan hala (10), Kigandu(7), UgembeII(13 ), Ifumba(4), Mwaluzwilo (4), Bujulu(2), Wela(8), Milamo Itobo(14), Kakulungu(5 ), Magukula(11 ), Malole(1), Budushi(2), Mbutu(12), Mogwa(8), Mambali(11) 
 Jumla Nzega68,461,670,348.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
981.Tabora UYUI  UYUI-DC To procure steel pipe MS 300 DN30 for extension of Kigwa water supply by june 2023KigwaB, Nzigala, Matanda, Igalula, Ipululu, Isenefu, Imalakaseko , Goweko , Kamama, Mwitikila, Tambuka reli, Nsololo, Kimungi, itunda ukulu, na Kawekapina.410,000,000.00
 Jumla Uyui1410,000,000.00
982.TABORAUramboUrambo Dc Ukarabati wa pampu 30 za mkono katika vijiji vya Usisya  (03), Songambele (04), Uyogo (04), Ugalla (04),  Nsenda (03), Uyumbu (03), Ussoke (03), Itundu (03), na Muungano (03) Usisya, Songambele , Uyogo, Ugalla, Nsenda, Uyumbu, Ussoke, Itundu, and Muungano30,000,000.00
983. UramboUrambo DCUtafiti na Uchimbaji wa Visima 32 chini ya Ardhi.Isongwa, Tebela, Kamalendi, Nkokoto, Chekeleni, Mlangale, Kasela, Igunguli, Mpigwa, Mapambano, Ifuta, Kinhwa,1,419,341,220.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Kiloleni, SipunguUso ngelani, Yelayela, Katungulu, Nsogolo, Unzali, Igembensab o, Kangeme, Tumaini, Kitete, Mabundulu, Mwinyi, Itegamatwi, Wema and Mtakuja  
 Jumla Urambo21,439,341,220.00
984.TaboraSikongeSikonge DcUkarabati wa pampu za mkono 40 katika vijiji vya Isunda (3), Lufwisi (2), Mgambo (2), Chabutwa (2), Ibumba ( 2), Muungano (1), Mwanamkata (2), Pangale (2), Usesula (1), Usupilo( 2),  Usega (2), Mkola (1), Mwenge (1), Mwitikio (1), Mitwigu (2), Kasandalala (2) , Mpombwe (2) na Mole Mlimani (1)  Isunda, Lufwisi, Mgambo, Chabutwa, Ibumba, Muungano, Mwanamkata, Pangale, Usesula , Usupilo,  Usega , Mkola , Mwenge , Mwitikio , Mitwigu , Kasandalala, mpombwe and Mole Mlimani17,409,898.00  
985. SikongeSikonge DCUtafiti na uchimbaji waMigumbu, Makibo,160,669,936.00  
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    visima 17 chini ya ardhiNyahuanga, Nyahua, Mwanamkata, Igalula, Idekamiso, Mwamulu, Mihamakumi, Kipanga Mlimani, Isongwa, Matagata, Kilumbi, Kidete, Ibumba, Mwamaluhgu and Mitwigu 
 Jumla Sikonge1178,079,834.00
986. KaliuaKaliua DCConstruction of Piped Water Supply Project for Kombe village in Kaliua District Kombe200,000,000.00
987.  Kaliua  Kaliua DC Rehabilitatiom of Fourty (40) Boreholes in 30 villages at in Kaliua District Usinge, Kamsekwa, Kaliua mashariki, Lumbe (2), Kangeme, Usinga, Ushokola, Isanjandugu, Ulindwanoni, Kazaroho(2), Usimba, Kanoge, Ichemba, Ibambo, Mwongozo, Sasu, Seleli, Usigala, Kagera,100,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Kaswa, Kashishi, Busondi, Uyombo, Ilege(2), Taba, Mapigano, Mgelela, Songambele , Nsimbo, Imalamihayo , Ugunga, Tuombemun gu, Limbula, Uhindi, Nsungwa, Mpagasha and Maboha  
988. KaliuaKaliua DCConstruction of water supply project for Usinga Village in Kaliua District  Usinga200,000,000
989. KaliuaKaliua DCConstruction of Ilege, Seleli and Kingwangoko water supply project  Ilege, Seleli and King’wangoko168,751,548
990. KaliuaKaliua DCGeophysical survey and drilling of 43 boreholes in various villages.Mwaharaja, Shella, Imagi, Ulanga, Utantamke, Ntwigu, Mwamashimb a, Mpangasha, Magele, Imalaupina, Usangi, Ibapa,622,520,415.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Mwanduti, Chemkeni, Mtapenda, Busanda, Busubi, Malanga, Tupendane, Imalabupina, Kabanga, Usinge, Ugansa, Mwendakulim a, Seleli, Lumbe, Kingwangoko , Ibambo, Nsungwa, Mwamnange, Kamsekwa, Ilege, Sasu, Ulindwanoni, Makingi, Nhwande, Mpwaga, Kamsekwa, Mpandamlow oka, Igwisi, Mkuyuni, ,Limbula siasa and Kangeme villages 
 Jumla Kaliua51,291,271,963.00
991. IgungaIgunga DcConstruction of Water Supply Project at Mwamloli Village Mwamloli251,316,075.31
 Jumla Igunga  251,316,075.31
 JUMLA MKOA TABORA1309,470,376,321.31
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
992.TangaLushotoLushoto DCTo Construct water Infrastructure at Mkundi Mbaru & Mtae VillagesMakundi mbara na Mtae150,000,000.00
993. LushotoLushoto DCTo Construct Water infrastructure at Kisiwani Villageskisiwani110,000,000.00
994. LushotoLushoto DCTo Construct water Infrastructure at Msamaka Villagemsaka100,000,000.00
995. LushotoLushoto DCTo Construct water infrastructure at TeweTewe100,000,000.00
996. LushotoLushoto DCTo Construct water infrastructure at Makole/ Kilole/ Kwekanga Makole, Kilole, Kwekanga121,703,765.00
997. LushotoLushoto DCConstruction of Hemtoe/Golog olo water supply projectHomtoe and Gologolo230,000,000.00
998. LushotoLushoto DCTo Extend Usambara water scheme to Bagamoyo, Kwamzuza and Kivilicha VillagesBagamoyo, Kivilicha na Kwamzuza120,000,000.00
999. LushotoLushoto DCExtension of water supply scheme Bumbuli Kwanguluwekwanguluwe60,000,000.00
1000 LushotoLushoto DCRehabilitation of Magilamagila60,000,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    Water Supply scheme   
1001 LushotoLushoto DCUtafutaji wa Vyanzo vya Maji Makanya, Gale na MkanyaGale, Makanya na Kwai100,000,000.00
 Jumla Lushoto10171,151,703,765.00
1002 MkingaMkinga DCExtension from Tanga UWSSA to Mkinga (Mradi wa Mto Zigi) – Priority (Design stage) Mtimbwani, Kibiboni, Doda, Mbambamw arongo, Mazola, Mwandusi, Magaoni, Mtundani, Manza, Gezani, Parungu Kasera, Mkingaleo, Mzingimwag ongo, Vuo, Zingibari, Moa, Mayomvoni, Sigaya, Kibewani, Bwagamach o, Maforoni, Mwakikoya na Kwale350,000,000.00
 Jumla Mkinga124350,000,000.00
1003 KilindiKilindi DCConstruction of Diburuma Songe water Project Tunguli, Msamvu, Mtoro, Lusane, Mafulila, Kikunde, Ludewa, Kwekivu, Ngeze, Mapanga,350,050,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
     Lusimbi, Kitingi, Sambu, Kigunga, Mheza, Songe, Vilindwa, Kwamba, Mvunge, Nkama, Bokwa, Kwastemba, na Kwamwande 
 Jumla Kilindi123350,050,000.00
1004 HandeniHandeni DCExtension of Kwadoya Water ProjectKwadoya200,000,000.00
1005 HandeniHandeni DCConstruction of Kwamagome Water Projectkwamagome461,147,163.88
 Jumla Handeni22661,147,163.88
1006 MuhezaMuheza DCRehabilitation of Potwe water supply SchemeNdondondo, Mpirani50,000,000.00
1007 MuhezaMuheza DCConstruction of Kigombe water tank and Mtiti water supply project Kigombe40,000,000.00
1008 MuhezaMuheza DCConstruction of treatment plant at water supply scheme at Ubembe, Mlingano, Kicheba, Mashewa na Misozwe Ubembe, Kibanda Nkumba, Kicheba A, B, C, Mlingano, Misozwe, Mashewa,  40,000,000.00
1009 MuhezaMuheza DCConstruction of MIZEMBWE water supply project phase IIMianga, Msowero, Bwembwera 44,121,931.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
1010 MuhezaMuheza DCConstructiion of Kwedunda water supply schemeKwedunda 23,197,506.07
 Jumla Muheza514197,319,437.07
 JUMLA TANGA1802,610,220,365.95
1011ShinyangaKishapuKishapu DCExtension of Mwandoma water supply scheme to Mwamalasa village and Mwamalasa Secondary school by June 2023Mwamalasa60,094,486.40
1012ShinyangaKishapuKishapu DCExtension of Shagihilu water supply scheme to Shagihilu Secondary school by June 2023Shagihilu29,432,742.00
1013ShinyangaKishapuKishapu DCExtension of Mhunze to Mwabusiga Water Supply Project by June 2023Mwabusiga48,696,787.97
1014ShinyangaKishapuKishapu DCTo extend Ukenyenge water supply project to Wila subvillage by June 2023Wila49,000,000.00
1015ShinyangaKishapuKishapu DCTo conduct water Source development i.e geophysical survey and drilling of boreholes, sumpwellMangu, Mwamalasa, Somagedi, Mwalata, and Bulekela40,787,072.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    construction for Mangu, Mwamalasa, Somagedi, Mwalata, and Bulekela villages by June 2023  
1016 Jumla Kishapu 59 228,011,088.37 
1017 KahamaMsalala DCConstruction of 11 hand dug wells at at Mhandu (1), Izumba (1), Ikinda (2) Nyamishiga (1), Nyaminje (1), Ndalilo (1), Wisolele (1), Kalagwa (1), Igundu (1) and Ilelema (1) villages at Msalala DC Mhandu, Izumba, Ikinda Nyamishiga, Nyaminje, Ndalilo, Wisolele, Kalagwa, Igundu and Ilelema 35,560,000.00
1018 KahamaMsalala DCRehabilitation of 13 hand dug wells at Busulwangili (1), Lunguya (1), Chela (2), Mhandu (2), Buganzo (1), Kalagwa (1) na Buluma (1) na Nyakandoni (1), Bukwangu (1), Ntobo B(1), Jomu (1) in Msalala DC  Mhandu, Izumba, Ikinda, Nyamishiga, Nyaminje, Ndalilo, Wisolele, Kalagwa, Igundu and Ilelema36,505,000.00
1019 KahamaMsalala DCExtension of water scheme from MwambokuMagongwa203,186,902.54
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    S/T to Magongwa sub village in Msalala DC   
1020 KahamaUshetu DCConstruction of water Project at Chona, Busenda, Bukomela, Ubagwe and Uyogo Village at Ushetu DCChona, Busenda, Bukomela and Uyogo38,766,575.00
1021 KahamaUshetu DCRehabilitation of 58 hand dug wells at uyogo 3, Bukomela 7, Chambo 15, Chona 6, Idahina, Igunda 3, Igwamanoni 2, Mpunze 8, Sabasabini 3, Ulowa 2 Ukune 2 Ulewe 4 ward in UshetuUyogo, Bukomela, Chambo, Chona, Idahina, Igunda, Igwamanoni, Mpunze, Sabasabini, Ulowa, Ukune, Ulewe97,500,000.00
