HOTUBA YA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, MHESHIMIWA. DKT. NDUMBARO WAKATI AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

1
HOTUBA YA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, MHESHIMIWA. DKT.
DAMAS DANIEL NDUMBARO (MB), WAKATI AKIWASILISHA
BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA
MWAKA WA FEDHA 2022/2023


A. UTANGULIZI

  1. Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa zilizowasilishwa leo katika
    Bunge lako na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na
    Sheria na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, naomba
    kutoa hoja kwamba Bunge lako sasa likubali kupokea, kujadili na kupitisha
    Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya
    Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.
    Salamu za Pongezi, Shukrani na Pole
  2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu
    mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana
    hapa leo kwa ajili ya kujadili taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa mpango na
    bajeti kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na mwelekeo wa mpango na bajeti
    ya Wizara na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Aidha,
    ninaomba kuwatakia heri ya Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani
    kwa Waislamu wote. Vilevile, nitumie fursa hii kuwatakia wananchi wote
    kheri ya sikukuu ya Eid.
  3. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naomba nichukue fursa hii
    kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa kutimiza mwaka
    mmoja tangu ashike nafasi ya kuongoza nchi yetu akiwa Rais wa Awamu
    ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika kipindi hicho,
    2
    tumeshuhudia mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta
    ya sheria. Naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge na Wananchi
    wenzangu kuendelea kumuombea Rais wetu kwa Mwenyezi Mungu
    amjaalie kila la kheri katika kuliongoza Taifa letu la Tanzania.
  4. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kuwapongeza Mheshimiwa
    Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
    Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na
    Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mheshimiwa Kassim Majaliwa
    Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
    uongozi wao mahiri katika kulitumikia Taifa letu.
  5. Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii kukupongeza wewe
    binafsi Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
    kwa kuchaguliwa kwako na Bunge na kwa kupata ushindi wa kishindo.
    Kuchaguliwa kwako kunaonesha imani kubwa waliyonayo Wabunge ya
    kuliongoza Bunge hili kwa umahiri mkubwa. Aidha, nimpongeze
    Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb.), kwa kuchaguliwa kuwa Naibu
    Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Vilevile,
    niwapongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na
    Sheria Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Madaba na
    Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mheshimiwa Sillo
    Daniel Baran, Mbunge wa Babati Vijijini, Makamu Wenyeviti pamoja na
    Wajumbe wa Kamati hizo mbili kwa ushauri na maelekezo ambayo
    yamewezesha Wizara na Taasisi zake kutekeleza majukumu yake kwa
    ufanisi.
    3
  6. Mheshimiwa Spika, Nitumie fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa
    Emmanuel Lekishon Shangai (Mb.) kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa
    Jimbo la Ngorongoro na Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha (Mb.) kwa
    kuteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
    Ni matumaini yangu kuwa Wabunge hao watashirikiana na Wabunge
    wengine katika kutekeleza majukumu yao.
  7. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee, nichukue fursa hii
    kumshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya
    Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kuiongoza
    Wizara hii ya Katiba na Sheria. Ninaahidi kuendelea kuitumikia nafasi hii
    kwa uaminifu na uadilifu ili kuwaletea maendeleo wananchi na Taifa kwa
    ujumla. Aidha, namshukuru na kumpongeza kwa dhati mtangulizi wangu
    Mheshimiwa George Boniface Simbachawene, Mbunge wa Kibakwe na
    Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) kwa
    kuingoza Wizara hii kwa umahiri. Vilevile, nimpongeze Mheshimiwa Balozi
    Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb.), kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na
    Utalii.
  8. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Bunge lako
    lilipoteza Waheshimiwa Wabunge ambao tulikuwa nao katika Bunge hili.
    Wabunge hao ni Mheshimiwa William Tate Olenasha, aliyekuwa Mbunge
    wa Ngorongoro na Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama, aliyekuwa
    Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Rukwa. Hivyo, naomba nitumie
    fursa hii kutuma salamu zangu za pole kwako wewe binafsi Mheshimiwa
    Spika, Bunge lako kwa ujumla, ndugu na wananchi wa majimbo husika
    waliopoteza wapendwa wao. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu
    hao mahala pema peponi. Amina.
    4
    B. DIRA NA DHIMA
  9. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Katiba na Sheria inaongozwa na Dira
    ambayo ni Katiba na Sheria wezeshi kwa maendeleo ya Taifa. Dira
    inalenga kuweka mazingira rafiki ya kisera na ya kisheria ya kuwezesha
    utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa, kudumisha hali ya amani,
    utulivu na utangamano wa kitaifa ambazo ni nguzo muhimu kwa mstakabali
    wa Taifa letu. Aidha, Dhima ya Wizara ni Kuwa na mfumo madhubuti wa
    Kikatiba na Sheria wenye kufanikisha utekelezaji wa sera na mipango kwa
    maendeleo ya Taifa. Dhima hii inahimiza ubunifu katika kujenga mazingira
    wezeshi ya upatikanaji haki na huduma bora za kisheria kwa wananchi.
    Aidha, Dira na Dhima hii imeakisiwa katika Dira na Dhima za Taasisi.
    C. MUUNDO NA MAJUKUMU YA WIZARA
  10. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Katiba na Sheria inajumuisha Mhimili
    wa Mahakama ya Tanzania, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi
    ya Taifa ya Mashtaka, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Wakala wa Usajili
    Ufilisi na Udhamini, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tume ya
    Kurekebisha Sheria Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahakama, Taasisi
    ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania na Chuo cha Uongozi
    wa Mahakama-Lushoto. Katika kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha
    kuwa nchi inaongozwa kwa kuzingatia Katiba, sheria, Kanuni na taratibu
    zilizowekwa na vyombo halali vya maamuzi, Wizara imeendelea kutekeleza
    majukumu yake kama yalivyoainishwa katika Hati ya Mgawanyo wa
    Majukumu kwa Mawaziri, kupitia Tangazo la Serikali Na. 534/2021
    majukumu hayo ni: –
    5
    (i.) Kutunga Sera zinazohusu masuala ya kisheria na kusimamia
    utekelezaji wake;
    (ii.) Kushughulikia mambo ya kikatiba;
    (iii.) Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki;
    (iv.) Uandishi wa sheria;
    (v.) Kuendesha mashtaka ya jinai;
    (vi.) Kushughulikia uendeshaji wa mashauri ya madai na
    usuluhishi;
    (vii.) Usuluhishi wa migogoro ya kibiashara, Sheria za kimataifa na
    Mikataba;
    (viii.) Kuratibu masuala ya haki za binadamu na utoaji wa huduma
    ya msaada wa kisheria;
    (ix.) Kuratibu shughuli za usajili wa matukio muhimu ya binadamu,
    ufilisi na udhamini;
    (x.) Kuratibu tathmini na maboresho ya Sheria;
    (xi.) Kuratibu ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Sheria za
    Utajiri na Maliasilia za nchi;
    (xii.) Kushughulikia urejeshwaji wa wahalifu na masuala ya
    ushirikiano wa kimataifa kwenye makosa ya jinai;
    (xiii.) Kuboresha utendaji na maendeleo ya rasilimali watu iliyo chini
    ya Wizara; na
    (xiv.) Kuratibu shughuli za taasisi, mipango na miradi chini ya
    Wizara.
    6
    D. UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA
    FEDHA 2021/2022
  11. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa
    mwaka wa fedha 2021/2022 umezingatia miongozo mbalimbali ya kisera
    ya Kitaifa, kikanda na kimataifa. Miongozo hiyo ni pamoja na Dira ya
    Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2025; Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa
    Taifa wa miaka Mitano 2021/22- 2025/26 ambao unalenga kujenga uchumi
    shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu; Ilani ya Uchaguzi ya Chama
    cha Mapinduzi ya mwaka 2020 hadi 2025; Maelekezo ya Mheshimiwa
    Samia Suluhu Hassan, Rais wa Awamu ya Sita wa Jamhuri wa Muungano
    wa Tanzania aliyoyatoa wakati akihutubia Bunge la 12 la Jamhuri ya
    Muungano wa Tanzania mwezi Aprili, 2021 pamoja na maelekezo ya
    viongozi wakuu wa Serikali. Aidha, Wizara inazingatia Malengo ya
    Maendeleo Endelevu ya Dunia 2030; Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063;
    Mpango Mkakati wa SADC wa Maendeleo 2020-2030; Mpango Mkakati wa
    Jumuia ya Afrika Mashariki wa Maendeleo 2021/2022 – 2025/2026; pamoja
    na Mpango Mkakati wa Wizara wa mwaka 2021/22-2025/26.
  12. Mheshimiwa Spika, kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa
    Fedha 2021/2022, Wizara na Taasisi zake ilibainisha masuala mahsusi
    ya kipaumbele kuwa msingi wa kutekeleza majukumu yake. Utekelezaji
    wa majukumu ya Wizara ni kama ifuatavyo:-
    7
    I. Kushughulikia Masuala ya Kisera ya Sekta ya Sheria na Kusimamia
    Utekelezaji wake
  13. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuratibu masuala ya kisera
    na kikatiba ili kuhakikisha kuwa haki inafikiwa na inapatikana kwa wakati na
    gharama nafuu. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Wizara
    iliendelea kuimarisha, kusimamia na kuratibu mfumo wa utatuzi wa
    migogoro kwa njia mbadala ndani na nje ya mfumo wa Mahakama. Wizara
    ilisimamia kutungwa kwa Sheria ya Usuluhishi, Sura ya 15 na Marekebisho
    ya Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Daawa, Sura ya 33. Sheria hizi
    zinaweka misingi ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi,
    upatanishi, majadiliano na maridhiano. Aidha, Waziri mwenye dhamana na
    masuala ya Sheria alitengeneza Kanuni za Sheria hizo ili kuwezesha utoaji
    haki kwa wakati, kupunguza gharama za uendeshaji mashauri, mlundikano
    wa mashauri na kurahisisha ufikiaji wa haki. Kanuni hizo zimeweka misingi
    ya ithibati ya watoa huduma za utatuzi wa migogoro na utambuzi wao.
    Vilevile, Wizara imefanikisha kuweka mfumo wa usajili wa Watatuzi wa
    migogoro kwa njia mbadala ambapo, jumla ya Wasuluhishi 192,
    Wapatanishi 106, Waendesha majadiliano 37 na Waendesha
    Maridhiano 23, walisajiliwa na kupatiwa vyeti.
  14. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Wadau wa Sekta
    imeratibu zoezi la maandalizi ya Sera ya Taifa ya Mashtaka ambapo
    Andiko la Mapendekezo ya kutunga sera hiyo limekamilika. Sera hiyo
    inalenga kuimarisha huduma za uendeshaji wa Mashtaka ya jinai nchini ili
    kuhakikisha Serikali inaimarisha hali ya amani na usalama katika jamii.
    Vilevile, Wizara iliandaa rasimu ya Kanuni za Sheria ya Kuwalinda
    Mashahidi na Watoa Taarifa za Uhalifu (Sura 446).
    8
  15. Mheshimiwa Spika, Kuhusu masuala ya ufuatiliaji haki, Wizara
    imeendelea kuratibu masuala ya kisera yanayohusu utoaji haki kwa
    kutembelea na kukagua maeneo ya vizuizi ikiwemo Magereza, Mahabusu
    za watoto na vituo vya Polisi. Aidha, Wizara ilitembelea Mahakama Kuu,
    Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo pamoja na vituo jumuishi
    vya utoaji haki vya Mahakama. Lengo la kaguzi hizi ni kufuatilia utekelezaji
    wa haki, kuainisha changamoto za kiutendaji na kiupelelezi na kutoa
    maelekezo stahiki ya kutatua changamoto hizo. Wizara ilikagua utendaji
    kazi wa Taasisi hizo ili kubaini endapo unazingatia misingi ya Utawala
    Bora, Utawala wa Sheria na utoaji haki kwa wananchi. Katika kipindi cha
    Julai, 2021 hadi Machi, 2022 jumla ya magereza 129 yalikaguliwa
    ikilinganishwa na magereza 64 yaliyokaguliwa kipindi cha Julai, 2020 hadi
    Machi, 2021. Aidha, vituo vya polisi 391 vilikaguliwa ikilinganishwa na vituo
    vya polisi 180 vilivyokaguliwa katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi,
  16. Zoezi hilo la ukaguzi wa maeneo ya vizuizi umewezesha kupunguza
    mlundikano wa Mahabusi kwa kuwaachia huru jumla ya Mahabusi 809.
    Kwa upande wa Zanzibar vyuo vya mafunzo tisa (9) na vituo vya polisi 17
    vilikaguliwa katika mikoa yote ya Zanzibar. Orodha ya vituo vya Polisi na
    Magereza vilivyokaguliwa na idadi ya Mahabusi walioachiwa huru kwa kila
    Mkoa imeoneshwa katika Kiambatisho A.
  17. Mheshimiwa Spika, Matokeo ya ukaguzi yalionesha kuwa hali ya
    magereza na vyuo vya mafunzo inaendelea kuboreshwa kwa kuzingatia
    vigezo vya haki za binadamu ikilinganishwa na kaguzi zilizopita. Maeneo
    yaliyoboreshwa ni pamoja na haki ya kupata chakula, malazi, afya na haki
    ya kupata habari. Aidha, kutokana na mapendekezo ya taarifa ya tathmini
    jitihada zinaendelea kufanyika ili kuboresha hali ya uzingatiwaji wa haki za
    9
    binadamu katika maeneo hayo.
    II. Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki
    (a) Usikilizwaji wa Mashauri
  18. Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu suala la kupunguza
    mlundikano wa mashauri mahakamani limekuwa ni moja ya vipaumbele
    muhimu vya Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata
    haki sawa na kwa wakati. Kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Julai 2021-
    Machi, 2022 kulikuwa na Jumla ya mashauri 241,793. Kati ya mashauri
    hayo mashauri 178,877 (sawa na asilimia 74) yalisikilizwa na kuhitimishwa.
    Mahakama inendelea na mipango ya kuboresha matumizi ya TEHAMA ili
    kuongeza kasi ya kuhitimisha usikilizwaji wa mashauri.
    (b) Kuboresha Miundombinu ya Utoaji Haki
  19. Mheshimiwa Spika, Mahakama imeendelea na utekelezaji wa
    Mpango wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26) wa Ujenzi na Ukarabati wa
    Miundombinu ya Mahakama, ambapo katika mwaka 2021/2022 miradi 37
    ilitekelezwa katika ngazi mbalimbali za Mahakama. Hadi kufikia Machi,
    2022 miradi imefikia katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama ifuatavyo:
    i. Miradi iliyokamilika; Ujenzi wa vituo Jumuishi sita (6) vya kutoa haki
    (IJCs) katika mikoa ya Dar es salaam (Kinondoni na Temeke),
    Dodoma, Morogoro, Mwanza na Arusha; Ujenzi wa Mahakama za
    Hakimu Mkazi mbili (2) katika Mikoa ya Katavi na Lindi; ujenzi wa
    Mahakama za Wilaya nne (4) katika wilaya za Bahi, Chemba, Rungwe
    na Bunda; ujenzi wa Mahakama za mwanzo tatu (3) za Matiri
    (Mbinga), Hydom (Mbulu), na Kibaigwa (Kongwa) na ujenzi wa Jengo
    10
    la Kuhifadhia Kumbukumbu – Tanga.
    ii. Miradi inayoendelea; ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama
    Dodoma ambapo ujenzi wa boma (structure) umekamilika kwa asilimia
    100; Ukarabati na upanuzi wa Mahakama Kuu Tabora; ujenzi wa
    Mahakama za Hakimu Mkazi katika Mikoa ya Songwe na Tabora;
    Ujenzi wa Mahakama za Wilaya za Nanyumbu, Namtumbo, Same,
    Tandahimba, Kilindi, Sikonge, Mwanga, Kakonko, Buhigwe, Uvinza,
    Butiama, Rorya, Itilima, Busega, Songwe, Mbogwe, Nyang’wale,
    Kyerwa, Misenyi, Gairo, Mvomero, Kilombero, Mkinga, Tanganyika na
    Kaliua. Miradi mingine inayoendelea ni ujenzi wa Mahakama za
    mwanzo Mang’ula na Mlimba (Morogoro), Nyakibimbili (Bukoba),
    Kabanga (Ngara), Chanika (DSM), na Kimbe (Kilindi); na Ujenzi wa
    bweni la wavulana katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama – Lushoto.
  20. Mheshimiwa Spika, Mahakama imeendelea kuanzisha na
    kuboresha mifumo ya utoaji haki kwa kutumia TEHAMA. Hadi kufikia Machi
    2022, Mahakama imeanzisha mfumo wa ‘SEMA NA MAHAKAMA’ wenye
    lengo la kupata mrejesho wa huduma zitolewazo, malalamiko na
    mapendekezo. Aidha, Mfumo wa Madalali wa Mahakama umeanzishwa
    wenye lengo la kuwasajili, kuwasimamia na kuwatambua. Vilevile,
    Mahakama imefanya maboresho mbalimbali katika mifumo ifuatayo:
    Mfumo wa kielektroniki wa usimamizi na uendeshaji wa mashauri (Judicial
    Statistical Dashboard System – JSDS II); Mfumo wa Mkutano Mtandao
    (Video Conferencing) unaowezesha kuendesha mashauri kwa njia ya
    mtandao; Mfumo wa kielektroniki wa kusajili na kuwatambua mawakili (eWakili); Mfumo wa kutambua Viwanja na Majengo ya Mahakama (JMap)
    wenye lengo la kutambua hali halisi ya majengo na viwanja vya mahakama
    11
    ili kuwezesha uandaaji wa mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya
    mahakama nchi nzima; na Mfumo wa kuratibu na kuhifadhi taarifa za mali
    na vitendea kazi Mahakamani.
    III. Uandishi, Urekebu na Ufasiri wa Sheria
  21. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
    Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa sheria za nchi zinakwenda na wakati
    na zinaakisi sera na vipaumbele vya Serikali katika nyanja za kisiasa,
    kiuchumi, kijamii, kiutamaduni, mazingira na teknolojia. Katika kipindi cha
    Julai 2021, hadi Machi, 2022, miswada ya sheria 11 iliandaliwa
    ikilinganishwa na Miswada mitatu (3) iliyoandaliwa katika kipindi cha Julai,
    2020 hadi Machi, 2021 sawa na ongezeko la asilimia 267. Miswada
    iliyoandaliwa ni kama ilivyooneshwa kwenye Kiambatisho Na. B. Aidha,
    Miswada hiyo 11 iliwasilishwa Bungeni na kusomwa kwa mara ya pili na ya
    tatu. Kati ya Miswada hiyo, tisa (9) imesainiwa na Mhe. Rais kuwa sheria
    na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama inavyoonekana kwenye
    Kiambatisho C. Aidha, Sheria Ndogo 542 ziliandaliwa na kuchapishwa
    katika Gazeti la Serikali au kutumika kama ilivyokusudiwa ikilinganishwa na
    sheria ndogo 807 zilizoandaliwa katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi,
    2022 sawa na upungufu wa asilimia 33. Upungufu huo ulitokana na
    kupungua kwa maombi yaliyopokelewa ya kuandaa Sheria ndogo.
  22. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Wadau imeendelea
    na zoezi la kutafsiri sheria kutoka Lugha ya Kingereza kwenda Lugha ya
    Kiswahili. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 kupitia zoezi hili
    jumla ya Sheria Kuu 214 zilitafsiriwa kwa hatua ya rasimu ya kwanza.
    Sheria kuu zilizofanyiwa ufasiri zimeoneshwa kwenye Kiambatisho Na. D.
    Ongezeko hili limetokana na kutekeleza maagizo ya Serikali kuwa
    12
    Mahakama zote nchini ziendeshe mashauri na kutoa hukumu katika lugha
    ya Kiswahili. Aidha, katika kipindi hicho, Wizara kupitia Ofisi ya
    Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilifanya urekebu wa Sheria Kuu 46 kama
    inavyoonekana kwenye Kiambatisho E.
    IV. Usimamizi wa Masuala ya Mikataba
  23. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
    Serikali, imeendelea kushiriki na kutoa ushauri wa kisheria katika
    majadiliano mbalimbali ya Mikataba ya kibishara, mikutano ya kitaifa,
    kikanda na kimataifa. Katika kipindi cha Julai, 2021, hadi Machi, 2022 jumla
    ya Mikataba 1,171 ilifanyiwa upekuzi ikilinganishwa na Mikataba 713 katika
    kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 sawa na ongezeko la asilimia 64.
    Ongezo hili linatokana na ongezeko la miradi inayotekelezwa na Serikali.
    Mikataba hiyo ilihusisha masuala ya ununuzi, ujenzi na ukarabati wa
    majengo, utoaji wa huduma za jamii kama vile ujenzi wa shule, hospitali na
    barabara. Kati ya mikataba hiyo 1,171 mikataba 511 ilithaminishwa katika
    sarafu mbalimbali katika mchanganuo ufuatao: Mikataba 407 ilikuwa na
    thamani ya Shilingi Trilioni 116.69; Mikataba 88 ilikuwa na thamani ya
    Dola za Marekani 3,254,993,763.98 sawa na Shilingi Trilioni 7.44; na
    Mikataba 16 ilikuwa na thamani ya fedha ya Jumuiya ya Ulaya (Euro)
    360,569,062.16 sawa na Shilingi Trilioni 0.92.
    V. Utoaji wa Ushauri wa Kisheria
  24. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
    Serikali ina jukumu la kutoa ushauri wa kisheria kwa Wizara, Idara
    zinazojitegemea, Mashirika ya Umma, Tawala za Mikoa na Serikali za
    Mitaa na kwa wananchi. Lengo ni kuhakikisha ushauri unaotolewa
    unazingatia maslahi ya umma na kusaidia Serikali kutoingia kwenye
    13
    migogoro kwa kuhakikisha sheria, kanuni na taratibu za nchi zinafuatwa.
    Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 jumla ya maombi ya
    ushauri wa kisheria 1,129 yalipokelewa na kufanyiwa kazi ikilinganishwa na
    maombi 768 katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 sawa na
    ongezeko la asilimia 47. Kati ya maombi 1,129, maombi 472 yalihusu
    maombi ya wananchi 657 yanatoka katika Wizara, Idara zinazojitegemea,
    Mashirika ya Umma, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa. Kuongezeka kwa
    maombi ya watu binafsi kunatokana na mwamko wa wananchi wanaoupata
    katika maadhimisho mbalimbali ikiwemo Wiki ya Sheria, Wiki ya Msaada
    wa Kisheria pamoja na makongamano mengine ya kisheria.
  25. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
    Serikali ilishiriki katika mikutano 402 ya ndani ya nchi ikilinganishwa na
    mikutano 149 katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 sawa na
    ongezeko la asilimia 170. Aidha, Ofisi ilishiriki katika mikutano 57
    inayohusu masuala ya Kikanda na Kimataifa ikiwemo mikutano ya Jumuiya
    ya Maendeleo ya Nchi zilizopo Kusini mwa Afrika (SADC), Jumuiya ya
    Afrika Mashariki (EAC) na Umoja wa Mataifa (UN).
    VI. Kuendesha Mashtaka ya Jinai
  26. Mheshimiwa Spika, Katika kulinda misingi ya utawala wa sheria
    ambayo ni nguzo muhimu ya kudumisha amani, utulivu na umoja wa
    kitaifa, Wizara kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka iliendelea kuratibu
    shughuli za upelelezi wa makosa ya jinai, kufungua na kuendesha
    mashauri ya jinai mahakamani. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi,
    2022 Wizara kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka iliendesha mashauri ya jinai
    katika Mahakama za Wilaya, Hakimu Mkazi, Mahakama Kuu na
    Mahakama ya Rufani ambapo Jumla ya mashauri ya jinai 42,138
    14
    yaliendeshwa ikilinganishwa na mashauri 26,993 yaliyoendeshwa katika
    kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021. Katika kipindi hiki, mashauri
    11,676 sawa na asilimia 28 yalihitimishwa ikilinganishwa na mashauri
    12,745 sawa na asilimia 47 ya mashauri yaliyohitimishwa katika kipindi cha
    Julai, 2020 hadi Machi, 2021. Kati ya mashauri yaliyohitimishwa, 7,117
    yalihitimishwa kwa washtakiwa kutiwa hatiani sawa na asilimia 61
    ikilinganishwa na mashauri 6,558 sawa na asilimia 52 zilizohitimishwa kwa
    kipindi cha kuanzia Julai, 2020 hadi Machi, 2021 na mashauri 30,462 sawa
    na asilimia 72 ya mashauri yaliyoendeshwa, yalikuwa yanaendelea
    mahakamani katika hatua mbalimbali ikilinganishwa na mashauri 14,248
    sawa na asilimia 53 ya mashauri yaliyoendeshwa, yaliyokuwa
    yanaendelea katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021. Katika kipindi
    cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Ofisi iliendesha jumla ya mashauri 871
    katika Mahakama za watoto (Juvenile Courts) ambapo mashauri 315
    yalihitimishwa na mashauri 556 yapo katika hatua mbalimbali mahakamani.
  27. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka pia
    imeendelea kushughulikia masuala ya rushwa kwa kushirikiana na Taasisi
    ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU). Katika kipindi husika
    Ofisi ilifanya kikao na vyombo vya upelelezi ambavyo ni TAKUKURU na
    Jeshi la Polisi ambapo majalada 28 ya mashauri za rushwa yalifanyiwa
    mapitio na majalada 14 yaliandaliwa Hati za Mashtaka, majalada sita (6)
    yalirudishwa kwa ajili ya upelelezi zaidi katika maeneo yaliyobainika kuwa
    na mapungufu, jalada moja (1) lilifungwa kwa kukosa ushahidi na majalada
    mengine saba (7) yanaendelea kufanyiwa kazi. Washtakiwa waliotiwa
    hatiani walipewa adhabu mbalimbali zikiwemo vifungo, faini na mali
    mbalimbali zilitaifishwa. Kiasi cha Shilingi 1,262,893,030.09 kililipwa
    15
    mahakamani kama faini katika mashauri 3,895 ikilinganishwa na Shilingi
    1,025,498,746.00 zilizolipwa kwenye mashauri 4,211 katika kipindi cha
    Julai, 2020 hadi Machi, 2021. Aidha, mali mbalimbali zilitaifishwa na
    Serikali ikiwa ni pamoja na fedha taslim kiasi cha Shilingi 321,068,400,
    Dola za Marekani 5,000, nyumba tatu (3), matrekta 24, magari 11, pikipiki
    tano (5), ng’ombe 25, sukari kilo 238, madini aina ya Almasi Karati 11 na
    vitendea kazi mbalimbali.
  28. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka
    imeendelea kutekeleza Progamu ya kutenganisha shughuli za upelelezi na
    uendeshaji mashtaka kwa kusogeza huduma za mashtaka karibu na
    wananchi katika ngazi za Mikoa na Wilaya. Katika kipindi cha Julai, 2021
    hadi Machi, 2022 Ofisi za Mikoa Mitatu (3) ya kimashtaka ya Kinondoni,
    Temeke na Ilala (Kinyerezi) zilifunguliwa. Vilevile uzinduzi wa jengo la Ofisi
    la Wilaya ya Serengeti mkoa wa Mara na hivyo kufanya jumla ya Ofisi za
    Mikoa ya kimashtaka kuwa 29 na Ofisi za Wilaya zilizofunguliwa kuwa 14.
    VII. Kushughulikia Uendeshaji wa Mashauri ya Madai na Usuluhishi
  29. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali
    imeendelea kuiwakilisha Serikali na Taasisi zake kwenye mashauri ya
    Madai na Usuluhishi yaliyofunguliwa na au dhidi ya Serikali kwenye
    Mahakama na Mabaraza mbalimbali ya usuluhishi ndani na nje ya nchi.
    Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Machi, 2022 Wizara kupitia Ofisi ya
    Wakili Mkuu wa Serikali iliendesha mashauri 701 ambapo mashauri ya
    madai 590 na mashauri ya usuluhishi 111 ikilinganishwa na Mashauri 543
    yaliyoendeshwa katika kipindi cha kuanzia Julai 2020 hadi kufikia Machi
    2021 sawa na ongezeko la asilimia 29. Kati ya mashauri 701
    yaliyoendeshwa, mashauri 247 yalihitimishwa ambapo Serikali ilishinda
    16
    mashauri 221 na kuokoa Shilingi Bilioni 236.6.
    VIII. Kuratibu Masuala ya Haki za Binadamu na Utoaji wa huduma ya
    msaada wa kisheria
    (a) Kuratibu Masuala ya Haki za Binadamu na Haki za Watu
  30. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuratibu masuala ya kisera
    yanayohusu, kukuza, kulinda na kuhifadhi misingi ya haki za binadamu.
    Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Wizara iliwasilisha Taarifa
    ya nchi chini ya Mfumo wa Mapitio katika kipindi Maalum ambapo kila nchi
    mwanachama anafanyiwa tathmini ya hali ya haki za binadamu kila baada
    ya miaka minne. Taarifa ya Nchi ilijadiliwa katika Kikao cha Baraza la Haki
    za Binadamu la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Geneva, Novemba, 2021.
    Katika kikao hicho Wizara ilitoa taarifa kuhusu jitihada za Serikali katika
    kukuza, kuheshimu na kulinda haki za kisiasa, kiraia, kiuchumi,
    kiutamaduni na kijamii kama ifuatavyo: –
    i. Kuhusu Haki ya Kisiasa, taarifa ilibainisha kuwa uchaguzi mkuu wa
    Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2020 ulifanyika kwa amani na
    utulivu,
    ii. Kuhusu haki za kiraia Serikali ilieleza kwamba ilifanya majadiliano na
    vyombo vya Habari ili kuimarisha haki ya uhuru wa kujieleza kwa
    kuboresha kanuni za Maudhui ya Mawasiliano ya Kielektroniki na
    Posta, 2020.
    iii. Kwa upande haki za kiuchumi, Serikali ilibainisha hatua ambazo
    zimechukuliwa kuboresha ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Hatua
    hizo ni pamoja na kuanzisha mfumo wa malipo kwa kielektroniki wa
    Ankara za malipo ya kodi za ardhi na kuharakisha usuluhishi wa
    17
    migogoro ya ardhi. Hatua nyingine iliyobainishwa ni Serikali kuboresha
    upatikanaji wa maji vijijini kutoka asilimia 47 mwaka 2015 hadi
    asilimia 70.1 mwaka 2020 kwa vijijini na kwa mijini kutoka asilimia 74
    mwaka 2015 hadi asilimia 84 mwaka 2020.
    iv. Kwa upande wa haki za kijamii Serikali ilianzisha mfumo wa kuwalea
    Watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika mikoa minne
    ambayo ni Mwanza, Dar es Salaam, Arusha na Iringa.
  31. Mheshimiwa Spika, Katika majadiliano hayo Serikali ilipokea
    mapendekezo 252 kutoka nchi wanachama yenye malengo ya kukuza na
    kulinda haki za binadamu na haki za watu. Aidha, Wizara iliratibu
    upatikanaji wa maoni juu ya mapendekezo hayo na kuwasilisha msimamo
    wa Serikali kutekeleza mapendekezo 187 kati ya mapendekezo
    yalipokelewa kwenye kikao cha Baraza la Haki za Binadamu mwezi Machi,
  32. Mapendekezo hayo yatakayotekelezwa yanahusu masuala ya Haki
    za binadamu, sera, sheria, kanuni, mikakati na mipango ya maendeleo ya
    nchi, mila, desturi na utamaduni wa watanzania. Hivyo, Serikali iliweza
    kutimiza wajibu wake kama nchi mwanachama wa umoja wa mataifa
    kwenye Baraza la Haki za Binadamu pamoja na kuahidi kutekeleza
    mapendekezo ambayo yamelenga kukuza na kulinda haki za kisiasa,
    kiraia, kiuchumi, kiutamaduni na kijamii kwa maendeleo ya watanzania.
  33. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma
    kuhusu hatua za kulinda na kuhifadhi haki za binadamu, Wizara katika
    kuadhimisha Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania bara ilishirikiana na Asasi za
    Kiraia kuandaa Kongamano la Haki za Binadamu na Miaka 60 ya Uhuru.
    Lengo la Kongamano hilo lilikuwa ni kujadili mafanikio ya Serikali katika
    kukuza na kulinda haki za binadamu tangu tulipopata uhuru miaka 60
    18
    iliyopita. Katika kongamano hilo Wizara na wadau walieleza mafanikio ya
    sekta kuhusu haki za binadamu ambayo ni pamoja na kuanzishwa kwa
    Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inayosimamia masuala ya
    haki za binadamu, Kuanzisha Idara mahususi inayoshughulikia masuala ya
    kisera kuhusu Haki za Binadamu kwenye muundo wa Wizara ya Katiba na
    Sheria.
    (b)Elimu kwa Umma
  34. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Haki za Binadamu na
    Utawala Bora ilitoa mafunzo kuhusu ukatili wa kijinsia kwa Madiwani na
    Masheha 243 (wanaume 145, wanawake 88) katika Mikoa mitatu (3) ya
    Tanzania bara ambayo ni Tabora, Iringa na Dodoma na Mikoa mitatu (3) ya
    Zanzibar ambayo ni Kaskazini Unguja, Kusini Unguja na Kaskazini Pemba.
    Mafunzo hayo yaliwajengea uwezo wa namna ya kutatua kero za wananchi
    kwa kuzingatia haki za binadamu na utawala bora. Vilevile, katika mikoa
    miwili ya Zanzibar, mafunzo yalifanyika kwa wananchi katika Wilaya nne
    (4) ambazo ni Magharibi A, Magharibi B, Wete na Chakechake ambapo
    jumla ya washiriki 509 (231 Unguja na 278 Pemba) walipata mafunzo hayo.
  35. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Haki za Binadamu na
    Utawala Bora imeandaa na kurusha hewani vipindi kumi na tano (15) vya
    Radio na vipindi sita (6) vya runinga kuhusu Haki za Binadamu na Utawala
    Bora na majukumu ya Tume. Katika hatua nyingine, Tume ilitumia njia
    mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii kama facebook, twitter na
    instagram kuhamasisha jamii katika kukabiliana na vitendo vya udhalilishaji
    dhidi ya wanawake na watoto.
    19
    (c) Kushughulikia Malalamiko ya Uvunjifu wa Haki za Binadamu na
    Utawala Bora.
  36. Mheshimiwa Spika, Katika kusimamia hifadhi ya Haki za Binadamu
    na ukiukwaji wa misingi ya Utawala Bora nchini, katika kipindi cha kuanzia
    Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Tume ilifanya ufuatiliaji wa Malalamiko 569
    katika Halmashauri za Wilaya 53 zilizopo katika Mikoa 20 ya Tanzania
    Bara ambayo ni Arusha, Dodoma, Dar es salaam, Geita, Iringa, Kagera,
    Kigoma, Kilimanjaro, Lindi, Mara, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza,
    Ruvuma, Singida, Songwe, Tabora na Tanga na mikoa mitano (5) ya
    Zanzibar ambayo ni Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja
    Kaskazini Pemba na Kusini Pemba. Katika Malalamiko 569 yaliyofuatiliwa,
    Malalamiko 337 yalihusu uvunjifu wa Haki za Binadamu na Malalamiko 232
    yalihusu ukiukwaji wa misingi ya Utawala Bora. Katika ufuatiliaji huo,
    Malalamiko 253 sawa na asilimia 45 ya Malalamiko yaliyofuatiliwa
    yalifanyiwa kazi.
  37. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Haki za Binadamu na
    Utawala Bora ilifanya chunguzi maalumu 16 katika maeneo yaliyohusu
    migogoro ya ardhi, madai ya fidia na matibabu, matumizi mabaya ya
    madaraka, kuchukua sheria mkononi na uharibifu wa mazingira. Chunguzi
    zilifanyika katika Mikoa 11 ya Tanzania Bara ambayo ni Dodoma, Manyara,
    Kigoma, Njombe, Kilimanjaro, Morogoro, Tabora, Shinyanga, Tanga, Dar
    es salaam, Mtwara na Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar. Kupitia chunguzi
    hizi Tume imesaidia wananchi kutatua kero zinazowakabili na kuzishauri
    mamlaka za Serikali namna ya kuzingatia masuala ya haki za binadamu na
    misingi ya utawala bora.
    20
    (d)Kuimarisha Utoaji wa Huduma za Msaada wa Kisheria
  38. Mheshimiwa Spika, Wizara inatekeleza jukumu la kuimarisha
    usimamizi na uratibu wa huduma ya msaada wa kisheria nchini. Katika
    kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Wizara imesajili Watoa huduma ya
    msaada wa kisheria 15 na wasaidizi wa kisheria 56 kwa ajili ya kutoa
    huduma ya msaada wa kisheria kwa wananchi. Idadi hii inafanya jumla ya
    Watoa huduma ya msaada wa kisheria waliosajiliwa kufikia 202 na
    Wasaidizi wa Kisheria 763. Aidha, katika kipindi husika jumla ya wananchi
    1,455,566 (wanawake 529,079, wanaume 514,051 na watoto 412,436)
    walipatiwa msaada wa kisheria. Hii ni ongezeko la wanufaika 1,133,124.00
    sawa na asilima 351 ikilinganishwa na idadi ya wananchi 322,442
    waliopatiwa huduma ya msaada wa kisheria katika kipindi cha Julai, 2020
    hadi Machi, 2021.
  39. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai 2021 hadi Machi, 2022
    Wizara kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania ilianzisha madawati ya
    msaada wa kisheria katika vituo jumuishi vya utoaji haki sita (6) katika
    Mikoa ya Dar es salaam (Kinondoni na Temeke), Arusha, Dodoma,
    Morogoro na Mwanza. Lengo la kuanzisha madawati hayo ni kurahisisha
    upatikanaji wa huduma ya msaada wa kisheria mahakamani kwa wananchi
    wenye uhitaji. Pamoja na kuanzisha madawati hayo, Wizara iliwapatia
    mafunzo wanasheria na mawakili wanaotoa huduma ya msaada wa
    kisheria katika vituo jumuishi vya utoaji haki. Aidha, Wizara iliwajengea
    uwezo Watumishi wa Mahakama wakiwemo Maafisa Utumishi na Watunza
    Kumbukumbu katika vituo jumuishi vya utoaji haki ili kurahisisha utoaji wa
    huduma ya msaada wa kisheria.
    21
  40. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi hicho, Wizara iliwezesha
    kufanyika kwa vikao viwili (2) vya Bodi ya Taifa ya Ushauri wa Msaada wa
    Kisheria ambapo bodi ilipendekeza kuimarisha uratibu wa msaada wa
    kisheria ambapo pendekezo hili lilifanyiwa kazi na Wizara imefanikiwa
    kupata kibali cha kuanzisha Kitengo cha Msaada wa Kisheria katika mwaka
    wa fedha 2021/2022. Aidha, mapendekezo mengine yaliyotolewa na bodi
    yanaendelea kufanyiwa kazi.
  41. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha huduma za msaada wa
    kisheria, Wizara iliwezesha Wasajili Wasaidizi kukagua utendaji wa Watoa
    huduma za msaada wa kisheria katika mikoa 26 Tanzania Bara, lengo ni
    kuhakiki ubora wa utendaji wa watoa huduma hao. Zoezi hili limewezesha
    kutambua watoa huduma ya msaada wa kisheria waliopo katika kila
    Halmashauri na utendaji kazi wake ikiwemo kutoa huduma kwa kuzingatia
    matakwa ya sheria.
    IX. Kuratibu shughuli za Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu,
    Ufilisi na Udhamini;
  42. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022,
    Wizara kupitia Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu iliimarisha shughuli za usajili wa
    vizazi, vifo, ndoa, talaka na watoto wa kuasili ikiwa ni haki ya msingi ya
    utambuzi na upatikanaji wa takwimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Ofisi
    ilitekeleza Mpango Wa Usajili wa Watoto wa Umri Chini ya Miaka Mitano
    katika Mikoa ya Mwanza, Rukwa na Katavi pamoja na Mpango wa Usajili
    wa Watoto wenye Umri wa Miaka 5 Hadi 17 walio Shuleni katika wilaya za
    Mlele, Arumeru, Kahama, Arusha na Misungwi. Hadi kufikia Machi, 2022
    jumla ya vizazi 1,173,752 vilisajiliwa.
    22
  43. Mheshimiwa Spika, maboresho ya Mfumo wa Usajili wa Matukio ya
    Vifo yenye lengo la kuhakikisha kila tukio la kifo linasajiliwa mara tu
    linapotokea, kumpunguzia mwananchi gharama za kupata huduma hiyo
    pamoja na kupata takwimu za sababu za vifo ili kuweka afua katika
    huduma za afya, yalifanyika katika Mkoa wa Songwe katika ngazi ya Vituo
    vya Afya na Ofisi za Kata. Hadi kufikia Machi, 2022 vituo vya usajili
    vimeongekeza kutoka vituo vinne (4) ambavyo ni wilaya hadi kufikia vituo
    130 ambavyo ni Ofisi za Kata 93 na Vituo vya Afya 37 katika Mkoa huo.
    Jitihada hizo zimewezesha kusajili jumla ya vifo 25,743 katika kipindi cha
    Julai, 2021 hadi Machi, 2022.
  44. Mheshimiwa Spika, Katika cha kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi,
    2022,Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu ilisajili ndoa 26,303 na talaka 303. Katika
    jitihada za kuboresha usajili wa matukio hayo, Mfumo wa Usajili wa Ndoa
    na Talaka kielektroniki umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha usajili na
    upatikanaji wa taarifa hizo nchini. Aidha, mfumo huo umeunganishwa na
    mfumo wa kielektroniki wa Mashauri wa Mahakama ili kurahisisha
    upatikanaji na uhakiki wa amri za mahakama kuhusu mashauri
    yanayohusu talaka. Sambamba na maboresho hayo ya kimfumo, mafunzo
    kuhusu ufungishaji ndoa yalitolewa kwa Viongozi wa Dini na Serikali katika
    Mikoa ya Pwani, Kilimanjaro, Iringa, Rukwa na Katavi.
  45. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    hati za kuasili watoto 24 zilisajiliwa pamoja na wosia 127 zilitayarishwa na
    kuhifadhiwa. Elimu kuhusu uandikaji na uhifadhi wa wosia ilitolewa Mkoani
    Dar es Salaam, Kilimanjaro, Rukwa na Katavi kwa Viongozi wa dini na
    Serikali. Aidha, elimu ilitolewa kwa wananchi katika maadhimisho ya Wiki
    ya Wajane mkoani Kagera na Dar es Salaam; na Mkoani Mbeya katika
    23
    maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria.
  46. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu
    katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 imesajili Bodi za Wadhamini
  47. Ili kuboresha huduma na upatikanaji wa taarifa za Bodi za Wadhamini,
    Ofisi imeanzisha Mfumo wa kieletroniki wa Usajili wa Bodi za Wadhamini
    ambao unasaidia upatikanaji na uhakiki wa taarifa za Bodi za Wadhamini
    kwa wakati pamoja na utoaji vibali vya umiliki ardhi hivyo kurahisisha utoaji
    huduma na kuongeza maduhuli ya Serikali.
    X. Kuratibu Tathmini na Maboresho ya Sheria
  48. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    Wizara kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria ilihakikisha sheria za nchi
    zinafanyiwa mapitio na maboresho ili ziendane na wakati kwa kuzingatia
    mabadiliko ya maendeleo katika nyanja za kijamii, kiuchumi, kisiasa na
    kiutamaduni. Katika kipindi husika Tume ya Kurekebisha Sheria
    imekamilisha Taarifa kuhusu Mapitio ya Mfumo wa Sheria zinazosimamia
    Masoko ya Mazao ya Kilimo Tanzania ambapo utafiti ulifanyika katika
    Mikoa tisa (9) ya Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Mtwara, Arusha,
    Kilimanjaro, Mwanza, Iringa na Njombe. Lengo la utafiti huo lilikuwa kubaini
    changamoto za mfumo wa masoko ya mazao ya kilimo Tanzania na kutoa
    mapendekezo yatakayohakikisha kunakuwepo mfumo thabiti na endelevu
    wa masoko ya mazao ya kilimo nchini.
  49. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria
    ilifanya Mapitio ya Mfumo wa Sheria unaosimamia Vyama vya Kijamii
    ambapo utafiti ulifanyika katika Mikoa saba (7) ya Dar es Salaam,
    Dodoma, Iringa, Mbeya, Morogoro, Mwanza na Shinyanga. Lengo la utafiti
    24
    huo ni kubaini changamoto za Mfumo wa Sheria unaosimamia vyama vya
    kijamii na kutoa mapendekezo yatakayohakikisha kunakuwepo na mfumo
    thabiti wenye uwazi na uwajibikaji.
  50. Mheshimiwa Spika, Kuhusu tathmini ya utekelezaji wa sheria,
    Wizara kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria ilikamilisha Taarifa nne (04) za
    tathmini ya utekelezaji wa sheria ambazo zinahusu mifumo ya Adhabu
    Mbadala; Sekta ya Utalii, Sekta ya Mifugo na Sekta ya Uvuvi. Kwa upande
    wa Adhabu Mbadala, sheria zilizofanyiwa tathmini ni pamoja na Sheria ya
    Magereza, Sura 58; Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura 20;
    Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumi, Sura 200, Sheria ya Huduma za
    Jamii, Sura 291; Sheria ya Bodi ya Msamaha, Sura ya 400 na Sheria
    Ukomo wa Adhabu, Sura 90. Lengo la tathmini ni kupima endapo malengo
    ya sheria husika yamefikiwa ikiwemo kupunguza msongamano wa
    Wafungwa Magerezani, kupunguza adha ya kupata magonjwa ya
    kuambukiza kwa Wafungwa na kuipunguzia Serikali gharama za
    kuendesha magereza.
  51. Mheshimiwa Spika, Katika Sekta ya Utalii, sheria zilizofanyiwa
    tathmini ni pamoja na Sheria ya Utalii, Sura 65; Sheria ya Wanyamapori,
    Sura 283; Sheria ya Mbuga za Wanyama, Sura 282; Sheria ya
    Makumbusho ya Taifa, Sura 281; Sheria ya Hifadhi ya Eneo la Mamlaka ya
    Ngorogoro, Sura 284; na Sheria ya Malikale, Sura 333. Tathmini katika
    Sekta ya Utalii ililenga kubaini endapo madhumuni yaliyokusudiwa na
    Sheria hizo yamefikiwa katika kuboresha na kukuza vivutio vya utalii,
    kuboresha kipato cha wananchi, kuongeza fedha za kigeni na kuongeza
    pato la Taifa. Aidha, Tume ilifanya tathmini ya utekelezaji wa sheria katika
    Sekta ya Mifugo. Sheria zilizofanyiwa tathmini ni pamoja na Sheria ya
    25
    magonjwa ya Mifugo, Sura 156; Sheria ya Madaktari wa Mifugo, Sura 319;
    Sheria ya Nyama, Sura 421; Sheria ya Maziwa, Sura 262; Sheria ya
    Biashara ya ngozi, Sura 120; Sheria ya Ustawi wa Wanyama, Sura 120;
    Sheria ya Utambulisho, Usajili na Ufuatiliaji wa Wanyama, Sura 184; Sheria
    ya Matumizi ya Ardhi, Sura 116 na Sheria ya Nyanda za Malisho na
    Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Sura 180. Dhumuni la tathmini ya sheria
    zinazosimamia sekta ya mifugo ni kupima endapo malengo yaliyokusudiwa
    katika sheria hizo yamefikiwa katika kuhakikisha ufugaji unakuwa wa
    kibiashara na wenye tija kwa wafugaji na Taifa kwa ujumla.
  52. Mheshimiwa Spika, Kuhusu tathmini ya utekelezaji wa Sheria
    zinazosimamia Sekta ya Uvuvi Tanzania, Sheria zilizofanyiwa tathmini ni
    pamoja na Sheria ya Uvuvi, Sura 279; Sheria ya Usimamizi na Maendeleo
    ya Uvuvi wa Bahari kuu, Sura 388; Sheria ya Hifadhi za Bahari na maeneo
    Tengefu, Sura 146; na Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania,
    Sura 280. Dhumuni la tathmini ya sheria zinazosimamia Sekta ya Uvuvi
    Tanzania ni kupima kufikiwa kwa malengo ya sheria hizo ya kuhakikisha
    kuwa Sekta ya Uvuvi inakuwa ya kibiashara na kuchangia katika ukuaji wa
    uchumi wa buluu wenye kuboresha maisha ya wananchi na kukuza Pato la
    Taifa.
  53. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria
    iilitoa elimu ya sheria kwa umma kupitia vipindi vya radio, runinga,
    vipeperushi, maonesho ya wiki ya sheria, na mikutano mbalimbali. Lengo
    lilikuwa kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu Sheria ya Mtoto; Sheria ya
    Ajira; Sheria ya utatuzi wa Migogoro ya Ardhi; Sheria ya Haki za Walaji na
    nafasi ya Tume katika maboresho ya sheria nchini. Taarifa za tathmini hizo
    zitawasilishwa kwenye mamlaka husika kwa hatua zaidi.
    26
    XI. Kuratibu ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Sheria za Utajiri
    na Maliasilia za nchi
  54. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuimarisha mifumo ya
    ufuatiliaji na tathmini ya shughuli za utajiri asilia na maliasilia za nchi kwa
    kuandaa Mfumo wa Kielektroniki utakaowezesha; kukusanya taarifa
    zinazobainisha sehemu zenye utajiri na Maliasili za Nchi na aina ya
    uwekezaji unaofanyika, kusajili mikataba ya utajiri na Maliasilia za Nchi
    iliyoingiwa na Wizara, Idara na Taasisi kwa niaba ya Serikali na kupata
    taarifa za utekelezaji wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi na Umiliki wa Utajiri
    na Maliasilia za Nchi Sura 449 na Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu
    Mikataba yenye Masharti Hasi Sura 450 kutoka kwa Wizara, Idara na
    Taasisi zinazosimamia utajiri asilia na maliasilia za nchi. Aidha, Wizara
    imeshiriki katika kutoa mafunzo na elimu kwa wadau mbalimbali
    wanaohusika na masuala ya utajiri asilia na maliasilia za nchi kwa Maafisa
    wa Serikali 260 kuhusu Sheria ya Mamlaka ya Nchi na Umiliki wa Utajiri na
    Maliasilia za Nchi Sura 449 na Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu
    Mikataba yenye Masharti Hasi Sura 450 na nafasi ya maafisa wanyamapori
    katika kulinda na kuhifadhi wanyamapori kwa mujibu wa sheria hizo.
    Wizara imesimamia jukumu la kufanya marekebisho ya Kanuni za ushiriki
    wa Serikali katika shughuli za uchimbaji wa madini nchini kwa mujibu wa
    kifungu cha 10 cha Sheria ya Madini, 2010. Wizara imeshiriki katika
    majadiliano na makampuni ya uchimbaji wa madini za Nyanzaga.
  55. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kushiriki kuweka mifumo
    mbalimbali ili kuhakikisha kwamba utajiri na maliasilia za nchi unasaidia
    kuinua uchumi wa nchi na wananchi kwa ujumla. Wizara inashirikiana na
    Wizara mbalimbali kuandaa sera na miongozo mbalimbali ambapo katika
    27
    kipindi husika imeshirikiana na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
    kuandaa Sera ya ushiriki wa wananchi katika miradi ya kimkakati (Local
    Content) pamoja na Sera ya uwekezaji.
    XII. Kuboresha Utendaji na Maendeleo ya Rasilimali Watu iliyo chini ya
    Wizara
  56. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022,
    Wizara imeendelea kusimamia na kuboresha maslahi ya watumishi na
    utendaji kazi katika kutekeleza majukumu yake. Katika kipindi hicho Wizara
    ya Katiba na Sheria iliajiri mtumishi mpya mmoja (1) na watumishi wawili
    (2) walipandishwa vyeo. Aidha, kwa upande wa Taasisi zilizo chini ya
    Wizara, zimeendelea kusimamia maendeleo ya rasilimaliwatu kama
    ifuatavyo: –
    i. Tume ya Utumishi wa Mahakama iliajiri jumla ya watumishi 45 wa
    kada mbalimbali kwa kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    ikilinganishwa na idadi ya ajira ya watumishi 239 wa kada
    mbalimbali kwa kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021. Vilevile,
    vikao vinne (4) vilifanyika kushughulikia masuala mbalimbali
    ikiwemo Uteuzi wa Naibu Wasajili 25 wa Mahakama Kuu ya
    Tanzania kwa ajili ya kuimarisha utendaji wa Mahakama;
    Kushughulikia mashauri 21 ya kinidhamu ambapo Mahakimu saba
    (7) walistaafishwa kwa manufaa ya umma; watumishi watano (5)
    wasio Mahakimu walifukuzwa kazi na Mahakimu tisa (9)
    walirejeshwa kazini. Aidha, mtumishi mmoja (1) wa Sekretarieti ya
    Tume alipandishwa cheo na mtumishi mmoja (1) aliteuliwa kuwa
    Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu;
    28
    ii. Ofisi ya Taifa ya mashtaka iliajiri watumishi wapya wanne (4),
    mtumishi mmoja (1) alithibitishwa kazini na watumishi 19
    walipandishwa vyeo;
    iii. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliajiri watumishi wapya
    wawili (2), watumishi wawili (2) walithibitishwa kazini, mtumishi
    mmoja (1) alipandishwa cheo;
    iv. Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali iliajiri watumishi wapya 23,
    watumishi 8 walithibitishwa cheo na mtumishi mmoja (1)
    alipandishwa cheo;
    v. Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora iliajiri watumishi
    wapya watano (5), watumishi wawili (2) walithibitishwa vyeo na
    watumishi wawili (2) walipata uteuzi kuwa Katibu Mtendaji na
    Naibu Katibu Mtendaji;
    vi. Chuo cha uongozi wa Mahakama Lushoto kiliajiri watumishi wapya
    wawili (2), mtumishi mmoja (1) alithibitishwa cheo na mtumishi
    mmoja (1) alipata uteuzi kuwa Mkuu wa Idara ya Mafunzo ya
    Sheria;
    vii. Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania
    kilipandisha cheo watumishi tisa (9); na
    viii. Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu iliwathibitisha vyeo watumishi sitini na
    saba (67), watumishi watatu (3) walipandishwa vyeo, watumishi
    wawili (2) walisimamishwa kazi na watumishi watatu (3)
    waliteuliwa katika nyadhifa za Kabidhi Wasii Mkuu, Naibu Kabidhi
    Wasii Mkuu na Meneja wa Usajili.
    29
  57. Mheshimiwa Spika, jumla ya watumishi 1,579 kwa Wizara na
    Taasisi zake walipatiwa mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi. Maelezo
    ya kina kuhusu maendeleo ya Rasilimaliwatu yameoneshwa katika
    Kiambatisho F.
    XIII. Kushughulikia urejeshwaji wa wahalifu na masuala ya ushirikiano
    wa kimataifa kwenye makosa ya jinai
  58. Mheshimiwa Spika, Tanzania imeendelea kushirikiana na mataifa
    mengine katika kupambana na kusimamia kurejeshwa kwa watuhumiwa
    wa uhalifu katika nchi walikofanya kosa. Wizara kwa kushirikiana na wadau
    imeandaa mkataba wa urejeshwaji wa Wahalifu na ushirikiano katika
    masuala ya mashauri ya jinai baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
    na Kenya. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Wizara ilipokea
    na kushughulikia maombi matano (5) ya kuwarejesha wahalifu wa makosa
    ya jinai waliokimbilia nchini kutoka katika mataifa ya Zimbabwe (2), Malawi
    (1), Uturuki (1) na Kenya (1). Lengo la kurejesha waharifu hao ni
    kuimarisha ushirikiano wa kisheria na mataifa mengine katika masuala ya
    jinai na kudhibiti watuhumiwa wa uhalifu kukimbilia katika mataifa mengine.
    XIV. Kuratibu shughuli za Taasisi, Mipango na Miradi chini ya Wizara
    (a)Kuimarisha Uendeshaji wa Mafunzo Endelevu na Elekezi ya
    Kimahakama na Kisheria
  59. Mheshimiwa Spika, Katika kuhakikisha watumishi wa Mahakama na
    wa sekta ya sheria wanakuwa na ujuzi na weledi wa kutosha katika
    kutimiza wajibu wao kwa ufanisi, Wizara kupitia Chuo cha Uongozi wa
    Mahakama, Lushoto imeendelea kuratibu na kutoa mafunzo endelevu na
    30
    elekezi ya Kimahakama kwa watumishi wa Mahakama na wadau wa sekta
    ya sheria nchini. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Chuo
    kimeratibu mafunzo yafuatayo;
    (i) Mafunzo endelevu: Wizara kupitia Chuo cha Uongozi wa
    Mahakama Lushoto imeendelea kuwajengea uwezo jumla ya
    wasaidizi wa sheria wa Majaji 84 kwenye eneo la kufanya utafiti wa
    kisheria ili waweze kuwasaidia majaji ipasavyo katika kutoa haki.
    Vilevile, jumla ya Mahakimu 200 walipatiwa mafunzo kuhusu
    uendeshaji wa mashauri ya rushwa na urejeshaji mali zilizopatikana
    kwa njia ya uhalifu na Mahakimu 36 walipatiwa mafunzo kuhusu
    uendeshaji wa mashauri yanayohusu ukatili wa kijinsia, na
    usafirishaji haramu wa binadamu. Chuo kwa kushirikiana na
    Mahakama kimekuwa kikiendesha mafunzo kwa njia ya mtandao
    kwa lengo la kuwafikia watumishi wengi na kutoa fursa ya
    kubadilishana uzoefu. Katika kipindi husika jumla ya Mahakimu 100
    waliokasimiwa mamlaka ya ziada na Jaji Mkuu ya kusikiliza
    mashauri ambayo yanaangukia kwenye mamlaka ya Mahakama
    Kuu ya Tanzania walipatiwa mafunzo endelevu na kupata fursa ya
    kubadilishana uzoefu wa namna mamlaka hayo yanavyotumika
    pamoja na kujadili changamoto na namna ya kuboresha usikilizaji
    wa mashauri. Aidha, Chuo kiliratibu mafunzo kwa njia ya mtandao
    kwa majaji, wasajili na Mahakimu wengine wa ngazi mbalimbali
    wapatao 150 yaliyolenga utekelezaji wa sheria ya wosia na
    usimamizi wa mirathi pamoja na kubadilishana uzoefu.
    (ii)Mafunzo elekezi: Wizara kupitia Chuo cha Uongozi wa Mahakama
    Lushoto iliendelea kutoa mafunzo elekezi kwa Mahakimu wapya 35,
    31
    Manaibu Wasajili wapya 25, Watendaji wa Mahakama wa kanda na
    mikoa wapya 11 pamoja na Wakurugenzi wasaidizi watatu 3,
    mafunzo ya udalali wa mahakama kwa washiriki 30 na wasambazaji
    nyaraka za Mahakama 16. Katika kipindi husika chuo kwa
    kushirikina na Mahakama ya Tanzania kupitia ufadhili wa Shirika la
    UNICEF kiliendesha Mafunzo kwa Wadau wa Haki Mtoto Kanda ya
    Kigoma wapatao 40 waliojumuisha Mahakimu 15 kutoka Mahakama
    Kuu Kanda ya Kigoma, Mahakimu 15 kutoka kanda ya Tabora,
    Maafisa Ustawi wa Jamii watano (5), Waendesha Mashtaka watatu
    (3) kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Waendesha Mashtaka
    wawili (2) kutoka jeshi la Polisi. Mahakimu walioshiriki ni wale
    wenye mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mtoto kutoka Mahakama
    za wilaya na baadhi ya mahakimu wa Mahakama za mwanzo
    kutoka kanda zilizotajwa.
  60. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 mpaka Machi,
    2022, Wizara kupitia Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto imeratibu
    ushiriki wa maafisa mbalimbali kutoka Mahakama ya Tanzania na Chuo
    kwenye vikao na mafunzo yaliyoendeshwa na wadau kama ifuatavyo:-
    (i).Mkutano wa wadau (High Level symposium) wa utoaji haki jinai na
    ulinzi kwa mashahidi, wahanga na washtakiwa ulioendeshwa na
    Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Mahakama ya
    Uingereza kupitia Taasisi ya Majaji Wastaafu iitwayo Slynn
    Foundation chini ya ufadhili wa Programu ya Kitaifa ya Kuzijengea
    Uwezo Taasisi zinazohusika na Kupambana na Rushwa (BSAAT).
    (ii).Mafunzo juu ya Uelewa wa utendaji kazi wa Mahakama ya Haki ya
    Afrika Mashariki, Utawala wa sheria na Utawala bora. Mafunzo haya
    32
    yaliendeshwa na Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki kwa
    kushirikiana na Centre for Public Interest Law na Ford Foundation
    kwa majaji wa mahakama ya Rufani watatu (3), majaji wa
    mahakama kuu watatu (3) na Naibu Wasajili saba (7).
  61. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa masomo 2021/22 Chuo
    kimedahili wanafunzi wapya 870 wa Astashahada na Stashahada ya sheria
    (wanawake 412 na wanaume 458). Kwa upande wa Astashahada ya sheria
    waliodahiliwa ni 492 (wanawake 224 na wanaume 268) na Stashahada ya
    sheria mwaka wa kwanza ni 378 (wanawake 188 na wanaume 190). Aidha,
    wanachuo wanaoendelea na Stashahada mwaka wa pili ni 231 (wanawake
    137 na wanaume 94). Jumla ya wanafunzi wote wa Chuo waliodahiliwa
    katika Astashahada na Stashahada ya sheria kwa mwaka wa masomo
    2021/2022 ni 1,101 (wanawake 549 na wanaume 552) ikilinganishwa na
    udahili wa jumla ya wanafunzi 944 (wanaume 420 na wanawake 524)
    katika mwaka wa masomo 2020/2021 sawa na ongezo la asilimia 17.
  62. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Chuo cha Uongozi wa
    Mahakama Lushoto imeendelea kusimamia haki za mtoto kwa kuandaa na
    kuzindua Kitabu cha Mkusanyiko wa Mashauri ya Watoto na Taarifa ya
    Tathmini ya Mafunzo ya Haki za Watoto kwa wadau wa haki za Watoto
    kwa ajili ya kurahisha rejea kuhusu mwenendo wa mashauri ya watoto.
    (b)Kuimarisha Uendeshaji na Usimamizi wa Utoaji wa Mafunzo ya
    Uanasheria kwa Vitendo
  63. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Taasisi ya Mafunzo ya
    Uanasheria kwa Vitendo Tanzania imeendelea kutekeleza jukumu lake la
    msingi la kutoa mafunzo ya uanasheria kwa vitendo. Katika kipindi cha
    33
    Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Taasisi imedahili jumla ya wanafunzi 1,507
    sawa na ongezeko la asilimia 0.5 ya lengo la udahili wa wanafunzi 1,500.
    Aidha, katika kipindi husika, Taasisi imetunuku vyeti kwa wahitimu 293
    wanaostahili kusajiliwa kuwa mawakili na kufanya idadi ya wahitimu
    waliopata mafunzo kupitia Taasisi hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka
    2007 kufikia 7,561.
    (c) Miradi ya Maendeleo Inayotekelezwa na Wizara
  64. Mheshimiwa Spika, Wizara na Taasisi zake imeendelea kubuni na
    kutekeleza miradi ya maendeleo ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu
    yake. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Wizara na Taasisi
    zake imeendelea kutekeleza miradi ifuatayo:
    i. Mradi wa Kujenga Mfumo Endelevu wa Kupambana na Rushwa.
    Mradi huu una lengo la kupunguza athari za rushwa ambazo ni
    kikwazo cha maendeleo na kupambana na umaskini nchini. Mradi
    huu unatekelezwa na Wizara ya katiba na Sheria, Ofisi ya
    Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mahakama ya Tanzania na Ofisi ya
    Taifa ya Mashtaka. Kazi zilizofanyika katika kipindi hicho ni pamoja
    na kutoa mafunzo kwa Mahakimu Wakazi 200 kuhusu uendeshaji wa
    mashauri ya rushwa na urejeshwaji mali; kuandaa Rasimu ya
    Mwongozo wa Upelelezi na Uendeshaji wa Mashauri ya Rushwa na
    mashauri mengine (Standard Operating Procedures – SOPs);
    kufanya mapitio ya majalada 55 ya mashauri ya rushwa kwa Wakuu
    wa Mashitaka wa Mikoa mitano (5) ya Dar es Salaam, Dodoma,
    Arusha, Mbeya na Mwanza kwa lengo la kuwajengea uwezo kwa
    vitendo na kuimarisha mifumo ya kupambana na rushwa; na kufanya
    34
    ufuatiliaji na tathmini za Programu ya Kujenga Mfumo Endelevu wa
    Kupambana na Rushwa Tanzania.
    ii. Mradi wa Haki Mtandao (e-Justice).
    Mradi huu unalenga kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji
    wa huduma za kisheria na upatikanaji haki. Aidha, mradi huu
    unalenga kuunganisha mifumo ya taasisi za utoaji haki kwa njia za
    kielektroniki ili kuongeza ufanisi, kuharakisha upatinaji wa haki na
    kupunguza gharama za upatikanaji wa huduma hizo. Katika kipindi
    cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 mradi umetekeleza kazi ya usanifu
    wa mfumo wa kielektroniki wa uangalizi na usimamizi wa utajiri wa
    maliasilia za nchi. Mfumo huu utawezesha usajili wa Mikataba
    iliyoingiwa na taasisi za Serikali, utambuzi wa maliasilia zote nchini
    na uwekezaji uliofanyika.
    iii. Mradi wa Kuboresha Uwajibikaji wa Kitaasisi katika kupambana
    na Rushwa na kuongeza Wigo wa Kuifikia Haki.
    Lengo la mradi huu ni kuimarisha mazingira ya wananchi kuifikia haki
    hususan wanawake na watoto pamoja na kuimarisha mapambano
    dhidi ya rushwa. Kazi zilizofanyika katika kipindi cha Julai 2021 hadi
    Machi, 2022 ni pamoja na: Kuwezesha utoaji wa huduma ya Msaada
    wa kisheria ambapo katika maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa
    Kisheria yaliyofanyika nchi nzima jumla ya wananchi 1,455,566
    (wanawake 529,079, wanaume 514,051 na watoto 412,436)
    walipatiwa huduma ya msaada wa kisheria.
    35
    iv. Mradi wa kisekta unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la
    Kuhudumia Watoto.
    Mradi huu unatekeleza Mkakati wa Haki Mtoto wa mwaka 2020/2021
  • 2024/2025 pamoja na kuimarisha usajili wa matukio Muhimu ya
    Binadamu na Takwimu, hususan usajili wa vizazi. Kazi zilizofanyika ni
    pamoja na Kusajili Vizazi kwa jumla ya watoto 573,888 kupitia
    Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri Chini ya Miaka Mitano, katika
    Mikoa ya Mwanza, Rukwa na Katavi na usajili wa vifo 480 katika
    Mkoa wa Songwe.
    v. Mradi wa Uimarishaji wa Upatikanaji Haki za Kisheria Ulinzi wa
    Haki za Binadamu Tanzania.
    Mradi huu unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
    (UNDP). Mradi huu unalenga kuimarisha uwezo wa taasisi za Umma
    na Asasi za Kiraia (AZAKI) katika kulinda na kutetea haki za
    binadamu. Kupitia mradi huu Katika eneo la uchunguzi, Tume ilifanya
    chunguzi maalum tano (5) kuhusu migogoro wa ardhi, matumizi
    mabaya ya madaraka na mazingira mkoani Dodoma, Morogoro,
    Tabora, Shinyanga na Manyara. Uchunguzi wa malalamiko haya
    unaendelea. Kupitia chunguzi hizi, Tume imeweza kusaidia wananchi
    kutatua kero zinazowakabili na kuzishauri mamlaka za Serikali
    namna ya kuzingatia masuala ya utawala bora.
    vi. Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Taasisi zilizokuwa Chini ya Ofisi ya
    Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
    Katika kipindi husika, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
    imekamilisha taratibu za awali za ujenzi wa Ofisi Jumuishi katika
    mkoa wa Mwanza, ambapo mkandarasi ameshapatikana na ujenzi
    unatarajiwa kuanza mwezi Juni 2022.
    36
  1. Mheshimiwa Spika, Mchanganuo wa fedha za Miradi ya Maendeleo
    zilizopitishwa katika mwaka wa fedha 2021/2022 na kupokelewa na Wizara
    na Taasisi katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 umeambatishwa
    kwenye KIAMBATISHO G.
    E. UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA MWAKA
    2020 HADI MWAKA 2025
  2. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza azma ya Serikali
    ya Awamu ya sita ya kuhakikisha kwamba inawajibika ipasavyo kwa
    wananchi kupitia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ahadi na
    maelekezo mbalimbali ya viongozi wa kitaifa. Miongoni mwa ahadi hizo ni
    pamoja na kuendeleza vita dhidi ya rushwa na ubadhirifu wa mali ya
    umma; kukuza, kulinda na kuhifadhi haki za binadamu na kuendeleza
    utawala wa sheria; na kuimarisha mfumo wa utoaji haki. Katika kipindi cha
    Julai 2021 hadi Machi, 2022 Wizara katika utekelezaji wa majukumu yake
    imetekeleza maelekezo mbalimbali ya Ilani ikiwa ni pamoja na yafuatayo:
    I. Kuendeleza Mapambano Dhidi ya Rushwa na Ubadhirifu wa Mali
    ya Umma
  3. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022,
    Wizara imechukua hatua mbalimbali za kuimarisha mapambano dhidi ya
    rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma. Hatua hizo ni pamoja na
    kuimarisha uwezo wa Mahakama ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu
    Uchumi kusikiliza mashauri yanayohusu makosa hayo. Kwa kipindi cha
    Julai 2021- Machi, 2022 kulikuwa na Jumla ya mashauri 46. Kati ya
    mashauri hayo, 21 yalikuwepo mwanzoni mwa Julai 2021 na mashauri
    mapya 25 yalifunguliwa katika mahakama hiyo. Hadi Machi, 2022 mashauri
    37
    20 yamehitimishwa na mashauri 26 yanaendelea kusikilizwa.
    II. Kuchukua Hatua za Kupunguza Mlundikano wa Mashauri
    Mahakamani
  4. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi kufikia Machi,
    2022, Mlundikano wa mashauri umepungua kwa asilimia 26 kutoka
    mashauri 9,399 mwezi Machi 2021 hadi Mashauri 6,994 mwezi Machi,
  5. Hatua zilizochukuliwa ili kupunguza mlundikano wa mashauri ni
    pamoja na kufuta mashauri yasiyokuwa na ushahidi; kutumia mfumo wa
    kumaliza mashauri kwa njia ya makubaliano na majadiliano (plea
    bargaining); kuimarisha mfumo wa ufifishaji wa makosa; kutumia
    mahakama zinazotembea na mikutano mtandao (video conference) katika
    kuendesha mashauri; na kutekeleza mkakati wa kumaliza mashauri ya
    muda mrefu.
    III. Kuhakikisha Huduma Bora za Sheria Zinapatikana Kwa Wakati
    na Gharama Nafuu kwa Kuongeza Wataalam, Miundombinu,
    Vitendea Kazi na Kusogeza Huduma Karibu na Wananchi
  6. Mheshimiwa Spika, Jumla ya Mahakama za Mwanzo tatu (3)
    zilikamilika katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    ambazo ni za matiri (Mbinga), Hydom (Mbulu) na Kibaigwa (Kongwa).
    Vilevile, mahakama inaendelea na ujenzi wa mahakama za mwanzo katika
    maeneo ya Mlimba na Mang’ula (Morogoro) Chanika (Dar es Salaam),
    Kabanga (Ngara), Nyakibimbiri (Bukoba) na Kimbe (Kilindi). Mahakama
    inaendelea na Mpango wa ujenzi wa Mahakama za Mwanzo 60 katika Kata
    ambazo zipo Makao Makuu ya Tarafa ili kusogeza huduma ya utoaji haki
    karibu na Wananchi.
    38
    IV. Kuimarisha Mfumo wa Wasajili Wasaidizi Katika Halmashauri
    zote Ili Kuwezesha Uratibu na Utoaji wa Msaada wa Kisheria Kwa
    Wananchi, Ikiwemo Msaada Wa Huduma za Kisheria Katika
    Masuala ya Mirathi na Ndoa.
  7. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    Wizara imezindua Kamati za Uratibu wa Wadau wa Msaada wa Kisheria
    katika mikoa ya Katavi, Mtwara, Dar es Salaam, Mara, Mbeya, Ruvuma,
    Lindi, Manyara, Mwanza na Mbeya na hivyo kufanya jumla ya mikoa 18
    kuwa na kamati za uratibu wa masuala ya huduma za msaada wa kisheria.
    Kamati hizi zinarahisisha upatikanaji wa watoa huduma kwani wadau wote
    wa msaada wa kisheria wanakutana na hivyo kuimarisha ushirikiano katia
    kutekleza majukumu yao.
    V. Kuimarisha Matumizi ya Lugha ya Kiswahili Katika Kutoa
    Huduma za Kimahakama na Kwenye Uandishi wa Nyaraka za
    Kisheria
  8. Mheshimiwa Spika, Idadi ya Sheria kuu zilizokamilika kutafsiriwa
    kutoka lugha ya Kiingereza kuwa Kiswahili hadi kufikia Machi, 2022 ni 212
    ambazo zilitafsiriwa kupata Rasimu ya Kwanza. Aidha, kupitia wasaidizi wa
    kisheria na watoa huduma za msaada wa kisheria, elimu kwa jamii kwa
    lugha ya Kiswahili na lugha za maeneo mahsusi imeendelea kutolewa kwa
    lengo la kujenga uelewa zaidi kwa jamii katika masuala mbalimbali ya
    kisheria. Lengo ni kuwezesha wananchi kusimamia na kulinda haki zao
    kwa kufahamu sheria.
    39
    VI. Kujenga Mifumo ya TEHAMA ya Kuendelea Kuhimiza Matumizi
    yake Katika Utoaji Haki
  9. Mheshimiwa Spika, Wizara pamoja na taasisi sita (6) ambazo ni
    (Mahakama, Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu), Tume ya Utumishi wa
    Mahakama, Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo, Tume ya Haki
    za Binadamu na Utawala Bora na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali)
    kati ya Taasisi 10 vimeimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji haki
    ikiwemo wananchi kuweza kufungua na kufuatilia malalamiko; kuwasilisha
    maombi ya nyongeza ya muda, usajili wa waendesha maridhiano,
    majadiliano, usuluhishi na upatanishi; kuwezesha kufungua mashauri kwa
    njia ya kielektroniki; kusajili vizazi, vifo na bodi za wadhamini kielektroniki;
    kusajili, kutambua na kusimamia madalali wa Mahakama na kutoa
    mrejesho wa huduma zitolewazo na Mahakama kupitia simu janja.
    F. MWENENDO WA BAJETI NA FEDHA ZILIZOPOKELEWA NA
    WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022
    (i) Makusanyo ya Maduhuli
  10. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022
    Wizara ilipanga kukusanya maduhuli ya jumla ya Shilingi
    12,672,599,000.00 kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato
    ambavyo ni pamoja na; ada za watoa huduma ya utatuzi wa migogoro kwa
    njia ya majadiliano, maridhiano, upatanishi na usuluhishi; ada za watoa
    huduma ya msaada wa kisheria; ada za kusajili mashauri, ada za mawakili
    na faini zinazotokana na mashauri mbalimbali pamoja na pango la ofisi.
    Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Wizara ilikusanya jumla ya
    Shilingi 6,018,450,524.81 sawa na asilimia 47 ya lengo la makusanyo
    40
    yaliyopangwa. Mchanganuo wa maduhuli kwa kila Fungu ni kama
    unavyoonekana kwenye Jedwali Na. 1.
    JEDWALI Na. 1 Mchanganuo wa maduhuli yaliyokusanywa kwa kila
    Fungu kwa kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    Mafungu
    KIASI
    KILICHOIDHINISHWA
    (SH)
    KIASI
    KILICHOKUSANYWA
    JULAI 2021-MACHI 2022
    (SH)
    Fungu 12 – –
    Fungu 16 – –
    Fungu 19 – –
    Fungu 35 56,400,000.00 56,400,000.00
    Fungu 40 12,571,199,000.00 5,921,836,129.00
    Fungu 41 45,000,000.00 40,214,395.81
    Fungu 55 – –
    Fungu 59 – –
    JUMLA 12,672,599,000.00 6,018,450,524.81
    (ii) Bajeti Iliyoidhinishwa
  11. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Wizara ya
    Katiba na Sheria iliidhinishiwa na Bunge jumla ya Shilingi
    231,693,745,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Miradi ya maendeleo.
    Kati ya hizo Shilingi 79,599,030,000 ni kwa ajili ya mishahara ya
    Watumishi, Shilingi 99,178,885,000 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo na
    Shilingi 52,915,830,000 ni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
    Kati ya fedha za Maendeleo jumla ya Shilingi 44,100,000,000 ni fedha za
    ndani na Shilingi 8,815,830,000 fedha za nje.
    41
    (iii) Fedha zilizopokelewa na Wizara na Taasisi
  12. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022
    Wizara ilipokea jumla ya Shilingi 194,115,559,872.30 sawa na asilimia
    84 ya Shilingi 231,693,745,000 zilizoidhinishwa katika mwaka wa fedha
    2021/2022. Kati ya hizo Shilingi 63,868,833,607.27 ni mishahara na
    Shilingi 81,691,778,331.58 ni matumizi mengineyo. Fedha za maendeleo
    zilizopokelewa ni Shilingi 49,616,082,804.44 ambazo zinajumuisha
    Shilingi 22,135,756,234.90 fedha za ndani na Shilingi 27,480,326,569.54
    ni fedha za nje. Ongezeko la fedha za nje zilizopokelewa limetokana na
    Mfuko wa Mahakama kupokea kiasi cha Shilingi 22,901,711,761.54
    ambazo zilitokana na Mkataba wa Benki ya Dunia na Serikali ambapo kiasi
    hicho cha fedha kiliongezeka wakati wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa
    fedha 2021/22. Muhtasari wa mchanganuo wa Bajeti iliyoidhinishwa
    umeoneshwa kwenye Jedwali Na. 2 na kiasi cha fedha zilizopokelewa na
    Wizara na Taasisi hadi Machi, 2022 zimeoneshwa kwenye KIAMBATISHO
    H.
    42
    JEDWALI: Na. 2: Muhtasari wa Bajeti na Fedha zilizopokelewa kwa
    Wizara na Taasis kwa Kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi 2022
    Na. Matumizi Bajeti
    iliyoidhinishwa
    Kiasi
    kilichopokelewa
    Hadi Machi,
    2022
    Asilimia ya
    kiasi
    kilichopokelewa
    hadi kufikia
    Machi, 2022

  13. Mishahara
    ya
    watumishi
    79,599,030,000 63,129,965,237 79%
  14. Matumizi
    mengineyo 99,178,885,000 81,369,511,831 82%

  15. Miradi ya
    Maendeleo
    (Ndani)
    44,100,000,000 22,135,756,235 50%

  16. Miradi ya
    Maendeleo
    (Nje)
    8,815,830,000 27,480,326,570 312%
    JUMLA 231,693,745,000 194,115,559,872 84%
    G. MAFANIKIO YALIYOPATIKANA
  17. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa majukumu ya Wizara katika
    kipindi cha Julai 2021 hadi Machi 2022 ulikuwa na mafanikio yafuatayo:-
    i. Kuimarisha mfumo wa utoaji haki nchini kwa kuanza kutumia
    lugha ya Kiswahili katika uandishi wa sheria na shughuli za utoaji
    haki mahakamani;
    ii. Kuongezeka kwa wigo wa mfumo wa utoaji haki kwa
    kuwawezesha Mawakili kuanza kutoa huduma za uwakili katika
    Mahakama za Mwanzo;
    iii. Kuimarisha mfumo wa utatuzi wa migogoro nje ya mahakama kwa
    43
    kutumia njia mbadala ambazo ni; majadiliano, maridhiano,
    upatanishi na usuluhishi;
    iv. Uteuzi wa Majaji tisa (9) wa Mahakama ya Rufani na Majaji 21 wa
    Mahakama Kuu na kufanya jumla ya idadi ya Majaji wa Mahakama
    ya Rufani kufikia 24 na Majaji wa Mahakama Kuu kufikia 82 na
    Mahakimu 245;
    v. Uteuzi wa Kabidhi Wasii Mkuu na Naibu Kabidhi Wasii Mkuu na
    hivyo kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya
    Kabidhi Wasii Mkuu;
    vi. Kuendelea na matumizi ya lugha ya Kiswahili katika Shughuli za
    mahakama na uandishi wa nyaraka za Kisheria ambao
    umeongeza uelewa wa sheria kwa wananchi na hivyo kurahisisha
    upatikanaji wa haki kwa wakati na kwa gharama nafuu;
    vii. Kuunganishwa kwa Mfumo wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na
    Udhamini na Mahakama ambapo imerahisisha upatikanaji wa
    taarifa za talaka na watoto wa kuasili kwa njia ya mtandao;
    viii. Tanzania kupitia Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu kuwa kinara wa
    Usajili wa matukio muhimu ya binadamu katika ukanda wa Afrika
    kupitia tangazo la Umoja wa Afrika mwaka 2021;
    ix. Kuimarika na kuboreshwa kwa utoaji wa mafunzo ya uanasheria
    kwa vitendo nchini na mafunzo ya uongozi wa mahakama;
    x. Kuendelea kuimarika kwa matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa
    huduma;
    xi. Kuiwakilisha Serikali katika mashauri ya madai na usuluhishi
    kulikowezesha kuokoa kiasi cha Shilingi bilioni 236.6; na
    xii. Kutoa taarifa kwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa na
    Ulimwengu kwa ujumla kuhusu jitihada za Serikali ya Jamhuri ya
    44
    Muungano wa Tanzania katika kukuza, kuheshimu na kulinda haki
    za kisiasa, kiraia, kiuchumi, kiutamaduni na kijamii.
    H. CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA
  18. Mheshimiwa Spika, Pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika
    utekelezaji wa majukumu, Wizara ilikabiliwa na changamoto mbalimbali
    kama ifuatavyo: –
    i. Kukosekana kwa ulinzi na usalama kwa watoa taarifa na
    mashahidi. Hali hii inasababisha watoa taarifa na mashahidi kusita
    au kutokutoa ushirikiano unaohitajika kwa vyombo vya haki jinai
    katika kutoa taarifa za uhalifu kwa kuhofia usalama wao;
    ii. Kuongezeka kwa uhitaji wa Wananchi kuelewa wajibu wao katika
    kudai haki zao za kijamii na kiraia ikilinganishwa na uwezo uliopo;
    iii. Mirathi kuchukua muda mrefu kufungwa kutokana na wanufaika
    kuendeleza migogoro hata baada ya Mahakama kumteua Kabidhi
    Wasii Mkuu kuwa msimamizi wa mirathi;
    iv. Kuwepo kwa migogoro ndani ya Bodi za Wadhamini za Taasisi
    zisizo za Serikali zilizosajiliwa na Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu
    inayotokana na kugombania madaraka, maslahi binafsi na
    ubadhilifu wa mali; na
    v. Kutofungamanishwa kwa mfumo wa utoaji haki kunakoathiri
    upatikanaji wa haki, uendeshaji na usimamizi wa vyombo vingine
    vya utoaji haki.
    45
    I. MIKAKATI YA KUTATUA CHANGAMOTO
  19. Mheshimiwa Spika, ili kutatua changamoto zilizotajwa hapo juu
    Wizara imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na:
    (i) Wizara inaratibu maandalizi ya kanuni za kutekeleza Sheria ya
    Kuwalinda mashahidi na Watoa taarifa za Uhalifu nchini;
    (ii)Kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu katiba na Sheria kupitia
    vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni pamoja kushirikisha Asasi za
    Kiraia ili kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu haki na wajibu wao
    katika kupata haki zao.
    (iii) Kutoa elimu kwa wanufaika kuhusu taratibu za usimamizi na ufungaji
    ili mirathi iweze kufungwa kwa wakati na warithi kupata haki zao.
    (iv)Kuendelea kuhakikisha taasisi zilizosajiliwa zinaweka vipengele
    bayana katika katiba zake vitakavyotoa miongozo ya kuepusha
    migogoro katika Bodi za Wadhamini na kuendelea kutoa elimu
    kuhusu majukumu na wajibu wa Bodi za Wadhamini; na
    (v) Kuendelea kuboresha na kufungamanisha mifumo ya utoaji haki kwa
    vyombo vya utoaji haki nchini.
  20. Mheshimiwa Spika, mafanikio yaliyopatikana ni juhudi za pamoja
    kati ya Wizara, Idara, Taasisi na wadau wa Sekta ya Sheria wakiwemo
    washirika wa maendeleo. Hivyo, nitumie fursa hii kutoa shukrani zangu za
    dhati kwa ushirikiano mzuri uliopo kati yetu na Washirika wa Maendeleo
    ikiwa ni pamoja na Benki ya Dunia, Shirika la Maendeleo la Umoja wa
    Mataifa (UNDP), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto
    46
    (UNICEF), Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UNWOMEN), Umoja
    wa Ulaya (EU), Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Uingereza (FCDO),
    Mahakama ya Uingereza, Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki. Wadau
    wengine walioshiriki katika kuleta mafanikio ya Wizara ni pamoja na;
    Kampuni ya Simu ya TIGO ambayo imeipatia Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu
    simu janja 1,046 kwa ajili ya usajili wa watoto chini ya umri wa miaka
    mitano (5) katika mikoa mitatu (3) ya Mwanza, Rukwa na Katavi na hivyo
    kufanya jumla ya mikoa iliyopokea simu janja kwa ajili ya shughuli za usajili
    kufikia 22. Ni matumaini yangu kuwa, Kampuni hiyo itaendelea kuipatia
    simu janja mikoa minne (4) iliyobaki ya Tabora, Kigoma, Kagera na Dar es
    Salaam kufanikisha usajili wa watoto. Wizara inatambua na kuthamini
    uhusiano mzuri uliopo kati ya Serikali na wadau hao, na tutahakikisha kuwa
    ushirikiano huo unaimarishwa kwa maendeleo ya sekta ya sheria na taifa
    kwa ujumla.
    J. MPANGO NA BAJETI YA WIZARA NA TAASISI ZAKE KWA
    MWAKA WA FEDHA 2022/2023
  21. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Wizara na
    Taasisi zake itaendelea kuboresha utoaji wa huduma kwa umma ili
    kuendana na Dhima yake. Ili kufikia azma hiyo Wizara na Taasisi zake
    zimeainisha maeneo mahsusi ya kipaumbele na kuyawekea malengo na
    shabaha kwa ajili ya utekelezaji.
    (a) Vipaumbele vya Wizara na Taasisi zake
  22. Mheshimiwa Spika, Maeneo ya vipaumbele muhimu ambavyo
    Wizara na taasisi zake itakavyovitekeleza kwa mwaka wa fedha 2022/2023
    ni ifuatavyo: –
    47
    i. Kuendelea na kuanza kujenga vituo jumuishi vya Taasisi za Sheria
    Nchini;
    ii. Kuendelea na kuanza kujenga majengo ya Makao Makuu ya Wizara na
    taasisi zake katika mji wa Dodoma;
    iii. Kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya kikatiba na
    utawala wa sheria;
    iv. Kuendelea kuhuisha sheria mbalimbali ili kuimarisha uhuru na wajibu wa
    wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo na kukuza demokrasia
    na utawala wa Sheria;
    v. Kuimarisha mifumo ya uangalizi wa matumizi ya utajiri na maliasilia za
    nchi ili kuleta manufaa kwa wananchi na maendeleo ya Taifa kwa
    ujumla;
    vi. Kuendelea kuhamasisha matumizi ya njia mbadala za utatuzi wa
    migogoro ambazo ni usuluhishi, upatanishi, maridhiano na majadiliano ili
    kurahisisha na kuharakisha upatikanaji wa haki nchini;
    vii. Kuimarisha mifumo ya kuhamasisha, kuzingatia na kulinda haki za watu
    na haki za binadamu;
    viii. Kuendelea kuimarisha mifumo ya utoaji Haki nchini na kuhimiza
    matumizi ya TEHAMA katika Sekta ya Sheria;
    ix. Kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa Huduma ya Msaada wa Kisheria
    nchini;
    x. Kutekeleza Programu ya Kutumia Lugha ya Kiswahili katika utoaji Haki
    Nchini;
    xi. Kuendelea na utekelezaji wa Mkakati wa Pili wa Taifa wa Haki Mtoto
    2020/2021-2024/2025;
    xii. Kuendelea kuimarisha Usajili wa matukio muhimu ya binadamu na
    takwimu pamoja na shughuli za ufilisi na udhamini;
    48
    xiii. Kuharakisha utatuzi wa mashauri ya kawaida na mkakati wa kumaliza
    mashauri ya muda mrefu (Backlog);
    xiv. Kuimarisha uwezo katika ukaguzi na usimamizi wa shughuli za
    Mahakama;
    xv. Kuendelea kutekeleza mpango wa ujenzi na ukarabati wa Majengo ya
    Mahakama katika ngazi mbalimbali;
    xvi. Kuendelea na ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya
    Tanzania ili kuhamia Dodoma;
    xvii. Kuimarisha maendeleo ya rasilimali watu, ikiwa ni pamoja na mafunzo,
    na nidhamu ya watumishi;
    xviii. Kuongeza ushirikiano na wadau wa haki jinai ili kuharakisha huduma ya
    utoaji haki;
    xix. Kuendesha vikao vya kisheria vya Tume na mchakato wa Ajira ya
    watumishi wa Mahakama;
    xx. Kutoa Elimu kwa Umma kuhusu majukumu ya Tume na Kamati za
    Maadili ya Maafisa wa Mahakama ngazi ya Mikoa na Wilaya
    xxi. Kufanya Tafsiri, Uandishi na Urekebu wa sheria;
    xxii. Kutoa ushauri wa kisheria na kufanya Upekuzi na Marejeo ya Mikataba;
    xxiii. Kuimarisha uendeshaji mashtaka na usimamizi wa mashauri ya jinai;
    xxiv. Kuimarisha uratibu na usimamizi wa upelelezi wa makosa ya jinai;
    xxv. Kuimarisha mfumo wa utaifishaji mali, usimamizi na urejeshwaji wa mali
    zinazohusiana na uhalifu;
    xxvi. Kuimarisha utekelezaji wa programu ya kutenganisha shughuli za
    Mashtaka na Upelelezi;
    xxvii. Kuratibu, kusimamia na Kuiwakilisha Serikali na Taasisi zake katika
    kuendesha mashauri ya madai na usuluhishi yaliyofunguliwa na au dhidi
    49
    ya Serikali katika mahakama na mabaraza mbalimbali ndani na nje ya
    nchi;
    xxviii. Kufanya uchunguzi kuhusu masuala ya haki za binadamu na utawala
    bora;
    xxix. Kutoa elimu kwa Umma kuhusu masuala ya haki za binadamu na
    utawala bora;
    xxx. Kuimarisha mahusiano na Taasisi za Kitaifa, Kikanda na Kimataifa;
    xxxi. Kufanya tafiti kuhusu masuala ya haki za binadamu na utawala bora
    xxxii. Kufanya Tathmini ya utekelezaji wa sheria za Kudhibiti na Kupambana
    na Dawa za Kulevya; na Mfumo wa Sheria unaosimamia Usafiri Majini.
    xxxiii. Kufanya Mapitio ya mifumo ya sheria za Usimamizi wa haki katika
    Mahakama za Mwanzo; Makosa ya uhujumu uchumi; na Usajili wa
    wadhamini.
    xxxiv. Kuimarisha maendeleo ya rasilimali watu na vitendea kazi.
    (b)Makusanyo ya Maduhuli ya Serikali
  23. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Wizara
    inatarajia kukusanya kiasi cha Shilingi 12,676,201,000.00 ikiwa ni
    maduhuli ya Serikali, kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 3:-
    Jedwali Na. 3: Makadirio ya Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha
    2022/2023
    Fungu 12 – Sh. 0.00
    Fungu 16 – Sh. 0.00
    Fungu 19 – Sh. 0.00
    Fungu 35 – Sh. 60,000,000.00
    50
    Fungu 40 – Sh. 12,571,199,000.00
    Fungu 41 – Sh. 45,000,000.00
    Fungu 55 – Sh. 2,000.00
    Fungu 59 – Sh. 0.00
    JUMLA Sh. 12,676,201,000.00

(c) Makadirio ya Fedha kwa ajili ya Kutekeleza Mpango na Bajeti kwa
Mwaka wa Fedha 2022/2023

  1. Mheshimiwa Spika, Ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake,
    Wizara inaomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 272,768,278,800.00 kwa
    ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha
    2022/2023. Kati ya Fedha hizo, Shilingi 207,703,708,800.00 ni kwa ajili ya
    matumizi ya kawaida na Shilingi 65,064,570,000.00 ni kwa ajili ya
    matumizi ya miradi ya maendeleo. Mchanganuo wa makadirio ya bajeti
    kwa mafungu nane (8) ya Wizara na taasisi zake ni kama ilivyooneshwa
    kwenye Jedwali Na. 4: –
    Jedwali Na. 4: Mchanganuo wa Makadirio ya Bajeti kwa Wizara ya
    Katiba na Sheria na Mafungu yake kwa mwaka wa fedha, 2022/2023
    Na. Fungu la Matumizi Bajeti 2022/23
  2. Mishahara ya watumishi 95,356,423,800.00
  3. Matumizi mengineyo 112,347,285,000.00
  4. Miradi ya Maendeleo 65,064,570,000.00
    JUMLA 272,768,278,800.00
    51
  5. Mheshimiwa Spika, Kiasi hicho cha fedha kinaombwa kupitia
    mafungu ya bajeti yaliyo chini ya Wizara yafuatavyo: –
    (i) Fungu 12: Tume ya Utumishi wa Mahakama
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 461,127,800.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 2,700,000,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 0
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 0
    Jumla – Sh. 3,161,127,800.00
    (ii) Fungu 16: Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 2,928,360,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 6,942,981,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 4,000,000,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 500,000,000.00
    Jumla – Sh. 14,371,341,000.00
    (iii) Fungu 19: Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 3,339,798,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 9,473,018,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 0
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 0
    Jumla – Sh. 12,812,816,000.00
    (iv) Fungu 35: Ofisi ya Taifa ya Mashtaka
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 14,548,751,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 22,068,944,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 8,000,000,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 630,000,000.00
    Jumla – Sh. 45,247,695,000.00
    (v) Fungu 40: Mfuko wa Mahakama
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 63,408,443,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 57,774,382,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 36,002,000,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 3,091,000,000.00
    Jumla – Sh. 160,275,825,000.00
    52
    (vi) Fungu 41: Wizara ya Katiba na Sheria
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 7,647,528,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 6,865,271,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 5,110,800,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 7,615,770,000.00
    Jumla – Sh. 27,239,369,000.00
    (vii) Fungu 55: Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 2,292,096,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 4,098,680,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 0
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 115,000,000.00
    Jumla – Sh. 6,505,776,000.00
    (viii) Fungu 59: Tume ya Kurekebisha Sheria
    Matumizi ya Mishahara – Sh. 730,320,000.00
    Matumizi Mengineyo – Sh. 2,424,009,000.00
    Matumizi ya Maendeleo (Ndani) – Sh. 0
    Matumizi ya Maendeleo (Nje) – Sh. 0
    Jumla – Sh. 3,154,329,000.00
    JUMLA KUU SH. 272,768,278,800.00
  6. Mheshimiwa Spika, maelezo ya kina na mchanganuo wa maombi ya
    fedha za bajeti ya kila Fungu umeainishwa kwenye vitabu vya Randama za
    mafungu husika ambavyo vimegawanywa kwa Waheshimiwa Wabunge
    kupitia Mfumo wa Kielektroniki wa Bunge.
  7. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuhitimisha hotuba yangu, naomba
    nitumie fursa hii kuwashukuru viongozi na watendaji wa Wizara na Taasisi
    zake kwa ushirikiano mkubwa wanaonipatia katika utekelezaji wa
    majukumu ya kila siku ya uwaziri. Hakika, ni kutokana na ushirikiano huo
    nimeweza kusimama leo hii mbele ya Bunge lako kueleza mafanikio,
    53
    mipango na mikakati tuliyonayo katika kuwahudumia wananchi. Hivyo,
    kipekee nimshukuru Mhe. Geophrey Mizengo Pinda (Mb.) Naibu Waziri wa
    Katiba na Sheria; Bi. Mary Gasper Makondo, Katibu Mkuu; Dkt. Khatibu
    Malimi Kazungu, Naibu Katibu Mkuu; Mhe. Prof. Ibrahimu Hamisi Juma,
    Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa
    Mahakama; Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (Mb.), Mwanasheria Mkuu
    wa Serikali; Mhe. Mustapher Mohamed Siyani, Jaji Kiongozi wa Mahakama
    Kuu ya Tanzania; Prof. Elisante Ole Gabriel, Mtendaji Mkuu wa Mahakama
    ya Tanzania na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama; Mhe. Wilbert
    Martin Chuma, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania; Bw. Sylvester
    Anthony Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka; Bw. Gabriel Pascal Malata,
    Wakili Mkuu wa Serikali; Bi. Angela Kemanzi Anatory, Kabidhi Wasii Mkuu
    na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini; Mhe. Jaji
    Mstaafu wa Mahakama ya Rufani January Henry Msoffe, Mwenyekiti wa
    Tume ya Kurekebisha Sheria; Bw. Casmir Sumba Kyuki, Katibu Mtendaji
    wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania; Mhe. Jaji Mstaafu wa
    Mahakama Kuu ya Tanzania Mathew Mhina Mwaimu, Mwenyekiti Tume ya
    Haki za Binadamu na Utawala Bora; Bw. Patience Kilanga Ntwina, Katibu
    Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora; Mhe. Jaji wa
    Mahakama ya Rufani Dkt. Paul Faustin Kihwelo, Mkuu wa Chuo cha
    Uongozi wa Mahakama Lushoto; Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Dkt. Benhajj
    Shaaban Masoud, Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa
    Vitendo Tanzania; Wakurugenzi na Watumishi wote wa Wizara na Taasisi
    zake. Aidha, nawashukuru familia yangu ikiwa ni pamoja na mke wangu
    Bibi. Flora Ndumbaro na watoto wangu kwa ushirikiano wanaoendelea
    kunipatia kwa kunivumilia na kunitia moyo wakati ninapokuwa natekeleza
    majukumu yangu ya kulitumikia Taifa. Mwisho lakini sio mwisho kwa
    54
    umuhimu, naomba nichukue fursa hii kwa namna ya kipekee kabisa
    kuwashukuru Wapiga kura wa Jimbo langu la Songea Mjini kwa kuendelea
    kunipa ushirikiano katika shughuli za kuleta maendeleo ya jimbo letu.
  8. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
    55
    KIAMBATISHO A
    ORODHA YA MAGEREZA NA VITUO VYA POLISI VILIVYOKAGULIWA
    KUANZIA JULAI, 2021 HADI MACHI, 2022
    NA. MKOA MAGEREZA
    YALIYOKAGULIWA
    VITUO VYA POLISI
    VILIYOKAGULIWA
    IDADI YA MAHABUSI
    WALIOACHIWA
    HURU
    1 Arusha 2 5 2
    2 Dodoma 6 11 37
    3 Dar es Salaam 16 79 35
    4 Geita 4 40 24
    5 Iringa 5 15 70
    6 Kagera 9 18 48
    7 Katavi 3 20 24
    8 Kigoma 3 10 5
    9 Kilimanjaro 4 11 0
    10 Lindi 8 5 2
    11 Manyara 3 7 3
    12 Mara 7 13 15
    13 Mbeya 4 5 10
    14 Morogoro 2 15 120
    15 Mtwara 5 9 10
    16 Mwanza 5 22 20
    17 Njombe 3 15 5
    18 Pwani 8 18 3
    19 Rukwa 3 9 52
    20 Ruvuma 3 8 5
    21 Shinyanga 4 19 1
    22 Simiyu 6 7 21
    23 Singida 3 5 10
    24 Songwe 2 3 61
    25 Tabora 4 8 205
    26 Tanga 7 14 21
    JUMLA 129 391 809

56
KIAMBATISHO B
MISWADA ILIYOANDALIWA KWA KIPINDI CHA JULAI, 2021 HADI
MACHI, 2022

  1. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 3) ya mwaka 2021
    (The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 3) Act, 2021);
  2. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 4) ya mwaka 2021
    (The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 4) Act, 2021);
  3. Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
    (The Fire and Rescue Force (Amendment) Act 2021);
  4. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 5) ya mwaka 2021
    (The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 5) Act, 2021);
  5. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 6) ya mwaka 2021
    (The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 6) Act, 2021);
  6. Sheria ya Ahueni za Biashara (The Trade Remedies Act);
  7. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 7) ya mwaka 2021
    (The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 7) Act, 2021)
  8. Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani (The Road
    Traffic (Amendment) Act 2021;
  9. Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa, 2022;
    10.Muswada wa marekebisho ya Sheria ya Kudhibiti Utakatishaji Fedha
    Haramu (The Anti Money Laundering Amendment Act); na
    11.Muswada wa Nyongeza ya Matumizi (The Appropriation Supplement
    Act)

57
KIAMBATISHO C
MISWADA ILIYOPITISHWA KUWA SHERIA NA KUSAINIWA NA MHE.
RAIS KUWA SHERIA NA KUTANGAZWA KWENYE GAZETI LA
SERIKALI
1.Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 3) ya mwaka 2021
(The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 3) Act, 2021);
2.Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 4) ya mwaka 2021
(The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 4) Act, 2021);
3.Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Usajili wa Wahasibu na
Wakaguzi ya mwaka 2021 (The Accountants and Auditors
Registration (Amendment) Act, 2021);
4.Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
(The Fire and Rescue Force (Amendment) Act 2021);
5.Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 5) ya mwaka 2021
(The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 5) Act, 2021);
6.Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 6) ya mwaka 2021
(The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 6) Act, 2021);
7.Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 7) ya mwaka 2021
(The Written Laws Miscellaneous Amendment (No. 7) Act, 2021);
8.Muswada wa marekebisho ya Sheria ya Kudhibiti Utakatishaji Fedha
Haramu (The Anti Money Laundering Amendment Act);
9.Muswada wa Nyongeza ya Matumizi (The Appropriation Supplement
Act)

58
KIAMBATISHO D
ORODHA YA SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA HATUA YA RASIMU YA
KWANZA KUTOKA LUGHA YA KINGEREZA KUWA LUGHA YA
KISWAHILI HADI KUFIKIA MACHI, 2022
Na. Jina la Sheria Sura Na.

  1. Sheria ya Adhabu ya Viboko 17
  2. Sheria ya Ardhi 113
  3. Sheria ya Ardhi ya Vijiji 114
  4. Sheria ya Barabara 167
  5. Sheria ya Baraza la Kiswahili la Taifa 52
  6. Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa 49
  7. Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa 204
  8. Sheria ya Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania 107
  9. Sheria ya Baraza la Taifa la Ujenzi 162
  10. Sheria ya Benki Kuu 197
  11. Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha 342
  12. Sheria ya Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza 230
  13. Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu 178
  14. Sheria ya Bodi ya Utalii Tanzania 364
  15. Sheria ya Bodi za Paroli 200
  16. Sheria ya Chama cha Mawakili Tanganyika 307
  17. Sheria ya Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania 66
  18. Sheria ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere 93
  19. Sheria ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama – Lushoto 405
  20. Sheria ya Dawa na Vifaa Tiba 219
  21. Sheria ya Elimu 353
  22. Sheria ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (VETA) 82
  23. Sheria ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro 284
  24. Sheria ya Fedha za Kigeni 271
  25. Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa 290
  26. Sheria ya Fedha za Umma 348
  27. Sheria ya Gharama za Uchaguzi 278
  28. Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki 218
  29. Sheria ya Hati za Makubaliano 26
  30. Sheria ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu, 146
  31. Sheria ya Hospitali ya Benjamini Mkapa
  32. Sheria ya Huduma kwa Jamii 291
    59
  33. Sheria ya Huduma za Habari 229
  34. Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi Wasaidizi 322
  35. Sheria ya Jeshi la zimamoto na Uokoaji 427
  36. Sheria ya Jumuiya 337
  37. Sheria ya Kamisheni za Uchunguzi 32
  38. Sheria ya Kanuni ya Adhabu 16
  39. Sheria ya Karadha 14
  40. Sheria ya Kinga na Upendeleo wa Kidiplomasia na
    Kikonseli
    356
  41. Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge 296
  42. Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya 95
  43. Sheria ya Kudhibiti Vinasaba vya Binadamu 73
  44. Sheria ya Kulinda Watoa Taarifa na Mashahidi 446
  45. Sheria ya Kuongeza Hukumu 7
  46. Sheria ya Kuratibu Usajili na Usimamizi wa Maabara
    Binafsi za Afya
    136
  47. Sheria ya Kuzuia na Kuthibiti VVU na Ukimwi 431
  48. Sheria ya Kuzuia Ugaidi 19
  49. Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, 432
  50. Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma 398
  51. Sheria ya Mabaraza Maalumu 126
  52. Sheria ya Madaktari wa Mifugo 319
  53. Sheria ya Madaktari, Madaktari wa Meno na Wataalam wa
    Afya Shirikishi
    152
  54. Sheria ya Madini 123
  55. Sheria ya Maeneo na Sehemu Zinazolindwa 74
  56. Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi 225
  57. Sheria ya Mafao ya Viongozi wa Kisiasa 255
  58. Sheria ya Magereza 58
  59. Sheria ya Magonjwa ya Wanyama 156
  60. Sheria ya Mahakama na Matumizi ya Sheria 358
  61. Sheria ya Mahakama za Mahakimu 11
  62. Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi, 216
  63. Sheria ya Majadiliano ya Pamoja Katika Utumishi wa
    Umma
    105
  64. Sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira 272
  65. Sheria ya Makumbusho ya Taifa 281
  66. Sheria ya Mamlaka na Majukumu ya Kabidhi Wasii Mkuu 27
  67. Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania 157
    60
  68. Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa
    Serikali
    177
  69. Sheria ya Mamlaka ya Nchi ya Utajiri Asili na Mali Asilia za
    nchi
    449
  70. Sheria ya Mapato ya Uhalifu 256
  71. Sheria ya Mapitio na Majadiliano ya Masharti Hasi Katika
    Mikataba ya Utajiri Asili na Mali Asilia
    450
  72. Sheria ya Mashirika ya Maendeleo ya Wilaya 382
  73. Sheria ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali 56
  74. Sheria ya Masoko la Mitaji na Dhamana 79
  75. Sheria ya Masuala ya Ofisi ya Rais 9
  76. Sheria ya Matamko ya Sheria za Kiislamu 375
  77. Sheria ya Mawakili 341
  78. Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta 306
  79. Sheria ya Mawaziri ya Utekelezaji wa Majukumu ya
    Uwaziri,
    299
  80. Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa 419
  81. Sheria ya Mfuko wa Elimu 412
  82. Sheria ya Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Majimbo 96
  83. Sheria ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) 422
  84. Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya 395
  85. Sheria ya Michezo ya Kubahatisha 41
  86. Sheria ya Mipango Miji 355
  87. Sheria ya Mirathi (Kwa Waasia) Wasio Wakristo 28
  88. Sheria ya Mishahara na Mafao ya Majaji 424
  89. Sheria ya Misitu 323
  90. Sheria ya Msaada wa Kisheria 21
  91. Sheria ya Mtoto 13
  92. Sheria ya Mwenendo wa Madai ya Serikali 5
  93. Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai 33
  94. Sheria ya Ndoa 29
  95. Sheria ya Optmetria 23
  96. Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria 42
  97. Sheria ya Petroli 392
  98. Sheria ya Probesheni 247
  99. Sheria ya Reli ya Tanzania na Zambia 143
  100. Sheria ya Serikali Mtandao 273
  101. Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) 288
  102. Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka Za Wilaya) 287
    61
  103. Sheria ya Shirika la Mawasiliano Tanzania 304
  104. Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa 295
  105. Sheria ya Shirika la Posta 303
  106. Sheria ya Shule za Udereva wa Vyombo vya Moto (Usajili) 163
  107. Sheria ya Sikukuu za Kitaifa 35
  108. Sheria ya Taasisi ya Bahari Dar es Salaam 253
  109. Sheria ya Taasisi ya Elimu Tanzania 142
  110. Sheria ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima 139
  111. Sheria ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo
    Tanzania
    425
  112. Sheria ya Taasisi ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) 59
  113. Sheria ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
  114. Sheria ya Taasisi ya Saratani 86
  115. Sheria ya Taasisi ya Taifa ya Usafirishaji 187
  116. Sheria ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam 144
  117. Sheria ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii 110
  118. Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania 280
  119. Sheria ya Tafsiri ya Alama za Taifa 10
  120. Sheria ya Tafsiri ya Sheria 1
  121. Sheria ya Taifa ya Mashtaka 430
  122. Sheria ya Taifa ya Uchaguzi 343
  123. Sheria ya Takwimu 351
  124. Sheria ya Taratibu za Uanzishaji wa Mikoa na Wilaya 397
  125. Sheria ya Tasnia ya Mifugo 262
  126. Sheria ya Tasnia ya Mkonge 30
  127. Sheria ya Tawala za Mikoa 97
  128. Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala 244
  129. Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora 391
  130. Sheria ya Tume ya Jeshi la Polisi na Magereza 241
  131. Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria 171
  132. Sheria ya Tume ya Sayansi na Teknolojia 266
  133. Sheria ya Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania 226
  134. Sheria ya Tume ya Taifa ya UNESCO 433
  135. Sheria ya Tume ya Ukimwi Tanzania 379
  136. Sheria ya Tume ya Vyuo Vikuu 346
  137. Sheria ya Tume za Uchunguzi, 32
  138. Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa 292
  139. Sheria ya Uchawi 18
  140. Sheria ya Uchunguzi wa Kifo 24
    62
  141. Sheria ya Udhamini wa Umma na (Mamlaka na Majukumu) 31
  142. Sheria ya Uendeshaji wa Bunge 115
  143. Sheria ya Ufilisi 25
  144. Sheria ya Ufuatiliaji Wahalifu Watoro 57
  145. Sheria ya Uhamiaji 54
  146. Sheria ya Uhamisho wa Mali zinazohamishika 210
  147. Sheria ya Uhamisho wa wafungwa 387
  148. Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori 283
  149. Sheria ya Uhujumu Uchumi 200
  150. Sheria ya Ukaguzi wa Umma 418
  151. Sheria ya Ukomo 89
  152. Sheria ya Umiliki wa Sehemu ya Jengo 416
  153. Sheria ya Ununuzi wa Umma 410
  154. Sheria ya Upangaji wa Matumizi ya Ardhi 116
  155. Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa 149
  156. Sheria ya Upimaji Ardhi 324
  157. Sheria ya Uraia 357
  158. Sheria ya Urejeshaji wahalifu 368
  159. Sheria ya Urekebu wa Sheria 4
  160. Sheria ya Usafiri Majini 165
  161. Sheria ya Usafiri wa Anga 80
  162. Sheria ya Usafirishaji wa Bidhaa kwa Njia ya Bahari 164
  163. Sheria ya Usajili na Utambuzi wa Watu 36
  164. Sheria ya Usajili wa Ardhi 334
  165. Sheria ya Usajili wa Makandarasi 235
  166. Sheria ya Usajili wa Nyaraka 117
  167. Sheria ya Usajili wa Rehani zinazohamishika
  168. Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo 108
  169. Sheria ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji
    Majenzi
    269
  170. Sheria ya Usajili wa Wahandisi 63
  171. Sheria ya Usajili wa Wataalam wa Afya ya Mazingira 428
  172. Sheria ya Usajili wa Wataalamu wa Mipango Miji 426
  173. Sheria ya Usajili Wataalamu wa Upimaji 270
  174. Sheria ya Usalama Barabarani 168
  175. Sheria ya Usambazaji Maji Safi na Usafi wa Mazingira 272
  176. Sheria ya Ushahidi 6
  177. Sheria ya Ushirikiano katika Makosa ya Jinai 254
  178. Sheria ya usimamizi Hospitali za watu Binafsi 151
    63
  179. Sheria ya Usimamizi na Uendelezaji wa Uvuvi wa Bahari
    Kuu
    388
  180. Sheria ya Usimamizi wa Kumbukumbu na Nyaraka 309
  181. Sheria ya Usimamizi wa Maafa. 242
  182. Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji 331
  183. Sheria ya Usimamizi wa Uthibiti wa Silaha na Risasi 223
  184. Sheria ya Usimamizi ya Waasibu na Wakaguzi 286
  185. Sheria ya Ustawi wa Wanyama 154
  186. Sheria ya Usuluhishi 15
  187. Sheria ya Utafiri wa Wanyamapori Tanzania 260
  188. Sheria ya Utalii 65
  189. Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo 184
  190. Sheria ya Utaratibu wa Heshima kwa Waasisi wa Taifa 194
  191. Sheria ya Utawala wa Mahakama 237
  192. Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Msingi na Wajibu 3
  193. Sheria ya Utekelezaji wa Hukumu ya Kigeni 8
  194. Sheria ya Utekelezaji wa Hukumu za Nchi Jirani 7
  195. Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Mwanasheria Mkuu
    wa Serikali
    268
  196. Sheria ya Uthamini na Usajili wa Wathamini 138
  197. Sheria ya Uthibiti wa Bidhaa za Tumbaku 121
  198. Sheria ya Uthibitisho na Usimamizi wa Mirathi 352
  199. Sheria ya Utumishi wa Umma 298
  200. Sheria ya Utwaaji Ardhi 118
  201. Sheria ya Utwaaji na Urejeshaji wa Mashamba Vijijini 22
  202. Sheria ya Uvuvi 279
  203. Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania 415
  204. Sheria ya Uwekezaji wa Wadhamini 53
  205. Sheria ya Viapo na Matamko ya Kisheria 34
  206. Sheria ya Vivuko 173
  207. Sheria ya Vyama vya Siasa 258
  208. Sheria ya Vyuo Vikuu 346
  209. Sheria ya Waasisi wa Taifa 195
  210. Sheria ya Wakala wa Serikali 245
  211. Sheria ya Wakimbizi 37
  212. Sheria ya Wanataaluma wa Kemia 160
  213. Sheria ya Wataalamu wa Maabara ya Afya 48
  214. Sheria ya ya Utekelezaji wa Wito wa Mashahidi wa kigeni 67
    64
    KIAMBATISHO E
    ORODHA YA SHERIA ZILIZOFANYIWA UREKEBU KWA HATUA YA
    USOMAJI WA AWALI KUANZIA JULAI, 2021 HADI MACHI, 2022
    S/N CHAPTER NAME
  215. 416 The Unit Titles Act
  216. 420 The Special Economic Zones Act
  217. 421 The meat Industry Act
  218. 422 The Universal Communications Services Access Act.
  219. 423 The Anti-money Laundering Act
  220. 425 The Law School of Tanzania Act
  221. 427 The Fire and Rescue Force Act
  222. 428 The Environmental Health Practitioners (Registration)
    Act.
  223. 429 The Medical Radiology and Imaging Professionals Act
  224. 430 The National Prosecutions Service Act
  225. 431 The HIV and AIDS (Prevention and control) Act
  226. 432 The Anti-Trafficking in persons Act
  227. 433 The UNESCO National Commission Act.
  228. 434 The Tanzania Livestock Research Institute Act
  229. 435 The National Irrigation Act
  230. 436 The Non-citizens (Employment Regulation Act
  231. 437 The National Payment System Act
  232. 438 Tax Administration Act
  233. 439 The Budget Act
  234. 440 The Referendum Act
  235. 441 The National Youth Council Act
  236. 442 The Electronic Transactions Act
  237. 443 The Cybercrimes Act
  238. 444 The One Stop Border Posts Act
  239. 445 The Commodity Exchange Act
  240. 446 The Whistleblower and Witness Protection Act
  241. 447 The Tanzania Extractive Industries (Transparency and
    Accountability) Act
  242. 448 The Teacher s’ Service Commission Act
  243. 449 The Natural Wealth and Resources (Permanent
    Sovereignty) Act

65
KIAMBATISHO E
ORODHA YA SHERIA ZILIZOFANYIWA UREKEBU KWA HATUA YA
USOMAJI WA AWALI KUANZIA JULAI, 2021 HADI MACHI, 2022
S/N CHAPTER NAME

  1. 450 The Natural Wealth and Resources Contracts (Review
    and Re-negotiation of Unconscionable Terms) Act
  2. 82 The Vocational Education and Training Act
  3. 93 The Mwalimu Nyerere Memorial Academy Act
  4. 102 The Tanzania Library Services Act
  5. 107 The National Examinations Council of Tanzania Act
  6. 129 The National Council for Technical Education Act
  7. 139 The Institute of Adult Education Act
  8. 142 The Tanzania Institute of Education Act
  9. 144 The Dar- Es –Salaam Institute of Technology Act
  10. 178 The Higher Education Students Loans Board Act
  11. 188 The Atomic Energy Act
  12. 226 The Tanzania Commissioner for Science and
    Technology Act
  13. 314 The Tanzania Teachers’ Professional Board Act
  14. 346 The Universities Act
  15. 352 The Education Act
  16. 412 The Education Fund Act
  17. 433 The UNESCO National Commission Act.

66
KIAMBATISHO NA. F
MAENDELEO YA RASILIMALIWATU 2021/2022
FUNG
U
TAASI
SI
AJIR
A
MPY
A
KUTHIBITI
SHWA
KAZINI
KUPAND
ISHWA
CHEO
UTEU
ZI
MAFUNZ
O
KUSIMAMI
SHWA
KAZI
KUACHIS
HWA
KAZI
KUACH
A KAZI
KUREJ
ESHWA
KAZINI
KUSTA
AFISH
WA
KWA
MASLA
HI YA
UMMA
12 0 0 1 1 10 0 0 0 0 0
16 21 2 0 1 19 0 0 0 0 0
19 23 8 0 0 13 0 0 0 0 0
35 4 1 19 0 258 0 0 0 0 0
40 45 199 0 25 1099 3 5 3 9 7
41 1 0 2 2 0 0 0 0 0 0
55 5 0 0 1 23 0 0 0 0 0
59 0 0 0 0 20 0 0 0 0 0
IJA 2 1 36 1 70 0 0 0 0 0
LST 0 0 9 0 20 0 0 0 0 0
RITA 0 67 3 3 47 2 0 0 2 0
JUML
A KUU 101 278 70 34 1579 5 5 3 11 7

67
KIAMBATISHO G
MCHANGANUO WA BAJETI NA FEDHA ZILIZOPOKELEWA ZA MIRADI YA MAENDELEO KUANZIA
JULAI, 2021 HADI MACHI 2022
Fungu
Bajeti iliyoidhinishwa kwa Mwaka wa Fedha
2021/2022 Fedha zilizopokelewa hadi Machi, 2022
Miradi ya Maendeleo Jumla Miradi ya Maendeleo Jumla Ndani Nje Ndani Nje
16-Ofisi ya
Mwanasheria
Mkuu wa Serikali 1,000,000,000 – 1,000,000,000 – – –
35-Ofisi ya Taifa
ya Mashtaka 3,000,000,000 993,616,000 3,993,616,000 214,155,912.00 84,000,000.00 298,155,912.00
40-Mfuko wa
Mahakama 39,100,000,000 1,090,000,000 40,190,000,000 21,492,475,322.90 23,133,893,261.54 44,626,368,584.44
41-Wizara ya
Katiba na Sheria 1,000,000,000 6,358,598,000 7,358,598,000 429,125,000.00 4,002,354,217.00 4,431,479,217.00
55-Tume ya Haki
za Binadamu na
Utawala Bora

  • 373,616,000 373,616,000 – 260,079,091.00 260,079,091.00
    Jumla 44,100,000,000 8,815,830,000 52,915,830,000 22,135,756,234.90 27,480,326,569.54 49,616,082,804.44

68
KIAMBATISHO H
MCHANGANUO WA BAJETI ILIYOIDHINISHWA NA KIASI CHA FEDHA ZILIZOPOKELEWA NA
WIZARA NA TAASISI HADI MACHI, 2022
Ndani Nje Ndani Nje
12-Tume ya Utumishi
wa Mahakama 420,191,000.00 2,700,000,000.00 – – 3,120,191,000.00 297,394,730.26 1,925,392,500.00 – – 2,222,787,230.26
16-Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa
Serikali
2,650,210,000.00 5,022,981,000.00 1,000,000,000.00 – 8,673,191,000.00 1,933,307,000.00 3,324,786,212.44 – – 5,258,093,212.44
19-Ofisi ya Wakili
Mkuu wa Serikali 2,658,329,000.00 9,473,018,000.00 – – 12,131,347,000.00 1,410,702,307.65 7,205,068,823.98 – – 8,615,771,131.63
35-Ofisi ya Taifa ya
Mashtaka 9,199,868,000.00 12,068,944,000.00 3,000,000,000.00 993,616,000.00 25,262,428,000.00 7,446,962,412.20 15,568,101,031.00 214,155,912.00 84,000,000.00 23,313,219,355.20
40-Mfuko wa
Mahakama 55,264,477,000.00 57,774,382,000.00 39,100,000,000.00 1,090,000,000.00 153,228,859,000.00 45,246,273,055.13 43,754,226,949.97 21,492,475,322.90 23,133,893,261.54 133,626,868,589.54
41-Wizara ya Katiba
na Sheria 6,089,479,000.00 5,865,271,000.00 1,000,000,000.00 6,358,598,000.00 19,313,348,000.00 4,491,024,764.03 4,875,315,587.41 429,125,000.00 4,002,354,217.00 13,797,819,568.44
55-Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala
Bora
2,495,556,000.00 3,850,280,000.00 – 373,616,000.00 6,719,452,000.00 1,762,074,968.00 2,829,482,951.00 – 260,079,091.00 4,851,637,010.00
59-Tume ya
Kurekebisha Sheria 820,920,000.00 2,424,009,000.00 – – 3,244,929,000.00 542,226,000.00 1,887,137,774.79 – – 2,429,363,774.79
Jumla 79,599,030,000.00 99,178,885,000.00 44,100,000,000.00 8,815,830,000.00 231,693,745,000.00 63,129,965,237.27 81,369,511,830.59 22,135,756,234.90 27,480,326,569.54 194,115,559,872.30
MCHANGANUO WA BAJETI ILIYOIDHINISHWA NA KIASI CHA FEDHA ZILIZOPOKELEWA NA WIZARA NA TAASISI HADI MACHI, 2022
Miradi ya Maendeleo Mishahara Matumizi Mengineyo Fungu
Bajeti iliyoidhinishwa kwa Mwaka 2021/2022
Jumla
Fedha zilizopokelewa hadi Machi, 2022
Mishahara Matumizi Mengineyo Miradi ya Maendeleo Jumla

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *