Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akiongoza kikao cha pamoja baina ya Tume ya Utumishi wa Bunge na Kamati ya Uongozi kilichokutana kujadili ratiba ya mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Marehemu Mhe. Irene Ndyamkama, leo tarehe 25 Aprili 2022, Bungeni Jijini Dodoma.