1022 KahamaUshetu DCRehabilitaion and installation of water solar system to the shallow wells at Makongoro, Nyambeshi, Ngokolo and Butibu villages in Ushetu DCMakongoro, Nyambeshi, Ngokolo and Butibu36,000,000.00
1023 KahamaUshetu DCConstruction of  Bugomba and Kinamapula Water Supply Project in Ushetu DCUbagwe, Bugomba and Kinamapula440,645,204.00
1024 KahamaUshetu DCConstruction of 14 hand dugUyogo – Manungu,46,120,000.00
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    wells at Ushetu Uyogo – Manungu, Nsunga, Idahina-Isanga, IgwamanoniNyakashatala, Mpunze-Bulima Sm, Butende, Ulewe-Itega, Ulowa Bugela, Ngirimba Ushetu. – Mkwangulwa, mhuge Villages in Ushetu DC Nsunga, Idahina- Isanga, IgwamanoniNyakashatala , MpunzeBulima Sm, Butende, Ulewe-Itega, Ulowa Bugela, Ngirimba Ushetu. – Mkwangulwa, mhuge  
  Jumla kahama  8 63 934,283,681.54 
1025 Shinyanga Shinyanga DcConstruction of distribution main and domestic water points at Nyaligongo Village by june 2023Nyaligongo615,304,866.00
1026 Shinyanga Shinyanga DcConstruction of water supply project for (Mwalukwa, Bulambila, Ng’hama and Kadoto” B”) in Shinyanga District Council by June 2023Mwalukwa, Bulambila, Ng’hama and Kadoto B455,447,678.00
1027 Shinyanga Shinyanga DcConstruction of Kilimawe water supply projects at Shinyanga district by June, 2023Kilimawe360,543,745.86
1028 Shinyanga Shinyanga DcExtension of Water SupplyNyaligomgo570,722,980.00 
Na.MkoaWilayaHalmashauriJina la MradiJina la Kijiji/ Vijiji NufaikaKiasi cha Fedha kilichotengwa Mwaka  2022/23  
    project from Mwakitolyo Storage Tank by June 2023  
1029 Shinyanga Shinyanga DcRehabilitation of 40 hand pamp at Bukene, Usule, Ilola, Imesela, Mwantini, Nyamalogo Lyabukande and Usanda in Shinyanga DCBukene, Usule, Ilola, Imesela, Mwantini, Nyamalogo Lyabukande and Usanda 12,000,000.00
 JUMLA KUU MIRADI MIPYA381495,112,000,802.07
 JUMLA KUU YA MIRADI YOTE1,029 304,899,693,093.33

Kiambatisho Na. 5: Orodha ya Mabwawa 15 yatakayotekelezwa katika mwaka 2022/23

Na.MkoaWilayaJina la Mradi Majina ya Vijiji Bajeti kwa 2022/23
1TangaMkingaConstruction of Mwakijembe Dam and Associated Civil WorksMwakijembe, Gombelo  Kwenkambala  Msomera  700,000,000
2TangaHandeniConstruction of Kwenkambala Earth damKivesa, Chanika, Kwamngumi, Chang`ombe, Zizini, Mji Mpya, Azimio, Mdoe and Zizini kati.1,302,313,232
3PwaniChalinzeConstruction of Mjembe DamKwamduma na Kwa Mjembe650,000,000
4RukwaKALAMBOConstruction of Kalemasha Earth damKalemasha1,770,686,092
5SongweSongwe Construction of Mbangala Earth damMbangala  1,000,000,000
6DodomaChamwinoConstruction of Msanga Earth damChamwino508,570,211
7DodomaChamwinoRehabilitation of Vikonje (Spilway, embankment and excavatuion of reservoir)Chamwino411,771,639
8DodomaChamwinoConstruction of Kuro Charco damChamwino179,658,150
9DodomaChamwinoConstruction of Magufuli Charco damChamwino61,155,250
10DodomaChamwinoConstruction of Pofu Charco damChamwino134,367,569
11DodomaChamwinoConstruction of CharcoChamwino61,155,250
Na.MkoaWilayaJina la Mradi Majina ya Vijiji Bajeti kwa 2022/23
   Earth dam  
12SimiyuItilimaRehabilitation of Mwamapalala SpillwayMwamapalala, Mwamunhu and Idefelo95,459,940
13ShinyangaKishapuRehabilitation of Sekeididi spillway Sekeididi, Bugoro, Ngwashinong’hela, Mwagalankulu & Wishitereja200,000,000
14MbeyaChunyaRehabilitation of Matwiga spillway Matwiga, Isengawana300,000,000
15DODOMA/ TANGA/ TABORAChembaConstruction of Kidoka Dam, Manga, Mandela, Mabanda, Kang’ata, Horohoro, Gendagenda, Rhombouti, Msente, Mkonde, Ichemba, Kalemela, Kizengi na Izimbili  Chemba Mjini, Chambalo, Makamaka, Paranga, Gwandi, Kambi ya Nyasa, Kidoka, Manga, Mandela, Mabanda, Kang’ata, Horohoro, Gendagenda, Rhombouti, Msente, Mkonde1,369,862,667
JUMLA    8,745,000,000

Kiambatisho Na. 6: Miradi 175 ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mijini Itakayotekelezwa mwaka 2022/2023

Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
1ArushaArusha jijiKukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka Jijini Arusha3,000,000,00015,863,122,00018,863,122,000GoT/ AfDB
2ArushaMonduliUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)500,000,0000500,000,000GoT
3ArushaMonduli Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Monduli-Enguiki1,100,000,00001,100,000,000NWF
4ArushaKaratuUjenzi wa miundombinu ya usambazaji maji kutoka visima vitatu vya maji 500,000,0000500,000,000GoT
5ArushaKaratu Ujenzi wa mradi wa majisafi wa Bwawani – Karatu225,000,0000500,000,000NWF
6ArushaLoliondoUkarabati na upanuzi wa mtandao wa maji safi.500,000,0000500,000,000GoT
7ArushaMereraniUjenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Mererani1,400,000,00001,400,000,000NWF
8ArushaOldonyo sambu Ujenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Oldonyosambu1,000,000,00001,000,000,000NWF
9ArushaArumeruMradi wa Maji Embaseni – Arumeru (Ngurdoto)1,000,000,00001,000,000,000NWF
10ArushaNgorong oroMradi wa Maji Mageri Ngorongoro600,000,0000600,000,000NWF

291

Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
11Dar es SalaamDar es SalaamKujenga mitandao ya kusambaza maji katika maeneo ambayo hayana huduma hiyo katika Jiji la Dar es Salaam2,000,000,00022,000,000,00024,000,000,000GoT/ World Bank
12Dar es SalaamDar es SalaamKujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Buguruni1,000,000,0008,000,000,0009,000,000,000GoT/So uth Korea
13Dar es SalaamDar es SalaamKujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Mbezi Beach 1,000,000,0004,624,274,9555,624,274,955GoT/  World Bank
14Dar es SalaamDar es SalaamKujenga miundombinu ya mfumo wa majitaka eneo la Kurasini1,000,000,0006,000,000,0007,000,000,000GoT/ AFD
15Dar es SalaamDar es SalaamUjenzi wa Bwawa la Kidunda52,500,000,00010,000,000,00062,500,000,000 GoT/BF
16Dar es SalaamDar es SalaamKuendelea na uchimbaji wa visima 20 Kimbiji na Mpera na ujenzi wa miundombinu ya majisafi.2,820,000,00002,820,000,000GoT
17Dar es SalaamDar es SalaamKujenga mradi wa majisafi kutoka mto Rufiji hadi Jijini Dar es Salaam1,000,000,00001,000,000,000GoT
18DodomaDodomaKukarabati na kupanua mtandao wa majisafi Jijini Dodoma 2,500,000,0007,000,000,0009,500,000,000GoT/Af DB
19DodomaDodomaKupanua na ukarabati wa mtandao wa majitaka Jijini Dodoma2,900,000,0004,000,000,0006,400,000,000GoT/N WF/ Korea
20DodomaDodomaUjenzi wa Mtandao wa Majisafi Mtera hadi Dodoma500,000,000500,000,0001,000,000,000GoT/W B
21DodomaDodomaUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Nala-Zuzu 400,000,0000  400,000,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
22DodomaChamwin oUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Chamwino1,000,000,00001,000,000,000GoT
23DodomaChamwin o- MtumbaUjenzi wa mradi wa majisafi wa Chamwino- Mtumba 550,000,0000550,000,000NWF
24DodomaBahiUjenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji 400,000,0000400,000,000GoT
25DodomaMpwapw aUpanuzi na ukarabati wa mradi wa majisafi wa Mpwapwa 550,000,0000550,000,000NWF
26DodomaKongwaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao ya maji, kuunganisha na kufungia wateja dira za maji)500,000,0000500,000,000GoT
27Singida & DodomaDodoma & SingidaKujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria hadi Mikoa ya Singida na Dodoma1,930,000,0005,449,000,0007,379,000,000GoT/Af DB
28GeitaChatoUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Chato1,000,000,00001,000,000,000GoT
29GeitaChatoUjenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Chato1,000,000,00001,000,000,000GoT
30GeitaGeitaKuboresha mfumo wa maji katika mji wa Geita1,100,000,00001,100,000,000GoT
31GeitaUshirom boUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
32GeitaUshirom boUboreshaji wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ushirombo303,676,0000303,676,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
33GeitaMbogweUjenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji 400,000,0000400,000,000GoT
34GeitaKatoroUjenzi wa bomba kuu kutoa maji katika chanzo na miundombinu ya usambazaji maji 500,000,0000500,000,000GoT
35GeitaKatoro- Buseres ereUpanuzi wa mtandao wa majisafi wa KatoroBuseresere awamu ya pili400,000,0000400,000,000NWF
36IringaKiloloUjenzi wa tanki lenye mita za ujazo 100, Kuchimba na kulaza bomba kuu kilomita 4 na ununuzi wa dira za maji 600300,000,0000300,000,000GoT
37IringaKiloloUjenzi wa mradi wa majisafi wa Isimani-Kilolo1,000,000,00001,000,000,000NWF
38IringaMafingaUboreshaji wa huduma ya maji mjini Mafinga (Ihongole, Changarawe, Kinyayambo & Sao Hill700,000,0000700,000,000GoT/N WF
39KageraBukobaUjenzi wa mtandao wa majitaka katika manispaa ya Bukoba2,000,000,00002,000,000,000GoT
40KageraBukobaKupanua mtandao wa majisafi Bukoba Mjini1,000,000,00001,000,000,000GoT
41KageraBukobaUpanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya pembezoni mwa mji na VETA 400,000,0000400,000,000NWF
42KageraMulebaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na300,000,0000300,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   kuunganisha wateja)    
43KageraNgaraUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
44KageraNgaraUchimbaji wa visima na upanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ngara 492,000,0000492,000,000NWF
45KageraBiharam uloUjenzi wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka Mji wa Biharamulo500,000,0000500,000,000GoT
46KageraBiharam uloUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi mjini Biharamulo (Biharamulo mjini, Nyarubungo, Runazi, Nyakahura, Bisibo, Nemba, Nyanza Areas)730,269,7230730,269,723GoT/N WF
47KageraKyaka- BunaziUjenzi wa mradi wa majisafi wa Kyaka-Bunazi 1,000,000,00001,000,000,000NWF
48KageraMulebaUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Muleba328,000,0000328,000,000NWF
49KataviMpandaKuboresha mfumo wa maji katika mji wa Mpanda (Shankala Water awamu ya II)1,400,000,00001,400,000,000GoT/N WF
50Kigoma, Rukwa, LindiSumbaw anga, Lindi & KigomaKujenga miundombinu ya majisafi na usafi wa mazingira katika miji ya Kigoma,1,800,000,0004,000,000,0005,800,000,000GoT/ EU/  KfW
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   Sumbawanga na Lindi    
51KigomaKibondoUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
52KigomaKibondoUjenzi, upanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Kibondo800,000,0000800,000,000NWF
53KigomaKasuluUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
54KigomaKasuluUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Kasulu (Kata za Murubona, Murusi, Kumnyika na Kumsenga Murubona)335,000,0000335,000,000NWF
55Kilimanj aroMoshiKupanua mtandao wa kupitisha majitaka katika Manispaa ya Moshi.1,000,000,00001,000,000,000GoT
56Kilimanj aroSame – MwangaUjenzi wa Mradi wa majisafi Same- Mwanga- Korogwe 10,648,000,0003,000,000,00011,648,000,000GoT/ NWF/B ADEA KUWAI T/SAUD FUND/ DFID
57Kilimanj aroHimoUpanuzi wa mitandao, ununuzi wa dira za maji na kuunganisha400,000,0000400,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   wateja    
58Kilimanj aroMoshi RuralUboreshaji wa huduma ya maji (upanuzi wa mtandao wa maji)500,000,0000500,000,000GoT
59Kilimanj aroRomboUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Rombo Mjini500,000,0000500,000,000GoT
60Kilimanj aroRomboUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Rombo (Mahorosha, Msaranga, Kwalakamu, Ngoyoni, in Rombo Mjini)600,000,0000600,000,000NWF
61Kilimanj aroMoshi MjiniUjenzi wa mtandao wa majisafi katika Kata 121,000,000,00001,000,000,000NWF
62Kilimanj aroMoshi Mjiniujenzi wa mtandao wa majisafi wa Miwaleni – Njiapanda 700,000,0000700,000,000NWF
63LindiNg’apa, Mitwero na MchingaKujenga miundombinu ya majisafi katika maeneo ya Ng’apa, Mwitero na Mchinga katika Mji wa Lindi     1,000,000,000 01,000,000,000GoT
64LindiMitwero, Mkwaya na KitundaKujenga miundombinu ya majisafi katika maeneo ya Mitwero, Mkwaya na Kitunda        500,000,000 0500,000,000NWF
65LindiMchinga Phase II Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Mchinga awamu ya kwanza    1,010,000,000 01010000000NWF
66LindiRuangw aUjenzi na upanuzi wa mtandao wa    1,000,000,000 01,000,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   majisafi katika Mji wa Ruangwa    
67LindiRuangw aUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika mji wa Ruangwa kwenye maeneo ya hospitali ya Wilaya, Mji mpya karibu na Majaliwa stadium A’, Magereza na Shule ya Msingi Dodoma        350,000,000 0350,000,000NWF
68LindiLiwaleUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)       400,000,000 0400,000,000GoT
69Manyara BabatiKujenga miundombinu ya majisafi katika Mji wa Babati1,000,000,00001,000,000,000GoT
70Manyara Babati, Lindi, Kigoma na Sumbaw anga Ujenzi wa mtandao wa majisafi Mjini Babati na mtandao wa majitaka katika Miji ya Babati, Sumbawanga, Lindi na Kigoma500,000,0002,000,000,0002,500,000,000GoT/Kf W
71Manyara BabatiUjenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Babati1,000,000,00001,000,000,000GoT
72Manyara Orkesum entUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Orkesment2,300,000,0007,500,000,0009,500,000,000GoT/ NWF/B ADEA
73Manyara MereraniUjenzi wa matanki mawili yenye jumla ya mita za ujazo 180, na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji.300,000,0000300,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
74Manyara KateshUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
75Manyara BashnetUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
76Manyara MaguguUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
77Manyara GallapoUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
78Manyara SaweUjenzi wav tanki la kuhifadhia majisafi (2,000m3) katika maeneo ya Sawe900,000,0000900,000,000NWF
79Manyara DaredaUjenzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Dareda -Singu-DagailoySiginoi1,000,000,00001,000,000,000NWF
80MaraMusomaUjenzi na upanuzi wa mtandao wa majisafi katika mji wa Musoma kwenye maeneo ya Kwangwa, Songambele, Bukoba, Bweri, Nyangwe and Kiara A areas300,000,0000300,000,000NWF
81MaraBundaUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Bunda2,700,000,00002,700,000,000GoT/N WF
82MaraMugangoUjenzi wa mradi wa Mugango- Kiabakari-Butiama, pamoja na vijiji4,000,000,0003,500,000,0006,500,000,000GoT/ NWF/B ADEA/ SAUDIA
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   vilivyo pembezoni mwa bomba kuu    
83MaraTarimeUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
84MaraMugumuKukamilisha Ujenzi wa mtambo wa kutibu majisafi katika bwawa la Manchira300,000,0000300,000,000GoT
85MbeyaMbeyaUjenzi wa miundombinu ya majisafi kutoka chanzo cha Kiwira 5,000,000,00005,000,000,000GoT/N WF
86MbeyaChunyaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
87MbeyaKyela Ujenzi wa mradi wa majisafi katika mji wa Kyela 800,000,0000800,000,000NWF
88MbeyaMbaliziMradi wa kuboresha huduma ya Maji Iwambi na Mbalizi (Ilunga Project)700,000,0000700,000,000NWF
89MbeyaMbakaMradi wa kuboresha huduma ya majisafi Tukuyu kutoka chanzo cha Mto Mbaka500,000,0000500,000,000NWF
90Morogor oMorogor oKukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka Mji wa Morogoro 1,000,000,0004,000,000,0005,000,000,000GoT/ AfD
91Morogor oMorogor oUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa maji700,000,0000700,000,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   Mindu     
92Morogor oIfakaraUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
93Morogor oMikumiUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
94Morogor oKilosaUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa maji wa Manzese kilosa na Kingolowira 807,794,9610807,794,961NWF
95MtwaraMtwaraKujenga mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma hadi Manispaa ya Mtwara-Mikindani, vikiwemo vijiji vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu1,000,000,000  4,000,000,000    5,000,000,000GoT/Af DB
96MtwaraMtwaraUpanuzi na ukarabati wa chujio la Mangamba na Mtawanya267,054,2770267,054,277NWF
97MtwaraMakondeKukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa Makonde1,500,000,00001,500,000,000GoT/N WF
98MtwaraMasasiUjenzi miundombinu ya majisafi katika mradi wa Masasi/Nachingwe a.1,240,000,00001,240,000,000GoT/N WF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
99MtwaraMangakaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
100MtwaraNanyam baUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
101MwanzaMwanza, Misungwi , Lamadi & MaguKupanua mtandao wa majitaka katika miji ya Mwanza, Bukoba na Musoma; na Kujenga mtandao wa majisafi katika miji ya Misungwi na Magu1,000,000,0004,000,000,0005,000,000,000GoT/ EIB & AFD
102MwanzaMwanza JijiUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya pembezoni mwa mji wa Mwanza; Kayenze, Igombe, Shibula, Lwanhima and Sangabuye.350,000,0000350,000,000NWF
103MwanzaKwimba, Malampa ka, SumveKujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria hadi miji ya Malampaka, Sumve na Malya2,000,000,00002,000,000,000GoT
104MwanzaSengere maUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Nyasigu – Lubungo – Ngoma 900,000,0000900,000,000NWF
105NjombeWanging’ ombeKukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka1,000,000,00001,000,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   mradi wa kitaifa wa Wanging’ombe    
106NjombeNjombeKuboresha mfumo wa maji katika mji wa Njombe1,000,000,00001,000,000,000GoT
107NjombeNjombeUpanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Livingstine (Ijunilo) 417,000,0000417,000,000NWF
108NjombeNjombeUjenzi wa mabwawa ya majitaka katika Mji wa Njombe1,000,000,00001,000,000,000GoT
109NjombeMaketeUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)500,000,0000500,000,000GoT
110NjombeMakamb akoUboreshaji wa huduma ya maji maeneo ya (Majengo, Kikula, Magavani na Mlowa)900,000,0000500,000,000GoT/N WF
111PwaniChalinzeUjenzi wa mradi wa maji wa Chalinze (Awamu ya Tatu)300,000,0006,051,000,0006,351,000,000GoT/Ind ia
112RuvumaTunduruUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)500,000,0000500,000,000GoT
113RuvumaTunduruUboreshaji wa mtandao wa majisafi katika mji wa Tunduru Township awamu ya II450,000,0000450,000,000NWF
114RuvumaMbingaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu,400,000,0000400,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)    
115RuvumaSongeaUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi katika hospitali ya rufaa ya ya Ruvuma maeneo ya Mwengemshindo465,000,0000465,000,000NWF
116RukwaSumbaw anga Ujenzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Muze250,000,0000250,000,000NWF
117RukwaSumbaw angaUjenzi wa mtandao wa majisafi katika eneo la Kirando Kamwanda 300,000,0000300,000,000NWF
118Shinyan gaShinyang aKujenga na kukarabati mtandao wa majisafi katika Mji wa Shinyanga300,000,0001,000,000,0001,300,000,000GoT/ AFD
119Shinyan gaUshetuUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
120Shinyan gaIsakaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
121Shinyan gaMalampa kaUjenzi wa mradi wa majisafi wa Lake Victoria kwenda miji ya Mhalo Malampaka na Mallya kwa umbali wa kilomita 79500,000,0000500,000,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
122Shinyan gaShinyang aUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Wilaya ya Shinyanga (Mwanubi, Didia, Iselamagazi, Kizumbi, Ibadakuli, Kolandoto, Chibe and Lubaga)800,000,0000800,000,000NWF
123Shinyan gaKahamaUpanuzi wa mtandao wa majisafi maeneo ya Kata ya Kilago na Kahama750,000,0000750,000,000NWF
124Shinyan gaKagongw a na KahamaUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Kata ya Isagehe; Mwenda Kulima na Kagongwa Isaka 400,000,0000400,000,000NWF
125SimiyuMaswaKukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa Maswa700,000,0000700,000,000GoT
126SimiyuMaswaUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Maswa (Vijiji vya Mwashegeshi na Buyupi)267,487,3180267,487,318NWF
127SimiyuBariadiKuboresha mfumo wa maji katika mji wa Bariadi1,000,000,00001,000,000,000GoT
128SimiyuBariadiUborreshaji wa mtandao wa majisafi Bariadi mjini kwenye maeneo ya Old Maswa and Kidinda 300,000,0000300,000,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
129SimiyuBusega, Bariadi, Laganga bilili na Mwanhu zi Kujenga mradi wa kutoa Ziwa Victoria hadi miji ya Busega, Bariadi, Lagangabilili na Mwanhuzi3,000,000,00016,510,000,00019,510,000,000GoT/ KFW/ GCF
130SimiyuLaganga bililiUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
131SimiyuMwanhu ziUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
132SimiyuMwanhu ziUboreshaji wa huduma ya majisafi katika mji wa Mwanhuzi300,000,0000300,000,000NWF
133SimiyuBusegaUpanuzi wa mtandao wa majisafi katika maeneo ya Mwalukonge, Bukabile – Bulima na Lukungu 300,000,0000300,000,000NWF
134SimiyuMaswaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)500,000,0000500,000,000GoT
135SingidaSingidaKukarabati na kupanua mtandao wa majisafi katika Mji wa Singida1,000,000,00001,000,000,000GoT
136SingidaSingidaUjenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Singida1,000,000,00001,000,000,000GoT
137SingidaSingidaUjenzi wa mradi300,000,0000300,000,000NWF
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   wa maji wa Unyambwa    
138SingidaManyoniUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati na upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
139SingidaItigiUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati na upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
140SongweVwawaKuboresha mfumo wa maji katika mji wa Vwawa/ Mlowo.1,000,000,00001,000,000,000GoT
141SongweVwawa & Tundum aKukarabati na kupanua mtandao wa majisafi na majitaka katika miji ya Vwawa na Tunduma1,000,000,0005,000,000,0006,000,000,000GoT/Kf W
142Songwe VwawaUboreshaji wa huduma ya majisafi katika mji wa Vwawa (chanzo cha Mwansyana )392,106,6010392,106,601NWF
143TaboraTaboraUjenzi wa bwawa la kutibu majitaka katika Manispaa ya Tabora1,000,000,00001,000,000,000GoT
144TaboraTaboraUkarabati wa bomba kuu la majisafi kutoka Msange JKT hadi Tumbi Area250,000,0000250,000,000NWF
145TaboraNzegaKukarabati na kupanua mfumo wa maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na mtandao mjini Nzega (Idudumo)2,350,000,00002,000,000,000GoT/N WF
146TaboraNzegaUjenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji1,000,000,00001,000,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   wa Nzega    
147TaboraIgungaUjenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Igunga1,000,000,00001,000,000,000GoT
148TaboraTinde na SheluiUjenzi wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda miji ya Tinde na Shelui. 340,000,0006,560,070,0006,900,070,000GoT/ INDIA
149TaboraSikongeUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
150TaboraUramboUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
151TaboraKaliuaUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
152TaboraIzikizyaUjenzi wa mtandao wa majisafi 400,000,0000400,000,000GoT
153TangaTangaUjenzi wa bwawa ya kutibu majitaka na mtandao wa majitaka katika Jiji la Tanga100,000,000334,478,000434,478,000GoT/ WB
154TangaTangaUjenzi wa miundombinu ya majisafi na ufungaji wa pampu maeneo ya Madanga na Kimang’a 357,843,2130357,843,213NFW
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
155TangaTangaUjenzi na ukarabati wa mradi wa majisafi wa Mabokweni areas – Kibafuta, Chongoleani, Mleni Water Supply Project in Tanga – awamu ya II600,000,0000600,000,000NFW
156TangaMkingaUpanuzi wa mradi wa majisafi kutoka Tanga hadi mji wa Mkinga 500,000,0000500,000,000NFW
157TangaHTMKukarabati mfumo wa maji katika maeneo yanayopata huduma kutoka mradi wa kitaifa wa HTM1,000,000,00000GoT
158TangaHTMUjenzi wa Chanzo cha maji cha Mandera, nyumba ya kuhifadhi pump na ukarabati wa tanki la Bongi 252,592,0470252,592,047NFW
159TangaHTMUpanuzi na ukarabati wa mtandao wa majisafi maeneo ya Segera – Kabuku 1,000,000,00001,000,000,000NFW
160TangaMuhezaUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Muheza.700,000,0000700,000,000GoT
161TangaMuhezaUboreshaji wa hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi katika Mji wa Muheza300,000,0000300,000,000NFW
162TangaPanganiUjenzi wa mfumo wa maji katika mji wa Pangani.1,000,000,00001,000,000,000GoT
163TangaPanganiUjenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji wa Pangani1,000,000,00001,000,000,000GoT
164TangaMuhezaUjenzi wa miundombinu ya majitaka katika Mji1,000,000,00001,000,000,000GoT
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   wa Muheza    
165TangaKorogweUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)500,000,0000500,000,000GoT
166TangaSongeUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)300,000,0000300,000,000GoT
167TangaHandeniUboreshaji wa huduma ya maji (ukarabati, ununuzi wa pampu, upanuzi wa mitandao na kuunganisha wateja)400,000,0000400,000,000GoT
168Miji ya MipakaniMiji ya MipakaniUjenzi na ukarabati wa mfumo wa majisafi katika miji ya mipakani ya Holili, Horohoro, Namanga, and Sirari1,000,000,00001,000,000,000GoT
169Mikoa yoteMiji 28Ujenzi na upanuzi wa mfumo wa majisafi katika Miji 28 (Muheza, Wanging’ombe, Kayanga, Makonde, Njombe, Makambako, HTM, Manyoni, Songea, Sikonge, Chunya,  Kasulu, Kilwa Masoko, Rujewa, Mugumu, Geita, Chato, Zanzibar, Singida7,000,000,00029,439,333,04536,439,333,045GoT/ India
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
   Mjini, Kiomboi, Mpanda, Chemba, Mafinga, UramboKaliua, Pangani, Ifakara, Rorya/Tarime na Chamwino)    
170Ruvuma, Mara, Lindi na IringaSongea, Rorya, Mafinga na Makonde Ujenzi na upanuzi wa mfumo wa majisafi katika Miji ya Songea, Rorya, Mafinga na Makonde 1,000,000,00001,000,000,000NWF
171 Mikoa yote Mamlaka Zenye Upotevu Mkubwa wa Maji Kutekeleza mikakati ya kupunguza upotevu wa maji katika Mamlaka za maji1,000,000,00001,000,000,000GoT
172 Mikoa yote Mamlaka zoteKufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya majitaka katika miji mikuu ya mkoa1,000,000,00001,000,000,000GoT
173Mikoa yoteMiji MingiKufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya maji katika miji mikuu ya wilaya na miji midogo2,000,000,00002,000,000,000GoT
174Mikoa yoteMiji midogo, Miji Mikuu ya Wilaya na Miradi ya KitaifaKufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya majitaka katika miji midogo, miji mikuu ya Wilaya na Miradi ya kitaifa1,000,000,0004,000,000,0005,000,000,000GoT/Af DB
Na.MkoaMji/EneoJina la Mradi/ KaziKiasi cha fedha kilichotengwa Jina la Mfadhili
Fedha za NdaniFedha za NjeJumla
175MoWMoWKujenga uwezo mamlaka za maji nchini kwa kujenga na kukarabati ofisi na kununua vitendea kazi 4,172,820,000400,000,0004,572,820,000GoT/BT
  JUMLA214,951,644,140184,731,278,000394,407,922,140 

[1] . Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee napenda kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan; kwa uongozi makini na thabiti aliouonesha katika mwaka wa kwanza wa Serikali ya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *