HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI-OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. JENISTA MHAGAMA KUHUSU MAKADRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2022/2023

UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, kutokana na taarifa iliyowasilishwa ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na

Serikali za Mitaa iliyochambua bajeti ya Ofisi ya Rais, Ikulu (Fungu 20 na 30); Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (Fungu 33); Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala

Bora (Fungu 32); Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (Fungu 67); Tume ya

Utumishi wa Umma (Fungu 94); na Idara ya

Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa (Fungu 04); 

Bunge lako Tukufu sasa lipokee na kujadili

Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2021/22. Aidha, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Mpango wa Utekelezaji na Makadirio ya Fedha kwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2022/23. 

  • Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kutujalia amani na utulivu ambavyo vimetuwezesha kutekeleza majukumu ya kuongoza Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kuwahudumia wananchi pamoja na kutuwezesha kukutana kwa ajili ya kupokea utekelezaji wa Ofisi yangu na kutafakari malengo yajayo katika mkutano huu wa saba wa Bunge la 12. Kwa namna ya pekee napenda kumshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa imani yake kubwa kwangu kwa kuniteua kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Pia, namshukuru Rais kwa imani yake kwa Naibu Waziri wangu Mheshimiwa Deogratius Ndejembi, Mbunge wa Jimbo la Chamwino kwa kumbakiza katika nafasi yake na ndani ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Pia, namshukuru Rais kwa safu nzuri ya Watendaji wa Ofisi yangu ambao amewaidhinisha. 
  • Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii, kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza mwaka mmoja kazini kwa mafanikio makubwa ya utendaji wa kazi yanayoonekana katika sekta mbalimbali nchini. Rais wetu amedhihirisha kuwa yeye ni kiongozi bora, muadilifu, mzalendo, mchapakazi, mcha Mungu, mwenye nia na maono makubwa ya kuleta ustawi wa taifa na maendeleo kwa Watanzania. 
  • Mheshimiwa Spika, naomba pianimpongeze Rais wetu kwa azma yake ya dhati ya kuuboresha Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Dhamira hiyo aliionesha wakati akilihutubia Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 22 Aprili, 2021 mara baada ya kuapishwa kuwa Rais. Alisema na anaendelea kutekeleza kwa vitendo dhamira yake ya kuwa, Serikali anayoingoza itaendeleza jitihada za kuimarisha maadili, nidhamu, uzalendo, uchapa kazi na uwajibikaji. Pia, aliahidi kusimamia haki na stahiki za Watumishi wa Umma na Watendaji serikalini ili kuongeza ari ya kufanya kazi kwa bidii na kukuza uwajibikaji wa hiari katika Utumishi wa Umma. Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inaahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, nidhamu, uadilifu, weledi na uzalendo wa kitaifa ili kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Philip

Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, kwa namna anavyomsaidia Rais kutekeleza majukumu ya kuiletea maendeleo nchi yetu. Aidha, napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa uongozi wake shupavu na nia yake thabiti ya kuleta maendeleo Zanzibar. 

  • Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kusimamia na kuratibu kazi za kila siku za Serikali na utendaji wa Serikali Bungeni kwa umahiri mkubwa. Pamoja na kumsaidia vyema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuliletea Taifa letu maendeleo.
  • Mheshimiwa Spika, naomba nikupongeze wewe binafsi kwa kuwa mwanamke wa pili kushika uongozi wa Mhimili huu wa Bunge. Pia, nampongeza Naibu Spika ambaye ameungana nawe kuchaguliwa kwa kishindo katika nafasi za kuliongoza Bunge letu Tukufu. Tunategemea  kuwa umakini, weledi, busara na hekima kubwa mliyodhihirisha katika nafasi mlizokuwa nazo zitaendelea kukua zaidi mnapotekeleza wajibu wenu katika nafasi hizi kubwa zaidi. Pia, nawapongeza Wenyeviti wa Bunge kwa kusimamia kwa ustadi wa hali ya juu kazi waliyopewa ya kuongoza vikao vya Bunge letu, kwa hakika mmekuwa msaada mkubwa sana katika uendeshaji wa Bunge kwa ujumla.
  • Mheshimiwa Spika, naomba pia kuwapongeza Mawaziri wenzangu wote wa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kupewa nafasi ya kuwatumikia Watanzania, hasa kutekeleza Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025. 
  • Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Abdallah Chaurembo, Mbunge wa Mbagala na Makamu wake Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, pamoja na Wajumbe wa Kamati kwa ushirikiano, maelekezo na ushauri mzuri walioutoa wakati wa kupitia Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/22 na Mapendekezo ya Mpango wa Utekelezaji na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa Mwaka wa Fedha 2022/23. Maoni, ushauri na ushirikiano wa Kamati umetuwezesha kuboresha utendaji kazi wa Ofisi yangu na maandalizi ya hotuba hii.
  1. Mheshimiwa Spika, nawashukuru Balozi Hussein A. Kattanga, Katibu Mkuu Kiongozi;  Dkt Moses M. Kusiluka, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Ikulu; Dkt. Laurean J. Ndumbaro, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Bw. Xavier M. Daudi, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Makamishna, Watendaji Wakuu wa Taasisi; Wakurugenzi na Watumishi wote wa Ofisi ya Rais Ikulu na Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kutekeleza majukumu yanayoiwezesha Ofisi kufikia malengo yake, ikiwa ni pamoja na kukamilisha Hotuba hii kwa wakati. Aidha, napenda kuwashukuru waajiri na watumishi wote wa Umma kwa kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi, uzalendo pamoja na imani yao kwa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita ambao umeiwezesha Serikali kutekeleza majukumu yake ya kuwahudumia wananchi.
  1. Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee napenda kuzishukuru Nchi Wahisani na Washirika wa Maendeleo ambao wamechangia jitihada zetu za kuleta maendeleo kwa wananchi. Hivyo, nachukua fursa hii kuwashukuru na kuwataja wachache ambao ni:- Jamhuri ya Watu wa China, Japan, Uingereza, India, Jamhuri ya Korea, Marekani, Sweden, Australia, Umoja wa Ulaya, Norway, Finland, Uswisi, Malaysia, Misri, Singapore, Cuba, Thailand na Ireland. Vile vile, nayashukuru Mashirika ya Maendeleo ya Kimataifa ambayo ni: Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Dunia (WB), OFID-OPEC Fund for International Development, Foreign Commonwealth Development Office (FCDO), KOICA, GIZ, USAID, SIDA, UNDP, Jumuiya ya Madola, JICA, UNICEF, ILO, WFP, UN Women, Global Fund, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na Taasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation.
  1. Mheshimiwa Spika, natumia fursa hii kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Peramiho kwa kuendelea kunipa ushirikiano wakati wote ninapoendelea kuwawakilisha. Vile vile, naishukuru familia yangu kwa ushirikiano wanaonipa na kwa dua zao wakati wote ninapotekeleza majukumu yangu.
  1. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa natoa pole kwa Watanzania wenzetu, Viongozi na Watumishi wa Umma waliopotelewa na ndugu zao kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza katika kipindi hiki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu awape faraja wote ili waendelee kujenga

Taifa letu. 

  1. Mheshimiwa Spika, tunampongeza sana Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa mikakati yake bora ya kupambana na UVIKO 19 kwa kuhimiza wananchi wote ikiwemo watumishi wa umma kupata chanjo. Aidha, Rais ametumia fursa ya UVIKO kupata fedha za kuiletea maendeleo nchi yetu. Natumia nafasi hii kutoa rai kwa watumishi wa umma kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga.
  1. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/22 tuliwasilisha mbele ya Bunge lako tukufu, maombi ya fedha kwa ajili ya kutekeleza mipango kazi inayowezesha Ofisi yangu kwa mazingatio ya kisera na kimkakati. Kwa mara nyingine tupo mbele ya Bunge lako Tukufu ili kutoa Taarifa ya Utekelezaji wa shughuli tulizoombea fedha kwa Mwaka wa Fedha 2021/22 pamoja na kuwasilisha mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2022/23.

MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MWAKA WA FEDHA 2021/22

16. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha 2021/22 ulizingatia miongozo ya kitaifa ambayo ni Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020, Hotuba ya Mhe. Samia Suluhu Hassan,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kuhutubia Bunge la 12 pamoja na maelekezo yake mbalimbali. Aidha, utekelezaji umezingatia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano Awamu ya Tatu (2021/22 – 2025/26), unaoitaka Tanzania iwe na Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu.

OFISI YA RAIS – IKULU NA TAASISI ZAKE

  1. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/22, Fungu: 20 Ofisi ya Rais, Ikulu iliidhinishiwa Shilingi 24,557,764,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Hadi kufikia Machi, 2022 Shilingi 18,339,003,333.31 zilipokelewa na kutumika.
  2. Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza majukumu yake, katika Mwaka wa Fedha 2021/22, Fungu 30 Ofisi ya Rais na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri inayojumuisha taasisi zilizo chini ya Ikulu, iliidhinishiwa Shilingi 639,780,318,000. Kati ya fedha hizo, Shilingi 467,921,917,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 171,858,401,000 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Hadi kufikia Machi, 2022 Shilingi 491,351,852,318.92 zilipokelewa na kutumika.Kati ya fedha hizo Shilingi 368,574,043,260.92 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 122,777,809,058 kwa ajili yaMiradi ya Maendeleo. Yafuatayo ni maelezo kwa kila taasisi:-

A: OFISI YA RAIS- IKULU

19. Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, Ikulu imeendelea kuongoza, kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali. Katika kipindi cha mwezi Julai, 2021 hadi Machi, 2022, kazi zifuatazo zilitekelezwa:- 

  • Ushauri umeendelea kutolewa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala ya Siasa, Uchumi, Jamii, Sheria, Diplomasia, Mawasiliano na Habari, Uhusiano wa Kikanda, Kimataifa na ushauri mwingine kwa lengo la kumsaidia Rais kufanya maamuzi; 
  • Ushauri umeendelea kutolewa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

kuhusu ratiba ya kila siku;

  • Huduma zimeendelea kutolewa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na familia yake;
  • Mikutano 25 ya Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri ilifanyika, ambapo nyaraka 43 zilichambuliwa. Mikutano 10 ya Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu (IMTC) ilifanyika na nyaraka 20 zilichambuliwa na ushauri kutolewa. Mikutano miwili ya kazi ya Kamati ya Makatibu Wakuu ilifanyika ambapo mada tano ziliwasilishwa na kujadiliwa. Mikutano mitano ya Baraza la Mawaziri ilifanyika ambapo nyaraka 21 zilijadiliwa na kutolewa maamuzi. Aidha, mikutano minne ya Kamati ya Katiba na Bunge ya Baraza la Mawaziri ilifanyika ambapo

miswada 13 ilijadiliwa;

  • Kumbukumbu za Mikutano ya Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri, Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu na Baraza la Mawaziri ziliandaliwa na kusambazwa kwa wakati kwa wahusika. Aidha, ufuatiliaji na tathmini ya Maamuzi ya Baraza la Mawaziri ulifanyika na taarifa ya utekelezaji wake iliandaliwa;
  • Ziara ya Maafisa wa Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri kutembelea Mradi wa Bwawa la Kuazalisha Umeme la Julius Nyerere na Uhifadhi katika mbuga za Ngorongoro, Loliondo na Serengeti ilifanyika ili kuona hali halisi ya utendaji na kushauri ipasavyo;
  • Mafunzo kuhusu utayarishaji na uwasilishaji wa Nyaraka za Baraza la Mawaziri kwa Menejimenti za Wizara tano za Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; Ofisi ya Rais – Ikulu; Wizara ya Afya; Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi; na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yalifanyika;
  • Mkutano wa Waratibu wa Shughuli za Baraza la Mawaziri (CLOs) katika Wizara

zote ulifanyika mwezi Machi, 2022 Mkoani Singida;

  • Vitabu vya Taarifa za Utekelezaji wa Kazi na Shughuli za Baraza la Mawaziri na Kamati zake kwa kipindi cha pili cha Serikali ya Awamu ya Nne (mwaka 2010 – 2015) na kipindi cha kwanza cha Serikali ya awamu ya 5 (2015 – 2020) vinaandaliwa;
  • Mafunzo ya kujenga uwezo kuhusu utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Awamu ya Tatu (NACSAP III) yamefanyika kwa Kamati za Kudhibiti Uadilifu za Taasisi 86 (zinazojumuisha Sekta ya Umma, Sekta Binafsi, na Asasi za Kiraia CSOs);
  • Tathmini ya utekelezaji wa Awamu ya Tatu ya Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa   imefanyika ambapo      rasimu iliyoboreshwa ya taarifa ya tathmini inafanyiwa uchambuzi   kabla    ya

kuwasilishwa Serikalini;

  • Uratibu na uendeshaji wa mikutano ya Makatibu   Wakuu na Waratibu     wa Programu za Maboresho umefanyika na kuwezesha kikao cha Katibu Mkuu Kiongozi na Makatibu Wakuu wanaosimamia utekelezaji wa Programu za Maboresho katika Sekta ya Umma kufanyika. Vile vile,  mikutano mitatu (3) ya Waratibu wa Programu za Maboresho imefanyika ili kuimarisha usimamizi, uongozi na umiliki wa mchakato wa maboresho katika sekta ya umma nchini;
  • Mkutano wa uhamasishaji baina ya Idara ya Utawala Bora na Maboresho, Menejimenti ya TPSF pamoja na AZAKI umefanyika ili kuhamashisha Sekta Binafsi kuzingatia malengo ya Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na kuishirikisha katika tathmini. Aidha, majadiliano na viongozi wa dini (TEC, BAKWATA na CCT) kuhusu utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa kwa lengo la kukusanya maoni

umefanyika; 

  • Taarifa mbili (2) za utekelezaji za robo mwaka za Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Awamu ya Tatu (NACSAP III) zimeandaliwa. Aidha, maandalizi ya awali

ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ufuatiliaji na Tathmini wa NACSAP III

yamefanyika; 

  • Ziara za ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa zimefanyika katika Mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Mara, Dar es salaam, Pwani na Singida. Aidha, ziara za ufuatiliaji wa Utekelezaji wa maboresho zimefanyika katika Mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Arusha, Manyara, Singida, Tabora na

Katavi;

  • Rufaa 222 za Watumishi wa Umma, Mamlaka ya Nidhamu na Waajiri zilichambuliwa na kutolewa uamuzi na Rais na Katibu Mkuu Kiongozi ambapo wahusika walijulishwa. Aidha, malalamiko 587 ya Watumishi wa Umma na wananchi wengine yalichambuliwa na kutolewa maelekezo; 
  • Majibu na ushahidi umetolewa kwenye kesi za madai tatu (3) kuhusu watumishi wa Umma na wananchi wengine zilizoko Mahakama Kuu zinazopinga uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Katibu Mkuu Kiongozi zilitolewa kwa kushirikiana na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali; na
  • Ujenzi    wa Ikulu     ya   Chamwino umeendelea kufanyika    na umefikia asilimia 94. Aidha, ukarabati wa baadhi ya majengo katika Ikulu ya Dar es Salaam      umefanyika   ukihusisha pia upakaji rangi wa majengo na ukuta.

B. TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA (TAKUKURU)

  • Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Kuzuia na

Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329. Majukumu hayo ni kuchukua hatua stahiki za kuzuia na kupambana na rushwa kwenye sekta ya umma, mashirika na sekta binafsi, ikijikita zaidi katika kuzuia vitendo vya Rushwa kwa watumishi wa umma na sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

  • Mheshimiwa Spika, juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kukabiliana na vitendo vya rushwa nchini zimeleta mafanikio makubwa kwa kuongeza nidhamu, uadilifu na uwajibikaji katika nyanja mbalimbali zikiwemo za utumishi wa umma, biashara, uwekezaji, ukusanyaji mapato na matumizi ya madaraka na fedha za umma. Mafanikio haya yameijengea Serikali uwezo imara wa kukuza uchumi na kuongeza kasi ya utoaji huduma bora kwa umma.
  • Mheshimiwa Spika, matokeo ya tafiti zilizofanywa na taasisi mbalimbali za kitaifa, kikanda na kimataifa kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na rushwa zimedhihirisha kuwa Tanzania inafanya vizuri katika kudhibiti vitendo vya rushwa na ufisadi nchini. Taarifa ya Transparency International ya mwaka 2021 iliyotoka Februari, 2022; kupitia Kiashiria cha Corruption Perception Index inaonesha kuwa Tanzania imeendelea kufanya vizuri kwa kupata alama 39 na kushika nafasi ya 87 kati ya nchi 180, ikiwa imepanda kwa nafasi 7 ikilinganishwa na alama 38 katika nafasi ya 94 ya mwaka 2020. Kwa mafanikio haya Tanzania imeshika nafasi ya pili kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia, Utafiti wa World Justice Project (WJP) unayotumia kiashiria cha

“The Rule of Law Index” unaonesha kuwa kwa mwaka 2020, Tanzania iliendelea kufanya vizuri kwa mwaka wa pili mfululizo katika kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka kwenye mihimili ya utawala, mahakama na bunge kwa kushika nafasi ya 93 kati ya nchi 128 duniani, ikiwa ni nchi ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki na nafasi ya 13 kwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara. Vilevile, utafiti wa taasisi binafsi ya Research on Poverty Alleviation (REPOA), uliotolewa mwezi 2022 unaonesha kuwa

Tanzania inafanya vizuri katika kulikabili tatizo la rushwa  na kuwa imepungua katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

  • Mheshimiwa Spika, Serikali imeongeza nguvu kwenye kudhibiti rushwa na ufisadi nchini kwa kuweka msisitizo kwenye eneo la uzuiaji rushwa. Katika kipindi cha mwezi Julai, 2021 hadi Machi, 2022, baadhi ya kazi zilizotekelezwa ni zifuatazo:-  

(i) Kazi 370 za uchambuzi wa mifumo zilifanyika katika maeneo mbalimbali yakiwemo: 

  1. Upatikanaji, usambazaji na udhibiti wa bidhaa za afya; 
    1. Usimamizi wa ajira, mitihani na fedha za utafiti/ushauri katika Vyuo Vikuu vya Umma nchini;
      1. Usimamizi wa mitihani katika vyuo vya kati; 
      1. Ufanisi wa mfumo wa huduma za ununuzi Serikalini;  na
      1. Rushwa ya ngono katika ajira na upandishwaji vyeo katika sekta ya elimu. 

Kutokana na kazi hizo, hatua zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kushauri mamlaka husika namna ya kudhibiti mianya ya rushwa katika maeneo hayo.

  • Warsha/vikao 161 vya wadau kujadili matokeo ya kazi za utafiti, ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma katika miradi ya maendeleo na uchambuzi wa mifumo kwa lengo la kuweka mikakati ya kudhibiti rushwa vilifanyika. Aidha, kazi 38 za ufuatiliaji wa utekelezaji wa maazimio ya kuziba mianya ya rushwa yatokanayo na vikao vya wadau zilifanyika katika maeneo mbalimbali yakiwemo: udhibiti wa rushwa ya ngono katika Chuo Kikuu cha Dodoma na utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi nchini;
    • Ufuatiliaji wa utekelezaji wa Miradi ya maendeleo 597 yenye thamani ya

Shilingi trilioni 4.7 umefanyika katika sekta za Afya, Maji, Fedha, Elimu, Kilimo, Ujenzi na Viwanda kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kama ilivyopangwa na thamani ya fedha inapatikana. Kati ya miradi hiyo, miradi 81 yenye thamani ya Shilingi bilioni 43 ilibainika kuwa na mapungufu mbalimbali katika utekelezaji hivyo watekelezaji wake walishauriwa namna bora ya kutekeleza miradi hiyo kupitia vikao kazi na      mingine inaendelea kufanyiwa

uchunguzi ili hatua stahiki zichukuliwe;

  • Elimu kuhusu madhara za rushwa na juhudi za Serikali za kudhibiti Rushwa na kupata uungwaji mkono ilitolewa kwa umma kupitia njia mbalimbali zikiwemo semina 2,178, mikutano ya hadhara/mijadala 2,269, vipindi vya redio na televisheni 278, maonesho 236 na taarifa kwa umma 56 kupitia vyombo vya habari. Aidha, habari/makala 394 ziliandaliwa kwa ajili ya wavuti na jarida la TAKUKURU;
    • Elimu kuhusu rushwa ilitolewa kwa vijana walio shuleni na vyuoni ambapo Klabu za wapinga rushwa 4,371 zilifikiwa ili kujenga kizazi cha vijana wenye maadili na wanaochukia rushwa. Aidha, Skauti wamejengewa mazingira ya kushirikishwa kwenye mapambano dhidi ya rushwa ambapo Mwongozo wa Wawezeshaji wa Kufundisha Vijana wa Skauti Kuzuia na Kupambana na Rushwa umezinduliwa na kusambazwa nchini kote kwa lengo la kuwajengea uwezo wawezeshaji wa Skauti namna ya kutoa elimu kwa vijana wa Skauti kuhusu namna ya kuzuia na kupambana na rushwa;
    • Uelimishaji Umma umefanyika kupitia mitandao ya kijamii kwa kutoa matangazo 2,415 dhidi ya rushwa yaliyoandaliwa na kusambazwa kwenye mitandao ya Twitter, Facebook na Instagram. Aidha, TAKUKURU Online TV imerusha jumla ya habari 32 na kufanikiwa kuwafikia wananchi wengi kwa gharama nafuu;
    • Kesi 865 za tuhuma dhidi ya rushwa na ufisadi ziliendeshwa mahakamani zikiwemo kesi mpya 305. Aidha, kesi 338 ziliamuliwa mahakamani ambapo kesi 191 watuhumiwa walipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo au kulipa faini na kesi 147 watuhumiwa wake hawakupatikana na hatia na kuachiwa huru. Kesi 527 bado zinaendelea mahakamani KIAMBATANISHO NA. 1

Uk. 137; 

  • Shilingi bilioni 1.42 zimeokolewa kutokana na operesheni mbalimbali za uchunguzi uliofanyika kote nchini. Aidha, Taasisi kwa kushirikiana na mamlaka nyingine imewezesha kutaifisha na kurejesha Serikalini fedha na mali zenye thamani ya Shilingi bilioni 6.3 na dola za kimarekani 1,468,364 ambazo zinahusisha fedha, nyumba tano (5), viwanja sita (6) na magari saba (7);
  • Mapitio ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007 yamefanyika katika ngazi mbalimbali za maamuzi na kuainisha mapungufu ya kisera yanashughulikiwa na Ofisi ya Rais kama msimamizi wa Sera na mengine yanafanyiwa kazi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Sheria inahuishwa ili iendane na hali ya sasa ya kiuchumi na kijamii pamoja na dhamira ya Serikali ya kudhibiti rushwa nchini;
  • Mfumo wa TEHAMA wa ndani ya TAKUKURU umeimarishwa   kwa kuunganisha Ofisi mpya za makao makuu zilizopo eneo la Nanenane na

Area D katika jiji la Dodoma kwenye mtandao wa Taasisi. Aidha njia za mawasiliano katika mikoa 28 na wilaya 13 zimeboreshwa kwa lengo la kurahisisha mtiririko mzuri wa majalada, upatikanaji wa takwimu na mawasiliano kutoka ngazi za Wilaya, Mikoa na Makao Makuu. Vile vile, mfumo wa masijala wa kielektroniki wa Ofisi (e-Office) ambao unaboresha utendaji kazi ndani ya Taasisi umewekwa na kuanza kutumika;  

  • Watumishi   wa TAKUKURU      406 wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kuongeza weledi wa kutekeleza majukumu kwa ufanisi; 
  • Kazi ya ujenzi wa Ofisi ya TAKUKURU Makao Makuu Dodoma umefikia asilimia 38 mbapo kazi inayoendelea ni ufungaji wa maboksi ya mbao (form work) kwa ajili ya kumwaga zege ghorofa ya kwanza;
  • Taratibu za kuwapata wakandarasi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya Ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Kilimanjaro, Morogoro na Iringa na Wilaya za Mvomero, Kilolo, Kongwa, Liwale na Kiteto zimekamilika; na
  • Taratibu za kuwapata wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa ukuta katika Ofisi za

TAKUKURU Wilaya ya Chamwino, Ruangwa na ujenzi wa karakana ya magari, Dodoma zimekamilika. 

C. TAASISI YA UONGOZI

24. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya UONGOZI imeendelea kuwa Kituo cha utaalam wa hali ya juu cha kuendeleza Viongozi Barani Afrika kwa kuanzia na Tanzania, Ukanda wa Afrika Mashariki na hatimaye Afrika kwa ujumla. Walengwa ni Viongozi Waandamizi waliopo na wanaojitokeza wakiwemo wanasiasa, watumishi wa Serikali na Mahakama. Katika kipindi cha mwezi Julai, 2021 hadi Machi, 2022 kazi zifuatazo zilitekelezwa:-

  • Kozi 46 za muda mfupi zimetolewa kwa viongozi 2,759 wakiwemo Mawaziri na Manaibu Waziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Uongozi ya Bunge

la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Maafisa Waandamizi na Makamanda wa

Mikoa wa Jeshi la Polisi la Tanzania, Maafisa Maandamizi wa Mamlaka ya Kodi Tanzania. Utekelezaji huu ni zaidi ya lengo la kutoa kozi fupi 14  kwa sababu ya ongezeko la mahitaji ya mafunzo;

  • Maafisa Waandamizi 43 kutoka Wizara, Taasisi na Mashirika ya Umma, Taasisi za Kiraia na Taasisi Binafsi wamepatiwa mafunzo katika ngazi ya stashahada ya uzamili. Mafunzo yalihusu moduli saba ambazo ni Ujuzi wa Fedha kwa

Watendaji, Uongozi wa Matokeo, Ubunifu, Maendeleo Endelevu, Usimamizi wa Rasilimali watu wa Kimkakati, Mawasiliano ya Kimkakati na Maadili. Moduli hizi zilitolewa kama ilivyopangwa. Mafunzo hayo ni ya awamu ya tano ya Programu ya Stashahada ya Uzamili inayoendeshwa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Aalto cha nchini Finland;

  • Maafisa Waandamizi 85 kutoka Wizara, Taasisi na Mashirika ya Umma, Taasisi za Kiraia na Taasisi Binafsi wamepatiwa mafunzo katika ngazi ya cheti ikiwa ni utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Programu ya Uongozi ngazi ya Cheti inayotolewa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Aalto cha nchini Finland;
  • Mikutano mitatu (3) ya kitaifa iliyohusu masuala ya uongozi na maendeleo endelevu iliandaliwa kama ilivyopangwa. Mikutano hiyo ilihudhuriwa na viongozi 1,157 wakiwemo Viongozi wa Umma,

Vyuo Vikuu, Taasisi za Utafiti, Taasisi za Kiraia, Taasisi Binafsi, viongozi wastaafu, wanazuoni na wanafunzi wa vyuo vikuu;

  • Utafiti tumizi ulifanyika katika maeneo matatu kati ya manne yaliyopangwa kufanyika kwa mwaka. Utafiti huu

ulihusu:-

  • Tathmini ya utekelezaji wa dhana ya ushiriki wa watanzania kwenye miradi ya kimkakati na matokeo yake nchini Tanzania;
    • Tathmini ya utekelezaji wa sheria kuu mbili za kimkakati ambazo ni Sheria ya Mamlaka ya Nchi Kuhusiana na Umiliki wa Maliasili ya Mwaka 2017;

na Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu Masharti Hasi katika

Mikataba Inayohusu Maliasili ya Mwaka 2017; 

  • Tathmini ya athari za kimazingira na za kijamii zinazotokana na ujenzi wa Reli ya Kisasa kipande cha tano kutokea Mwanza mpaka Isaka.
  • Vipindi vinne (4) vya mahojiano na viongozi waandamizi na wataalam vilindaliwa kama ilivyopangwa. Mahojiano hayo yanahusu masuala ya Uchumi wa kijani Barani Afrika, Ujumuisho katika masuala ya Fedha Barani Afrika, Uchumi wa Buluu na Nishati Mbadala. Vipindi hivi vilirushwa kwenye runinga na kuwekwa kwenye tovuti ya Taasisi ya UONGOZI na mitandao ya kijamii kwa lengo la kubadilishana taarifa, maarifa na uzoefu. Vipindi hivi vinaonekana Bara zima la

Afrika; 

  • Ushauri wa kitaalamu ulitolewa kwa TASAF katika kupitia Mpango Mkakati wa Pili. Aidha, Taasisi kwa kushirikiana

na Ofisi ya Waziri Mkuu imeratibu na kushiriki kuandaa Mwongozo wa

Kutengeneza Sera Nchini; 

  • Kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kushirikisha umma katika kujadili masuala      ya   Uongozi      na Maendeleo endelevu; na
  • Machapisho saba juu ya masuala ya Uongozi na Maendeleo Endelevu yameandaliwa na kutolewa.

D. MPANGO WA KURASIMISHA RASILIMALI

NA BIASHARA ZA WANYONGE TANZANIA (MKURABITA)

25. Mheshimiwa Spika, Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) umeendelea kutekeleza jukumu la kuandaa na kusimamia mfumo wa kitaifa wa umiliki wa rasilimali na uendeshaji wa Biashara nchini unaotambulika na kukubalika kisheria. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, MKURABITA imetekeleza kazi zifuatazo:-

  • Vituo Jumuishi vitano vya Urasimishaji na Uendelezaji Biashara vimeanzishwa  katika Mamlaka za Serikali za Mitaa za  Shinyanga, Moshi, Tarime,  Rungwe na Sumbawanga kwa kufanya ukarabati wa majengo katika maeneo hayo;
  • Urasimishaji na uendelezaji biashara umefanyika kwa kutoa mafunzo ya Urasimishaji wa Biashara kwa wafanyabiashara 2,042 katika Manispaa za Shinyanga (1095) na Moshi (947). Aidha, Wafanyabiashara 1,210 wamesajili biashara zao na kuanza kufanya biashara katika Mfumo rasmi, Wafanyabiashara 470 wamefungua akaunti za benki na Wafanyabiashara 255 wamejiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii;
  • Ujenzi wa Masjala 12 za Ardhi za Vijiji umekamilika katika Mamlaka saba za Serikali za Mitaa ambazo ni Masasi (2), Newala (2), Chamwino (1), Moshi (2),

Meru (2), Mbarali (1), Itigi (1) na Nachingwea (1). Ujenzi wa Masjala 10 za Ardhi za  Vijiji umefikia katika hatua za umaliziaji  katika  Mamlaka  za Serikali za Mitaa za Kibiti (1), Mvomero

(1), Nachingwea (1), Sumbawanga (1),

Makete (2), Kalambo (1) na Mwanga (3) 

  • Urasimishaji wa Waendesha Bodaboda umefanyika kwa kutoa mafunzo kwa Waendesha Bodaboda 3,993 katika Halmashauri tatu za Jiji la Dodoma (2,639), Manispaa za Shinyanga (605) na Moshi (749). Kati ya hao waliopata mafunzo, Waendesha Bodaboda 2,720 wamepata leseni za usafirishaji na udereva ambapo Jiji la Dodoma ni 1,650, Manispaa za Shinyanga ni 350 na Moshi ni 720. Aidha, jumla ya mikopo ya Shilingi 841 imetolewa kwa Waendesha Bodaboda 909 ambapo shillingi Milioni 554 zimetolewa na Halmashauri zao kutoka fungu la asilimia 10 kwa Vijana na Shilingi milioni 287 zimekopeshwa  na Benki za CRDB na NMB;
  • Hatua za awali za uanzishwaji wa vituo jumuishi viwili vya urasimishaji wa biashara katika Wilaya ya Kusini – Unguja na Chakechake – Pemba zimefanyika ili kupata maeneo kwa ajili ya uanzishwaji wa vituo husika. Aidha, jumla ya wafanyabiashara 50 wamepata mafunzo na kusajili biashara zao;
  • Mafunzo kuhusu fursa na matumizi ya kiuchumi ya Hati za Haki Milki za Kimila yametolewa kwa wakulima 2,400 wa mashamba yaliyorasimishwa katika Halmashauri za Wilaya za Mufindi (395), Kilolo (220), Sikonge (507), Butiama (210), Moshi (706), Rufiji (147) na Kibiti (215). Aidha, mafunzo kwa wakulima 58 wa jamii ya kifugaji yametolewa na mizinga 30 ya nyuki imetolewa;
  • Urasimishaji wa ardhi mijini umefanyika kwa kuandaa Hati miliki 3,083 katika Mamlaka 4 za Serikali za Mitaa za Chamwimo, Babati, Tunduma,   na

Makete. Aidha, jumla ya Hati Miliki 1,152 katika Halmashauri za  Chamwimo (328), Babati (120), Tunduma (338) na Makete (366) ziko tayari kutolewa kwa wananchi;

  • Ufuatiliaji na Tathmini ya shughuli za urasimishaji ardhi umefanyika Tanzania Bara katika Halmashauri za Jiji la Arusha, Wilaya za Makete, Momba, Kiteto, Meru na Halmashauri za Mji mdogo wa Tandala na Tunduma, wilaya ya Uyui na manispaa yaTabora kwa lengo la kubaini matokeo na vikwazo vya uendelevu wa urasimishaji ardhi na biashara  kwenye Halmashauri hizo. Aidha, kwa upande wa Zanzibar, ufuatiliaji na tathmini umefanyika katika

Wilaya sita za Wete, Mkoani, Chakechake, Mjini, Magharibi A na Magharibi B kwa nia ya kubaini upatikanaji wa mikopo kwa kutumia fursa za urasimishaji wa ardhi na biashara; na 

  • Vipindi 14 vya redio na runinga kuhusu utekelezaji wa shughuli za urasimishaji vimezalishwa na kurushwa hewani kupitia TBC Taifa na TBC1. Aidha, baadhi ya taarifa na maudhui ya vipindi vilivyozalishwa yameendelea kutolewa kwa njia ya runinga kupitia baadhi ya vipindi vya taarifa za habari ikiwemo ARIDHIO na vipindi vya Harakati.

E. MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII

(TASAF)

26. Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Maendeleo ya

Jamii umeendelea kutekeleza Awamu ya Tatu ya TASAF kwa kuyapa kipaumbele maeneo ya Ukuzaji wa uchumi na kupunguza umaskini wa kipato; Kuinua ubora wa maisha na ustawi wa jamii; na Utawala bora na uwajibikaji. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Mfuko wa Maendeleo Jamii (TASAF) umetekeleza kazi zifuatazo:-

  • Uhakiki wa awali wa Kaya umefanyika katika Mamlaka 186 za utekelezaji. Jumla ya Kaya 886,724 zilihakikiwa  ambapo kaya 781,342 zimekidhi vigezo vya uhakiki wa awali wa kuendelea kuwepo katika Kipindi cha Pili cha Mpango na kaya 105,382 zimeboreka kiuchumi ambapo zimepewa muda wa kujiandaa ili kutoka kwenye mpango na kujitegemea kiuchumi;
  • Utambuzi na uandikishaji wa kaya maskini kwa Vijiji/Mitaa/Shehia ambazo hazikufikiwa na Mpango wa Kipindi cha Kwanza umefanyika na umekamilika katika Mamlaka zote 186 ambapo Mitaa/Vijiji/Shehia 7,217 vimefikiwa na jumla ya Kaya 602,672 zimetambuliwa. Kati ya hizo, Kaya mpya 498,091 ziliandikishwa na hivyo kufanya Mpango kuwa na Kaya za Walengwa 1,279,325;
  • Ruzuku ya Shilingi bilioni 213 ilihawilishwa kwa kaya 1,279,325 zilizokidhi vigezo vya kuingia katika Kipindi cha Pili cha Mpango kutoka maeneo yote ya utekelezaji 184 kwa Tanzania Bara na Pemba na Unguja kwa Zanzibar.  Maelezo ya mgawanyo wa Ruzuku hiyo yapo katika KIAMBATANISHO NA. 2 Uk. 138 – 148; 
  • Miradi 2,674 ya Kutoa Ajira za Muda kutoka katika mamlaka za utekelezaji 51 imeibuliwa na jamii. Miradi hii ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na inatoa Ajira ya Muda kwa kaya 253,117. Kufikia Machi, 2022, jumla ya Shilingi bilioni 16.14 zimeshalipwa kwa Walengwa kama Ujira. Pia mafunzo ya usimamizi wa miradi yamefanyika kwa wawezeshaji 1,399 kutoka mamlaka 51 za utekelezaji zinazotekeleza miradi kwa mwaka 2021/2022. Mgawanyo wa Miradi hiyo imeoneshwa katika KIAMBATANISHO

NA. 2 Uk. 138 – 148;

  • Miradi 550 imeandaliwa na kutekelezwa ambapo miradi mitatu (3) kati ya hiyo yenye thamani ya Shilingi 321.21 milioni imekamilika wakati mingine 547 yenye thamani ya Shilingi bilioni 16.0 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Miradi hiyo itawezesha upatikanaji wa huduma za elimu, afya, maji, mazingira, barabara za vijijini na miradi ya ujasiriamali kwa wananchi wanaoishi maeneo husika. Aidha, jumla ya wataalam 120 kutoka mamlaka 44 za utekelezaji wamepatiwa mafunzo ya uwezeshaji na usimamizi wa miradi. Maelezo zaidi yapo katika KIAMBATANISHO NA. 2 Uk. 138 – 148;
  • Jumla ya Vikundi 2,385 viliundwa vyenye wanachama 30,255 (wanawake 26,977 na wanaume 3,278), kwenye mamlaka 10 za utekelezaji. Wawezeshaji 269 walipatiwa mafunzo ya uundaji wa vikundi vya Kuweka Akiba na Kuwekeza. Mafunzo yamefanyika kwa wawezeshaji 59 wa kitaifa yanayohusu uhamasishaji na uundaji wa vikundi, uwekaji kumbukumbu za taarifa za fedha, usimamizi wa mikopo na utatuzi wa migogoro. Kiasi cha Shilingi bilioni 2.25 kama ruzuku ya vikundi imetolewa kwa walengwa 4,884 wa mamlaka za utekelezaji za Bagamoyo na

Chalinze kwa ajili ya miradi ya ujasiriamali;

  • Idadi ya mamlaka za utekelezaji zilizoingizwa katika malipo ya njia ya Kielektroniki imeongezewa hadi kufikia mamlaka za utekelezaji 122.  Njia hii ya malipo inawezesha fedha kutumwa moja kwa moja kwa Mlengwa kupitia mitandao ya simu, Benki kwa namba ya NIDA) na kumfikia kwa haraka na kupunguza gharama za uendeshaji. Asilimia 19 ya walengwa katika maeneo hayo wameanza kupokea fedha kwa njia ya kielektroniki na uhamasishaji unaendelea ili kuandikisha walengwa zaidi kutumia mfumo huu wa malipo; 
  • Mifumo    ya   Teknolojia, Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ya utunzaji wa kumbukumbu za walengwa, uendeshaji na utoaji taarifa iliendelea kuboreshwa na kuimarishwa. Mfumo wa kuwasilisha na kupokea malalamiko umeendelea kutumika katika maeneo yote ya utekelezaji. Mifumo ya TASAF imeunganishwa na mifumo mingine ya kitaifa kama vile NIDA na Malipo ya Serikali Mtandao (Government Electronic Payment Gateway – GePG). Aidha, utengenezaji wa Mfumo wa Ukusanyaji wa Taarifa za Walengwa kwa kutumia vifaa vya kidijitali ‘tablets’’ ili kuondokana na matumizi ya karatasi ulikamilika na kutumika kwenye uhakiki na utambuzi wa kaya. Mfumo huu ni rahisi na unapunguza gharama za ukusanyaji na uingizaji wa takwimu;
  • Tathmini ya msingi ya Kipindi cha Pili cha Mpango imefanyika katika Maeneo ya Utekelezaji 32 ambapo Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (OCGS) zilihusika. Aidha, tafiti mbalimbali zimefanyika na kuonesha jinsi Mpango unavyowanufaisha walengwa ambapo jumla ya Shilingi bilioni 3.5 zimetumika kwa kazi hizo; na
  • Mapitio ya pamoja ya Timu ya Serikali na Wadau wa Maendeleo kuhusu utekelezaji wa shughuli za Mpango yamefanyika katika vipindi vitano vya Julai, 2021 mpaka Februari, 2022. Taarifa zote za mapitio zimeonesha utekelezaji wa Mpango unaendelea vizuri na unawasaidia walengwa kuondokana na umaskini na kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kuwaendeleza watoto katika afya na elimu bora. Wadau wa Maendeleo wameahidi kuendelea kushirikiana katika utekeleza wa mpango. Aidha, wadau hao wameahidi kushirikiana na Serikali katika kuongeza muda wa utekelezaji kwa miaka miwili ili kufidia muda uliopotea kutokana na kuchelewa kuanza kwa utekelezaji.

F. WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI

  • Mheshimiwa Spika, Wakala ya Ndege za Serikali ina jukumu la kutoa huduma ya usafiri wa anga kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Viongozi wengine Wakuu wa Kitaifa. Wakala ilianzishwa ili kuboresha huduma na kuimarisha usalama wa usafiri wa ndege kwa viongozi wanaotumia huduma hizo. 
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Wakala wa Ndege za

Serikali ilitekeleza kazi zifuatazo:

  • Ukarabati na upanuzi wa karakana ya Ndege za Serikali awamu ya kwanza katika Uwanja wa Ndege Julius Nyerere umefikia asilimia 60 na kazi itakamilika ndani ya mwaka huu wa fedha 
    • Huduma za usafiri wa anga zimetolewa kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa;
    • Gharama za bima za ndege pamoja na bima za Wanaanga zililipwa; 
    • Wakala imeendelea kuratibu ununuzi wa ndege na kusimamia mikataba ya ukodishwaji wa Ndege za Serikali kwa Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL);
    • Matengenezo makubwa ya Ndege mbili aina ya Gulfstream 550  na Fokker 50 zinazowahudumia Viongozi Wakuu wa Kitaifa yamefanyika kwa mujibu ya kalenda ya matengenezo iliyotolewa na watengenezaji; na
    • Mafunzo ya kisheria kwa wanaanga 31 yamefanyika ili kuhuisha leseni zao. 

OFISI YA RAIS, SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ilitengewa Shilingi  9,216,921,000.00. Kati ya fedha hizo Shilingi 7,366,921,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 1,850,000,000.00 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Hadi kufikia mwezi Machi, 2022 kiasi cha Shilingi 5,273,418,955.38 kimepokelewa na kutumika. Kati ya fedha hizi, Shilingi 5,198,908,955.38 ni kwa ajili yaMatumizi ya Kawaida na Shilingi 74,510,000.00 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Sekretarieti ya Maadili ya

Viongozi wa Umma ilitekeleza shughuli zifuatazo:- (i) Matamko ya viongozi wa Umma kuhusu rasilimali na madeni yapatayo 14,020 kati ya 15,522 yamepokelewa ikiwa ni sawa na asimilia 90.3 ya matarajio hadi kufikia Desemba, 2021;

  • Malalamiko 115 ya ukiukwaji wa maadili dhidi ya Viongozi wa Umma yalipokelewa na kuchambuliwa. Kati ya malalamiko hayo, malalamiko 66 yalihusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na malalamiko 49 hayakuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma hivyo

yalipelekwa kwa taasisi husika;

  • Uhakiki wa matamko ya rasilimali na madeni kwa Viongozi wa Umma na mgongano wa masilahi umefanyika kwa viongozi 425. Kati yao, viongozi wanaume ni 302 na wanawake ni 123. Kati ya viongozi waliohakikiwa asilimia 11 ya viongozi walibainika kuwa na dosari katika matamko. Aidha, viongozi asilimia moja watafanyiwa uchunguzi wa kina na viongozi ambao tuhuma zitathibitika watafikishwa kwenye Baraza la Maadili;
  • Elimu kwa Viongozi wa Umma 3,180, Watumishi wa Umma 5,629 na Wananchi 1,386 kuhusu jinsi ya kujiepusha na mgongano wa masilahi na kuishi kwa

kuzingatia kiapo cha Ahadi ya Uadilifu;

  • Klabu 143 za Maadili zenye wanachama 4,000 zilianzishwa katika shule za msingi na sekondari. Klabu 33 zilitembelewa kwa lengo la kukuza na kuendeleza maadili miongoni mwa wanafunzi na wanachama wa klabu. Lengo la klabu hizi ni kukuza na kuendeleza vijana katika kuzingatia maadili na kujiandaa kuwa Viongozi wa kesho;
  • Mapitio ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 yamefanyika katika ngazi mbalimbali za maamuzi na yanafanyiwa kazi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali; na
  • Ujenzi wa jengo la Ofisi ya Makao Makuu na Kanda ya Kati Dodoma la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma umefikia hatua ya ghorofa ya tano ambayo ni sawa na asilimia 55.

OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA NA TAASISI ZAKE

A.  MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2021/2022, Fungu 32 Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma: inayojumuisha taasisi zilizo chini yake iliidhinishiwa jumla ya Shilingi 45,869,114,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizi, Shilingi   

38,219,114,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 7,650,000,000 kwa ajili yaMiradi ya Maendeleo.

  • Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Machi, 2022 kiasi cha Shilingi 33,727,642,021.89 kimepokelewa na kutumika. Kati ya fedha hizo Shilingi  30,664,972,854.79 zilikuwa kwa ajili ya

Matumizi ya Kawaida na Shilingi 3,062,669,167.10 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

  • Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na Taasisi zake imeendelea kutoa huduma kwa kuzingatia misingi ya utawala bora. Aidha, watumishi wa Umma wanawajibika na kutekeleza majukumu yao ya msingi kwa bidii, uadilifu, weledi na maarifa na kwa kuzingatia Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo na Taratibu.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Machi, 2022 Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na Taasisi zake ilitekeleza shughuli zifuatazo:-
    • Ujenzi wa Mfumo mpya wa Usimamizi wa Utendaji Kazi kwa Watumishi wa Umma (PEPMIS) umeanzishwa ili kuondokana na changamoto za usimamizi wa utendaji kazi zilizojitokeza katika utekelezaji wa mfumo wa awali wa OPRAS, ambao haukuakisi hali halisi ya utendaji kazi wa watumishi hali iliyoleta hisia za kupendeleana au kuoneana na kutokutumika kwa matokeo ya utendaji kazi katika kufanya maamuzi ya kiutumishi. 

Mfumo mpya wa PEPMIS utakuwa ni wa kielektroniki na utaondokana na matumizi ya makaratasi. Pia utaongeza uwazi katika usimamizi wa watumishi na kuondoa upendeleo na uonevu katika upimaji wa utendaji wa watumishi. Utaweka mifumo ya ufuatiliaji wa utendaji kazi wa watumishi kwa kuzingatia malengo yaliyowekwa na yanayopimika. Mifumo huu pia utahamasisha uwajibikaji wa hiari na kurahisisha upatikanaji wa taarifa za utendaji kazi wa watumishi;

  • Ujenzi wa Mfumo mpya wa Usimamizi wa Utendaji kazi katika ngazi ya Taasisi (PIPMIS) umeanzishwa. Mfumo huu ni makubaliano ya kimaandishi kati ya Serikali na Taasisi ya Umma kuhusu malengo ambayo Taasisi husika itayatekeleza katika kipindi cha mwaka mmoja. Makubaliano hayo yatakuwa kati ya viongozi wakuu wa Taasisi na Viongozi wao wanaowasimamia katika masuala ya kisera na utendaji wa kila siku.  Malengo yaliyomo ndani ya mikataba yatakuwa na vigezo, shabaha na viashiria vitakavyotumika katika utendaji wa taasisi kila mwaka. Utekelezaji wa Mfumo wa PIPMIS utaongeza uwajibikaji katika utekelezaji wa sera, mikakati na vipaumbele vya taasisi, sekta na taifa kwa ujumla; kuimarisha utamaduni unaojali matokeo; na kuleta matumizi bora ya rasilimali za umma.  Manufaa haya yatatokana na kuwepo kwa vigezo na viashiria vya kupima utendaji wa taasisi katika maeneo hayo, kulinganisha na kushindanisha utendaji wa taasisi na kutoa Tuzo za utendaji mzuri kila mwaka;  
    • Maelekezo ya Rais kuhusiana na utendaji wenye matokeo katika sekta ya Umma yametekelezwa kwa kuanza kuandaa Mifumo mipya miwili ambayo ni PEPMIS na PIPMIS kwa lengo la kuimarisha dhana ya utendaji unaojali matokeo; kutoa huduma bora kwa wananchi; na kuongeza uwajibikaji wa viongozi na watumishi katika Taasisi za Umma;
    • Mfumo wa Tathmini ya Hali ya Rasilimaliwatu katika taasisi za umma umesanifiwa, umejengwa na kuanza kutumika mwezi Machi, 2022 katika kukusanya, kuhakiki na kuonesha mgawanyo na mtawanyiko wa watumishi ili kubainisha mahitaji ya watumishi kwenye  taasisi  zote za umma;
    • Mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Malipo ya Mishahara (HCMIS) yamefanyika kwa Maafisa

Masuuli; Wakuu wa Idara za Utawala/Utumishi; Maafisa

Utumishi/Utawala; Wakaguzi wa Ndani na Wahasibu;

  • Uhakiki wa watumishi kwenye Taasisi za Umma 150 pamoja na usafishaji na uboreshaji wa taarifa za kiutumishi na mishahara kwenye Mfumo wa HCMIS umefanyika ili kuhakikisha kunakuwa na matumizi bora ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma;
    • Usimamizi wa Mfumo mpya wa HCMIS umefanyika katika Taasisi 541 ambazo zimeanza kutumia mfumo huo na kuhakikisha huduma za mfumo zinapatikanaji wakati wote. Vile vile, watumiaji wapya 558 kutoka katika Taasisi 241 walisajiliwa kwenye mfumo; 
    • Maafisa    TEHAMA    na Maafisa wanaoshughulikia malalamiko 675 kutoka taasisi zilizo Kanda ya Kaskazini, Nyanda za Juu Kusini, Magharibi, Kati, Ziwa na Kanda ya Kusini wamepatiwa mafunzo ya utekelezaji wa mfumo wa kidijitali wa e-

Mrejesho    na Sema   na Waziri   wa UTUMISHI;

  • Uimarishaji na uboreshaji wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA umefanyika ili kurahisisha utendaji kazi na utoaji wa huduma. Vile vile, ununuzi wa vitendea kazi na mahitaji muhimu ya TEHAMA ikiwemo mifumo, programu, kompyuta, printa, skana, simu, umefanyika ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya matumizi bora na salama ya mifumo na vifaa vya TEHAMA;
    • Uhuishaji wa Mkakati wa Taifa wa Serikali

Mtandao wa Mwaka 2021-2026 unaendelea ambapo rasimu ya mkakati imekamilika na hatua za mwisho za uidhinishaji zinafuatiliwa. Vile vile, rasimu ya kwanza ya Mkakati wa Serikali wa Kujilinda na Majanga ya Kimtandao ya Mwaka 2017 imeandaliwa na kukamilika. Ukusanyaji wa maoni kutoka kwa wadau ili kuboresha Mkakati huu unaendelea;

  • Uratibu wa uanzishwaji wa Vituo 3 vya Huduma Pamoja (One Stop Centres) umefanyika ambapo Vituo 2 vya Huduma Pamoja vimeanzishwa katika Ofisi za Shirika la Posta Dar es Salaam na Dodoma. Vile vile, Mwongozo wa kusimamia utekelezaji wa Mradi wa Huduma Pamoja umeandaliwa na kuanza kutumika mwezi Desemba, 2021. Mwongozo huo umeainisha majukumu ya wadau muhimu katika mradi huo;
    • Uratibu wa uanzishwaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali umefanyika ambapo nyaraka zote za Mradi zimekamilika na mradi umeanza kutekelezwa mwezi

Septemba, 2021. Utekelezaji wa maeneo ya mradi yanayohusu masuala ya Serikali Mtandao unaendelea kuratibiwa;

  • Watumishi 190,781 wenye sifa stahiki wamepandishwa vyeo/madaraja;
    • Madeni ya mishahara ya Watumishi wa Umma 65,394 yenye thamani ya Shilingi 91,087,826,006.34 yamelipwa;

(xv) Watumishi       wa Umma 19,386 wamebadilishwa kada; (xvi) Vibali vya ajira mpya na mbadala kwa nafasi 12,336 vimetolewa;

  • Taasisi za Umma 42 zimewezeshwa kuandaa Mipango ya Rasilimaliwatu, Taasisi 44 zimewezeshwa kuandaa Mipango ya Urithishanaji Madaraka na Taasisi 8 zimewezeshwa kuandaa Mipango ya Mafunzo ili kuhakikisha wanakuwepo watumishi wa umma wenye sifa stahiki na weledi katika nafasi zote kwenye utumishi wa umma; 
  • Miundo ya Wizara 22 na Taasisi za Umma 28 imekamilishwa na kuidhinishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwasilishwa kwenye Wizara na Taasisi husika kwa ajili ya utekelezaji. Vile vile, Miundo ya Taasisi 35 imechambuliwa na imepitishwa   na Kamati ya      Rais     ya

Utekelezaji (PIC) na kuwasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya kupata idhini ya utekelezaji. Aidha, uchambuzi wa miundo ya Taasisi 80 umefanyika na ipo kwenye hatua ya kujadiliwa kwenye vikao vya Kamati ya Rais ya Utekelezaji (PIC) na miundo ya Wizara tatu zilizofanyiwa marekebisho inafanyiwa mapitio ili kukidhi mabadiliko ya hati idhini; (xix) Mapitio ya Sheria na Miongozo ya Kiutumishi yamefanyika kwa lengo la kuboresha utendaji kazi pamoja na kutoa miongozo ya kuimarisha Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Shughuli hizo zilihusisha ukamilishaji wa marekebisho ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003; Kutafsiri Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2009 kutoka lugha ya Kiingereza kwenda lugha ya Kiswahili; Uandaaji wa Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na. 2 kuhusu Utaratibu wa Matumizi, aina na Stahili za Magari kwa Viongozi katika Utumishi wa Umma; na Waraka wa Utumishi Na. 1 wa mwaka 2022 kuhusu Utaratibu wa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma kuhudhuria Vikao vya Menejimenti za Wizara Mama; 

  • Marekebisho ya Kanuni za Kudumu Katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2009 yamefanyika na mchakato wa tathmini ya Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma ya Mwaka 2008

umeanzishwa; 

  • Masharti ya kazi ya viongozi wa umma walio katika nafasi za kisiasa yameandaliwa na kutolewa; 
  • Taasisi 20 za Umma zimefanyiwa ufuatiliaji wa namna ya kutekeleza miongozo ya anuai za jamii mahali pa kazi. Aidha, imeandaliwa Rasimu ya Mwongozo wa ujumuishaji wa masuala ya jinsia katika Utumishi wa Umma; 
  • Taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Afrika wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala (The African Charter on Values and Principles of Public Service and Administration) imeandaliwa;
  • Sera za Usimamizi wa Rasilimali watu katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) zimepitiwa na kuhuishwa; 
  • Miundo ya Maendeleo ya Utumishi ya Kada mbalimbali zilizo chini ya Wizara 22 na Wakala za Serikali na Mashirika ya Umma 47 imehuishwa;
  • Utawala   wa Utumishi     wa Umma umeendelea kufanyika    kwa      kuchakata mahitaji ya vibali kwa Waajiri na watumishi mbalimbali ikiwemo vibali vya uhamisho (4,405), kushikizwa (36), kuazimwa (1,490) na vibali (384)  vya likizo bila malipo;
  • Uwianishaji na uoanishaji wa mishahara na mipango ya motisha katika Utumishi wa Umma    umeendelea      kufanyika    ikiwemo kuandaa Mwongozo wa Posho na Masilahi katika Utumishi wa Umma kwa lengo la kuoanisha masilahi katika utumishi wa Umma na kuhuisha Miundo ya Mishahara ya Wakala za Serikali na Mashirika ya Umma 47;
  • Maombi   ya   vibali     mbalimbali yameshughulikiwa ikiwemo vibali 959 vya uteuzi ili kujaza nafasi za uongozi, vibali 830 vya kukaimu nafasi za uongozi na vibali 665 vya ajira za mikataba, ili kuimarisha uwepo wa viongozi wenye sifa stahiki, weledi na maono ya utumishi wa umma pamoja na

kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi;

  • Taasisi    za   Umma 16 zimewezeshwa kuandaa Mahitaji ya Watumishi wa Umma ili kupata uwiano mzuri wa watumishi katika kutekeleza majukumu ya Taasisi husika;
  • Upatikanaji wa fursa za mafunzo 216 ya muda mrefu na mfupi zinazotolewa na Wadau wa Maendeleo umeratibiwa kwa lengo la kuwaongezea watumishi wa umma ujuzi na maarifa katika utekelezaji wa majukumu. Kati ya fursa hizo, nafasi za mafunzo 67 ni za mafunzo ya muda mrefu kutoka Jamhuri ya Watu wa China, nafasi 24 kutoka Serikali ya Korea na nafasi za mafunzo 125 ni za mafunzo ya muda mfupi kutoka Serikali ya Korea, Malaysia, Thailand na China;
  • Utoaji wa mafunzo elekezi kwa Viongozi 59 ambao ni Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa ya Tanzania Bara umeratibiwa ili kuwajengea uwezo katika usimamizi na utoaji wa maamuzi ya kimkakati;
  • Usimamizi wa Mikataba ya Ushirikiano wa Kimataifa       na Kikanda      umefanyika ili kuhakikisha kuwa watumishi wa umma wanapata fursa za ajira katika taasisi ambazo Tanzania ni mshirika.  Nafasi 13 za ajira kutoka Jumuiya ya Madola, UNEP, UNWTO, ICGRL, SADC, AFDB na nafasi katika Jopo la Wataalamu wa Umoja wa Mataifa kushughulikia masuala ya Sudan zilipokelewa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kutangazwa ili watanzania wenye sifa waweze kuomba;
  • Uratibu na ufuatiliaji wa ajira za wageni katika Utumishi wa Umma na Miradi ya Kimkakati umefanyika ambapo vibali 391 vyenye msamaha wa ada vimetolewa kwa wataalam wa kigeni kufanya kazi katika Utumishi wa Umma na Miradi mbalimbali ya kimkakati;
  • Watumishi wa Umma 1,772 kutoka Taasisi za Umma 38 wamejengewa uelewa kwa kupatiwa mafunzo kuhusu Uzingatiaji wa Maadili ya Utendaji kazi katika Utumishi wa Umma;
  • Taasisi za Umma 15 zimefanyiwa ufuatiliaji wa uzingatiaji wa maadili ya Utendaji kazi katika Utumishi wa Umma. Pia, Mfumo wa Ushughulikiaji wa Malalamiko ya Wananchi katika Utumishi wa Umma umefuatiliwa;
  • Kampeni za uimarishaji wa uzingatiaji wa maadili kwenye taasisi za umma na vyama vya Kitaaluma zimefanyika kupitia Kikao

kazi ambapo walishiriki 40 kutoka taasisi za Umma walihudhuria;

  • Wananchi      wamehabarishwa    kuhusu huduma zitolewazo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na namna ya upatikanaji wake ambapo taarifa 72, matukio 447 katika picha, makala fupi za mwendo (Video clips)

                                  114,      makala       mbili      za       mwendo

(documentary) na nakala 27 za Gazeti la Serikali zenye taarifa za kiutumishi zilitolewa kwa umma kupitia magazeti, televisheni, redio, mitandao ya kijamii ya watu binafsi, mitandao ya kijamii ya ofisi na tovuti ya ofisi;

  • Ujenzi wa jengo la ghorofa  tano la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora umeanza na umefikia hatua ya ghorofa ya tatu; na
  • Huduma zimeendelea     kutolewa     kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa (Wastaafu 11 na wajane 7) kwa mujibu wa sheria.

B. CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA (TPSC)

  • Mheshimiwa Spika, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kilianzishwa ili kutoa mafunzo, ushauri, kufanya utafiti tumizi na kutoa machapisho mbalimbali katika nyanja za Uongozi, Menejimenti na Utawala. Chuo kinaendesha mafunzo ya muda mfupi kwa Watumishi wa Umma yanayolenga kuwajengea uwezo katika nyanja za utawala, usimamizi wa utendaji kazi za kila siku, menejimenti pamoja na uongozi. Mafunzo hayo hutolewa katika hatua ya awali kwa watumishi wapya wa umma, (induction) hatua ya kati kwa Maafisa Waandamizi na Maafisa Wakuu, hatua ya juu kwa  Viongozi wa Umma wanaochipukia na mengine kulingana na mahitaji ya wadau wa Chuo. Mafunzo yote hayo yanalenga kuboresha utendaji kazi katika utumishi wa umma ili kuleta tija na ufanisi katika huduma zinazotolewa kwa umma. Vile vile, Chuo kinasaidia Serikali kukuza Sera za Utamaduni wa kujifunza na kusaidia utumiaji wa teknolojia miongoni mwa watendaji katika kutekeleza majukumu yao.
  • Mheshimiwa Spika, Chuo kinatoa mafunzo ya muda mrefu katika ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada katika nyanja za Utunzaji wa Kumbukumbu, Uhazili, Menejimenti ya Rasilimaliwatu, Ununuzi na Ugavi, na Utawala wa Umma. Chuo cha Utumishi wa Umma ndicho chuo pekee hapa nchini kinachotoa shahada ya

Uhazili.

  • Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza majukumu yake Chuo kina Kampasi sita zilizoko kwenye Mikoa ya Dar es Salaam, Tabora, Mtwara, Singida, Tanga na Mbeya. Pia, Chuo kinatoa huduma za mafunzo kwa njia ya mtandao kupitia kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao kilichopo Dar es Salaam – TPSC Global Learning Centre (TGLC).
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022 shughuli zifuatazo zimetekelezwa: 

(i) Watumishi wa Umma 1,102 walipatiwa mafunzo ya kujiandaa kufanya Mitihani ya Utumishi wa Umma hiyo ni sawa na asilimia

157 ya Watumishi waliolengwa; 

  • Watumishi wa Umma 5,722 wamepatiwa mafunzo yahusuyo Uongozi na Maendeleo; pamoja na Manejimenti na Usimamizi wa Ofisi katika Taasisi za umma, sawa na asilimia 78 ya lengo la mwaka. Kati yao watumishi 4,398 walipatiwa mafunzo kwa njia ya ana kwa ana na watumishi 1,024 walipatiwa mafunzo kwa njia ya mtandao; 
  • Mafunzo ya Awali yalitolewa kwa Watumishi wa Umma wapatao 721 sawa na asilimia 28 ya lengo la mwaka, pia hamasa kwa waajiri ilitolewa kwa waajili kuwasisitiza kupeleka watumishi kupata mafunzo ya awali mara baada ya kuajiriwa;
  • Wanafunzi 10,598 walidahiliwa katika ngazi ya Shahada ya Kwanza, Stashahada na Cheti, kwa ajili ya mafunzo ya muda mrefu katika fani za utunzaji wa kumbukumbu, uhazili, TEHAMA, utunzaji wa fedha za umma, na Menejimenti ya Rasilimaliwatu, usimamizi wa ununuzi wa umma, uongozi na utawala bora; 
  • Maandiko ya ushauri katika maeneo tano ya kitaalamu yameandaliwa na kuwasilishwa kwa wateja. Aidha, shauri katika maeneo matano ya kitaalam katika Menejimenti ya Utumishi wa Umma  sawa na asilimia 83 ya lengo ulitolewa;
  • Watumishi 40 wa Chuo cha Utumishi wa Umma wamewezeshwa kujenga uwezo katika taaluma mbalimbali, kama ifuatavyo: Shahada ya uzamivu 5, Shahada ya uzamili

6 na mafunzo ya muda mfupi watumishi 29; 

  • Ujenzi wa majengo katika Kampasi ya Singida awamu ya kwanza unaohusisha ujenzi wa Maabara za Kuchapa (Typing Labs) umefikia asilimia 55. Mradi huu utakamilika kufikia Juni 30, 2022. Mradi wa Tanga utaanza baada ya taratibu za umilikishaji wa eneo kukamilika. Aidha, mradi wa ujenzi wa katika Kanda ya Ziwa utaanza baada ya miradi ya Singida na Tanga kumamilika;na
  • Maeneo ya ujenzi wa Kampasi za Dodoma, Tanga na kanda ya ziwa yamepatikana na taratibu za umilikishwaji wa maeneo husika zinaendelea. Aidha, ufuatiliaji wa upatikanaji wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kampasi ya Mbeya unaendelea.

C. MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (eGA)

  • Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), ilianzishwa kwa Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya Mwaka 2019. Mamlaka ilianzishwa ili Kuratibu, Kusimamia na Kukuza jitihada za Serikali Mtandao pamoja na kuhimiza utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao kwa taasisi za umma. Mamlaka imerithi iliyokuwa Wakala ya Serikali Mtandao ambayo iliundwa kwa Sheria Na. 30 ya Wakala za Serikali, Sura ya 245 ya Mwaka 1997 na kuwa na jukumu la Kuratibu, Kusimamia na Kukuza Jitihada za Serikali Mtandao nchini bila kuwa na nguvu ya kisheria ya kuhimiza utekelezaji (kuwa chombo rekebu). Wakala ilitekeleza majukumu yake kwa kipindi cha miaka nane tangu kuzinduliwa kwake Mwezi Aprili, 2012 mpaka Mwezi Machi, 2020.
  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Julai 2021, hadi Machi, 2022, Mamlaka imetekeleza majukumu yake kama ifuatavyo:
  • Mfumo maalum (Government Enterprise Service Bus, GovESB) wa kuwezesha mifumo ya Serikali kusomana na kubadilishana taarifa umesanifiwa, umejengwa na taasisi 12 zimeunganishwa.  Pia, mpango kazi wa kuziunganisha Taasisi zote za Serikali zenye mifumo umeandaliwa. Aidha, viwango na miongozo imeandaliwa kuwezesha ubadilishanaji wa taarifa kuwa endelevu, wenye tija na usalama wa taarifa; 
  • Mifumo ya kidijitali ya kurahisisha utoaji huduma kwa umma kupitia sekta mbalimbali imesanifiwa na kujengwa kwa kushirikiana na Taasisi husika, baadhi ya mifumo hiyo ni: 
    • Mfumo wa kusimamia vyama vya ushirika – Tume ya Ushirika:  Lengo la mfumo huu ni kusimamia usajili na uendeshaji wa shughuli za vyama vya ushirika nchi nzima;
    • Mfumo wa Kusimamia Shughuli za Mamlaka za Maji – Wizara ya Maji: Lengo la mfumo huu wa pamoja ni kusimamia ankara za maji za wateja, malipo na maeneo yote yanayohusu mteja wa maji. Mamlaka za maji 71 kati ya 94 zinautumia mfumo huo.

Taasisi 26 zilizobaki zitaunganishwa na mfumo huo ndani ya Mwaka wa

Fedha 2022/2023; 

  • Mfumo wa Kuratibu Vibali vya Kazi nje ya nchi – Wizara ya Kazi: Lengo la mfumo huu ni kuratibu vibali vya kufanya kazi nje ya nchi;
    • Mfumo wa Kusimamia Huduma za Wakala wa Ununuzi – GPSA: Lengo la mfumo huu ni kusimamia shughuli za usimamizi wa mafuta ya magari ya Serikali, uondoshaji wa mizigo kupitia

GPSA na ununuzi wa magari ya Serikali. Mfumo huu umeanza kutumika kuanzia tarehe 1 Machi,

2022;

  • Mfumo wa Kusimamia Stakabadhi Ghalani – Bodi ya Kusimamia

Stakabadhi Ghalani: Kuandikisha na kusimamia uendeshaji wa maghala ya mazao;

  • Mfumo wa Kupokea Mrejesho kutoka kwa wananchi – Ofisi ya Rais, Utumishi. Lengo ni kuwawezesha wananchi kuwasiliana na serikali ili kuleta malalamiko, maoni, pongezi na ushauri;
    • Mfumo wa Kusimamia Shughuli za Wasanii – BASATA na Bodi ya Filamu (Wizara ya Michezo): Lengo la mfumo huu ni kuwezesha wasanii kuwasilisha kazi zao na kupata vibali mbalimbali kutoka BASATA na Bodi ya Filamu; na
    • Mfumo wa Kusimamia Leseni za usafirishaji – LATRA: Lengo la mfumo huu ni kusimamia shughuli za LATRA katika utoaji leseni za usafirishaji n.k.
  • Tathmini za Utendaji na Usalama wa Mifumo mbalimbali ya TEHAMA kwenye Taasisi za Serikali zimefanyika, mapungufu yameainishwa na kutoa ushauri juu ya maboresho; aidha ukaguzi wa mifumo ya Serikali kama inakidhi vigezo vya viwango na miongozo imefanyika na maeneo ya kuboresha yameainishwa kwa Taasisi

husika kuyafanyia kazi;

  • Mifumo Shirikishi ya TEHAMA imesimamiwa na kuboreshwa kwa lengo la kuihuisha na kuiendeleza ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia, kuboresha usalama na kukidhi mahitaji mapya ya watumiaji, mfano: GMS, MGov, e-Office, ERMS, GePG, n.k;
  • Kusimamia, kuendesha na kuendeleza miundombinu shirikishi ya TEHAMA, mfano vituo vya kutunzia mifumo, mtandao wa mawasiliano wa Serikali (Govnet), nk; 
  • Vituo maalum vya kuhifadhi miundombinu na mifumo ya Serikali Kimtandao vimeendelea kuboreshwa ikiwa ni pamoja na kununua vifaa vinavyohitajika ili kuwezesha Government Private Cloud (GovCloud);
  • Usimamizi wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA ya Serikali iliyohifadhiwa kwenye vituo vya Serikali vya kuhifadhi taarifa za Serikali na Taasisi za Umma, ikiwa ni pamoja na  kuongeza vitendea kazi/vifaa na masafa ya Intaneti ili kuhakikisha mifumo inafanya kazi kwa usahihi, inapunguza gharama za utendaji kazi na kuboresha utoaji wa  huduma kwa Umma;
  • Uandaaji     wa Viwango     na Miongozo mbalimbali umekamilishwa ili kuiwezesha Mifumo ya TEHAMA ya kimkakati na ya kisekta kuwasiliana, pia uzingatiaji wa

Viwango na Miongozo umefuatiliwa;

  • Mafunzo ya Serikali Mtandao yametolewa kwa Viongozi, Wasimamizi wa TEHAMA na watumiaji wa huduma za Serikali Mtandao kwa Taasisi za Serikali ili kuongeza umiliki (ownership), uelewa katika kutumia TEHAMA, kuongeza ufanisi wa kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi; aidha, mafunzo yametolewa kwa watumishi wa Mamlaka ili kuwaongezea uwezo;  
  • Ushauri wa kitaalam na msaada wa kiufundi kwenye maeneo ya TEHAMA kwa taasisi za Serikali kuhusu uendeshaji wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA na utoaji wa huduma mbalimbali ulitolewa. Vile vile, ushauri kwenye Miradi ya TEHAMA ulitolewa ili miradi hiyo iweze kutoa matokeo yenye tija na inayozingatia viwango; na
  • Utafiti na ubunifu wa matumizi ya teknolojia mpya za TEHAMA katika utoaji huduma kwa umma na utendaji wa Serikali, ambapo mifumo mipya imeweza kubuniwa, mfano, mfumo wa e-Mrejesho, e-Mikutano, nk.

D. WATUMISHI HOUSING COMPANY (WHC)

41. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Julai 2021, hadi Machi, 2022, Watumishi Housing Company imetekeleza majukumu yake kama ifuatavyo:

  • Mpango umeandaliwa wa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutatua tatizo la makazi kwa watumishi kwa maeneo ya pembezoni;
  • Mfumo wa kuendesha Mfuko wa kukopesha (revolving fund) umeanza kutengenezwa na utasaidia ujenzi wa nyumba zenye gharama nafuu zitakazowanufaisha wafanyakazi wa kada zote;
  • Ujenzi wa nyumba 80 katika eneo la Njedengwa jijini Dodoma umeendelezwa; na
  • Upatikanaji wa kiwanja katika eneo la Mtumba karibu na Mji wa Serikali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 1000 za gharama nafuu umesimamiwa. Ununuzi wa viwanja namba 383, 384, 385 na 549 vyenye jumla ya mita za mraba 42,753 eneo la Chamwino – Dodoma na kiwanja namba

695 chenye ukubwa wa mita za mraba 76,774 eneo la Mtumba umefanyika. Vile vile, taarifa ya Upembuzi Yakinifu (Feasibility Study) kwa ajili ya ujenzi wa nyumba katika viwanja husika imewasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango kwa ajili ya kupata kibali cha kukopa fedha za ujenzi. 

OFISI YA RAIS, SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

  • Mheshimiwa       Spika, Ofisi     ya   Rais,

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni idara inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Kifungu 29 (1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma 

Sura  298 ili kusimamia mchakato wa ajira katika Utumishi wa Umma. Katika Mwaka wa Fedha

2021/22, Fungu 67: Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma iliidhinishiwa Shilingi 3,388,771,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Hadi kufikia Machi, 2022, Shilingi 3,238,198,766.09 zilipokelewa na kutumika.

  • Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Sekretarieti imetekeleza shughuli zifuatazo:- 
    • Michakato ya ajira ilisimamiwa ili kuwezesha waajiri kupata watumishi wenye sifa zinazotakiwa kwa mujibu wa miundo ya taasisi husika, ambapo saili 13 kwa niaba ya Mamlaka za Ajira mbalimbali zimesimamiwa na waliofaulu usaili walipangiwa vituo vya kazi. 
    • Utaalam wa masuala ya uendeshaji wa michakato ya ajira ulitolewa kwenye usaili   unaoendeshwa na Taasisi

zinazotumia Sheria zilizokasimiwa;

  • Mchakato     wa ajira      za   Muungano umeboreshwa kwa kuongeza majukumu ya kawaida na idadi ya watumishi katika Ofisi ya Sekretarieti ya Ajira iliyopo Zanzibar;
    • Ujenzi wa programu ya “Ajira Portal App” ambayo itawarahisishia waombaji kazi kupata taarifa za ajira na mrejesho wa michakato ya Ajira kupitia simu zao za kiganjani umekamilika na imeanza kutumika na kupunguza gharama za matangazo kwenye vyombo vya habari

na kuwafikia waombaji wengi kwa urahisi na uharaka; 

  • Utoaji wa elimu kwa Umma na matangazo kuhusu ajira umefanyika kupitia runinga za TBC, ITV na Azam Media, tovuti na mitandao ya kijamii. Elimu na matangazo hayo yalihusu majukumu ya Sekretarieti ya Ajira, ufafanuzi wa maswali na maoni ya wadau, uwepo wa nafasi za kazi, kuitwa kwenye usaili, kupangiwa vituo vya kazi pamoja na taarifa mbalimbali zinazohusiana na mchakato wa ajira na matumizi ya Mfumo wa maombi ya kazi;
    • Vyeti 3,328 vya waombaji kazi vilifanyiwa uhakiki kwa ushirikiano na Taasisi mbalimbali ili kubaini uhalali ambapo vyeti 3,313 kati ya hivyo vilithibitishwa  kuwa ni halali ikiwa ni sawa na asilimia 99.5 na vyeti 15 vilithibitishwa kuwa sio halali ambavyo ni sawa na asilimia 0.5 ya vyeti vilivyohakikiwa;
    • Utafiti wa kupata mrejesho wa utekelezaji wa majukumu ya  Sekretarieti ya Ajira kutoka kwa wadau wake umefanyika;
    • Vitendea kazi vinavyojumuisha magari mawili kwa ajili ya usimamizi wa saili mbalimbali zinazofanywa na Sekretarieti ya Ajira vimeongezwa. Vile vile, Huduma za kiutawala na kiutumishi kwa Ofisi ya Zanzibar zilitolewa; na
    • Ujenzi wa jengo la Ofisi za Makao Makuu ya   Sekretarieti ya   Ajira     Dodoma umeanzishwa kwa kukamilisha utafiti wa udongo na michoro. 

OFISI YA RAIS, TUME YA UTUMISHI WA UMMA

  • Mheshimiwa Spika; Tume ni chombo rekebu chenye mamlaka na wajibu wa kuhakikisha kuwa masuala ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma yanasimamiwa na kuendeshwa kwa kuzingatia Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali kama inavyotolewa na Mamlaka. 
  • Mheshimiwa Spika; katika Mwaka wa Fedha 2021/22, Tume ya Utumishi wa Umma iliidhinishiwa kiasi cha Shilingi 6,560,233,829 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Hadi kufikia Machi, 2022 kiasi cha Shilingi 5,184,280,712.96 zilipokewa na kutumika ikiwa ni matumizi ya kawaida. Katika kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Machi, 2022,  Tume imetekeleza majukumu yafuatayo:-
    • Ukaguzi wa Rasilimaliwatu kwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za

Nidhamu kwenye Taasisi 110 kati ya 150 umefanyika; 

  • Rufaa 206 zimeshughulikiwa na kutolewa uamuzi na malalamiko 125 ya Watumishi wa Umma yalihitimishwa;
    • Rufaa     90 na malalamiko nane yamechambuliwa      tayari    kuwasilishwa mbele ya Tume kwa uamuzi; 
    • Taarifa ya Hali ya Utumishi wa Umma na Utekelezaji wa Majukumu ya Tume kwa Mwaka wa Fedha 2021/22 imeandaliwa;
    • Maulizo 1,022 ya watumishi wa Umma, waajiri, mamlaka za ajira na nidhamu kuhusu      rufaa   na malalamiko yalipokelewa kwa njia mbalimbali na kushughulikiwa; 
    • Mafunzo kwa watumishi 67 wa Tume kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu uchambuzi wa rufaa na malalamiko na ukaguzi wa Rasilimaliwatu yalitolewa. Vile vile, Mafunzo ya kuwajengea uwezo Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu kuhusu uzingatiaji wa Sheria,

Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma yalitolewa kwa Taasisi tisa; 

  • Uhuishaji wa Miongozo ya Tume kuhusu uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu na kuisambaza kwa Wadau ulifanyika ambapo,   Mwongozo kuhusu ushughulikiaji wa masuala ya Nidhamu, Rufaa na Malalamiko umehuishwa; 
    • Elimu kwa wadau kuhusu Sheria, Kanuni, Taratibu, na Miongozo inayosimamia Utumishi wa Umma na kuhusu majukumu ya Tume ilitolewa kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na tovuti ambapo vipindi sita  vya Televisheni vilirushwa kupitia TBC 1, Star TV, Channel 10 na AZAM TV na vipindi vitano  vya Radio vilirushwa kupitia Magic Radio, TBC Taifa na  92.6 AFM ya Dodoma;
    • Ukarabati wa jengo la Ofisi Dodoma baada ya kuhamia makao makuu

ulifanyika; na

  • Watumishi 74 wa Tume walielimishwa kuhusu VVU/UKIMWI, Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi na Mapambano dhidi ya Rushwa. Vile vile, huduma kwa watumishi wa Tume wanaoishi na VVU/UKIMWI na watumishi wenye mahitaji maalum zilitolewa.

OFISI YA RAIS, IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

  • Mheshimiwa Spika; kwa mujibu wa Sheria ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Na. 3 ya mwaka 2002, Idara ya Kumbukumbu ya Nyaraka za Taifa ina jukumu la kusimamia na kuratibu utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo na Taratibu za utunzaji kumbukumbu na nyaraka katika Taasisi za Umma. Aidha, jukumu lingine ni kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Kuwaenzi Waasisi wa Taifa Na. 18 ya Mwaka 2004 kwa kukusanya, kutunza na kuhifadhi kumbukumbu na vitu vya Waasisi wa Taifa letu (Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume).
  • Mheshimiwa Spika; katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Ofisi ya Rais – Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa iliidhinishiwa jumla ya Shilingi 4,571,018,000.  Kati ya fedha hizo, Shilingi 2,571,018,000 nimatumizi ya kawaida na Shilingi 2,000,000,000 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Katika kipindi cha Julai, 2021 hadi Machi, 2022. jumla ya Shilingi 2,098,975,110.97 zilipokewa na kutumika. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,758,975,110.97 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 340,000,000 kwa ajili ya matumizi ya miradi ya Maendeleo.
  • Mheshimiwa Spika; kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai, 2021 hadi Machi, 2022, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa imetekeleza shughuli zifuatazo:-

(i)     Jumla ya nyaraka 3,224 zenye umuhimu katika   historia ya   Nchi     yetu zimekusanywa kutoka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 17 na Taasisi zingine za

Umma tatu. KIAMBATANISHO NA. 12

Uk. 237 – 238;

  • Jumla     ya   majalada     ya   mashauri yaliyofungwa 3,192 kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza na Kagera yamekusanywa na kuhifadhiwa katika Kituo cha Kanda ya Ziwa – Mwanza;
  • Mfumo wa masijala mtandao (e-File Management     System)     umewekwa katika Taasisi za Umma 24 na kufikia taasisi 140 tangu mfumo huu uanzishwe. KIAMBATANISHO NA. 13 Uk. 239;
  • Mfumo wa Utunzaji wa Kumbukumbu za Kiutendaji (Keyword Filing System) umewekwa katika Taasisi za Umma 27. KIAMBATANISHO NA. 14 Uk. 240;
  • Ukaguzi wa hali ya utunzaji wa kumbukumbu katika Taasisi za Umma 26 umefanyika kwa lengo la kujua hali halisi ya utunzaji wake ili kubaini changamoto wanazokabiliana nazo na kuzipatia ufumbuzi. KIAMBATANISHO NA. 15 Uk. 241;
  • Mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu yalitolewa katika Taasisi za Umma 16. KIAMBATANISHO NA. 16 Uk. 242;
  • Taasisi tatu zimewezeshwa kutengeneza mwongozo wa utunzaji na uteketezaji wa kumbukumbu      kwa      mujibu wa

Sheria.Taasisi hizo ni Shirika wa Uwakala wa Meli (TASAC), Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi ya Elimu ya Juu (HESLB),  na Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) – Lushoto; 

  • Ukarabati wa nyaraka zilizohifadhiwa katika Ghala Kuu la Taifa katika ofisi za Kanda ya Mashariki Dar es salaam umefanyika, ambapo nyaraka kongwe 61 zimekarabatiwa zikiwemo za uliokuwa utawala wa  kikoloni wa Mwingereza (33), Government gazette (15) na

Hansard (13);

  • Tathimini ya majalada ya iliyokuwa Wizara ya Ushirika na Masoko zilizohifadhiwa katika Kituo cha Taifa cha Kumbukumbu Dodoma  ilifanyika ili kubaini zile zenye umuhimu ili ziendelee kuhifadhiwa katika viwango stahiki na kubaini zile ambazo umuhimu wake wa matumizi umefika ukomo kwa mujibu wa Sheria;
  • Majalada     335       yamewekwa      kwenye mfumo wa kielekroniki (Digital Records Management and Preservation System) ili kurahisisha upatikanaji wake na kwa lengo la kulinda nakala halisi za nyaraka hizo ili ziweze kudumu kwa muda mrefu;
  • Kumbukumbu 437 za Waasisi wa Taifa (Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Sheikh         Abeid    Amani   Karume) zimetambuliwa,        kukusanywa      na

kuhifadhiwa;

  • Vipindi    viwili     vimerushwa      kupitia Televisheni ya Taifa (TBC) kuhusu majukumu mbalimbali ya Idara kwa lengo la kutoa elimu kwa umma; na
  • Uwezo wa utendaji wa watumishi wa ndani umeimarishwa, ambapo watumishi wawili waliwezeshwa kuhudhuria kongamano la Bodi ya Manunuzi na Ugavi (PSTB), mtumishi mmoja anaendelea na mafunzo ya muda mrefu katika shahada ya uzamili katika Sanaa ya Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mtumishi mmoja alihudhuria mafunzo ya viwango vya uhasibu vya sekta ya umma vya kimataifa (IPSAS) yanayotolewa na Bodi ya Wahasibu (NBAA), wahudumu watatu walihudhuria mafunzo ya uhudumu yanayotolewa na Chuo cha NIP mkoani Morogoro na Watumishi wawili walihudhuria mafunzo ya ukutubi yanayoandaliwa na Bodi ya Wakutubi Tanzania.

MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA MWAKA 2022/23 NA MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIWA

49. Mheshimiwa Spika, Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 umeandaliwa kwa kuzingatia, Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano

(2021/22 – 2025/26), unaotaka Tanzania iwe na Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu. Maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 ni nguzo muhimu ya mpango unaotarajiwa kutekelezwa. Shughuli zitakazotekelezwa na kila taasisi ni kama ifuatavyo:-

OFISI YA RAIS, IKULU NA TAASISI ZAKE A. OFISI YA RAIS – IKULU

50. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Ofisi ya Rais, Ikulu imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:-

  • Kutoa ushauri kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala ya Siasa,   Uchumi,      Jamii,   Sheria, Diplomasia, Mawasiliano na Habari, Uhusiano wa Kikanda, Kimataifa na ushauri     mwingine kwa      lengo    la

kumsaidia Rais kufanya maamuzi;

  • Kutoa ushauri kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu ratiba

ya kila siku;

  • Kutoa huduma kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na familia yake;
  • Kuratibu, kuandaa na kushiriki mikutano 60 ya Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri, mikutano 40 ya Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu (IMTC) na mikutano 20 ya Baraza la Mawaziri;
  • Kuandaa mikutano miwili ya tathmini wa mwaka kati ya Waratibu wa Shughuli za Baraza la Mawaziri     wa Wizara,

Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri na wadau wengine;

  • Kutoa mafunzo kuhusu utayarishaji na uwasilishaji wa Nyaraka za Baraza la Mawaziri na uchambuzi wa sera kwa

Maofisa wa Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri na Waratibu wa Shughuli za Baraza la Mawaziri wa Wizara;

  • Kuchambua na kutoa ushauri kwa Katibu Mkuu Kiongozi     katika   masuala      ya kiuchumi, kijamii, kisheria, kiulinzi na kiusalama, kimataifa     na masuala mengine yote yanayowasilishwa;
  • Kufanya       mafunzo     na ufuatiliaji     wa utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Awamu ya Tatu na Programu za Maboresho katika ngazi za Wizara, Mikoa na Serikali za Mitaa;
  • Kuratibu utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Awamu ya Tatu kwa kushirikisha wadau wa Sekta ya Umma na Binafsi;
  • Kuandaa na Kutekeleza Mkakati mpya wa Taifa wa Mapambano Dhidi ya Rushwa;
  • Kukamilisha tathmini ya utekelezaji wa Awamu ya Tatu  ya Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa;
  • Kupokea na kuchambua taarifa za robo mwaka za utekelezaji wa Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa na Programu nyingine za maboresho;
  • Kuendelea kujenga uwezo wa Taasisi za Umma kuhusu uzingatiaji wa utawala bora katika kutoa huduma kwa umma;
  • Kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Programu za maboresho katika ngazi za utekelezaji;
  • Kupokea, kupitia na kuchambua rufaa na malalamiko ya watumishi wa umma na wananchi;
  • Kuendesha mikutano     mitatu   ya Watendaji na Maafisa      wa Serikali kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko na rufaa pamoja na kufuatilia utekelezaji wa maagizo mbalimbali ya Katibu Mkuu Kiongozi;
  • Kufanya ziara ya ufuatiliaji wa uzingatiaji wa sheria na maelekezo yanayotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi      wa Umma yanayohusu masuala ya Usimamizi wa utawala wa Utumishi kwenye Wizara, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa; na
  • Kuratibu      na kusimamia Miradi   ya Maendeleo ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) na Programu ya Kujenga Uwezo wa Taasisi za Serikali     Kupambana      na Rushwa

(BSAAT).

  • Kuendelea na uboreshaji wa Ikulu ya Chamwino kwa      kuanza ujenzi   wa ukumbi wa mikutano (multi purpose hall) na baadhi ya ofisi; na
  • Kukarabati majengo ya Ikulu Ndogo za Mwanza, Tabora, Shinyanga, Lushoto Arusha na rest house moja Zanzibar.

B. TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA (TAKUKURU)

51. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, TAKUKURU imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:-

  • Kufanya utafiti na uchambuzi wa mifumo ya kiutendaji na utoaji huduma katika sekta za umma na binafsi ili kubaini maeneo yenye mianya ya rushwa na kushauri namna ya kuziba mianya hiyo;
  • Kufanya      warsha/vikao     vya

kuwashirikisha wadau kuweka mikakati  ya kudhibiti mianya ya rushwa na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa mikakati hiyo;

  • Kufuatilia matumizi ya fedha za umma katika utekelezaji wa miradi   ya maendeleo ili kuhakikisha utekelezaji wake unazingatia thamani halisi ya fedha;
  • Kutekeleza Mkakati wa Mawasiliano wa TAKUKURU ili kujenga uwezo na uelewa kuhusu rushwa, ufisadi na juhudi za Serikali katika kupambana na rushwa kwa makundi mbalimbali katika jamii

kwa kutumia njia mbalimbali za mawasiliano kuyashawishi makundi haya kuunga mkono na kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa nchini;

  • Kutumia      njia       za   mawasiliano      za kimkakati kulifikia kundi la vijana ili washiriki katika shughuli zinazowajenga kimaadili na kushiriki kupambana na rushwa ili kuwa na jamii inayochukia rushwa;
  • Kutumia      vyombo      vya       habari   na mitandao ya kijamii kubeba agenda ya mapambano      dhidi     ya   rushwa ili kuushirikisha umma katika mapambano hayo;
  • Kukamilisha uchunguzi wa majalada ya tuhuma za rushwa unaoendelea pamoja na tuhuma  mpya zitakazojitokeza;
  • Kuhuisha    Sheria ya   Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007;
  • Kuimarisha mfumo wa TEHAMA katika taasisi ili kurahisisha na kuwezesha mtiririko mzuri wa majalada, takwimu na mawasiliano kutoka ngazi za wilaya, mkoa na makao makuu; na
  • Kutoa mafunzo ya weledi kwa watumishi ili kuongeza ufanisi. Kujenga karakana kwa ajili ya kutengeneza magari ya taasisi     ili kupunguza gharama     za uendeshaji zinazotumika     katika kutengeneza magari hayo;
  • Ujenzi wa majengo ya Ofisi za Mikoa ya Simiyu na Iringa, Ofisi za Wilaya za Momba na Nyasa  pamoja na Safe house moja Dodoma;
  • Ujenzi wa uzio katika Ofisi nne za

                                                Wilaya      ya      Mpwapwa,       Masasi,

Namtumbo na Bahi; na

  • Kufanya ukarabati mkubwa wa Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Dodoma, Ofisi za

Mkuu    wa TAKUKURU      Mkoa    wa Mwanza na Ofisi     ya   Mkuu    wa

TAKUKURU Wilaya ya Chato.

C. TAASISI YA UONGOZI

52. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya UONGOZI itaendelea kujengea uwezo viongozi ili kuongeza tija katika utekelezaji wa kazi zao kwa kupitia mafunzo na semina katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Taasisi ya UONGOZI imepanga

kutekeleza kazi zifuatazo:-

  • Kutekeleza programu maalum ya mafunzo ya uongozi kwa Bodi za Mashirika ya Umma, Taasisi na Wakala wa Serikali kwa lengo la kuimarisha usimamizi na utendaji wa mashirika. Mafunzo haya yatatolewa kwa Bodi 40;
  • Kutoa mafunzo ya Stashahada ya Uzamili ya Uongozi kwa lengo la kuwajengea uwezo Viongozi 35 katika maeneo ya kufanya maamuzi ya kimkakati, kusimamia rasilimaliwatu na rasilimali nyingine na kuimarisha sifa binafsi za kiongozi;
  • Kutoa mafunzo ya Cheti ya Uongozi kwa njia ya mtandao kwa Viongozi 50;
  • Kutoa mafunzo ya muda mfupi kupitia kozi 30 kwa lengo la kuwajengea uwezo Viongozi 750 katika maeneo ya Uongozi

na Maendeleo Endelevu, kutokana na mahitaji na maombi ya walengwa;

  • Kutekeleza programu maalum ya mafunzo ya Uongozi kwa wanawake viongozi waandamizi na viongozi wanaochipukia 40 kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi ya kimkakati, usimamizi wa rasilimali za Serikali na rasilimali watu. Vile vile mafunzo haya yanalengo la kukuza vipaji vya uongozi kwa viongozi wanawake wanaochipukia;
  • Kuandaa mikutano sita ya kitaifa katika masuala ya uongozi na maendeleo endelevu kwa viongozi 440;
  • Kufanya tafiti tumizi nne kuhusu masuala ya uongozi na maendeleo endelevu; 
  • Kuandaa vipindi nane vya runinga vitakavyoshirikisha viongozi waandamizi na wataalam mbalimbali ndani na nje ya nchi, juu ya Uongozi na Maendeleo Endelevu. Vipindi hivi vitarushwa kwenye runinga, tovuti na mitandao ya kijamii na kuonekana katika Bara zima la Afrika;
  • Kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kushirikisha umma katika kujadili masuala ya Uongozi na Maendeleo endelevu;
  • Kutoa machapisho 16 juu ya masuala ya Uongozi na Maendeleo Endelevu ikiwepo Tawasifu ya Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya kwanza ya Uongozi;
  • Kutoa ushauri wa kitaalam katika maeneo yanayohusu masuala ya

Uongozi na Maendeleo Endelevu; na

  • Kuandaa michoro ya majengo na maandalizi ya awali ya ujenzi wa Kituo cha mafunzo katika Kijiji cha Kondo, Bagamoyo.

D. MPANGO WA KURASIMISHA RASILIMALI NA BIASHARA ZA WANYONGE TANZANIA (MKURABITA)

53. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, MKURABITA imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:

  • Urasimishaji na Uendelezaji wa Biashara 7,000 Katika Mamlaka 7 za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara ambazo ni Temeke, Ilemela, Sumbawanga, Korogwe, Karagwe, Bunda na Mafinga. Aidha, Urasimishaji na uendelezaji wa biashara utafanyika katika  wilaya mbili za Zanzibar;
  • Kurasimisha na kukamilisha uandaaji Hati miliki za ardhi na kuzitoa kwa wananchi katika Mamlaka Tano za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara za Kondoa, Kiteto, Newala. Nachingwea, Mwanga na Moshi. Aidha, kwa upande wa Zanzibar

urasimishaji utafanyika katika Wilaya sita;

  • Kujengea      uwezo wananchi    3,000 waliorasimisha rasilimali na biashara kwa kuwapa mafunzo     ya   umuhimu    wa matumizi ya Hati katika Mamlaka 6 za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara za Kondoa, Kiteto, Newala, Nachingwea, Mwanga na Moshi;
  • Kuanzisha Studio ya Matangazo ambayo itawezesha uandaaji na urushaji wa matangazo ya utekelezaji wa shughuli za MKURABITA katika Radio, Runinga na

Mitandao ya Kijamii;  

  • Kufanya ufutiliaji       na Tathimini     ya utekelezaji wa shughuli za urasimishaji ardhi na biashara katika Mamlaka 19 za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara ambazo ni Aidha, kwa upande wa

Zanzibar, ufuatiliaji na Tathmini utafanyika katika wilaya 6;

  • Kuboresha Vitendea kazi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za urasimishaji na uendeshaji wa ofisi ambapo ununuzi wa

gari moja na vitendea kazi vingine 

utafanyika; 

  • Kuwezesha mafunzo ya muda mfupi kwa watumishi wa MKURABITA ili kuongeza ujuzi na maarifa katika utendaji wa kazi;
  • Kurasimisha mashamba ya wakulima wa  Alizeti katika  Mamlaka 3 za Serikali  za

Mitaa za Iramba, Chemba na Kondoa 

kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa alizeti ili kuongeza mchango wa Alizeti katika upatikanaji wa mafuta nchini; 

  • Kujenga Vituo Jumuishi 5 vya Urasimishaji na uendelezaji wa biashara katika Mamlaka 5 za Serikali za Mitaa za Kigamboni, Bunda, Mpanda, Karagwe na Tunduma ambavyo vitawezesha huduma za urasimishaji kupatikana katika jengo moja; na
  • Kujenga Masjala 3 za za Ardhi za Vijiji katika Mamlaka 2 za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara ambazo ni Chemba, na Iramba. Kwa upande wa Zanzibar, itajengwa Masjala moja ya ardhi katika wilaya moja.

E.   MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII (TASAF)

54. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, TASAF imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:-

  • Kufanya zoezi la Utambuzi wa Kaya 186,500 kwenye Mamlaka 142 za utekelezaji ambazo zimeachwa katika Vijiji/Mitaa/Shahia kwa sababu mbalimbali;
  • Kufanya zoezi la kuhakiki na kutambua hali za ustawi wa maisha ya Kaya za Walengwa wa Mpango zipatazo 713,350 iwapo zimeimarika kiuchumi kwa kutumia vigezo vya umaskini na utaratibu

uliokubaliwa kitakwimu;

  • Kuendelea kuhawilisha ruzuku kwa kaya maskini 1,279,325 zilizokidhi vigezo vya kuingia katika kipindi cha Pili cha Mpango;  
  • Kuwezesha utekelezaji wa Miradi ya Jamii ya Kutoa Ajira ya Muda kwa Kaya Maskini katika mamlaka za utekelezaji 123. Jumla ya miradi 6,900 ya Jamii na ya Kutoa Ajira za Muda itatekelezwa katika ngazi ya Vijiji/Mitaa/Shahia 6,500 na inategemewa kutoa ajira za muda kwa Walengwa

550,000; 

  • Kuwezesha Jamii kutekeleza miradi ya kuendeleza miundombinu ya huduma za jamii katika sekta mbalimbali. Jumla ya miradi 515 itatekelezwa katika Vijiji/Mitaa ya Mamlaka za Utekelezaji 43. Miradi ya mingi itakuwa katika sekta za afya, elimu , maji, mazingira na ujasiriamali;
  • Kuwezesha uundaji wa Vikundi vya Kuweka Akiba na Kuwekeza katika mamlaka za utekelezaji 82. Jumla ya Vikundi 24,000 vya jamii vya Kuweka Akiba na Kuwekeza vyenye wanachama takribani 240,000 vinatarajiwa kuundwa katika Mamlaka 82 za Utekelezaji kwa mwaka 2022/2023. Aidha, Walengwa 50,000 kutoka mamlaka za utekelezaji 20 waliokamilisha mipango yao ya biashara inayokidhi vigezo vilivyowekwa watapatiwa Ruzuku ya Uzalishaji mali ili kutekeleza mawazo yao ya biashara zao; 
  • Kuongeza maeneo ya utekelezaji  39 yatakayoshiriki malipo kwa njia ya mtandao. Jumla ya mamlaka za utekelezaji 186 zinatarajiwa kukamilisha taratibu na kuingia katika malipo kwa njia ya mtandao (Benki na mitandao ya simu) kwa mwaka 2022/2023 na hivyo kukamilisha utekelezaji kwa kuziingiza Mamlaka zote za Utekelezaji nchini katika malipo ya mtandao;
  • Kuimarisha   Usimamizi, Ufuatiliaji     na tathmini ya shughuli za Mpango pamoja na matumizi ya rasilimali ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji katika ngazi zote za utekelezaji wa Mpango; na
  • Kufanya Mapitio ya pamoja baina ya Timu ya Serikali na Wadau wa Maendeleo kuhusu   utekelezaji wa shughuli      za Mpango.

F. WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI

  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Wakala ya Ndege za Serikali imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:-
    • Kutoa huduma ya usafiri wa anga kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa;
    • Kuratibu ununuzi pamoja na kusimamia mikataba ya ukodishaji wa ndege kwa Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL);
    • Kulipia gharama za bima za ndege pamoja na wanaanga; 
    • Kugharamia uendeshaji wa Ofisi na kulipia gharama za mafuta ya ndege; 
    • Kufanya matengenezo makubwa ya Ndege aina ya Gulfstream 550     inayohudumia Viongozi Wakuu kwa mujibu ya kalenda ya matengenezo

inayotolewa na mtengenezaji; 

  • Matengenezo makubwa ya injini (Engine overhaul) ya akiba ya ndege aina ya Fokker 50;
    • Ukarabati na upanuzi karakana ya Ndege za Serikali iliyopo katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere awamu ya pili; na
    • Kutoa mafunzo ya kisheria kwa wanahewa kwa ajili ya kuhuisha leseni zao.
  • Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza Mpango wa Mwaka wa Fedha wa 2022/23, Fungu 20 Ofisi ya Rais, Ikulu inaomba kiasi cha Shilingi 29,828,203,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Aidha, Fungu 30: Ofisi ya Rais na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri inaomba kiasi cha Shilingi 741,299,267,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizi, Shilingi 577,206,673,000 niMatumizi ya Kawaida na Shilingi 164,092,594,000 kwa ajili yaMiradi ya Maendeleo.

SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeweka vipaumbele vikuu viwili ambavyo ni kuongeza matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma kwa Taasisi na kwa wananchi ili kuweza kuwafikia kwa urahisi; na pili ni kuimarisha uwajibikaji wa pamoja miongoni mwa viongozi wa umma hasa katika suala la viongozi kukinzana kunakopelekea shughuli za maendeleo kutotekelezeka kwa wakati. Kada za viongozi zitakazojumuishwa katika eneo hili litajumuisha Wakuu wa Idara na Madiwani kutoka katika baadhi ya Halmashauri na kupatiwa mafunzo husika. Kupitia vipaumbele hivyo shughuli zifuatazo zimepangwa kutekelezwa: 
    • Kupokea Tamko la Viongozi wa Umma kuhusu Rasilimali na Madeni kwa viongozi wapatao 15,522 linalopaswa kutolewa kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa

Umma;

  • Kupokea malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa

wananchi;

  • Kuchunguza tuhuma yoyote ya kuvunjwa kwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma dhidi ya Viongozi wa Umma;
    • Kufanya uhakiki wa matamko ya Rasilimali na Madeni kwa Viongozi wa Umma 2,000;
    • Kuratibu na kuwezesha utekelezaji wa majukumu ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma;
    • Kuelimisha Viongozi wa Umma na Wananchi kwa ujumla kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Hati ya Ahadi ya Uadilifu;
    • Kuandaa Taarifa ya Mwaka ya Utekelezaji wa shughuli za Sekretarieti na kuiwasilisha kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; 
    • Kuanzisha na kuendeleza Klabu za Maadili katika shule na vyuo nchini; na
    • Kuendelea na kukamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu na ile ya Kanda ya Kati Jijini Dodoma pamoja na Kuanza ujenzi kwa kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Ziwa.
  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetengewa Shilingi  12,730,049,000.00. Kati ya fedha hizo Shilingi 9,260,049,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 3,470,000,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo. 

OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA TAASISI ZILIZO CHINI YAKE 

59. Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Fungu 32, katika Mwaka wa Fedha 2022/23 itaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kuhakikisha kuwa Utumishi wa Umma unaendeshwa kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na kwamba Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu mbalimbali za Utumishi wa Umma zinazingatiwa.  Aidha, Ofisi itahakikisha inasimamia Utawala wa Utumishi wa Umma, mikataba ya utendaji kazi Serikalini, Orodha ya Mishahara katika Utumishi wa Umma na Maadili ya watumishi wa Umma.

Pia, itahakikisha mipango na uendelezaji rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma inafanyika kwa ubora zaidi. Kwa kuzingatia pia kuwa Serikali imeingia awamu nyingine, Ofisi itaandaa na kusimamia miundo, mifumo ya utendaji kazi na uboreshaji wa utoaji huduma wa Utumishi wa Umma  pamoja na kuhakikisha kunakuwa na uwajibikaji na uwazi. Ofisi pia, itasimamia utendaji kazi na uendelezaji wa rasilimaliwatu katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya

Utumishi wa Umma. Kwa nafasi yake kama wizara mama, Ofisi itasimamia taasisi, programu na miradi iliyo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

A. MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

60. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:

  • Kukamilisha ujenzi wa Mfumo mpya wa Utendaji kazi na Upimaji kwa Watumishi wa Umma (Public Employees’ Performance Management Information System – PEPMIS) na kuzijengea uwezo taasisi za umma katika kutumia mfumo huu ili kuimarisha Usimamizi na Uwajibikaji wa Watumishi wa Umma;
  • Kukamilisha marekebisho ya Mfumo wa Utendaji kazi na Upimaji wa Taasisi za Umma kupitia mikataba ya utendaji kazi (Public Institutions Performance Management Information System – PIPMIS) na kuzijengea uwezo taasisi za umma wa kutumia mfumo huu ili kuimarisha Uwajibikaji wa Viongozi wa Taasisi za Umma; 
  • Kusimamia utekelezaji wa mfumo mpya wa HCMIS katika taasisi 600 za Serikali kwa kutoa huduma za usaidizi za TEHAMA;
  • Kuimarisha na kuboresha miundombinu ya TEHAMA kwa ajili ya kuwezesha utendaji kazi wa mifumo na watumiaji wa mifumo;
  • Kusimamia, kufanya  ukaguzi wa usalama na ufanisi, kuendeleza, kujenga uwezo na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa mifumo ya TEHAMA ya HCMIS, PEPMIS, PIPMIS, e-HRP, Sema na Waziri wa UTUMISHI, eMrejesho, UTUMISHI Call Centre,

Biometric Attendance, Watumishi Portal na Staff Assessment katika Taasisi zote za Umma;

  • Kufanya tathmini ya utekelezaji wa sheria na miongozo ya Serikali Mtandao katika

taasisi za Serikali;

  • Kuendelea na hatua za kuhuisha Mkakati wa Taifa wa Serikali Mtandao na Mkakati wa Serikali wa Kujikinga na Majanga ya Mtandao;
  • Kuendelea na uratibu wa ukamilishaji  wa kituo  kimoja cha  Huduma Jamii (One Stop Centres);
  • Kuratibu utekelezaji wa mradi wa Tanzania ya Kidijitali (Digital Tanzania) eneo la Serikali Mtandao; 
  • Kusimamia na kuwezesha Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kutekeleza majukumu yake
  • Kuendelea kuziwezesha Taasisi za Umma kuandaa Mipango ya Rasilimaliwatu, Mipango ya Urithishanaji Madaraka na Mipango ya Mafunzo ili kujenga misingi ya utekelezaji wa usimamizi wa Rasilimaliwatu utakaohakikisha kuwa wanakuwepo watumishi wa umma wenye sifa stahiki na weledi katika nafasi zote kwenye utumishi wa umma (Meritocracy) katika muda wa kati na muda mrefu;
  • Kuendelea na maandalizi ya Mwongozo wa

                                  Kitaifa     wa     Kuandaa      Mpango       wa

Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma;

  • Kuratibu upatikanaji wa fursa za mafunzo zitolewazo na washirika wa maendeleo kwa ajili ya kuwajengea uwezo na ustadi watumishi wa Umma ndani na nje ya nchi;
  • Kuratibu utoaji wa  mafunzo kwa viongozi  katika utumishi wa umma ili kuwajengea uwezo katika usimamizi na utoaji wa maamuzi ya kimkakati;
  • Kusimamia Mikataba ya Ushirikiano wa Kimataifa na Kikanda ili kuhakikisha kuwa watumishi wa umma wanapata fursa za ajira katika taasisi ambazo Tanzania ni mshirika; 
  • Kuratibu na kufuatilia ajira za wageni katika utumishi wa umma na miradi ya kimkakati ili kuhakikisha       pia kuwa    wazalendo wanapata     fursa     ya   kujifunza     kama waambata kwa wataalamu hao wa kigeni;
  • Kusimamia na kuwezesha Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kutekeleza majukumu yake;
  • Kutoa mafunzo kwa watumiaji wa Mfumo wa Utumishi/Watumishi Mtandao; 
  • Kusimamia zoezi la Tathmini ya hali ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma kwa kutumia mfumo uliojengwa kwa ajili ya kukusanya, kuchakata na kuainisha mahitaji halisi ya watumishi kwenye Taasisi za Umma;
  • Kuendelea kutoa mafunzo ya namna ya kutumia Mfumo mpya wa HCMIS kwa Maafisa Utumishi/Tawala na viongozi wa Taasisi za Umma;
  • Kuendelea na uidhinishaji wa taarifa za kiutumishi na mishahara kwenye Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na  Malipo ya Mishahara katika utumishi wa umma;
  • Kufanya uhakiki wa watumishi kwenye Taasisi za Umma ili kuhakikisha kunakuwa na matumizi bora ya Rasilimaliwatu katika

Utumishi wa Umma sambamba na kusafisha na kuboresha taarifa za kiutumishi na mishahara kupitia Mfumo wa HCMIS;

  • Kujenga uwezo wa Maafisa TEHAMA na maafisa wanaoshughulikia    malalamiko katika Utumishi wa Umma kutumia Mfumo wa Kidijitali wa Kushughulikia Malamiko ya

                                  Wananachi    uitwao    Sema    na      Waziri

Utumishi/e-Mrejesho;

  • Kusimamia ajira za watumishi wa umma kwa kuajiri watumishi wapya 30,000 katika kada mbalimbali ambao wataigharimu Serikali kiasi     cha       Shilingi

120,776,130,000. Vile vile, utekelezaji wa zoezi la kuwapandisha vyeo watumishi 120,210 ambao watalipwa kiasi cha Shilingi 42,395,425,000 na watumishi 8,080 waliotengewa nafasi za kubadilishwa vyeo ambao wataigharimu Serikali kiasi cha Shilingi 2,211,098,663 katika Mwaka wa Fedha 2022/23 kulingana na maelekezo yatakayotolewa; 

  • Kuchambua na kuhakiki      madai   ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma kwa kadiri yatakavyowasilishwa. Aidha, kiasi cha Shilingi 103,883,257,000 kimetengwa kwa ajili ya malipo ya madai yatakayoidhinishwa; 
  • Kukagua na kuidhinisha watumishi wapya wanaostahili kuingizwa katika Orodha ya Malipo ya Mishahara;
  • Kutoa vibali vya ajira mpya na mbadala ili kujaza    nafasi   stahiki   kwenye       taasisi mbalimbali za Umma;
  • Kuwezesha Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali na Mashirika ya Umma kuandaa Orodha ya Kazi na Maelezo ya Kazi ili kupata uwiano mzuri wa watumishi katika kutekeleza majukumu ya Taasisi husika;
  • Kuendelea na uboreshaji wa michakato ya utoaji huduma na kuimarisha usimamizi wa Mifumo na Viwango vya utendaji kazi kwa kufanya ufuatiliaji pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam katika Taasisi za Serikali ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi;
  • Kuendelea na ukamilishaji wa Mfumo Jumuishi wa Ufuatiliaji     na Tathmini Serikalini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ambao utaunganisha Mifumo ya Ufuatiliaji na Tathmini iliyopo katika  Taasisi zote za Umma;
  • Kufanya Tathmini ya kina ya Utendaji kazi wa Wakala za Serikali ili kubaini utekelezaji wa malengo ya dhana ya uanzishaji wa Wakala hizo katika Utumishi wa Umma;
  • Uwezeshaji wa uandaaji na uhuishaji wa Miundo ya Maendeleo ya Utumishi katika Utumishi wa Umma; 
  • Kuwianisha na kuoanisha mishahara na mipango ya motisha katika Utumishi wa Umma; 
  • Kusimamia utawala wa utumishi wa umma kwa kushughulikia mahitaji ya vibali vya uhamisho, kushikizwa, kuazimwa na likizo bila malipo kwa watumishi na baina ya waajiri mbalimbali katika Utumishi wa Umma;
  • Kuimarisha uwepo wa viongozi wenye sifa stahiki, weledi na maono ya utumishi wa umma wenye kuzingatia dira ya maendeleo na mikakati mbali mbali ya kitaifa kwa kupokea na kushughulikia mapendekezo ya nafasi za uteuzi, mikataba ya ajira na vibali vya kukaimu nafasi za uongozi kadiri maombi hayo yatakavyokuwa

yanawasilishwa na waajiri mbalimbali;

  • Kuimarisha upatikanaji wa taarifa (Kanzi data) za Viongozi wa Serikali waliopo kwenye nafasi na wanaoonesha mwelekeo na uwezo wa kukidhi uteuzi katika nafasi za uongozi; ili kuwa na viongozi wenye kukidhi matarajio ya utumishi wa umma na

watanzania; 

  • Kujenga uwezo wa Taasisi za Serikali katika kuandaa     Sera     za   Kisekta zinazozingatia utafiti ili kuziwianisha na kuondoa migongano na urudufu wakati wa utekelezaji; 
  • Kufanya mapitio ya Sheria na Miongozo ya Kiutumishi kwa lengo la kuboresha utendaji kazi pamoja na kutoa miongozo ya kuimarisha Menejimenti ya Utumishi wa Umma kupitia nyaraka za kiutumishi;
  • Kuendeleza ufuatiliaji na uhamasishaji wa ujumuishwaji wa masuala ya Anuai za Jamii katika   Utumishi     wa Umma ili kuhakikisha kuwa makundi yote yanapata huduma zinazozingatia   usawa. Aidha, maandalizi ya Mwongozo wa ujumuishaji

wa masuala ya jinsia katika Utumishi wa Umma yataendelezwa;

  • Kuendelea na uhamasishaji  wa uzingatiaji wa maadili kupitia vyombo vya habari na kuelimisha watumishi wa Umma na waajiri kuhusu umuhimu wa kupunguza malalamiko ya wateja na kushughulikia ipasavyo malalamiko yanayowasilishwa; 
  • Kuendelea kujenga uelewa wa wadau kuhusu Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma;
  • Kuendelea na ufuatiliaji wa uzingatiaji wa maadili   katika   Wizara,       Idara

Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na taasisi nyingine za umma;

  • Kukamilisha utafiti wa uzingatiaji wa maadili katika utumishi wa umma (Public Service Integrity Survey) kwa nia ya kubaini kiwango cha uzingatiaji wa maadili na kutoa ushauri wa uboreshaji unaozingatia

taarifa sahihi za utafiti;

  • Kuendelea na kampeni za uimarishaji wa uzingatiaji wa maadili kwenye taasisi za umma;
  • Kuendelea kuhabarisha wananchi kuhusu huduma zitolewazo na Ofisi na namna ya upatikanaji wake kupitia njia mbalimbali za mawasiliano ikiwemo magazeti, redio, runinga, tovuti, mitandao ya kijamii, Gazeti la Serikali, majarida, vipeperushi na vitabu, mikutano ya wadau na semina; 
  • Kuratibu       maandalizi ya   Mradi    wa Kuboresha Utoaji Huduma katika sekta ya umma chini ya Shirika la Maendeleo la Dunia (UNDP);
  • Kuendeleza ujenzi wa jengo la Ofisi la ghorofa tano la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika eneo la Mtumba – Dodoma; na
  • Kuendelea kutoa huduma kwa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu (Viongozi 11 na wajane saba) kwa mujibu wa sheria. 

B.   CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA (TPSC)

61. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23 Chuo cha Utumishi wa Umma kimepanga kutekeleza shughuli zifuatazo: 

  • Kutoa mafunzo ya kujiandaa kufanya mitihani ya Utumishi wa Umma kwa watumishi 950  ili kuwajengea uwezo wa utendaji kazi na kutoa huduma bora kwa wananchi; 
  • Kutoa mafunzo ya Uongozi na Maendeleo, Menejimenti na Usimamizi wa ofisi kwa watumishi wa umma 5,315 ili kuendeleza stadi, weledi na ujuzi katika maeneo hayo. Vile vile, mafunzo hayo yatatolewa kwa njia ya mtandao kwa Watumishi wa Umma

2,500; 

  • Kutoa Mafunzo ya Awali katika Utumishi wa Umma kwa Watumishi wa Umma 4,800  ili kujenga uelewa wa kitendaji wa Serikalini kwa waajiriwa wapya; 
  • Kuwezesha midahalo kwa washiriki wa ndani na nje ya nchi wapatao 800  ili kupunguza gharama za serikali kupeleka watumishi nje ya nchi na kubadilishana uzoefu wa kitaalam; 
  • Kutoa mafunzo ya muda mrefu kwa washiriki 13,025 katika fani za Utunzaji wa Kumbukumbu, Uhazili na Utawala, Uhazili, Menejimenti ya Rasilimali Watu, Utawala na Manunuzi ya Umma; 
  • Kutoa ushauri katika maeneo mbali mbali 15  ya kitaalam kwa Taasisi za Umma kwa ajili ya kutambua changamoto halisi za utendaji na kuchangia katika utoaji wa maamuzi yanayozingatia matokeo ya utafiti; 
  • Kuratibu midahalo kwa njia ya mtandao katika maeneo 35  kwa Watumishi wa Umma na sekta binafsi; 
  • Kuwezesha mafunzo ya muda mrefu kwa watumishi 7 wa Chuo cha Utumishi wa Umma katika ngazi za Shahada ya

Uzamivu na Shahada ya Uzamili;

  • Kuendelea na ujenzi wa majengo katika Kampasi ya Singida awamu ya pili ambao utahusisha ujenzi wa Ukumbi kwa ajili ya shughuli mbalimbali za Chuo;
  • Kuanza ujenzi wa Ukumbi Dodoma katika kiwanja cha Chuo kilichopo eneo la NCC awamu ya kwanza. Ukumbi huo unatarajiwa kutumika kwa ajili ya mafunzo, midahalo na semina kwa Watumishi wa

Umma;

  • Kuanza ujenzi wa uzio awamu ya kwanza katika Kampasi ya Tabora kuzunguka eneo la Chuo; na
  • Kufuatilia upatikanaji wa eneo katika Jiji la Mbeya kwa ajili ya ujenzi wa Kampasi ya Mbeya.

C.  MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (eGA)

62. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Mamlaka ya Serikali Mtandao imepanga kutekeleza shughuli zifuatazo: 

  • Kuendelea kuiunganisha mifumo ya Taasisi za Serikali kwenye Mfumo wa kuwezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa (Government Enterprise Service Bus (GovESB) kwa kufuata mpango kazi;
  • Kusimamia na kutathmini hali ya usalama wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA, hatimaye kushauri maeneo ya kuboresha na kufuatilia utekelezaji wake ili kuhakikisha kuwa mifumo na miundombinu ya TEHAMA ya Serikali inafanya kazi na kutoa huduma kwa taasisi za umma na wananchi wakati wote kwa ufanisi na usalama;
  • Kujenga mifumo itakayoboresha utoaji wa huduma wa Taasisi mbalimbali za Serikali katika Utumishi wa Umma.  Baadhi ya mifumo hiyo ni:
    • Mfumo Maalum wa Kusimamia Utoaji Huduma kwenye Zahanati na Vituo vya Afya (GoTHOMIS Lighter Version) – TAMISEMI. Lengo la mfumo huu ni kuongeza ufanisi katika usimamizi wa utoaji huduma katika Zahanati na vituo vya afya;
    • Mfumo wa Uendeshaji wa Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja – Watumishi Housing (WHC): Lengo la mfumo huu ni kuendesha kwa ufanisi uwekezaji wa pamoja;
    • Mfumo wa Kusimamia Mikopo ya Asilimia 10 kwenye Halmashauri kwa kushirikiana na TAMISEMI. Lengo la mfumo huu ni kusimamia mikopo ya vijana, wanawake na walemavu ili

iweze kuwa na udhibiti na ilete tija;

  • Mfumo wa Kusimamia Shughuli za Mamlaka za Viwanja vya Ndege – TAA. Lengo la mfumo huu ni kusimamia utendaji na rasilimali za Mamlaka za viwanja vya ndege;
    • Mfumo wa Kusimamia Shughuli za Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali – Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali. Lengo la mfumo huu ni kuboresha utendaji kazi wa ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa

Serikali;

  • Mfumo wa Usajili wa Wahandisi (awamu ya pili) – Bodi ya Usajili wa wahandisi. Lengo la mfumo ni kurahisisha usajili wa wahandisi na kuweza kutoa ripoti zinazohitajika kwa wakati;
    • Mfumo wa Tiketi za Kielektroni ulioboreshwa – Shirika la Meli Tanzania (MSCL). Lengo la mfumo ni kuongeza ufanisi na kuongeza mapato ya shirika kutokana na shughuli za

usafirishaji;

  • Mfumo wa Usimamizi wa Manunuzi ya Umma – Wizara ya Fedha. Lengo la mfumo huu ni kuboresha manunuzi ya umma;
    • Mfumo wa Kusimamia Usambazaji wa Mbolea – TFRA. Lengo la mfumo huu ni kuongeza ufanisi katika kusimamia uagizaji na usambazaji wa mbolea nchini;
    • Mfumo wa Taarifa za Soko la Ajira (National Labor Market System) – Ofisi ya Waziri Mkuu. Lengo la mfumo huu ni kuwezesha kuwa na taarifa zote za ajira nchini, nafasi za kazi na kuweza kupata takwimu kamili za hali ya soko la ajira nchini; na
    • Mfumo wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (awamu ya tatu);
  • Kuendeleza utafiti na ubunifu katika matumizi ya teknolojia mpya za TEHAMA ili kuibua huduma mpya kwa umma kupitia TEHAMA na kuwezesha matumizi sahihi ya teknolojia mpya zinazoibuka;
  • Kupanua Miundombinu ya Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali (Government Network) ili kufikisha katika Wilaya zote nchini; 
  • Kuziwezesha Taasisi 160 kutumia Mfumo wa Ofisi Mtandao (e-Office), hivyo kufanya Taasisi zinazotumia mfumo huo kufikia 300;
  • Kukagua mifumo ya kimkakati, kisekta na kitaasisi ili kuhakikisha kuwa imetengenezwa na inatumika kwa kufuata sheria, kanuni, viwango na miongozo iliyopo na kushauri maeneo ya kuboresha na kufuatilia utekelezaji wake;
  • Kusimamia, kuendesha na kuendeleza Mifumo na Miundombinu Shirikishi ya TEHAMA ya Serikali na Taasisi zake; hii ni pamoja na kusimamia na kuboresha vituo vya Kuhifadhi Mifumo na Taarifa za Serikali pamoja na vituo vya kujikinga na majanga;
  • Kuwajengea uwezo watumishi katika kusimamia mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika Taasisi za Umma; pia kutoa mafunzo kwa watumiaji kuhusu matumizi sahihi na salama ya mifumo na miundombinu ya TEHAMA; na
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu na msaada wa kiufundi kwenye maeneo ya TEHAMA kwa taasisi za Serikali ili viwango na miongozo iweze kufuatwa, ili kuwa na matumizi ya TEHAMA yenye tija na kupunguza gharama.

D. WATUMISHI HOUSING INVESTMENT (WHI)

  • Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/23, Watumishi     Housing      Investment imepanga kutekeleza shughuli zifuatazo: 
    • Kuendeleza mradi wa ujenzi wa nyumba 1,000 jijini Dodoma pamoja na mikoa mingine zikiwemo wilaya mpya;
    • Kubuni na kutekeleza miradi ya nyumba za gharama nafuu katika Halmashauri mpya;
    • Kujenga na kuuza viwanja 300 vilivyopimwa jijini Arusha; 
    • Kuendelea kuuza nyumba zilizojengwa na zitakazojengwa maeneo mbalimbali nchini;
    • Kuanzisha rasmi Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa FAIDA Fund; 
    • Kuendelea na shughuli za kikandarasi kwa kutoa huduma za ujenzi wa majengo katika taasisi mbalimbali za umma; 
    • Kutoa huduma za ushauri wa majenzi katika miradi inayoendelea na miradi mipya; na
    • Kukarabati nyumba na miundombinu katika miradi     ya   WHC    ya   nyumba zilizopangishwa.
  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2022/23, Fungu 32: Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma inaomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 47,611,581,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizi, Shilingi 39,541,381,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 8,070,200,000 kwa ajili yaMiradi ya Maendeleo.  

SEKRETARIETI      YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 

2022/23, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika

Utumishi wa Umma, imepanga kutekeleza majukumu yafuatayo:- 

  • Kusimamia na kuendesha michakato ya ajira   ili    kuwezesha waajiri   kupata watumishi wenye sifa zinazotakiwa kwa mujibu wa miundo ya utumishi husika;
    • Kushiriki kama Wataalam waalikwa kwenye usaili unaoendeshwa na Taasisi zinazotumia Sheria zilizokasimiwa kwa Taasisi husika;
    • Kuendelea kuimarisha Ofisi ya Sekretarieti ya Ajira Zanzibar kurahisisha michakato ya ajira kwa ajira za Muungano;
    • Kuanza ujenzi wa mfumo wa usaili wa mchujo kwa njia ya mtandao “Online aptitude test” mfumo huu utasaidia Serikali kupunguza gharama kwa kiasi kikubwa hasa gharama za uendeshaji wa saili za mchujo. Aidha mfumo huu utasaidia kuwapunguzia gharama zinazotumika wakati wa usaili kwani saili zitafanyika katika maeneo wanayotoka.
    • Kuanza ujenzi wa mfumo wa kupima haiba za wasailiwa “psychometric testing system”ili kuiwezesha serikali kutambua haiba na tabia za wasailiwa kwa lengo la kuwasaidia waajiri kubaini maeneo ya kuwajengea uwezo waajiriwa wapya
    • Kutoa taarifa na elimu kwa umma ili kukuza    uelewa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Sekretarieti ya Ajira katika mUtumishi wa Umma.
    • Kuboresha mifumo ya usaili kuwa ya kisasa zaidi kwa kutumia TEHAMA.
    • Ununuzi wa vitendea kazi hususani magari ya viongozi na wafanyakazi ili kusaidia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi kwa wakati.
    • Kuanza ujenzi wa jengo la Ofisi za Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Jijini Dodoma.
    • Kuongeza uwezo wa Taasisi kufanya usaili kwa kanda.
  • Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza majukumu yake kwa Mwaka wa Fedha wa

2022/23, Fungu 67: Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inaomba kuidhinishiwa kiasi cha Shilingi 8,721,849,000. Kati ya fedha hizo, Shilingi 5,063,849,000 ni kwa ajiliyaMatumizi ya Kawaida na Shilingi 3,658,000,000 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.  

OFISI YA RAIS, TUME YA UTUMISHI WA UMMA

  • Mheshimiwa Spika; katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Tume imepanga kutekeleza majukumu yafuatayo:-
    • Kufanya ukaguzi wa kawaida katika Taasisi za Umma 150 na Ukaguzi Maalum katika Taasisi za Umma 10 kuangalia uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya usimamizi wa

Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma;

  • Kufanya mikutano minne  ya kisheria ya Tume kujadili na kutolea uamuzi rufaa, malalamiko, taarifa za ukaguzi na masuala mengine ya kiutumishi kadri yatakavyopokelewa;
    • Kuandaa Taarifa ya Hali ya Utumishi wa Umma na Utekelezaji wa Majukumu ya Tume kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha wa 2021/2022 na kuiwasilisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; 
    • Kuandaa mfumo wa TEHAMA kwa ajili ya kuongeza ufanisi kwenye ushughulikiaji wa rufaa na ukaguzi wa rasilimaliwatu;
    • Kufanya utafiti kuhusu uendeshaji na usimamizi   wa Rasilimaliwatu   katika Utumishi wa Umma;
    • Kuhuisha Miongozo miwili ya Tume kuhusu uzingatiaji wa masuala ya Ajira na Uwasilishaji wa Taarifa Tume na kuisambaza kwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na Nidhamu; 
    • Kuelimisha Taasisi za Umma na Watumishi wa Umma kuhusu majukumu ya Tume na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma; na
    • Ujenzi wa jengo la Ofisi za Tume Makao Makuu Dodoma.
  • Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza Mpango wa Mwaka wa Fedha 2022/23, Fungu 94, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma inaomba kuidhinishiwa kiasi cha Shilingi 5,981,824,000. Kati ya fedha hizo, Shilingi 5,681,824,000 ni kwa ajiliyaMatumizi ya Kawaida na Shilingi 300,000,000 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

OFISI YA RAIS, IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

  • Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/23, Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa itatekeleza shughuli zifuatazo:-
    • Kukusanya taarifa, kumbukumbu na nyaraka mbalimbali zinazohusu historia ya nchi yetu kutoka Taasisi za Umma, Taasisi na watu binafsi;
    • Kufanya ukarabati wa nyaraka kongwe zilizohifadhiwa katika Ghala Kuu la nyaraka na zile zinazotarajiwa kukusanywa; 
    • Kuimarisha uhifadhi wa kumbukumbu na nyaraka katika teknolojia ya kisasa kwa kuingiza nyaraka katika mfumo wa kidigitali wa kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka (Digital Records Management and Preservation System) ili kurahisisha upatikanaji wake na kulinda nakala halisi;
    • Kuweka na kuhuisha mifumo ya utunzaji wa kumbukumbu katika Taasisi za

Umma ili kuongeza ufanisi na tija katika utoaji wa huduma Serikalini; 

  • Kujenga uwezo wa Taasisi za Umma katika usimamizi wa kumbukumbu na nyaraka za Serikali kwa kuandaa mikutano na mafunzo kazi kwa watumishi wa umma kuhusu Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya utunzaji wa taarifa, kumbukumbu na nyaraka za

Serikali;

  • Kufanya tathmini (appraisal) ya kumbukumbu tuli za Taasisi za Umma zilizohifadhiwa katika Vituo vya Kumbukumbu vya Idara ili kubaini zenye umuhimu wa kuendelea kuhifadhiwa na zile ambazo umuhimu wake wa matumizi umefikia ukoma kwa lengo la

kuziteketeza kwa mujibu wa Sheria; 

  • Kukagua, kuchambua na kuhamisha kumbukumbu tuli kutoka katika Taasisi za Umma na kuzihifadhi katika Vituo vya Kumbukumbu vya Idara; 
    • Kuwezesha Taasisi za   Umma kutengeneza Miongozo ya kuhifadhi na kuteketeza   kumbukumbu    (Record Retention   Disposal   Schedule)   kwa

mujibu wa Sheria; 

  • Kufanya Ukaguzi wa hali ya utunzaji wa kumbukumbu katika Taasisi za Umma; 
    • Kutambua, kukusanya, kutunza na kuhifadhi kumbukumbu na vitu vya

Waasisi waTaifa; 

  • Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa utunzaji na uhifadhi wa kumbukumbu       na   nyaraka      katika

maendeleo ya Taifa letu;

  • Kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu  na nyaraka kwa kununua vitendea kazi na vifaa vya uhifadhi  vikiwemo kuongeza mashubaka, scanner na magari maalumu ya kubebea nyaraka; na
    • Kuanza ujenzi wa jengo la Utawala Makao Makuu Dodoma.
  • Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza majukumu yake kwa Mwaka wa Fedha wa 2022/23, Fungu 4: Idara ya Kumbukumbu ya Nyaraka za Taifa inaomba kuidhinishiwa kiasi cha Shilingi 4,914,791,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizi, Shilingi 3,504,791,000 ni kwaajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 1,410,000,000 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

MAJUMUISHO

  • Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais ikiongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo yenye dhamana ya maamuzi juu ya nchi na menejimenti ya Utumishi wa Umma ambayo ni nguzo muhimu na mtambuka katika uendeshaji na uendelezaji wa nchi. Utumishi wa Umma umeendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi yetu. Tunayo matarajio makubwa kuwa mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya nchi yetu utaendelea kukua kwa kasi kubwa ili kuiwezesha nchi yetu kufikia uchumi wa kati wa kiwango cha juu.
  • Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais itaendelea kuimarisha uwezeshaji wa vyombo vinavyosaidia kwenye maamuzi ya nchi, usalama na kuimarisha vita dhidi ya rushwa. Maadili kwa viongozi wote na watumishi wa umma yanatarajiwa kuchangia ipasavyo kwenye nchi kupata tija ya rasilimaliwatu  na ufanisi katika matumizi ya rasilimalifedha wakati wote. Kati ya mambo ambayo Serikali itayapa kipaumbele ni usimamizi thabiti wa rasilimaliwatu na rasilimalifedha kwa kusisitiza uwajibaji wa hiari. 
  • Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kufanya maboresho ya kisekta na mtambuka ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji wake. Wajibu wa Ofisi ya Rais ni kuhakikisha maboresho yanayofanywa katika nchi yetu hayana urudufu na yanaleta tija na ufanisi katika

Utumishi wa Umma na kuwa chachu ya maendeleo. Aidha, itahakikisha kunakuwepo na utawala bora ulio imara kuanzia ngazi ya juu ya uongozi hadi chini. Katika kuimarisha uwazi Ofisi ya Rais itahakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu maamuzi ya Serikali na kuweka imara mifumo ya mrejesho wa utoaji huduma. 

  • Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa miundo na mgawanyo wa majukumu kwa mawaziri, utekelezaji kwa ujumla unajumuisha, Ofisi ya Rais Ikulu; Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma; Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma; Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma; na Ofisi ya Rais, Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa.
  • Mheshimiwa Spika, Mipango na Bajeti kwa Mafungu niliyoyataja yamezingatia vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha utendaji kazi wa Utumishi wa Umma, uzingatiaji wa matumizi bora ya rasilimalifedha, maadili ya uongozi na kuongeza kasi ya kufanya maamuzi na kutoa huduma bora kwa wananchi na hivyo kuongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika ngazi zote.
  • Mheshimiwa Spika, Bajeti ya Mafungu yote yaliyo chini ya Ofisi ya Rais, Ikulu na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imelenga kuwa na Utumishi wa Umma unaotoa huduma bora kwa haraka na staha, ukizingatia Katiba, Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo katika kujenga imani zaidi kwa wananchi na kuendana na kauli ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa 22 Aprili, 2021 wakati akilihutubia Bunge la 12 aliposema: ‘Tutawapima viongozi na watumishi kwa namna wanavyotimiza majukumu yao, hatutawaonea aibu viongozi na watumishi wazembe, wezi na wabadhirifu wa mali za umma. Tutaendeleza pia juhudi za kupambana na rushwa kwenye utumishi wa umma. Wajibu wa watumishi wa umma ni lazima uendane na haki zao’. Katika kuendana na wakati, jitihada zaidi zitawekwa kwenye kujenga uwezo na mifumo ya kimenejimenti na utoaji huduma ikiwemo matumizi sahihi na salama ya fursa zinazopatikana katika utoaji huduma kwa TEHAMA ndani ya Serikali, hivyo tunataka kujenga utumishi wa umma wa kidijitali.
  • Mheshimiwa Spika, napenda kulikumbusha Bunge lako tukufu kuwa, Waziri mwenye dhamana ya menejimenti ya Utumishi wa Umma ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye katika hotuba zake amekuwa akisisitiza dhamira yake ya kushughulikia haki na masilahi ya Watumishi wa Umma. Hivyo, kabla ya kuomba fedha kwenye Bunge lako tukufu, naomba kueleza kuwa kilio cha masilahi na motisha kwa Watumishi wa Umma kinaendelea kufanyiwa kazi na Serikali sikivu ya CCM chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Mheshimiwa Spika, baada ya kueleza kwa kina utekelezaji wa majukumu kwa Mwaka wa Fedha 2021/22 na Mipango na Bajeti ya Ofisi ya Rais, Ikulu na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 20212/23 sasa naomba kuwasilisha rasmi mapendekezo ya maombi yetu kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 kwa muhtasari kama ifuatavyo:-
(i)Fungu 20: Ofisi ya Rais, Ikulu  
 Matumizi ya KawaidaSh. 29,828,203,000
           JumlaSh.29,828,203,000
(ii)Fungu 30: Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri  
 Matumizi ya KawaidaSh. 577,206,673,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.164,092,594,000
          JumlaSh.741,299,267,000
(iii)Fungu 33: Ofisi ya  
 Rais, Sekretarieti ya Maadili  ya Viongozi wa Umma  
 Matumizi ya KawaidaSh.     9,260,049,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.3,470,000,000
         JumlaSh.12,730,049,000
iv)Fungu 32: Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma    
 Matumizi ya KawaidaSh. 39,541,381,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.8,070,200,000
           JumlaSh.47,611,581,000
(v)Fungu 67: Ofisi ya Rais,  Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma      
 Matumizi ya KawaidaSh.     5,063,849,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.3,658,000,000
          JumlaSh.8,721,849,000
vi)Fungu 94: Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma  

(

 Matumizi ya KawaidaSh.     5,681,824,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.300,000,000
          JumlaSh.5,981,824,000
vii)Fungu 04: Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa  
 Matumizi ya KawaidaSh.     3,504,791,000
 Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.1,410,000,000
         JumlaSh.4,914,791,000
    
79. Mheshimiwa Spika na Wabunge wenzangu, Jumla kuu ya Bajeti ninayoomba kwa mafungu yote yaliyo chini ya Ofisi ya Rais (Ikulu na Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) kwa mwaka 2022/23, ni kama ifuatavyo:-
 Jumla kuu – Matumizi ya KawaidaSh.670,086,770,000
 Jumla kuu – Matumizi ya Miradi ya MaendeleoSh.181,000,794,000
 Jumla Kuu kwa Mafungu yoteSh.851,087,564,000

( (

80. Mheshimiwa Spika   na Wabunge wenzangu, mwisho naomba kuwasilisha maombi haya ili muweze kuyajadili na kuyaidhinisha.

Ahsanteni kwa kunisikiliza, naomba kutoa hoja.

Jenista J. Mhagama (Mb.)

WAZIRI WA NCHI – OFISI YA RAIS

(MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA)

KIAMBATISHO NA. 1 TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

TAKWIMU ZA UCHUNGUZI KWA KIPINDI CHA JULAI 2021 – MACHI, 2022

MAELEZOJUL. 2021AUG. 2021SEP. 2021OCT. 2021NOV. 2021DEC. 2021JAN. 2022FEB. 2022MACH. 2022JUMLA
Malalamiko Yaliyopokelewa***1,1069819778501,1729218558237818,466
Majalada yaliyokamilika56134551911084082102588
Majalada Yaliyopelekwa kwa DPP12444246862176463358
Majalada yaliyorudi na kibali cha DPP4034395812123211193
Majalada Yaliyofungwa219201005332
Kesi Mpya Zilizofikishwa Mahakamani293447173940223641305
Kesi zilizoamuli wa Mahakama niKesi Zilizoshinda31263112241681627191
Kesi Zilizoshindwa15172717231461216147
Kesi zinazoendela mahakamani642589540571517532428521527527
 Thamani ya Fedha Iliyookolewa (Tshs)   Fedha Taslimu782,323,0259,951,40041,302,58042,998,93240,140,59331,580,153.758,835,0002,900,0004,446,500964,478,183.75
 Fedha zilizodhibitiwa 100,914,698.6945,388,00099,218,01154,687,372102,066,771.06 36,102,3443,835,0004,566,16610,397,500457,175,862.75
Jumla ya Fedha zilizookolewa883,237,723.6955,339,400140,520,59198,336,304142,207,364.06 67,032,497.7512,145,5007,466.68714,844,0001,421,654,047

*** Siyo malalamiko yote yanayopokelewa yanahusu rushwa.

KIAMBATISHO NA. 2

MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII

UHAWILISHAJI WA FEDHA KWA WALENGWA NA MIRADI YA AJIRA ZA MUDA NA MIUNDO MBINU

        NA.ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZI YA KIJIJI/ MTAA/ SHEHIAMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA  MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI
WILAYAKATAMIUNDO MBINUAJIRA ZA MUDA
 Arusha       
1.         Arusha8114,6232,396,320,78806,210,00043,316,14505 464,449,175   2,910,296,108
2.         Arusha CC1514,968923,765,220011,100,00059,254,85006 445,554,091   1,439,674,161
3.         Karatu608,6611,641,601,45004,770,00042,080,38505 464,449,175   2,152,901,010
4.         Longido579,0591,594,306,00004,260,00049,612,01005 450,492,217   2,098,670,227
5.         Meru1058,1231,331,650,24308,070,00050,195,74005 401,864,120   1,791,780,103
6.         Monduli637,4551,421,414,00004,710,00049,638,56004 380,987,159   1,856,749,719
7.         Ngorongoro6810,4141,755,190,00005,160,00065,763,98006 347,182,159   2,173,296,139
 Jumla Ndogo58563,30311,064,247,701044,280,000359,861,670036 2,954,978,096 0 14,423,367,467
 Dar es Salaam         
8.         Ilala MC933,946637,058,02106,960,00043,520,000072 193,769,879 172,053,000 1,053,360,900
9.         Kigamboni MC671,599312,093,93905,190,00037,884,88000   355,168,819
10. Kinondoni MC1033,938830,251,47808,070,00048,249,65500 –   886,571,133
11. Temeke MC1426,8051,415,667,691010,890,00058,423,20000 –   1,484,980,891
12. Ubungo MC912,896582,007,03606,930,00043,841,55000 –   632,778,586
 Jumla Ndogo49619,1843,777,078,165038,040,000231,919,285072 193,769,879 172,053,000 4,412,860,329
       ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOAMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI
Dodoma   
13. Bahi50        7,256         970,037,866                     03,870,000          43,765,815      038 345,969,000      1,363,642,681
14. Chamwino75      15,876      1,986,457,872                     06,480,000          60,672,165      0110 504,711,000      2,558,321,037
15. Chemba113        7,144      1,122,942,000                     08,280,000          63,340,950      0    1,194,562,950
16. Dodoma CC193        9,297      1,288,403,667                     013,860,000          68,820,000      078 172,797,000      1,543,880,667
17. Kondoa79        9,125      1,325,436,238                     06,600,000          54,102,560      064 628,134,000      2,014,272,798
18. Kondoa TC35        2,875         422,267,239                     02,700,000          27,900,000      021 129,978,000         582,845,239
19. Kongwa88      11,419      1,976,524,892                     06,810,000          51,274,255      0    2,034,609,147
20. Mpwapwa120        9,720      1,184,040,745                     08,850,000          65,819,345      064 308,304,000      1,567,014,090
 Jumla Ndogo753      72,712    10,276,110,519                     057,450,000        435,695,090      0375 –    2,089,893,000  12,859,148,609
 Geita           
21. Bukombe86        8,910      1,536,994,000                     06,480,000          58,315,080      05 437,621,592   2,039,410,672
22. Chato117        9,864      1,812,820,160                     09,090,000          57,647,070      05 335,122,988   2,214,680,218
23. Geita164      13,734      2,443,744,127                     012,660,000          77,520,625      05 438,945,454   2,972,870,206
24. Geita TC805,9511,133,846,011                     06,090,00042,551,45505 474,832,304   1,657,319,770 
25. Mbogwe905,894899,768,00007,140,00048,865,4000119 433,313,062 127,398,000 1,516,484,462 
26. Nyang’hwale624,562841,822,00004,950,00039,450,33005 448,409,318   1,334,631,648 
 Jumla Ndogo59948,9158,668,994,298                     046,410,000324,349,9600144 2,568,244,718127,398,00011,735,396,976
 Iringa           
27. Iringa14210,5791,754,795,392                     010,770,00098,179,0000    1,863,744,392 
28. Iringa MC1903,639655,712,242014,370,00054,633,6500    724,715,892 
29. Kilolo1109,6871,398,858,000                     08,670,00068,786,4200    1,476,314,420 
30. Mafinga TC321,102149,876,000                     02,580,00029,362,930032 57,027,000 238,845,930 
        31. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 6,990,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI  967,248,960 
Mufindi795,342691,868,000                     057,340,960076 211,050,000
 Jumla Ndogo55330,3494,651,109,634                     043,380,000308,302,9600108 – 268,077,000 5,270,869,594 
 Kagera           
32. Biharamulo8011,875 1,829,396,000                     06,270,00056,320,3000    1,891,986,300 
33. Bukoba949,917 1,701,610,000                     07,530,00049,000,7500    1,758,140,750 
34. Bukoba MC653,159 611,168,643                     05,220,00037,456,4700    653,845,113 
35. Karagwe8511,294 1,999,046,128                     06,870,00053,738,3150    2,059,654,443 
36. Kyerwa10410,929 1,933,914,254                     07,980,00052,551,6250    1,994,445,879 
37. Missenyi777,534 1,288,538,893                     06,120,00046,245,3750    1,340,904,268 
38. Muleba16917,189 3,148,667,985                     013,410,00074,399,4900    3,236,477,475 
39. Ngara84      10,7521,473,071,6120          6,660,000          49,201,5000      52 563,574,000    2,092,507,112
 Jumla Ndogo758      82,64913,985,413,5150        60,060,000        418,913,8250      52 563,574,000 15,027,961,340
 Katavi            
40. Mlele18            915119,474,0000          1,200,000          37,345,1430            158,019,143
41. Mpanda58        5,303733,970,0880          4,170,000          68,105,8100      22 111,120,000        917,365,898
42. Mpanda MC38        1,480200,395,8330          2,550,000          27,350,0000      19 82,230,000       312,525,833
43. Mpimbwe DC31        2,447428,394,0000          2,610,000          43,629,8250            474,633,825
44. Nsimbo56        3,041432,218,0000          3,840,000          25,851,9620            461,909,962
 Jumla Ndogo201      13,1861,914,451,9210        14,370,000        202,282,7400      41 193,350,000    2,324,454,661
 Kigoma            
45. Buhigwe45        8,3751,425,073,8260          3,780,000          34,954,8300            1,463,808,656
46. Kakonko44        9,3301,669,372,0000          3,600,000          35,737,4400            1,708,709,440
47. Kasulu6210,698 1,832,452,000                     05,010,00051,157,7800    1,888,619,780 
48. Kasulu TC1168,410 1,407,380,940                     07,950,00049,024,1600    1,464,355,100 
        49. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 4,470,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI  2,057,756,390
Kibondo5510,5951,454,761,390                     061,105,000074 537,420,000
50. Kigoma51        6,921      1,431,738,985                     04,050,000          55,455,000        0     1,491,243,985
51. Kigoma MC68      11,562      2,351,605,755                     05,550,000          40,495,420        0     2,397,651,175
52. Uvinza61        5,855         851,570,000                     04,530,000          55,277,135        024         187,329,000      1,098,706,135
 Jumla Ndogo502      71,746    12,423,954,896                     038,940,000        383,206,765        098 –        724,749,000  13,570,850,661
 Kilimanjaro            
53. Hai76        5,724         948,490,446                     05,850,000          41,303,610        0     995,644,056
54. Moshi166      10,422      1,625,130,886                     012,750,000          68,243,500        0     1,706,124,386
55. Moshi MC59        1,719         314,535,778                     04,500,000          27,262,054        0     346,297,832
56. Mwanga81        4,407         820,136,414                     06,330,000          46,553,000        0     873,019,414
57. Rombo75        6,138      1,061,837,267                     05,790,000          42,252,905        0     1,109,880,172
58. Same103      10,060      1,795,210,000                     08,070,000          60,374,155        0     1,863,654,155
59. Siha56        3,570         614,145,740                     04,080,000          35,458,880        0     653,684,620
 Jumla Ndogo616      42,040      7,179,486,531                     047,370,000        321,448,104        00 –                            0      7,548,304,635
 Lindi            
60. Kilwa60        4,442         549,888,350                     05,280,000          70,821,200        055         146,067,000         772,056,550
61. Lindi112      10,305      1,263,196,510                     09,150,000          66,911,125        089         572,907,000      1,912,164,635
62. Lindi MC702,236262,966,442                     03,870,00032,015,205030 192,624,000 491,475,647 
63. Liwale492,472285,808,000                     04,230,00053,802,586047 158,796,000 502,636,586 
64. Nachingwea734,667467,122,294                     06,270,00054,296,125069 424,605,000 952,293,419 
65. Ruangwa908,2061,130,374,000                     06,960,00052,800,38001 103,500,000   1,293,634,380 
 Jumla Ndogo45432,3283,959,355,596                     035,760,000330,646,6210291 103,500,000 1,494,999,000 5,924,261,217 
 Manyara           
        66. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 8,280,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI  2,771,239,000 
Babati10414,5352,703,502,000                     059,457,0000   
67. Babati TC482,351390,037,577                     03,510,00030,870,0000    424,417,577 
68. Hanang1038,4091,577,659,186                     07,410,00052,641,9800    1,637,711,166
69. Kiteto697,0091,214,230,000                     05,430,00064,511,9750    1,284,171,975
70. Mbulu784,328803,500,000                     06,120,00045,493,2450    855,113,245
71. Mbulu TC913,605633,834,000                     06,450,00045,536,0050    685,820,005
72. Simanjiro696,0491,069,228,000                     05,400,00065,014,3650    1,139,642,365
 Jumla Ndogo56246,2868,391,990,763                     042,600,000363,524,57000 – 0 8,798,115,333
 Mara           
73. Bunda DC745,434957,439,215                     06,030,00044,924,8650    1,008,394,080
74. Bunda TC783,204588,449,095                     06,300,00042,630,9750    637,380,070
75. Butiama598,2131,547,160,000                     04,920,00040,355,50001 199,562,000   1,791,997,500
76. Musoma DC676,9221,304,164,483                     04,980,00036,260,0000    1,345,404,483
77. Musoma MC803,232629,469,369                     06,150,00040,550,0000    676,169,369
78. Rorya8911,3371,869,082,146                     07,050,00047,960,0000    1,924,092,146
79. Serengeti934,444809,408,089                     07,260,00067,545,5800    884,213,669
80. Tarime DC886,6061,099,126,000                     06,600,00045,261,9500    1,150,987,950
81. Tarime TC811,773343,924,000                     07,080,00044,262,0850    395,266,085 
 Jumla Ndogo70951,1659,148,222,397                     056,370,000409,750,95501 199,562,000 0 9,813,905,352 
 Mbeya           
82. Busokelo564,043494,326,000                     04,500,00034,500,000036 126,876,000 660,202,000 
83. Chunya546,6291,090,104,000                     04,110,00060,091,1950    1,154,305,195 
84. Kyela1116,6161,086,360,178                     08,910,00053,251,0800    1,148,521,258 
        85. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 8,730,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI  2,136,520,364 
Mbarali10812,5942,048,108,219                     079,682,1450   
86. Mbeya15211,5791,836,557,832                     012,270,00069,796,1600    1,918,623,992 
87. Mbeya CC1765,7341,059,085,493                     014,250,00072,818,7500    1,146,154,243 
88. Rungwe1255,596668,215,474                     09,540,00059,463,525089 169,950,000 907,168,999 
 Jumla Ndogo78252,7918,282,757,196                     062,310,000429,602,8550125 – 296,826,000 9,071,496,051 
 Morogoro           
89. Gairo678,8171,487,188,000                     05,220,00041,196,5700    1,533,604,570 
90. Ifakara TC595,545943,492,810                     04,290,00041,730,1150    989,512,925 
91. Kilombero504,758726,268,000                     03,660,00054,076,3750    784,004,375 
92. Kilosa1096,324922,142,000                     09,000,00080,275,530085 453,426,000 1,464,843,530 
93. Malinyi DC323,294492,564,000                     02,400,00057,031,1050    551,995,105 
94. Morogoro13614,4772,354,322,000                     011,220,00096,130,00001 190,593,000   2,652,265,000 
95. Morogoro MC2603,660672,132,020                     020,070,00063,902,7150    756,104,735 
96. Mvomero1399,4571,491,126,000                     010,890,00071,560,8150    1,573,576,815 
97. Ulanga594,924783,464,000                     04,500,00063,608,2150    851,572,215 
 Jumla Ndogo91161,2569,872,698,830                     071,250,000569,511,440086 190,593,000 453,426,000 11,157,479,270
 Mtwara           
98. Masasi1039,538      1,162,303,736                       0          8,880,000          58,792,330          0 101         362,355,000  1,592,331,066 
99. Masasi TC885,743         734,007,662                       0          6,480,000          43,307,415          0     39         122,412,000       906,207,077 
100. Mtwara DC947,717         749,799,965                       0          5,880,000          43,996,745          0     62         335,217,000  1,134,893,710 
101. Mtwara MC691,186         152,207,781                       0          3,630,000          21,526,099          0     35           55,188,000       232,551,880 
102. Nanyamba705,848         541,723,464                       0          4,500,000          37,455,090          0     42         241,293,000       824,971,554 
103. Nanyumbu586,371         752,374,000                       0          5,100,000          47,392,165          0     56         503,160,000  1,308,026,165 
        104. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 5,010,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI        499,548,460 
Newala572,384         303,156,555                    0          39,392,905        056         151,989,000
105. Newala TC452,173         288,023,691                    03,870,000          33,536,025        043         159,894,000       485,323,716 
106. Tandahimba15710,221      1,204,684,545                    012,060,000          66,428,640        090         414,558,000  1,697,731,185 
 Jumla Ndogo74151,181      5,888,281,399                    055,410,000        391,827,414        0524 –  2,346,066,000  8,681,584,813 
 Mwanza                                                                                           
107. Buchosa818,323      1,630,224,999                    06,840,000          56,760,135        05 435,382,841  2,129,207,975 
108. Ilemela MC1935,865      1,131,132,684                    014,550,000          71,874,025        05 324,113,863  1,541,670,572 
109. Kwimba12011,492      2,285,501,441                    09,780,000          60,546,970        05 444,875,284  2,800,703,695 
110. Magu1047,157      1,396,849,913                    07,980,000          50,404,150        05 411,591,401  1,866,825,464 
111. Misungwi908,125      1,438,040,135                    07,170,000          49,589,845        058 475,934,659        499,398,000  2,470,132,639 
112. Mwanza CC1707,238      1,354,561,800                    012,540,000          64,356,065        05 418,125,558  1,849,583,423 
113. Sengerema9810,126      1,955,645,281                    07,440,000          63,398,935        05 413,429,999  2,439,914,215 
114. Ukerewe968,878      1,657,894,650                    07,410,000          46,460,540        05 423,591,115  2,135,356,305 
 Jumla Ndogo95267,204    12,849,850,903                    073,710,000        463,390,665        093 3,347,044,720  499,398,000  17,233,394,288
 Njombe                                                                                           
115. Ludewa774,446         697,160,000                    06,240,000          46,952,932        07 429,745,795  1,180,098,727 
116. Makambako TC381,948         323,303,459                    03,270,000          29,433,470        05 437,463,711      793,470,640 
117. Makete1004,703         697,062,000                    08,040,000          55,691,780        05 446,757,841  1,207,551,621 
118. Njombe454,147         651,136,000                    04,020,000          39,825,640        05 414,443,183  1,109,424,823 
119. Njombe Mji724,115         664,874,289                    05,640,000          45,958,810        07 744,871,716  1,461,344,815 
120. Wang’ing’om be1096,489         882,486,000                    08,520,000          56,309,200        05 437,992,458      1,385,307,658 
 Jumla Ndogo44125,848      3,916,021,748                    035,730,000        274,171,832        034 2,911,274,704  0  7,137,198,284 
       ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA                  MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI  
Pwani                                                                                         
121. Bagamoyo192,515         354,244,041                       0          1,350,000          24,891,975          0     33           29,385,000       409,871,016 
122. Chalinze DC586,527         824,179,816                       0          4,890,000          52,456,310          0     53 35,957,326        316,203,000  1,233,686,452 
123. Kibaha473,855         516,750,689                       0          4,140,000          36,266,610          0     47         256,095,000       813,252,299 
124. Kibaha TC612,579         479,025,254                       0          4,800,000          37,050,830          0       2 206,000,000  726,876,084 
125. Kibiti DC614,691         794,842,000                    04,590,000          42,749,970        00 –  842,181,970 
126. Kisarawe773,300         505,053,488                    06,060,000          37,508,611        0     37       66,693,000       615,315,099 
127. Mafia231,432         282,731,000                    02,070,000          24,392,200        00 –  309,193,200 
128. Mkuranga1245,646         995,502,005                    09,690,000          59,078,500        00 –  1,064,270,505 
129. Rufiji544,451         743,814,000                    04,020,000          52,231,675        01 75,000,000  875,065,675 
 Jumla Ndogo52434,996      5,496,142,293                    041,610,000        366,626,681        0173 316,957,326  668,376,000  6,889,712,300 
 Rukwa                                                                                           
130. Kalambo1158,934      1,407,438,000                    08,880,000          62,024,845        0    1,478,342,845 
131. Nkasi11510,876      1,818,912,000                    08,490,000          69,318,320        0    1,896,720,320 
132. Sumbawanga734,644         776,256,700                    06,450,000          52,389,430        097         357,366,000  1,192,462,130 
133. Sumbawanga MC1867,788      1,535,518,368                    013,950,000          71,881,095        0        1,621,349,463 
 Jumla Ndogo48932,242      5,538,125,068                    037,770,000        255,613,690        097 –  357,366,000  6,188,874,758 
 Ruvuma                                                                                           
134. Madaba DC181,691         217,777,543                    01,560,000          23,720,000        021           53,235,000       296,292,543 
135. Mbinga1178,672      1,573,524,000                    09,480,000          62,706,200        0    1,645,710,200 
136. Mbinga TC783,400         613,328,000                    06,270,000          40,990,000        0    660,588,000 
137. Namtumbo7611,566      1,827,454,000                    05,820,000          84,067,075        0    1,917,341,075 
138. Nyasa858,243      1,551,412,000                    06,690,000          50,051,300        0    1,608,153,300 
        139. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 2,910,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI        909,789,200 
Songea333,739         533,203,715                    0          57,495,485        073 151,000,000        165,180,000
140. Songea MC845,712      1,022,836,163                    06,600,000          43,424,780     0    1,072,860,943 
141. Tunduru9612,763      1,655,597,047                    07,590,000          83,670,770     0149     1,170,705,000  2,917,562,817 
 Jumla Ndogo58755,786      8,995,132,468                    046,920,000        446,125,610     0243 151,000,000  1,389,120,000  11,028,298,078
 Shinyanga                                                                                           
142. Kahama TC603,363         653,884,989                    04,440,000          37,080,965     040         247,404,000       942,809,954 
143. Kishapu1257,477      1,386,944,000                    09,840,000          62,674,010     0    1,459,458,010 
144. Msalala936,491      1,247,500,033                    07,530,000          51,024,925     0    1,306,054,958 
145. Shinyanga DC12611,080      2,041,461,422                    010,020,000          62,072,240     0        2,113,553,662 
146. Shinyanga MC734,300         968,546,510                    05,700,000          40,040,525     0        1,014,287,035 
147. Ushetu1129,272      1,501,490,000                    08,250,000          59,164,105     0    1,568,904,105 
 Jumla Ndogo58941,983      7,799,826,954                    045,780,000        312,056,770     040 –  247,404,000  8,405,067,724 
 Simiyu                                                                                           
148. Bariadi DC849,655      1,969,994,742                    06,510,000          41,870,000     0 5  425,813,636  2,444,188,378 
149. Bariadi TC994,686         894,337,188                    07,830,000          46,710,000     0 5  438,268,404  1,387,145,592
150. Busega594,843         922,506,525                    04,680,000          37,856,160     0 5  396,664,769  1,361,707,454
151. Itilima1028,593      1,486,046,000                    08,100,000          57,337,950     0 63 396,664,769        515,649,000      2,463,797,719
152. Maswa12812,512      2,519,093,376                    09,990,000          62,163,630     0 5  392,453,034  2,983,700,040
153. Meatu1085,915      1,137,282,000                    08,550,000          67,879,935     0 5  435,640,272  1,649,352,207
 Jumla Ndogo58046,204      8,929,259,831                    045,660,000        313,817,675     088 2,485,504,884  515,649,000  12,289,891,390
 Singida                                                                                           
154. Ikungi10112,510      2,151,157,424                    07,770,000          64,699,355     0    2,223,626,779
        155. ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 4,830,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI       1,043,641,785
Iramba545,166         655,760,000                    0          44,930,785     051         338,121,000
156. Itigi393,366         635,448,154                    03,300,000          30,100,000     0    668,848,154
157. Manyoni6810,311      1,628,372,200                    05,010,000          95,829,370     0    1,729,211,570
158. Mkalama757,243      1,010,802,534                    05,880,000          45,973,655     046         385,965,000      1,448,621,189
159. Singida497,211      1,092,596,000                    03,870,000          37,122,000     072         647,040,000      1,780,628,000
160. Singida MC532,524         444,905,252                    03,210,000          31,249,600     030         166,539,000         645,903,852
 Jumla Ndogo43948,331      7,619,041,564                    033,870,000        349,904,765     0199 –  1,537,665,000      9,540,481,329
 Songwe                                                                                           
161. Ileje715,145         788,150,000                    05,760,000          45,038,400     0    838,948,400
162. Mbozi12711,508      1,878,127,037                    09,930,000          62,338,190     0    1,950,395,227
163. Momba725,883         883,848,000                    05,700,000          50,855,990     0    940,403,990
164. Songwe424,583         728,506,668                    03,420,000          63,563,850     0    795,490,518
165. Tunduma681,700         301,460,000                    05,670,000          38,790,000     0    345,920,000
 Jumla Ndogo38028,819      4,580,091,705                    030,480,000        260,586,430     00 –  0      4,871,158,135
 Tabora                                                                                           
166. Igunga12710,606      1,729,386,000                    09,240,000          66,396,520     0    1,805,022,520
167. Kaliua1009,566      1,620,776,000                    07,950,000          78,889,475     0    1,707,615,475
168. Nzega1589,470      1,599,793,994                    012,210,000          75,595,255     0    1,687,599,249
169. Nzega TC361,906         311,906,023                    02,820,000          29,819,600     0    344,545,623
170. Sikonge654,868         910,700,000                    05,250,000          73,597,920     0    989,547,920
171. Tabora MC1634,580         961,653,508                    013,200,000          66,400,000     0    1,041,253,508
172. Urambo635,912      1,106,480,196                    05,100,000          47,827,825     0    1,159,408,021
173. Uyui794,718         730,026,000                    06,750,000          67,342,185     066         292,623,000      1,096,741,185
       ENEO LA UTEKELEZAJIIDADI YA VIJIJI/ MITAA/ SHEHIAIDADI YA KAYAMALIPO KWA WALENGWAMALIPO YA USIMAMIZ I NGAZIMALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA MKOA 62,520,000MALIPO YA USIMAMIZI NGAZI YA WILAYA NA KATAIDADI YA MIRADITHAMANI YA MIRADI YA MIUNDOMBINU NA AJIRA ZA MUDA  JUMLA YA FEDHA KILA HALMASHAURI       9,831,733,501
Jumla Ndogo79151,626      8,970,721,721                    0        505,868,780     066 –  292,623,000
 Tanga                                                                                           
174. Bumbuli DC854,857         732,869,650                    06,720,000          42,640,000     0    782,229,650
175. Handeni9110,577      1,480,413,760                    07,080,000          57,377,095     052         129,393,000      1,674,263,855
176. Handeni TC604,101         760,469,862                    04,800,000          37,574,855     0    802,844,717
177. Kilindi1029,879      1,784,747,600                    08,130,000          61,050,365     0    1,853,927,965
178. Korogwe1228,647      1,533,898,298                    09,720,000          60,222,165     0    1,603,840,463
179. Korogwe TC292,670         504,308,452                    02,460,000          27,576,905     0    534,345,357
180. Lushoto1408,085      1,350,701,196                    011,280,000          81,089,060     0    1,443,070,256
181. Mkinga856,270      1,003,756,000                    06,810,000          48,543,160     0    1,059,109,160
182. Muheza1408,347      1,447,572,693                    011,130,000          61,888,390     0    1,520,591,083
183. Pangani353,336         644,988,000                    03,150,000          33,158,580     0    681,296,580
184. Tanga1705,436      1,038,171,083                    013,110,000          67,389,310     0    1,118,670,393
 Jumla Ndogo1,05972,205    12,281,896,594                    084,390,000        578,509,885     052 –  129,393,000  13,074,189,479
 Zanzibar                                                                                           
185. Pemba13722,661      3,622,604,135                    03,570,000          99,467,120     074600,000,000    1,064,757,000      5,390,398,255
186. Unguja23019,580      3,163,710,782                    06,240,000        147,834,840     0112  709,716,000      4,027,501,622
 Jumla Ndogo36742,241      6,786,314,917                    09,810,000        247,301,960     0186600,000,000    1,774,473,000      9,417,899,877
 Jumla Kuu16,4201,286,576 213,246,579,127                    01,262,250,000     9,854,818,997     0322416,022,429,327 16,141,878,000  256,527,955,451

KIAMBATISHO NA. 3

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 604 ZILIZOUNGANISHWA KATIKA MFUMO WA BARUA PEPE SERIKALINI (GMS)

NA.JINA LA TAASISI
1Accountant General 
2Agency for The Development of Educational Management
3Ministry of Health
4The Office of Attorney General
5Agricultural Inputs Trust Fund
6Arusha International Conference Centre
7Airports
8Air Tanzania
9Public Service Recruitment Secretariat
10Amana Hospital
11Architects and Quantity Surveyors Registration Board
12Wizara Ya Ardhi
13Ardhi Institute Morogoro
14Ardhi Institute Tabora
15Ardhi University
16Arusha Region
17Arusha City Council
18Arusha District Council
19Agricultural Seed Agency
20Arusha Technical College
21Arusha Urban Water Supply and Sanitation Authority
22Babati District Council
23Babati Town Council
24Bagamoyo District Council
25Bahi District Council
26Baraza La Kiswahili Tanzania
27Bariadi District Council
29Bariadi Town Council
30Bariadi Urban Water Supply and Sanitation Authority 
31Baraza La Sanaa La Taifa 
32Babati Urban Water Supply and Sanitation Authority
33Biharamulo District Council Website
34Bugando Medical Centre
NA.JINA LA TAASISI
35Benjamin Mkapa Hospital
36Business Registrations and Licensing Agency
37Buchosa District Council
38Bugando Medical Centre
39Buhigwe District Council
40Bukoba District Council
41Bukoba Municap Council
42Bukombe District Council
43Bumbuli District Council
44Bunda District Council
45Bunda Town Council
46Mamlaka Ya Maji Bunda
47Parliament of Tanzania
48Busega Distict Council
49Busega Water Supply and Sanitation Authority
50Busekelo District Council
51Butiama District Council
52Bukoba Urban Water Supply and Sanitation Authority
53Bunda Water Supply and Sanitation Authority
54Cashewnut Board of Tanzania
55College of Business Education
56Capital Development Authority
57Cereals and Other Produce Board
58Chalinze District Council
59Chamwino District Council
60Chato District Council
61Chato Zonal Refferal Hospital
62Chato Water Supply and Sanitation Authority 
63Chemba District Council
64Commision For Human Rights and Good Governance
65Chunya District Council
66Capital Market and Securities Authority
67Co-Operative Audit and Supervision Corporation
68Tanzania Coffee Board
69Dar Es Salaam Institute of Technology
70Copyright Society of Tanzania
71Tanzania Commission for Science and Technology
72Contractors Registration Board
73Corporation Sole Works Superintendent
NA.JINA LA TAASISI
74Dar Rapid Transit Agency
75Dar-Es-Salaam Water Supply and Sanitation Authority
76Dar Es Salaam City Council
77Drug Control and Enforcement Authority
78Drilling and Dam Construction Agency
79Dar Es Salaam Institute of Technology
80Dar Es Salaam Maritime College
81Dodoma Region
82Dodoma City Council
83Dodoma Regional Referral Hospital
84Deep Sea Fishing Authority
85Dodoma Urban Water Supply and Sanitation
86e-Government Authority
87Export Processing Zones Authority
88Engineers Registration Board 
89Eastern and Southern Africa Anti-Money Laundering Group
90President’s Office – Ethics Secretariat
91Energy and Water Utilities Regulatory Authority 
92Energy and Water Utilities Regulatory Authority Consumer Consultative Council
93Fair Competition Commission
94Tanzania Fertilizer Company Ltd
95Fisheries Education and Training Agency
96Tanzania Film Board
97Forest Industries Training Institute
98Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
99Fire and Rescue Force
100Forestry Training Institute
101Gairo District
102Gairo District Council
103Gaming Board of Tanzania
104Government Chemist Laboratory Authority
105Geita Region
106Geita District Council
107Geita Town Council
108Geita Urban Water and Sanitation Authority
109Government Procurement Services Agency
110Geological Survey of Tanzania 
111Hai District Council
NA.JINA LA TAASISI
112Hanang District Council
113Handeni District Council
114Handeni Town Council
115Handeni Water Supply and Sanitation Authority
116Ministry of Finance (Hazina)
117Higher Education Students’ Loans Board
118Information and Communication Technologies (Ict) Commission
119Ifakara Town Council
120 Ifakara Water Supply and Sanitation Authority
121 Institute of Finance Management 
122Igunga District Council
123Igunga Urban Water Supply and Sanitation Authority
124Institute of Judicial Administration Lushoto
125Ikungi District Council
126Ikwiriri Water Supply and Sanitation Authority
127Ilala 
128Ilala Municipal Council
129Ileje District Council
130Ilemela Municipal Council
131Ilala Municipal Council
132Tanzania Immigration Department
133Prime Minister’s Office (Investment) 
134Iramba District Council
135Iringa Region
136Iringa District Council
137Iringa Municipal Council
138Iringa Water Supply And Sanitation Authority
139Institute Of Social Work
140Itigi District Council
141Itilima District Council
142Itumbai Songole Water Supply And Sanitation Authority
143Ministry Of Community Development, Gender, Women And Special Groups
144Joint Finance Commission
145Jakaya Kikwete Cardiac Institute
146Judical Service Commision
147Judiciary
148Kilimanjaro Airport Development Company
149Kagera Region
NA.JINA LA TAASISI
150Kahama Municipal Council
151Kahama Town Council
152Kakonko District Council
153Kalambo District Council
154Kaliua District 
155Kaliua District Council
156Karagwe District Council
157Karagwe Water Supply and Sanitation Authority
158Karatu District Council
159Shirika La Masoko Ya Kariakoo
160Karatu Urban Water Supply and Sanitation Authority
161Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority 
162Kasulu District Council
163Kasulu Town Council
164Mamlaka Ya Maji Kasulu
165Katavi Region
166Katavi Regional Referal Hospital
167Ministry of Labour, Youth, Employment And Persons With Disability
168Kibaha Education Association
169Kibaha District Council
170Kibaha Town Council
171Kibiti District Council
172Kibondo District Council
173Kibondo Urban Water Supply and Sanitation Authority
174Kigamboni Municipal Council
175Kigoma Region
176Kigoma District Council
177Kigoma Ujiji Municipal Council
178Kilimanjaro Airport 
179Kilimanjaro Region
180Ministry of Agriculture
181Kilindi District Council
182Kilindoni Water Supply and Sanitation Authority
183Kilolo District Council
184Kilolo District 
185Kilombero District 
186Kilombero District Council
187Kilosa District 
NA.JINA LA TAASISI
188Kilosa District Council
189Kilwa District Council
190Kilwa Masoko Urban Water Supply and Sanitation Authority
191Kinondoni Municipal Council
192Kiomboi Water Supply and Sanitation Authority
193Kisarawe District Council
194Kishapu District Council
195Kiteto District Council
196Kishapu Water Supply and Sanitation Authority (Kiwassa)
197Kilimanjaro International Leather Industries Co. Ltd
198Kondoa District Council
199Kondoa Town Council
200Kondoa Urban Water Supply Authority
201Kongwa District Council
202Korogwe District Council
203Korogwe Town Council
204Korogwe Water Supply and Sanitation Authority
205Kahama Urban Water Supply and Sanitation Authority
206Kigoma Urban Water Supply and Sanitation Authority 
207Kwimba District Council
208Kyela District Council
209Kyerwa District Council
210Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development
211Ministry of Education
212Land Transport Regulatory Authority
213Land Transport Consumer Advisory Council
214Local Government Training Institute
215Lindi Region
216Lindi District Council
217Lindi Municipal Council
218Livestock Training Agency
219Liwale District Council
220Loliondo Urban Water Supply and Sanitation Authority 
221Longido District Council
222Law Reform Commission of Tanzania
223Ludewa District Council
224Lushoto District Council
225Lindi Urban Water Supply and Sanitation Authority
NA.JINA LA TAASISI
226Lushoto Water Supply and Sanitation Authority
227Lake Victoria Basin Water Board 
228Madaba District Council
229Ministry of Minerals
230Mafia District Council
231Mafinga Town Council
232Mafinga Water Supply and Sanitation Authority 
233Maganzo Water Supply and Sanitation Authority (Magawassa)
234Magu District Council
235Mahenge Urban Water Supply and Sanitation Authority
236Ministry of Water
237Makambako Town Council
238Makete District Council
239Makete Water Supply and Sanitation Authority
240Makambako Urban Water Supply and Sanitation Authority
241Ministry of Natural Resources and Tourism
242Malinyi District Council
243Masasi Nachingwea Water Supply and Sanitation Authority
244Manyara Region
245Manyara Regional Referal Hospital
246Manyoni District Council
247Mara Region
248Mikocheni Agricultural Research Institute
249 Marine Parks and Reserves Unit 
250Masasi District 
251Masasi District Council
252Masasi Town Council
253Maswa District Council
254Maswa Water Supply and Sanitation Authority
255Manyoni Urban Water Authority
256Ministry of Information, Communication And Information Technology
257Mawenzi Regional Referal Hospital
258Mbarali District Council
259Mbeya Region
260Mbeya City Council
261Mbeya District Council
262Mbeya Regional Referal Hospital
263Mamlaka Ya Majisafi Na Usafi Wa Mazingira Jiji La Mbeya
NA.JINA LA TAASISI
264Mbinga District Council
265Mbinga Town Council
266Mbinga Urban Water Supply and Sanitation Authority
267Mbogwe Distict Council
268Mbozi Distict Council
269Mbulu Distict Council
270Mbulu Town Council
271Medical Council of Tanganyika
272Meatu Distict Council
273Meru Distict Council
274Tanzania Meteorological Authority
275Maritime Education and Training Fund
276Ministry of Natural Resources and Tourism Tanzania Forest Fund
277Ministry of Culture Arts and Sports
278Ministry of Livestock and Fisheries 
279Ministry of Livestock and Fisheries
280 Institute of Rural Development Planning
281Missenyi Distict Council
282Misungwi Distict Council
283Ministry of Investment, Industry And Trade
284 Mwalimu Julius K.Nyerere University Of Agriculture And Technology
285Mkalama Distict Council
286Mkinga Distict Council
287Mkulazi Holding Company Limited
288Mpango Wa Kurasimisha Rasilimali Na Biashara Za Wanyonge Tanzania
289Mkuranga Distict Council
290Mlele Distict Council
291Mlimba Distict Council
292Muleba Urban Water Supply and Sanitation 
293The Mwalimu Nyerere Memorial Academy
294Ministry of Natural Resources and Tourism 
295Moshi Co-Operative University
296Ministry of Defence And National Service
297Ministry of Education Science and Technology
298Ministry of Finance
299Ministry of Health
NA.JINA LA TAASISI
300Ministry of Home Affairs
301Muhimbili Orthopaedic Institute
302Momba Distict Council
303Monduli Distict Council
304Morogoro Region
305Morogoro Distict Council
306Morogoro Municipal Council
307Morogoro Regional Referal Hospital
308Morogoro Town Council
309Morogoro Water Supply and Sanitation Authority
310Moshi Distict Council
311Moshi Municipal Council
312Ministry of Works, Transport and Communications
313Mpanda Distict Council
314Mpanda Municipal Council
315Mpanda Water Supply and Sanitation Authority
316Mpimbwe Distict Council
317Mpwapwa Distict Council
318Makonde Plateau Water Supply and Sanitation Authority 
319Mpwapwa Urban Water Supply and Sanitation Authority 
320Mineral Resources Institute
321Msalala Distict Council
322Marine-Service-Co-Ltd
323Medical Stores Department 
324Ministry of Science And Technology
325Mount Meru Regional Referal Hospital
326Mtwara Water Supply and Sanitation Authority
327Mtwara Region
328Mtwara Distict Council
329Mtwara Mikindani Municipal Council
330Mufindi Distict Council
331Muheza Distict Council
332Muleba Distict Council
333Musoma District Council
334Musoma Municipal Council
335Mbeya University of Science and Technology
336Musoma Urban Water Supply and Sanitation Authority
337Moshi Urban Water Supply and Sanitation Authority
338Mvomero District 
NA.JINA LA TAASISI
339Mvomero District Council
340Mwananyamala Regional Referal Hospital
341Mwanga District Council
342Mwanhuzi Urban Water Supply & Sewerage Authority
343Mwanza Region
344Mwanza City Council
345Mwanza Urban Water Supply and Sanitation Authority
346College of African Wildlife Management, Mweka
347Ministry of Works And Transport
348Nachingwea District Council
349Namtumbo District Council
350Nanyamba Town Council
351Nanyumbu District Council
352Nanyumbu District Council
353National Audit Office
354National Ranching Company
355Unesco National Commission of The United Republic of Tanzania
356National Museum of Tanzania
357National Sports Council Of Tanzania
358National Board Of Accountants And Auditors
359National Bureau Of Statistics
360Ngorongoro Conservation Area Authority
361National Construction Council
362National College Of Tourism
363National Development Corporation
364National Defence College
365National Electoral Commission
366National Examinations Council Of Tanzania
367National Environment Management Council
368Newala District Council
369Newal Town Council
370National Fish Quality Control Laboratory
371National Food Reserve Agency
372Ngara District Council
373Ngara Water Supply And Sanitation Authority
374Ngaramtoni_Urban_Water_Supply_And_Sanitation_Authority
375Ngorongoro District Council
376National Housing And Building Materials Research Agency
NA.JINA LA TAASISI
377National Housing Corporation
378National Health Insurance Fund
379National Insurance Corporation 
380Mamlaka Ya Vitambulisho Vya Taifa
381National Institute For Medical Research
382National Irrigation Commission
383Ministry Of Energy
384National Institute Of Transport
385Ministry Of Foreign Affairs And East African Cooperation
386Njombe Region
387Njombe District Council
388Njombe Regional Referal Hospital
389Njombe Town Council
390Njombe Urban Water Supply And Sanitation Authority
391Nkasi District Council
392National Land Use Planning Commission
393Nelson Mandela African Institution Of Science And Technology
394The National Museum Of Tanzania
395National Meteorological Training Centre
396National Prosecutions Service
397National Sugar Insitute
398Nsimbo District Council
399National Social Security Fund
400Neglected Tropical Diseases Control Program
401National Water Fund
402Nyanghwale District Council
403Records And Archives Management Department
404Nyasa District Council
405Nzega District Council
406 Nzega Urban Water Supply And Sanitation Authority 
407Tanzania Open Government Partnership
408Ocean Road Cancer Institute 
409Orkesumet Urban Water Supply & Sewerage Authority.
410Office Of Registrar Of Political Parties
411The Office Of The Solicitor General
412Occupational Health And Health Agency In The Workplace
413Pangani Basin Water Board
414Pangani District Council
415Pan African Postal Union
NA.JINA LA TAASISI
416Tanzania Pyrethrum Board
417Parliament Of Tanzania
418Institute Of Wildlife Sciences Pasiansi
419Petroleum Bulk Procurement Agency
420Pharmacy Council
421Prevention And Combation Of Corruption Bureau (Pccb)     
422Office Of The Prime Minister
423President’s Office, Regional Administration And Local Government
424Tanzania Posts Corporation
425Public Procurement Appeals Authority
426Public Procurement Regulatory Authority
427Tanzania Prisons
428Public Service Commission
429 Procurement And Supplies Professionals And Technicians Board
430Petroleum Upstream Regulatory Authority
431Pwani Region
432Registration Insolvency And Trusteeship Agency
433Roads Fund Board
434Rombo District Council
435Rombo Water Supply And Sanitation Authority 
436Rorya District Council
437Ruangwa District Council
438Ruangwa Water Supply And Sanitation Authority 
439Rufiji Basin Water Board
440Rufiji District Council
441 Rujewa Water Supply And Sanitation Authority
442Rukwa Region
443Rukwa Basin Water Board
444Rungwe District Council
445Ruvuma Region
446Ruvuma Basin Water Board
447Rural Water Supply And Sanitation Agency
448Southern African Development Community Tanzania
449Same District Council
450Same Mwanga Water Supply And Sanitation Authority 
451Sugar Board Of Tanzania
452Self Microfinance Fund
NA.JINA LA TAASISI
453Sengerma District Council
454Serengeti District Council
455Sengerema Urban Water Supply And Sanitation Authority
456Ministry Of Constitutional And Legal Affairs
457Shinyanga Region
458Shinyanga District Council
459Shinyanga Municipa Council
460Mamlaka Ya Majisafi Na Usafi Wa Mazingira Mjini Shinyanga
461Small Industries Development Organization
462Siha District Council
463Sikonge District Council
464Simanjiro District Council
465Simiyu Region
466Singida Region
467Singida District Council
468Singida Municipal C Ouncil
469Sisal Board
470Songea District Council
471Songea Municipal Council
472Songwe Region
473Songwe District Council
474Songea Urban Water Supply And Sanitation Authority
475State Mining Corporation
476Stamigold Company Limited
477Sumbawanga District Council
478Sumbawanga Municipa Council
479Sumbawanga Regional Referal Hospital
480Singida Urban Water And Sanitation Authority 
481Sumbawanga Urban Water Supply And Sanitation Authority
482Tanzania Airports Authority
483Tabora Region
484Tabora Municipal Council
485Tanzania Commission For Aids
486Tanzania Agricultural Development Bank (Tadb)
487Tanzania Atomic Energy Commission
488Tanzania Forestry Research Institute
489Tanzania Global Learning Agency
490Tanzania Livestock Research Institute
491President’s Office Regional Administration And Local
NA.JINA LA TAASISI
 Government
492Tandahimba District Council
493Tanga Region
494Tanga City Council
495Tanganyika District Council
496Tanga Urban Water Supply And Sanitation Authority 
497Tanrail Investment Limited
498Tanzania National Roads Agency
499Tanzania Trade Development Authority
500Tanzania Government Portal
501Tanzania High Commission
502 Tanzania National Park
503Tanzania Tourist Board
504Tanzania Tourist Board
505Tanzania Agricultural Research Institute
506Tarime District Council
507Tarime Town Council
508Tarime Water Supply And Sanitation Authority
509Tanzania Rural And Urban Roads Agency
510Tanzania Shipping Agencies Corporation
511Tanzania Social Action Fund
512Taasisi Ya Sanaa Na Utamaduni Bagamoyo
513Tanzania Wildlife Management Authority
514Tanzania Wildlife Research Institute
515Tanzania Zambia Railway
516Tanzania Buildings Agency
517Tanzanian Broadcasting Corporation
518Tanzania Bureau of Standards 
519Tanzania Civil Aviation Authority
520Tanzania Civil Aviation Authority-Consumer Consultative Council
521Tanzania Cotton Board
522Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA)
523Tanzania Communications Regulatory Authority Consumer Consultative Council 
524Tanzania Commission for Universities
525Tanzania Milk Board
526Tanzania Education Authority
527Tea Board of Tanzania
528Tanzania Extractive Industries Transparency Initiatives
NA.JINA LA TAASISI
529Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organization
530Temeke Municipal Council
531Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency
532Tanzania Food and Drugs Authority
533Tanzania Food and Nutrition Centre
534Tanzania Fertilizer Regulatory Authority
535Tanzania Forest Service Agency
536Tanzania Gemmological Centre
537Tanzania Geothermal Development Company
538Tanzania Government Flight Agency
539Tanzania Institute of Accountancy
540Tanzania Investment Centre
541Tengeru Institute of Community Development
542Tanzania Institute of Education
543Tanzania Insurance Ombudsman
544Tanzania Insurance Regulatory Authority
545Tanzania Industrial Research and Development Organization
546Tanzania Library Services Board
547Tanzania Meat Board
548Tanzania Medicines and Medical Devices Authority
549 Tanzania Mercantile Exchange 
550National Business Council
551Tanzania Nursing & Midwifery Council
552Tanzania Tobacco Board
553Tobacco Research Institute of Tanzania
554Tanzania Official Seed Certification Institute
555Tanzania Ports Authority
556Tanzania Petroleum Development Corporation
557Tanzania People’s Defense Forces
558Tanzania Police Force
559Town Planners Registration Board
560Tropical Pesticides Research Institute
561Tanzania Public Service College
562Tanzania Railways Corporation
563Office of Treasury Registrar 
564Teachers’ Service Commission
565Tanzania Telecommunication Corporation
566Tanzania Tree Seed Agency
NA.JINA LA TAASISI
567Mining Commission
568Tunduma Town Council
569Tunduma Water Supply and Sanitation Authority
570Tunduru District Council
571Turiani Urban Water Supply and Sanitation Authority 
572Tunduru Urban Water Supply and Sanitation Authority 
573Tabora Urban Water Supply and Sanitation Authority
574 Tukuyu Water Supply and Sanitation Authority 
575Tanzania Veterinary Laboratory Agency
576Ubungo Municipal Council
577Ministry of Works and Transport 
578Communication Fund for All
579 University of Dodoma
580University of Dar Es Salaam
581Ukerewe District Council
582Ulanga District Council
583Uongozi Institute
584Ubungo Plaza Limited
585Urambo District Council
586Ushetu District Council
587Tume Ya Maendeleo ya Ushirika
588Ushirombo Water Supply and Sanitation Authority
589Ofisi Ya Rais – Menejimenti Ya Utumishi Wa Umma Na Utawala Bora
590Uvinza District Council
591Wizara Ya Uvuvi
592National Economic Empowerment Council
593Uyui District Council
594Vocational Education and Training Authority
595Vice President’s Office
596Valuers Registration Board
597Wangingombe District Council
598Wanging’ombe Water Supply and Sanitation Authority
599Water Institute
600Workers Compensation Fund
601Water Development and Management Institute
602Watumishi Housing Company
603 Weights and Measures Agency 
604Warehouse Receipt Regulatory Board

KIAMBATISHO NA. 4

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 172 ZILIZOUNGANISHWA KWENYE MFUMO WA OFISI MTANDAO-e-OFFICE

S/NJINA LA TAASISI
1Prime Minister’s Office Investment
2National Health Insurance Fund (NHIF)
3Tanzania Social Action Fund – TASAF
4Co-Operative Audit and Supervision Corporation (COASCO)
5National Identification Authority (NIDA)
6Tanzania Tourist Board (TTB)
7College of African Wildlife Management, Mweka
8Songwe Regional Administrative Secretariat Office (Songwe Ras)
9Tanzania Airports Authority – TAA
10Tanzania Tobacco Board 
11Air Tanzania Company Limited – ATCL
12Higher Education Students’ Loans Board (HESLB)
13Town Planners Registration Board (TPRB)
14Arusha City Council
15Tanzania Film Board
16Dar Es Salaam Water and Sewerage Authority (DAWASA)
17Prevention and Combation Of Corruption Bureau (PCCB)
18Tanzania Posts Corporation
19Tanzania Trade Development Authority (TANTRADE)
20Tanzania Government Flight Agency
21Commission for Human Rights and Good Governance
22Cereals and Other Produce Board of Tanzania
23Land Transport Regulatory Authority (LATRA)
24Institute of Judicial Administration (IJA)
25Architects and Quantity Surveyors Registration Board (AQRB)
26Medical Stores Department (MSD)
27Benjamin Mkapa Hospital
28Law Reform Commission of Tanzania
29College of Business Education (CBE)
S/NJINA LA TAASISI
30National Audit Office of Tanzania (NAOT)
31Judicial Service Commission
32Nelson Mandela African Institution of Science and Technology
33Tanzania Revenue Authority (TRA)
34Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA)
35National Water Fund
36The University of Dodoma
37Tanzania Agricultural Development Bank (Tadb)
38The Geological Survey of Tanzania
39Tanzania Institute of Education
40Tanzania Bureau of Standards (TBS)
41Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA)
42Tanzania Ports Authority (TPA)
43National Electoral Commission-NEC
44Tanzania Wildlife Authority – TAWA
45The Clerk National Assembly of Tanzania
46National Museum of Tanzania
47Mbeya Regional Administrative Secretariat Office
48Rukwa Region
49Lindi Regional Administrative Secretariat
50The Office of Attorney General
51Judiciary of Tanzania
52Mkulazi Holding Company – Mkulazi
53Institute of Finance Management (IFM)
54State Mining Corporation (STAMICO)
55Universal Communications Service Access Fund (UCSAF)
56Tanzania National Parks (TANAPA)
57Workers Compensation Fundd (WCF)
58Agricultural Inputs Trust Fund (AGITF)
59Fair Competition Tribunal
60National Examinations Council of Tanzania (NECTA)
61Dodoma Region
62Warehouse Receipt Regulatory Board (WRRB)
63Local Government Training Institute (LGTI)
64Tanzania Commission for Universities (TCU)
S/NJINA LA TAASISI
65Roads Fund Board
66Moshi Urban Water Supply and Sanitation Authority
67Ethics Secretariat
68Tanzania Food and Nutrition Centre
69Tanzania Meat Board
70Joint Finance Commission
71National Bureau of Statistics
72Njombe Ragional Administrative Secretariat
73Ikungi District Council
74Tanzania Veterinary Laboratory Agency
75Drug Control and Enforcement Authority (DCEA)
76Petroleum Upstream Regulatory Authority (PURA)
77Tume Ya Madini
78Mbeya University of Science and Technology
79Uongozi Institute
80Jeshi La Magereza Tanzania
81Public Procurement Appeal Authority (PPAA)
82Marine Services Company Limited (MSCL)
83Ministry Of Home Affairs
84Office of Registrar of Political Parties (ORPP)
85Dar es Salaam Maritime Institute
86Morogoro Regional Administrative Secretariat
87Kilimanjaro Airport Development Company (KADCO)
88Tanzania Fertilizer Regulatory Authority (TFRA)
89Livestock Training Agency (LITA)
90Rural Water Supply and Sanitation Agency (RUWASA)
91Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA)
92Singida Regional Administrative Secretariat
93Mwanza Regional Administrative Secretairet
94Mtwara Ragional Administrative Secretariat
95Tanzania Insurance Regulatory Authority (TIRA)
96Tanga Water Supply and Sanitation Authority
97Dar es Salaam Regional Administrative Secretariat
98Tabora Regional Administrative Secretariat
99National Development Corporation – NDC
S/NJINA LA TAASISI
100National Environment Management Council – NEMC
101Tanzania Education Authority
102Tanzania Investment Centre (TIC)
103Iringa Regional Administrative Secretariat
104Kilimanjaro Regional Administrative Secretariat
105Tanzania Forest Service Agency
106Fair Competition Commission (FCC)
107Tanzania Wildlife Research Institute (TAWIRI)
108Arusha Regional Administrative Secretariat
109Ministry of Livestock and Fisheries – Fisheries Sector
110Tanzania Cooperative Development Commission (TCDC)
111Property and Business Formalization Programme (MKURABITA)
112Tanga Regional Administrative Secretariat
113Kigoma Regional Administrative Secretariat
114Manyara Regional Administrative Secretariat
115Public Procurement Regulatory Authority (PPRA)
116Ministry of Livestock and Fisheries (Livestock)
117Tanzania Broadcasting Corporation (TBC)
118National Insurance Corporation (NIC)
119Gaming Board of Tanzania (GBT)
120Business Registrations and Licensing Agency (BRELA)
121Tanzania Railways Corporation (TRC)
122Occupational Safety and Health Authority (OSHA)
123The Office of Treasury Registrar
124Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board (PSPTB)
125Public Service Recruitment Secretariat (PSRS)
126Weights and Measures Agency (WMA)
127Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)
128Ministry of Health Community Development, Gender, Elderly and Children
129Government Chemist Laboratory Authority (GCLA)
130National Institute of Transport (NIT)
131Tanzania Building Agency (TBA)
132Pharmacy Council – Tanzania
S/NJINA LA TAASISI
133Tanzania Institute of Accountancy (TIA)
134The Office of The Solicitor General (OSG)
135Tanzania Medicines and Medical Devices Authority (TMDA)
136Engineers Registration Board (ERB)
137National Food Reserve Agency (NFRA)
138National Board of Accountants and Auditors (NBAA)
139Ministry of Natural Resources and Tourism
140Prime Minister’s Office, Labour, Youth, Employment and Persons with Disability
141Teachers’ Service Commission
142Ministry of Water
143Ministry of Finance
144Wizara ya Nishati
145Wizara ya Madini
146Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA)
147Wizara ya Elimu, Sayansi Na Teknolojia
148Tanzania Rural and Urban Roads Agency (TARURA)
149Government Procurement Services Agency (GPSA)
150National Housing and Building Research Agency (NHBRA)
151Tanzania Meteorological Agency (TMA)
152Ministry of Health
153Ministry of Agriculture
154Wizara Ya Ujenzi
155Tamisemi
156Vice President’s Office
157Ministry of Information, Culture, Arts and Sports
158Wizara ya Viwanda, Biashara Na Uwekezaji
159Wizara ya Katiba na Sheria
160Dar Rapid Transit (DART)
161Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
162Tanzania Global Learning Agency (TAGLA)
163Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
164Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
165Tanzania Public Service College (TPSC)
S/NJINA LA TAASISI
166Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi – Uchukuzi
167Public Service Commision
168Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
169Prime Minister’s Office
170Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
171Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa.
172e-Government Authority (e-GA)

KIAMBATISHO NA. 5

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 236 ZILIZOUNGANISHWA KATIKA MFUMO WA KUTOA

HUDUMA KWA NJIA YA SIMU ZA MKONONI (GOVERNMENT

MOBILE PLATFORM SYSTEM)

NA.JINA LA TAASISI
1Ministry of Finance
2Dar es salaam Water and Sewerage Corporation
3Tanzania Revenue Authority
4National Health Insurance Fund – NHIF
5Arusha Urban Water Supply and Sanitation Authority (AUWSA)
6Dodoma Urban Water Supply and Sewerage Authority
7Tanzania Livestock Research Institute (TALIRI)
8National Electoral Commission – NEC
9Mwanza Urban Water and Sewerage Authority
10Tanga Urban Water Supply and Sewerage Authority
11Iringa Urban Water Supply and Sewerage Authority
12Tanzania Rural and Urban Roads Agency-TARURA
13Shinyanga Urban Water Supply and Sanitation Authority
14Mbeya Urban Water supply and Sewerage Authority
15Tabora Urban Water Supply and Sewerage Authority
16Kahama Urban Water Supply and Sanitation Authority-Kahama UWASA
17Singida Urban Water and Sanitation Authority
18Workers Compensation Fund
19Bank of Tanzania – BOT
20National Council for Technical Education-NACTE
21Public Service Pensions Fund – PSPF
22Energy and Water Utilities Regulatory Authorities – EWURA
23Ministry of Agriculture, Food Security and Co-operatives
24Nationa Social Security Fund – NSSF
25Moshi Urban Water Supply and Sewerage Authority
26Morogoro Urban Water Supply and Sanitation Authority
27National Housing Corporation – NHC
28Sumbawanga Urban Water Supply and Sewerage Authority
NA.JINA LA TAASISI
29Nzega Urban Water Supply and Sanitation Authority
30Geita Urban Water Supply and Sanitation Authority (GEUWASA)
31Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Developments
32Mtwara Urban Water Supply and Sewerage Authority
33The Judiciary of Tanzania
34Musoma Urban Water and Sewerage Authority
35Masasi-Nachingwea Water Supply and Sanitation Authority
36Babati Urban Water Supply and Sewerage Authority
37Tanzania Railways corporation
38Bukoba Urban Water Supply and Sewerage Authority
39Bunda Urban Water Supply and Sanitation Authority (BUWSSA)
40Tanzania Electrical Supply Company Limited – TANESCO (Dodoma)
41Ministry of Regional Administration and Local Government (TAMISEMI)
42Songea Urban Water and Sewerage Authority
43Ethics Secretariate
44Njombe Urban Water Supply and Sanitation Authority
45Kigoma Urban Water Supply and Sewerage Authority
46Tanzania Commission for Universities – TCU
47Tanzania Atomic Energy Commission – TAEC
48Sengerema Water Supply and Sanitation Authority (SEUWASA)
49e-Government Authority
50Lindi Urban Water Supply and Sewerage Authority
51Chalinze Water Supply and Sanitation Authority-CHALIWASA
52Surface and Marine Transport Authority – SUMATRA
53Contractors Registration Board – CRB
54Igunga Urban Water Supply and Sanitation Authority – IGUWASA
55Medical Store Department
56Mbinga water supply and sanitation authority(mbingawssa)
57e-Government Zanzibar
58Kibaigwa water supply and sanitation authority
59Ministry of Health and Social Welfare
60JAKAYA KIKWETE CARDIAC INSTITUTE (JKCI)
61Ardhi University
NA.JINA LA TAASISI
62Occupational Health and Safety Authority – OSHA
63Tanzania Broadcasting Corporation – TBC
64Vocational Education and Training Authority – VETA
65Parastatals Pension Fund – PPF
66LAMADI WATER PROJECT(LAWAP)
67Mpanda Water Supply and Sanitation
68Tanzania Electrical Supply Company Limite – TANESCO (HQ)
69Makambako Urban Water Supply and Sanitation Authority (MAKUWASA)
70TUKUYU URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
71Fire Rescue Force (FRF)
72Public Service Recruitment Secretariate – PSRS
73Mzumbe University
74National Examination Council of Tanzania – NECTA
75Pharmacy Council Tanzania
76National Insurance Corporation (NIC)
77Tanzania Communications Regulatory Authority – TCRA
78Tanzania Buildings Agency – TBA
79Korogwe water supply and sanitation authority
80Tanzania Electric Supply Company Mwanza Region
81Handeni Trunk Main Water Supply and Sanitation Authority
82Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board (PSPTB)
83Chato Water Supply and Sanitation Authority
84Tanzania Electric Supply Company Limited Kinondoni North Region
85Mafinga Urban Water Supply and Saniration Authority (MAUWASA)
86Maswa water supply and sanitation authority
87University of Dodoma
88Manyoni Water Supply and Sanitation Authority
89Wanging’ombe Water Supply and Sanitation Authority
90Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC)
91Tanzania Insurance Regulatory Authority – TIRA
92The Parliament of Tanzania
NA.JINA LA TAASISI
93Eastern Africa Statistical Training Centre – EASTC
94Tanzania Electric Supply Company Limited Shinyanga Region
95Tanzania Trade Development Authority – TANTRADE
96Tanzania Electric Supply Company Limited Geita Region
97Tanzania Ports Authority – TPA
98Kinondoni Municipal Council
99Muleba Water Supply and Sanitation Authority …
100Mwanhuzi Urban Water Supply and Sanitation Authority (MWANHUZI UWSSA)
101Institute of Accountancy Arusha
102Sokoine University of Agriculture – SUA
103Mugumu Urban Water Supply and Sanitation Authority
104Bariadi urban water supply and sanitation authority
105Architects and Quantity Surveyors Registration Board
106NGARA URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY(NGUWASA))
107College of Business Education (CBE)
108Local Authority Pensions Fund – LAPF
109Kishapu Water Supply and Sanitation Authority
110Ministry of Natural Resources and Tourism
111Tanzania electric supply company limited tabora region
112Same mwanga water supply and sanitation authority (samwasa)
113BIHARAMULO WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
114Kilwa Urban Water Supply and Sanitation Authority
115Mamlaka ya Maji Kondoa (KONDOA WSSA)
116Tanzania Social Action Fund – TASAF
117Mpwapwa Water Supply and Sanitation Authority
118Arusha City Council
119Makonde Plateau Water Supply and Saniation Authority
120Vwawa-mlowo water supply and sanitation authority
121Tanzania National Parks – TANAPA
122Tanzania electric supply cooperation temeke region
123Ministry of Livestock and Fisheries (Livestock Sector)
124Tanzania Bureau of Standards – TBS
125Bank of tanzania training institute
NA.JINA LA TAASISI
126Institute of Rural Development Planning IRDP
127Maganzo Water Supply and Sanitation Authority
128National Audit Office
129Public Procurement Regulatory Authority – PPRA
130Ministry of Water
131Tanzania Electric Supply Company Limited Kilimanjaro Region
132Tanzania Electric Supply Company Limited Rukwa Region
133Benjamin Mkapa Hospital
134Tanzania Electric Supply Company Limited Arusha Region
135Institute of Finance Management (IFM)
136Dar es Salaam Rapit Transit Agency – DART
137Loliondo urban water supply and sanitation authority (loluwasa)
138Medical Council of Tanganyika
139Makete Urban Water Supply and Sanitation Authority- Makete – WSSA
140Tanzania electric supply company songwe
141Ngorongoro Conservation Area Authority – NCAA
142Tanzania Nurses and Midwives Council
143Dar es Salaam Stock Exchange-DSE
144Mugango/kiabakari water and supply authority
145Tanzania National Roads Agency – TANROADS
146Kasulu Water Supply and Sanitation Authority- Kasulu WSSA
147Government Procurement Service Agency – GPSA
148Tanzania Meat Board (TMB)
149National Environment Management Council
150Kibondo Water Supply and Sanitation Authority- Kibondo UWSSA
151Ministry of Minerals
152Tanzania Electric Company Limited Kagera
153Ministry of Works
154Muhimbili Orthopaedic Institute
155Karatu Water Supply and Sanitation Authority – Karatu-WSSA
156Tanzania Forest Services Agency – TFS
157Zanzibar housing corporation (zhc)
158ICT Commission (ICTC)
159Ifakara urban water supply and sanitation authority
NA.JINA LA TAASISI
160Tarime urban water supply and sanitation authority (taruwasa)
161Mbulu Water Supply and Sanitation Authority
162President’s Office, Public Service Management and Good Governance (UTUMISHI)
163Engineers Registration Board (ERB)
164Tanzania wildlife authority
165Roads Fund Board (RFB)
166Temeke Municipal Council
167Tanzania Electric Supply Company Limited-kigoma Region
168WATUMISHI HOUSING COMPANY
169Arusha Technical College-ATC
170Rufiji basin water board
171Tunduru Water Supply and Sanitation Authority- Tunduru WSSA
172Lindi Municipal Council
173College of African Wildlife Management, Mweka
174Tanzania Electric Supply Company Limited Mororogoro
175Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dae es Salaam
176Orkesumet urban water supply and sanitation authority (ouwasa)
177Ministry of of Constitution and Legal Affairs
178Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority
179Pangani Basin Water Board
180SUMA JKT
181Karagwe WSSA
182Open University of Tanzania
183Kinondoni Hospital
184Lake victoria basin water board
185Kibaya water supply and sanitation authority
186National Kiswahili Council of Tanzania
187Gaming Board of Tanzania
188Arusha Regional Commisioner
189National Housing Building Research Agency – NHBRA
190The National Economic Empowerment Council-NEEC
191Commission for Human Rights and Good Governance
192President office, Revolutionary Council
193Tanzania Electric Supply Company Limited Katavi
NA.JINA LA TAASISI
194Tanzania Electric Supply Company Limited Mara Region
195Wami Ruvu Basin
196Rural Water Supply and Sanitation Authority
197Katavi Regiona
198Meru District Council
199Tanzania Airports Authority
200High Court of Tanzania-labour Division
201Korogwe Town Council
202Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO)
203THE TANZANIA COOPERATIVE DEVELOPMENT COMMISSION
204Tanzania Film Board
205Mwanza City Council
206Tanzania Public Service College – TPSC
207National Kiswahili Council (BAKITA)
208Prime Minister’s Office, Labour, Youth Employment and Persons with Disability
209Kigoma Ujiji Municipal Council
210Kigoma Region
211Ruangwa Water Supply and Sanitation Authority- Ruangwa WSSA
212zanzibar disaster management commission
213Lake Rukwa Basin Water Board
214Ministry of Trade and Industry Zanzibar
215University of Dar es Salaam (UDSM)
216Ilala Municipal Council
217Agency for the Development of Educational Management – ADEM
218Water Development Management Institute – WDMI
219State Mining Corporation – STAMICO
220Misungwi District Council
221Marine Services Company Limited – MSCL
222Dar es Salaam City Council (DCC)
223EWURA Consumer Consultative Council
224RAS-MOROGORO
225Social Security Regulatory Authority – SSRA
226Export Processing Zones Authority – EPZA
NA.JINA LA TAASISI
227Police Force
228Business Registrations and Licensing Agency – BRELA
229Tanzania Food and Drugs Authority – TFDA
230Tanzania Government Chemistry Laboratory Agency – GCLA
231Tanzania Meteorological Agency – TMA
232RAS-IRINGA
233Registration, Insolvency and Trusteeship Agency – RITA
234Tanzania Investment Center – TIC
235Immigration
236Tanzania Tourist Board

KIAMBATISHO NA. 6

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 610 ZINAZOTUMIA MFUMO WA VIBALI VYA KUSAFIRIA

NJE YA NCHI (e-VIBALI SYSTEM)

NaJINA LA TAASISI
1.       Agency for the Development of Educational Management (ADEM)
2.       Agricultural Seed Agency (ASA)
3.       Agriculture Inputs Trust Fund – AGITF
4.       Air Tanzania Company Limited
5.       Amana Regional Referral Hospital
6.       Appropriate Technology Training Institute – ATTI
7.       Architects and Quantity Surveyors Registration Board – AQSRB
8.       Ardhi Institute Morogoro
9.       Ardhi Institute Tabora
10.  Ardhi University – ARU
11.  Arnautoglu Folk Development College
12.  Arusha City Council
13.  Arusha District Council
14.  Arusha International Conference Centre
15.  Arusha Regional
16.  Arusha Technical College
17.  Arusha Urban Water Supply and Sewerage Authority
18.  Babati District Council
19.  Babati Town Council
20.  Babati Urban Water Supply and Sanitation Authority
21.  Bagamoyo District Council
22.  Bahi District Council
23.  Bank of Tanzania – BOT
24.  Baraza la Kiswahili la Taifa – BAKITA
25.  Baraza la Michezo Tanzania – BMT
26.  Baraza la Sanaa la Taifa – BASATA
27.  Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
28.  Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA)
29.  Baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za Nishati na Maji
NaJINA LA TAASISI
 (EWURA CCC)
30.  Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi
31.  Bariadi District Council
32.  Bariadi Town Council
33.  Benjamin Mkapa Hospital
34.  Bigwa Folk Development College
35.  Biharamulo District Council
36.  Bodi ya Filamu Tanzania – TFB
37.  Buchosa District Council
38.  Bugando Medical Centre
39.  BUHANGIJA FDC
40.  Buhigwe District Council
41.  Bukoba District Council
42.  Bukoba Municipal Council
43.  Bukoba Urban Water Supply and Sanitation Authority (BUWASA)
44.  Bukombe District Council
45.  Bumbuli District Council
46.  Bunda District Council
47.  Bunda Town Council
48.  Busega District Council
49.  Busokelo DC
50.  BUSTANI TC
51.  Butiama District Council
52.  BUTIMBA TC
53.  Capital Markets and Securities Authority (CMSA)
54.  Cashewnut Board Of Tanzania
55.  CENTRE FOR AGRICULTURAL MECHANIZATION AND RURAL TECHNOLOGY (CAMARTEC)
56.  CEREALS AND OTHER PRODUCE BOARD
57.  CHALA FDC
58.  Chalinze District Council
59.  Chamwino District Council
60.  Chato District Council
61.  Chato District Council
62.  Chemba District Council
NaJINA LA TAASISI
63.  Chisalu fdc
64.  CHUO CHA DIPLOMASIA
65.  Chuo cha Ualimu Bunda
66.  CHUO CHA UALIMU KATOKE
67.  Chuo cha Ualimu Kitangali
68.  CHUO CHA UALIMU KOROGWE
69.  Chuo cha Ualimu Mamire
70.  CHUO CHA UALIMU MOROGORO
71.  Chuo cha ualimu Mpuguso
72.  CHUO CHA UALIMU MURUTUNGURU
73.  Chuo cha Ualimu Nachingwea
74.  Chuo Cha Ualimu Ndala
75.  Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM)
76.  Chuo cha Ualimu Sumbawanga
77.  CHUO CHA UALIMU TUKUYU
78.  Chuo cha ualimu Ufundi Mtwara
79.  Co-operative Audit and Supervision Corporation (COASCO)
80.  College of African Wildlife Management (MWEKA)
81.  College of Business Education – CBE
82.  Contractors Registration Board – CRB
83.  Copyright Society of Tanzania -COSOTA
84.  Dakawa Tc
85.  Dar Es Salaam City Council
86.  Dar es Salaam Maritime Institute – DMI
87.  Dar es Salaam RAS
88.  Dar es Salaam Stock Exchange PLC
89.  Dar es Salaam University College of Education (DUCE)
90.  Dar es Salaam Water and Sewerage Authority (DAWASA)
91.  Dar Rapid Transit (DART)
92.  Dar-es-Salaam Institute of Technology (DIT)
93.  Dodoma City Council
94.  Dodoma Regional Referral Hospital
95.  Dodoma Urban Water and Sanitation (DUWASA)
96.  Dodoma Urban Water Supply and Sanitation Authority
97.  e-Government Authority – eGA
NaJINA LA TAASISI
98.  Eastern Africa Statistical Training Centre
99.  Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA)
100.  Engineers Registration Board – ERB
101.  Ethics Secretariat
102.  Export Processing Zones Authority – EPZA
103.  Fair Competition Commission – FCC
104.  Fair Competition Tribunal – FCT
105.  Financial Intelligence Unit
106.  FISHERIES EDUCATION AND TRAINING AGENCY – FETA
107.  Gaming Board of Tanzania
108.  GEITA DISTRICT COUNCIL
109.  Geita Region
110.  Geita Town Council
111.  Geological Survey of Tanzania
112.  GEPF Retirement Benefits Fund
113.  GERA FDC
114.  Government Chemist Laboratory Authority – GCLA
115.  Government Procurement Services Agency – GPSA
116.  HAI DISTRICT COUNCIL
117.  HAITUMIKI – Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
118.  Halmashauri ya Mji Ifakara
119.  Halmashauri ya Mji wa Korogwe
120.  Halmashauri ya Walaya ya Lushoto
121.  Halmashauri ya Wilaya Kilwa
122.  Halmashauri ya Wilaya Misungwi
123.  Halmashauri ya Wilaya ya Gairo
124.  Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi
125.  Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero
126.  Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga
127.  Halmashauri ya Wilaya ya Muheza
128.  Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
129.  Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga
130.  Hanang District Council
131.  HANDENI DISTRICT COUNCIL
132.  HANDENI FDC
NaJINA LA TAASISI
133.  HANDENI TOWN COUNCIL
134.  Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu
135.  Higher Education Student’s Loans Board(HESLB)
136.  IFAKARA FDC
137.  Igunga District Council
138.  Ikungi District Council
139.  IKWIRIRI FDC
140.  Ilala Municipal Council
141.  Ileje District Council
142.  Ilemela Municipal Council
143.  ILONGA TC
144.  Ilula Folk Development College
145.  IMMIGRATION
146.  Immigration Services Department – ISD
147.  Information and Communication Technology (ICT) Commission
148.  INSTITUTE OF ACCOUNTANCY ARUSHA
149.  Institute of Adult Education (IAE)
150.  Institute of Judicial Administration Lushoto
151.  Institute of Rural Development Planning
152.  Institute of Social Work
153.  IRAMBA DISTRICT COUNCIL (IRAMBA DC)
154.  Iringa District Council
155.  Iringa Municipal Council
156.  IRINGA RAS
157.  Iringa Water Supply and Sanitation Authority
158.  Itigi District Council
159.  Itilima District Council
160.  Jakaya Kikwete Cardiac Institute – JKCI
161.  Jeshi la Magereza Tanzania
162.  Jeshi la Polisi Tanzania – TPF
163.  Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
164.  Joint Finance Commission – JFC
165.  Julius Nyerere International Airport – JNIA
166.  Kabanga TC
167.  KAGERA REGIONAL
NaJINA LA TAASISI
168.  Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority
169.  Kahama Town Council
170.  Kahama Urban Water Supply and Sanitation Authority
171.  Kakonko District Council
172.  Kalambo District Council
173.  Kaliua District Council
174.  Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
175.  KARAGWE DISTRICT COUNCIL
176.  KARATU DISTRICT COUNCIL
177.  KASULU DISTRICT COUNCIL (KASULU DC)
178.  KASULU FDC
179.  Kasulu Teachers’ College
180.  Kasulu Town Council
181.  Katavi Regional Referral Hospital
182.  Katumba FDC
183.  KIBAHA DISTRICT COUNCIL
184.  Kibaha Education Centre
185.  Kibaha Town Council
186.  KIBITI DISTRICT COUNCIL
187.  KIBONDO DISTRICT COUNCIL
188.  KIBONDO FDC
189.  Kibongoto Hospital
190.  Kigamboni Municipal Council
191.  Kigoma District Council
192.  KIGOMA REGION
193.  Kigoma Ujiji Municipal Council
194.  KIHINGA FDC
195.  Kilimanjaro Airport Development Company Limited – KADCO
196.  Kilimanjaro RAS
197.  Kilolo DC
198.  KILOSA DISTRICT COUNCIL
199.  Kilwa Masoko FDC
200.  KINAMPANDA
201.  Kinondoni Municipal Council
202.  KISANGWA FDC
NaJINA LA TAASISI
203.  Kisarawe District Council
204.  Kisarawe Folk College Development
205.  Kishapu District Council
206.  KITETO DISTRICT COUNCIL
207.  KIWANDA F.D.C
208.  Klerruu TC
209.  KONDOA DC
210.  KONDOA TOWN COUNCIL
211.  Kongwa District Council
212.  Korogwe District Council
213.  Kwimba Disrtrict Council
214.  KYELA DISTRICT COUNCIL
215.  Kyerwa District Council
216.  Ligula Regional Referral Hospital
217.  Lindi District Council (Lindi DC)
218.  Lindi Municipal Council
219.  Lindi Region
220.  LINDI URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY (LUWASA)
221.  LIVESTOCK TRAINING AGENCY
222.  Liwale District Council
223.  Local Government Training Institute – LGTI
224.  Longido District Council
225.  Ludewa District Council
226.  MADABA DISTRICT COUNCIL
227.  Mafia DC
228.  Mafinga Town Council
229.  Magu District Council
230.  MAHAKAMA YA TANZANIA
231.  MAKAMBAKO TOWN COUNCIL
232.  MAKETE DISTRICT COUNCIL
233.  MALINYI DC
234.  Malya Folk Development College
235.  Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA)
236.  Mamlaka ya Kudhibiti Kupambana na Dawa za Kulevya
NaJINA LA TAASISI
237.  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
238.  Mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)
239.  Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)
240.  MAMTUKUNA FDC
241.  Mandaka Tc
242.  Manyara Regional
243.  Manyara Regional Referral Hospital
244.  Manyoni District Council
245.  MARA REGION
246.  Marangu Teacher College
247.  MARINE SERVICES COMPANY LIMITED (MSCL)
248.  Masasi District Council
249.  MASASI FDC
250.  Masasi Town Council
251.  MASWA DISTRICT COUNCIL
252.  Maweni Regional Referral Hospital
253.  MBARALI DISTRICT COUNCIL
254.  Mbeya City Council
255.  Mbeya District Council
256.  Mbeya Region
257.  Mbeya Regional Referral Hospital
258.  Mbeya University of Science and Technology
259.  MBEYA WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
260.  Mbeya Zonal Referral Hospital
261.  Mbinga District Council
262.  Mbinga Town Council
263.  MBOGWE DISTRICT COUNCIL
264.  Mbozi District Council
265.  MBULU DISTRICT COUNCIL
266.  MBULU TOWN COUNCIL
267.  MEATU DISTRICT COUNCIL
268.  Medical Stores Department – MSD
269.  Meru District Council
270.  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)
NaJINA LA TAASISI
271.  Mhonda chuo cha Ualimu
272.  Mineral Resources Institute
273.  Mining Commission
274.  Mirembe Mental Health Hospital -MMHH
275.  MISSENYI DISTRICT COUNCIL
276.  MKALAMA DISTRICT COUNCIL
277.  Mkoa wa Dodoma
278.  Mkoa wa Katavi
279.  Mkulazi Holding Company Limited
280.  Mkuranga District Council
281.  Mkwawa University College of Education – MUCE
282.  Momba District Council
283.  Monduli District Council
284.  Monduli Teachers College
285.  Morogoro District Concil
286.  Morogoro Municipal Council
287.  Morogoro RAS
288.  Morogoro Regional Referral Hospital
289.  Morogoro Urban Water Supply and Sanitation Authority
290.  Morogoro Works Training Institute – MWTI
291.  Moshi Co-operative University
292.  MOSHI DISTRICT COUNCIL
293.  Moshi Municipal Council
294.  Mount Meru Regional Referral Hospital
295.  MPANDA DISTRICT COUNCIL
296.  MPANDA MUNICIPAL COUNCIL
297.  MPIMBWE DISTRICT COUNCIL
298.  MPWAPWA DISTRICT COUNCIL
299.  Mpwapwa Tc
300.  MSINGA FDC
301.  MTO WA MBU FDC
302.  MTWARA DISTRICT COUNCIL
303.  Mtwara Mikindani Municipal Council
304.  Mtwara Region
305.  Mtwara Teachers College
NaJINA LA TAASISI
306.  Mufindi District Council
307.  Muhimbili National Hospital – MNH
308.  Muhimbili Orthopaedic Institute – MOI
309.  Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS)
310.  Muleba District Council
311.  Musoma District Council
312.  MUSOMA FDC
313.  Musoma Municipal Council
314.  Musoma Regional Referral Hospital
315.  Musoma Urban Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)
316.  Mvomero District Council
317.  Mwalimu Julius K. Nyerere University of Agriculture and Technology (MJNUAT)-Butiama
318.  Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA)
319.  Mwananyamala Regional Referral Hospital
320.  MWANGA DISTRICT COUNCIL
321.  MWANVA FDC
322.  Mwanza City Council
323.  Mwanza Regional
324.  Mwanza Urban Water Supply and Sanitation Authority
325.  Mzinga Corporation – MZC
326.  Mzumbe University – MU
327.  NACHINGWEA DISTRICT COUNCIL
328.  NANDEMBO FOLK DEVELOPMENT COLLEGE
329.  NANYAMBA TOWN COUNCIL
330.  Nanyumbu District Council
331.  National Aids Control Programme – NACP
332.  National Audit Office
333.  National Board of Accountants and Auditors
334.  National Bureau of Statistics
335.  NATIONAL COLLEGE OF TOURISM
336.  National Construction Council – NCC
337.  National Development Corporation – NDC
338.  National Environment Management Council (NEMC)
339.  NATIONAL FOOD RESERVE AGENCY (NFRA)
NaJINA LA TAASISI
340.  National Housing Building Research Agency
341.  National Housing Corporation
342.  National Institute for Medical Research
343.  National Institute for Productivity
344.  National Institute of Transport (NIT)
345.  National Insurance Corporation (T) Limited – NIC
346.  National Irrigation Commission (nirc)
347.  National Land Use Planning Commission
348.  National Malaria Control Program
349.  National Museums of Tanzania
350.  NATIONAL RANCHING COMPANY LIMITED (NARCO)
351.  National Social Security Fund (NSSF)
352.  National Tuberculosis and Leprosy Programme
353.  Neglected Tropical Diseases Control Programme
354.  Nelson Mandela African Institute of Science and Technology – NMAIST
355.  Newala District Councill
356.  Newala Town Council
357.  Ngara District Council
358.  Ngorongoro Conservation Area Authority
359.  Ngorongoro District Council
360.  Njombe District Council
361.  Njombe RAS
362.  Njombe Regional Referral Hospital
363.  NJOMBE TOWN COUNCIL
364.  Nkasi District Council
365.  Nsimbo District Council
366.  Nyang’hwale District Council
367.  Nyasa District Council
368.  Nzega District Council
369.  NZEGA TOWN COUNCIL
370.  NZOVWE FDC
371.  Occupational Safety and Health Authority – OSHA
372.  Ocean Road Cancer Institute – ORCI
373.  OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA
NaJINA LA TAASISI
 UTAWALA BORA
374.  Ofisi ya Rais, Ikulu
375.  Ofisi ya Bunge, Tanzania
376.  Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
377.  Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
378.  Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
379.  Ofisi ya Rais, TAMISEMI
380.  OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA
381.  Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali
382.  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge
383.  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
384.  Ofisi ya Waziri Mkuu-Uwekezaji
385.  Open University of Tanzania (OUT)
386.  PANGANI DISTRICT COUNCIL
387.  Parastatal Pensions Fund
388.  Patandi ttc kanda ya kaskazini
389.  Petroleum Bulk Procurement Agency – PBPA
390.  Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA
391.  Pharmacy Council – Tanzania
392.  Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board
393.  Public Procurement Appeals Authority – PPAA
394.  Public Procurement Regulatory Authority (PPRA)
395.  Public Service Comminision – PSC
396.  Public Service Remuneration Board – PSRB
397.  PUBLIC SERVICE SOCIAL SECURITY FUND (PSSSF)
398.  Pwani RAS
399.  RECORDS AND ARCHIVES MANAGEMENT DEPARTMENT
400.  Records and Archives Management Department – RAMD
401.  Road Fund Board – RFB
402.  Rombo District
403.  Rombo District Council
404.  Rorya District Council
405.  Ruangwa District Council
406.  RUBONDO FDC
407.  Rufiji District Council
NaJINA LA TAASISI
408.  Rukwa RAS
409.  Rungwe District Council
410.  Rural Energy Agency – REA
411.  Rural Water Supply and Sanitation Agency (RUWASA)
412.  Ruvuma RAS
413.  SAME DISTRICT COUNCIL
414.  Sekou Toure Hospital
415.  SEKRITARIET YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA
416.  Self-Microfinance Fund
417.  Sengerema District Council
418.  Serengeti District Council
419.  SHINYANGA DISTRICT COUNCIL
420.  SHINYANGA MUNICIPAL COUNCIL
421.  Shinyanga RAS
422.  Shinyanga Regional Referral Hospital
423.  Shinyanga Urban Water Supply and Sanitation Authority
424.  Shirika la kuhudumia ya Viwanda Vidogo – SIDO
425.  Shirika la Masoko ya Kariakoo
426.  SIHA District Council
427.  Sikonge District Council
428.  SIMANJIRO DISTRICT COUNCIL
429.  Simiyu RAS
430.  Simiyu Regional Referral Hospital
431.  SINGACHINI TC
432.  Singida District Council
433.  SINGIDA FDC
434.  Singida Municipal Council
435.  Singida Regional Referral Hospital
436.  Singida Regional Secretariat
437.  Singida Urban Water Suppy and Sewerage Authority
438.  SOFI FDC
439.  Sokoine Regional Referral Hospital
440.  Sokoine University of Agriculture – SUA
441.  SONGEA DISTRICT COUNCIL
442.  Songea Municipal Council
NaJINA LA TAASISI
443.  Songea Regional Referral Hospital
444.  SONGEA URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
445.  SongeaTeachers’ College
446.  SONGWE DISTRICT COUNCIL
447.  Songwe RAS
448.  Songwe Regional Referral Hospital
449.  State Mining Corporation (STAMICO)
450.  State University of Zanzibar
451.  Sugar Board Tanzania – SBT
452.  Sumatra Consumer Consultative Council – SUMATRACCC
453.  SUMBAWANGA DISTRICT COUNCIL
454.  SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
455.  Surface and Marine Transport Regulatory Authority – SUMATRA
456.  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)
457.  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo- TASUBA
458.  TABORA MUNICIPAL COUNCIL
459.  TABORA REGION
460.  TABORA TEACHERS COLLEGE
461.  Tabora Urban Water Supply and sanitation authority (TUWASA)
462.  TANDAHIMBA DISTRICT COUNCIL
463.  TANDALA TC
464.  Tanga City Council
465.  Tanga RAS
466.  Tanga Regional Referral Hospital
467.  Tanga Urban Water Supply and Sewerage Authority
468.  TANGO FOLK DEVELOPMENT COLLEGE
469.  Tanzania Agricultural Development Bank Limited
470.  Tanzania Agriculture Research Institute
471.  Tanzania Airport Authority – TAA
472.  Tanzania Atomic Energy Commission – TAEC
473.  Tanzania Automotive Technology Centre
474.  Tanzania Broadcasting Corporation – TBC
475.  Tanzania Buildings Agency – TBA
476.  Tanzania Bureau of Standards – TBS
NaJINA LA TAASISI
477.  Tanzania Civil Aviation Authority – TCAA
478.  Tanzania Coffee Board
479.  TANZANIA COMMISSION FOR AIDS
480.  Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)
481.  Tanzania Cotton Board – TCB
482.  TANZANIA DAIRY BOARD
483.  Tanzania Education Authority (TEA)
484.  Tanzania Electric Supply Company Limited – TANESCO
485.  Tanzania Electrical,Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA)
486.  Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organization – TEMDO
487.  Tanzania Fertilizer company – TFC
488.  Tanzania Fertilizer Regulatory Authority (TFRA)
489.  Tanzania Fisheries Research Institute (TAFIRI)
490.  TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE – TFNC
491.  Tanzania Forest Reseach Institute (TAFORI)
492.  Tanzania Forestry Services Agency
493.  Tanzania Gemological Centre – TGC
494.  Tanzania Geothermal Development Company – TGDC
495.  TANZANIA GLOBAL LEARNING AGENCY
496.  Tanzania Global Learning Agency – TAGLA
497.  Tanzania Government Flight Agency (TGFA)
498.  Tanzania Industrial Research and Development Organization – TIRDO
499.  Tanzania Institute of Accountancy
500.  Tanzania Institute of Education (TIE)
501.  Tanzania Insurance Regulatory Authority – TIRA
502.  Tanzania Investment Centre (TIC)
503.  TANZANIA LIBRARY SERVICES BOARD(TLSB)
504.  TANZANIA LIVESTOCK RESEARCH INSTITUTE (TALIRI)
505.  TANZANIA MEAT BOARD – TMB
506.  Tanzania Medicines and Medical Devices
507.  Tanzania Mercantile Exchange PLC
508.  Tanzania Meteorological Agency – TMA
509.  Tanzania National Business Council
NaJINA LA TAASISI
510.  Tanzania National Road Agency (TANROADS)
511.  Tanzania Official Seed Certification Institute – TOSCI
512.  Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC)
513.  Tanzania Ports Authority (TPA 
514.  Tanzania Postal Bank
515.  Tanzania Postal Corporation – TPC
516.  TANZANIA PUBLIC SERVICE COLLEGE
517.  Tanzania Railway Corporation (TRC)
518.  Tanzania Revenue Authority
519.  Tanzania Shipping Agencies Corporation – TASAC
520.  Tanzania Sisal Board
521.  Tanzania Smallholders Tea Development Agency
522.  Tanzania Social Action Fund – TASAF
523.  TANZANIA SOCIAL SECURITY ASSOCIATION
524.  Tanzania Standard (Newspapers) Limited -TSN
525.  Tanzania Telecommunication Corporation – TTCL
526.  Tanzania Tobacco Board – TTB
527.  Tanzania Tourism Board
528.  Tanzania Trade Development Authority – TANTRADE
529.  Tanzania Veterinary Laboratory Agency – TVLA
530.  TANZANIA WILDLIFE MANAGEMENT AUTHORITY (TAWA)
531.  Tanzania Wildlife Research Institute
532.  Tanzania Zambia Railway Authority – Tazara
533.  TARIME DISTRICT COUNCIL
534.  Tarime Teachers College
535.  Tarime Town Council
536.  TARURA
537.  Tax Revenue Appeals Board
538.  Tax Revenue Appeals Tribunal
539.  TCAA – Consumer Consultative Council (TCAA-CCC)
540.  Tea Board of Tanzania – TTB
541.  Tea Research Institute of Tanzania (TRIT)
542.  Temeke District
543.  Temeke Municipal Council
544.  Temeke Regional Referral Hospital
NaJINA LA TAASISI
545.  Tengeru Institute of Community Development
546.  The Institute of Finance Managment – IFM
547.  The Land Transport Regulatory Authority (LATRA)
548.  The Law School of Tanzania
549.  TIB CORPORATE BANK LIMITED
550.  TIB Development Bank Limited
551.  Tobacco Research Institute of Tanzania
552.  Town Planners Registration Board
553.  Treasury Registrar – TR
554.  Tropical Pesticides Research Institute (TPRI)
555.  Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
556.  Tume ya Kurekebisha Sheria
557.  TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
558.  Tume ya Taifa ya Uchaguzi
559.  Tume ya usuluhuhishi na Uamuzi (CMA)
560.  Tume ya Utumishi wa Waalimu
561.  Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)
562.  Tunduma Town Council
563.  Tunduru District Council
564.  Twiga Bancorp
565.  Ubungo Municipal Council
566.  Ukerewe District Council
567.  UNESCO NATIONAL COMMISSION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
568.  Unit Trust of Tanzania
569.  Universal Communication Services Access Fund (UCSAF)
570.  University of Dar es Salaam (UDSM)
571.  University of Dodoma – UDOM
572.  UONGOZI INSTITUTE
573.  Urambo District Council
574.  URAMBO FDC
575.  Urban Water Supply and Sewerage Authority
576.  Ushetu District Council
577.  UTT Projects and Infrastructure Development Plc
578.  UVINZA DISTRICT COUNCIL
NaJINA LA TAASISI
579.  VIKINDU TEACHERS COLLEGE
580.  Vocational Education and Training Authority – VETA
581.  Vwawa-mlowo Water Supply and Sanitation Authority
582.  Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA)
583.  Wakala wa Usajili wa Biashara na leseni (BRELA)
584.  Wakala wa Vipimo – WMA
585.  Wanging’ombe DC
586.  Warehouse Receipts Regulatory Board – WRRB
587.  Water Institute
588.  Watumishi Housing Company
589.  Wizara ya Afya
590.  Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
591.  Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi
592.  Wizara ya Fedha na Mipango
593.  Wizara ya Katiba na Sheria
594.  WIZARA YA KILIMO
595.  Wizara ya Madini
596.  Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum
597.  Wizara ya Maji
598.  Wizara ya Maliasili na Utalii
599.  Wizara ya Mambo ya Ndani- MOHA
600.  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
601.  Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
602.  Wizara ya Mifugo na Uvuvi (MIFUGO)
603.  WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI – (UVUVI)
604.  Wizara ya Nishati
605.  Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Uchukuzi)
606.  Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi)
607.  Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
608.  Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo
609.  Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
610.  Workers Compensation Fund (WCF)

KIAMBATISHO NA. 7

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 277 ZINAZOTUMIA MFUMO WA KUSIMAMIA MIFUMO YA TEHAMA SERIKALINI (GISP)

NAJINA LA TAASISI
1Agency for The Development of Education Management
2Air Tanzania Company Limited
3Architects and Quantity Surveyors Registration Board (AQRB)
4Ardhi Institute Morogoro
5Arusha City Council
6Arusha Urban Water Supply and Sanitation Authority (AUWSA)
7Bagamoyo District Council
8Bank of Tanzania
9Bumbuli District Council
10Bunda urban water supply and sanitation authority
11Business Registrations and Licensing Agency (BRELA)
12Capital Markets and Securities Authority
13Cashewnut Board of Tanzania
14Central medical store-zanzibar
15Cereals and Other Produce Board of Tanzania (CPB)
16Coastal Region
17College of African Wildlife Management, Mweka
18Commission For Human Rights and Good Governance
19Contractors Registration Board
20Copyright Society of Tanzania (COSOTA)
21Dar es Salaam City Council
22Dar es Salaam Institute of Technology
23Dar es Salaam Maritime Institute
24Dar es Salaam Reginal Administrative Secretariat
25Dar es Salaam Stock Exchange-DSE
26Dar es Salaam Water and Sewerage Authority (DAWASA)
27Dar Rapid Transit (DART)
28Dodoma Region
NAJINA LA TAASISI
29Dodoma urban water supply and sanitation authority(duwasa)
30Driling and Dam Construction Agency (DDCA)
31Eastern africa statistical training centre (eastc)
32E-government authority
33e-Government Zanzibar
34Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA)
35Engineers Registration Board
36Ethics Secretariat
37Export Processing Zones Authority
38Fair Competition Commission
39Financial Intelligent Unit (FIU)
40Fisheries Education and Training Agency
41Gaming board of tanzania
42Government Chemist Laboratory Authority
43Government Procurement Services Agency (GPSA)
44Handeni District Council
45Higher education students’ loans board (heslb)
46Igunga Urban Water Supply and Sanitation Authority – IGUWASA
47Immigration Services Department
48Institute of Finance Management (IFM)
49Institute of Judicial Administration
50Institute of Social Work (ISW)
51Iringa water supply and sanitation authority(iruwasa)
52Jakaya Kikwete Cardiac Institute
53Kagera Region
54Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority
55Kahama Urban Water Supply and Sanitation Authority – (KAHAMA UWASA)
56Karagwe Water Sewarage and Sanitation Autority
57Kasulu District Council
58Katavi Regional
59Kibong’oto Infectious Diseases Hospital (KIDH)
60Kigoma regional administrative secretariat
61Kigoma ujiji urban water supply and sanitation authority
62Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO)
NAJINA LA TAASISI
63Korogwe Town Council
64Kyerwa District Council
65Land Transport Regulatory Authority
66Law Reform Commission of Tanzania
67Law School of Tanzania (LST)
68Lindi Municipal Council
69Lindi Region
70Lindi Urban Water Supply and Sanitation Authority
71Liwale District Council
72Local Government Training Institute
73Longido District Council
74Lushoto Water Sewarage and Sanitation Autority
75Makete Urban Water Supply and Sanitation Authority- Makete – WSSA
76Marine Services Company Limited
77Masasi-nachingwea water supply and Sanitation Authority (MANAWASA)
78Mbeya City Council
79Mbeya Regional Commissioner’s Office
80Mbeya University of Science and Technology (MUST)
81Mbeya Urban water supply and sanitation Authority
82Mbozi District Council
83Meatu District Council
84Medical Council of Tanganyika
85Medical Stores Department
86Mining Commission
87Ministry of Agriculture
88Ministry of communication and information technology (mcit)
89Ministry of Constitutional and Legal Affairs
90Ministry of Defence and National Service
91Ministry of education science and technology
92Ministry of Energy
93Ministry of Finance and Planning
94Ministry of foreign affairs and east african cooperation
95Ministry of Health,Community Development, Gender, Elderly and Children
NAJINA LA TAASISI
96Ministry of health community development gender elderly children (community development)
97Ministry of Home Affairs
98Ministry of industry, trade and investment
99Ministry of information, culture, arts and sports
100Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development
101Ministry of Livestock and Fisheries (Fisheries Sector)
102Ministry of Livestock and Fisheries (Livestock Sector)
103Ministry of Minerals
104Ministry of natural resources and tourism (mnrt)
105Ministry of water
106Ministry of Works, Transport and Communications
107Ministry Of Works, Transport And Communications (Communication Sector)
108Ministry of Works,Transport and Communications (Works Sector)
109Mkalama District Council
110Mkoa wa kaskazini unguja
111Mkulazi Holding Company
112Momba District Council
113Morogoro Municipal Council
114Morogoro Regional Administrative Secretary
115morogoro water supply and sanitation authority
116Mpwapwa District Council
117Mtwara Mikindani Municipal Council
118Mtwara Region
119Mtwara Urban Water Supply and Sewerage Authority
120MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL-MLOGANZILA
121Muhimbili National Hospital (MNH)
122Muhimbili orthopedic institute
123Muhimbili University College of Health and allied Sciences
124Muleba District Council
125Musoma Urban Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)
126Mwanza City Council
127Mwanza urban water and sanitation Authority
128Mzumbe University
NAJINA LA TAASISI
129National Audit Office of Tanzania
130National board of accountants and auditors
131National Bureau of Statistics
132National College of Tourism
133National Construction Council
134National council for technical education (NACTE)
135National Economic Empowerment Council
136National Electoral Commission
137National Environment Management Council (NEMC)
138National Examinations Council of Tanzania (NECTA)
139National food reserve agency (nfra)
140National health insurance fund (nhif)
141National Housing Corporation (NHC)
142National Identification authority (NIDA)
143National Institute for Medical Research
144National insurance corporation (nic)
145National Internet Data Center
146National Irrigation Commission (Nic)
147National Kiswahili Council (BAKITA)
148National Museum of Tanzania
149National Social Security Fund
150National Sports Council
151National water fund(nwf)
152Newala Town Council
153Ngorongoro Conservation Area Authority
154Nsimbo District Council
155Nyasa District Council
156Occupational Safety and Health Authority
157Ocean Road Cancer Institute
158Office of Registrar of Political Parties (ORPP)
159Ofisi ya mkuu wa mkoa mjini magharibi
160Petroleum Bulk Procurement Agency (PBPA)
161Pharmacy Council
162President’s Office Public Service Management and Good Governance
163President’s office regional administration and local
NAJINA LA TAASISI
 government(tamisemi)
164Prime minister office
165Prime Minister’s Office, Labour, Youth Employment and Persons with Disability
166Procurement and supplies professionals and technicians board (psptb)
167Property and Business Formalization Programme (MKURABITA)
168Public Procurement Appeals Authority
169Public Procurement Regulatory Authority
170Public Service Commission (PSC)
171Public Service Recruitment Secretariat (PSRS)
172PUBLIC SERVICE SOCIAL SECURITY FUND-(PSSSF)
173RECORDS AND ARCHIVES MANAGEMENT DEPARTMENT
174Registration Insolvency Trusteeship Agency
175Roads Fund Board
176Rural Water Supply and Sanitation Authority
177Ruvuma Region
178SELF Microfinance Fund
179Sengerema Urban Water Supply and Sanitation Authority (SEUWASA)
180Shinyanga Regional Administrative Secretariat
181Shinyanga urban water supply and sanitation authority (SHUWASA)
182Singida Region
183Singida Urban Water Suppy and Sewerage Authority
184Small industries development organization (SIDO)
185Sokoine University of Agriculture (SUA)
186Songea Urban Water Supply and Sanitation Authority
187Songwe Region
188State Mining Corporation (STAMICO)
189Sugar board of tanzania
190Sumbawanga Urban Water and Sewarage Authority
191Tabora Urban Water Supply and Sanitation Aauthority
192Tandahimba District Council
193Tanganyika District Council
194TANGA REGION
195Tanga water supply and sanitation authority
NAJINA LA TAASISI
196Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)
197Tanzania Agricultural Research Institute (TARI)
198Tanzania Airports Authority
199Tanzania Atomic Energy Commission
200Tanzania broadcasting corporation
201Tanzania Buildings Agency (TBA)
202Tanzania Bureau of Standards (TBS)
203Tanzania Commission for Aids
204Tanzania Commission for Science and Technology
205Tanzania Commission for Universities (TCU)
206Tanzania communications regulatory authority (TCRA)
207Tanzania cooperative development commission
208Tanzania Drugs Enforcement Authority
209Tanzania Education Authority
210Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA MT DEPOT)
211Tanzania Employment Services Agency
212Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organisation
213Tanzania Fertilizers Regulatory Authority
214Tanzania Fisheries Research Institute
215Tanzania Food and Nutrition Centre
216Tanzania Forest Research Institute (TAFORI)
217Tanzania Geothermal Development Company
218Tanzania Global Learning Agency
219Tanzania Institute of Accountancy
220Tanzania Institute of Education
221Tanzania Insurance Regulatory Authority
222Tanzania Investment Centre (TIC)
223Tanzania library services board
224Tanzania medicines and medical devices authority
225Tanzania Meteorogical Authority
226Tanzania National business Council
227Tanzania National Parks (TANAPA)
228Tanzania National Roads Agency
229Tanzania Official Seed Certification Institute
NAJINA LA TAASISI
230Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC)
231Tanzania Police Force
232Tanzania Ports Authority (TPA)
233Tanzania Postal Bank PLC
234TANZANIA POSTS CORPORATION
235Tanzania Prisons Service
236Tanzania Public Service College
237Tanzania railways corporation
238Tanzania Regional Immigration Training Academy (TRITA)
239Tanzania Revenue Authority
240Tanzania Rural and Urban Roads Agency
241Tanzania Shipping Agencies Corporation (TASAC)
242Tanzania Social Action Fund
243TANZANIA TELECOMMUNICATION CORPORATION
244Tanzania Tobacco Board
245Tanzania Tourist Board
246Tanzania Trade Development Authority (TANTRADE)
247Tanzania Veterinary Laboratory Agency
248Tanzania wildlife authority
249Tanzania Wildlife Research Institute
250Tanzania Zambia Railway Authority-TAZARA
251Tarime District Council
252Tax Revenue Appeals Board (TRAB)
253Tax Revenue Appeals Tribunal (TRAT)
254Teachers’ Service Commission
255Temeke Municipal Council
256The Clerk National Assembly of Tanzania
257The Geological Survey of Tanzania
258The Office of Attorney General
259The Open University Of Tanzania (OUT)
260THE UNIVERSITY OF DODOMA
261Tib development bank ltd
262Treasury Registrar Office
263Tunduma Water Supply and Sanitation Authority- Tunduma WSSA
NAJINA LA TAASISI
264Tunduru Water Supply and Sanitation Authority- Tunduru WSSA
265Universal Communications Service Access Fund (UCSAF)
267University of Dar es Salaam (UDSM)
268Uongozi Institute
269Urambo District Council
270Ushirombo urban water supply and sanitation authority- ushirombo wssa
271Utt asset management and investor services (uttamis)
272Vice President Office
273Vocational Education and Training Authority (VETA)
274Wanging’ombe Water Supply and Sanitation Authority
275Water Institute (WI)
276Watumishi Housing Company
277Weights and Measures Agency

KIAMBATISHO NA. 8

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 299 ZILIZOUNGANISHWA KWENYE MTANDAO WA

MAWASILIANO SERIKALINI (GOVERNMENT COMMUNICATION NETWORK -GOVNET)

NAJINA LA TAASISI
1Treasury Registrar (DSM,Mirambo-DSM,Dodoma)
2TANZANIA RAILWAY COOPERATION (TRC)(DSM)
3TACAIDS(DSM)
4Business Registration and Licensing Agency (BRELA) (DSM, MAGEREZA)
5Tanzania Government Flight Agency (TGFA) (DSM)
6Public Service Commission (DSM)
7Ministry of Home Affairs (DSM,UDOM-Dodoma,MtumbaDodoma)
8Judicial Service Commission (DSM)
9Vice President’s Office (Dodoma)
10PSRS (Dodoma)
11Ministry of Lands, Housing and Human Settlements (DSM,Dodoma,Udom-Dodoma)
12Ministry of Community Development, Gender and Children (Dodoma,Mtumba-Dodoma)
13Ministry of Education and Vocational Training (Dodoma,MtumbaDodoma)
14Government Chemist Laboratory Agency (GCLA) (DSM)
15Tanzania Public Service College (TPSC) (DSM)
16Attorney General (DSM,Mtumba-Dodoma,Ipagala_dom)
17eGA (DSM,Dodoma,Iringa,NOC-DSM,Research-Dodoma)
18Human Rights & Good Governance Commission (DSM)
19Prime Minister Office (Mlimwa-Dodoma,DSM)
20Registrar of Political Parties (DSM,Dodoma)
21National Assembly (DSM,Dodoma)
22Tanzania Building Agency (TBA) (DSM)
23Ministry of Finance (DSM,Dodoma,Mtumba-Dodoma,GepgDodoma)
24Ministry of Foreign Affairs and International Relations (JKCI- DSM,DSM,Mtumba-Dodoma,Dodoma,Udom-Dodoma)
NAJINA LA TAASISI
25Controller and Auditor General, National Audit Office (Dodoma)
26Registrar Court of Appeal (DSM)
27National Bureau of Statistics (NBS) (Dodoma)
28Ethics Secretariat (Dodoma)
29Ministry of Defence and National Service (MoDANS) (DSM,Mtumba-Dodoma,Msalato-Dodoma)
30Registration Insolvency and Trusteeship Agency (RITA) (DSM)
31Prevention and Combat of Corruption Beareu (PCCB) (DSM)
32National Archive Office (Dodoma)
33Ministry of Water and Irrigation (Dodoma)
34Drilling and Dam Construction Agency (DDCA) (DSM)
35Eastern Africa Statistical Training Centre (EASTC) (DSM)
36TMDA (DSM)
37Tanzania Meteorological Agency (TMA) (DSM)
38Dar es Salaam Rapid Trans (DART) (DSM)
39Water Development and Management Institute (WDMI) (DSM)
40Tanzania National Housing Research Bureau (DSM)
41Occupational Safety and Health Agency (OSHA) (DSM)
42National ID Authority (NIDA) (DSM)
43Ministry of Livestock Development and Fisheries (Dodoma,Mtumba-Dodoma)
44Ministry of Agriculture, Food Security and Co-operatives (Dodoma,)
45Ministry of Natural Resources and Tourism (Dodoma)
46National Electoral Commission (NEC) (DSM,Dodoma)
47National College of Tourism (NCT) (DSM)
48Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA) (DSM,Dodoma,Magogoni-DSM))
49Tanzania Airport Authority (TAA) (DSM)
50Tanzania Institute of Accountancy (TIA) (DSM)
51National Food Reserve Agency (NFRA) (Dodoma)
52Government Procurement Services Agency (GPSA) (DSM,Kurasini-DSM,Dodoma)
53Medical Stores Department (Mabibo-DSM, DSM)
54Weight and Measure Agency (DSM)
55TAMISEMI (Dodoma)
56Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA)
NAJINA LA TAASISI
 (Bagamoyo)
57Agency for Education Management (ADEM) (Bagamoyo)
58Office of Solicitor General (OSG) (DSM)
59State House (DSM,Dodoma)
60Tanzania National Road Agency (TANROAD) (DSM, DSM)
61President’s Office, Public Service Management (MtumbaDodoma,Udom-Dodoma)
62Ministry of Information, Culture and Sports(MtumbaDodoma,Dodoma)
63Ministry of Industries, Trade and Marketing (MtumbaDodoma,Dodoma)
64Pharmacy Councilm (DSM,Dodoma)
65Ministry of Health (Dodoma)
66Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Bunge na Uratibu (Mtumba-Dodoma)
67National Land Information Center(Kinondoni-DSM,UbungoDSM,Kurasini-DSM,DSM)
68 Mfuko wa Maji(National Water Fund) (Dodoma)
69MINISTRY OF WORKS AND TRANSPORT (MtumbaDodoma,Dodoma)
70Ministry of Communication and Information Techology(Dodoma)
71PRIME MINISTER’S OFFICE, LABOUR, YOUTH EMPLOYMENT AND PERSONS WITH DISABILITY(Dodoma,Mtumba-Dodoma)
72National Prosecutions Service (Ofisi ya Mashitaka-DPP)(DSM,Dodoma)
73Tanzania Rural and Urban Roads Agency(TARURA) (Dodoma)
74Ofisi ya Magereza (Dodoma)
75COSTECH (DSM)
76NBAA (DSM,Bunju-DSM)
77Ministry of Minerals (Mtumba-Dodoma,Dodoma)
78Ministry of constitutional and Legal Affairs (MtumbaDodoma,Udom-Dodoma)
79ERB (DSM,Dodoma)
80Ministry of Energy (Mtumba-Dodoma,Dodoma)
81High Court(DSM)
82TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA (Dodoma)
83Teachers Service Commission (Dodoma)
84Benjamin William Mkappa Hosp-udom (Dodoma)
NAJINA LA TAASISI
85Marine Services Company Limited (Mwanza)
86TTCL (DSM)
87SIDO (DSM)
88PSPTB (DSM)
89NIT (DSM)
90RUWASA (Dodoma)
91Drug Control and Enforcement Authority(DCEA) (DSM,Dodoma)
92COASCO (Dodom)
93National Development Corporation(NDC) (DSM)
94Tanesco – GePG (eBGP) (DSM)
95Gaming Board Tanzania (DSM,Dodoma)
96Public Procurement Regulatory Authority (PPRA) (DSM,Dodoma)
97NCC (DSM)
98National Insurance Corporation (NIC) (DSM)
99Tanzania-Zambia Railway Authority (TAZARA) (DSM)
100Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) (DSM)
101Muhimbili National Hospital (MNH) (DSM)
102MKULAZI HOLDINGS (Morogoro)
103Tanzania Vetinary Laboratory Agency (TVLA) (DSM)
104LATRA (DSM)
105Geological Survey of Tanzania (Dodoma)
106Mkurabita (Dodoma)
107FCC (DSM,Dodoma)
108AcGEN (Dodoma)
109UDOM (Dodoma)
110MUHAS  (DSM)
111Tanzania Investment Centre (TIC)  (DSM)
112Tanzania Wildlife Management Authority (TAWA) (DSM)
113TTB (DMS)
114NEMC  (DSM)
115TEA (DSM)
116TANGA UWASA (Tanga)
117LAW REFORM (Dodoma)
118Tanzania Broadcasting Corporation(TBC)  (DSM)
119UCSAF (Dodoma)
NAJINA LA TAASISI
120TCAA (DSM)
121TIRA (DSM)
122Mbeya University of science and Tech(MUST) (Mbeya)
123CHUO CHA DIPLOMASIA (CFR) (DSM)
124KADCO  (Kilimanjaro)
125CBE (DSM)
126TANZANIA FILM BOARD (DSM)
127IRDP (Dodoma)
128IVD (DSM)
129SUGAR BOARD OF TANZANIA (DSM)
130PBPA (DSM)
131TPC (DSM)
132TLSB (DSM)
133AQRB (DSM)
134ASA (Morogoro)
135CHUO CHA MWEKA (Moshi)
136TALIRI (Dodoma)
137TAWIRI (Arusha)
138SELF-MICROFINANCE (DSM)
139WMA (DSM)
140Road Fund Board(RFB) (Dodoma)
141Tanzania Library Service Board(TLSB) (DSM)
142Fair Competition Tribunal(FCT ) (Dodoma)
143Tanzania Nursing and Midwifery Council(TNMC) (Dodoma)
144Arusha Technical College(ATC)(Arusha)
145Mifugo Uvuvi(Mwanza,Mwanza)
146Tanzania Meat Board(TMB)
147DIT(DSM)
148TCRA
149JKCI(DSM)
150TFNC(DSM)
151NATIONAL MUSEUM TANZANIA (NMT)(DSM)
152CBE(DOM)
153IFM(DSM)
154Commission for human rights and good governance (DOM)
NAJINA LA TAASISI
155MANAWASA(Masasi)
156VETA(DOM)
157Agricultural Inputs Trust Fund (AGITF) — Ministry of Agriculture(DODOMA)
158IAA(ARUSHA)
159LGTI_HOMBOLO(DOM)
160MZUMBE(MOROGORO)
161NHIF(DAR)
162TANTRADE(DAR)
163SUA(MOROGORO)
164Moshi Urban WSSA(MOSHI)
165CBE(MWANZA)
166Institute Of Judicial Administration(LUSHOTO)
167Ardhi University(DSM)
168Law School(DSM)
169Medical Council of Tanganyika(MCT)(DODOMA)
170TAEC(ARUSHA)
171BMT(DSM)
172Instute of Social Works(DAR)
173TBS(DAR)
174Marine Park and Reserve Unit (MPRU)(DAR)
175JFC(DAR)
176COSOTA(DAR)
177TIE(DAR)
178BASATA(DAR)
179CashewNut Board(Mtwara)
180Fair Competition Tribunal(FCT ) (Dar es Salaam)
181TEMDO(ARUSHA)
182TAEC(DSM)
183Ministry of Health(NHIF_Building)(Dodoma)
184TNBC(Dar es Salamma)
185Milembe Hospital(Dodoma)
186TARI(DODOMA)
187TACAIDS(DOM)
188BODI YA TUMBAKU(TABORA)
NAJINA LA TAASISI
189Cereals Board (Dodoma)(CPBT)
190MOCU(Moshi)
191HELSB(DSM)
192MWANANYAMALA HOSPTAL
193National Stadium(Dar es Salaam)
194NBTS (Damu Salama)(Dar es Salaam)
195TMB(Dodoma)
196Digital Tanzania Office(Dodoma)
197Nelson Mandela African Institution of Science and Technology (NM-AIST) (Arusha)
198PSC(DODOMA)
199Njombe RRH(Njombe)
200TCB(Mwanza)
201IRDP (Mwanza)
202TCU(Dar es Salaam)
203Uongozi Institute(Dar es Salaam)
204RUFIJI WATER BASIN(Iringa)
205NIMR (Dar es Salaam)
206UTT AMIS (Dar es salaam )
207PSC-DODOMA
208MBEYA ZONAL RRH(MBEYA)
209NLUPC(DODOMA)
210NPHL(DAR ES SALAAM)
211CHATO RRH(GEITA)
212TEMESA_DODOMA(DOM)
213AUWSA(ARUSHA)
214TRA(DSM)
215Judical delivery service commission(DSM)
216CAMARTEC(ARUSHA)
217TASAC(DSM)
218Nida(Zanzibar)
219MWAUWASA (Mwanza)
220MORUWASA (Morogoro)
221Songwe RRH (Songea)
222IMMIGRATION Kurasini (Dar es Salaam)
NAJINA LA TAASISI
223Dodoma RS
224Dodoma DC
225Dodoma MC
226Dodoma Regional Hospital
227Dar es Salaam RS
228Morogoro RS
229Morogoro DC
230Morogoro MC
231Morogoro Regional Hospital
232Lindi RS
233Lindi DC
234Lindi MC
235Sokoine Hospital (Lindi)
236Mtwara RS
237Mtwara DC
238Mtwara MC
239Lugala Regional Hospital
240Arusha RS
241Arusha CC
242Arusha DC
243Mount Meru Regional Hospital
244Kilimanjaro RS
245Moshi MC
246Moshi DC
247Mawenzi Hospital
248Tanga RS
249Mkinga DC
250Tanga CC
251Bombo Hospital
252Manyara RS
253Batati DC
254Babati TC
255Manyara Regional Hospital
256Songea MC
258Songea DC
NAJINA LA TAASISI
259Ruvuma RS
260Ruvuma Regional Hospital
261Iringa RS
262Iringa MC
263Iringa DC
264Iringa Regional Hospital
265Mbeya RS
266Mbarali DC
267Mbeya DC
268Mbeya Regional Hospital
269Shinyanga RS
270Shinyanga MC
271Shinyanga DC
272Shinyanga Regional Hospital
273Kagera RS
274Bukoba MC
275Bukoba DC
276Kagera Regional Hospital
277Mwanza RS
278Mwanza CC
279Ilemela MC
280Sekoutoure Regional Hospital
281Mara RS
282Musoma MC
283Musoma DC
284Mara Regional Hospital
285Tabora RS
286Tabora MC
287Tabora DC
288Kitete Regional Hospital
289Rukwa RS
290Sumbawanga DC
291Rukwa Regional Hospital
292sumbawanga MC
293Kigoma RS
NAJINA LA TAASISI
294Kigoma DC
295Kigoma MC
296Maweni Regional Hospital
297Singida RS
298Singida DC
299Singida MC

KIAMBATISHO NA. 9

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 121 ZILIZOWEZESHWA KUHIFADHI MIFUMO KWENYE

VITUO VYA KUHIFADHIA TAARIFA NA MIFUMO YA SERIKALI

(GOVERNMENT DATA CENTRES)

NA.JINA LA MFUMOTAASISI
1. Government Mailing System (eGA)e-Government Authority
2. Government Mobile Platform (mGOV)e-Government Authority
3. Government ICT Service Portal (GISP)e-Government Authority
4. Government Websites (GWS)Government Websites
5. Enterprise Resource Planning (ERMS) e-Government Authority
6. Helpdesk System, e-Mikutano, eProject, e-Boarde-Government Authority
7. e-Office ApplicationRAMD
8. e-Vibali System (PO)Presidents Office
9. Government e_payment Gateway (MoF)Ministry of Finance and Planning (MoFP)
10.Government Payment System (MUSE)Ministry of Finance and Planning (MoFP)
11.Ajira portal (PSRS)Public Services Recruitment Secretariat (PSRS)
12.Government Websites (GWF)President Office – Regional Administration and Local Government Authority
13.e-Ticketing System (MSCL)Marine Services Company Limited (MSCL)
14.Parliament Online Information System (BUNGE)Parliament of Tanzania (BUNGE)
15.Hospital Management System (ORCI)Ocean Road Cancer Institute 
16.Judicial Statistical Dashboard SystemJudiciary of Tanzania
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
 (Judiciary) 
17.Case Inventory Management Information SystemOffice of Solicitor General (OSG)
18.Water Sector Development Programme Management Information System (MoWI)Ministry of Water and Irrigation (MoWI)
19.Online Passport Application System (OPAS)Immigration Department
20.Agriculture Trade Management Information System (ATMIS) (Ministry of Agriculture)Ministry of Agriculture
21.Ardhi Management Information System (Ardhi Institute Tabora)Ardhi Institute Tabora
22.Online Registration System (PSPTB)PSPTB
23.PMO Dashboard SystemPMO Dashboard System
24.Gaming Board of Tanzania (GMB)Gaming Board Of Tanzania (GBT)
25.NBAA payment portalNBAA Agency
26.Shipping Business Management SystemTanzania Shipping Agency Cooperation (TASAC)
27.Tanzania electronic Single Windows System (TeSWS)TPA/TRA
28.Online booking SystemTanzania Railways Corporation (TRC)
29.e-Document Management SystemParliament of Tanzania
30.DSE mobile trading platformDar es Salaam Stock Exchange (DSE)
31.LATRALATRA
32.MAJI Information System (billing system)Ministry of Water (MoW)
33.Dar City NavigatorDART
34.Judicial Statistical Dashboard System (Judiciary)Judiciary of Tanzania (JUDICIARY)
35.Fertilizer Management SystemTanzania Fertilizer Regulatory Authority (TFRA)
36.Bakita Experts Database Registration Systems  BAKITA
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
37.Complain Management Information SystemCHRAGG
38.Case Management SystemAttorney Generals Office (AG)
39.Tarura e-Revenue Management Information System (TeRMIS)TARURA
40.Government Portal Ministry of Information, Culture, Arts and Sports
41.Mweka Management Information System Mweka Wildlife College
42.Electronic Case Management SystemCommission for Mediation and Arbitration (CMA)
43.Management Information System Engineers Registration Board (ERB)
44.Human Resource Compliance Information System (HRCIS)Public Service Commission (PSC)
45.Association and Accounting SystemNational Sports Council (NSC)
46.PLANREPOffice of Treasury Registrar (TRO)
47.WorkPlace Information Management System OSHA
48.Mineral Market Management Information System Minerals Commission
49.Billing  SystemMafinga Urban Water Supply and Sanitation Authority (MAUWASA)
50.Billing  SystemNgaramtoni Urban Water Supply and Sanitation Authority (NGUWASA)
51.Billing  System (WACOMS)Sengerema Urban Water Supply and Sanitation Authority (SEUWASA)
52.Billing  SystemTANTRADE
53.Billing  SystemNgudu Water Supplies and Sanitation Authority
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
54.Students Information Management SystemBandari College (TPA)
55.E-Office ApplicationTanzania Airport Authority (TAA)
56.Online RAC Application Tanzania Atomic Energy Commission (TAEC) 
57.Enterprise Resource Planning (ERP) Cereal Board of Tanzania
58.Cotton Classification Information System Tanzania Cotton Board (TCB)
59.OSIMDar es Salaam Institute of Technology (DIT)
60.Cloud ServiceDar es Salaam Maritime Institute (DMI)
61.TIRA Management Information SystemTanzania Insurance Regulatory Authority (TIRA)
62.Farmers Registration Management Information System Cashewnut Board of Tanzania
63.Lawyers Database System Ministry of Constitutional and Legal Affairs (MoCLA)
64.Fire Safety Inspection and Revenue Management System (FSIRMS)Fire and Rescue Force (FRF)
65.Online Application System Medical Council of Tanganyika (MCT)
66.Mineral Information System PortalMinerals Commission
67.MoCLA Management Information SystemMoCLA
68.Private Sector Integrated Surveillance SystemMoHDCGEC
69.Registration of Society Management Information SystemMinistry of Home Affairs (MoHA)
70.Online Madini ForumMinistry of Minerals
71.Online Commodity Trading SystemTanzania Merchantile Exchange (TMX)
72.AQRB Management Information SystemAQRB
73.Online Registration System COSOTA
74.Laboratory Information Management System Ministry of Water
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
75.Cap price systemEnergy Water Utilities Regulatory Authority
76.Open Public Acess CatalogParliament of Tanzania (BUNGE)
77.e-MrejeshoPoPSMGG
78.Automated Fare Collection System (AFCS)DART
79.Voter Identification System (VIS)NEC
80.Observers Management System (OMS)NEC
81.Online Application System University of Dodoma (UDOM)
82.WRRB License Application Management SystemWarehouse Receipt Regulatory Board (WRRB)
83.SIDO PortalSIDO
84.Coffee Marketing SystemTanzania Coffee Board (TCB)
85.TIC Billing SystemTanzania Investiment Center (TIC)
86.College of Information and Communication Technology (CoICT)UDSM
87.VETA Online Application SystemVETA
88.Electronic Appointment System (MoI)MOI
89.Natural Gas Billing SystemTPDC
90.TNMC Information SystemTNMCIS
91.Registration and management of information for nurses and midwives in TanzaniaTNMCIS
92. TALIRITALIRI
93.Management Information System NIC(LTD)
94.AMCOS Management SystemAMCOS
95.Information Resource Center SystemMinistry of Foreign Affairs
96.Ushirika ApplicationKINONDONI MC
97.RUWASA Service Delivery and Management SystemRUWASA
98.WebsiteTBC
99.Online Application System TBS
100.Billing SystemKishapu Water
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
  Supplies and Sanitation System
101.Water Use Management Information SystemWRBWB
102.Birth and Death Registration System (RITA)RITA
103.Tanzania National Business Portal (TNBP)BRELA
104.Traffic Management System (TMS+ Mailing SystemTPF
105.e-Procurement System (PPRA)PPRA
106.Water Point Mapping (MoWI)Ministry of Water and Irrigation (MoWI)
107.Mailing system for Tanzania Ports Authority/Other systemsTanzania Ports Authority (TPA)
108.Disaster recovery for RFB core systemsRoad Fund Board (RFB)
109.Disaster recovery for SSRA core systemsSSRA
110.Water Point Data Manager (MoWI)Ministry of Water and Irrigation (MoWI)
111.Government Real Estate Management System (GRMS)Tanzania Building Agency (TBA)
112.TCU Registration SystemTanzania Commission for Universities (TCU)
113.TASAF MIS applicationTASAF
114.Integrated Financial Management System (GPSA)GPSA
115.Integrated Financial Management Information System (WMA)WMA
116.Workers Compensation Fund mailing system (DR)WCF
117.Financial Management System (UVUVI)Mifugo Uvuvi
118.Financial Port management system and other systems (TPA)Tanzania Ports Authority (TPA)
119.Online Declaration SystemEthics Secretariat
120.Human Capital Management Information System (HCMIS)PoPSMGG
121.Tanzania Instant Payment System (TIPS)Bank of Tanzania (BoT)
122.Various SystemsNational Health
NA.JINA LA MFUMOTAASISI
  Insurance Fund (NHIF)
123.Various SystemsMSD
124.Various SystemsEWURA
125.TANePSPublic Procurement Regulatory Authority
126.Billing SystemTEMESA
127.Various SystemsUCSAF
128.Various SystemsFCC
129.TERMISTARURA

KIAMBATISHO NA. 10

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 28 ZINAZOTUMIA MFUMO WA ENTERPRISE RESOURCE

MANAGEMENT SUITE – ERMS

NA.TAASISI
1Tanzania Commission for Science and Technology
2Kahama Urban Water Supply and Sanitation Authority – (KAHAMA UWASA)
3Sugar board of Tanzania
4National Food Reserve Agency (NFRA)
5Iringa water supply and sanitation authority (IRUWASA)
6Tanzania Civil Aviation Authority
7Tanzania Library Services Board
8TANZANIA TELECOMMUNICATION CORPORATION
9Tanzania Railways Corporation
10Tanzania cooperative development commission inspection and supervision fund
11Procurement and supplies professionals and technicians board (PSPTB)
12National insurance corporation (NIC)
13e-Government Authority
14Mkulazi Holding Company
15Mtwara Urban Water Supply and Sewerage Authority
16National Board of Accountants and Auditors
17Small industries development organization (SIDO)
18President’s Office Public Service Management and Good Governance
19National Health Insurance Fund (NHIF)
20Workers Compensation Fund (WCF)
21Tanzania Telecommunication Regulatory Authority (TCRA)
22Ministry of Health – IVD
23Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu
24Muhimbili Orthopedic Institute
25Vice President’s Office
26Tanzania Medicines and Medical Devices Authority
27Fair Competition Commission
28Tanzania Broadcasting Corporation

KIAMBATISHO NA. 11

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)

TAASISI 427 ZILIZOUNGANISHWA NA KUTUMIA DAWATI LA

HUDUMA KWA WATEJA (HELPDESK SYSTEM)

Na.JINA LA TAASISI
1.  Accountant General (ACGEN)
2.  Authority for The Development of Educational Management (ADEM)
3.  Agricultural Inputs Trust Fund (AGITF)
4.  Air Tanzania Company Limited (ATCL)
5.  Tanzania Fertilizer Regulatory Authority (Tfra)
6.  Ardhi Institute Tabora (Arita)
7.  Ardhi University (Aru)
8.  Architect‘S And Quantity Surveyors Registration Board (Aqrb)
9.  Arusha City Council
10.Arusha District Ouncil
11.Arusha Regional And Administrative Secretariat
12.Arusha Urban Supply And Sewerage Authority (Auwsa) 
13.Attorney General‘S Chambers (Agc)
14.Babati District Council
15.Babati Town Council
16.Bagamoyo College Of Arts (Tasuba)
17.Bagamoyo District Council
18.Bahi District Council
19.Bariadi District Council 
20.Bariadi Town Council
21.Biharamulo District Council
22.Bokoba Municipal Ouncil
23.Buhigwe District Council
24.Buchosa District Council
25.Bukoba  District Council
26.Bumbuli District Council
27.Bunda District Council
28.Busega District Council 
29.Business Registration And Licencing Authority  (Brela)
30.Butiama District Council
Na.JINA LA TAASISI
31.Capital Market And Security Authority (Cmsa)
32.Centre For Agricultural Mechanization And Rural Technology (Camartec)
33.Cereals And Other Produce Board Of Tanzania (Cpb)
34. Commission For Human Rights And Good Governance (Chragg)
35.Cooperative Audit And Supervision Corporation (Coasco)
36.Dar Es Salaam Ras
37.Dar Es Salaam City Council
38.Dar Es Salaam Marine Institute (Dmi)
39.Dar Es Salaam Rapid Transport (Dart)
40.Dar Es Salaam University College Of Education (Duce)
41.Dar Es Salaam Water And Sewerage Cooperation (Dawasco)
42.Dar Es Salaam Water And Sewerege Authority (Dawasa)
43.Deep Sea Fishing Authority (Dfsa)
44.Dodoma Ras 
45.Dodoma Urban Water Supply And Sewerege Athority (Duwasa)
46.Drilling And Dam Construction Authority  (Ddca)
47.Drug Control  And  Enforcement  Authority
48.East Africa Statistical Training Institute 
49.Energy And Water Utilities Regulatory Authority (Ewura)
50.Engineering Registration Board
51.Ethics Secretariat
52.Export Processing Zones Authority (Epza)
53.Fire And Rescue Force (Frf)
54.Fisheries Education And Training Authority  (Feta) 
55.Gairo Regional And Administrative Secretariate
56.Gaming Board
57.Geita District Council
58.Geita Regional Administrative Secretariat 
59.Geita Town Council
60.Geological Survey Of Tanzania
61.Government Chemist Laboratory Authority (Gcla)
62.Government Procurement Service Authority 
63.Hanang District Council
64.Handeni District Council
Na.JINA LA TAASISI
65.Handeni Town Council
66.Higher  Education Student‘S Loan Board  (Heslb)
67.Chalinze District Council 
68.Chalinze Water Supply  And Sewerege Authority
69.Chamwino  District  Council
70.Chato District Council
71.Chemba District Council
72.Chunya District Council
73.Ict Commission 
74.Ifakara Town Council
75.Igunga Council
76.Ikungi District Council
77.Ilala Municipal Council
78.Ilemela Municipal Council
79.Institute Of Accountancy Arusha
80.Institute Of Finance Management (Ifm)
81.Institute Of Judicl Administration
82.Iramba District Council
83.Iringa District Council
84.Iringa Regional And Administrative Secretary (Ras-Iringa)
85.Iringa Urban Water Supply And Sanitation Authority (Iruwasa)
86.Itilima District Council
87.Jakaya Kikwete Cardiac Institute (Jkci)
88.Judiciary Of Tanzania 
89.Kagera Regional Administrative Secretariat 
90. Kahama Shinyanga Water Supply And Sewerage Authority (Kashwasa)
91.Kalambo District Council
92.Kaliua District Council
93.Karagwe District Council
94.Karatu District Council
95.Kariakoo Markets Corporation 
96.Kasulu District Council
97.Kasulu Town Council
98.Katavi Regional And Administrative Secretary (Ras Katav
Na.JINA LA TAASISI
99.Kibaha Education Centre (Kec)
100.Kibaha Town Council
101.Kibaha District Council
102.Kibondo District Council
103.Kigamboni Municipal Council
104.Kigoma District Council
105.Kigoma Regional And Administrative Secretary (Ras Kigoma)
106.Kigoma Ujiji Municipal Council
107.Kilimanjaro Ras 
108.Kilindi District Council
109.Kilolo District Council
110.Kilombero District Council
111.Kilosa District Council
112.Kinondoni Municipal Council
113.Kisarawe District Council
114.Kishapu District Council
115.Kiteto District Council
116.Kondoa District Council
117.Kondoa Town Council
118.Kongwa District Council
119.Korogwe District Council
120.Kwimba District Council
121.Kyela District Council
122.Kyerwa District Council
123.Law Reform Commission
124.Lindi Municipal Council
125.Lindi Regional Administrative Secretary (Ras Lindi)
126.Liwale District Council
127.Longido District Council
128.Ludewa District Council
129.Lukwa Urban Water Supply And Sanitation Authority  (Luwasa) 
130.Madaba District Council
131.Mafia District Council
132.Magu District Council
133.Makambako Town Council
Na.JINA LA TAASISI
134.Makete District Council
135.Manyara Ras 
136.Manyoni District Council
137.Mara Ras 
138.Marine Parks And Reserves Unit 
139.Masasi District Council
140.Masasi Ras 
141.Masasi Town Council
142.Maswa District Council
143.Mbalali District Council
144.Mbeya City Council
145.Mbeya District Council
146.Mbeya Ras 
147.Mbeya Regional Referral Hospital 
148.Mbeya Urban Water Supply And Sanitation Authority 
149.Mbinga Town Council
150.Mbogwe Disctrict Council
151.Mbozi District Council
152.Mbulu District Council
153.Mbulu Town Council
154.Meatu District Council
155.Medial Stores Department
156.Meru District Council
157.Mikocheni Agricultural Research Insitute (Mari)
158.Mikocheni Research Institute
159.Ministry Of Agriculture 
160.Ministry Of Constitutional And Legal Affairs 
161.Ministry Of Defence And National Service (Modans)
162.Ministry Of Foreign Affairs And East African Cooperation (East African Cooperation)
163.Ministry Of Education, Science And Technology 
164.Ministry Of Energy 
165.Ministry Of Foreign Affairs And East African Cooperation (Foreign Affairs)
166.Ministry Of Health, Community Development, Gender, Elderly And Children 
Na.JINA LA TAASISI
167.Ministry Of Healthy, Community Development, Gender, Elderly And Children (Community Development) 
168.Ministry Of Home Affairs
169.Immigration Service Department
170.Ministry Of Industry Trade And Investments 
171.Ministry Of Information, Culture Arts And Sports 
172.Ministry Of Lands, Housing And Human Settlement (Landtenure Support Program)
173.Ministry Of Lands, Housing And Human Settlement Development  
174.Ministry Of Livestock And Fisheries 
175.Ministry Of Minerals 
176.Ministry Of Natural Resources  And Tourism 
177.Ministry Of Water 
178.Ministry Of Work, Transport And Communications (Mwtc)
179.Ministry Of Works, Transport And Communications (Communication)
180.Ministry Of Works, Transport And Communications (Transport)
181.Ministy Of Finance And Planning 
182.Missenyi District Council
183.Misungwi District Council
184.Mkalama District Council
185.Mkinga District Council
186.Mkurabita
187.Mkuranga District Council
188.Mlele District Council
189.Monduli District Council
190.Morogoro Municipal Council
191.Morogoro Ras 
192.Morogoro Urban Water Supply And Sewerage Authority (Moruwasa)
193.Moshi District Council
194.Moshi Municipal Council
195.Mpanda District Council
196.Mpimbwe District Council
197.Mtwara District Council
198.Mtwara Mikindani Municipal Council
Na.JINA LA TAASISI
199.Mtwara Ras
200.Mtwara Urban Water And Sewerage Authority (Mtuwasa)
201.Mufindi District Council
202.Muheza District Council
203.Muhimbili National Hospital
204.Muhimbili Orthopaedic Institute (Moi)
205.Muhimbili University Of Health And Allied Science (Muhas)
206.Musoma District Council
207.Musoma Municipal Council
208.Mvomero Dostrict Council 
209.Mwalimu Nyerere Memorial Academy
210.Mwanga District Council
211.Mwanza City Council
212.Mwanza Ras
213.Mwanza Urban Water Supply And Sewerage Authority (Mwauwasa)
214.Namtumbo District Council
215.Nanyamba Town Council
216.Nanyumbu District Council
217.National Arts Council Tanzania (Nact)
218.National Assembly Of Tanzania
219.National Audit Office
220.National Board Of Accountants And Auditors (Nbaa) 
221.National Bureau Of Statistics (Nbs) 
222.National College Of Tourism
223.National Collegiate Athletic Association (Ncaa)
224.National Construction Council (Ncc)
225.National Defense College (Ndc)
226.National Economic Empowerment Council (Neec)
227.National Electoral Commission (Nec)
228.National Environment Management Council (Nemc)
229.National Examinations Council Of Tanzania. (Necta)
230.National Fish Quality Control Laboratory (Nfqclab)
231.National Food Reserve Authority (Nfra)
232.National Health Insurance Fund (Nhif)
Na.JINA LA TAASISI
233.National Housing And Building Research Authority (Nhbra)
234.National Identification Authority (Nida)
235.National Institute For Medical Research (Nimr)
236.National Institute Of Transport (Nit)
237.National Irrigation Commission
238.National Land Use Planning Commision (Nlupc)
239.National Museum Of Tanzania (Nmt)
240.National Prosecution Service 
241.National Records And Archives. Management Department 
242.National Sports Council (Nsc)
243.Neglected Tropical Diseases Control Programme (Ntdcp)
244.Nelson Mandela African Institute Of Science And Technology (Nm-Aist)
245.Newala District Council
246.Newala Town Council
247.Ngara District Council
248.Ngorongoro Conservation Area Authority
249.Ngororngoro District Council
250.Njombe District Council
251.Njombe Regional Administrative Secretariat 
252.Nkasi District Council
253.Nyanghwale Disctrict Council
254.Nyasa District Council
255.Nzega District Council
256.Nzega Town Council
257.Occupational Safety And Health Authority (Osha)
258.Ocean Road Cancer Institute (Orci)
259.Office Of Solicitor General
260.Office Of The Registrar Of Political Parties (Orpp)
261.Open University Of Tanzania
262.Pangani District Council
263.Petroleum Bulk Procurement Authority (Pbpa)
264.Pharmacy Council Of Tanzania
265.President‘S Office – Regional Administration And Local Government (Po-Ralg) 
Na.JINA LA TAASISI
266.President’s Office – Public Services Management And Good Governance 
267.President’s Office – Revolutionary Council
268.Prevention And Combating Of Corruption Bureau (Pccb)
269.Prime Minister‘S Office, Labour, Youth, Employment And Persons With Disability
270.Prime Minister’s Office (Pmo)
271.Prisons (Magereza)
272.Procurement And Supplies Professionals And Technicians Board (Psptb)
273.Public Service Pension Fund (Pspf)   
274.Public Service Recruitment Secretariat (Psrs)  
275.Public Service Remuneration Board (Psrb)
276.Public Service Social Security Fund  (Psssf)
277.Public Sevirvice Commision (Psc)
278.Pwani Ras Pwani
279.Registration, Insolvency And Trusteeship Authority  (Rita)
280.Rombo District Council
281.Ruangwa District Council
282.Rufiji District Council
283.Rukwa Regional Administrative Secretariat 
284.Rural Water Supply And Sanitation 
285.Ruvuma Regional And Administrative Secretary (Ras Ruvuma)
286.Same District Council
287.Self Micro-Finance Fund
288.Serengeti District Council
289.Shinyanga Municipal Council
290.Shinyanga Regional And Administrative Secretary (RasShinyanga)
291.Shinyanga Urban Water Supply  And Sewerage Authority (Shuwasa)
292.Siha District Council
293.Sikonge District Council
294.Simiyu Regional And Administrative Secretary (Ras-Simiyu)
295.Singida District Council
296.Singida Municipal Council
297.Singida Ras
Na.JINA LA TAASISI
298.Small Industries Development Organization (Sido)
299.Songea District Council
300.Songea Municipal Council
301.Songea Urban Water Supply And Sewerage Authourity (Souwasa)
302.Songwe District Council
303.Songwe Ras
304.State Mining Corporation (Stamico)
305.Sugar Board Of Tanzania (Sbt)
306.Sumbawanga District Council
307.Sumbawanga Municipal Council
308.Suwasa Rukwa
309.Tabora District Council
310.Tabora Municipal Council
311.Tabora Regional And Administative Secretary (Ras Tabora)
312.Tabora Urban Water Supply And Sanitation Authority (Tuwasa)
313.Tandahimba District Council
314.Tanga City Council
315.Tanga Regional And Administrative Secretary (Ras Tanga)
316.Tanga Urban Water And Sewerage Authority (Tanga Uwasa)
317.Tanzania Agricultural Research Institute (Tari)
318.Tanzania Airports Authority (Taa)
319.Tanzania Atomic Energy Commission (Taec)
320.Tanzania Broadcasting Corporation (Tbc)
321.Tanzania Building Authority (Tba)
322.Tanzania Bureau Of Standards (Tbs)
323.Tanzania Civil Aviation Authority (Tcaa)
324.Tanzania Commission For Aids (Tacaids)
325.Tanzania Cooperative Development Commission (Tcdc)  
326.Tanzania Dairy Board (Tdb)
327.Tanzania Drug Control Commission
328.Tanzania Education Authority
329.Tanzania Engineering And Manufaturing Design Organiation (Temdo)
330.Tanzania Fire And Rescue Force
331.Tanzania Food And Nutrition Ccentre (Tfnc)
Na.JINA LA TAASISI
332.Tanzania Forest Services Authority (Tfsa)
333.Tanzania Geothermal Development Company (Tgdc)
334.Tanzania Global Learning Authority (Tagla)
335.Tanzania Government Flight Authority (Tgfa) 
336.Tanzania Industrial Research And Development Organization (Tirdo)
337.Tanzania Institute Of Accountancy (Tia)
338.Tanzania Institute Of Education (Tie)
339.Tanzania Insurance Ombudsman 
340.Tanzania Investment Bank (Tib)
341.Tanzania Investment Centre (Tic)
342.Tanzania Library Services Board (Tlsb)
343.Tanzania Livestock Research Institute (Taliri)
344.Tanzania Meat Board
345.Tanzania Meteorological Authority (Tma)
346.Tanzania Mining Commission 
347.Tanzania National Business Council
348.Tanzania National Parks (Tanapa)
349.Tanzania Official Seed Certication Institute (Tosci)
350.Tanzania People‘S Defence Force (Tpdf)
351.Tanzania Postal Bank (Tpb)
352.Tanzania Railways Corporation (Trc) 
353.Tanzania Railways Limited (Trl)
354.Tanzania Regional Immigration Training Academy (Trita) 
355.Tanzania Roads Agency  (Tanroads)
356.Tanzania Roads Fund
357.Tanzania Rural And Urban Roads Authority (Tarura)
358.Tanzania Shiping Agencies Cooperation (Tasac)
359.Tanzania Sisal Board (Tsb)
360.Tanzania Social Action Fund (TASAF)
361.Tanzania Telecommunications Company Limited (Ttcl)
362.Tanzania Tobacco Board (Ttb) 
363.Tanzania Trade Development Authority (Tantrade)
364.Tanzania Tree Seed Authority (Ttsa)
365.Tanzania Veterinary Laboratory Authority (Tvla)
Na.JINA LA TAASISI
366.Tanzania Wildlife Authority (TAWA)
367.Tanzania Wildlife Research Institute (Tawiri)
368.Tanzania Electrical, Mechanical And Electronics Services Authority (TEMESA)  
369.Tarime District Council
370.Tarime Town Council
371.Teacher‘S Service Commision (Tsc)
372.Temeke Municipal Council
373.Treasury Registrar Office (Tro)
374.Tropical Pesticides Research Institute (Tpri) 
375.Ubungo Municipal Council
376.Ukerewe District Council
377.Ulanga District Council
378.Unesco National Commission Of The United Republic Of Tanzania (NATCO)   
379.Universal Communication Services Access Fund (UCSAF)
380.Uongozi Institte
381.Urambo Disctrict Council 
382.Vocational Educational And Training Authority (VETA)
383.Waqf And Trust Commission (Wtc)
384.Wanging‘Ombe District Council
385.Water Development And Management Institute (WDMI)
386.Weights And Measures Authority (Wma)
387.Workers Compesation Fund (Wcf)
388.Zanzibar Business And Property Registration Authority 
389.Marine Service Company Limited 
390.Kahama Urban Water Supply And Sanitation Authority (Kuwasa) 
391.Tanzania Insurance Reguratory Authority (Tira)
392.Shinyanga District Council
393.National Aids Control Program – Nacp.Go.Tz
394.Bukoba Urban Water Supply And Sanitation Authority (Buwasa)
395.Msalala District Council
396.Shinyanga District Council 
397.Mwanhuzi Urban Water Supply And Sanitation Authority 
398.Contractors Registration Board (Crb)
Na.JINA LA TAASISI
399.Tanzania Nursing&Midwifery Council (Tnmc)
400.Moshi Urban Water Supply&Sewerage Authority (Muwsa) 
401.Tanzania Petroleum Development Corporation (Tpdc)
402.Tanzania Extractive Industries Transparency Initiative (Teiti)
403.Mpanda Municipal Council 
404.Kilwa District Council 
405.Mweka Wildlife
406.Tanzania Revenue Authority (Tra)
407.Geita Urban Water Supply And Sanitation Authority (Geuwasa)
408.Medical Council Tanzania 
409.Mpanda Water Supply And Sanitation Authority (Mpandawasa) 
410.Kishapu Urban Water Supply And Sanitation Authority (Kiwassa)
411.Rungwe Dc
412.Kibiti Dc
413.National Development Corporation (Ndc) 
414.Tanzania Coffee Board 
415.Tanganyika Dc
416.National Internet Data Center(Nidc)
417.Petroleum Upstream Regulatory Authority (Pura)
418.Local Government Training Institute (Lgti)
419.Mugumu Urban Water Supply And Sanitation Authority 
420.Kilimanjaro Airport Development Company (Kadco)
421.Livestock Training Authority (Lita)
422.Mombo District Council 
423.Tanzania Film Board
424.Mzinga Corporation
425.Zanzibar Higher Education Loan Board
426.Singida District Council 
427.Public Procurement Appeals Court 

KIAMBATISHO NA. 12

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

NYARAKA ZILIZOKUSANYWA ZILIZOKUSANYWA KUTOKA

KATIKA TAASISI MBALIMBALI

Na.TAASISI/OFISINYARAKA ZA WAZINYARAKA ZA  SIRI/SIRI SANAJUMLA
1. Halmashauri                  ya Manispaa ya Bukoba5199150
2. Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo32638
3. Halmashauri ya Wilaya ya Ngara5150101
4. Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe125125
5. Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Vijijini16466330
6. Halmashauri ya Wilaya ya Magu437
7. Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba7613
8. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe12744171
9. Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema3131
10.Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Vijijini23326
11.Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti37643
12.Halmashauri ya Wilaya ya Meatu10767174
13.Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga125466
14.Halmashauri ya Manispaa ya Kahama8524109
15.Halmashauri ya Wilaya ya Igunga1111
16.Halmashauri ya Wilaya ya Iramba24428
Na.TAASISI/OFISINYARAKA ZA WAZINYARAKA ZA  SIRI/SIRI SANAJUMLA
17.Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni34147181
18.Halmashauri ya Jiji la Dodoma (nyaraka za iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma – CDA237194  
19.TANAPA412061
20.Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)6687761,444
                                                                  JUMLA KUU  3,224

KIAMBATISHO NA. 13

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

TAASISI ZA UMMA ZILIZOWEKEWA MFUMO WA MASIJALA MTANDAO (E-FILE MANAGEMENT SYSTEM)

NAJINA LA TAASISI
1Ofisi ya Rais – Ikulu,
2Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji,
3Mahakama Kuu ya Tanzania,
4Tume ya Utumishi wa Mahakama
5Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
6Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma,
7Ofisi ya Katibu Tawala – Dar e Salaam
8Wizara ya Maji
9Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute),
10Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA),
11Wakala wa Huduma za Mifugo (TVLA),
12Wakala wa Lishe na Chakula
13Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)
14Chuo cha Serikali za Mitaa Homboro
15wakala wa mbolea Tanzania (AGITF)
16Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB),
17Mfuko wa Taifa wa Maji
18Halmashauri ya Manispaa ya Arusha,
19Hospitali ya Benjamini Mkapa
20Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST)
21Mamlaka ya Usimamizi wa Mbolea (TFRA)
22Shirika la Posta
23Chuo cha Maendeleo ya Mifugo (LITA),
24Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB,)

KIAMBATISHO NA. 14

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

TAASISI ZA UMMA ZILIZOWEKEWA MFUMO WA UTUNZAJI WA

KUMBUKUMBU ZA KIUTENDAJI (KEYWORD FILING SYSTEM)

NAJINA LA TAASISI
1Ofisi ya Rais – Ikulu,
2Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji,
3Ofisi ya Rais,Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma,
4Ofisi ya Mkuu wa Mkoa – Dar es Salaam
5Ofisi ya Mkuu wa Mkoa –Singida
6Ofisi ya Mkuu wa Wilaya – Serengeti
7Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
8Wizara ya Maji
9Mfuko wa Taifa wa Maji
10Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)
11Chuo cha Serikali za Mitaa Homboro
12Halmashauri ya Manispaa ya Arusha,
13Mamlaka ya Majisafi na  Usafi wa Mazingira – Arusha (AUWASA
14Hospitali ya Benjamini Mkapa
15Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST)
16Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
17Chuo cha Ustawi wa Jamii
18Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA)
19Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
20Chuo cha Wanyamapori Mweka
21Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)
22Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT)
23Hospitali ya Benjamin Mkapa,
24Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzani
25Bodi ya Korosho Tanzania.
26Bodi ya Nyama (TMB)
27Bodi ya Maziwa (TDB)

KIAMBATISHO NA. 15

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

TAASISI ZA UMMA ZILIZOFANYIWA UKAGUZI WA HALI YA

UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU

NAJINA LA TAASISI
1Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu
2Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Songwe
3Ofisi ya Mkuu wa Wilaya  ya Bariadi
4Halmashauri ya Manispaa ya Songea
5Halmashauri ya Jiji la Tanga
6Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)
7Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini  (RUWASA)
8Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (BPA)
9Bodi ya Pamba
19Shirika la Reli Tanzania (TRC)
11Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)
12Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania
13Mamlaka ya Eneo Maalum la Uwekezaji wa Mauzo Nchini (EPZA),
14Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA),
15Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogovidogo (SIDO)
16Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO)
17Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE)
18Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI),
19Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TASUBA
20Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Shrika la Posta Tanzania (TPC),
21Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo
22Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero
23Halmashauri ya Wilaya ya Ilala
24Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba
25Halmashauri ya Wilaya ya Magu
26Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe

KIAMBATISHO NA. 16

IDARA YA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

TAASISI ZA UMMA ZILIZOPATIWA MAFUNZO YA UTUNZAJI WA

KUMBUKUMBU

NAJINA LA TAASISI
1Ofisi ya Rais – Ikulu
2Tume ya Utumishi wa Mahakama
3Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza
4Wizara ya Kilimo
5Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania
6Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWASA)
7Bodi ya  Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)
8TANESCO kanda ya Mwanza,
9Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
10Chuo cha Uongozi wa Mahakama(IJA) –  Lushoto
11Chuo Kikuu cha Dar es salaam
12Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)
13Mfuko wa Maendeleo ya Jamii ( TASAF)
14Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA)
15Halmashauri  ya jiji la Arusha
16Halmashauri ya Jiji la Mwanza

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *