Na Emmanuel Charles

Mbunge wa Jimbo la Momba Mhe. Condester Sichalwe amesema kuna haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa Kurasimisha Pombe za Kienyeji ili kutumika kama vinywaji rasmi na kuachana na Pombe kutoka nje.
Mhe. Condester ameyasema hayo leo Mei 09, 2022 Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda, na Biashara